Suphian Juma
Senior Member
- Apr 2, 2019
- 133
- 546
UFUATILIAJI WA MAJIBU YA RUFAA YANGU- SUPHIAN.
Napata simu, maswali ana kwa ana na jumbe nyingi za wananchi wa Jimbo la Singida Magharibi, marafiki, ndugu na jamaa kutoka sehemu mbalimbali nchini kuhusu rufaa niliyokata Agosti 27, 2020 baada ya uteuzi wangu kuenguliwa na Msimamizi wa Uchaguzi baada ya kuwekewa Pingamizi na Mgombea wa CCM na kwamba kampeni naanza lini; majibu yangu ni kama ifuatayo:
Jana Septemba 10, 2020 nimeenda Ofisi ya Tume ya Uchaguzi (NEC) Taifa Dar es salaam kufuatilia majibu ya rufaa yangu YALIYOTOLEWA Septemba 9, 2020 na Tume hiyo;
TUME IMENIJIBU: Barua imetumwa kwa Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Singida Magharibi NINAPOGOMBEA UBUNGE. Aidha nimewasiliana pia na Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo jana na leo na majibu yake ni kwamba bado hawajapata barua kutoka Tume ya Uchaguzi licha ya wao kukiri kuona kupitia vyombo vya habari kwamba majibu ya rufaa yametoka.
Ndugu zangu Nani tatizo hapa? Kutoa barua panashindikana kwanini? Muda wa kampeni unazidi kuyoyoma, tutaongezewa muda? Wenzetu wa CCM wanaendelea na kampeni, sisi upinzani tuseme ni watoto wa kambo? Kuna nini zaidi ya kuendelea kutuhujumu Upinzani na wananchi?
Chama changu cha ACT wazalendo kinaendelea kufuatilia hili kwa karibu, HAKI ITENDEKE.
NEC INAFIKIRISHA sana. Indeed Disgusting!!!
Suphian Juma,
Mgombea Ubunge,
ACT wazalendo,
Singida Magharibi.
Septemba 11, 2020.
Napata simu, maswali ana kwa ana na jumbe nyingi za wananchi wa Jimbo la Singida Magharibi, marafiki, ndugu na jamaa kutoka sehemu mbalimbali nchini kuhusu rufaa niliyokata Agosti 27, 2020 baada ya uteuzi wangu kuenguliwa na Msimamizi wa Uchaguzi baada ya kuwekewa Pingamizi na Mgombea wa CCM na kwamba kampeni naanza lini; majibu yangu ni kama ifuatayo:
Jana Septemba 10, 2020 nimeenda Ofisi ya Tume ya Uchaguzi (NEC) Taifa Dar es salaam kufuatilia majibu ya rufaa yangu YALIYOTOLEWA Septemba 9, 2020 na Tume hiyo;
TUME IMENIJIBU: Barua imetumwa kwa Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Singida Magharibi NINAPOGOMBEA UBUNGE. Aidha nimewasiliana pia na Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo jana na leo na majibu yake ni kwamba bado hawajapata barua kutoka Tume ya Uchaguzi licha ya wao kukiri kuona kupitia vyombo vya habari kwamba majibu ya rufaa yametoka.
Ndugu zangu Nani tatizo hapa? Kutoa barua panashindikana kwanini? Muda wa kampeni unazidi kuyoyoma, tutaongezewa muda? Wenzetu wa CCM wanaendelea na kampeni, sisi upinzani tuseme ni watoto wa kambo? Kuna nini zaidi ya kuendelea kutuhujumu Upinzani na wananchi?
Chama changu cha ACT wazalendo kinaendelea kufuatilia hili kwa karibu, HAKI ITENDEKE.
NEC INAFIKIRISHA sana. Indeed Disgusting!!!
Suphian Juma,
Mgombea Ubunge,
ACT wazalendo,
Singida Magharibi.
Septemba 11, 2020.