Siri Imefichuka! Babu wa Loliondo ametumwa na Shetani

Naomba nikujibu hoja zako kama ifuatavyo:
- Huyo babu anatumiwa tu na shetani. Nguvu za giza zikiondoka ndani yake atakuwa mtu "normal" tena atashangaa kwanini alikuwa anapoteza muda wake kugawa vikombe. * Tunachofanya sasa ni kupambana na roho hiyo inayotenda kazi ndani ya babu. Na hiyo roho ya shetani itashindwa tu kwa Jina la Yesu. Time will tell.
- Agizo la kuponya liliishatolewa na Yesu mara moja(Mathayo 10:1) na halitarudiwa kutolewa tena kwa ndoto wala kwa maono. Na agizo hilo ni la kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila aina. Mungu hana kigeugeu(Malaki 3:6) Aliyesema ponyeni magonjwa yote hawezi leo kubadilisha kauli yake na kusema ponya magonjwa manne tu. HA-TU-DA-NGA-NYI-KI!!
- Agizo la kuponya linaenda sambamba na agizo la kuhubiri Injili(na kuanzisha makanisa - Marko 16:15-18). Anayesema ametumwa kuponya tu, Mungu amsamehe kwa kuwa hajui alisemalo wala alitendalo.
- Yesu aliwaambia waliopona ukoma waende wakajionyeshe kwa makuhani. Hao waliopona kwa babu nao waende wakajionyeshe kwa madaktari(wapimwe) na ukweli ujulikane maana Waongo ni wengi na wachakachuaji ni wengi.
- Wanaosema watu wanapona kwa babu kwa imani hawajui hata maandiko yanasema nini juu ya imani. Imani huja kwa kulisikia Neno la Kristo(Warumi 10:17). Kama babu anataka tuamini anachokisema, ni lazima ahubiri Neno la Kristo. Watumishi wa Mungu(Mitume: Paulo, Petro...walihubiri Injili na kuwaombea watu). walifanya yote. Yesu alihubiri Injili na kuponya. Alifanya yote. Waganga wa kienyeji ndio wanaofanya moja tu "kuponya" na uponyaji wao ni feki. Shetani ataumbuka tu. Roho Mtakatifu yupo kazini kutujulisha kweli yote nayo kweli itatuweka huru.

Mungu akubariki ndugu, hayo uliyosema ni kweli kabisa yanayo tokea kwa babu hayaendani kabisa na maandiko. kwani tunatakiwa kuutafuta ufalme wake kwanza halafu mengine yote tutazidishiwa. kwa maneno mengine tuponye roho zetu kwanza halafu ndiyo tuponye miili.

Naelewa kuwa kweli itapingwa kwa nguvu zote hapa kwasabubu hiyo ni kazi ya yule mwovu kufanya hivyo kuzuia ukweli. Yeye ni mwongo toka mwanzo na ni baba wa uongo.

Mungu akubariki sana.
 
What u ve said nakubaliana na wewe....Bwana medium uliyepost acha watu wakatibiwe kwa Imani zao if u think that is devil funga na kuomba ulikemee kwa jina unalolijuwewe kuliko kuja na kuleta upupu wako hapo hujaumwa wewe thts why u talk like tht..
Nimeumwa magonjwa mengi sana katika maisha yangu. Lakini kwakuwa ninamwamini Yesu nimekuwa nikiliitia Jina lake na kukemea hayo magonjwa, na kwa jina hilo kuu la Yesu nimepona magonjwa mengi. Ndio maana nawahurumia Watanzania wenzangu wanaopoteza pesa(nauli) na muda wa kwenda na kukaa kwa babu wakati kuna uponyaji bure unaopatikana katika Yesu. Kama ulienda kanisani ukaombewa na hujapona huenda imani yako ni haba au labda unataka uponyaji tu lakini Yesu mwenye kutoa huo uponyaji humtaki.
 
Sijawahi kuona mtu anayechukia watu kuwekwa huru na magonjwa yao kwa kuponywa ila shetani. Hatafurahi hata kidogo magonjwa yawaache watu maana ndio kazi yake kubwa kusababisha magonjwa. Hivyo anatapatapa baada ya kuona ufalme wake wa giza la magonjwa tena sugu unavunjwa kwa kasi kuu. Shetani anafurahi sana anapoona watu wameinamisha vichwa vyao na kulia kwa maumivu ya magonjwa yaliyowasababishia kukata tamaa ya kuishi. Hii ndio raha yake. USHINDWE EWE MTESI NA BWANA YESU AKUKEMEE!!!
.
 
Sijawahi kuona mtu anayechukia watu kuwekwa huru na magonjwa yao kwa kuponywa ila shetani. Hatafurahi hata kidogo magonjwa yawaache watu maana ndio kazi yake kubwa kusababisha magonjwa. Hivyo anatapatapa baada ya kuona ufalme wake wa giza la magonjwa tena sugu unavunjwa kwa kasi kuu. Shetani anafurahi sana anapoona watu wameinamisha vichwa vyao na kulia kwa maumivu ya magonjwa yaliyowasababishia kukata tamaa ya kuishi. Hii ndio raha yake. USHINDWE EWE MTESI NA BWANA YESU AKUKEMEE!!!
.
Sichukii watu kuwekwa huru na kuponywa magonjwa. Namchukia yeye(shetani) anayewadanganya watu kwa miujiza ya uongo, WASIONE UMUHIMU WA KUSIKILIZA TENA NENO LA MUNGU ili waendelee kukaa katika dhambi zao na kisha siku ya mwisho waangamie pamoja naye katika moto wa milele. Kama unaamini kikombe cha babu kinaweza kukuponya kisukari, kwanini usiamini kwamba Yesu anaweza kukuponya bila kutoa pesa? Hujui kwamba Yesu ni Mungu na kwa Neno lake vitu vyote viliumbwa? Aliyeumba madini au material yaliyotengeneza hivyo vikombe na miti inayotumiwa na babu, atashindwa kukuponya kisukari? Unakubali kutapeliwa mchana kweupe? THINK TWICE
 
Tatizo la kusoma biblia kama novo! Kaisome tena...otherwise crap
Wanaoisoma Biblia kama "novo" ndio hao wanaokuwa wepesi kuamini wakisikia mtu anasema "Nimetumwa..." "Nimeoteshwa..." Hawajui hata mungu wa dunia hii(shetani) anawaotesha watu!
Manabii wa uongo(kama babu) tunawatambua kwa matunda(matendo, maneno) yao. Huyu babu anayedai kwamba yeye ni mtumishi wa Mungu na huku hataki kuwahubiri maelfu ya watu wanaokwenda kwake kupata kikombe, ni nabii wa uongo maana anapingana na Neno la Mungu linalotuagiza kuhubiri Injili. Mtume Paulo alifanya miujiza mingi ya kupita kawaida hata hivyo alijua ni lazima ahubiri Injili. Ndio maana akasema "Ole wangu nisipoihubiri Injili" (1 Wakorintho 9:16). Wana JF, mshukuruni Mungu maana ametufunulia siri iliyokuwa imefichika. Ametujulisha kuwa babu ni mbwa mwitu aliyevaa ngozi ya kondoo. Anafananishwa pia na panya anayeuma huku anapuliza. "Unapona" leo, halafu kesho unaenda Jehanam, crap!
 
kuna ukweli kwenye hii mada ingawaje nina sababu tofauti...............................

1) Babu alidai ya kuwa Mwenyezi Mungu alimwagiza atibu watu ndani ya msitu lakini alikaidi amri hiyo kwa kuwathamini viumbe badala ya Muumba........................Babu aliona ni vyema kutuliza adha za viumbe kwa maana ya wanadamu wasipate shida ya kuingia msituni na huku hakuna usafiri.....................................Nabii Musa naye Mwenyezi Mungu alimwadhibu kwa kutotii amri yake ya kupiga mwamba mara moja na Musa alipiga mara mbili na hivyo kumdhalilisha mbele ya watu wa taifa la Mungu...............................Mwenyezi Mungu alimwadhibu kwa kumzuia kuingia nchi ya ahadi................................

Ipo mifano mingi ndani ya Biblia ambapo mwanadamu alipingana na maagizo ya Muumba na kifo kilikuwa ni adhabu aliyopewa mwanadamu........................mfalme wa kwanza wa wayahudi - Saul- aliyechaguliwa na Muumba alibeza agizo la Mungu la kutochukua chochote kutoka kwa maadui wa Muumba ambao watawashinda vita.................................majemedari wake wakabeba mali kibao na hakuwakataza kwa sababu alitaka kumpendeza kiumbe badala ya Muumba.........................


2) Katika kitabu cha torati sura ya 18: 20- 22 tunajifunza ya kuwa adhabu ya Nabii wa uongo ni kifo..........hivyo tuangalie huyu Babu ana miezi mingapi humu duniani baada ya kudai ya kuwa ana mwasiliano na Muumba bila ya kupitia kwa Yesu Kristu kama Biblia takatifu inavyothibitisha katika Yohana 14:6 na Yohana 15: 5-7 ...............katika maandiko tajwa Yesu Kristu kwenye utukufu wake amesema hakuna njia ya ukweli na uzima bila ya kupitia kwake na hakuna mawasiliano ya moja kwa moja na Baba bila ya kupitia kwake.................na Kristu alifunga kazi kwa kusema hakuna tuwezalo kulifanya bila ya kupitia kwake..................................Huyu Babu asiyemtaja Kristu na kudai ana mawasiliano ya moja kwa moja na Baba.............................ni dhahiri anamkashifu Kristu na adhabu yake imetajwa kwenye Zaburi ya 110:1: "The Lord said to My Lord; sit at My right hand till I make your enemies your foostool."

3) kuhusu mwanandamu kutafuta ushauri kwa waganga wa kienyeji au spiritualists...........inabidi turudi kwenye kitabu cha Torati 23: 12-15 tunajifunza ya kuwa Mwenyezi Mungu anachukia uchafu wa vinyesi vya mwanadamu na waliagizwa watumie miti kufukua na kuvifukia vinyesi vyao vinginevyo Mwenyezi Mungu atawapa kisogo...............................kwa babu ambaye anadai alipewa maono kuanzia 1991 na kuanza shughuli za tiba 2010 Agosti ni swala la kujiuliza ni kwa nini hakushughulikia suala la vyoo ili kutomfukuza Mwenyezi Mungu katika eneo lake..........hivi sasa watu Loliondo wanajisaidia hovyo na wala hawafukii vinyesi vyao..........................kweli Mwenyezi Mungu yupo kwenye mazingira machafu namna hiyo?

