Simulizi:The President and I(Mimi Na Rais)

Imeandikwa na Lello Mmassy


UTANGULIZI
Naitwa Joseph Kaduma Ndani Ya Serikali Ya Nchi Ya STANZA Watu Hupenda Kuniita Joe.Nina Nusu Saa Tu Ya Kuamua Kati Ya Maisha Yangu,Familia Yangu Na Utajiri Wangu Ama Uhai Wa Rais. Rais Anaeongoza Zaidi Ya Watu Milioni 70,Mwenye Ulinzi Zaidi Ya Ma Rais Wengi Hapa Duniani Leo Hatma Ya Maisha Yangu Ipo Mikononi Mwake Na Yake Mikononi Mwangu.

Nimwache Animalize Au Nimmalize Nibaki Salama?.Siwezi Kurudia Kosa Nililolitenda Hapo Kabla.Ni Ama Mimi Ama Rais.

Inaendelea..
**************************
NIMESOMA HIVI VIPANDE VYOTE AM SO MUCH INTERESTED KUPATA HARDCOPY/SOFTCOPY PIA NATAMANI KUJUA KAMA NAPATAJE NIPO DOM
 
SEHEMU YA TATU

Joe Achagua Kikosi Kazi Chake Cha Misheni Ya Korea Kaskazini. Wakutana China. Rais Costa Atuma Kijana Wa Ki Vietinam Kuwafatilia Kwa Siri.
Korea ya Kaskazini ni taifa lililo na balozi 48 duniani kote lakini ni nchi 25 tu ndio zenye balozi zao jijini Pyongyang. Taifa hili hutegemea zaidi biashara kati yake na nchi za Uchina na India, ambapo asilimia 95 ya biashara zake za nje na uagizwaji wa ndani hufanywa baina ya nchi hizi mbili na asilimia iliyobaki kwingineko kama vile Ufilipino.
Tangu mtawala wa nchi hiyo Kim Jong Un atangaze majaribio ya makombora ya nyuklia ya masafa marefu, Marekani na Umoja wa mataifa iliiwekea vikwazo. Pia taifa la Marekani liliwataka washirika wake kutojihusisha kibiashara na Korea Kaskazini hata hapo itakapositisha majaribio yake. Hali hii ilifanya hali ya kiuchumi ya Korea Kaskazini kudorora na hata wananchi walipotaka kudai haki zao, ukatili uliongezeka dhidi yao na udikteta ukaota mizizi, ingawa katika utambulisho rasmi wa jina la nchi hiyo ni ‘Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Korea’.

Nchi nyingi za kiAfrika ziliingia kwenye wakati mgumu wa namna gani kukubaliana na Marekani na Umoja wa mataifa juu ya vikwazo walivyoweka dhidi ya Korea na wakati huohuo kuendelea kuwa na mahusiano mema na taifa hilo lenye historia kubwa ya kikomunisti na mataifa mengi ya kiAfrika.
Mahusiano mengi kati ya Korea Kaskazini na nchi nyingi za kiAfrika hayapo kisiasa tu lakini pia kiuchumi kwani inakadiriwa kati ya mwaka 2007 na 2015 biashara iliyofanywa kati ya taifa hili na nchi za kiAfrika yafikia dola za kimarekani milioni 217.
Korea ikilitumia shirika lake la Mansudae wametekeleza miradi kadhaa ya ujenzi katika nchi baadhi za kiAfrika lakini hasa Namibia ambapo Ikulu na Makazi ya Rais yamejengwa na Korea Kaskazini. Nchi za Uganda, Tanzania na Mozambique mwaka 2017 zilishutumiwa kuiomba Korea iwasaidie katika Nyanja za jeshi, shutuma ambazo nchi kama Tanzania ilizikana lakini Uganda walikubali na kuahidi kusitisha.
Mbali na miradi ya ujenzi barani Afrika, Korea Kaskazini pia hufanya biashara kubwa ya silaha za kivita. Katika nchi za Eritrea, Jamuhuri ya Afrika ya Kati, Congo na nchi nyingine, Korea ni washirika wazuri katika biashara hiyo. Pia, ripoti ya kiuchunguzi ya Forbasi, taasisi inayoaminika kwa uchambuzi wa masuala ya usalama duniani yenye makao makuu Uskochi inasema kuwa taifa hili la Korea Kaskazini ndilo husaidia ulinzi binafsi wa Rais wa Congo kwa kutoa mafunzo, utaalamu na ufuatiliaji wa usalama wake. Taarifa ambazo serikali ya Congo inakanusha hata leo.
Mwezi Septemba, 2017 Rais wa Marekani Chriss Donald kupitia agizo lake namba 13810 aliomba nchi zote marafiki wa Marekani kuungana nae katika kusitisha aina yoyote ya biashara na mahusiano na Korea Kaskazini kama kuunga mkono jitihada za kuhakikisha taifa hilo haliendelei na majaribio yake ya makombora ambayo Marekani ilihofia yangeachwa kuendelea, hatimaye wangefikia uwezo wa kitaalamu wa kutengeneza makombora ya nyuklia yanayoweza kusafiri masafa marefu na kufikia ardhi ya Marekani.
Stanza, moja ya nchi barani Afrika na mshirika mkubwa wa Marekani leo inafanya jitihada wanazotaka ziwe za siri kujenga mahusiano na Korea Kaskazini. Wakati asilimia 50 ya bajeti ya Stanza ikiwa inatokana na mapato ya ndani na asilimia 50 iliyobaki ikitoka kwa nchi wahisani, Marekani pekee inachangia asilimia 20, achilia mbali fedha nyingine nyingi inazopokea kupitia mashirika ya maendeleo ya ki Marekani. Ni katika hali hiyo Rais Costa anataka kukiuka maagizo ya Marekani juu ya mashirikiano yake na Korea Kaskazini.
Rais Sylvester Costa anataka kwenda mbali kuwaingiza kabisa watoe mafunzo, vifaa na mfumo mzima wa mawasiliano wa Serikali, Jeshi na Idara ya Usalama wa taifa la Stanza.
********************************
“Mh. Rais kutokana na hayo niliyokwishaeleza, basi kwa kuwa sisi hatuna ubalozi Pyongyang wala Korea Kaskazini hawana ubalozi wao hapa kwetu ni vema tukautumia ubalozi wetu pale China kama Sehemu ya kufanyia mikakati mimi na timu yangu nitakayoipendekeza. China wana mahusiano ya karibu sana na Korea na hivyo ninaweza kuwatumia baadhi ya marafiki pale katika, kwanza kujenga mahusiano kisha ndio nitaendelea na mengine uliyoniagiza.
Lakini nikuombe Mh. Rais kuwa wakati haya yakiendelea ni vyema usiwe na makwazo mengi kwa nchi za magharibi kwani wanaweza wakaanza kutufatilia sana kwa ukaribu na kuharibu mikakati na pia kuwekewa vikwazo vitakavyofanya hali ya uchumi wetu iwe mbaya.
Lakini pia angalia namna ya kuzungumza na Rais wa Urusi, Kamaradi Vijisky na Rais wa China pia juu ya yale mlioshindwa kuelewana. Njia hiyo itanisaidia sana mimi kuwatumia kwenye misheni yangu hii na pindi wa magharibi watakapoanza kutuletea zengwe wao watasimama kidete nasi”, Joe aliwasilisha mapendekezo yake kwa umakini wakati akielezea mikakati yake kwa Rais Costa.
Meza ile ilikuwa na watu watano, Rais Sylvester Costa, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali Ernest Nduta, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Chonge Kalumanzila, Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Stanley Macha, na Joseph Kaduma.
Mara baada ya Joe kumaliza kuongea, kila mtu alikuwa kimya na kuonekana kumuelewa vyema. Aliyekata ukimya ule alikuwa ni Rais Costa, “Joe, tutajitahidi kufanya uliyopendekeza lakini niseme mambo haya kwasasa ni siri kubwa na nimewaeleza wenzangu namna ya kuenenda. Ninajua suala hili likiwafikia Marekani na washirika wake tutakuwa kwenye wakati mgumu na ninajua watang’amua mapema sana ndio maana sitaki tushindwe”, Rais Costa alimsisitiza Joe.

Joe aliomba timu ya watu wawili wa kusaidiana nae alimtaja Habibu Chamchua Balozi wa Stanza nchini India ambae ni kijana mpendwa wa Joe na Luteni Jenerali Pius Kihaka Mnadhimu Mkuu wa Jeshi na Mkuu wa kitengo cha Idara ya usalama wa jeshi na mmoja kati ya vijana wadogo na wasomi sana katika jeshi la wananchi wa Stanza.
Pius Kihaka ni Rafiki mkubwa wa Joe, hawa wote; Habibu na Pius ni wanafunzi wa Joe katika chuo cha Diplomasia walipokuwa wanafanya Shahada zao za Uzamili. Joe anaamini hawa ni baadhi ya vijana wenye upeo mkubwa sana katika uwanda wa kidiplomasia, ushawishi na ushushushu. Ndio watu aliowataka kufanya nao kazi. Lakini pia alikuwa na ajenda nao nyingine nyuma ambayo hakuna mtu alieijua. Rais Costa alimkubalia na kutoa maagizo vijana hao wataarifiwe na kuwa sasa watafanya kazi kwa maelekezo ya Joe.
Kikao kile kiliisha vyema. Joe aliridhika kuwa sasa anaweza kuanza kutimiza majukumu yake. Alipatiwa kila aina ya mahitaji na nyaraka alizohitaji ili kutekeleza kazi aliyopewa. Rais Costa alipeleka salamu za kutaka mazungumzo na Rais Kim wa Korea na kuwa ujumbe wake utaelekea huko. Rais Kim aliridhia na kutaka kujua haswa ni nini taifa kutoka Afrika tena wenye ushirika mkubwa na Marekani linataka kuzungumza. Hakika kila nchi ilijitayarisha kwa mazungumzo hayo.
*******************************
Habibu Chamchua, kijana mahiri katika medani za kidiplomasia, machachari katika ushushushu na sasa balozi wa Stanza nchini India alifurahishwa na taarifa kuwa anahitajika kufanya kazi na Joe. Habibu alikuwa kijana makini na aliyefanya vyema kwenye chuo cha diplomasia, alishawishiwa na Joe aingie kwenye siasa ili kushika nafasi za uongozi wa nchi.
Ni Joe aliyempa moyo Habibu kwa kumwambia kuwa anamuona siku moja kama Rais wa Stanza. Mara baada ya Habibu kuingia kwenye siasa alifanikiwa kwa kiasi kikubwa sana kuteka nyoyo za vijana wengi wa chama tawala mpaka upinzani. Ni yeye aliewezesha kubadili hali ya kisiasa kwa wakati fulani kwa jinsi alivyoweza kujenga hoja na kujieleza.
Katika chama tawala alionekana sana tishio na ni hapo Rais Costa ili kumpunguza nguvu aliona yafaa amtoe nchini na kumpangia ubalozi ili apotee machoni na masikioni mwa wengi. Habibu sasa anapewa jukumu la kuhakikisha Korea Kaskazini inasaidia Stanza kijeshi lakini hususani kufanya kazi na Joe, ilikuwa ni heshima kubwa kwake.
*******************************
Zilipita wiki mbili tangu mashtaka ya Joe dhidi ya uhujumu uchumi kufutwa na mahakama ya uhujumu uchumi na ufisadi ya Stanza. Waziri wa Fedha alimteua Elizabeth Kidampa Kaduma kuwa Mkurugenzi wa benki ya Kilimo ya Stanza. Elizabeth, mke wa Joseph Kaduma aliwasili makao makuu ya benki na kupokelewa kwa heshima kubwa. Eliza alijaa haiba na tabasamu, ni mwanamke asiejikweza mwenye uwezo mkubwa wa kusikiliza na kung’amua mambo.
Mara baada ya kusomewa taarifa fupi ya maendeleo ya benki, alibainisha wazi kuwa vipaumbele vyake ni pamoja na kuhakikisha fedha zote zinazotengwa na serikali kwa ajili ya ruzuku zinawafikia wakulima kwa wakati na hilo hatakuwa na msamaha na mtendaji yeyote atakayezembea, lakini pili ataanzisha maghala yatakayosimamiwa na benki na kuwa mazao yote ya biashara yatapangiwa bei elekezi na mfanyabishara atapaswa kuyanunua kwa bei hiyo kutoka kwa wakulima, vinginevyo basi benki itayanunua na kuyatafutia masoko.

Alitanabaisha benki ile ni lazima iwe msaada kwa wakulima kwa kutoa mikopo nafuu na kuhakikisha wakulima wa Stanza wananufaika. Pia, alielezea mpango wa benki kwa kushirikiana na wizara kujenga mabwawa makubwa na ya kisasa kwa ajili ya umwagiliaji katika kanda tano zinazoongoza kwa kilimo cha mazao ya biashara na chakula kwa kuanzia ili nchi itoke kwenye kutegemea mvua pekee kwa ajili ya umwagiliaji. Ilikuwa ni taarifa njema.
*********************************
“Kaka shikamoo”, alikuwa ni Habibu akimsalimia Joe kwa bashasha na tabasamu kubwa huku akimkumbatia ndani ya ofisi za ubalozi wa Stanza jijini Beijing China zilizopo mtaa wa Liang Ma He, Nan Lu. Ilikuwa ni faraja kubwa kwa Habibu kukutana na Joe. “Luteni Jenerali” Habibu alimwita Pius huku akionyesha ishara ya kupiga saluti kisha kumkubatia kwa kicheko kikubwa.
Habibu alikuwa akiwalaki Joe na Luteni Jenerali Pius Kihaka waliokuwa wamewasili kutoka Stanza, yeye akiwa amewatangulia siku moja kabla akitokea India. Habibu ndio alikuwa mdogo kiumri kati ya Joe na Luteni Jenereli Pius Kihaka. Wote kwa pamoja walilakiwa na balozi Kimweri anaeiwakilisha Stanza huko China.
Walielekea kwenye chumba walichotengewa na ubalozi maalumu kwa ajili ya vikao vyao na Joe alikuwa tayari kutoa muhtasari na mwongozo wa namna kazi itakavyofanyika. “Ni jukumu letu kuleta matokeo yanayotegemewa na Mh. Rais. Tutaingia kwenye vitabu vya historia kwa kuanzisha mahusiano na Korea Kaskazini lakini pia kwa kufanikisha kazi hii Mh. Rais aliyotutuma”, Joe alimalizia. Habibu na Pius walionekana kutikisa vichwa ishara ya kuelewa na kuafiki. Wakati Joe akiongea walikuwa wakipitia baadhi ya nyaraka Joe alizowagawia waziangalie na kuzisoma. Tayari ubalozi wa Stanza pale China ulishaanda utaratibu mzima wa Joe na wenzake kuingia Korea Kaskazini.
Baada ya maongezi yale yaliyodumu kwa masaa mawili wakiweka mikakati na nini cha kuzungumza na nani azungumze nini. Joe alipendekeza jioni wakutane mgahawa wa Cheng Lee ulio jirani na Ubalozi kwa ajili ya kupata kahawa.
**********************************
Ilikuwa ni habari iliyowasisimua viongozi wa taifa la Korea Kaskazini kusikia kuwa kuna taifa kutoka Afrika linataka kuanzisha mahusiano nao ukizingatia tamko na maazimio ya Marekani na Umoja wa mataifa. Rais Kim alikuwa akisubiria ujumbe kutoka Stanza kwa shauku kubwa.

Kuonyesha shauku yake na kwa ajili ya usalama aliagiza ndege kutoka shirika la ndege la Korea Kaskazini, Air Koryo llyushin II-62M ndiyo iwabebe kwa kuwatengea siti maalum. Viongozi wa Korea walijipanga kusikia nini ujumbe kutoka Stanza utawaeleza na mashirikiano gani wanahitaji, watafaidika vipi na wamejipangaje kushindana na shinikizo kutoka nchi za Magharibi zisizowaunga mkono hasa Marekani.
********************************
“Kimweri niambie kinachoendelea”, alikuwa ni Rais Sylvester Costa akiongea na balozi Kimweri aliyeko China kupitia mfumo salama wa mawasiliano ya kiserikali. “Mpaka sasa hakuna tishio lolote walilojadili ila jioni wamekubaliana kukutana mgahawa wa Cheng Lee kwa ajili ya kupata kahawa”, balozi Kimweri alimjibu Rais Costa. “Kuna mtu kule tayari? Nahitaji ufuatiliaji kwao hatua kwa hatua hasa wakiwa hapo China”, Rais Costa alisisitiza. “Ndiyo mkuu”, balozi Kimweri alijibu.
Bila Joe na wenzake kujua Rais Costa alishaweka namna ya kufatilia kila wanaloongea Joe, Habibu na Pius. Alihakikisha vyumba vyote watakavyokuwa wanakutana vimewekewa vinasa sauti kwa siri vyenye uwezo mkubwa sana. Maongezi yao na simu zao zote zilikuwa zikirekodiwa.
Rais Costa alikuwa akipata kila kinachoendelea kwenye maongezi ya Joe na wenzake. Japo alimwita Joe amsaidie kazi lakini hakumwamini. Alianza kupata mashaka hasa Joe alipotaka kazi ile asaidiane na Habibu na Pius watu anaowajua ni watiifu kwa Joe. Rais Costa hakutaka kupitwa na kitu hivyo tayari balozi Kimweri alishatuma mtu mgahawani kuangalia namna atakavyoweza kurekodi maongezi ya kina Joe bila wao kujua.
Kimweri alifanya hivyo mara baada ya kuona Joe ametoka kwenye kikao na kwenda kupumzika lakini hakumualika kwenye kahawa jioni wakati yeye ndo mwenyeji wao. Aliwaza ni nini Joe alitaka kwenda kuongelea huko. Kati ya watu watiifu na vipenzi wa Rais Costa basi balozi Kimweri ni mmoja wapo.
***********************************
Jioni ilifika na Joe, Habibu na Pius walitoka kwenda mgahawani. Walipofika Joe alichagua meza iliyo mwishoni mwa mgahawa ili apate kuona kila anaeingia ndani ya mgahawa na alihakikisha upande aliokaa hakuna anaeweza kingia bila yeye kumuona. Kati ya Habibu na Pius hakuna aliyekuwa anajua kinachotaka kujadiliwa pale, walidhani ni maongezi ya kawaida tu.
Waliketi, na baada ya kumaliza kuagiza kahawa Joe alivunja ukimya. “Guys, ninyi ni vijana wangu na ninaelewa nguvu yenu. Mfano Habibu unaelewa jambo nililoongea nawe miaka mitano iliyopita lililokufanya ujiingize kwenye siasa kwa mara ya kwanza. Pius wewe pia unaelewa au sio? Huu ndio wakati wa kuanza utekelezaji, tunaenda na yote mawili ndani ya moja”, Joe alitulia na kunywa kahawa.
Habibu na Pius walionekana ni kama watu wasioelewa Joe anazungumza kitu gani, walibaki wameshangaa wakiangaliana. Joe alikuwa akizungusha macho mgahawani kuhakikisha hakuna yeyote anakaa meza karibu yao ama hata kuwasogelea.
Akiwa amemaliza kunywa tena kahawa kwa mara ya pili simu yake ilitoa sauti kuashiria kuna ujumbe umeingia. Alipoangalia vyema aligundua ujumbe umeingia kupitia App ya game uliosomeka “Hakikisha mdudu yeyote hakukaribii wakati wowote wa mazungumzo nje ya Ubalozi”, Joe aliposoma alivuta pumzi na kujikaza ili Habibu na Pius wasishtuke kisha akaanza kuzungusha macho kila kona hasa maeneo ya ukuta na dirisha lililo umbali mchache kutoka pale walipokaa. Alipokuwa akiangalia aliona mdudu kama nzi akiwa anawasogelea.
Akaja akatua juu ya kichwa cha Joe kwa ukutani. Joe alishtuka sana akajikaza. Pius akawa kama kuna jambo ameshtukia akamuuliza Joe kulikoni? Joe hakujibu akamwonyeshea Pius ishara ya kuwa anyamaze, kisha akaonyesha ishara kuwa waondoke. Waliposimama na kuanza kuondoka Joe aliwasogelea wenzake na kukaa katikati yao kisha akawaambia atawaambia kilichotokea ila wasiwe na wasiwasi.
******************************
Stanley Macha, mkuu wa Idara ya Usalama wa taifa Stanza na Rafiki mkubwa wa Joe alikuwa akifuatilia hatua kwa hatua safari na misheni aliyotumwa Joe nchini Korea Kaskazini. Ni ukweli usiopingika Macha na Joe walikuwa ni zaidi ya marafiki, ni yeye alietengeneza mazingira misheni ya kutafuta mahusiano na Korea Kaskazini isifanikishwe na mtu yeyote katika serikali ya Rais Costa mpaka Joe aitwe.
Ilikuwa ni ngumu kumuacha Joe peke yake hasa akijua mahusiano ya kutilia shaka aliyonayo Joe na Rais Costa. Mara baada ya Joe kukubali kutumika na Rais Costa katika misheni ya Korea Kaskazini Macha aliamua kutafuta njia ya siri ya kuwa wanawasiliana na Joe. Waliamua wote kuwekagame (mchezo wa kwenye simu) unaoitwa Clash Royale ambao wachezaji huweza kutumiana jumbe na kuwasiliana. Ili mtu mwingine kuweza kufatilia jumbe zinazotumwa humu ni lazima uwe na wewe umeweka huu mchezo kwenye simu yako ama uwaombe wamiliki wakupe.
Lakini pia majina yanayotumika huwa sio ya halisi hivyo pia ni ngumu kujua ujumbe huu unatoka na kwenda kwa nani. Macha na Joe hutumia njia hii kuwasiliana. Macha alichelewa sana kupata taarifa juu ya mpango unaondelea juu ya Joe na wenzake unaofanywa na Rais Costa na balozi Kimweri. Hakuna anaejua alipataje hasa ukizingatia maelekezo ya Rais kwa balozi Kimweri ni ufuatiliaji wa Joe ufanywe baina yake na Kijana ambae Rais Costa alimpelekea balozi Kimweri kutoka Vietnam.
Balozi Kimweri na yule kijana wa kiVietnam walitumia kinasa sauti mfano wa Nzi kinachoweza kuendeshwa kwa rimoti ya kwenye simu kutokea mbali. Hivyo kutokea meza ya mbele kabisa ya mgahawa kijana yule wa kiVietinam alikitoa kile kinasa sauti na kuanza kukiendesha kwa simu kama mtu aliekuwa akichat kuelekea mwisho wa mgahawa walipokuwa wamekaa Joe na wenzake.
Macha alipopata ile taarifa alimtumia ujumbe Joe kuwa awe mwangalifu na mdudu yeyote arukae atakaesogea karibu nao. Joe aliona yule mdudu kama nzi na aligundua kilichokuwa kikiendelea. Waliondoka.
***********************************
Joe Alitaka Kuwaambia Nini Wenzake? Je, Rais Costa Atafanikiwa Kumfuatilia Joe Au Ndio Joe Kashamtoka?Vipi Kuhusu Misheni Ya Korea?...
inataka bajeti hii series kali sana,nimeianza kuiona
 
Back
Top Bottom