Sina muda mrefu ,nitamuomba msamaha Jose Mourinho

marcoveratti

JF-Expert Member
Sep 21, 2017
967
1,693
Wanasema wanataka kujenga timu,sawa wanataka kuijenga timu kwa namna ipi . Timu bora inatengenezwa kwa kutumia wachezaji bora ,haijalishi wawe wenye majina na wasio na majina . Ni lazima upate wachezaji wenye viwango vya hali ya juu kufanikisha jambo lako.

Kiuhalisia kwa nyakati tulizonazo sasa kwenye Dunia ya soka ,wachezaji wenye vipaji vikubwa wanapatikana kwa uchache sana na kwa gharama kubwa , yaani kwa ufupi vipaji halisi vimekua adimu .

Na ikitokea vikapatikana, vilabu vingi hutolea macho klabu inayonekana kuwa na wachezji hao ,mfano ni Monaco au Southampton , kisha Ajax msimu huu .. Wanaweza kuuza zaidi ya wachezaji 6 kwenye kikosi chao cha kwanza .

Ili kuendana na matakwa ya kasi katika usajili ,Vilabu vyenye kujua maana ya ununuzi wa wachezaji imara na vijana huwa wanawahi kuingia nao mikataba hata kama atakua bado anacheza kwenye timu yake.

Ukiwangalia Barcelona ni timu yenye wachezaji imara ,yaaani imekamirika lakini mpaka sasa imeshasajili wachezji mahili wawili (Antoine Griezman na De Jong ) ili kuongeza nguvu kwenye kikosi chao . Hii ndio maana halisi ya kutengeneza timu kwa nyakati hizi ,Vijana wenye vipaji ni adimu ,ili uwaapate ni lazima uwe shap kufanya usajili na kuwachukua .

Mfano Klabu ya Real Madrid ,Venisius Jr kachukuliwa kwa pesa kibao ,wao sio wajinga .. Mchezaji kama Ibrahim Diaz ni moja kati ya wachezaji wacheche wenye vipaji, ambao sio rahisi kupatikana; lakini watu wanakata mpunga na wanasajili .

Uongozi wa Madridi wakikwambia wapo kwenye harakati ya kuijenga timu mpya,lazima utakubaliana nao kwa sababu wanachokifanya kinaonaneka ,Wanafanya vitu kwa vitendo na sio maneno .

Hii ni tofauti na Manchester United wanakwambia wanataka kutengeneza timu upya ,lakini mpaka sasa hakuna kinachofanyika ,Hakuna ingizo lolote la wachezaji mahili walionunuliwa. Wenye vipaji ndio hao sokoni wanazidi kuisha .

Sasa unajiuliza hiyo timu inayotaka kutengenezwa itatengenezwa kwa muundo upi ,au wanataka kutumia Ciment . Timu inatengenezwa na wachezaji mahili ,ili kuwapata unahitaji uharaka zaidi kwa sababu sio wewe mwenye malengo peke yako . Wakina Psg nao wanatawaka (Nao wanamalengo ) Na wameshamchukua Ander Herrera, anayeenda kusaidizana na Marco Verati .

Bayern Munich nao wanaitaji kuunda timu yao Upaya, wanahitaji wachezaji imara vijana,wanataka kuingia sokoni kama hawana akili vizuri ,Manchester city ndio hao wameshampa Pep Guardiola ndani takribani £200M za usajili wa msimu ujao ,utashangaa wamemchukua Diabara .

Wenzako wanaweka fungu la usajili mapema ,ili wawahi kuchukua wachezaji mapema ,wanawahi sokoni mapema ,Manchester United wanatenga fungo la kuwaongeza mkataba wakina Smalling . Siku wakikumbuka kwenda sokoni watakuta kuna mabondo samaki wameshanunuliwa .

Kwa hali hii ya maneno bila vitendo washabiki wa Manchester United wajiandae kuwaona wakina Fellain wengine ,maana waswahili wanamsemo wao mmoja ,"kosakosa ya samaki chukua hata kaa". Hivi kule championship kunaweza kuwa na mchezaji mahili mwenye kipaji na mpaka akafikisha umri wa miaka 23 na vilabu vikubwa visiwe vimemuona ..?

Kuna mtu atakwambia wanaweza kutumia wachezaji wa academy ,sawa ila umeshajiuliza academi hio inaweza kutoa wachezaji wenye vipaji na kuja kuwa washindani . Au inaweza kuleta wakina Lingard wengine ..?? Tatizo sio kuunda timu upya ,Je umejiandaje kwenye kuiunda timu hiyo .

Timu inaundwa na wachezaji ,lakini sio kila wachezaji wanaweza kuunda timu bora ,timu bora inaundwa na wachezaji wenye ufanisi wa hali ya juu .

Kuna wakati unaifikiria hii klabu (Unatamani hata kulia )muda mwingine unawaza hivi hii timu inauongozi madhubuti kweli ,inamaskauti wenye sifa zinazoendana na matakwa ya soka la kisasa ..? Na kama wapo wanafanya kazi gani .?

Kama wataendelea na maneno ya mdomoni kama walionao sasa, binafsi watanifanya nimuombe radhi jose Mourinho. Inawezekana tatizo halikua kwake ,uongozi wa Manchester United ni wanasiasa wafanya biashara .

Daima usitegemee maendeleo .
 
Wanasema wanataka kujenga timu,sawa wanataka kuijenga timu kwa namna ipi . Timu bora inatengenezwa kwa kutumia wachezaji bora ,haijalishi wawe wenye majina na wasio na majina . Ni lazima upate wachezaji wenye viwango vya hali ya juu kufanikisha jambo lako.

Kiuhalisia kwa nyakati tulizonazo sasa kwenye Dunia ya soka ,wachezaji wenye vipaji vikubwa wanapatikana kwa uchache sana na kwa gharama kubwa , yaani kwa ufupi vipaji halisi vimekua adimu .

Na ikitokea vikapatikana, vilabu vingi hutolea macho klabu inayonekana kuwa na wachezji hao ,mfano ni Monaco au Southampton , kisha Ajax msimu huu .. Wanaweza kuuza zaidi ya wachezaji 6 kwenye kikosi chao cha kwanza .

Ili kuendana na matakwa ya kasi katika usajili ,Vilabu vyenye kujua maana ya ununuzi wa wachezaji imara na vijana huwa wanawahi kuingia nao mikataba hata kama atakua bado anacheza kwenye timu yake.

Ukiwangalia Barcelona ni timu yenye wachezaji imara ,yaaani imekamirika lakini mpaka sasa imeshasajili wachezji mahili wawili (Antoine Griezman na De Jong ) ili kuongeza nguvu kwenye kikosi chao . Hii ndio maana halisi ya kutengeneza timu kwa nyakati hizi ,Vijana wenye vipaji ni adimu ,ili uwaapate ni lazima uwe shap kufanya usajili na kuwachukua .

Mfano Klabu ya Real Madrid ,Venisius Jr kachukuliwa kwa pesa kibao ,wao sio wajinga .. Mchezaji kama Ibrahim Diaz ni moja kati ya wachezaji wacheche wenye vipaji, ambao sio rahisi kupatikana; lakini watu wanakata mpunga na wanasajili .

Uongozi wa Madridi wakikwambia wapo kwenye harakati ya kuijenga timu mpya,lazima utakubaliana nao kwa sababu wanachokifanya kinaonaneka ,Wanafanya vitu kwa vitendo na sio maneno .

Hii ni tofauti na Manchester United wanakwambia wanataka kutengeneza timu upya ,lakini mpaka sasa hakuna kinachofanyika ,Hakuna ingizo lolote la wachezaji mahili walionunuliwa. Wenye vipaji ndio hao sokoni wanazidi kuisha .

Sasa unajiuliza hiyo timu inayotaka kutengenezwa itatengenezwa kwa muundo upi ,au wanataka kutumia Ciment . Timu inatengenezwa na wachezaji mahili ,ili kuwapata unahitaji uharaka zaidi kwa sababu sio wewe mwenye malengo peke yako . Wakina Psg nao wanatawaka (Nao wanamalengo ) Na wameshamchukua Ander Herrera, anayeenda kusaidizana na Marco Verati .

Bayern Munich nao wanaitaji kuunda timu yao Upaya, wanahitaji wachezaji imara vijana,wanataka kuingia sokoni kama hawana akili vizuri ,Manchester city ndio hao wameshampa Pep Guardiola ndani takribani £200M za usajili wa msimu ujao ,utashangaa wamemchukua Diabara .

Wenzako wanaweka fungu la usajili mapema ,ili wawahi kuchukua wachezaji mapema ,wanawahi sokoni mapema ,Manchester United wanatenga fungo la kuwaongeza mkataba wakina Smalling . Siku wakikumbuka kwenda sokoni watakuta kuna mabondo samaki wameshanunuliwa .

Kwa hali hii ya maneno bila vitendo washabiki wa Manchester United wajiandae kuwaona wakina Fellain wengine ,maana waswahili wanamsemo wao mmoja ,"kosakosa ya samaki chukua hata kaa". Hivi kule championship kunaweza kuwa na mchezaji mahili mwenye kipaji na mpaka akafikisha umri wa miaka 23 na vilabu vikubwa visiwe vimemuona ..?

Kuna mtu atakwambia wanaweza kutumia wachezaji wa academy ,sawa ila umeshajiuliza academi hio inaweza kutoa wachezaji wenye vipaji na kuja kuwa washindani . Au inaweza kuleta wakina Lingard wengine ..?? Tatizo sio kuunda timu upya ,Je umejiandaje kwenye kuiunda timu hiyo .

Timu inaundwa na wachezaji ,lakini sio kila wachezaji wanaweza kuunda timu bora ,timu bora inaundwa na wachezaji wenye ufanisi wa hali ya juu .

Kuna wakati unaifikiria hii klabu (Unatamani hata kulia )muda mwingine unawaza hivi hii timu inauongozi madhubuti kweli ,inamaskauti wenye sifa zinazoendana na matakwa ya soka la kisasa ..? Na kama wapo wanafanya kazi gani .?

Kama wataendelea na maneno ya mdomoni kama walionao sasa, binafsi watanifanya nimuombe radhi jose Mourinho. Inawezekana tatizo halikua kwake ,uongozi wa Manchester United ni wanasiasa wafanya biashara .

Daima usitegemee maendeleo .
Timu iuzwe ndio ninachotaka mimi
 
Alipowaambia kuwa mafanikio makubwa kabisa aliyowahi kuyapata tangu aanze kufundisha mpira ilikuwa ni kuifanya Manchester United kushika nafasi ya pili mlimcheka.
 
Nilishasema toka mwanzo na narudia tena.
Jose mourinho mtakuja kumpigia magoti nyie mliokuwa mnamsena na kumponda.
Time will tell
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom