Sokomoko
JF-Expert Member
- Mar 29, 2008
- 1,915
- 127
Habari zenu wanaJF,
Kwa kipindi kirefu sasa nimekuwa nikifatilia hoja mbalimbali ziletwazo hapa jamvini, katika kupitia huwa nakutana na replies ambazo kusema ukweli zinasikitisha sana. Majibu ya post nyingi yanakuwa ya jazba na anaejibu anakuwa kama mtu asiekuwa na akili timamu. Katika pitapita yangu nikakutana na kitu kinaitwa "udumavu" au kwa umombo "stanting" ninachoweza kusema kuwa ni ukweli usiopingika kuwa baadhi yetu kaktika kile kipindi cha miaka mitano ya mwanzo tulikumbwa na tatizo hili. Hili tatizo linasababishwa na lishe duni, maradhi na kutolea watoto vizuri. Hili tatizo ni kubwa sana kwenye nchi nyingi zinazoendelea Tanzania ikiwa moja katika kundi hilo.
Ni ukweli usiopingika na uliodhibitishwa na wataalamu wa afya kuwa..kuanzia 0 day up to 5 years mtoto anakuwa mwili sambamba na akili, na ikiwa anakumbwa na udumavu basi atadumaa mwili na akili! Tujichunguze kutokana na tabia zetu pengine tutagundua tatizo letu ni nini. kwani haiingii akili mtu akitoa mawazo kwasababu wewe huyaafiki basi umkashifu "umetumwa" "crap" "hoja isiyo na mashiko" "Uongo usio na tija"
Kuna swala jingine linalonikera sana mpaka huwa nasikia kichefuchefu nalo ni "udini" hivi jamani mtu akiwa kiongozi dini yake inakukera kitu gani? sidhani kama Slaa akiwa Rais atatulazimisha watanzania wote tuvae rozari! na kadhalika sifikirii kuwa JK ataamka asubuhi siku moja wakati ana taulo kiunoni atawaza leo niwaambie watanzania wasilimu! Au nikienda kuhutubia bunge wabunge wote wavae kanzu hata wale "wanaomkimbia"
Ni wajibu wetu kushikama kwenye umoja wetu na kuto kumbatia aina yoyote ya utengano, tupinge hoja kwa hoja zenye nguvu na ushawishi kwani hapo ndipo tutakuwa tumelitumia jukwaa hili effectively.
Natanguliza shukrani zangu wa management ya JF pamoja na JF members wote. Hatujachelewa tutafakari tuangalie je hatujawa "stunted" kweli?
Kwa kipindi kirefu sasa nimekuwa nikifatilia hoja mbalimbali ziletwazo hapa jamvini, katika kupitia huwa nakutana na replies ambazo kusema ukweli zinasikitisha sana. Majibu ya post nyingi yanakuwa ya jazba na anaejibu anakuwa kama mtu asiekuwa na akili timamu. Katika pitapita yangu nikakutana na kitu kinaitwa "udumavu" au kwa umombo "stanting" ninachoweza kusema kuwa ni ukweli usiopingika kuwa baadhi yetu kaktika kile kipindi cha miaka mitano ya mwanzo tulikumbwa na tatizo hili. Hili tatizo linasababishwa na lishe duni, maradhi na kutolea watoto vizuri. Hili tatizo ni kubwa sana kwenye nchi nyingi zinazoendelea Tanzania ikiwa moja katika kundi hilo.
Ni ukweli usiopingika na uliodhibitishwa na wataalamu wa afya kuwa..kuanzia 0 day up to 5 years mtoto anakuwa mwili sambamba na akili, na ikiwa anakumbwa na udumavu basi atadumaa mwili na akili! Tujichunguze kutokana na tabia zetu pengine tutagundua tatizo letu ni nini. kwani haiingii akili mtu akitoa mawazo kwasababu wewe huyaafiki basi umkashifu "umetumwa" "crap" "hoja isiyo na mashiko" "Uongo usio na tija"
Kuna swala jingine linalonikera sana mpaka huwa nasikia kichefuchefu nalo ni "udini" hivi jamani mtu akiwa kiongozi dini yake inakukera kitu gani? sidhani kama Slaa akiwa Rais atatulazimisha watanzania wote tuvae rozari! na kadhalika sifikirii kuwa JK ataamka asubuhi siku moja wakati ana taulo kiunoni atawaza leo niwaambie watanzania wasilimu! Au nikienda kuhutubia bunge wabunge wote wavae kanzu hata wale "wanaomkimbia"
Ni wajibu wetu kushikama kwenye umoja wetu na kuto kumbatia aina yoyote ya utengano, tupinge hoja kwa hoja zenye nguvu na ushawishi kwani hapo ndipo tutakuwa tumelitumia jukwaa hili effectively.
Natanguliza shukrani zangu wa management ya JF pamoja na JF members wote. Hatujachelewa tutafakari tuangalie je hatujawa "stunted" kweli?