UpoHuu mzigo naona ndio umekwisha
SEVEN DAYS IN HELL (SIKU SABA KUZIMU)- 70
ILIPOISHIA:
Wakati wote wakiendelea kulia, nilisikia mlango ukifunguliwa tena, nikamuona Junaitha akiingia lakini tofauti na wengine, yeye uso wake ulikuwa mkavu kabisa, akatembea harakaharaka mpaka pale nilipokuwa nimelala, akanitazama usoni, na mimi nikamtazama, tukawa tunatazamana huku nikiwa na shauku kubwa ya kutaka kusikia ataniambia nini.
SASA ENDELEA...
“Najua unataka kujua kuhusu Firyaal!” alisema na kabla sijamjibu chochote, akaniambia kwamba kulikuwa na habari mbaya kwa sababu inaonekana maisha yake yanashikiliwa na uzi mwembamba sana unaotenganisha kati ya uhai na kifo. Kwa maelezo yale, nilielewa kwamba anamaanisha kwamba tayari Firyaal alishatoka kwenye ulimwengu wa kawaida, hakuwa na uhai tena.
“Tunaweza kumuokoa kutoka kwenye mdomo wa mauti lakini itatugharimu kukaa siku saba kuzimu,” alisema Junaitha, kauli ambayo ilitufanya wote ndani ya wodi ile tubaki tukimshangaa.
“Inabidi kwanza tuhakikishe wewe umerejewa na nguvu zako kwa sababu unahitajika sana kwenye kazi ya kukata minyororo ya kuzimu ambayo tayari Firyaal ameshafungwa. Nilishusha pumzi ndefu na kutulia pale kitandani.
Akaanza kutupa maelekezo kwamba, nikisharejewa na nguvu zangu, tutaomba ruhusa ya kutoka hospitalini hapo kwa sababu za kiusalama, kisha tutaomba kuondoka na Firyaal kwa ajili ya taratibu nyingine.
“Kuna kitu sijaelewa.”
“Hujaelewa nini?”
“Umesema itatulazimu kukaa siku saba kuzimu?”
“Utaelewa tu,” alijibu Junaitha huku akigeuka na kutoka, akatutaka wote tutulie pale wodini na kama akina Shamila wakitolewa, basi wasiende mbali na mlango wa kuingilia kwenye ile wodi niliyokuwa nimelazwa kwa sababu za kiusalama.
Sikukaa muda mrefu sana, Junaitha alirudi na kunisogelea pale kwenje jeraha langu, akalishika kwa kulikandamiza huku akiongea maneno ambayo hakuna aliyeyaelewa, kisha akato kichupa kilichokuwa na ungaunga fulani, akafungua bandeji upande mmoja na kunyunyizia ule unga kwenye jeraha lango.
Hapohapo nikaanza kuhisi kama moto mkali unawaka kifuani na kadiri ulivyokuwa unaongezeka, maumivu nayo yalikuwa yakipungua na mwili wangu ukaanza kurejewa na nguvu zake.
“Nashughulikia usafiri, kaeni tayari,” alisema kisha akatoka tena, wote wakawa wananitazama kwa makini usoni kuona hali yangu inaendeleaje, kwa mbali nikaanza kutoa tabasamu hafifu lililoamsha matumaini mapya kwenye moyo wa kila mmoja.
Baadaye, Junaitha alirudi tena, safari hii akiwa ameongozana na manesi ambao waliniandaa vizuri, tayari kwa kuondoka. Wakanisaidia kuninyanyua pale kitandani, na kunitoa mpaka kwenye maegesho ya magari, wote tukaingia ndani ya gari na kushtuka kugundua kwamba mwili wa Firyaal pia ulikuwa ndani ya lile gari, akionesha kutokuwa na uhai kabisa.
Akawasha gari na kutusisitiza kwamba hatutakiwi kumgusa Firyaal wala kuzungumza chochote kumhusu mpaka atakapotuambia, akabadili gia na kukanyaga mafuta, gari likawa linaondoka, tukaenda mpaka kwenye geti la kutokea ambapo alizungumza na wale walinzi, wakamfungulia geti.
Tukatoka ambapo alizidi kukanyaga mafuta, gari likawa linakimbia kwa kasi kubwa.
Tuliendelea na safari huku wote tukiwa kimya kabisa ndani ya gari, kila mtu akiwaza lake lakini kubwa tukifikiria hatma ya Firyaal. Safari iliendelea na hatimaye tulifika nyumbani kwa Junaitha, akaingiza gari mpaka ndani ya geti, wote tukashuka huku tukionesha dhahiri kuchoka.
Mimi ndiyo nilionekana kuchoka zaidi kwa sababu bado mwili wangu haukuwa na nguvu kutokana na kupoteza damu nyingi kwenye lile tukio la kupigwa risasi, sambamba na maumivu ambayo yalikuwa yakizidi kupungua kadiri muda ulivyokuwa unasonga mbele.
Shamila na Raya walisaidiana kunishika huku na kule kama ilivyokuwa kule mwanzo, tukaingia ndani na kwenda moja kwa moja kukaa sebuleni. Shenaiza na Junaitha wao walisaidiana kumbeba Firyaal na kumpitisha moja kwa moja mpaka kwenye kile chumba ambacho ndiyo huwa tunafanyia shughuli mbalimbali pale ndani.
Muda mfupi baadaye, Shenaiza alirudi na kujumuika na sisi pale sebuleni, akaenda kuwasha runinga na kwenda kutoa chupa ya maji ya kunywa kwenye friji, akanimiminia kwenye glasi na kuniletea, wote watatu wakakaa pembeni yangu.
Junaitha yeye aliendelea kubaki kwenye kila chumba akiwa na Firyaal, hatukujua anafanya nini kwa sababu yeye ndiye aliyetoa maagizo kwamba sote tubaki sebuleni. Bado ukimya ulikuwa umetawala nyumba nzima, sauti pekee iliyokuwa inasikika ilikuwa ni ya TV tu ambayo hata hivyo hakuna aliyekuwa akiitazama.
Kila mmoja alikuwa akiwaza lake lakini ghafla tulishtushwa na kiashirio cha ‘breaking news’ kwenye runinga, wote tukainua vichwa vyetu na kuanza kuitazama runinga hiyo kubwa na ya kisasa, iliyokuwa imebandikwa ukutani.
“Mungu wangu,” nilisema baada ya kushuhudia picha zetu tukiwa pale hospitalini zikioneshwa, zikifuatiwa na maelezo kwamba sisi ndiyo tulikuwa mashujaa wa lile sakata ambalo sasa lilikuwa limebatizwa jina jipya la Kurasini Scandal, likiwa na maana ya skendo ya Kurasini.
Mtangazaji aliwaambia watazamani kwamba hatimaye walikuwa wamefanikiwa kupata picha za watu ambao ndiyo waliokuwa mstari wa mbele katika kufichua uovu mikubwa uliokuwa ukifanywa na mfanyabiashara mkubwa mwenye asili ya Uturuki, Loris kwa kivuli cha Shirika la Black Heart.
Alitumwagia sifa kedekede kisha baada ya hapo, alisema kwamba mheshimiwa rais alikuwa na maneno ya kuzungumza na wananchi wake ana kwa ana muda huo, ukapigwa wimbo wa taifa kisha mheshimiwa rais akaonekana, akiwa amesimama kwenye viunga vya hospitali alianza kuzungumza na wananchi moja kwa moja kupitia runinga.
Alianza kwa kueleza kuhusu mtikisiko mkubwa uliolikumba taifa baada ya kugundulika kwa kile mwenyewe alichokiita machinjio ya binadamu eneo la Kurasini, akafafanua kwamba mtu aitwaye Loris, ambaye serikali ilimuamini na kumpa kibali cha kuendesha Shirika la Black Heart, ambalo alilisajili kama shirika la kusaidia jamii, alivyogundulika kwamba anafanya biashara nyingine haramu na hatari mno kwa maisha ya wananchi.
