Simulizi za ndoto toka kwa babu

Malupelupe

Member
Oct 28, 2012
55
13
Babu yangu aliwahi kunisimulia ndoto yake kuwa,katika kisiwa cha Donge waliishi wanyama na viumbe wengine walioshirikiana sana kwa kila jambo.Mfalme wa kisiwa hicho aliiamini kuwa kila kiumbe amepewa kipqji cha kufanya jambo.

Sikumoja Mfalme aliitisha mkutano mkubwa na kutaka kila kiumbe abuni na.kufanya jambo ambalo litakuwa na manufaa kwa kisiwa hicho.Ajabu sana,wanyama na viumbe wengine walikataa kufanya chochote nakulazimika kuhamia kisiwa jirani cha Ngewe.Waliamini kuwa kisiwa cha Ngewe ndicho bora zaidi japo kulionekana kuwa na neema za kusimuliwa tu,kamavile uhuru wakuzaliana,vyakula visivyo isha,na manoti ya kuokota kwa kila hatua kiumbe apigayo.

Maisha ya kisiwa cha Ngewe yaliwachosha ndani ya muda mfupi sana na hata kutamani tena kurudi walipo toka.Walipo kumbuka safari ndefu ya miguu walokwisha tembea,hawakutamani hata kugeuka nyuma
Walibaki na sintofahamu iliyo waumiza kwa kila pigo la sekunde iliyopita.

Mwisho wa simulizi ya ndoto yake,Babu aliniambia nisiwe nasimulia ndoto mbaya.Kwani ukiota wachawi wamekutembelea na kukusulubu usiku kucha na kisha ukawabaini na kusema,watakudhuru,ama watakuchukua mzimamzima na kukupeleka kuzimu.Huko watakulisha nyama za viumbe usiyo wajua na kukunywesha maji yasiyo fahamika.

Wakuu tuendelee kukaa kimya mara tuotapo ndoto mbaya ili tuwaenzi WAHENGA au tuwe tunasimulia ndoto zote nzuri na mbaya
ili twende na dunia?karibu uchangie simulizi hii toka kwa babu.
 
Mimi Nimekuelewa

Ingawa nina hakika hakuna aliyekuelewa hata mmoja

Nikiwemo mimi!
 
Hapo kabla mliishi nchi ambayo haikuwa ikiwabana, ukaja uchaguzi mkuu mkashindwa kufanya uchaguzi sahihi, mkakaa mkisubiri maisha mazuri bila kufanya kazi sasa imeshindikana. Mnaishi ugenini, yaani zama mpya, huku mkisahau kwamba nyie ndio mlifanya uchaguzi. Na sasa hamuwezi kurudi nyuma kwa kuwa mliyataka wenyewe. Mnaota na mnataka kupiga kelele dhidi ya utawala wakati ni zao lenu, kaeni kimya mtashughulikiwa. Mwenye masikio na asikie.

Pangu Pakavu
 
Hapo kabla mliishi nchi ambayo haikuwa ikiwabana, ukaja uchaguzi mkuu mkashindwa kufanya uchaguzi sahihi, mkakaa mkisubiri maisha mazuri bila kufanya kazi sasa imeshindikana. Mnaishi ugenini, yaani zama mpya, huku mkisahau kwamba nyie ndio mlifanya uchaguzi. Na sasa hamuwezi kurudi nyuma kwa kuwa mliyataka wenyewe. Mnaota na mnataka kupiga kelele dhidi ya utawala wakati ni zao lenu, kaeni kimya mtashughulikiwa. Mwenye masikio na asikie.

Pangu Pakavu
hahahaaaaa!
 

Similar Discussions

2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom