Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 152,998
- 453,945
Mtunzi Nyemo Chilongani
Sehemu ya 01
“Shadya! Wewe ni msichana mzuri sana, mrembo, msichana ambaye ninajisikia fahari sana kuwa nae,” ilisikika sauti ya mwanaume mmoja aliyekuwa amejibanza kwenye ukuta wa chuo cha madrasa ya Al Munira Siraja kilichokuwa katika Mtaa wa Michenzani huko Zanzibar.
Shadya alikuwa kimya, macho yake aliyatuliza usoni mwa kijana aliyesimama mbele yake. Alivalia kanzu ndefu nyeupe, kichwani alikuwa na kofia aina ya baghalashia na mkononi mwake alishika tasbih, chini alikuwa peku.
Hapo waliposimama ilikuwa ni rahisi kusikia sauti za wanafunzi waliokuwa wakijifunza koran ndani ya madrasa hiyo.
Kijana aliyekuwa akizungumza aliitwa kwa jina la Ngwali Shangali, alikuwa mwalimu wa madrasa hiyo ambaye alipewa jukumu la kuwafundisha watoto wadogo waliotakiwa kuishi katika misingi ya kumtumikia Mungu.
Shadya alikuwa kimya, alimwangalia kijana huyo, maneno aliyokuwa akiyazungumza yalimgusa kupita kawaida. Alimpenda, alimthamini, katika maisha yake hapakuwa na mwanaume aliyekuwa akimpenda kama huyo.
Kwa kumwangalia, Shadya alikuwa msichana mrembo mno, alivutia, alikuwa na asili ya Pemba, mweupe, macho ya goroli na kila alipokuwa akicheka ama kutabasamu ilikuwa ni rahisi sana kuviona vishimo vidogo mashavuni mwake.
Weupe wake ulimfanya kuvutia, sura ya kitoto ilimfanya kupendwa na kila mtu katika mtaa huo wa uswahili.
Wanaume wengi walimfuata tangu alipokuwa na miaka kumi na tatu, walihitaji nafasi ndani ya moyo wake, alikuwa mdogo lakini urefu wake ulimfanya kila mmoja kuhisi alikua, alifaa kulalishwa kitandani na kuvuliwa nguo.
Wengi walimmendea, walimtolea macho huku wakitamani hata kuiona miguu yake, ilifananaje, ule weupe uliokuwa ukionekana usoni ulikwenda mpaka miguuni na mapajani, tumboni ama la.
Japokuwa hapo Unguja lilikuwa jambo gumu kwa mwanaume kumsimamisha mwanamke waziwazi na kuongea naye stori za kimapenzi lakini kwa Shadya walishindwa kuvumilia kabisa, hivyo wakajikuta wakianza kufanya hivyo.
Mpaka anafikisha umri wa miaka ishirini na moja Shadya alimvulia nguo mwanaume mmoja tu, naye alikuwa Ngwali ambaye alisimama mbele yake muda huo.
Sehemu ya 01
“Shadya! Wewe ni msichana mzuri sana, mrembo, msichana ambaye ninajisikia fahari sana kuwa nae,” ilisikika sauti ya mwanaume mmoja aliyekuwa amejibanza kwenye ukuta wa chuo cha madrasa ya Al Munira Siraja kilichokuwa katika Mtaa wa Michenzani huko Zanzibar.
Shadya alikuwa kimya, macho yake aliyatuliza usoni mwa kijana aliyesimama mbele yake. Alivalia kanzu ndefu nyeupe, kichwani alikuwa na kofia aina ya baghalashia na mkononi mwake alishika tasbih, chini alikuwa peku.
Hapo waliposimama ilikuwa ni rahisi kusikia sauti za wanafunzi waliokuwa wakijifunza koran ndani ya madrasa hiyo.
Kijana aliyekuwa akizungumza aliitwa kwa jina la Ngwali Shangali, alikuwa mwalimu wa madrasa hiyo ambaye alipewa jukumu la kuwafundisha watoto wadogo waliotakiwa kuishi katika misingi ya kumtumikia Mungu.
Shadya alikuwa kimya, alimwangalia kijana huyo, maneno aliyokuwa akiyazungumza yalimgusa kupita kawaida. Alimpenda, alimthamini, katika maisha yake hapakuwa na mwanaume aliyekuwa akimpenda kama huyo.
Kwa kumwangalia, Shadya alikuwa msichana mrembo mno, alivutia, alikuwa na asili ya Pemba, mweupe, macho ya goroli na kila alipokuwa akicheka ama kutabasamu ilikuwa ni rahisi sana kuviona vishimo vidogo mashavuni mwake.
Weupe wake ulimfanya kuvutia, sura ya kitoto ilimfanya kupendwa na kila mtu katika mtaa huo wa uswahili.
Wanaume wengi walimfuata tangu alipokuwa na miaka kumi na tatu, walihitaji nafasi ndani ya moyo wake, alikuwa mdogo lakini urefu wake ulimfanya kila mmoja kuhisi alikua, alifaa kulalishwa kitandani na kuvuliwa nguo.
Wengi walimmendea, walimtolea macho huku wakitamani hata kuiona miguu yake, ilifananaje, ule weupe uliokuwa ukionekana usoni ulikwenda mpaka miguuni na mapajani, tumboni ama la.
Japokuwa hapo Unguja lilikuwa jambo gumu kwa mwanaume kumsimamisha mwanamke waziwazi na kuongea naye stori za kimapenzi lakini kwa Shadya walishindwa kuvumilia kabisa, hivyo wakajikuta wakianza kufanya hivyo.
Mpaka anafikisha umri wa miaka ishirini na moja Shadya alimvulia nguo mwanaume mmoja tu, naye alikuwa Ngwali ambaye alisimama mbele yake muda huo.