permist
JF-Expert Member
- Feb 23, 2017
- 615
- 360
Str nzur
Sehemu ya 22
Tulizungumza mambo mengi tu, na kwa kuwa suala la ndoa lilikuwa likiratibiwa zaidi na upande wa kiumeni, mume wangu mtarajiwa aliniaga akisema anakwenda kuendelea na shughuli zilizo salia kabla ya ndoa.
Hata hivyo, kabla hajatoka ndani, aliniachia mabusu motomoto huku akinitekenya tekenya kwa hila. Alizibinya binya taratibu embe zangu wakati mwingine akawa anakipapasa kiuno changu.
Kama isingekuwa mkandamizo wa wa kifikra niliokuwa nao dhidi ya yule fedhuli mwenye picha zangu za utupu, basi asubuhi ile lazima tungeikaribisha kwa mambo yetu yale ya kiutu uzima.
Baada ya kuhakikisha Alex ameondoka kabisa nyumbani kwangu, nilirudi kwenye simu yangu na kumpigia yule bwana, simu ikiwa sikioni nikapokea ujumbe kwamba simu ile ilikuwa haipatikani.
“Kwa nini sasa umezima simu!” niliongea peke yangu kwa masikitiko.
Masikitiko yangu yalikuwa katika tafsiri moja tu. Nilitaka nimalizane na mtu yule kabla ya siku ya ndoa yangu, kitendo cha kutompata katika simu, maana yake ni kwamba, ningeendelea kuishi kwa mashaka na wasiwasi siku zote.
“Nifanye nini?” nilinong’ona mwenyewe.
Kwa kweli nilishikwa na hofu kubwa moyoni, nilirudia kumpigia tena simu yule bwana, ujumbe nilio upata ulikuwa uleule. Namba ilikuwa haipatikani.
Au nimwambie ukweli Alex juu ya mambo niliyowahi kufanya maishani! Sauti moja kichwani ilinishauri. Hata hivyo, wasiwasi wangu ukawa vipi kama nikimwambia halafu nikaishia kuachwa!
Siku hiyo kutwa nzima nilishinda kama mgonjwa. Si chakula wala maji, vyote vilikuwa vichungu kinywani mwangu.
Jioni ilipotimu, mpenzi wangu Alex akanipigia simu. “Unaendeleaje mpenzi?”
“Nimepona.”
“Kuna jambo nataka tuongee,” “Jambo gani?” “Kuna bwana kanipigia simu…” alisema. Mapigo ya moyo wangu yakaanza kunienda mbio, nikatishika vibaya sana. Nikawaza isije kuwa yule jamaa mshenzi, amekwisha weka wazi kila kitu. Akaendelea.
“Jina lake naitwa Kaheza,amesema kuna kitu anataka kunionyesha kuhusu wewe.”
“Kitu gani hiko?” hatimaye mtoto wa kike nikajikaza na kumuuliza bila kuonesha wasiwasi wowote simuni.
“Amenieleza ataniambia kesho asubuhi?”
“Kwa hiyo unasemaje Alex?”