Kila ukiuliza Watanzania 10 nini kinachowaumiza kichwa, 8 kati yao watakuambia changamoto za maisha ni jinamizi linalotesa familia, mahusiano, urafiki na hata taaluma zao.
Wengi wanaishi na swali lini mambo yatakua sawa? au wapi ninafeli?
Kutafuta jibu hilo -wengine wameamua kukimbia familia zao, wengine wanashinda kwa manabii na mitume- wakiongeza upako na kukanyaga mafuta ili kuvunja nira na uchawi, wengine kutwa kuvunja nazi njia panda na kuchomewa hubani kwa mashekhe- ili kuvunja mikosi na laana, wengine wamezama kwenye ulaibu wa pombe na madawa ili tu kujipa fursa za kusahau shida na matatizo yao.
Yote haya ni kuonyesha kuwa hakuna jibu la moja kwa moja juu ya swali hili la lini mambo yatajipa.
Napenda ufahamu hili ni fumbo la maisha. Hata waliofanikiwa wengi ukiwaeleza nini special walifanya ili kufanikiwa Unaweza shangazwa na majibu ya wengi wakikuambia Kuna U-turn moja ilitokea bila kutarajia ikabadiri upepo kabisaa. Mchongo , au fursa moja ilitokea from no where ika change game kabisaaaaa.
Fumbo hili sio ruksa ya kubweteka na kutokimbizana na fursa. Daima do your best, weka mipango, Jenga uwezo na ujuzi, pambana na wala usikate tamaa, na zaidi ya yote ishi kwa matumaini chanya.
Kuna usemi mmoja husema fursa huwapata waliojiaandaa.
Wakuu ebu tujengane - nini kilikutoa kimaisha? Na je, ulikikusudia au ndo zali la mentali?
Wengi wanaishi na swali lini mambo yatakua sawa? au wapi ninafeli?
Kutafuta jibu hilo -wengine wameamua kukimbia familia zao, wengine wanashinda kwa manabii na mitume- wakiongeza upako na kukanyaga mafuta ili kuvunja nira na uchawi, wengine kutwa kuvunja nazi njia panda na kuchomewa hubani kwa mashekhe- ili kuvunja mikosi na laana, wengine wamezama kwenye ulaibu wa pombe na madawa ili tu kujipa fursa za kusahau shida na matatizo yao.
Yote haya ni kuonyesha kuwa hakuna jibu la moja kwa moja juu ya swali hili la lini mambo yatajipa.
Napenda ufahamu hili ni fumbo la maisha. Hata waliofanikiwa wengi ukiwaeleza nini special walifanya ili kufanikiwa Unaweza shangazwa na majibu ya wengi wakikuambia Kuna U-turn moja ilitokea bila kutarajia ikabadiri upepo kabisaa. Mchongo , au fursa moja ilitokea from no where ika change game kabisaaaaa.
Fumbo hili sio ruksa ya kubweteka na kutokimbizana na fursa. Daima do your best, weka mipango, Jenga uwezo na ujuzi, pambana na wala usikate tamaa, na zaidi ya yote ishi kwa matumaini chanya.
Kuna usemi mmoja husema fursa huwapata waliojiaandaa.
Wakuu ebu tujengane - nini kilikutoa kimaisha? Na je, ulikikusudia au ndo zali la mentali?