Uchaguzi 2020 Sio CCM wala CHADEMA wote sielewi chochote

zagarinojo

JF-Expert Member
Jul 26, 2020
2,622
2,835
Habari wana JF wenzagu. Huu ni mwaka wa Uchaguzi mkuu na tarehe 28.10.2020 ni kama imekaribia hivi ili maamuzi ya wananchi yatimie katika
Kisanduku cha faragha cha kupigia kura.

Ila ni kama nimeshikwa na butwaa kwa sababu nikisikiliza sera za pande zote mbili naona kama sielewi chochote.

Chadema wanasema kwamba wanakubalika na wanachi ila kwenye mikutano ya CCM naona mafuriko ya watu tena wanaoneshwa kupendezwa na yale ayasemayo Mgombea tena na kuhudhuria mikutano wanahudhuria kwenye mikutano.

Sikutegemea kuona wingi wa watu endapo CCM sasa basi au kwamba wanataka kuiondoa madarakani.

Nikija upande wa pili TL anasema kuwa anaijua sheria vizuri ila ameshindwa kupingana na sheria kandamizi za wenzetu hata kulinda kura zao kisheria ameshindwa.

Kama ni kweli walimtendea ubaya mbona asifungue kesi mahakamani ya mambo aliyotendewa ikiwemo kuvuliwa ubunge kunyimwa mshahara wake kisheria. Labda ingesaidia kidogo.

Mwisho wa Siku mambo yanajirudia yale yale Ma Raisi Wa CCM miaka kumi ni lazima hata ufanyeje. Tumia usomi wako Tundu Lissu unaonekane kweli unaijua sheria sio kuongea kwa maneno bali kwa vitendo
 
Utakuwa mjinga sana na upumbavu juu

Chadema
1. Kodi
2. Afya
3. Katiba mpya ya jaji Warioba
4. Uhuru wa raia kuhoji
5. Uhuru wa vyombo vya habari
6. Uhuru na haki ya kuchaguwa viongozi
7. Elimu, bora bila ubaguzi mikopo
8. Uhuru wa mahaka bila kuingiliwa
9. Uhuru wa vyombo vya dola kutenda kwa haki
10. Uhuru, haki na maendeleo ya mtanzania
 
Utakuwa mjinga sana na upumbavu juu

Chadema
1. Kodi
2. Afya
3. Katiba mpya ya jaji warioba
4. Uhuru wa raia kuhoji...
Itabidi unishukuru kwa ujinga wangu kwasababu mjinga humfanya muelewa aneonakane mwelewa pale anapomwelezea mjinga.

Mwelewa atapata funzo kutokana na swali la mjinga.

Hata hivyo wasomi na watu waelewa hujibu maswali rahisi kwa njia ngumu na maswali magumu kwa njia nyepesi.

Tafsiri ya neno mjinga ni mtu asiye elewa kuhusu kitu au jambo flani

Ukispecialize kwenye Mechanic Engineering na hujui kuhusu Agriculture wewe ni mjinga

Kwa hiyo ujinga haujawahi Kuisha
Ili usiwe mjinga lazima uwe unaelewa kila kitu
 
Yaani chama kilichokaa madarakani miaka 59 na kukusanya Kodi , unakilinganisha na chama ambacho hakijawahi kushika madaraka wala kukusanya kodi?
 
Back
Top Bottom