UNDENIABLE
JF-Expert Member
- Feb 26, 2013
- 2,326
- 1,314
Heshima mbele!
Haya ni mawazo yangu binafsi naomba kutangulia kusema hivyo.
Natazama kwa ukaribu sana jinsi move ya urais ndani ya CCM inavyoendelea. Jana alikuwa Lowassa, leo ni Wassira na Nchemba. Move bado itaendelea!
Sijawahi kuamini kama nchi hii inaongozwa na rais kwa utashi wa urais baada tu ya kifo cha Hayati Mwalimu Nyerere. Japo Nyerere pia alipata tabu sana kukabiliana na hili genge, hata naamini ndio waliomstaafisha Nyerere (ni mawazo yangu). Hili genge lina nguvu za ajabu sana, you cant beat them!
Kumbuka urais wa Mwinyi baada ya kifo cha Nyerere. Mwinyi alishindwa kabisa kuhimili nguvu za hili kundi akakata tamaa na kuamua nchi ijiendee yenyewe. Angalia pia urais wa mkapa. Mkapa alitumia mkono wa chuma kuhakikisha kuwa habari nyingi za serikali yake hazipatikani kirahisi. Lengo kuu ni kuficha umafia wa hili genge.
Akaja kikwete. Kila mtu ni shahidi kwa yanayoendelea kila kukicha. Ni kama serikali imeparakanyika vipande vipande. Mapema kabisa alisalimu amri kwa genge hili ambalo ndilo lililomuingiza madarakani na ndilo linalotaka kumuingiza madarakani mh Lowassa. Ndipo naposema simuogopi Lowassa kuwa rais bali naogopa genge hili la mafia linalomuingiza madarakani.
Uongozi wa ki rais kwa sasa ni wa kinadharia tu kukidhi matakwa ya dunia na si vinginevyo. Hii nchi inaongozwa na genge la mafia ambapo wao sio viongozi wa kisiasa kwa namna yeyote ile. Sio rais kuwaona kwenye ulingo wa kisiasa. Watu hawa hata hawazidi kumi, naweza kusema hivyo.
Hili genge la mafia wana kazi moja tu nayo ni biashara zao. Ni wafanyabiashara haramu mfano madawa ya kulevya kwa kutaja biashara moja tu. Kwao wanasiasa ni daraja la kufanya mambo yao ya kibiashara, basi. Watapambana kwa kila namna wawezavyo kuwaweka viongozi wa kisiasa kwa nafasi za kisiasa kwa namna watakavyo wao.
Mwanasiasa yeyote aliepo mrengo wa kushoto na genge hili la mafia hastahili kuwa kiongozi. Kumbuka sakata la madawa ya kulevya la Mwakyembe na kuhamishiwa wizara ya afrika mashariki! Kumbuka sakata la bandari la sitta na mwakyembe, ni kama sitta alitumika kumchafua mwakyembe. Mwakyembe alishughulikiwa vilivyo. Hili genge ni invisibles kwa wananchi wa kawaida lakini ni genge hatari lenye nguvu kupita kiasi.
Tatizo kubwa la genge hili la mafia ni kuwa hawaangalii maslahi mapana ya taifa wao ni biashara zao tu. Na hapa ndipo ndipo kulipo na shida kubwa.
Angalia namna genge hili linavyofanya kazi.
Leo Wassira anatangaza nia, pia Mwigulu anatangaza nia. Nakuhakikishia hawa wote wanatumika na lile genge la mafia kumuingiza Lowassa madarakani. Usijisumbue kutafakari.
Simuogopi Lowassa kuwa rais bali naogopa genge linalomuingiza kwenye kiti cha urais!
Haya ni mawazo yangu binafsi naomba kutangulia kusema hivyo.
Natazama kwa ukaribu sana jinsi move ya urais ndani ya CCM inavyoendelea. Jana alikuwa Lowassa, leo ni Wassira na Nchemba. Move bado itaendelea!
Sijawahi kuamini kama nchi hii inaongozwa na rais kwa utashi wa urais baada tu ya kifo cha Hayati Mwalimu Nyerere. Japo Nyerere pia alipata tabu sana kukabiliana na hili genge, hata naamini ndio waliomstaafisha Nyerere (ni mawazo yangu). Hili genge lina nguvu za ajabu sana, you cant beat them!
Kumbuka urais wa Mwinyi baada ya kifo cha Nyerere. Mwinyi alishindwa kabisa kuhimili nguvu za hili kundi akakata tamaa na kuamua nchi ijiendee yenyewe. Angalia pia urais wa mkapa. Mkapa alitumia mkono wa chuma kuhakikisha kuwa habari nyingi za serikali yake hazipatikani kirahisi. Lengo kuu ni kuficha umafia wa hili genge.
Akaja kikwete. Kila mtu ni shahidi kwa yanayoendelea kila kukicha. Ni kama serikali imeparakanyika vipande vipande. Mapema kabisa alisalimu amri kwa genge hili ambalo ndilo lililomuingiza madarakani na ndilo linalotaka kumuingiza madarakani mh Lowassa. Ndipo naposema simuogopi Lowassa kuwa rais bali naogopa genge hili la mafia linalomuingiza madarakani.
Uongozi wa ki rais kwa sasa ni wa kinadharia tu kukidhi matakwa ya dunia na si vinginevyo. Hii nchi inaongozwa na genge la mafia ambapo wao sio viongozi wa kisiasa kwa namna yeyote ile. Sio rais kuwaona kwenye ulingo wa kisiasa. Watu hawa hata hawazidi kumi, naweza kusema hivyo.
Hili genge la mafia wana kazi moja tu nayo ni biashara zao. Ni wafanyabiashara haramu mfano madawa ya kulevya kwa kutaja biashara moja tu. Kwao wanasiasa ni daraja la kufanya mambo yao ya kibiashara, basi. Watapambana kwa kila namna wawezavyo kuwaweka viongozi wa kisiasa kwa nafasi za kisiasa kwa namna watakavyo wao.
Mwanasiasa yeyote aliepo mrengo wa kushoto na genge hili la mafia hastahili kuwa kiongozi. Kumbuka sakata la madawa ya kulevya la Mwakyembe na kuhamishiwa wizara ya afrika mashariki! Kumbuka sakata la bandari la sitta na mwakyembe, ni kama sitta alitumika kumchafua mwakyembe. Mwakyembe alishughulikiwa vilivyo. Hili genge ni invisibles kwa wananchi wa kawaida lakini ni genge hatari lenye nguvu kupita kiasi.
Tatizo kubwa la genge hili la mafia ni kuwa hawaangalii maslahi mapana ya taifa wao ni biashara zao tu. Na hapa ndipo ndipo kulipo na shida kubwa.
Angalia namna genge hili linavyofanya kazi.
Leo Wassira anatangaza nia, pia Mwigulu anatangaza nia. Nakuhakikishia hawa wote wanatumika na lile genge la mafia kumuingiza Lowassa madarakani. Usijisumbue kutafakari.
Simuogopi Lowassa kuwa rais bali naogopa genge linalomuingiza kwenye kiti cha urais!