Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #81
SEHEMU YA 61
Wakati tukinywa chai hiyo yapata saa kumi na moja za alfajiri. Gari moshi lilikuwa limechelewa sana njiani kutokana na mafuriko katika maeneo mbalimbali. Ilibidi gari hilo liendeshwe taratibu sana. Tulikuwa tumeketi nje ya stesheni, kwenye benchi la chuma ambalo bila shaka lilijengwa kwa ajili ya wasafiri.
Nilishangaa pale Mmanyema aliponiambia kuwa tulisafiri katika behewa moja toka Tabora hadi hapo. Kuwa aliniona lakini hakuwa na hakika na macho yake hadi aliposikia sauti yangu na kuniona nikimkumbuka.
Alikuwa mzungumzaji sana mzee huyu. Alinieleza jinsi alivyoacha kazi ya kumtumikia yule Mwarabu baada ya kufilisika. “Yaelekea Mwarabu yule hakuwa na ujuzi wowote zaidi ya biashara ya watumwa. Kila alichojaribu kushika kiliteleza. Hata mishahara yetu alishindwa kulipa. Tukaachana naye na kuanza shughuli zetu binafsi,” Alinieleza kwamba yeye sasa alikuwa akifanya biashara ya kununua dagaa toka kwa wavuvi wadogowadogo wa kandokando ya ziwa Tanganyika na kuwauza kwa walanguzi wakubwa ambao waliwapeleka Tabora, Dodoma na Dar es Salaam kwa matumizi ya binadamu na mifugo. Kwamba sasa hivi alikuwa na mtaji wa kutosha ambao utamwezesha kupeleka mwenyewe dagaa hao hadi Dar es Salaam ili apate faida kubwa zaidi. “Toka huku nitanunua nyavu na vifaa vingine vya uvuvi na kuwauzia watu Kigoma na Kongo. Nikijaliwa miaka miwili baadaye nitakuwa mmoja wa matajiri wakubwa wa nchi hii,” alisema kwa kujipamba.
“Sasa unakwenda wapi? Mbona huku hakuna dagaa?” nilimuuliza.
“Nakwenda Sumbawanga.” “Kufanya nini?”
Alinitazama na kucheka kidogo kabla hajasema, “Unaonekana wewe ni mtoto mdogo sana kuliko umbile lako. Hujui watu huenda Sumbawanga kufanya nini?”
Mie: Sijui
Yeye: Pole sana. Kwa hiyo, hata maana ya jina Sumba
- Wanga hujui?
Mie : Sijui
Alitikisa kichwa kwa namna ya kunisikitikia. Kisha alisema, “Sumba-Wanga maana yake ‘Tupa Uchawi.’ Kwa maana ya kuwa mji huo ni wa watu wazito, watu waliokomaa. Hivyo, ukiingia huko na vijiuchawiuchawi vyako utaumbuka. Ni huko ambako watu wazima huenda kugangwa, ili wasichezewechezewe ovyo kishirikina. Huwezi kufanya biashara kama hujafundwa ukafundika.”
Ilikuwa habari mpya kwangu. Niliipokea kwa mshangao na kutoamini. “Lakini Biblia inasema…” nilijaribu kumwambia. “Achana na Biblia. Mimi ni Mwislam. Tunatumia Msahafu wa Mwenyzi Mungu. Ulioshushwa toka peponi kwa
mkono wa mtume Mohamed S.A.W.”
“Lakini hata Uislam unakataza ushirikina.”
“Kujikinga sio ushirikina. Hayo ni mambo ya wakoloni tu, walipoamua kututawala miili na mioyo yetu. Walitarajia kuwa mila na tamaduni zetu kupotea huku wao wakihifadhi za kwao. Kila binadamu ana nyota na anahitaji kuisafisha mara kwa mara. Kila binadamu ana wahenga ambao anahitaji kuwaenzi kwa sadaka na tambiko. Asiyefanya hivyo kamwe hawezi kufanikiwa.”
Lilikuwa somo jipya kwangu, somo ambalo sikuwa na ujuzi nalo. Nikaamua kunyamaza. Mmanyema alichukulia ukimya wangu kama dalili ya kumwelewa.
“Haya na wewe nieleze ukweli wa kile kilichokufanya ufike huku. Kama nakumbuka vizuri babu yako alikupeleka Uhayani ukasome. Nadhani ulipata shule kwani nilipoonana naye mwaka mmoja baadaye alinidokeza kuwa ulishaingia shuleni,” alisema.
Nusura niruke kwa shauku, “Ulionana na babu?” “Ndiyo!”
“Wapi?”
“Nyumbani kwenu. Kasulu. Tulilala pale siku mbili na alituchinjia beberu mkubwa sana. Babu yako ni mkarimu sana.”
Bila kutegemea nilijikuta nikitokwa na machozi. Babu yuko hai! Babu alirudi salama! Sikupata kupokea habari njema kama hiyo kwa miaka nenda rudi.
Sikuiona haja yoyote ya kumficha chochote Mmanyema huyu. Nilimwona kama baba yangu. Kama malaika, kwa kuweza kunipa walao fununu tu ya habari za nyumbani. Nikamweleza kila kilichonisibu, toka mwanzo wa mikasa yangu hadi nilipofikia.
Alinisikiliza kwa makini sana, mara kwa mara akitikisa kichwa kwa masikitiko. Mwisho wa maelezo yangu alinishika mkono na kuninong’oneza, “Pole sana mtani. Usijali. Hujafika mwisho wa safari yako kimaisha. Nitakusaidia.”
Nilimwamini. Sikujua kwa nini nilimwamini haraka kiasi hicho.
* * *
Safari ya Ikola au Karema ilikufa. Ndoto ya kuchimba dhahabu nayo ilikufa. Safari ya Sumbawanga ikazaliwa.
Tulikaa kwa siku mbili kabla ya kupata gari lililotufikisha
Wakati tukinywa chai hiyo yapata saa kumi na moja za alfajiri. Gari moshi lilikuwa limechelewa sana njiani kutokana na mafuriko katika maeneo mbalimbali. Ilibidi gari hilo liendeshwe taratibu sana. Tulikuwa tumeketi nje ya stesheni, kwenye benchi la chuma ambalo bila shaka lilijengwa kwa ajili ya wasafiri.
Nilishangaa pale Mmanyema aliponiambia kuwa tulisafiri katika behewa moja toka Tabora hadi hapo. Kuwa aliniona lakini hakuwa na hakika na macho yake hadi aliposikia sauti yangu na kuniona nikimkumbuka.
Alikuwa mzungumzaji sana mzee huyu. Alinieleza jinsi alivyoacha kazi ya kumtumikia yule Mwarabu baada ya kufilisika. “Yaelekea Mwarabu yule hakuwa na ujuzi wowote zaidi ya biashara ya watumwa. Kila alichojaribu kushika kiliteleza. Hata mishahara yetu alishindwa kulipa. Tukaachana naye na kuanza shughuli zetu binafsi,” Alinieleza kwamba yeye sasa alikuwa akifanya biashara ya kununua dagaa toka kwa wavuvi wadogowadogo wa kandokando ya ziwa Tanganyika na kuwauza kwa walanguzi wakubwa ambao waliwapeleka Tabora, Dodoma na Dar es Salaam kwa matumizi ya binadamu na mifugo. Kwamba sasa hivi alikuwa na mtaji wa kutosha ambao utamwezesha kupeleka mwenyewe dagaa hao hadi Dar es Salaam ili apate faida kubwa zaidi. “Toka huku nitanunua nyavu na vifaa vingine vya uvuvi na kuwauzia watu Kigoma na Kongo. Nikijaliwa miaka miwili baadaye nitakuwa mmoja wa matajiri wakubwa wa nchi hii,” alisema kwa kujipamba.
“Sasa unakwenda wapi? Mbona huku hakuna dagaa?” nilimuuliza.
“Nakwenda Sumbawanga.” “Kufanya nini?”
Alinitazama na kucheka kidogo kabla hajasema, “Unaonekana wewe ni mtoto mdogo sana kuliko umbile lako. Hujui watu huenda Sumbawanga kufanya nini?”
Mie: Sijui
Yeye: Pole sana. Kwa hiyo, hata maana ya jina Sumba
- Wanga hujui?
Mie : Sijui
Alitikisa kichwa kwa namna ya kunisikitikia. Kisha alisema, “Sumba-Wanga maana yake ‘Tupa Uchawi.’ Kwa maana ya kuwa mji huo ni wa watu wazito, watu waliokomaa. Hivyo, ukiingia huko na vijiuchawiuchawi vyako utaumbuka. Ni huko ambako watu wazima huenda kugangwa, ili wasichezewechezewe ovyo kishirikina. Huwezi kufanya biashara kama hujafundwa ukafundika.”
Ilikuwa habari mpya kwangu. Niliipokea kwa mshangao na kutoamini. “Lakini Biblia inasema…” nilijaribu kumwambia. “Achana na Biblia. Mimi ni Mwislam. Tunatumia Msahafu wa Mwenyzi Mungu. Ulioshushwa toka peponi kwa
mkono wa mtume Mohamed S.A.W.”
“Lakini hata Uislam unakataza ushirikina.”
“Kujikinga sio ushirikina. Hayo ni mambo ya wakoloni tu, walipoamua kututawala miili na mioyo yetu. Walitarajia kuwa mila na tamaduni zetu kupotea huku wao wakihifadhi za kwao. Kila binadamu ana nyota na anahitaji kuisafisha mara kwa mara. Kila binadamu ana wahenga ambao anahitaji kuwaenzi kwa sadaka na tambiko. Asiyefanya hivyo kamwe hawezi kufanikiwa.”
Lilikuwa somo jipya kwangu, somo ambalo sikuwa na ujuzi nalo. Nikaamua kunyamaza. Mmanyema alichukulia ukimya wangu kama dalili ya kumwelewa.
“Haya na wewe nieleze ukweli wa kile kilichokufanya ufike huku. Kama nakumbuka vizuri babu yako alikupeleka Uhayani ukasome. Nadhani ulipata shule kwani nilipoonana naye mwaka mmoja baadaye alinidokeza kuwa ulishaingia shuleni,” alisema.
Nusura niruke kwa shauku, “Ulionana na babu?” “Ndiyo!”
“Wapi?”
“Nyumbani kwenu. Kasulu. Tulilala pale siku mbili na alituchinjia beberu mkubwa sana. Babu yako ni mkarimu sana.”
Bila kutegemea nilijikuta nikitokwa na machozi. Babu yuko hai! Babu alirudi salama! Sikupata kupokea habari njema kama hiyo kwa miaka nenda rudi.
Sikuiona haja yoyote ya kumficha chochote Mmanyema huyu. Nilimwona kama baba yangu. Kama malaika, kwa kuweza kunipa walao fununu tu ya habari za nyumbani. Nikamweleza kila kilichonisibu, toka mwanzo wa mikasa yangu hadi nilipofikia.
Alinisikiliza kwa makini sana, mara kwa mara akitikisa kichwa kwa masikitiko. Mwisho wa maelezo yangu alinishika mkono na kuninong’oneza, “Pole sana mtani. Usijali. Hujafika mwisho wa safari yako kimaisha. Nitakusaidia.”
Nilimwamini. Sikujua kwa nini nilimwamini haraka kiasi hicho.
* * *
Safari ya Ikola au Karema ilikufa. Ndoto ya kuchimba dhahabu nayo ilikufa. Safari ya Sumbawanga ikazaliwa.
Tulikaa kwa siku mbili kabla ya kupata gari lililotufikisha