Simulizi: Scaila Michael

SEHEMU YA 25

Kwa hayo yote niliyokuwa nikiyafanya, unaweza kuona ni kwa jinsi gani nilikuwa nikimpenda Scaila, kwangu, msichana huyo alikuwa kila kitu na nilidhamiria kumuoa na kuishi naye maisha yangu yote.

Tulifanya mambo mengi sana chumbani, kitu ambacho nilikuwanacho makini ni kumpa ujauzito tu. Ndani kwangu nikaanza kuwa na mipira ya kiume, ilikuwa ni kwa ajili ya siku zote ambazo aliniambia alikuwa kwenye hatari.

Maisha yalikuwa matamu, muda mwingi nilikuwa na tabasamu pana, kwa kipindi hicho hata biashara zangu zilikuwa zikifanya vizuri kwa sababu sikuwa na stresi, nilipambana kwa ajili ya Scaila na watoto ambao baadaye tungekwenda kuwapata.

Wakati hayo yote yakiendelea huku nikijiona mwanaume mwenye bahati sana, kwa chini sana nilikuwa nikifanya mikakati ya kufunga ndoa na msichana huyo.

Japokuwa sikuwa nimewaonyesha lakini niliwaambia kuhusu mpango wangu, nilihitaji mikakati ianze mapema kwani nilidhamiria ndani ya miezi sita nimuoe msichana huyo.

Huo ndiyo upumbavu mkubwa ambao niliufanya. Yaani sikuwa nikimfahamu Scaila kwa undani lakini nilihitaji kufunga naye ndoa.

Sikufanya kwa kupenda, nilifanya kwa sababu mapenzi yangu juu yake yalikuwa makubwa kupita kawaida. Nilipomwambia Hiza na Ngumije, wakaahidi kunifanyia mipango yote ila walitamani sana kuonana na huyo shemeji yao.
“Hilo halina tatizo!” niliwaambia.
“Ila utatakiwa kufanya jambo moja,” alisema Hiza.

“Lipi tena Hiza?”
“Umekuwa na presha sana ya kutaka kufunga ndoa na huyo msichana, kitu cha msingi unachotakiwa ni kuanza kuishi naye, japo kwa miezi kadhaa ili umfahamu kwa undani,” aliniambia Hiza, japokuwa wakati mwingine alikuwa na masihara sana lakini kile alichoniambia muda huo kilikuwa cha muhimu.

“Anachokisema Hiza ni muhimu sana. Nyemo! Ndoa si kitu cha mchezo mchezo mshikaji wangu, unapoingia kwenye ndoa ni kama umejifunga pingu za maisha, tena hapo kwa nyie Wakristo mpaka mmoja wenu afe,” alisema Ally huku akiniangalia.

“Ni jambo sahihi pia!”
“Basi zungumza naye,” aliniambia Ally.
“Sawa.”
 
SEHEMU YA 26

Nilikubaliana nao, wazo lao halikuwa baya, kilikuwa kitu kizuri sana, kuzungumza na Scaila halikuwa tatizo lolote lile, ilikuwa kazi nyepesi mno ila niliitaji kuzungumza na mama yake na kumwambia ukweli wa mambo.

Kabla ya kumwambia mama yake, nikaamua kumwambia yeye juu ya mpango wa kuishi naye kabla ya ndoa. Wala hakupinga, akakubali na kuniambia kwamba mama yake hakuwa na tatizo lolote lile.

“Kweli?”
“Wala usijali mpenzi!”
Hilo ndilo likafanyika, baada ya siku tatu, huyu Scaila akahamia nyumbani kwangu na kuanza kuishi naye. Kwa kweli kipindi hicho nilikuwa na furaha tele, niliamini kuwa watu wanaokutana katika mazingira ya utata mwingi huishi maisha marefu wakiwa pamoja.

Kumbuka kwamba mpaka kipindi hicho sikujua chochote kile kuhusu Scaila, kwangu aliendelea kuonekana kama malaika aliyeshushwa kutoka Mbinguni.

Alikuwa na sifa zote, kitandani alikuwa mtu hatari, alijua kucheza michezo ya hatari mpaka wakati mwingine nikahisi kama kuna siku ingetokea nikamsaliti, basi hakika nisingeweza kupata ufundi mwingi kama aliokuwa akinipa tulipokuwa faragha.

Mara nyingi huwa sifuatilii simu yake, nilipanga hivyo. Kwa kawaida kwenye simu kunakuwa na majanga mengi, sikutaka kuona hayo yakitokea, na siku zote nilikuwa nikimwambia awe huru na simu yake, sikutaka kabisa kuipekua simu yake na kuangalia kilichokuwa kikiendelea.

“Unaniambia hivyo ili nisiwe naangalia simu yako?” aliniuliza kiutani huku akitabasamu.

“Kuangalia yangu ruksa, wala sijakuzuia,” nilimwambia, na mimi nikaanza kutoa tabasamu.

“Basi nitakuwa naiangalia kila siku! Sitaki kuchukuliwa mume wangu,” aliniambia Scaila, alikuwa akitania lakini nilipomwangalia usoni, wakati mwingine alionekana kumaanisha alichokuwa akikizungumza.

Maisha yaliendelea. Nilikuwa na biashara zangu tatu ambazo ziliniweka mjini na kwa mwezi zilikuwa zikiniingizia kama milioni tatu.

Nilipanga hapo Kijitonyama lakini kipindi hicho nilikuwa nikijenga nyumba yangu mwenyewe huko Boko. Hilo nilimueleza Scaila, nilitamani agundue mwanaume aliyekuwa naye hakuwa mbabaishaji, ni mtu aliyesimama kwenye maendeleo, nilipenda kuendelea kuliko starehe kama vijana wengine.
 
SEHEMU YA 27

Wakati mwingine nilimchukua na kwenda naye huko ilipokuwa nyumba hiyo, mafundi walikuwa wakiendelea kuijenga kwa nguvu kubwa, kila siku ilikuwa ni lazima wafike hapo na kuendelea na mambo yao.

Nilipanga kuhamia ndani ya nyumba hiyo siku ambayo nitafunga ndoa na Scaila. Nilimueleza hilo kabisa lakini sikutaka kumwambia ni siku gani nilitamani sana kumuoa.

Nakumbuka siku hiyo ilikuwa ni Jumapili ya mwezi wa tatu, nilipokea simu kutoka kwa Hiza na Ally ambao waliniambia walikuwa wakija nyumbani kumuona shemeji yao maana kila siku niliwaambia waje kumuona ila walikuwa na mambo mengi.

Nilimwambia Scaila, nikamwambia ni lazima ahakikishe anavaa vizuri, anapendeza ili marafiki hao watakapokuja basi wachanganyikiwe na kuona nimekuwa mwanaume ninayejua kuchagua mwanamke mzuri.

Hawa wawili huwa wananijua, sikuwa mtu mwepesi kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi, ninapenda sana kukaa singo kwa kipindi kirefu nikifanya mambo yangu binafsi ila ninapoamua kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi, huwa ninamchagua mwanamke mzuri mno.
Walinizoea hivyo tangu tulipokuwa chuo mpaka kipindi hicho.

Katika kipindi chote huko nyuma waliniambia siku ambayo ningeoa, basi ningemuoa mwanamke mbaya kuliko wote katika dunia hii kwa sababu tu nilipenda kutembea na wanawake wazuri.

“Huyo mkeo, najua atakuwaje! Nishapata picha yale,” aliniambia Hiza huku akicheka, kipindi hicho tulikuwa chuo.
“Mke wangu atakuwa mkali sana, zaidi ya mkeo, zaidi ya mke wa Ally, yaani atakuwa pini, pini kweli,” nilimwambia.
“Hahaha! Mzee baba utachagua koroma!” alisema Ally.

“Mtaona tu.”
Maneno hayo niliyakumbuka vilivyo, niliwatambia sana na sasa ulikuwa muda wa kuwaonyeshea nilikuwa makini kwa kile nilichowaambia miaka ya nyuma, niliamini kila mmoja angemkubali huyu Scaila kwani hakuwa na uzuri wa kawaida.

Ilipofika majira ya saa tisa alasiri, wakanipigia simu na kuniambiwa walikuwa njiani wakija. Nikawakaribisha na kumwambia Scaila ajiandae.

“Wanakuja!” nilimwambia.
“Haina shida. Nawasubiri!” alisema Scaila, hapohapo akamwambia Grace aandae chakula kabisa kwani muda si mrefu wageni wangeingia.
 
SEHEMU YA 27

Wakati mwingine nilimchukua na kwenda naye huko ilipokuwa nyumba hiyo, mafundi walikuwa wakiendelea kuijenga kwa nguvu kubwa, kila siku ilikuwa ni lazima wafike hapo na kuendelea na mambo yao.

Nilipanga kuhamia ndani ya nyumba hiyo siku ambayo nitafunga ndoa na Scaila. Nilimueleza hilo kabisa lakini sikutaka kumwambia ni siku gani nilitamani sana kumuoa.

