Simulizi : Ukweli Wenye Kuuma (Painful Truth)

SEHEMU YA 108

yakaonekana kubadilika, Andy akaanza kutafutwa kwa ajili ya kurudishwa hospitalini na kuendelea na kazi yake kama kawaida ya kuwaokoa wamarekani wengi ambao walikuwa wameathiriwa na ugonjwa wa kansa.
Andy hakuonekana kabisa japokuwa alitafutwa katika kila sehemu. Matangazo yakaanza kutolewa kwamba popote alipokuwa alikuwa akihitajika kwa ajili ya kuokoa maisha ya watu ambao walikuwa wakizidi kufa kwa kansa. Ingawa kila siku tangazo lile lilikuwa likitolewa lakini Andy hakujitokeza kutoka alipokuwa japokuwa alikuwa akiliona tangazo lile.
“Kuna nini?” Kamanda mkuu aliuliza mara baada ya kupokea simu kutoka katika shirika la habari la CNN.
“Kuna mkanda umeletwa hapa” Mwandishi wa habari wa shirika hilo alijibu.
“Mkanda gani?”
“Njoo uuone. Unamhusu Andy”
Kamanda Simons hakutaka kuendelea kukaa ofisini mwake, akainuka na moja kwa moja kutoka nje kwa ajili ya kwenda kuuangalia mkanda huo. Maswali mengi yakaanza kumiminika kichwani mwake juu ya huo mkanda, ulikuwa ukizungumzia nini?
Mara baada ya kusaifiri kwa ndege mpaka kufika Atalanta, moja kwa moja akaanza kuelekea katika kituo kikubwa cha shirika hilo la habari na kisha kuelekea kule alipokuwa akihitajika. Alipoufikia mlango akaugonga na kukaribishwa ndani katika chumba ambacho waandishi wengi wa habari walikuwa wamejazana kana kwamba kulikuwa na kitu kinaendelea.
“Vipi?” Simons aliuliza.
“Kuna mkanda umeletwa ofisini”
“Unahusu nini?”
“Andy amejirekodi. Ameuita UKWELI WENYE KUUMA”
“Mungu wangu! Ukweli gani huo aliouzungumzia? Amesemaje?”
“Anachokitaka yeye ni kwamba mkanda huu tuurushe hewani ili dunia ijue kila kinachoendelea” Mkurugenzi wa shirika lile, Peters alijibu.
“Amezungumzia nini?”
“Mambo ya ajabu, mambo yanayotisha sana”
“Mmmh! Hebu uweke tuuone kabla ya kuurusha hewani” Simons aisema na kisha mkanda kuwekwa.
Mkanda ule wa saa moja ulikuwa ukimuonyesha Andy, tena akiwa katika sura yake halisi. Alikuwa akiongea huku akilia tu. Aliongea kuhusu historia yake toka kipindi ambacho alikuwa amezaliwa mpaka katika kipindi hicho. Hakuficha kitu chochote kile, aliuelezea uhusiano wake na Annastazia, akaelezea kuhusu virusi vya katapillar ambavyo vilikuwa vikieneza ugonjwa wa PENINA.
Andy hakuficha, alieleza kila kitu jambo ambalo lilimfanya kila mtu kushika kinywa kwa mshtuko. Bwana Simons ndiye ambaye alionekana kushtua zaidi, hakuamini kama Andy ndiye ambaye alikuwa nyuma ya kila kitu kilichotokea. Maneno yake ambayo alikuwa ameongea katika mkanda ule yalionekana kumshtua kila aliyekuwa akiuangalia na kuusikiliza.
“Urushe haraka sana” Simons alimwambia Peters huku akionekana kuchanganyikiwa.
Kichwa chake kilikuwa kinauma kwa wakati huo, Andy akaonekana kuwa tatizo kubwa kwa wakati huo. Mkanda ule ukaanza kurushwa, watu walipoona kwamba ni habari zilizofika punde tena zilizomhusu Andy, watu wakatulia katika televisheni zao. Picha ya Andy ilipoonekana tu, kila mmoja alionekana kumuhitaji.
 
SEHEMU YA 109

Maneno ambayo yalikuwa yakiongelewa na Andy yalionekana kumuumiza kila mtu, hapo ndipo walipojua kwamba Andy ndiye alikuwa nyuma ya kila kitu. Magonjwa mawili ambayo yalikuwa yakiusumbua dunia kwa wakati huo, dawa ilikuwa ikipatikana kwa mtu mmoja tu, Andy.
“Mtu mbaya ndiye mtu mzuri. Sasa afanywe nini huyu?” Jamaa mmoja aliuliza.
“Tuangalie kwanza umuhimu. Ni lazima tufikirie sana kwamba ni kitu gani kikifanyika kitakuwa suluhisho, kuuawa au kuachwa hai” Jamaa alimjibu mwenzake.
Hiyo ndio hali ambayo ilionekana kusumbua vichwa vya watu duniani kwa wakati huo. Magonjwa hayo mawili yalizidi kuwamaliza watu kupita kawaida. Hakukuwa na jinsi, kwa kuwa Tanzania ilionekana kuwa nchi ndogo ambayo ilikuwa ikitaka Andy akamatwe na kuhukumiwa kifo, ombi lao likafichwa chini ya kapeti, watu walichokuwa wakikitaka kwa wakati huo ni kumuona Andy akirudi na kuendelea na utengenezaji wa dawa za magonjwa yale.
Matangazo yalizidi kutolewa zaidi na zaidi kumtaka Andy ajitokeze lakini bado alikuwa kimya hali ambayo ilimchanganya kila mtu.
*****
Maisha ya chini ya andaki bado yalikuwa yakiendelea kama kawaida. Muda mwingi Andy alikuwa akionekana kuwa na mawazo kupita kawaida. Kitu ambacho alikuwa ameamua na mke wake, Sofia kwa wakati huo ni kujirekodi na kuelezea kila kitu ambacho kilikuwa kimetokea katika maisha yake. Wakafungua mlango wa kutokea ndani ya chumba chao na kisha kutoka na kuanza kutafuta kamera ndani ya nyumba ile na kujirekodi.
“Huu ndio ukweli wangu ambao utakwenda kuwaumiza watu wengi duniani” Andy alisema mara baada ya kamera kuanza kumchukua.
Andy akaanza kuelezea, kila kitu ambacho alikuwa akikielezea katika kipindi hicho alikuwa akilia tu, maneno ambayo alikuwa akiyaongea yalikuwa yakimuumiza hata yeye mwenyewe. Si yeye tu aliyekuwa akilia, bali hata mke wake, Sofia alikuwa akiumia kupita kawaida. Ni kweli alikuwa ameangamiza watu wengi duniani lakini katika kipindi hicho hakutakiwa kuuawa.
Kama angeuawa lisingekuwa suluhisho kabisa kwani watu wengi wangezidi kufa ila kama angeachwa hai basi watu wengi wangetibiwa juu ya magonjwa yale ambayo yalikuwa yakiwasumbua. Mkanda ulichukua dakika thelathini na ndipo ambapo wakampa mfanyakazi wa nyumba yao na kumuambia aupeleke katika jengo la shirika la habari la Cnn na kuwaambia kwamba waurushe hewani ili dunia nzima ijue ni kitu gani ambacho kilikuwa kimetokea.
*****
Watu walikuwa wakihuzunika kupita kawaida huku wengine wakilia kupita kawaida. Kitendo cha kuuona mkanda ule ambao alikuwa ameurekodi Andy kwamba yeye ndiye alikuwa nyuma ya kila kitu kilichokuwa kikitokea kuhusiana na ugonjwa mbaya wa PENINA kilionekana kuwauma kupita kawaida.
Ugonjwa ule ulikuwa umemaliza watu wengi duniani, kwa kipindi hicho dawa za ugonjwa ule zilikuwa adimu sana kupatikana na hata kama zilikuwa zikipatikana basi zilikuwa na gharama kubwa kiasi ambacho watu maskini hawakuweza kuzinunua.
 
SEHEMU YA 110 MWISHO

Maanamano yakaanza kufanyika mitaani katika nchi ya New York huku yakimtaka Andy ajitoe kule alipojificha ili aje kuiokoa dunia kutokana na janga kubwa la magonjwa ambalo lilikuwa limeikumba dunia hii. Maandamano yale yalipoonekana yakiendelea kufanyika kila siku nchini Marekani, nao nchi nyingine zikaanza kuandamana, na mwisho wa siku nusu na robo ya nchi duniani zilikuwa zikiandamana.
Si Andy wala mke wake ambaye walitoka kutoka kule walipokuwa, bado waliendelea kujificha huku wakiangalia hali inaendelea vipi. Ugonjwa wa PENINA na magonjwa ya kansa ndio yalikuwa magonjwa ambayo yaliwamaliza sana, watu walizidi kuteketea kila siku jambo ambalo uhitaji wa Andy ulikuwa ukizidi kuongezeka.
Mwezi wa kwanza ukapita na ndipo kipindi ambacho Andy akaanza kujitokeza. Ilionekana kuwa furaha ya dunia, matumaini ambayo yalikuwa yamepotea mioyoni mwa watu yakaanza kurudi tena. Waandishi wa habari wakaanza kukusanyika nyumbani kwake, Washington kwa ajili ya kufanya nae mahojiano. Siku hiyo Andy aliongea mambo mengi sana huku akimtaja Dawson kuwa mtu ambaye alimfanyia ushawishi mkubwa wa kutengeneza virusi vile vya Katapillar.
Mapolisi hawakutaka kukaa kimya, walichokifanya ni kufanya maandalizi ya kumkamata Bwana Dawson kwa sababu alionekana kuwa chanzo cha kila kitu. Andy hakukamatwa japokuwa alionekana kuwa na makosa makubwa. Makosa yote ya kuangamiza mamilioni ya watu duniani yakaonekana kusahaulika.
“Bora alivyoua mamilioni ili aokoe mabilioni” Mwananchi mmoja aliwaambia wenzake maneno ambayo alitaka yaandikwe kwenye bango lake huku akijiandaa na maandamano.
Siku mbili baadae, Andy akaitwa Ikulu na kula chakula cha jioni na mheshimiwa rais wa nchi hiyo na baada ya siku mbili kazi ya kutengeneza dawa ikaanza rasmi. Hiyo ikaonekana kuwa neema kwa watu wote duniani, mara baada ya kila kitu kukamilika, dawa zikaanza kusambazwa dunia nzima, haikujalisha kama ulikuwa masikini au tajiri, dawa zile zilikuwa zikipatikana bure kabisa.
Andy hakuishia hapo, akaanza kutengeneza dawa nyingi za magonjwa ya kansa ambazo zilikuwa na nguvu kupita kawaida. Kila dawa ambayo alikuwa akiitengeneza ilikuwa ikipatikana bure na serikali ya Marekani ndio ambayo ilikuwa ikimlipa. Faraja ikaonekana kurejea duniani, watu ambao walikuwa wametumia dawa zile walikuwa wamepona kabisa.
Lengo kubwa la Andy katika kipindi hicho lilikuwa ni kuupoteza kabisa ugonjwa wa PENINA. Alitengeneza dawa usiku na mchana. Kwa sababu yeye ndiye ambaye alikuwa ameutengeneza ugonjwa ule, alitakiwa kuua kwa mikono yake mwenyewe.
Kutoka asilimia thelathini ya watu ambao waliuwa wameambukizwa ugonjwa ule duniani mpaka kufikia asilimia tano ilionekana kuwa kazi kubwa kupita kiasi. Andy hakupata muda mwingi wa kupumzika, bado alikuwa akiendelea kutengeneza dawa zaidi na zaidi.
Maisha yake yaliendelea hivyo hivyo, alizidi kutengeneza dawa zaidi na zaidi. Bwana Wayne na mke wake, Bi Happy walionekana kuwa na furaha kumuona tena mtoto wao machoni mwao. Kwa sababu alikuwa amekiri kila kitu ambacho kilikuwa kimetokea, wote tena kwa moyo mmoja wakamsamehe na kuendelea na maisha yake kama kawaida mpaka pale ambapo alikuwa kupata mtoto wa kwanza wa kike ambaye alimpa jina la Loveness.
Maisha yaliendelea kama kawaida, kila kitu ambacho kilikuwa kimetokea katika maisha yake kaamua kukisahau. Nchi ya Marekani pamoja na Umoja wa Mataifa ukawa umemkingia kifua Andy. Hata nchi ya Tanzania ilipokuwa ikilalamika kuhusiana na Angy, hakukuwa na mtu yeyote ambaye aliwaelewa.
Dawa zikatengenezwa za kutosha, Andy akaamua kufungua chuo cha uuguzi nchini Marekani na kuwafundisha wanafunzi namna ya kutengeneza dawa mbalimbali za kuua baadhi ya magonjwa. Ndani ya mwaka mmoja, wanafunzi wote ambao walikuwa wakitoka katika chuo chake alikuwa akiwaajiri katika hospitali yake jambo ambalo lilimfanya kumuingizia fedha kupita kawaida.

**SEMA LOLOTE KUHUSIANA NA SIMULIZI HII...maoni yako

MWISHO
 
KURA*KURA KURA** 🔥 🔥 🔥

SIMULIZI TATU ZA MWISHO, MSIMU HUU WA PILI, BAADA YA KUTUMA SIMULIZI SABA JAMII FORUM NA BURE SERIES

CHAGUA SIMULIZI IPI TUANZE NAYO.

1. SAFARI NDEFU KUELEKEA KABURINI - NYEMO CHILONGANI ~ Simulizi ya Kusisimua

2. DEAD LOVE ( PENZI LILILOKUFA ) - AZIZ HASHIM ~ Simulizi ya Maisha

3. MIKONONI MWA NUNDA - BEN R. MTOBWA ~ Simulizi ya Kijasusi

4. OOH!! KUMBE TAMU - YONA FUNDI ~ Simulizi ya Mapenzi




Simulizi yenye kura 10. itatumwa, kura hazijafika 10 msimu wa pili utaishia hapa.
 
CHAGUA SIMULIZI IPI TUANZE NAYO.

SAFARI NDEFU KUELEKEA KABURINI - NYEMO CHILONGANI ~ Simulizi ya Kusisimua
......(Kura 0/10)

DEAD LOVE ( PENZI LILILOKUFA ) - AZIZ HASHIM ~ Simulizi ya Maisha.
.....(Kura 0/10)

MIKONONI MWA NUNDA - BEN R. MTOBWA ~ Simulizi ya Kijasusi
......(Kura 3/10)

OOH!! KUMBE TAMU - YONA FUNDI ~ Simulizi ya Mapenzi.
.....(Kura 0/10)

Simulizi yenye kura 10. itatumwa, kura hazijafika 10 msimu wa pili utaishia hapa
 
Bado tunaendelea na Uchaguzi, Simulizi yenye kura 10 itarusha, tupia kura yako.

SAFARI NDEFU KUELEKEA KABURINI - NYEMO CHILONGANI ~ Simulizi ya Kusisimua ......(Kura 2/10)

DEAD LOVE ( PENZI LILILOKUFA ) - AZIZ HASHIM ~ Simulizi ya Maisha......(Kura 0/10)

MIKONONI MWA NUNDA - BEN R. MTOBWA ~ Simulizi ya Kijasusi......(Kura 4/10)


OOH!! KUMBE TAMU - YONA FUNDI ~ Simulizi ya Mapenzi......(Kura 0/10)
 
SEHEMU YA 110 MWISHO

Maanamano yakaanza kufanyika mitaani katika nchi ya New York huku yakimtaka Andy ajitoe kule alipojificha ili aje kuiokoa dunia kutokana na janga kubwa la magonjwa ambalo lilikuwa limeikumba dunia hii. Maandamano yale yalipoonekana yakiendelea kufanyika kila siku nchini Marekani, nao nchi nyingine zikaanza kuandamana, na mwisho wa siku nusu na robo ya nchi duniani zilikuwa zikiandamana.
Si Andy wala mke wake ambaye walitoka kutoka kule walipokuwa, bado waliendelea kujificha huku wakiangalia hali inaendelea vipi. Ugonjwa wa PENINA na magonjwa ya kansa ndio yalikuwa magonjwa ambayo yaliwamaliza sana, watu walizidi kuteketea kila siku jambo ambalo uhitaji wa Andy ulikuwa ukizidi kuongezeka.
Mwezi wa kwanza ukapita na ndipo kipindi ambacho Andy akaanza kujitokeza. Ilionekana kuwa furaha ya dunia, matumaini ambayo yalikuwa yamepotea mioyoni mwa watu yakaanza kurudi tena. Waandishi wa habari wakaanza kukusanyika nyumbani kwake, Washington kwa ajili ya kufanya nae mahojiano. Siku hiyo Andy aliongea mambo mengi sana huku akimtaja Dawson kuwa mtu ambaye alimfanyia ushawishi mkubwa wa kutengeneza virusi vile vya Katapillar.
Mapolisi hawakutaka kukaa kimya, walichokifanya ni kufanya maandalizi ya kumkamata Bwana Dawson kwa sababu alionekana kuwa chanzo cha kila kitu. Andy hakukamatwa japokuwa alionekana kuwa na makosa makubwa. Makosa yote ya kuangamiza mamilioni ya watu duniani yakaonekana kusahaulika.
“Bora alivyoua mamilioni ili aokoe mabilioni” Mwananchi mmoja aliwaambia wenzake maneno ambayo alitaka yaandikwe kwenye bango lake huku akijiandaa na maandamano.
Siku mbili baadae, Andy akaitwa Ikulu na kula chakula cha jioni na mheshimiwa rais wa nchi hiyo na baada ya siku mbili kazi ya kutengeneza dawa ikaanza rasmi. Hiyo ikaonekana kuwa neema kwa watu wote duniani, mara baada ya kila kitu kukamilika, dawa zikaanza kusambazwa dunia nzima, haikujalisha kama ulikuwa masikini au tajiri, dawa zile zilikuwa zikipatikana bure kabisa.
Andy hakuishia hapo, akaanza kutengeneza dawa nyingi za magonjwa ya kansa ambazo zilikuwa na nguvu kupita kawaida. Kila dawa ambayo alikuwa akiitengeneza ilikuwa ikipatikana bure na serikali ya Marekani ndio ambayo ilikuwa ikimlipa. Faraja ikaonekana kurejea duniani, watu ambao walikuwa wametumia dawa zile walikuwa wamepona kabisa.
Lengo kubwa la Andy katika kipindi hicho lilikuwa ni kuupoteza kabisa ugonjwa wa PENINA. Alitengeneza dawa usiku na mchana. Kwa sababu yeye ndiye ambaye alikuwa ameutengeneza ugonjwa ule, alitakiwa kuua kwa mikono yake mwenyewe.
Kutoka asilimia thelathini ya watu ambao waliuwa wameambukizwa ugonjwa ule duniani mpaka kufikia asilimia tano ilionekana kuwa kazi kubwa kupita kiasi. Andy hakupata muda mwingi wa kupumzika, bado alikuwa akiendelea kutengeneza dawa zaidi na zaidi.
Maisha yake yaliendelea hivyo hivyo, alizidi kutengeneza dawa zaidi na zaidi. Bwana Wayne na mke wake, Bi Happy walionekana kuwa na furaha kumuona tena mtoto wao machoni mwao. Kwa sababu alikuwa amekiri kila kitu ambacho kilikuwa kimetokea, wote tena kwa moyo mmoja wakamsamehe na kuendelea na maisha yake kama kawaida mpaka pale ambapo alikuwa kupata mtoto wa kwanza wa kike ambaye alimpa jina la Loveness.
Maisha yaliendelea kama kawaida, kila kitu ambacho kilikuwa kimetokea katika maisha yake kaamua kukisahau. Nchi ya Marekani pamoja na Umoja wa Mataifa ukawa umemkingia kifua Andy. Hata nchi ya Tanzania ilipokuwa ikilalamika kuhusiana na Angy, hakukuwa na mtu yeyote ambaye aliwaelewa.
Dawa zikatengenezwa za kutosha, Andy akaamua kufungua chuo cha uuguzi nchini Marekani na kuwafundisha wanafunzi namna ya kutengeneza dawa mbalimbali za kuua baadhi ya magonjwa. Ndani ya mwaka mmoja, wanafunzi wote ambao walikuwa wakitoka katika chuo chake alikuwa akiwaajiri katika hospitali yake jambo ambalo lilimfanya kumuingizia fedha kupita kawaida.

**SEMA LOLOTE KUHUSIANA NA SIMULIZI HII...maoni yako

MWISHO
Story nzuri sana...

Chapter Closed...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom