Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 152,886
- 453,430
Mtunzi Nyemo Chilongani
Sehemu ya 01.
Nilikuwa chumbani kwangu, kichwa changu kilikuwa na mawazo tele. Akili yangu ilichanganyikiwa, kulikuwa na mambo mengi ambayo yalinichanganya kipindi hicho, ila kubwa zaidi ni kuhusu msichana niliyekuwa nikimpenda kwa moyo wangu wote, Shasta Karina.
Naweza kusema kwamba miongoni mwa wasichana ambao nilikuwa nao katika maisha yangu, huyu nilimpenda mno. Alikuwa msichana mrembo ambaye ninaweza kusema alistahili kuwa mke wangu wa ndoa, nimuoe na hatimaye tujenge familia pamoja.
Nilikutana na Shasta miaka miwili iliyopita maeneo ya Victoria, Mikocheni kaika Mgahawa wa KFC. Siku hiyo nilikuwa nikitoka kumtembelea rafiki yangu aliyekuwa akiishi Msasani.
Nakumbuka nilipofika maeneo hayo, nilipaki gari langu na kwenda kwenye mgahawa huo uliokuwa mahali hapo, nikaingia na kukaa kwenye meza moja.
Nilikuwa kimya mno, sikutaka kuwa na presha yoyote ile, humo ndani macho yangu yalikuwa yakiangalia huku na kule kama nilikuwa namtafuta mtu fulani hivi, macho yangu yakatua kwa mhudumu mmoja, aliyevalia nguo zake safi, harakaharaka akaja pale nilipokuwa.
“Karibu!” aliniambia kwa sauti nyembamba, na kwa jinsi alivyokuwa mzuri, nilihisi kama nikipata hali fulani moyoni.
“Ahsante sana!” niliitikia na kumkazia macho, sikutaka kuyatoa kutoka usoni mwake.
Nilibaki nikimwangalia kwa sekunde kadhaa, alikuwa akiangalia pembeni huku akionekana kusikia aibu kupita kawaida. “Karibu!” alinikaribisha tena, akasindikiza na tabasamu fulani pana.
“Nashukuru sana! Ninahitaji chakula kizuri kama ulivyo,” nilimwambia kiutani huku macho yangu yakiendelea kubaki usoni mwake.
“Oh!”
“Ndiyo! Chipsi combo!” nilimwambia.
Msichana huyo akaondoka, nilibaki nikimwangalia, alionekana kuwa miongoni mwa wasichana warembo mno ambao niliwahi kukutana nao katika maisha yangu.
Kipindi hicho nilikuwa singo, niliachana na msichana aliyeitwa kwa jina la Evelyne kwa sababu tu hakuwa na sifa za kuwa mwanamke wa kuishi naye.
Ninapomfuata msichana kuna vitu vingi ninaviangalia, cha kwanza ni uwezo wa akili yake, je, nikiwa naye anaweza kulea watoto wangu kwa staili ninayoitaka?
Sehemu ya 01.
Nilikuwa chumbani kwangu, kichwa changu kilikuwa na mawazo tele. Akili yangu ilichanganyikiwa, kulikuwa na mambo mengi ambayo yalinichanganya kipindi hicho, ila kubwa zaidi ni kuhusu msichana niliyekuwa nikimpenda kwa moyo wangu wote, Shasta Karina.
Naweza kusema kwamba miongoni mwa wasichana ambao nilikuwa nao katika maisha yangu, huyu nilimpenda mno. Alikuwa msichana mrembo ambaye ninaweza kusema alistahili kuwa mke wangu wa ndoa, nimuoe na hatimaye tujenge familia pamoja.
Nilikutana na Shasta miaka miwili iliyopita maeneo ya Victoria, Mikocheni kaika Mgahawa wa KFC. Siku hiyo nilikuwa nikitoka kumtembelea rafiki yangu aliyekuwa akiishi Msasani.
Nakumbuka nilipofika maeneo hayo, nilipaki gari langu na kwenda kwenye mgahawa huo uliokuwa mahali hapo, nikaingia na kukaa kwenye meza moja.
Nilikuwa kimya mno, sikutaka kuwa na presha yoyote ile, humo ndani macho yangu yalikuwa yakiangalia huku na kule kama nilikuwa namtafuta mtu fulani hivi, macho yangu yakatua kwa mhudumu mmoja, aliyevalia nguo zake safi, harakaharaka akaja pale nilipokuwa.
“Karibu!” aliniambia kwa sauti nyembamba, na kwa jinsi alivyokuwa mzuri, nilihisi kama nikipata hali fulani moyoni.
“Ahsante sana!” niliitikia na kumkazia macho, sikutaka kuyatoa kutoka usoni mwake.
Nilibaki nikimwangalia kwa sekunde kadhaa, alikuwa akiangalia pembeni huku akionekana kusikia aibu kupita kawaida. “Karibu!” alinikaribisha tena, akasindikiza na tabasamu fulani pana.
“Nashukuru sana! Ninahitaji chakula kizuri kama ulivyo,” nilimwambia kiutani huku macho yangu yakiendelea kubaki usoni mwake.
“Oh!”
“Ndiyo! Chipsi combo!” nilimwambia.
Msichana huyo akaondoka, nilibaki nikimwangalia, alionekana kuwa miongoni mwa wasichana warembo mno ambao niliwahi kukutana nao katika maisha yangu.
Kipindi hicho nilikuwa singo, niliachana na msichana aliyeitwa kwa jina la Evelyne kwa sababu tu hakuwa na sifa za kuwa mwanamke wa kuishi naye.
Ninapomfuata msichana kuna vitu vingi ninaviangalia, cha kwanza ni uwezo wa akili yake, je, nikiwa naye anaweza kulea watoto wangu kwa staili ninayoitaka?