Sindano za makalioni; wale tusiopenda /waoga wa hii kitu tukutane hapa.

ukute nesi analibinya binya kabla ya kuchoma sindano..
huku anakwambia we kaka ivi hili tako unalipakaga mafuta kweli?
 
Kama zipi mkuu
1- mgonjwa anatakiwa awekwe sawa kisaikolojia na arelax misuli kabla ya kuchomwa sindano
2- kabla ya kumchoma mgonjwa sindano nesi anatakiwa kumtaarifu mgonjwa eneo sindano inapoenda kutua ili asikaze misuli ya sehemu hiyo ili kutosababisha maumivu yasiyo ya lazima
3- sindano inapochomwa inatakiwa kuwa angle 90° na iingizwe kwa haraka kidogo kiasi cha nusu kichuma cha sindano kuzuia kugusa mfupa; dawa inaposukumwa kwa syringe inatakiwa iingizwe taratibu mwilini tofauti na jinsi sindano ilivyo ingizwa mwilini ili kupunguza maumivu.
4- utoaji wa sindano unatakiwa itolewe mwilini ktk angle 90°kama jinsi ilivyoingizwa.
5- mgonjwa kupewa pole na kupongezwa kwa uvumilivu😀😀
 
1- mgonjwa anatakiwa awekwe sawa kisaikolojia na arelax misuli kabla ya kuchomwa sindano
2- kabla ya kumchoma mgonjwa sindano nesi anatakiwa kumtaarifu mgonjwa eneo sindano inapoenda kutua ili asikaze misuli ya sehemu hiyo ili kutosababisha maumivu yasiyo ya lazima
3- sindano inapochomwa inatakiwa kuwa angle 90° na iingizwe kwa haraka kidogo kiasi cha nusu kichuma cha sindano kuzuia kugusa mfupa; dawa inaposukumwa kwa syringe inatakiwa iingizwe taratibu mwilini tofauti na jinsi sindano ilivyo ingizwa mwilini ili kupunguza maumivu.
4- utoaji wa sindano unatakiwa itolewe mwilini ktk angle 90°kama jinsi ilivyoingizwa.
5- mgonjwa kupewa pole na kupongezwa kwa uvumilivu

Kwa sasa sina uvumilivu wa kulegeza kalio aisee nilikaza tu sindano ivunjike
Hongera kwa kunieleweshaa
 
Nipe vidonge mwezi mzima sio sindano...

Mara ya mwisho nakumbuka yule doctor alikuwa na huruma sana, anajua kubembelezaa ila ilikuwa ya mkononi
 
Yupo mmoja pale KAIRUKI... alinchoma sindano ya TACKLE.... yaani mpk anamaliza kupress dawa mm sina habari...
Kuna manesi wanakuchoma sindano huku wakisindikiza na maneno mazuuri yenye mvuto "pooooleeee"...... Lakini kuna wale uso wa mbuzi na akikuchoma sindano maumivu yake hayaelezeki halafu inachukua muda sana kupoa
 
Back
Top Bottom