Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,955
- 22,133
MKUU wa Wilaya ya Maswa, James Yamungu, amesema kama Rais Jakaya Kikwete atamfukuza kazi kwa kumuunga mkono aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Vijijini, Albert Mnali, kwa kuwacharaza viboko walimu, yeye hatishiki, badala yake atarejea kijiji kwake lakini atasimamia alichokisema na wananchi ndiyo watakaoamua.
Yamungu alitoa kauli hiyo jana alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu tamko la Chama cha Walimu Tanzania (CWT) mkoani Shinyanga, kumtaka Rais Kikwete kumfukuza kazi Yamungu kwa kuunga mkono kitendo cha Mnali cha kuwachapa viboko walimu wa wilaya yake, kwa madai ya kushusha kiwango cha elimu.
Akizungumzia na Tanzania Daima jana kwa njia ya simu kutoka Maswa, Yamungu alisema yeye alitoa kauli hiyo kwa moyo mweupe kama raia wa Tanzania bila kuathiri jambo lolote kama ilivyoainishwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 18, inayoeleza uhuru wa kujieleza.
Alisema hata kama Rais Kikwete ataamua kumfukuza kazi kama alivyofanya kwa Mnali, kuhusu suala la kuwachapa viboko walimu, hatishiki kwani atakwenda kijiji kwao Songea lakini ameeleza ukweli na wananchi ndiyo watakaopembua mchele na pumba.
Hata kama Rais atanifukuza kazi kwa kumuunga mkono Mnali, nitakwenda kijijini kwetu huko Songea, lakini ukweli lazima uelezwe na wananchi ndiyo watakaotoa maamuzi ya kupembua pumba na mchele ni upi, alisema Yamungu.
Awali akizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, kulaani kauli ya Yamungu, Katibu wa CWT mkoani hapa, Emmanuel Samala, alisema ameshangazwa na kauli ya DC huyo ya kumpongeza Mnali kuwa ni shujaa kwa kuwachapa walimu.
Alisema Yamungu amelewa madaraka kiasi cha kumkosoa mkubwa wake wa kazi - Rais Kikwete - ambaye hakupendezwa na kitendo alichokifanya Mnali.
Ni wazi sasa kuwa Yamungu amelewa madaraka kiasi cha kumkosoa mkubwa wake (Rais Kikwete), kwa maamuzi aliyoyatoa dhidi ya kitendo alichofanya Mnali...nafikiri naye anapaswa kuchukuliwa hatua, alisema.
Kauli ya DC huyo ni ishara kuwa Rais Kikwete amekuwa akiwapa watu madaraka makubwa huku baadhi yao wakiwa hawana uwezo wa kuongoza, hali inayofanya kuwa na viongozi mizigo ndani ya serikali yake na kushindwa kuwahudumia wananchi na kusababisha migomo ya mara kwa mara.
Ifike mahali Rais Kikwete asitumie kigezo cha kumteua mtu kuwa kiongozi kwa sababu ya kuwa mwanajeshi, kwani walio wengi wamekuwa wakitumia vibaya madaraka yao na mfano ni katika Mkoa wa Shinyanga.
Hili liwe fundisho kwa Rais ili anapoteua watu wa kumsaidia asitumie kigezo cha mtu kuwa mwanajeshi, kwani kwa sasa wengi ni wakuu wa wilaya na baadhi wamekuwa wakitumia vibaya madaraka yao na mfano hai ni katika Mkoa wa Shinyanga, alisema.
Aliendelea kueleza kuwa hapendi kubishana na Yamungu, aliyezoea amri za kijeshi na kumtaka aende akajifunze taratibu na sheria zinazoongoza ajira ya walimu ili asiongelee mambo asiyoyajua na matokeo.
Katibu huyo wa CWT alisema chama hicho mkoani Shinyanga kimelaani kauli ya Yamungu na kumwomba Rais Kikwete kuchukua hatua kama alizochukua kwa aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Bukoba Vijijini, Mnali.
Kauli ya Yamungu ikiachwa inaweza kusababisha walimu waendelee kudhalilishwa na baadhi ya viongozi aina ya Mnali na Yamungu. Yamungu juzi wakati akifungua mkutano wa tatu wa Nyalikungu SACCOS mjini Maswa, alimpongeza Mnali aliyefukuzwa kazi na Rais Kikwete, baada ya kuwachapa walimu viboko na kumwita kuwa ni shujaa.
Alisema licha ya Mnali kufukuzwa kazi na Rais Kikwete, anabaki kuwa shujaa aliyekuwa akiwatetea Watanzania kuhusu suala la elimu.
Ndugu zangu pamoja na Rais kumfukuza kazi Mnali, wazazi katika wilaya ya Bukoba Vijijini pamoja na umma wa Watanzania wanamuunga mkono na kumwona kama shujaa ambaye ana uchungu na taifa letu hasa katika sekta ya elimu, alisema DC huyo.
Yamungu ambaye pia ni Katibu wa Wakuu wa Wilaya Tanzania Bara, alisema kitendo alichokifanya Mnali ni sawa na kauli aliyotoa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alipokuwa katika ziara mikoa ya Kanda ya Ziwa, baada ya kukerwa na vitendo vya baadhi ya watu wanaowaua walemavu wa ngozi (albino) na kutaka nao wauawe bila kujali sheria.
Klabu ya Wakuu wa Wilaya Tanzania Bara inasikitika kumpoteza mtu muhimu, kwani alikuwa mchapakazi mzuri na mambo aliyofanya wilayani Geita akiwa mkuu wa wilaya, ni mfano wa kuigwa kwani alihamasisha wananchi kujenga shule nyingi za sekondari na alifanikiwa.
Ni vizuri kwa wanachama wa chama hicho kuiga mfano huo wa kutetea mambo yaliyo na manufaa kwao, kwa ajili ya kuendeleza SACCOS hiyo na hatimaye kuwa benki kwa lengo la kuwainua kiuchumi.
Mnali aliamrisha kuchapwa viboko kwa walimu wa shule za msingi za wilaya yake ya Bukoba Vijijini, kwa kile alichodai kukithiri kwa utoro, uvivu na kusababisha wilaya hiyo kuwa ya mwisho katika matokeo ya mtihani wa Darasa la Saba.
Kutokana na kosa hilo, Rais Kikwete aliamua kumvua madaraka kwa madai kuwa alikiuka kanuni za utumishi wa umma na kulidhalilisha taifa, huku mwenyewe akijigamba kuwa
Yamungu alitoa kauli hiyo jana alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu tamko la Chama cha Walimu Tanzania (CWT) mkoani Shinyanga, kumtaka Rais Kikwete kumfukuza kazi Yamungu kwa kuunga mkono kitendo cha Mnali cha kuwachapa viboko walimu wa wilaya yake, kwa madai ya kushusha kiwango cha elimu.
Akizungumzia na Tanzania Daima jana kwa njia ya simu kutoka Maswa, Yamungu alisema yeye alitoa kauli hiyo kwa moyo mweupe kama raia wa Tanzania bila kuathiri jambo lolote kama ilivyoainishwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 18, inayoeleza uhuru wa kujieleza.
Alisema hata kama Rais Kikwete ataamua kumfukuza kazi kama alivyofanya kwa Mnali, kuhusu suala la kuwachapa viboko walimu, hatishiki kwani atakwenda kijiji kwao Songea lakini ameeleza ukweli na wananchi ndiyo watakaopembua mchele na pumba.
Hata kama Rais atanifukuza kazi kwa kumuunga mkono Mnali, nitakwenda kijijini kwetu huko Songea, lakini ukweli lazima uelezwe na wananchi ndiyo watakaotoa maamuzi ya kupembua pumba na mchele ni upi, alisema Yamungu.
Awali akizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, kulaani kauli ya Yamungu, Katibu wa CWT mkoani hapa, Emmanuel Samala, alisema ameshangazwa na kauli ya DC huyo ya kumpongeza Mnali kuwa ni shujaa kwa kuwachapa walimu.
Alisema Yamungu amelewa madaraka kiasi cha kumkosoa mkubwa wake wa kazi - Rais Kikwete - ambaye hakupendezwa na kitendo alichokifanya Mnali.
Ni wazi sasa kuwa Yamungu amelewa madaraka kiasi cha kumkosoa mkubwa wake (Rais Kikwete), kwa maamuzi aliyoyatoa dhidi ya kitendo alichofanya Mnali...nafikiri naye anapaswa kuchukuliwa hatua, alisema.
Kauli ya DC huyo ni ishara kuwa Rais Kikwete amekuwa akiwapa watu madaraka makubwa huku baadhi yao wakiwa hawana uwezo wa kuongoza, hali inayofanya kuwa na viongozi mizigo ndani ya serikali yake na kushindwa kuwahudumia wananchi na kusababisha migomo ya mara kwa mara.
Ifike mahali Rais Kikwete asitumie kigezo cha kumteua mtu kuwa kiongozi kwa sababu ya kuwa mwanajeshi, kwani walio wengi wamekuwa wakitumia vibaya madaraka yao na mfano ni katika Mkoa wa Shinyanga.
Hili liwe fundisho kwa Rais ili anapoteua watu wa kumsaidia asitumie kigezo cha mtu kuwa mwanajeshi, kwani kwa sasa wengi ni wakuu wa wilaya na baadhi wamekuwa wakitumia vibaya madaraka yao na mfano hai ni katika Mkoa wa Shinyanga, alisema.
Aliendelea kueleza kuwa hapendi kubishana na Yamungu, aliyezoea amri za kijeshi na kumtaka aende akajifunze taratibu na sheria zinazoongoza ajira ya walimu ili asiongelee mambo asiyoyajua na matokeo.
Katibu huyo wa CWT alisema chama hicho mkoani Shinyanga kimelaani kauli ya Yamungu na kumwomba Rais Kikwete kuchukua hatua kama alizochukua kwa aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Bukoba Vijijini, Mnali.
Kauli ya Yamungu ikiachwa inaweza kusababisha walimu waendelee kudhalilishwa na baadhi ya viongozi aina ya Mnali na Yamungu. Yamungu juzi wakati akifungua mkutano wa tatu wa Nyalikungu SACCOS mjini Maswa, alimpongeza Mnali aliyefukuzwa kazi na Rais Kikwete, baada ya kuwachapa walimu viboko na kumwita kuwa ni shujaa.
Alisema licha ya Mnali kufukuzwa kazi na Rais Kikwete, anabaki kuwa shujaa aliyekuwa akiwatetea Watanzania kuhusu suala la elimu.
Ndugu zangu pamoja na Rais kumfukuza kazi Mnali, wazazi katika wilaya ya Bukoba Vijijini pamoja na umma wa Watanzania wanamuunga mkono na kumwona kama shujaa ambaye ana uchungu na taifa letu hasa katika sekta ya elimu, alisema DC huyo.
Yamungu ambaye pia ni Katibu wa Wakuu wa Wilaya Tanzania Bara, alisema kitendo alichokifanya Mnali ni sawa na kauli aliyotoa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alipokuwa katika ziara mikoa ya Kanda ya Ziwa, baada ya kukerwa na vitendo vya baadhi ya watu wanaowaua walemavu wa ngozi (albino) na kutaka nao wauawe bila kujali sheria.
Klabu ya Wakuu wa Wilaya Tanzania Bara inasikitika kumpoteza mtu muhimu, kwani alikuwa mchapakazi mzuri na mambo aliyofanya wilayani Geita akiwa mkuu wa wilaya, ni mfano wa kuigwa kwani alihamasisha wananchi kujenga shule nyingi za sekondari na alifanikiwa.
Ni vizuri kwa wanachama wa chama hicho kuiga mfano huo wa kutetea mambo yaliyo na manufaa kwao, kwa ajili ya kuendeleza SACCOS hiyo na hatimaye kuwa benki kwa lengo la kuwainua kiuchumi.
Mnali aliamrisha kuchapwa viboko kwa walimu wa shule za msingi za wilaya yake ya Bukoba Vijijini, kwa kile alichodai kukithiri kwa utoro, uvivu na kusababisha wilaya hiyo kuwa ya mwisho katika matokeo ya mtihani wa Darasa la Saba.
Kutokana na kosa hilo, Rais Kikwete aliamua kumvua madaraka kwa madai kuwa alikiuka kanuni za utumishi wa umma na kulidhalilisha taifa, huku mwenyewe akijigamba kuwa