Sipendi Matumizi ya Neno Hili Hapa JF.

SHIEKA

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
8,244
4,258
Wadau wa lugha habari zenu?
Lipo hili neno wadau.Silipendi na napinga sana matumizi yake hapa JF.
Nimeona WanaJF wengi pale anaposifia kitu anasema: hatareeeee!
Je, huyu anataka kusema: hatariiii?au? Sasa hatareee ndo nini?
Mimi naona hiyo ni lugha ya mtaani tu inatafuta kuhalalishwa hapa.
Wanaopenda kutumia hatareee ndo haohao wa xaxa, ctaki nk.
Wachakachuaji wa lugha hawa!

Najua kabisa kwamba lugha ni kitu hai kinachokuzwa na watumiaji wenyewe
ila kama mamlaka za lugha hazijarasimisha matumizi haya mimi bado napata kichefuchefu!

Nini maoni yako kwenye hili?
 
Wadau wa lugha habari zenu?
Lipo hili neno wadau.Silipendi na napinga sana matumizi yake hapa JF.
Nimeona WanaJF wengi pale anaposifia kitu anasema: hatareeeee!
Je, huyu anataka kusema: hatariiii?au? Sasa hatareee ndo nini?
Mimi naona hiyo ni lugha ya mtaani tu inatafuta kuhalalishwa hapa.
Wanaopenda kutumia hatareee ndo haohao wa xaxa, ctaki nk.
Wachakachuaji wa lugha hawa!

Najua kabisa kwamba lugha ni kitu hai kinachokuzwa na watumiaji wenyewe
ila kama mamlaka za lugha hazijarasimisha matumizi haya mimi bado napata kichefuchefu!

Nini maoni yako kwenye hili?
Hizo na mimi huwa nashindwa kuelewa kwa nini wanaandika hivyo, huwa sipendi kabisa, lakini pengine wameathiriwa na kiingereza, huwezijua! Nafikiri watu wa lugha wanaweza kuanzia utafiti wao hapa, mtu anaweza kutengeneza tasnifu katika hili.
 
Back
Top Bottom