Sinema ya Lion King na kibwagizo cha hakuna matata: haki yetu ipo wapi?

NANDERA

JF-Expert Member
Mar 18, 2014
2,024
2,486
Jambo! Hakuna matata! Nimezaliwa nikayakuta maandishi haya kwenye t-shirts na kazi zingine za sanaa hasa katika maduka ya watalii kule Moshkwetu. Yamekuwa pia kibwagizo katika matangazo ya utalii kwa miaka mingi. Sina shaka kuwa ni mali ya Tanzania. Nilijisikia fahari kusikia Hakuna Matata katika sinema mpya ya The Lion King ambapo Simba mtoto wa Mufasa alitamkiwa maneno haya na rafiki zake wawili waliompokea ukimbizini ili kumtuliza. Swali langu ni je, huko Dysney Hakuna Matata imefikafikaje? Anayewahi studio ndo mmiliki wa wimbo au bado tuna nafasi ya kudai haki yetu? Hii si mara ya kwanza kuibiwa haki zetu (japo hatuzijui sometimes) na watengeneza sinema wa mbele. Muziki wa Saida Karoli uliwahi kutumika kwenye sinema huko majuu na sidhani kama kuna mtu alimsaidia kupata haki yake. Naiomba serikali iamke. Isione ni jambo dogo. Hawa mabepari siyo wa kuwachekea. Angalia walichowafanyia Wasotho. LV kajimiliksha blanketi lao la asili katengeneza vijishati anauza dola 1000 na ushee eti kawahi studio. Tusishangae mashuka ya wamasai nayo akatokea 'designer' huko akajitwalia umiliki. Wale wanaharakati wetu, hili ni pia ni swala la haki za bindamu; siyo kukomalia siasa tu.
 
Ahahahahaha wabongo bana kwel tuna gombea neno wakat sisi tunatumia lugha yao yote kwenye elimu yetu daladala imetokana na lugha yao kwel unasema tuache kupigana na madini mgodini kwel serikali ipiganie neno hakuna matata alafu neno limekuwa registrated marekani kuwa wanatumia wao sasa kaguse unate nadhani hao jamaa wanajua akili za waafrica zikoje wametusoma kama wanavyosoma wanyama pori ndo mana wanatuweza sana kutumiliki
 
Mbona
Jambo! Hakuna matata! Nimezaliwa nikayakuta maandishi haya kwenye t-shirts na kazi zingine za sanaa hasa katika maduka ya watalii kule Moshkwetu. Yamekuwa pia kibwagizo katika matangazo ya utalii kwa miaka mingi. Sina shaka kuwa ni mali ya Tanzania. Nilijisikia fahari kusikia Hakuna Matata katika sinema mpya ya The Lion King ambapo Simba mtoto wa Mufasa alitamkiwa maneno haya na rafiki zake wawili waliompokea ukimbizini ili kumtuliza. Swali langu ni je, huko Dysney Hakuna Matata imefikafikaje? Anayewahi studio ndo mmiliki wa wimbo au bado tuna nafasi ya kudai haki yetu? Hii si mara ya kwanza kuibiwa haki zetu (japo hatuzijui sometimes) na watengeneza sinema wa mbele. Muziki wa Saida Karoli uliwahi kutumika kwenye sinema huko majuu na sidhani kama kuna mtu alimsaidia kupata haki yake. Naiomba serikali iamke. Isione ni jambo dogo. Hawa mabepari siyo wa kuwachekea. Angalia walichowafanyia Wasotho. LV kajimiliksha blanketi lao la asili katengeneza vijishati anauza dola 1000 na ushee eti kawahi studio. Tusishangae mashuka ya wamasai nayo akatokea 'designer' huko akajitwalia umiliki. Wale wanaharakati wetu, hili ni pia ni swala la haki za bindamu; siyo kukomalia siasa tu.
Haki gani mnaitaka mbona sisi tunaongea kiingereza hawatutozi kukilipia
Pia nawashangaa sana wabongo hamjaona kama disney wanapromote lugha ya kiswahili izidi kujulikana zaidi duniani ,pia imevaa jukumu la kuutangaza mlima Kilimanjaro na wanyama wanaopatikana east africa BURE kwa faida yao na ya east africa,baada ya sisi kushindwa kutangaza utalii wetu disney wamejitolea na fedha zinaweza kuja indirect kwa watalii kuongezeka kuja Tanzania na kenya
Tusizoee hela za direct tu,hata za indirect ni nyingi tu mbona tz na kenya watazipata
 
Hey
IMG-20190805-WA0012.jpeg
 
Unashangaa hakuna matata, ngoma ya "Nakuchambua kama Karanga" ya Saida Karoli ishatumika katika movie ya Hollywood na sidhani kama bi mkubwa alipewa chochote...
 
Ahahahahaha wabongo bana kwel tuna gombea neno wakat sisi tunatumia lugha yao yote kwenye elimu yetu daladala imetokana na lugha yao kwel unasema tuache kupigana na madini mgodini kwel serikali ipiganie neno hakuna matata alafu neno limekuwa registrated marekani kuwa wanatumia wao sasa kaguse unate nadhani hao jamaa wanajua akili za waafrica zikoje wametusoma kama wanavyosoma wanyama pori ndo mana wanatuweza sana kutumiliki
Mh! Unanichanganya kama hiyo picha yako. Sasa kama hilo neno ni lugha tu kama daladala kwa nini unasema wameli-register kuwa wanatumia wao?
 
hakuna matata
Disney waliikatia hatimiliki hilo neno,wakenya wakapambana lakini wapi.......
ndio basi tena....
 
Upuuzi mtupu kwahiyo kwahyo hayo maneno mawili yana hati miliki kwamba hayapaswi kutumika huko mbele?

mbona nyie mnatumia maneno kibao tu ya kiingereza, kifaransa na hata kispaniola na hakuna anayewasumbua kulipia
 
Back
Top Bottom