Nakumbuka siku hiyo ilikuwa ni Jumapili ya mwezi wa tatu, nilipokea simu kutoka kwa Hiza na Ally ambao waliniambia walikuwa wakija nyumbani kumuona shemeji yao maana kila siku niliwaambia waje kumuona ila walikuwa na mambo mengi.

Nilimwambia Scaila, nikamwambia ni lazima ahakikishe anavaa vizuri, anapendeza ili marafiki hao watakapokuja basi wachanganyikiwe na kuona nimekuwa mwanaume ninayejua kuchagua mwanamke mzuri.

Hawa wawili huwa wananijua, sikuwa mtu mwepesi kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi, ninapenda sana kukaa singo kwa kipindi kirefu nikifanya mambo yangu binafsi ila ninapoamua kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi, huwa ninamchagua mwanamke mzuri mno.
Walinizoea hivyo tangu tulipokuwa chuo mpaka kipindi hicho.

Katika kipindi chote huko nyuma waliniambia siku ambayo ningeoa, basi ningemuoa mwanamke mbaya kuliko wote katika dunia hii kwa sababu tu nilipenda kutembea na wanawake wazuri.

“Huyo mkeo, najua atakuwaje! Nishapata picha yale,” aliniambia Hiza huku akicheka, kipindi hicho tulikuwa chuo.
“Mke wangu atakuwa mkali sana, zaidi ya mkeo, zaidi ya mke wa Ally, yaani atakuwa pini, pini kweli,” nilimwambia.
“Hahaha! Mzee baba utachagua koroma!” alisema Ally.

“Mtaona tu.”
Maneno hayo niliyakumbuka vilivyo, niliwatambia sana na sasa ulikuwa muda wa kuwaonyeshea nilikuwa makini kwa kile nilichowaambia miaka ya nyuma, niliamini kila mmoja angemkubali huyu Scaila kwani hakuwa na uzuri wa kawaida.

Ilipofika majira ya saa tisa alasiri, wakanipigia simu na kuniambiwa walikuwa njiani wakija. Nikawakaribisha na kumwambia Scaila ajiandae.

“Wanakuja!” nilimwambia.
“Haina shida. Nawasubiri!” alisema Scaila, hapohapo akamwambia Grace aandae chakula kabisa kwani muda si mrefu wageni wangeingia.
@shunie
 
SEHEMU YA 27

Wakati mwingine nilimchukua na kwenda naye huko ilipokuwa nyumba hiyo, mafundi walikuwa wakiendelea kuijenga kwa nguvu kubwa, kila siku ilikuwa ni lazima wafike hapo na kuendelea na mambo yao.

Nilipanga kuhamia ndani ya nyumba hiyo siku ambayo nitafunga ndoa na Scaila. Nilimueleza hilo kabisa lakini sikutaka kumwambia ni siku gani nilitamani sana kumuoa.

Nakumbuka siku hiyo ilikuwa ni Jumapili ya mwezi wa tatu, nilipokea simu kutoka kwa Hiza na Ally ambao waliniambia walikuwa wakija nyumbani kumuona shemeji yao maana kila siku niliwaambia waje kumuona ila walikuwa na mambo mengi.

Nilimwambia Scaila, nikamwambia ni lazima ahakikishe anavaa vizuri, anapendeza ili marafiki hao watakapokuja basi wachanganyikiwe na kuona nimekuwa mwanaume ninayejua kuchagua mwanamke mzuri.

Hawa wawili huwa wananijua, sikuwa mtu mwepesi kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi, ninapenda sana kukaa singo kwa kipindi kirefu nikifanya mambo yangu binafsi ila ninapoamua kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi, huwa ninamchagua mwanamke mzuri mno.
Walinizoea hivyo tangu tulipokuwa chuo mpaka kipindi hicho.

Katika kipindi chote huko nyuma waliniambia siku ambayo ningeoa, basi ningemuoa mwanamke mbaya kuliko wote katika dunia hii kwa sababu tu nilipenda kutembea na wanawake wazuri.

“Huyo mkeo, najua atakuwaje! Nishapata picha yale,” aliniambia Hiza huku akicheka, kipindi hicho tulikuwa chuo.
“Mke wangu atakuwa mkali sana, zaidi ya mkeo, zaidi ya mke wa Ally, yaani atakuwa pini, pini kweli,” nilimwambia.
“Hahaha! Mzee baba utachagua koroma!” alisema Ally.

“Mtaona tu.”
Maneno hayo niliyakumbuka vilivyo, niliwatambia sana na sasa ulikuwa muda wa kuwaonyeshea nilikuwa makini kwa kile nilichowaambia miaka ya nyuma, niliamini kila mmoja angemkubali huyu Scaila kwani hakuwa na uzuri wa kawaida.

Ilipofika majira ya saa tisa alasiri, wakanipigia simu na kuniambiwa walikuwa njiani wakija. Nikawakaribisha na kumwambia Scaila ajiandae.

“Wanakuja!” nilimwambia.
“Haina shida. Nawasubiri!” alisema Scaila, hapohapo akamwambia Grace aandae chakula kabisa kwani muda si mrefu wageni wangeingia.
Mmmh natabiri kuumbuka kwa Scaila pindi Ally na Hiza wakimuona.... ngoja tuone.
 
SEHEMU YA 28

Baada ya dakika kadhaa, wakafika, nikawakaribisha na kukaa kwenye makochi. Scaila hakuwepo, alikuwa jikoni akiandaa chakula kwani tayari alisikia wageni wamefika na nilikuwa nikiongea nao sebuleni.

“Hebu muite kwanza,” alisema Ally, alionekana kuwa na presha kubwa ya kumuona Scaila.

“Tulia kwanza! Acha papara!” nilimwambia
“Haiwezekani!” alisema Hiza, kama kawaida yake akaanza kuita.
“Scaila...hebu njoo huku kwanza tukuone,” alisema Hiza kwa sauti.

Nilisikia Scaila akitoka jikoni na kuja pale sebuleni, alipotokezea tu na macho yake kugongana na ya Hiza, nilimuona rafiki yangu huyo akishtuka kupita kawaida.
Nilishangaa! Sikujua kilichomshtua namna ile, baada ya sekunde kadhaa, akaanza kutoa tabasamu pana huku akiniangalia.

Kwa jinsi nilivyoliangalia tabasamu lile halikuwa kama la mtu mwenye furaha, nikagundua kulikuwa na kitu nyuma ya pazia ila aliamua kulificha kwa tabasamu lile.

Sikujua kama Scaila alilitambua hilo, yeye alitoa tabasamu pana kwa wageni, tena alionekana kuwa na furaha sana kuwaona watu wale mahali pale.

“Mbona umeshtuka sana?” nilimuuliza Hiza, sikutaka kuchelewa, nilihitaji kujua kilichokuwa kikiendelea kichwani mwake.
“We’ jamaa unajua kuchagua...” alisema Hiza huku akiendelea kutabasamu.

“Hahaha! Nilikwambia!”
“Huyu ndiye Scaila mwenyewe, ama nilipoita Scaila akashuka malaika na kuja sebuleni?” aliuliza Hiza maneno ambayo nilijipa uhakika kwamba nilikuwa nuksi kwenye kufanya maamuzi ya msichana niliyetaka kuwa naye.

“Ndiye yeye!”
“Kuanzia leo nakuvisha nyota zote! Nyemo wewe nuksi sana. Kashemeji kazuri, halafu kapole, kana tabasamu pana, jamani Nyemo ukikaudhi haka kashemeji siku moja, tutakuja kukufunga kwenye kiroba tukakutupe baharinini,” alisema Hiza huku akituangalia mimi na Scaila kwa zamu.

“Hahaha!” nilicheka.
Scaila akaanza kuwasalimia kwa kuwashika mikono. Kwa heshima zote, mtoto akaanza akainama kama mtu aliyekuwa akitaka kupiga goti.

“Jamani na siku nikija kwako na kukuta huu mkono umekuwa mgumu, Nyemo tutagombana,” alisema Ally, naye aliingizia utani huku akiwa ameushika mkono wa Scaila, wote tukaanza kucheka.
 
SEHEMU YA 29

Nilifurahi sana! Scaila akaelekea jikoni kuendelea na kazi lakini kitu cha ajabu kila nilipokuwa nikimwangalia Hiza, hakuonekana kuwa sawa japokuwa alikuwa akionyesha tabasamu na hata kucheka kila wakati.

Hilo lilinipa mawazo lukuki, sikujua kilichokuwa kikiendelea zaidi, inawezekana kulikuwa na jambo lililokuwa likimtatiza lakini hakutaka kuliweka wazi.
“Mzee baba niaje? Mbona umebadilika?” nilimuuliza.

“Mzee baba huyu demu mkali! Mpaka natamani angekuwa demu wangu!” alisema Hiza na wote kuanza kucheka.
Chakula kiliandaliwa na kuletwa mezani, tukaanza kula huku muda mwingi tukiendelea kuwa na furaha kupita kawaida.

Tulikula kwa dakika arobaini na tano na tulipomaliza, wageni wakaaga, nikaamua kuwasindikiza kwa gari.
“Mmemuonaje kwanza?” niliuliza kwa mbwembwe, nilitaka nianze kusifiwa, nilijisikia raha sana.

“Una mchumba mzuri sana,” alisema Ally.
“Najua kuchagua! Ila niliwaambia tangu chuo, mke wangu atakuwa mkali si mchezo,” niliwaambia
“Sasa cha msingi, kama utaingia ndani ya ndoa, vumilia kwa kila kitu,” alisema Hiza.
“Kivipi?”

“Utakuwa na mke mzuri, sasa kila mwanaume macho yatakuwa juu-juu. Ila nataka uwe na uhakika kama moyo wako unakwambia yule ni mke wako wa ndoa,” alisema Hiza.

“Moyo unaniambia hivyohivyo!”
“Una uhakika?”

“Jamani! Mpaka mikakati ya ndoa nimeanza kwa chini! Hilo wala usijali! Yaani nina uhakika!” nilimjibu.
“Basi inshallah!” alisema Hiza.
“Halafu kingine!” alisema Ally.

“Kipi?”
“Kwenye uhusiano inabidi mvumiliane sana! Sio unakuja kusikia alikuwa na jamaa fulani mzee baba ukapaniki! Haiko hivyo, ni lazima ujue mmepanga kuishi pamoja, hivyo ziba masikio.

Kwenye mapungufu, mvumiliane, hakuna mtu aliyekamilika,” alisema Ally.
“Hilo halina shida pia.”
“Na kingine!” alisema Hiza.

“Kipi?”
“Utakapogundua mabaya yake, usimwambie, fanyia upelelezi wa kina, yaani usikurupuke,” alisema Hiza.
“Mh! Nitaweza kweli?”
“Kwa nini ushindwe? Utaweza tu.”
“Basi sawa.”


|
|
Tukutane Jumatatu.
 
SEHEMU YA 29

Nilifurahi sana! Scaila akaelekea jikoni kuendelea na kazi lakini kitu cha ajabu kila nilipokuwa nikimwangalia Hiza, hakuonekana kuwa sawa japokuwa alikuwa akionyesha tabasamu na hata kucheka kila wakati.

Hilo lilinipa mawazo lukuki, sikujua kilichokuwa kikiendelea zaidi, inawezekana kulikuwa na jambo lililokuwa likimtatiza lakini hakutaka kuliweka wazi.
“Mzee baba niaje? Mbona umebadilika?” nilimuuliza.

“Mzee baba huyu demu mkali! Mpaka natamani angekuwa demu wangu!” alisema Hiza na wote kuanza kucheka.
Chakula kiliandaliwa na kuletwa mezani, tukaanza kula huku muda mwingi tukiendelea kuwa na furaha kupita kawaida.

Tulikula kwa dakika arobaini na tano na tulipomaliza, wageni wakaaga, nikaamua kuwasindikiza kwa gari.
“Mmemuonaje kwanza?” niliuliza kwa mbwembwe, nilitaka nianze kusifiwa, nilijisikia raha sana.

“Una mchumba mzuri sana,” alisema Ally.
“Najua kuchagua! Ila niliwaambia tangu chuo, mke wangu atakuwa mkali si mchezo,” niliwaambia
“Sasa cha msingi, kama utaingia ndani ya ndoa, vumilia kwa kila kitu,” alisema Hiza.
“Kivipi?”

“Utakuwa na mke mzuri, sasa kila mwanaume macho yatakuwa juu-juu. Ila nataka uwe na uhakika kama moyo wako unakwambia yule ni mke wako wa ndoa,” alisema Hiza.

“Moyo unaniambia hivyohivyo!”
“Una uhakika?”

“Jamani! Mpaka mikakati ya ndoa nimeanza kwa chini! Hilo wala usijali! Yaani nina uhakika!” nilimjibu.
“Basi inshallah!” alisema Hiza.
“Halafu kingine!” alisema Ally.

“Kipi?”
“Kwenye uhusiano inabidi mvumiliane sana! Sio unakuja kusikia alikuwa na jamaa fulani mzee baba ukapaniki! Haiko hivyo, ni lazima ujue mmepanga kuishi pamoja, hivyo ziba masikio.

Kwenye mapungufu, mvumiliane, hakuna mtu aliyekamilika,” alisema Ally.
“Hilo halina shida pia.”
“Na kingine!” alisema Hiza.

“Kipi?”
“Utakapogundua mabaya yake, usimwambie, fanyia upelelezi wa kina, yaani usikurupuke,” alisema Hiza.
“Mh! Nitaweza kweli?”
“Kwa nini ushindwe? Utaweza tu.”
“Basi sawa.”


|
|
Tukutane Jumatatu.
Santeeeeehhh
 

Similar Discussions

14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom