Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 152,975
- 453,778
- Thread starter
- #61
Sehemu ya 21
Hapo ndipo akapata jibu sababu iliyomfanya Sharifu kuchelewa kuufungua mlango alipokuwa akipiga hodi.
Akahisi moyo wake ukiwaka kwa hasira, hakuweza kuvumilia pale ukutani alipojificha, kwa kasi ya ajabu akachomoka, akawafuata kule walipokuwa, hawakuwa wamemuona, ile ghafla, msichana Nusrat akashtukia akikabwa roba kali na kuanza kushambuliwa kwa ngumi mpaka kuanguka chini.
“Sabrinaaa....” alijikuta akiita Sharifu, hata kumtoa Sabrina alishindwa kwani alikuwa na nguvu mno, alimkalia Nusrat juu huku akimpiga mfululizo.
*****
Mapenzi yakawa motomoto, kila walipokuwa, walikuwa pamoja, hakukuwa na kitu ambacho kingeweza kuwatenganisha kutoka katika penzi zito walilokuwa nalo zaidi ya kifo tu.
Kila mmoja alichanganyikiwa, kwa Aisha, hakuamini kama kweli maisha yote aliyoishi kipindi cha nyuma yalibaki na kuwa historia, yaani asingeweza kurudi tena mitaani, kuombaomba na kutafuta mabaki ya chakula katika hoteli mbalimbali zilizokuwa Kariakoo.
Maisha yake yalikuwa mapya kabisa, alitakiwa kusahau kila kitu, alitakiwa kujua kwamba kwa kipindi hicho yeye alikuwa mpenzi wa mtoto wa bilionea, hivyo shida zote alizokuwa nazo kipindi cha nyuma alitakiwa kuzisahau.
Aisha hakutaka kuwaacha mapacha ambao ndiyo walionekana kuwa sababu ya yeye kukutana na Razak, alihakikisha nao wanapata maisha bora kama aliyokuwa akipata, hilo, kwa Razak wala halikuwa tatizo, kwa sababu umri wao haukuwa mkubwa sana, akawahamisha katika nyumba hiyo na kuwapeleka katika nyumba nyingine nzuri iliyokuwa Sinza, walitakiwa kuishi huko, wakawekewa mfanyakazi na kupewa kila kitu walichokihitaji.
Yote hayo aliyafanya kwa kuwa alitaka kumuona mpenzi wake akiwa na furaha tele, hakutaka ayakumbuke maisha aliyopitia kipindi cha nyuma, kila kitu kilichopita, alitaka kiwe historia ambayo isingeweza kujirudia tena maishani mwake.
“Unapenda nikufanyie nini katika maisha yako?” aliuliza Razak huku akiwa amemlaza Aisha miguuni mwake.
“Ninataka unioe...” alijibu Aisha huku akiachia tabasamu pana.
“Hilo tu?”
“Yapo mengi, ila hilo ndilo la kwanza!”
“Usijali mpenzi, nitahakikisha nakuoa haraka iwezekanavyo...” alisema Razak huku akiachia tabasamu pana.
Razak alikuwa na fedha, hilo kwake halikuwa tatizo hata kidogo, mara kwa mara walikuwa wakitoka na kuelekea sehemu mbalimbali kula maisha, walikwenda Zanzibar, katika Visiwa vya Komoro na Shelisheli, kote huko alitaka kumuonyesha Aisha jinsi maisha ya kuwa na fedha yalivyokuwa.
Kwa jinsi walivyopendana, kusikilizana na kujaliana, hakukuwa na aliyefikiri kwamba wakati mwingine kwenye mapenzi kuna kugombana na kufarakana, kwao, mapenzi yalikuwa motomoto.
Razak hakutaka kumkumbuka Sabrina, alitaka kumfuta kabisa kwenye akili yake.
Moyoni mwake alihisi kwamba kuna kitu kingeweza kutokea, hivyo alichokifanya ni kujihami mapema kabisa.
Akamwambia Aisha kuhusu msichana huyo, jinsi alivyokuwa naye na mapenzi kuja kuyumba na hatimae kuachana kabisa.
Kwa Aisha, hilo halikuwa tatizo, alifurahi kupewa taarifa na hivyo akajiandaa kwa lolote ambalo lingeweza kutokea.
Je nini kitaendelea....
Hapo ndipo akapata jibu sababu iliyomfanya Sharifu kuchelewa kuufungua mlango alipokuwa akipiga hodi.
Akahisi moyo wake ukiwaka kwa hasira, hakuweza kuvumilia pale ukutani alipojificha, kwa kasi ya ajabu akachomoka, akawafuata kule walipokuwa, hawakuwa wamemuona, ile ghafla, msichana Nusrat akashtukia akikabwa roba kali na kuanza kushambuliwa kwa ngumi mpaka kuanguka chini.
“Sabrinaaa....” alijikuta akiita Sharifu, hata kumtoa Sabrina alishindwa kwani alikuwa na nguvu mno, alimkalia Nusrat juu huku akimpiga mfululizo.
*****
Mapenzi yakawa motomoto, kila walipokuwa, walikuwa pamoja, hakukuwa na kitu ambacho kingeweza kuwatenganisha kutoka katika penzi zito walilokuwa nalo zaidi ya kifo tu.
Kila mmoja alichanganyikiwa, kwa Aisha, hakuamini kama kweli maisha yote aliyoishi kipindi cha nyuma yalibaki na kuwa historia, yaani asingeweza kurudi tena mitaani, kuombaomba na kutafuta mabaki ya chakula katika hoteli mbalimbali zilizokuwa Kariakoo.
Maisha yake yalikuwa mapya kabisa, alitakiwa kusahau kila kitu, alitakiwa kujua kwamba kwa kipindi hicho yeye alikuwa mpenzi wa mtoto wa bilionea, hivyo shida zote alizokuwa nazo kipindi cha nyuma alitakiwa kuzisahau.
Aisha hakutaka kuwaacha mapacha ambao ndiyo walionekana kuwa sababu ya yeye kukutana na Razak, alihakikisha nao wanapata maisha bora kama aliyokuwa akipata, hilo, kwa Razak wala halikuwa tatizo, kwa sababu umri wao haukuwa mkubwa sana, akawahamisha katika nyumba hiyo na kuwapeleka katika nyumba nyingine nzuri iliyokuwa Sinza, walitakiwa kuishi huko, wakawekewa mfanyakazi na kupewa kila kitu walichokihitaji.
Yote hayo aliyafanya kwa kuwa alitaka kumuona mpenzi wake akiwa na furaha tele, hakutaka ayakumbuke maisha aliyopitia kipindi cha nyuma, kila kitu kilichopita, alitaka kiwe historia ambayo isingeweza kujirudia tena maishani mwake.
“Unapenda nikufanyie nini katika maisha yako?” aliuliza Razak huku akiwa amemlaza Aisha miguuni mwake.
“Ninataka unioe...” alijibu Aisha huku akiachia tabasamu pana.
“Hilo tu?”
“Yapo mengi, ila hilo ndilo la kwanza!”
“Usijali mpenzi, nitahakikisha nakuoa haraka iwezekanavyo...” alisema Razak huku akiachia tabasamu pana.
Razak alikuwa na fedha, hilo kwake halikuwa tatizo hata kidogo, mara kwa mara walikuwa wakitoka na kuelekea sehemu mbalimbali kula maisha, walikwenda Zanzibar, katika Visiwa vya Komoro na Shelisheli, kote huko alitaka kumuonyesha Aisha jinsi maisha ya kuwa na fedha yalivyokuwa.
Kwa jinsi walivyopendana, kusikilizana na kujaliana, hakukuwa na aliyefikiri kwamba wakati mwingine kwenye mapenzi kuna kugombana na kufarakana, kwao, mapenzi yalikuwa motomoto.
Razak hakutaka kumkumbuka Sabrina, alitaka kumfuta kabisa kwenye akili yake.
Moyoni mwake alihisi kwamba kuna kitu kingeweza kutokea, hivyo alichokifanya ni kujihami mapema kabisa.
Akamwambia Aisha kuhusu msichana huyo, jinsi alivyokuwa naye na mapenzi kuja kuyumba na hatimae kuachana kabisa.
Kwa Aisha, hilo halikuwa tatizo, alifurahi kupewa taarifa na hivyo akajiandaa kwa lolote ambalo lingeweza kutokea.
Je nini kitaendelea....