Sio kweli chakula cha Rais lazima kipimwe kabla ya kuliwa

Kuna incidents hazihitaji kupima, chakula kile hakikuandaliwa kwa ajili ya Rais kwa hiyo hakungekuwa na intention yoyote kwamba kimefanyiwa ujanja.

Najua utajifanya hujaelewa ili kumtetea Rais wenu wa wanyonge na upate buku 7 yako mkono iende kinywani.
Nadhani hili ndilo jibu sahihi...
 
Umbea wa Polepole ni nini hapo!?
Unyenyekevu wa binadamu ni moja ya nguzo bora sana maishani. Mwanadamu aliyekosa Unyenyekevu mara nyingi huwa amejawa na kutawaliwa na Kiburi, Ujuaji, Uzandiki, Unafiki, Ushirikina, Chuki, Wizi/Uporaji, Uzinzi n.k. Na Dini zote zinatufundisha tuwe WANYENYEKEVU.
Dini ndio kitu gani,pamoja na ubovu wa hizo dini zinatutaka tuwe wanyenyekevu kwa mungu na sio wenye mamlaka.
 
Dini ndio kitu gani,pamoja na ubovu wa hizo dini zinatutaka tuwe wanyenyekevu kwa mungu na sio wenye mamlaka.
Utakuwa una matatizo makubwa sana ya akili kiongozi. Kuna maandiko katika kitabu cha Matayo 22, mstari wa 15-22, yanasema hivi;
15:Kisha, Mafarisayo wakaenda zao, wakashauriana jinsi ya kumnasa Yesu kwa maneno yake. 16:Basi, wakawatuma wafuasi wao pamoja na wafuasi wa kikundi cha Herode. Wakamwuliza, “Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu mwaminifu, na kwamba wafundisha njia ya Mungu kwa uaminifu; humwogopi mtu yeyote, maana cheo cha mtu si kitu kwako. 17:Haya, tuambie maoni yako. Je, ni halali au la, kulipa kodi kwa Kaisari?” 18:Lakini Yesu alitambua uovu wao, akawaambia, “Enyi wanafiki mbona mnanijaribu? 19:Nionesheni fedha ya kulipia kodi.” Nao wakamtolea sarafu ya fedha. 20:Basi, Yesu akawauliza, “Sura na chapa hii ni ya nani?” 21:Wakamjibu, “Ni ya Kaisari.” Hapo Yesu akawaambia, “Basi, ya Kaisari mpeni Kaisari, na ya Mungu mpeni Mungu.” 22:Waliposikia hivyo wakashangaa; wakamwacha, wakaenda zao."

Acha Unafiki Kijana.
 
Kuna tofauti kati ya mtu na mtu mwenye madaraka na nguvu kama Rais au kiongozi wa Nchi.
Mimi na Wewe ni watu....lakini Mh. Rais wa JMT ni mtu mwenye madaraka mazito sana na kauli yake inaweza kuamua kama uendelee kuishi au hapana. Nafikiri utakuwa umenielewa.
Mkuu Una uhakika kauli ya Rais ina amua uhai wako!? Kwanini yeye ni Mungu, Majaribio mangapi yanayokuwa na baraka labda za Rais wa nchi fulani ila yana kwama!? Unachopaswa kujua Rais ni mtu na kila mtu ana mapungufu, Leo Zuma wa SA anawekwa kizibani kusomewa mashtaka, R. mugabe anaweka zuria jekundu kwake anatembea hapo huku akisema leo hakuna hata waandishi wa habari wa kumuandika na bado mke wake anakabiliwa na mashtaka kem kem
 
Kwa akili yako unavyofikir kwahy prezidaa hakuwa na kitu mfukoni/mtonyo/ngawira?? Hizo busara za jk kuwahadaa km hana kitu mfanane nae kwa muda!
Hii incidence alimkanya mpk mondi wakati kapiga picha na maburungutu na pesa akitambia @ig,mzee akamwambia unajenga chuki na raia ambao hata kula yao shida na hao hao ndo mashabiki wanaojinyima kukusapoti leo wanaona unawakejeri kwa kuwaringishia haipendezi#busara za jk

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkwere mtoto wa Mjini sana yani Mzee yule hatari sana
 
Kulikuwa na urongo unaenezwa chakula cha mh Rais lazima kipimwe tena lazima ale MTU mwingine kabla yake..

Magufuli amethibitisha sio kweli,km mnakumbuka alikula kwenye mgahawa mwanza,Jana kala dafu adharani bila kutest MTU wala kupimwa.

Mi najua madafu uwa yanakaaga wiku3 hayajauzwa na kwavile hayajakomaa maji yake yanavunda hivyo ni raisi kuumwa tumbo..ila mh hakujali ilo wala hakuwaza madafu ni ya lini..

Tuache kudanganyana acheni urongo urongo....

Sent using Jamii Forums mobile app
Uko gizani kweli kwa taarifa yako mtaani siyo wauza uji wote ama wachoma mahindi, nyama, washona viatu au wapiga debe wote ni kazi zao. Usipende kuamini kila unachokiona.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vitu ambavyo Rais kabla ya kula lazima vipimwe Ni vile vya kupikwa kwa Mazingira Kama ya hotel Au event maalum kuepuka sumu Ila sio Kila anachokula lazima kipimwe



Mie kilichonifurahisha sio Rais kula dafu bali kiherehere Cha Humphrey Polepole kushikilia dafu wakati Rais anakunywa Maji ya dafu!


Watu tunajua Sana kuji pendekeza kwa Kweli

Na Gerson Msigwa kaiweka Kwenye page yake ya Instagram kuonesha maana ya Unyenyekevu kwa Mkuu wa Dola

Ila Pia Nimejifunza kitu Kuwa Ndugu Rais Magufuli huwa anatembea Na Fedha Mfukoni tofauti Na Jakaya ambae kuna Siku 2006 nusura adhalilike ambae akiwa Mtaa wa Samora ilipo NBC Samora akiwa Kwenye Ziara ya kutembelea zilizokuwa ofisi Za Idara ya Misitu alikatiza Ombaomba ambae akamuomba Fedha Na Jk bila ya hiyana akazama mfukoni akajipiga 'sachi' Sana akakosa pesa ndipo Mpambe wake akaokoa Jahazi kwa kutoa Za kwake Na kumpa Rais amabe akamkabidhi pale pale.
Hapo mwisho wachache watakuelewa
 
Socrates anasema ukweli Ni kwajili tu ya watawala na wanaume. Na siyo kwajili ya wapumbavu, wanawake , watoto na watumwa.
Ukionacho kwa macho, humu uraiani Kama hayo ya dafu na MJP ni nje kabsa na ukweli halisi.
Na ukitakacho kuujua ukweli lazima uwe mwanaume, na mtawala ...Hapo hapo isiwe mpumbavu, mtoto, mwanamke Wala mtumwa wa akili na mwili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Socrates anasema ukweli Ni kwajili tu ya watawala na wanaume. Na siyo kwajili ya wapumbavu, wanawake , watoto na watumwa.
Ukionacho kwa macho, humu uraiani Kama hayo ya dafu na MJP ni nje kabsa na ukweli halisi.
Na ukitakacho kuujua ukweli lazima uwe mwanaume, na mtawala ...Hapo hapo isiwe mpumbavu, mtoto, mwanamke Wala mtumwa wa akili na mwili.

Sent using Jamii Forums mobile app
Pengine HAO wengi wameanzia kuona 'pale' na ni bora waachwe kuelewa tukio lile kuanzia 'pale pale' walipoRUHUSIWA kuona! HAWA wengineo RUKSA kudurusu durusu iwafaavyo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom