Simulizi: Soka Lilivyonikutanisha Na Shetani

Kuna hii apa pia
Thanks dearest one...

I'll simply go to your profile page, then from there nitatafuta stories zote ambazo umefanya kupost na ku subscribe kwa hizo threads...
 
Thanks dearest one...

I'll simply go to your profile page, then from there nitatafuta stories zote ambazo umefanya kupost na ku subscribe kwa hizo threads...
Karibu
 
Sehemu ya 31

“Yupo binti anaitwa Lawalawa, mwezi uliopita aliwahi kumtolea uboho baba yake mzazi, na leukocyte antigens yake nahisi inaweza kumsaidia mtoto wenu. “Lawalawa!!” nilimaka. Nilishituka sana.

“Ndio Lawalawa, binti mmoja ana asili ya kiarabu, unamfahamu?” Kauli ya daktari yule ilinishitua sio kidogo, nilihisi kama daktari yule mzee kuna kitu alikuwa akijua juu yangu na lawalawa na alitaka kunichomea kwa mke wangu juu ya mpenzi wangu Lawalawa. “Unamjua?” nikaulizwa tena.

“Ndio namjua” hatimaye nilijibu. Mke wangu, alitabasamu baada ya kauli yangu, akaonekana kuwa na shauku kubwa ya kumpata mwanamke huyo.
“Basi kama unaweza kumpata anaweza kuwa mkombozi wa mwanao?”dokta alihitimisha. Hakuonekana kujua wala kuwa na hisia kama mimi na Lawalawa kulikuwa na uhusiano wa siri.

Ni Lawalawa....Hawara wangu....Huyu huyu niliyekuwa na mpango wa kumfuata mjini Tabora kabla ya ligi daraja la kwanza kuanza. Ndiye awe mwokozi wa maisha ya mwanangu. Itawezekana? Atakubali hali nilimdanganya sikuwahi kuwa na mke wala mtoto.

Leo natakiwa nimfuate nimwambie nilimdanganya. Ninaye mke na mtoto mmoja, ambaye yupo hoi kitandani kwa saratani ya damu na yeye awe ndiye mwokozi wake. Atanielewa?? Vipi kuhusu penzi langu kwake. Ndio itakuwa mwisho wake, Je mimi niko tayari kumpoteza Lawalawa.? Jibu ni hapana. Je niko tayari kumpoteza mwanangu? Jibu pia ni hapana. Nifanyeje sasa?

Nilijiuliza mambo yote hayo tukiwa tumekwisha toka chumbani kwa daktari, nilikuwa pembeni ya kitanda alichokuwa amelala mtoto wangu, Maganga.
Penzi la Lawalawa na uhai wa mtoto wangu kipi zaidi? Jibu ni rahisi tu, uhai wa mwanangu ni zaidi . Basi lazima nimkabili Lawalawa nimweleze ukweli, naye anisaidie. Niliafiki mawazo hayo.

Nilimwita mke wangu na kumtaka ajitulize pale hospitali ya Bugando mimi nifunge safari ya kumfuata mwanamke yule mjini Tabora. “Umemjulia wapi huyo Lawalawa?” mke wangu aliniuliza.
“Ni shabiki wangu wa soka uwanjani,” nilimdanganya.
Aiseee
 
Sehemu ya 39

Kwenye soka la bongo kuna mambo mengi, kama jamaa wamefika bei nzuri hata kama mimi siwezi kupiga teke kapu la pesa” Side aliongea katika namna ya kutojali utetezi wangu, hata yeye aliamini nilikuwa nimechukua fedha.

“Side nielewe basi, wakati wote kwenye maisha yangu ya soka siwajawahi kufanya hila ya namna yoyote kuihujumu timu yangu.”

“Unataka kuniambia jamaa wanakusingizia?”
“Mwananipakazia Side, siwez kufanya ujinga huo.”
“Na unataka kunimbia jamaa wa Igogo Fc hawajakufuata kabisa kuongea na wewe.”
“Hajaniafuata mtu.”

“Mmh!!! Mbona inasemekana jana asubuhi ulikwenda kuonana nao?”swali hilo lilinishitua mno. Kwa kweli jamaa walikuwa wamewaza mbali sana.
“Jana sikwenda kuonana na mtu yeytote zaidi ya daktari” nilimwambia nikiwa nimesawikija kwa hasira.

“Unaumwa nini?” swali hili halikujibika. Sio kwamba sikuwa na jibu. Laa! bali niliona kumjibu swali lake ningelazmika kutoa hadithi yote iliyonipeleka Bugando kitu ambacho sikuwa tayari. “Unaumwa nini?” Side aliniuliza tena.

“Ni mambo yangu binafsi, sio lazima kila mtu ajue.” “Basi ndio hivyo comredi Ajibu, inasemekana umepewa mlungura ili usicheze.” Side aliendelea kukazia jambo lile.

“Kwa hiyo Side leo ningecheza tusingefungwa goli saba?”
Nilimuliza. Akabakia amenikodolea macho kama mpumbavu.

Tangu Side aliponiambia mambo hayo, nilikosa kabisa amani ya roho. Sikuitwa kuhojiwa na kiongozi yeyote juu ya jambo hilo ingawa liliendelea kuzungumzwa chini chini.
Siku ya pili, tuliondoka na kurudi mjini Tabora, bado hakuna kiongozi yeyote aliyeniuliza japokuwa walionekana kunichukia.

Kwa kuwa sikuwa nahusika na aina yoyote ya hila dhidi ya timu yangu, na mimi sikujisumbua kabisa kwenda na kuhoji juu ya skendo hiyo, niliendelea na shughuli zangu bila kujali uvumi huo. *****

Wiki tatu zilipita. Nikiwa mjini Tabora, angalau kidogo nafsi yangu ilipata ahuni juu ya kifo cha mtoto wangu. Kwa kuwa kilichokuwa kinaniunganisha na mke wangu ni mtoto ambaye naye amekwisha fariki. Niliweka nadhiri ya kutorudi kabisa kijijini kwetu.
Aisee
 
Sehemu ya 46

Siku iliyofuatia tulirudi kwa Majeed, tulimkuta anakunywa chai yeye na yule mwanamke aliyetukaribisha ile siku ya jana. Kimwonekano tu nikabaini yule mrembo alikuwa ni mke wa, mganga yule, jamaa alikuwa na mke mzuri sana. Hadi leo sijui mganga yule wa kienyeji alifanya fanyaje hadi akaweza kuwa na kifaa bomba kama kile.

Alitukaribisha jamvini, tukazungumza mawili matatu, kisha akatukaribishia kwenye kile chumba chake cha kiganga. Alivaa kanzu nyeusi na balaghashia nyekundu, akatoka nje kisha akarudi na kuku mweusi tii.

Akanipa nimshike yule kuku, halafu akatoa kipande cha sanda kwenye fuko la rambo, akampa Cholo ashike. Yeye akachukua kakitabu kadogo kalikokuwa kamendikwa kiarabu akaketi kitako.
“Wewe uliyeshika kuku sogea karibu yangu hapa.” Aliniambia.

Nikiwa na yule kuku mweusi, nilisogea karibu na miguu yake, kuku niliyekuwa nimemshika alikuwa akipiga kelele huku akijisuka suka na kuniparua na makucha yake.

“Mshike vizuri hadi nitakapokwambia umuachie...sawa?”
“...sawa.” nilitikia.

aliwasha ubani katika kichezo. Baada ya kuhakikisha kila kitu kipo sawa, mganga Mageed akaanza kusoma kile kitabu kidogo kilichoandikwa kwa lugha ya kiarabu(sio quran)

Wakati anaanza kusoma kile kitabu kuku niliyekuwa nimemshika akajisuka suka kwa nguvu na kupiga kelele, nikamkashika kwa nguvu zaidi. Mganga naye akazidi kusoma zile dua.

Akasoma na kusoma, mara yule kuku akanyong’onyea. Mganga Majeed kwa kuona hivyo akaniambia:
“Muachie sasa huyo kuku.” Taratibu nikamtenga chini, ule uchakaramu wa yule kuku ulikuwa haupo tena, alibaki amesimama, karegea kama ameshikwa na maradhi ya tauni. Hadi leo sijui zile dua zilikuwa zimeathiri kitu gani kwa kiumbe yule.

Mganga Mageed akaendelea kusoma dua zake kwenye kale kakitabu kakiganga , kadiri alivyozidi kusoma ndivyo kuku alivyizidi kunyong’onyea. Akaendelea kusoma. Mara yule kuku akaanguka chini. Akafa!!

Ilikuwa ni tukio la ajabu kuwahi kuliona, siku hiyo ndio nilisaidiki kwamba uchawi upo. Aliletwa kuku mwingine naye akasomewa dua hadi akafa. Kuku weusi karibu wanne, wote walikufa kwa kusomewa dua na mganga yule.
Baada ya hapo akachukua vile vipande vya sanda na kuwafunikia wale kuku wanne kisha akasema:
 
Sehemu ya 47

“Nitajieni majina ya wachezaji wote mnaotaka wawapishe kwenye nafasi zenu uwanjani.”

Tukaanza kumtajia, miongoni mwa majina niliyotaja ni mchezaji Mkongoman ambaye alikuwa tegemeo kwenye timu yetu Didir Bukungu na mwingine ni Felex Kisu, pande la mtu kutoka mkoani Mbeya.

Majina yote hayo yaliandikwa kwenye zile sanda zilizofunikiwa wale kuku. Cholo naye alitaja majina ya makipa wenzie wawili. “Kilichosalia ni kwenda makaburini na kuwazika hawa kuku juu ya kaburi jipya, kuwazika hawa kuku ni ishara ya kuwazika hao mahasimu wenu kwenye timu yenu, hawatopata namba tena.” Mganga alisema.

Nilijisikia furaha, niliona mambo yangu muda si mrefu yatakuwa mazuri. Jioni ilipotimu tulibeba ile mizoga ya kuku weusi, iliyofunikwa kwa sanda zenye majina ya wachezaji wenzetu, tayari kwa kwenda kuzikwa makaburini.

Baada ya kufika makaburini, tukaanza kutafuta kaburi jipya, ambalo tungelifukua na kuzika ile mizoga ya kuku.

WAKATI huo giza lilikuwa limekwishaingia. Eneo lile la makaburi, lilikuwa pweke na tulivu. Baada ya kutafuta kaburi jipya kwa muda, hatimaye tukapata makaburi mawili.

Kaburi moja lilikuwa la mtoto, jingine lilikuwa la mtu mzima. Kilichofuata baada ya hapo ni kuanza kufukua yale makaburi.Tulifukua kiasi kama mita moja. Baada ya hapo tukazika ile mizoga ya kuku.
 
Sehemu ya 48

Baada ya kumaliza, tukaondoka bila kutakiwa kugeuka nyuma. Tulirudi hadi kwenye kilinge cha yule mganga wa kienyeji. Akatuambia baada ya kumaliza kuzika wale kuku, jambo la mwisho ni kuoga dawa ya kuondoka nuksi na mikosi.

Nyumbani kwa mganga tulifanya mambo yote. Mimi na Cholo tulioga kwa zamu maji yenye dawa ya kuondoa mikosi, kisha tukachanjwa chale, miguuni, kichwani, kifuani na mikononi.
“Hapa sasa mpo safi, mnaweza kurudi Dar, nafasi ya kucheza mpira mtaipata,”mganga yule kijana alituambia.

Siku ya pili, tuliondoka Unguja na boti ya asubuhi. Nyakati hizo timu ilikuwa kambini. Hivyo, baada ya kufika Dar es salam, ikabidi tusiongozane pamoja kwenda kuripoti klabuni. Nilitangulia mimi, jioni Cholo naye akaripoti.

Hakuna mtu hata mmoja aliyetambua ama hata kuhisi kwamba mimi na Cholo tulikuwa Zanzibar kwa mganga wa kienyeji kuwaroga baadhi ya wachezaji wenzetu. Siri hiyo ilibaki vifuani mwetu.

Siku ya pili asubuhi, tuliungana na wachezaji wenzetu kwenye mazoezi ya pamoja, tulikuwa tukijiandaa na mchezo wa ligi na moja ya timu kubwa kabisa hapa nchini, ambayo maskani yake ya timu hiyo ni Kariakoo, jijini Dar.

Ilikuwa ni mechi iliyokuwa ikingojewa kwa hamu kubwa kutokana na mambo mawili, kwanza ubora na ukubwa wa timu hiyo yenye mashabiki wengi hapa nchini, lakini ilikuwa ni ubora wa timu yetu ya Mzizima.
Tulikuwa na kikosi bora kabisa kipindi hicho, jambo kubwa zaidi, katika msimamo wa ligi kuu timu yetu ilikuwa inaongoza kileleni.

Kila mchezaji kwenye timu, alikuwa na presha na mchezo huo, kila mtu alikuwa amedhamiria kujitoa kwa nguvu na uwezo wake wote kwa ajili ya mechi hiyo.
Asubuhi hiyo tulifanya mazoezi ya viungo, kisha badaye tukafanya mazoezi ya pumzi kabla ya kumalizia yale ya kimbinu ambapo hufanyika uwanjani kwa mgawanyo wa wa timu mbili.
Kasheshe lilianzia hapo.

Nakumbuka kocha likuwa akiwapa mbinu wale washambuliaji wawili tegemeo, yule Mkongomani, Didier Bukungu na Felex Kisu, pande la mtu kutoka mkoani Mbeya. Alikuwa akiwaeleza namna ya kushambulia kwa kasi kupitia pembeni huku viungo washambuliaji nao wakisogea karibu zaidi na wale washambuliaji.
 
Sehemu ya 49

Na uongo mbaya wale jamaa walikuwa na uwezo wa ajabu sana. Maelekezo ya kocha, waliyafuata na kuyafanya kwa asilimia mia moja. Mimi kama mshambuliaji, pia nilitakiwa kumwonyesha kocha kile ambacho alikuwa akikitaka.

Naam! Hata mimi nilifanya kile aliachokitaka mwalimu kwa ufanisi mkubwa. Bahati mbaya kama nilivyosema awali, bado sikuwa chaguo namba moja kwa kocha yule Mzungu.

Tukiwa tunaendelea na mazoezi, sijui kilitokea kitu gani, Felex Kisu, pande la mtu kutoka mkoani Mbeya, alikuwa akiambaa na mpira kuelekea golini.
Kipa namba moja wa timu yetu, kuona Felex anakaribia langoni kwake, akatokea kwenda kuokoa hatari.

Felex naye kuonyesha umahiri wake, akampiga chenga ya maudhi kipa yule, lakini tayari goli kipa naye alikwishaliona kosa hilo, kuonyesha ubora wake akacheza rafu mbaya sana. Mpira ukatoka nje.
Wachezaji wale wawili wakawa wanagaagaa chini huku wote wawili wakilia kwa maumivu mkali.

“Wamevunjika!” mtu mmoja alibweka.
Wachezaji wote tukasogea kwenda kuwaangala. Nilichokiona kilitisha. Jamaa walikuwa wamevunjika vibaya sana. Mfupa wa mguuni kwa yule mshambuliaji ulikuwa umetokeza nje.

Yule golikipa yeye alikuwa akilia huku akishika mbavu zake, kulikuwa na kila dalili kuwa alikuwa amevunjika mbavu.
Mimi na Cholo tuliangaliana kisha tukapeana ishara ya kufurahia tukio lile. Tuliamini uchawi wa yule mganga wa Unguja ulikuwa umefanya kazi.

Wakati taharuki ikiwa imetawala, ni mimi na Cholo peke yetu ndio tulikuwa tukishangalia moyoni. Tuliamini kupitia ajali ile, ulikuwa ni mwanzo wa kupata nafasi kwenye kikosi cha kwanza kwenye timu ile.

Jamaa walipewa huduma ya kwanza na madaktari wa timu, kisha wakaingizwa kwenye gari na kukimbizwa Hospitali ya Muhimbili.

Kwa kuwa muda wa mazoezi ulikuwa umefikia ukingoni, tuihairisha mazoezi kwa siku hiyo. Kuumia kwa wachezaji wale wawili. Kulimfanya kocha na benchi lake la ufundi kuchanganyikwa.

Ilahali iliniudhi mno, sikupenda namna benchi la ufundi lilivyokuwa likihaha kwa kuumia kwa jamaa wale. Nilikuwa na wivu sana.

“Umeona mambo yameanza kujibu,” Cholo aliniambia baada ya kufika nyumbani.
“Yule mganga kiboko.”
 
Sehemu ya 50

Bado windo linaendelea, kwako wewe ni kama umemaliza, maana wewe unaweza kucheza nafasi yoyote akitoka Felex ama ama Mkongoman, mimi bado kipa namba mbili naye dawa yake inachemka,” Cholo alisema.

Sote tukafurahia. Kuumia kwa Felex, niliamini panga pangua lazima mimi nianze dimbani siku ya mchezo.
Siku ya pili, taarifa za madaktari zilitoka. Zilionesha wachezaji wale walikuwa wamevunjika vibaya sana, Felex alikuwa amevunjika mfupa ambao ulitoboa ngozi, wakati yule kipa yeye alikuwa amevunjika mbavu ya ubavu wa kulia.

Ripoti zilionesha jamaa wangekaa nje ya uwanja kwa miezi 10. Zilikuwa ni taarifa za kushitua, lakini kwetu zilikuwa ni taarifa nzuri mno.

***** SIKU ya mchezo kati yetu na timu moja kubwa hapa nchini, (nisingependa niitaje jina) ila itoshe tu kujua timu hiyo kubwa inatokea Kariakoo jijini Dar, iilikuwa inakaribia.

