Samweli Mathayo
JF-Expert Member
- Aug 1, 2017
- 1,577
- 1,700
Hallo jamii mko salama ndo matumaini yangu,
Haya ni maoni yangu kama mtanzania, nina sababu zangu zinazopelekea niamini kuwa sioni sababu ya kumuachia Lissu mapema, anastahili kukaa angalau miezi minne au mitano,
Lissu anapaswa kuwekwa hapo hadi mazungumzo ya Tanzania na Barrick yaishe, maana kwa imani yangu lissu ana mkono sana katika kuyumbisha mazungumzo yanayoendelea pale jijini dsm, kuwekwa kwake ndani kutakata ushirikiano au cordination ya sehemu zinazotoa maelezo ya kusaidia upande wa pili.
Lissu akiendelea kuwekwa ndani inasaidia sana katika kudhoofisha hatua zinazopangwa kuchukuliwa na ACCACIA dhidi ya serikali ya Tanzania hakuna asiyeelewa kuwa Lissu ni miongoni mwa watu watanzania wanaotegemewa na ACCACIA kukamilisha suala lao.
Lissu kuwekwa ndani ni kwamba inarudisha heshima ya kitengo cha usalama na ikulu ya Tanzania maana tumedharauliwa sana na wageni hawa wanaotusumbua sana, na litakuwa fundisho kuwa ukitoa habari ya kupototsha Umma kuhusu rais wao mamlaka hazijanyamaza.
Lissu kuachwa azurure mtaani ingeshangaza ulimwengu kwa kuwa wangeamini rais alifanya ambayo Lissu amesema.
Lissu kuendelea kukaa ndani tutaona hata reaction za wale wenye maslahi naye, yaani wa nje wanaotaka kumtumia katika masuala yao kukwamisha taifa,
Kuachiwa kwa Lissu haraka kutasababisha mzaha kila siku kwa watanzania na police, huu utakuwa mchezo sasa, kila siku kamata achia.
Lissu kuendelea kuwa ndani inakumbusha kuwa rais ana nguvu sema nguvu hiyo watu waliisahau kwa sababu ya upole wa Kikwete.
Kwa maoni yangu wakimuachia mapema sitaona sababu ya kumkamata tena pindi akifanya kosa.
Njia pekee ni kumuweka mahabusu na kesi kuahirishwa, mara hakimu kuumwa kupata udhuru, mara utaratibu wa kumpeleka mahakaman unaandaliwa, mara bado tunasubiri maelezo ya juu.
Itasaidia kujua hata mengine ambayo hatujui maana kila mmoja ataanza kufunguka, na pili itasaidia kuwaelimisha vijana watovu wa nidhamu wa mitandaoni kuwa kashikiliwa Lissu tunayemuamini, je sisi wa hapa Manzese tukipotosha ndo itakuwaje?
Ninavyojua mimi rais wa nchi yeyyote ile hueshimiwa, uwe ulimchagua au hukumchagua,
Ikumbukwe Lissu hakuwekwa ndani kwa sababu ya ishu ya ndege ya CANADA, ila kumkashifu rais wa nchi ya Tanzania na Usalama wake, maana wanachi wenye hasira kali hawana mchezo
Samuel
Haya ni maoni yangu kama mtanzania, nina sababu zangu zinazopelekea niamini kuwa sioni sababu ya kumuachia Lissu mapema, anastahili kukaa angalau miezi minne au mitano,
Lissu anapaswa kuwekwa hapo hadi mazungumzo ya Tanzania na Barrick yaishe, maana kwa imani yangu lissu ana mkono sana katika kuyumbisha mazungumzo yanayoendelea pale jijini dsm, kuwekwa kwake ndani kutakata ushirikiano au cordination ya sehemu zinazotoa maelezo ya kusaidia upande wa pili.
Lissu akiendelea kuwekwa ndani inasaidia sana katika kudhoofisha hatua zinazopangwa kuchukuliwa na ACCACIA dhidi ya serikali ya Tanzania hakuna asiyeelewa kuwa Lissu ni miongoni mwa watu watanzania wanaotegemewa na ACCACIA kukamilisha suala lao.
Lissu kuwekwa ndani ni kwamba inarudisha heshima ya kitengo cha usalama na ikulu ya Tanzania maana tumedharauliwa sana na wageni hawa wanaotusumbua sana, na litakuwa fundisho kuwa ukitoa habari ya kupototsha Umma kuhusu rais wao mamlaka hazijanyamaza.
Lissu kuachwa azurure mtaani ingeshangaza ulimwengu kwa kuwa wangeamini rais alifanya ambayo Lissu amesema.
Lissu kuendelea kukaa ndani tutaona hata reaction za wale wenye maslahi naye, yaani wa nje wanaotaka kumtumia katika masuala yao kukwamisha taifa,
Kuachiwa kwa Lissu haraka kutasababisha mzaha kila siku kwa watanzania na police, huu utakuwa mchezo sasa, kila siku kamata achia.
Lissu kuendelea kuwa ndani inakumbusha kuwa rais ana nguvu sema nguvu hiyo watu waliisahau kwa sababu ya upole wa Kikwete.
Kwa maoni yangu wakimuachia mapema sitaona sababu ya kumkamata tena pindi akifanya kosa.
Njia pekee ni kumuweka mahabusu na kesi kuahirishwa, mara hakimu kuumwa kupata udhuru, mara utaratibu wa kumpeleka mahakaman unaandaliwa, mara bado tunasubiri maelezo ya juu.
Itasaidia kujua hata mengine ambayo hatujui maana kila mmoja ataanza kufunguka, na pili itasaidia kuwaelimisha vijana watovu wa nidhamu wa mitandaoni kuwa kashikiliwa Lissu tunayemuamini, je sisi wa hapa Manzese tukipotosha ndo itakuwaje?
Ninavyojua mimi rais wa nchi yeyyote ile hueshimiwa, uwe ulimchagua au hukumchagua,
Ikumbukwe Lissu hakuwekwa ndani kwa sababu ya ishu ya ndege ya CANADA, ila kumkashifu rais wa nchi ya Tanzania na Usalama wake, maana wanachi wenye hasira kali hawana mchezo
Samuel