Simulizi Ya Kweli:Nilimuoa Jini Nikamsaliti

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Apr 29, 2016
20,744
25,438
d865f1098164609b52c9a6f55edbbdc7.jpg

SEHEMU YA 01
SAA nane usiku jini Nargis aliamka na kukaa kitako akiliangalia tumbo lake lililokuwa kubwa na kubakiza siku chache za kujifungua, alilipapasa taratibu kwa kuzungusha mkono pembeni.
Aliyahamisha macho yake toka kwenye tumbo lake na kumuangalia mumewe Thabit aliyekuwa katikati ya usingizi. Aliinama na kumbusu shavuni na kurudi kukaa kitako. Alijikuta akibubujikwa na machozi bila kizuizi.
Siku ile ilikuwa ngumu maishani kwake kutengana na mumewe waliyezoeana na kuishi kama mke na mume kwa muda mrefu. Pamoja na kuwa jini lakini alimpenda sana mwanaume yule kuliko kitu chochote chini ya jua na maji.
Alikumbuka mpaka kufika pale, alimpigania Thabit kwa hali na mali kwa muda mrefu kwa vita kali na nzito toka kwa wanadamu na majini wenzake waliyoyatamani maisha ya mpenzi wake.
Ili kuhakikisha anamlinda mpenzi wake iliyagharimu maisha ya wanadamu na majini kwa kuwaua.
Aliweza kuishi na mumewe maisha ya raha mustarehe baada ya kutokwa na jasho na machozi ya damu. Matunda ya kwanza yalikuwa kupata ujauzito alioutamani usiku na mchana kwa kuamini ile ndiyo sababu ya kuishi naye milele.
Baada ya kupata ujauzito wazazi wake walimweleza arudi haraka ujinini akailee mimba yake ili wanadamu wasiichezee. Lakini aliwaomba sana abakie duniani mpaka ikibakia wiki mbili kujifungua ndipo aende.
Wazazi wake walipinga, lakini aliwapa masharti yaliyokuwa magumu kwao kuwa aende na mumewe ambaye hakutakiwa kwa kipindi kile. Baada ya kushindwa masharti ya mtoto wao walikubaliana naye akae mpaka akibakiza wiki mbili kujifungua ndipo aende.
Sharti lingine lililomuumiza akilini Nargis ni kukaa miaka kumi chini ya bahari baada ya kujifungua ndipo atoke kurudi duniani na kuishi na familia yake japokuwa wazazi walitaka watoto waendelee kuishi ujinini mpaka watakapokuwa wakubwa.
Kwa mapenzi aliyokuwa akimpenda Thabit hakutaka kumuacha, alitaka aende naye akaishi naye kipindi chote cha kujifungua na kulea watoto wao. Lakini familia yake ilimruhusu kitu kimoja kuolewa na mwanadamu tu na si kumpeleka mwanadamu kuishi ujijini kipindi kirefu. Alijikuta akilia kwa zaidi ya saa nzima kutokana na maumivu ya moyo kwa kutengana na kipenzi chake.
Akiwa amezama kwenye lindi la mawazo, muda nao ulikuwa ukikaribia alikuwa na saa moja tu kuwepo duniani. Huko baharini majini waliokwenda kumpokea walikuwa wamejaa juu ya bahari huku wakiimba nyimbo tamu za kumkaribisha malaika wa majini Nargis. Alijizuia kulia na kumtikisa Thabit ili amuage kwa kumwita jina.
“Thabit…Thabit.”
“Mmh!” Thabit aliitika bila kufumbua macho na kujigeuza upande wa pili.
“Thabit mume wangu hebu amka basi,” alisema huku akimtikisa.
“Naam.”
“Hebu amka mwenzio nachelewa.”
“Ha! Kwani sasa ni saa ngapi?” Thabit alikurupuka usingizini.
“Nina nusu saa tu ya kuendelea kuwa hapa.”
“Mungu wangu! Mbona umechelewa kuniamsha?”
“Nisamehe mpenzi wangu.”
“Mbona macho yamevimba?”
“Acha tu, Thabit sikupenda kuwa mbali na wewe kwa kipindi kirefu, kitendo walichonifanyia wazazi wangu kimeniumiza sana. Kama walikubali uwe mume wangu kwa nini hawataki tukae wote kipindi cha kujifungua na kulea watoto wetu?” Nargis alianza kulia tena.
“Hatuna budi kukubaliana nao, hata mimi najua nitateseka sana, miaka kumi ni mingi sana Nargis, nitakuwa mpweke sana. Pamoja na kukupenda lakini ulikuwa mtu muhimu sana katika maisha yangu, nilikuzoea sana, nitacheka na nani na nitacheza na nani?” Thabit alijikuta akizungumza sauti ya kilio kutokana na kutengana na mpenzi wake Nargis.
“Hilo hata mimi linaniumiza, lakini naomba uniombee nijifungue salama.”
“Nitakuombea siku zote.”
“Thabit naondoka nikiwa nimekuachia utajiri mkubwa ambao hutaumaliza mpaka unakufa, unajua kiasi gani nilivyopigana na majini wenzangu na wanadamu kukulinda.
“Nina dhambi ya kuua majini na wanadamu kwa ajili yako. Nimewatia wanadamu na majini vilema ambavyo watakufa navyo kwa ajili yako.
“Thabit naondoka nakuacha peke yako, kwa utajiri ulio nao una mtihani mzito kwa wanadamu, kila mwanamke atakutaka, wapo watakaokuendea kwa waganga ili wakupate. Kipindi changu cha kujifungua sitaweza kutoka mpaka miaka kumi hivyo sitakuwa karibu na wewe tena.
“Mpenzi naomba usinisaliti nimechoka kubeba dhambi za wanadamu na majini kwa ajili yako.
Nakuomba baada ya kuondoka kaa mbali na wanadamu, mafuta niliyokuachia siku ukinikumbuka sana jipake usiku wakati wa kulala utaniota usingizini lakini hatutaonana mpaka miaka kumi ipite,” Nargis alisema kwa hisia kali.
“Nakuahidi kuwa muaminifu kwako, sitakusaliti nakupenda sana Nargis, nilitamani niwapokee wanangu wakati wa kuzaliwa lakini sina jinsi. “Nenda mpenzi wangu ukijua nakupenda kuliko kiumbe chochote kilichoumbwa na Mungu. Nakuahidi kukusubiri hata kwa miaka mia moja,” Thabit alimuahidi Nargis.
“Kweli Thabit?” Nargis alimuuliza Thabit huku akimkazia macho yake makubwa lakini yenye urembo wa aina yake.
“Kweli kabisa.”
“Hutanisaliti?” alimuuliza tena.
“Siwezi.”
“Na hii nyumba ya baharini kuanzia leo utaihama na kwenda kuishi kwenye nyumba tuliyojenga. Naogopa kukuacha hapo unaweza kufanya kosa nyumba ikayeyuka na wewe kufa maji. Sitaki kukupoteza mpenzi wangu nakupenda sana.”
“Nitajilinda kulilinda penzi letu.”
“Basi amka tukaoge ili niwahi, wenzangu wamefika zaidi ya saa nne kunisubiri.”
Walikwenda kuoga kisha alibadili nguo na kuvaa mavazi ya kijini na kumkumbatia Thabit wote waliruka hadi pembeni ya bahari ambako walikuta bahari ikimeremeta kwa mishumaa iliyokuwa imebebwa na majini.
Walitembea wameshikana mkono kama siku ya harusi yao mpaka walipokaribika kwenye kina kirefu, waliagana kila mmoja alilia kutengana na mwenzie.
Nargis kabla ya kuondoka alisema neno moja la mwisho.
“Thabit nakupenda sana usinisaliti, kwa heri.”
Ghafla juu ya bahari kiza kizito kilitokea, Thabit alijiona kama akizamishwa ndani ya bahari.
Itaendelea
 
SEHEMU YA 02


Ghafla juu ya bahari kiza kizito kilitokea, Thabit alijiona kama akizamishwa ndani ya bahari, alipotaka kupiga kelele maji tayari yalikuwa yamejaa mdomoni. Aliposhtuka alijikuta amelala kwenye nyumba yao mpya waliyojenga kama Nargis akiondoka kwenda kujifungua ili aishi maisha ya kawaida ya kibinadamu.
Nyumba ilikuwa na kila kitu, kama kawaida Nargis alimuachia mumewe vijakazi toka ujinini kwa ajili ya kumpikia na kumfanyia usafi. Yalikuwa maisha mapya ya Thabit kuishi bila ya mpenzi wake jini Nargis.
SASA ENDELEA...
Thabirt aliyaanza maisha mapya wakati huo alikuwa amefunguliwa miradi mingi ambayo itamfanya awe bize ili watu washtuke kutaka kujua maisha yake ya kukaa tu akiwa na maisha mazuri. Thabit kila asubuhi alikwenda mjini kwenye moja ya duka lake kusaidiana na wafanyakazi wake kufanya biashara na jioni alirudi nyumbani.
Maduka mawili yalikuwa Posta na mengine mawili Kariakoo, yalikuwa maduka makubwa sana yaliyouza vitu mbalimbali. Moja liliuza vifaa vya elektoroniki ambavyo ni simu, redio, feni, friji na vifaa vyote vya umeme.
Lingine lilikuwa likiuza nguo za kike na kiume na viatu. Maduka ya Kariakoo moja liliuza vyombo vya ndani na lingine liliuza nguo za majumbani kama mashuka mapazia na vitu vyote vya ndani.
Pia alikuwa akimiliki magari ya kifahari, kila mtu alimfahamu mjini kwa utajiri wake. Wafanyakazi wake walifurahi malipo aliyowalipa na kufanya wamheshimu sana.
Kwa muda mfupi aliweza kufungua kampuni kubwa iliyokusanya miradi yake yote na yeye kuwa mkurugenzi wake. Jina la Thabit lilisambaa haraka kama moto kwenye nyasi kavu. Alikuwa ni mmoja wa watu wenye utajiri nchini huku kila mmoja akishamgaa uwezo wake wa kifedha kwa watu waliomfahamu toka enzi wakifanya kazi pamoja za vibarua kwenye makampuni ya Wahindi miaka ya nyuma kabla hajaonana na Jini Nargis.
Maisha yalimwendea vizuri japokuwa aliyakosa mapenzi ya mkewe Nargis, lakini kila usiku ulipoingia alijipaka mafuta. Usiku wote huwa na mpenzi wake Nargis ndotoni mpaka kunakucha ile kidogo ilimfariji na kujiona kama walikuwa pamoja.
Wasichana wengi kazini walimshangaa bosi mzima kama yule kutokuwa na mke, walipomuuliza aliwaeleza ana mke ambaye muda ule alikuwa amesafiri. Aliwaonesha mpaka pete ya ndoa kuonesha yeye ni mume wa mtu.
Lakini walishangaa toka awaeleze miaka zaidi ya mitatu ilikatika bila kumuona huyo mkewe kitu kilichoanza kuwafanya wawe na maswali labda bosi wao si rijali.
Subira sekretari wake siku zote alimpenda sana bosi wake lakini alishindwa kumwambia mateso ya moyo wake toka alipomweleza ana mke. Lakini muda ulizidi kukatika bila kumuona huyo mwanamke.
Alijiuliza kwa nini bosi wake hakuwa na mke! Siku zote aliumia sana lakini hakutaka kuendelea kuteseka, alimfuata shoga yake Sofia naye alikuwa mchemsha chai mpaka mpenzi wa bosi na kuwekwa kuwa sekretari wa kampuni tofauti.
Kwa vile walikuwa wameshibana na kuujua machepele wake wa kubadilisha wanaume alimweleza anavyompenda bosi wake.
“Si ana mke yule?”
“Ndiyo anavyosema lakini mwaka wa tatu unakatika hatujawahi kumuona mke wake.”
“Mmh! Basi atakuwa na tatizo!”
“Hapana naamini hana tatizo ila bado hatujamvutia kati yetu.”
“Sasa utafanyaje?”
“Ndiyo maana nimekuja unipe mawazo.”
“Labda tumwendee kwa babu.”
“Wewe unamjua nani mkali?”
“Mzee Mukti Buguju dawa za mapenzi mzee yule anatisha. Si unakumbuka yule shemeji yako Muhindi aliyekuwa bosi wa kampuni yetu? “
“Eeh! Mukesh, kweli siku hizi yupo wapi?”
“Shoga yaani majanga, nilipewa siku tatu nikamtia mikoni.
Aliniahidi vitu vingi wiki moja kabla ya kuvitekeleza si akaondoka kumbe mkataba wake ulikuwa umekwisha. Yaani kama angekuwepo mpaka sasa ningekuwa na nyumba na gari. Mzee Mukti Buguju namuamini sana.“
“Dawa zake hazima masharti magumu?”
“Wala zipo za kwenye chai na zingine za kufusha usiku chumbani na kuoga basi.”
“Yaani hivyohivyo tu mwanaume anakuwa wako?” Subira kama hakuamini vile.
“Tena anakutamkia mwenyewe.”
“Mmh! Nikipata bosi wangu mbona nitakuwa tajiri, nashangaa mwanaume mwenye pesa kama nini hana hata mtoto!”
“Basi shoga ukiwa tayari twende kwa mzee Mukti Buguju.”
“Anakaa wapi?”
“Mji mwema.”
“Si kuvuka Kigamboni?”
“Ndiko hukohuko.”
“Mmh! Huko panafaa mwisho wa wiki siku ambayo siendi kazini.”
“Kwani chai anamtengea nani?”
“Mimi.”
“Basi amekwisha, jihesabu ni wako.”
“ Yaani shoga nakuahidi zawadi kubwa kama nikimpata hata gari nitakununulia.”
“ Mmh! Gari?” Sofia alishtuka.
“Jamaa ana hela kama nini, nikimpata utakubaliana na mimi.”
“Ukifika kwa mzee Mukti Buguju utakubaliana na mimi.”
****
Wakati Thabit akifarijika kuwa na mkewe jini Nargis ndotoni, Subira naye alikuwa mawindoni. Mwisho wa wiki walielekea Mji Mwema kwa mganga mzee Mukti Buguju. Kama walivyopanga walipitiana na kupanda daladala mpaka feri na kuvuka kisha walipanda daladala kuelekea Mji Mwema.
Walipofika waliteremka na kutembea kwa dakika kumi kuingia ndani kidogo hadi kwa mganga Mukti Buguju. Alikuta nje ya nyumba kuna magari manne ya kifahari, alipita ndani na kukaa kwenye mkeka. Watu hawakuwa wengi sana kutokana na siku yenyewe.
Mzee Mukti Buguju alikuwa na wasaidizi wengi ambao ndiyo waliopokea wateja. Baada ya kukaa alipewa namba ya kuonana na mzee na kutulia baada ya kuelezwa wataitwa kwa namba. Wakiwa wamekaa waliona watu wazito serikalini wakitoka ndani na kuingia kwenye magari yao na kuondoka.
Sofia alimnong’oneza Subira kwa kumwambia:
“Yaani huyu mzee kiboko hakuna anachoshindwa kwake mpaka nanii anakuja hapa!”
“Muongo, ulimuona?”
“Hapana alinieleza mzee Mukti, siku anayokuja huwa hakuna mteja.”
“Mmh! Basi atakuwa kiboko.”
“Wee utaniambia mwenyewe baada ya kumpata bosi wako.”
Baada ya muda namba yao iliitwa, waliingia ndani ya chumba kikubwa chenye mikeka ya kisasa kila kona kulikuwa na udi uliokuwa ukiwaka na kukifanya chumba kinukie.
“Karibuni,” mzee Mukti aliwakaribisha, alikuwa mzee wa makamo mwenye mwili ulioshiba. Alivalia kanzu nyeupe na kibalaghashia.
“Asante mzee, shikamoo.”
“Marahaba, mmh! Mna shida gani?”
“Ni mwenzangu hapa, mimi nimemleta tu,” Sofia alisema.
“Ndiyo nimeona hapa mwenye matatizo ni mmoja, haya bibi shida yako nini?”
Subira alielezea shida iliyompeleka pale, baada ya kumsikiliza alisema:
“Mwanangu shida huyo imekwisha, dawa nitakayokupa nitakupa siku tatu usipompata njoo uchome moto dawa zangu.”
Inaendelea.
 
SEHEMU YA 03

“Karibuni,” mzee Mukti aliwakaribisha, alikuwa mzee wa makamo mwenye mwili ulioshiba. Alivalia kanzu nyeupe na kibalaghashia.
“Asante mzee, shikamoo.”
“Marahaba, mmh! Mna shida gani?”
“Ni mwenzangu hapa, mimi nimemleta tu,” Sofia alisema.
“Ndiyo nimeona hapa mwenye matatizo ni mmoja, haya bibi shida yako nini?”
Subira alielezea shida iliyompeleka pale, baada ya kumsikiliza alisema:
“Mwanangu shida hiyo imekwisha, dawa nitakayokupa nitakupa siku tatu usipompata njoo uchome moto dawa zangu.”
“Nitashukuru mzee wangu.”
SASA ENDELEA...
Subira alipewa dawa ya kuweka kwenye chai na juisi, kufukiza chumbani kwake na ya kuoga, kazi yake haikuchukua muda mrefu.
“Mzee wangu ndiyo kiasi gani?”
“Hapana leo sitaki hela yoyote kwa vile huna hela ya kunipa, najua baada ya mwezi utaleta zawadi yangu.”
“Nashukuru mzee.”
“Haya kwaheri.”
Walitoka kwa mganga kuelekea barabarani huku Subira akiwa haamini kwa vile hawakutumia muda mrefu kupata huduma tofauti na watu waliowakuta. Walipanda daladala na kurudi nyumbani, wakiwa njiani Subira alikumbuka kuna kitu alisahau kuuliza.
“Sofi kuna kitu nimesahau kuuliza.”
“Kitu gani?”
“Kuhusu matumizi ya kwenye chai na juisi naweka kiasi gani?”
“Kumbe hilo, kiasi kidogo tu nusu kijiko cha chai.”
“Mara ngapi?”
“Subira mara moja, kwani mumeo useme utampa hata jioni.”
“Nilitaka kujua tu si unajua dawa hizi ukikosea masharti umeharibu kila kitu?”
“Ni kweli, lakini dawa za mzee huyu hazina masharti magumu kwa vile anaziamini.”
Baada ya kufika nyumba wakiagana kila mmoja alikwenda kwake, Subira pamoja na kuhakikishiwa kumpata Thabit kwake aliona kama ni uongo usiowezekana kwa mtu kumuwekea dawa kwenye chai na kumkubali kimapenzi.
Aliachana na mawazo yale aliangalia dawa alizofunga kwenye karatasi na kuzisoma, alichukua ya kuoga na kuweka kidogo kwenye maji na kwenda kuoga kisha alipata chakula.
Kabla ya kulala aliwasha moto wa mkaa na kuweka mikaa michache ya moto kwenye bakuli. Alichukua dawa ya kujifusha na kujifunika shuka kisha aliiweka kwenye moto huku akinuiza maneno ya kuhakikisha Thabit anaingia mikononi mwake. Baada ya kujifusha alipanda kitandani kulala.
***
Siku ya pili Subira aliwahi kazini na kufanya usafi kisha alimchemshia chai bosi wake na kuiweka kwenye chupa na kurudi sehemu yake kuendelea na kazi. Baada ya muda Thabit aliingia na kumsalimia kama ilivyo kawaida yake siku zote huwa mcheshi kitu kilichomchanganya Subira kushindwa kueleza badadiliko lolote kutokana na dawa alizofanya usiku.
Subira muda wote kazi ilimshinda macho yake hayakucheza mbali na saa yake ndogo ya mkononi kuangalia muda wa kumpelekea chai bosi wake. Kila alipoiangalia aliona kama mishale imesimama. Mapigo muda wote yalimwenda kasi kutokana na kuwa na wasiwasi na kitu alichotaka kukifanya kitakuwa na matokeo gani.
Wasiwasi wake mkubwa ulikuwa kama bosi wake akigundua na kuamua kumfukuza kazi itakuwa kilio kwake. Aliona kama saa ya mkononi inamdanganya alibadili na kuangalia ya kwenye kompyuta. Nayo hakuiamini aliangalia kubwa ya ukutani ilimuonesha bado dakika tano muda wa kupeleka chai utimu.
Aliporudia kuangalia saa zingine zilionesha zilikuwa sawa ila wasiwasi wake ulifanya azione kama zimesimama. Alinyanyuka hadi jikoni na kuchukua kikombe cha bosi wake na kufungua kikaratasi alichoweka dawa ya unga na kuchukua kidogo na kuiweka kwenye kikombe huku akinuiza kumpata bosi wake na kuiweka chai ya maziwa na kukoroga huku akinuiza kuukoroga moyo wake kama ile chai na kumfanya amejaze moyoni kama utamu wa chai ile.
Baada ya kukoroga alijifuta vizuri na kuibeba chai na kwenda ofisini, alipofungua mlango alikutana na tabasamu pana la bosi wake.
“Karibu Subira.”
“Asante bosi.”
“Hongera umependeza,” kauli ile ilimpa matumaini, tangu aanze kazi pale hakuwahi kusifiwa na bosi wake.
Subira aliitenga chai juu ya meza ya bosi wake na kumkaribisha.
“Karibu bosi.”
“Asante.”
Alisema huku akishika mkono wa kikombe na kunyanyua ili apeleke mdomoni. Subira alikuwa amesimama pembeni kumuangalia bosi wake akipiga funda la chai ndipo aondoke kwenda kuendelea na kazi kusubiri kutoa vyombo na kuangalia matokea ya siku tatu aliyopewa kumtia mikononi Thabit.
Kikombe kilipokaribia mkononi alishtuka kukiona kikipasuka na kutoa mlio huku chai ikitawanyika na kumuunguza kifuani kitu kilichofanya Thabit apige kelele za maumivu huku Subira akipigwa bumbuwazi na kutoamini kikombe kupasuka kama kimefungwa bomu.
“Bosi nini?” Subira aliuliza kwa mshtuko.
“Hata najua nashangaa kikombe kupasuka kama kimefungwa bomu.”
“Pole sana bosi hukuungua?”
“Kiasi si sana.”
“Itabidi uende hospitali.”
“Lazima kwanza nirudi nyumbani nikabadili nguo.”
Thabit alivua shati lililochafuka kwa chai alivaa koti na kutoka kuelekea nyumbani kubadili nguo. Baada ya kuondoka bosi wake, Subira aliingia woga moyoni mwake na kujiuliza kile kilichotokea ni nini. Kwa nini hakikutokea siku zote kitokee alipoweka dawa?
Alijiuliza Thabit akigundua alitaka kumuwekea dawa atamchukulia hatua gani. Mawazo yale yalimchanganya sana na kujikuta akikosa raha na kuanza kujilaumu kujiingiza kwenye mambo ya kishirikina. Aliamua kumpigia simu shoga yake kumueleza yaliyotokea ofisini.
Baada ya simu kuita ilipokelewa upande wa pili.
“Haloo shoga vipi?”
“Mambo mabaya.”
“Kivipi?” Sofia alishtuka.
Alimweleza kilichotokea muda mfupi na kuichanganya akili yake.
“Wewee! Hakijamponyoka?”
“Hakijamponyoka kimepasuka.”
“Amekwambia au umekiona kwa macho yako?”
“Yaani nimeona mwenyewe kwa macho yangu.”
“Kimepasuka kabisa?”
“Tena kimelia kama bomu.”
“Mmh! Hukukosea kitu?”
“Sijakosea nimefuata kila hatua toka jana usiku.”
“Sasa itakuwa nini, mbona mara zote haikikutokea kitu kama hicho.”
“Nikuulize wewe!”
Inaendelea.
 
SEHEMU YA 04

“Amekwambia au umekiona kwa macho yako?”
“Yaani nimeona mwenyewe kwa macho yangu.”
“Kimepasuka kabisa?”
“Tena kimelia kama bomu.”
“Mmh! Hukukosea kitu?”
“Sijakosea nimefuata kila hatua toka jana usiku.”
“Sasa itakuwa nini, mbona mara zote haikutokea kitu kama hicho?”
“Nikuulize wewe.”
SASA ENDELEA…
“Basi turudi kwa mzee Mukti.”
“Kwa lililotokea, leoleo twende jioni.”
“Hakuna tatizo.”
***
Baada ya muda Thabit alirudi akiwa amebadili nguo, Subira alishtuka na kujiuliza ataambiwa nini.
“Vipi bosi?” aliuliza kwa unyenyekevu.
“Nipo sawa.”
“Vipi umeenda hospitali?”
“Sijaenda kwa vile sijaumia chochote.”
“Pole sana.”
“Asante, nipo ofisini.”
“Sawa.”
Subira aliendelea na kazi zake huku akihofia kumuwekea dawa kwenye juisi kwa kuhofia tukio lile kutokea tena. Muda wote alifanya kazi bila amani moyoni, akili yake iliwaza kwenda kuonana na mzee Mukti ili ajue tatizo nini.
Muda wa kutoka kazini Subira alikodi teksi na kumpitia shoga yake na kwenda Mji Mwema kwa mganga Mukti Buguju. Kutokana na foleni walifika saa kumi na mbili na nusu jioni. Walikuta kuna wateja wengi ilibidi wasubiri kuonana naye mpaka saa mbili na nusu usiku ndipo walipokutana.
Baada ya kuingia kwenye chumba cha uganga walikaa kwenye mkeka na kumsalimia mzee Mukti.
“Marahaba warembo, kama sikosei mlikuja jana?”
“Ndiyo mzee.”
“Vipi mbona ghafla?”
“Kuna tatizo mzee wangu,” Sofi alisema kwa niaba ya Subira aliyekuwa amenyamaza kimya.
“Tatizo gani?”
“Subira mueleze,” Sofi alimgeukia Subira na kumwambia.
“Ndiyo binti,” mzee Mukti alimsemesha Subira aliyekuwa ameinama.
“Kumetokea tatizo ofisini.”
“Tatizo gani?”
“Kuhusiana na ile dawa ya chai.”
“Imefanya nini?”
Subira alielezea yote yaliyotokea baada ya kufuata maelekezo ya kutumia dawa kuanzia usiku na asubuhi alipomtengenezea chai na maajabu yalitokea.
“Hicho kikombe kimemdondoka wakati anakunywa chai au vipi? Hebu nifafanulie.”
“Kimepasuka kabla hajainywa, kikombe kilipokaribia mdomoni kilipasuka kama bomu.”
“Eti?” mzee Mkuti alishtuka.
“Hakikumponyoka bali kimepasuka kama bomu kabla hakijagusa mdomo,” Subira alirudia.
“Chai haikumuunguza?”
“Kidogo lakini hakwenda hospitali.”
“Mmh! Kazi ipo,” mzee Mukti alisema huku akichukua unga kwenye kichupa kidogo kilichokuwa kwenye chupa nyingi za dawa na kumwaga kwa kuusambaza na kutulia kuutaza sehemu alizotupa kwa muda akiwa ameshika tama kisha aligeuka na kusema.
“Mmh! Kazi hii niliidharau kumbe ni nzito sana, bosi wako ni mume wa jini lililopo chini ya bahari na utajiri ule jini yule ndiye aliyempa. Kwa sasa yupo ujinini amekwenda kujifungua na atarudi baada ya miaka kumi. Kwa hiyo ametegesha mawasiliano yake na kuona kila kinachotendeka duniani ili kumlinda mumewe.
“Jini yule ni mpole sana ila ni mkorofi anapotaka kuingiliwa katika maisha yake hasa kumchukua kipenzi mume wake. Ile pete anayovaa bosi wako ndiyo mawasiliano makuu kati yake na mkewe jini Nargis. Kila kitu kinachofanyika lazima ajue na kutumia nguvu zake za kijini kupitia pete ile kuzuia Thabit asipatwe na tatizo lolote, ndiyo maana nikasema kazi ile sikuiangalia mapema kumbe nzito sana.”
“Kwa hiyo tutafanyaje maana kama ni hivyo rafiki yangu yupo hatarini?” Sofi aliuliza kwa niaba ya shoga yake.
“Kama mna nia ya dhati, itabidi muingie gharama za kuweza kuvunja mawasiliano kati ya Thabit na mkewe jini, kisha nikutengeneze wewe hata miaka kumi ikiisha akirudi asikufanye kitu kwa vile tutakuwa tumemdhibiti.”
“Kama kiasi gani?”
“Laki tatu.”
“Mzee wangu mbona nyingi sana?” Sofi aliuliza.
“Ni kweli ni nyingi lakini ni ndogo kulingana na kazi yenyewe, kumbuka nikikosea hata mimi naweza kufa kwa vile vita hiyo lazima itageukia kwangu. Pia baada ya zoezi letu utakuwa na maisha mazuri sana.”
“Sawa nitalipa,” Subira alikubali.
“Kazi hii inatakiwa ifanyike haraka sana kwa vile tayari tumeichokoza.”
“Sawa mzee wangu, lini?”
“Kwa vile mwezi bado haujamezwa na mawingu, kazi yako itafanyika kesho usiku saa sita baharini. Unatakiwa uje kulala huku na ukitoka hapa unafikia moja kwa moja kazini.”
“Sawa hakuna tatizo.”
“Nina imani lile ni tatizo ambalo halina madhara kwako, endelea kutumia dawa kujifusha kuoga ya chai na juisi achana nayo kwa muda.”
“Sawa mzee wangu, naweza kukutumia leo kutoka katika simu?” Subira aliuliza.
“Hakuna tatizo.”
Mganga alimtajia namba za simu, Subira alimtumia fedha yote kisha waliagana na kuondoka kuwahi nyumbani kwa vile muda ulikuwa umekwenda sana.
***
Siku ya pili majira ya jioni Subira alielekea Mji Mwema kwa mzee Mukti Buguju peke yake kwa vile siku ile alitakiwa kulala kule. Alifika saa moja usiku na kwenda moja kwa moja kwa mzee Mukti alipomuona alimkaribisha na kumuomba atulie kwa vile kazi yake ilitakiwa kufanyika saa sita usiku mwezi ukiwa katikati.
Majira ya saa tano usiku alifuatwa na kijana wa mzee Mukti na kumwambia ajiandae kuna safari ya kwenda baharini. Alipewa shuka nyekundu na kilemba chekundu na kuambiwa avue nguo zote ajifunge zile kisha asuburi. Baadaye aliitwa nje, alipofika alikuta watu wanne na mzee Mukti na kuelezwa;
“Sasa mama kazi ndiyo inakwenda kuanza kwa vile hali ya hewa inaruhusu.”
Inaendelea.
 
SEHEMU YA 05

Majira ya saa tano usiku alifuatwa na kijana wa mzee Mukti na kumwambia ajiandae kuna safari ya kwenda baharini.
Alipewa shuka nyekundu na kilemba chekundu na kuambiwa avue nguo zote ajifunge zile kisha asuburi. Baadaye aliitwa na nje alipofika alikuta watu wanne na mzee Mukti na kuelezwa.
“Sasa mama kazi ndiyo inakwenda kuanza kwa vile hali ya hewa inaruhusu.”
“Sawa.”
SASA ENDELEA…
Waliongozana kuelekea baharini wakiwa wamebeba kikapu chenye vitendea kazi na mbuzi mwekundu aliyekuwa amefungwa vitambaa vyekundu kwenye pembe. Subira kwa vile alikuwa mgeni alikaa katikati, msafara ulichukua dakika ishirini kufika baharini.
Walikuta maji yamejaa pomoni, alisimama pembeni ya maji, mzee Mukti alitoa vitendea kazi na kutengeneza mavazi yake mekundu. Baada ya mganga kupanga vitu vyake, Subira alielezwa ampande mgongoni na yule mbuzi alishikwa kwa mbele na kuingia naye ndani ya bahari.
Subira alikuwa akitetemeka kwa vile hali ya bahari ilikuwa tulivu lakini kulikuwa na milio ya kutisha. Hawakuijali waliendelea na kazi yao, alitembea na mbuzi yule mpaka maji ya kifuani wakiwa bado yupo chini. Wasiwasi wa Subira mbuzi yule kufa kwa kukosa hewa.
Baada ya kufika usawa ule mzee Mukti alishika usinga na kibuyu kidogo na kuingia nacho ndani ya maji. Baada ya kumsogelea Subira alizungumza kwa lugha anayoijua huku akimshika sikio la kulia kisha kumuwekea mkono katikati ya kichwa. Aliambiwa autazame mwezi na asipumue mpaka amalize kumshika kichwani. Baadaye alimuachia na kufanyika maombi mengine kazi iliendelea kwa zaidi ya saa mbili bila mbuzi aliyemkalia kutolewa ndani ya maji.
Baada ya zoezi kwenda vizuri alielezwa atoke, ajabu mbuzi aliyemkalia hakuwepo kwenye miguu yake. Alielezwa atoke ndani ya maji naye alifanya kama alivyoekekezwa. Alitoka mwenyewe bila mbuzi na kusikia wakisema:
“Kazi imekwenda vizuri tofauti na tulivyofikiria.”
Baadaye aliambiwa asogee pembeni ili aoge kisha warudi nyumbani, Subira alisogea pembeni na kuoga baada ya kuoga alipewa shuka nyeupe kujifunga kisha walirudi nyumbani. Walipofika mzee Mukti alimweleza:
“Kazi yako imekuwa rahisi tofauti na tulivyofikiria, mpeni chakula kisha apumzike ili asubuhi awahi kazini.”
“Sawa mzee,” waliitikia wasaidizi wake.
Baada ya kupata chakula na kuoga tena, alijifunga shuka nyeupe na kulala nayo hadi alfajiri alipoamshwa kuoga tena ili kujiandaa awahi kazini. Kabla ya kuondoka alipewa dawa nyingine.
“Hii utaiweka ndani ya maji kisha haya majani utatumia kunyunyiza kila kona ya ofisi kisha yatupe. Dawa hii inaua nguvu za kijini ambazo zipo pale ofisini.
Hii nyingine utainyunyizia kwenye meza ya bosi wako akigusana na pete mawasiliano yatakuwa yamekatika kati yake na mkewe jini, hivyo utatumia ile dawa ya chai na juisi kwa vile tayari tutakuwa tumekata mawasiliano.
Mtakapoanza uhusiano usikubali kukutana naye mpaka uje huku kuna dawa nitakupa kuhakikisha unakuwa salama katika penzi lako na kuifanya ndoa yako iwe ya haraka. Nina imani ikifanya kwa kuzingatia maelezo yangu utashangaa mwenyewe.”
“Nashukuru mzee wangu, nakuahidi zawadi kubwa.”
“Wewe tu kazi yangu nimemaliza.”
Baada ya kupewa dawa na maelekezo Subira aliondoka kuwahi kazini, alikodi Bajaj ambayo ilimpeleka moja kwa moja mpaka ofisini. Siku ile aliwahi kazini tofauti na siku zote mpaka mlinzi alishangaa.
Baada ya kuingia ofisi kwa bosi wake, alianza usafi mara moja kisha alichukua kikombe cha chai na kuweka maji kidogo na kuweka dawa ya unga na kuikoroga kisha alichukua majani aliyopewa na kuanza kunyunyiza ndani ya ofisi. Ghafla mle ndani ulitokea mtikisiko mkubwa , Subira alitoka mbio kuhofia uhai wake na kwenda kusimama pembeni ya ofisi huku akitweta.
Bahati nzuri alitoka na mkoba wake na kumpigia simu mzee Mukti ili kumweleza yaliyotokea huku yakizidi kumkatisha tamaa. Baada ya kuita kwa muda mfupi ilipokelewa upande wa pili.
“Haloo.”
“Haloo mzee.”
“Vipi mbona hivyo?”
“Huku kuna tatizo lingine limetokea.”
“Tatizo gani?”
Subira alimwelezea kilichotokea muda mfupi baada ya kuanza kunyunyiza dawa aliyompa.
“Kumbe ni hilo endelea tu.”
“Mzee yaani mtikisiko mpaka mwenyewe nikashtuka, hapa nilipo natetemeka mwili hauna nguvu kabisa halafu unaniambia niendelee?”
“Zile ndizo nguvu za kijini zilizomo ofisini, unaponyunyiza maji huo mtikisiko uliousikia ni kuvunjika kwa nguvu hizo. Kwa hiyo kaendelee wala usihofu, jitahidi umalize zoezi kabla bosi wako hajafika.”
“Sawa.”
Subira alirudi ofisini akiwa hajiamini, alichukua kikombe chenye maji na kuanza kunyunyiza ile dawa. Mtikisiko wa mwanzo ulijirudia tena lakini hakuacha aliendelea kufanya hivyo kila kona ya ofisi na hali ya mtikisiko ilitulia. Baada ya zoezi lile kwenda vizuri alichukua dawa nyingine na kuipaka kwenye meza na kurudi sehemu yake ya kazi.
Majira ya saa tatu na nusu asubuhi Mustafa aliingia ofisini, kama kawaida aliachia tabasamu lililokuwa likimtesa Subira. Baada ya kusalimiana aliingia ofisini kwake kuendelea na kazi. Haikuchukua muda kishindo kizito kilitokea ndani ya ofisi kilichomshtua Subira na kujiuliza kulikuwa na kitu gani ndani.
Inaendelea
 
SEHEMU YA 06

Majira ya saa tatu na nusu asubuhi Mustafa aliingia ofisini, kama kawaida aliachia tabasamu lililokuwa likimtesa Subira. Baada ya kusalimiana aliingia ofisini kwake kuendelea na kazi. Haikuchukua muda kishindo kizito kilitokea ndani ya ofisi kilichomshtua Subira na kujiuliza kuna kitu gani ndani.
ENDELEA...
Alinyanyuka taratibu huku mapigo ya moyo yakiwa juu na kugonga ofisini kwa bosi wake taratibu. Hakukuwa na majibu yoyote, ile hali ilizidi kumtisha aligonga tena kwa nguvu kidogo huku akimwita kwa jina lake.
“Bosi…bosi.”
Vilevile hakukuwa na jibu, aliufungua mlango taratibu na kuchungulia ndani, alishtuka kumuona bosi wake akiwa amejilaza kwenye meza huku kidoleni pete yake ikionesha kama moto unawaka. Alijiuliza kile ni nini kwa vile hakuelezwa na mganga kutokea na kitu kile.
Alimsogelea huku akitetemeka alimtikisa akimwita, lakini hakukuwa na jibu, alipomuangalia vizuri aligundua amepoteza fahamu. Haraka alirudi ofisini kwake na kumpigia simu mzee Mukti ili kumpa kinachoendelea pale ofisini.
“Vipi binti?” aliuliza baada ya kupokea.
“Mzee wangu kila dakika kunatokea kitu cha ajabu.”
“Kitu gani?”
“Baada ya bosi kuingia, ilichukua muda mfupi kusikia kishindo kizito, nilipoingia ndani nimemkuta amelalia meza akiwa amepoteza fahamu. Kilichonishtua zaidi pete aliyovaa inawaka moto.”
“Hiyo kawaida wala usihofu zoezi limekwenda vizuri sana, umenifurahisha kufanya kama nilivyokuelekeza.”
“Mzee zoezi limeenda vizuri wakati hali ya bosi ni mbaya?” Subira alimshangaa mzee Mukti kusema vile.
“Kazi imeisha, sasa fanya hivi mvue pete hiyo iweke kwenye maji yaliyochanganywa na dawa iliyopakaza kwenye meza kwa dakika tano. Kisha utaitoa na kumvisha kidoleni na kumuacha bila kumfanya chochote.
Ukitoka hapo kamuandalie chai, akishtuka mpe chai kisha endelea na kazi. Mchana mpe juisi kitakachofuata utanijulisha. Nilitaka kusahau na lingekuwa kosa kubwa, kabla hujaishika pete jipake dawa hiyo mkononi.”
“Sawa mzee.”
Subira alifanya kama alivyoelekezwa kwa kuweka maji kidogo kwenye kikombe na kuchanganya na dawa, alijipaka dawa mikononi kisha alimvua pete iliyokuwa ikiwaka moto huku akitetemeka na kuiweka kwenye kikombe.
Ilipogusa maji moto ilizimika kama kaa la moto huku ikitoa moshi na kutulia. Baada ya zoezi lile aliifuta pete kumvisha tena na kutoka ofisini kwa bosi wake kwenda kumtengeneza chai ili amalize zoezi la asubuhi.
Baada ya kuchemsha chai aliweka kwenye chupa na kurudi kuendelea na kazi, lakini kazi ilimshinda kwani hakujua hatima ya bosi wake.
Kompyuta aliiwasha na kutulia akiiangalia huku akisubiri kitakachoendelea. Baada ya dakika kumi alishtushwa na sauti ya Thabit.
“Subira.”
“E..eeeh! Abee bosi,” Subira alishtuka toka katika dimbwi la mawazo.

Chai tayari maana nashangaa nasikia mwili kuchoka ghafla,” Thabit alisema huku akijinyoosha.
“Tayari.”
“Ndiyo maana nakupenda.”
“Nioe basi,” Subira alijikuta akiropoka.
“Kila kitu mipango.”
Subira alijikuta alijishtukia kwenda mbali zaidi wakati zoezi aliloambiwa na mzee Mukti lilikuwa halijakamilika.
Alikwenda jikoni kuchukua chai kabla ya kuibeba aliweka dawa na kuikoroga vizuri kisha alibeba kikombe kumpelelea bosi wake. Aliitenga juu ya meza na kusema kwa unyenyekevu:
“Karibu chai bosi.”
“Asante,” Thabit alisema huku akichukua kikombe cha chai ili akipeleke mdomoni.
Subira alishindwa kuondoka alisimama akiangalia nini kitatokea wakati huo mapigo ya moyo yalikuwa juu. Wakati akikipeleka kikombe mdomoni hali ilikuwa mbaya kwake jasho la hofu lilimtoka na kubana pumzi.
Thabit alipiga funda mbili za haraka kutokana na moto wa chai na kumumunya midomo kisha alisema:
“Dah! Subira unajua kupika chai, umeolewa?”
“Sijaolewa.”
“Mmh! Sawa, chai tamu sana.”
“Kwani vipi?”
“Kaendelee na kazi.”
Subira hakuongeza neno alitoka na kwenda ofisini kwake huku akizidi kuyaona maajabu ya mzee Mukti pale bosi wake alipokunywa chai bila kikombe kupasuka. Alitaka kumpigia simu mzee Mukti Buguju kumweleza alipofikia lakini aliona mapema alisubiri aone kinachoendelea.
***
Thabit akiwa ofisini kwake alijiona mtu tofauti na alivyojizoea kwa kipindi kirefu, aliushangaa uzuri wa sekretari wake. Kwake alikuwa kama kiumbe kipya ambacho hakuwahi kukiona siku za nyuma. Alinyanyua simu na kumwita ofisini kwake ili amuulize kitu.
Baada ya muda Subira alisimama mbele yake huku akiachia tabasamu pana lililozidi kuuteketeza moyo wa bosi wake.
“Abee bosi.”
“Kaa.”
Subira alikaa na kumtazama bosi wake aliyeonekana kumshangaa kitu kilichomfanya amuhoji.
“Bosi mbona unanishangaa?”
“Una muda gani hapa kazini?”
“Miaka mitano sasa.”
“Miaka hiyo mitano! Ulikuwa ukifanya sehemu gani?”
“Kama msaidizi wako.”
“Muongo, mbona nilikuwa sikuoni?”
“Kweli bosi, basi tu labda sina mvuto moyoni mwako.”
“Hapana, umeolewa?”
“Bado.”
“Una mchumba?”
“Sina.”
“Jiandae mchana tukapate chakula cha pamoja kwa mazungumzo zaidi.”
“Bosi wewe si unakula kwako?”
“Ndiyo.”
“Kwa hiyo nikale na wewe kwako?”
Itaendelea
 
SEHEMU YA 07

“ Ndiyo.” “Kwa hiyo nikale na wewe kwako?” “Hapana leo tutakwenda hotelini.” “Hakuna tatizo.” “Basi kaendelee na kazi yako.” Subira alitoka huku moyo wake ukicheka alitamani kupiga vigelele, hakukaa alimpigia simu mzee Mukti ili kumjulisha kilichoendelea.
“Basi binti kazi imekwisha, jioni njoo tumalize kazi kabisa.” “Sawa mzee wangu.” Subira alijiandaa kutoka na bosi wake kwenda kupata chakula cha mchana, alifanya kazi iliyobakia haraka ili asibakishe kiporo. Baada ya muda Thabit alimpigia simu ajiandae watoke wakapate chakula cha mchana.
Alikwenda maliwatoni kujitengeneza akiwa pamoja na kuupodoa uso wake ili azidi kuonekana mpya kwa bosi. Thabit alitoka na kumpitia Subira aliyekuwa tayari amejiandaa, walitoka hadi kwenye gari, Kabla ya kuondoka Thabit alimuuliza Subira: “Twende wapi?” “Sijui, utakapotaka wewe.”
“Nimekupa upendeleo chagua unapopaona panafaa wewe.” “Mmh! Basi Steers.” “Hakuna tatizo.” Thabit aliwasha gari kuelekea Steers kwa ajili ya chakula cha mchana na sekretari wake.
Walipofika waliagiza chakula na kuanza kula, muda wote moyo wa Thabit ulikuwa ukimsukasuka kutokana na kumpenda sana Subira. Alijikuta akishindwa kuzuia hisia zake japokuwa alikuwa akikumbuka masharti aliyopewa na jini Nargis.
“Subira unajua wewe ni mzuri?” Thabit alisema huku akipeleka kijiko cha chakula mdomoni. “Nitajuaje wewe ndiye unayeuona,” Subira alijibu kwa tabasamu la mtego. “Unajua Subira lazima niseme ukwe…” Thabit alinyamaza baada ya kusikia sauti ya mkewe aliyosema muda mfupi kabla ya kuondoka kurudi ujinini.
Alitulia akiwa kama anaangalia tivii baada ya kuona marudio ya siku ambayo mkewe Nargis alipomuamsha ili amuage na kumkuta akilia. “Mbona macho yamevimba?” “Acha tu, Thabit sikupenda kuwa mbali na wewe kwa kipindi kirefu, kitendo walichonifanyia wazazi wangu kimeniumiza sana.
Kama walikubali uwe mume wangu kwa nini hawataki tukae wote kipindi cha kujifungua na kulea watoto wetu?” Nargis alianza kulia tena. “ Hatuna budi kukubaliana nao, hata mimi najua nitateseka sana, miaka kumi ni mingi sana Nargis, nitakuwa mpweke sana.
Pamoja na kukupenda lakini ulikuwa mtu muhimu sana katika maisha yangu, nilikuzoea sana nitacheka na nani nitacheza na nani?” Thabit alijikuta akizungumza sauti ya kilio kutokana na kutengana na mpenzi wake Nargis. “Hilo hata mimi linaniumiza, lakini naomba uniombee nijifungue salama.”
“Nitakuombea siku zote.” “Thabit naondoka nikiwa nimekuachia utajiri mkubwa ambao hutaumaliza mpaka unakufa, unajua kiasi gani nilivyopigana na majini wenzangu na wanadamu kukulinda. “Nina dhambi ya kuua majini na wanadamu kwa ajili yako.
Nimewatia wanadamu na majini vilema ambavyo watakufa navyo kwa ajili yako. “Thabit naondoka nakuacha peke yako, kwa utajiri ulionao una mtihani mzito kwa wanadamu kila mwanamke atakutaka, wapo watakaokuendea kwa waganga ili wakupate.
Kipindi changu cha kujifungua sitaweza kutoka mpaka miaka kumi hivyo sitakuwa karibu na wewe tena. “Mpenzi naomba usinisaliti nimechoka kubeba dhambi za wanadamu na majini kwa ajili yako.
N akuomba baada ya kuondoka kaa mbali na wanadamu, mafuta niliyokuachia siku ukinikumbuka sana jipake usiku wakati wa kulala utaniota usingizini lakini hatutaonana mpaka miaka kumi ipite,” Nargis alisema kwa hisia kali.
“Nakuahidi kuwa muaminifu kwako, sitakusaliti nakupenda sana Nargis, nilitamani niwapokee wanangu wakati wa kuzaliwa lakini sina jinsi. Nenda mpenzi wangu ukijua nakupenda kuliko kiumbe chochote kilichoumbwa na Mungu. Nakuahidi kukusubiri hata kwa miaka mia moja,” Thabit alimuahidi Nargis.
“Kweli Thabit?” Nargis alimuuliza Thabit huku akimkazia macho yake makubwa lakini yenye urembo wa aina yake. “Kweli kabisa.” “Hutanisaliti?” ulimuuliza tena. “Siwezi.” Thabit alijikuta amehama kimawazo kitu kilichomshtua Subira.
“Vipi bosi?” “Ee...ee...eeh,” Thabit alishtuka na kujikuta akifuta uso kwa mikono kama anaondoa kitu na kutuliza macho kwa Subira huku mapigo ya moyo yakienda mbio. Alitikisa kichwa kujiweka sawa huku uzuri wa Subira ukijaa tena machoni mwake.
“Bosi mbona hivyo una nini?” Subira alimuuliza akiwa amemkazia macho huku akirudisha kijiko chenye chakula kwenye sahani. “Mmh! Achana nayo tuendelee na yetu, vipi mbona huli?” Thabit alisema huku akichota chakula na kupeleka mdomoni.
“Nakula,” Subira alijibu huku akichota chakula. W aliendelea kula kimyakimya hakukuwa na mazungumzo yoyote mpaka walipomaliza na kuondoka. Walipofika ofisini Thabit alionekana amechoka hakukaa alimuaga Subira kuwa anatoka kidogo.
Baada ya kutoka Subira alijiuliza maswali mengi juu ya hali ya bosi wake kugeuka vile wakati alikuwa amechangamka na kumpa matumaini hasa pale alipoonesha kumuulizia kuhusu uhusiano wake.
Itaendelea
 
SEHEMU YA 09

Waliendelea kula kimyakimya hakukuwa na mazungumzo yoyote mpaka walipomaliza na kuondoka. Walipofika ofisini Thabit alionekana amechoka hakukaa alimuaga Subira kuwa anatoka kidogo.
SASA ENDELEA…
Baada ya kutoka Subira alijiuliza maswali mengi juu ya hali ya bosi wake kugeuka vile wakati alikuwa amechangamka na kumpa matumaini hasa pale alipoonesha kumuulizia kuhusu uhusiano wake aliamini dawa za mzee Mukti zilikuwa zikifanya kazi.
Lakini hali iliyomtokea muda mfupi baada ya kufika Steers ilimshtua sana, alijiuliza hali ile ilitokana na nini. Alinyanyua simu yake na kumpigia mzee Mukti, baada ya kuita ilijibu kuwa inatumika. Alisubiri kwa muda kidogo na kupiga tena ambayo muda ule ilipokelewa.
“Haloo.”
“Haloo mzee wangu.”
“Ndiyo mama unasemaje?”
Subira alimweleza yote yaliyotokea muda mfupi, baada ya kumsikiliza mzee Mukti Buguju alishusha pumzi ndefu na kusema:
“Subiri kidogo,” mzee Mukti alisema na kukata simu ili aangalie kilichotokea kimetokana na nini.
Baada ya muda mfupi alipiga simu iliyopokelewa na Subira.
“Ndiyo mzee wangu.”
“Nimeona.”
“Umeona nini mzee wangu?”
“Hali iliyomtokea bosi wako ilitokana na kuhama kimawazo yalikuwa ni mawasiliano kati yake na mkewe jini Nargis. Lakini yalikuwa ya kumbukumbu baada ya kuingia, Jini Nargis alijitahidi kumvuta ili azungumze naye lakini hayakuweza kumpata vizuri. Mkewe ameisha jua nini kinatendeka duniani lakini kwa sasa hana nguvu tena baada ya kuiua nguvu ya pete ambayo ndiyo iliyokuwa kiunganishi kikubwa kati ya bosi wako na mkewe jini.
Walichoweza ni kumtia uchovu ili akalale awaze kuwasiliana naye, kwa vile pete haikuwa na nguvu, lazima Jini Nargis atawatuma vijakazi wake waichukue na kuirudisha chini ya bahari kwenda kuongezewa nguvu kisha atarudishwa kabla hajaamka na kuvisha kuanzia hapo mawasiliano yatarudi kama kawaida. Na tukichelewa tutakosa kila kitu na wewe kufukuzwa kazi”
“Mungu wangu! Sasa itakuwaje?” Subira aliuliza.
“Kuna kazi nataka nikupe muda huu ili kumuwahi.”
“Kazi gani?”
“Ile dawa ya unga ipo?”
“Ndiyo.”
“Unajua anapokaa bosi wako?”
“Ndiyo, lakini sijawahi kufika.”
“Chukua hiyo dawa, kanunue maji safi lita moja na nusu kisha chukua dawa kidogo changanya. Ondoka na hayo maji nenda moja kwa moja hadi anapokaa bosi wako ukifika getini mwaga kidogo kisha ingia ndani ya uzio mwaga kidogo. Nenda mpaka kwenye nyumba ya bosi wako mwaga kidogokidogo kuizunguka nyumba yote kisha ingia ndani na kumwaga kidogokidogo nyumba nzima.
“Kuna vitu utavisikia wakati ukiendelea na zoezi hilo usiogope fanya kazi niliyokuelekeza, hata viwe vinatisha vipi endelea na zoezi lako kwa vile havitakudhuru kwani utakuwa ukiua nguvu za kijini. Utashangaa kukuta jumba lote lile hakuna mtu, kama nilivyokueleza awali baada ya mkewe jini Nargis kuondoka alimuachia vijakazi ambao walimfanyia kazi zote za usafi na kumpikia. Lakini dawa utakayoimwaga ndiyo itakayo waondoa na kutimka kwa maumivu.

Ukiisha maliza zoezi hilo ingia chumbani kwa bosi wako utamkuta amelala lakini kidoleni hana pete ambayo itakuwa imepelekwa ujinini kurudishiwa nguvu ya awali. Mpake maji kichwani na kumuacha, nenda bafuni weka maji kwenye beseni, weka dawa hiyo oga maji hayo na kubakisha mengine. Rudi ndani muamshe Thabit akiamka mshike mkono atakuwa kama zezeta kwa vile nguvu za kijini zitakuwa zimetoka.
“Mpeleke bafuni mwogeshe maji ya dawa, muda ule atarudi katika hali yake ya kibinadamu. Mtarudi chumbani mtalala kama wapenzi. Ukifanya zoezi zima kwa umakini huo ndiyo utakuwa mwanzo wako wa kuishi na Thabit.
“Najua vita itakuwa kubwa ya kutaka kukutoa mikononi mwake lakini kuna dawa nitakupa hakuna jini wala mchawi atakae kugusa. Kisha kuna kazi nyingine nzito ya kulinda mali ya Thabit ambayo ni ya majini ambao watataka kuirudisha mikononi mwao kama wakishindwa kumpata Thabit. Japokuwa najua ni ngumu lakini tutashinda na zawadi mtanipa.”
“Sawa mzee wangu nikikwama nitakupigia simu.”
“Hakuna tatizo lakini zoezi hilo lifanye sasa hivi.”
“Sawa mzee.”
“Nilitaka kusahau hakikisha baada ya kukutana naye kimwili unaondoka kuja kwangu, jitahidi kabla kivuko hakijasimama.”
“Sawa mzee wangu.”
Baada ya mazungumzo Subira alivuta droo ya meza yake na kutoa karatasi iliyokuwa na dawa ya unga, aliirudisha na kutoka kwenda dukani na kununua maji ya lita moja na nusu na kurudi nayo ofisini. Aliingia ofisini kwa bosi wake ambako aliamini ni sehemu salama na kuitia dawa kwenye maji na kuitikisa kisha aliiweka kwenye mfuko wa plastiki.
Alitoka na kukodi bodaboda hadi nyumbani kwa bosi wake, aliteremka na kumlipa dereva. Alisogea karibu ya mlango wa kuingilia, alitoa chupa yake kwenye mfuko na kuishikilia mkononi. Huku mapigo ya moyo yakimwenda kwa kasi alitembea kuelekea mlango mkuu.
Aliifungua chupa na kuanza kumwaga getini, maji yalipogusa chini alisikia mtikisiko, japokuwa mapigo ya moyo yaliongezeka lakini alijikaza na kuingia ndani. Kila alipomwaga maji mtikisiko mkubwa ulitokea. Akwenda hadi kwenye jumba la kifahari na kuendelea na zoezi la kumwaga maji kuizunguka nyumba ile.
Mtikisiko uliongezeka mara dufu aliona kama nyumba inataka kudondoka, kama asingepewa maelekezo angekimbia hali ilikuwa ikitisha sana. Baada ya kumaliza zoezi la kuzunguka nyumba aliingia ndani na kuendelea na zoezi lake. Alishangaa kukuta nyumba tupu lakini ikinukia manukato mazuri sana.
Alipoanza kunyunyiza maji ndani alisikia vishindo na sauti za vilio vya maumivu.
Itaendelea
 
SEHEMU YA 10

“Kwani pete yake si anayo?” dada yake Hailat aliuliza.
“Ndiyo lakini nashangaa simuoni.”
“Basi atakuwa ameivua.”
“Hebu rudi kwanza ndani ukaangalie vizuri,” mama yake alimshauri.
Nargis alirudi ndani kuangalia tena, lakini alikuta hali ni ileile kiza kizito kilitanda eneo lile.
SASA ENDELEA...
Alitoka kwenda kuwaeleza nao walinyanyuka na kuingia naye chumbani kwake kuangalia. Walishtuka kuona kiza kizito sehemu iliyokuwa ikimuwezesha Nargis kumuona mumewe.
“Mmh! Itakuwa nini?” Dada yake Hailat alishtuka.
“Mmh! Lazima kuna mchezo umechezwa si bure,” mama yake alijibu.“Kibaya hata sioni dalili za pete,”Nargis alisema kwa kukata tamaa.
“Siyo tatizo, watume Watwana wakamtie uchovu akirudi nyumbani wamvue pete na kuileta huku na kuirudishia nguvu yake kisha tutamchukua na kumwekea kivuli kisha tunamrudisha duniani huku tukiwaondoa wafanyakazi wote wanadamu na kampuni yake itaendeshwa na majini, kila atakapokuwa wanadamu hawatamuona,” alisema mama yake.
“Hilo ndilo la kufanya japokuwa najua vita ya wanadamu ni nzito sana, basi tu mdogo wangu mbishi kwa nini usiachane na huyo mwanaume kwa vile tayari amekupatia watoto,” dada yake alimshauri.
“Dada hayo ni maneno gani? Kumbuka yule ni mume wangu wa ndoa halali, baba wa watoto wangu, siwezi kurudi nyuma nitapambana hadi tone la mwisho la damu yangu,” Nargis alisema kwa uchungu.
“Basi tu ingekuwa amri yangu ningemuulia mbali mwanaume anayekosa uaminifu,” dada yake alisema kwa hasira.
“Mmh! Sasa hebu waite watwana wafanye hiyo kazi muda huu,” Malkia Zabeda alitoa amri.
Nargis alijishika katika paji la uso, mara walitokea watwana na kupiga magoti mbele yake na kuuliza.
“Mwana wa mfalme una shida gani?”
Aliwapa maelekezo ya kumtia uchovu Thabit, akilala wachukue ile pete haraka na kuipeleka chini ya bahari. Baada ya kuelezwa vile walitoweka ghafla na kwenda moja kwa moja ndani ya ofisi alipokuwa Thabit amerudi muda mfupi toka hotelini walipokwenda kupata chakula cha mchana na Subira.
Waliingia na kumpuliza kisha walisimama pembeni, ghafla Thabit alianza kujinyoosha baada ya kusikia uchovu mkubwa mwilini mwake. Aliona hawezi kuendelea na kazi alitoka na kumuaga Subira aliyeshtuka na kurudi nyumbani kulala. Alipopanda kitandani usingizi mzito ulimchukua.
Watwana waliotumwa walimvua pete na kuondoka nayo kurudi nayo chini ya bahari, walipofika walimkabidhi Nargis. Aliipokea na kuishangaa ilivyokuwa imepoteza mvuto kwani ilikuwa imechakaa sana. Hakuamini kama ile ndiyo pete aliyomvalisha mumewe Thabit.
Baada ya kuichunguza sana aligundua ilikuwa yenyewe isipokuwa ilichezewa na kuondolewa nguvu za kijini. Baada ya kugundua hali ile roho ilimuuma sana mpaka machozi yakamtoka. Moyoni alijikuta akiwachukia wanadamu kwa kitendo cha kumchokonoa kila kukicha.
Aliishika ile pete na kumpelekea mama yake huku akilia.
“Mama hebu ona jinsi wanadamu wanavyonitafuta ubaya.”
“Mmh! Kazi ipo kama pete imekuwa hivi basi kweli wamefanya kazi kubwa.”
“Sasa tutafanyaje?”
“Irudishiwe nguvu, irudishwe kwa Thabit kisha aletwe hapa mara moja.”
Ilichukuliwa pete na kurudishiwa nguvu kubwa kuliko ya awali ambayo kila atakayeigusa kwa nia mbaya anaungua moto.
Pete ilikuwa ikiwaka mwanga mkali, kama una nia mbaya ukiutazama lazima ukupofue macho.
Pete ilikuwa nzito kubebeka hata Nargis ilimshinda kuinyanyua na kumuuliza mama yake.
“Mama mbona imekuwa nzito hivi?”
“Uzito wake ndiyo utakavyokuwa uzito wa mumeo, hataguswa na kitu chochote.”
“Sasa ataivaaje?’
“Hebu ibebe tena.”
Nargis alibeba na kushangaa kuona ikiwa nyepesi kama kawaida:
“Mbona imekuwa nyepesi?”
“Ilikuwa haijapoa sasa hivi ukimvisha mumeo hataguswa na kitu chochote.”
“Asante mama,” Nargis alimshukuru mama yake.
Baada ya zoezi lile waliitwa watwana na kutwa wairudishe pete kwa Thabit na kumchukua kurudi naye chini ya bahari kwa ajili ya kumtengeneza ili asiweze kuonekana kwa macho ya kibinaadamu. Safari ile aliyewaita watwana alikuwa Malkia Zabeda mama wa Nargis ambaye alitoa kauli nzito kuhakikisha hawafanyi mchezo siku zote atakacho watuma na kwenda kinyume ningegharimu maisha yao.
Walipofika kwake walilala kifudifudi ili kusikilia mke wa mfalme anataka kuwatuma nini. Lakini kabla hajawatuma walishtushwa na vilio vya wajakazi walioingia ghafla.
“Kuna nini?” Malkia Zabeda aliuliza kwa mshtuko.
“Hatari, “ walisema kwa pamoja huku wakijilaza kifudifudi mbele na malkia wa bahari.
“Ya nini?”
“Nyumba inawaka moto.”
“Nyumba inawaka moto! Nyumba gani?”
“Ya..ya..dada.”
“Nyumba ya mume wangu Thabit, baba Zumza?” Nargis aliuliza kwa mshtuko.
“Ndi...yo mwana wa mfalme.”
“Mungu wangu!” Nargis alisema huku akishika mikono kichwani.
“Hebu kwanza elezeni vizuri kuna nini?” Hailat dada yake Nargis aliuliza.

Tulikuwa ndani tumepumzika, baba Zumza alirudi mapema na siyo kawaida yake na kusema amechoka na kwenda chumbani kwake kupumzika. Ghafla walikuja kina Suunu ambao walisema umewatuma pete ya mumeo. Baada ya kuichukua waliondoka na kutuacha tukimuandalia kinywaji,” alisema mmoja wao.
taendelea
 
SEHEMU YA 11


“Hebu kwanza elezeni vizuri kuna nini?” Hailat dada yake Nargis aliuliza.
“Tulikuwa ndani tumepumzika, baba Zumza alirudi mapema na siyo kawaida yake na kusema amechoka na kwenda chumbani kwake kupumzika.
Ghafla walikuja kina Sunu walisema umewatuma pete ya mumeo. Baada ya kuichukua waliondoka na kutuacha
tukimuandalia kinywaji. Alisema mmoja wao.
SASA ENDELEA...“
Lakini ghafla tulianza kusikia mtikisiko mkubwa nje ya nyumba na baadaye nyumba ikaanza kutikisika ghafla tukaanza kuona moto kila kona kitu kilichotufanya tutoke mbio kuokoa maisha yetu.”
“Mmh! Wakati nyumba inaungua mume wangu alikuwa wapi?” Nargis aliuliza kwa hofu.
“Ndani amelala.”
“Mungu wangu mume wangu atakufa, mama watume wakamuokoe.”
Watwana waliokuwa bado wamelala kifudifudi walitumwa kwenda kumuokoa Thabit, baada ya amri ile walitoweka mara moja na kwenda moja kwa moja nyumbani kwa Thabit.
Walipofika eneo la nyumba walishangaa kukuta bahari, hali ile iliwashtua sana na kujikuta
wakijiuliza labda wamekosea kila waliporudia ramani yao eneo lilikuwa lilelile.
Walijikuta wakiulizana wenyewe:
“Jamani tumekosea wapi?”
“Hatujakosea hapo kwenye bahari ndipo kwenye hiyo nyumba kwani nyumba tuliyofikia kabla ya kuingia ndani si hiyo hapo pembeni
ya bahari?” mmoja alisema.
“Sasa tutafanyaje kama hakuna nyumba tuliyotumwa na mume wa mwana wa mfalme tutamuona wapi?”
“Jamani ile si bahari basi tuingie ndani ya maji ili tujue ndani kuna nini.”
“Poa.”
Walikubaliana na kuteremka ndani ya ile bahari, walipoyagusa maji wote walitoka haraka kila mmoja akipiga kelele za maumivu ya kuungua na moto.
“Motooo!”
Bahari ilikuwa inaunguza walisimama huku kila mmoja akionesha majeraha ya moto.
“Jamani hii ngoma nzito turudishe taarifa.”
“Hatuna jinsi.”
Walikubaliana kurudi chini ya bahari kurudisha taarifa ya hali halisi waliyokutana nayo sehemu yenye nyumba ya Thabit.
Walirudi chini ya bahari kurudisha taarifa, walipofika walimkuta Nargis akiwasubiri kwa hamu kutaka kujua wamefikia wapi
badala ya kurudi bila mumewe.
“Vipi?”
“Hali ni mbaya.”
“Kuna nini?”
“Nyumba haionekani zaidi ya bahari.”
“Bahari imefanya nini?”
“Sehemu yenye nyumba kuna bahari kubwa sana.”
“Sasa kwa nini msiingie ndani?”
“Yaani hali inatisha tumeingia tumeungua vibaya, bahari ina maji ya moto ajabu,” walionesha majeraha.
“Mmh! Sasa nimeelewa,” malkia Zabeda alisema.
“Nini mama?” Nargis aliuliza huku machozi yakimtoka.
“Wametuwahi.”
“Kivipi mama?”
“Inaonesha jinsi gani aliyepanga mpango wa kumchukua mumeo amefanikiwa. Tulitakiwa tumchukue badala ya kuichukua pete tu lakini tumechelewa.”
“Mama sikubali... sikubali nitakufa na mtu.”
“Lazima tujipange la sivyo safari hii tutapotea kabisa.”
“Sasa nitafanyaje?” Nargis aliuliza huku machozi yakimtoka.
“Labda dada yako akusaidie kwa vile wewe huwezi kwenda huko kwa sasa.”
“Mama mimi siendi kokote nilimueleza toka zamani akawa mbishi juu ya wanadamu, mimi nawafahamu vizuri kuliko yeye anayekurupukia mambo.
Wanadamu tunawapenda tu lakini ni viumbe wabaya kuliko hata nyoka mwenye sumu kali. Kama walishindwa kuishi katika bustani ya edeni waliyopendelewa na Mungu wataweza vipi kukaa na viumbe wengine.
“Ningekuwa mimi ningemuulia mbali tena mdogo wangu una bahati umepata watoto ulikuwa ukiwatafuta. Muulie mbali uachane na
maisha ya mashaka, wapo majini wazuri kuliko Thabit wanaokupenda Zahal au Mehoob wapo tayari kukuoa hata leo.”
“Dada bado hujanishawishi yule ni mume wangu hivyo siwezi kumuua kwa ajili ya yaliyotokea, vilevile hakuna mwanaume wa kijini atakayemshinda uzuri mume wangu Thabit.
Najua aliyefanya vile ni mwanamke, kwani siku zote wanawake tumekuwa ndiyo chanzo cha
matatizo.
Hao wanadamu wasingetoka katika bustani ya edeni bila sisi wanawake ambao ndiyo chanzo cha kufukuzwa kwao.
“Hata kama hamtanisaidia nitapigana peke yangu hata nikifa kwa ajili ya kupigania haki yangu siogopi kitu.”
“Ukifa nani atakulelea wanao?” dada yake alimuuliza.
“Mtavyowafanya mtajua nina imani nao wakikua watalipa kisasi kwa atakayeniua mama yao.”
“Nargis mwanangu, inavyonekana watu tutakaopambana nao wamejizatiti. Kama wameweza kuua nguvu ya pete na kuingia kwenye nyumba tuliyoitengeneza, basi kazi ipo tunatakiwa kuongeza nguvu.”
“Ninyi piganeni mimi simo, siwezi kuumia kwa kitu kisicho na faida, atajua mwenyewe atakavyofanya. Kwa nini kila siku tuwe tunapambana na wanadamu hamuoni nao wana akili pengine wameshatujulia, ndiyo maana wanafanya wanavyotaka,” dada yake Hailat alisema kwa uchungu.
“Mama naomba mnisikilize kwa makini, nina miaka minne ya kuwa huku, naomba mniachie kila kitu, sihitaji msaada wenu muda wangu ukifika nitapambana mwenyewe.
Tusije tukakosana bure kwa jambo linalonihusu mwenyewe,” Nargis alisema.
“Hilo ndilo neno hata mimi nakuunga mkono,” dada yake aliunga mkono kauli ya mdogo wake.
“Dawa iliyopo ni kuiharibu mali yake ili kumtia umaskini,” mama yao alitoa wazo.
“Mama hiyo siyo dawa, Thabit hana kosa lolote zaidi ya huyo aliyefanya mchezo ule,” Nargis alimtetea mumewe.
“Sawa lakini tukimtia umaskini, lazima yule mwanamke atamkimbia na wewe utapata nafasi ya kumpata mume wako.”
“Una uhakika gani kama huyo mwanamke atamkimbia, sitaki kuharibu chochote kwenye mali ya Thabit. Sitaki apate tatizo lolote ila nitahakikisha anarudi mikononi mwangu.”
Itaendelea
 
SEHEMU YA 12

“Sawa lakini tukimtia umaskini lazima yule mwanamke atamkimbia na wewe kupata nafasi ya kumpata mume wako.”
“Una uhakika gani kama huyo mwanamke atamkimbia, sitaki kuharibu chochote kwenye mali ya Thabit. Sitaki apate tatizo lolote ila nitahakikisha anarudi mikononi mwangu kwa jasho na damu.”
SASA ENDELEA...
“Sawa, kwa vile umeamua mwenyewe hatutaingilia uamuzi wako,” mama naye aliunga mkono.
Walikubaliana kuliacha lile jambo mpaka muda wa Nargis kurudi duniani na kujua watafanya nini. Baada ya Nargis kwenda chumbani kwake mama na dada yake walikuwa na kikao cha faragha kuhusiana na jambo lile ambalo Malkia Zabeda lilimuumiza sana akili kutokana na kumpenda sana mtoto wake wa mwisho Nargis.
“Mwanangu sasa tutafanyaje suala la mdogo wako?”
“Mama mimi msimamo wangu ni uleule, kama upo tayari nikamuulie mbali baba Zumza ili tumalize kero zote.”
“Hapana tutafute njia nyingine kwa vile unamjua vizuri mdogo wako kifo chochote na mumewe tutazua ugomvi mkubwa hata kupoteza uhai wa mmoja wenu.”
“Ndiyo maana mimi nimejitoa kwenye jambo hili najua lina lawama baadaye.”
“Kwa nini usitekeleze mpango nilioupanga?”
“Mpango gani?”
“Wa kumtia umaskini Thabit ili mwanamke aliyenaye amkimbie kwa vile najua amempenda kwa ajili ya mali kisha mdogo wako ampate mumewe.”
“Mamaaa! Bado tatizo litakuwa palepale.”
“Kwa nini?”
“Hata tukimrudisha, kwa vile wataendelea kuishi duniani tatizo lazima litajirudia huenda hilo likawa kubwa kuliko yaliyotangulia.”
“Wee fanya kwanza nilivyokutuma kilichobaki niachie mimi.”
“Sawa basi kazi hiyo nitaifanya usiku wa kesho ili akiamka siku ya pili akute amerudi katika umaskini.”
“Tena itatusaidia kwa vile miaka minne atamkuta amechoka kama mpira wa makaratasi.”
“Sawa mimi nitatekeza ulichonituma.”
“Ukifanya hivyo utanifurahisha sana, kazi itakayobaki niachie mimi,” Malkia Zabeda alifurahi mwanaye mkubwa kukubali kumsaidia mdogo wake.
Baada ya kikao kile cha faragha waliendelea na mambo mengine huku mpango ukiwa wa siri ambao Nargis hakuujua. ***
Baada ya Subira mipango yake kwenda kama alivyotaka na kufanikiwa kumteka kimapenzi Thabit bila kujua, aliianza siku kwa Thabit.
Alimuandalia kifungua kinywa kitamu kilichochanganywa na dawa ili asione tofauti ya mapishi ya kijini na kibinaadamu.
Baada ya kufungua kinywa waliondoka pamoja hadi kazini kama mke na mume. Thabit aliingia katika ofisi yake na kumuacha Subira akifanya majukumu yake kama msaidizi. Akiwa anaendelea na kazi alikumbuka kumueleza mzee Mukti kuhusu mipango ilivyokwenda.
Baada ya kumueleza hatua waliyofikia mganga naye alimueleza kuwa ameota ndoto iliyomtisha sana kuwa mali zote za Thabit zinateketea na moto na Thabit kawa maskini anayetembea mjini akiomba.
“Mungu wangu! Hilo si tatizo?” Subira alishtuka.
“Ni kweli tatizo, lazima usiku wa manane tuzunguke sehemu zote kwenye mali za mpenzi wako kuzizindika kwa vile inaonesha hali ya hatari ipo mbele juu ya mali hizo.”
“Sawa mzee wangu.”
Walikubaliana usiku wafanye zindiko kwenye maduka yote ya Thabit kabla kitu kibaya hakijatokea. Subira alifanya kazi moyo wake ukiwa umejaa hofu, alifikiria kumweleza Thabit ndoto ya mganga lakini alihofia kuulizwa ilikuwaje akajuana na mganga. Alitamani usiku uingie upesi ili wakaifanye kazi ile kabla tatizo halijatokea.
Majira ya saa saba usiku mganga Mukti Buguju aliongozana na Subira katika maduka ya Thabit kuyafanyia zindiko kabla tatizo aliloota halijatokea. Alianza na maduka mawili ya Kariakoo yaliyokuwa karibukaribu. Mzee Mukti na wasaizidi wake wakiwa katika vazi la shuka nyekundu waliyojifunga chini mgongo wazi na vilemba vyekundu. Mkononi alishika usinga huku msaizidi wake akiwa ameshika beseni lenye dawa.
Mganga alichovya usinga kwenye maji ya dawa na kumwagia kuzunguka ofisi kisha aliingia ndani na kufanya dawa zake kila kona na kutoka. Baada ya kumaliza duka moja alikwenda la pili na kufanya aliyofanya duka la kwanza. Baada ya kumaliza zoezi lile walipanda gari kuelekea Posta kwenye duka lililobakia.
Mzee Mukti hakuvua nguo za kazi na vijana wake mpaka maeneo ya Posta, walipokaribia jengo lenye duka la Thabit walishtuka kuona moto ukiwaka.
“Ha! Jengo linaungua,” Subira alipiga kelele.
“Kwani tunakwenda jengo gani?” mganga aliuliza.
“Hilo linaloungua.”
“Mmh!” mganga aliguna na kufanya Subira kushtuka.
“Vipi mbona unaguna?”
“Tunachelewa,” alisema mganga kwa sauti ya kukata tamaa.
“Tumechelewa nini?” Subira aliuliza.
“Ule moto si wa kawaida, kwani duka lake lipo wapi?”
“Pale moto unapowaka.”
“Tungejua tungeanza zoezi letu mapema, inaonesha ile ndoto leo ndiyo siku yake ya kuteketeza mali za Thabit ili arudi katika hali ya umaskini,” alisema mzee Mukti.
“Mungu wangu!” Subira alishika mikono kichwani.
“Majini wana hasira baada ya kushindwa kumrudisha Thabit kwao wameamua kuharibu mali zake ili arudi katika umaskini.”
“Kwa hiyo na yale maduka nayo yatateketea?”
“Yale yatakuwa salama hawataweza kufanya chochote kwa vile tumewahi tungechelewa ingekuwa kilio cha kusaga meno.”
Itaendelea
 
SEHEMU YA 13

“Majini wana hasira baada ya kushindwa kumrudisha Thabit kwao wameamua kuharibu mali zake ili arudi katika umaskini.”
“Kwa hiyo na yale maduka nayo yatateketea?”
“Yale yatakuwa salama hawataweza kufanya chochote kwa vile tumewahi tungechelewa ingekuwa kilio cha kusaga meno.”
SASA ENDELEA...
Wakati wakizungumza walishangaa moto kuzimika ghafla na kujikuta wote wakishangaa.
“Mmh! Mbona moto umezimika ghafla?” aliuliza subira na kumfanya mzee Mukti naye kushangaa.
“Hii ajabu!”
Waliteremka kwenye gari na kuelekea kwenye duka lililokuwa sehemu ya chini, kama kawaida alianza kufanya dawa zake kwa nje ya duka kisha aliingia ndani. Walipoingia ndani walishtuka kukuta vitu vyote vimeteketea kwa moto. Ajabu ilikuwa vilivyoungua ni vitu vyote vya dukani tu lakini ndani hakukuwa na dalili za moto kuwaka.
“Mungu wangu mbona maajabu haya,” Subira alisema huku akishika mikono kichwani.
“Ule moto ni wa kijini ambao huaribu kilichokusudiwa tu.”
“Jamaniiii!” Subira alisema kwa sauti ya kukata tamaa.
“Huku tumechelewa, hatuna jinsi turudini nyumbani.”
Kwa vile muda ulikuwa umekwenda sana waliingia kwenye gari na kurudi nyumbani.
***
Subira ilibidi akae kimya kuhusiana na tukio zito la usiku ule huku akiwa haamini kama kweli moja ya duka la Thabit lilikuwa limeunguzwa na moto wa kichawi. Walilala mpaka asubuhi ili asikie nini kimetokea au ilikuwa ndoto na wala hakuna kilichotokea.
Asubuhi wakiwa bado wapo kitandani simu iliingia, Thabit aliichukua na kuweka sikioni na kupokea.
“Haloo Juma,” alikuwa msimamizi wa duka la Posta.
“Za asubuhi bosi.”
“Nzuri, kwema.”
“Si kwema bosi.”
“Kuna nini?”
“Duka limeungua lakini moto wake wa ajabu.”
“Mungu wangu! Jengo zima limeungua?” Thabit alitaharuki.
“Siyo jengo lote ni duka letu tu.”
“Hakuna hata kimoja kimepona.”
“Kumebakia majivu tu.”
“Na maduka ya mjini?”
“Huko sijui.”
”Subiri.”
Alikata simu na kupiga mjini, baada ya kuita kwa muda ilipokelewa.
“Haloo bosi.”
“Sadiki upo wapi?”
“Kazini.”
“Kwema?”
“Kwema, tena bosi lile kontena nasikia linatua kesho usiku, nina imani tutatumia mwezi mzima na kazi ya kupakua na kupanga vitu madukani.”
Kutokana na nguvu za kijini zilizowekwa na jini Nargis kwa mumewe kila kukicha utajiri wa Thabit ulikuwa ukikua kutokana na kuwa karibu kiutendaji na majini waliosimamia mali zake chini ya usimamizi wa mkewe.
Zaidi ya maduka yale matatu, alikuwa amepanga kufungua maduka makubwa ya vyakula kila wilaya pia duka kubwa sana maeneo ya kituo cha daladala cha Mwenge, lingine kubwa kuliko yote City Center. Alikuwa ameagiza kontena kumi za bidhaa mbalimbali. Kati ya maduka hayo matatu la City center matano, la Mwenge matatu na mengine mjini.
Ndoto ya Nargis kuhakikisha Thabit anakuwa tajiri mkubwa dunia hiyo alipanga atakaporudi duniani na kuishi na mumewe kama mwanadamu wa kawaida basi wawe na maisha mazuri. Kila kukicha alihakikisha utajiri wa Thabit unazidi kuongezeka na si kupungua.
“Hakuna tatizo lolote.”
“Hakuna tupo shwari.”
“Sawa.”
Alikata simu na kupiga duka lingine na kukuta nako hali shwari, alirudia kupiga tena Posta na kupokelewa.
“Naam bosi.”
“Kuna mabadiliko yoyote?”
“Hakuna.”
“Nakuja.”
“Sawa.”
Alikata simu na kuteremka kitandani kitu kilichofanya Subira aulize.
Mpenzi mbona umeamka haraka hivyo?” Subira alijifanya hajui kitu.
“Kuna tatizo.”
“Tatizo gani?”
“Sijajua ila nimeambiwa niende duka la Posta.”
“Twende wote,” Subira alisema huku akinyanyuka kitandani na kumfuata Thabit, walikwenda bafuni kuoga na kutoka pamoja hata kifungua kinywa hawakunywa siku hiyo.
Waliingia kwenye gari na kuelekea Posta, walikwenda hadi eneo la tukio na kukuta nje ya jengo kazi zikiendelea kama kawaida hakukuwa na mshtuko wowote kama kuna tukio kwani jengo lilikuwa katika hali ya kawaida hakukuwa na dalili zozote za moto kutokea. Aliwakuta wafanyakazi wake zaidi ya arobaini wakiwa ndani ya jengo wakiwa wameshika tama na wengine kutoka machozi.
Walishangaa kukuta ndani ya duka kumejaa jivu vitu vyote vya mamilioni ya fedha vikiwa vimeteketea. Ilikuwa ni hasara kubwa kwani ilikuwa ni wiki tu aliingiza dukani mali ya zaidi ya milioni mia sita na nusu. Alijisikia miguu kumwisha nguvu lakini alijikaza na kujiuliza kile ni kitu gani, kwani kuta na sakafu za duka zilikuwa hazioneshi dalili zozote za kuungua na moto ulioteketeza mali ya mamilioni.
Wote walikuwa wapo kwenye usiku wa giza kasoro Subira alikuwa akijua kila kitu na sababu ya kuwa vile. Alimshukuru kimoyomoyo mzee Mukti kwani kama angechelewa maduka yote yangeteketea na kuwa kilio cha kusaga meno. Kutokana na dawa alizolishwa Thabit na Subira alijikuta akisahau kabisa chanzo cha mali ile ni mkewe jini Nargis.
“Hii si bure lazima kuna mkono wa mtu,” alisema mmoja wa wafanyakazi.
“Wameona sisi ndiyo tunafanya vizuri hivyo lazima wametuendea mbali, moto gani usiounguza sehemu yoyote zaidi ya bidhaa za dukani wanataka tukale wapi?” msichana mmoja alisema huku akili.
Itaendelea
 
SEHEMU YA 14


“Hii si bure lazima kuna mkono wa mtu,” alisema mmoja wa wafanyakazi.
“Wameona sisi ndiyo tunafanya vizuri hivyo lazima wametuendea mbali, moto gani usiounguza sehemu yoyote zaidi ya bidhaa za dukani, wanataka tukale wapi?” msichana mmoja alihoji huku akilia.
Endelea...
“Nendeni nyumbani ili nitafakari kisha kesho nitawajulisha kinachoendelea, kuna kontena kumi za bidhaa zinaingia kesho usiku ambazo zilikuwa za maduka mengine nitapunguza baadhi ya makontena na kuleta hapa ili muendelee na kazi,” Thabit aliwaambia wafanyakazi wake waliokuwa wamechanganyikiwa.
“Tutashukuru bosi,” walijibu kwa pamoja.
Subira muda wote alikuwa akilia kitu kilichomfanya Thabit ambembeleze.
“Mpenzi nyamaza tutarudisha kila kilichopotea.”
“Lazima tuhangaike yasije tokea tena,” Subira alitoa wazo mbadala.
“Tutafanya hivyo.”
“Basi tumtafute mtaalamu wa kulinda mali zetu.”
“Tutamtafuta wapi?”
“Mi namjua.”
“Basi tutakwenda.”
“Tena leo hiihii.”
“Hakuna tatizo, twende tukaangalie sehemu nyingine, maana mpaka sasa moyo wangu hauna amani. Moto wa leo umenipotezea zaidi ya milioni mia nane.”
Kusikia vile Subira aliangua kilio na kumfanya Thabit aingie kazi ya kumbembeleza.
“Mpenzi nyamaza japo zimepotea hizo bado hatutatetereka.”
“Naomba jioni twende kwa mtaalamu ili alinde mali zetu.”
“Lazima tufanye hivyo ni wapi?”
“Kigamboni.”
“Itabidi tuwahi kwenda.”
“Tuondoke saa kumi na mbili.”
Walikubaliana saa kumi na mbili kwenda Kigamboni kwa mganga, kukubali kwenda kwa mganga kulimfanya Subira kufurahia kuweza kumpeleka Thabit bila kujua na yeye kumaliza mambo yake ya kumdhibiti ikiwemo ndoa ya haraka.
Baada ya kukubaliana Subira alimpigia simu mzee Mukti kumjulisha mpango wa kumpeleka kwake umefanikiwa.
“Niambie binti,” alisema mzee Mukti baada ya kupokea simu.
“Babu kila kitu kimekwenda vizuri, jamaa kakubali kuja hivyo maliza kila kitu.”
“Hilo si la kuniambia bali ndiyo nilichokuwa nikikiomba usiku na mchana, mkitoka hapa utaniambia ndoa itavuma kwa kasi kama vumbi kwenye upepo mkali.”
“Yaani nitashukuru mzee wangu.”
“Kama amekubali mwenyewe jua amekwisha.”
“Basi jioni wageni wako.”
“Karibuni sana.”
Baada ya kukubaliana na mganga Subira alijipanga jioni kumpeleka Thabit ili akammalize kabisa.
CHINI YA BAHARI
hini ya bahari jini Hailat dada wa Nargis alirudi akiwa amechoka sana mwili ukiwa na mabaka ya moto. Mama yake alipomuona alishtuka na kutaka kujua mwanaye safari aliyokwenda amekutana na nini kilichomfanya aumie vile.
“He! Vipi tena mwanangu?”
“Mama hatari, wametuwahi!” alisema huku akijiangalia makovu ya moto.
“Kivipi?”
“Wamewahi kuzikinga mali zao japo tumefanikiwa kuharibu duka moja ambalo ndilo kubwa. Lakini mengine wameyakinga yanaonekana kama bahari nilipojaribu kuingia niliungua, bila uwezo wa kijini ningekufa kifo kibaya.
Mama sikubali nami naingia katika vita hii kuhakikisha namuondoa duniani Thabit na mganga wake sijali atakachokifanya Nargis, nipo tayari kwa lolote,” Hailat alisema huku akimwaga machozi ya hasira.
“Hebu tulia basi kazi hii nimekutuma mimi, nataka unisikilize mimi si mtu mwingine.
Kama umefanikiwa kuharibu mali moja tutajipanga kuharibu zote. Kuna kitu kimeingia kwenye akili yangu muda si mrefu. Kuna mali ya mabilioni ya Thabit ipo baharini inapita usiku huu utakwenda kuimaliza yote, hakikisha linabaki jivu.
Kwa pigo hilo tutakuwa tumemmaliza na mali zake zote zitakazopitia majini tutaziharibu, lazima atafilisika tu,” Malkia Zabeda alipanga kuyateketeza makontena yote kumi ya mali za Thabit na mali zote zitakazopita baharini.
“Sawa mama, kwa kazi hii sina haja ya kupumzika wala kusikilizia maumivu ya moto, tena nitaifanya mwenyewe bila kumshirikisha mtu,” Hailat alikubaliana na mama yake.
Hailat pamoja na maumivu ya moto lakini alifurahia kuziteketeza mali zote za Thabit zilizokuwa zikipita baharini usiku ule.
Alipanga kutopumzika na kuifanya usiku uleule ili asubuhi kila kitu kiwe kimekwisha. Alijipanga kuifuata meli yenye makontena ya bidhaa za watu na kuharibu za Thabit tu.
Hakutaka kuwashirikisha majini wengine kwa kuogopa taarifa kumfikia Nargis na kuharibu mpango mzima.
Aliamini hasara ya kuteketeza mali zile lazima zingemtia umaskini kwa kujua kwa mtindo ule lazima atayumba kifedha kwa vile wangeendelea kuharibu vitu vyote vitakavyopita njia ya bahari. Alihakikisha kila kona atakayoitumia kuingiza mali zake wanaziharibu. ***
Majira ya saa kumi na mbili jioni Thabit na Subira walivuka kivuko cha Feri mpaka Kigamboni. Baada ya kuvuka waliendelea na safari yao kuelekea Mji Mwema kwa mganga Mukti Buguju. Baada ya muda mfupi walifika nyumbani kwa mganga. Kwa vile Subira aliishamtaarifu kuwa wanakwenda walipokewa kwa heshima zote.
Hakukuwa na haja ya kukaa foleni, waliingizwa moja kwa moja chumba cha matibabu.
“Karibuni sana.”
“Asante,” waliitikia pamoja.
“Karibu mzee,” mzee Mukti alimkaribisha Thabit aliyeoneka kapendeza kwa fedha.
“Asante mzee wangu.”
“Jamani mna tatizo gani?” mzee Mukti alijifanya kama ndiyo siku ya kwanza kuonana na watu wale.
“Mzee wangu tuna tatizo, kuna vitu vimetutokea leo asubuhi ambavyo vinaonekana si vya kawaida,” Subira alianza kutoa maelezo.
Itaendelea
 
SEHEMU YA 15

Karibuni sana.”
“Asante,” waliitikia pamoja.
“Karibu mzee,” mzee Mukti alimkaribisha Thabit aliyeonekana kapendeza kwa fedha.
“Asante mzee wangu.”
“Jamani mna tatizo gani?” mzee Mukti alijifanya kama ndiyo siku ya kwanza kuonana na watu wale.
“Mzee wangu tuna tatizo, kuna vitu vimetutokea leo asubuhi ambavyo vinaonekana si vya kawaida,” Subira alianza kutoa maelezo.
sasa endelea...
“Eti mzee kuna nini?” mzee Mukti alimgeukia Thabit hakutaka Subira azungumze.
“Mzee wangu leo nimetokewa na jambo la ajabu baada ya moto wa ajabu kuteketeza duka langu lenye thamani ya mamilio ya fedha. Kwa kweli mpaka sasa nimechanganyikiwa sana sijui tatizo lile linatokana na nini.”
Mzee Mukti alijifanya akipiga ramli ya uongo kwa vile kila kitu alijua kisha alisema:
“Hapa panaonesha kuna kijicho kwa watu wasiopenda maendeleo yako ambao ndiyo wamefanya mchezo huu.”
Ilibidi atengeneze uongo kuogopa kumwambia ukweli kuwa aliyefanya vile ni jini anayetaka kumtia umaskini baada ya kuchukuliwa mumewe. Aliamini angemwambia vile lazima angekumbuka ahadi aliyomuahidi mkewe jini Nargis kwamba hatamsaliti akiwa mbali naye.
“Nani aliyefanya hivyo?” Thabit alitaka kujua.
“Kwa kweli hapa kuna giza hawaonekani vizuri, lakini najitahidi kuliondoa giza ili tuwajue.
“Kwa hiyo shida yao nini?”
“Kutaka kukurudisha katika umaskini.”
“Kwa hiyo mzee utatusaidiaje?”
“Kwa vile tatizo nimeshaliona nitazindika mali zako zote pamoja na nyumba yako kuhakikisha hupotezi tena mali zako. Na zoezi lifanyike usiku wa leo pia nitakupeni dawa za kuwalinda wote na watu hao wabaya.”
“Na mali zilizopotea zitapatikana?”
“Ile haitapatikana ila iliyopo haitapotea tena.”
“Mmh! Nitashukuru.”
“Kwa hiyo kuna dawa nitawapa mnywe na kuoga pamoja, kisha nitawapa zindiko.”
“Hakuna tatizo.”
Baada ya kusema vile mganga aliandaa tiba ili baadaye waende kwenye kazi ya kuzindika maduka kwa kulashia kwa vile kazi alikwisha imaliza toka jana yake usiku.
Mzee Mukti aliwaandalia dawa ambayo ilikuwa ya aina mbili moja ya kumlinda Thabit na majini na nyingine kumsukumia kwa Subira ili ndoa iwahi mapema.
Baada ya zoezi lile waliondoka mpaka kwenye maduka na mzee Mukti alijifanya yupo bize kumbe uongo alikuwa akipaka maji tu. Baada ya zoezi ambalo halikuchukua muda mrefu walirudi nyumbani. Mzee Mukti siku hiyo alilala nyumbani kwa Thabit na kuongeza nguvu kwenye zindiko lake la awali usiku uleule.
Baada ya zoezi lake alipewa chumba kizuri akalala, katikati ya usingizi alishtuliwa na ndoto iliyomtisha, aliota bahari yote ikiwaka moto. Alijiuliza ndoto ile ina maana gani, kwani kila alipoangalia kwenye rada zake hakuona kitu kingine zaidi ya moto mkubwa umetanda baharini.
Baada ya kushindwa kutambua ndoto ile aliachana nayo na kuendelea kulala akisiburi taarifa yoyote kutokana na njozi yake.
Usiku mkubwa jini Hailat dada wa Nargis pamoja na uchovu alitoka chini ya bahari na kwenda kwenye meli iliyokuwa imebeba Makontena ya bidhaa mbalimbali yakiwemo ya Thabit. Alipofika aliyachagua ya Thabit na kuyawasha moto wa kijini na kurudi chini ya bahati kumpelekea taarifa mama yake. Alipofika alimueleza mama yake kazi aliyomtuma aliifanya.
“Vipi hukukutana na vikwazo?” mama yao Malkia Zabeda aliuliza.
“Walaa, kazi ilikuwa nyepesi kuliko ya madukani.”
“Basi kapumzike mwanangu na jambo hili libakie siri yetu.”
“Hakuna tatizo.”
“Ila bado kuna kazi nyingine nitakupa.”
“Juu ya Thabit?”
“Ndiyo, nina imani hiyo ukiifanya japo utakutana na upinzani mkubwa lakini utaifanikisha. Mdogo wako Nargis kwa sasa hawezi kutuelewa lakini baadaye atatushukuru.”
“Na kuhusu yule mganga?”
“Achana naye, huyo atuhusu alichofanya ni kazi.”
“Nilitaka kula naye sahani moja hawezi kunitia makovu ya ukubwani.”
“Achana naye inaweza kumbumbulua Nargis.”
“Sawa mama nimekuelewa.”
Kwa vile muda ulikuwa umekwenda sana waliagana kila mmoja aliingia chumbani kwake kulala.
Kama kawaida meli ilitia nanga katika bandari ya Dar es Salaam, baada ya taratibu zote mizigo ilianza kupakuliwa na kuwekwa sehemu kwa ajili ya kuchukuliwa na wenyewe. Vijana wa Thabit nao walikuwepo na magari makubwa ya kubebea mizigo ili kuisambaza.
Magari yalibeba mizigo kama kawaida na kuisambaza kwenye maduka yote ikiwemo kutenga makontena mawili kwa ajili ya duka la Posta lililounguzwa vitu vyake na moto wa ajabu. Baada ya kufikishwa zoezi la kufungua makontena lilianza mara moja. Msimamizi alishtuka kuona majivu ndani ya kontena bila bidhaa zilizoagizwa.
Itaendelea
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom