Simulizi ya beyond pain

lameckkawawa

JF-Expert Member
Sep 13, 2015
944
665
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 1
MTUNZI : PATRICK .CK

Ni saa kumi jioni nikiwa maeneo ya Kimandolu nikielekea Usa river katika baa iliyotulia ya Roterdam garden mahala panapofanyika vikao vya harusi yangu.Wanakamati ya maandalizi walichagua mahala hapa kutokana na utulivu wake kwani kuna bustani nzuri na hata huduma zake ni nzuri sana.Nikiwa maeneo haya ya Kimandolu gari ikienda taratibu kutokana na magari mengi kukaa pembeni ya bara bara kwa muda mrefu kwa kupisha misafara ya viongozi wa jumuia ya Afrika mashariki waliokuwa na kikao chao hapa Arusha.Siku zote kunapokuwa na mikutano ya namna hii jijini Arusha huwa kunakuwa na adha kubwa kwa watumiaji wa bara bara hii ya Moshi - Arusha kwa sababu ndiyo bara bara kuu waitumiayo viongozi hawa wakitokea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).Mara simu yangu ikaita nikaitazama na kukuta ni Mr Cheleo mmoja kati ya wanakamati.
“Haloo kaka” nikasema
“Haloo ,uko wapi? Sisi tumeshafika tunakusubiri wewe tu.”
“Niko njiani kaka si unajua leo njia ilikuwa imefungwa viongozi walikuwa wanaondoka.Ndani ya dakika kumi nitakuwa nimefika hapo Usa river.”
“Ok kaka tunakusubiri”
Hiki kilikuwa ni mojawapo ya kikao cha maandalizi ya harusi yangu inayotarajiwa kufanyika muda wa kama mwezi mmoja ujao.Harusi ambayo kila mmoja wa rafiki zangu alikuwa akiisubiri kwa hamu sana.Nimekuwa mchangiaji mzuri wa harusi za rafiki zangu na kuhakikisha zinafana safari hii walikuwa wamepania sana kufanya sherehe ya harusi yangu kuwa ya kihistoria.
Tulipofika maeneo ya madukani gari zikaanza kwenda kasi na dakika tano baadae nikawasili usa river katika baa tulivu ya Roterdam.Nikapaki gari na kuelekea bustanini.Nikawasalimia wanakamati na kuwaomba radhi kwa kuchelewa kisha kikao kikaendelea.Kilikuwa ni kikao kirefu .
Wakati kikao kikiendelea nikachukua simu na kumtumia mpenzi wangu Emmy ujumbe mfupi.Kwa siku tatu nilikuwa na shughuli nyingi na sikupata hata muda wa kuonana naye.Kwa sasa emmy anasoma digrii ya sheria katika chuo kikuu cha Tumaini makumira.Kila jioni huwa ana desturi ya kupita kwangu na hata kama sipo kwa kuwa ana ufunguo wa nyumbani kwangu huwa ananisubiri mpaka nikirudi tunakaa wote kisha namrudisha kwake.

“Hallow sunshine,niko kwenye kikao hapa roterdam.Baada ya kutoka hapa nitapita kwako.Missing you soooo much.” Huu ndio ujumbe mfupi niliomtumia Emmy kipenzi cha moyo wangu.

Tukaendelea na kikao.Baada ya kama robo saa hivi tangu niutume ule ujumbe mfupi wa maandishi kwa mpenzi wangu Emmy simu yangu inaita kuangalia zilikuwa ni namba za emmy.Nikainuka na kwenda mbali kidogo ili niweze kuongea naye.
“Halloo Darling “Nikasema kimahaba.kwani ndivyo tulivyozoea wakati tunaongea simuni.
Nusura moyo unipasuke kwa mstuko pale nilipoisikia sauti nzito ya kiume ikijibu.
“Mwanaharamu wewe,mpenda wake za watu.Huna haya unamwita nani Darling? Kumbe ndio mchezo wako huo wa kudandia wanawake wa watu.Leo nimekupata.”
Nilibaki nimeduwaa kwa sekunde kadhaa nisijue nini cha kusema.sikuelewa yule jamaa alikuwa akimaanisha nini.Huku nikitabasamu nikauliza
“Mbona sikuelewi wewe.Unasemaje? samahani kama simu zimeingiliana”
‘Simu hazijaingiliana we juha.We si ndio Wayne? Wayne mkotela….
“yah ndio mimi” Nikajibu huku mapigo ya moyo yakinienda kwa kasi baada ya yule jamaa kulitamka jina langu
“ Wewe si ndio umemtumia Sarafina ujumbe wa maandishi sasa hivi ukisema unakuja kumuona ukitoka kwenye kikao?
“Mimi nimemtumia ujumbe Emmy na sio sarafina”
“sasa sikiliza wewe mjinga….”Nilihamaki baada ya kuitwa vile lakini nikavumilia nimsikie alichotaka kusema
“Iwe ni huyo Sara au Emmy kama unavyojua lakini nakwambia kuwa huyu ni mke wa mtu na mimi ndio bwana wake.”..
“Unasemaje wewe??..Nikauliza kwa hamaki
“Hebu mpe Emmy simu yake haraka.Mpuuzi wewe” Nikasema tena kwa hasira
“Mpumbavu wewe ! hivi nikwambie mara ngapi Hakuna Emmy hapa…Huyu anaitwa Sarafina.Kama alikwambia anaitwa Emmy alikudanganya.Huyu ni sarafina na mimi ndio mumewe,mimi ndio ninayemlipia hii nyumba anayoishi na ni mimi ndio niliyemtafutia kazi pale AICC na baadae nikamtafutia nafasi ya masomo pale Makumira.Mimi ndiye ninayemlipia ada na kila kitu.Mimi ndiye ninayemuweka mjini.Nilikuwa nje ya nchi nilikuwa napata taarifa kuwa kuna mtu anatembea na mke wangu nikajua ni utani.Leo ndio nimegundua kuwa ni kweli” akasema Yule jamaa.
“Mjinga mkubwa wewe,huna haya mimi ndie ninayemlipia Emmy ada zote za masomo na hata nyumba anayokaa mimi ndiye ninayelipa.Na kwa taarifa yako mpumbavu wewe,sasa hivi tuko katika maandalizi ya harusi yetu na kesho jumapili kanisani wanasoma tangazo la kwanza la ndoa yetu.Hivyo nakuomba usijaribu kwa namna yoyote ile kuleta upumbavu wako “ Tayari hasira ilikwisha nipanda nikatamka maneno yale kwa hasira.
“Sikiliza we mjinga yaani pamoja na kukueleza kote huku bado hunielewi sasa Emmy huyu hapa hebu ongea naye”
Nikasikia akimpa mtu simu na kumlazimisha
“Hebu ongea na huyu mbwa mwenzako mweleze ukweli mimi ni nani na mkanye akome kuanzia leo kukufuata fuata la sivyo nitamfanyia kitu kibaya sana ,hanijui mimi ni nani mjinga huyu” maneno haya nikayasikia kwa mbali.Mara nikasikia kitu ambacho sikukitegemea kukisikia maishani mwangu.Niliomba ardhi ipasuke niingie ndani.Nilitamani nijimalize pale pale.sikuona thamani tena ya kuendelea kuishi katika dunia hii.
Niliisikia sauti ile tamu na nyororo iliyozoea kuniburudisha kila siku na kunifanya nione kama niko peponi,sauti ambayo niliamini ni sauti nzuri kuliko zote duniani,sauti ya mpenzi wangu,bibi harusi mtarajiwa Emmy.Huku akilia kwa kwikwi akatamka maneno ambayo yalinifanya niichukie dunia na watu wake na hasa wanawake.
“Wayne I’m sorry mimi ni mke wa mtu,na ninaomba usiendelee tena kumtukana mume wangu”
Ilikuwa ni kama niko ndotoni nikazubaa kwa sekunde kadhaa kisha nikajikaza kiume na kuuliza tena.
“Emmy is that you??…….
“Yes Wayne please leave me alone.Usinipigie simu tena.Mimi nina bwana wangu”
Machozi yalianza kunitoka.Sikuamini kile nilichokisikia.
“Please Emmy tell me its not true ” Nikasema tena huku machozi yakinitoka.
“My name is not Emmy…..Akashindwa kuendelea alikuwa akilia.Yule jamaa akachukua tena simu
“Sasa umeamini we kijana.Tafadhali usiendelee kumfuata fuata sarafina.Kitakachokupata usije kumlaumu mtu………..”Akamalizia kwa tusi zito na kukata simu
Nikahisi miguu ikiisha nguvu nikaakaa chini.
Christopher rafiki yangu mkubwa alihisi lazima nitakuwa na tatizo akanifuata .Akastuka baada ya kunikuta nimekaa chini.
“Wayne.. “Akaita nikamuangalia sikuwa na nguvu za kujibu.
“Wayne una tatizo gani?
Akawaita wanakamati wote wakaja mbio na kuanza kunipepea.Nikaletewa maji nikanywa.Dakika kama tano hivi baadae nikaweza kuongea
“Take me home” Nikamwambia Chris
“Wayne una tatizo gani.Twende hospitali” Akasema Chris
“No ! take me home” Nikasema huku nikijaribu kuinuka.Wakanisaidia kutembea hadi garini kisha Chris akawasha gari na kuondoka kunipeleka nyumbani.
Picha mbali mbali zikawa zinakuja na kupotea.Nilihisi kama vile niko ndotoni .Chris aliendesha kwa kasi bila kunisemesha.Tulipofika maeneo ya sanawari nikafungua mdomo na kumwambia Chris.
“Nipeleke kwa Emmy” Chris alikuwa akipafahamu anapoishi Emmy hivyo tulipofika maeneo ya Ilboru akakata kushoto na moja kwa moja akaelekea nyumbani kwa Emmy.
Alisimamisha gari nje ya nyumba ya Emmy.Sikuongea kitu nikafungua mlango nikashuka garini.Mlinzi wa kimasai wa nyumba ya Emmy alinifahamu hivyo aliponiona akanisalimia nikapita zangu hadi ndani.Chris naye alikuwa akinifuata kwa nyuma.Nilisimama mlangoni na kusikia watu wakinong’ona kwa ndani.Nilikuwa na funguo ya mlango nikaufungua bila kugonga na kuingia ndani.Sebuleni nilimshuhudia Emmy akiwa kifuani kwa baba mmoja mnene wakiwa katika mahaba mazito.Nikaanguka na kupoteza fahamu.

* * * *

Nilizinduka na kujikuta mahala nisipopafahamu.Nilikuwa katika chumba chenye harufu ya dawa.Ndani ya chumba hiki kulikuwa na watu kadhaa.Mtu wa kwanza kumtambua alikuwa Chris.
“Pole sana Wayne”.Akasema huku akinishika kichwa.”Tafadhali usiinuke , endelea kupumzika.” Muda huo huo akaja daktari akiwa ameongozana na wauguzi wawili,nikajua hapa nipo hospitali.daktari akanipima kisha akasema
“Kwa sasa unaendelea vizuri.Itabidi ulale hapa leo ili tuendelee kukuangalia zaidi”
Sikuwa na ubishi ingawa sikuhisi kuumwa sehemu yoyote ile zaidi ya kichwa kuwa kizito mno.Daktari akatoa maelekezo kadhaa kwa wale wauguzi akaandika pia katika kijikadi kisha akatoka.Pale mlangoni nilisikia akiongea kama na kundi la watu.na dakika hiyo hiyo watu zaidi ya ishirini wakaingia mle chumbani.Walikuwa ni wanakamati ya maandalizi ya harusi yangu pamoja na baadhi ya rafiki zangu.Walinipa pole nami nikawahakikishia kuwa niko salama wakanitakia usiku mwema wakaondoka.pale hospitali nikabaki na Chris
“Chris nini kilitokea mpaka nikaletwa hapa?
Chris akanitazama kisha akajibu
“Wayne ulianguka ukapoteza fahamu ,ikanibidi nikulete hapa katika hospitali hii .Usijali kila kitu kinakwenda vizuri.Daktari anasema kesho asubuhi atakuruhusu”
Niliposikia kuanguka na kupoteza fahamu ,ndipo nikalikumbuka tukio zima lililotokea.Ghafla fahamu zikanipotea tena.
Nilirejewa na fahamu baadae sikujua ni saa ngapi.Ukiacha yule daktari mmoja aliyekuwapo mida ile sasa walikuwapo watatu.hali hii iliniogopesha sana.Nikaogopa pengine hali yangu si nzuri.Daktari mmoja mzee mwenye miwani akanisogelea na kuniuliza
“Wayne unajisikiaje sasa hivi?…
“Najisikia safi ila kichwa ni kizito sana.Nahisi kama kizungu zungu kwa mbali”
“Ok sawa.Hali yako inaendelea vizuri,vipimo vyote vinaonyesha uko sawa ila unachotakiwa kwa sasa ni kujaribu kutokuwaza kitu chochote kinachoweza kukusababishia ukapoteza fahamu kwa mara nyingine.Jaribu kupata mapumziko ya kutosha na jitahidi sana kutokuwaza…..”
Nilimtazama yule daktari sikuwa na jibu la kumpa.Nafikiri hakujua kitu gani kilichonipata.Hakuyaelewa maumivu yaliyokuwa moyoni mwangu.
“Ok dokta nitajitahidi”.Nilisema huku machozi yakinilenga.
Madaktari na wauguzi wakatoka na kuniacha chumbani mimi na Chris.hawakutaka Chris aniache peke yangu kwa kuwa waliogopa pengine ningeweza kujidhuru.
Niliinuka na kukaa kitandani.Chris akanisaidia nikakaa sawa.
“Chris I hate the world”Nikasema kwa sauti ndogo
Chris akanitazama akasema.
“Wayne jitahidi upumzike.Usiwaze lolote kwa sasa.Everything will be ok”
“No Chris.Nothing is ok.Emmy lied to me…………………”Nikasema huku machozi yakinitoka.
“Don’t cry buddy,be strong” akasema chris huku akinipiga piga mgongoni
“ I loved her .I loved her Chris more than I love myself.Lakini ona kitu alichonifanyia…..Nitauweka wapi uso wangu mimi?.”.Uso wote ulijaa machozi.Iliniuma kupita kiasi.
“Wayne lala kwanza.Tutaongea asubuhi” Akasisitiza Chris.
“No Chris siwezi lala wakati mwanamke niliyempenda amenisaliti….why me????? Why this pain???”
“Ok brother let it out……let it out….”Akasema Chris.
“Emmy amenidanganya muda wote huu kumbe ni mke wa mtu….”
“what!!!!!!!!” Akahamaki Chris
“Yah! ana bwana wake.Ndiye yule tuliyemkuta amelala naye kwenye sofa pale sebuleni kwake.Kwa mdomo wake mwenyewe ameniambia nisimsumbue yeye ana mume wake ”
Chris akainuka na kuanza kuzunguka mle chumbani huku ameshika kichwa.
“Is this true brother”Akauliza
“Yah..kwa mdomo wake amenitamkia maneno haya….It hurt Chris it hurt so much.”
“Mwanaharamu huyu…….”Akasema Chris kwa hasira
“Kesho ndoa yetu inatangazwa kanisani kwa mara ya kwanza…….nikashindwa kuendelea.Nilishindwa kujizuia kuangusha machozi.
“Wayne its gonna be ok.Jitahidi ulale kesho tutayaongea mambo haya.Usiwaze sana kilichotokea.Hii ni mitihani tu ya maisha”
Chris alijaribu kwa kila njia kunibembeleza ili niweze kuwa katika hali yangu ya kawaida lakini kwa hali halisi jinsi ilivyo ni ngumu sana.
Ni Jumatano ya wiki hii tumetoka kuandikisha ndoa kanisani na kesho tangazo la kwanza linaanza kusomwa.tayari maandalizi yote ya harusi yamekamilika .Nitauweka wapi uso wangu mimi.Nitawaeleza nini watu wanaoisubiri harusi yangu??Nitawaleleza nini wazazi na ndugu zangu? Simlaumu mtu.Emmy nilimchagua mwenyewe.Hakunichagulia mtu yeyote.Iwapo ningechaguliwa na wazazi au mtu mwingine , ningekuwa na kila sababu ya kuwatupia mzigo wa lawama wao kwa uchaguzi wao usiofaa.Lakini hili lilikuwa ni chaguo langu mwenyewe..Huu ni mzigo wangu na inanibidi nisimame kidete niukabili.Nilijilaza kitandani na sijui hata saa ngapi nilipata usingizi.
Saa tano asubuhi tayari nilikuwa nyumbani kwangu maeneo ya majengo.Nilikuwa najisikia mzima wa afya isipokuwa kichwa kilikuwa kikiniuma kwa mbali.Chris ndiye aliyenichukua hospitali na kunirudisha nyumbani.
Mpaka sasa hivi hakuna mtu mwingine aliyekuwa akijua nini kilichotokea na kupelekea kupoteza fahamu na kulazwa hospitali zaidi yangu na Chris.Sikutaka kuharakisha kuliweka wazi jambo hili gumu.Nilitaka kuacha kwanza akili yangu itulie.Nilikaa kidogo sebuleni ,halafu nikamwambia Chris aniache nikapumzike.
“Brother naomba nikapumzike,halafu tutaongea jioni.Ila tafadhali naomba usimwambie mtu yeyote nini kilichotokea..”
‘Ok wayne nenda kampumzike ila tafadhali don’t do anything stupid”Akasema Chris huku akitoa tahadhari kwani madaktari walimuonya asikubali kuniacha peke yangu kwa kuhofia pengine ninaweza kujidhuru.
“C’mon Chris,I’m not a kid.Haya ni mambo ya kawaida katika maisha.Let me have a rest then I’ll know what to do next.”
“Ok wayne..nitapita mchana kukuangalia.Nikuletee chakula gani mchana?
“Nothing Chris.Usiniletee chochote.I don’t feel like eating anything.”
“Unatakiwa ule Wayne.unatakiwa uwe na nguvu.”
Sikumjibu kitu nikamtazama na kuondoka kuelekea chumbani kwangu.
Nilikaa kitandani,nikalifungua kabati langu na kutoa albamu kubwa la picha.Humu kuna picha nyingi ambazo nimepiga na emmy tangu tulipoanza mapenzi yetu .Picha yetu ya kwanza mimi na yeye ikanikumbusha tulikwenda picnic Ziwa Duluti.Ni siku tuliyofurahi sana.Siwezi kuisahau siku hii.Nikaendelea na kuzifunua picha nyingine.Wakati nikiendelea na kuzitazama picha simu yangu inalia.Alikuwa ni mama yangu.
“mama shikamoo” nikamsalimu
“Marahaba baba ,hamjambo”
“hatujambo mama,vipi mnaendeleaje?
“Huku wote wazima.Ni baba yako tu kichwa chake kile kinamsumbua sana lakini anaendelea vizuri”
‘Mpe pole sana “Nikajibu kwa ufupi.
“Vipi mkwe wangu hajambo?
Nikasita kujibu.
“eenh jamani hajambo mama mkwe? Mama akauliza tena baada ya kuona sijamjibu
“Hajambo mama”Nikajibu huku nikiuma meno kwa hasira.Mwanamke huyu amewadanganya hadi wazazi wangu.Iliniuma sana.
“nashukuru kama ni mzima.Vipi mnaendeleaje na maandalizi ya harusi?
“mama maandalizi ni mazuri.Tunaendelea vizuri”
“sawa baba.Leo huku wamesoma Tangazo la kwanza..Hivi ninavyokwambia watu wanajiandaa isivyo kawaida,kila ndugu anataka aje kwenye harusi yako.”
Sikuwa na cha kusema.Machozi yalikuwa yananitoka.
“Mama nashukuru.Nitakupigia baadae tutaongea vizuri zaidi”
“Sawa baba”
Nilikata simu na kuitupia kitandani.hasira zikanipanda.
“Damn you Emmy…..”
Nilizungunguka zunguka mle chumbani nikijaribu kuwaza na kuwazua bila kupata jibu.Nikatoka na kurudi sebuleni.Nikafungua kabati ninamoweka cd na kuchukua moja ya cd niipendayo sana ya mmoja kati ya wanamuziki mahiri kwenye mziki wa bongo fleva,Hamis mwinjuma au Mwana F.A .Huu wimbo wake niliona ni kama vile alinitungia mimi kwa sababu ulinihusu mimi.Ubeti wa pili ndio uliniumiza zaidi ukanifanya niurudie tena na tena
“hata nikitaka kuoa niambie ntamuoa nani?/
watu wana watu wao wengine toka zamani/
ukiambiwa we ni boyfriend haimaanishi uko peke yako/
wadogo usoni wanahifadhi wazee wako/
sijui ni dhiki au tamaa tu??/
watoto wanaanika njaa tu/
hawafikirii mapenzi wanachoona wao ni mkwanja tu/”
Maneno haya yalinichoma moyo.Kijana huyu aliimba vitu vya kweli kabisa na yote aliyoyaimba yamenikuta mimi.
Nikarudi tena chumbani sikujua nini cha kufanya.Nilikuwa kama nimechanganyikiwa vile.Nikaona ni bora nijilaze kitandani na kijiusingizi kikanipitia.
Nilistuka na mlio wa simu iliyokuwa kichwani kwangu,alikuwa ni Chris.
“ Haloo” Nikasema
“Wayne umelala?”
“Ndiyo nilikuwa nimelala”
“Ok .Sasa wayne naomba uwe na moyo mgumu na usihamaki tafadhali.Ni kwamba Emmy amenifuata na hapa nilipo niko naye na ni yeye ndiye alinisisitiza nikupigie simu hii.”
“Unasemaje Chris????? “Nikasema kwa ukali.Sikutegemea kusikia kitu kama kile.
“Wayne niko na Emmy hapa.amenitafuta na kuomba nafasi ya kuongea na wewe”
“Chris…………..”Nilidakia,sikutaka aendelee tana kunipa habari za yule baradhuli
“Chris tafadhali.Kama na wewe unataka tukosane hamna shida ila tafadhali naomba usinipe habari zozote kuhusu huyu mwanamke.”
Nikakata simu.Mwili wote ulikuwa unanichemka kwa hasira.Sikutaka kumsikia tena emmy katika maisha yangu.Nilikuwa na hasira mbaya mno kwa kitendo alichonifanyia na kama angekuwa karibu yangu sijui hata ningemfanya kitu gani.

TUKUTANE SEHEMU IJAYO………………………..
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 2
MTUNZI : PATRICK .CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Haloo” Nikasema
“Wayne umelala?”
“Ndiyo nilikuwa nimelala”
“Ok .Sasa wayne naomba uwe na moyo mgumu na usihamaki tafadhali.Ni kwamba Emmy amenifuata na hapa nilipo niko naye na ni yeye ndiye alinisisitiza nikupigie simu hii.”
“Unasemaje Chris????? “Nikasema kwa ukali.Sikutegemea kusikia kitu kama kile.
“Wayne niko na Emmy hapa.amenitafuta na kuomba nafasi ya kuongea na wewe”
“Chris…………..”Nilidakia,sikutaka aendelee tana kunipa habari za yule baradhuli
“Chris tafadhali.Kama na wewe unataka tukosane hamna shida ila tafadhali naomba usinipe habari zozote kuhusu huyu mwanamke.”
Nikakata simu.Mwili wote ulikuwa unanichemka kwa hasira.Sikutaka kumsikia tena emmy katika maisha yangu.Nilikuwa na hasira mbaya mno kwa kitendo alichonifanyia na kama angekuwa karibu yangu sijui hata ningemfanya kitu gani.

ENDELEA……………………….

“Hana haya mwanamke huyu.Kwa hiki kitu alichokifanya halafu leo anataka kuongea na mimi!! Aongee na mimi kitu gani? Kwanza si ana nguo zake humu .Zote nazipiga moto.Sitaki kumuona tena machoni mwangu huyu mwanamke.Amenifanyia kitendo cha kikatili sana.”
Nikalifungua kabati kwa hasira na kuanza kutoa ngo zote za Emmy.Nyingi nilimnunulia mimi mwenyewe na ni nguo za thamani kubwa.
“Nguo zote hizi nimegharamia hela nyingi kumbe alikuwa akiniona mimi mjinga namna hii…….”
Nikazikusanya zote na kwa hasira nikaenda nazo katika shimo la taka taka na kuzichoma moto.Sikuondoka mpaka nikahakikisha zimeteketea kabisa .
Nikarudi sebuleni na kuangalia kama kuna kitu chochote kinachoweza kumuhusu Emmy,nikaiskia geti linagongwa.haraka haaka nikafuta uso na kujiweka vizuri ili mtu asije gundua nilivyosawajika.
Nilifungua geti na kukuta ni rafiki yangu anaitwa Erasto.
“karibu Erasto “ilijilazimisha kuchangamka.
“Ahsante sana wayne”
“Nimekuja kukujulia hali ,niliambiwa na akina mangi jana ulipata matatizo ukalazwa hospitali” Akasema Erasto tukiwa tumekaa sebuleni
“Ndiyo,jana nilipatwa na matatizo ya mstuko nikaanguka na kupoteza fahamu.Ni mambo ya uchovu.Si unajua tena ,mambo yamekuwa mengi sana.” Nikadanganya.Sikutaka mtu yeyote agundue kilichotokea kati yangu na Emmy
“Du! Pole sana.lakini hivi sasa unaendeleaje?
“Kwa sasa naendelea vizuri.Madaktari wamenipima na hakuna tatizo lolote,wameniomba niongeze muda wa kupumzika.”
Nilishukuru kwa erasto kuja kunitazama kwani kidogo kichwa changu kilitulia.Tuliongea na kucheka nikaona kichwa kinakuwa chepesi.Mida ya kama saa nane hivi Chris naye akaja akiwa amefungasha chakula,tukajumuika wote kula.Kwa masaa haya machache nilifarijika sana na kujiona kama vile sina matatizo.
Ilipata saa kumi na moja jioni tukiwa katika maongezi na rafiki zangu ,geti langu likagogwa.Nikainuka na kwend akumuona mgongaji.Nilistushwa na ujio usio wa kawaida wa mwalimu wangu wa dini.katekista Nzomola ndiye mwalimu wetu aliyetufundisha mafundishoya ndoa mimi Emmy na watu wengine kama nane hivi.
“Ouh Mwalimu,Shikamoo” Nikamsalimia kwa furaha,sikutaka kuonyesha aina yoyote ya mstuko kwa ujio wake.hajawahi kuja nyumbani kwangu hata mara moja.
“Marahaba Wayne.Habari za Jumapili?
“Nzuri katekista.”
“Leo sijakuona kanisani,hata mwenzio naye sikumuona “
“Leo sikuwa najisikia vizuri ndio maana sikuja.Si unajua mwalimu nyakati hizi mambo yanakuwa mengi “
Katekista akatabasamu.nikamkaribisha ndani.Nikamtambulisha kwa Chris na Erasto amabo baada ya kuona nimepata mgeni wakaaga na kuondoka.
“Ndio mwalimu karibu sana.hapa ndio nyumbani kwangu.”
“Ahsante nimeshakaribia.”
Kimya kikapita cha kama dakika moja hivi ,katekista akaanzisha maongezi
“Wayne nimekuja hapa ili tuzungumze juu ya matatizo yaliyotokea”
Kauli ile inanistua.
“Matatizo?” yapi hayo” ikauliza
“yaliyotokea kati yako na mwenzako”
“nani kakwambia kuna matatizo? Nikauliza tena
“Mwanzako amenifuata nyumbani .Tangu saa saba mpaka mida hii ndio tumeachana.Amekuja analia na kutaka tukae tuyaongee masuala haya”
Nilimtazama mwalimu yule kwa hasira mpaka akaogopa.
“Mzee Nzomola nakuheshimu mno kama mzee wangu,umenijenga sana kiroho.Lakini kwa hili lililotokea naomba usiingilie kabisa.Hakuna kitu tunachoweza kuongea hapa.Halafu mpaka hapa nilipo kichwa changu bado hakijatulia,bado nina hasira na hatuwezi kuongea lolote na tukafikia muafaka .Mzee wangu naomba uniache kwanza nitulie halafu kwa heshima yako nitakuita mimi mwenyewe tutakaa ,tutaongea.Usione kama nimekudharau mzee wangu ,hali niliyonayo sasa hatuwezi kuongea tukafikia muafaka.Niachie siku mbili tatu,kichwa kitulie halafu nitakutafuta mimi mwenyewe.Nakuahidi hivyo.”
Nashukuru mzee Nzomola alinielewa na akaondoka.
Jumatatu sikwenda kazini,nilituma taarifa kwa wakuu wangu wa kazi kuwa ninaumwa.Mida ya kama saa tano nikiwa nimepumzika sofani nikitafakari simu yangu inalia.Nikaangalia mpigaji alikuwa ni baba mkwe yaani baba yake na Emmy.Niliiangalia simu ile ikiita na kukata ,ikaanza kuita tena.Nilikuwa na hasira na sikutaka kusikia lolote juu ya Emmy.Mwishowe nikakata shauri niipokee tu.
“Haloo mzee shikamoo”
“Nzuri baba hujambo?”
“Sijambo mzee wangu ,sijui nyie mnaendeleaje?
“Sie huku wazima.Vipi ali yako kwa sasa unaendeleaje?
“Naendelea vizuri tu mzee.Nashukuru Mungu”
Kimya kikapita cha sekunde kadhaa ,halafu akasema.
“sasa Wayne nimekupigia simu hii nilikuwa na maongezi na wewe ya muhimu sana.Tafadhali ni muhimu mno.Uko kazini?
Nikasita kujibu ,nilijua hakuna kingine kinachoongelewa hapa zaidi ya suala la Emmy.
“Niko nyumbani mzee” Nikajibu kwa ufupi.
“Ok vizuri .Basi nitakuja mida ya saa kumi za jioni ili tuongee mwanangu.Tafadhali naomba unisubiri”
“Sawa mzee wangu nitakusubiri hapa hapa nyumbani”
Nikakata simu na kuirushia katika kiti.Nadhani hata huyu mzee aligundua kuwa sikuwa katika hali yangu ya kawaida.

* * * *

Saa Tisa kama na nusu hivi za jioni nikasikia honi ikipigwa nje ya geti langu.Nilikuwa nimejilaza chumbani nikaamka na kwenda kufungua mlango.Ilikuwa ni gari ya baba yake Emmy pamoja na gari nyingine mbili jumla gari tatu.Nikawakaribisha ndani.Sikutegemea kama kungekuwa na ujumbe mkubwa vile.Watu zaidi ya kumi.Wengine nilikuwa nawafahamu kama shangazi yake zake Emmy na baba zake wadongo lakini wengine ikawa ni mara yangu ya kwanza kuwaona.Kwa picha ile ya ule ugeni nilielewa dhahiri kuwa hapa linaloongelewa ni suala langu na Emmy hakuna lingine.
Katika friji kulikuwa na vinywaji,hivyo nikamkirimu ila mmoja na kinywaji alichohitaji.
Nilisikia wakiongea kichaga,kana kwamba walikuwa wakielekezana jambo.Halafu mzee mmoja mwenye mvi na kitambi akakohoa kidogo na kusema.
“Bwana Wayne tunashukuru sana kwa ukarimu wako na kwa jinsi ulivyotupokea.hatukutegema kabisa kama ungeweza kutukirimu kwa upendo namna hii.Unaowaona hapa mbele yako ni baba,mama ,mashangazi na wajomba wa mchumba wako emmy”
Alipotaja neno “mchumba wako Emmy” nikauma meno kwa hasira,nikainama chini.Nafikiri hata wao waligundua kitu.
“Bwana wayne kwa ufupi tumekuja hapa sisi kama wazazi wa emmy ili kujaribu kuweka sawa mambo yaliyotokea.Hatukuwa tunajua nini kinaendela.Sisi tulikuwa katika maandalizi ya harusi.hatukujua kilichojificha nyuma ya pazia.Jana usiku ndio baba yake akatupigia simu na kutukusanya na kutueleza kuwa kuna tatizo limetokea.Emmy alitueleza yote mwanzo hadi mwisho bila kuficha hata kitu kimoja.Kwa kweli tulistuka sana sana.mama yake presha ikapanda ikabidi apelekwe hospitali.Tunashukuru Mungu hali yake imeendelea vizuri na mpaka sasa tunaye hapa.Kwa kweli kwanza sisi kama wazazi na wanafamilia ya Emmy tunakupa pole sana kwa yaliyotokea na vile vile tunakupongeza kwa ujasiri na uvumilivu wako.Umeonyesha uvumilivu na busara ya hali ya juu sana.Angekuwa ni mtu mwingine sijui tungekuwa tunaongea nini saa hizi.Ni wazi angefanya mambo ya ajabu sana.”
Akatulia akakohoa kidogo halafu akaendelea.
“ Wayne narudia tena kuwa hata sisi suala hili limetuuma mno.hatukutegemea kama tungepata aibu ya namna hii.Hii ni aibu kubwa na hata kuja kukuona na kuongea na wewe leo hii ni kwa sababu hatuna jinsi.Lengo letu kubwa la kuja hapa sisi ni kujaribu kuona nini tufanye ili kuweza kuokoa kile ambacho tumekwisha kianza.pamoja na kuwa inauma na bado una hasira lakini najua ndani kabisa ya moyo wako bado kuna kiasi Fulani cha upendo kwa emmy.Emmy Amelia sana na kuomba msamaha mno na kuahidi kuwa amekwisha achana na yule mtu wake aliyemsababishia haya yote.Amelia sana na ametutuma tuje sisi kama wazee tuombe msamaha kwa niaba yake .pamoja na shetani aliyepita kutaka kuvuruga mipango mizuri ya mbeleni ya maisha yenu lakini nina tumaini kuwa bado kuna kila dalili ya upendo wa kweli kati yenu.Suala la nyumba ni gumu na mambo kama haya huwa yanatokea.hakuna nyumba inayokosa majaribu na misuko suko.Na mnapojaribiwa ni wazi yupo atakayeanguka au mkaanguka wote.lakini sikuzote upendo wa kweli husimama panapo majaribu na hata mkijaribiwa mwisho wa siku mtabaki mnapendana na kusimama imara.Sikuzote wapendanao kweli hata kama wakianguka hushikana mikono ,wakasimama na kusonga mbele.Upendo wa kweli siku zote haushindwi na lolote.Ninaona picha ya upendo wa kweli ulio kati yenu.Ni upendo hu wa kweli ndio uliokuzuia kufanya lolote mpaka leo hii.Roho wa Mungu yuko pamoja nawe na ndiye anayekuongoza katika kufanya maamuzi haya yenye busara.kwa maana hiyo Wayne sisi wazee wako tumekuja rasmi kama wazazi kukuangukia na kuomba msamaha na kufuta kila kilichotokea ,tusimame pamoja tushikane mikono na tusonge mbele.Tumekosa sisi tunaomba utusamehe sisi.Emmy yuko tayari kuja kuomba msamaha mbele yetu sisi wazee wake.hatukuweza kuja naye mpaka tutakapoongea na wewe na tuone kama utakuwa tayari kumsamehe mwenzako”
Akamalizia mzee yule ambaye alikuwa akiongea kama mchungaji vile.Sijui wazee hawa walikuja na nini manake nilijisikia maneno yao yakiniingia moyoni na kujikuta licha ya hasira nilizokuwa nazo kutaka kumsamehe Emmy.Kuna wakati ulikuwa unakuja moyo wa kusamehe lakini papo hapo inakuja picha ya Emmy akiwa amekumbatiana na lile libaba.Ikija picha hii hasira zinarudi tena.
Niliinua kichwa niliposikia baba yake Emmy akikohoa na kutaka kuongea machache.
“Wayne mwanangu,na mimi naona niongezee machache katika yale aliyoyasema mkubwa wangu.Kwa kweli pamoja na uzee wangu huu nilikuwa nimeishiwa maneno ya kusema ndio maan nikamuachia mkubwa wangu.Ameeleza kila kitu na sitaki kurudia yale aliyoyasema ila nata kusema machache kuwa Emmy ni binti niliyemlea katika maadili mazuri ya kiroho na kwa kweli alikuwa ni binti mwenye heshima kubwa.Sikutegemea kwa jinsi nilivyomlea aje afanye yale aliyoyafanya.Ndio maana hata mama yake aliposikia mambo haya presha ikapanda kwa sababu hatukumlea awe mtu wa namna hii.Nina imani tabia hii aliyoifanya ni mambo ya tamaa na kuiga.Tena ni baada ya kutoka nyumbani.Pale alipoanza maisha yake ya kujitegemea.Mwanzoni alipotaka kuhama nyumbani na kwenda kuishi mweneyewe nilikataa kwa kuhofia asije akaambukizwa kufanya mambo yasiyofaa katika jamii lakini aliomba sana kuwa anataka ajifunze maisha ya kuishi mwenyewe ndipo nikamruhusu.Hii si tabia yake hata kidogo.Hakuwa na tabia hizi.Ni tamaa tu ya kuwa na pesa na vitu vizuri vizuri.Toka akiwa mdogo nilimfundisha kutambua mara moja anapokosea na kuomba msamaha.Kweli amelitambua kosa alilolifanya na kuomba msamaha.Mimi kama baba yake nilikataa kabisa kabisa kuishughulisha tena na masuala yake baada ya kusikia aibu aliyoifanya.Aliniomba sana sana nimsamehe na nimsaidie kuomba msamaha kwako.Kwa macho yangu niliona katika macho yake kuwa alikuwa akimaanisha toba ya dhati.Ni hilo ndilo lilinisukuma mie nimsamehe na kunifanya nifike hapa leo pamoja na wenzangu hawa kuomba msamaha kwa niaba yake kwanza na baadae yeye mwenyewe atafika hapa na kuomba msamaha kwako mbele yetu.Wayne hatutaki katika hatua kubwa mliyofikia mshindwe kuendelea.Mkisameheana katika hili nina imani mtakuwa mmejenga kitu kikubwa sana na nyumba yenu itajengwa katika kusameheana hata likitokea kubwa la aina gani.Kwa hayo machache Wayne mimi kama baba yake naomba sana niko chini ya miguu yako msamehe mwenzio na muendelee na mipango yenu ya ndoa kama kawaida.”
Baada ya baba yake Emmy kumaliza kuongea akafuata shangazi yake na baba zake wadogo.Du ! niliombwa kila aina ya msamaha.Kila aina ya ushawishi ilitumika ili niweze kumsamehe Emmy.Kwa kweli sijui wazee hawa walikuwa na kitu gani manake niliwasikiliza na kujikuta ninakuwa na moyo mweupe tena wa kumsamehe Emmy.Pamoja na kwamba zile picha mbaya zilikuwa bado zikinijia nilijawa na moyo wa kusamehe.Hatimaye ikaja zamu yangu kuongea.Kila mmoja akatulia kutaka kunisikiliza nitasema nini.
“wazee wangu nimewasikilza vizuri.Ujio wenu leo umenipa faraja sana.Sijui mmekuja na kitu gani lakini kwa kweli najiona mwepesi na mwenye furaha sana.Mmenisaidia kuutua mzigo mzito niliokuwa nimeubeba.Ahsanteni sana.Wazee wangu kwa kweli lililotokea ni pigo kubwa kwa moyo wangu.Nimeumia sana.Kwa kweli sikutegemea jambo kama lile kutokea kwa mtu kama Emmy tena kwa wakati kama huu.kama mzee pale alivyosema ni kwa maongozi ya Mungu niliamua kutumia busara zaidi katika suala hili.Sijamueleza mtu yeyote zaidi ya rafiki yangu wa karibu.Sikuwa na haraka ya kutaka kuutangazia ulimwengu nini Emmy kafanya.Sikutaka dunia imchukie.naamini kama mzee alivyosema ni tamaa za pesa ,mali na vitu vizuri vizuri ndio ilmponza.Iwapo ningeamua kumdhalilisha Emmy kwa kutangaza aliyoyafanya ,nisingekuwa nafanya hivyo kwake tu bali hata kwa wazee wake waliomlea katika madili mema,ndugu zake,ndugu zangu na hata wazazi wangu.Pamoja na yote yaliyotokea,machungu yote niliyoyapata,maumivu ya ndani na nje,bado ninathubutu kusimama nakutamka mbele yenu wazee wangu kuwa nimemsamehe Emmy na niko tayari kurudiana naye tena na mipango ya ndoa yetu kuendelea kama kawaida”
Hawakuamini ,wakanitaka nirudie tena kauli yangu.Nikarudia tena na kuwahakikishia kuwa Emmy nimemsamehe kwa moyo mmoja na wala sina kinyongo naye tena.
Wazee wakainuka na kuja kunipongeza.Kilikuwa ni kipindi cha furaha sana.Baada ya kupongezana baba yake mkubwa Emmy akasimama na kusema.
“Wayne wewe ni kijana wa ajabu .Katika kuishi kwangu mpaka nimefika uzee huu sijawahi kuona mtu mwenye moyo wa ajabu kama wako Wayne.laiti dunia ingekuwa na vijana 100 kama wewe basi pangekuwa ni sehemu nzuri sana kwa kuishi.Mimi binafsi sijui hata niseme kitu gani.Sijui hata nikushukuru vipi kwa ujasiri wa kumsamehe mwenzako.Narudia tena kijana unaongozwa na roho wa Mungu.Kwa ulimwengu wa sasa si rahisi mtu kumsamehe mwenzake aliyemfanyia kitendo kama alichokufanyia emmy.Ahsante sana kijana.ahsante sana wayne”
akanishika mkono tena.Akawageukia wazee wengine na kuwaambia kuwa ni wakati muafaka kwa Emmy kuitwa .Ikapigwa simu na baada ya kama dakika kumi hivi Emmy akaingia ndani.Moyo wangu ukastuka tena baada ya kuiona sura ya Emmy ikiwa na macho mekundu yaliyovimba ikiashiria jisni alivyokuwa akilia.hakutaka kuniangalia usoni.Uso wake alikuwa kuinamisha chini.Nilishindwa kuwa na hasira nikamuonea huruma.
Baba mkubwa wa Emmy akasimama na kuongea machache.
“Kijana wetu Wayne,na ndugu wote ambao mko hapa leo,napenda kuchukua nafasi hii kuongea machache kwa sababu mengi yamekwisha semwa na nisingependa kuyarudia tena.Tumemsikia kijana wetu alivyosema.Toka ndani ya moyo wake amekubali kumsamehe Emmy .Kwa kuwa kijana wetu Wayne si mtenda kosa basi hatuna budi sasa kumpa nafasi mtenda kosa yeye mwenyewe kwa mdomo wake akiri kosa na kuomba msamaha kwa mchumba wake,wazazi wake na kwa Mungu wake.Emmy uwanja ni wako ,waangukie wazazi wako uwaombe msamaha pamoja na mchumba wako”
Kimya kikatanda mle sebuleni.Emmy huku akilia akainuka na kwenda kupiga magoti mbele ya baba yake na kulia akiomba kusamehewa.Baba yake akamshika kichwa na kumuombea kwa Mungu amsamehe na kumtangulia katika kila jambo alifanyalo,halafu akatangaza kuwa tayari amemsamhehe mwanae kwa kosa alilolifanya.Emmy akaenda tena kwa mama yake na kuomba msamaha kama alivyofanya kwa baba yake.Naye halikadhalika akamsamehe.Kazi ikawa kwangu.Akasita kuja kwangu pale tulipogonganisha macho.Nadhani ni nafsi yake ilikuwa ikimsuta kwa mambo aliyoyafanya.Wazee wake wakamuangalia kwa ukali hali iliyomlazimu kujikaza kisabuni na kunisogelea.akapiga magoti mbele yangu na kunishika miguu.
“Wayne, nakosa hata neno la kusema.Nashindwa nikwambie kitu gani cha kuweza kulifuta doa nililoliweka moyoni mwako kwa tamaa zangu.Nimekuumiza Wayne,na sistahili hata huruma yako.lakini pamoja na hayo yote niliyokufanyia naomba ufahamu kitu kimoja kuwa toka ndani ya moyo wangu bado nakupenda sana na ninaomba msamaha wa dhati kabisa .Naomba unisamehe na tuendelee na mipango yetu ya ndoa kama tulivyokuwa tumepanga.naahidi sintafanya tena kosa kama hili katika maisha yangu.nakuahidi kuwa mke mwema kama utanisamehe.naomba msamaha wako Wayne..”
Emmy macho yalikuwa yamejaa machozi,akilia kwa kosa alilokuwa amelifanya.Hata mimi ilikuwa ikiniuma sana na nilikuwa nikijiuliza mara mbili mbili kama ni kweli nimeamua kwa dhati kumsamehe? Nikakubaliana na moyo wangu kuwa nikubali kumsamehe.Nikamshka mkono nikamuinua na kumtazama usoni.
“Emmy,nakubali ulinikosea.Lakini kama tunavyofundishwa kila siku nav iongozi wetu wa dini na kama maandiko yanavyosema kuhusu kusamehemana,mimi kwa moyo wangu wote nimekubali kukusamehe.Nakuombea kwa Mungu naye akusamehe na tuendelee na mipango yetu ya ndoa kama kawaida “
Maneno yale machache yakampa Emmy faraja kubwa na kumfanya ainuke na kunikumbatia kwa furaha.Sebule yangu ikageuka sehemu ya furaha kubwa.Watu tukashikana mikono na kupongezana.Lilikuwa nitukio kubwa na la kihistioria katika maisha yangu.Vinywaji vikaletwa tukaendelea kuburudika hadi ilipotimu saa mbili za usiku tukaagana wakaondoka.Walipoondoka nikabaki mwenyewe nikitafakari juu ya kilichotokea.Pamoja na kumsamehe Emmy lakini bado roho yangu haikuwa ikimtazama kama nilivyokuwa nikimtazama hapo zamani.
“Hivi ni kweli roho yangu imekubali kwa dhati kumsamehe Emmy kwa kitu alichonifanya?? Nikajiuliza tena kwa mara ya pili.Saa chache zilizopita sikutamanai kkumuona tena Emmy katika maisha yangu kuokana na kitendo kile lakini sasa nimeamua kumsamehe.
“Kwa vile nimamua kumsamehe acha tu nimamehe.Nahisi amekiri toka moyoni mwake.”Nikajisemea mwenyewe.
Maisha mapya yakaanza tena.Penzi letu likaonekana kama vile limechipua upya.Upendo ukaongezeka mara dufu.Enmmy alionekana kubadilika sana na hiyo ikanihakikishia kuwa hawezi kurudia tena kosa alilolifanya.
Taratibu jeraha lililokuwa moyoni mwangu likaanza kufutika.Nikaanza kusahau yote yaliyokuwa yamepita.

TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………………..
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 3
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Maneno yale machache yakampa Emmy faraja kubwa na kumfanya ainuke na kunikumbatia kwa furaha.Sebule yangu ikageuka sehemu ya furaha kubwa.Watu tukashikana mikono na kupongezana.Lilikuwa nitukio kubwa na la kihistioria katika maisha yangu.Vinywaji vikaletwa tukaendelea kuburudika hadi ilipotimu saa mbili za usiku tukaagana wakaondoka.Walipoondoka nikabaki mwenyewe nikitafakari juu ya kilichotokea.Pamoja na kumsamehe Emmy lakini bado roho yangu haikuwa ikimtazama kama nilivyokuwa nikimtazama hapo zamani.
“Hivi ni kweli roho yangu imekubali kwa dhati kumsamehe Emmy kwa kitu alichonifanya?? Nikajiuliza tena kwa mara ya pili.Saa chache zilizopita sikutamanai kkumuona tena Emmy katika maisha yangu kuokana na kitendo kile lakini sasa nimeaua kumsamehe.
“Kwa vile nimamua kumsamehe acha tu nimamehe.Nahisi amekiri toka moyoni mwake.”Nikajisemea mwenyewe.
Maisha mapya yakaanza tena.Penzi letu likaonekana kama vile limechipua upya.Upendo ukaongezeka mara dufu.Enmmy alionekana kubadilika sana na hiyo ikanihakikishia kuwa hawezi kurudia tena kosa alilolifanya.
Taratibu jeraha lililokuwa moyoni mwangu likaanza kufutika.Nikaanza kusahau yote yaliyokuwa yamepita.

ENDELEA……………………..

Ni siku yetu ya kufunga ndoa.Sikuweza kupata usingizi usiku mzima.Nilikuwa nikiwaza kama ni kweli baada ya kupitia msuko suko mkubwa hatimaye ninakwenda kufunga ndoa.Ilikuwa ni kama ndoto.
Asubuhi nilikuwa ni mtu mwenye mawazo na wasi mwingi.Mpambe wangu aliliona hilo ,akajaribu kunitoa wasi wasi na kunifanya nichangamke.Kwa mara nyingine tena nikajikuta niukijiuliza kama ninalokwena kulifanya leo hii ni sahihi na nina uhakika nalo.Baada ya tafakari ya kina nikaona hakuna haja ya kuendelea kujiuliza maswali mengi.Maji nimekwisha yavulia nguo hivyo sina budi kuyaoga.
“mwenzangu,pokea pete hii iwe ishara ya upendo na uaminifu kwako.Kwa jina la baba nan mwana na la roho mtakatifu.Amina” Nilitamka maneno haya huku nikimvisha pete ya Ndoa emmy kama mke wangu halali mbele ya kanisa lililofurika watu wakiwa kama mashahidi.Wakati nayatamka maneno haya bado ndnai ya nafsi yangu kuna kitu kilikuwa kikiniuliza “Wayne are you sure with what you are doing? Sauti ile ilikuwa ikiniuliza kama ninayatamka manenoyale kwa dhati toka moyoni mwangu..Sikuijali sana sauti ile ,kwa sababu nilijua nimekubali kwa dhatiya moyo wangu kufunga ndoa na Emmy.Niliamini mwangwi ule ulitokana na tukio lililotokea na ambalo bado jeraha lake halijapona sawa sawa..Tukio ambalo kusema ukweli haliwezi kufutioka kiurahisi.
Baada ya kumalizika kwa shughuli za kanisanii,shghuli kubwa ikafanyika ukumbini.Ilikuwa ni sherehe ya aina yake na kila mmoja aliyehudhuria alisuuzika moyo.Saa sita za usiku tukaondoka ukumbini na kuwaacha bado watu wakishereheka,tukaenda katika hoteli tuliyoandaliwa maalum kwa ajili ya kulala kwa usiku huo kabla ya kuelekea katika fungate letu tuliloamua kwenda Zanzibar.
Huo ukawa ni usiku wetu wa kwanza kama mke na mume.Ni usiku huo ambao naweza nikasema kuwa maisha yangu yalianza upya.

* * * *

Maisha ya ndoa yalikuwa mazuri na yenye furaha.Nilionyesha kila aina ya upendo kwa Emmy.naye hali kadhalika alionyesha upendo wa kila namna kwangu ilimradi ilikuwa ni furaha na mashamsham kila siku.Kila asubuhi ni kama penzi letu lilianza upya.Miezi hii sita ya kwanza sikuona kitu chochote kibaya cha kunikwaza na ambacho kingenifanya niseme ule msemo uliozoeleka wa ndoa ndoano.Sikuyaona magumu ya ndoa.Niliwashangaa wale wote wanaodai kuumizwa na ndoa zao.Sikuelewa ni kwa nini wengine hawakutaka kabisa kusikia kitu ndoa.Kwa furaha niliyokuwa nayo nikwa ndani ya ndoa sikuweza kufikiri kama iko siku ninaweza kutembea nje ya ndoa.Niliwashangaa wale watu ambao wamekuwa na wapenzi nje ya ndoa zao.Sikuhitaji mpenzi wa nje kwa sababu nilipata kila kitu nilichohitaji toka kwa mke wangu Emmy.Kwa muda huu mfupi nikanawiri na kuvutia zaidi.Nikawa mshauri maarufu wa kuwashauri vijana wenzangu ambao bado walikua wakisita na kuogopa ,kufanya maamuziya kufunga ndoa kwa sababu ndoa ni tamu ajabu. .Nilitolea mfano wa raha nizipatazo mimi .
Mwezi wa saba toka tufunge ndoa Emmy akanitaarifu kuwa tayari alikuwa mjamzito.Hii ikaongeza furaha na upendo mara dufu ndani ya familia yetu.

Furaha hii haikuwa tu baina yetu bali hata kwa ndugu na jamaa zetu.Nilimshukuru Mungu kwa kunipa mke kama Emmy.Nilimpenda mno mke wangu na hasa katika kipindi hiki cha ujauzito.Siku zikazidi kusonga na hatimaye siku ya kujifungua ikafika na Emmy akafanikiwa kujifungua mtoto mzuri wa kiume aliyekuwa na afya bora.Nilifurahi kupita kiasi kwa zawadi ile ya mtoto.Ndugu ,jamaa na marafiki wakaungana nasi katika furaha ile kubwa ya kupata mtoto.Kwa furaha niliyokuwa nayo nilimzawadia Emmy zawadi ya gari jipya kabisa kama shukrani zangu kwake kwa kumleta duniani mtoto wetu mpendwa ambaye nilipendekeza aitwe Baraka.niliamini mtoto yule alikuwa ni baraka za mweneyezi Mungu kwetu.Emmy akafurahi mno kwa zawadi le niliyompa.
Ukurasa mpya wa malezi ukaanza nikiwa baba na Emmy akiwa mama.Nilifurahi kushirikiana na mke wangu katika malezi ya mwanetu Baraka.Muda wa mapumziko ya uzazi ulipokwisha ikatyulazimu kumtafuta msaidizi atakayetusaidia kumlea mtoto wakati tukiwa kazini.Tulifanikiwa kumpata msaidizi kwa msaada wa jiani yetu.
Siku zilikatika kama mvua na ikafika miezi sita.Tukajadili tukaona kuwa huo ndio muda unaofaa kwa ajili ya kumbatiza mwanetu.maandalizi yakafanywa na hatimaye tukafanikiwa kumbatiza mwanetu kwa jina la baraka.Mtoto akaendelaa kukua akiwa na afya njema mno.

* * * *

Miaka minne ilipita.Maisha yakiwa ni yenye furaha na upendo mkubwa.Mtoto wetu baraka alikuwa anasoma katika shule ya awali ya Maria Theresa academy.Baraka alikuwa akiendelea kukua kwa furaha na upendo mkubwa.
Kwa muda wa miaka yote hiyo hali ya upendo ndani ya ndoa yetu ilikuwa kubwa na hii ilitufanya tuwe mfano wa kuigwa.Nilikwisha sahau yote yaliyotokea kipindi cha nyuma.Nilichokuwa nikiangalia kwa sasa ni malezi ya mtoto wetu na kumtengenezea maisha mazuri ya baadae.
Ilikuwa siku ya Ijumaa siku ambayo sikuwa na shughuli nyngi za kufanya nikaamua kuwahi kurudi nyumbani ili kujumuika na famili na yangu .Siku zote huwa nikipata nafasi hupendelea kuwahi kurudi nyumbani na kuitumia nafasi hiyo nikiwa na familia yangu tukifurahi pamoja.
Nikiwa mita kadhaa kabla ya kufika nyumbani kwangu nikaona geti likifunguliwa na gari ya mke wangu ikitoka.Tulipokutana akasimamamisha gari,akashusha kioo tukasalimiana.
“Hello Darling” akasema mama Baraka
“Hello honey” nikajibu
“Mbona leo mapema hivi kulikoni? Akauliza
“Nimeamua kuja kukaa na familia yangu.Sikuwa na kazi nyingi.Safari ya wapi tena? Nikauliza
“Kuna mama mmoja jirani yetu ni mjamzito sasa ameanguka ghafla ndio tunataka tumkimbize hospitali”
“Ouh ! basi wahini mara moja.” Nikajibu naye akaliondoa gari kwa kasi kumuwahi mgonjwa..Nikaingiza gari ndani nikasalimiana na mwanangu Baraka halafu nikamwacha akicheza mimi nikaelekea chumbani kwangu.Kitandani kulikuwa na kompyuta aina ya Laptop ya mke wangu.Kwa kuwa nilikuwa nikihitaji kupumzika nikaamua kuitoa na kuiweka pembeni.Kompyuta ile ilikuwa imechomekwa katika umeme na ilionyesha kuwa muda mfupi uliopita alikuwa akiitumia.Kwa haraka haraka nikaona kama alikuwa akiwasiliana na watu wake kwa kutumia Yahoo messenger.Kuna meseji ilikuwa ikikonyeza kuashiria kuwa haikuwa imesomwa,nikang’amua kuwa Mama Baraka alikuwa ameondoka ghafla na kumfanya asahau kuizima kompyuta yake.Nikaamua kufunga ile Yahoo messenger ili watu wale aliokuwa akiwasiliana nao wajue kuwa hayupo.Kabla sijaifunga kabisa ile Yahoo messenger,nikaliona jina moja limeandikwa My special one.nikapata udadisi Fulani.Nikafungua ule ukurasa waliokuwa wakiwasiliana nikaanza kuusoma .Meseji ya mwisho ilisema
“Vipi Darling mbona kimya? Are you there??”
Baada ya meseji hiyo zikafuata BUZZ nyingi..Nilikuwa nimesimama nikaamua kukaa na kusoma sawa sawa.Nikaanza kuisoma tokea mwanzo.Kutokana na muda ilionyesha kuwa walikuwa wameanza kuwasiliana kama dakika ishirini zilizopita.Mfululizo wa mawasiliano yao ulikuwa hivi
EMMY: Nimeshafika nyumbani dear
MY SPECIAL ONE : Ouh ! good.Mimi bado niko ofisini
EMMY: Unatoka saa ngapi leo
MY SPECIAL ONE : Leo nitachelewa kutoka kidogo.
EMMY: Ok poa Darl ,sasa hebu tuendelee kujadili lile suala la mtoto manake mimi linalipa wakati mgumu sana
MY SPECIAL ONE: Darl ni kama nilivyokueleza kuwa mtoto ni lazima nikamtambulishe kwa babu zake.Nataka mtoto aanze kunizoea taratibu ili hata baadae akielezwa kuwa huyu ndiye baba yako mzazi asishangae.Nataka aanze taratibu kuwafahamu ndugu zake.
EMMY: Darl unanipa wakati mgumu sana.Nashindwa hata nifanye nini
MY SPECIAL ONE: Usiogope Darl.Unajua mtoto anakua kwa kasi na anazidi kupata akili.Kwa maana hiyo inabidi aanze kujua toka mapema ,nani baba yake nani siye.Nashukuru kwa ile safari ya mbuga za wanyama imeniweka karibu naye sana.
EMMY: Yah hata mimi nimefurahi kwa hilo kwa sababu kila siku ni lazima akuulizie.
MY SPECIAL ONE: Hivyo ndivyo ninataka.Jaribu kwa kadiri uwezavyo kumuweka karibu zaidi na mimi.
EMMY: Nakubali Honey mtoto ni wako lakini siku huyu jamaa akigundua najua ataumia mno.Hujui ni jinsi gani anavyompenda Baraka
MY SPECIAL ONE: Yah ! I now that.Ni wazi ataumia lakini hakuna jinsi.Ni lazima ifike mahala akubaliane na ukweli kuwa mtoto si wake.Na kwa kweli darling sitaki tuendelee kulificha hili kwa muda mrefu.nataka ifike wakati tuchukue uamuzi wa kumueleza ukweli kuwa mtoto si wake.Tukiendelea kukaa kimya tutakuwa hatumtendei haki mtoto.
EMMY: Lakini darling ni wazi siku Wayne akiufahamu ukweli hakutakuwa na jingine zaidi ya kuachana.Niliwahi kumuumiza mara moja miaka kadhaa ya nyuma na nikamuahidi kuwa sintamuumiza tena.Sasa akigundua hili sijui nini kitatokea.
MY SPECIAL ONE: Honey usijali kitu chochote.bado naendelea kuweka mazingira mazuri ili kama kutatokea la kutokea pindi utakapomueleza ukweli basi moja kwa moja unahamia kwangu na tunaanzisha familia,mimi ,wewe na mtoto wetu baraka.
EMMY : (smiley) Are you sure darling?
MY SPECIAL ONE :Yes baby I’m sure.Lengo langu mimi sikuzote limekuwa kuishi na wewe.Nataka kuishi na mwanangu.nataka mwanangu akasome Ulaya.Nataka siku moja sisi sote tukaishi Ulaya.
EMMY : Ingawa nakupenda na niko tayari kufanya lolote kwa ajili yako lakini kila ninapomfikiria mume wangu nafsi inanisuta sana.Wayne ananipenda kupita maelezo.
MY SPECIAL ONE: Usijidanganye baby kuwa mumeo anakupenda.Unachotakiwa ni kuangalia wapi unapata furaha ya maisha.Fuata moyo wako unavyokutuma.
EMMY : Ok tuachane na hayo.Umepanga lini umpeleke mtoto kwa babu zake?
MY SPECIAL ONE: Jumamosi ya wiki ijayo.Anza kuandaa tararibu mazingira ili
Mumeo asiweze kugundua chochote.
EMMY: Nitajitahidi darling
MY SPECIAL ONE: Vipi weekend hii una ratiba gani?
MY SPECIAL ONE: BUZZ
BUZZ
BUZZ
MY SPECIAL ONE : “Vipi Darling mbona kimya? Are you there??”
BUZZ

Mawasiliano yakaishia hapa.nadhani ni wakati huu Emmy alipopata taarifa ya ugonjwa wa jirani yetu na kumfanya aondoke ghafla bila hata kukumbuka kuizima kompyuta yake.Ilikuwa ni kama ndoto ya mchana.Sikuamini nilichokuwa nimekisoma,nikakaa vizuri na kurudia tena na tena .Nikafungua archive na kukuta kumbukumbu ya mawasiliano kati ya Emmy na my special one.Jasho lilikuwa likinitiririka,mapigo ya moyo yakaanza kwenda kwa kasi isiyoelezeka.Nikakaa kitandani huku nikihisi kuishiwa nguvu taratibu.

TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………………..
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 4
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
MY SPECIAL ONE: Jumamosi ya wiki ijayo.Anza kuandaa tararibu mazingira ili
Mumeo asiweze kugundua chochote.
EMMY: Nitajitahidi darling
MY SPECIAL ONE: Vipi weekend hii una ratiba gani?
MY SPECIAL ONE: BUZZ
BUZZ
BUZZ
BUZZ
MY SPECIAL ONE : “Vipi Darling mbona kimya? Are you there??”
BUZZ
BUZZ
BUZZ

Mawasiliano yakaishia hapa.nadhani ni wakati huu Emmy alipopata taarifa ya ugonjwa wa jirani yetu na kumfanya aondoke ghafla bila hata kukumbuka kuizima kompyuta yake.Ilikuwa ni kama ndoto ya mchana.Sikuamini nilichokuwa nimekisoma,nikakaa vizuri na kurudia tena na tena .Nikafungua archive na kukuta kumbukumbu ya mawasiliano kati ya Emmy na my special one.Jasho lilikuwa likinitiririka,mapigo ya moyo yakaanza kwenda kwa kasi isiyoelezeka.Nikakaa kitandani huku nikihisi kuishiwa nguvu taratibu.

ENDELEA………………..
‘No this must be a joke.Its not true” Nikasema mwenyewe huku nikijifuta jasho
“Emmy cant do to me something like this” Nikasimama na kuzunguka zunguka mle chumbani ,nikapata wazo.Nikachukua flash disk yangu nikaichomeka katika ile kompyuta ya Emmy na kurekodi kumbukumbu zote za mawasiliano baina yake na huyo special one.baad ya hapo nikaiacha kompyuta ile kama ilivyokuwa .Sikutaka Emmy aje agundue kuwa nilikuwa nimezisoma meseji zake.Mambo yakle niliyoyasoma amabayo nilihisi ni kama utani vile ni makubwa na yalihitaji uchunghuzio wa hali ya juu.Nilipohakikisha kuwa hataweza kugundua kitu chochote nikatoka,na kwenda kukaa sebuleni.Sikuwa na nguvu hata za kuendesha gari.Nikaanza kutafakari yale niliyoyasoma.
“MY SPECIAL ONE” Who is my special one? Nilihitaji kumfahamu huyo aliyeandikwa kama my special one.
“I need to find out the truth.I’ll find out the truth.And if its true,you’ll cause me another pain … this will be BEYOND PAIN” Nikasema mwenyewe huku nikiuma meno kwa uchungu.
Sikumbuki usingizi ulinipitia saa ngapi ila nilistuka kwa busu zito nililopigwa katika paji la uso.kwa haraka nikafumbua macho ,kumbe alikuwa ni mke wangu Emmy amerudi toka hospitali.Moyo ukastuka sana nilipomuona.Ghafla kumbukumbu ya nilichokisoma katika kompyuta yake ikaja kwa kasi .Hasira ikanipanda kwa ghafla sana lakini nikajikaza kiume na kuonyesha sura ya tabasamu ili kumfanya asiwe na wasi wasi.Sikutaka kupeleka mambo kwa haraka hadi pale nitakapokuwa na uhakika wa kutosha kama yale niliyoyasoma ni mambo ya kweli au si kweli
“hello darling” Nikasema kwa sauti ya chini na ya uchovu
“Ouh my love,mbona umenyong’onyea hivyo ,unaumwa? Akauliza emmy huku amekaa karibu yangu na kunishika kichwa.
“Siumwi kitu honey ni uchovu tu unanisumbua” Niliumia tena moyoni kutamka neno honey.lakini kwa kuwa nimeshaamua kuliendea suala hili taratibu sikuwa na jinsi zaidi ya kuendelea kuonyesha mapenzi kwa Emmy ili asije kung’amua kama ninafahamu lolote kuhusu siri zake.
“Baba baraka kwa nini hujaenda kulala chumbani ?.Toka umerudi umelala hapa kwenye kochi ? Akauliza emmy
“Kuna kipindi nilikuwa naangalia katika Tv nikajikuta nimepitiwa na usingizi.Vipi mgonjwa anaendelaje? Mbona mmewahi kurudi namna hiyo?
Nikauliza na kumfanya Emmy ajibu kwa wasi wasi kidogo
“Tumemfikisha hospitali ,nimeacha anashughulikiwa mimi nikaondoka”
“Yaani mama baraka unaondoka na kuwaacha wenzako hospitali bila hata kujua mgonjwa anaendeleaje?
“baba Baraka nilikuwa nakuwahi wewe,nilijua ungekuwa mwenyewe ungeboreka sana”
Nilitabasamu baada ya kujua kuwa ananidangaya.Nafikiri alipofika hospitali alikumbuka kuwa hakuizima kompyuta yake na ndio maana akarudi haraka namna ile.
“Ngoja nikabadili nguo nioge,pengine nitajisikia vizuri “Nikainuka kuelekea chumbani kwangu na kumuacha mama Baraka akiwa kwene sofa akionekana mwingi wa mawazo.Chumbani sikuikuta ile kompyuta yake kitandani ,alikuwa ameishaitoa na kuizima kabisa halafu akaifungia katika kabati lake.Nikatabasamu nikavua nguo na kwenda kuoga kisha nikarudi na kijilaza kitandani.Mlango ukafunguliwa Emmy akaingia,akanifuata pale kitandani nilikokuwa nimelala akanikumbatia na kunibusu.
“Honey nikupikie chakula gani leo? Akauliza
“Chochote utakachopika mi nitakula tu” Nikajibu huku nikitabsamu
“Ok honey nitakupikia chakula kitamu ajabu.Halafu honey kuna jambo nataka tuongee”
“Jambo gani hilo “ Nikauliza
Emmy akakaa kimya akafikiri kwa sekunde kadhaa na kusema
“unajua kuna rafiki yangu mmoja tuko naye ofisi.moja ana harusi ya mdogo wake jumamosi ijayo na inafanyikia nyumbani kwao Same .Ameniomba nimsindikize .Sijampa jibu lolote nikaona ni bora nije nikuombe ruhusa wewe..”
Emmy akasema.
Nusura chozi linidondoke baada ya kusikia maneno yale.Nilianza kuamini kile nilichokisoma .Emmy na mu aliyemwandika kama my special one walikuwa wamepanga kwenda nyumbani kwa huyo special one kumtambulisha Baraka kwa babu zake yaani baba na mama yake huyo special one.Iliniuma kupita kiasi.Nikakaa kimya nikifikiri nini cha kusema.
“Darling niambie basi,utaniruhusu kwenda?” akasema Emmy
Sikujibu kitu nikaendelea kufikiri
“Honey say yes please” akanibembeleza Emmy.
“hakuna shida ,waweza kwenda”nikajibu kwa ufupi.
“Ouh honey thank you..mwaaahh” akasema na kunibusu mdomoni.akatoka na kuelekea jikoni
“Ee Mungu kwa nini mambo haya yananikuta mimi? Nikawaza kwa uchungu huku machozi yakinilenga lenga.Nilikuwa nimejilaza kitandani ikanilazimu niinuke na kukaa.
Kichwa nikaanza kukiona kizito mno.Mateso na maumivu niliyoyapata miaka kadhaa iliyopita yamerudi tena.
“Daddy !!….’Nikastuliwa na sauti ya Baraka aliyekuwa amerudi toka shuleni
“Ouh Baraka.umerudi ! Nikasema.
“Ndiyo baba.pole na kazi”Akasema
“ahsante mwanangu.Habari ya shule?
“Nzuri baba”
Mtoto hyu akaniongezea tena machungu.Nilimpenda Baraka kupita kitu chochote kile katika maisha yangu.
“ This cant be.Baraka is my son” Nikasema kimoyo moyo.
“daddy mbona unalia? Akaniuliza Baraka na kunifanya nistuke.Nilikuwa nimeshindwa kujizuia kutokwa na machozi nilipomuona baraka.
“macho yananisumbua sana leo” Nikajibu na kujilazimisha kutabasamu.
“Haya Baraka nataka nipumzike,nenda kabadili nguo halafu baadae uje unionyeshe umejifunza nini shuleni leo”
“Ok Daddy” baraka akasema na kutoka mle chumbani.Nilimsindikiza kwa macho mtoto yule mzuri mwenye akili nyingi ,niliyemkuza katika adabu na tabia njema kiasi cha kumfanya kuwa mfano wa kuigwa mtaani na hata shuleni kwao.
“Kwa nini Emmy anifanyie mimi mambo haya?Kwa nini anitese namna hii? Nikawaza.
“.Ni lazima nifanye utafiti nigundue ukweli uko wapi..halafu huyu mtu anayemuita special one…Ni nani? Lazima nimfahamu mtu huyu”
Mawazo yakawa mengi nikaona ni bora nikakae sebuleni .Nikaanza kutazama televisheni lakini hakuna kitu nilichokuwa nikielewa.Bado mawazo yangu yote yalikuwa katika suala zito linaloniumiza kichwa.Muda wa chakula ulipofika tukakaa mezani,tukala chakula huku nikijilazimisha kutabasamu na kucheka ili kumfanya emmy asihisi lolote.
“baraka kesho ni weekend,siku ya mapumziko,right? Nikamuuliza baraka mara tulipomaliza kula chakula cha usiku.
“Yes daddy ,kesho ni jumamosi’ Akajibu
“Ok pretty boy,now take you guitar.We’re going to play out in the moon and have fun”
Nilikuwa nimemfundisha Baraka kupiga gitaa.Naye kama mimi alikuwa mpenzi sana wa nyimbo za country.Kila mara tupatapo wasaa huwa tunakaa bustanini na kupiga magita yetu .
Tukaelekea bustanini,mimi ,Baraka emmy na mbwa wetu aitwaye Chesa.
“Daddy leo tunapiga wimbo gani? Baraka akauliza
“Leo tunaimba I believe in you wa Don Williams.This song is special for your mother ,the love of my life.I want to show your mother how much I do believe in her” Nikasema na kumfanya Emmy atabasamu lakini nikagundua tabasamu lake lilikuwa na uoga ndani yake.
“One,two,three….Tukaanza kupiga huku nikiimba.Nilikuwa mpigaji mzuri sana wa gitaa
“I don't believe in superstars,
Organic food and foreign cars.
I don't believe the price of gold;
The certainty of growing old.
That right is right and left is wrong,
That north and south can't get along.
That east is east and west is west.
And being first is always best.

But I believe in love.
I believe in babies.
I believe in Mom and Dad.
And I believe in you.

Well, I don't believe that heaven waits,
For only those who congregate.
I like to think of God as love:
He's down below, He's up above.
He's watching people everywhere.
He knows who does and doesn't care.
And I'm an ordinary man,
Sometimes I wonder who I am.

But I believe in love.
I believe in music.
I believe in magic.
And I believe in you.

I know with all my certainty,
What's going on with you and me,
Is a good thing.
It's true, I believe in you.

I believe in Mom and Dad.
And I believe in you…………………
“Honey its enough.This song is so touching.” Emmy akanikatisha nisiendelee kuimba.Nilikuwa ninaimba kwa hisia kali sana huku machozi yakinitoka.Nilipomtazama Emmy naye alikuwa akifuta machozi.Nadhani hata yeye wimbo ule ulimgusa.
Usiku ule ulikuwa ni moja kati ya usiku mrefu ambao sikuwahi kuupata katika maisha yangu.Sikuweza kupata usingizi.Kichwa changu kilikuwa kimejaa mawazo.Hostoria ya maumivu yaliyonipata miaka kadhaa ya nyuma yakanirudia tena.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO………………
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 5
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
I know with all my certainty,
What's going on with you and me,
Is a good thing.
It's true, I believe in you.

I believe in Mom and Dad.
And I believe in you…………………
“Honey its enough.This song is so touching.” Emmy akanikatisha nisiendelee kuimba.Nilikuwa ninaimba kwa hisia kali sana huku machozi yakinitoka.Nilipomtazama Emmy naye alikuwa akifuta machozi.Nadhani hata yeye wimbo ule ulimgusa.
Usiku ule ulikuwa ni moja kati ya usiku mrefu ambao sikuwahi kuupata katika maisha yangu.Sikuweza kupata usingizi.Kichwa changu kilikuwa kimejaa mawazo.Hostoria ya maumivu yaliyonipata miaka kadhaa ya nyuma yakanirudia tena.
ENDELEA………………………..
Siku iliyofuata ilikuwa jumamosi,niliamka asubuhi na mapema nikamuaga Emmy kuwa ninaenda ofisini kuna kazi nilitakiwa nikaifanye asubuhi hii na nisinge chelewa kurudi.Siku ya leo ni mapumziko hivyo ofisini nilikuwa mwenyewe.Nikaiwasha kompyuta yangu nikachomeka ile flash disk niliyokopi mawasiliano kati ya Emmy na my special one,mtu ambaye sikumjua ni nani.Nilianza kupitia tarehe moja baada ya nyingine,nikagundua kuwa mawasiliano yao yameanza muda mrefu.Kwa mujibu wa mawasiliano yao ilionesha kuwa walikuwa katika kipindi cha mapenzi mazito.Walikuwa wakiongea mambo mengi kuhusiana na raha na starehe wanazopeana.Nikagundua kuwa huwa wanakutana katika mahoteli makubwa makubwa na kupeana maraha.Kumbe mara zote Emmy akiniaga kuwa wana semina au makongamano huwa anakwenda kuponda raha na huyo special one.Yote haya niliyagundua katika meseji walizokuwa wakiandikiana.Iliniuma mno siwezi ficha.Nilitamani kutokuendelea kuzisoma meseji zile lakini ilinibidi nizisome zote ili kuupata ukweli wote.
Mpaka nilipomaliza kuzisoma chat history zote nikajikuta sina hata nguvu za kuinuka kweye kiti.Jasho lilikuwa likinitiririka.
“God where are you? Please help me” Nikasema kwa uchungu mwingi.

* * * *
Wiki iliyofuata ilikuwa ni wiki ngumu kwangu kupita maelezo.Nilijitahidi kutokuonesha dalili zozote zile kuwa kuna jambo lolote linanisumbua kichwani kwangu.Kila nilipomuona Baraka furaha yote ikapotea.Masikini malaika yule hakuwa na kosa lolote,hakuwa akifahamu kilichokuwa kikiendelea.Alifahamu fika kuwa baba yake mzazi ni mimi.Hata mimi bado niliendelea kuamini hivyo bado sikuwana na uhakika wa kutosha kwa yale niliyoyanasa kati ya mke wangu emmy na my special one ni ya kweli.Nilihitaji ushahidi wa kutosha..Jumanne jioni baada ya kazi nikaenda kuonana na rafiki yangu mmoja aitwaye beka anayefanya biashara ya kuuza magari.Nilimuomba anisindikize kwenda Same siku ya jumammosi tukitumia gari lake.Japokuwa alitaka kufahamu kwa undani juu ya safari hiyo lakini sikumpa jibu la moja kwa moja.Kutokana na ukaribu wetu akakubali kunisindikiza Same kwa kutumia gari lake.
Siku zikaenda kwa kasi na hatimaye ikafika siku ya Ijumaa.Usiku tukiwa kitandani Emmy huku akikichezea kifua changu bila kujua kama alikuwa akinikera kupita kiasi ,akasema
“darling ,kesho ndio ile safari niliyokwambia .Nasikitika kukuacha mwenyewe,utakuwa mpweke sana.”
Nikatabasamu na kusema
“Ni kwa nini usimuache baraka ?
“hapana honey .Unajua Baraka kuna wakati anakuwa msumbufu sana.Acha tu niende naye asije akabaki akakusumbua .”
“Hawezi kusumbua.Yupo dada yake wa kazi atakuwa akimlea.”Nikajibu.
“Siku hizi Baraka amekuwa mtundu sana.Honey acha niende naye.Siku mbili tu si nyingi .”
“Mtaondoka na usafiri gani? Nikauliza
“Mimi nitaondoka na gari yangu”
Akajibu Emmy huku usoni akionesha dalili za kutopendezwa na jinsi nilivyokuwa nikinga’ngania Baraka abaki.Nilikuwa nikielewa kila kitu hivyo haikunipa shida yoyote.
“Ok nadhani hat mimi kesho nitaondoka asubuhi na mapema kuna kazi ninawahi kwenda kuifanya “ Nikasema
“Ok baby” Akajibu Emmy akanibusu na kulala.Alipogeuka upande wa pili nikafuta mdomo wangu mahala aliponibusu kwa kiganja cha mkono.
Emmy hakujua kilichokuwa kikiendelea moyoni mwangu lakini ukweli nilikuwa namchukia kupita kiasi kwa mambo anayonifanyia.Pamoja na hayo niliendelea kujifanya mjinga ili niweze kupata ukweli wa mambo.Sikutaka kuyaendea haraka mambo haya mazito.
Asubuhi na mapema,nikaamka ,nikaoga na kuagana na Emmy.Nikapanda gari langu na kuelekea nyumbani kwa Beka maeneo ya Sakina.Nilimkuta tayari amejiandaa ananisubiri.
Hatukupoteza muda tukaingia katika gari lake na safari ikaanza.
“Beka najua bado unajiuliza maswali mengi toka nilipokwambia kuhusu safari hii.lakini ukweli ni kwamba kuna gari ambayo itabidi tuifuatilie inakwenda Same.” Nikasema
“Tunaifuatilia gari?”Beka akauliza
“yes..kuna gari tunakwenda kuisubiri Bomang’ombe na tutaifuatilia mpaka Same.”
Beka akakaa kimya akabadili gia na kulipita lori la mafuta halafu akanigeukia.
“Wayne whats going on? Toka nimekufahamu sijawahi hata siku moja kukuona ukiwa katika hali kama hii.Kuna kitu unanificha .Hebu kuwa muwazi kama kuna tatizo ili tusaidiane jinsi ya kulitatua. Wewe ni rafiki yangu na tatizo lako ni la kwangu”
Ni kweli Beka alikuwa mmoja kati ya marafii wangu amabao naweza kusemea ni wa kweli.Sikuona sababu ya kumficha tatizo langu Nikatabasamu na kujibu
“beka,kusema ukweli nina tatizo kubwa lakini siwezi kukueleza kwa sasa hadi hapo nitakapokuwa na uhakika wa kutosha.Kwa sasa naomba tu unisaidie kulifuatilia hilo gali nitakalokuonesha.”
Beka hakujibu kitu tena,akakubaliana nami.Akakanyaga mafuta hadi tulipofika eneo la Boma,tukasimamisha gari pembeni ya bara bara.
Mpaka saa nne za asubuhi bado Emmy alikuwa hajapita ,nikawa na wasi wasi pengine anaweza akawa amepanda gari jingine,nikaamua kumpigia simu.
“hallow Emmy,umeshaondoka?
“yes’ darling nimeondoka muda si mrefu,kwa sasa nelekea maeneo ya KIA”akasema Emmy.
“Unatumia usafiri gani,wa kwako au umepanda basi? Nikauliza ili kupata uhakika zaidi
“Ninatumia gari yangu”
“Ok honey Mimi ndio natoka kazini muda huu,msalimu baraka”
Nikakata simu huku beka akiniangalia kwa jicho kali.
“unaongea na mkeo?
“yah ! ni mke wangu” Nikajibu
“Tunamfuatilia mke wako?
Sikujibu kitu nikakaa kimya
“Wayne tell me please.Tunamfuatilia mke wako.?
“Yes Beka tunamfuatilia mke wangu.”
“ouh My God whats going on Wayne? Beka akauliza
“Nitakwambia Beka lakini sio sasa.Ni habari ndefu sana.”
Beka akajua lazima liko tatizo kati yangu na Emmy.akawa na subira akisubiri muda ukifika nimueleze mimi mwenyewe kwa mdomo wangu nini kinaendelea.Tuliendelea kusubiri huku tukiburudishwa na muziki ,mara nikaliona gari la mke wangu mama baraka likija.Nikamstua Beka aliyekuwa nje akiongea na simu.Akaingia garini tukaanza kulifuatilia gari lile.
Beka alilifuatilia gari lie kwa ustadi mkubwa ili tusije shukiwa kuwa tunawafuatilia.gari la Emmy likaongoza hadi katika hoteli moja mpya na ya kisasa sana ijulikanayo kama Uhuru white peak hotel.Hatukuweza kuingia mle ndani ya ile hoteli kubwa ya kifahari tukabana sehemu tukiwasubiri watoke.Baada ya kama saa moja hivi wakatoka na safari ya kuelekea Same ikaanza.Nadhani walikuwa wameenda kupata mlo wa mchana
Tulifika Same saa nane za mchana,.Pale hatukutaka kuendelea kulitumia gari letu hivyo ikatulazimu tulipaki mahala penye usalama tukakodisha gari aina ya Noah,tukaendelea kuifuatilia ile gari ya Emmy.Gari ya Emmy ikasimama nje ya nyumba moja kubwa yenye geti la kijani,na kupiga honi.Mara mlango ukafunguliwa na akashuka mwanaume mmoja ambaye sura yake haikuwa ngeni kwangu.Nikavua miwani myeusi niliyokuwa nimeivaa ili nimuangalie vizuri mtu yule .Sikutaka kuamini kuwa akili yangu ilikuwa sahihi.Sikutaka kuamini mtu niliyemuona toka ndani ya ile gari ni yeye kweli au wamefanana.Nilibaki mdomo wazi.
“No Its not true.Chris!!!! Nikasema kwa uchungu.
Ndugu msomaji aliyeshuka toka ndani ya ile gari ya Emmy alikuwa ni rafiki yangu wa siku nyingi aitwaye Chris ambaye alifanya kazi kubwa katika kufanikisha harusi yangu mimi na emmy.Ni mmoja kati ya watu ambao mchango wao kwangu sina uwezo wa kuulipa.Chris mtu ambaye nilimhesabu kama mmoja wa ndugu zangu kabla ya uhusiano wetu kuanza kupungua taratibu kiasi cha kuweza kumaliza hata mwaka mzima hatujaonana.
Nikiwa naendelea kushangaa nilichokiona,geti linafunguliwa na gari linaingia ndani..Nilikuwa nimelowa jasho mwili mzima.
“Tuondoke eneo hili Wayne” akasema Beka
Tuliondoka eneo lile na kurudi hadi mahala tulipoacha gari letu.Tukamlipa yule jamaa mwenye ile gari tuliyoitumia akaondoka zake
“Tunaelekea wapi baada ya hapa? Beka akauliza
Sikujibu kwa haraka.Nilitafakari nini kifuate baada ya hapo.Niendelee kumfuatilia Emmy au nirudi nyumbani? Nikajiuliza mwenyewe na mwishowe nikaamua kurudi nyumbani.
“Twende turudi nyumbani Beka.tayari nimeshaujua ukweli” Nikasema huku Beka akiniangalia na kisha akaondoa gari.
Safari yetu ilikuwa ya kimya kimya .Nilikuwa na mawazo mengi mno .Tulipofika maeneo ya kwa Sadala Beka akauvunja ukimya.
“Wayne najua si vizuri kuingilia mambo yasiyonihusu lakini wewe ni rafiki yangu na kama una jambo lolote linalokusumbua basi hata mimi linanihusu.Hebu niambie kuna tatizo gani?
Sikuona sababu yoyote ya kumficha Beka juu ya tatizo linalonikabili.Nikaamua kumweleza ukweli wote ulivyo.Beka akasimamisha gari pembeni ya bara bara baada ya kuusikia ukweli.Hata yeye alistuka sana.
“Wayne ni ya kweli hayo unayonieleza? Beka akauliza
“kwa nini nikudanganye Beka.Haya yote ni ya kweli kabisa.”Nikasema.Beka akavuta pumzi ndefu na kusema kwa sauti ndogo
“ I cant believe this.”
Akanyamaza kidogo halafu akasema
“Kwa jinsi ninavyomfahamu mke wako niliamini ni mmoja kati ya wanawake waadilifu mno katika ndoa zao.”
“hata mimi nilikuwa naamini hivyo na sikujua kama anaweza akanifanyia kitu kama hiki.Namsikitikia mtoto kwa sababu hajui lolote.Ninampenda mno Baraka.Niliamini yeye ndiye mrithi wangu na ndiye furaha ya maisha yangu.baada ya kugundua kuwa si mwanangu sijui hata nifanye nini.Ninampenda mno mtoto yule Beka” Nikasema kwa uchungu.
“Kwa hiyo umepanga kufanya kitu gani? Beka akauliza.Swali hili kwangu lilikuwa moja kati ya maswali magumu kujibu.Sikuwa nimepanga kufanya chochote na wala sikujua ningefanya nini.Kwa kitendo alichokifanya Emmy sikuona hata adhabu gani inayomstahili.
“Beka sijapanga bado nifanye kitu gani.bado nahitaji ushahidi wa kutosha ili niweze kujiridhisha na hatua nitakazozichukua..I think I need more time” Nikasema
“More time?….Beka akauliza kwa mshangao.
“More time? Akarudia tena.
“ Wayne naona kama unafanya utani na suala kama hili.Hili si suala dogo kama unavyolichukulia.Ni suala zito mno.Mkeo ameisaliti ndoa yenu na ushahidi wa uhakika unao.Umemfuatilia mkeo hadi Same na umegundua kuwa anaetembea na mkeo ni rafikiyo sasa ushahidi gani tena unaouhitaji? Hebu chukua hatua stahili mapema” Beka akasema kwa hasira.Beka alikuwa sahihi kwa upande Fulani lakini bado moyo wangu ulikuwa mzito kuchukua hatua za haraka.Beka alikuwa ameukunja uso kwa hasira.Kitendo kile ni wazi kilikuwa kimemuumiza mno.
“Beka uko sahihi kuwa ushahidi unajitosheleza kwa kiasi kikubwa.lakini bado nahitaji muda zaidi wa kufikiri nini cha kufanya.Sitaki suala hili limuumize baraka.Nataka suala hili niliendee taratibu” Nikasema
“Taratibu? Beka akauliza tena.
“Wayne sidhani kama suala hili linakuumiza.Naona unalifanyia mzaha.Taratibu wakati mkeo bado anaendelea kukudanganya ,bado anakuona hayawani,anatembea na rafiki zako halafu unasema unachukulia mambo taratibu..Be serious my friend” beka akasisitiza.
“nakuelewa Beka,lakini hizo hatua unazonisisitiza nichukue ni hatua zipi? Hebu nishauri” Nikasema
“Hakuna ushauri hapa.Fukuza tu aende kwa huyo hawara yake.” Beka akajibu kwa hasira kali.
Nilishindwa kukasirika ikanibidi nicheke .
“sasa unacheka nini Wayne? Wanawake wa namna hii dawa yao ni kuwatimulia mbali ili wakafunzwe na dunia.Sipendi watu wasiokuwa na hisani”
“Huo ndio ujinga wa wanawake.kwa jinsi ninavyofahamu ni kwamba Chris ana mchumba wake na tayari amezaa naye mtoto mmoja.Kwa sasa binti huyo yuko nje ya nchi kimasomo.Kwa maana hiyo ahadi kwamba atamuoa Emmy na kwenda kuishi naye nje ya nchi ni uongo mtupu.Chris akisafiri na kwenda nje ya nchi huwa anakwenda kumtazama mchumba wake na si vinginevyo.Iwapo nikimtimua Emmy hatakuwa na mahala pa kwenda kwa sababu ninamfahamu vizuri Chris.Hii ndiyo tabia yake kuwahadaa wanawake.Ninayemuonea huruma hapa ni Baraka.”
Beka bado hakuridhika na maelezo yangu
“Wayne mimi nakuonya ,mwanamke huyu si mzuri na hafai katu kuishi naye.Sikushauri uendelee kuishi naye.Mtimue haraka sana.”
“Beka najua unachokiongea lakini kumbuka Emmy bado ni mke wangu wa ndoa na kama tulivyoelezwa siku tunakula kiapo cha ndoa kuwa kilichofungwa duniani kimefungwa na mbinguni.Hilo ndilo tatizo kubwa linalonifanya nisite kuchukua maamuzi.Nitawezaje kutengua ndoa hii? “ Nikasema huku nikishika kichwa.
“Hivi Wayne huyu mwanamke amekupa kitu gani? Kuna dawa amekulisha wewe si bure.Haiwezekani ugundue mtu amekufanyia kitendo kama hiki halafu bado unamruhusu kulala ndani ya chumba chako.” Beka akasema kwa hasira
“hahahaha Beka achana na mambo ya dawa.Unajua mimi huwa sipendi kuchukua maamuzi ya haraka haraka.Hili ni jambo zito linahitaji utulivu na busara ya hali ya juu kulitatua.usiwe na wasi wasi rafiki yangu suala hili litakwisha.Suala kama hili ni lazima washirikishwe wazee,viongozi wa dini n.kTwende tuendelee na safari tutaongea zaidi tukifika.”
Beka akawasha gari tukaendelea na safari ya kurudi Arusha huku akionyesha dhahiri kuchukizwa na msimamo wangu.

TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………………
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 6
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Beka najua unachokiongea lakini kumbuka Emmy bado ni mke wangu wa ndoa na kama tulivyoelezwa siku tunakula kiapo cha ndoa kuwa kilichofungwa duniani kimefungwa na mbinguni.Hilo ndilo tatizo kubwa linalonifanya nisite kuchukua maamuzi.Nitawezaje kutengua ndoa hii? “ Nikasema huku nikishika kichwa.
“Hivi Wayne huyu mwanamke amekupa kitu gani? Kuna dawa amekulisha wewe si bure.Haiwezekani ugundue mtu amekufanyia kitendo kama hiki halafu bado unamruhusu kulala ndani ya chumba chako.” Beka akasema kwa hasira
“hahahaha Beka achana na mambo ya dawa.Unajua mimi huwa sipendi kuchukua maamuzi ya haraka haraka.Hili ni jambo zito linahitaji utulivu na busara ya hali ya juu kulitatua.usiwe na wasi wasi rafiki yangu suala hili litakwisha.Suala kama hili ni lazima washirikishwe wazee,viongozi wa dini n.kTwende tuendelee na safari tutaongea zaidi tukifika.”
Beka akawasha gari tukaendelea na safari ya kurudi Arusha huku akionyesha dhahiri kuchukizwa na msimamo wangu.

ENDELEA……………………
Jumapili jioni nikiwa nimepumzika bustanini nikitafakari Emmy akarudi.Baraka aliposikia niko bustanini akaja mbio akanikumbatia na kunisalimu.Emmy naye akaja bustanini haraka .Nilipomuona tu nikahisi hasira kali moyoni.Picha ya Chris ikanijia tena.Nikabadilika ghafla.Emmy akanibusu shavuni .Nilitamani nimkate shingo kwa hasira nilizokuwa nazo.Alionyesha mapenzi mazito kumbe ulikuwa ni unafiki mtupu.Huku akinipapasa kifuani akamwamuru Baraka aende ndani akapumzike .Nadhani hii ilikwa ni janja yake ili nisiweze kumuuliza Baraka kuhusu safari yao.
“Honey habari ya toka juzi? Akasema kwa sauti laini ya kimahaba.
“Nzuri .Pole kwa safari” Nikasema
“Safari nzuri.Jamani honey I missed you so much.” Akasema na kunibusu tena.
“Unajua kukaa mbali nawe hata kwa siku moja naumia sana.Nilipata wakati mgumu mno kwa kuwa mbali nawe.” Akasema huku moyoni akinizidishia hasira.
“Mwanamke shetani huyu..” Nikasema moyoni kwa hasira.
“baby are you ok? Akauliza baada ya kuniona nimekaa kimya
“yah I’m ok” Nikajibu kwa kifupi.Akainua kichwa na kunitazama usoni halafu akakilaza kifuani kwangu.Sikuwa na msisimko wowote kama alivytarajia.Laiti angejua kilichokuwa moyoni mwangu katu asingethubutu kunisogelea karibu.
Baada ya mlo wa usiku nikamuaga baraka na kumtaka aende akalale ili kesho asichelewe shule.Haikuwa kawaida yangu kuingia chumbani kulala mapema vile.Dakika chache baadae Emmy akanifuata.Akavaa nguo za kulalia na kuja kujilaza pembeni yangu.
“baba baraka una tatizo gani? Akauliza
Nilimtazama kwa makini usoni nikaona jinsi alivyokuwa na wasi wasi.
“Sina tatizo lolote “ Nikajibu
“hapana mume wangu .nakufahamu vizuri una tatizo.Kuna kitu kinakusumbua.Hebu nieleze mume wangu.haipendezi kama una kitu kinakuumiza halafu hutaki kukisema.Mimi ndiye mke wako sasa usiponiambia mimi utamwambia nani tena?
Nilitamani kucheka kwa jinsi alivyokuwa akijibalaguza pale kitandani.
“Ni kweli nina tatizo.” Nikasema.
“tatizo gani hilo mume wangu? Akauliza huku akinishika kichwa.
Nilikaa kimya kwa sekunde kadhaa nikatafakari kisha nikasema
“Jumamosi ijayo tunasafari ya kwenda dar es salaam.nataka tukafanye DNA test”
Emmy akastuka kama vile ameona jini.Akainuka kwa kasi na kukaa huku kijasho kikianza kumtoka usoni.Akaniangalia kwa macho makali.
“DNA test? Akauliza kwa ukali.
“Yes DNA test.Nataka nijue Baraka ni mwanangu au si mwanangu” Nikasema
“Unajua bado sijakuelewa baba Baraka.Unamaanisha nini unaposema unataka ujue Baraka ni mwanao au si mwanao?
“Kwani kuna tatizo gani la kutaka kuwa na uhakika wa mwanao? Nikauliza
“baba Baraka hivi umepatwa na kitu gani? Iweje ukampime mwanao wa kumzaa ? Ina maana umefikia mahala pa kutokuniamini hata mimi mkeo wa ndoa?
“si hivyo mama baraka.Ni katika kujiridhisha tu.Nakuamini sana mke wangu lakini kwa hili utanisamehe kwa sababu nahitaji kufahamu kama Baraka ni mwanangu au si mwanangu”
Emmy akakaa kimya.akainuka pale kitandani akasimama na kuanza kuzunguka mle chumbani.Ghafla akageuka huku uso wake umejaa machozi.
“Nasema hivi kama mimi ni mke wako wa ndoa hufanyi hiyo test.Hivi mimi nitakuwa mjinga kiasi gani nikudanganye kuwa Baraka ni mwanao wakati si mwanao?Nasema baraka ni mwanao na hiyo Test haifanyiki”
“na mimi nasema hivi ,kama mimi ni mumeo wa ndoa nitafanya hiyo Test.Lazima nijue Baraka ni mwanangu au si mwanangu”Nikasema kwa ukali.
“Kitu gani kinachokupa wasi wasi kuwa Baraka anaweza kuwa si mwanao? Emmy akauliza.
“Hakuna kitu chochote Emmy nimeamua tu nifanye hivyo ili niwe na uhakika”
Emmy akaanza kulia kwa kwikwi huku akilalama kuwa nimevuka mipaka kwa kumuona yeye ni msaliti wa ndoa yetu.Sikumjali nikavuta shuka nikajifunika na kulala.

* * * *

Ni wiki ambayo naweza kusema ilikuwa ni nyeusi ndani ya nyumba yangu.Maongezi na vile vicheko vilivyozoeleka vilikuwa nadra sana kusikika.Emmy hakutaka maongezi na mimi kwani muda mwingi alipotoka kazini alikuwa analala chumbani kwa kisingizio cha kazi nyingi.Sikuijali hali hiyo ,ila nilikuwa makini sana ili hali kama ile isije kumuathiri Baraka..Mtoto hakuwa na kosa na hakutakiwa kusulubishwa kwa makosa ya wazazi wake.Nilijitahidi kuwa naye karibu,kumsaidia kazi za shuleni zilizomshinda,na wakati mwingine tulikwenda bustanini kupiga magitaa yetu.Sikutaka aone kama kuna tofauti yoyote imetokea kati ya wazazi wake.Siku ya ijumaa usiku tukiwa mezani tunapata chakula nikakumbushai juu ya safari ya Dar es salaam kesho yake na kuuliza kama kila kitu kiko tayari..
“Kila kitu umekwisha kiweka tayari kwa safari” Nikauliza
Emmy hakujibu kitu akaniangalia kwa jicho kali .
“Hivi ni kweli umemaanisha kwenda kufanya hiyo DNA test au unanitania? Emmy akauliza
“mama baraka sikutanii.Kesho tunasafri kwenda Dar kwa ajili ya DNA.It’s a serious issue.”Nikasema
“Kama unakwenda nenda mwenyewe.Mimi wala mwanangu Baraka hatutakwenda” Emmy akasema kwa kiburi
“Mama Baraka ,mimi ndiye mwenye kauli ya mwisho katika nyumba hii na ndiye mwenye kuamua nini kifanyike na nini kisifanyike.Kwa maana hiyo basi nasema kuwa kesho alfajiri na mapema wote tunakwenda Dar es salaam.Hili halina kipingamizi na wala sihitaji mjadala tena” Nikasema kwa sauti iliyoashiria hasira ndani yake .Nilifahamu ni kwa nini Emmy hakutaka kwenda kufanya kipimo cha vinasaba.Nina uhakika mkubwa kuwa Baraka hakuwa mwanangu wa damu lakini nilikuwa nataka kuwa na ushahidi mkubwa zaidi wa kibaolojia.
“Kama mnakwenda nyie nendeni lakini mimi sintakwenda Dar es salaam.Mimi ndiye mwenye ukweli wote na hata kama ukienda kupima bado ukweli hautabadilika “Emmy akasema huku akiubetua mdomo wake kwa dharau akakiweka kijiko chini na kuondoka mezani kwa hasira.Niliumia sana moyoni kwa majibu yake ya kiburi namna ile lakini sikutaka kuonyesha mbele ya mtoto.

* * * *

Siku ya jumanne nilirejea toka jijini Dar es salaam nilikokuwa nimekwenda kwa ajili ya kufanya kipimo cha vinasaba ili kubaini kuwa Baraka ni mwanangu au si mwanangu.Emmy alikataa kata kata kuungana nasi kwenda Dar kwa ajli ya vipimo hivyo ikanuilazimu kwenda mimi na Baraka.Majibu niliyopewa yalinitoa machozi kwani yalionyesha dhahiri kuwa Baraka hakuwa mwanangu wa damu.Japokuwa nilikuwa naelewa kabla kuwa Baraka hakuwa mwanangu lakini sikuwa na uhakika sana hadi majibu haya yaliponidhihirishia wazi .Majibu haya yalinifanya nifikie hatua ya mwisho ya kuutafuta ukweli kama Baraka ni mwanangu au sivyo.Kila nilipomuangali mtoto yule niliyempenda kuliko kitu chochote kile roho iliniuma sana.Emmy alinifanyia unyama mkubwa sana.Ni bora Emmy angenieleza toka mapema nikafahamu kuwa yule si mwanangu.Ameuficha ukweli miaka hii yote na kwa sasa Baraka amekwisha kuwa mkubwa na ana akili za kutosha na hivyo kuambiwa ukweli kuwa mimi si baba yake ni kitendo ambacho kitamchanganya akili na kumuathiri kisaikolojia.
Saa moja za za jioni tukawasili Arusha na kuelekea moja kwa moja nyumbani.Nyumbani alikuwepo mtumishi wa ndani peke yake.Nikamuuliza alikoenda Emmy akasema kuwa siku tulipoondoka kwenda Dar es salaam na yeye akaondoka na hajarudi tena hadi leo hii na wala hakusema anaelekea wapi.Sikushangaa wala kuumia rohoni kwa kitendo kile kwa sababu kuendelea kumuona Emmy machoni pangu kungeniongezea hasira.Nikaingia chumbani na kukuta baadhi ya vitu vyake havipo.Nadhani alitambua kuwa kwenda kwangu Dar es salaam kungeweka ukweli wa mambo kuwa baraka hakuwa mwanangu na kwa maana hiyo akaamua kuondoka mapema kabla sijarudi ili kuepusha matatizo..
Nilikaa kitandani nikitafakari kwa kina juu ya maisha yangu na matatizo ambayo Emmy amenisababishia.Toka nimegundua uchafu alionifanyia Emmy nimekuwa nikijipa ujasiri mkubwa kuwa haya ni masuala madogo ambayo katu hayawezi kuniumiza kichwa lakini nikiwa pale kitandani kwa mara ya kwanza nikahisi kitu kama kisu kikali kikiupenya moyo wangu .Nilihisi maumivu makali ya moyo.pamoja na ujasiri wangu wote nilioahidi kuwa nao lakini nilishindwa kuyazuia machozi kunitoka.Hayakuwa maumivu ya kawaida.Ilikuwa ni zaidi ya maumivu..
Kesho yake nikadamka asubuhi na mapema na kujiandaa kumpeleka Baraka shule.Emmy hakurejea na wala sikusumbuka kumtafuta katika simu na kumuuliza yuko wapi ingawa nilipaswa kujua aliko akiwa kama mke wangu.Kwa hasira niliyokuwa nayo moyoni sikuwa tayari kumuona tena akitia mguu nyumbani kwangu.Macho yalikuwa yamevimba na mekundu kwa kukosa usingizi .Baraka alipokuwa tayari akaingia garini nikampeleka shule halafu nikaelekea ofisini.Japokuwa nilijitahidi kuuficha ukweli kuwa kuna jambo linanisumbua lakini wafanyakazi wenzangu walihisi sikuwa sawasawa.Nikiwa ofisini niliegemea kitini na kuanza kutafakari kwa kina juu ya maisha ya furaha niliyoishi na Emmy kumbe nyuma yake kumejaa usaliti na uchafu wa hali ya juu mno.Niliufikiria pia urafiki kati yangu na Christopher ulivyokuwa wa karibu.Tulikuwa ni marafiki tulioshibana sana na tuliishi kama ndugu.Ni Christopher ndiye aliyesaidia mpaka mimi na Emmy tukarudiana tena baada ya Emmy kunifanyia usaliti miaka ya nyuma kabla hatujaoana.Leo mke wangu wa ndoa anadiriki kuzaa na rafiki yangu wa karibu.Sikuwa tayari kuendelea kuteseka na kuumia moyo kwa ajili yao tena.Nikaamua kuliweka wazi suala hili.Nikachukua simu na kumpigia baba mkwe wangu yaani baba yake Emmy na kumuomba kama ana nafasi nionane naye jioni yeye pamoja na mama.Hakuwa na tatizo mzee yule ,halafu nikampigia tena simu rafiki yangu Beka na kumuomba aje nyumbani kwangu jioni kwa ajili ya maongezi mafupi , nikampigia pia simu mwalimu wa dini ambaye amekuwa karibu nasi na kutulea kiroho kwa muda mrefu.Niliwataarifu vile vile wasimamizi wetu wa ndoa kuwa wafike jioni hiyo kuna masuala muhimu ya kuongea.Nilihitaji na Emmy awepo katika kikao cha jioni hiyo wakati nikiusema ukweli mbele ya wazee na mashahidi lakini sikuwa na hamu hata ya kuongea naye simuni.Baada ya kufikiri mara kadhaa nikaamua kumpigia simu japokuwa moyo ulikuwa hautaki .
“Unasemaje wewe? Akauliza kwa ukali mara tu alipoipokea simu.Nilistushwa na ukali ule na kauli ile ya dharau kwani hakutaka hata kunisalimu.Nilisita kidogo kuongea kutokana na hasira zilizonipanda ghafla.Leo emmy amefikia hatua ya kuniita mimi “wewe”
“Sema unachokitaka kama husemi nitakata simu” Akasema tena kwa ukali baada ya kuona nimekaa kimya.
“nakuhitaji nyumbani jioni” Nikasema
“Nije kufanya nini? Hivyo vipimo ulivyoenda kufanya si vimeshakupa ukweli sasa unataka nije kwako kufanya nini tena?
“nataka uje tuongee”
“Tuongee nini tena? Hatuna cha kuongea wayne.tayari ukweli unaufahamu kwa hiyo sioni kama kuna kitu tunatakiwa kuongea mimi na wewe.Umeshatambua Baraka siyo mwanao kwa hiyo hata mimi si mkeo.Sifikirii tena kuishi na wewe .Nimechoka mimi maisha ya kubanwa banwa na kufugwa fugwa ndani kama njiwa.Nahitahi maisha ya uhuru,maisha ya kufanya nitakacho.Naomba uniache Wayne.Mimi sifai kuwa mkeo.Unahitaji mwanamke bora wa kuishi naye na si mimi.”
Nilivuta pumzi ndefu baada ya maneno yale mazito.Sikutegemea Emmy mwanamke niliyempenda na mbele ya mashahidi kanisani akala kiapo cha kuwa nami katika maisha yote mpaka kufa lakini leo ananitamkia maneno kama haya.Ni shetani gani amemwingia mwanamke huyu hadi akabadilika na kuwa namna hii?
“Emmy mimi sina ugomvi na wewe na hata kama ukitaka kuondoka kwangu mimi sikuzuii kwani ni uamuzi wako.Ninaujua ukweli wote.Ninafahamu Baraka si mwanangu wa damu.Ninafahamu Baba yake ni nani kwa hiyo ninachotaka tukae chini tuongelee suala la huyu mtoto .Tukilimaliza hilo mimi sina tatizo na wewe hata kidogo.You can do anything you want” Nikasema huku moyo ukiniuma kupita maelezo.
“Ok kama nitapata muda nitakuja.” Emmy akajibu kwa dharau na kukata simu.Nilihisi kama dunia inazunguka .sikuwa nimetegemea kama itatokea siku mimi na Emmy tungefikia mwisho wa namna hii.

* * * *

Saa kumi na moja za jioni Baba mkwe akiwa ameongozana na mkewe wakawasili nyumbani kwangu.Niliwakaribisha kwa furaha japokuwa nyuso zao zilikuwa na wasi wasi mwingi.Nadhani mwito ule wa dharura ulikuwa umewastua sana.Tayari Beka,mwalimu wangu wa dini na wasimamizi wetu wa ndoa walikuwa wamekwisha fika muda mrefu na waliokuwa wakisubiriwa ni wakwe.Zaidi ya Beka hakuna aliyekuwa akijua nini niliwaitia jioni ile,hali iliyowafanya wote wazidi kuwa na wasi wasi .Baada ya salamu na maongezi mafupi,nikafanya utambulisho kwa wageni wote halafu nikafungua kikao.
“Baba na mama mkwe,kwanza kabisa ninapenda kuchukua nafasi hii kuwaomba samahani kwa kuwasumbua jioni hii.Najua mna majukumu mengine mengi ya kufanya .Nashukuru sana kwa kuitikia mwito wangu na kufika hapa.Nawashukuru pia wengine wote mliofika,rafiki yangu Beka,mwalimu wangu wa dini, na wasimamizi wetu wa ndoa.”
Kabla sijaendelea mbele zaidi,baba mkwe akadakia.
“Samahani kwa kukukatisha Wayne.Mbona simuoni Emmy hapa?
Swali lile linanipa wakati mgumu kidogo kulijibu.Nikafikiri kwa sekunde chache na kusema
“ Emmy atakuja si muda mrefu.amepata dharura kidogo” Nikadanganya.Sikutaka kuharakisha mambo.Nilitaka kwanza niwape picha kamili ya mambo jinsi ilivyo.Nikawatazama wote na kila mmoja alikuwa na sura iliyoniashiria niendelee na maongezi.
“Nimewaiteni jioni hii ya leo kuna mambo muhimu ya kuongelea.Nadhani nyote mnafahamu kuwa ndani ya ndoa migongano,mikwaruzano huwa haikosekani.Kunapotokea mikwaruzano au migongano ndani ya ndoa na wanandoa mkashindwa kuisuluhisha basi hamna budi kuwashirkisha watu wa karibu kama wazazi na ndugu wengine wa karibu.Kwa ufupi ni kwamba ndani ya ndoa yetu kumetokea matatizo kidogo ambayo sisi kama wanandoa tumeshindwa kuyatatua ikanilazimu kuwaita na kuwashirikisha katika suala hili.”
Nikanyamaza na kuwaangalia wote mle ndani ,kila mmoja alikuwa na hamu ya kutaka kujua nini kimetokea.
“nafikiri nyote mnakumbuka kuwa kipindi kifupu kabla ya ndoa yangu na Emmy kulitokea mtafaruku ambao ulichangiwa na mwenzangu kutokuwa mwaminifu katika uchumba wetu.Sitaki kurudia kulielezea hilo kwa sababu lilikwisha pita na limesahaulika,ila nimelisema tu ili kuweka kumbukumbu sawa.Baada ya usuluhishi wa wazazi na ndugu tulilimaliza suala lile na ndoa ikafungwa.Tumeishi vizuri na mwenzanguu hadi tukabahatika kupata mtoto mmoja.Maisha yetu yamekuwa ni ya furaha kubwa siku zote.”
Nikanyamaza tena na kuvuta pumzi halafu nikaendelea
“Siku chache zilizopita,niligundua kuwa mwenzangu amekuwa si mwaminifu katika ndoa yetu.Labda kwa kuelezea tu ilimpate picha halisi ni nini ninakiongea ni kwamba kuna siku niliwahi kutoka kazini,sikuwa na kazi nyingi za kufanya hivyo ikanibidi kuwahi kazini na kuja kukaa na familia yangu .Nilipofika getini nikakutana na mke wangu akitoka nikamuuliza alikokuwa akielekea kasema kuwa wanampeleka jirani yetu hospitali.Nikaingia ndani na kuikuta kompyuta yake iko kitandani,nikaona ni bora niizime.Kabla sijaizima nikagundua kuwa kabla hajatoka alikuwa akiwasiliana na mtu .Kwa kuligundua hilo nikaona ni bora mtu huyo aliyekuwa akiwasiliaana naye nimjibu kuwa asubiri hadi baadae.Nilipatwa na udadisi wa kusoma zaidi baada ya kuona jina la mtu aliyekuwa akiwasiliana mke wangu limeandikwa my special one.Nikajiuliza huyu my special one ni nani? Hata kama ungekuwa ni wewe ni lazima ungepatwa na udadisi wa kutaka kujua huyo special one ni nani.kwa sababu mimi kama mume mke wangu ndiye mtu wangu muhimu,ndiye my special one.Kwa mantiki hiyo hata mke wangu mimi ndiye special one wake kwa sababu aliamua kuwaacha wanaume wote na kuolewa na mimi.Sasa nikastuka baada ya kujua kuwa mwenzangu ana special one mwingine ambaye si mimi.”
Nikatulia na kuwaangalia watu wote mle sebuleni.walikuwa kimya kabisa wakiniskiliza.mama yake Emmy alikuwa ameinama ameshika shavu .Nikaendelea.
“Baada ya uchunguzi nikagundua kwamba walikwisha anza kuwasiliana muda mrefu toka Emmy akiwa kazini,na aliporudi nyumbani wakaendelea tena kuwasiliana.Na hiyo haikuwa mara yao ya kwanza kuwasiliana.Baadae nikagundua kuwa kulikuwa na message za kimapenzi walizokuwa wakitumiana.Nikabaini kuwa Emmy ana uhusiano na mtu huyu wa kimapenzi kwa sababu kwa mujibu wa meseji wanazotumiana walikuwa wakikumbushana juu ya siku za nyuma wanazokutana katika mahoteli makubwa na kufanya mapenzi.Si mara moja Emmy huwa ananiaga kuwa anakwenda semina au katika makomngamano au kikazi nje ya mji kumbe huwa anautumia muda huo kukutana na huyo mtu wake muhimu.Ushahidi wa meseji zote hizo ninao toka walipoanza kuwasiliana.”
Mama mkwe akainama chini kwa aibu .Baba mkwe yeye akatoa kitambaa na kufuta jasho lililoanza kumtoka.Kila mmoja mle sebuleni sura yake ikabadilika.Sikutaka kumung’unya maneno,nikaendelea.
“Niliumia sana baada ya kuligundua hilo lakini nashindwa hata kuelezea maumivu niliyoyapata baada ya kugundua kuwa ……….” Kabla sijaendelea mbele mlango ukagongwa.Nikaomba samahani na kwenda kuangalia ni nani aliyekuwa akigonga.Alikuwa ni jirani yetu mama Mwantumu.Mama yule akaniambia kuwa Emmy alikuwa akihitaji kuonana na mimi nje ya nyumba.Amegoma kuinia ndani baada ya kuliona gari la baba yake liko mle ndani.Nikaingia ndani na kumwita mama mkwe nje.

TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………………….
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 7
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Baadae nikagundua kuwa kulikuwa na message za kimapenzi walizokuwa wakitumiana.Nikabaini kuwa Emmy ana uhusiano na mtu huyu wa kimapenzi kwa sababu kwa mujibu wa meseji wanazotumiana walikuwa wakikumbushana juu ya siku za nyuma wanazokutana katika mahoteli makubwa na kufanya mapenzi.Si mara moja Emmy huwa ananiaga kuwa anakwenda semina au katika makomngamano au kikazi nje ya mji kumbe huwa anautumia muda huo kukutana na huyo mtu wake muhimu.Ushahidi wa meseji zote hizo ninao toka walipoanza kuwasiliana.”
Mama mkwe akainama chini kwa aibu .Baba mkwe yeye akatoa kitambaa na kufuta jasho lililoanza kumtoka.Kila mmoja mle sebuleni sura yake ikabadilika.Sikutaka kumung’unya maneno,nikaendelea.
“Niliumia sana baada ya kuligundua hilo lakini nashindwa hata kuelezea maumivu niliyoyapata baada ya kugundua kuwa ……….” Kabla sijaendelea mbele mlango ukagongwa.Nikaomba samahani na kwenda kuangalia ni nani aliyekuwa akigonga.Alikuwa ni jirani yetu mama Mwantumu.Mama yule akaniambia kuwa Emmy alikuwa akihitaji kuonana na mimi nje ya nyumba.Amegoma kuinia ndani baada ya kuliona gari la baba yake liko mle ndani.Nikaingia ndani na kumwita mama mkwe nje.

ENDELEA…………………….
“Mama samahani,Emmy amekuja yuko nje lakini amegoma kuingia humu ndani baada ya kuliona gari la baba.Ninaomba ukamshawishi aingie ndani kwa sababu kama nikienda mimi hatakubali kuingia ndani” Mama mkwe akakubali na akaenda nje ya nyumba kuonana na Emmy.
“Wayne vipi,uko salama? Kuna tatizo lolote? Akauliza baba mkwe baada ya kuniona nimerudi ndani na kukaa kimya kimya
“Hapana mzee.Ni mambo ya kawaida ,mama anayashughulikia” Nikasema
Baada ya dakika tano hvi mlango unafunguliwa,mama mkwe akiwa ameongozana na Emmy wanaingia ndani.Emmy akiwa ni mwenye sura ya aibu akamsalimu baba yake na mwalimu wa dini halafu akakaa sofani huku amekiinamisha kichwa chake chini.hakutaka kumuangalia mtu yeyote usoni.
“Nadhani tunaweza kuendelea.” Nikasema na kuwatazama watu wote mle ndani.Baba mkwe alikuwa akimuangalia Emmy kwa jicho la hasira mpaka nikaogopa .
“Endelea Wayne” Akasema baba mkwe.
“Kabla hatujasimama nilikuwa nasema kwamba,niliumia sana baada ya kugundua kuwa mwenzangu alikuwa akitoka nje ya ndoa yetu.Mwenzangu hakuwa mwaminifu hata kidogo.Kikubwa zaidi ya yote ni kwamba niligundua kuwa mtoto Baraka hakuwa mwanangu wa damu.Alikuwa na baba yake……”
“Yarabi toba….” Mama mkwe akasema kwa sauti kubwa huku ameshika kichwa chake.baba mkwe akamshika mkono na kumtoa nje.Mama mkwe ana matatizo ya shinikizo la damu.Baba mkwe aliamua kumtoa nje baada ya kuona hali yake inanza kubadilika.
Baada ya dakika kadhaa,baba mkwe akarudi ndani.
“Tuendelee…mama yenu huwa ana matatizo ya shinikizo la damu na habari kama hizi huwa zinamstua sana ndiyo maana nimemtoa nje apumzike.”
“Mwanzoni sikuamini hata kidogo kuwa ni kweli Baraka anaweza kuwa si mwanangu.Kwa mujibu wa meseji nilizozipata ,walizokuwa wakitumiana Emmy na My special one ni kwamba kwa kuwa Baraka tayari amekwisha kuwa mkubwa, anapaswa kuanza kuwafahamu ndugu zake na kwa kuanzia walipanga waanze kumpeleka kwa babu zake huko Same.Ni kweli siku hiyo kama walivyokuwa wamepanga Emmy aliniomba ruhusa kuwa anamsindikiza rafikiye kwenye sherehe ya ndugu yake.Nilimfuatilia bila ya yeye kujua mpaka Same ndipo nilipogundua kuwa huyo mtu aliyemuita kama special one alikuwa ni rafiki yangu wa siku nyingi sana aitwaye Chris.Nilipolitambua hilo nikataka nipate uhakika zaidi nikamuomba emmy tuende tukapime DNA ili tuwe na uhakika mtoto ni wangu au si wangu.Emmy alikataa kata kata ikanilazimu kuondoka mimi na Baraka hadi Dar es salaam na kufanya kipimo hicho cha DNA na majibu ylidhihirisha kuwa ni kweli Baraka si mwanangu.Niliporudi toka dar es salaam nikiwa na majibu ya vipimo vya DNA Emmy tayari alikwisha ondoka nyumbani na nilipompigia simu ni kwa nini aliondoka nyumbani bila ruhusa yangu akaniambia kwamba kwa sasa sina nguvu yoyote ya kuweza kumzuia,na akaenda mbele zaidi kwa kunitaka nisiendelee kumfuatilia.Nilimuelewa lakini nikamuomba aje katika kikao hiki cha jioni ya leo kwa ajili ya kujadili kuhusu suala la mtoto.Kwa ufupi hayo ndiyo niliyowaitia jioni hii ya leo na imekuwa vyema mhusika mkuu naye amefika”
Nikamaliza na kuwatazama watu wote mle ndani.Kila mmoja alikuwa kimya .Ukimya mkuu ukatanda mle sebuleni halafu babamkwe akasema kwa hasira.
“Emmy ,japokuwa umechelewa ,lakini umeyasikia yote aliyoyaongea mwenzio.Je una lolote la kuongea?
Emmy hakujibu kitu akakaa kimya huku machozi yakimtoka
“nakuuliza tena Emmy una lolote la kuongea kutokana na haya aliyoyasema mwenzio? Naomba usikae kimya nijibu haraka” baba mkwe akasema kwa ukali
Emmy akiwa ameuficha uso wake kwa viganja vya mikono akasema
“Yote aliyoyasema ni kweli baba”
Baba mkwe akashika kichwa kwa mstuko.
.Alipatwa na mstuko wa ghafla.Kila mtu mle ndani alikuwa amepigwa na butwaa.baba mkwe akainama akatafakari kwa sekunde kadhaa halafu akainua kichwa na kusema
“Emmy naomba urudie tena,haya aliyoyatamka mwenzako ni mambo ya kweli?
Huku akifuta machozi akiwa ameinama chini akasema bila kusita
“Ni ya kweli baba”
Ghafla baba mkwe akainuka kwa kasi ya ajabu na kutaka kumvaa Emmy kwa kipigo,nashukuru mwalimu wa dini alikuwa karibu akawahi kumshika na kumketisha chini.
“Mtoto una laana wewe.Unawezaje kufanya upuuzi kama huu ? Baba mkwe akasema kwa hasira
“Mzee.Punguza hasira tuyaongee haya mambo kiutu uzima tuyamalize.Najua inauma kama mzazi lakini jitahidi kujizuia mzee wangu ili tuyamalize mambo haya magumu kwa amani”Mwalimu wa dini akasema taratibu akijaribu kumtuliza baba mkwe aliyekuwa amewaka kwa hasira.
“Mwalimu hebu niachieni nafasi nimshikishe adabu baradhuli huyu .Amenitia aibu kubwa .Tutaziweka wapi sura zetu sisi? ..Ouh My God…..” Akasema kwa hasira baba mkwe.
“Aibu hii si yako peke yako.Suala hili limetugusa sisi sote.Wote tunaumia mioyoni mwetu.lakini tunajitahidi kujizuia .Nakuomba mzee wangu tuliza hasira tuyaongee mambo haya na kuwasaidia hawa vijana.”
Baba mkwe akatulia lakini alikuwa akihema kwa hasira.Emmy uso ulikuwa umejaa machozi.Mambo haya mimi niliyaona kama ya kawaida kwa sababu nilikwisha yazoea tayari.Nilikwisha umia vya kutosha kwa hiyo sikuwa mgeni wa maumivu haya.Wote tulikuwa kimya tukisubiri kusikia baba mkwe atasema kitu gani.
“Emmy nataka uniambie.Ni kitu gani kimepelekea wewe ukafanya uchafu wa namna hii.Nataka uwe wazi ili tujue na tuone jinsi gani tunaweza kulimaliza suala hili”
Emmy alikuwa ameinama akilia.Hakuweza kuinua uso wake kwa aibu.Sebule yote ikawa kimya ikimsubiri yeye aweze kujibu swali aliloulizwa na baba yake.
“Emy nimekuuliza,na ninataka unijibu sasa hivi ni kitu gani kimepelekea wewe ukafanya uchafu wa namna hii ? Hii ni aibu kubwa kwetu kama familia,umetuumiza sana siwezi kukuficha na hasa mama yako ameumia mno.Umemuumiza mwenzako pia kiasi ambacho hakielezeki.Bado kuna mtoto Baraka ambaye ataumia kupita kiasi atakapoelezwa kuwa huyu si baba yake mzazi.Tafadhali usikae kimya hebu tueleze ni kwa nini ulifanya mambo kama haya? Baba mkwe akauliza tena huku hasira zikianza kumpanda. Emmy akafuta machozi kwa kitambaa chake halafu akainua sura yake na kusema kwa kwikwi.
“ baba …kusema ukweli..nilifanya hivi kwa sababu………’ Emmy akashindwa kuendelea akaanza kulia.
“Emmy naomba tafadhali usipoteze muda wetu hapa.hebu tueleze ni kitu gani kimekufanya wewe ukamfanyia mwenzako namna hii? Baba mkwe akasema kwa sauti kali
“baba ..niliamua kutoka nje ya ndoa kwa sababu sikuwa naridhika….Wayne haniridhishi”….
Kauli ile inanifanya nihisi kama vile moyo wangu unataka kupasuka kwa jinsi ulivyoyabadilisha mapigo yake na kuanza kwenda kasi.Katika maisha yangu sikuwa nimetegemea kama iko siku Emmy atakuja kutamka kitu kama kile.Nilijitahidi kwa kila niwezavyo kumridhisha kwa kila kitu alichokihitaji bila kujali gharama yake.na hata katika mapenzi ya kitandani nilikuwa mjuvi wa mambo na kila tulipofanya mapenzi siku zote hunisifia na kuniita kidume huku akiapa na kuwatukana wanaume wengine kuwa hawana hadhi ya kumgusa mtu kama yeye kutokana na raha ninazompatia.Sasa iweje tena leo mbele ya wazee atamke kuwa sikuwa namridhisha?Baada ya tafakari fupi nikagundua kuwa alisema vile kama utetezi wake.Uongo ule ukaniuma sana.baba mkwe akamtazama Emmy kwa hasira na kuuliza.
“Emmy unadai kuwa ulifanya uchafu huu kwa sababu mumeo hakuwa akikuridhisha,je kuna siku yoyote uliwahi kukaa naye na ukamueleza kuhusu suala hilo?
Emmy hakujibu kitu akakaa kimya.Nilijua alikuwa akiongopa ndiyo maana hakuwa na jibu.Alipoona Emmy amekaa kimya hana jibu baba mkwe akanigeukia mimi
“wayne hebu tuelze.Kua siku yoyote mkeo alikwisha wahi kukueleza kuwa humridhishi?
“Hapana baba hakuna hata siku moja aliyowahi kuneieleza kuwa haridhiki.Kinachonishangaza ni kwamba mara zote amekuwa akinisifia kuwa hajawahi ona mwanaume kama mimi ,kwa maana hiyo ni kwamaba alikuwa akiridhika saa iweje leo atamke kwamba hakuwa akiridhika? Zaidi ya yote hakuna kitu alichowahi kukitaka mke wangu akakosa hata cha gharama gani.Kuna siku nyingine akiwa nyumbani huwa ananipigia simu na kunieleza kuwa ananihitaji,kwa kumridhisha huwa natoroka kazini na kuja kukaa naye.Hebu muulizeni kama ninasema uongo”
“Emmy umemsikia mwenzio alivyosema.Ni kweli?
Emmy hakujibu kitu.Baba mkwe akawagekia wasimamizi wa ndoa yetu na kuwaliza.
“Au alikuwa kushitaki kwenu wasimamizi?
“hapana baba.Hakuna hata siku moja Emmy amewahi kuja kushitaki kwetu kuhusu jambo lolote lile linalohusiana na masuala ya ndani ya ndoa yao”
baba mkwe akatafakari kwa muda na kusema
“Inaonekana Emmy umeamua kutunga uongoHuna sababu yoyote ya msingi iliyopelekea wewe kuamua kutoka nje ya ndoa yako,na hata kufikia hatua ya kuzaa nje ya ndoa na kumdanganya mumeo.Mara ya kwanza mwenzio alikufuma na mwanaume akakusamehe na mkafunga ndoa.Niliamini kuwa ulijifunza na ukabadilika .Siku zote hizi umekuwa ukiishi kama mke mwema kumbe ni chui ndai ya ngozi ya kondoo.Inaonekana hii tabia ya umalaya imekwisha kuingia ndani ya damu yako na hautaweza kuiacha.Sasa nakuambia hivi kwa kosa hili ulilolifanya mimi sintakuwa na kusema .Nitamuachia wayne yeye ndiye atakaye amua afanye nini.” Baba mkwe akasema kwa ukali.mwalimu wa dini ambaye alikuwa amekaa kimya muda wote akakohoa kidogo na kusema.
“Jamani naomba na mimi niseme kidogo.Nakubali kuwa Emmy amefanya kosa kubwa sana.Amemkosea mwenzake na hata kuvunja ahadi ya ndoa aliyoiweka mbele ya altare ya bwana.Lakini kama Mungu anavyotuagiza kwamba tusiwe na mipaka katika kusamehe kama yeye anavyowasamehe hata wale wanaomkosea kupita kiasi.kwa maana hiyo kabla hatujaendelea mbele na kikao hiki ningeomba kwanza tujenge mazingira ya kusameheana.Ni kwa njia hiyo pekee tunaweza kuyamaliza mambo haya kwa amani.Halafu kitu kingine ni kwamba tunataka Emmy atueleze nani ni baba wa mtoto ili tuone ni vipi tutafanya kuhusu mtoto huyu.” Mwalimu wa dini akasema lakini kabla hajaendelea zaidi baba mkwe akadakia
“Mwalimu,nafahamu wewe ni mtu wa Mungu na siku zote kazi yenu ni kuhubiri upendo na kusameheana.Lakini nadhani wewe hujaguswa na jambo hili.maumivu ya kufanyiwa kitu kama hiki hayapimiki..Suala la kusameheana naona tumuachie Wayne yeye ndiye atakayeamua kama atamsamehe huyu mke wake au vipi.Tuendelee na kikao chetu.Emmy hebu tueleze huyu mtoto Baraka baba yake ni nani?
Kwa upande Fulani nilimuunga mkono baba mkwe kwa kauli yake.Kumsamehe Emmy ilihitaji moyo wa ajabu sana.haikuwa rahisi kusamehe .Emmy hakuwa tayari kusema nani alikuwa ni baba wa Baraka.ote tukakaa kimya tukimsubiri.
“Emmy tunakusubiri wewe ,hebu tueleze ni nani baba wa mtoto ?
Emmy hakuwa tayari kusema lolote kuhusiana na mtu aliyezaa naye.Kwa kuwa nilikuwa nikimfahamu ni nani baba wa Baraka nikaona ni bora niwe wazi.
“ Baba mkwe hawezi kutujibu huyu.Lakini tayari ninamfahamu baba wa mtoto.”
“unamfahamu baba wa mtoto? Baba mkwe akauliza kwa mshangao
“Ndiyo tayari ninamfahamu” Nikajibu
“Hebu tutajie ni nani huyo?
“Ni rafiki yangu Chris” Kimya kikatanda mle sebuleni.Kila mmoja hakuamini kama Emmy angeweza kuzaa na rafiki yangu.
“Yaani Emmy anadiriki kuzaa na rafiki yako? Baba mkwe akauliza.
“Si tu rafiki yangu,bal ni mtu aliyekuwa rafiki yangu wa karibu sana.Ni Chris ndiye aliyekuwa muandaaji mkuu wa harusi yangu na Emmy.Nilimwamini na kumuona kama ndugu.Sikujua kama iko siku anaweza akafanya kitu kama hiki alichokifanya.” Nikasema kwa uchungu.Ilikuwa inauma sana.
“mambo haya yanazidi kuwa magumu.Na huyo rafikiyako mmekwiha wasilia ana kwa siku za hivi karibuni? Aba mkwe akauliza
“Hapana baba.Ni kitambo kirefu sijawasiliana naye.Mawasilaiano baina yangu na yeye yalianza kufiifia na hatimaye kufa kabisa.Kwa sasa sina mawasilano naye yoyoite yale”
Baba mkwe akamgeukia Emmy
“Emmy ni kweli umezaa na rafiki wa Wayne?
Kwa sauti yenye kitetemeshi Emmy akajibu
“Ni kweli baba,nimezaa na Chris” jibu lile linampandisha baba mkwe hasira
“Mtoto una laana wewe.Unawezaje kuzaa na rafiki wa mumeo?
“baba Chris ninampenda .Sitaki kuendelea kuishi na Wayne.Nataka nikaishi na Chris tulee mtoto wetu.”
Chumba chote kikawa kimya kwa kauli ile ya Emmy.Kila mmoja alikuwa amepatwa na mshangao mkubwa .Kwa wale waliokuwa pale sebuleni ilikuwa ni kama wanaangalia mchezo wa kuigiza lakini ilikuwa kweli.
“baba wewe una mawazo gani ? Baba mkwe akanigeukia na kuniuliza.Watu wote mle sebuleni macho yao yakanielekea mimi ili kunisikia ninatoa wazo gani.Kila mmoja alikuwa akikwepa kutoa hukumu kwa kesi ile ngumu.Nililitambua hilo na nikaamua kuweka wazi yaliyokuwa moyoni mwangu
“baba nadhani nyote mmesikia kwa kauli yake kuwa hana haja ya kuishi tena na mimi.Hili amelitamka mbele yako wewe baba ambaye ni mzazi wake na mbele ya mashahidi ambao walishuhudia ndoa yetu.Mpaka hapa ilipofika mimi nina imani huyu mke wangu amekwisha nichoka na hana mpango na mimi tena.hata kama tukiamua kuyamaliza mambo haya kwa kusameheana na kuanza maisha mapya ni wazi ndani ya nyumba hakutakuwa na amani yoyote wala upendo tena.Mimi kwa moyo mweupe mbele yenu ninyi wazazi na mashahidi ninapenda kuweka wazi lililo moyoni mwangu.”
Nikatulia kidogo huku kila mmoja akisikiliza kwa makini sana ili kusikia nitaongea kitu gani
“Kama tulivyoapa siku ya ndoa yetu na padri akatamka kwamba kilichofungwa duniani kimefungwa pia mbinguni kwa maana hiyo ndoa yangu mimi na Emmy haitaweza kuvunjika hadi pale kifo kitakapotutenganisha.Pamoja na yote aliyonitendea lakini bado Emmy ni mke wangu na siku zote sintalisahau hilo.Pamoja na hayo lakini yeye kwa upande wake amelisahau hilo na kutamka wazi kwamba hajisikii tena kuwa na mimi mume wake wa ndoa na kwamba anahitaji kwenda kuishi na mwanaume mwingine ili walee mtoto wao.Natamka wazi kwamba yuko huru kwenda huko atakako kwenda.siwezi kumzuia kufanya atakavyo hata kama tunafungwa na ahadi ya ndoa.Kwa hiyo Emmy mimi nakuruhusu uende huko unakotaka kwenda,ukaishi kwa amani.Inaniuma sana lakini sina namna nyingine ya kufanya.Naamini mateso haya uliyonisababishia Mungu anayaona na iko siku atanipa faraja.Kwa hiyo mama uko huru kwenda unakotaka kwenda.Una ruhusa ya kuchukua chochote ukitakacho humu ndani.Mimi ya kwangu ni hayo tu” Nikasema na kuinama.Nilihisi maumivu makali ya moyo.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………………….
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 8
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Kama tulivyoapa siku ya ndoa yetu na padri akatamka kwamba kilichofungwa duniani kimefungwa pia mbinguni kwa maana hiyo ndoa yangu mimi na Emmy haitaweza kuvunjika hadi pale kifo kitakapotutenganisha.Pamoja na yote aliyonitendea lakini bado Emmy ni mke wangu na siku zote sintalisahau hilo.Pamoja na hayo lakini yeye kwa upande wake amelisahau hilo na kutamka wazi kwamba hajisikii tena kuwa na mimi mume wake wa ndoa na kwamba anahitaji kwenda kuishi na mwanaume mwingine ili walee mtoto wao.Natamka wazi kwamba yuko huru kwenda huko atakako kwenda.siwezi kumzuia kufanya atakavyo hata kama tunafungwa na ahadi ya ndoa.Kwa hiyo Emmy mimi nakuruhusu uende huko unakotaka kwenda,ukaishi kwa amani.Inaniuma sana lakini sina namna nyingine ya kufanya.Naamini mateso haya uliyonisababishia Mungu anayaona na iko siku atanipa faraja.Kwa hiyo mama uko huru kwenda unakotaka kwenda.Una ruhusa ya kuchukua chochote ukitakacho humu ndani.Mimi ya kwangu ni hayo tu” Nikasema na kuinama.Nilihisi maumivu makali ya moyo.

ENDELEA………………………..

Wote wakakaa kimya ni baba mkwe pekee aliyethubutu kufungua kinywa chake na kusema
“Wayne tumeyasikia mawazo na maamuzi yako.Wote tulikuwa tukisubiri kusikia kauli yako ya mwisho kwa sababu wewe ndiye mwenye mke na sisi ni washauri tu.Wayne najua ni maumivu kiasi gani uliyoyapata kwa kitendo hiki alichokufanyia mwenzio.najua umeumia kupita kiasi japokuwa ni wewe mwenyewe unayejua ni kiasi gani umeumia.Pamoja na hayo yote Wayne napenda nipendekeze jambo moja kwamba bado kuwe na fursa ya majadiliano na kusameheana.Sisi sote ni binadamu na sote tunakosea.Baba wa mbinguni anaagiza kwamba mara zote tuishi kwa kusameheana hata pale ambapo mioyo yetu inakuwa migumu kusamehe.Sijui wenzangu mnalionaje suala hili? Baba mkwe akauliza
Mwalimu wangu wa dini akasema kwa haraka
“Mzee hata mimi nakuuunga mkono kwa hilo.Japokuwa masuala haya bado ni magumu na yanaumiza moyo lakini bado tunapaswa kusameheana kwa kila jambo.Hata mimi napendekeza hivyo kwamba tupate fursa ya kulijadili suala hili kwa undani na kusameheana ili maisha yaendelee na mtoto asiweze kuathiriwa na haya yaliyotokea kwani yeye ndiye atakayekuwa muathirika mkubwa”
Mawazo yao yalikuwa mazuri lakini moyoni sikuwa hata na hamu ya kumuona tena Emmy.Nikainua kichwa na kusema kwa haraka.
“wazee wangu mna wazo zuri lakini naomba niweke wazi kwamba mimi nilikwisha msamehe Emmy siku nyingi.Najua aliteleza kitu ambacho kila binadamu kinaweza kumtokea.Pamoja na kufanya hayo yote aliyoyafanya , bado Emmy ndiye aliyekuwa wa kwanza kuondoka hapa nyumbani bila kufukuzwa.Kwa maana hiyo ni kwamba hata tukikesha usiku na mchana tunajadili tayari mwenzangu hana mpango wa kuwa na mimi tena.Angekuwa ni mtu mwenye busara na mwenye kulitambua kosa lake angeweza kuomba msamaha lakini mpaka leo hajafanya hivyo.Ninyi wenyewe mmekuwa mashuhuda wa majibu anayoyatoa hapa mbele yenu.Mzee tusipoteze muda yeye aende tu anakotaka kwenda.” Nikasema huku hasira tayari ikianza kunipanda.Baba mkwe akamgeukia Emmy
“Emmy umeyasikia aliyoyasema mwenzako? Baba mkwe akauliza .Emmy kwa sauti ndogo akajibu.
“baba mimi nimekwisha sema siwezi tena kuishi na Wayne.hakuna haja ya kupoteza wakati kwa usuluhishi.Yeye amekwishanipa ruhusa niende kwa hiyo hakuna kitu cha kuendelea kujadili hapa.hata mkisema nini mimi siwezi kurudiana na Wayne.” Emmy akasema kwa kiburi.
Baba mkwe akatafakari kwa sekunde chache halafu akasema
“sawa Emmy tumekusikia.Tumekuelewa unataka kitu gani.nenda unakotaka kwenda lakini ukumbuke kwamba hii ni dunia.mambo uliyomfanyia mwenzio leo na wewe yatakukuta kesho.Siku zote asiyefunzwa na mamaye atafunzwa na dunia.nakutakia kila la kheri huko uendako.” Baba mkwe akasema kwa hasira
Baada ya kama dakika moja hivi ya ukimya baba mkwe akasema.
“ Wayne vipi kuhusu mtoto Baraka.Kuna utaratibu gani kuhusu yeye?
“Baraka ana haki ya kumfahamu baba yake mzazi.Haitakuwa jambo la busara kama tutamficha ukweli mtoto.Ni jambo zuri ikiwa atafahamu mapema kwamba baba yake si mimi.Iwapo tutamficha na akaja kufahamu tayari akiwa amekuwa mkubwa sana itamuumiza mno.Mimi naona ni bora kama tutafanya utaratibu ili aweze kufahamishwa na kwa baba yake.Hata kama nikiendela kumlea lakini awe akifahamu kwamba mimi si baba yake mzazi.Bado nampenda sana Baraka.Na endapo wazazi wake watakubali wanaweza wakamuacha hapa mimi nikaendelea kumlea……”
Sikumaliza sentensi yangu emmy akajibu kwa haraka
“Siwezi kumuacha mtoto wangu hapa.Ninapoondoka hapa leo ninaondoka na mwangu.Siwezi kuruhusu mwanangu aje kulelewa na mwanamke mwingine.Mwanangu nitamlea mimi mwenyewe.”
Emmy alisema kwa ukali halafu akainuka na kuelekea chumbani kwa baraka.Kila mmoja alikuwa akishangaa
“Wayne hivi huyu mwenzio amepatwa na matatizo gani? Kwa sababu naona si yule Emmy niliyemlea mimi.Amebadilika ghafla” Baba mke akauliza
“baba hata mimi mwenyewe ninashangaa kwa mabadiliko haya .”
Wakati tukiendelea kujadiliana kule sebuleni nikasikia Baraka akipiga kele chumbani kwake.Nikainuka na kuelekea chumbani kwa Baraka
Emmy alikuwa akipakia nguo na vitu vya Baraka katika begi huku Baraka akilia kwa nguvu.
“Baraka kuna nini ? Nikauliza baada ya kumkuta Baraka akigalagala chini.
Aliponiona akakimbia na kunikumbatia.
“Daddy ,mama anasema eti leo tunahama mimi na yeye tunakuacha peke yako.Halafu anasema eti anataka kunipeleka kwa baba yangu” Nilimuonea huruma malaika yule asiye na kosa. Nikambembeleza akanyamaza kulia halafu nikamwambia.
“Baraka ni kweli mama yako anakupeleka ukamfahamu baba yako mzazi.Hatukukutaarifu toka mapema kwamba mimi si baba yako mzazi.Kwa hiyo B…….” kabla sijamalizia sentensi yangu baraka akachoropoka na kukimbia akajifungia bafuni akilia.
Nikamfuata na kukuta tayari amekwisha ufunga mlango kwa ndani.Alikuwa akilia kwa nguvu
“Baraka fungua mlango..Nikasema.
“Sifungui mlango hadi uniambie wewe ndiye baba yangu.”
Nikakosa jibu la kumpa.Roho ikaniuma sana kwa malaika yule kuteseka bila kosa.
“Fungua mlango Baraka” Nikasema tena .
“daddy sifungui mlango hadi uniambie wewe ndiye baba yangu.Mimi simtaki baba mwingine zaidi yako……….”
Nilichomwa na maneno yale ya Baraka nikasimama na kuuma meno kwa hasira
“Kwa nini Emmy unafanya hivi? Nikajisemea moyoni.
.Kwa jinsi nilivyokuwa ninampenda mtoto yule sikutazamia kama itakuja tokea siku ambayo ataumia kama hivi.Nilisimama pale mlangoni nikiwa na hasira huku Baraka akiendelea kulia mle ndani bafuni.
“Baraka fungua mlango ,nataka kuongea na wewe.Fungua mlango mwanangu” Nikaendelea kumbembeleza Baraka afungue mlango.Bado aliendelea kulia.
“Baraka mwanangu nyamaza kulia na ufungue mlango.” Nikasema tena
“baba sifungui hadi uniambie kwamba hautanipeleka huko mama anakotaka kunipeleka.Simtaki baba mwingine.wewe ndiye baba yangu” Baraka akasema.
Wakati nikiendelea kumbembeleza baraka afungue mlango wa bafuni baba mkwe akatokea.
“Wayne nini kinaendelea huku? Akauliza baba mkwe.
“Mzee,Baraka amekimbia na kujifungia huku bafuni.Hataki kwenda sehemu yoyote ile.Nimejaribu kumbembeleza afungue mlango lakini amekataa hadi nitakapomuhakikishia kwamba mimi ni baba yake”
baba mkwe akainama na kufikiri kwa sekunde kadhaa halafu akasema
“Emmy amesababisha mambo makubwa mno.Sikutegemea kama itakuja tokea siku Emmy atakuja fanya mambo kama haya.” Baba mkwe akanong’ona.
Kwa muda wa kama dakika moja tulikuwa tumesimama pale mlangoni huku Baraka akiendelea kulia mle bafuni.
“Kwa hiyo umeamua nini Wayne? Baba mkwe akauliza.
“Ni kama tulivyoamua pale sebuleni.Emmy ataondoka na Baraka na kwenda kumkabidhi mtoto kwa baba yake mzazi,halafu taratibu nyingine za kisheria na kikanisa zitafuata baadae.lakini kwanza baraka amfahamu baba yake”Nikasema
“Sawa Wayne mimi siwezi kupingana na uamuzi wako japokuwa Emmy ni mwanangu lakini kwa dharau aliyoionyesha leo kwetu sisi wazazi wake na kwako wewe mume wake wa ndoa sina budi kukubali uamuzi wako huo kwamba aende anakotaka kwenda lakini ni dunia ndiyo itakayomfundisha.Mpaka umefikia uamuzi huu nina imani atakuwa amekufanyia mambo mengi ambayo huwezi kuyaweka wazi.lakini pamoja na hayo nina wazo moja.”
“wazo gani baba?Nikauliza
“Nataka nimpeleke Emmy huko anakotaka kwenda.Nataka nikamkabidhi kwa huyo mume wake mpya ambaye yeye ametamka mbele yetu kwamba ndiye anayemfaa kuishi naye.Kwa sababu yeye ameamua kuachana na kiapo chake cha ndoa alichoapa mbele ya mwenyezi Mungu,nitampeleka kwa huyo mwanaume ambaye yeye anamuona ni wa muhimu kwake .Inaniuma sana kufanya hivyo kama mzazi ambaye nilipaswa kuhakikisha mambo haya yanakwisha na mnakuwa pamoja tena lakini hata kama tukijaribu kuyaweka sawa mambo haya ili muishi pamoja Emmy atakuumiza sana na anaweza hata kukutoa uhai wako.Wayne acha tu niende nikamkabidhi huko halafu nitanawa mikono.Huyo Chris ndiye atakayekuwa ni baba na mama yake.” Baba mkwe akasema
Nikakaa kimya kwa muda halafu nikasema
“Baba tutakwenda sote”
‘Hapana Wayne nadhani ingekuwa vizuri kama ungebaki hapa halafu mimi na huyu mzee wa kanisa tutampeleka Emmy huko anakotaka kwenda.”
“Nalijua hilo baba.Lakini ninaomba niongozane na ninyi .Hakuna chochite kitakachoharibika.Chris alikuwa rafiki yangu mkubwa sana.Sintamweleza chochote isipokuwa nataka aione sura yangu ili aendelee kuikumbuka katika maisha yake yote.”
“sawa wayne kama umesisitiza basi hakuna shida.Sasa tunafanyaje kuhusu huyu mtoto aliyejifungia humu bafuni? Muda unazidi kusonga.”Baba mkwe akauliza
“Nimekumbuka kuna ufunguo wa akiba.Ngoja nikauchukue “ Kwa haraka nikaelekea chumbani nikauchukua ufunguo wa akiba .Emmy bado alikuwa akikusanya nguo pamoja na vitu vyake vidogo vidogo.Sikusumbuka kumsemesha nikatoka chumbani na kurudi kule bafuni alikokuwa amejifungia Baraka.Nikachomeka ufunguo na kuufungua mlango.Baraka alikuwa amejikunyata katika pembe ya bafu akilia.Nilimuonea huruma sana mtoto yule lakini sikuwa na namna nyingine ya kufanya.
Nilimfuata pale chini alipokuwa amekaa nikapiga magoti na kumfuta machozi.
“baba naomba usinipeleke huko mahala mama anakotaka kunipeleka.” Baraka akasema
“Nyamaza kwanza kulia baraka” Nikambembeleza
“Baba mimi sitaki kuwa na baba mwingine.wewe ndiye baba yangu” Baraka akasisitiza
“Nalijua hilo Baraka ,lakini huko mama yako anakotaka muende ni muhimu sana.Ila usijali tutakwenda wote.Mimi pia ninakwenda.”
“na wewe unakwenda baba? Akauliza Baraka
“Ndiyo Baraka.hata mimi ninakwenda huko.Inuka basi twende ukajiandae”
Baraka akakubali ,akainuka nikamshika mkono na kumuongoza kwenda chumbani kwake.Nguo zake pamoja na vitu vyake vilikuwa tayari vimepakiwa katika masanduku .Niliumia sana moyoni .Sikutegemea kama ingetokea siku ningeachana na mtoto huyu niliyempenda kupita kitu chochote.Machozi yalikuwa yakinilenga lakini nikajikaza ili baraka asigundue chochote.Alipokuwa tayari nikamfuata mama yake kule chumbani.
“baraka yuko tayari.Vipi uko tayari? Nikamuuliza Emmy lakini hakunijibu kitu.
“kama kuna vitu vitabaki kesho nitamtuma dereva akuletee kila kitu unachohitaji” Nikasema
“Sihitaji kitu chochote toka kwako Wayne.Nilichokuwa nikihitaji nimeshakipata.Nilikuwa nahitaji kuondoka tu hapa ndani.na tafadhali wayne nakuomba nikitoa mguu ndani ya nyumba hii usiendelee kunifuata wala kunipigia simu.Forget if I exist.Na wala usimfuate fuate Chris.hana kosa lolote mimi ndiye niliyemchagua”
Emmy akasema huku amenikazia macho.Sikutaka kuendelea kubisha naye.Nikainua mabegi yake mawili nikaanza kuyatoa nje na kuyafungia katika gari lake.Mama yake aliyekuwa amekaa ndani ya gari baada ya kutolewa mle sebuleni kutokana na hali yake kuanza kubadilika alianza kulia aliponiona nikitoka na mabegi na kuyapakia katika gari la Emmy.nadhani alifahamu fika kwamba mambo yalikwisha haribika.
“wayne baba usijali Mungu atakulipia.Mambo aliyokufanyia huyu mwenzio ni mambo mabaya sana” Akasema mama mkwe.
“usijali mama hii ndiyo dunia na hii ni mitihani ambayo hatuna budi kuishinda.Nitakuwa salama mama usijali” Nikasema huku nikipiga hatua kurudi tena ndani.Nilijitahidi kutokuonesha hali yoyote ya huzuni japokuwa nilikuwa na maumivu makubwa ndani ya moyo.Nikachukua mabegi ya Baraka na kuyapakia pia ndani ya gari ya Emmy.
“baba naona kila kitu kiko tayari.nadhani tunaweza kuondoka sasa” Nikamwambia baba mkwe.
“Emmy tunakwenda wote hadi kwa huyo mume wako mpya.Tunataka tukakukabidhi huko” baba mkwe akamwambia Emmy aliyekuwa amesimama mlangoni akiwa na Baraka.
“baba mimi nakwenda peke yangu.Sitaki mtu yeyote anifuate” Emmy akasema na kumfanya baba mkwe akunje uso kwa hasira
“Emmy nakuonya kwa mara ya mwisho kwamba sintaendelea kuvumilia dharau zako kwetu.Umetudhalilisha kiasi ambacho wewe huwezi jua,lakini kama haitoshi bado unaendelea kutudharau.Nakwambia sintavumilia zaidi dharau zako.Kuanzia sasa nataka unisikilize mimi kama baba yako.Nakuonya usiendelee kunijaribu tena…” baba mkwe akasema kwa hasira huku akitoa kitambaa na kujifuta jasho.
“wayne kama hakuna tunachokisubiri tena ,funga nyumba twendeni “ baba mkwe akaamuru.tayari alikuwa amekasirika .Nilimsifu sana baba huyu kwa ustahimilivu wake mkubwa kwa dharau za mtoto wake wa kumzaa.Dharau za Emmy hazikuwa zikimithirika.Sikujua sababu ya mabadiliko yale ya tabia ya Emmy.
Nilifunga milango ya nyumba yangu huku roho ikiniuma kila nikimfikira baraka.Mimi na Beka pamoja na wale wasimamizi wetu wa ndoa tukaingia katika gari la Beka,halafu mzee wa kanisa akapanda gari moja na baba na mma mkwe ,Emmy akapanda gari lake akiwa na Baraka.Safari ikaanza ya kuelekea Njiro mahala anakoishi Chris.
Usiku huu hakukuwa na msongamano mkuwa wa magari katika barabara iendayo Njiro.Kwa wakazi wa Arusha wanaufahamu msongamano mkubwa wa magari uliopo siku hizi katika barabara za jiji hili linalokua kwa kasi. Haikutuchukua muda mrefu sana toka maeneo ya Majengo ninakoishi mimi hadi maeneo ya Njiro. Safari yetu ilikuwa ni ya kimya kimya.Kila mtu alikuwa akiwaza lake.Tulikuwa tukilifuata gari la Emmy ambaye ndiye aliyekuwa akituongoza njia.Hatimaye gari ya Emmy ikasimama nje nyumba moja yenye geti kubwa jeusi.Akafungua mlango na kushuka garini.Baba mkwe naye akashuka garini.Kuona hivyo na sisi ikatubidi tushuke.
“nadhani ni hapa” baba mkwe akasema.Nilipatazama mahala pale nikapatambua kwamba pale hapakuwa kwa Chris.
“Mzee hapa si nyumbani kwa Chris.Ninapafahamu nyumbani kwake.Emmy anataka kutuchezea mchezo” Nikasema.Ni wazi pale hapakuwa nyumbani kwa Chris.Haraka haraka baba mkwe akamwita Emmy ambaye alikuwa getini akisubiri geti lifunguliwe.
“Emmy nilikuonya toka mwanzo kwamba sintavumiia tena dharau na michezo yako ya kijinga.Hebu niambie hapa ndipo nyumbani kwa Chris?
Babamkwe akauliza.Emmy hakujibu kitu akabaki kimya.Tukiwa hatuna hili wala lile tulitahamaki baba mkwe akimchapa Emmy kofi kali la shavuni linalompeleka Emmy chini.Alitaka kumfuata tena pale pale chini ili aendelee kumuadhibu lakini kwa jitihada zangu na Beka tukafanikiwa kumtuliza.
“Haya ingia garini sasa hivi tunaelekea kwa Chris.Wayne ongoza njia kwenda kwa huyo mshenzi mwingine” baba mkwe akatamka kwa hasira.Emmy akasimama huku akilia akaingia garini na kuligeuza gari lake.Mimi nikatangulia mbele halafu gari la Emmy likafuatia na mwisho lilikuwa ni gari la baba mkwe.Dakika chache baadae tukawasili katika nyumba ya Chris.Gari zikasimama nikashuka na kumfuata baba mkwe.
“baba ,Chris anakaa hapa” Nikasema
“una uhakika Wayne? Baba mkwe akauliza
“Nina ukakika baba” Nikajibu.Baba mkwe akashuka na kumfuata Emmy ambaye alikuwa ameuinamia usukani akilia
“Hebu tuambie hapa ndipo nyumbani kwa Chris? Baba mkwe akauliza kwa ukali
“Ndiyo .Ni hapa” Akajibu huku akijifuta machozi.
“haya wapigie simu ndani watufungulie mlango”
Sekunde chache geti likafunguliwa tukaingiza magari ndani.Baada tu ya kushuka ndani ya Gari Baraka akaja na kuung’angania mkono wangu.hakutaka kuniachia.Emmy akatuongoza na kuelekea sebuleni.Mara tu tulipoingia sebuleni nilipatwa na kitu ambacho siwezi kukielezea kama ni hasira au ni nini baada ya kumuona aliyekuwa rafiki yangu mkubwa Chris akiwa amekaa sofani akiangalia luninga huku mezani kukiwa na chupa kubwa ya mvinyo. Mapigo ya moyo yalibadilika na kuanza kwenda kwa kasi ya ajabu.Nikahisi jasho likilowanisha shati langu jepesi.Kichwa kiliwaka moto kwa hasira.Chris aliponiona nimesimama alipatwa na mstuko mkubwa akainuka na kusimama huku akiwa na wasi wasi mwingi.Niliushuhudia uso wake ukivuja jasho jingi.
“Hallow…W..way.ne..” Akasema kwa sauti yenye kutetemeka.

TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………………
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 9
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“baba ,Chris anakaa hapa” Nikasema
“una uhakika Wayne? Baba mkwe akauliza
“Nina ukakika baba” Nikajibu.Baba mkwe akashuka na kumfuata Emmy ambaye alikuwa ameuinamia usukani akilia
“Hebu tuambie hapa ndipo nyumbani kwa Chris? Baba mkwe akauliza kwa ukali
“Ndiyo .Ni hapa” Akajibu huku akijifuta machozi.
“haya wapigie simu ndani watufungulie mlango”
Sekunde chache geti likafunguliwa tukaingiza magari ndani.Baada tu ya kushuka ndani ya Gari Baraka akaja na kuung’angania mkono wangu.hakutaka kuniachia.Emmy akatuongoza na kuelekea sebuleni.Mara tu tulipoingia sebuleni nilipatwa na kitu ambacho siwezi kukielezea kama ni hasira au ni nini baada ya kumuona aliyekuwa rafiki yangu mkubwa Chris akiwa amekaa sofani akiangalia luninga huku mezani kukiwa na chupa kubwa ya mvinyo. Mapigo ya moyo yalibadilika na kuanza kwenda kwa kasi ya ajabu.Nikahisi jasho likilowanisha shati langu jepesi.Kichwa kiliwaka moto kwa hasira.Chris aliponiona nimesimama alipatwa na mstuko mkubwa akainuka na kusimama huku akiwa na wasi wasi mwingi.Niliushuhudia uso wake ukivuja jasho jingi.
“Hallow…W..way.ne..” Akasema kwa sauti yenye kutetemeka.

ENDELEA………………………….

“Karibu….Kar…karibuni…” Akatamka Chris huku akionekana kuogopa kwa namna nilivyomuangalia.Skumjibu kitu nikaendelea kumtazama.Sikutazamia kama ningepatwa na hasira za namna ile baada ya kumuona mtu ambaye awali alikuwa ni rafiki yangu mkubwa .Beka alitambua kwa haraka jinsi nilivyopandwa na hasira akanishika mkono na kuniketisha sofani.
Hakuna mtu aliyeitikia salamu ya Chris.Wote tukaingia sebuleni na kukaa kimya kimya.Emmy alikuwa ameinama hakutaka kututazama usoni.
“jamani karibuni sana..Chris akasema huku akiwa bado amesimama na mwenye wasi wasi mwingi.
“Mnatumia vinywaji gani? Chris akasema huku akiliendea friji
“Kijana hebu tulia na ukae chini.Hatujaja hapa kutumia vinywaji”
Baba mkwe akasema kwa ukali.Chris akaenda kuketi sofani karibu na Emmy halafu akazima kabisa luninga ile iliyokuwa mle sebuleni kukawa kimya.Baraka akaja na kusimama pembeni yangu.nadhani kuna kitu alikuwa amekihisi.Hakutaka kukaa mbali nami.Akanishika mkono kwa nguvu.
“Habari za siku nyingi wayne? Chris akasema baada ya kuona sebule iko kimya huku akijilazimisha kutabasamu.Sikumjibu kitu bali nikaendelea kumtazama.Baba mkwe akakohoa kidogo halafu akasema
“Kijana ,wewe ndiye Chris? Baba mkwe akauliza
“Ndiye mimi mzee” Chris akajibu
“Vizuri. Nadhani kabla hatujaendelea ningetoa utambulisho mfupi.Mimi ni baba yake mzazi Emmy.Yule pale ni mama yake mzazi Emmy.Yule mzee pale ni Mzee wa kanisa na mwalimu wa dini wa Emmy na Wayne.Yule pale anaitwa ndugu…nani jina lako ndugu” baba mkwe akamuuliza Beka.
“naitwa beka”
“Exactly.Anaitwa ndugu Beka ni rafiki wa Emmy na Wayne .Wale pale nadhani unawajua ni wasimamizi wa ndoa ya Wayne na Emmy.Wa mwisho sina haja ya kumtambulisha kwa sababu unamfahamu fika kwa sababu ni rafiki.. I mean alikuwa rafiki yako.Kwa kukumbusha jina lake anaitwa Wayne ni mume wa ndoa wa Emmy ”
Baba mkwe akanyamaza kidogo halafu akaendelea.
“Chris nadhani mpaka hivi sasa umekwisha elewa ni kwa nini tuko hapa.Sina haja ya kutoa maelezo marefu sana kwa sababu hivi unavyotuona tumetoka katika kikao kizito na mambo mengi tayari tumekwisha yaongea huko.kwa ufupi ni kwamba tulipigiwa simu na wayne akatuomba tuonane jioni.Jioni ya leo kama alivyokuwa ametuomba tumeitika wito tukakusanyika bila kufahamu ni jambo gani alilokuwa akituitia.Baadae alitueleza jambo alilotuitia ,jambo ambalo kwa mtu mwenye moyo mwepesi unaweza ukaanguka na kufariki mara tu ukihadithiwa.Ni jambo lenye kuumiza na kusikitisha sana.Kwa mujibu wa maelezo ya wayne ni kwamba wewe na mkewe Emmy mna mahusiano ya kimapenzi.Wewe uliwahi kuwa rafiki mkubwa wa wayne na hata kulipotokea matatizo kati ya wayne na Emmy mara ya kwanza ni wewe ndiye uliyekuwa mstari wa mbele katika kutafuta suluhu.Baada ya Emmy na wayne kuelewana ni wewe ndiye uliyekuwa kiongozi wa jopo lililofanikisha sherehe za harusi yao.Sielewi ni shetani gani alikuingia hadi ukaamua kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mke wa rafiki yako.si tu rafiki yako bali rafiki yako mkubwa na wa karibu.Hilo lilikuwa dogo,kubwa zaidi ikabainika kwamba katika mahusiano hayo baina yako na Emmy mlipata mtoto ambaye Wayne alijua ni wa kwake kumbe mtoto huyu ni wako wewe .Hili ni jambo baya sana na halivumiliki.Umemtendea vibaya sana rafiki yako na vile vile umemtendea vibaya sana mwanao Baraka.Nadhani akiwa mkubwa na kuufahamu ukweli kiundani atakuchukia katika maisha yake yote kwa kitendo ulichokifanya.Baada ya kuligundua hilo Wayne alimtaka Emmy wakafanye kipimo cha DNA ili kubaini kama ni kweli Baraka ni mwanae au si mwanae.kwa ujeuri kabisa Emmy alikataa kata kata.Wayne alifunga safari hadi dar es salaam na kufanya kipimo hicho ambapo ilidhihirika kwamba ni kweli Baraka hakuwa mwanae wa damu.Hebu pata picha ni maumivu kiasi gani aliyoyapata mwenzio baada ya kugundua kwamba mtoto aliyemlea na kumpenda na kumthamini kuliko kitu chochote kumbe si mwanae wa damu.Namshukuru sana wayne kwa sababu ni kijana mwenye roho ya ujasiri sana ambaye siku zote anaongozwa na mwenyezi Mungu kutokufanya maamuzi mabaya.Kama si kwa maongozi ya mwenyezi Mungu hivi sasa tungekuwa tukiongea mambo mengine kabisa.Lakini kama hiyo haitoshi bado Emmy aliamua kuondoka nyumbani na kuja kuishi kwako kwa kiburi bila ruhusa ya mumewe.Linaumiza sana jambo hili.Wayne alivumilia mwishowe akaona hataweza kuvumilia suala hili zaidi ya hapa lilipofikia hivyo akatuita na kuamua kuliweka wazi suala hili ikiwa ni pamoja na maamuzi yake.Katika kikao tulichokaa,mbele ya wazazi wake,mume wake,mzee wa kanisa pamoja na mashahidi wao wa ndoa emmy alitamka kwa ulimi wake kwamba hataki tena kuishi na Wayne na kwamba wewe Chris ndiye mwanaume wa maisha yake.Anataka aishi na wewe ili mumlee mtoto wenu Baraka.Kama mzazi nilipaswa kuhakikisha kwamba watoto hawa wanamaliza tofauti zao na kuendelea kuishi kwa amani na kujenga familia iliyo bora.Sikuweza kulifanya hilo kwa sababu Emmy kwa kiburi kabisa alisema kwamba hana haja na masuluhisho ya namna yoyote ile.yeye anachohitaji ni kupewa nafasi ya kuishi na wewe.Niliyatazama macho yake na nikabaini kwamba hakuwa hata na chembe ya mapenzi kwa Wayne tena kwa hiyo hata kama tungewasuluhisha ingekuwa ni kumuongezea matatizo wayne.”
Baba mkwe akanyamaza kidogo akatutazama wote halafu akasema
“bwana Chris,nimekuja hapa mimi kama baba wa Emmy nikiwa na mama yake Emmy na mashahidi wao Nataka mbele yao utamke wazi kwamba ni kweli Baraka ni mtoto ambaye umezaa na emmy halafu masuala mengine yafuate.”
Baba mkwe akasema huku amemkazia macho Chris. ambaye alikuwa ameinama asijue afanye nini.Jasho lilikuwa likimtiririka.Nilikumbuka jinsi urafiki wetu ulivyokuwa mkubwa na wala sikutegemea kama ingetokea siku angenifanyia kitu kama hiki.Ni wazi ulimi ulikuwa mzito kutamka lolote.
“Chris tunakusubiri wewe.hebu ongea haraka bado tuna mambo mengi ya kuongea”
Usoni kwa Chris kulikuwa na michirizi ya machozi ambayo sikujua kama alikuwa akilia kwa kulijutia kosa lake au yalikuwa ni machozi ya uongo.
“baba..na mama naombeni mnisamehe..Nimek…..” Alisema Chris lakini kabla hajaendelea mbele zaidi baba mkwe akadakia
“Chris usipoteze wakati wetu.Ninachotaka kusikia ni kauli yako kwamba ni kweli umezaa na Emmy.Just short and clear” baba mkwe akasema kwa ukali
“baba ni kweli,nimezaa na Emmy” Chris akasema huku akitazama chini kwa aibu.
Kwa fundo nililokuwa nalo moyoni nilitamani niichukue chupa ile ya mvinyo iliyokuwa mezani nimtwange nayo kichwani.Nilianza kujilaumu kwa kuamua kuja huku kwa sababu kuja kwangu huku kumeyaamsha upya mateso na maumivu yote aliyonisababishia Emmy.Awali nilijipa moyo kwamba maumivu yale ni ya kupita na tayari nimekwisha yazoea lakini kumbe nilikuwa najidanganya.maumivu yale hayakuwa yakizoeleka wala kuvumilika.
“Nadhani nyote mmmesikia kwa kauli yake kwamba ni kweli amezaa na emmy mtoto ambaye ni huyu Baraka.” Baba mkwe akasema halafu akanyamaza na kumkazia macho Emmy halafu akamtazama Baraka aliyekuwa amesimama pembeni yangu amenishika mkono.Hakutaka kuuachia mkono wangu.
“Chris ,baada ya kukiri wewe mwenyewe kwa ulimi wako kwamba Baraka ni mwanao ,kitu cha kwanza tunachokifanya hapa usiku huu ni kukukabidhi mtoto wako baraka ili umtunze na kumlea kama baba yake mzazi .Baadae taratibu za kisheria na kidini zitafuata ili tuone ni jinsi gani tunaweza kulibadilisha jina la mtoto ili liweze kuendana na jina la baba yake mzazi.Tungeweza kumzuia mtoto huyu abaki kwa Wayne na asikutambue wewe kama baba yake,lakini kwa kufanya hivyo tungekuwa bado hatumtendei haki mtoto mdogo kama huyu ambaye ana haki ya kumfahamu baba yake mzazi.Kwa hiyo kuanzia usiku huu utakuwa na mwanao Baraka na utamtunza na kumlea kwa jinsi unavyoona inafaa kama baba yake.Tunasikitika sana kwa sababu mateso anayoyapata mtoto huyu kwa hivi sasa ni makubwa .”baba mkwe akasema
Baraka ambaye alikuwa amesimama pembeni yangu amenishika mkono kwa nguvu akawa akitokwa na machozi na kuniambia kwa sauti ndogo
“Baba mimi sitaki kubaki hapa.Tunaondoka wote” Sebule nzima ikawa kimya wote wakimtazama Baraka na kumuonea huruma malaika yule anayeteseka bila sababu.Iliniuma sana kumpoteza mtoto kama yule niliyekuwa nikimpenda kupita maelezo.Sikuwa na jinsi zaidi ya kumuachia aende kwa baba yake mzazi.Nilihisi kama vile nilikuwa naadhibiwa kwa kosa ambalo silijui kwa maumivu yaliyokuwa ndani ya moyo.
“baraka baba njoo hapa.” Baba mkwe akamwita Baraka
“Babu mi sitaki.mi sibaki hapa nitarudi kwetu na baba” Baraka akasema huku akilia.
Baba mkwe akasimama,akamshika mkono Baraka na kwenda kukaa naye sofani.
“Baraka najua bado u mtoto mdogo lakini tayari una akili ya utambuzi.Nadhani mpaka sasa hivi unamfahamu baba yako ,si ndiyo? Baba mkwe akauliza na baraka akaitika kwa kichwa
“Good boy.baba yako anaitwa nani” Baba mkwe akauliza tena huku akitabasamu
“baba yangu anaitwa wayne” baraka akajibu
“Vizuri sana . Sasa Baraka kuna kitu kimoja ambacho tunataka ukifahamu Ni kwamba Wayne si baba yako mzazi.baba yako mzazi ni yule pale anaitwa Chris.Kwa hiyo kuanzia leo wewe utaishi hapa kwa baba yako mzazi pamoja na mama yako.Umesikia Baraka? Baba mkwe akasema na kumfanya Baraka akaangue kilio.Ikanibidi nimchukue na kumbembeleza.
“Sikia baraka utabaki hapa kwa baba,mama yako pia atabaki hapa.Nitakuwa nakuja kukuangalia na kukuletea zawadi kila jumamosi.”
“baba mimi sitaki kubaki hapa” Baraka akapiga kelele
“baraka utabaki na mama yako”
“Mimi simpendi mama.nakupenda wewe baba” Baraka akasema huku akilia na kuwaacha watu wote midomo wazi.
Nilishindwa kuyazuia machozi kunitoka kwa kauli ile ya Baraka.Ni wazi aliufahamu ukatili wa mama yake .
“baba ,itakuwa ngumu sana kwa baraka kubaki hapa.naombeni mniruhusu nirudi naye nikaendelee kuishi naye ili hata kama ni kumkabidhi kwa baba yake basi tumfanyie maandalizi ya kutosha ya kisaikolojia lakini si hivi tunavyotaka kufanya.Tunamuumiza mtoto bure.” Nikasema
Emmy akainuka pale sofani na kuja kumchukua Baraka kwa nguvu
“Nimeshasema mtoto wangu haendi popote.Hapa ni kwa baba yake na ataishi hapa atake asitake.” Emmy akanyanyua Baraka na kuondoka naye huku mtoto akipiga kelele nyingi.
Baada ya muda akarejea bila baraka.nadhani alikuwa amekwenda kumfungia chumbani.
Baba mkwe akaendelea baada ya Emmy kuirejea.
“ Bwana Chris baada ya zoezi la kwanza kukamilika kitu kingine kinachofuata ni kukukabidhi rasmi Emmy”
Chris akastuka sana kwa kauli ile ya baba mkwe akataka kuongea jambo baba mkwe akamuonyeshea ishara anyamaze.
“kaa kimya kabisa na sitaki unijibu chochote.Huna nafasi ya kunijibu lolote.” Baba mkwe akasema kwa ukali.
“Chris naomba usistuke kwa sababu Emmy kwa mdomo wake ametamka kwamba hataki kuendelea kuishi na Wayne na anataka kuja kuishi na wewe ili mumlee mtoto wenu baraka.Tokea mwanzo ulifahamu fika kwamba Emmy ni mke wa mtu tena mke wa rafiki yako wa karibu lakini ukadiriki kuwa na uhusiano naye na hatimaye mkazaa mtoto.Nina imani ulikwisha jiandaa kwa lolote litakalotokea.Ulikuwa ufahamu nini kitatokea baada ya mambo yote haya kuwekwa bayana.Niwazi ulitegemea ndoa ya Wayne na Emmy kuvunjika na wewe kupata nafasi ya kuwa na Emmy.Imetokea kama ulivyokuwa umekusudia.Ndoa kati ya Emmy na wayne naweza sema kwamba haipo tena.Sababu kubwa ya kutokuwepo kwa ndoa hii kati ya Wayne na Emmy ni wewe.Kwa hiyo Bwana Chris nimekuja hapa mimi pamoja na hawa wote unaowaona ili nikukabidhi rasmi Emmy.Kuanzia sasa chochote kitakachomtokea Emmy kitakuwa ni jukumu lako.Mimi kama baba mzazi wa Emmy pamoja na mama yake wote kwa pamoja tumekwisha nawa mikono,hatutahusika tena na jambo lolote linalomuhusu .Kwa sasa wewe ndiye utakuwa baba na mama yake.Kitendo mlichokifanya si kitendo cha kibinadamu na hakistahili kuvumilika.Tokea sasa Emmy yuko mikononi mwako.Mlee na kumtunza jinsi unavyotaka wewe Mimi nimemaliza.” Akasema Baba mkwe na taratibu nikauona uso wa Chris ulivyokuwa umelowa jasho.Hakuwa ametegemea mambo haya kufika hapa yalipokuwa yamefika.Nilimsikitikia sana Emmy kwa ujinga aliokuwa ameufanya kwa sababu Chris ninamfahamu fika kwamba hakuwa na lengo lolote naye.Chris tabia yake ndiyo hiyo ya kuchezea wanawake na kisha kuwatelekeza.Siwezi elezea uchungu unaonipata kila nikimuwaza mtoto Baraka.Ni wazi alikuwa katika wakati mgumu mno licha ya umri wake kuwa mdogo.
“Jamani kuna mtu ana jambo la kuongeza? Baba mkwe akauliza baada ya ukimya mkubwa kutanda mle ndani.Macho ya watu wote mle ndani yakanigeukia mimi .Wote walijua labda nilihitaji kusema machache.Nilikuwa na mengi ya kuongea lakini kila nilipojaribu kutaka kusema neno kuna kitu kilikuwa kimenikaba koo kiasi cha kushindwa kutamka neno.Fundo la hasira lilikuwa limenikaa.Niliutumia mkono wangu kuwafanyia ishara kwamba sina lolote la kuongea.
“Nadhani hakuna yeyote mwenye jambo la kuongea.Tunaweza kuondoka” Baba mkwe akaamuru.Wakati tukiinuka kwa ajili ya kuondoka Chris akasimama na kusema jambo
“Baba samahani naomba mkae kidogo .Hata mimi nina mambo ya kuongea.Mbona hamjanipa nafasi ya kuongea? Hivi mnavyonifanyia si vizuri.Haiwezekani mje mnimwagie mtu hapa ndani katika mfumo huu.Tafadhalini jamani naomba na mimi nisikilizwe japokuwa nimekosea..” Chris akasema huku akiwa ameifumbata mikono yake kifuani kwake na sauti yake ilikuwa ni yenye kukwama kwama.
“Tumekumwagia mtu? Baba mkwe akauliza kwa ukali
“Unadiriki kusema tumekumwagia mtu? Kweli kijana huna haya.Baada ya mambo yote haya uliyoyafanya bado unadiriki kusema kwamba una kitu cha kuongea? Huna nafasi wala kitu chochote cha kuongea baradhuli wewe.Ulitegemea nini baada ya kuivuruga ndoa ya rafikiyo? Ulichokuwa umekitegemea ndicho hicho umekipata.Emmy sasa ni mke wako halali.Na kwako Emmy,kwa kuwa umemkana mumeo wa ndoa mbele yetu na kutamka kwa ulimi wako kwamba hutaki kuishi naye tena,na sisi hatutaki kukuona tena nyumbani kwetu.na hatukutambua kama mwanetu.Lolote litakalokupata kuanzia sasa ,baba na mama yako ni huyu mwenzio ambaye leo hii amekuwa ni mtu wa maana sana kwako.Usitutambue kwa lolote lile.Na ninakwambia wazi wazi kwamba kitendo ulichomfanyia mwenzio na wewe kitakurudia.Utafanywa kama ulivyomfanyia mwenzio”. baba mkwe akafoka
“lakini baba…..” Chris akataka kusema jambo lakini kabla hajaendelea akazuiwa na Emmy.
“Chris usiseme chochote.kwa kuwa wamekwisha nikataa kuwa mimi si mtoto wao sasa ya nini uendelee kuwabembeleza? Achana nao Chris.Let them go.”
Nilimtazama Emmy kwa hasira.Alikuwa akiongea kwa kiburi sana.Sikutegemea kama ni kweli Emmy niliyemfahamu leo hii anadiriki kutamka maneno yale kwa kiburi kikubwa na tena mbele ya wazazi wake.Baba mkwe hakutaka kuongea tena neno lolote akatuongoza tukatoka nje.Nilimuona Chris akiwa amesimama pale sebuleni akiwa haamini kilichokuwa kimetokea.
“Wayne baba, nenda nyumbani kapumzike.Tutaongea zaidi kesho.Ninachokuomba usiwaze sana kuhusu haya yaliyotokea.Hii ni mitihani ya dunia na huna budi kuishinda.Ninachokusihi jitahidi sana kuomba Mungu ili aweze kukupa nguvu ya kuweza kuyashinda majaribu haya.Muda si mrefu mambo haya yatakwisha na utasahau kabisa” baba mkwe akaniambia huku akinipiga piga mgongioni wakati tukijiandaa kuingia katika magari yetu .Sikujibu kitu nilikuwa nimeinama chini nikitafakari..Sikutegemea kama mwisho wangu na Emmy ungekuwa namna hii.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………………
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 10
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Chris usiseme chochote.kwa kuwa wamekwisha nikataa kuwa mimi si mtoto wao sasa ya nini uendelee kuwabembeleza? Achana nao Chris.Let them go.”
Nilimtazama Emmy kwa hasira.Alikuwa akiongea kwa kiburi sana.Sikutegemea kama ni kweli Emmy niliyemfahamu leo hii anadiriki kutamka maneno yale kwa kiburi kikubwa na tena mbele ya wazazi wake.Baba mkwe hakutaka kuongea tena neno lolote akatuongoza tukatoka nje.Nilimuona Chris akiwa amesimama pale sebuleni akiwa haamini kilichokuwa kimetokea.
“Wayne baba, nenda nyumbani kapumzike.Tutaongea zaidi kesho.Ninachokuomba usiwaze sana kuhusu haya yaliyotokea.Hii ni mitihani ya dunia na huna budi kuishinda.Ninachokusihi jitahidi sana kuomba Mungu ili aweze kukupa nguvu ya kuweza kuyashinda majaribu haya.Muda si mrefu mambo haya yatakwisha na utasahau kabisa” baba mkwe akaniambia huku akinipiga piga mgongioni wakati tukijiandaa kuingia katika magari yetu .Sikujibu kitu nilikuwa nimeinama chini nikitafakari..Sikutegemea kama mwisho wangu na Emmy ungekuwa namna hii.

ENDELEA……………………..

“Wayne anayosema baba yako mkwe ni ya kweli kabisa.Jipe moyo na Mungu atakusaidia.Jitahidi sana kudumu katika maombi na Mungu atakusikia.Inawezekana Mungu ana mpango mwingine na wewe.Mimi binafsi nitakuombea sana kila siku ili upate nguvu uweze kuendelea na maisha yako.Ila kesho nitaonana na baba Paroko na kumweleza kuhusu suala hili ili tuone ni kitu gani anaweza akafanya kwa sababu kwa mahali ndoa yako ilipofikia ni pagumu sana.” Mwalimu wangu wa kanisa naye akasema machache.Niliwashukuru sana wazee wale kwa nasaha zao na kwa jinsi walivyoniunga mkono ,tukaingia magarini na kuondoka zetu.
“Beka sikutegemea kama mwisho wangu na Emmy ungekuwa namna hii.mwanamke niliyempenda na kumthamini leo amenifanyia kitendo kama hiki du ! sikutegemea kabisa.Nilikuwa mjinga sana kwa kumuamini Emmy kupita kiasi .Alinitenda mara ya kwanza nikamsamehe na kurudiana naye tena.Nilifanya kosa kubwa sana kuamua kurudiana naye baada ya kosa lile la kwanza.Nimepoteza muda mwingi katika kulihudumia penzi lisilokuwa na matunda yoyote zaidi ya maumivu kila kukicha.” Nilisema kwa hisia kali wakati tukiendelea na safari ya kurudi nyumbani.Nilikuwa na uchungu mwingi.
“Wayne najua ni jinsi gani ulivyoumizwa na suala hili.Hata mimi ninapata wakati mgumu sana kuamini kama ni kweli yametokea haya.Ni kweli kama mambo haya ameyafanya Emmy ninayemfahamu mimi.kama nisingeshuhudia mwenyewe kwa macho yangu nisingeamini katu kama Emmy angeweza kufanya mambo kama yale.Kitu cha msingi ni kukubali kilichotokea.Jipe moyo na maisha yaendelee.Jipange na uanze maisha mapya.Msahau kabisa Emmy katika maisha yako.Bado hujachelewa Wayne katika kuyapanga upya maisha yako.Jipange vizuri na mwisho wa siku utasahau kila kitu kuhusu Emmy” beka akasema.
“Beka hakuna mtu anayeweza kuyaongelea au kupima maumivu niliyoyapata kwa kitendo hiki cha Emmy.Amenisababishia majeraha makubwa moyoni ambayo si rahisi kufutika mapema.Itanichukua muda mrefu sana kumsahau Emmy na mambo yote aliyonitendea.Kinachoniuma zaidi ni ukatili alioufanya kwa mtoto Baraka.Inaniwia vigumu kuamini kwamba mtoto yule si mwanangu.Bado ninampenda kupita maelezo na sijui hata nifanye kitu gani ili niweze kuyaondoa maumivu haya makali kuhusiana na mtoto huyu .” Nikasema huku Beka akikanyaga mafuta na kuongeza mwendo wa gari
“Huwezi kumsahau kwa haraka namna hiyo Wayne.Nakushauri uchukue likizo ndefu na uende mbali na hapa ukae huko kwa muda .Utakapokuwa mbali na mazingira haya utajifunza ni jinsi gani ya kuanza maisha mapya.Nadhani hii itakuwa njia bora sana ya kuweza japo kwa asilimia chache kukusahaulisha na mkasa huu wa kuumiza.” Beka akasema.Ushauri wa Beka ulikuwa mzuri nikauona unafaa
“nakubaliana nawe Beka.Hilo ni wazo zuri.Itanibidi nilifanyie kazi mapema iwezekanavyo.I need to go far away from here.I need to forget everything.” Nikasema.Wazo lile la Beka lilikuwa ni wazo zuri ambalo hata mimi nilikuwa bado sijalifikiria.Ni kweli ,ningezidi kuumia sana kama ningeendelea kukaa ndani ya nyumba ambayuo kila siku kumbu kumbu ya Emmy na baraka zingekuwa zinanijia.
Beka alinipeleka nyumbani akaniacha pale na yeye kuondoka.Nikaingia ndani na kukaa sebuleni.Ukutani kulikuwa na picha kubwa niliyopiga na Emmy siku ya harusi yetu.Niliiangalia picha ile kwa umakini mkubwa .Emmy alikuwa amejaa tabasamu zito,alikuwa amependeza sana.Ni kipindi ambacho tulikuwa katika mapenzi makubwa.Tulikuwa katika mahaba mazito sana.Ni katika kipindi hicho nilikuwa ni mmoja kati ya wanaume wenye furaha kubwa duniani.Sikutaka tena kuendelea kuiangali a picha ile,nikaitoa na kuiweka chini,nikaanza kukusanya vitu vyote ambavyo vitanisababisha nimfikirie Emmy .Nilikusanya kila kitu chenye uhusiano na Emmy kuanzia picha hadi vyombo nikavifunga pamoja katika boksi kubwa na kwenda kuvihifadhi stoo.Saa nane za usiku nikapanda kitandani na kulala.

* * * *

Niliamka saa nne za asubuhi.Kichwa kilikuwa kizito sana.Nyumba yote ilikuwa kimya kabisa.Nilizoea kuamka asubuhi na kuikuta nyumba ikiwa imechangamka kwa muziki ,maongezi na vicheko lakini leo hii hali ilikuwa tofauti kabisa.Hakukuwa na sauti yoyote iliyokuwa inasikika.Mtu pekee niliyeamini angekuwapo ndani muda ule ni mtumshi wa ndani .Kwa kuwa nilikuwa nimedhamiria kuchukua likizo ndefu na kuondoka kabisa Arusha niliamua kumpa likizo binti yule wa ndani akapumzike hadi hapo nitakapomuhitaji tena.Nilijizoa zoa pale kitandani nikaenda nje na kumkuta Sharifa akifua nguo.
“Shikamoo kaka” akanisalimu kwa adabu.
“marahaba Sharifa hujambo?
“Sijambo kaka” akajibu msichana yule mwenye adabu nyingi.Msichana yule aliyekuwa akitokea mkoani Singida nimeishi naye kwa muda mrefu na ninamchukulia kama mmoja kati ya ndugu zangu.
“Sharifa kuna jambo ninataka kuongea na wewe” Nikamwambia na kumfanya astuke na kuacha kazi aliyokuwa akiifanya.
“Sharifa nadhani unafahamu kila kitu kilichotokea hapa nyumbani.Hali hapa nyumbani si shwari.Dada yako ameondoka na kwa sasa niko mwenyewe hapa nyumbani.Kutokana na mambo yaliyotokea hata mimi nimeamua kuchukua likizo na kusafiri ,kwa maana hiyo nimeona nikupe likizo uende nyumbani ukapumzike kwa muda halafu nitakaporudi nitakuita tena..Kwa hiyo leo ungejiandaa na kesho uanze safari” Nilimpatia kiasi cha shilingi laki tatu kwa ajili ya maandalizi ya kwenda nyumbani kwao.Ingawa hakuwa na pingamizi lakini niliamini moyoni hakuwa amependezwa na suala lile la kumtaka arudi nyumbani kwa muda hadi hapo nitakapomuita tena.Sikulijali hilo .Baada ya kuoga nikapata kifungua kinywa halafu nikarudi tena chumbani kwangu kulala.Sikuwa na hamu ya kwenda mahala popote.Niliutumia muda huo kutafakari mustakabali mzima wa maisha yangu yaliyopita na yajayo.Nilijaribu kuitumia nafasi hiyo katika kuyapanga maisha yangu yajayo bila ya kuwa na Emmy na Baraka.
Saa kumi za jioni niliamua kutoka na kwenda sehemu tulivu kwa ajili ya kupata upepo na kupunguza mawazo.Sikutaka kwenda sehemu zenye mkusanyiko mkubwa wa watu.Nilihitaji kwenda mahala ambako ni tulivu ,nitakapopata wasaa wa japo muda mfupi kuyasahau maisha yangu ya nyuma.Arusha tulivu garden ni moja kati yua sehemu tulivu sana kama lilivyo jina lake.Ni sehemu ambayo imekuwa inapendwa sana na wageni toka nchi mabalimbali.nafikiri mahala hapa panapendwa kutokana na utulivu wake na mandhari ya kuvutia mno.Ninaifahamu sehemu hii na ndiyo maana nikachagua kuja huku kwa sababu ni sehemu pekee niliyoamini ingeweza kunisaidia kunisahaulisha na dhahama iliyonikumba japo kwa masaa machache
Niliwasili katika geti la sehemu hii tulivu na kuingia ndani.Nilikuwa nikitabasamu kwa mandhari safi na tulivu ya mahala hapa.Ndani ya bustani hii tulivu kulikuwa na sura nyingi za wageni ambao kama nilivyosema wanapapenda sana mahala hapa.Niliegesha gari na kushuka nikatafuta mahala nikaketi.Ukimya ulikuwa umetawala sehemu hii.Ni milio ya ndege na muziki laini wa ala ndivyo vilivyokuwa vikisikika.Hakika nilipafurahia mno mahala hapa.Muhudumu aliyevalia nadhifu,suti safi nyeusi na tai nyekundu akafika na kwa adabu akanikaribisha na kuniuliza kile ambacho ningependa kutumia.Nilimuomba aniletee wine safi aina ya Lion hills.Mkononi nilikuwa na kitabu cha hadithi tamu ya kusisimua nilichokinunua majuma kadhaa yaliyopita,kitabu kilichoandikwa na mmoja kati ya waandishi wa riwaya ninaopenda kusoma riwaya zao kiitwacho “Before I die” Kwa siku hii niliamua kutumia muda huu niliouapata kwa ajili ya kuisoma hadithi hii tamu na ya kusisimua.Nilikuwa nikisoma huku nikiendelea kupiga mafunda kadhaa ya wine ile nzuri.Nilijisikia furaha sana kwa muda ule niliokuwa pale.
“habari yako kaka” Nilistuliwa na sauti tamu na nzuri ya mwanamke.Kwa kuwa nilikuwa nimezama katika simulizi nzito ya kitabu hiki cha “before I die” nilionesha kama kustushwa kidogo na sauti ile.Nikainua kichwa na kukutana na sura ya mwanamke mmoja mrembo sana aliyekuwa amesuka nwele zake katika mtindo wa rasta zilizokuwa zimemkaa vyema.Alikuwa mwembamba wa wastani na mwenye sura nzuri .
“Nzuri dada habari yako” Nikasema huku nikimtazama mwanadada yule .
“habari yangu nzuri. Naruhusiwa kukaa? Akauliza dada yule mwenye sauti tamu .
“Hakuna shida unaweza kukaa” Nikasema na dada yule akavuta kiti na kuketi.Mara moja muhudumu akafika dada yule akamuomba amletee kinywaji chake alichokiacha katika meza aliyokuwa amekaa.
“Sahamani kaka kama nimekusumbua ,nilikuwa nimekaa kule peke yangu lakini nikaona ninazidi kuboreka.Nimekuona muda mrefu uko hapa mwenyewe nikaona nisogee hapa walau nione kama ninaweza kupata mtu wa kuongea naye mawili matatu.Sahamani kama nimekukwaza.” Akatamka dada yule na kunifanya nitabasamu kutokana na adabu na ustaarabu wake
“Bila samahani dada yangu.Mimi mwenyewe nilikuja hapa kwa ajili ya kupumzika na kupoteza mawazo lakini kwa kuwa sikuwa na mtu yeyote wa kuweza kubadilishana naye mawazo nikaamua kujisomea kitabu changu hiki cha hadithi ilimradi siku iende” Nikasema huku nikikifunika kitabu changu nilichokuwa nakisoma na kukiweka mezani.
“Wow ! “before I die” ! Nimesikia kwamba kitabu hiki kimetoka.Nilikuwa nakitafuta sana.Napenda sana riwaya za huyu kaka.mara nyingi nisomapo riwaya zake huwa nahisi msisimko wa ajabu sana” Akasema dada yule.
“Kumbe hata wewe ni mpenzi wa mtunzi huyu? Nikauliza huku nikitabasamu.
“Mimi ni shabiki wake mkubwa.Kinachonifurahisha ni kwamba amekuwa akiandika simulizi tamu ambazo mara nyingi ni vitu vinavyotokea katika jamii yetu.Kuna kitabu aliwahi kukitoa kinaitwa Malaika wa Valentine,kwa kweli kitabu kile kila ninapokisoma huwa ninatoa machozi kwa sababu hadithi ile inanigusa mno kwani mambo yaliyomo katika kitabu kile yaliwahi kunitokea hata mimi.Tokea wakati huo siachi kusoma hadithi yake hata moja.” Akasema mwanadada yule ambaye tayari muhudumu alikwisha mletea kinywaji chake alichokuwa anakitumia.Nilipotazama alikuwa akitumia Miami 24 whisky.Nilistuka kidogo kwa sababu kutokana na umbo lake na jinsi alivyo sikutegemea kama angeweza kutumia kinywaji kikali kama kile.Nilipatwa na shauku ya kutaka kumfahamu zaidi yule dada.Akamimina mvinyo kidogo katika glasi halafu akanywa yote akainua kichwa na kunitazama.
“Nimefurahi sana kumpata shabiki mwingine wa simulizi za Patrick.” Nikasema huku nikitabasamu.
“Hata mimi ninafurahi sana kila ninapokutana na mtu ambaye anapenda kusoma hadithi za watunzi mbali mbali.Itabidi tufanye mpango wa kuanzisha klabu ya wasomaji wa riwaya ,wewe mwenyekiti mimi katibu ,au unasemaje? Akauliza na kufanya wote tuangue kicheko kikubwa.Hiki kilikuwa ni kicheko changu cha kwanza toka nimekumbwa na masahibu ya Emmy.
“Hiloni wazo zuri sana.Tunaweza tukaanzisah kitu cha namna hiyo ambacho kinaweza kusaidia sana kuamsha ari ya usomaji vitabu hapa nchini.Katibu wewe unaitwa nani? Nikauliza na kumfanya dada yule acheke kicheko kikubwa kinachosababisha na mimi nicheke.Akatoa kitambaa katika pochi yake ndogo na kujifuta machozi yaliyotokana na kucheka.
“naitwa Clara.na wewe mwenyekiti wangu unaitwa nani? Akauliza
“Mimi naitwa wayne”
“Ouh Jina zuri sana wayne.Nafurahi mno kukufahamu.” Akasema Clara huku akitabasamu.
“Wayne wewe ni mkaazi wa hapa Arusha? Akauliza.
“Haswaa.Mimi nimkaazi wa hapa hapa Arusha.Ninaishi maeneo ya Majengo.wewe unaishi wapi?
“Kwa sasa mimi makazi yangu ni Pretoria afrika kusini japokuwa wazazi wangu wanaishi Dar es salaam.Hapa Arusha nimekuja kwa siku chache kwa ajili ya kutoa mada katika semina ya mitindo na mavazi inayoendelea katika hoteli ya Naura spring.Siku ya leo nimeamua kuja hapa kwa ajili kupata hewa safi na kutuliza kichwa.” Clara akasema.
“Ouh kumbe unajishughulisha na masuala ya mitindo na mavazi? Nikauliza
“ ndiyo .Ninajishughulisha na mambo ya ubunifu na mitindo kwa ujumla.” Akajibu.
“Nilipokuona nilijua ni lazima ungekuwa mwanamitindo” Nikasema na kumfanya atabasamu.
“Unaionaje fani ya mitindo na mavazi hapa Tanzania ukilinganisha na afrika ya kusini? Nikauliza. Clara akamimina mvinyo katika glasi akanywa halafu akasema.
“Kwa hapa Tanzania fani hii ya mitindo bado iko chini japokuwa kuna wanamitindo wazuri na wabunifu wazuri.Wenzetu wamepiga hatua kubwa sana.Kuna kila sababu ya kuongeza juhudi ili kuweka kufikia hatua waliyopiga wenzetu kama afrika kusini .Wenzetu wakojuu sana.Ninachokifanya kwa sasa ninajaribu kuwatafutia wanamitindo na wabunifu wa kitanzania nafasi katika majukwaa makubwa ya kimataifa na kuwafanya wajulikane.Ni kazi kubwa lakini tunajitahidi na maendeleo si mabaya” Clara akasema.
“ Nimefurahi sana kusikia hivyo Clara.Unajua hata mimi hapo awali nilikuwa na ndoto za kuwa mbunifu lakini baadae nikajikuta nikiingia katika masuala mengine kabisa na kuamua kuachana na mawazo ya kuwa mbunifu” Nikasema
“Unayoyasema ni kweli kabisa Wayne.Wengi wanakuwa na ndoto za kuwa watu Fulani lakini si wote wanaoweza kuzifanya ndoto zao kuwa kweli.Mimi sikuwa na wazo la kuwa mwanamitindo na wala sikuwahi kuota kwamba iko siku nitajulikana katika majukwa makubwa ya mitindo na mavazi.Kitaaluma mimi ni daktari lakini kwa sasa nimeachana na shughuli za udaktari na kuamua kujikita zaidi katika mitindo.Ilikuwa mwaka juzi wakati nikiwa katika mapumziko nchini afrika kusini nilipokutana na mtu ambaye alinishawishi nijaribu fani ya mitindo kwani aliona nina vigezo vyote vya kuwa mwanamitindo.Nilikuwa nataka kuyabadili maisha yangu kwa hiyo nikaona niingie katika mitindo.Nashukuru Mungu kwani baada tu ya kuingia katika mitindo maisha yangu yalibadilika na mpaka sasa ni mmoja kati ya wanamitindo wanaofahamika na kuheshimika sana nchini afrika kusini.” Clara akasema na kuzidi kuniongezea udadisi juu yake.
“amesema alitaka kuyabadili maisha yake? Kwa nini alitaka kuyabadili maisha yake? Lazima kuna sababu iliyomlazimu afanye vile Aliwezaje kufanikiwa kuyabadili maisha yake? Hata mimi ninahitaji kuyabadili maisha yangu na kuyasahau maisha yangu yaliyopita.Natakiwa kuwa karibu na Clara ili aweze kunisaidia kuyabadili maisha yangu kama yeye alivyofanikiwa” Nikawaza huku nikimuangalia Clara usoni.
“ Kwa hiyo wayne usishangae kwamba ulikuwa na ndoto za kuwa mbunifu lakini ukajikuta ukifanya kazi nyngine tofauti kabisa na ubunifu .” Clara akasema na kunifanya nitabasamu
“Una bahati sana Clara .Umeweza kufanikiwa katika fani ambayo hukuwahi hata kuota kama siku moja ungekuwa mmoja kati ya wanamitindo wakubwa.” Nikasema
“Nashukuru Wayne.Niliweza kufanikiwa kwa sababu nilikuwa najituma sana na nilikuwa nahitaji kufanya kitu ambacho kingenifanya niyasahu maisha yangu ya nyuma na kuanza maisha mapya.Hii ndiyo sababu iliyonifanya nijitume mno kitu kilichopelekea kufanikisha ndoto zangu.” Akasema
“nafurahi jinsi ulivyojituma na ukafanikiwa.Ila ninachofurahi zaidi katika jitihada zako za kuyasahu maisha ya nyuma kama unavyodai , hujasahau nyumbani” Nikasema na wote tukaangua kicheko kikubwa.
“You are so funny wayne..Siku zote nyumbani kutabaki nyumbani.Nilizaliwa Tanzania ,nimekulia Tanzania.Afrika ya kusini nimekwenda miaka minne iliyopita.Kwa hiyo Tanzania ni nyumbani na siwezi kusahau nyumbani na ndiyo maana unaniona niko hapa mida hii.Niko nyumbani” Clara akasema huku akitabasamu.Natamani ungesikia mrembo huyu akiongea.Hutatamani amalize kuongea.Alijua kupangilia maneno na sauti Kama angekuwa mtangazaji katika redio au televisheni nina imani angejizolea maelfu ya wapenzi.
“ Ulitaka kusahau kitu gani Clara? Nikauliza kwa umakini na kumfanya Clara acheke kwa sauti.Kitu kingine alichojaaliwa mrembo huyu ni ucheshi.Kwa muda huu mchache niliokaa naye nimegundua kwamba ni mmoja kati ya wasichana wachache wenye mafanikio na ambao hawana ile silica ya kujivuna au kujiona wao ni bora zaidi kuliko wengine.Clara ni mcheshi na mchangamfu sana.
“Wayne hilo swali la kichokozi” akasema huku akiendelea kucheka.
“Si vibaya kufahamu Clara kwa sababu unapoamua kufanya mabadiliko fulani basi ni lazima kuwe na sababu fulani .Wewe ni sababu gani zilikupelekea kuamua kuyabadili maisha yako na kuanza maisha mapya? Nikauliza na kumfanya acheke tena.
“wayne wewe ni mwandishi wa habari? “ akauliza na kunifanya na mimi nicheke.
“Hapana Clara mimi si mwandishi wa habari” Nikajibu.
Clara akatoa kitambaa chake cha mkononi na kujifuta macho halafu akaniangalia
“Ni hivi Wayne,katika haya maisha tunapitia mambo mengi sana .Kuna nyakati tunapitia mambo ambayo kwa kweli yanatusababishia tuweze kuyachukia maisha ,kuichukia dunia na watu waliomo ndadni yake.Kuna nyakati vile vile tunaamua kuyabadii maisha yetu na kuamua kuwa wapya tena kutokana na maisha tuliyoishi huko nyuma..Kwa sasa mimi ni mtu mwenye furaha na amani maishani mwangu tofauti na maisha niliyokuwa nikishi hapo awali.Kuhusu ni kitu gani kilipelekea mimi kuamua kubadili maisha yangu..its uhh…something personal.I’m sorry for that” Clara akasema
“Usijali Clara.Ila nakubaliana nawe kwamba kuna mambo yanayotutokea katika maisha na ambayo yanatulazimu kuachana kabisa na maisha yetu ya nyuma na kuishi maisha mapya.” Nikasema na mara kumbukumbu za Emy zikanijia kichwani na kunifanya nikae kimya ghafla.
“Wayne are you ok? Clara akanistua.
“Yah I’m ok “Nikajibu.
“Unaonekana kama umezama katika mawazo ghafla” Clara akasema.Sikujibu kitu nikatabasamu
“Thinking of your wife? Akauliza tena.Nikamtazama usoni na kusema
“I don’t have a wife” Clara akanikazia macho na kuniuliza.
“whats that ring for?
“A ring? Nikauliza kwa mshangao.Ni kweli katika kidole changu cha mkono pete ya ndoa bado ilikuwa iko kidoleni.Nilighafirika sana baada ya kugundua ujinga niliokuwa nimeufanya wa kumdanganya mrembo yule.Midomo ilikuwa ikinitetemeka na kunifanya nishindwe kutamka neno.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………………
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 11
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Usijali Clara.Ila nakubaliana nawe kwamba kuna mambo yanayotutokea katika maisha na ambayo yanatulazimu kuachana kabisa na maisha yetu ya nyuma na kuishi maisha mapya.” Nikasema na mara kumbukumbu za Emy zikanijia kichwani na kunifanya nikae kimya ghafla.
“Wayne are you ok? Clara akanistua.
“Yah I’m ok “Nikajibu.
“Unaonekana kama umezama katika mawazo ghafla” Clara akasema.Sikujibu kitu nikatabasamu
“Thinking of your wife? Akauliza tena.Nikamtazama usoni na kusema
“I don’t have a wife” Clara akanikazia macho na kuniuliza.
“whats that ring for?
“A ring? Nikauliza kwa mshangao.Ni kweli katika kidole changu cha mkono pete ya ndoa bado ilikuwa iko kidoleni.Nilighafirika sana baada ya kugundua ujinga niliokuwa nimeufanya wa kumdanganya mrembo yule.Midomo ilikuwa ikinitetemeka na kunifanya nishindwe kutamka neno.

ENDELEA……………………

Clara akaona jinsi nilivyobadilika ghafla akasema
‘Usijali Wayne ,its ok.Sikuuliza kwa ubaya” Picha za Emmy zilikuwa zikija kwa kasi kichwani kwangu
“baba mimi nimekwisha sema siwezi tena kuishi na Wayne.hakuna haja ya kupoteza wakati kwa usuluhishi.Yeye amekwishanipa ruhusa niende kwa hiyo hakuna kitu cha kuendelea kujadili hapa.hata mkisema nini mimi siwezi kurudiana na Wayne.”
Ni maneno ambayo aliyatamka Emmy mbele ya wazazi wake,yalinifanya nikae kimya na fundo kunijaa rohoni.Siwezi kuyasahau maneno yale yaliyojaa kiburi.Nikakumbuka pia siku niliyompigia simu na kumtaka afike nyumbani kwa ajili ya kikao alinijibu majibu ambayo sintaweza kuyasahu kama yalitoka kwa aliyekuwa mke wangu wa ndoa.
“Tuongee nini tena? Hatuna cha kuongea wayne.tayari ukweli unaufahamu kwa hiyo sioni kama kuna kitu tunatakiwa kuongea mimi na wewe.Umeshatambua Baraka siyo mwanao kwa hiyo hata mimi si mkeo.Sifikirii tena kuishi na wewe .Nimechoka mimi maisha ya kubanwa banwa na kufugwa fugwa ndani kama njiwa.Nahitahi maisha ya uhuru,maisha ya kufanya nitakacho.Naomba uniache Wayne.Mimi sifai kuwa mkeo.Unahitaji mwanamke bora wa kuishi naye na si mimi.”
Uchungu na maumivu niliyokuwa najaribu kuachana nayo vikarudi upya.
“Nilizama katika penzi la mtu asiyependeka.Nilikuwa kipofu.Nilipoteza muda kupalilia penzi ambalo halikuwa na faida wala manufaa yoyote.She was right.may be I wasn’t a man enough for her.I wasn’t her choice.Its time to let her go.Its time to forget her” Nikawaza.Nikauinua mkono na kuitazama pete ile ambayo toka emmy amenivisha siku tunakula kiapo cha ndoa yetu haijawahi kutoka mkononi mwangu.Nilisikia uchungu mwingi kwa jinsi alivyoweza kuivunja ahadi aliyoiweka mbele ya madhabahu ya Mungu.Aliahidi kunipenda katika kila hali lakini ameshindwa kutimiza ahadi yake.hakuwa na thamani yoyote tena kwangu.Bado niliendelea kuitazama pete ile kwa uchungu huku machozi yakinitoka.Sikuona tena ulazima wa kuendelea kuivaa pete ile kidoleni.Taratibu nikaanza kuizungusha na kuitoa kidoleni kwangu.Niliitoa kidoleni na kuishika mkononi.Clara alikuwa amenitumbulia macho asiamini alichokuwa amekiona.Niliitazama pete ile kwa hasira nikainuka na kelekea moja kwa moja lilipokuwa bwawa kubwa ambalo ndani yake kulikuwa na bata wazuri weupe wakiogelea.Nikaishika mkononi pete ile nikaitazama na kunong’ona
“ I have t do this to forget you Emmy.As from today I erase every memory of you in my heart.You ‘ll have no chance in my heart. From today I don’t know you,..from today I never married you…from today you are out of my life.I’m moving forward with my life” Nilisema maneno yale kwa uchungu mwingi huku machozi yakinitoka.Nikainua mkono na kuirusha pete ile mbali kati kati ya bwawa.Niliitazama pete ile ikidumbukia kati kati ya bwawa lile.Nilibaki nimeishikilia nguzo iliyokuwa pembeni ya bwawa kwa dakika kadhaa.Bado machozi yalikuwa yakinitoka.
“Wayne its ok.” Ilikuwa ni sauti ya upole ya Clara aliyekuwa akinitazama kwa wasi wasi.Alinishika mkono na kuniongoza kunirudisha mahala tulipokuwa tumekaa.
“Calm down Wayne ,its gonna be fine” akasema Clara kwa sauti ya upole huku akinisugua bega.
“Whysky please” Nikasema na kulisogeza glasi karibu na Clara ili animimie mvinyo
Clara akanitazama kwa mshangao.Akanimiminia mvinyo katika glasi nikaunywa wote kwa mara moja.
“One more please” Nikasema.Clara akanimiminia tena mvinyo katika glasi nikanywa na kuweka glasi mezani.
“I’m sorry Wayne” Clara akasema
“Usijali Clara,ni mambo ya kwaida.”
Kimya kikapita cha dakika mbili hivi halafu nikasema
“Clara samahani kwa hali ilivyobadilika ghafla,lakini nimeshindwa kuvumilia.I feel so much pain inside.This is beyond pain Clara.” Nikasema kwa uchungu mwingi huku Clara akinisugua sugua
“Its ok Wayne.You are gonna be fine.You are gonna be ok” Akasema Clara.
“I don’t think so Clara.No body knows how I feel inside.” Nikajibu.Kikapita kimya kidogo Clara akauliza
“Wayne what happened? Can you tell me? “
“Clara sijui hata nikueleze kitu gani.Lets not talk about it now.Lets not ruin our evening.Tumekuja hapa kupoteza mawazo na si kuongeza mawazo.Lets drink and have fun” Nikasema na kujimiminia mvinyo katika glasi nikanywa.Clara naye akamimina mvinyo akanywa..
Muda ulizidi kwenda na kiza kikaanza kuingia.Tulikuwa tukiongea na kucheka kwa furaha sana .Kwa mara ya kwanza toka matatizo ya Emmy yamenikuta nilikuwa na furaha iliyopitiliza.Tuliongea mambo mengi huku tukicheka na kupata mvinyo.Ilikuwa ni siku nzuri . Kwa muda wa masaa haya machache nilisahau kabisa kama muda mfupi uliopita nilikuwa nimezama katika dimbwi la matatizo.Nilistaajabia uwezo wa Clara wa kuweza kunisahaulisha japo kwa masaa machache machungu yote yaliyonisibu .Mwanamke huyu alikuwa na uwezo wa ajabu sana.Alikuwa miongoni mwa wale watu wachache mno ambao wana uwezo wa kutamka neno moja likasababisha mabadiliko makubwa katika maisha ya watu.Nilivutiwa mno kuwa karibu na Clara .Japokuwa hapo kabla niliweka ahadi kwamba kwa jinsi alivyonitenda Emmy sintathubutu kuwa na mwanamke mwingine tena maishani .Nilikuwa nikiamini kwamba wanawake wote ni sawa.Baada ya kukutana na Clara msimamo wangu umeanza kutetereka na nimeanza kuamini bado wapo wanawake wazuri na wenye kunifaa na mmoja wao ni huyu mrembo aliyekaa nami mezani,ambaye amenisahaulisha machungu yote niliyoyapata .Clara alikuwa mwanamke mcheshi,mkarimu ,na mwenye uelewa wa mambo wa kiasi cha juu mno.Ni mwamanke msomi,mzuri na mwenye ndoto za kufanya kazi kwa bidii na kufikia malengo aliyojiwekea.Nilipata shauku ya kutaka kumfahamu Clara kiundani zaidi .Sikufichi ndugu msomaji nilikuwa nimevutiwa mno na Clara.Mvuto huu haukutokana na ya pombe tulizokuwa tunakunywa lakini nilihisi kuna kitu kipo moyoni ambacho ni vigumu kukielezea.Nilihisi kuna kitu kipo kati yetu sisi wawili .Nilikuwa na hisia na furaha ya ajabu sana ambayo sijawahi kuipata wakati nikiwa na Emmy.
“Nilipoteza muda mwingi kwa Emmy na kumbe wako wanawake wengine wazuri wenye kujiheshimu “ niliwaza huku nikimuangalia Clara usoni.
“Wayne nimekuona unaniangalia sana usoni kwa muda mrefu sasa.Whats wrong? Clara akauliza baada ya kugundua kwamba nilikuwa nikimuangalia usoni.Ni kweli nilikuwa nikimuangalia.Sikuisha hamu ya kuitazama sura ile nzuri .
Nilitabasamu na kujibu
“Clara imenibidi nikuangalie tena na tena usoni ili nithibitishe kama mwanamke niliyenaye mezani ni binadamu wa kawaida au ni roho.” Nikasema na kumfanya Clara acheke kwa sauti.
“Kwa nini unasema hivyo Wayne? Clara akauliza
“Its ..uhhmm …I feel something strange with you…kwa muda wa masaa haya machache tuliyokaa pamoja hapa najiona kama mtu mpya.Najisikia huru na mwenye furaha kupita kiasi.Kwa muda huu mfupi nimeweza kuyasahau matatizo yangu yote niliyonayo.Kwa muda huu mfupi ninajiona ni kama vile ninaishi katika dunia isiyokuwa na matatizo ya aina yoyote..I feel like you have some power..a magic power which makes people forget their problems.”Nikasema huku Clara akiwa hana mbavu kwa kucheka.Alicheka sana na kunifanya nami nicheke pia.Akachukua kitambaa na kujifuta machozi yaliyotokana na kucheka.
“Wayne umenifurahisha sana leo.Sijawahi kukutana na mtu aliyenifurahisha kama wewe.Hebu leta mkono wako hapa” Clara akasema nami bila kukawia nikaunyoosha mkono wangu akaushika na kuupeleka katika bega lake.
“Hiki umeshika ni kitu gani? Akauliza
“Hili ni bega” Nikajibu.
“Una hakika umeshika bega?
“Ndiyo Clara hili ni bega”
“Ok Good..kama una hakika kwamba hili ni bega basi mimi si mzimu.Mzimu ni roho na hauna nyama and above all mzimu haunywi mvinyo” Akasema Clara na wote tukajikuta tukiangua kicheko kikubwa.
“I wish like I could be this happy everyday” Nikasema
“Me too” akasema Clara huku akitabasamu.
“Bado nina muda wa wiki nzima wa kuwapo hapa Arusha.Kama na wewe utakuwa na muda wa kutosha bado tunaweza kuendelea kukutana na kuwa na furaha kila siku.Siwezi kukataa Wayne kwamba leo nimefurahi sana. I had a very great time with you.Nimeipenda kampani yako” Nilitabasamu kuisikia kauli ile ya Clara .Akainua mkono wake na kuitazama saa
“wayne inakaribia saa tano za usiku.Nikiendelea kukaa na wewe hapa tunaweza tukafika asubuhi.Its time to go now.I had a very great time Wayne.” Clara akasema kwa sauti ya chini ambayo ilionyesha wazi ni kwamba alipenda kuendelea kukaa nami.
“Clara sipati neno la kukushukuru kwa jinsi ulivyoifanya siku yangu ya leo kuwa yenye furaha .Nashukuru sana Clara.” Nikasema huku nikimalizia mvinyo uliokuwa ndani ya glasi.
“Hapa arusha umefikia wapi? Nikauliza
“Nimefikia SEAN 11 Lodge wewe unaishi maeneo gani?……” Akasema
“.Mimi ninaishi Majengo” Nikasema huku nikisimama
“Nashukuru kukufahamu Wayne.You are such a wonderfull guy…” Clara akasema na kunipa mkono.
“Hata mimi nafurahi sana kukufahamu Clara.Sikutegemea kama siku ya leo ingeisha nikiwa na furaha ya ajabu namna hii.uhhm .if its ok with you can you give me your phone number ? Nikasema.
“Nipe wewe namba yako kwa sababu bado sina namba ya simu ya Tanzania.Nitakupigia mimi” Clara akasema.Nikamuandikia namba zangu na kumpa.
“Kesho tutaonana wapi? Nikamuuliza.
“Ratiba yangu ya kesho inaonyesha nitakuwa na shughuli nyingi lakini nitakutaarifu kama nitapata nafasi ama vipi” Clara akasema huku akianza kupiga hatua kuondoka na mimi nikiwa pembeni yake.Nilihisi msisimko wa ajabu kutembea na mlimbwende yule.Mwendo wake wa maringo ulinifanya nijione kama ninatembea na malaika.
“Are you sure you can drive? Kama hujisikii kuendesha let me take you to a hotel” Nikamuuliza
“No thank you Wayne.I’m a bit drunk but I can manage”
Nilimsindikiza Clara katika gari lake akaingia na kuliwasha.Sikuondoka pale hadi alipoligeuza na kuliweka tayari kwa kuondoka.Akashusha kioo na kunipungia mkono.
“Good night Wayne” Akasema .
“Good Night Clara” Nikajibu .Clara akafunga kioo na kuliondoa gari.Nililitupia macho gari lile likiondoka hadi lilipopotea kabisa machoni pangu.Nikaelekea katika gari langu nikaingia na kukaa nikiwa nimeuinamia usukani
“What a wonderfull woman…sidhani kama atakuwa binadamu wa kawaida yule..si mzimu kweli yule? Lakini hapana, nimeushika mkono wake na kuhakikisha ni binadamu wa kawaida.Mwanamke huyu mbona ameuteka moyo wangu ghafla namna hii? Gosh hizi ni hisia za kweli au ni hizi pombe nilizokunywa?…Nikawaza.”
“Yeroo…..Mbona unainamia sukani..umesidiwa tukupeleke sipitali?” Sauti ya mlinzi wa kimasai aliyekuwa akilinda eneo lile ndiyo inanistua katika mawazo .
“Ouh Rafiki..niko mzima siumwi kitu” Nikawasha gari na kuondoka

**********

Saa tisa za usiku bado nilikuwa sijapata usingizi.Toka nimerudi nimekuwa nikihangaika kitandani kujaribu kutafuta usingizi bila mafanikio.Sikuelewa sababu ilikuwa ni pombe nilizokunywa au ni mawazo niliyokuwa nayo.Mawazo mengi sana yamekuwa yakinijia kichwani .Kubwa ilikuwa ni kumbukumbu ya mambo yaliyotokea jioni ya siku iliyotangulia.Kumbukumbu hii ilikuwa ikijirudia kichwani kama filamu na kunifanya nitabasamu.
“Clara…” Nilisema kwa sauti ndogo huku nimekaa kitandani
“You are such an amazing woman.” Nikasema huku nikitabasamu.
“ hatimaye nimekutana na mwanamke wa ndoto zangu.Clara is a perfect woman for me.Ana kila kitu ninachokihitaji kwa mwanamke wa ndoto zangu” Nikajilaza tena kitandani.
“ I think like I’ve lost her.Itakuwaje kama sintaonana naye tena? Vipi kama hatanipigia simu tena? Ouh Mungu wangu ninakufa na mawazo ya huyu mwanamke.”
Nikainuka kitandani na kwenda kuketi sofani.
“Sintasafiri tena kama nilivyokuwa nimepanga.Kuonana na Clara kumenifanya nimsahau Emmy ghafla.Nilazima nionane tena na Clara.Siwezi kukubali kumpoteza.Nitamsaka dunia nzima hadi nimpate……..” Nikawaza huku nikiwa nimejilaza sofani.
Sikumbuki saa ngapi usingizi ulinichukua .Nilistushwa na mvumo wa simu iliyokuwa pembeni yangu.Nikafumbua macho yaliyokuwa mazito kutokana na usingizi.Nikaichukua simu na kuangalia mpigaji.Alikuwa ni baba mkwe.
“baba shikamoo” Nikamsalimu.
“marahaba Wayne habari za leo?
“nzuri tu baba habari za kwenu?
“Huku kwema.Nimekupigia ili nijue unaendelea vipi “ baba mkwe akauliza
“Ninaendelea vizuri baba Nashukuru” Nikajibu
“Ok Nashukuru sana kama unaendelea vizuri.Ukiwa na tatizo lolote lile tafadhali tupigie simu sisi wazee wako tupo tutakusaidia”
“Sawa baba nashukuru” Nikajibu na baba mkwe akakata simu.
Niliyafikicha macho ili niweze kuona vizuri.Nilitazama saa ilipata saa tatu za asubuhi.Haikuwa kawaida yangu kulala kwa muda mrefu namna hii .Nadhani hii ilitokana na pombe tulizokuwa tumekunywa jana yake.Tulimaliza chupa nzima ya mvinyo mkali.Mvinyo ule tuliokunywa jana yake ukanifanya niikumbuke sura ya kuvutia yenye nuru na tabasamu muda wote,sure yenye macho mazuri meupe ambayo ungependa yakuangalie muda wote,sura yenye midomo laini na mizuri ambayo kila anapotasamu huanikiza meno meupe yaliyojipanga vyema kinywani,ni sura ya mwanamke wa kipekee kabisa Clara ambaye toka nimekutana naye jana yake amenikosesha usingizi na kunifanya usiku mzima nikeshe nikimuwaza yeye.
Niliipekua simu ili kuangalia kama Clara alipiga wakati nikiwa usingizini au alituma ujumbe wa maneno lakini hakukuwa na simu yoyote iliyopigwa wala ujumbe toka kwa Clara.Nikaitupa simu pembeni.
“Laiti kama ningezifahamu namba za simu za hoteli aliyofikia ningempigia walau kumjulia hali.Nina hamu ya kutaka kuisikia tena sauti yake nzuri.Lakini bado mapema ndiyo kwanza saa tatu.Ni lazima atanipigia .Kwa namna nilivyokuwa nimemgusa ni lazima atanipigia.Ngoja niendelee kusubiri” Nikawaza.
Mwili ulikuwa mzito kuinuka pale kitandani.Nilihisi njaa kali.Nikaenda jikoni nikatazama katika friji lakini sikupata chochote cha kuweza kula..Nikaamua nioge halafu nitoke kwenda kutafuta supu safi.Kisha oga niliigia garini na kuondoka kwenda kutafuta chochote cha kutia tumboni asubuhi ile hususan supu .Bado sura ya Clara ilikuwa ikinijia akilini kila mara na kuniweka katika fikara nzito.
“This is what they call love at first sight.Yaani kumuona jana tu tayari ameniteka akili namna hii.Sina shaka na hisia zangu.Ninaamini moyo wangu haunidanganyi kwamba Clara ndiye mwanamke anayenifaa maishani.” Nikawaza huku nikipata supu.
Mpaka saa nne za usiku Clara hakuw amenipigia simu kama alivyokuwa ameahidi.Niliumia sana kwa kitendo hiki.Mishale ya saa ilizidi kusonga kwa kasi hadi ilipofika saa sita za usiku lakini sikuwa nimepokea simu yoyote au hata ujumbe wa maneno toka kwa Clara.Kichwa kilijaa mawazo mengi.Mwishowe nikaamua kulala.
Siku ya pili ikakatika bila ya kupokea tena simu toka kwa Clara.Nilijiuliza maswali mengi kulikoni asipige simu wakati alikwisha ahidi kunipigia? Nini kimetokea? Ndugu msomaji nilikuwa na mawazo mengi mno kwa Clara kushindwa kunipigia simu.Nilianza kupatwa na mawazo pengine hakuwa na nia ya kweli ya kunipigia simu na aliongea vile kwa ajili ya kuniridhisha.Nilianza kukata tamaa ya kuonana tena na Clara .Nilijiona kama ni mtu nisiyekuwa na bahati katika suala la urafiki na watoto wakike.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………….
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 12
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“This is what they call love at first sight.Yaani kumuona jana tu tayari ameniteka akili namna hii.Sina shaka na hisia zangu.Ninaamini moyo wangu haunidanganyi kwamba Clara ndiye mwanamke anayenifaa maishani.” Nikawaza huku nikipata supu.
Mpaka saa nne za usiku Clara hakuw amenipigia simu kama alivyokuwa ameahidi.Niliumia sana kwa kitendo hiki.Mishale ya saa ilizidi kusonga kwa kasi hadi ilipofika saa sita za usiku lakini sikuwa nimepokea simu yoyote au hata ujumbe wa maneno toka kwa Clara.Kichwa kilijaa mawazo mengi.Mwishowe nikaamua kulala.
Siku ya pili ikakatika bila ya kupokea tena simu toka kwa Clara.Nilijiuliza maswali mengi kulikoni asipige simu wakati alikwisha ahidi kunipigia? Nini kimetokea? Ndugu msomaji nilikuwa na mawazo mengi mno kwa Clara kushindwa kunipigia simu.Nilianza kupatwa na mawazo pengine hakuwa na nia ya kweli ya kunipigia simu na aliongea vile kwa ajili ya kuniridhisha.Nilianza kukata tamaa ya kuonana tena na Clara .Nilijiona kama ni mtu nisiyekuwa na bahati katika suala la urafiki na watoto wakike.

ENDELEA………………………..

Siku ya alhamisi saa tatu za usiku nikiwa nimepumzika nyumbani nikiangalia filamu,mara simu yangu ikaita.Nikaichukua na kutazama mpigaji.Zilikua ni namba ngeni katika simu yangu.Nikabonyeza kitufe cha kupokelea simu.
“Hallo” Nikasema
“Hallo naongea na Wayne? Sauti ya kike ikauliza ambayo moja kwa moja niliitambua ilikuwa ni sauti ya Clara.Nikapatwa na furaha ya ghafla.
“yah hapa unaongea na Wayne.Nani mwenzangu? Nikauliza huku nikijifanya kutoifahamu sauti ile .
“Unaweza ukaikumbuka sauti hii? Akauliza Clara huku akicheka kicheko cha chini chini kama kawaida yake
“yah …nadhani…uhhm hii itakuwa ni sauti ya Clara..” Nikasema halafu Clara akacheka kicheko kikubwa.
“Nilitegemea utakuwa umeshaisahau sauti hii” Clara akasema huku akicheka
“katika sauti zote za dunia hii sauti hii sintaweza kuisahau hata sekunde moja.hata Ukiwa katika kundi la watu elfu moja sauti yako nitaitambua tu kwa sababu ni sauti ya kipekee sana….” Nikasema huku sura yangu ikiwa imepambwa na tabasamu zito.Clara akaendelea kucheka
“Wayne habari za toka tulipoonana?
“habari nzuri Clara.Sijui wewe.Niliona kimya kingi nikajua pengine umeshazipoteza namba zangu” Nikasema
“Ouh No Wayne..siwezi kuipoteza namba yako.Nilishindwa kukupigia nilikuwa nimebanwa mno na ratiba.Unajua siku zenyewe ni chache na mambo yalikuwa mengi sana kwa hiyo ikanibidi kufanya kazi hadi usiku wa manane kila siku.Nasuhukuru Mungu tunamalizia leo” Clara akasema kwa sauti tulivu
“Ouh kumbe mnamaliza leo?
“Ndiyo Wayne leo tunamaliza .Lakini kesho kutakuwa na sherehe za kuchangia kituo cha watoto wanaoishi katika mazingira magumu cha Future generation Hafla hiyo itafanyika kuanzia saa moja za usiku.Ninaomba kama utakuwa na nafasi twende wote”
“Clara nitakuwa na nafasi ya kutosha hivyo usihofu tutakwenda wote.”
“Nashukuru sana kwa kukubali kwenda nami katika hafla hiyo.Nitakutegemea unipitie hapa hotelini kwangu saa kumi na mbili za jioni.” Clara akasema
“Hakuna tatizo Clara nitafika hapo hotelini kwako mida hiyo uliyosema.”
“Ok Wayne goodnight”
“Goodnight Clara” Nikajibu na simu ikakatwa.Nilipatwa na furaha ya aina yake.Nilikwisha kata tamaa ya kuonana tena na Clara.Simu hii aliyopiga ilinirudishia furaha na matumaini ya kumuona tena mrembo yule.

* * * *

Saa kumi na mbili juu ya alama ilinikuta katika geti la kuingilia SEAN 11 LODGE alikofikia Clara.Sikutaka kuchelewa miadi na mrembo huyu wa kutukuka.Nilishuka katika gari nikajiangalia na kujiona niko safi kabisa kwa ajili ya shughuli ya usiku huu.Nilikuwa nimependeza kupita maelezo.Nilikuwa nimevaa suti kali nyeusi .Ukiwa umeambatana na mrembo kama huyu inakubidi na wewe uwe umependeza isivyo kawaida ili muendane.Nilitembea kwa mikogo hadi mapokezi.Nikawasalimu akina dada wawili waliokuwa pale wenye nyuso za furaha.Nikawaomba wamtaarifu Clara kwamba mgeni wake amekwisha fika.dada mmoja akachukua simu akapiga halafu akaiweka simu chini akaongea na mwenzake ambaye akaja akanichukua na kunipeleka katika ukumbi.Nilionyeshwa meza moja iliyokuwa na viti viwili ambayo ilikuwa pembeni kabisa mwa ukumbi ule uliokuwa na mwanga hafifu na watu wachache.Muhudumu yule akanivutia kiti na kunikaribisha.
“Clara amesema ukae hapa utumie chochote kile unachoona kitakufaa kwa muda huu unapomsubiri.yeye bado anajiandaa.” Akasema dada yule mwenye lafudhi ya kichaga
Nilimwambia aniletee mvinyo mwepesi .Nilikuwa na mawazo mengi juu ya Clara.Niliwaza jinsi muonekano wake utakavyokuwa usiku wa leo ,niliwaza jinsi tutakavyoongozana katika shughuli hiyo.Niliwaza mambo mengi sana.Dakika ishirini toka nifike pale mara kwa mbali nikamuona mtu akija kwa mwendo wa madaha mno.Toka kwa mbali niliweza kumtambua alikuwa ni Clara.Mrembo yule alikuwa aking’aa usiku huu.Kadiri alivyopkuwa akisogelea pale mezani ndivyo moyo wangu ulivyoongeza kasi ya mapigo yake. Alikuwa amevaa gauni refu jekundu lililokuwa likingaa kila limulikwapo na mwanga wa taa.Shingoni alikuwa amevaa mkufu mdogo wa dhahabu wenye kung’aa na mkononi alikuwa na pochi ndogo nyekundu.Chini alikuwa amevaa viatu virefu vyekundu.kwa ujumla alikuwa amependeza isivyo kawaida.
“Waoo !! Wayne you are amazing tonight….samahani sana kwa kuchelewa” Akasema Clara akiwa amesimama pembeni ya ile meza huku akinipa mokono.
“Bila samahani Clara.You look like a heaven angel tonight ” Nikajibu huku nikitabasamu.Clara akacheka na kusema
“Angels don’t wear high hills ” Tukacheka wote kicheko kikubwa.
“nadhani tunaweza kuondoka..” akasema Clara.Tukatoka na kuingia katika gari langu tukaondoka kuelekea katika hafla ya uchangiaji wa kituo cha watoto wanaoishi katika mazingira magumu.
“Nimefurahi sana kukuona tena Clara” Nikaanzisha mazungumzo ndani ya gari.
“ I missed you Wayne…did you miss me? Akauliza Clara .
“I missed you so badly.Siku zilivyokuwa zikikatika bila ya kupata simu yako nilikuwa na mawazo mengi mno.Niliwaza pengine labda umepoteza namna yangu,au pengine …….”
“Pengine nini” akauliza Clara huku akitabasamu
“pengine labda hukujisikia kunipigia kwa kuogopa usumbufu wa namna moja au nyingine”
“Pole sana Wayne kwa usumbufu huo ulioupata .Sikufanya makusudi kutokukupigia simu.Nilikuwa nimebanwa sana na ratiba ndiyo maana sikuweza kupata muda wa kukaa na wewe.mambo yalikuwa mengi na siku zilikuwa kidogo.”
Tuliendelea na maongenzi na kutaniana huku tukicheka kwa furaha na hatimaye tukafika mahala inapofanyikia hafla hiyo.Hapo nje palikuwa na magari mengi ya watu waliokuwa wamekuja katika kuchangia.
Tuliposhuka garini Clara akaukamata mkono wangu na kisha tukaanza kuingia ukumbini kama wapenzi.
“Do you mind? Akaniuliza iwapo nitajali kwa kitendo kile cha kunikamata mkono.Sikujibu kitu nikatabasamu naye akatabasamu .Nilikuwa nimefurahi moyoni kupita kiasi kwa kitendo kile cha kuingia ukumbini huku tumeshikana mikono kama wapenzi.Yeyote ambaye angetuona angefikiri kwamba sisi ni wapenzi tena tunaopendana mno.Nilifarijika mno kwa kitendo kile.Nilijiona ni mwanaume mwenye thamani tena.
Watu walikuwa ni wengi ndani ya ukumbi huu mkubwa.Watu walikuwa wakitukodolea macho wakati tukipita kutafuta meza.Wengine walikuwa wakinong’onezana.Sikuelewa ni kwa nini ilitokea vile.labda ni namna tulivyokuwa tumependeza.Ghafla bila kutegemea niliona kitu ambacho sikuwa nimekitegemea kukiona mahala pale.Katika meza moja nilimuona Emmy akiwa amekaa na Chris pamoja na watu wanaofanya kazi kampuni moja na Chris ambao baadhi yao niliwafahamu kupitia kwa Chris.Macho yangu na Emmy yakagongana.Niliuona mstuko wa wazi uliompata.Akainamisha kichwa chake chini kukwepa macho yangu.Chris alistuka baada ya kuona jinsi mpenzi wake alivyo badilika ghafla.Alipogeuka kuangalia tukagonganisha macho.Amani ikamtoweka ghafla.Sikuwajali nikamshika mkono Clara tukaendelea kwenda mbele katika meza zilizokuwa wazi.
Sikuwa nimefikiria kama ningeweza kuonana na Emmy mapema namna hii.Niliamini kwamba kwa sasa mwanamke yule hayuko moyoni mwangu kwa sababu pamoja na kugonganisha macho katu sikuwa na mstuko wowote .Nilijisikia amani kubwa moyoni.Hiki kilikuwa ni kipimo tosha kwamba tayari hana nafasi yoyote tena moyoni mwangu.Kilichokuwa kikinijia mara kwa mara na kunipa mawazo mengi ni sura ya Baraka.Sikujua mpaka sasa hivi atakuwa katika hali gani.Nilizoea kucheza naye kila siku,nilikumbuka jinsi tulivyokuwa tukikaa bustanini hasa nyakati za usiku tukipiga magitaa yetu na kuimba.Zilikuwa ni nyakati za furaha sana.Sikutegemea kama huko aliko alikuwa akipata furaha kama aliyokuwa akiipata alipokuwa na mimi.Sikuwa na namna ya kufanya ili niweze kuonana naye tena.Sikutaka kuwa karibu na Emmy kwa namna yoyote ile.Sikutaka kumbughudhi katika maisha yake mapya.Nilichokifanya ni kuomba Mungu siku moja anikutanishe na Baraka japo kwa dakika mbili ili niweze kufurahi naye tena.
“Wayne mbona huagizi vinywaji? Akauliza Clara baada ya kurudi toka katika meza ya jirani alikokuwa amekwenda kuwasalimia wanamitindo wenzake.
“Ninakusubiri wewe ili tuagize kwa pamoja” Nikasema na mara muhudumu akafika tukaagiza vinywaji.
“Nilikuwa nawasalimia marafiki zangu.” Akasema Clara.
“Nimewaona.They are so pretty” Nikatania.
“Shhhhhhh!!! Don’t ever say that to me Wayne.I’m so jelousy…don’t talk to any woman tonight..I wont allow any woman to steal you from me tonight ..I’m gona kill the one who try” Clara akasema huku akicheka kwa nguvu sana na mimi pia nikacheka.
“Kusema ukweli umependeza sana Wayne.You are the cutest man tonight.Naogopa nisije nikaibiwa” Clara akasema huku akiendelea kucheka.Kama hujamfahamu Clara unaweza ukadhani labda amekwisha lewa lakini hivi ndivyo alivyo.Ni mtu mcheshi ,mchangamfu na mwenye utani mwingi.Manenoyale ya utani aliyoyaongea yanazidi kunipandisha joto la mwili.Nilitamani kama angekuwa akimaanisha kile alichokuwa anakisema.Nilitmani kuwa na Clara muda wote.Ni mwanamke ambaye ana heshima,mstaarabu ,mwenye kujipenda,mwenye kujali watu,mcheshi na mkarimu.Sifa zote hizi zilinifanya nivutike kutaka kuwa naye muda wote.
“Ok here’s the deal.I’m not going to talk to any woman and you don’t talk to any man..deal?
“Deal” akajibu Clara huku akicheka kicheko kikubwa.Watu waliokuwa meza za karibu walikuwa wakitushangaa kwa jinsi tulivyokuwa tunafurahi.
“mwanaume yeyote akikaribia meza hii ninamtoa kwa makofi” Nikasema na tukaendelea kucheka.
“Wayne umeshawahi kupigana katika maisha yako”
“Yes ! “ nikajibu kwa ufupi
“Sura yako ya upole haionyeshi kama ni mtu wa vurugu.” Akasema huku akitabasamu
Sherehe zilifunguliwa na mgeni rasmi aliyekuwa mbunge wa jimbo la Arusha mjini.Baadae shughuli za uchangiaji zikaanza.Baadhi ya makampuni yaliyokuwa yamealikwa yalikuwa yametuma wawakilishi wao kuleta michango yao ambao walikuwa wakipita mbele na kukabidhi kiasi kilichotolewa na kampuni husika.Kampuni zilikuwa ni nyingi na mara nikasikia kampuni anayofanyia kazi Chris ya Amazora safari ikitajwa.Chris ndiye aliyekuwa akiongoza kundi la wafanyakazi wa Amazora safari kwenda kukabidhi michangoya kampuni .Miongoni mwao alikuwepo Emmy.Sikutaka kuwatazama tena nikayarudisha macho na mawazo yangu mezani.
Michango bado iliendelea kutolewa Makampuni na watu mbali mbali walikwisha toa michango yao na ndipo muongoza shughuli akachukua kipaza sauti na kumkaribisha muandaaji wa shughuli ile mama Blandina chokasi ambaye alifika pale mbele akakabidhiwa kipaza sauti ili aweze kuongea jambo.Ukumbi wote ukakaa kimya ili kumsikiliza mama yule.
“Ndugu mgeni rasmi,mheshimiwa mbunge wetu wa Arusha mjini,wawakilishi wa makampuni mbali mbali,ndugu wageni waalikwa mabibi na mabwana ninapenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru kwa namna mlivyojitokeza kwa wingi kuchangia kituo hiki cha watoto wanaoishi katika mazingira magumu cha future generation.Kujitokeza kwenu kunaonyesha ni jinsi gani nyote mnavyoguswa na matatizo ya watoto hawa ambao wengi wao hawana wazazi au wazazi wao hawana uwezo wa kuwatunza.Najua nyote mna majukumu mengi lakini mmejibana na kutoa kile mlichokuwa nacho kwa ajili ya kuwasaidia watoto hawa masikini.Sisi hatutaweza kuwalipa chochote il tunawaombea kwa Mungu awazidishie wote mara mbili ya mlicho nacho na awape moyo wa kuweza kujitolea zaidi kwa ajili ya watu masikini na wasio na uwezo.” Akatulia na ukumbi wote ukalipuka kwa makofi na vigere gere halafu akaendelea.
“Ndugu wageni waalikwa mabibi na mabwana,bado shughuli yetu inaendelea lakini nimesimama hapa kwa ajili ya jambo maalum kabisa.Nimesimama hapa kwa ajili ya kutoa shukrani za kipekee kwa mtu ambaye kampuni yake ndiyo imefanikisha jambo hili muhimu la leo.Ni mwanadada wa kitanzania ambaye kazi zake za mitindo na urembo zimevuka mipaka ya nchi yetu na kufika mbali .Kwa sasa mwanadada huyu anafanya kazi za mitindo na ubunifu nchini afrika ya kusini.Ni mbunifu mkubwa wa kimataifa na kampuni yake inafahamika kote duniani.Amekuwa akishiriki katika matamasha na majukwaa mbali mbali makubwa ya urembo duniani.Mbunifu huyu amekuwa akifanya juhudi kubwa katika kuhakikisha kwamba wabunifu na wanamitindo wa kitanzania wanafahamika duniani.Kupitia kampuni yake ya Black angels amekwisha wasaidia wanamitindo zaidi ya 30 kupata mikataba na kufanya kazi na makampuni makubwa ya urembo duniani,vile vile amefanikisha kuwatangaza wabunifu wa kitanzania katika majukwaa makubwa ya mitindo duniani.Mbunifu huyu amekuwa na mchango mkubwa sana katika umoja wa wabunifu na wanamitindo wa Tanzania.Mara kwa mara amekuwa akija na kutoa semina kwa wabunifu na wanamitindo wachanga.Kwa muda wa wiki mbili sasa tumekuwa naye hapa Arusha akiendesha semina ya mambo haya ya ubunifu na urembo.Kwa kuifanya fani hii ya mitindo na urembo izidi kukua hapa nchini aliona haitakuwa vizuri kama semina ile itaisha hivi hivi ,akabuni lifanyike jambo hili la kuichangia jamii.Kila mwaka tutakuwa tunafanya kitu kama hiki na kuichangia jamii yetu katika matatizo mbali mbali iliyokuwa nayo.Mabibi na mabwana naomba sasa nimtambulishe kwenu rais wa kampuni ya Black angels Bi Clara msikongo.Kokote uliko tafadhali Clara simama uwasalimu wageni waalikwa.”
Clara akasimama na kupunga mikono,ukumbi wote ukalipuka kwa makofi na vigere gere.Nilikuwa nimestuka sana.Sikujua kama nimekaa na mtu mkubwa na maarufu namna ile.Nilimtazama Clara akiwapungia mikono wageni mle ukumbini huku akiwa na tabasamu zito Sikuamini macho yangu.
“Clara tafadhali naomba upite uje huku mbele ili uongee neno lolote kwa hadhira hii iliyokusanyika hapa usiku huu” mama Blandina akasema.
Clara akachukua pochi yake pale mezani halafu akanisogelea akaniinua mkono.Nilielewa alikuwa akitaka niinuke pale kitini.Moyo ulikuwa ukinienda mbio sana.Alitambua kwamba nilikua mzito kusimamam akaniinamia na kuninong’oneza sikioni.
“Don’t be nervous..smile” akasema.Nikainuka na kuanza kutabasamu.Akanishika mkono tukaanza kutembea kwa madaha kuelekea jukwaani.Makofi na vigere gere vilikaribia kulichana paa la ukumbi ule mkubwa.Miguu ilikuwa ikinitetemekaSikuelewa hofu ile ilikuwa imetoka wapi.Tulipanda jukwaani nikasimama pembeni ya Clara ambaye akapewa kipaza sauti ili aongee machache
“mabibi na mabwana habari zenu.”
“Nzuriiii” Ukumbi wote ukaitikia huku makofi yakipigwa.
“Awali ya yote napenda kuwashukuru sana kwa kuitika mwito wetu.Japokuwa ilikuwa ni taarifa ya muda mfupi lakini mmeweza kujitokeza kushirikiana nasi katika kuchangia jambo ili muhimu.Kila siku tunashuhudia ongezeko la watoto wanaoishi mitaani katika mazingira magumu.Kama wana jamii tuna jukumu la kuwasaidia watoto hawa ambao wengi wao hawana wazazi au kama wana wazazi basi ni masikini sana.Ni jukumu la kila mwanajamii kuhakikisha kwamba anatoa kile kidogo alicho nacho kwa ajili ya kuwasaidia watoto hawa .Kuna makundi mengi yanayohitaji msaada kama vile wanawake wenye maradhi ya Fistula,wanawake wanaosumbuliwa na kansa ya matiti n.k Sisi kama jukwaa la wanamitindo tumeamua kuanza kwanza na kundi hili la watoto hawa na kisha tutachangia makundi mengine.” Clara akatulia na ukumbi wote ukalipuka kwa makofi
“Ndugu zangu uwingi wenu usiku huu wa leo umenipa faraja sana kwamba sasa fani hii ya urembo imeanza kueleweka katika jamii kwamba si uhuni kama ilivyokuwa ikidhaniwa hapo awali bali ni kazi kama kazi nyingine zozote.Fani hii ya urembo kama ikitiliwa mkazo inaweza kuwa ni mkombozi wa ajira kwa vijana wetu wengi.Tunaiomba serikali iitazame fani hii kwa upana wake kwa sababu ni fani ambayo inaweza ikatutangaza sana kimataifa kama tunavyojitahidi kufanya hivi sasa japokuwa mchango wa serikali bado ni mdogo mno.Ndugu zangu sitaki kuchukua muda mrefu wa kuongea kwa sababu bado kuna mambo mengine yanaendelea.napenda kabla ya kumaliza niseme kwamba pamoja na kwamba mimi ni mmoja wa waandaaji wa shughuli hii lakini mimi na mwenzangu hapa tunao mchango wetu ambao tunautoa kwa ajili ya watoto hawa.Kwa pamoja tunatoa cheki yenye thamani ya fedha za kitanzania shilingi millioni hamsini.” Ukumbi wote ukalipuka kwa kelele za shangwe.Nilistuka sana.Sikuwa nimeongea na Clara kuhusu jambo lolote lile kuhusiana na fedha zile alizosema tumetoa kwa pamoja mimi na yeye.Clara akatoa cheki akaikabidhi huku makofi na vigere gere vikizidi.

TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………….
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 13
MTUNZI :pATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Ndugu zangu uwingi wenu usiku huu wa leo umenipa faraja sana kwamba sasa fani hii ya urembo imeanza kueleweka katika jamii kwamba si uhuni kama ilivyokuwa ikidhaniwa hapo awali bali ni kazi kama kazi nyingine zozote.Fani hii ya urembo kama ikitiliwa mkazo inaweza kuwa ni mkombozi wa ajira kwa vijana wetu wengi.Tunaiomba serikali iitazame fani hii kwa upana wake kwa sababu ni fani ambayo inaweza ikatutangaza sana kimataifa kama tunavyojitahidi kufanya hivi sasa japokuwa mchango wa serikali bado ni mdogo mno.Ndugu zangu sitaki kuchukua muda mrefu wa kuongea kwa sababu bado kuna mambo mengine yanaendelea.napenda kabla ya kumaliza niseme kwamba pamoja na kwamba mimi ni mmoja wa waandaaji wa shughuli hii lakini mimi na mwenzangu hapa tunao mchango wetu ambao tunautoa kwa ajili ya watoto hawa.Kwa pamoja tunatoa cheki yenye thamani ya fedha za kitanzania shilingi millioni hamsini.” Ukumbi wote ukalipuka kwa kelele za shangwe.Nilistuka sana.Sikuwa nimeongea na Clara kuhusu jambo lolote lile kuhusiana na fedha zile alizosema tumetoa kwa pamoja mimi na yeye.Clara akatoa cheki akaikabidhi huku makofi na vigere gere vikizidi.

ENDELEA…………………….

“Kabla hatujaondoka nadhani mwenzangu hapa na jambo la kusema” Clara akasema akiwa na maana ya mimi.Sikuwa nimejiandaa kusema lolote na sikujua niseme nini.Nilihisi kutetemeka.Sikuwa na uzoefu wa kuongea mbele ya hadhira kubwa kama ile iliyobeba watu mashuhuri na matajiri.Clara akanipa kipaza sauti huku akitabasamu.Nilikipokea japo mikono ilikuwa ikinitetemeka.Nilikishika kipaza sauti nikakisogeza karibu na mdomo wangu.Clara akaniangalia kwa tabasamu.Sijui nilipata wapi nguvu na uwezo wa kuongea ghafla nikajikuta nikisema
“Mabibi na mabwana,sina mengi ya kuongea kwa sababu mengi amekwisha yaongea mwenzangu hapa.Ninachotaka kukisema ni kwamba kadiri muda ulivyokuwa ukienda mimi binafsi nimejikuta nikizidi kuguswa na maisha ya watoto hawa.Nimejikuta nikitaka kuchangia tena na tena lakini uwezo unakuwa hauruhusu.Kwa namna nilivyoguwa naomba kama mimi nitoe ahadi ya kuchangia tena shilingi millioni thelathini pesa ambayo nitaitoa kesho.” Ukumbi wote ukalipuka kwa shangwe .Nikatabasamu baada ya kuiona furaha ile ya watu.Nikamrudishia Clara kipaza sauti lakini kabla hajakikabidhi kwa mama Blandina akaniomba nisogee karibu yake.Nikasogea akauinua mkono wake na kuuzungusha shingoni kwangu akaniangalia kwa tabasamu na kusema.
“Mabibi na mabwana na mimi naongeza tena shilingi millioni ishirini .Jumla mimi na mwenzangu hapa tunatoa shilingi za kitanzania millioni mia moja.Ahsanteni sana” Ukumbi ukalipuka kwa kelele za shangwe.Clara akanishika mkono tukaanza kushuka ngazi huku ukumbi wote ukiwa umesimama ukitushangilia .Nilihisi kama miguu inagongana wakati tukirudi katika meza yetu.Sikuwa nimetegemea kitu kama kile kutokea.Mambo yale makubwa yalitokea kwa haraka sana.Niliona ni kama ndoto vile.
“You did great..I didn’t expect you could be such a smart guy….Wayne you are amazing..congraturations” Clara akaninong’oneza sikioni wakati tukikaa kwenye viti vyetu.Sikujibu kitu nilikuwa nikitabasamu.Nikatoa kitambaa na kujifuta jasho lililokuwa likinitoka kama nimemwagiwa maji.
Mambo yaliyokuwa yametokea pale ukumbini yalikuwa ni kama ndoto .Sikuwa nimetarajia kuwa mambo yangekuwa kama vile.Siwezi kuelezea ni jinsi gani nilivyokuwa nimefurahi moyoni.
Baada ya kushuka toka jukwaani meza yetu ilikuwa haikauki watu waliokuja kutupa mikono ya pongezi..Huu ulikuwa ni usiku wa kipekee sana kwangu.Nilifurahia sana kwa namna Clara alivyonifanya niyasahau masahibu yote yaliyokuwa yamenikumba .Kila nilipomtazama Clara usoni nilishindwa kuamini kama ni yeye kweli ndiye aliyeweza kunifanya nikawa na furaha kubwa namna ile.Katika usiku ule nilikuwa nimepata heshima kubwa na ya kipekee kwanza kwa kuongozana na mwanamke mwenye sifa kubwa kama Clara, na pili kitendo cha kusimama jukwaani na kuongea na hadhira ile kubwa ya watu na kuwafanya wote walipuke kwa shangwe kilinipa heshima kubwa mno ambayo sikuwa nimetarajia kuipata.Emmy alinidharau na kuniona si mtu mbele ya watu lakini leo Clara amenirudishia heshima yangu iliyopotea..Nilipokumbuka kwamba Emmy naye alikuwepo pale ukumbini nikatabasamu Sikujua nimshukuruje Clara kwa namna alivyoirudisha tena furaha yangu iliyopotea.
“Ninaamini Clara ndiye mwanamke ambaye Mungu ameniandalia.Moyo wangu umekuwa rahisi mno kumkubali na kumpa nafasi kubwa.Sina shaka na moyo wangu kwani naamini safari hii haunidanganyi kama ulivyofanya kwa Emmy.Lakini Clara si kama Emmy.Utofauti wao ni kama ardhi na mbingu.Safari hii sitaki kufanya makosa.Nitaenda naye taratibu na mpaka niuteke moyo wake.Ninachotakiwa kukifanya kwa sasa ni kuanza kumfahamu kiundani Natakiwa niwe na subira kwa sababu iwapo nitaanzisha masuala ya mapenzi mapema namna hii ninaweza kumpoteza malaika huyu.Natakiwa nianze kwa kujenga urafiki mkubwa na baadae ndipo masuala ya mapenzi yafuate.Sitaki kumpoteza mtu muhimu kama huyu.” Niliwaza huku nikimtazama Clara kwa kuibia akiwa anazungumza na wanamitindo wenzake.
Saa saba za usiku ndipo tulipopata nafasi ya kuondoka pale ukumbini.Hatukuweza kuondoka mapema kutokana na Clara kuwa na maongezi na watu wengi ambao wengi wao walikuwa ni wanamitindo na wabunifu.Mpaka anaingia garini bado walikuwepo wasichana waliokuwa wanamfuata ili kujaribu kupata walau namba yake ya simu kwa sababu hawakujua ni wapi wangeweza kumuona tena baada ya semina ile kumalizika.
“Pole na kazi nzito” Nikasema wakati tukiondoka maeneo yale
Clara akaniangalia na kusema huku akitabasamu
“ahsante sana Wayne.Sikutegemea kama watu wangekuwa wengi namna hii.Nasikitika muda umekuwa mdogo sana na sijaweza kuonana na wote waliokuwa wakihitaji kuniona.Nitatafuta muda nirudi tena Arusha.Nimepapenda sana”
“Kwa hiyo unategemea kuondoka lini ? Nikauliza
“Kesho kutwa natakiwa niwe nimeondoka Tanzania.Kuna shughuli moja muhimu natakiwa kwenda kuifanya afrika kusini” Clara akasema na kunifanya nistuke na ninyong’onyee ghafla.Katika mawazo yangu nilitegemea kwamba pamoja na semina kumalizika lakini angeendelea kubaki arusha kwa siku kadhaa .Laiti kama ningekuwa na uwezo ningeweza kumzuia asiondoke kwa sababu bado nilihitaji kuwa naye.
“Mbona kimya hivyo Wayne” Clara akauliza.Nadhani aligundua kwamba nilikuwa kimya ghafla.Kwa kweli kutoka moyoni sikutaka Clara aondoke,lakini uwezo wa kumzuia asiondoke sikuwa nao.
“ Nilidhani baada ya kumaliza semina ile ungebaki Arusha japo kwa siku mbili tatu.Nilikuwa nimepanga nikupeleke ukatembelee hifadhi ya Ngorongoro.” Nikasema .Clara akanitazama halafu akasema
“Wayne hata mimi sikuwa nimepanga kuondoka mapema namna hii.Nilipanga kuwa na siku kadhaa za mapumziko baada ya semina kumalizika lakini nilipigiwa simu jana usiku na mmoja wateja wangu wakubwa kuwa kuna kazi moja muhimu sana ambayo natakiwa kwenda kuifanya.I’m sorry Wayne kwa kuikosa ofa hii ya kwenda kutembea Ngorongoro lakini usijali nitatafuta nafasi nitakuja tena Arusha.Nimepapenda sana .Kuna hewa safi,warembo wazuri and above all I’ve met with so wonderfull people especially you Wayne.Toka siku tumekutana umekuwa ni mmoja kati ya watu wangu muhimu sana japokuwa hatujapata muda mwingi wa kukaa na kufurahi pamoja.Wayne naomba ufahamu kwamba uko katika orodha ya watu wangu muhimu wanaonifanya niwe na furaha katika maisha haya.You are so wonderfull.I’ll miss you a lot but don’t worry I’ll come back I promise” Clara akasema kwa ile sauti yake nzuri yenye kuvutia.Nilifarijika mno kwa maneno yale ya Clara.Kuwa miongoni mwa watu wake ambao yeye anawaita ni wa muhimu ilikuwa ni faraja kubwa kwangu.Japokuwa hakunifahamu kiundani lakini alitokea kuniamini na kunweka miongoni mwa watu muhimu.Ulikuwa ni mwanzo mzuri ambao sikutaka kuuharibu.
“Usijali Clara.Siku yoyote ukitaka kuja Arusha naomba unitaarifu tafadhali ili nikufanyie maandalizi kama mwenyeji wako” Nikasema na kumfanya Clara acheke kicheko kikubwa.
“hakuna haja ya maandalizi Wayne.Hapa ni kama nyumbani.Hata nikija bila taarifa nafahamu nina watu wangu wa muhimu.” Clara akasema huku akicheka
“Kwa hiyo Clara kama umepanga kuondoka kesho kutwa,siku ya kesho utakuwa na kazi gani? Nikauliza ili kujua kama ninaweza kupata walau nafasi ya mwisho ya kuwa na mwanamke huyu mrembo.
“kesho nitaondoka na ndege ya saa saba mchana kwenda kuwaaga wazazi Dar es salaam halafu kesho kutwa ndiyo nitaondoka kuelekea South Afrika.”Akajibu.
Nilimpeleka Clara hadi katika hoteli aliyokuwa amepanga.Nilimsindikiza hadi katika chumba chake akanikaribisha ndani,sikujivunga nikaingia ndani na kuketi sofani.
“Clara kwa kuwa muda umekwenda sana na kesho unatakiwa kusafiri ,mimi naomba nikuage ili nikupe nafasi ya kujiandaa kwa safari ya kesho.” Nikasema huku nikijiandaa kuinuka.
“Wayne please sit down.” Clara akasema ,nikakaa chini.
“Mbona una haraka namna hiyo? Kesho ninaondoka lakini zitapita siku nyingi kabla hatujaonana tena ,Don’t you like to spend sometimes with me? Don’t you wanna talk about it? Clara akauliza
“about what? Nikauliza na mimi
“about what happened at the party” akasema Clara na kunifanya nicheke .
“Please Wayne just for tonight,stay with me and we can have wine,talk,laugh and have fun.I know after I’m gone I’ll miss someone to laugh with.” Clara akasema Hakujua ni jinsi gani nilivyokuwa nimefurahi kwa kuniomba niendelee kukaa pale.
“Ok Nitabaki kwa saa moja au mawili halafu nitaondoka” Nikasema
“Thank you so much Wayne.It means a lot to me.Now wait there and I’ll be back in a second” Akasema Clara huku akifungua mlango na kuingia katika chumba cha kulala.Baada ya kama dakika mbili akarudi akiwa amevaa suruali ndefu ya kitambaa chepesi pamoja na koti jeusi lenye manyoya laini.Akalifungua friji na kutoa chupa za mvinyo akazipanga mezani.
“Nina furaha ya ajabu sana leo Wayne.Naomba tunywe na tufurahi mpaka tuchoke” Akasema Clara.Tulipoanza kunywa Clara akasema
“Wayne naomba nichukue nafasi hii kukuomba samahani kwa kilichotokea pale ukumbini”
“Nothing wrong happened Clara” Nikasema
“Najua utasema hakuna kilichotokea lakini nilikupandisha jukwaani bila ridhaa yako.Haukuwa umepanga kuongea na hadhira kubwa kama ile.najua vile vile hata zile fedha ulizochangia hukuwa umepanga kuzitoa kwa hilo usijali nitakurudishia zile fedha zote…..”
“no no no Clara” Niliingilia kati kabla hajamaliza sentensi yake.
“Nimetoa fedha zile kwa moyo mmoja na wala sihitaji unirudishie.Uliponiomba niambatane nawe katika uchangiaji wa kituo kile nilikwisha andaa mchango wangu kama mshiriki.Tafadhali Clara mchango ule niliutoa kwa moyo wangu wote kwa ajili ya watoto hawa wenye mazingira magumu,na kuhusu kunipandisha jukwaani yah ! I was a bit nervous lakini kwa kuwa karibu nawe nilipata ujasiri mkubwa hata nikaweza kuongea na umati ule mkubwa wa watu.” Nikasema kwa msisitizo na kumfanya Clara atabasamu,akaniangalia kisha akasema
“Wayne you are amazing.Nilifanya makusudi kukuomba nipande nawe jukwaani.Lengo langu lilikuwa kukupima ni jinsi gani unavyojiamini.I know you were nervous but what you did was wonderfull.Nimefurahi sana Wayne kwa sababu hukuweza kuniangusha.Kwa dakika kadhaa tuliweza kuziteka akili za kila mmoja pale ukumbini.Wayne sijawahi kuwa na furaha kama siku ya leo.Na furaha yote hii imechangiwa na wewe.You made my evening.” Clara akasema huku akiinua glasi yake tukagonganisha maglasi yetu
“cheers!! Tukasema kwa pamoja.
Kitu kimoja ambacho sikuwa na uwezo nacho ni kusimamisha muda uliokuwa ukienda kwa kasi ya ajabu.Nilitaka niendelee kubaki na mrembo yule asiyechosha kuwa naye.Nilihisi kuipata furaha ya ajabu ambayo sikuwa nimeipata kwa miaka mingi.
“Wayne mbona kimya? Unawaza nini? “ .akauliza Clara baada ya kuniona nikiwa kimya ghafla nikimtazama
“Nothing Clara” Nikajibu
“Wayne do you have a family? Clara akauliza.Sikujibu swali lile kwa haraka.Sikujua nimpe jibu gani.Swali lile likanikumbusha mateso aliyonipa Emmy ,papo hapo nikamkumbuka mtoto Baraka.
“Not anymore” Nikajibu kwa sauti iliyoonyehsa kuwa na chembe za hasira ndani yake
“You had one? Clara akauliza tena.
“Clara it’s a very log story.Nisingependa kuiongelea hadithi hii kwa usiku huu wenye kila aina ya furaha,sipendi kuufanya usiku huu mzuri uwe ni usiku wa simanzi” Nikasema huku nikiongeza mvinyo katika glasi
“can you be strong enough to tell me? Clara akaendelea kusisitiza.
“Clara I’m sorry but its not a nice story to hear tonight.There is nothing interested in it.It’s a beyond pain story.So why don’t we skip this and talk some other sweet things like nice places in South Africa..your handsome boyfriend..”
“Hahahahaaaa…….hahahaa…….” Clara akacheka kicheko kikubwa mara tu nilipomaliza sentensi yangu.
“Boyfriend? .. akauliza
“yes you boyfriend,Don’t you have one” Nikauliza na kumfanya acheke tena kicheko kikubwa.Sikushangaa kwa sababu toka nimemfahamu nimegundua kwamba Clara anapenda mno kucheka.
“Wayne unamaanisha nini unaposema boyfriend? Akauliza huku akipiga funda la mvinyo
“I mean someone you love,someone whom your heart belong to…………” sikumalizia sentensi yangu Clara akaanza tena kucheka
“wayne unanifurahisha sana.I don’t have a boyfriend or believe in love.Kama unamaanisha mpenzi,mpenzi wangu mimi ni kazi yangu ninayoifanya kwa mapenzi yote toka moyoni.After what I got from men,I don’t think I will ever love again.Ninaishi maisha yangu ya furaha,I have lots of friends,I have a job,I do whatever I want to do,I drink,I dance I sing and I’m happy.so what do I need a man for? ………Clara akasema huku akiinuka na kwenda katika friji kuchukua vipande vya barafu.Maneno yale yalikuwa mazito sana kiasi kwamba nilianza kukata tamaa kama ningeweza kumpata mwanamke kama yule maishani.Manenoyale yalionyesha wazi kwamba aliwahi kutendwa huko nyuma na kumfanya asione tena thamani ya mapenzi.Kwa sasa alikuwa na maisha yake mazuri yaliyojaa furaha na amani hivyo hakutaka kupata tena matatizo.Kwa upande Fulani nilikubaliana na mawazo yake kwa sababu hata mimi kwa jinsi nilivyokuwa nimetendwa na Emmy sikutaka tena kujiingiza katika masuala ya mahusiano kwa sababu niliamini wanawake wote ni sawa.Sielewi ni kitu gani kilichonikutanisha na Clara ambaye kwa muda mfupi niliokutna naye ameweza kuufuta mtazamo huo kichwani kwangu na kunijengea mtazamo mpya kwamba wanawake wote si sawa.kwa mbali nilisikia kitu kama sauti ikininiambia nisikatishwe tamaa na maneno yale ya Clara.
“ You can have all that Clara,money,friends job,cars and everything,but are you happy?” Nikamuuliza Clara.Akachukua glasi yake,akapiga funda kubwa la mvinyo akaliweka chini na kukaa kimya kwa sekunde kadhaa akiniangalia.
“Mbona hunijibu? Nikamwambia Clara.Akanitazama na kusema
“Sorry Wayne, this conversation brings me lots of things in my mind..Uliniuliza swali gani?.” Clara akasema .Nilimtazama usoni nikagundua kuna mambo aliyokuwa akiyawaza.
“Nilikuuliza kwamba ,unasema una kila kitu,pesa,marafiki,kazi na kila kitu unachokitaka unakipata.Lakini je una furaha moyoni mwako?
“Furaha ipi unayoizungumzia Wayne” Clara akauliza
“nazungumzia furaha ya moyo.Pamoja na kuwa na vitu vyote hivyo maishani lakini moyo wako una furaha? Nikauliza
“Wayne nina furaha.Kwa sababu kila kitu ninachokitaka ninakipata Nina furaha.Kikubwa kinachonifanya niwe na furaha maishani ni kwamba niko huru,moyo wangu una amani.Nina uhuru wa kufanya chochote nikitakacho.Hebu niambie kuna furaha zaidi ya hiyo? Clara akauliza
“Nafahamu hilo Clara ,nazungumzia ndani ya moyo wako una furaha? Nikauliza tena
“Wayne nimeshakwambia nina furaha moyoni mwangu” Clara akajibu akanitazama na kusema
“Please Wayne can we change the subject.Can we talk of something else like..uhhm tell me of your love life,about your girfriend” Clara akasema huku akitabasamu,akainua glasi yake na kupiga funda la mvinyo.Nilifikiri kidogo nimweleze nini nikaamua kusema ukweli
“ I don’t have a girlfriend.”
Clara akanitazama kwa makini usoni baada ya kauli ile na kusema
“Wayne ,tell me what happened? Kila ninapokutajia kuhusu masuala ya mahusiano yako unabadilika ghafla.Kitu gani kimekutokea? Tafadhali naomba uniambie.Nitakusaidia” Clara akasema kwa msisitizo huku amenikazia macho
Nilivuta pumzi ndefu na kusema
“Clara ni hadithi ndefu sana na nisingependa kuongelea masuala hayo kwa sasa”
“C’mon Wayne mimi ni rafiki yako.naomba uniamini.Nieleze nini kilikutokea ? Usiponieleza leo utanieleza lini? Clara akauliza
“Sawa Clara kwa vile umesisitiza kutaka kujua ukweli ,nitakueleza ukweli.”
Nilimweleza Clara kila kitu toka tulipoanza mahusiano yetu mimi na Emmy na hadi tulipokuja kuachana..Nilipomaliza kumsimulia mkasa ule ulionipata niliona michirizi ya machozi machoni pa mrembo yule.
“Wayne hadithi yako imenichoma moyo sana.Kwa nini binadamu wengine wanakuwa na ukatili wa namna hii? Pole sana wayne.Nafahamu kwa sasa uko katika wakati mgumu mno.Jipe moyo na yatakwisha” Clara akasema huku akifuta machozi
“Usijali Clara,nimemwachia Mungu ndiye atakayenilipia.Sihitaji kulipa ubaya kwa Emmy..Nashukuru hata hivyo kwa kukutana nawe kwa sabahu umenifanya kwa siku hizi chache tulizofahamiana niwe mtu mwenye furaha na kusahau yote yaliyonipata.Nakiri kwamba wewe ni mwanamke wa pekee sana.Mwanaume atakayekuwa nawe atakuwa na bahati kubwa mno”
Clara akacheka sana baada ya kuongea vile.
“Wayne kila mara unaongelea kuhusu mwanaume.Ninayafurahia maisha yangu bila mwanaume kwa hiyo sifikirii kuwa na mume” Clara akasema
“what about children? Nikauliza.Clara akakaa kimya akafikiri kwa muda na kusema
“Kids ?
“Yes.Hujawahi kufikiri kuwa na watoto siku moja?
“I love children and I’d like to have two .Nafikiri furaha yangu itakamilika siku nikiwa na mtoto wangu”
“Good . kama ni hivyo utawapataje hao watoto bila kuwa na mume? Nikauliza
“Ouh Wayne please just forget about that..lets talk of something else..” Clara akasema akionyesha wazi kulikwepa swali langu.Lengo langu lilikuwa kutaka kufahamu undani wake kuhusu maisha yake ya kimapenzi.Toka nimekutana naye Clara amekuwa mgumu sana kunieleza kuhusu maisha yake ya kimapenzi.Kila ninapoanzisha mazungumzo hayo huwa anapenda tubadilshe maongezi.Nilisimama,nikamsogelea karibu na kumshika bega lake la kulia kwa mkono wangu
“Nisikilize Clara,pamoja na kwamba umekiri kuwa una furaha ya kutosha maishani,lakini ukweli ni kwamba hauna furaha ya moyo.Kusema kwamba haufikirii kuwa na mpenzi hauutendei haki moyo wako.Moyo wako unahitaji upate mwenza na hivyo kuufanya uwe na furaha maishani.Clara you are a great woman.You deserve to be loved and be happy.You need someone who can complete your happiness.Don’t lie to yourself Clara that you have happiness.You don’t..Utakuwa mwanamke mwenye furaha pindi utakapompata mwanaume wa maisha yako.Tafadhali naomba usilisahau hilo”

TUKUTANE SEHEMU IJAYO………………..
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 14
MTUNZI:pATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Ouh Wayne please just forget about that..lets talk of something else..” Clara akasema akionyesha wazi kulikwepa swali langu.Lengo langu lilikuwa kutaka kufahamu undani wake kuhusu maisha yake ya kimapenzi.Toka nimekutana naye Clara amekuwa mgumu sana kunieleza kuhusu maisha yake ya kimapenzi.Kila ninapoanzisha mazungumzo hayo huwa anapenda tubadilshe maongezi.Nilisimama,nikamsogelea karibu na kumshika bega lake la kulia kwa mkono wangu
“Nisikilize Clara,pamoja na kwamba umekiri kuwa una furaha ya kutosha maishani,lakini ukweli ni kwamba hauna furaha ya moyo.Kusema kwamba haufikirii kuwa na mpenzi hauutendei haki moyo wako.Moyo wako unahitaji upate mwenza na hivyo kuufanya uwe na furaha maishani.Clara you are a great woman.You deserve to be loved and be happy.You need someone who can complete your happiness.Don’t lie to yourself Clara that you have happiness.You don’t..Utakuwa mwanamke mwenye furaha pindi utakapompata mwanaume wa maisha yako.Tafadhali naomba usilisahau hilo”

ENDELEA……………………

Nilimwambia Clara ambaye alikuwa ametulia akinisikiliza.Akachukua glasi yake ya mvinyo akapiga funda moja akainama na kufikiri kisha akasema
“Wayne katika wanaume niliowahi kukutana nao,sijawahi kukutana na mwanaume aliyeniambia maneno yaliyonigusa kama uliyoniambia leo hii.Maneno yako yamenigusa sana moyo.Umeamsha kitu kipya ambacho sikuwa nikikifikira katika maisha yangu.Namkabidhi Mungu ndiye atakayejua hatima ya maisha yangu .Kama itampendeza mimi kupata mwanaume wa maisha yangu na iwe hivyo” Clara akasema taratibu akiwa ameinamisha kichwa.Nilitabasamu baada ya kuisikia kauli ile.
Nilitazama saa na kukuta ni saa tisa za usiku.
“Clara muda umekwenda sana.Nahitaji kukuacha upumzike na ujiandae kwa safari ya kesho” Nikasema huku Clara akinitazama
“No Wayne you cant go now and leave me alone.Stay with me just for tonight..” Clara akaomba.Niimtazama machoni na kugundua kwamba alikuwa akimaanisha alichokisema.Hakujua ni furaha kiasi gani nilikuwa nayo kwa kuniomba nibaki naye usiku ule kitu nilichokuwa nikikiomba kila siku.Nilitabasamu na kumsogelea,akasimama na kunishika shingo yangu kwa mikono yake laini.
“I’ll stay with you tonight” Nikasema kwa sauti ya tayatibu yenye kukwama kwani nilihisi msisismko wa ajabu baada ya kuguswa shingo yangu na mrembo yule.Msisimko ule ukanifanya niichukue mikono yangu na kuizungusha kiunoni mwake na kumfanya astuke ghafla na kuanza kuhema kwa kasi.
“Wayne what do you want from me tonight? Clara akauliza kwa sauti laini
“I just want a wonderfull night with you..unforgetable night” Nikasema na kwa kasi ya ajabu akanivuta kwake na kunipiga mabusu mfululizo.Nilihisi kama napaa mawinguni kwa mpasuko wa furaha nilioupata.Ulikuwa ni usiku wa aina yake.Kwa miaka mingi sikuwa nimepata usiku niliohisi kama niko peponi kama huu.

* * * *

“Wayne you are amazing” Ilikuwa ni sauti ya laini ya Clara iliyonistua toka usingizini.Niliyafumbua macho na kujikuta nikiwa pembeni ya mrembo mwenye uzuri uliotukuka.Nilijihisi kama vile niko ndotoni.Kiumbe aliyekuwa amelala pembeni yangu alifanana na wale wanaopatikana katika simulizi mbali mbali au kwenye picha za kuchora.
“Wayne..thank you for the wonderfull night “ Akasema Clara na kunitoa katika fikra kuwa nilikuwa ndotoni.Sikuwa nikiota.Ni kweli nilikuwa nimelala na Clara.Nilimtazama Clara ambaye alikuwa amenigeukia akinitazama usoni huku macho yake mazuri yakifanya mwili wangu uhisi msisimko wa ajabu
“Wayne sikutegemea kama ningekuja kukutana na mwanaume ambaye angenipa furaha kama uliyonipa usiku wa kuamkia leo.Katika maisha yangu sijawahi kukutana na mwanaume wa shoka kama wewe.Nilichokipata katika maisha yangu ya kimapenzi ni karaha na mateso kiasi kwamba niliwachukia wanaume wote na kuwaona ni wanyama,wabinafsi na hakuna mwanaume ambaye angeweza kunipa raha niliyokuwa nikiihitaji.Wayne naomba nikiri kwamba umenibadilisha mtazamo wangu.Umenifanya niamini kwamba bado wako wanaume ambao Mungu amewajaalia uwezo mkubwa wa kuwaridhisha wanawake.Wayne you are one of those few men hard to find in this world.I don’t know what I should do to make you forever mine.Sikujua kama itatokea siku nitatokea kumuhusudu mwanaume kama ilivyonitokea kwako.Wayne naomba usinielewe vibaya lakini toka nimekutana nawe nimejikuta nikiwa tofauti sana na nilivyokuwa awali.Nimejikuta nikiwa na furaha ya ajabu kitu ambacho hakijawahi kunitokea hapo kabla.Nimejikuta nikitoka nje ya msimamo wangu kwa mara ya kwanza na kuhisi kwamba ninahitaji kuwa na mtu wa kunifanya niendelee kuipata furaha hii ya ajabu niipatayo sasa.Wayne sihitaji kuwa mbali nawe tena kuanzia sasa.Kwa mara ya kwanza toka nimezaliwa ninathubutu kupiga magoti na kuomba nafasi ndani ya moyo wa mtu.Wayne tafadhali naomba unipe nafasi ndani ya moyo wako.Sintakuumiza kama alivyokufanya mwanamke uliyekuwa naye.Nitakupenda na kuwa nawe daima kwa sababu you are so special Wayne.” Clara akashindwa kuendelea akakiangusha kichwa chake kifuani kwangu.Nilihisi joto la ghafla.Nilihisi ile ilikuwa njozi na si kitu cha kweli.Clara mwanamke mrembo anayeupeleka mbio moyo wangu toka nimekutana naye leo hii kwa mdomo wake anatamka kwamba anahitaji kuwa nami maishani.Niliona ni kama muujiza mkubwa ulionitokea.
Sikuwa na kitu cha kujivunga tena.Sikuwa na kipingamizi wala sababu yoyote ya kukataa ombi lile la Clara.Niliamini yale yalikuwa ni majibu ya maombi yangu niliyomuomba Mungu baada ya kutendwa na Emmy.
Siku mpya ikaanza kwa penzi zito kati yangu na Clara.
“ Wayne nasikitika sana kwa sababu sitaki kubanduka pembeni yako lakini kazi hii inayonilazimu kwenda afrika kusini leo ni muhimu mno.Itanilazimu kwenda na baada ya muda mfupi nitarejea.Nahisi miguu mizito kuondoka hapa lakini sina namna nyingine ya kufanya.Wayne umeniteka ghafla kiasi kwamba sijielewi.nini kimenitokea.Kabla sijaondoka ningependa nikapafahamu nyumbani kwako ili nikija kwa mara nyingine nisifikie tena hotelini” Clara akasema .
Sikuwa mbishi kwa kila alichokuwa akikiongea Clara.Nilimsikiliza kama malkia wangu.Kwa kuwa alikuwa na safari mchana wa siku hiyo,hatukuwa na muda wa kupoteza tukaingia garini na kuelekea nyumbani kwangu.
Tulifika nyumbani kwangu na kwa ghafla nilipatwa na mstuko wa ajabu kwa nilichokiona katika geti la kuingilia ndani .Nilisimamisha gari na kushuika kwa haraka. Katika geti la nyumbani kwangu alikuwepo Baraka amekaa juu ya tofali.Nilimwinua na kumkumbatia kwa furaha kubwa.
“baraka umekuja saa ngapi? Nikamuuliza
“Nimekuja asubuhi ,nimekuta geti limefungwa kwa kufuli nikajua haupo nikaamua kukaa hapa nje nikusubiri” Baraka akajibu
“Mama na baba wamekuruhusu uje huku asubuhi hii?
“hapana hawajaniruhusu.Nimetoroka nyumbani.Simtaki uncle Chris.Kila siku ananilazimisha nimuite yeye baba.Nataka kuendelea kukaa na wewe.Sitaki tena kurudi kule kuishi na mama.Nataka kuishi na wewe.” Baraka alisema huku akitoa machozi.Mtoto huyu aliniumiza sana na kukitonesha tena kidonda kilichoanza kupona.Niliendelea kumlaani Emmy kwa kitendo alichokifanya na kumfanya mtoto mdogo kama yule kuteseka namna ile.
“basi usilie baraka.Tutakaa wote siku ya leo halafu jioni nitakupeleka nyumbani na kama mama yako atakubali uishi huku basi tutaishi wote.” Nilimwambia Baraka ambaye alionyesha wazi kutokuridhika na uamuzi wangu wa kumrudisha nyumbani kwao jioni.Nilimtambulisha Baraka kwa Clara,akamshika mkono nikaingiza gari ndani.Kwa muda mfupi Clara na Baraka wakazoeana na kuwa marafiki .Dakika zile chache za kuwa pamoja zilileta furaha kubwa miongoni mwetu.
Tukiwa bado katika maongezi na vicheko pale sebuleni mara ghalfa mlango unafunguliwa na anaingia Emmy akiwa ameongozana na askari wanne .Alikuwa amefura kwa hasira.Wote tukapigwa na butwaa kwa hali ile.Moja kwa moja Emmy akaninyooshea kidole mimi na mmoja wa wale askari akanikaribia.
“Ndugu wewe ndiye Wayne?”
“Ndiye mimi.Kuna nini afisa? Nikauliza kwa mshangao
“Wayne tunakuhitaji kituoni.Unatuhumiwa kumchukua mtoto aitwaye Baraka bila ridhaa ya wazazi wake.Tafadhali tunaomba tuongozane kwenda kituoni kwa ajili ya maelezo zaidi.”
Mwili wote ukajikuta ukilowa jasho na midomo kunitetemeka kwa hasira.
“Afande nafahamu kwamba mko kazini lakini naomba mnieleweshe ninakamatwa kwa kosa lipi? Sielewi nimefanya kosa gani “ Nikawaambia wale askari ambao walionyesha hawakuwa na muda wa kupoteza.
“ Bwana Wayne,huyu mama unamfahamu? Akauliza yule askari aliyeonekana ndiye kiongozi wa msafara ule
“Ninamfahamu.Alikuwa mke wangu” Nikajibu huku nikimtazama Emmy kwa macho makali
“Huyu mama ndiye mlalamikaji ,na ameleta malalamiko kwamba mtoto wake amepotea na moja kwa moja akakuhisi wewe kwamba ndiye uliyemchukua mtoto huyo bila ridhaa ya wazazi wake kitu ambacho ni kosa kisheria.Tumekuja hapa na kumkuta mtoto huyo anayedaiwa kupotea yuko hapa kwako.Kwa hiyo tunakuhitaji hapa tuende wote kituoni ili ukatoe maelezo yako kuhusiana na suala hili” akasema afande yule ambaye sikuweza kuzisoma namba zake kwa sababu ya sweta alilokuwa amevaa.Niliuma meno kwa hasira nikawatazama wale maaskari kisha nikasema
“naomba tusikilizane maafande.Mimi siwaelewi mnaongea kitu gani kwa sababu mimi ndiyo kwanza nimefika hapa nyumbani sina hata nusu saa,sasa huyo mtoto nimemuiba saa ngapi? Isitoshe nimefika hapa na kumkuta Baraka amekaa getini.Nikamuuliza amefikaje fikaje hapa akaniambia kwamba ametoroka nyumbani kwao basi nijkamchukua na kuingia naye ndani.Kama hamuamini ninachokisema hebu muulizeni mtoto huyu hapa yeye mwenyewe atasema ukweli” Nikasema kwa msisitizo
“Afande msimuamini huyo.Amemuiba mtoto wangu na kuja kumficha huku.Tafadhali afande tusizidi kupoteza muda mchukueni tuelekee kituoni,atajitetea mahakamani” Emmy akasema akiwa amefura kwa hasira.Nilitamani nimrukie na kumpa kipigo kikali mwanamke yule lakini nikajitahidi kujizuia ili nisifanye jambo kama hilo japokuwa nilikuw ana hasira zisizomithilika..
“Afande samahani naomba na mimi niongee kidogo” Clara aliyekuwa ameduwaa akiangalia mambo yanavyokwenda akafunguka na kusema
“Nyamaza kimya hasidi wewe….” Emmy akasema kwa ukali akimwambia Clara lakini afande akamzuia
“Emmy hebu nyamaza tumsikilize na mwenzio anataka kusema nini.Endelea mama…” afande akampa ruhusa Clara aongee
“Afande mimi sioni kosa ambalo Wayne anatuhumiwa nalo.Nimekuwa na Wayne toka jana jioni,tulihudhuria wote hafla ya uchangishaji fedha za kusaidia kituo cha watoto wanaoishi katika mazingira magumu.Tumetoka pale ukumbini na kuelekea hotelini kwangu.Nimekuwa na Wayne usiku mzima na hakurejea nyumbani kwake.Asubuhi hii tumeongozana wote kuja hapa kwake na tulipofika getini tumemkuta mtoto amekaa,Wayne akamuuliza kama ameruhusiwa kuja huku na mama yake ,Baraka akasema kwamba hakuruhusiwa na mtu yeyote kuja huku ila ametoroka yeye mwenyewe baada ya kutokuridhishwa na maisha anayoyaishi huko kwao.Nimeona niongee ukweli kwa sababu inaonekana huyu mwanamke hana uhakika na anachokiongea.” Clara akasema na ghafla Emmy akakurupuka na kutaka kumvaa Clara,akazuiwa na askari.
“Niacheni nimfundishe adabu huyu mwanamke naona bado hajanifahamu mimi ni nani.nakuonya wewe mwanamke usiingilie mambo yasiyokuhusu.kama unahitaji mtoto zaa wa kwako na si kusubiri wengine wakuzalie ili uibe.Ninakwambia wewe na huyu baradhuli mwenzio mtanikoma mwaka huu.” Emmy akaongea kwa sauti kali.Niliitazama sura ya Clara nikaona ni jinsi gani alivyoumizwa na maneno yale ya Emmy.Hasira zikanipanda nikashindwa kujizuia nikataka kumvaa Emmy na kumpa kipigo lakini askari wakafanya kazi yao na kunizuia.
“Afande sintakubali hata siku moja mwanamke huyu akaja na kuanza kuporomosha matusi ndani ya nyumba yangu. Kama ni kutukana anitukane mimi na hata siku moja asije akamgusa Clara.Hahusiki na kitu chochote .”Nikasema kwa ukali.
“Anhaa kumbe huyu ndiye anayekupa kiburi,basi nitakula naye sahani moja.Yeye si ndiye anayeona fahari kuchukua mabwana za watu, nakwambia nitamfundisha adabu.Nitamuonyesha mimi ni nani.Wayne fahamu kwamba wewe bado ni mume wangu halali wa ndoa na ninakuonya kwamba sintakupa muda wa kupumzika.Nitakufundisha adabu” Emmy akaongea kwa kujiamini sana.Chuki ya wazi wazi ikajidhihuirisha machoni pake.Sikuelewa nini sababu ya chuki ile kubwa na ya dhahiri aliyokuwa nayo Emmy kwangu.Alitaka kuwa huru na nikamruhusu aende anakotaka kwenda .Kwa ulimi wake alitamka kwamba hanitaki tena katika maisha yake sasa kwa nini aanze kunifuatilia maisha yangu wakati kila mmoja amekwisha anza maisha yake? Nilikasirika sana
“jamani hapa hatukuja kwa ajii ya kugombana.Sasa sikilizeni.Wayne na mwenzio,wote tunaelekea kituoni kwa ajili ya kupata maelezo ya kina juu ya suala hili lenye utata.Mambo yote yatajulikana huko huko kituoni” Afande akasema.
“Sawa hakuna shida afande.Lakini huyu mwenzangu Clara naomba mumuache aende zake kwa sababu kwanza hahusiki kwa namna yoyote na masuala haya na pili ana safari ya kwenda Dar es salaam saa tano asubuhi ya leo kwa ndege na tayari amekwisha kata tiketi.” Nikawaomba wale maaskari lakini kwa haraka Clara akasema
“wayne usijali nitakuwa nawe mpaka mwisho.Siwezi kukuacha peke yako katika tuhuma ambazo si za kweli.Safari yangu ninaweza kwenda siku yoyote ile lakini sintakubali kuona ukinyanyaswa na mijitu yenye roho za kishetani” Clara akasema huku ameukunja uso wake kwa hasira.Moyoni nilisikitika sana kwa kumuingiza Clara katika matatizo yangu na Emmy,mwanamke mwenye roho ya shetani.Maneno yale ya Clara yalionyesha kumchoma moyo Emmy ambaye alibetua midomo na kusonya kisha kwa ghadhabu akamuendea Baraka aliyekuwa sofani akilia ,akamchukua kwa nguvu.
“hebu twende ,wewe ndiye unayesababisha mpaka mimi natukanwa namna hii” Emmy akaongea kwa hasira huku akimvuta mkono baraka ambaye alikuwa akipiga kelele akigoma kuondoka.
“Bwana wayne tafadhali ingia garini wewe na mwenzio twende kituoni ” Afande akaniamuru nipande gari la polisi lililokuwa imeegeshwa pale nje kwangu.
“Afande sijakataa kwenda kituoni.Nimetii bila shuruti na ninaomba niruhusiwe kuongoza kituoni mimi mwenyewe na gari yangu.Siwezi kupanda gari moja na huyo mwanamke” Afande akanitazama na kukubaliana nami kwamba nitumie gari langu.Mimi na Clara tukaingia katika gari langu na kuongoza kuelekea kituoni.Clara alikuwa kimya na hakuongea kitu chochote.Ni wazi alikuwa ameumizwa sana na kitendo alichokifanya emmy.Nilikuwa nikimtazama kwa kuibia .
“Clara samahani sana kwa yote yaliyotokea.Sifahamu nini sababu ya mwanamke yule kunifanyia mambo kama haya..Kama uhuru nimekwisha muachia na anaishi na mtu ambaye yeye mwenyewe alitamka kwamba ndiye anayempa furaha maishani sasa iweje tena aanza kunifuatilia katika maisha yangu? Ameniumiza sana lakini nitamuonyesha mimi ni nani” Nikasema
“Wayne tafadhali usiendelee kugombana na yule mwanamke kichaa.Utajikuta ukipoteza muda mwingi kwa mambo yasiyokuwa na maana yoyote.Kitu cha msingi jaribu kujipanga na kuangalia maisha yako ya mbeleni.Mtu kama yule usimuweke katika akili yako.Ukisema upambane naye utapoteza muda wako bure.Nakushauri achana naye kabisa na wala usijishughulishe naye hata kidogo” Clara akasema huku akiweka mkono mmoja begani kwangu
“Vipi kuhusu safari yako ya Afrika kusini? Itakuwaje iwapo hautaonekana? Nikauliza
“Usijali kuhusu hilo wayne.safari yangu si muhimu kwama ulivyo wewe.Mimi ninafahamu thamani yako kwangu na ndiyo maana niko tayari kufanya lolote lile kwa ajili yako.Niko tayari kwenda hadi mwisho wa dunia kwa ajili yako.Kwa hiyo kuhusu hilo la safari lisikupe shida kabisa Wayne.” Maneno yale yakanifanya nitabasamu .Clara alimaanisha alichokuwa amekisema.Aliiona thamani yangu kwake na hivyo kuwa tayari kufanya chochote kile kwa ajili yangu.Niliapa moyoni kufanya kila niwezalo kwa ajili ya kuwa na mwanamke kama huyu ambaye ananijali na kunithamini .
Tulifika kituoni na kushuka kisha tukawasubiri askari wale wafike kwa sababu tulikuwa tumewatangulia kufika.Walipofika tukaongozana wote hadi ndani ambako nilichukuliwa maelezo.Nilipomaliza Clara naye akaomba atoe maelezo yake kama nyongeza kwa yale ya kwangu akakubaliwa.
Baada ya masaa manne ya mjadala mkali baina yetu na maafisa wa polisi ikaonekana wazi kwamba sikuwa na kosa lolote nililolifanya ila zilikuwa ni hila za Emmy kutaka kunichafua.Alipewa onyo kali kwanza kwa kusumbua chombo cha dola na pili kwa kutaka kunichafua.Vile vile ikaamriwa kwamba aniombe radhi mimi pamoja na Clara kwa usumbufu aliotusababishia na mwisho akakanywa kwamba kama tumeachana asijaribu tena kuyafuatilia maisha yangu.
Baada ya kikao kile tukaagana na maafisa wa polisi tukatoka na kuelekea lilipo gari letu huku tumeshikana mikono.Nikamfungulia Clara mlango aingie garini lakini kabla hajaingia nikamuona Baraka akija mbio kule kwenye gari letu.
“daddy naomba usiniache nirudi tena kwa mama.naomba tuondoke wote” Baraka akasema huku akilia.Nilimuonea huruma sana mtoto yule kwa namna alivyokuwa akiteseka lakini sikuwa na jinsi ya kumsaidia.Nilibaki nikimtazama.Clara akainama na kumbembeleza
“Baraka nenda kwa mama .Mimi na baba yako tutakuja kuomba kwa mama yako ili akuruhusu ukae nasi..” Clara akamwambia Baraka ambaye akanigeukia na kuniuliza
“Eti daddy ni kweli ?
“kweli Baraka.Tutakuja kuongea na mama yako ili akuruhusu uje kukaa kule kwetu” Nikajibi na ghafla akatokea Emmy na kumnyakua Baraka kwa nguvu toka kwa Clara
“Nakwambia hivi wewe mwanamke,lazima nikuonyeshe kazi.Nitakufundisha adabu.Wewe ndiye unayempa kiburi huyu kunguru,basi jiandae kupambana na mimi” Emmy akasema kwa shari.Clara akamtazama na kutabasamu kisha akanisogelea akanikumbatia na kunipa busu moja zito.
“Let’s get out of here darling.She is crazy” Clara akasema huku akicheka kichini chini kisha tukaingia garini na kuondoka tukimuacha Emmy amevimba kwa hasira.
“Darling ,sababu iliyopelekea wewe ukaachana na yule mwanamke ni ile ile uliyonieleza au kuna sababu nyingine? Clara akauliza tukiwa garini
“Kwa nini umeuliza hivyo Clara?
“Kwa sababu naona chuki aliyokuwa nayo yule mwanamke ni kubwa sana na ya wazi.Ni kama vile anataka kukuangamiza kabisa.Ni kama vile anataka kulipiza kisasi kwa jambo baya ulilomfanyia” Clara akasema na kunifanya nitabasamu
“Clara yule mwanamke sijui anachokitafuta kwangu ni kitu gani.Kama ni chuki nilipaswa kuwa nayo mimi kwa sababu yeye ndiye aliyenifanyia mambo ya ajabu sana.Mimi sijamfanyia jambo lolote lile baya na wala hastahili kuwa na chuki na mimi.Alihitaji uhuru na nikampatia uhuru sasa tatizo liko wapi? Clara nakuomba umpuuze hayawani yule.Hana chochote cha kukufanya” Nikasema na kumfanya Clara atabasamu,akanisogelea karibu na kubusu

TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………….
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 15
MTUNZI:pATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Let’s get out of here darling.She is crazy” Clara akasema huku akicheka kichini chini kisha tukaingia garini na kuondoka tukimuacha Emmy amevimba kwa hasira.
“Darling ,sababu iliyopelekea wewe ukaachana na yule mwanamke ni ile ile uliyonieleza au kuna sababu nyingine? Clara akauliza tukiwa garini
“Kwa nini umeuliza hivyo Clara?
“Kwa sababu naona chuki aliyokuwa nayo yule mwanamke ni kubwa sana na ya wazi.Ni kama vile anataka kukuangamiza kabisa.Ni kama vile anataka kulipiza kisasi kwa jambo baya ulilomfanyia” Clara akasema na kunifanya nitabasamu
“Clara yule mwanamke sijui anachokitafuta kwangu ni kitu gani.Kama ni chuki nilipaswa kuwa nayo mimi kwa sababu yeye ndiye aliyenifanyia mambo ya ajabu sana.Mimi sijamfanyia jambo lolote lile baya na wala hastahili kuwa na chuki na mimi.Alihitaji uhuru na nikampatia uhuru sasa tatizo liko wapi? Clara nakuomba umpuuze hayawani yule.Hana chochote cha kukufanya” Nikasema na kumfanya Clara atabasamu,akanisogelea karibu na kubusu

ENDELEA……………………..

Niliendelea kumshukuru Mungu kwa kunisaidia kushinda tuhuma zile nzito alizokuwa ameziibua Emmy.Bado sikuelewa ni kwa nini Emmy alikuwa na chuki ya namna ile kwangu.Sikufahamu nilimkosea jambo gani baya kiasi cha kumfanya anichukie namna ile.Kama ni kuachana na mimi yeye ndiye aliyetaka tuachane sasa ni kwa nini anifanyie vile? Kwa nini aliahidi kuendelea kupambana na mimi? Pengine labda kile kitendo cha kuniona niko na Clara kilimuuma sana .Yawezekana alikuwa akiugulia moyoni kwa wivu.Lakini wivu wa nini kwa sababu ni yeye ndiye aliyeyaanzisha mambo yote haya.
Mawazo haya yaliendelea kuniumiza kichwa sana na mara Clara akanistua
“wayne unawaza nini?
“Mambo mengi Clara.Nawaza ni namna gani ulivyoumia moyoni kwa jambo alilolifanya Emmy.Nawaza ni namna gani nitakuomba msamaha kwa jambo la aibu kama lile.Ni siku yetu ya kwanza tu kuwa pamoja halafu unakutana na jambo kama lile na kupelekea ukafika hadi polisi na kikubwa zaidi amekufanya uahirishe hadi shughuli zako muhimu.Kila nikifikiria suala hili ninaumia sana Clara”
Clara akanitazama akatabasamu na kuunyoosha mkono wake ,akasugua sugua shingo yangu kidogo huku akisema
“Wayne naomba usikwazike kwa kitendo alichokifanya Emmy.Kwangu mimi sikuumia kwa mambo aliyoyafanya bali nilimuonea huruma sana kwa sababu hana amani moyoni kwa mambo aliyoyafanya.Kama hatabadilika basi hatakuwa na amani maishani mwake hadi siku yake ya mwisho.Mimi sina tatizo naye hata kidogo na nina imani kwamba hawezi kunifanyia kitu chochote kibaya kama alivyoahidi.Yale yalikuwa ni maneno ya kujipa moyo.Ninachokushauri kwa sasa inabidi uondoke hapa Arusha kwa muda wa mwezi mmoja au zaidi ili umsahau kabisa Emmy.Utakapofanya hivyo utakuwa umempa nafasi hata yeye mwenyewe ya kuweza kuendelea na mambo mengine yanayomuhusu kwa sababu kila atakapokuwa akijaribu kukutafuta hatakupata.”
“wazo lako zuri Clara.Hata hivyo nilikuwa na mawazo kama hayo toka zamani na niliahirisha baada ya kukutana nawe.”
“Uliahirisha safari kwa ajili yangu? Clara akauliza
“Ndiyo Clara .Nilikwisha andaa safari ya kuelekea Zanzibar mahala ambako niliamini ni sehemu nzuri na ambayo ingenifanya nisahau kabisa yote yaliyonitokea lakini nilipokutana nawe siku ile mipango yote ikavurugika.”
Clara akacheka kicheko kikubwa kama kawaida yake halafu akasema
“kama uliahirisha safari kwa ajili yangu,na mimi leo nimeahirisha safari kwa ajili yako.Ngoma droo” wote tukacheka kicheko kikubwa.
“Ulikuwa umepanga kwenda Zanzibar? Clara akaniuliza
“Ndiyo Clara nilikuwa nimepanga kwenda kupumzika Zanzibar.Nilitaka nikaishi mbali kabisa na hapa na nikaona kwamba Zanzibar ni sehemu nzuri na salama sana kwa mapumziko.”
“hata mimi sijawahi kufika Zanzibar.Unaonaje kama tukienda wote kupumzika Zanzibar? Clara akauliza.Nikamtazama na kusema.
“Kokote utakakotaka twende ,nitakuwa tayari.hata ukisema leo hii tunywe sumu tufe wote mimi niko tayari” Nikasema na kumfanya Clara acheke sana .Akafunua pochi yake na kutoa kitambaa cha mkononi na kufuta machozi yaliyotokana na kucheka
“Wayne unanifurahisha sana.You make me feel a very special woman in this world.Najisikia furaha sana.You are very special to me”
Sikujibu kitu zaidi ya kutabasamu ,halafu nikapunguza mwendo wa gari na kukata kona ya kuelekea nyumbani kwangu.
“Wayne naomba usinielewe vibaya kwa haya nitakayokwambia “ akasema Clara tukiwa tumejipumzisha kitandani nyumbani kwangu
“Nakusikiliza Clara” Nikamwambia huku nikilisugua bega lake la kulia kwa mkono wangu
“Ni muda mrefu sana nimeishi maisha yangu nikiwa mwenyewe bila kuwa na mpenzi na niliweka nadhiri kwamba sintakuwa na mtu aitwaye mpenzi katika dunia hii hadi kifo changu.Nilikuwa nikiwachukia wanaume.Niliamini wanaume wote baba yao mmoja kwa hiyo wote wako sawa.Wayne sifahamu kilinitokea kitu gani lakini baada ya kukutana na wewe nimejikuta nikiivunja nadhiri yangu.Nimejikuta nikibadili msimamo na matazamo wangu.Kilichotokea hata mimi bado nashangaa.Hata marafiki zangu wakifahamu kuhusu uhusiano wetu huu watanishangaa sana kwa sababu walielewa fika ni jinsi gani nilivyokuwa nikiwachukia wanaume.Wayne nimevunja nadhiri yangu ya kutokuwa na mwanaume na nimeamua kukukabidhi moyo wangu wewe pekee kwa kuamini kwamba uko tofauti sana na wengine.Nimekupa moyo wangu kwa sababu nakupenda sana.Nakukabidhi moyo na mwili wangu uvitunze.Nakuahidi nitakupenda hadi mwisho wa maisha yangu.Nitakuwa mwaminifu kwako hadi kifo kitutenganishe.Nitaishi nawe katika kila hali ,iwe masika kiangazi,kwenye jua na mvua.Ugonjwa na faraja sintakuacha Wayne.Pamoja na hayo yote nakuomba kitu kimoja tu”
Clara akasema kwa hisia kali huku macho yake yamejaa machozi
“Chochote utakachoomba Clara nitakutimizia.” Nikasema taratibu huku nikishika mikono yake.
“Wayne don’t ever make me cry. Promise me that you’ll never hurt me.Promise me that you’ll make me a happiest woman” Clara akasema huku amenikazia macho.Nilimtazama mrembo yule mwenye macho ya kimalaika.Macho yake yalinieleza kila kitu kilichokuwamo moyoni mwake.Nikamshika mikono yake na kumsogeza zaidi kwangu.Nikambusu na kusema
“Clara My angel naomba nikueleze ukweli kwamba hadi sasa najihisi kama vile niko ndotoni kwa sababu sikutegemea kama wanawake kama wewe bado wanaishi katika dunia hii.Baada ya kutengana na Emmy niliumia sana na sikufichi kwamba niliwachukia wanawake kupita kiasi.Kila mwanamke niliyemuona nilijenga picha kwamba ana tabia kama za Emmy.Siku ile nilipokutana nawe nilijikuta nikibadili kabisa mtazamo wangu kuhusu wanawake.Nilijikuta nikipata furaha ya ajabu na kusahau kama nilikuwa nimeumizwa muda mfupi uliopita.Toka siku ile nilikuwa naota ni namna gani ningeweza kuwa na furaha kama ningekuwa na mwananke kama wewe.Nilisali na kumuomba Mungu anirejeshee tena furaha yangu iliyopotea na leo hii amesikia sala zangu na niko nawe hapa kitandani.Clara nakupenda na ninakuahidi kwamba nitakuheshimu na kukutunza kwa sababu wewe ni kitu cha thamani kubwa maishani mwangu .Thamani yako inazidi hata ile ya Lori zima la almasi.Siku zote nitakuwa nawe na kukuenzi kama malkia wangu.Sintakuumiza na wala kukutoa machozi.nakuahidi hivyo ” Clara akanivuta kwake na kunikumbatia kwa nguvu..
Tulishinda nyumbani kwangu hadi jioni ,nikampeleka Clara hotelini alikofikia akabadili mavazi kisha tukaelekea katika klabu moja ya usiku ambako kulikuwa na muziki wa bendi.Tulicheza na kufurahi hadi saa nane za usiku kisha tukarejea hotelini kwa Clara tukalala hadi asubuhi.Sikuwahi kupata raha za namna hii katika maisha yangu.Nilimuona Clara kama malaika aliyeshushwa ili kunipa furaha maishani mwangu.
Asubuhi ya siku iliyofuata tulirejea nyumbani kwangu kwa ajili ya kubadili nguo kisha tuelekee matembezini.Tulipanga tukatembee katika bustani ya nyoka .Clara alikuwa akisikia kwamba kuna nyoka wanafugwa na hivyo alihitaji kwenda kuangalia. .
Baada ya kuingia chumbani kwangu nilihisi kama vile chumba hakikuwa sawa.Sikutilia maanani sana nikalifungua kabati na kutoa nguo nikavaa.Nikiwa naendelea kuvaa simu yangu ikaita.Nikaangalia namba za mpigaji,zilikuwa ni namba ngeni kabisa katika simu yangu.
“hallow” Nikasema baada ya kuipokea simu ile
“hallow Wayne.Ni mimi Emmy”
“Bastard ! unanitafutia nini wewe baradhuli ? Nikajikuta nikisema kwa ukali.Nilipatwa na hasira za ghafla
“Ama kweli umenichoka.Umefikia hatua ya kuniita baradhuli ? Akasema Emmy
“Emmy nakuonya . Acha kabisa kunifuata fuata katika maisha yangu.Naomba hii iwe ni mara ya mwisho kuisikia sauti yako ”
“ Nafurahi kusikia hivyo Wayne.Nafahamu sihitaji kukusumbua tena katika maisha yako.Nakuacha ule raha na mwanamitindo wako.Sintakupigia tena simu lakini nadhani wewe ndiye utakayenipigia simu na kunitafuta.Kabla sijakata simu na kuachana nawe kabisa kuna jambo naomba nikueleze ”
“unataka kunieleza nini wewe mwanamke ? nikauliza
“usiwe na haraka hivyo Wayne.Mimi ndiye niliyekupigia simu na ninaomba unisikilize.Nakuomba tafadhali unisikilize kwa makini kwa mara ya mwisho.Nafahamu una shilingi millioni mia moja na arobaini katika benki ya kimataifa ya European Africa Bank.Nafahamu ni jinsi gani ulivyozipata fedha zile na ninaufahamu mtandao wenu wote.Sitaki kukuchosha sana lakini ninakupa masaa ishirini na manne uhamishe shilingi millioni mia moja katika akaunti yangu benki ya Stanbic. Iwapo hautatekeleza hilo fahamu kwamba utakwenda mahakamani na ninakuhakikishia kwamba ni lazima utafungwa kifungo kirefu gerezani kwa sababu ushahidi wote ninao.kama huamini angalia kabati lako unalohifadhi kumbukumbu zako.Kumbuka masaa ishirini na nne Wayne ama la utafia gerezani na utamuacha mrembo wako akiponda raha na wanaume wenzako.hahahahahaa bye Wayne”
Nilikuwa nimepigwa na butwaa nikashindwa hata kufunga mkanda wa suruali nikaiacha ikaanguka chini.Jasho lilianza kunitoka.
“wayne whats wrong” Akasema Clara ambaye alistuka kutokana na mabadiliko yangu ya ghafla.
“Documents !! documents ! ……” Nikasema huku nikilivuta kabati kubwa la nguo na kwa nyuma yake nikaanza kubonyeza namba za sefu ambalo huwa natunzia kumbu kumbu zangu muhimu.Sefu hili huwa linafunguliwa na namba maalum na kwa bahati mbaya Emmy alikuwa akizifahamu
Nilitamani ardhi ipasuke niingie ndani baada ya kulifungua sefu langu na kukuta nyaraka zangu muhimu hazimo.
“damn you Emmy..” Nikaishiwa nguvu na kukaa chini.
Clara alistuka sana kwa hali niliyokuwa nayo akanisogelea na kuniuliza
“Wayne whats wrong? Sikumjibu kitu .Akakimbia na kuniletea glasi ya maji
“Kunywa maji Wayne.” Nikaishika glasi ile nikanywa maji kisha akaniinua na kunipeleka kitandani.
“My documents” Nikasema kwa uchungu
“what documents? Clara akauliza
Niliendelea kutikisa kichwa kwa hasira
“wayne document zipi hizo? Clara akaendelea kuuliza
“She was here..that bastard was here last night !! Nikasema kwa sauti kali
“Wayne nani alikuja hapa? Clara akauliza
“ Emmy” Nikajibu na kumfanya Clara astuke
“Emmy ?
“Ndiyo Emmy alikuja hapa jana usiku na amechukua nyaraka zangu muhimu sana”
“Ouh Emmy why are you doing this to me? Nikasema huku nikiuma meno kwa uchungu.
“Calm down Wayne.” Clara akasema huku akinipiga piga mgongoni.
“Wayne nyaraka hizo zilikuwa zinahusu nini? Akauliza Clara.Nilishindwa nimjibu nini.akanitazama tena na kuuliza
“Wayne hebu niambie nyaraka hizo zilikuwa zinahusu nini?
“mshenzi yule alifahamu mahala nilipokuwa naweka nyaraka zangu muhimu na amekuja kuzichukua” Nikasema
“wayne please answer me.Nyaraka hizo zilikuwa ni za nini? Pengine ninaweza kukusaidia kuzipata”
“Clara nyaraka hizo ni za muhimu sana na kama nikifanya mchezo ninaweza kufungwa.” Clara akastuka na kuniangalia kwa macho makali
“Kufungwa ?” akauliza
“Ndiyo Clara.Ninaweza kufungwa” Nikajibu
“Ufungwe kwa kupoteza nyaraka ? Clara akauliza
“Its not simple as you think Clara.This is something very serious” Nikasema huku nikiinuka pale kitandani na kwenda kusimama dirishani.Nilikuwa nikihema kwa kasi kutokana na hasira nilizokuwa nazo.
“Wayne kama amekuja Emmy na kuingia ndani mwako bila ruhusa yako na kisha akachukua nyaraka zako,basi tunaweza kusema kwamba mtu huyo ni mhalifu.Amevunja na kuiba.Twende tukamshitaki polisi haraka ili wamkamate” Clara akasema
“No Clara hili si suala la polisi.Ndiyo maana amenipigia simu na kunifahamisha kwamba nyaraka zangu anazo kwa sababu anafahamu kwamba sintaweza kwenda polisi kushitaki.”
“Why Wayne? Kwa nini usiende kumshitaki polisi wakati ameingia nyumbani kwako ,akachukua nyaraka zako na kuondoka.Huo ni uhalifu.Lets report her to the police.That’s the best way to teach her a lesson.Huwezi kumuacha mtu kama huyu .Huyu ni mhalifu na huwezi kujua anaweza hata akakuua.Ouh Wayne I’m so sacred.lets go to police” Clara akasema.Uso wake ulionyesha wasi wasi.
“hapana Clara .Hili si suala la kwenda kushitaki polisi.Hili ni suala langu mimi na yeye”
“Wayne tell me why ?? kwa nini tusimshitaki polisi ili achukuliwe hatua?
“ No Clara we cant do that” Clara akanisogelea na kusema
“Wayne niambie ni kwa nini Emmy asichukuliwe hatua kwa kosa alilolifanya? Sikujibu kitu nikainama chini
“Whats going on Wayne? Don’t tell me you are scared of her.” Nilinyamaza kimya na kumtazama Clara ambaye alianza kupata mashaka.Niliogopa kumweleza ukweli kwa sababu ilikuwa ni mapema sana kuanza kukumbana na mambo kama haya.hakupaswa kuanza kuumizwa na masuala yangu kwa muda huu mfupi.Nilimchukia Emmy kupita kiasi kwani sasa niliamini lengo lake lilikuwa ni kunifanya niishi maisha magumu .Nikiwa nimezama katka dimbwi la mawazo nikastukia bega langu likiguswa na Clara.Nikainua kichwa na kumtazama
“Wayne do you real love me? Clara akauliza
“Clara I love you more than you think” Nikajibu
“kama kweli unanipenda Wayne tell me the truth.Whats going on here.If you love and trust me tell me the truth and I’ll understand you.Hata kama umeua mtu,niambie ukweli.As far as I love you I will understand.” Clara akasema huku akinitazama usoni.
Nilimtazama usoni,nikajisikia vibaya sana.Clara hakustahili kuteseka kwa ajili yangu.macho yake yalikuwa yakitoa machozi ,nikamuonea huruma nikaamua kumweleza ukweli.
“Clara nitakueleza ukweli” Nikasema huku nikimshika mkono na kumpeleka kitandani,.Tukaa na kutazamana.
“I’m listening Wayne.” Clara akasema.Nikakohoa kidogo kusafisha koo langu kisha nikasema
“Hapo awali nilikuwa nafanya kazi katika halmashauri ya jiji la Arusha nikiwa katika kitengo cha ukarabati wa miundombinu.Mimi ndiye niliyekuwa nikiratibu shughuli zote za ukarabati wa miundombinu mbalimbali ya halmashauri ya jiji kama vile barabara n.k.Miaka mitatu iliyopita aliletwa mkurugenzi mpya ambaye kwa sasa ni marehemu.Mkurugenzi huyu ambaye naweza kusema kwamba ndiye aliyenifundisha namna ya kubuni miradi hewa na kuingiza mfukoni pesa ya halmashauri.Akiwa kama kiongozi ,aliunda mtandao wa watu ambao kwa pamoja tulishirikiana katika kubuni miradi mingi ambayo haikuwepo au kama ilikuwepo basi ilikarabatiwa au kujengwa kwa kiwango cha chini sana tofauti na gharama zilizoainishwa katika taarifa za mradi.Tulitengeneza fedha nyingi sana.Tulibuni miradi mingi iliyogharmu mabilioni ya shilingi lakini mingi kati ya hiyo haikuwepo na au ilikuwa ya kiwango cha chini sana.Haikuwa rahisi kugunduliwa kwa sababu mkaguzi mkuu wa ndani wa halmashauri na wahasibu wote walikuwa katika mtandao wetu hivyo kila ripoti za ukaguzi zilipohitajika zilipelekwa ripoti nzuri na za kufurahisha.Ilitokea bahati mbaya mkaguzi wetu wa ndani alihamishwa na kuletwa mkaguzi mwingine ambaye hakuweza kushirikiana na sisi hivyo kutaka kutibua mambo.Ili kulizima sakata hilo ikatulazimu kuwanyamazisha huyo mkaguzi pamoja na mkurugenzi .Baada ya hapo nikaacha kazi halmashauri na kutafuta kazi mahala kwingine.Wakati mambo yote haya yanafanyika nilimshirikisha Emmy kama mke wangu katika kila kitu.Alichokifanya Emmy ,jana usiku amekuja na kuchukua nyaraka zangu zote muhimu na anazo kwa sasa.Alikuwa akifahamu kwamba nina shilingi millioni mia moja na ishirini benki ambazo nilizipata wakati ninafanya kazi halmashauri.Anataka nihamishie shilingi milioni mia moja katika akaunti yake ya benki na nisipofanya hivyo ataripoti suala hili polisi.Amenipa saa ishirini na nne niwe nimetekeleza hilo agizo”
Nilimaliza kumweleza ukweli Clara ambaye akainuka na kushika kichwa chake kwa mikono yake miwili.
“Ouh my god ! what a scandal.Why me? “ Clara akasema kwa hali ya kukata tamaa.Nilihisi kuchanganyikiwa.
Clara akavuta pumzi ndefu akaenda kukaa kitandani,akainama na kujishika kichwa kwa mikono yake miwili.Sikuelewa alikuwa akiwaza kitu gani lakini ni wazi alikuwa katika hali ya kukata tamaa.Aliumizwa mno na maneno niliyomwambia.Nilimtazama kwa makini huruma ikaniingia.Clara alikuwa akiishi maisha yake kwa raha mustarehe na hakuwa na matatizo .Aliogopa kuingia katika mahusiano tena baada ya kutendwa katika uhusiano wake wa awali.Japokuwa hajawahi kunieleza ni kitu gani kilimtokea hapo kabla kiasi cha kumfanya awachukie wanaume lakini ni wazi kitu alichofanyiwa kilimuumiza sana kiasi cha kumfanya awachukie wanaume wote .Baada ya miaka kadhaa kupita ameamua kumuamini na kumpa mwanaume mwingine nafasi katika moyo wake,mwanaume huyo ni mimi.Siku mbili tu tangu awe na mimi amekutana na mambo ambayo yametonesha donda lililokwisha pona muda mrefu.Clara amejikuta akiuumiza tena moyo wake.Jana nilituhumiwa kumchukua mtoto Baraka bila ridhaa ya wazazi wake kitu kilichopelekea kushikiliwa na polisi kwa masaa kadhaa tukihojiwa.Kutokana na sakata hilo Clara aliahirisha safari yake ya muhimu sana.Leo hii limeibuka tena jambo jingine jipya.Sikuhitaji kumuumiza Clara namna ile lakini sikuwa na namna nyingine ya kufanya zaidi ya kumueleza ukweli.Sikuona umuhimu wa kumficha kitu kwa sababu hata kama ningeficha ingekuja kufahamika tu.

TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………………
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom