Simulizi za Kusisimua: Nyerere alipoingiwa huruma Mwana-TANU Mwenzake kukosa Nauli...

Kaka asante kwa Reply nzuri juu ya bandiko hapo juu, na mimi niseme hivi, mleta bandiko ameanza vizuri sana kwa kuelezea namna mwasisi wa taifa hili alivyokuwa na upeo mpana na wa mbele sana katika kupambanua mambo, ubinafsi haukuwa sehemu yake, upendeleo ulikuwepo na kuwatanguliza wengine alikuweka mbele hakuwaacha nyuma Watu wote waliokuwa chachu ya uhuru wa nchi yetu,

Ila alikuwa na akili sana yakujua wapi ni muweke nani na wapi nisimweke, ukitaka kuangalia kwa undani sana wanaharakati wote walioasisi uhuru wa nchi hii familia zao hazijabeba Legacy walioacha wazazi wao hata familia ya Nyerere yenyewe haijafanikiwa kwenye hili, nadhani nikwasababu ya filosofi iliyokuwepo wakati ule ambayo ilibebwa na kufuatiliwa vizur na wazazi wao, imebadilika sana kiasi hawakuweza kuendana na mabadiliko....

Pia viongozi wengi waliofuta katika utaawala wa Tanzania ubinafsi, kujipendeza, madili na ufisadi vimetawala hawakumbuki mtu Ila mfumo uliopo. Ndio maana matabaka na kubaguana Ndio moto unaotutafuna kimyakimya. Bado nauhusudu namna ya utaawala na approach aliyokuwa anaitumia Mwalimu katika kuyakabili matatizo na kutatua changamoto na namna alivyokuwa akiyaangalia mambo

Mungu adumishe Uhuru wa Tanzania katika Amani, umoja na Ushirikiano thabiti na madhubuti. Amen
Barikiwa sana mkuu,umenena yaliyo ya kweli.Mungu ibariki Tanzania.
 
Iparamasa,
Leo nilikuwa Radio Kheri mubashara nikifanya Kipindi Maalum
cha Uhuru wa Tanganyika:

Sikiza kipindi hapo chini:
Mohamed Said Salum | Facebook
TEWA SAID TEWA MEMBER WA ''WEDNESDAY TEA CLUB,'' TAA, MUASISI WA TANU, RAIS WA EAMWS, WAZIRI SERIKALI YA KWANZA, BALOZI, MBUNGE NA KIONGOZI WA WAISLAM WA TANGANYIKA
Anaandika mwandishi wa historia Mohammed Said

Picha hizi (hapo chini)zinatoka katika Maktaba ya Said Tewa mtoto wa marehemu Tewa Said Tewa ambae kwa miaka mingi amekuwa akiishi Denmark. Said anasema ameniletea picha hizi baada ya kuona juhudi zangu katika kuhifadhi historia ya Tanzania na viongozi wake baba yake akiwa mmoja wao iliyokuwa karibu ipotee. Hayo maandishi, ‘’caption,’’ katika baadhi ya picha ni mwandiko wake mwenyewe Mzee Tewa. Picha nilizopokea ni nyingi sana zikimwonyesha Tewa Said Tewa katika mengi lakini nimeona nichukue hizi chache ambacho zitamuunganisha yeye na matokeo muhimu zaidi katika historia ya Tanzania na katika nafasi yake kama kiongozi wa Waislam akiwa Rais wa East African Muslim Welfare Society upande wa Tanzania. Binafsi nimejifunza mengi kutoka kwa Mzee Tewa tukiwa tumekaa sisi wawili tu nyumbani kwake Magomeni Mikumi akinihadithia historia ya uhuru wa Tanganyika.

Msikilize Mzee Tewa:

Tewa Said anakumbuka siku kabla ya uchaguzi pale Ukumbi wa Arnatouglo, Abdulwahid alikwenda nyumbani kwake jioni. Wakati huo Tewa alikuwa akikaa mtaa huo huo wa Aggrey na Swahili, si mbali sana kutoka nyumbani kwa Abdulwahid. Abdulwahid alimwambia Tewa maneno haya kuhusu mabadiliko ya uongozi ambayo waliamua kuyafanya katika TAA:

‘’Tewa, kesho tunakwenda kumpa huyu mtu, Nyerere, mamlaka ya kuendesha nchi hii. Kuanzia hapo, mara tu tutakapomchagua kutuongoza hakuna namna tena ya kumnyangíanya madaraka tuliyompa. Hatumfahamu vizuri sana lakini natumaini kila kitu kitakwenda sawa.’’

Mengi kuhusu Tewa Said Tewa unaweza kuyasoma hapo chini:
Mohamed Said: Tewa Said Tewa Mmoja wa Waasisi wa TANU 1954
 
Nyie wa
Iparamasa,
Leo nilikuwa Radio Kheri mubashara nikifanya Kipindi Maalum
cha Uhuru wa Tanganyika:

Sikiza kipindi hapo chini:
Mohamed Said Salum | Facebook
Nyie wazee ndio fursa ziliwapitia pemben mmebaki na chuki zenu za kimaisha mnamtafuta mtu wa kumwangushia lawama. Watu Kama nyie hupati taabu kuwajua angalia tu vitu anavyomiliki ndio utajua maneno yake yamefunikwa na nini
 
Kwa kawaida historia haipatikani katika nyaraka moja.Mara nyingi historia hujengwa na mkusanyiko wa nyaraka nyingi tofautitofauti.

Hawa wazee wengine tumewafahamu kupitia maandiko mbalimbalia ambayo kwa pamoja yanajenga historia ya nchi yetu.

Sasa kama wameandikwa na historia inawatambua.Tatizo liko wapi!

Leo hii hata familia ya Nyerere haisikiki kwa kuwa hakutaka kuwa mbinafsi na kujipendelea yeye na familia yake eti kisa alipigania Uhuru na kuwa Rais wa kwanza.

Don,
Hiuna taarifa kuhusu historia ya TANU na kitendawili kilichokuja baada ya
uhuru kupatikana.

Ghafla pakazuka jambo kuwa TAA hakikuwa chama cha siasa bali ni cha
starehe.

Ghafla pakawa na njama za kufuta historia ya African Association na kuleta
historia mpya inayoanza na Nyerere.

Bahati nzuri wenye African Association yao na TANU yao walikuwa na nyaraka
zote.

Walifutwa katika historia rasmi na wakawa kwa miaka mingi hawatajwi popote
hadi nilipoanza kuandika historia hii kwanza kwa njia za makala kisha nikaandika
kitabu.

Ndiyo wengi kwa mara ya kwanza wakasikia majina ya Mshume Kiyate, Sheikh
Suleiman Takadir, Mufti Sheikh Hassan bin Amir....

Na hawakusoma majina tu bali walisoma yale waliyofanya katika kuunda TANU
na kuwaleta Watanganyika pamoja
Nyie wa

Nyie wazee ndio fursa ziliwapitia pemben mmebaki na chuki zenu za kimaisha mnamtafuta mtu wa kumwangushia lawama. Watu Kama nyie hupati taabu kuwajua angalia tu vitu anavyomiliki ndio utajua maneno yake yamefunikwa na nini
Kitali,
Hakuna chuki ni kumbukumbu tu.
 
Mwalimu aliwapurge out comrades waliofanikisha Uhuru na kutuwekea kina yes man! . Ndiyo maana labda tumekuwa masikini kwa muda mrefu kwa sababu wale waliowekwa na Mwalimu kwa kigezo cha kumuogopa na kumtii hawakuwa na Uzalendo kama wale Makamanda wazalendo waliomng'oa Mkoloni!
 
Kwa hiyo hao wazee walipigania Uhuru kwa maslahi yao binafsi na sio nchi ?

Mbona Nyerere kafa maskini, isingekuwa Jeshi kumjengea nyumba angekufa kama mtu masikini mwingine.

Nepotism ndiyo inaharibu nchi hii ,Nyerere angekumbatia kundi dogo la watu eti kisa walipigania Uhuru nchi hii ingekuwa na matabaka ya koo za watawala na watwana.
Nyerere kafa maskin,nani kasema? Familia yake inalindwa na kulishwa hadi kesho,ya Sykes au Dossa umeisikia ikipewa hzo huduma?Kumsikiliza Dossa na kumpa fursa stahiki ndo nepotism? Watu wanalipwa asilimia themanin ya mshahara wa waziri mkuu leo bila mchango wa maana kwa taifa eg,Pinda,alifanya nini zaid ya kulia lia tuu!
 
We ni chuki tu zinakusumbua na watu Aina yenu ni wale watu ambao walishapoteza muda wao so wamejikuta hawana uwezo wa Kubadilisha hali zao. Mimi kosa kubwa ninaloliona kwa hawa walalamikaji ni kuwa ni kweli walipigania uhuru lakin lengo lao ilikuwa baada ya kushinda walitaka kupewa chochote kitu au kutunzwa au kuwekwa mezan muda wote tabia za kiswahiliswahili hebu nenden Kenya wale walioanzisha mapambano ya uhuru akina dedan kimathi uniambie Kama kuna jamii yake inakumbukwa. Unalia watoto kukumbukwa Kwan hii ni nchi ya kifalme au Kama hujawaandaa watoto ulitaka wapewe kaz tu Kama zawadi polen. Mi Nadhan unachojaribu kutuambia hapa ni kuwa Uislam ulihusika Sana kuleta uhuru umesahau hata Kama ndivyo kuleta uhuru na kuudumisha ni vitu viwili tofauti.
 
We ni chuki tu zinakusumbua na watu Aina yenu ni wale watu ambao walishapoteza muda wao so wamejikuta hawana uwezo wa Kubadilisha hali zao. Mimi kosa kubwa ninaloliona kwa hawa walalamikaji ni kuwa ni kweli walipigania uhuru lakin lengo lao ilikuwa baada ya kushinda walitaka kupewa chochote kitu au kutunzwa au kuwekwa mezan muda wote tabia za kiswahiliswahili hebu nenden Kenya wale walioanzisha mapambano ya uhuru akina dedan kimathi uniambie Kama kuna jamii yake inakumbukwa. Unalia watoto kukumbukwa Kwan hii ni nchi ya kifalme au Kama hujawaandaa watoto ulitaka wapewe kaz tu Kama zawadi polen. Mi Nadhan unachojaribu kutuambia hapa ni kuwa Uislam ulihusika Sana kuleta uhuru umesahau hata Kama ndivyo kuleta uhuru na kuudumisha ni vitu viwili tofauti.
Umeanza kwa kunishambulia na kunihusisha na chuki na kupoteza mwelekeo.Umenihusisha na dini,je,nikikuuliza mimi dini gani unaweza kunijibu? Mimi,ni mtu toka bara na sina maslahi na niyasemayo sema nataka ukweli ujulikane.Mkuu nikwambie,hata kama hatukubaliani lakini tusizibane midomo,acha kila mtu aseme.Nimalizie kwa kusema,serikali ilitakiwa ifanye kitu kwa waasisi hawa,hata kuanzisha foundation kwa jina lao na kisha ikasaidia watu kutoka maeneo mbalimbali imeshindikana? Ni ya Nyerere tuu,na ipo kimaslahi binafsi tuuu.
 
Nilitakiwa nisisimuke kwa kipi kwa mfano?

Au hii ya habari ya kwamba Nyerere alifisidi nchi kiasi cha kuwa hata wale waliokuwa matajiri enzi za Mkoloni wamegeuka mafukara wa kutupwa chini ya utawala wake?

Na hilo nalo halikunisisimua. Limenisikitisha
 
We ni chuki tu zinakusumbua na watu Aina yenu ni wale watu ambao walishapoteza muda wao so wamejikuta hawana uwezo wa Kubadilisha hali zao. Mimi kosa kubwa ninaloliona kwa hawa walalamikaji ni kuwa ni kweli walipigania uhuru lakin lengo lao ilikuwa baada ya kushinda walitaka kupewa chochote kitu au kutunzwa au kuwekwa mezan muda wote tabia za kiswahiliswahili hebu nenden Kenya wale walioanzisha mapambano ya uhuru akina dedan kimathi uniambie Kama kuna jamii yake inakumbukwa. Unalia watoto kukumbukwa Kwan hii ni nchi ya kifalme au Kama hujawaandaa watoto ulitaka wapewe kaz tu Kama zawadi polen. Mi Nadhan unachojaribu kutuambia hapa ni kuwa Uislam ulihusika Sana kuleta uhuru umesahau hata Kama ndivyo kuleta uhuru na kuudumisha ni vitu viwili tofauti.

sasa kuna mtu alipigania uhuru ili aje awe irrelevant baada ya uhuru?
wewe unaweza kujitoa kwa hali, jasho na damu then usionje ujira wa juhudi zako?

kama ingekuwa hivyo mbona yeye Nyerere baada ya kustaafu aliendelea kupata priviledge za kiserikali?
 
Nilitakiwa nisisimuke kwa kipi kwa mfano?

Au hii ya habari ya kwamba Nyerere alifisidi nchi kiasi cha kuwa hata wale waliokuwa matajiri enzi za Mkoloni wamegeuka mafukara wa kutupwa chini ya utawala wake?

Na hilo nalo halikunisisimua. Limenisikitisha

Sasssy, kuna namna nyingi za kusisimka! Ndio maana tunasema mwanadamu hata akikutana na simba anaweza kusisimka!
 
Balibabambonahi,
Asante, uko sahihi, na moja ya shida ya baadhi ya wachangiaji ni kukurupuka. Baadhi pia huona baya kwa kila kinachoandikwa na mtu wanayemchukia. Hao wapo mpaka mwisho wa dunia.
Maggid
maggid una tabia ya kueleza mambo mengi amabyo sio kweli hata kule facebook ulieleza historia ya abood jumbe ukaumbuliwa ttzo unapenda kujifanya nguli wa kila kitu historia ni jambo adhimu angalia hapa unaleta jambo kuhusu chief kunambi kumbe sio kweli
 
Nyerere kafa maskin,nani kasema? Familia yake inalindwa na kulishwa hadi kesho,ya Sykes au Dossa umeisikia ikipewa hzo huduma?Kumsikiliza Dossa na kumpa fursa stahiki ndo nepotism? Watu wanalipwa asilimia themanin ya mshahara wa waziri mkuu leo bila mchango wa maana kwa taifa eg,Pinda,alifanya nini zaid ya kulia lia tuu!
Sasa hizo nadhani ni chuki binafsi,hujui Pinda alikuwa nani nchi hii!!??Pinda analipwa kwa mujibu wa Sheria na Nyerere alikuwa Rais wa nchi hii.Yaani wewe ulitaka wagimbea Uhuru wote wawe marais au ulitaka wawe wanalipwa mshara.

Acheni propaganda ,nchi hii imekomblewa kwa harakati za maelfu ya watu na sio tu hao wachache ambao ninyi mnawapigania kwa kigezo cha dini zao.

Hao akina Sykes na Nyerere sio watu pekee walipigania Uhuru wa nchi hii.Hao walikuwa viongozi tu lakini kuna wengine pia walipata madhara mengine mbali na kifirisika.

Hata leo hii CHADEMA ikitwaa madaraka akina Mbowe watasomeka kwenye historia lakini vijana walipigwa mabomu Arusha wanaweza wasitajwe japo wamemwaga damu kupigania Demokrasia .Kuna watu leo hii wanazihakiwa kuwa "wanywa viroba" na bodaboda lakini ndio kundi kubwa lenye hamasa katika kupigania demokrasia.

Kwa hiyo tukisema kila aliyepigania Uhuru wa nchi hii wapewe heshima sawa hata Mimi na yule tunaweza kutaja babu zetu ambao nao walichangia mapambano ya Uhuru.tuache hisia potofu za kuona tunatengwa ilihali historia inawatambua wazee hao,labda kama walitegemea madaraka na kuwa first class citizens kitu ambacho sio sahihi katika kujenga nchi yenye usawa.
 
sasa kuna mtu alipigania uhuru ili aje awe irrelevant baada ya uhuru?
wewe unaweza kujitoa kwa hali, jasho na damu then usionje ujira wa juhudi zako?

kama ingekuwa hivyo mbona yeye Nyerere baada ya kustaafu aliendelea kupata priviledge za kiserikali?
Kama hilo ndio lengo lao wape Pole. Mwambie nchi hii kila mtu alijitolea kwaajili uhuru waache ubinafs Kama walikuwa wanatafuta uhuru wao ningewatetea lakin Kama walimaanisha uhuru wa nchi nadhan wamepteza Raman hao. Ni sawa na mimi eti ukute namsomesha mtoto eti ili aje kunisaidia hayo ni mawazo mfu Msomeshe mtoto ili aje kupambana na dunia yao. Hawa wazee ndio wamebaki kulalamika mpaka wamekufa bila kuwaandaa watoto matokeo yake watoto wamekuja kuuza nyumba zote walizoacha pale kkoo
 
Kama hilo ndio lengo lao wape Pole. Mwambie nchi hii kila mtu alijitolea kwaajili uhuru waache ubinafs Kama walikuwa wanatafuta uhuru wao ningewatetea lakin Kama walimaanisha uhuru wa nchi nadhan wamepteza Raman hao. Ni sawa na mimi eti ukute namsomesha mtoto eti ili aje kunisaidia hayo ni mawazo mfu Msomeshe mtoto ili aje kupambana na dunia yao. Hawa wazee ndio wamebaki kulalamika mpaka wamekufa bila kuwaandaa watoto matokeo yake watoto wamekuja kuuza nyumba zote walizoacha pale kkoo

Wengine walikuwa wakiwaambia waumini wao kuwa tii mamlaka !
tahamaki ghafla tulivyopata uhuru wao ndo wakashika hatamu
 
Sasa hizo nadhani ni chuki binafsi,hujui Pinda alikuwa nani nchi hii!!??Pinda analipwa kwa mujibu wa Sheria na Nyerere alikuwa Rais wa nchi hii.Yaani wewe ulitaka wagimbea Uhuru wote wawe marais au ulitaka wawe wanalipwa mshara.

Acheni propaganda ,nchi hii imekomblewa kwa harakati za maelfu ya watu na sio tu hao wachache ambao ninyi mnawapigania kwa kigezo cha dini zao.

Hao akina Sykes na Nyerere sio watu pekee walipigania Uhuru wa nchi hii.Hao walikuwa viongozi tu lakini kuna wengine pia walipata madhara mengine mbali na kifirisika.

Hata leo hii CHADEMA ikitwaa madaraka akina Mbowe watasomeka kwenye historia lakini vijana walipigwa mabomu Arusha wanaweza wasitajwe japo wamemwaga damu kupigania Demokrasia .Kuna watu leo hii wanazihakiwa kuwa "wanywa viroba" na bodaboda lakini ndio kundi kubwa lenye hamasa katika kupigania demokrasia.

Kwa hiyo tukisema kila aliyepigania Uhuru wa nchi hii wapewe heshima sawa hata Mimi na yule tunaweza kutaja babu zetu ambao nao walichangia mapambano ya Uhuru.tuache hisia potofu za kuona tunatengwa ilihali historia inawatambua wazee hao,labda kama walitegemea madaraka na kuwa first class citizens kitu ambacho sio sahihi katika kujenga nchi yenye usawa.
Hivi hili swala la viongozi wastaafu kulipwa asilimia 80 halina kikomo! Mbona uraisi una kikomo?
Inawezekanaje mtu kulipwa pasipo kufanya kazi?
Anyway, ninachojua ni kuwa kuna watu wameifanyia hii nchi makubwa kuliko hawa wanaolipws na hawalipwi chochote baada ya kustaafu.
 
Mkuu unamaanisha historia ipi ?maana watz wengi tunawajua hao watu akina Dosa ,Sykes, Aziz n.k kama wapigania Uhuru Wa nchi hii.Je, labda wewe ungependa waandikweje ?

Umesema hao watoto wa wapigania Uhuru kama akina Bibi Titi ,Kambona hawasikiki.Je, ulitaka wasikike vipi? Wawe magavana ,mawaziri au ?Mkuu, hii nchi ni ya watanzania wote ,Fanya bidii tafuta fursa utasikika tu.Au mkuu ungependa labda wapewe vyeo vya bure bila jitihada kwa kuwaenzi baba/mama zao ?

Kama ulitaka hivyo,utakuwa umepotoka hatuwezi kuijenga nchi yenye usawa ikiwa tutawapendelea watu kwa majina yao/koo zao.Tukifanya hivyo tutatengeneza koo za watawala na koo za watwana.

Asante.
Umenena kweli hii nchi si ya kifalme, watoto wengi wa viongozi na matajiri wanakuwa wazembe na wavuta unga hakuna juhudi yeyote hata ktk elimu wapewe tu eti babu yake au mdogo wake na babu alikuwa mpigania uhuru. Ubinafsi huo walifanya kazi kwa uzalendo kwa nchi yao acheni ubinafsi na udini. Jitihada zako binafsi ndy njia pekee ya kufanya vizuri kuna wengine waimba singeli, haki bin haki
 
maggid una tabia ya kueleza mambo mengi amabyo sio kweli hata kule facebook ulieleza historia ya abood jumbe ukaumbuliwa ttzo unapenda kujifanya nguli wa kila kitu historia ni jambo adhimu angalia hapa unaleta jambo kuhusu chief kunambi kumbe sio kweli

Bafa,
Ahasante, lakini nawe, kama kawaida, unaishia kusema sio kweli bila kusema la kweli ni lipi na kwa ushahidi gani.
 
Bafa,
Ahasante, lakini nawe, kama kawaida, unaishia kusema sio kweli bila kusema la kweli ni lipi na kwa ushahidi gani.
Mwenyekiti nakufuatilia sana makala zako ww ni mwandishi nguli kwa hyo kwenye historia sensitive kama hizi ni wajibu kujiridhisha sio kukusanya kukusanya kama barza
 
Back
Top Bottom