LOVINTAH GYM
JF-Expert Member
- Oct 22, 2015
- 459
- 643
Hadithi Hadithiii..
Kulikuwa na mvuvi mmoja kwa bahati mbaya akiwa kwenye kazi yake ya kuvua basi boti yake ilizama. Kwa bahati nzuri alifanikiwa kuogelea na kufika kwenye kisiwa kimoja kilicho kuwa karibu na sehemu ambapo boti yake ilizama.
Basi siku zikazidi kwenda na kwa bahati mbaya hakuna mtu aliyejua kuwa yupo kwenye hiko kisiwa. Akawa amejizoelea maisha yake na akafanikiwa kujijengea kibanda chake.
Baada ya miezi kupita, msimu wa baridi ukaanza, akawa amewasha moto wake ili apate joto. Kwa bahati mbaya ule moto ukatapakaa na kuunguza kibanda chake.
Yule mvuvi alisikitika sana, na kumlaumu Mungu kwanini anampitisha kwenye shida. Kulikuwa na meli inapita, ikaona moshi mkubwa, basi wakaamini kutakuwa na uwepo wa binadamu katika kisiwa hiko na kwa bahati nzuri ikamkuta na kumrudisha nyumbani kwake.
Point of the story ni kwamba.
Kuna muda unaweza pitia tabu flani bila kujua kuwa mapito yako ndio yatakayokuletea neema katika maisha.
Usiwe mwepesi kulaumu, kulalamika, jitahidi kushukuru kwa kila jambo.
Karibuni kutoa mifano kuhusu changamoto ambazo umepitia kwenye maisha ambazo mwisho wake ukawa mzuri kwako.
#lifechallenges #changamotozamaisha #swahili
Kulikuwa na mvuvi mmoja kwa bahati mbaya akiwa kwenye kazi yake ya kuvua basi boti yake ilizama. Kwa bahati nzuri alifanikiwa kuogelea na kufika kwenye kisiwa kimoja kilicho kuwa karibu na sehemu ambapo boti yake ilizama.
Basi siku zikazidi kwenda na kwa bahati mbaya hakuna mtu aliyejua kuwa yupo kwenye hiko kisiwa. Akawa amejizoelea maisha yake na akafanikiwa kujijengea kibanda chake.
Baada ya miezi kupita, msimu wa baridi ukaanza, akawa amewasha moto wake ili apate joto. Kwa bahati mbaya ule moto ukatapakaa na kuunguza kibanda chake.
Yule mvuvi alisikitika sana, na kumlaumu Mungu kwanini anampitisha kwenye shida. Kulikuwa na meli inapita, ikaona moshi mkubwa, basi wakaamini kutakuwa na uwepo wa binadamu katika kisiwa hiko na kwa bahati nzuri ikamkuta na kumrudisha nyumbani kwake.
Point of the story ni kwamba.
Kuna muda unaweza pitia tabu flani bila kujua kuwa mapito yako ndio yatakayokuletea neema katika maisha.
Usiwe mwepesi kulaumu, kulalamika, jitahidi kushukuru kwa kila jambo.
Karibuni kutoa mifano kuhusu changamoto ambazo umepitia kwenye maisha ambazo mwisho wake ukawa mzuri kwako.
#lifechallenges #changamotozamaisha #swahili