Homa ya mchezo ilikuwa kubwa, kocha Mzungu alikwishanieleza waziwazi kwamba, nitakuwa kwenye kikosi kitakochoanza siku hiyo.

Nilikuwa na furaha kubwa, kwa kuwa nilikuwa nazijua timu zile za Kariakoo mara nyingi ukizifunga, kwanza unakuwa maarufu, jina lako litaongelewa wiki nzima huko mtaani na kwenye magazeti mbalimbali. Pia huwa ni rahisi kusajiriwa na timu hiyo au hata yule hasimu wake. Niliapa kupambana siku hiyo.

Lengo langu ilikuwa ni kuonyesha uwezo, nipate nafasi ya kuwa kwenye timu kubwa na yenye mashabiki wengi Afrika Mashariki. Nikiamini hilo lingekuwa ni daraja jepesi la kunifikisha kwenye soka la kimataifa.

Siku moja kabla ya mchezo nilipokea barua kutoka kwa mpenzi wangu Lawalawa. Barua hiyo aliniletea meneja wa timu, ambaye muda mwingi alikuwa na wachezaji kambini.

Nilipoipokea barua ya mwanamke huyo ni mpendaye, sikupenda kuwa na pupa kuisoma, kwa kuwa wakati huo nilikuwa katika presha kubwa ya mechi niliona nitaisoma wakati ambapo akili yangu itakuwa imetulia.

Hayawi hayawi, mwisho yakawa. Siku ya mchezo ikawadia. Ilikuwa ni asubuhi ya siku ya Ijumaa, Siku yenye rapsha na pilika za huku na kule.

Kila kona ya jiji ajenda kubwa ilikuwa ni mchezo kati ya timu iliyokuwa bora kipindi hicho, Timu ya Mzizima Fc dhidi ya timu kongwe na kubwa kutoka Kariakoo.
 
Sehemu ya 51

Asubuhi hiyo, baada ya kupata stafutahi ya asubuhi, wachezaji tuliruhusiwa kuchangamsha akili, kwa mambo mbalimbali, mfano, kuangalia runinga, kusikiliza muziki, kutizama filamu na kadhalika.

Mimi nilikuwa nasikiliza muziki kwenye walkman yangu ya CD, nikiwa kwenye utulivu mkubwa. Mara, nikaikumbuka barua ya mpenzi wangu Lawalawa. Mwanamke mrembo Chotara.

Haraka nikalindeea begi langu la nguo na kutoa bahasha iliyokuwa na barua. Nikairarua bahasha hiyo, nikaichomoa.

Ilikuwa ni barua yenye maneno machache, Niliketi na kuanza sofani na kuanza kuisoma barua ile. Kadiri nilivyokuwa nikisoma mstari mmoja baada ya mwingine ndivyo mapigo yangu ya moyo yakawa yananienda kasi hadi nikaogopa.

Barua Iliandikwa hivi:
Mpenzi Ajibu
Bila shaka u mzima na unaendelea na vema na shughuli zako.
Lengo la ujumbe huu ni kukwambia kwamba, nimepitisha maamuzi magumu kwangu lakini mabaya kwako.

Kuanzia sasa, unavyosoma barua hii, mimi sio wako tena. Muda wowote nitafunga ndoa takatifu na mwanaume mwingine kutoka nchini Yemen.

Ajibu, nasikitika kukukwambia kwamba, nina mimba ya miezi minne ya mume wangu huyo mtarajiwa, huna budi kunisahau maishani mwako. Endelea na maisha yako ya soka, mimi na wewe hadithi yetu imeishia hapa.
Wako wa zamani.
Lawalawa.

Nilipomaliza kusoma barua hiyo, mwili ulikuwa unanitetemeka kama mgonjwa wa homa kali. Jasho jekejeke lilikuwa linanichuruzika maungoni.

Mate yalikuwa yamenikauka kinywani, donge kavu lilikuwa limenikaba kooni, barua kutoka kwa mwanamke ninaye mpenda ilikuwa inanikaanga vibaya sana. “Lawalawa!!!” nilinong’ona. Nilihisi dunia inazunguka kwa kasi mno. Akili yangu ilikuwa imechanganyikiwa.

Nilitamani muda huo huo, niondoke nikaonane na mpenzi wangu yule, anieleze maneno yale kwa mdomo wake. “Ajibu umesikia hiyo?” Cholo, rafiki yangu wa wakati wote alinisemesha, uso wake ulionekana kuwa na furaha. Nikaishia kumwangalia tu bila kumjibu swali lake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom