Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,744
- 25,426
KIJIJI cha Nangose kipo jirani na mji wa Masasi njiani kuelekea kijijini kuna mimea mingi sana iitwayo mianzi ambayo watu huikata kwa matumizi mbalimbali kama vile kujengea nyumba, kutengenezea ungo au vyombo maalum wenyeji huviita ichinumba ambavyo hutumika kunywea pombe ya kienyeji ya mtama, wengine hutengeneza fimbo maalum ya kutembelea, au mipini ya majembe na kadhalika.
Mimi naitwa Issa Namakoto, nakusimulia simulizi hii nikikurudisha nyuma miaka kadhaa iliyopita tukiwa Dar es Salaam tulipata taarifa kuwa Nangose kuna bustani ya ajabu ya mianzi iliyopandwa kimstari na mtu asiyejulikana.
Siku moja mimi na rafiki zangu 25 tuliamua kwenda kujionea bustani hiyo, tulifunga safari yetu tukitokea Dar es Salaam, tulikuwa vijana watupu wa kike na kiume.
Tuligeuza ziara hiyo kama pikiniki fulani. Wakati tunasafiri tulipofika Nangurukulu, njia panda ya kwenda Kilwa, tulipumzika kwa ajili ya kula chakula cha mchana.
Tulijaribu kuhoji wenyeji tuliokuwa nao kwenye basi na tuliambiwa kuwa ndani ya bustani hiyo kuna maua mazuri yaliyokuwa yamezunguka mianzi hiyo ya ajabu na kulikuwa na mtunzaji ambaye alikuwa ni mtu mwenye umri mkubwa aliyekuwa akisimulia mambo ya bustani hiyo.
Aliyekuwa anatusimulia pale Nangurukulu alitufanya tutamani kufika mapema katika bustani hiyo ili tushuhudie maajabu tuliyoambiwa yapo. Msimuliaji huyo alisema kuwa watu wanaokwenda kujionea maajabu hayo lazima watimize masharti fulani ambayo mtunza bustani huwaambia.
Baada ya kula safari ilianza kwa furaha kubwa, ndani ya basi ‘kosta’ kulikuwa na mazungumzo yanayohusu bustani hiyo ya ajabu na mwenzetu mmoja alisema aliambiwa kuwa ndani yake kuna matunda pori matamu sana ambayo hayana msimu.
Basi letu dogo lilipita Lindi mjini saa nane mchana na dakika chache baadaye tukafika Mnazi Mmoja, njia panda ya Lindi na Masasi na Mtwara.
Hapo pana pilikapilika na kuna mizani ya kupimia magari mazito.
Baada ya kufika hapo, dereva alituambia tushuke kwa ajili ya kununua chochote tulichohitaji na kujisaidia, alitupa dakika kumi na tano.
Kwa kuwa mimi ni mpenzi sana wa korosho, nilinunua za shilingi mia tano na soda.
Muda tuliopewa na dereva ulipoisha tuliingia kwenye gari na kuanza safari na kwenda moja kwa moja hadi Mtama, (Jimbo la Mbunge Nape Nnauye) tukafika saa nane na nusu na njiani kabisa tukakutana na umati ukicheza ngoma, ulikuwa ukikatiza barabara kuu ikabidi dereva asimame, kuwapisha.
“Nadhani hawa wanasherehekea mambo ya jando na unyago kwa sababu kipindi chenyewe kilikuwa cha mavuno,” nilijisemea.
Tulipotoka pale Mtama usingizi ulinishika, nikalala usingizi mzito na nilishtukia nikiambiwa kuwa tumefika Ndanda. Hapa ni maarufu kwa mikoa ya kusini kutokana na kuwa na hospitali kubwa ya misheni na shule ya sekondari.
Nilifikicha macho na kuona mji. Siyo mji mkubwa, una barabara ya lami moja tu na kando ya barabara kuu tunayopita kuna soko. Tulikuta wenyeji wakiuza mbaazi kwa mafungu na abiria waliokuwa wakisafiri kwa mabasi makubwa walikuwa wanajinunulia mbaazi hizo.
Wakati tunatoka Dar tulielezwa kwamba tukifika Ndanda kuna mtu mmoja anaitwa Ngalipambone ataungana nasi na ndiye atakayetuongoza hadi Nangose. Kutokana na urefu wa jina lake watu wanakatiza na kumuita bwana Ngali.
Haikuwa ngumu kumpata kwa sababu alikuwa anawasiliana na dereva wa basi letu mara kwa mara kwa njia ya simu.
“Habari zenu jamani!” Alisalimia bwana Ngali.
“Nzuri, shikamoo!” tuliitikia na kuamkia kwa pamoja kama vile kulikuwa na mtu aliyekuwa akituamuru.
“Marahaba. Mimi naitwa Ngali. Nimeambiwa niwapeleke kwenye bustani ya mianzi ya Nangose.”
“Ni kweli bwana,” alisema dereva.
“Kutoka hapa siyo mbali sana na tutafika leoleo,” akasema bwana Ngali na kuketi kwenye kiti cha mbele kwa dereva msaidizi, ambaye aliinuka na kwenda kusimama mlangoni kama kondakta wa daladala afanyavyo.
Bwana Ngali ndiye alikuwa kinara au dira ya kwenda kwenye bustani hiyo ya ajabu ambayo watu wamekuwa wakiisifia.
Baada ya kufika mjini Masasi hatukukaa, basi lilielekezwa kuifuata barabara ya Nachingwea. Ni mwendo mfupi tu kutoka hapo kwenye njia panda ya kwenda Tunduru ambapo kuna gereza la wilaya tukamsikia bwana Ngali akimuamuru dereva afuate njia ya Nachingwea;
“Pinda kushoto,” tukaiacha barabara kuu na kuifuata ya vumbi. Dakika kama tano bwana Ngali akasema;
“Saa tumefika Nangose, pinda kulia kama tunaelekea Nchoti.”
Lakini baadaye tukaingia barabara yenye vumbi jekundu ilikuwa kama tunaelekea Kijiji cha Nchoti lakini tukapinda tena kulia.
Tulianza kuona bustani ya ajabu na tulipofika eneo fulani bwana Ngali alisimama katikati ya basi akasema:
“Jamani mimi hapa ndiyo mwisho wa safari yangu. Bustani ya mianzi ni hii kuanzia hapa, huko mbele kuna mtu mtamkuta ambaye ndiye atakuwa mwenyeji wenu.”
Nilijiuliza huku ni porini sasa huyu bwana Ngali atarudi kwa njia gani mjini? Hata hivyo, wakati nawaza hayo nilishtukia pikipiki ikitoa mlio, kumbe alimpigia mtu wa bodaboda akawa anatufuata kwa nyuma.
Alishuka kwenye basi letu, akapanda pikipiki na kutoweka. Dereva wetu aliendelea na safari hadi katikati ya bustani ya mianzi. Ilikuwa nzuri sana ambayo sijapata kuona maishani mwangu.
Mianzi ilikuwa imepandwa kwa mstari na pia kulikuwa na maua ya kila aina. Ajabu ni kwamba sehemu zote tulizopita zilikuwa kavu, majani yalikauka lakini katika bustani hiyo ni tofauti sana. Mianzi yote, maua na miti ni ya kijani kibichi.
Alitokea mzee mmoja ambaye alionekana kuwa ni chotara, alikuwa na ndevu nyingi nyeupe na alikuwa na mvi karibu kichwa chote, mashavu yalikuwa yamemshuka kwa uzee.
“Karibuni wajukuu zangu,” alisema mzee huyo tukamuamkia.
Nilimsogelea kwa kuwa mimi ndiye nilikuwa mkuu wa msafara. Alinishika mkono mwilini nikaona kama nimepigwa shoti ya umeme! Nikapiga yowe!
Je, nini kitatokea?
Mimi naitwa Issa Namakoto, nakusimulia simulizi hii nikikurudisha nyuma miaka kadhaa iliyopita tukiwa Dar es Salaam tulipata taarifa kuwa Nangose kuna bustani ya ajabu ya mianzi iliyopandwa kimstari na mtu asiyejulikana.
Siku moja mimi na rafiki zangu 25 tuliamua kwenda kujionea bustani hiyo, tulifunga safari yetu tukitokea Dar es Salaam, tulikuwa vijana watupu wa kike na kiume.
Tuligeuza ziara hiyo kama pikiniki fulani. Wakati tunasafiri tulipofika Nangurukulu, njia panda ya kwenda Kilwa, tulipumzika kwa ajili ya kula chakula cha mchana.
Tulijaribu kuhoji wenyeji tuliokuwa nao kwenye basi na tuliambiwa kuwa ndani ya bustani hiyo kuna maua mazuri yaliyokuwa yamezunguka mianzi hiyo ya ajabu na kulikuwa na mtunzaji ambaye alikuwa ni mtu mwenye umri mkubwa aliyekuwa akisimulia mambo ya bustani hiyo.
Aliyekuwa anatusimulia pale Nangurukulu alitufanya tutamani kufika mapema katika bustani hiyo ili tushuhudie maajabu tuliyoambiwa yapo. Msimuliaji huyo alisema kuwa watu wanaokwenda kujionea maajabu hayo lazima watimize masharti fulani ambayo mtunza bustani huwaambia.
Baada ya kula safari ilianza kwa furaha kubwa, ndani ya basi ‘kosta’ kulikuwa na mazungumzo yanayohusu bustani hiyo ya ajabu na mwenzetu mmoja alisema aliambiwa kuwa ndani yake kuna matunda pori matamu sana ambayo hayana msimu.
Basi letu dogo lilipita Lindi mjini saa nane mchana na dakika chache baadaye tukafika Mnazi Mmoja, njia panda ya Lindi na Masasi na Mtwara.
Hapo pana pilikapilika na kuna mizani ya kupimia magari mazito.
Baada ya kufika hapo, dereva alituambia tushuke kwa ajili ya kununua chochote tulichohitaji na kujisaidia, alitupa dakika kumi na tano.
Kwa kuwa mimi ni mpenzi sana wa korosho, nilinunua za shilingi mia tano na soda.
Muda tuliopewa na dereva ulipoisha tuliingia kwenye gari na kuanza safari na kwenda moja kwa moja hadi Mtama, (Jimbo la Mbunge Nape Nnauye) tukafika saa nane na nusu na njiani kabisa tukakutana na umati ukicheza ngoma, ulikuwa ukikatiza barabara kuu ikabidi dereva asimame, kuwapisha.
“Nadhani hawa wanasherehekea mambo ya jando na unyago kwa sababu kipindi chenyewe kilikuwa cha mavuno,” nilijisemea.
Tulipotoka pale Mtama usingizi ulinishika, nikalala usingizi mzito na nilishtukia nikiambiwa kuwa tumefika Ndanda. Hapa ni maarufu kwa mikoa ya kusini kutokana na kuwa na hospitali kubwa ya misheni na shule ya sekondari.
Nilifikicha macho na kuona mji. Siyo mji mkubwa, una barabara ya lami moja tu na kando ya barabara kuu tunayopita kuna soko. Tulikuta wenyeji wakiuza mbaazi kwa mafungu na abiria waliokuwa wakisafiri kwa mabasi makubwa walikuwa wanajinunulia mbaazi hizo.
Wakati tunatoka Dar tulielezwa kwamba tukifika Ndanda kuna mtu mmoja anaitwa Ngalipambone ataungana nasi na ndiye atakayetuongoza hadi Nangose. Kutokana na urefu wa jina lake watu wanakatiza na kumuita bwana Ngali.
Haikuwa ngumu kumpata kwa sababu alikuwa anawasiliana na dereva wa basi letu mara kwa mara kwa njia ya simu.
“Habari zenu jamani!” Alisalimia bwana Ngali.
“Nzuri, shikamoo!” tuliitikia na kuamkia kwa pamoja kama vile kulikuwa na mtu aliyekuwa akituamuru.
“Marahaba. Mimi naitwa Ngali. Nimeambiwa niwapeleke kwenye bustani ya mianzi ya Nangose.”
“Ni kweli bwana,” alisema dereva.
“Kutoka hapa siyo mbali sana na tutafika leoleo,” akasema bwana Ngali na kuketi kwenye kiti cha mbele kwa dereva msaidizi, ambaye aliinuka na kwenda kusimama mlangoni kama kondakta wa daladala afanyavyo.
Bwana Ngali ndiye alikuwa kinara au dira ya kwenda kwenye bustani hiyo ya ajabu ambayo watu wamekuwa wakiisifia.
Baada ya kufika mjini Masasi hatukukaa, basi lilielekezwa kuifuata barabara ya Nachingwea. Ni mwendo mfupi tu kutoka hapo kwenye njia panda ya kwenda Tunduru ambapo kuna gereza la wilaya tukamsikia bwana Ngali akimuamuru dereva afuate njia ya Nachingwea;
“Pinda kushoto,” tukaiacha barabara kuu na kuifuata ya vumbi. Dakika kama tano bwana Ngali akasema;
“Saa tumefika Nangose, pinda kulia kama tunaelekea Nchoti.”
Lakini baadaye tukaingia barabara yenye vumbi jekundu ilikuwa kama tunaelekea Kijiji cha Nchoti lakini tukapinda tena kulia.
Tulianza kuona bustani ya ajabu na tulipofika eneo fulani bwana Ngali alisimama katikati ya basi akasema:
“Jamani mimi hapa ndiyo mwisho wa safari yangu. Bustani ya mianzi ni hii kuanzia hapa, huko mbele kuna mtu mtamkuta ambaye ndiye atakuwa mwenyeji wenu.”
Nilijiuliza huku ni porini sasa huyu bwana Ngali atarudi kwa njia gani mjini? Hata hivyo, wakati nawaza hayo nilishtukia pikipiki ikitoa mlio, kumbe alimpigia mtu wa bodaboda akawa anatufuata kwa nyuma.
Alishuka kwenye basi letu, akapanda pikipiki na kutoweka. Dereva wetu aliendelea na safari hadi katikati ya bustani ya mianzi. Ilikuwa nzuri sana ambayo sijapata kuona maishani mwangu.
Mianzi ilikuwa imepandwa kwa mstari na pia kulikuwa na maua ya kila aina. Ajabu ni kwamba sehemu zote tulizopita zilikuwa kavu, majani yalikauka lakini katika bustani hiyo ni tofauti sana. Mianzi yote, maua na miti ni ya kijani kibichi.
Alitokea mzee mmoja ambaye alionekana kuwa ni chotara, alikuwa na ndevu nyingi nyeupe na alikuwa na mvi karibu kichwa chote, mashavu yalikuwa yamemshuka kwa uzee.
“Karibuni wajukuu zangu,” alisema mzee huyo tukamuamkia.
Nilimsogelea kwa kuwa mimi ndiye nilikuwa mkuu wa msafara. Alinishika mkono mwilini nikaona kama nimepigwa shoti ya umeme! Nikapiga yowe!
Je, nini kitatokea?