4) Katika kitabu cha Torati 18: 9- 13 Mwenyezi Mungu aliwakataza taifa lake kutumia ushirikina katika kutatua matatizo yao na ya kuwa Yeye Muumba huwachukia washirikina......................................................

5) Kwenye katiabu cha Torati 17: 19- 20 Mwenyezi Mungu ametoa agizo la viongozi kuwa wanasoma kila siku Biblia Takatifu na hususani amri zake....................sijamwona babu akiwa ameshika Biblia Takatifu kila wakati na kuisoma.....................bali naona akikishika kikombe tu...........................na kwa kutoisoma Biblia Takatifu kila siku..................................maisha ya Babu hayatakuwa marefu.............

6) Kitabu cha Torati sura ya 13 hususani aya za 13: 1-12 na kwa sura yote ya 13 kwa ujumla wake inatukataza kuwasikiliza manabii wauongo na ambao wanatushawishi kuabudu miungu wengine.....hata ukitibiwa Mwenyezi Mungu anakujaribu tu kukupima akama unajua ni nani mwenye mamlaka ya uhai na vifo juu yetu soma Torati 13: 1-12........nimeshtushwa na taarifa ya kuwa usiku wagonjwa huimba nyimbo za kumtukuza babu badala ya Yesu Kristu..............tukumbuke babu ni kiumbe na Yesu Kristu ni sehemu ya Muumba.........soma Yohana 14:7, 14:11, 14:21, 14:23........vile vile soma waraka wa Paulo kwa Wafilipo 2:9-11.

7)Kwenye kitabu cha Leviticus 19:31 Mwenyezi Mungu ametukataza kuwasiliana na mapepo..............kiumbe katika kuchanganyikiwa anaweza kuyaiita mapepo kuwa ni Muumba.......................tiba za babu siyo za papo kwa hapo na huo ndiyo mushkeli mkubwa sana katika utapeli wake.......................Mwenyezi Mungu alisema neno lake ni uzima...na wala siyo pata potea kama babu anavyodai.........soma kitabu cha Torati 32:39 na Matayo 4:4.

8) Kama unaamini dawa za babu zinatibu nenda katafute tiba yako lakini ukumbuke Muumba pia atakuwa anakujaribu nafsi yako.....soma Torati 13: 1-12...je wasujudia kiumbe alichokiumba yeye Mwenyewe Muumba au wamsujudia Muumba Mwenyewe?............

9) magonjwa yasiyotibika ni adhabu za kilaana ambazo Muumba ametutumia kutokana nasi kumwasi Yeye..........................soma Leviticus 26:14-46.

10) katika kitabu cha Torati 5:11 Mwenyezi Mungu ametukataza tusilitumie jina lake kwa mambo maovu.....na Aliahidi kutuadhibu sote tunaokaidi amri hii..................hivi kuna uzima na ukweli nje ya Kristu Yesu?
 
Magari yafurika tena Loliondo

Imeandikwa na Shadrack Sagati; Tarehe: 20th March 2011 @ 23:57 Imesomwa na watu: 71; Jumla ya maoni: 0








HALI katika Kijiji cha Samunge wilayani Ngorongoro mkoani Arusha, ni mbaya kutokana na kuongezeka msururu wa magari yanayopeleka ‘wagonjwa' kupata tiba kwa Mchungaji mstaafu Ambilikile Mwaisapile.

Hali hiyo imemtisha Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali ambaye ametangaza
magari yanayofanya safari za kwenda huko kusimamisha safari zake kwa siku 10 ili yaliyopo eneo hilo yapungue.

Kuongezeka kwa magari katika kijiji hicho ni kutokana na madereva wake kukiuka amri ya Serikali ambayo imeagiza magari yanayoenda kwa Babu yawekewe utaratibu wa kwenda katika kijiji hicho kwa mpango baada ya kupungua yaliyopo.

Lali ameutupia lawama uongozi wa Wilaya ya Serengeti mkoani Mara, kuwa umeshindwa kutoa ushirikiano kutokana na kutoweka vizuizi katika barabara zinazoingia Loliondo, hivyo kufanya magari yamiminike kwa wingi kutoka Kanda ya Ziwa.

Akizungumza kwa simu, Lali aliliambia gazeti hili kuwa msururu uliopo katika kijiji hicho kwa sasa ni mrefu kuliko iliyopita siku za nyuma na magari hayo yanaweza kupungua ndani ya wiki moja.

"Nilienda asubuhi nimekuta foleni ya magari iko porini ambako hamna namna ya kupata huduma za chakula," alisema na kuongeza. "Hawa watu wa Kanda ya Ziwa ni wakorofi, wameleta watu wengi na safari hizi wanazifanya nyakati za usiku," alisema.

Alisema magari ya kutokea njia zinazotoka mjini Arusha yamepungua kutokana na vizuizi vilivyowekwa.

Ila alisema mabasi mengi ya Kanda ya Ziwa yameacha biashara yao ya kawaida na sasa yamejazana katika Kijiji cha Samunge mjini Loliondo ambako yamepeleka watu kwa ajili ya kupata matibabu.

DC huyo alisema amekuwa anajaribu kumpigia Mkuu wa Wilaya ya Serengeti amweleze waweke vizuizi barabarani "lakini simpati kwa simu na hata Katibu Tawala wake hapokei simu yangu."

Alionya kuwa iwapo mikoa na wilaya zinazopakana na wilaya yake wakigoma kutoa ushirikiano, ni wazi kuwa agizo la Serikali la kutaka kuingiza watu katika eneo hilo kwa utaratibu litashindikana.

Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi aliliambia
gazeti hili kuwa tayari amemwagiza Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Isidori Shirima kukutana na wakuu wa mikoa ambao wanapakana na mkoa wake ili kuweka utaratibu wa kupeleka watu Loliondo.

"Njia zote zinazoingia Loliondo na Arusha ni mali yake ni lazima akutane na wenzake waweke utaratibu mzuri," alisema Lukuvi ambaye alikiri kuwa naye ameambiwa na DC wa Ngorongoro kuwa foleni ya magari imeongezeka maradufu kuliko ilivyokuwa wiki zilizopita.

Lukuvi alisema Serikali haiwezi kuvumilia watu wanaoenda kwa Babu wakae siku tano hadi nane wakisubiri tiba hasa katika kipindi hiki ambacho mvua zinanyesha.

Alisema utaratibu alioshauri ni magari yabaki yanasubiri zamu yao ifike kwenye maeneo ya miji ili watu wawe wanapata huduma muhimu.

"Wanaweza kuweka utaratibu wa kufungulia magari 100 kila njia inayoingia Loliondo baada ya kujiridhisha kuwa magari yaliyoenda yamerudi," alisema Lukuvi.

Alisema namna ya kuyatambua magari hayo ni kwa wakuu wa mikoa kuhakikisha magari yanayofanya safari za kwenda Loliondo yanaegeshwa eneo moja na kupewa namba ili utaratibu wa kuyatambua uwe rahisi zaidi.

Naye Kiongozi wa chama cha DP, Mchungaji Christopher Mtikila amedai kitendo cha maofisa wa Serikali kumiminika kwa wingi kwenda Loliondo ni ushahidi wa wazi kuwa nchi
inaongozwa na watu wenye magonjwa sugu na ni kinyume cha Katiba, lakini pia ni alama ya "utapiamlo wa kiroho."

"Katiba imeruhusu imani ya dini kwa watu wote, lakini haijaruhusu dini kuchanganywa na siasa huku Serikali ikitoa huduma kwa watu wa dini zote," alisema Mtikila mjiniDar es Salaam alipozungumza na wanahabari.

Hata hivyo, Lukuvi katika ufafanuzi wake, alisema Serikali haingilii mambo ya imani za watu, ila kwa mkusanyiko wa watu ni lazima iingilie ili huduma za muhimu zipatikane kwani watu hao ni mali ya Serikali.

"Ndio maana unaona pale kuna ulinzi wa Polisi na sasa tunataka watu waende kwa utaratibu, Serikali haihusiki na imani ya yule Mchungaji ila watu wanaoenda ni wa kwetu," alisema Lukuvi.
 
Anayedai kutibu kama Babu azuiwa

Imeandikwa na Arnold Swai, Hai; Tarehe: 20th March 2011 @ 23:50 Imesomwa na watu: 95; Jumla ya maoni: 0








KUTOKANA na kujitokeza kwa mtu mwingine wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro anayetoa dawa ya kutibu magonjwa sugu kama alivyo Mchungaji mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwaisapile 'Babu', mtu huyo amesitishwa na Ofisa Mtendaji wa Kata kuendelea na huduma hiyo.

Akizungumza na gazeti hili kwa simu, kijana huyo aliyejitambulisha kwa jina la Hilali James (28), alisema endapo Serikali itashikilia msimamo wake wa kuendelea kuisitisha huduma yake, tayari ameoteshwa ndoto kuwa atatokea mtu mwingine ambaye ataendelea kuitoa huduma hiyo.

James alisema huduma hiyo alikuwa akiitoa katika Kijiji cha Mbomani Chini Kata ya Tarakea wilayani Rombo, ambapo masharti yake ni mtu kutakiwa kunywa vikombe viwili kwa wakati mmoja na hairuhusiwi kurudia.

Mbali na kunywa, alisema alioteshwa ndoto kuwa atapokea Sh 500, ambazo kati ya hizo, Sh 200 ni kwa ajili ya matumizi yake ya kuwalipa wafanyakazi, na Sh 300 za kuwasaidia yatima na watu wasiojiweza.

Akizungumzia magonjwa yanayotibiwa na dawa yake, alidai inatibu shinikizo la damu, kisukari pumu, saratani, figo, Ukimwi na magonjwa ya tumbo.

Alidai tayari watu wapatao 100 wamekwisha inywa dawa hiyo na kupata uponyaji.

Kijana huyo mwenye mke na watoto wanne, alibainisha kuwa awali alikuwa fundi wa baiskeli, na kwamba chanzo cha kuanza kutoa dawa hiyo ni kutokana na kuoteshwa ndoto na Yesu Kristo usiku na mchana.

Alisema mti aliooteshwa kuutumia hadi sasa hajaufahamu jina lake, na kuwa ulikuja katika ndoto na hajawahi kuuona tangu kuzaliwa kwake.

