Hussein Massanza
JF-Expert Member
- Dec 26, 2012
- 918
- 1,994
Watu wa Soka,
Tunapenda kuwafahamisha wapenzi, wadau na mashabiki wa klabu ya Singida Big Stars kuwa tumepokea mwaliko kutoka kwa wenzetu Rayon Sports FC ya nchini Rwanda kwa ajili ya mechi ya kirafiki ya kimataifa.
Timu yetu inatarajia kusafiri kuelekea Rwanda siku ya Ijumaa ya tarehe 02/09/2022 kwa ajili ya mechi hii ambayo inatarajiwa kuchezwa tarehe 04/09/2022 katika Uwanja wa Nyamirambo uliopo mjini Kigali.
Mwaliko huu umekuja wakati sahihi ambapo timu zote mbili zipo kwenye mapumziko mafupi ya Ligi, hivyo tutautumia mchezo huu kwa ajili ya kuendelea kujiandaa vyema na msimu mrefu wa Ligi Kuu 2022/2023.
Bodi ya Wakurugenzi na Menejimenti ya Klabu ya Singida Big Stars inaishukuru Rayon Sports FC kwa mwaliko. Pia kwa kugharamia safari nzima ya kikosi chetu pamoja na baadhi ya viongozi watakaoambatana na timu katika kipindi chote timu itakapokuwepo nchini Rwanda hadi kurejea nyumbani Singida, Tanzania.
Tunapenda kuwafahamisha wapenzi, wadau na mashabiki wa klabu ya Singida Big Stars kuwa tumepokea mwaliko kutoka kwa wenzetu Rayon Sports FC ya nchini Rwanda kwa ajili ya mechi ya kirafiki ya kimataifa.
Timu yetu inatarajia kusafiri kuelekea Rwanda siku ya Ijumaa ya tarehe 02/09/2022 kwa ajili ya mechi hii ambayo inatarajiwa kuchezwa tarehe 04/09/2022 katika Uwanja wa Nyamirambo uliopo mjini Kigali.
Mwaliko huu umekuja wakati sahihi ambapo timu zote mbili zipo kwenye mapumziko mafupi ya Ligi, hivyo tutautumia mchezo huu kwa ajili ya kuendelea kujiandaa vyema na msimu mrefu wa Ligi Kuu 2022/2023.
Bodi ya Wakurugenzi na Menejimenti ya Klabu ya Singida Big Stars inaishukuru Rayon Sports FC kwa mwaliko. Pia kwa kugharamia safari nzima ya kikosi chetu pamoja na baadhi ya viongozi watakaoambatana na timu katika kipindi chote timu itakapokuwepo nchini Rwanda hadi kurejea nyumbani Singida, Tanzania.