Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 152,959
- 453,698
Mtunzi Ally Katalambula
Sehemu ya 01
SIKUJUA kama nina kipaji cha mpira wa miguu, hadi watu wa pembeni walipoanza kunieleza hivyo. Mtu wa kwanza kuniambia nina kitu miguuni mwangu, alikuwa ni mwalimu wangu wa michezo. Mwalimu Keneth Edson.
Kipindi hicho nilikuwa nina miaka 13 na nilikuwa darasa la tano. Mchezo wa mpira wa miguu kwetu tulicheza kama sehemu ya kujifurahisha. Faida pekee iliyoujaza moyo wangu katika mchezo huo ni SIFA.
Nilipokuwa nikisifiwa kwa umahiri nichezapo mchezo wa soka, ilitosha kabisa kuyafurahia maisha, hakukuwa na la ziada lenye thamani katika kipindi hicho cha utoto zaidi ya sifa kemkem nilizo mwagiwa niwapo uwanjani.
Sikuwa na matarajio yoyote kwenye mchezo wa soka. Sio kwa kutojua tija inayopatikana katika mchezo huo bali hata kuamini.
Nani angeniona huku kijijini Nyamakobiti? Kijijini. Makalioni mwa Tanzania. Kiongozi gani wa soka angesadiki, eti mimi nina kipaji zaidi ya vijana wa Dar es salam?
Fikra hizi zilinifanya nione na kuamini, ukomo wa soka langu ni pale nitakapomaliza shule. Kwa kuwa mchezo huo hakuwa kipaumbele changu maishani, nilikazana na masomo ili niweze kufauli kwenda sekondari. Mara chache sana nilipopata nafasi nililisakata kabumbu barabara.
kiasili mimi ni msukuma wa Bariadi, na ninatokea au niseme nilikuwa natoka katika familia ya wafugaji. Wazazi wangu walilowea mkoa wa mara wilaya ya Serengeti katika kijiji cha Nyamakobiti nje kidogo ya mji wa Maji moto.
Pamoja na kwamba baba yangu alisifika kwa utajiri wa idadi kuwa ya ng’ombe, lakini hatukuwa tunaishi maisha bora. Kwa kweli hatukutofautiana na watoto wa wakulima na masikini wengine pale kijijini!. Nitaeleza kwa nini nasema kauli hiyo.
Kwa milongo miwili iliyopita, watu wengi waliokuwa mashuhuri katika vijiji vya wafugaji, walijisikia fahari kusifiwa kwa utajiri wa idadi kubwa ya mifugo, hususasani Ng’ombe. Ilikuwa haijalishi makazi, mavazi na chakula unachokula.
Baba yangu alikuwa ni moja ya matajiri wa aina hiyo, pamoja na kuwa na idadi kubwa ya mifugo, lakini kula yetu na lala yetu ilikuwa ni duni mno, mavazi yangu yalikuwa yamechanika chanika na kujaa viraka
Sehemu ya 01
SIKUJUA kama nina kipaji cha mpira wa miguu, hadi watu wa pembeni walipoanza kunieleza hivyo. Mtu wa kwanza kuniambia nina kitu miguuni mwangu, alikuwa ni mwalimu wangu wa michezo. Mwalimu Keneth Edson.
Kipindi hicho nilikuwa nina miaka 13 na nilikuwa darasa la tano. Mchezo wa mpira wa miguu kwetu tulicheza kama sehemu ya kujifurahisha. Faida pekee iliyoujaza moyo wangu katika mchezo huo ni SIFA.
Nilipokuwa nikisifiwa kwa umahiri nichezapo mchezo wa soka, ilitosha kabisa kuyafurahia maisha, hakukuwa na la ziada lenye thamani katika kipindi hicho cha utoto zaidi ya sifa kemkem nilizo mwagiwa niwapo uwanjani.
Sikuwa na matarajio yoyote kwenye mchezo wa soka. Sio kwa kutojua tija inayopatikana katika mchezo huo bali hata kuamini.
Nani angeniona huku kijijini Nyamakobiti? Kijijini. Makalioni mwa Tanzania. Kiongozi gani wa soka angesadiki, eti mimi nina kipaji zaidi ya vijana wa Dar es salam?
Fikra hizi zilinifanya nione na kuamini, ukomo wa soka langu ni pale nitakapomaliza shule. Kwa kuwa mchezo huo hakuwa kipaumbele changu maishani, nilikazana na masomo ili niweze kufauli kwenda sekondari. Mara chache sana nilipopata nafasi nililisakata kabumbu barabara.
kiasili mimi ni msukuma wa Bariadi, na ninatokea au niseme nilikuwa natoka katika familia ya wafugaji. Wazazi wangu walilowea mkoa wa mara wilaya ya Serengeti katika kijiji cha Nyamakobiti nje kidogo ya mji wa Maji moto.
Pamoja na kwamba baba yangu alisifika kwa utajiri wa idadi kuwa ya ng’ombe, lakini hatukuwa tunaishi maisha bora. Kwa kweli hatukutofautiana na watoto wa wakulima na masikini wengine pale kijijini!. Nitaeleza kwa nini nasema kauli hiyo.
Kwa milongo miwili iliyopita, watu wengi waliokuwa mashuhuri katika vijiji vya wafugaji, walijisikia fahari kusifiwa kwa utajiri wa idadi kubwa ya mifugo, hususasani Ng’ombe. Ilikuwa haijalishi makazi, mavazi na chakula unachokula.
Baba yangu alikuwa ni moja ya matajiri wa aina hiyo, pamoja na kuwa na idadi kubwa ya mifugo, lakini kula yetu na lala yetu ilikuwa ni duni mno, mavazi yangu yalikuwa yamechanika chanika na kujaa viraka