Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,462
- 154,344
Hizi n dizo tabia za wasichana ambazo sipendi kabisa:
- kuamka usiku na kuanza kupekua simu yangu
- msichana mwenye gubu
- msichana ambaye anajisafisha sana kwa nje huku hajakumbuka kutandika kitanda alichokilalia.
- msichana mchoyo, ambaye wakija wageni anauvuta mdomo kwa hasira na kuficha chakula.
- msichana ambaye anapekua mifuko ya shati na suruali kusaka mshiko.
- msichana ambaye anajidai hawezi kuwatembelea wagonjwa na wenye shida mbalimbali kwa kuwa yuko busy.
- msichana ambaye anawaza kujiremba na kujipodoa kuliko mustakabari wa maisha yake yajayo.
- msichana anayefitinisha wanandugu.
- msichana mwenye maringo na kiburi wakati hamna anachojua.
- msichana muongo.
- msichana asiye na hofu ya mungu
- msichana anayehusudu habari na hadithi za kishirikina.