Alieleza kila kitu, akasema wamegundua kwamba kumbe Black Heart, kazi yake ilikuwa ni kuwasafirisha watu kwenda nje ya nchi ambako wengi wao walikuwa wakienda kuuawa kisha kutolewa viungo muhimu kwenye miili yao, huku wengine wakiuawa hapahapa nchini na viungo vyao kwenda kuuzwa nje ya nchi.
Alionesha kusikitishwa mno na kugundulika kwa sakata hilo ikiwa ni muda mrefu umepita tangu kuundwa kwa shirika hilo, jambo ambalo lilimaanisha kwamba wananchi wengi tayari walishatolewa sadaka kwa sababu ya dhiki zao.
“Najua ni watu wengi ambao walienda kuonana na Loris kwa lengo la kuomba misaada, iwe ni kwenda kusomeshwa nje ya nchi, kufadhiliwa matibabu nje ya nchi au kutafutiwa kazi lakini wakaishia kutolewa kafara,” alisema mheshimiwa rais na alipofika eneo hilo, alishindwa kuzuia machozi yasimtoke, akavua miwani yake na kutoa kitambaa, akajifuta machozi na kuendelea kuzungumza.
Mwisho alitutaja majina, akianza na Junaitha, akaja mimi, Raya na Shamila huku akiwataja Shenaiza na Firyaal kwa utambulisho wa juujuu, nadhani alifanya hivyo kwa sababu za kiusalama, akasema anahitaji kuonana na sisi ikulu na kutoa maagizo tutafutwe mahali popote tulipo ili akatupongeze kwa kazi nzuri tuliyoifanya.
Alieleza kwa kirefu jinsi tulivyofanikisha suala hilo na vikwazo ambavyo tulikumbana navyo, akasema kwamba anajua tulipingwa sana lakini kwa sababu ya ushujaa wetu, tumefanikisha kufichuka kwa sakata hilo kubwa. Akatupa pole kwa yote na kutupongeza sana.
Alipofikia hapo, picha zetu zilirushwa tena runingani tukiwa tunatoka hospitalini kisha wimbo wa taifa ukapigwa tena na huo ukawa mwisho wa habari hiyo. Kwa muda wote huo tulikuwa kimya kabisa, tukiwa ni kama hatuamini tulichokuwa tunakiona.
Kwangu mimi kila kitu kilikuwa zaidi ya muujiza, yaani sisi ndiyo tulikuwa tukitangazwa na mheshimiwa rais mwenyewe kwamba ni mashujaa wa nchi? Hakika ilikuwa ni zaidi ya muujiza. Nilijikita nikishindwa kuyazuia machozi ya furaha yasiulowanishe uso wangu, hali ilikuwa hivyohivyo kwa wenzangu wote, hakuna ambaye hakutoa machozi ya furaha.
“Tunastahili, uwezo wetu wa kutumia nguvu za ndani ndiyo uliotufikisha hapa,” alisema Junaitha, wote tukageuka na kumtazama, hatukuwa na habari kwamba kumbe na yeye alikuwa akiitazama taarifa hiyo ya habari, akaja pale tulipokuwa tumekaa, tukakumbatiana huku wakiwa makini wasinitoneshe kidonda changu.
“Nimeshamaliza kumuandaa Firyaal twendeni tukamalizie kazi iliyosalia,” alisema Junaitha, tukainuka na kuanza kutembea taratibu kuelekea chumbani, kila mmoja akiwa na furaha kubwa sana ndani ya moyo wake.
“Niliwaambia lakini, bila shaka sasa mnaamini,” alisema Junaitha, wote tukamuunga mkono kwa sababu ni kweli alituambia kwamba tukifanikisha suala lile, nchi nzima itatujua sisi ni akina nani na kutupa heshima tuliyokuwa tukistahili.
Tulienda mpaka chumbani ambako Firyaal alikuwa amelazwa chini huku mishumaa saba ikiwa imewashwa na kuzungushiwa pande zote, kuanzia kichwani mpaka miguuni. Alikuwa amemfunga kwa sanda nyeupe ambayo hata sikujua ameipata wapi lakini eneo la usoni lilikuwa wazi.
“Mpendwa wetu Firyaal amelala usingizi wa kifo, kuna uwezekano wa asilimia 50 kwa 50 wa kumrudisha duniani lakini hata ikitokea tumeshindwa, bado kwetu hayo yatakuwa ni mafanikio makubwa kwa sababu kwa kipindi kifupi alichoishi duniani, Firyaal alikuwa ameishi kikamilifu.
Alituelekeza nini cha kufanya, wote tukakaa chini kwa mtindo wa tahajudi, mimi nilikaa upande wa kichwa cha Firyaal, Junaitha yeye alikaa upande wa kushoto wa kifua chake, jirani kabisa na moyo wake, Shamila alikaa upande wa miguuni kwa namna ambayo mimi na yeye tulikuwa tukitazamana, Raya na Shenaiza wao wakakaa upande wake wa kulia.
“Inatakiwa wote tuanze kwa kufanya tahajudi ya pumzi huku tukiunganisha nguvu, kila mmoja akitulia kwa kadiri ya uwezo wake na kuweka uzingativu, tunaweza kuiamsha upya pumzi ya Firyaal, akaanza upya kupumua na kurejea duniani,” alisema, akaanza kutuelekeza nini cha kufanya lakini mwisho alitoa angalizo:
“Kazi haitakuwa nyepesi kwa sababu tayari pumzi zake zimeshahama upande na kuelekea upande wa pili ambao ni kuzimu, kwa hiyo suala la kuzirudisha lilikuwa ni lazima lihusishe safari ya kuelekea kuzimu, kengele ya hatari ikalia ndani ya kichwa changu.
Je, nini kitafuatia?
kidonda cha kisu cha kifua tena cha wiki mbili!!!!.......ukaweza kupiga KOKROCH DETH....tena bila kujitonesha!!!....mwanangu we mkaliSEHEMU YA 43
ILIPOISHIA:
Kauli yake hiyo ilitufurahisha sana mimi na Shamila, tukawa na uhakika kwamba sasa kazi itakuwa nyepesi kwa sababu tayari tutakuwa na mtu kutoka ndani kabisa, ambaye angetusaidia kutimiza lengo letu la kupambana na mtu huyo hatari.
SASA ENDELEA…
“Kwa hiyo tunaanzia wapi?” nilimuuliza Shamila, akawa ni kama anayetafakari kitu kisha akaniambia ameshapata majibu.
“Ngoja niende kwanza na huyu binti nikampe hiyo hard disk yake,” alisema Shamila.
“Utaweza kuichomoa kwenye kompyuta?”
“Mimi naweza, nasomea Information Technology niko mwaka wa pili,” alisema Firyaal ambaye alikuwa amefanana sana na Shenaiza, yaani hata bila kuuliza ungemjua tu kwamba ni ndugu yake.
“Sijamaliza kukopi data ninazozihitaji lakini.”
“Nitakusaidia pia, ninayo ‘back up’ kubwa tu nyumbani, naweza kuhamisha data zote na kukuletea,” alisema msichana huyo, nikawa namtazama usoni kwani aliyokuwa akiyasema hayakuwa yakifanana na umri wake.
Kwa kumtazama alionekana kama msichana mdogo ambaye kwa makadirio ungeweza kudhani yupo kidato cha pili au cha tatu lakini kumbe tayari alishafika kidato cha sita na sasa alikuwa chuoni.
“Nitashukuru sana ukinisaidia dada’angu,” nilisema kwa sauti ya kiungwana, Firyaal akanitazama usoni, na mimi nikamtazama, macho yetu yakagongana, harakaharaka akakwepesha macho yake huku aibu za kikekike zikiwa zimemtawala.
“Basi usitoke kwenda sehemu yoyote, mimi ngoja niende naye nyumbani,” alisema Shamila, akanisogelea pale kitandani na kunibusu kisha harakaharaka akamshika mkono Firyaal na kuanza kutoka naye nje.
>>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Walipofika mlangoni, nilimuona Firyaal akigeuka na kunitazama, na mimi nikamtazama, macho yetu yakagongana kwa mara nyingine. Tofauti na mwanzo, safari hii hakukwepesha macho yake, tukaendelea kutazamana mpaka walipotoka nje. Sikuelewa sababu iliyofanya awe ananitazama vile kwa sababu kimsingi hiyo haikuwa mara ya kwanza mimi na yeye kuonana.
Ilikuwa ni mara ya pili. Hata hivyo sikutilia sana maanani, nikampotezea.
Nikashusha pumzi ndefu na kutulia kitandani, mawazo mengi yakiendelea kupita ndani ya kichwa changu. Ni kweli nilikuwa bado sijapona vizuri lakini ilikuwa ni lazima niondoke hospitalini hapo kabla mambo hayajaharibika. Kutokana na sifa nilizokuwa nazisikia, nilijikuta nikimuogopa mno baba yake Shenaiza kama malaika mtoa roho.
Niliendelea kutulia pale kitandani, japokuwa Shamila aliniambia nisitoke, nilipata wazo la kwenda kwenye wodi aliyokuwa amelazwa Shenaiza kwenda kuangalia anaendeleaje. Hata hivyo, nilipomkumbuka yule mtu aliyekuwa akinitazama sana kwa makini mle ndani ya wodi ya vichaa, nilijikuta nikipatwa na hofu moyoni, nikaghairi.
Kwa hesabu zangu za harakaharaka ukichanganya na maelezo niliyoyapata kutoka kwa Shamila, nilikuwa nimekaa hospitalini hapo kwa wiki mbili mfululizo, huku kati ya hizo, siku saba nikiwa nimepoteza kabisa fahamu.
Nilijaribu kuvuta kumbukumbu ya mambo yote yaliyotokea ndani ya kipindi hicho nilichokuwa hospitalini hapo, ungeweza kudhani kama nimekaa hospitalini kwa kipindi cha mwaka mzima. Kila kitu kilikuwa kikitokea kwa kasi kubwa mno kiasi cha kufanya hata akili yangu isipate muda wa kupumzika.
Kitu ambacho kilinipa faraja kubwa ndani ya moyo wangu, ni kuona jinsi wafanyakazi wenzangu pamoja na bosi wetu walivyokuwa wakinijali. Japokuwa nilikuwa chini ya uangalizi maalum ambapo watu hawakuwa wakiruhusiwa kuja mara kwa mara kunitazama, Raya alinihakikishia kwamba katika zile siku nilizokuwa nimepoteza fahamu karibu kila siku watu kutoka kazini walikuwa wakija kunitazama.
Baada ya kama dakika arobaini tangu Shamila na yule mdogo wake Shenaiza waondoke, Raya alikuja tena. Kiukweli japokuwa nilikuwa nikimuendea kinyume, Raya alikuwa akijitahidi sana kuwa karibu na mimi.
>>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Muda wote yeye alikuwa akinifikiria mimi tu kiasi cha kumfanya kazini asiwe anaenda wala nyumbani kwao asiwe anatulia, muda wote ilikuwa ni kiguu na njia, kuja hospitali na kurudi kwao.
“Vipi unaendeleaje mume wangu,” alisema Raya kwa sauti ya chini, akionesha kuwa na mawazo lukuki ndani ya kichwa chake.
“Naendelea vizuri mke wangu, vipi mbona nakuona kama mudi yako iko chini sana, nini kinakusumbua,” nilimwambia Raya kwa upole, akajisogeza na kupitisha mkono wake mmoja shingoni kwangu, akanibusu kwenye paji langu la uso na kuanza kuniambia kwamba tangu nilipomweleza ukweli wa kilichokuwa kinaendelea nyuma ya pazia, alikosa raha kabisa.
“Nahisi kama nitakupoteza mpenzi wangu na mimi siwezi kuishi bila wewe, hata sijui itakuwaje,” alisema kwa huzuni, nikashusha pumzi ndefu na kuanza kumtuliza. Nikamwambia asiwe na wasiwasi, hakuna jambo lolote baya litakalotokea nakuhakikishia,” nilimwambia.
Kidogo kujiamini kwangu kulimfanya naye aanze kuona kwamba kumbe halikuwa tatizo kubwa mbele yetu, nikamueleza pia juu ya mipango ya kutoroka tuliyokuwa tumeipanga kwa ajili ya kumkimbia baba yake Shenaiza. Nilimuona naye akiniunga mkono, nadhani hata yeye hakuwa na imani kabisa juu ya usalama wangu hospitalini hapo.
Tulizungumza mambo mengi, Raya akawa ananisisitiza kwamba yeye amejitoa kwa asilimia mia moja kunisaidia, isije ikatokea kwamba nikamgeuka na kumuona hana maana tena. Kauli yake iliugusa sana moyo wangu kwa sababu ni kweli Raya alikuwa amejitoa kwa kila kitu lakini kwa bahati mbaya sana shetani alionekana kunizidi nguvu.
Nikawa namhakikishia kwamba asiwe na wasiwasi lakini ukweli, sikuwa namaanisha kile nilichokuwa nakisema. Akaniambia kwamba atashirikiana na Shamila kuhakikisha wananitorosha hospitalini hapo usiku bila mtu yeyote kujua, swali likawa nikishatoroshwa nitaenda kukaa wapi?
Raya alisema anataka nikakae nyumbani kwao kwa sababu pale kuna usalama zaidi, nikamwambia ni rahisi wabaya zangu kujua kwamba niko pale kwa sababu kuna baadhi ya watu walikuwa wakijua kuhusu uhusiano wetu wa kimapenzi. Nikatumia nafasi hiyo kumpigia chapuo Shamila, nikamwambia Raya kwamba amesema yupo tayari kunificha nyumbani kwake.
Nilimuona Raya akishtushwa kidogo na nilichokisema lakini nikamtoa wasiwasi na kumwambia kwamba mimi na yeye tutakuwa pamoja kwa hiyo asiwe na wasiwasi wowote. Akakubali kwa shingo upande, nadhani bado alikuwa na wivu juu ya ukaribu wangu na Shamila.
Muda ulizidi kuyoyoma, baadaye Shamila alirudi akiwa peke yake, akaniambia kwamba kila kitu kimeenda kama tulivyokubaliana, akaniambia kwamba Firyaal alikuwa mtundu sana kwenye mambo ya kompyuta na kwamba tayari alishanikopia data zote na kuziacha pale nyumbani kwake kama tulivyokubaliana, tukaanza kupanga mipango ya namna ya kutoroka usiku huku Raya naye akiwepo.
Jambo ambalo kuanzia mwanzo Raya hakuwa akilijua, ni kwamba katika mpango wetu huo ilikuwa ni lazima pia tumtoroshe na Shenaiza, akashtuka kusikia hivyo.
Bado nikaendelea kumsisitiza kwamba ilikuwa ni lazima tuondoke na Shenaiza kwa sababu bila yeye mimi nisingeingia kwenye mtego huo na kuanzia mwanzo alikuwa akinisisitiza kwamba mimi ndiye mtu pekee ninayeweza kumsaidia.
“Usiwe na wasiwasi, hawa wote wataenda kukaa nyumbani kwangu, mimi nina nyumba kubwa, hata na wewe ukitaka tukae pamoja tusaidiane kuwahudumia wagonjwa haina shida,” alisema Shamila, nikamuona Raya akishusha pumzi ndefu na kunitazama, akatingisha kichwa kama ishara ya kukubaliana na mimi.
Ilibidi Raya abaki palepale hospitalini mpaka usiku ili iwe rahisi kufanya kazi yetu, muda ukazidi kuyoyoma na hatimaye giza likaingia, ule muda tuliokuwa tukiusubiri kwa hamu ukawa umewadia.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue