Kwa macho ya kawaida unaweza kufikiri lengo la daraja hili ni kupunguza foleni ya Salender Bridge na kuwaondolea wananchi wa Dar kero ya foleni. La hasha daraja hili linalojengwa kwa gharama kubwa halitapunguza foleni kwa sababu watakaotumia daraja hili ni idadi ndogo sana ya wakazi wa jiji la dar es salaam.
USHAURI: Kama lengo ni kupunguza foleni ya Salender Bridge ingefaa zaidi lijengwe daraja kubwa la nchi kavu kutokea maeneo ya Hananasifu au Magomeni hadi Muhimbili au Fire kuvuka bonde la Jangwani linalojaa maji kipindi cha mvua.
Daraja hili la Hananasifu - Muhimbili/Fire, lingehudumia watu wengi hasa wafanyabiashara wa Kariakoo na katikati ya jiji, ambulance, zimamoto na wafanyakazi wa kada za chini ambao ndio walio wengi, tofauti na daraja la Aga Khan - Coco beach ambalo litahudumia 'sana sana' wakazi wa Masaki na pengine kubaki 'idle' kwa kipindi kirefu.
Daraja kubwa la Jangwani si tu lingepunguza adha ya foleni ya Magomeni-Kariakoo/Posta lakini pia lingesaidia kupunguza magari yanayopita Salender Bridge.
Anyways kupanga ni kuchagua, tumechagua daraja la Coco beach kwa wadosi tukawaacha wa Mbagala wahangaike na foleni yao.
Ni ushauri na mawazo huru ya MwanaJF mzoefu Quinine.
(under utilised bridge?).
Ukiangalia kwa jicho la tatu, lengo hasa ni kuwasaidia viongozi, mabalozi na wazungu wachache wanaoishi maeneo ya Osterbay na Masaki ambao hawazidi hata 200, labda wasikae kwenye foleni kwa muda mrefu wakichanganyika na walalahoi wa maeneo ya Mwenge, Kawe, Kunduchi, Tegeta, Boko na Bunju.
USHAURI: Kama lengo ni kupunguza foleni ya Salender Bridge ingefaa zaidi lijengwe daraja kubwa la nchi kavu kutokea maeneo ya Hananasifu au Magomeni hadi Muhimbili au Fire kuvuka bonde la Jangwani linalojaa maji kipindi cha mvua.
Daraja hili la Hananasifu - Muhimbili/Fire, lingehudumia watu wengi hasa wafanyabiashara wa Kariakoo na katikati ya jiji, ambulance, zimamoto na wafanyakazi wa kada za chini ambao ndio walio wengi, tofauti na daraja la Aga Khan - Coco beach ambalo litahudumia 'sana sana' wakazi wa Masaki na pengine kubaki 'idle' kwa kipindi kirefu.
Daraja kubwa la Jangwani si tu lingepunguza adha ya foleni ya Magomeni-Kariakoo/Posta lakini pia lingesaidia kupunguza magari yanayopita Salender Bridge.
Anyways kupanga ni kuchagua, tumechagua daraja la Coco beach kwa wadosi tukawaacha wa Mbagala wahangaike na foleni yao.
Ni ushauri na mawazo huru ya MwanaJF mzoefu Quinine.