ndyoko
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,971
- 1,649
Imekuwa ni tabia ya kawaida sana miongoni mwa wamiliki wa simu kutopokea simu ambayo namba yake ahijui. Hata hivyo ni ujinga wa kutojua matumizi hasa ya simu. Inawezekana nduguyo kapatwa na shida-sema ajali au jambo lingine lolote ambapo anahitaji msaada toka kwako na kuamua kutumia simu ya msamaria mwema kuwasiliana nawe. Kwa ujinga wako unaamua kutopokea. Au ukipokea, baada ya kuona usumbufu, unatoa lugha ya ukali-una shida gani, unataka nini, wewe nani unanisumbua? Na mengine mengi ya mtindo huo.
Tabia hii majuzi imemkosesha jamaa kazi nzuri-hebu fikiria kaenda kafanya usaili vizuri-computer interview, written interview, oral na mwishowe driving interview. Baada ya siku tatu wamarekani wakafika bei kwake, wakaamua kumpigia simu kumtaka waende wakakubaliane siku ya kuanza kazi na kufanya preliminary arrangement. Ile anapigiwa simu, kwanza ikamchukua muda kupokea.alipigiwa mara nne, ya tano ndo akaamua kupkea.
Ile anapokea tu maneno ya karaa tupu: 'Wewe nani unanisumbua, haya sema shida yako'. Ghafla akakumbana na kiingereza, "oooh, sorry james for the disturbance, I am (akataja cheo chake na ofisi). I just called to tell you that our office has decided to hire you. However, I am sorry my friend, the expression you have shown me when you received my call may not be good for our organisation with respect to the post you were to hold in our organsation'.
Jamaa akabaki, ooooh i am sorry Sir. Mshikaji akamwambia tu, 'thanks for your time', akakata simu. Mchezo ukaisha. Hebu fikiria, maana katika majadiliano ya interview walikubaliana mshikaji awe anakamata mshahara wa milioni 5.5.
Tuna la kujifunza hapa jamani. Kama huna matatizo ktk jamii kwa nini uogope kupokea simu yako mwenyewe? Yaani simu yako lakini ikipigwa unapata shinikizo la damu, why?
Tabia hii majuzi imemkosesha jamaa kazi nzuri-hebu fikiria kaenda kafanya usaili vizuri-computer interview, written interview, oral na mwishowe driving interview. Baada ya siku tatu wamarekani wakafika bei kwake, wakaamua kumpigia simu kumtaka waende wakakubaliane siku ya kuanza kazi na kufanya preliminary arrangement. Ile anapigiwa simu, kwanza ikamchukua muda kupokea.alipigiwa mara nne, ya tano ndo akaamua kupkea.
Ile anapokea tu maneno ya karaa tupu: 'Wewe nani unanisumbua, haya sema shida yako'. Ghafla akakumbana na kiingereza, "oooh, sorry james for the disturbance, I am (akataja cheo chake na ofisi). I just called to tell you that our office has decided to hire you. However, I am sorry my friend, the expression you have shown me when you received my call may not be good for our organisation with respect to the post you were to hold in our organsation'.
Jamaa akabaki, ooooh i am sorry Sir. Mshikaji akamwambia tu, 'thanks for your time', akakata simu. Mchezo ukaisha. Hebu fikiria, maana katika majadiliano ya interview walikubaliana mshikaji awe anakamata mshahara wa milioni 5.5.
Tuna la kujifunza hapa jamani. Kama huna matatizo ktk jamii kwa nini uogope kupokea simu yako mwenyewe? Yaani simu yako lakini ikipigwa unapata shinikizo la damu, why?