Simulizi: Scaila Michael

Naomba kuuliza, Mrisho mpoto aliwahi kuimba tabia ya mtu ni kama ngozi ya mwili hauwezi kuibadili, Mbona hapo mzee baba kafanikiwa kumdalisha tabia huyo mwanadada, so ukweli ni upi hapo unaweza kubadili tabia ya mtu?
 
Naomba kuuliza, Mrisho mpoto aliwahi kuimba tabia ya mtu ni kama ngozi ya mwili hauwezi kuibadili, Mbona hapo mzee baba kafanikiwa kumdalisha tabia huyo mwanadada, so ukweli ni upi hapo unaweza kubadili tabia ya mtu?
Inawezekana mkuu
 
SEHEMU YA 20

Yaani nilivyokuwa nikiwaangalia marafiki wa Scaila niligundua walikuwa ‘malaya’ tu lakini kwa jinsi nilivyokuwa nikimpenda msichana huyo, nilimuona kama malaika vile, yaani eti malaika alikuwa kwenye kundi la mashetani.

Baada ya kuwasindikiza, akarudi na nikaanza kuongea naye mambo mengi sana. Alionekana kuwa mtu aliyechangamka sana, alinisifia kwa jinsi nilivyokuwa na mambo mengine mengi.
“Kwanza naomba namba yako,” nilimwambia.

“Tena afadhali! Jana nilitaka tuongee lakini ilishindikana!” aliniambia.
Tukabadilishana namba na mambo mengine kuendelea. Sikufichi, kipindi hicho nilijisikia furaha isiyo kifani, kuwa karibu na Scaila ilionekana kuwa bahati moja kubwa mno.

Pale kochini alipokuwa, nikamsogelea, nikamwangalia usoni na kuanza kutoa tabasamu pana ambalo lilikuwa ni kama matayarisho ya kitu fulani.

“Unataka kufanya nini? Hapana! Hapana Nye...” aliniambia huku akitoa tabasamu lakini hata kabla hajamaliza, alichokuwa akitaka kunikataza tayari nikaanza kukifanya, tukaanza kubadilishana mate kwa sekunde kadhaa, halafu tukaanza kuangaliana.

“Oh! It my fault, I’m sorry...” (Oh! Ni kosa langu, samahani...) nilimwambia huku tukiangaliana.

“Kwa nini umenifanyia hivi?” aliniuliza.
“Ndiyo maana nimesema samahani! Nilizidiwa!” nilijitetea, nikaona haitoshi, kulikuwa na kiumbe kingine nilikuwa sijakisingizia kesi, haraka sana nikakisingizia.

“Shetani alinipitia...”
Scaila akatabasamu, hapohapo haraka sana akanisogelea na kuanza tena. Niliona mtoto alidhamiria hivyo kumshika zaidi kwa dakika moja na kuachiana.

Naweza kusema huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa mapenzi yetu. Nikatokea kumpenda Scaila kuliko mwanamke yeyote yule. Niliona kama malaika fulani ambaye Mungu aliamua kunishushia, kumbe sikujua kama mwanamke huyu alikuwa na roho mbaya, ya kikatilia hata zaidi ya shetani.

Nilihisi kama nimeokota embe chini ya muarobaini kumbe niliopata shubiri chini ya mkomamanga.


|
|
|


Hii hadithi itakuwa inatoka Jumatatu na Alhamisi.
Twende kazi sasa "...shubiri kimejiuza...".
 
SEHEMU YA 14.

“Una picha zake?”
“Hapana! Lakini ni mzuri..yaani ni mzuri! Grace, duniani kuna wanawake wazuri sana. Yule Scaila, yaani ni mzuri balaa,” nilimwambia kwa msisitizo, yaani yote hiyo nilitaka aamini kwa asilimia mia moja nilichokuwa nikimwambia.

Grace alibaki akicheka tu. Huyu alikuwa mfanyakazi wangu, nililetewa na dada yangu kutoka mkoani Mwanza, alikuwa Msukuma mzuri, mwenye umbo matata sana ila kipindi alichokuwa amekuja jijini Dar es Salaam, hakuwa na muonekano mzuri.

Nilikubali awe dada wa kazi, kwanza kitu cha kwanza nilichokifanya ni kuanza kumbadilisha. Huyu Grace alitakiwa kuwa na muonekano mzuri, msafi kwa sababu pale nyumbani kwangu kulikuwa na marafiki zangu wengi waliokuwa wakifika kunitembelea.

Kipindi cha kwanza walimchukulia kawaida sana ila baada ya kumbadilisha, kila mtu aliyekuwa akifika nyumbani hapo alichanganyikiwa.

Alipendeza mno, wengi waliniambia niwaunganishe naye ila sikutaka kufanya hivyo kwa sababu nilijua ni kwa namna gani marafiki zangu walivyokuwa wahuni, hawakuwa waoaji, na wale waoaji hawakutaka kutulia kwenye ndoa zao kabisa.

“Hebu cheki wezele ile...dah! Nyemo unafaidi sana! Yaani huyu mtoto ukimuweka kwenye kumi na nane zako, usiku mzima wewe unaimba wimbo wa CCM mbele kwa mbele,” aliniambia rafiki yangu, aliitwa Juma Hiza.
“Acha ujinga wako! Dada yangu huyo,” nilimwambia Juma.

“Sasa inakuwaje?”
“Kuhusu nini?”
“Nimeshachanganyikiwa, yaani siambiwi wala sisikii hapa,” aliniambia.
“Tubadilishane basi. Namuomba Amina!” nilimwambia, huyo alikuwa dada yake.
“Hahah! We mjinga sana, nikupe Amina mimi!” aliniambia.

“Kwani kuna ubaya gani! Si mara moja moja unakuja kula kwa shemeji, ukiniona unanipiga mizinga,” nilimwambia kwa utani.

Juma alikuwa na dada yake aliyeitwa Amina, alimpenda mno, alimchunga sana na wanaume hasa sisi marafiki zake kwa kuwa tulikuwa tunajuana ni watu wa aina gani.

Hakutaka kusikia kitu chochote kuhusu Amina, alijitahidi kumlinda na sisi lakini siku ambayo nilikutana naye maeneo ya Mwenge ndipo nilipochukua namba yake na kuisave kama Fundi Bomba.
Duuh
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom