Josh Michael
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,523
- 77
MKAKATI wa kuwadhoofisha kisiasa baadhi ya wabunge waliojipambanua kuwa wapambanaji wa vita ya ufisadi ambayo imekigawa Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na Bunge umebainika.
Wabunge walioandaliwa mkakati huo ni Christopher ole Sendeka (Simanjiro), Samuel Sitta (Urambo), Fred Mpendazoe (Kishapu) Lucas Selelii (Nzega), James Lembeli (Kahama) Anna Kilango Malecela (Same Mashariki) na Dk. Harisson Mwakyembe (Kyela).
Tanzania Daima Jumapili, imebaini kuwa mkakati huo ambao umeanza kutekelezwa na Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, wameamua kuziba mashimo na kuzima moto wa hoja hiyo ili isionekana kuwa ni kundi la wabunge wachache bali ni ajenda ya chama hicho.
Mbali na hatua hiyo, CCM imepania kwa kiasi kikubwa kufanya ajenda hiyo kuwa ya kitaifa ili kutishia nguvu na uhai wa kambi ya upinzani ambayo ndiyo iliibua mjadala huo.
Wachunguzi wa masuala ya kisiasa wanasema, ajenda hiyo ambayo iliibuliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa kutaja hadharani majina ya viongozi waliowaita mafisadi, sasa inaonekana kupokwa kwa nguvu zote na CCM ili kujijenga mbele ya macho ya jamii.
Licha ya hali hiyo, kinachoonekana sasa ni kuwa nguvu ya kina Dk. Mwakyembe na wenzake ya kukinusuru chama hicho inaelekea kupwaya.
CCM chini ya Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete, wamekuja na mkakati mzima ambao wanaamini utawasaidia dhidi ya wabunge wapambanaji.
Kwa mujibu wa chanzo kimoja cha Tanzania Daima Jumapili, kimedokeza mkakati huo umeanza kwa viongozi hao kuwa pamoja na baadhi ya wabunge hao katika majimbo yao kila wanapofanya mikutano ya hadhara ili ionekane vita wanayoipigana ni ya chama na si ya watu fulani kama inavyoonekana hivi sasa.
Wabunge walio mstari wa mbele katika vita ya ufisadi wameonekana kuwa tishio ndani ya chama na kukubalika katika jamii, hivyo kutoa hofu kwa CCM kuwa kama isipoungana nao inaweza kupoteza viti vingi vya ubunge, hususan watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi.
Mkakati huo ambao kwa hivi sasa pia umekuwa ukitumika kama mapambano baina ya wale wanaotajwa kujijenga ndani na nje ya chama kwa lengo la kuwania nafasi ya urais mwaka 2015.
Wakati mkakati huo ukianza kutekelezwa, tayari baadhi ya watu wamekwisha kubaini mbinu hizo na kuwapa tahadhari wabunge hao ambao katika siku za hivi karibuni, wamekuwa vinara wa mapambano ya ufisadi unaodaiwa kufanywa na wanachama wenzao waliopata kushika nafasi za juu serikalini na ndani ya CCM.
Kitendo cha Rais msataafu Mwinyi, ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya kuchunguza chanzo cha uhusiano mbaya kati ya wabunge wa CCM na mawaziri, kupanda jukwaani katika Jimbo la Same Mashariki akiwa na Mbunge, Anne Kilango Malecela, kumezusha maswali kadhaa miongoni mwa wafuatiliaji wa masuala ya siasa hapa nchi.
Wachambuzi wa masuala ya siasa wanabainisha kuwa Mwinyi hataweza kuwa msuluhishi mzuri au mtafutaji wa chanzo cha uhusiano mbaya kama ataendelea kushiriki katika mkakati huo unaotabiriwa kuwa mgumu na wenye kuhitaji ujasiri.
Kilango, ambaye ni mmoja wa wabunge walio mstari wa mbele kutoa hoja nzito zinazoitoa jasho serikali na chama tawala, nafasi yake hivi sasa inaonekana kupata mpinzani ambaye ni mwanamke mmoja aliyekuwa kambi ya upinzani.
Mwanamke huyo ambaye mpaka sasa bado hajatangaza hadharani licha ya kuwaambia jamaa zake wa karibu nia yake hiyo, ameonekana kusaidiwa na vigogo wa chama hicho wenye nia ya kumngoa Kilango.
Miongoni mwa vigogo hao wanaomsaidia mwanamke huyo ni wale waliokumbwa na kashfa ya ufisadi, ambao katika siku za hivi karibuni wamekuwa wakihaha kujinusuru na tuhuma zinazoelekezwa kwao.
Wakati kukiwapo taarifa za mikakati ya kuwadhoofisha wabunge hao, Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, amebainisha kuwa uamuzi wa kusimama jukwaani akiwa na Spika Sitta ni kukiimarisha chama na wala si vinginevyo.
Katibu Mkuu huyo amepuuza taarifa hizo kwa kudai zina lengo la kukichafua na kupandikiza chuki miongoni mwa wanachama ili wasiweze kuwa na umoja na mshikamano, vitakavyowawezesha kushinda katika chaguzi mbalimbali.
Makamba kwa muda mrefu amekuwa akitaka watu wasikihusishe chama hicho na ufisadi, bali unafanywa na baadhi ya wanachama wa chama hicho ambao pia hawawezi kuwajibishwa kwa tuhuma mpaka watakapofikishwa mahakamani na kutiwa hatiani.
Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wameweka wazi kuwa mkakati huo wa kuwadhoofisha wabunge machachari kwa hivi sasa ni hatari, kwa kuwa upepo wa wananchi ni kuona wale wote wanaotuhumiwa kwa ufisadi wanawajibishwa ndani ya chama na serikali.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete amekwisha kuweka wazi kuwa hajawafunga midomo wabunge wa chama hicho kujadili mijadala mbalimbali, lakini ni vema wakaangalia isije ikakibomoa pamoja na serikali kinayoiongoza.
Kikwete pia aliwataka vigogo kuacha kuzungumza mambo mazito hadharani, bali watumie vikao vya kichama kuzungumzia matatizo yao, hasa yale yanayokihusu chama na serikali.
Kauli hiyo inaonekana kutofuatwa na baadhi ya vigogo, ambapo aliyekuwa Waziri Mkuu na Katibu Mkuu wa Umoja wa Afrika (OAU) mstaafu, Dk. Salim Ahmed Salim, ameweka bayana kuwa nchi haielekei pazuri, kwani serikali inaonekana kuwakumbatia matajiri na kuwasahau maskini.
Dk. Salim, alisema kamwe serikali haiwezi kupambana na rushwa kwa kuwa mapambano yake yamejikita katika rushwa hiyo badala ya kuangalia mfumo.
Wakati Dk. Salim akitoa kauli hiyo, aliyekuwa Waziri Mkuu Jaji Joseph Warioba naye hakuwa nyuma kutoa kauli nzito na kuonya kuwa kama pengo la walionacho na wasionacho lisipozibwa kuna kila dalili ya kutokea machafuko kwa siku za usoni.
Warioba alibainisha kuwa wakati wa awamu ya kwanza chini ya hayati Baba wa Taifa, Julius Nyerere, wala rushwa walikuwa wakidhibitiwa sana na hakukuwa na pengo kati ya walionacho na wasionacho. Onyo la viongozi hao wawili dhidi ya serikali inayoongozwa na CCM limeonekana kuwakera baadhi ya wanasiasa wa chama tawala, kiasi cha kudai kuwa viongozi hao wamekuwa wakosoaji wakuu wa serikali na hawaoni zuri linalofanywa.
Wabunge walioandaliwa mkakati huo ni Christopher ole Sendeka (Simanjiro), Samuel Sitta (Urambo), Fred Mpendazoe (Kishapu) Lucas Selelii (Nzega), James Lembeli (Kahama) Anna Kilango Malecela (Same Mashariki) na Dk. Harisson Mwakyembe (Kyela).
Tanzania Daima Jumapili, imebaini kuwa mkakati huo ambao umeanza kutekelezwa na Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, wameamua kuziba mashimo na kuzima moto wa hoja hiyo ili isionekana kuwa ni kundi la wabunge wachache bali ni ajenda ya chama hicho.
Mbali na hatua hiyo, CCM imepania kwa kiasi kikubwa kufanya ajenda hiyo kuwa ya kitaifa ili kutishia nguvu na uhai wa kambi ya upinzani ambayo ndiyo iliibua mjadala huo.
Wachunguzi wa masuala ya kisiasa wanasema, ajenda hiyo ambayo iliibuliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa kutaja hadharani majina ya viongozi waliowaita mafisadi, sasa inaonekana kupokwa kwa nguvu zote na CCM ili kujijenga mbele ya macho ya jamii.
Licha ya hali hiyo, kinachoonekana sasa ni kuwa nguvu ya kina Dk. Mwakyembe na wenzake ya kukinusuru chama hicho inaelekea kupwaya.
CCM chini ya Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete, wamekuja na mkakati mzima ambao wanaamini utawasaidia dhidi ya wabunge wapambanaji.
Kwa mujibu wa chanzo kimoja cha Tanzania Daima Jumapili, kimedokeza mkakati huo umeanza kwa viongozi hao kuwa pamoja na baadhi ya wabunge hao katika majimbo yao kila wanapofanya mikutano ya hadhara ili ionekane vita wanayoipigana ni ya chama na si ya watu fulani kama inavyoonekana hivi sasa.
Wabunge walio mstari wa mbele katika vita ya ufisadi wameonekana kuwa tishio ndani ya chama na kukubalika katika jamii, hivyo kutoa hofu kwa CCM kuwa kama isipoungana nao inaweza kupoteza viti vingi vya ubunge, hususan watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi.
Mkakati huo ambao kwa hivi sasa pia umekuwa ukitumika kama mapambano baina ya wale wanaotajwa kujijenga ndani na nje ya chama kwa lengo la kuwania nafasi ya urais mwaka 2015.
Wakati mkakati huo ukianza kutekelezwa, tayari baadhi ya watu wamekwisha kubaini mbinu hizo na kuwapa tahadhari wabunge hao ambao katika siku za hivi karibuni, wamekuwa vinara wa mapambano ya ufisadi unaodaiwa kufanywa na wanachama wenzao waliopata kushika nafasi za juu serikalini na ndani ya CCM.
Kitendo cha Rais msataafu Mwinyi, ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya kuchunguza chanzo cha uhusiano mbaya kati ya wabunge wa CCM na mawaziri, kupanda jukwaani katika Jimbo la Same Mashariki akiwa na Mbunge, Anne Kilango Malecela, kumezusha maswali kadhaa miongoni mwa wafuatiliaji wa masuala ya siasa hapa nchi.
Wachambuzi wa masuala ya siasa wanabainisha kuwa Mwinyi hataweza kuwa msuluhishi mzuri au mtafutaji wa chanzo cha uhusiano mbaya kama ataendelea kushiriki katika mkakati huo unaotabiriwa kuwa mgumu na wenye kuhitaji ujasiri.
Kilango, ambaye ni mmoja wa wabunge walio mstari wa mbele kutoa hoja nzito zinazoitoa jasho serikali na chama tawala, nafasi yake hivi sasa inaonekana kupata mpinzani ambaye ni mwanamke mmoja aliyekuwa kambi ya upinzani.
Mwanamke huyo ambaye mpaka sasa bado hajatangaza hadharani licha ya kuwaambia jamaa zake wa karibu nia yake hiyo, ameonekana kusaidiwa na vigogo wa chama hicho wenye nia ya kumngoa Kilango.
Miongoni mwa vigogo hao wanaomsaidia mwanamke huyo ni wale waliokumbwa na kashfa ya ufisadi, ambao katika siku za hivi karibuni wamekuwa wakihaha kujinusuru na tuhuma zinazoelekezwa kwao.
Wakati kukiwapo taarifa za mikakati ya kuwadhoofisha wabunge hao, Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, amebainisha kuwa uamuzi wa kusimama jukwaani akiwa na Spika Sitta ni kukiimarisha chama na wala si vinginevyo.
Katibu Mkuu huyo amepuuza taarifa hizo kwa kudai zina lengo la kukichafua na kupandikiza chuki miongoni mwa wanachama ili wasiweze kuwa na umoja na mshikamano, vitakavyowawezesha kushinda katika chaguzi mbalimbali.
Makamba kwa muda mrefu amekuwa akitaka watu wasikihusishe chama hicho na ufisadi, bali unafanywa na baadhi ya wanachama wa chama hicho ambao pia hawawezi kuwajibishwa kwa tuhuma mpaka watakapofikishwa mahakamani na kutiwa hatiani.
Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wameweka wazi kuwa mkakati huo wa kuwadhoofisha wabunge machachari kwa hivi sasa ni hatari, kwa kuwa upepo wa wananchi ni kuona wale wote wanaotuhumiwa kwa ufisadi wanawajibishwa ndani ya chama na serikali.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete amekwisha kuweka wazi kuwa hajawafunga midomo wabunge wa chama hicho kujadili mijadala mbalimbali, lakini ni vema wakaangalia isije ikakibomoa pamoja na serikali kinayoiongoza.
Kikwete pia aliwataka vigogo kuacha kuzungumza mambo mazito hadharani, bali watumie vikao vya kichama kuzungumzia matatizo yao, hasa yale yanayokihusu chama na serikali.
Kauli hiyo inaonekana kutofuatwa na baadhi ya vigogo, ambapo aliyekuwa Waziri Mkuu na Katibu Mkuu wa Umoja wa Afrika (OAU) mstaafu, Dk. Salim Ahmed Salim, ameweka bayana kuwa nchi haielekei pazuri, kwani serikali inaonekana kuwakumbatia matajiri na kuwasahau maskini.
Dk. Salim, alisema kamwe serikali haiwezi kupambana na rushwa kwa kuwa mapambano yake yamejikita katika rushwa hiyo badala ya kuangalia mfumo.
Wakati Dk. Salim akitoa kauli hiyo, aliyekuwa Waziri Mkuu Jaji Joseph Warioba naye hakuwa nyuma kutoa kauli nzito na kuonya kuwa kama pengo la walionacho na wasionacho lisipozibwa kuna kila dalili ya kutokea machafuko kwa siku za usoni.
Warioba alibainisha kuwa wakati wa awamu ya kwanza chini ya hayati Baba wa Taifa, Julius Nyerere, wala rushwa walikuwa wakidhibitiwa sana na hakukuwa na pengo kati ya walionacho na wasionacho. Onyo la viongozi hao wawili dhidi ya serikali inayoongozwa na CCM limeonekana kuwakera baadhi ya wanasiasa wa chama tawala, kiasi cha kudai kuwa viongozi hao wamekuwa wakosoaji wakuu wa serikali na hawaoni zuri linalofanywa.