Simulizi - Umepima ?

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
“ Dear naomba uje “
“ nije ? kuna nini tena mama Vanessa ?”
“ wewe njoo wasi wasi wako nini ?”
“ sawa nimeshakuja nieleze mama Vanessa “

“ Unakumbuka nilivyokuwa nakuambia naumwa sana ?”
“ ndio nakumbuka si ulienda kupima leo ?
“ yes nilienda kupima leo ndio nimekuja na majibu “

“ duh ndio umekuja na majibu mbona wanitisha mrembo ?”
“ nakutisha na nini si nimekuja na majibu tu uko tayari kuyapokea ?”
“ mhh mama Vanessa mbona unaniuliza hivyo ?”
“ nimekuuliza uko tayari kuyapokea au nisikuambie ?”
“ subiri kwanza nifikirie “

Wanandoa wengi au watu wengi walio katika mahusiano hawajui jinsi ya kumweleza mpenzi wake jambo Fulani linalohusu afya yake kama hapa hadithi yetu inavyoendelea , baba Vanessa hana uhakika kama apewe majibu au la kama yuko katika ndoa kuna ubaya gani kupokea majibu ?

“ mama vanesa naona tulale kesho uniambie “
“ kesho si unaweza kushindwa kwenda kazini bora nikuambie sana baba watoto “
“ hapana sasa hivi moyo wangu unaenda mbio sitaki “

Unaona ? mtu yuko katika ndoa lakini anaogopa kujua afya ya mke wake sasa nini maana ya ndoa ? si kushirikiana ? hapa ushirikiano upo kweli ? jibu ni kwamba hakuna baba Vanessa anaogopa majibu

“ Haya basi niambie mpenzi wangu “
“ baba Vanessa nimeathirika na ugonjwa “
“ mhh – ugonjwa gani umeathirika nao ?”
“ ukimwi ?”

“ aaaaha baba Vanessa mbona unanipiga ?”
“ umeupata wapi huu ukimwi ?”
“ sijamaliza kukuelezea mbona umeaza ugomvi ?”
“ baba Vanessa siwezi kusema chochote wala lolote mpaka na wewe ukapime “

“ sikia mama Vanessa mimi siendi kupima sina ukimwi kwani umeniona nikiumwa ?”
“ baba Vanessa , wewe huwa unasafiri sana maeneo mengi na sijui kuhusu afya yako kwa muda mrefu sasa mbona hivyo leo ?”
“ aaaaaahhh , baba Vanessa utaniua “
“ ndio leo lazima unikome yaani umeambukizwa ukimwi huko na watu wengine unasema mimi ?”
“ sijasema kama wewe ndio umeniambukiza nimekuambia na wewe ukapime tuwe na uhakika na afya zetu ili tuishi kwa amani na furaha “
“ nimeshasema siendi kupima halafu beba vitu vyako uondoke naona ndoa yetu imefikia kikomo usiku wa leo mama Vanessa , na nikiona umeniambukiza ukimwi nakuja kukuwa huko huko kwenu umesikia ? mbwa we “

“ Leo ndio unaniita mbwa ? “
“ ndio wewe mbwa tena mbwa jike , sitaki uongee na mimi sasa hivi naomba ujiandae kuondoka sikutaki tena ntakuletea talaka kwenu “

ASUBUHI IKAFIKA

“ Haya dear kwahere , nilikupenda na kukupa kila kitu bora uondoke na ukimwi wako huko huko , kwani nani anataka magonjwa na maradhi nyumbani kwake ? uniambukize mimi na watoto wangu ? si ajabu umeshawaambukiza pia kwanza hakuna kupanda gari langu nakuletea taxi ije kukubeba “

“ nimekuchukua kwenu huna kitu umekuja hapa kufanya umalaya na sasa unaondoka kwangu na kitu kitu chenyewe ni hicho ukimwi , tafadhali usiniangalie nikiongea angalia pembeni kule sawa ? Mbwa we

“Taxi naomba umpeleke huyo mbwa standi ya basi apande basi aondoke kwao hela yako hii chukuwa chenji mpe huyo huyo mbwa ondoka nae kimbiza gari manake akiendelea kukaa hapa ndio napandwa na hasira zaidi “.

MIEZI 5 TOKA MAMA VANESSA AONDOKE

Barua toka kwa Baba Vannessa kwenda kwa Aliyekuwa mama Vanessa

Habari mama Vanessa

Sijui kama unaendelea vizuri na maisha au sijui maisha yako yameenda mramba toka tufukuzane enzi zile , kwa kweli nilifikiria mara mbili na nyingi zaidi kwanini nilikufukuza siku zile kama mbwa na matusi mazito kwako wewe , na jinsi nilivyokupiga na kashfa nyingine nzito nilizokupa nilikosea sana siku zile baadaye nilikaa na kuona ukweli kwamba nimekukosea lakini sikupata njia za kuwasiliana na wewe ili tuongee vizuri mpenzi wangu .

Nilipitiwa na shetani wakati ule na kwa kweli sikuwa na jinsi ya kumzuia yule shetani nilimuacha tu aniingilie na aanze kufanya kazi katika mawazo yangu mpaka nilipokuja kupata ukweli na huyo shetani kutoka katika maisha yangu na akili yangu

Mama Vanessa sijui kama utanielewa .

Kuna siku nilienda safarini Nairobi , nikiwa na rafiki yangu tulikunywa sana pombe tukalewa kisha tukaenda katika kumbi moja ya starehe pale tulichukuwa wasichana wanaojiuza kila mtu alienda na wake kulala nae usiku huo kuanzia siku hiyo nikazoea kwa miaka 4 mfululizo nikienda Kenya nikawa napitia ile clabu na kuchukuwa wasichana kwa ajili ya kujipumzisha nao usiku kucha kwa siku 4 hivi na siku zote ninazokuwa kule .

Nilizoeana nao sana nikawafanya kama wake zangu hata mapenzi tulikuwa hatufanyi tena kwa kutumia kinga na sikuwa na wasi wasi wowote juu ya maisha yangu kwanza sikuamini kama kulikuwa na kitu kinaitwa ukimwi kwa sababu sikuwahi kuona mfano nilisikia tu watu wanaongelea ukimwi na kadhalika sikuwa na uhakika wa uwepo wake kabisa .

Sasa hivi niko zangu hapa nyumbani na mimi hali imezidi kuwa mbaya nimeathirika ndio najaribu kutumia dawa za kuongeza maisha na kuhudhuria kwa waganga wa kienyeji kwa sana naona hata nafuu sipati wala ahueni

Pesa zangu zote sasa karibu zinaisha kwa sababu nyingi nimetumia kwedna kwa waganga na kununulia dawa za kuongeza nguvu mpenzi wangu , yaaani machozi yananitoka na kulia nashindwa lakini nifanyeje ?

Watoto wetu wanahitaji matunzo na malezi bora kwenda shule na kufundishwa maadili mema , mama yao ambaye alikuwa anaishi nao nyumbani saa zote ndio wewe nilishakukimbiza roho inaniuma sana mpenzi wangu

Nilikuwa nakuomba kama unaweza nisamehe na usahau yaliyopita urudi nyumbani tuendelee na maisha yetu mpaka hapo ndoa itakapokuja kutunganisha hali imeshakuwa hivi hakuna la kufanya zaidi ya kuwa wote tena mpenzi wangu mimi nalia sana

Nimeshaona makosa yangu na nimeshakusamehe basi naomba na wewe unisamehe kama una moyo huo wa huruma urudi nyumbani tuishi pamoja tena dear wangu

Nafikiri umenielewa mpenzi

Mama vanessaa

Ni mimi

Baba Vanessa
 
very sad story...
i like stories with happy endings...
(Hizi zinani sikitisha sana)
 
Afu huyu dudumizi kamaliza watu jamani .........sijui tufanyeje .........tuelewe hili somo
 
Asanye sana Shy kwa hadithi fupi lakini nzuri lakini mbona hujamalizia hadithi yako mama Vanessa aliipokeaje hiyo barua na je alimsamehe mmewe na kuanza maisha mapya ?
 
Very sad story. Hapo Baba Vanesa alichofanya ndio hufanywa na mtu yoyote mwanaume au mwanamke atakayeelezwa na mwenzie kuwa ameathirika na wewe nenda kapime. UKIMWI si mchezo kuambiwa unao lazima utapanic tu hata uwe na roho gani. Tujifunze katika hili
 
" Dear naomba uje "
" nije ? kuna nini tena mama Vanessa ?"
" wewe njoo wasi wasi wako nini ?"
" sawa nimeshakuja nieleze mama Vanessa "

" Unakumbuka nilivyokuwa nakuambia naumwa sana ?"
" ndio nakumbuka si ulienda kupima leo ?
" yes nilienda kupima leo ndio nimekuja na majibu "

" duh ndio umekuja na majibu mbona wanitisha mrembo ?"
" nakutisha na nini si nimekuja na majibu tu uko tayari kuyapokea ?"
" mhh mama Vanessa mbona unaniuliza hivyo ?"
" nimekuuliza uko tayari kuyapokea au nisikuambie ?"
" subiri kwanza nifikirie "

Wanandoa wengi au watu wengi walio katika mahusiano hawajui jinsi ya kumweleza mpenzi wake jambo Fulani linalohusu afya yake kama hapa hadithi yetu inavyoendelea , baba Vanessa hana uhakika kama apewe majibu au la kama yuko katika ndoa kuna ubaya gani kupokea majibu ?

" mama vanesa naona tulale kesho uniambie "
" kesho si unaweza kushindwa kwenda kazini bora nikuambie sana baba watoto "
" hapana sasa hivi moyo wangu unaenda mbio sitaki "

Unaona ? mtu yuko katika ndoa lakini anaogopa kujua afya ya mke wake sasa nini maana ya ndoa ? si kushirikiana ? hapa ushirikiano upo kweli ? jibu ni kwamba hakuna baba Vanessa anaogopa majibu

" Haya basi niambie mpenzi wangu "
" baba Vanessa nimeathirika na ugonjwa "
" mhh – ugonjwa gani umeathirika nao ?"
" ukimwi ?"

" aaaaha baba Vanessa mbona unanipiga ?"
" umeupata wapi huu ukimwi ?"
" sijamaliza kukuelezea mbona umeaza ugomvi ?"
" baba Vanessa siwezi kusema chochote wala lolote mpaka na wewe ukapime "

" sikia mama Vanessa mimi siendi kupima sina ukimwi kwani umeniona nikiumwa ?"
" baba Vanessa , wewe huwa unasafiri sana maeneo mengi na sijui kuhusu afya yako kwa muda mrefu sasa mbona hivyo leo ?"
" aaaaaahhh , baba Vanessa utaniua "
" ndio leo lazima unikome yaani umeambukizwa ukimwi huko na watu wengine unasema mimi ?"
" sijasema kama wewe ndio umeniambukiza nimekuambia na wewe ukapime tuwe na uhakika na afya zetu ili tuishi kwa amani na furaha "
" nimeshasema siendi kupima halafu beba vitu vyako uondoke naona ndoa yetu imefikia kikomo usiku wa leo mama Vanessa , na nikiona umeniambukiza ukimwi nakuja kukuwa huko huko kwenu umesikia ? mbwa we "

" Leo ndio unaniita mbwa ? "
" ndio wewe mbwa tena mbwa jike , sitaki uongee na mimi sasa hivi naomba ujiandae kuondoka sikutaki tena ntakuletea talaka kwenu "

ASUBUHI IKAFIKA

" Haya dear kwahere , nilikupenda na kukupa kila kitu bora uondoke na ukimwi wako huko huko , kwani nani anataka magonjwa na maradhi nyumbani kwake ? uniambukize mimi na watoto wangu ? si ajabu umeshawaambukiza pia kwanza hakuna kupanda gari langu nakuletea taxi ije kukubeba "

" nimekuchukua kwenu huna kitu umekuja hapa kufanya umalaya na sasa unaondoka kwangu na kitu kitu chenyewe ni hicho ukimwi , tafadhali usiniangalie nikiongea angalia pembeni kule sawa ? Mbwa we

"Taxi naomba umpeleke huyo mbwa standi ya basi apande basi aondoke kwao hela yako hii chukuwa chenji mpe huyo huyo mbwa ondoka nae kimbiza gari manake akiendelea kukaa hapa ndio napandwa na hasira zaidi ".

MIEZI 5 TOKA MAMA VANESSA AONDOKE

Barua toka kwa Baba Vannessa kwenda kwa Aliyekuwa mama Vanessa

Habari mama Vanessa

Sijui kama unaendelea vizuri na maisha au sijui maisha yako yameenda mramba toka tufukuzane enzi zile , kwa kweli nilifikiria mara mbili na nyingi zaidi kwanini nilikufukuza siku zile kama mbwa na matusi mazito kwako wewe , na jinsi nilivyokupiga na kashfa nyingine nzito nilizokupa nilikosea sana siku zile baadaye nilikaa na kuona ukweli kwamba nimekukosea lakini sikupata njia za kuwasiliana na wewe ili tuongee vizuri mpenzi wangu .

Nilipitiwa na shetani wakati ule na kwa kweli sikuwa na jinsi ya kumzuia yule shetani nilimuacha tu aniingilie na aanze kufanya kazi katika mawazo yangu mpaka nilipokuja kupata ukweli na huyo shetani kutoka katika maisha yangu na akili yangu

Mama Vanessa sijui kama utanielewa .

Kuna siku nilienda safarini Nairobi , nikiwa na rafiki yangu tulikunywa sana pombe tukalewa kisha tukaenda katika kumbi moja ya starehe pale tulichukuwa wasichana wanaojiuza kila mtu alienda na wake kulala nae usiku huo kuanzia siku hiyo nikazoea kwa miaka 4 mfululizo nikienda Kenya nikawa napitia ile clabu na kuchukuwa wasichana kwa ajili ya kujipumzisha nao usiku kucha kwa siku 4 hivi na siku zote ninazokuwa kule .

Nilizoeana nao sana nikawafanya kama wake zangu hata mapenzi tulikuwa hatufanyi tena kwa kutumia kinga na sikuwa na wasi wasi wowote juu ya maisha yangu kwanza sikuamini kama kulikuwa na kitu kinaitwa ukimwi kwa sababu sikuwahi kuona mfano nilisikia tu watu wanaongelea ukimwi na kadhalika sikuwa na uhakika wa uwepo wake kabisa .

Sasa hivi niko zangu hapa nyumbani na mimi hali imezidi kuwa mbaya nimeathirika ndio najaribu kutumia dawa za kuongeza maisha na kuhudhuria kwa waganga wa kienyeji kwa sana naona hata nafuu sipati wala ahueni

Pesa zangu zote sasa karibu zinaisha kwa sababu nyingi nimetumia kwedna kwa waganga na kununulia dawa za kuongeza nguvu mpenzi wangu , yaaani machozi yananitoka na kulia nashindwa lakini nifanyeje ?

Watoto wetu wanahitaji matunzo na malezi bora kwenda shule na kufundishwa maadili mema , mama yao ambaye alikuwa anaishi nao nyumbani saa zote ndio wewe nilishakukimbiza roho inaniuma sana mpenzi wangu

Nilikuwa nakuomba kama unaweza nisamehe na usahau yaliyopita urudi nyumbani tuendelee na maisha yetu mpaka hapo ndoa itakapokuja kutunganisha hali imeshakuwa hivi hakuna la kufanya zaidi ya kuwa wote tena mpenzi wangu mimi nalia sana

Nimeshaona makosa yangu na nimeshakusamehe basi naomba na wewe unisamehe kama una moyo huo wa huruma urudi nyumbani tuishi pamoja tena dear wangu

Nafikiri umenielewa mpenzi

Mama vanessaa

Ni mimi

Baba Vanessa

kaaaaaaaaazi kweli kweli
 
dah,so touching aisee!asante kwa kunikumbusha wajibu wangu maana sometimes nasahau pia
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom