Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #141
SEHEMU YA 108
yakaonekana kubadilika, Andy akaanza kutafutwa kwa ajili ya kurudishwa hospitalini na kuendelea na kazi yake kama kawaida ya kuwaokoa wamarekani wengi ambao walikuwa wameathiriwa na ugonjwa wa kansa.
Andy hakuonekana kabisa japokuwa alitafutwa katika kila sehemu. Matangazo yakaanza kutolewa kwamba popote alipokuwa alikuwa akihitajika kwa ajili ya kuokoa maisha ya watu ambao walikuwa wakizidi kufa kwa kansa. Ingawa kila siku tangazo lile lilikuwa likitolewa lakini Andy hakujitokeza kutoka alipokuwa japokuwa alikuwa akiliona tangazo lile.
“Kuna nini?” Kamanda mkuu aliuliza mara baada ya kupokea simu kutoka katika shirika la habari la CNN.
“Kuna mkanda umeletwa hapa” Mwandishi wa habari wa shirika hilo alijibu.
“Mkanda gani?”
“Njoo uuone. Unamhusu Andy”
Kamanda Simons hakutaka kuendelea kukaa ofisini mwake, akainuka na moja kwa moja kutoka nje kwa ajili ya kwenda kuuangalia mkanda huo. Maswali mengi yakaanza kumiminika kichwani mwake juu ya huo mkanda, ulikuwa ukizungumzia nini?
Mara baada ya kusaifiri kwa ndege mpaka kufika Atalanta, moja kwa moja akaanza kuelekea katika kituo kikubwa cha shirika hilo la habari na kisha kuelekea kule alipokuwa akihitajika. Alipoufikia mlango akaugonga na kukaribishwa ndani katika chumba ambacho waandishi wengi wa habari walikuwa wamejazana kana kwamba kulikuwa na kitu kinaendelea.
“Vipi?” Simons aliuliza.
“Kuna mkanda umeletwa ofisini”
“Unahusu nini?”
“Andy amejirekodi. Ameuita UKWELI WENYE KUUMA”
“Mungu wangu! Ukweli gani huo aliouzungumzia? Amesemaje?”
“Anachokitaka yeye ni kwamba mkanda huu tuurushe hewani ili dunia ijue kila kinachoendelea” Mkurugenzi wa shirika lile, Peters alijibu.
“Amezungumzia nini?”
“Mambo ya ajabu, mambo yanayotisha sana”
“Mmmh! Hebu uweke tuuone kabla ya kuurusha hewani” Simons aisema na kisha mkanda kuwekwa.
Mkanda ule wa saa moja ulikuwa ukimuonyesha Andy, tena akiwa katika sura yake halisi. Alikuwa akiongea huku akilia tu. Aliongea kuhusu historia yake toka kipindi ambacho alikuwa amezaliwa mpaka katika kipindi hicho. Hakuficha kitu chochote kile, aliuelezea uhusiano wake na Annastazia, akaelezea kuhusu virusi vya katapillar ambavyo vilikuwa vikieneza ugonjwa wa PENINA.
Andy hakuficha, alieleza kila kitu jambo ambalo lilimfanya kila mtu kushika kinywa kwa mshtuko. Bwana Simons ndiye ambaye alionekana kushtua zaidi, hakuamini kama Andy ndiye ambaye alikuwa nyuma ya kila kitu kilichotokea. Maneno yake ambayo alikuwa ameongea katika mkanda ule yalionekana kumshtua kila aliyekuwa akiuangalia na kuusikiliza.
“Urushe haraka sana” Simons alimwambia Peters huku akionekana kuchanganyikiwa.
Kichwa chake kilikuwa kinauma kwa wakati huo, Andy akaonekana kuwa tatizo kubwa kwa wakati huo. Mkanda ule ukaanza kurushwa, watu walipoona kwamba ni habari zilizofika punde tena zilizomhusu Andy, watu wakatulia katika televisheni zao. Picha ya Andy ilipoonekana tu, kila mmoja alionekana kumuhitaji.
yakaonekana kubadilika, Andy akaanza kutafutwa kwa ajili ya kurudishwa hospitalini na kuendelea na kazi yake kama kawaida ya kuwaokoa wamarekani wengi ambao walikuwa wameathiriwa na ugonjwa wa kansa.
Andy hakuonekana kabisa japokuwa alitafutwa katika kila sehemu. Matangazo yakaanza kutolewa kwamba popote alipokuwa alikuwa akihitajika kwa ajili ya kuokoa maisha ya watu ambao walikuwa wakizidi kufa kwa kansa. Ingawa kila siku tangazo lile lilikuwa likitolewa lakini Andy hakujitokeza kutoka alipokuwa japokuwa alikuwa akiliona tangazo lile.
“Kuna nini?” Kamanda mkuu aliuliza mara baada ya kupokea simu kutoka katika shirika la habari la CNN.
“Kuna mkanda umeletwa hapa” Mwandishi wa habari wa shirika hilo alijibu.
“Mkanda gani?”
“Njoo uuone. Unamhusu Andy”
Kamanda Simons hakutaka kuendelea kukaa ofisini mwake, akainuka na moja kwa moja kutoka nje kwa ajili ya kwenda kuuangalia mkanda huo. Maswali mengi yakaanza kumiminika kichwani mwake juu ya huo mkanda, ulikuwa ukizungumzia nini?
Mara baada ya kusaifiri kwa ndege mpaka kufika Atalanta, moja kwa moja akaanza kuelekea katika kituo kikubwa cha shirika hilo la habari na kisha kuelekea kule alipokuwa akihitajika. Alipoufikia mlango akaugonga na kukaribishwa ndani katika chumba ambacho waandishi wengi wa habari walikuwa wamejazana kana kwamba kulikuwa na kitu kinaendelea.
“Vipi?” Simons aliuliza.
“Kuna mkanda umeletwa ofisini”
“Unahusu nini?”
“Andy amejirekodi. Ameuita UKWELI WENYE KUUMA”
“Mungu wangu! Ukweli gani huo aliouzungumzia? Amesemaje?”
“Anachokitaka yeye ni kwamba mkanda huu tuurushe hewani ili dunia ijue kila kinachoendelea” Mkurugenzi wa shirika lile, Peters alijibu.
“Amezungumzia nini?”
“Mambo ya ajabu, mambo yanayotisha sana”
“Mmmh! Hebu uweke tuuone kabla ya kuurusha hewani” Simons aisema na kisha mkanda kuwekwa.
Mkanda ule wa saa moja ulikuwa ukimuonyesha Andy, tena akiwa katika sura yake halisi. Alikuwa akiongea huku akilia tu. Aliongea kuhusu historia yake toka kipindi ambacho alikuwa amezaliwa mpaka katika kipindi hicho. Hakuficha kitu chochote kile, aliuelezea uhusiano wake na Annastazia, akaelezea kuhusu virusi vya katapillar ambavyo vilikuwa vikieneza ugonjwa wa PENINA.
Andy hakuficha, alieleza kila kitu jambo ambalo lilimfanya kila mtu kushika kinywa kwa mshtuko. Bwana Simons ndiye ambaye alionekana kushtua zaidi, hakuamini kama Andy ndiye ambaye alikuwa nyuma ya kila kitu kilichotokea. Maneno yake ambayo alikuwa ameongea katika mkanda ule yalionekana kumshtua kila aliyekuwa akiuangalia na kuusikiliza.
“Urushe haraka sana” Simons alimwambia Peters huku akionekana kuchanganyikiwa.
Kichwa chake kilikuwa kinauma kwa wakati huo, Andy akaonekana kuwa tatizo kubwa kwa wakati huo. Mkanda ule ukaanza kurushwa, watu walipoona kwamba ni habari zilizofika punde tena zilizomhusu Andy, watu wakatulia katika televisheni zao. Picha ya Andy ilipoonekana tu, kila mmoja alionekana kumuhitaji.