Singida: Wawili wafariki na 20 kujeruhiwa katika ajali ya basi la National Express

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
Watu wawili wamefariki dunia na wengine wapatao 20 wamejeruhiwa baada ya basi la Kampuni ya National Express lolilokuwa likitoka Iramba mkoani Singida kwenda Dar es Saalam kuacha njia na kupinduka katika eneo liitwalo Tumuli.


IMG-20161230-WA0007.jpg

IMG-20161230-WA0006.jpg

IMG-20161230-WA0004.jpg

IMG-20161230-WA0003.jpg

IMG-20161230-WA0002.jpg
 
Pole kwa wafiwa, Nawaombea majeruhi wapate nafuu haraka, Pole kwa Mheshimiwa Mwigulu Lameck Nchemba kwa kupoteza wapiga kura katika jimbo lako
 
Ni bus lililokua linatoka wilayani kiomboi mkoa wa Singida kwenda jijini Dar es Salaam. Limepata ajali eneo la Tumuli mkoani Singida.

Chanzo cha ajali: Mashuhuda wamesema ni mwendokasi na hivyo bus kumshinda dereva lilivyofika kwenye kona na ikizingatiwa palikua na hali na unyevu barabarani.

Vifo:
Mpaka sasa kumeripotiwa vifo viwili yani dereva wa bus na abiria mmoja.

Majeruhi ni wengi pia.

Note:
Madereva tuweni makini barabarani na trafiki fanyeni kazi sio mnakaa na tochi kama chanzo cha mapato tu.
23c24a7cc63a3a5840d304ac25e9353b.jpg
bc0492e317ea6b931abb37fe3a7dbe1c.jpg
36db3e794bcdeab7f1ab87951acca4a0.jpg
058182472c18eb21de16bbed6c8298b2.jpg
 
waache kusingizia mwendo kasi. hakuna bus linalokimbia siku hizi.
pole zao majeruhi Mungu awafanyie wepesi
 
Poleni wafiwa kwa kweli...hilo bus linaonekana ni jepesi sana haliwezi likawa mwendo mkubwa na balance iwepo hapo hakuna kitu kama hicho...
 
Back
Top Bottom