Alisema yeye kuibuka baada ya Mchungaji Mwaisapile si tatizo kwa sababu, kila jambo lina wakati wake, hivyo wakati huu ni wake.

Juhudi za kumpata Ofisa Mtendaji aliyesitisha utoaji wa huduma hizo hazikuzaa matunda, kwani simu yake ya mkononi ilikuwa haipatikana.
 
PHP:
Mbali na kunywa, alisema alioteshwa ndoto kuwa atapokea Sh 500,  ambazo  kati ya hizo, Sh 200 ni kwa ajili ya matumizi yake ya kuwalipa   wafanyakazi, na Sh 300 za kuwasaidia yatima na watu wasiojiweza.

Hizi ndoto na utajirisho wa papo kwa papo unatia mashaka........................Karama za Mwenyezi Mungu amezitoa kwa bure sasa hizi kodi za kiumbe zatoka wapi?
 
Ndodi: Wanaoponda dawa ya Babu wana wivu


na Shabani Matutu


amka2.gif
DAKTARI wa dawa asili wa kituo cha Haleluya Sanitarium, Isack Ndodi, amewaponda wachungaji wanaodai dawa za Mchungaji Ambilikile Mwaisapile ni za kishirikina.
Akizungumza na Tanzania Daima mwishoni mwa wiki nyumbani kwake maeneo ya Mbezi Juu, alisema tatizo la Askofu Zakaria Kakobe na mtume na nabii wa kanisa la Efatha, Josephat Mwingira, ni wivu wa kumuona mwenzao kapata dawa ya kutibu magonjwa sugu ambayo yalikuwa yameshindikana.
"Kakobe na wenzake walitakiwa kusema Amina kwa watu kupona kuliko kuanza kuonyesha wivu wao na kumtaka azuiliwe.
"Kitendo cha Kakobe kutaka kujua majibu ya serikali kwa dawa hiyo inayotolewa kwa maombi haiwezekani kwa kuwa ina miujiza hivyo haiwezi kugunduliwa na vyombo vya kisayansi," alisema.
Alisema walichopaswa kusema ni kwamba wale wanaopona ugonjwa huo wawe wanatoa ushuhuda kwa kuonyesha kipimo chao cha kwanza kinachoonyesha wameathirika na baadaye waonyeshe baada ya kunywa kikombe na kupona.
Kauli kama hiyo ilitolewa na mhubiri Anthony Lusekelo maarufu kama Mzee wa Upako aliyesema kuwa dawa hiyo isiwekewe kipingamizi kwani Mungu ana nguvu; anaweza kufikisha ujumbe kwa mtu asiyetegemewa.
 
PHP:
"Kakobe na wenzake walitakiwa kusema Amina kwa watu kupona kuliko kuanza kuonyesha wivu wao na kumtaka azuiliwe.
   "Kitendo cha Kakobe kutaka kujua majibu ya serikali kwa dawa hiyo   inayotolewa kwa maombi haiwezekani kwa kuwa ina miujiza hivyo haiwezi   kugunduliwa na vyombo vya kisayansi," alisema.
   Alisema walichopaswa kusema ni kwamba wale wanaopona ugonjwa huo wawe   wanatoa ushuhuda kwa kuonyesha kipimo chao cha kwanza kinachoonyesha   wameathirika na baadaye waonyeshe baada ya kunywa kikombe na kupona.
   Kauli kama hiyo ilitolewa na mhubiri Anthony Lusekelo  maarufu kama   Mzee wa Upako aliyesema kuwa dawa hiyo isiwekewe kipingamizi kwani Mungu   ana nguvu; anaweza kufikisha ujumbe kwa mtu asiyetegemewa.


what we see is a crisis of faith..........even the Elect will be deceived............................
 
Wagonjwa wakwama porini Loliondo Send to a friend Sunday, 20 March 2011 21:37

mch%20mwasapile%20loliondo.jpg
Mchungaji Ambilikile Mwasapile

Mussa Juma, Arusha
MAMIA ya wagonjwa kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi, ambao walikuwa wanakwenda kupata matibabu kwa Mchungaji Ambilikile Mwasapile wamekwama njiani kutokana na mvua kubwa iliyonyesha jana na kuharibu barabara.Barabara ya kwenda katika Kijiji cha Samunge aliko mchungaji huyo inayochepukia eneo la Kigongoni na Selela, Engaruka na Ngaresero, sasa haipitiki kutokana na kuharibika.

Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali alisema jana kwamba kuharibika kwa barabara hiyo kumesababisha mamia ya wagonjwa na jamaa zao waliokuwa wakielekea Samunge kukwama porini hivyo kukosa huduma muhimu za kijamii ikiwamo chakula na hata usalama wao. Kutokana na hali hiyo, amekiomba Kitengo cha Maafa cha Ofisi ya Waziri Mkuu, kuingilia kati na kufika eneo hilo kutoa msaada... "Hali ni mbaya sana. Idadi ya watu sasa ni kubwa kuliko kipindi kingine chochote"

Lali aliwataka viongozi wa mikoa inayopakana na wilaya yake kuweka udhibiti wa watu wanaokwenda Samunge kutokana na uharibifu huo wa miundombinu... "Nawaomba wadhibiti watu hadi hawa waliokwama na waliopo Samunge watakapopungua."

Kukwama kwa wagonjwa hao, kumekuja takriban siku tatu tangu, Mchungaji Mwasapile alipoiomba Serikali kuharakisha kukarabati barabara hiyo akihofia kukatisha mawasiliano ya kumfikia.
Magari mbalimbali ya abiria yakiwapo mabasi na mengine madogo ya kukodi yamekwama kati ya Vijiji vya Engaruka na Ngaresero na hivyo kutishia afya za wagonjwa wengi.

Mmoja wa madereva waliofanikiwa kupita katika njia hiyo, Jonathan Mrema alisema Serikali isipokarabati barabara hiyo sasa, wagonjwa wengi watakwama hata kupoteza maisha.

Alisema kutokana na ubovu wa barabara hiyo na hivyo wagonjwa kukaa muda mrefu kabla ya kufika kwa mchungaji huyo, amewashuhudia wanne waliofariki dunia juzi na jana."Watu wanakufa barabarani. Hali ni mbaya sana tunaomba Serikali ikarabati barabara hii japo kwa kiwango cha changarawe," alisema Mrema.

Mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya kukodi magari yanayokwenda Samunge, Saidi Kakiva alisema kutokana na barabara kuharibika nauli zimepanda kwa kiwango kikubwa."Tunaomba Serikali iwajali hawa wagonjwa. Sasa gharama ya usafiri imefikia kati ya Sh120,000 na 150,000 kwenda na kurudi wakati bei ya awali ilikuwa ni kati ya 35,000 na 80,000," alisema Kakiva.

Jijini Arusha, nyumba nyingi za kulala wageni zimejaa wateja wengi wakiwa ni wagonjwa na jamaa zao ambao wanataka kwenda huko Samunge Loliondo kwa Mchungaji Mwasapile.

Baadhi ya wagonjwa kutoka mikoa mbalimbali nchini wamelazimika kuhifadhiwa katika hospitali na vituo binafsi vya afya wakisubiri usafiri wa kwenda Samunge ambao umekuwa mgumu baada ya baadhi ya magari yaliyokuwa yakiwapeleka kusitisha huduma kutokana na ubovu wa barabara.

Tangu kuanza kutolewa kwa tiba hiyo ambayo imewavutia wananchi wengi wakiwemo viongozi waandamizi wa Serikali, wanasiasa, wananchi na watu wa mataifa mbalimbali, kumekuwa na kilio cha huduma za jamii na miundombinu vitu ambavyo vimekuwa vikikwamisha upatikanaji wa huduma hiyo.
 
Wavamia msitu Loliondo kusaka dawa Send to a friend Saturday, 19 March 2011 10:36

mch%20mwaisapile.jpg
Mchungaji Ambilikile Mwasapile akiweka dawa katika vikombe ambavyo husambazwa kwenye magari kwa wagonjwa na wananchi walifika upata tiba katika kijiji cha Samunge, Loliondo, mkoani Arusha. Picha na Mussa Juma

Waandishi Wetu
WAKATI dawa aliyoigundua Mchungaji Ambilikile Mwasapile ikionekana kuwavuta watu karibu nchi nzima kutaka kuinywa, baadhi ya wakazi wa Arusha wameamua kwenda maporini kusaka dawa hiyo.Taarifa ambazo pia zimemfikia mchungaji huyo mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), zimeeleza kuwa watu hao tayari wamevamia pori la mlima Sonjo kuchimba dawa anayotumia kutibu.Hata hivyo, Mchungaji Mwasapile alisema haitawasaidia kwa vyovyote kwa sababu ni yeye pekee aliyepewa uwezo na Mungu ili awaponye watu.

Hata hivyo, Mchungaji Mwasapile, ameiomba Serikali kuingilia kati kwa kuwadhibiti watu hao, aliowaita kuwa ni matapeli ambao tayari wamevamia pori hilo kwa sababu watasababishawatasababisha watu wengine kuikosa kwa vile uchimbaji utakuwa ni wa vurugu na pia utasababisha uharibifu wa mazingira.

Akizungumza na waandishi wa habari, mchungaji huyo alisema watu hao, wamekuwa wakiwatumia baadhi ya vijana wa kijiji cha Samunge ambao wanaujua mti wa Mugariga, au Mungamuryogo na wameanza kuchimba mizizi na kusafirisha nje ya kijiji hicho.

"Naomba nitoe angalizo, hii dawa ni mimi pekee ndiye Mungu ameniotesha kuitoa na inakwenda pamoja na maombi sasa hawa wanachimba mizizi na kwenda kutengeneza haitawasaidia ni utapeli," alisema Mchungaji Mwasapile.

Mchungaji huyo aliiendelea kuiomba Serikali kukarabati miundombinu ya kufika katika kijiji cha Samunge kwa sababu sasa mvua zimeanza kunyesha na kwamba siku si nyingi barabara za kumfikia zitakuwa hazipitiki.
Kutokana na ubovu wa barabara hiyo, gari lililokuwa limembeba Waziri Mkuu Mstaafu lilikwama juzi jirani tu na kwa mchungaji huyo sambamba na magari mengine kadhaa.

Kukwama kwa magari hayo, kulitokana na mvua ambazo zimeanza kunyesha na kuharibu barabara ya kwenda katika kijiji hicho, inayotokea eneo la Kigongoni Mto wa Mbu, kupitia kata za Selela, Engaruka na Ngaresero.
Magari mengi yalikuwa yameharibika na kukwama kati kati ya miti juzi, hali ambayo inatishia usalama wa barabara hiyo ambayo ni ya vumbi.

Akizungumzia barabara hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali, aliwataka madereva kuwa makini ili kuzuia mfululizo wa ajali.

Katika hatua nyingine, Mchungaji Mwasapile alirudia tena onyo lake la kuwataka watu kuacha kuwapeleka kwake wagonjwa waliotoroshwa hospitali huku wengine wakiwa na chupa za kuongezewa maji mwilini.

"Wanakuja huku wakiwa na Dripu za maji. Sasa hapa sio hospitali ya rufani. Wagonjwa waletwe hapa kwa tahadhari kubwa kwanza barabara zetu sio nzuri," alisema Mwasapile.
Idadi ya magari na watu toka ndani na nje ya nchi inaongezeka katika kijiji hicho na sasa kupata dawa mgonjwa inachukuwa kati ya siku mbili hadi tatu.

Mwandishi wa habari hizi juzi alishuhudia wagonjwa toka nchi za Kenya, Zambia, Malawi, Uganda na Afrika Kusini wakiwa wamepanga foleni ya kupata dawa.

Madaktari wa Moshi
Kutoka Moshi, madaktari mbalimbali wameitaka Serikali kuandaa kongamano la wanasayansi kujadili tiba inayotolewa na Mchungaji Mwasapile, ikiwamo kutolewa kwa ripoti za kisayansi za wagonjwa waliopona. Wakizungumza na Mwananchi, madaktari hao wamedai kisayansi haiwezekani kupima dawa inayotokana na imani ya dini, lakini ni vyema wakapatikana wagonjwa wanaodai kupona wakiwa na kumbukumbu za matibabu ya siku za nyuma.

Mmoja wa madaktari bingwa, Profesa Waitoki Nkya, ambaye sasa amestaafu serikalini alisema Taifa bado liko gizani kuhusu ukweli wa nguvu ya dawa hiyo katika kutibu magonjwa sugu ukiwamo Ukimwi, kisukari na saratani.

"Binafsi siamini katika jambo hilo lakini, naishangaa Serikali na vyombo vyake kwamba kweli vimeshindwa kutuambia mgonjwa X wa Ukimwi alikuwa na CD4 200, baada ya kunywa zimeongezeka hadi 1,000?" alijoji.

Profesa Nkya ambaye aliwahi kufanya kazi Hospitali ya Rufaa ya KCMC na kuhamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya kabla ya kustaafu, alisema taifa linaweza kuondokana na giza hilo kwa wataalamu kuthibitisha nguvu ya dawa hiyo.

Profesa Nkya alisema Tanzania kama Taifa haliwezi kuruhusu watu waliokunywa dawa hiyo kujisemea wenyewe kuwa wamepona wakati hakuna hata mmoja anayethubutu kutoa vipimo vya awali na vya sasa kuthibitisha amepona.

Hata hivyo, daktari mmoja ambaye ni mratibu wa Ukimwi kwa zaidi ya miaka 10 sasa, alisema katika suala la Ukimwi bado hajathibitisha nguvu ya dawa hiyo isipokuwa kwa magonjwa ya kisukari na shinikizo la damu (BP).

"Kwa kisukari na BP naweza kusema kuna mafanikio kidogo kwa sababu kuna wagonjwa wetu wa kisukari walikuwa katika hatua ya kudungwa sindano kila siku lakini, sasa wana wiki hawajachoma sindano na wako vizuri," alidai.

Daktari mwandamizi katika Hospitali ya Mkoa Kilimanjaro ya Mawenzi, Dk Issa Mbaga, ambaye alisema anatoa maoni binafsi na sio ya Taasisi yake, alisema tatizo ni waliokunywa dawa kutopima upya kuthibitisha kupona.
"Unajua ni vigumu kupima jambo kiimani kama ilivyo kunywa dawa ya Babu kule Loliondo lakini, hawa waliorudi na kutuambia wanaendelea vizuri kwa nini wasipime upya wakatupa ripoti?" alihoji Dk. Issa.

Wazidi kwenda Loliondo
Wakati huo huo, kitimutimu cha wananchi kutaka kwenda huko kimesikika karibu kila mkoa hapa nchini ila tatizo kubwa ni gharama za usafiri pamoja na chakula.Katika Manispaa ya Shinyanga watu wengi wamejitokeza kwenda kujiandikisha ili waende Loliondo baada ya kupata taarifa kuwa Mbunge wao, Steven Masele amekusudia kuwagharimia usafiri.

Wananchi hao walikusanyika jana kwenye ofsi ya mbunge kujiandikisha na awamu ya kwanza ya kundi la watu hao ilitarajia kuondoaka jana.Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu mbunge huyo alisema kuwa amegharimia safari hiyo bila kujali wanaoenda ni wagonjwa au la.

Hata hivyo, alisema wale wenye uwezo washiriki watapaswa kuchangia kiasi kidogo cha fedha ili kutoa nafasi ya watu wengi wanaomiminika katika ofisi yake ili kujiandikisha kwa safari.

Mwanza nako
Jijini Mwanza nako watu wengi wamesikika wakitaka kupata tiba hiyo miongoni mwao ni wafanyakazi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambao tayari wameanza kuchangishana ili kugharimia safari.

Habari zilizopatikana toka ofisi ya mkuu wa mkoa huo na kuthibitishwa na Ofisa Usafirishaji wa Mkoa, William James zilieleza kwamba wafanyakazi hao wamekusudia kwenda kabla ya kufika mwishoni mwa mwezi huu.

James alisema hadi jana wafanyakazi 26 walikuwa wamejiorodhesha kwenda na kila mmoja tayari amelipa Sh80,000.Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Abbasi Kandoro, alielezea kuwa hahusiki katika mpango huo kwa sababu hiyo ni safari binafsi."Hii siyo suala la ofisi ni wafanyakazi binafsi, ndiyo maana uliponiuliza nilishangaa na kwa vile mimi sikuwepo nilikuwa sijui lolote," alisema Kandoro.

Morogoro nao wamo
Kutoka mkoani Morogoro, inaripotiwa kuwa Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (Wavumo) wamemwomba mbunge wa jimbo la Morogoro Mjini, Aziz Abood kuwapa msaada wa kuweza kufika Loliondo ili kupata dawa ya 'Babu'.Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi za Wavumo, katibu wa kikundihicho, Said Shija alisema kuwa wao nao wamehamasika na dawa hiyo.

Alisema kuwa wao wana imani na dawa hiyo na kwamba kinachowashinda hadi sasa kufika huko Loliondo ni kwamba hawana uwezo na kumudu gharama za usafiri.

Askofu Kakobe
Jijini Dar es Salaam, Askofu wa Kanisa la Full Gospel Fellowship, Zacharia Kakobe, ameendelea kutoa maneno ya shutuma dhidi ya mchungaji Mwasapile.

Hii ni baada ya Mwasapile kusema kwamba anawakaribisha ili kunywa dawa hiyo licha ya kumdharau pamoja na tiba anayoitoa. Kakobe amerusha kombora lingine akidai haendi ng'o na yeye sio nyasi zinazotikiswa na upepo kama watu wengine wanaokwenda huko.

Mwasapile maarufu kwa jina la ‘Babu' aliwajibu viongozi hao waliomtuhumu kuwa tiba anayoitoa ni ya nguvu za giza, akisema kuwa waliotoa tuhuma hizo wana mtazamo wa kifedha zaidi na sio imani.

Akizungumza na gazeti hili jana kwa simu, Askofu Kakobe alisema kwanza anawahurumia wanaoendelea kwenda huko kwa sababu tayari wameshatekwa na huduma hiyo ya 'kitapeli.'

"Siwezi kwenda kunywa dawa hata kidogo, kwa sababu mimi sio nyasi zinazotikiswa na upepo kama wengine waliokwenda huko," alisema Askofu Kakobe.

Ajali Loliondo
Kwa upande mwingine, ajali za magari yanayoenda, au kutoka kwa 'Babu' nazo zinaendelea kuongezeka.
Jumatano iliyopita mtu mmoja alikufa na wengine watano kujeruhiwa baada ya gari lililokuwa njiani kwenda Loliondo kupasuka tairi na kupinduka eneo la Makuyuni, wilayani Monduli.

Ajali hiyo inafanya idadi ya watu waliokufa tokea msururu wa watu toka pembe zote za nchi walipoanza kumimika katika kijiji cha Samunge, Wilayani Ngorongoro kufiki saba.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Akili Mpwapwa alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo. Alisema ajali hiyo ilitokea saa nane mchana kufuatia kupasuka kwa gurudumu la nyuma la gari hilo, kisha kupinduka.
Alimtaja aliyefariki dunia kuwa ni Fatuma Badru (34), mkazi wa Soweto mjini Moshi.

Aliwataja majeruhi kuwa ni Ruth Lyimo, Mary Sembugao na Salma Badru na mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Omary.

Habari hii imeandikwa na Mussa Juma-Loliondo, Daniel Mjema-Moshi, Suzy Butondo-Shinyanga, Frederick Katulanda-Mwanza, Filbert Rweyemamu-Arusha, Lilian Lucas-Morogoro na Elizabeth Suleyman - Dar.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites

Comments

123



0 #31 Alma 2011-03-20 19:26 Mungu ujitukuza kwa njia za pekee bila kujali nani kasema nini. Kakobe ajiitaye mutume wa Mungu nani anahoji utume wake tunangoja Mungu mwenyewe aonyeshe ukweli huo: halazimishwi kwenda kwa babu na wala halazimiki kumzuaia yeyote. Babu kama ni hukumu au baraka tutaviona hapa hapa.
Quote









0 #30 mdomo-wa-chui 2011-03-20 18:04 kakobe ni nani ee bwana mpaka akukere babu. mwisho wa siku najua kakobe atakuja kwako. atakapokuja mpe dawa ili apone ugonjwa sugu alionao wa matunguri. unapomtaja yesu huku unachumba cha siri kanisani unataka kutuambia umemfungia yesu huyo kwenye chumba hicho. ninyi wachungaje uchwara mnawatapeli watu kuwa unawaombea wenye magonjwa sugu. kwa nini anapotokea mtu ambae kakuzidi usikubali na kukubali kuwa anajaribu kwa nafasi yake kama ulivyojaribu? wachungaji aina ya kakobe ni wanafiki na wenye tamaa ya dhahabu na magari kama ambavyo ulikuwa wewe kakobe unanyang'anya dhahabu na funguo za gari za watu waliokufia kwa mbwembwe zako kakoo. WACHA BWANA MAMBO YAKIKUZIDIA KUBALI. HUJALAZIMISHWA NA BABU UMKUBALI.
WANAFIKI WAKUBWA NYIE MAFISADI WA KANISANI.
Quote









0 #29 mawazo dolonyi 2011-03-20 16:23 Quoting Mahmod:
We ulikuwa tapeli. Huna lolote.Quoting mrusi:
:oops: ninasikitika sana kuona mambo yanavyoenda.Kwa elimu yangu ndongo niliokua ninayo naona watu wanapokwenda nipabaya mno na kwakweli tutatengeneza Resistense"usugu wa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI na kupelekea kwa ongezeko la vifo kwa Watu wanaoishi na VVU/UKIMWI.Najua wengi sana watakua wameacha kutumia dawa zao na ilo nikosa kubwa mno ambalo madhara yake yatakuja onekana baadaye.Babu wenda nimnzuri nikikusudia tiba yake yakutumia iyo mizizi,lakini lazma akubali ifanyiwe uchunguzi inatibu magonjwa yapi?Swala lakiimani alipingwi,Mungu kampa binadamu akili yakufikiria,wat u wafikirie.Kinachotakiwa kwanza ni icho,lasivyo fundisho tumepeta,twapen da mno mambo ya Deso.........Mtanikumbuka baadae.mimi nilikua mtaalamu ktk hayo magonjwa sugu moja apo ni mambo ya HIV/AIDS miaka ya nyuma​
Ndugu yangu unasema ukweli mimi binafsi nashangaa kwa nini Serikali mpaka sasa ipo kimya, jamani yaani hata tu kupima wagonjwa ambao wasemekena kupona ili kujuwa ukweli wa mambo haiwezekani! badala yake tunaona viongozi wa nchi wanakwenda huko kimyakimya na usalama wa taifa ukizuia publication. jambo hili lina madhara sana kama unavyosema ila sijuwi itakuwaje maana serikali imekaa kimya utadhani haipo. ona sasa leo wameanza kuvuna miti hovyo kesho wataanza kuwauwa na hao twiga wenyewe maana ndo chakula chao huo mti.
Quote









0 #28 Mahmod 2011-03-20 15:26 We ulikuwa tapeli. Huna lolote.Quoting mrusi:
:oops: ninasikitika sana kuona mambo yanavyoenda.Kwa elimu yangu ndongo niliokua ninayo naona watu wanapokwenda nipabaya mno na kwakweli tutatengeneza Resistense"usugu wa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI na kupelekea kwa ongezeko la vifo kwa Watu wanaoishi na VVU/UKIMWI.Najua wengi sana watakua wameacha kutumia dawa zao na ilo nikosa kubwa mno ambalo madhara yake yatakuja onekana baadaye.Babu wenda nimnzuri nikikusudia tiba yake yakutumia iyo mizizi,lakini lazma akubali ifanyiwe uchunguzi inatibu magonjwa yapi?Swala lakiimani alipingwi,Mungu kampa binadamu akili yakufikiria,wat u wafikirie.Kinachotakiwa kwanza ni icho,lasivyo fundisho tumepeta,twapen da mno mambo ya Deso.........Mtanikumbuka baadae.mimi nilikua mtaalamu ktk hayo magonjwa sugu moja apo ni mambo ya HIV/AIDS miaka ya nyuma​
Quote









0 #27 na mie 2011-03-20 14:28 Quoting mzurimie:
Quoting na mie:
Naomba wanasayansi wauchunguze mti huo, licha ya imani naomba waangalie ni nini kinachofanya wadudu sugu wauawe.
Watakapogundua kama kuna nguvu ya pekee kwenye mti huo basi kampeni zianze kuupanda kama ilivyo muarobaini. Halafu babu naomba umuombe Mungu ili uweze kuwaepoer wachungaji wengine wa mikoani ili tiba hiyo ipatikane kwa urahisi, nadhani Mungu atakubali.​
Wewe Yesu aligeuza maji kuwa wine nini tena unakuwa negative yeye ndie amechaguliwa na bwana na yeye ndie mtoaji nini tena apitishe kwa wenggine je mungu kawachagua

Mtu atakae ukombozi uponyaji etc bila imani haufanikiwi kutatua matatizo na hiyo ndio tabu ya wengi hata katika kuhudhuria makanisani au kusali wenyewe.

Tuombe mungu serikali itengeneze barabara​
Quoting mzurimie:
Quoting na :
Naomba wanasayansi wauchunguze mti huo, licha ya imani naomba waangalie ni nini kinachofanya wadudu sugu wauawe.
Watakapogundua kama kuna nguvu ya pekee kwenye mti huo basi kampeni zianze kuupanda kama ilivyo muarobaini. Halafu babu naomba umuombe Mungu ili uweze kuwaepoer wachungaji wengine wa mikoani ili tiba hiyo ipatikane kwa urahisi, nadhani Mungu atakubali.​
Wewe Yesu aligeuza maji kuwa wine nini tena unakuwa negative yeye ndie amechaguliwa na bwana na yeye ndie mtoaji nini tena apitishe kwa wenggine je mungu kawachagua

Mtu atakae ukombozi uponyaji etc bila imani haufanikiwi kutatua matatizo na hiyo ndio tabu ya wengi hata katika kuhudhuria makanisani au kusali wenyewe.

Tuombe mungu serikali itengeneze barabara​
Nimeangalia fingerprint zako ni mdogo kwa umri nashangaa unavyokuwa na mawazo ya kizee cha miaka 1723. Katika karne ya 15 ulaya na afrika zilikuwa sawa kwa mambo mengi sana na waafrika wengi walikuwa wanatibu magonjwa sugu mengi sana lakini kutokana na ubinafsi wa waafrika hawakuwaambia wengine hivyo wamekufa na mizizi yao.
Tuje kwenye Bible knowledge au divinity kama unaijua. Kabla ya upao wa nabii eliya kwenda juu mungu alimpa maagizo matatu Eliya moja ni kumuweka wakfu Elisha achukue nafasi yake ya unabii.
Tukumbuke kuwa BAbu, Kakobe (ug uban pa)wote watakufa, tutake tusitake.
Huyo mungu ambaye atakataa kumteua mtu mmoja kufuzwa na babu na kupewa nguvu basi huyo ni Mungu wa "giza". Toka awali baada ya peter alisimikwa mwingine hadi leo.Kumbukeni maisha yetu yapo mikononi mwa Mungu akiamua muda wote unaondoka.
Ushauri wa kiroho na kisaikojia Contact. Asia +62 98456321984
Quote









0 #26 Embu 2011-03-20 13:50 Ni kweli, hao wote ni matapeli wapenda pesa (Kakobe, Mwingira, n.k.)ndio maana wanaona miradi yao inadoda. Waacheni watu waende kwa Babu.
Quote









+1 #25 Twaha Lema 2011-03-20 12:04 Hao wanaompinga Babu wanamuonea wivu wanatamani wangeshushiwa wao huo uwezo ili waweze kujiongezea wao kipato coz engine tunawajua ni matapeli tu,BABU NI MWOKOZI WETU TULIYEBARIKIWA NA MUNGUUUUUUUUUUU UUUUUUUUUUUUUUU UUUUUU!
Quote









0 #24 Shuhuda 2011-03-20 11:17 [Mungu asante sama kwa kumleta Mchungaji Mwapesile. Ni kweli baba na mama yangu wamepona kabisa baada ya kuwa kwenye que for 5 days. Baba alikuwa anaumwa kisukari na pressure na Mama alipata stroke yenye maumivu makali miaka mingi. Wapo wanatoa shuhuda kwa watu kila siku, NENDENI. Hivi sh/500 ni nini bwana? kwanza ni dawa za aina ngapi umezilipiaaaa???? na sadaka mafungu mangapi uliyodanganywa kutoa ili Mungu akuone??????? Mungu katupa gifts kwa watumishi zenye nguvu tofauti eg, Mwakasege, Kakobe, Rwakatare, Mwasapile etc.
Ila kama utarudi kwenye kanisa lako la(KAKOBE) angalia wasikutenge. Hapa itabidi usitoe shuhuda!
Wachungaji wanawivu! DUH!!!
Quote









+1 #23 Gaston 2011-03-20 11:17 Babu Mungu akujalie maisha marefuuu!!Achan a kujibizana na Kakobe yeye ni mfanyabiashara! !
Quote









+1 #22 Ya kweli 2011-03-20 11:09 Mungu asant kwa kumleta Mchungaji Mwapesile. Ni kweli baba na mama yangu wameponya. Baba kisukari na pressure na Mama alipata stroke yenye maumivu makali. Wapo wanatoa shuhuda. Hivi sh/500 ni nini? kwanza ni dawa aina ngapi umezilipia na sadaka mafungu mangapi uliyodanganywa kutua??????? Mungu katupa gifts kwa watumishi na zote zimetofau[NENO BAYA] eg, Mwakasege, Kakobe, Rwakatare, Mwasapile etc.Ila kama utarudi kwenye kanisa lako la(KAKOBE) angalia wasikutenge. Hapa itabidi usitoe shuhuda!
Wachungaji wanawivu! DUH!!!!
Quote









+1 #21 nkyandwale 2011-03-20 10:56 Babu kaza kamba kuokoa maisha ya wenye imani, yote wasemayo kwako yawe sawa. Imani kwanza na tiba mbele. Acha malumbano wewe gawa vikombe vya mantindili watu wapone.Mungu akujalie hekima na afya tele.
Quote









0 #20 ibwe 2011-03-20 10:15 Quoting DESRE:
BABU ONDOA HOFU MUNGU SIO WA PEKE YAKO NA HAO PIA WAMEOTESHWA PIA
KAAZI KWELI KWELI TZ​
BABU hajiamini. ana uhakika gan kuwa hawatafanikiwa
Quote









0 #19 CAROLINE 2011-03-20 09:44 WAZIRI WA AFYA NENDA KACHIMBE VYOO KULE LOLIONDO ACHANA NA UMBEA. WATU WAKIFA NA KIPINDU PINDU UJIUZULU WEWE MWENYEWE USINGOJE BAKORA.MNAACHA WATU WA NJE WANACHUKUA MIKANDA YA VIDEO JUU YA VINYESE.
MSIDHANI USTAARABU NI KUVAA SUTI PEKE YAKE NA USAFI PIA MUHIMU.
Quote









0 #18 LENGAI 2011-03-20 09:40 PILIPILI MSIYOILA INAWASHIA NINI BABU TOA DOZI WACHA WENYE MIDOMO INANUKA WAENDELEZE UMBEA WAO. KAMA HUPENDI DOZI UNAONGELEA DOZI YA NINI NA NYIE NI WAVAA MATUNGURI HUKU MNAJIITA WACHUNGAJI, NA MASHEHE KWENDENI ZENU.BABU PIGA KAZI!
Quote









+1 #17 simon 2011-03-20 09:24 Babu wewe toa dozi mpaka kieleweke,wasio penda wajinyonge tena wapotezee.
Quote







123
Refresh comments list
 
Wavamia msitu Loliondo kusaka dawa Send to a friend Saturday, 19 March 2011 10:36

mch%20mwaisapile.jpg
Mchungaji Ambilikile Mwasapile akiweka dawa katika vikombe ambavyo husambazwa kwenye magari kwa wagonjwa na wananchi walifika upata tiba katika kijiji cha Samunge, Loliondo, mkoani Arusha. Picha na Mussa Juma

Waandishi Wetu
WAKATI dawa aliyoigundua Mchungaji Ambilikile Mwasapile ikionekana kuwavuta watu karibu nchi nzima kutaka kuinywa, baadhi ya wakazi wa Arusha wameamua kwenda maporini kusaka dawa hiyo.Taarifa ambazo pia zimemfikia mchungaji huyo mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), zimeeleza kuwa watu hao tayari wamevamia pori la mlima Sonjo kuchimba dawa anayotumia kutibu.Hata hivyo, Mchungaji Mwasapile alisema haitawasaidia kwa vyovyote kwa sababu ni yeye pekee aliyepewa uwezo na Mungu ili awaponye watu.

Hata hivyo, Mchungaji Mwasapile, ameiomba Serikali kuingilia kati kwa kuwadhibiti watu hao, aliowaita kuwa ni matapeli ambao tayari wamevamia pori hilo kwa sababu watasababishawatasababisha watu wengine kuikosa kwa vile uchimbaji utakuwa ni wa vurugu na pia utasababisha uharibifu wa mazingira.

Akizungumza na waandishi wa habari, mchungaji huyo alisema watu hao, wamekuwa wakiwatumia baadhi ya vijana wa kijiji cha Samunge ambao wanaujua mti wa Mugariga, au Mungamuryogo na wameanza kuchimba mizizi na kusafirisha nje ya kijiji hicho.

"Naomba nitoe angalizo, hii dawa ni mimi pekee ndiye Mungu ameniotesha kuitoa na inakwenda pamoja na maombi sasa hawa wanachimba mizizi na kwenda kutengeneza haitawasaidia ni utapeli," alisema Mchungaji Mwasapile.

Mchungaji huyo aliiendelea kuiomba Serikali kukarabati miundombinu ya kufika katika kijiji cha Samunge kwa sababu sasa mvua zimeanza kunyesha na kwamba siku si nyingi barabara za kumfikia zitakuwa hazipitiki.
Kutokana na ubovu wa barabara hiyo, gari lililokuwa limembeba Waziri Mkuu Mstaafu lilikwama juzi jirani tu na kwa mchungaji huyo sambamba na magari mengine kadhaa.

Kukwama kwa magari hayo, kulitokana na mvua ambazo zimeanza kunyesha na kuharibu barabara ya kwenda katika kijiji hicho, inayotokea eneo la Kigongoni Mto wa Mbu, kupitia kata za Selela, Engaruka na Ngaresero.
Magari mengi yalikuwa yameharibika na kukwama kati kati ya miti juzi, hali ambayo inatishia usalama wa barabara hiyo ambayo ni ya vumbi.

Akizungumzia barabara hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali, aliwataka madereva kuwa makini ili kuzuia mfululizo wa ajali.

Katika hatua nyingine, Mchungaji Mwasapile alirudia tena onyo lake la kuwataka watu kuacha kuwapeleka kwake wagonjwa waliotoroshwa hospitali huku wengine wakiwa na chupa za kuongezewa maji mwilini.

"Wanakuja huku wakiwa na Dripu za maji. Sasa hapa sio hospitali ya rufani. Wagonjwa waletwe hapa kwa tahadhari kubwa kwanza barabara zetu sio nzuri," alisema Mwasapile.
Idadi ya magari na watu toka ndani na nje ya nchi inaongezeka katika kijiji hicho na sasa kupata dawa mgonjwa inachukuwa kati ya siku mbili hadi tatu.

Mwandishi wa habari hizi juzi alishuhudia wagonjwa toka nchi za Kenya, Zambia, Malawi, Uganda na Afrika Kusini wakiwa wamepanga foleni ya kupata dawa.

Madaktari wa Moshi
Kutoka Moshi, madaktari mbalimbali wameitaka Serikali kuandaa kongamano la wanasayansi kujadili tiba inayotolewa na Mchungaji Mwasapile, ikiwamo kutolewa kwa ripoti za kisayansi za wagonjwa waliopona. Wakizungumza na Mwananchi, madaktari hao wamedai kisayansi haiwezekani kupima dawa inayotokana na imani ya dini, lakini ni vyema wakapatikana wagonjwa wanaodai kupona wakiwa na kumbukumbu za matibabu ya siku za nyuma.

Mmoja wa madaktari bingwa, Profesa Waitoki Nkya, ambaye sasa amestaafu serikalini alisema Taifa bado liko gizani kuhusu ukweli wa nguvu ya dawa hiyo katika kutibu magonjwa sugu ukiwamo Ukimwi, kisukari na saratani.

“Binafsi siamini katika jambo hilo lakini, naishangaa Serikali na vyombo vyake kwamba kweli vimeshindwa kutuambia mgonjwa X wa Ukimwi alikuwa na CD4 200, baada ya kunywa zimeongezeka hadi 1,000?” alijoji.

Profesa Nkya ambaye aliwahi kufanya kazi Hospitali ya Rufaa ya KCMC na kuhamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya kabla ya kustaafu, alisema taifa linaweza kuondokana na giza hilo kwa wataalamu kuthibitisha nguvu ya dawa hiyo.

Profesa Nkya alisema Tanzania kama Taifa haliwezi kuruhusu watu waliokunywa dawa hiyo kujisemea wenyewe kuwa wamepona wakati hakuna hata mmoja anayethubutu kutoa vipimo vya awali na vya sasa kuthibitisha amepona.

Hata hivyo, daktari mmoja ambaye ni mratibu wa Ukimwi kwa zaidi ya miaka 10 sasa, alisema katika suala la Ukimwi bado hajathibitisha nguvu ya dawa hiyo isipokuwa kwa magonjwa ya kisukari na shinikizo la damu (BP).

“Kwa kisukari na BP naweza kusema kuna mafanikio kidogo kwa sababu kuna wagonjwa wetu wa kisukari walikuwa katika hatua ya kudungwa sindano kila siku lakini, sasa wana wiki hawajachoma sindano na wako vizuri,” alidai.

Daktari mwandamizi katika Hospitali ya Mkoa Kilimanjaro ya Mawenzi, Dk Issa Mbaga, ambaye alisema anatoa maoni binafsi na sio ya Taasisi yake, alisema tatizo ni waliokunywa dawa kutopima upya kuthibitisha kupona.
“Unajua ni vigumu kupima jambo kiimani kama ilivyo kunywa dawa ya Babu kule Loliondo lakini, hawa waliorudi na kutuambia wanaendelea vizuri kwa nini wasipime upya wakatupa ripoti?” alihoji Dk. Issa.

Wazidi kwenda Loliondo
Wakati huo huo, kitimutimu cha wananchi kutaka kwenda huko kimesikika karibu kila mkoa hapa nchini ila tatizo kubwa ni gharama za usafiri pamoja na chakula.Katika Manispaa ya Shinyanga watu wengi wamejitokeza kwenda kujiandikisha ili waende Loliondo baada ya kupata taarifa kuwa Mbunge wao, Steven Masele amekusudia kuwagharimia usafiri.

Wananchi hao walikusanyika jana kwenye ofsi ya mbunge kujiandikisha na awamu ya kwanza ya kundi la watu hao ilitarajia kuondoaka jana.Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu mbunge huyo alisema kuwa amegharimia safari hiyo bila kujali wanaoenda ni wagonjwa au la.

Hata hivyo, alisema wale wenye uwezo washiriki watapaswa kuchangia kiasi kidogo cha fedha ili kutoa nafasi ya watu wengi wanaomiminika katika ofisi yake ili kujiandikisha kwa safari.

Mwanza nako
Jijini Mwanza nako watu wengi wamesikika wakitaka kupata tiba hiyo miongoni mwao ni wafanyakazi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambao tayari wameanza kuchangishana ili kugharimia safari.

Habari zilizopatikana toka ofisi ya mkuu wa mkoa huo na kuthibitishwa na Ofisa Usafirishaji wa Mkoa, William James zilieleza kwamba wafanyakazi hao wamekusudia kwenda kabla ya kufika mwishoni mwa mwezi huu.

James alisema hadi jana wafanyakazi 26 walikuwa wamejiorodhesha kwenda na kila mmoja tayari amelipa Sh80,000.Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Abbasi Kandoro, alielezea kuwa hahusiki katika mpango huo kwa sababu hiyo ni safari binafsi.“Hii siyo suala la ofisi ni wafanyakazi binafsi, ndiyo maana uliponiuliza nilishangaa na kwa vile mimi sikuwepo nilikuwa sijui lolote," alisema Kandoro.

Morogoro nao wamo
Kutoka mkoani Morogoro, inaripotiwa kuwa Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (Wavumo) wamemwomba mbunge wa jimbo la Morogoro Mjini, Aziz Abood kuwapa msaada wa kuweza kufika Loliondo ili kupata dawa ya 'Babu'.Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi za Wavumo, katibu wa kikundihicho, Said Shija alisema kuwa wao nao wamehamasika na dawa hiyo.

Alisema kuwa wao wana imani na dawa hiyo na kwamba kinachowashinda hadi sasa kufika huko Loliondo ni kwamba hawana uwezo na kumudu gharama za usafiri.

Askofu Kakobe
Jijini Dar es Salaam, Askofu wa Kanisa la Full Gospel Fellowship, Zacharia Kakobe, ameendelea kutoa maneno ya shutuma dhidi ya mchungaji Mwasapile.

Hii ni baada ya Mwasapile kusema kwamba anawakaribisha ili kunywa dawa hiyo licha ya kumdharau pamoja na tiba anayoitoa. Kakobe amerusha kombora lingine akidai haendi ng’o na yeye sio nyasi zinazotikiswa na upepo kama watu wengine wanaokwenda huko.

Mwasapile maarufu kwa jina la ‘Babu’ aliwajibu viongozi hao waliomtuhumu kuwa tiba anayoitoa ni ya nguvu za giza, akisema kuwa waliotoa tuhuma hizo wana mtazamo wa kifedha zaidi na sio imani.

Akizungumza na gazeti hili jana kwa simu, Askofu Kakobe alisema kwanza anawahurumia wanaoendelea kwenda huko kwa sababu tayari wameshatekwa na huduma hiyo ya 'kitapeli.'

“Siwezi kwenda kunywa dawa hata kidogo, kwa sababu mimi sio nyasi zinazotikiswa na upepo kama wengine waliokwenda huko,” alisema Askofu Kakobe.

Ajali Loliondo
Kwa upande mwingine, ajali za magari yanayoenda, au kutoka kwa 'Babu' nazo zinaendelea kuongezeka.
Jumatano iliyopita mtu mmoja alikufa na wengine watano kujeruhiwa baada ya gari lililokuwa njiani kwenda Loliondo kupasuka tairi na kupinduka eneo la Makuyuni, wilayani Monduli.

Ajali hiyo inafanya idadi ya watu waliokufa tokea msururu wa watu toka pembe zote za nchi walipoanza kumimika katika kijiji cha Samunge, Wilayani Ngorongoro kufiki saba.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Akili Mpwapwa alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo. Alisema ajali hiyo ilitokea saa nane mchana kufuatia kupasuka kwa gurudumu la nyuma la gari hilo, kisha kupinduka.
Alimtaja aliyefariki dunia kuwa ni Fatuma Badru (34), mkazi wa Soweto mjini Moshi.

Aliwataja majeruhi kuwa ni Ruth Lyimo, Mary Sembugao na Salma Badru na mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Omary.

Habari hii imeandikwa na Mussa Juma-Loliondo, Daniel Mjema-Moshi, Suzy Butondo-Shinyanga, Frederick Katulanda-Mwanza, Filbert Rweyemamu-Arusha, Lilian Lucas-Morogoro na Elizabeth Suleyman - Dar.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites

Comments

123



0 #31 Alma 2011-03-20 19:26 Mungu ujitukuza kwa njia za pekee bila kujali nani kasema nini. Kakobe ajiitaye mutume wa Mungu nani anahoji utume wake tunangoja Mungu mwenyewe aonyeshe ukweli huo: halazimishwi kwenda kwa babu na wala halazimiki kumzuaia yeyote. Babu kama ni hukumu au baraka tutaviona hapa hapa.
Quote









0 #30 mdomo-wa-chui 2011-03-20 18:04 kakobe ni nani ee bwana mpaka akukere babu. mwisho wa siku najua kakobe atakuja kwako. atakapokuja mpe dawa ili apone ugonjwa sugu alionao wa matunguri. unapomtaja yesu huku unachumba cha siri kanisani unataka kutuambia umemfungia yesu huyo kwenye chumba hicho. ninyi wachungaje uchwara mnawatapeli watu kuwa unawaombea wenye magonjwa sugu. kwa nini anapotokea mtu ambae kakuzidi usikubali na kukubali kuwa anajaribu kwa nafasi yake kama ulivyojaribu? wachungaji aina ya kakobe ni wanafiki na wenye tamaa ya dhahabu na magari kama ambavyo ulikuwa wewe kakobe unanyang'anya dhahabu na funguo za gari za watu waliokufia kwa mbwembwe zako kakoo. WACHA BWANA MAMBO YAKIKUZIDIA KUBALI. HUJALAZIMISHWA NA BABU UMKUBALI.
WANAFIKI WAKUBWA NYIE MAFISADI WA KANISANI.
Quote









0 #29 mawazo dolonyi 2011-03-20 16:23 Quoting Mahmod:
We ulikuwa tapeli. Huna lolote.Quoting mrusi:
:oops: ninasikitika sana kuona mambo yanavyoenda.Kwa elimu yangu ndongo niliokua ninayo naona watu wanapokwenda nipabaya mno na kwakweli tutatengeneza Resistense"usugu wa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI na kupelekea kwa ongezeko la vifo kwa Watu wanaoishi na VVU/UKIMWI.Najua wengi sana watakua wameacha kutumia dawa zao na ilo nikosa kubwa mno ambalo madhara yake yatakuja onekana baadaye.Babu wenda nimnzuri nikikusudia tiba yake yakutumia iyo mizizi,lakini lazma akubali ifanyiwe uchunguzi inatibu magonjwa yapi?Swala lakiimani alipingwi,Mungu kampa binadamu akili yakufikiria,wat u wafikirie.Kinachotakiwa kwanza ni icho,lasivyo fundisho tumepeta,twapen da mno mambo ya Deso.........Mtanikumbuka baadae.mimi nilikua mtaalamu ktk hayo magonjwa sugu moja apo ni mambo ya HIV/AIDS miaka ya nyuma​
Ndugu yangu unasema ukweli mimi binafsi nashangaa kwa nini Serikali mpaka sasa ipo kimya, jamani yaani hata tu kupima wagonjwa ambao wasemekena kupona ili kujuwa ukweli wa mambo haiwezekani! badala yake tunaona viongozi wa nchi wanakwenda huko kimyakimya na usalama wa taifa ukizuia publication. jambo hili lina madhara sana kama unavyosema ila sijuwi itakuwaje maana serikali imekaa kimya utadhani haipo. ona sasa leo wameanza kuvuna miti hovyo kesho wataanza kuwauwa na hao twiga wenyewe maana ndo chakula chao huo mti.
Quote









0 #28 Mahmod 2011-03-20 15:26 We ulikuwa tapeli. Huna lolote.Quoting mrusi:
:oops: ninasikitika sana kuona mambo yanavyoenda.Kwa elimu yangu ndongo niliokua ninayo naona watu wanapokwenda nipabaya mno na kwakweli tutatengeneza Resistense"usugu wa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI na kupelekea kwa ongezeko la vifo kwa Watu wanaoishi na VVU/UKIMWI.Najua wengi sana watakua wameacha kutumia dawa zao na ilo nikosa kubwa mno ambalo madhara yake yatakuja onekana baadaye.Babu wenda nimnzuri nikikusudia tiba yake yakutumia iyo mizizi,lakini lazma akubali ifanyiwe uchunguzi inatibu magonjwa yapi?Swala lakiimani alipingwi,Mungu kampa binadamu akili yakufikiria,wat u wafikirie.Kinachotakiwa kwanza ni icho,lasivyo fundisho tumepeta,twapen da mno mambo ya Deso.........Mtanikumbuka baadae.mimi nilikua mtaalamu ktk hayo magonjwa sugu moja apo ni mambo ya HIV/AIDS miaka ya nyuma​
Quote









0 #27 na mie 2011-03-20 14:28 Quoting mzurimie:
Quoting na mie:
Naomba wanasayansi wauchunguze mti huo, licha ya imani naomba waangalie ni nini kinachofanya wadudu sugu wauawe.
Watakapogundua kama kuna nguvu ya pekee kwenye mti huo basi kampeni zianze kuupanda kama ilivyo muarobaini. Halafu babu naomba umuombe Mungu ili uweze kuwaepoer wachungaji wengine wa mikoani ili tiba hiyo ipatikane kwa urahisi, nadhani Mungu atakubali.​
Wewe Yesu aligeuza maji kuwa wine nini tena unakuwa negative yeye ndie amechaguliwa na bwana na yeye ndie mtoaji nini tena apitishe kwa wenggine je mungu kawachagua

Mtu atakae ukombozi uponyaji etc bila imani haufanikiwi kutatua matatizo na hiyo ndio tabu ya wengi hata katika kuhudhuria makanisani au kusali wenyewe.

Tuombe mungu serikali itengeneze barabara​
Quoting mzurimie:
Quoting na :
Naomba wanasayansi wauchunguze mti huo, licha ya imani naomba waangalie ni nini kinachofanya wadudu sugu wauawe.
Watakapogundua kama kuna nguvu ya pekee kwenye mti huo basi kampeni zianze kuupanda kama ilivyo muarobaini. Halafu babu naomba umuombe Mungu ili uweze kuwaepoer wachungaji wengine wa mikoani ili tiba hiyo ipatikane kwa urahisi, nadhani Mungu atakubali.​
Wewe Yesu aligeuza maji kuwa wine nini tena unakuwa negative yeye ndie amechaguliwa na bwana na yeye ndie mtoaji nini tena apitishe kwa wenggine je mungu kawachagua

Mtu atakae ukombozi uponyaji etc bila imani haufanikiwi kutatua matatizo na hiyo ndio tabu ya wengi hata katika kuhudhuria makanisani au kusali wenyewe.

Tuombe mungu serikali itengeneze barabara​
Nimeangalia fingerprint zako ni mdogo kwa umri nashangaa unavyokuwa na mawazo ya kizee cha miaka 1723. Katika karne ya 15 ulaya na afrika zilikuwa sawa kwa mambo mengi sana na waafrika wengi walikuwa wanatibu magonjwa sugu mengi sana lakini kutokana na ubinafsi wa waafrika hawakuwaambia wengine hivyo wamekufa na mizizi yao.
Tuje kwenye Bible knowledge au divinity kama unaijua. Kabla ya upao wa nabii eliya kwenda juu mungu alimpa maagizo matatu Eliya moja ni kumuweka wakfu Elisha achukue nafasi yake ya unabii.
Tukumbuke kuwa BAbu, Kakobe (ug uban pa)wote watakufa, tutake tusitake.
Huyo mungu ambaye atakataa kumteua mtu mmoja kufuzwa na babu na kupewa nguvu basi huyo ni Mungu wa "giza". Toka awali baada ya peter alisimikwa mwingine hadi leo.Kumbukeni maisha yetu yapo mikononi mwa Mungu akiamua muda wote unaondoka.
Ushauri wa kiroho na kisaikojia Contact. Asia +62 98456321984
Quote









0 #26 Embu 2011-03-20 13:50 Ni kweli, hao wote ni matapeli wapenda pesa (Kakobe, Mwingira, n.k.)ndio maana wanaona miradi yao inadoda. Waacheni watu waende kwa Babu.
Quote









+1 #25 Twaha Lema 2011-03-20 12:04 Hao wanaompinga Babu wanamuonea wivu wanatamani wangeshushiwa wao huo uwezo ili waweze kujiongezea wao kipato coz engine tunawajua ni matapeli tu,BABU NI MWOKOZI WETU TULIYEBARIKIWA NA MUNGUUUUUUUUUUU UUUUUUUUUUUUUUU UUUUUU!
Quote









0 #24 Shuhuda 2011-03-20 11:17 [Mungu asante sama kwa kumleta Mchungaji Mwapesile. Ni kweli baba na mama yangu wamepona kabisa baada ya kuwa kwenye que for 5 days. Baba alikuwa anaumwa kisukari na pressure na Mama alipata stroke yenye maumivu makali miaka mingi. Wapo wanatoa shuhuda kwa watu kila siku, NENDENI. Hivi sh/500 ni nini bwana? kwanza ni dawa za aina ngapi umezilipiaaaa???? na sadaka mafungu mangapi uliyodanganywa kutoa ili Mungu akuone??????? Mungu katupa gifts kwa watumishi zenye nguvu tofauti eg, Mwakasege, Kakobe, Rwakatare, Mwasapile etc.
Ila kama utarudi kwenye kanisa lako la(KAKOBE) angalia wasikutenge. Hapa itabidi usitoe shuhuda!
Wachungaji wanawivu! DUH!!!
Quote









+1 #23 Gaston 2011-03-20 11:17 Babu Mungu akujalie maisha marefuuu!!Achan a kujibizana na Kakobe yeye ni mfanyabiashara! !
Quote









+1 #22 Ya kweli 2011-03-20 11:09 Mungu asant kwa kumleta Mchungaji Mwapesile. Ni kweli baba na mama yangu wameponya. Baba kisukari na pressure na Mama alipata stroke yenye maumivu makali. Wapo wanatoa shuhuda. Hivi sh/500 ni nini? kwanza ni dawa aina ngapi umezilipia na sadaka mafungu mangapi uliyodanganywa kutua??????? Mungu katupa gifts kwa watumishi na zote zimetofau[NENO BAYA] eg, Mwakasege, Kakobe, Rwakatare, Mwasapile etc.Ila kama utarudi kwenye kanisa lako la(KAKOBE) angalia wasikutenge. Hapa itabidi usitoe shuhuda!
Wachungaji wanawivu! DUH!!!!
Quote









+1 #21 nkyandwale 2011-03-20 10:56 Babu kaza kamba kuokoa maisha ya wenye imani, yote wasemayo kwako yawe sawa. Imani kwanza na tiba mbele. Acha malumbano wewe gawa vikombe vya mantindili watu wapone.Mungu akujalie hekima na afya tele.
Quote









0 #20 ibwe 2011-03-20 10:15 Quoting DESRE:
BABU ONDOA HOFU MUNGU SIO WA PEKE YAKO NA HAO PIA WAMEOTESHWA PIA
KAAZI KWELI KWELI TZ​
BABU hajiamini. ana uhakika gan kuwa hawatafanikiwa
Quote









0 #19 CAROLINE 2011-03-20 09:44 WAZIRI WA AFYA NENDA KACHIMBE VYOO KULE LOLIONDO ACHANA NA UMBEA. WATU WAKIFA NA KIPINDU PINDU UJIUZULU WEWE MWENYEWE USINGOJE BAKORA.MNAACHA WATU WA NJE WANACHUKUA MIKANDA YA VIDEO JUU YA VINYESE.
MSIDHANI USTAARABU NI KUVAA SUTI PEKE YAKE NA USAFI PIA MUHIMU.
Quote









0 #18 LENGAI 2011-03-20 09:40 PILIPILI MSIYOILA INAWASHIA NINI BABU TOA DOZI WACHA WENYE MIDOMO INANUKA WAENDELEZE UMBEA WAO. KAMA HUPENDI DOZI UNAONGELEA DOZI YA NINI NA NYIE NI WAVAA MATUNGURI HUKU MNAJIITA WACHUNGAJI, NA MASHEHE KWENDENI ZENU.BABU PIGA KAZI!
Quote









+1 #17 simon 2011-03-20 09:24 Babu wewe toa dozi mpaka kieleweke,wasio penda wajinyonge tena wapotezee.
Quote







123
Refresh comments list
 
Tatizo la kukariri maandiko bila kuchanganua maana yake ndiyo imekupelekea kuandika UPUPU HUU!
Unaonekana kabisa una matatizo ya akili, nakushauri ukanywe kikombe cha babu ndio utapata ufahamu wa kuandika maada yako kwa usahihi.


Babu wa Loliondo ni mganga wa kienyeji tu kama Sheikh Yahaya hakutumwa na Mungu.
 
Wakati ni mwamuzi mzuri sana wa haya mambo!!! Tutaifahamu kweli na hiyo kweli itatuweka huru.
 
Ukienda kwa babu, hata maandiko utashindwa kuyaelewa! Huo mti unaozungumzwa katika Ufunuo 22 ni mti unaozaa matunda aina 12 na haupo sasa duniani. Utakuwepo wakati wa utawala wa Yesu. Huo mti wa Loliondo una sumu. Usiulinganishe mti wa uzima na mti wa Loliondo.
Na kama babu anataka kufuata nyayo za Yesu kwa kuponya kwa tope, si atumie tope basi? matope ni mengi Loliondo kuliko huo mti. Isitoshe anaharibu mazingira kwa kukata miti ya kuni za kuchemshia hiyo dawa!

Ha ha ha,mediaman nshakuelewa vizuri ww ni mtu wa namna gani!!Mungu ni muweza na Babu hajasema anafuata nyayo za Yesu, nilikupa mfano wa tope ili ujue mti nizaidi ya tope! Kuna mifano mingi sana kweny biblia,pia wengine waliambiwa wakajitose baharin mara saba watapona kikubwa ni IMANI na NENO (MAOMBI),leo hii Babu anakupa kkombe na maombi, wapi ametofautiana na Biblia? Ndio maana nlikuambia umekariri mistari ila ungekua una general knowledge ya Bible ungeelewa wat i mean 2u!! Ushauri wangu kwako 'Fanya maombi,jinyenyekeze kwa Mungu,usijione mjuaji then soma Bible'
 
Ukienda kwa babu, hata maandiko utashindwa kuyaelewa! Huo mti unaozungumzwa katika Ufunuo 22 ni mti unaozaa matunda aina 12 na haupo sasa duniani. Utakuwepo wakati wa utawala wa Yesu. Huo mti wa Loliondo una sumu. Usiulinganishe mti wa uzima na mti wa Loliondo.
Na kama babu anataka kufuata nyayo za Yesu kwa kuponya kwa tope, si atumie tope basi? matope ni mengi Loliondo kuliko huo mti. Isitoshe anaharibu mazingira kwa kukata miti ya kuni za kuchemshia hiyo dawa!

Ha ha ha,mediaman nshakuelewa vizuri ww ni mtu wa namna gani!!Mungu ni muweza na Babu hajasema anafuata nyayo za Yesu, nilikupa mfano wa tope ili ujue mti nizaidi ya tope! Kuna mifano mingi sana kweny biblia,pia wengine waliambiwa wakajitose baharin mara saba watapona kikubwa ni IMANI na NENO (MAOMBI),leo hii Babu anakupa kkombe na maombi, wapi ametofautiana na Biblia? Ndio maana nlikuambia umekariri mistari ila ungekua una general knowledge ya Bible ungeelewa wat i mean 2u!! Ushauri wangu kwako 'Fanya maombi,jinyenyekeze kwa Mungu,usijione mjuaji then soma Bible'
 
Totally Poor Arguments. Point zako (1 hadi mwisho) zote ni WRONG. Tumia maandiko vizuri si kwa kumpingia mtu ati kwa sababu mmetofautiana naye dini.
Sina uhakika na babu, ila nina uhakika arguments zako sio sahihi, umecreate akilini ndo ukaanza kutafuta maandiko. So weak arguments, I repeat!
1: Sio lazima Mungu ampe dawa ya magonjwa yote. Huduma tunafanya kwa sehemu, yeye akipewa ashughulike na manne hiyo ndo portion yake. That's biblical!
2: Yap, ni yeye tu ndo amepewa hiyo neema. Nini kinakupa shaka? Wewe kivuli chako kinaponya magonjwa kama Petro? Usichanganye kila anachofanya mkristo ukakiita ishara, nyingine ni specific assignment kwa kila mtu individually.
3: kwani wagonjwa wote wanaoponywa wamewekewa mikono? That spoken by Jesus was ONE way, Not the ONLY way. Mbona huongelei wanaotumia vitambaa, waliotumia vivuli, walioambiwa wakanawe Siloamu n.k. Yawezekana kunywa ni hatua tu ya imani.
4: DAWA haiuzwi! Nafikiri unaijua hiyo distribution vizuri. Allocate hiyo pesa kwa individual units, utagundua ni sadaka. Hakuna pesa kwa ajili yake na dawa anayotoa.
5: Babu amewaonya, wasitende dhambi tena la sivyo dawa haitaweza tenda kazi tena. Ulitaka agawe dawa na kuhubiri kwa wakati mmoja? Unajua jinsi anavyochoka? Wewe unaeweza kuhubiri zaidi nenda kasaidie palipobakia. Tunafanya kwa sehemu!
6: kama yule jemedari aliponeshwa kwa imani kwa nn aliambiwa akaoge mara saba?
7: It's just an instruction. Mungu ameipa nguvu dawa akiitoa yeye, ukiondoka nayo ni kinyume na instructions. Kwani hukumbuki sadaka ya Sauli baada ya kushinda vita ilileta laana na si baraka kama sadaka nyingine? God wants u to follow instructions, not questioning his wisdom.
8:unataka apokee nyumba na magari, au unataka afanye kazi yake? Hili wala silijibu ni la kipuuzi zaidi.
9: Rejea, dawa inatibu kwa imani. Kupona nusu au robo ni kazi ya mwamini si ya babu tena.
10: kama alisababisha vifo kwa kuchelewa kuitika, SIO KAZI YAKO KUHUKUMU. Kama Mungu ameshamruhusu kuendelea yatosha wewe kujua hilo.
Sijatoa biblical reference maana najua unajua biblia na kilichopo ndani yake unakitambua.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom