Simulizi: Lisa

mireille

JF-Expert Member
Mar 4, 2020
523
568
JINA LA SIMULIZI.......................LISA
WHATSAPP.....................0628924768
SPONSORED BY.. SIMULIZI ZA DULLY
SURA YA .......................................1&2

SURA YA 1

“Paah!” Kofi kali lilitua usoni kwa Lisa Jones Masawe. Kofi hilo halikutoka kwa mwingine zaidi ya mama yake, aliyejulikana zaidi kama Mama Masawe.

“Umeniangusha sana. Dada yako amekuwa na wakati mgumu kwa zaidi ya miaka 20, sasa amerejea na anataka kuolewa. Bila aibu unapanga kumpokonya mwanaume wake. Huna aibu kabisa!” Mama Masawe alimuwakia mwanae Lisa.

Akiwa amejifunika sehemu ya uso wake iliyokuwa inauma, Lisa alimtazama mama yake bila kuamini. “Mama, Ethan ni mpenzi wangu tangu nikiwa shule. Kila mtu anajua hilo. Mnawezaje kuwa watu wasioelewa kiasi hiki?” Maneno yaliyokosa chembe ya heshima kwa mama yake yalimtoka Lisa kwa jazba.

Ndo kwanza Lisa alikuwa anafika nyumbani baada ya safari ya masomo nchini Marekani. Alimkuta dada yake mkubwa aliyepotea kwa muda mrefu, Lina Jones Masawe, akiwa amerudi. Wakati huo alikuwa ameketi na mpenzi wake Ethan kwenye kochi. Walioketi upande wa pili wa kochi walikuwa wazazi wa Ethan, Zackaria Lowe na Sonya Mushi ambao walionekana kuwa na mazungumzo ya kupendeza.

Kwa kweli, Ethan alikuwa mpenzi wa Lisa. Wamekuwa pamoja kama majirani lakini walipokuwa shule ya sekondari ambapo walisoma kidato kimoja, urafiki wamapenzi ukachanua kati yao na walikuwa wameahidiana kuoana. Baada ya kuhitimu chuo kikuu, Ethan alijiunga na baishara ya familia yao kama msimamizi wa kampuni ya Lowe Enterprises.

Lisa naye alifanya kazi muda mfupi tu kwenye kampuni yao ya familia, Kibo Building Desing Group kabla ya kwenda kuongeza elimu ya juu ya uinjinia katika ujenzi kwenye chuo kikuu cha New South Wales nchini Marekani. Kwa muda wa miaka miwili walikuwa wakiwasiliana kwa simu tu.

Sasa baada ya Lina kurudi, Lisa anashangaa imekuaje tena Ethan amgeuke na kumchukua dada yake? Hakuweza kujizuia kumwendea Lina ili kumuuliza. Hata hivyo aliishia kupigwa kofi kali la uso na mama yake hapo hapo!

"Mama, tafadhali acha kumpiga Lisa ." Kwa sura ya wasiwasi, Lina alisema. “Ni kosa langu. Sikupaswa kurudi.”

Ethan alimshika mabega haraka. “Hapana Lina, ni kosa langu. Siku zote nilikuwa namchukulia Lisa kama dada yangu mdogo na rafiki yangu. Huenda kuna kitu amechanganya kati ya mapenzi na urafiki.”

Kuna kitu kilionekana kulipuka kichwani mwa Lisa . Maumivu ndani ya moyo wake yalikuwa makali sana hivi kwamba alishindwa kupumua.

“Eti Dada? Yaani leo hii mimi nimekuwa dada yako?” Macho yalimtoka Lisa sawia na maneno yake. “Kwa nini uliniahidi utanioa ikiwa ulinichukulia kama dada yako?

Kwa nini kila mara ulinikumbatia kwa nguvu na kunibusu na kunaimbia maneno matamu matamu ikiwa tu ulinichukulia kama dada yako?”

“Lisa..” Lina alitaka kusema neno lakini akazimishwa na karipio kali la Lisa.

"Nyamaza!" Alijikuta maneno hayo hayavumiliki na yalikuwa yakimjaza karaha.

“Wewe ndio unapaswa kufunga mdomo wako. Hivi ndivyo unavyotakiwa kuongea na dada yako?” Mama Masawe aliimfokea Lisa. "Je, huwezi kumheshimu dada yako? Ukizingatia kwamba amepitia miaka ishirini ya maisha magumu akiwa nje ya familia hii?"

Kwa mshtuko, Lisa alilegea kidogo. Ilibidi kuwe na kikomo cha uvumilivu hata hivyo. Kwa nini aache mapenzi yake yapotee? Yeye pia ni binadamu, ana moyo unaouma.

Wakati huo, baba wa familia hiyo, Jones Masawe alisimama na kumwambia Lisa kwa ukali pia. “Umemaliza? Ethan ameshasema yeye si mchumba wako. Bado tunahitaji kujadili sherehe ya uchumba ya Lina sasa. Kama hutaweza kunyamaza bora uondoke. Usituletee zogo hapa."

Lisa alitetemeka na kumtazama Ethan ambaye hamkujali kabisa. Kisha akamtazama Lina ambaye alikuwa amemng'ang'ania. Ghafla, alihisi kama moyo wake unaganda kwa hasira. Watu hawa ndio alikuwa anawajali sana, lakini kila mmoja wao alikuwa akiegemea upande wa Lina kwa wakati huo.

Machozi yalionekana kumtoka. Baada ya kufuta machozi, Lisa aligeuka na kuondoka na mkoba wake bila kuangalia nyuma. Bila kujua pa kwenda, alisimama na kumpigia simu rafiki yake wa karibu, Pamela Masanja.

"Pamela, ni mimi Lisa, nimerudi. Njoo tunywe pombe, leo nataka tulewe mpaka tukeshe." Sauti yake ilisikika kuwa ya kishindo katikati ya kwikwi zake.

Pamela alikubali mara moja. “Hakika. Nitakuwepo baada ya muda mfupi.

SURA YA 2

Pamela alipofika kwenye baa maarufu ya Mambo Garden, Lisa alikuwa tayari amemaliza chupa nzima ya mvinyo mwekundu peke yake!

“Umekuja kwa wakati muafaka shosti. Nitakuagizia chochote unachotaka. Huruhusiwi kuondoka hadi umalize vinywaji.” Lisa alimiminia Pamela glasi ya mvinyo.

"Nini tatizo?" Pamela alimuuliza kwa wasiwasi. Ilikuwa ni nadra sana kwa Pamela kumkuta Lisa akiwa anakunywa pombe kiasi hicho. Aliingiwa na wasiwasi sana kuhusu Lisa. Isitoshe hakujua kama alikuwa na furaha ama matatizo kwani ni miaka miwili walikuwa hawajaonana kwenda masomoni Marekani, japo walikuwa wakiwasiliana kwa simu na mitandao ya kijamii. Sasa baada ya kurejea tena nyumbani ni kitu gani kilikuwa kimemkuta?

“Ethan yuko wapi, kakufanyia nini?” Pamela alihisi huenda ni mpenzi wake, Ethan ndiye aliyemzingua, bila kujua kwamba alikuwa anatchoma msumari wa moto kwenye jeraha bichi la Lisa.

Alipotaja tu jina la Ethan, Lisa alihisi kana kwamba kuna kisu kikali kinakwaruza moyo wake. "Ameniacha, na sasa yupo na Lina na wanapanga sherehe za uchumba."

Pamela alicheka kwa hudhuni. Hakuamini kabisa alichosikia. "Hii ni kweli au naota?"

Lisa alimweleza kwa ufupi kilichotokea jioni hiyo wakati anafika nyumbani kwao. Pamela alihisi hali ya kutokuamini. Ethan na Lisa walikuwa marafiki wa karibu tangu utotoni na walikuwa wameanzisha uhusiano wa kimapenzi tangu shule ya sekondari. Hata hivyo, katika miaka miwili hivi, Lisa alikuwa anasoma nje ya nchi huku Ethan akiwa na shughuli nyingi za kazi.

Hiyo ndiyo sababu iliyowachelewesha kuchumbiana rasmi. Lakini, wazazi wao wote wa pande zote mbili waliufahamu fika uhusiano wao. Pia walitoa baraka zao kwa wanandoa hao watarajiwa. Kila mtu katika mzunguko wao wa ndugu jamaa na marafiki alijua kwamba Ethan na Lisa wangefunga ndoa mapema au baadaye.

Sasa, ikawaje kwamba Ethan alikuwa amemtosa Lisa na kuangukia kwa Lina? Hilo lilimchanganya Pamela na kumfanya Lisa aonekane kama kituko cha mwaka.

“Baba yako na mama yako wamerukwa na akili?” Pamela alishindwa kuelewa. “Huu ni upuuzi. Wewe na Lina wote mna umuhimu kwa wazazi wenu.”

Lisa alishika glasi ya mvinyo na kuongea kabla hajaigida mdomoni mwake. "Labda wanahisi kwamba Lina ameteseka sana huko alikokuwa. Kwa kuwa sasa amerudi, wanataka tu kumpa kilicho bora zaidi.”

Pamela bado alikuwa katika hali ya kutoamini. "Lakini wewe ni binti yao pia!"

Lisa alilazimisha tabasamu. “Hah. Sasa Lina amerudi, wanachojali ni Lina tu. Lisa lipigida funda jingine la mvinyo na kuendelea kuongea, “tangu mwanzo wao ndio walitaka kunioza kwa Ethan. Sasa kwa kuwa ninalichukulia suala hilo kwa uzito, wananiita sijakomaa. Pia, Ethan aliahidi kuwa nami milele, lakini amebadili mawazo yake hivyohivyo. Ninamchukia…” Maneno ya Lisa yalikuwa na ladha ya uchungu.

Mwishoni mwa sentensi yake, Lisa alianza kulia. Akiwa ameshika glasi alichukua mikupuo kadhaa ya mvinyo na kuruhusu machozi ya uchungu kumwagika machoni mwake. Wakati huo, alianza kuhisi kizunguzungu kidogo.

“Usinywe pombe kupita kiasi. Una kichwa chepesi sana. Utajisikia vibaya ikiwa utakunywa kupita kiasi.” Pamela alimpa angalizo. Alinyakua glasi ya mvinyo ya Lisa ili kugeuza mawazo yake kutoka kwayo. Baada ya hapo, alitazama macho yake kuzunguka baa. Kamwe hakutarajia kuona mtu aliyemjua. “Haya, tazama hapo!”

Pamela alimsukuma Lisa na kumuonyesha mtu aliyekuwa amekaa pembeni. Licha ya mwanga hafifu kwenye kona hiyo, mtu huyo alionekana vizuri. Alivaa suti ambayo haikufaa kwa mazingira hayo. Alivaa suti maridadi ya kibiashara. Mwanamume huyo alikuwa amefumba macho yake na alikuwa ameegemea kochi, akitoa nuru ya uzuri wakati mwangaza wa taa iliyozunguka ulipomwangazia mara kwa mara.

Alionekana kuvutia sana hivi kwamba uso wake ulikuwa mzuri kama masanamu yale yanayovalishwa nguo kwenye maduka ili kuzitangaza kwa wateja. Baada ya kumtazama, Lisa alikwepesha macho yake kutoka kwake. "Hata awe ni mzuri kiasi gani, siko katika hali ya kufurahia kitu chochote kinachopendeza macho sasa hivi."

"Najaribu kukuambia kuwa mtu huyo ni mjomba wa Ethan." Pamela alimwambia.

Lisa alipigwa na butwaa kwa muda. "Una uhakika?" Ethan hapo awali aliwahi kumwambia Lisa kuwa alikuwa na mjomba wake tajiri sana. Hata hivyo, mjomba wake huyo alikuwa anafanya baishara zake nje ya nchi, kwa hiyo Lisa hakuwahi kumwona.

“Ndio, nina uhakika kuwa ni yeye. Kaka yangu alinionyesha tulipohudhuria hafla ya chakula siku moja. Nikasikia ni kijana mdogo tu na ana pesa sana. Hata baba yake Ethan hamfikii kwa utajiri alionao. Siku chache zilizopita, nilisikia kwamba alikuwa amerudi Bongo.

Macho ya Lisa yakaangaza. Mara moja akapata wazo lililomjia kichwani. “Naam! Unafikiri nini kitatokea nikiolewa na mjomba wa Ethan?”

“Pff…” Kwa mshtuko, Pamela akapaliwa mvinyo mdomoni mwake. “Sema hivyo tena?”

Lisa alimtazama kwa makini tena kijana yule aliyevuti kisha akafafanua hoja yake kwa Pamela. “Kwa kuwa siwezi kuwa binti-mkwe wa familia ya Lowe, nitakuwa shangaziya Ethan tu kwa kuolewa ha mjomba wake ili nipate nafasi ya kuwakomesha Ethan na Lina wake!”

Pamela alipigwa na butwaa kwa muda, kisha baada ya kufikiria kwa undani hoja ya Lisa, aliona imekaa poa! Akamwonyesha Lisa dole gumba mara moja. “Yeye ni mzuri, mzuri sana kwa kweli. Niko upande wako! Muonekano wa mjomba wake Ethan ni mkamilifu. Hata Ethan si mzuri ukimlinganisha naye. Utajiri na uwezo wake pia unazidi ule wa familia ya Lowe. Utakuwa umejiheshimisha sana ukiolewa na huyu kijana” Pamela alizidi kuchombeza. “Lakini je, utawezaje?”

Lisa alizidi kuchangamshwa na maneno ya uchochezi ya Pamela, akili yake ikapagawa namna ya kumpata huyo mtu.

"Ninahitaji kukukumbusha kwamba unapaswa kupata mume bora, msomi, mwenye pesa, au nafasi yako katika kampuni ya ‘Kibo Group’ itakuwa duni kuliko ya Lina. Kwa hiyo nadhani huyu mjomba wa Ethan anakufaa!” Pamela alitia maneno yake.

Lisa aliduwaa kwa sekunde. Alichokisema Pamela kilionekana kumwingia akilini. Ikiwa Lina angeolewa na Ethan na kuungwa mkono na familia ya Lowe basi nafasi ya Lisa ya kuwa mrithi wa kampuni ya familia yao Kibo Group ingekuwa hatarini. Kwa hiyo ujanja hapo ulikuwa ni kumpindua ili yeye aolewe na mtu maarufu zaidi kuliko Ethan ili heshima irudi kwake.

“Sawa, nitauteka moyo wake sasa hivi kama jambazi vile!” Lisa alijipa moyo wakati akimpokonya Pamela mkoba kisha akatoa lipstick na foundation. Alijipodoa kidogo na uso wake ulionekana kung'aa.

Pamela akaangaza macho. "Uh, una uhakika unaweza kukabiliana naye sasa hivi?"

“Unanionaje kwanza, mimi ni binti mrembo na yeye ni mwanaume tu, sivyo? Haha!” Lisa alijigamba kisha akafagia nywele zake kwenye bega moja na kumimina nusu ya mvinyo kwenye glasi. Akiwa na sura ya kuvutia na ya kupendeza, alitembea kuelekea kwa kijana huyo kwa maringo na madaha.

Kadiri alivyozidi kumkaribia mwanaume huyo, ndivyo uso wake wa kupendeza ulivyozidi kuwa wazi. Macho yake safi yakionekana kuwa na huzuni kidogo na muundo mzuri wa sura yake vyote vilionekana kuvutia.

“Hi! Samahani kwa kukusumbua, lakini unaweza kuniambia muda sasa?" Lisa aligonga kidole chake begani kwa yule mtu mara mbili.

Mwanaume huyo alipofumbua macho yake yaliyolewa chini ya mwanga hafifu, neno ‘malaya’ lilimjia kichwani. Alimwona Lisa kama malaya tu anayejiuza.

Ubongo wa Lisa uliganda kwa sekunde chache. Baada ya kupata fahamu zake, alitabasamu na kusema, “Nafikiri kukutana kwetu kwa mara ya kwanza hapa ni mwanzo wa furaha yetu.”

Akiwa na uso uliobeba dalili za kukereka, yule mwanamume alisema kwa upole, “Mimi si daktari, sitoi matibabu kwa vichaa.”

"Nini?" Lisa aliuliza.

“Wewe ni kichaa, sivyo?” Midomo ya kupendeza ya mwanaume huyo ilivutia sana, lakini, maneno yaliyotoka kinywani mwake yalikuwa machafu sana.

“Mh!” Lisa akaguna. Wakati huo, Lisa alibidi atoe kioo ili ajiangalie tena kwa makini kama kweli sura yake haikutosha kumvutia yule jamaa. Lisa hakuona kasoro yoyote kwenye sura yake. Hata hivyo, hakukata tamaa. Haikuwezekana kufahamu mawazo ya wanaume vinginevyo Ethan asingemsaliti.

“Kweli mimi ni mgonjwa wa kichaa na kichaa changu ni cha mapenzi.” Lisa alitulia haraka na kutoa tabasamu la aibu. "Na kichaa changu cha mapenzi kilinipanda nilipokuona wewe kwa mara ya kwanza hapa."

Kijana yule mtanashati alipoinua uso wake, mara Lisa alichukua fursa hiyo kusema, "Wanasema mtu hawezi kujizuia kujisikia furaha anapokutana na mwanamume anayeweza kumfanya aonekane kama kichaa. Huyo ndiye mpenzi wa maisha yake, na hivi ndivyo ninavyohisi kwa sasa."

“Sawa, nimezisikia tenzi zako tamu za mapenzi, nimeburudika. Unaweza kuondoka sasa?” Mwanaume huyo alikwepesha macho yake mbali naye kwa namna ya kukatisha tamaa. Yale yote aliyoyasema Lisa yalionekana ni usumbufu tu kwake.

Lisa aliumia sana. Alikuwa mrembo wa kuvutia kwenye macho ya wanaume wengi. Kila siku alikabiliana na usumbufu mwingi wa wanaume waliokuwa wakimtaka kwa gharama yoyote ile. Kwenye mitandao ya kijamii wanaume walipagawa kila alipochapisha picha zake.

Lakini kwa wakati huo ilikuwa tofauti. Kijana yule alikuwa anajisikia kwelikweli. Lisa alitamani kugeuka na kuondoka, lakini alipoifikiria nafasi ya kuwa shangazi wa Ethan, hata hivyo, akapata ujasiri wa kuendelea kumshawishi tena.

"Mpenzi mzuri, unaweza kunitajia namba yako ya WhatsApp?" Kimya!

“Kijana mzuri, unaweza kunipa namba yako?” Kimya!

“Handsome boy, unaweza kuniambia jina lako?” Kimya!

"Baby boy, unaonekana kupendeza na kuvutia sana kiasi kwamba mwanamke lazima apagawe anapokuangalia tu..."
Hapo walau akaambulia mguno tu wa yule jamaa. Kwa kukerwa na sauti ya Lisa aliyeonekana kukosa haya kabisa, mwanamume yule alifumbua macho yake na kuuliza kwa sauti ya kuudhika, “Unataka nini?”

“Nataka unioe, nataka niwe mke wako!” Lisa alifunguka moja kwa moja.

Mdomo wa mwanamume yule ukatetemeka kwa mshangao! Kwa muda akasalia kimya akimtazama Lisa kana kwamba ni kinyago. “Kweli wewe sikichaatu, bali mwendawazimu kabisa. Sijawahi kuona mwanamke akitafuta mwanamume wa kumuoa baa, tena asiye mfahamu.”

Huku akitabasamu, Lisa aliongeza, “Kusema kweli nina mpango wa kuwa mkeo. Japo nilichokisema kitaonyesha kuwa nimekosa aibu, au mimi ni mhuni ama malaya, vyovyote vile. Lakini nimesema ukweli wangu. Nina umri wa miaka 24 mwaka huu, na nilihitimu kutoka Chuo Kikuu cha New South Wales Marekani.

Mimi ni mwanamke mwenye uwezo wa kufanya vizuri nyumbani na kazini. Zaidi ya hayo, nitamtunza mume wangu. Nina uwezo wa kujitafutia pesa pia. Mimi ni mzima wa afya na sijawahi kufanya tabia yoyote mbaya. Zaidi ya yote, mimi si mpenzi kigeugeu.” Lisa aliitumia nafasi yake kujinadi vyema.

Yule mwanamume alikosa la kusema. Akayapapasa macho yake, kisha akamtazama kwa mshangao, bado mdomo wake uligoma kutoa neno lolote.

Lisa aliinua mkono wake. "Naweza kuapa kuwa kuanzia sasa na kuendelea, nitakutendea mema tu na kukuahidi kutekeleza kila kitu nilichosema..."

"Nyamaza. Hatimaye mwanamume yule alishoshwa na maneno yake, akasimama.

Lisa alipoinua macho ndipo akagundua kuwa kweli mwanamume yule alikuwa mrefu. Alikuwa karibu futi sita na inchi mbili juu, na zaidi ya hayo, alikuwa na umbo pana la kiume haswa.

"Ikiwa unataka kuolewa na mimi, kesho saa nne kamili asubuhi ufike na cheti chako cha kuzaliwa katika ofisi ya mkuu wa wilaya ya Ilala." Mwanaume yule alimtazama akiwa kasimama, mkono mmoja ukiwa unasisitiza maneno yake huku mkono mwingine ukiwa mfukoni.

Lisa alipigwa na butwaa, hakuamini kabisa alichokisikia licha ya kuwa ndicho alichokuwa akikitaka, akajikuta anauliza kwa kigugumizi, “u..uu..uko seriuos?”

"Ukipenda uje ukipenda uache, ni juu yako." Yule mwanamume alimjibu kijeuri na kwa mkato kisha akageuka na kuondoka zake.

Wakati huohuo, gari aina ya Bentley Mulsanne lilisogea taratibu kuelekea lango la baa hiyo. Mlango wa gari hilo ulipofunguliwa, mwanamume aliyetoka kwenye baa ile akaingia ndani kwa madaha na kukaa kwenye kiti cha nyuma. Alifungua vifungo viwili vya shati lake juu ya kifua chake kupata hewa huku akiegemea kiti cha ngozi kwa uvivu.

“Si nilikuambia nataka nionekane wa hadhi ya chini safari hii, mbona umeniijia na gari la gharama hivi?” Mwanamume yule alimuuliza dereva wake.

Hans, ambaye alikuwa ni msaidizi wa kazi wa jamaa huyo mtanashati alijibu kwa upole. "Samahani mkuu, lakini Sam amesema hili ndilo gari la gharama ndogo zaidi kwa sasa katika familia ya Harrison."

“Kesho ukanunue Harrier, sitaki kuvutia umakini wa watu.” Yule mwanamume alikunja uso kidogo. "Nani mwingine anajua kuwa nipo Dar?"

"Ukiachana na Sam Harrison, hakuna mwingine isipokuwa Bibi Kimaro pekee." Hans alijibu.

Mwanamume huyo akamfikiria tena yule msichana aliyetoka kuongea naye ndani ya baa, na akamkabidhi Hans kazi ya kupepeleza wasifu wake. "Tafuta mtu huyu ni nani. Nataka kujua habari zake kabla ya mapambazuko.” Hans akakabidhiwa picha za Lisa alizopigwa kistadi na huyo jamaa wakati akiongea naye kwenye baa.
•••
Mpango wa Lisa ulienda haraka sana kiasi kwamba alijishuku kuwa alikuwa amelewa kupita kiasi. Japo alitaka sana kufakiwa jambo lake, hakutarajia kama yule mwanamume angekubali kirahisi vile. Lisa alihisi kama utani vile.

Wazo hilo lilibaki akilini mwake hadi Pamela alipokuja kumshtua kwa kumgonga begani, akamwambia kwa huruma, “Usikasirike sana. Si rahisi kuunasa moyo wa mwanamume handsome, tajiri na maaruf kama huyu. Endelea kujaribu hivyo hivyo—”

“Hapana, amekubali!” Lisa alionyesha wasiwasi huku akionekana kuduwaa. “Kaniambia tukutane kwenye lango la ofisi ya mkuu wa wilaya kesho saa nne asubuhi, ndiyo nipo nawaza, hivi kweli anamaanisha ama ananichora tu?”

“Wee!” Pamela alikaa kimya kwa muda kabla ya kuangua kicheko. “Hongera kwa kuwa shangaziwa Ethan!”

Lisa akauliza, “wewe unaamini kuwa kasema ukweli?”

Pamela aliubana kwa nguvu uso laini wa Lisa . "Kwa nini isiwe hivyo? Kwa mwonekano wako safi na wa asili, hakuna mwanamume anayeweza kukukatalia. Ikiwa ningekuwa mwanaume, ningekupenda mara ya kwanza tu kukuona. Twende tukanywe kusherehekea ndoa yenu.”

Lisa alijiuliza sana Pamela alikuwa amekunywa pombe kiasi gani baada ya kumuacha kwa muda ule mfupi. Alipotazama matupu mezani, alielewa kilichokuwa kwenye akili yake.
Hata hivyo, Lisa alianza kujisikia kulewa sana baada ya kunywa pombe kupita kiasi. Alihisi kichwa kuwa kizito.

ITAENDELEA....

Kwa leo tuishie hapa niseme tu tukutane katika sura ya 3 kujua nini kitafuata Je, mwanaume huyo mtanashati atatokea kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya kama ambavyo amlimwambia Lisa?, pia ndioa ya Lina na Etham itakuwaje, basi sehemu inayofuata itakupa majibu zaidi.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
JINA LA SIMULIZI..........................LISA
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP...........................0628924768
SURA YA...................................3&4

SURA YA 3

Jua la asubuhi liliangaza kupitia mapazia. Lisa akiwa amelala usingizi mzito aliamshwa na kelele za nje. Alipofumbua tu macho yake, akamuona Ethan akifungua mlango na kuingia chumbani kwake.

Pamela, ambaye alimfuata ndani ya chumba, alinguruma kwa hasira. "Hii ni nyumba yangu! Kimsingi hutakiwa kuingia bila idhini yangu!”

"Hakika, lakini samahani. Nina shida na Lisa na ninajua yupo hapa." Ethan alimtazama kwa makini Lisa ambaye macho yake yalikuwa mekundu na nywele zimevurugika kidogo. Lisa alikuwa macho wakati huo, macho yake yakionyesha huzuni.

Pamela aliwatazama wawili hao na kuwaambia. "Ethan na Lisa, mnapaswa kuwa na mazungumzo mazuri. Haikuwa rahisi kuachana namna hii baada ya kuwa pamoja kwa miaka mingi.” Baada ya kufikiria kidogo, Pamela aligeuka na kuondoka, akifunga mlango nyuma yake.

Chumba kilikuwa kimya. Akiwa amekaa pembeni ya kitanda, Ethan akanyoosha mkono wake kugusa nywele za Lisa. Kwa sura ya dharau, Lisa alikwepa mkono wake na kumtwanga swali. "Lina anajua kuwa uko hapa?"

Uso mzuri wa Ethan uliganda, kisha akakunja ngumi na kuongea kwa msisitizo. "Lisa , labda hujui kuwa familia ya Masawe imeamua kumpa Lina asilimia 80 ya hisa za kampuni yenu, Kibo Group."

Lisa alishtuka sana hadi midomo ikabadilika rangi. "Hii haiwezekani."

"Ni kweli. Baba yako alisema mwenyewe." Ethan alimhakikishia.

Lisa alionekana kufahamu kila kitu ndani ya dakika chache. Aliinua kichwa chake na kumtazama mpenzi wake wa shuleni ambaye alikuwa akimpenda enzi hizo. Machozi yakaanza kumtoka. "Ndio maana uliniacha mimi na kumchagua Lina, sivyo? Kwa sababu Lina ndiye mrithi!"

Ethan alimshika mikono na kumwambia, “hii ni mbinu yangu ya muda tu. Nimemchumbia Lina, lakini sitamwoa. Hili ni shinikizo la wazazi tu, wanataka nimwoe Lina kwa sababu ndiye mrithi wa familia yenu. Kama unavyojua, baba yangu ana mtoto wa nje. Nisipofanya hivi sitaweza hata kushindana naye kwenye urithi. Lisa , nataka tu kukupa maisha mazuri ya baadaye!.”

"Bullsh*t." Lisa alimpokonya mkono wake kutoka kwake na kumrushia matusi. "Una umri wa miaka 26 tu. Hata kama huna urithi wowote kutoka kwa familia yako, huwezi kupambana na kuanzisha biashara yako mwenyewe? Wewe ni mjinga sana. Toka hapa!”

Ethan alisimama taratibu huku akificha hisia zake machoni mwake. Alisema kwa upole, "Si katika uwezo wangu kuchagua cha kufanya kutokana na asili ya ukoo wetu. Kwa hiyo lazima tu nitimize kile nilichoambiwa kufanya"

Lisa alionekana kupoa bila kutamka neno lolote kwani aliona haina maana.
Katikati ya ukimya, Ethan alihema kwa sauti ndogo. “Nipe miaka mitatu Lisa. Wewe bado mdogo. Unaweza kumudu kusubiri.”

Lisa karibu aingiwe na wazimu. “Unanichukulia mpumbavu sivyo? Umechagua kumchumbia Lina kwa ajili ya tamaa ya urithi. Nani anajua kama hutamuoa miaka mitatu baadaye? Tafadhali toka usoni mwangu. Sitaki kukuona tena!”

"Wakati ndiyo utaoonyesha upendo wangu kwako. Unaweza kukasirika na mimi, lakini usitoke nje na kuelekeza hasira zako kwenye pombe. Sio nzuri kwa afya yako." Kwa kuwa Lisa hakuwa akielewa alichomwambia, alimshauri tu kabla ya kugeuka na kuondoka.

Aliposikia mlango ukifungwa, Lisa alitupa mto ukutani kwa hasira huku macho yake yakiwa mekundu na kutulia kwa sekunde kadhaa. Baada ya hapo, alivaa shati lake kwa hasira na kutoka nje.

“Unaenda wapi? Ethan kakuacha, kuna faida gani kumfuata?” Pamela alimsimamisha haraka.

Lisa akashusha pumzi ndefu, kisha akamkumbusha Pamela. "Simfuati Ethan. Nilikubaliana kukutana na mjomba wake saa nne asubuhi bomani ili tufunge ndoa."

Pamela akauliza kwa mshangao, “Unamwamini kweli?”

“Wewe mwenyewe si ulisema unamwamini jana usiku, au zilikuwa pombe?” Lisa akamshangaa.
Pamela akajibu kwa aibu, "Sikumbuki chochote nilichosema, hiyo ilikuwa tungi tu."

“Itakuwaje ikiwa yuko serious kuhusu hilo?” Lisa alimsukuma na kukimbia nje. “Wacha niwahi.”

Lisa aliendesha gari moja kwa moja hadi nyumbani kwao. Wakati huo baba yake, Jones Masawe, alikuwa tayari ameenda kazini. Alikimbia ghorofani kuchukua cheti chake cha kuzaliwa. Alipofika sebuleni tu, alimuona Lina akitoka nje ya chumba cha maktaba na rundo kubwa la nyaraka mkononi. Lina alionekana mtulivi na asiye na wasiwasi wowote ule.

“Hatimaye umerudi mdogo wangu. Bado nilikuwa na wasiwasi kuhusu kilichotokea jana.” Mwonekano wa kinafiki ulienea kwenye uso wa Lina. “Ni kwamba Ethan havutiwi na wewe. Huwezi kumlazimisha mtu asiyekupenda akupende.”

Lisa alimpiga Lina macho ya hasira. "Imetosha. Unaweza kuacha kuizungumzia tena habari za Ethan kwa kuwa mimi sina mpango naye tena. Nimekudharau sana dada yangu. Hukuona mwanamume mwingine hadi ung’ang’ane na Ethan tu?"

“Usinifanyie hivi mdogo wangu.” Lina akauma mdomo, machozi ya uongo na kweli yakimtoka. "Nitakupatia chochote unachotaka Lisa sawa? Sitahusika katika masuala yanayohusiana na kampuni. Nitakupa hati hizi." Alipokuwa akiongea, aliziweka zile nyaraka mikononi mwa Lisa. Lisa aliona ni ajabu na akanyoosha mikono yake kuzisukumia mbali nyaraka zile. Matokeo yake, nyaraka zote zikatawanyika kwenye sakafu.

“Mnafanya nini jamani?” Ghafla, Mama Masawe, alishuka ngazi na kuuona uso wa Lina uliokuwa na machozi pamoja na nyaraka zilizotawanyika. “Hizi si hati za kampuni ambazo baba yako alikupa uzipitie? Kwanini zimetawanyika hovyo hapa?”

“Usimkasirikie, Mama. Ni kosa langu." Akiwa na uso ulio na huzuni ya kulazimisha, Lina alieleza kwa haraka, “Lisa aliniomba niache kujihusisha na masuala ya kampuni na kumkabidhi hati hizi. Nilikuwa nikipanga kumpa hati hizo, lakini pengine hajafurahishwa na suala la Ethan, kwa hivyo—”

“Wewe ni mpuuzi—” Lisa alimkemea dada yake lakini gahfla akakatishwa na karipio kali kutoka kwa mama yake.

“Nyamaza!” Mama Masawe alimkazia macho makali. “Nani alikupa haki ya kuwa na amri katika masuala ya kampuni? Ni baba yako na mimi tuliyempatia Lina hizo nyaraka. Lina atakuwa rasmi meneja wa kampuni hiyo wiki ijayo. Afadhali ufahamu hili mapema.”

Lisa alipigwa na butwaa. "Nikizungumzia juu ya elimu na uzoefu, nina sifa zaidi kuliko yeye. Licha ya kujiunga na kampuni mwaka mmoja mapema kuliko yeye, mimi si meneja bado. Ni nini kinachompa haki ya kuruka hadi cheo kama hicho?”

“Mama, afadhali nisiwe meneja. Sitaki kuharibu uhusiano wangu na Lisa,” Lina alisema mara moja huku akilia.

Moyo wa Mama Masawe ulimuuma sana. “Angalia jinsi Lina anavyojali udada wako. Lakini wewe je? Una akili finyu na umejaa ubinafsi. Hufai hata kuwa meneja. Si ajabu kwamba Ethan ameemchagua Lina badala yako.”

Lisa aliposikia maneno ya kikatili ya mama yake alihisi kana kwamba anapigwa na fimbo ya moyoni. Lina na Lisa walikuwa binti zake. Hata hivyo, Mama Masawe alikuwa na upendeleo kwa Lina hivi kwamba aliamini yote aliyosema na alikuwa tayari kumgandamiza Lisa kwa ajili yake. Lisa alikuwa kando ya mama yake tangu mtoto. Je, Mama Masawe hakujua tabia yake? Hakuna aliyemfariji Lisa tangu Lina arejee. Kila kitu kilichotokea kilichukuliwa kama jambo la kweli.

Huku hasira zikizidi kuutawala mwili wake kwa namna ambayo haikuwahi kutokea, Lisa alipiga hatua mbili nyuma. “Sawa. Kwa kuwa mimi ni mbaya sana, nitaondoka, sawa?" Alienda chumbani kwake mara moja baada ya kumaliza kuongea. Alichukua begi na kisha kuingiza nguo zake ndani yake.

Sauti ya Lina ilitoka mlangoni. “Mama, Lisa ana wazimu. Tunapaswa kuzungumza naye asiondoke.”

“Usijisumbue naye. Hivyo ndivyo alivyo. Tumemdekeza kupita kiasi, we mwache tu aende atarudi tu siku mbili baadaye. Twende tukanunue nguo kwani utakuja kuchumbiwa hivi karibuni.” Punde, sauti zikafifia polepole wakati wawili wale wakiondoa.

Huku matone makubwa ya machozi yakianguka nyuma ya mkono wake, Lisa alibeba begi lake kuteremka ngazi za mjengo na kutoka nje. Baada ya hapo, aliendesha gari lake na kutokomea kabisa. Aliondoka akiwa anasikitika kwamba alionekana kupoteza kila kitu ndani ya siku moja tu. Kwa nini kila mtu alimtenda vile wakati hakufanya lolote baya? Alishika usukani huku macho yake yakiangaza kwa hali ya kutoamini kilichokuwa kinaendelea.


SURA YA 4

Baada ya dakika 40, Lisa alifika kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya ya Ilala. Alipofika tu aliona sura ya mtu aliyemfuata hapo akiwa kasimama kwenye mlango wa ofisi ya msajili wa ndoa, vizazi na vifo. Mwanaume huyo alionekana nadhifu akiwa amevalia shati la khaki liililopigwa pasi kabisa na suruali nyeusi. Alikuwa mrefu na mwenye nguvu. Alimkimbilia mara moja baada ya kupaki gari lake.

“Kweli umekuja.” Sauti ya Lisa ilijawa na mshangao wa kutoamini.

Mwanamume yule alipogeuka nyuma, alisikia harufu ya pombe iliyokuwa imetanda mwilini mwa Lisa tangu usiku uliopita. “Hukuoga?”

Lisa aliona aibu mara moja. Alipojinusa akasikia kweli harufu ya pombe ikitoka mwilini mwake. “Nilikunywa pombe kupita kiasi jana usiku, hivyo nilikuwa tayari nimepoteza fahamu nilipofika nyumbani, na nilipoamka asubuhi ya leo nilikuwa na haraka sana, kwa hiyo nikakurupuka tu bila kuoga ili niwahi…”

Alipogundua kwamba mtu huyo alikuwa akizidi kumdharau, aliapa haraka, “Leo ilikuwa bahati mbaya tu. Kwa kawaida mimi huoga kila siku na ninapenda kujiweka safi.”

Mwanamume yule hakuonekana kuyajali maneno ya Lisa. Sifa zake ziliongezeka maradutu baada ya Lisa kumuona vizuri asubuhi ile. Aligundua kuwa mwanamume huyo hakuwa tu mtanashati bali pia alikuwa makini.

Alijua kutunza muda na hakuwa na ahadi za uwongo. Mavazi yake pia yaliongeza haiba yake ya mvuto na kumfanya apendeze zaidi. Kama angeamua amchunguze kipengele kimoja kimoja basi Lisa huenda angeshinda kutwa nzima akielezea umaridadi wa mwanamume huyo.

Lisa alijua kwamba wasichana wachache waliokuwa wakienda katika ofisi ya usajili kwa shida mbalimbali pia walikuwa wakimtazama mwanamume huyo kwa wivu mkubwa.

"Ni mwanaume mzuri kama nini." Mwanamke mmoja aliongea waziwazi.
Mwanamume aliyekuwa kando ya mwanamke huyo naye akasema, “yule msichana naye anapendeza pia.”

"Hiyo ni kweli. Wanalingana vizuri. Watoto wao wa baadaye labda watakuwa wazuri, tofauti na wetu, wamebarikiwaje…!”

Majadiliano hayo yalipofika masikioni mwa mwanamume yule, mume mtarajiwa wa Lisa, alisema mara moja, “Hatutapata watoto. Hilo ndilo sharti la kwanza la ndoa yetu.”

Lisa alishangaa lakini alishindwa cha kusema. Tamaa ya kuwa shangaziwa Ethan ilimziba masikio na kumfanya aone sharti hilo kuwa si kitu.

Mwanamume yule aliendelea kusema, “Nitakupa talaka miaka mitatu baadaye na nitakulipa kiasi cha pesa ambacho kitakutosha kuishi maisha yako yote. Pia, sitakutana na familia yako. Fikiria juu ya mashariti haya kwa makini. Ikiwa huwezi kukubaliana na mpango huu, unaweza kuondoka."

Lisa hakuhisi chochote moyoni mwake. Licha ya kwamba alikuwa anaenda kuoana na mwanamume huyo aliyeonana naye siku moja tu tena usiku, dhamira yake haswa haikuwa kuolewa bali alikuwa anatafuta njia tu ya kuwa shangazi yake na Ethan kwa kuolewa na mjomba wake. Kwa hiyo mambo mengine hakuyajali kabisa.

Kwa hivyo, hakuwa na nia ya kumbishia masharti yake. Aliamini kwa nguvu yake angeweza kubadilisha sharti moja hadi jingine kama angetaka. Kwa haiba yake, aliamini kwamba angeweza kuuteka moyo wa mwanamume huyo katika muda wa miaka hiyo mitatu. Kwa wakati huo ilimbidi aweke hiyana pembeni na afikirie zaidi kuunganisha utambulisho wake kama shangaziwa Ethan.

“Sawa.” Lisa alitamka kukubali.

Mara tu Lisa alipokubali wawili hao walienda kwanza kupiga picha pamoja kabla ya kuingia kwenye ofisi ya msajili. Mpiga picha ambaye alikuwa ametumia muda mrefu kuwapiga picha, hakuridhika na matokeo kutokana na wawili wale kuonekana wapo mbalimbali sana kihisia.

“Hamwezi kukaribiana na kuonekana kama wapenzi? Pia,wewe bwana, tafadhali tabasamu hata kwa mbali basi.” Alilalamika mpiga picha.

Sura ya papara ilivuka usoni mwa mwanamume yule. Lisa mara moja akaushika mkono wake, kisha akasema kwa tabasamu, “Mishipa yake ya uso imeharibika, kwa hiyo anasumbuliwa na ugonjwa wa kupooza usoni. Usimlazimishe tena. Mwache tu.”

Yule mwanamume akaguna lakini hakusema chochote. Alihisi kuwa amedhalilishwa sana kwa usemi wake na alimtupia jicho la hasira Lisa ambaye alikuwa amevaa tabasamu la furaha.

“Afadhali uache kuongea upuuzi ikiwa unataka kufunga ndoa na mimi.” Mwanamume yule alimnong’oneza Lisa sikioni kwa ujeuri huku akisimama kwa utulivu pembeni yake. Harufu nzuri ilitoka kwenye mdomo wake, ikimsisimua Lisa.

Mwanamume yule aliganda na kukaa kimya. Mpiga picha alimuonea huruma moyonim kwa kuamini maneno aliyoyasema Lisa, kwamba kijana mzuri kama yeye alikuwa na ugonjwa wa kupooza usoni.

Baada ya Lisa na mumewe mtarajiwa kumaliza zoezi la kupiga picha, walielekea ghorofa ya kwanza kuandikisha ndoa yao. Ilikuwa tu wakati mwanamume yule alipochukua cheti chake cha uraia ndipo Lisa hatimaye aliliona jina lake kamili-Alvin Kimaro!

Hata hivyo, jina la ukoo la mama yake Ethan lilikuwa ni Mushi. Katika hali hiyo, jina la ukoo la mjomba wake Ethan lilipaswa kuwa Mushi pia. Kwa mshangao, Lisa aliuliza, "Kwa nini jina lako la mwisho ni Kimaro?"

“Uh-huh.” Alvin akiwa ameinamisha kichwa chini kusaini nyaraka za ndoa hakujishughulisha kujua Lisa anamaanisha nini. Alijibu kwa tu kwa urahisi, "Nnatumia jina la ukoo la upande wa mama yangu."

“Oh.” Hatimaye Lisa alielewa. Alikuwa amejawa na hofu mapema akifikiri kwamba huenda alikuwa kajiingiza kwa mwanamume ambaye si sahihi kulingana na matarajio yake. Aliamua tu kuolewa na mwanamume huyo kwa sababu yeye ndiye mjomba wa Ethan. Hata hivyo, alihisi kwamba kuna jambo fulani halikuwa sawa, lakini aliendelea tu kukamilisha zoezi.

Dakika kumi baadaye, vyeti vya ndoa vilitolewa. Lisa alihisi huzuni na furaha ya ajabu kwa wakati mmoja. Tangu utotoni, alikuwa akidhani kwamba angeolewa na Ethan. Kinyume na matarajio yake, aliolewa na mwanamume ambaye alikuwa amekutana naye mara moja tu.

“Hii hapa namba yangu ya mawasiliano. Nina jambo la muhimu la kushughulikia sasa hivi, kwa hiyo nitaondoka kwanza.” Alvin aliandika namba yake kwenye karatasi tupu na kumpatia Lisa kabla hajaondoka.

“Subiri kidogo…” Lisa alimzuia mara aliporudi kwenye fahamu zake. “Sasa kwa kuwa sisi ni wenzi wa ndoa, tunapaswa kuishi pamoja.”

Kwa sauti mbaya, Alvin alijibu, “Sipendelei kuishi na mtu mwingine.”

“Mimi ni mke wako halali wa ndoa, si mtu mwingine. Hata kama tutaachana miaka mitatu baadaye, bado tunapaswa kuishi pamoja.” Lisa alijitetea.

Alvin alimwangalia tu akihisi kusumbuliwa. Hakutaka kuongea tena. Akitikisa cheti cha ndoa mkononi mwake, Lisa alipiga kelele akijaribu kupata huruma yake. “Nina huzuni sana. Tangu dada yangu aliyepotea kwa muda mrefu arudi, wazazi wangu wamekuwa wakinitendea kwa dharau. Na kwa sasa nimefukuzwa kabisa nyumbani na sina mahali pa kukaa.”

"Unaweza kwenda na kukodisha nyumba mahali, nitakupatia pesa." Alvin alijibu kikatili huku akiondoka bila kujali.

"Usiniache, mume wangu!" Lisa alipiga yowe ghafla, akiushika mkono wake kwa nguvu kwa mikono yake laini. "Sina chochote ila wewe tu sasa hivi." Sauti yake iliyozidi kuwa kubwa ilikuwa imevutia umakini wa watu wengi kuwatazama kando ya ofisi ile ya mkuu wa wilaya yenye purukushani ya watu kibao.

Huku akivuta uso wa hasira, Alvin alijuta kuoaoa hovyo. “Sawa. Ninaishi Oyster Bay, mtaa wa Buzwagi. Nenda huko mwenyewe, anuani ya nyumba ni hii na namba za siri za kufungulia mlango ni hizi hapa." Alvin alimwambia huku akimkabidhi tena kijikadi kingine, kisha akamuonya kwa upole, “Utalala kwenye chumba cha wageni. Huruhusiwi kuingia chumbani kwangu.”

Akiwa na furaha, Lisa alicheka kisirisiri. Aliamini kuwa yeye ndiye angemsihi aingie chumbani kwake siku si nyingi.

"Na pia, usimsumbue Charlie." Alvin alimpa angalizo jingine.

“Charlie?” Lisa alishtuka. “Tayari una mtoto wa kiume?”

Alvin hakujibu swali la kipuuzi, badala yake aliinua macho yake kwa msisitizo na kumwambia kwa mkato. “Mtunze vizuri. Hakikisha anapata chakula chake mara tatu kwa siku.” Mara baada ya kumaliza sentensi yake, aliondoka moja kwa moja.

Lisa alishtuka sana hadi akasahau kumfuata tena Alvin. Ingawa alikuwa amejizatiti kuolewa na mtu ambaye hakumpenda, hakuwa tayari kabisa kuwa mama wa kambo kwa mtoto yoyote. Alisimama kando ya barabara kwa muda wa nusu saa akiwaza na kuwazua, akifikiria utambulisho wake wa wakati ujao wenye kutatanisha—yaani, mama wa kambo wa ‘Charlie’ na shangazi wa Ethan....ITAENDELEA....

Kwa leo tuishie hapa na tumeona tayari ndoa imepita kati ya Lisa na Alvin lakini ni ndoa ya mkataba na mashariti mengi sasa je mashariti hayo yatatimia au vipi pia Etham atamuoa Lina ambae ni dada wa Lisa kama wazazi wao wanavyotaka au penzi litaingia dosari...basi nikusihi tukutane katika sura ya 5 kujua nini kitafuata kwenye mkasa huu wa kusisimua..

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
JINA LA SIMULIZI............................LISA
SPONSODER BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP.........................0628924768
SEHEMU............................................5&6

SURA YA 5

Hatimaye Lisa alikimbia kwenye maduka kununua vinyago vya watoto. Mtoto anayeitwa ‘Charlie’ alipaswa kuwa mvulana. Baada ya kuchagua aina kadhaa za magari ya kuchezea na seti za Lego(michezo ya watoto), aliendesha gari hadi Oyster Bay na kutia nanga mtaa wa Buzwagi mbele ya nyumba aliyoelekezwa na Alvin.

Akiwa amebeba vitu mbalimbali, akashusha pumzi ndefu mbele ya mlango wakati akiingiza namba za siri za kufungulia geti. Geti lilifunguka na hapakuwa na mlinzi yeyete. Alipofika kwenye mlango wa kuingilia ndani aliingiza nambari za siri tena kwenye kitasa na mlango ukafunguka bila ubishi. Tabasamu la kirafiki lilienea usoni mwake wakati anapaza sauti kwa nguvu na kuita, “Charlie! Charlie! Hujambo! Charlie—”

“Meo!” Sauti ya paka ikampokea Lisa.

Kwa mshangao, Lisa alipepesa macho na kuita tena,“Charlie?”

Charlie alikuwa ni paka mnene mwenye mwili mweupe na masikio mepesi ya weusi na weupe. Alionekana akiwa amelala kwenye kochi kivivu. Alitoa sauti nzuri kwenye sebule tulivu, “meowww!”

Lisa akaduwaa!

Baada ya paka mnene kunyoosha mwili wake, aliruka chini ya kochi na kuelekea kwenye miguu ya Lisa ili kunusa furushi alilokuwa amebeba akidhani kuna chakula. Alipoona hakuna kilichomvutia, Charlie alirudi kwenye kochi na kulala juu yake kwa kiburi.

Lisa alikosa la kusema. Alvin alipaswa kumueleza hili mapema. Alikuwa ametumia muda mwingi kuhangaikia kuwa mama wa kambo! Sasa amekutana na paka badala ya mtoto wa kiume aliyemtarajia. Alichoka! Licha ya hayo, paka huyo mwenye manyoya safi alipendeza na kumvutia.

Lisa akasogea mbele, akimuinua kuyabana mashavu yake yaliyonona, lakini paka huyo alijitoma kwenye chumba cha kulala cha Alvin kwa kasi ya umeme. Chumba cha kulala cha Alvin sehemu ambayo Lisa hakuwa na sifa ya kukanyaga kulingana na mashariti ya ndoa yao.

Lisa alishusha pumzi na kukaa. Kisha, alichunguza kuzunguka nyumba hiyo iliyokuwa na vitatu vya kulala na sehemu mbili za kupumzikia. Kulikuwa na chumba cha kulala master, cha mwenyewe Alvin, chumba cha wageni, na chumba cha kusomea, au maktaba.

Mapambo ya ndani ya nyumba yalikua ‘simple’ tu, yakipambwa kwa mtindo wa kisasa kutumia rangi nyeusi, nyeupe, na kijivu kama mpango wake mkuu wa rangi. Ilikuwa ya kupendezani lakini ilitoa hali ya kupooza na isiyo na uchangamfu kwa wakati mmoja. Upambaj huo labda haukugharimu sana.

‘Haya kweli ndo makazi ya mjomba wa Ethan?’ Alijiuliza Lisa. Alikuwa amesikia kuwa mjomba wa Ethan ni mjasiriamali aliyefanikiwa sana huko nje ya nchi. Ilikuwa ni jambo moja ikiwa alichagua kutoishi katika jumba kubwa la jarida, lakini hakukuwa na dalili za kunyesha kwamba aliyeishi mahali hapo alikuwa mtu aliyefanikiwa sana. Bila kusahau rafu za vitabu katika chumba cha kusomea zilijazwa na vitabu vya kisheria, kama vile ‘The Science of Law’, ‘The Law Society Gazette’, na ‘Are We Slaves to Our Genes?’

Kuna hisia mbaya zilimwingia Lisa. Je, kwamba mtu huyo hakuwa mjomba wa Ethan? Hapana, hilo lisingewezekana! Pamela anaweza kuwa mzembe wakati fulani, lakini kwa jambo zito kama hilo, hakuweza kuwa amefanya makosa. Lisa hakutaka kuamini kama mapato na makosa kwenye hilo.

Kufikiria kupita kiasi kumchosha Lisa. Alichukua simu yake kumpigia rafiki yake. “Una uhakika kuwa yeye ni mjomba wa Ethan?”

“Ni kweli nilisikia kutoka kwa kaka yangu. Hata alikula chakula pamoja naye hapo awali. Pamela alijibu na kuuliza, “vipi kwani?”

Akiwa ametulia, Lisa akaweka kifuani mwake kwenye hofu yake. "Niliogopa kwamba nimeolewa na mtu tofauti."

"Mungu wangu, umeolewa naye kweli?" Kelele ya mshangao ikasikika kwenye simu. “Amejitokeza kweli?”

"Uh-huh," Lisa alijibu upande wa pili wa simu, macho ya Pamela yalikuwa yakilengwa na machozi. “Tuliahidiana kuwa malaika wa kila mmoja wetu. Unawezaje kuniacha kwa kufumba na kufumbua tu?” Maneno yale yalimfanya Lisa ahisi huzuni tena. Alitakakuongea lakini maneno yake yakakwama kooni. "Sawa, wewe na mumeo mnapaswa kunihudumia kwa chakula cha angalau angalau." Lisa alichombeza.

"Um ... Hakuna chochote kinachoendelea kati yetu, ni ndoa ya mkataba tu." Lisa akapata ujasiri wa kueleza mashariti waliyowekeana na mwanaume huyo.

"Una sura nzuri sana lakini mapenzi hayajawa rahisi kwako." Pamela alionyesha huruma yake. "Lakini usijali, nina uhakika atajisalimisha kwako ndani ya muda mfupi, labda si kwa sura na umbo lako la ulimbo."

“Naamini hivyo pia.” Lisa aliunga mkono.

Baada ya simu kukatika, Lisa alishuka karibu na duka kubwa la karibu. Nyumba yake mpya ilikuwa imepoa sana na ilionekana kupwaya machoni pake. Haikustahili kuitwa nyumba. Kwa hakika ilihitaji mahitaji mapya.

SURA YA 6

Alvin Kimaro alifika Dar kama mwanasheria na wakili msomi wa kimataifa ambaye muda mrefu alikuwa akifanyia kazi zake jijini Nairobi nchini Kenya. Alikuwa amekuja Tanzania kwa mwaliko wa rafiki yake, Sam Harrison, kampuni wa kampuni ya Mawakili ya ‘Jennings Solicitors’ kuja kumsaidia kesi kadhaa ngumu. Hata hivyo, huko Nairobi bibi yake alikuwa amemwandalia mke wa kuoa lakini yeye hakuwa tayari.

Tangu afariki mpenzi wake Sarah, hakuwa na mpango wa kuwa na mwanamke mwingine, lakini bibi yake alimwambia asipooa kabla ya mwaka kuisha basi angemwachia radhi yake. Ili kuwaridhisha wazee wake, ilibidi atafute mwanamke wa kuoa ambaye angeendana na mashariti yake.

Mungu si Athumani Lisa akawa kajitokeza na kutegua kitendawili cha Alvin. Sasa baada ya kuwaonyesha cheti cha ndoa wazazi wake, hatimaye presha ingepungua.

Saa kumi kamili za jioni, Alvin alikuwa ametoka kufungua kesi aliyokuwa a kushughulikiai wakati Sam Harrison rafiki na mshirika wake, ambaye pia ndiye bosi mkuu wa kampuni hiyo alipoingia ofisini kwake.

“Hongera sana! Je, tupate chakula cha jioni na mke wako mpya usiku wa leo?” Sam aliuliza akitabasamu.

“Siyo kwamba hujui sababu halisi iliyonifanya nioe, Sam!” Alvin alimjibu bila kuinua kichwa chake, macho yake yakiwa yamebaki kwenye maandishi kwenye nyaraka.

"Kweli wewe huamini katika mapenzi? Nilisikia kwamba Lisa Jones ni mrembo kabisa. Ina maana hupendezwi naye hata kidogo?" Sam alijawa na msisimko.

Alvin alijishusha kwenye kiti cha ofisi kinachozunguka huku akichunguza matumizi ya rafiki yake kwa macho ya udadisi. Alvin akasitisha alichokuwa anakifanya kwa sekunde moja. Alikumbuka laini ya rangi ya kuwaka ya msichana huyo na uso wake uliokuwa mzuri kama unaochanua. Hata hivyo, tabia yake isiyo na aibu ilimchefua.

“Kwa hiyo umeamua kumuoa huyu binti haraka haraka ili kuzima jitihada za bibi yako anayetaka kukuza kwa nguvu kwa yule mwanamke tajiri?” Sam aliuliza.

Alvina alijibu sekunde kadhaa baadaye, “Nadhani unanijua vizuri Sam. Ukiachana na Sarah aliyenipenda kwa moyo wake wote, siamini kabisa wanawake, wengi wao huja kwangu kwa sababu ya hadhi yangu. Ningekuwa na shida ya mke ningekuwa nimeshaoa siku nyingi.

Lakini huyu binti amejitokeza wakati sahihi. Sipendi kugombana na Bibi Kimaro kila wakati kwa sababu ya kuoa. Baada ya miaka mitatu mambo yatakuwa yamepoa, nitampa talaka kuendelea na mambo yangu.

Waliendelea suala hili kwa kirefu kidogo, baadaye Sam akahamisha mada kwa kutoa mapendekezo. "Nifanyie upendeleo kidogo, ningependa tule chakula cha jioni pamoja na mawakili wengine wa kampuni usiku wa leo."

"Hmm," Alvin alijibu. Kisha simu yake ikalia kwa sauti ya meseji. Alichukua simu yake kuona maandishi yaliyokuwa yakiingia kutoka kwa mtu anayeitwa 'Alvlisa'.

[Hubby, huyu ni Lisa.]

Alvin hakujua la kujibu. Alipunguza macho kwa ukali wa mwanga wa simu na kukubali ombi la ujumbe.

[Mume, utarudi nyumbani jioni kwa chakula?] Lisa alituma ujumbe mwingine ndani ya sekunde chache.

Alvin: [Hapana. Usifanye hivyo.]

Alvlisa: [Sawa basi, nitakuita Alvlisa. Ni jina zuri.]

Alvin hakujua la kusema zaidi.

Baadaye usiku huo, kundi la watu walifurahia chakula cha jioni katika maeneo maarufu na kuvutia katkati ya jiji la Dar es Salaam, ‘City Restaurant’. Kundi hilo la mawakili kutoka kampuni ya ‘Jennings Solicitors’ walibadilishana maoni kuhusu mwenendo wa kesi mpya zilizochukuliwa hivi karibuni na kampuni ya mawakili. Alvin alisikiza huku akili yake ikiwa mbali sana. Mara akasikia tena taarifa ya ujumbe kwenye simu yake.

Lisa alimtumia picha. Chini ya mwangaza wa taa laini za njano alionekana paka wake Charlie. Alikuwa akifurahia mlo wa kipande kidogo cha samaki mkavu.

Ujumbe kutoka kwa Lisa, aliyeamua kujisevu kwa jina la Alvlisa ukasomeka hivi.

Alvlisa: [Hubby, usijali kuhusu sisi. Ninamtunza vizuri Charlie mdogo.]

Alvin alihema kwa huzuni. Paka mwenye pupa alikuwa amehongwa na kutekwa kilaini kabisa....ITAENDELEA....

Mambo bado ni moto sana na ndoa ya mchongo inazidi kujongea taratibu sana lakini Alvin ataweza kweli kumpa Lisa talaka baada ya miaka mitatu kama masharti yanavyosema au ndio masharti yaliyowekwa ili yavunjwe...basi acha tusubiri sehemu ambayo ni sehemu ya 7&8 kujau nini kitajiri kwenye simulizi hii ya kusisimua.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
JINA LA SIMULIZI.............................LISA
SPONSORED BY.........SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP...........................0628924768
SEHEMU.............................................7&8

SURA YA 7

Saa tatu na nusu usiku, namba ya siri iliingizwa kwenye mlango wa nyumba ya Alvin. Alipofungua mlango tu, Alvin alipigwa na butwaa mara tu alipotia mguu ndani ya nyumba yake. Ilikuwa ni nyumba yake lakini alidhani kapotea kwani haiukuwa kama alivyoiacha wakati akiondoka asubuhi yake. Ilikuwa imefanyiwa marekebisho makubwa. Kochi nyeusi ilipambwa kwa matakia ya bluu ya tausi.

Meza nyeupe ya kulia ilifunikwa kwa kitambaa cha kijani kibichi. Vase ya glasi iliyojaa maua ya rose ilikaa kwa kutulia juu yake. Nyumba nzima ilipambwa kwa mimea ya kijani kibichi na maua safi. Alvin kidogo apotee kwenye nyumba yake mwenyewe!
Aliangaza huku na kule kwa mshangao hadi Lisa alipomshtua.

"Alvin, uko nyumbani, mbona unashangaa sana?" Lisa alitoka nje ya chumba cha wageni akiwa amevalia gauni la hariri la mikono mirefu. Nywele zake nene na ndefu zenye weusi wa asili iliyokoza zilimwagika juu ya mabega yake. Chini ya upindo wa gauni lake kulikuwa na miguu yake ya kupendeza na myembamba. Alionekana anayevutia kana kwamba kulikuwa na jambo kalikusudia kwa Alvin.

Macho ya Alvin yaliingiwa na utata. "Ni nani aliyekuruhusu kuvaa hivyo nyumbani kwangu?" Ndita kwenye paji la uso wake zilikunjamana huku akisema kwa ukali kusisitiza kutoridhishwa kwake.

"Kwani vipi?" Lisa alizunguka bila kujali. “Kifua, tumbo na matako yangu yamefunikwa vizuri. Magoti yangu na miguu tu ndio viko wazi, tatizo liko wapi? Wasichana wengi warembo wanatoka mitaani wakiwa wamevaa zaidi hata ya hivi. Hata hivyo nipo ndani na wewe ni mume wangu, hata kama ningekuwa mtupu mbele yako hakuna cha ajabu.” Lisa alimjibu kwa upole.

Alvin hakujua aangalie wapi. Hakika, hakuwa amevaa nguo zinazoonyesha wazi tu, lakini pia hakuwa amevaa chochote ndani ya nguo hiyo.

Alvin akakwepesha macho yake na kubadili mada. "Nilikubali kukuruhusu uingie kwenye hii nyumba, lakini sikukupa ruhusa ya kubadilisha chochote nyumbani kwangu."

“Hilo nalo limekuchukiza? Nyumba hii illikuwa tupu sana hapo awali hata haikuwa kama vile nyumba wanayokaa watu.” Lisa akamwonyesha kiganja chake. " Hata hunihurumii nilivyohangaika kupamba vizuri, angalia, nina michubuko michache kwenye kiganja changu kutokana na kusogeza vitu huku na kule."

Alvin akashusha macho yake kumtazama. Hakika, kulikuwa na mikwaruzo michache kwenye ngozi yake laini ya kiganja chake maridadi. "Unastahili, hiyo ndiyo faida ya kiherehere chako. Nataka kuiona nyumba yangu kama ulivyoikuta" Aliongea kwa mkwara kabla ya kuelekea chumbani kwake.

Akiwa amekasirika, Lisa alivuta uso kwenye umbo la mwanamume yule wakati akiondoka. Alvin hakuonyesha kumjali hata kidogo. Lisa asingejaribu kukubali kuolewa huyo mtu mgumu kama si kwa mpango wa kuwa shangazi wa Ethan.

Saa moja asubuhi siku iliyofuata, Alvin aliamka mapema na kugongana na Lisa aliyekuwa anapiga mswaki bafuni. “Habari za asubuhi, Alvlisa. Unaenda kukimbia asubuhi?" Macho ya Lisa yakatua kwenye nguo yake ya michezo.

Alvin alikuwa na hasira mbaya. Uso wake ulivyoonekana asubuhi ile ni kama alikuwa akigombana na mtu usiku kucha. Lakini Lisa alivutiwa na tabia yake ya kutoka nje kwa ajili ya kukimbia asubuhi. Kama alifanya vile kila siku basi ilionyesha kwamba alikuwa mtu wa nidhamu.

“Ndiyo.” Alvin akamjibu kwa kujisikia. Na yeye pia alishangaa kidogo kwa Lisa. Wasichana wa umri wake hawakuwa na kawaida ya kuamka mapema.

“Sawa, usipate kifungua kinywa huko kabla hujarudi nyumbani. Nitakuandalia kitu kizuri sana hapa,” aliongea kama mama wa nyumbani anayefaa, “kifungua kinywa cha nyumbani ni safi zaidi kuliko cha huko migahawani.”

Alvin akakunja uso. “Hakuna haja ya hilo. Unapanga kuhama lini?" Uso wake mzuri uliganda kwa sekunde moja. “Ingawa tumeoana, sitaki kujihusisha sana na wewe. Usijipotezee muda wako maana sina hamu na wewe hata kidogo,” Alvin aliyatoa maneno yale ya kuchoma moyo bila kujali hisia za Lisa. Kisha kusema hayo akaondoka nyumbani.

Lisa alivuta nywele zake kidogo huku machozi yakimtoka mara moja. Alisimama pale sebuleni akiwa ametulia kwa muda mfupi. Haraka akajikusanya na kuanza kuandaa kifungua kinywa. Alvin aliporudi baada ya kukimbia kuzunguka bustani alikutana na harufu ya kupendeza ikisambaa nyumba nzima kutokea jikoni, na kumfanya ashikwe na njaa mara moja.

Lisa alitengeneza kifungua kinywa murua. Kulikuwa na chai nzito ya maziwa, chapati za kumimina zenye mchanganyiko wa mayai na viungo anuwai zilizotawanyisha harufu yake tamu nyumba nzima. Halafu pia alitengeneza kababu na visheti. Mchanganyiko wa matunda fresh yaliyoymenywa na kukatwakatwa kwa umaridadi pia yalinongesha utamu wa kifungua kinywa kile.

"Sipendi vitu vitamu kwa kifungua kinywa. “Alvin alikataa kwa kiburi. Maneno ya moja kwa moja aliyotoa mapema asubuhi yake yalikusudiwa kumfukuza Lisa nyumbani kwake. Bila kutarajia alimkuta hana hata habari na hata kishamtengenezea kifungua kinywa.

Alvin alishangaa kimyakimya! Kwa mtazamo wa harakaharaka, Lisa alionekana kama msichana mrembo aliyedekezwa ambaye hakuwahi kufanya kazi hata moja maishani mwake. Allvin alikuwa amezoea kuona wanawake kama yeye. Lakini kwa Lisa aliona tofauti iliyomshangaza.

Alvin alipuuzia kifungua kinywa alichoandaa Lisa, akachukua katoni ya maziwa kutoka kwenye friji. Lisa alimbembeleza kidogo lakini hakukubali. Ilionekana kuwa Alvin alikuwa amedhamiria kukitosa chakula alichotengeneza. Ni mtu wa kujidai! Bila kujali, hakuwa na shida. Akaamua kufurahia kifungua kinywa mwenyewe.

Lisa alirudi jikoni kuendelea kutengeneza kababu. Alvin naye akaingia jikoni sekunde chache baadaye kupasha joto maziwa. Kutoka kwenye pembe za macho yake, alimwona Lisa akiwa busy akitengeneza unga kuwa vijiti kadhaa virefu kabla ya kuviweka kwenye mafuta ya moto. Ndani ya sekunde chache, magogo ya dhahabu yalielea juu ya mafuta. Ilitoa harufu nzuri ambayo ilishambulia pua za Alvin.

Ustadi huu lazima uwe umepatikana kutoka kwa miaka mingi ya uzoefu. Alvin akageuza macho yake kuelekea kwa Lisa tena. Chapati nzuri za kumimina kwenye kikaango cha mafuta zilitoa harufu iliyoteka kabisa hamu yake, lakini akajidhatiti kuwa mbishi na kuvumilia kwa ndani tu.

Mashavu ya Lisa yaliyonenepa kidogo yalibadilika rangi kwa sababu ya joto jikoni, na kumfanya aonekane mrembo na mwenye kupendeza. Ngozi yake ilikuwa nzuri bila shaka. Lisa alimwona Alvin akimtazama na kwa staili yakuchezacheza akainua kababu moja, akiipungia mbele ya macho yake. “Alvin, una uhakika hutaki kuonja ladha hii?”

"Sipendezwi." Alvin akajibu kikauzu. Aligeuza macho yake na kuweka sandwich ndani ya microwave. Kisha, akasubiri zipate joto kwa sekunde kadhaa. Alvin akakusanya vikorokoro vingine kibao akijfanya naye ni mjuvi wa kuandaa kifungua kinywa akishindana na Lisa. Mwisho wa siku vyakula vyake vyote vikakosa ladha mdomoni na kubaki akimezea mate makaangizo ya Lisa! Mwanamke ni mwanamke tu bana, lakini jeuri ya Alvin haikumruhusu kukiri hilo.

Sandwichi kinywani mwake ilikosa ladha ghafla alipofikiria kababu za rangi ya dhahabu zilizotengenezwa na Lisa zilizotoa harufu tamu ya kuvutia. Akiwa amechanganyikiwa, alifunika upande mmoja wa slesi ya mkate na safu nene ya jamu ya matunda.

Hapo hapo, Lisa akatokea tena kutoka jikoni na kuweka mlo kamili mbele ya macho yake. Kababu, chapati za kumimina za mayai na viungo, pancakes, kikombe cha chokoleti moto, na kadhalika. Alvin aligeuza paji la uso wake kukwepesha asione vyakula vile vya kuvutia alivyotengeneza Lisa.

"Alvlisa, naamini hautoujali mimi nikikaa hapa na kula, sivyo?" Lisa alimwambia kichokozi.

Alvin alimtazama kimya wakati akianza onyesho lake la misosi. Lisa sasa alikuwa akimwigizia Alvin kichokozi na uigizaji wake ulikuwa bora kuliko alivyotarajia.

“Naomba unisamehe, lakini kwa kweli siwezi kuvumilia kuanza siku yangu na viporo vya kuchemsha na maziwa ya kupasha. Vitaninyong’onyesha utumbo na kunilegeza mwili." Lisa alimkejeli Alvin kisanii. Kisha, alichukua chapati ya kumimina yenye viungo vya kunukia akaikunja na kumega kipande mdomoni. Alifumba macho kusikilizia utamu wake huku akionekana kuridhishwa na radha yake usoni mwake. "Ladha murua kabisa. Mmmh, ni kitamu sana.”

Alvin akabaki kimya lakini moyo ulikuwa ukimkereketa kwa tamaa. Uigizaji wa Lisa ulimteka sana hata akajikuta anatamani ampokonye kipande kile cha chapati. Angewezaje kuendelea kula sandwich zilizokosa ladha kutokana na kukaa siku nyingi kwenye friji, wakati kuna madikodiko yakinukia na kumtoa udenda?

“Ni lazima kufurahia chapati moto na siagi ya hali ya juu. Kisha, kunywa chokoleti ya moto ili kuchangamsha mwili…" Lisa aliendelea na show yake ya misosi. Alikuwa akionja kila kipande cha chakula kwa bidii. Kwa kuzingatia sura yake nzuri pia, uigizaji wake ulikuwa wa kuburudisha na kusadikisha zaidi kuliko vipindi vingine vya mapishi alivyowahi kuona kwenye televisheni. Alvin hakuweza kuvumilia zaidi.

"Mieww!" Wakati huo huo, Charlie aliruka juu ya meza ya chakula huku akilia kwa tamaa na kutingisha mkia wake. Akifikiri paka lazima awe na njaa, Alvin akatembea hadi kwenye kabati. Alirudi na sahani ya chakula cha paka na kuiweka mbele ya Charlie.

Charlie alinusanusa tu chakula kile kwa sekunde chache kabla ya kugeuza kichwa chake. Macho ya huruma ya paka yule yalimtazama Lisa kwa tamaa kubwa.
Uso wa Alvin ulibadilika na kuwa mbaya kwa hasira lakini hakuongea kitu.

Lisa alizuia hamu ya kucheka iliyomkumba ghafla kabla ya kumrushia paka kipande kidogo cha chapati ya kumimina yenye mayai ndani yake. Paka mdogo alikishambulia kipande kile ndani ya sekunde chache tu.

"Paka mzuri." Lisa alimpigapiga paka kichwani kwa upendo. 'Una tabiaa nzuri zaidi kuliko mmiliki wako,' alijiwazia lakini hakuthubutu kuyatamka maneno hayo hadharani.

Alvin aliona aibu. Baada ya paka kula vipande viwili zaidi vya chapati, aliendelea kufurahia kababu. Hii ilimfanya Alvin ajikute anakenua mdomo kwa midadi. Lisa alipochukua fursa hiyo kumchomekea kipande cha kababu kinywani mwake.

“Wewe...” Alvin alishtuka na alama ya hasira iliangaza machoni pake.

Alvin alitaka kuitemea, lakini ile kababu iliyokuwa imepakwa asali ya mdalasini iliyeyuka kwenye ulimi wake. Bila kupenda, alijikuta anaanza kutafuna kipande kile kitamu. Kwa nje ilikuwa ngumungumu lakini kwa ndani ilikuwa laini. Ilikuwa na ladha tamu sana.

Hakika, aliwahi kula kababu hapo awali. Wapishi kutoka familia ya Kimaro wangeweza kutengeneza aina nyingi za vitafunwa, lakini hakuna kilichokuwa na ladha nzuri kama ile kababu ya Lisa. Kwa sababu fasizoweza kufahamu, Alvin akajikuta anavutiwa sana na kitafunwa kile.

“Ni nzuri?” Lisa aliuliza huku akishika kidevu chake kwa mikono miwili. Alijiamini katika upishi wake. Nuru ilimtoka machoni mwake alipoona tabasamu la kuridhika usoni mwa Alvin.

“Ni za kawaida tu.” Alvin alijibu kwa sauti ya wivu.

Kisha, Lisa akachukua kipande kingine cha Kabab na kuendelea kumlisha. Kipande kidogo kutoka awali hakikutosha kwake kuonja ladha yake kamili vizuri. Lisa allikonyeza macho kwa kucheza alipoona Alvin ameanza kushambulia zile kababu kwa fujo.

"Si ulisema siyo nzuri?"

“Sasa wewe unaweza kumaliza haya yote peke yako? Sipendi kuharibu chakula!” Alvin alijibu kwa kisingizio huku akiendelea kuzishambulia kwa pupa.

Lisa alitaka kufungua mdomo na kuongea kitu, lakini Alvin alihisi kuwa anataka kumsema yeye, aliwahi kumkatiza kwa kukunja uso, “Nyamaza, sipendi uongee wakati wa chakula.”

Lisa aliguna kwa mshangao huku akizuia kicheko ndani yake. Hakuwahi kuona mtu asiye na haya kama Alvin. Alikuwa amesema kwa upole kwamba hapendi kula vyakula vitamu kwa kiamsha kinywa, lakini sasa alikuwa akila kila kitu alichoandaa; kababu, chapati za kumimina—chokoleti ya moto pia. Hapo awali, Alvin alitaka tu kuonja chakula kidogo, lakini kila kitu alichotengeneza Lisa kilikuwa kitamu sana. Kilikuwa bora zaidi kuliko kile alichojaribu kwenye migahawa.

Hakika ilikuwa nje ya matarajio yake kwamba mwanamke huyu angeweza kuandaa kifungua kinywa kizuri kama hicho. Mawazo ya Alvin kwa Lisa yalibadilika kidogo baada ya kifungua kinywa kile. Kwa bahati mbaya, alielekeza uso wake kwake na macho yao yakagongana.

“Alvilisa, unataka kula nini kwa chakula cha jioni? Nitakutengenezea chochote utakachosema. ”Lisa alisema kwa upole.

"Nina miadi sehemu ya chakula cha jioni leo." Alijibu Alvin kwa sauti ya jeuri kama kawaida yake. Kisha aliondoka kwenda kubadilisha nguo chumbani bila neno lingine. Hili halikumkera Lisa. Ilikuwa kawaida kwa bosi yoyote, achilia mbali bosi wa biashara za kimataifa kama yeye, kuwa busy na kazi. Hata hivyo, bado ilikuwa muhimu kudumisha uhusiano mzuri kati yao. Alisafisha meza mara moja na kutoka haraka kwenda kubadilisha nguo za kazi pia.

Alvin alipokaribia kuondoka pale nyumbani, harakaharaka Lisa naye akatokea chumbani kwake akiwa na mkoba wake.

“Alvlisa, unaweza kunipa lifti? Naenda kazini pia. Ikiwa ni shida sana, unaweza kuniacha kwenye kituo cha daladala. Tafadhali.” Lisa alimwomba Alvin kwa nidhamu. Siyo kwamba hakuwa na uwezo wa kuendesha gari, gari alikuwa nalo sema tu alitaka kujibebisha. Si unajua tena?

Alvin akaminya midomo yake huku akiwaza kumkatalia. Hata hivyo, hatimaye alitikisa kichwa kwa kuzingatia kwamba alikuwa amefurahia sana kifungua kinywa alichokiandaa siku hiyo. Wawili hao walichukua hatua zao hadi sehemu ya maegesho.

Lisa alifikiri angeingia kwenye gari aina ya Bentley Molsane, Maybach, V8 au hata Range Rover basi! Lakini mwanamume huyo aliposimama kando ya gari nyeusi aina ya Harrier, Lisa akashtuka!

“Um… Je, hili ni ndo gari lako?” Lisa aliuliza.

"Ndio." Alijibu Alvin wakati akifungua mlango na kukaa kwenye kiti cha dereva.
Akiwa amechanganyikiwa kidogo, Lisa akafuata mfano na kuingia ndani ya gari.

"Alvlisa, kwa nini umechagua gari hili?" Alimwuliza swali hilo kwa sababu Alvin alipaswa kuwa mkurugenzi wa biashara ya kimataifa, lakini alikuwa akiendesha gari ambalo lilikuwa na thamani ya chini ya shilingi milioni 30 tu?

“Ni nafuu na haitumii mafuta kwa wingi,” Alvin alijibu kitupi tu huku akiwasha gari.

"Unajua njia bora ya kuishi, mume wangu wa kipekee." Lisa alipotezea mawazo yake kwa kujifanya anamuunga mkono. Lisa bado aliendelea na upekuzi wake ndani ya gari. Aligeuza kichwa chake kando akakuta kuna pakiti ya tishu za bei nafuu kwenye dashibodi.

Maelezo yake yalisomeka ' Kituo cha Mafuta—nafuu zaidi na rahisi zaidi.' Lisa alichanganyikiwa. Mjomba wa Ethan alikuwa tajiri mkubwa kwanini aliishi maisha ya kibahili namna hiyo? Inawezekana kwamba hakuwa tajiri kama ilivyokuwa inasemwa na watu, ama alikuwa kajichomeka kwa mtu mwingine tofauti? Lisa aliingia katika mawazo mazito huku akitafakari juu ya Alvin.

Dakika kumi baadaye, gari lilisimama karibu na kituo cha daladala. Alvin akageuka kumtazama Lisa na kumwambia. “Telemka wewe.” Lisa akaguna tu kwa kukosa la kusema. Hata hivyo alilshukuru kwa uungwana na kufanya kama alivyoambiwa.

“Naam, vizuri.” Alvin akamwambia wakati anashuka.

Huku akivumilia hasira iliyopanda ndani yake, Lisa alilazimisha tabasamu la aibu usoni mwake na kushukuru. "Asante, Alvlisa."

Mara tu Lisa alipotoka ndani ya gari, Alvin aliondoka kwa kasi kabla hajasema jambo lingine.

SURA YA 8

Lisa alifika kwenye ofisi za kampuni yao, ‘Kibo Group’ mwendo wa saa tatu subuhi. Tangu arejee kutoka masomoni nje ya nchi, alikuwa akifanya kazi katika kampuni yao hiyo ya mambo ya ujenzi. Ilikuwa kampuni kubwa ya familia ya Jones Masawe. Hata hivyo, mara tu alipoingia ndani ya jengo hilo, meneja wa mradi wa ujenzi wa hoteli aliyokuwa akishughulika nayo, James Komba, alimwambia kwa sauti ya ajabu iliyojaa umbea, “si lazima uje kazini kuanzia leo. Mradi huu wa hoteli ya Lublin si wako tena.”

"Unamaanisha nini?" Lisa aliuliza kwa mshangao baada ya kusikia mabadiliko hayo ya ghafla.

James alisita kidogo kumjibu Lisa baada ya kumwona mtu nyuma yake. “Lina, uko hapa.”

Lisa alizungusha kichwa chake na kumuona Lina akikaribia uelekeo wao akiwa amevalia nguo ya juu nyeupe na suruali ya jeans. Kulia kwake alikuwa Ethan ambaye alikuwa amevalia shati la rangi moja na suruali ya jeans pia. Mikono yao iliunganishwa pamoja. Mwangaza wa jua ulioingia ndani ya chumba hicho kupitia dirishani uliwafunika wawili hao. Walionekana kama wanandoa wenye furaha katika mavazi yao yanayofanana.

Kwa kushuhudia hayo kwa macho yake, Lisa alihisi kana kwamba kuna mtu amempiga ngumi nzito kfuani mwake. Maumivu makali yalikuwa yanamwelemea, hasa pale macho ya Ethan ya kejeli yalipompita huku yakimwangalia kwa dharau.

James akakimbia kuelekea kwa Lina huku akisema, "makao makuu imetoa agizo la kukabidhi mradi wa hotel ya Lublin kwa Lina."

Kitu kama shoti ya umeme kilimpitia Lisa kabla hajamgeukia Lina.

"Lisa , usifadhaike." Lina alijikongoja nyuma kana kwamba ameshtuka sana. Kwa bahati nzuri, Ethan aliweka mkono wake kwenye sehemu ndogo ya mgongo wake. Tukio hili lilichochea moto wa maumivu kwa Lisa.

“Lina, unataka nini tena? Tayari umemchukua mtu wangu na sasa unajaribu kunyakua mradi ambao nimetumia muda mwingi na bidii kuujenga. Unahusudu sana kila kitu nilicho nacho?" Lisa alilalamika.

“Ujinga ulioje! Tangu lini Ethan akawa mtu wako?" James alidhihaki. “Wewe si kitu kabisa. Umekuwa ukimsumbua Ethan hapo awali, lakini hajaonyesha kuvutiwa nawe hata kidogo. Mbali na hilo, unafikiri ungeweza kupata mradi wa hoteli hii kama Ethani asingekuwa na uhusiano fulani na familia ya Clark?”

"James, inatosha." Lina alimpa ishara ya kunyamaza mtu huyo.

“Nasisitiza. Wewe ni mchumba wa Ethan, kwa hivyo ni sawa kuchukua mradi huo.” James alikazia hoja yake.

“Na wewe unaunga mkono pia?” Lisa alimkazia macho Ethan ambaye muda wote huo alikuwa amenyamaza. Kwa hakika, Ethan ndiye aliyefanya mchongo ili kumkutanisha Lisa na bosi wa mradi huo anayejulikana kama Clark Zongo.

Lakini, Ethan hakuwa karibu sana na Clark. Ni Lisa ambaye alichukua muda mwingi wa kukutana na Clark kwa mwezi mzima ili waweze kujadili mipango ya mradi huo mara kwa mara kabla ya kukamilisha masharti.

Ethan alikunja uso kidogo. " Clark alikubali kukutana nawe kwa sababu yangu."

James alidhihaki, "Kila mtu anajua hili, lakini yeye anasisitiza tu ili kujidhalilisha."

“Siamini hili. Naenda kwa Baba.” Lisa aliendesha gari hadi kampuni kuu kumtafuta Jones Masawe.

“Baba, kwa nini ulimkabidhi Lina mradi wa hoteli ya Lublin? Unajua kwamba nimetumia bidii nyingi katika mradi huu mahususi.” Lisa alisikitika mbele ya baba yake.

Jones Masawe, ambaye alikuwa katikati ya kazi muhimu, alichukizwa na Lisa aliyeingia ghafla. “Nitakugawia mradi mwingine. Vipi kuhusu mradi wa ukumbi wa burudani wa Bwana Maige? Na wenyewe ni mzuri pia."

“Mradi huu mdogo unafaa zaidi kwa Lina. Yeye hana uzoefu katika tasnia hii, kwa hivyo ni bora ikiwa ataanza kutoka chini…” Lisa alimwambia baba yake.

Masawe aligonga kiganja chake kwenye meza kuonyesha msisitizo. “Ni dada yako mkubwa na unapaswa kumuonyesha heshima. Si ajabu mama yako amekuwa akisema unatoka nje ya mstari.”

Lisa alishtuka. Sauti yake ilijaa malalamiko alipozungumza baadaye. “Aliiba mchumba wangu na sasa anaiba mradi wangu pia. Ninawezaje kuonyesha heshima yangu kwa mwanamke huyo?”

“Hakuiba mradi wako kwani kila mradi ni wa kampuni ya Kibo. Mimi ndiye mkurugenzi wa kampuni, na ninaweza kukabidhi mradi wowote kwa mtu yeyote kama ninavyotaka. Isitoshe, Ethan hakuwa wako kamwe. Alimchagua dada yako mkubwa yeye mwenyewe kwa upendo wake.” Masawe alimkandamiza Lisa bila huruma.

Maneno yakamtoka Lisa kabla hajajizuia. "Ethan hangemchagua Lina kama usingengawia asilimia 80 ya hisa za kampuni."

“Dada yako amepatwa na maumivu yasiyofikirika kwa miaka yote. Mpe msaada wako kila unapoweza. Pia, muombe msamaha kwa yaliyotokea jana,” Mzee Masawe alihimiza.

“Siwezi kufanya hivyo,” Lisa alijibu kwa kusisitza.

Mzee Msawe aligonga meza kwa mara nyingine. “Ondoka kama huwezi kufanya hivyo, Paka usiye na shukrani wewe. Wewe si kitu bila familia ya Masawe na kampuni ya Kibo Group!”

Maneno yake ya hasira yalimpiga Lisa usoni kama upepo mkali. Mashavu yake yakatuna kwa hasira isiyomithilika. Kwa uchungu Lisa akasema, “sawa, nitaondoka. Siamini kwamba mbunifu aliyehitimu kwa kiwango cha juu kama mimi aliye na cheti cha injinia mbunifu wa daraja la kwanza atakosa kupata kazi mahali pengine.”

Lisa alirudi ofisini kwake baada ya hapo. Akiwa na moyo uliojaa manung'uniko na hasira, alipakia vitu vyake kwenye sanduku la kadibodi kabla ya kuelekea mlangoni. Watu wengi walimsengenya alipokuwa akipita.

"Nilisikia alifukuzwa kazi na bosi Masawe kwa sababu alikuwa mkaidi dhidi ya dada yake!"

"Nasikia haziivi na dada yake. Inasemekana kuwa Lina alitekwa nyara akiwa mdogo na ni hivi majuzi tu ndipo walipokutana tena baada ya miaka mingi. Lazima alipatwa na maumivu yasiyoweza kuelezeka katika miaka hiyo.”

“Hakika! Kando na hilo, Lina sio mzuri tu bali ni mkarimu pia. Hata alitununulia chakula cha jioni kwa ajili ya kufanya kazi ya ziada jana usiku. Lakini huyu Lisa ni mjeuri kama nini…”

"Mwanamke huyu anapata anachostahili!"

Lisa alilazimisha tabasamu la kujidharau. Tangu ajiunge na kampuni hiyo, hata mara moja hakuwahi kujivunia cheo. Siku zote alifanya kazi kwa tahadhari na uangalifu mwingi. Angekuwa wa kwanza kuingia na wa mwisho kuondoka ofisini kila siku, akifanya kazi ya ziada na kuwatendea wengine kwa heshima nyakati zote. Hakutarajia kwamba mambo yangefikia hatua ile.

Baada ya kuondoka kwenye kampuni hiyo, alizungukazunguka peke yake bila lengo maalum. Wakati huo, Ethan alimpigia simu mara kadhaa lakini Lisa alikataa kujibu simu zake. Mwishowe aliamua kurudi nyumbani kwa Alvin, Oyster Bay, baada ya kununua vyakula kadhaa na viungo kutoka super market.....ITAENDELEA.......

Mh....Lisa anapitia wakati mgumu sana yaani wazazi wake wa kumzaa kama sio wake, basi kwa leo naomba tuishie hapa tusubiri sehemu zinazofuata ambazo ni 9&10 ili kujua nini kitaendelea kwenye mkasa huu wa kusisimua unaokwenda kwa jina la LISA..

Kusoma simulizi hii kitabu cha kwanza mpaka mwisho gharama ni 2000, lipia sasa kisha unicheki whatsapp utumiwe simulizi yako haraka.

Namba za kulipia

0628924768 (Halotel) JUMA HEMBA
0694288555 (Airtel) JUMA HEMBA
0764736557 (Voda) HADIJA KIRUNGI

Ukilipa njoo whatsapp kwa namba 0628924768

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
JINA LA SIMULIZI...........................LISA
SPONSORED BY.....SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP........................0628924768
SEHEMU YA...................................9&10

SURA YA 9

Ndani ya nyumba ya Alvin, Charlie alijitokeza mbele kumsalimia huku akitingisha mkia wake hewani. Alimpigapiga paka kichwani mwake kwa upendo na kunung'unika, "Charlie, ni wewe pekee uliyesalia ambaye unanipenda sasa."

"Meow," paka akajibu huku akifumba macho kwa kuridhika, akimpa Lisa ruhusa kamili ya kumchezea.

Lisa alitabasamu kwa uchungu wakati anaongea na paka yule aliyempenda. “Nadhani unataka vitafunio vya samaki waliokaushwa, sivyo? nitakuletea kidogo.”

Alvin hakuwepo nyumbani mchana huo. Lisa na paka wake walifurahia chakula cha mchana kwa kujiachia. Kisha, akajitupa kwenye kochi na kuanza kutafuta kazi mtandaoni kwa kutumia kompyuta yake ndogo.

Saa nne usiku, Alvin alirudi nyumbani kwake na kupokelewa sebuleni kukiwa na mwanga mkali. Juu ya kochi, Lisa alikuwa katikati ya kumlisha Charlie kipande kidogo cha chips.

“Hii ndiyo aina ya takataka unayomlisha paka wangu wakati sipo nyumbani?"
Macho ya Alvin ya kupendeza yalichanganua meza iliyojaa vitafunio kwa jeuri. Kulikuwa na mifuko ya chipsi, viungo, jibini, biskuti za chokoleti na takataka nyingine kibao ambazo Lisa alitoka kununua super market mchana ule. Fundo dogo la chokoleti lililoonekana kwenye visharubu vya Charlie, likawa chanzo cha Alvin kufoka mfululizo.

"Nilimlisha Charlie kiduchu tu, yaani kidogo kweli." Lisa alionyesha kwa kidole gumba na cha shahada, akionyesha jinsi kilivyokuwa kidogo. “Charlie aliendelea kunisumbua ili nimpe kiasi, kwa hivyo sikuwa na la kufanya ila—”

“Paka anajua nini? Ina maana wewe unafuatisha akili za paka?” Akiwa amekasirika, Alvin alifagia kila kitu kilichokuwa mezani na kuvimwaga kwenye pipa la takataka. “Usilete tena takataka kama hizi nyumbani kwangu. Sipendi hata kusikia harufu yake tu.”

Lisa alitazama vitafunio ndani ya pipa la takataka kwa masikitiko. Ee Mungu, hakuweza kujuwa Alvin alikuwa anachukizwa na hivyo vitu tu au alikuwa na lake moyoni! Lakini, alipokumbuka kwamba hapaswi kumchukiza Alvin ili lengo lake litimie, Lisa alijilazimisha kugeuza midomo yake iliyojikunja kwa hasira na kuwa tabasamu la kupendeza. “Umesema kweli, Alvlisa. Hizi ni takataka. Sitarudia tena kuleta vitu kama hivi humu ndani.”

"Jiangalie kwenye kioo na uone jinsi unavyofanana." Alvin hakutaka kusumbuliwa. Akamnyanyua yule paka na kuelekea chumbani kwake.

“Alvlisa, ulikuwa na siku ndefu, hivyo utakuwa na njaa. Nikuandalie chakula? Ninatengeneza pasta tamu sana.” Lisa alimfuata bila aibu kwa hatua ndogo.

Maneno ya Lisa yakamtuliza Alvin. Chakula kilichotolewa katika mgahawa alioenda hapo awali kwa ajili ya mkutano wa kibiashara kilikuwa kimechujuka ladha sana hivi kwamba alikula kwa shida. Tumbo lake lilinung'unika kidogo baada ya kusikia pendekezo lake.

Lisa alichukulia kusita kidogo kwa Alvin kama ishara ya kukubali hivyo akajipa ruhusa mara moja, akisema, “Nitapika tambi tamu sana sasa hivi. Nenda ukaoge."

Alvin akageuka na kumtupia jicho la haraka. Mwanga laini wa rangi ya chungwa ukimumulika kutoka juu ulimfanya aonekane mrembo na mwenye mvuto kuliko kawaida.

Dakika 15 baadaye, Lisa alifika kwenye mlango wa chumba cha kulala cha Alvin akiwa ameshikilia bakuli la tambi. Aligonga mlango, lakini hakujibiwa. Akiwa hana njia nyingine, alifungua mlango kidogo na kumwambia, "Alvlisa, chakula kiko tayari."

Hakukuwa na mtu chumbani. Muhtasari hafifu wa kivuli cha mtu kiliweza kuonekana kwenye mlango wa kioo kizito cha bafuni. Akiwa ameduwaa na macho hayo, hakuweza kujizuia kuwaza jinsi mwanaume huyo angeonekana bila nguo. Alijikuta akisisimka sana wakati akiunda wazo hilo akilini mwake.

“Aaah! Bullshit, hivi nilikuwa nawaza nini?” Lisa alijizindua mwenyewe kutoka kwenye njozi zake.

Alipotaka kugeuka na kuondoka, mlango wa kioo ulioganda ukasukumwa. Alvin akatoka ndani, akiwa hajavaa nguo. Hata hivyo kulikuwa na taulo ambalo lilikuwa limefungwa kuanzia kiunoni mwake kwenda chini. Nywele zake, ambazo bado zilikuwa na unyevunyevu kutokana na kuoga, zilitoa matone ya maji yaliyotiririkia kwenye taya yake hadi kwenye kifua chake kilichotuna na kustawisha vinyweleo vya kutosha. Macho yake yalisogea chini taratibu, yakifuata mwendo wa matone ya maji. Akashtuka. Lisa alijua kwamba Alvin alikuwa na sura nzuri, lakini hakutarajia na mwili wake ungekuwa mzuri zaidi ya sura yake. Alikuwa na ngozi nzuri ya rangi ya ngano, bila kusahau misuli iliyoboreshwa iliyounda mwili wake. Mwanamume huyo hakuwa na misuli kupita kiasi kama mjenzi wa mwili, lakini kila sehemu ya mwili wake ilifafanuliwa. Mwili uliofaa ulitoa haiba ya kiume ambayo mtu mzima tu alikuwa nayo. Akashusha macho yake zaidi na kuona kiuno chake kikiwa kimefungwa vizuri kwa taulo...

“Umeona vya kutosha?” Ghafla sauti ya Alvin ilisikika masikioni mwake na kumshtua Lisa. Lisa alijikusanya papo hapo. Alihisi joto likiwaka kwenye mashavu yake.

“Mimi… niko hapa kukuletea chakula chako. Fanya haraka kula au tambi zitapoa na kugandamana muda si mrefu." Lisa alijitetea kinyonge. Alikuwa kishabebwa na hisia dhaifu baada ya kumtazama Alvin katika mazingira yale.

Aliweka bakuli la tambi mara moja. Wakati anatoka tu chumbani, alitembea kwenye ukingo wa zulia na kujikwaa. Alikosa usawa wake na kujikuta anaanguka kwa mbele. Katika muda wa sekunde hizo chache, alifikiri alikuwa ameshika kitu lakini bado akaanguka kifudifudi chini. Kwa bahati nzuri, alitua kwenye zulia la manyoya kwa hivyo haukuumia. Alipofumbua tena macho yake, kitu cha kwanza kilichomwingia machoni mwake kilikuwa ni miguu mirefu ya Alvin na…

"Ah, kwa nini umenivuta taulo langu?!" Alvin alimuuliza kwa sauti kali.

Lisa alipigwa na bumbuwazi kabisa kwani ilikuwa ni mara ya kwanza kukutana na hali ya aina hiyo. Alinyoosha mkono kuyafunika macho yake na hapo ndipo akagundua taulo jeupe lilikuwa mkononi mwake.

‘Nilivuta taulo kwa bahati mbaya, au kilitokea nini?’ Lisa alijiuliza.
Kumbe taulo limetoka?" Lisa akashangaa.

"Sijawahi kuona mwanamke asiye na aibu kama wewe!" Sauti ya Alvin yenye kila sifa ya ujeuri ilipita kwenye masikio yake kama barafu baridi.

Lisa alijisikia kulia, lakini machozi hayakumtoka, akaishia kujitetea tu kwa wogawoga. “Sikupanga kufanya hivyo. Nilijikwaa kwenye zulia kwa bahati mbaya.”

"Nimekuwa nikitembea kwenye zulia hili kila siku lakini sijawahi kujikwaa hapo awali hata mara moja. Huwezi kunishawishi kwa kisingizio hiki cha kipuuzi.” Alvin hakumwamini hata kidogo.

Lisa akatumbua macho. Hali ilikuwa ngumu kurekebishwa sasa, kwa hivyo alijibu bila hatia, "Labda baada ya kuona mwili wako mzuri na mkamilifu kabisa kama wa malaika, akili yangu ilififia na nikapoteza uwezo wangu wa kuzingatia ..."

“Kwa hiyo sasa unapeleka lawama kwangu?” Alvin alidhihaki kwa hasira. Alikuwa amekutana na wanawake wengi maishani mwake, lakini hakuna hata mmoja aliyekuwa shupavu na mjanja kama Lisa.

“Hapana, hata kidogo. Ni kosa langu, kwa kweli, kwa sababu sijawahi kabisa kuona…” Lisa alijiumauma.

“Bado unataka kutazama?” Alvin alimkatisha kwa sauti iliyoongezeka ukali maradufu.

“Ha..Hapana…” Lisa alijing’atang’ata na kushindwa kuongea.

Toka nje.” Alvin hakuweza kuvumilia kuendelea kumwona tena pale. Alihisi damu ikichemka kwenye mishipa yake akajitahidi sana kujizuia kumpiga teke la uso.

“Ndiyo, bila shaka nitaondoka mara moja.” Lisa alinyanyuka haraka haraka na kuelekea mlangoni.

“Simama hapo hapo!” Sauti iliyochanganyika na hasira ilipiga kelele tena nyuma yake. Lisa akageuka tena kumwangalia. "Nipe taulo yangu." Akayashusha macho yake mkononi kwenye taulo alilokuwa amelishika. Aliona aibu sana hivi kwamba alitamani kungekuwa na shimo ambalo angeingia tu.

"Hili hapa." Aliweka uso wa ujasiri na kumsukumia lile taulo mikononi mwake. Hakuwa na la kusema alipotambua uelekeo aliokuwa akitazama. Ujasiri wa mwanamke huyo ulimshangaza zaidi Alvin.

“Slam!” Lisa alifunga mlango kwa nguvu huku akihema. Picha ya kile alichokiona kwa Alvin ilikataa kabisa kutoka kichwani mwake. Alisimama pale kwa muda akiwa kaegamia ukuta akihisi kama vile ametoka kuona onyesho la video la kupendeza kweli. Hata hivyo, baada ya tukio hilo, hakuthubutu tena kukaa sebuleni na kuamua kurudi chumbani kwake mara moja. Akili yake haikuonekana kuwa na uwezo wa kupona kutokana na mshangao huo.

Hakujua ni muda gani ulikuwa umepita pale Alvin alipogonga mlango ghafla. Lisa aliruka juu kwa hofu. Sekunde chache baadaye alijibu kwa unyonge, “tunaweza kuzungumza kuhusu hili kesho? Nina usingizi."

"Unalala na taa ikiwa inawaka?" Sauti nzito ya Alvin ilipenya kwenye pengo lililokuwa chini ya mlango. "Usinifanye nivunje mlango!"

Lisa alijikuna kichwa kwa kufadhaika kabla ya kufungua mlango.

“Nimekuambia habari ya taa tu, unafungua mlango wa nini?” Alvin alimwambia akiwa amesimama kando ya mlango huku amevalia nguo zake za kulalia za kijivu. Harufu ya kuvutia ya manukato aliyopaka kidevuni na kwenye mashavu baada ya kunyoa iliyafanya mandhari yaliyowazunguka kuwa ya kupendeza. Vifungo vyote vya shati lake vilifungwa, hata vile vya juu.

"Unaangalia nini?" Alvin alikasirika zaidi baada ya kuhisi macho yake.

Lisa hakujua uwepo wa Alvin pale ulimaanisha nini. Akamjibu.“Hakuna kitu.”

"Unajikuta mjanja kuliko mtu mwingine yeyote." Alvin aliongea lakini alionekana hakuna la maana lililompeleka pale. Mwanzoni alikuwa akilalamika kuhusu taa, baada ya kufunguliwa mlango akazua hoja nyingine. Alvin akainamisha kichwa kumtazama Lisa kuanzia chini mpaka juu. Kutoka pembe aliyokuwa amesimamai, shingo yake ilionekana nyembamba na ndefu. Labda ilikuwa ni mwanga au sababu nyingine, lakini uso wake ulionekana kuwa na rangi ya kupendeza ya machweo ya jua. Macho yake yalisogea hadi kwenye mstari wa shingo ya pajama zake za pamba. Mara moja, macho yake yalimkazia kwenye kifua kilichokuwa kimetuna kiasi, dodo zake zikiwa zimesimama kama mishale inayolenga moja kwa moja kwenye moyo wa Alvin.

"Naam, na wewe unatazama nini?" Lisa alimuuliza swali lile lile. Macho ya kuchoma ya Alvin yalikuwa ya kutisha sana hivi kwamba Lisa alijikuta akibabaika. Alitupa macho yake chini na mara moja akatumia mikono yake kufunika kifua chake kwa haya.

Alvin alimdhihaki. “Najaribu kuona utanitega vipi.”

“Sina haja ya kukutega, wewe ni mume wangu hata hivyo.” Lisa alijikanyaga. Uso wake usio na vipodozi ulionekana kuwa mzuri kiasili.

Alvin akaondoa macho yake kifuani, na bila kujali mara moja akarudi kwenye sifa za uso wake mzuri. "Naweza kukupa pesa za kukodisha mahali pengine? Haifai sisi kuishi katika nyumba moja.” Alikuwa akimfuku.
isa aliingiwa na woga baada ya kusikia hivyo. “Haifai vipi? Tumefunga ndoa kihalali.”

Tabasamu la kejeli lilienea usoni mwa Alvin. "Nadhani unajua masharti ya ndoa hii."

Aliposikia hivyo, alijaribu kuweka tabasamu lake la kuvutia huku akijaribu kuonekana mwenye haya kwa wakati mmoja. “Si ni kwa sababu mimi ndiye nilikuanza? Tangu wakati huo, moyo wangu mchanga umeunganishwa sana na wewe.” Alvin akaguna bila kusema chochote. Lazima alirogwa usiku ule.

Lisa akatumia nafasi hiyo kuendelea kusema, "Nimekuelewa sasa. Bado una wazimu kuhusu tukio hilo la mapema. Najua unahisi kana kwamba nilikufanyia kusudi na ni kawaida kufikiria hivyo.” Aliuma mdomo wake wa waridi, akionekana kama anajaribu kufanya uamuzi. “Naam… Vipi kuhusu mimi kukuonyesha nilicho nacho pia, ili umalize hasira yako?” Kisha, alinyoosha mkono kutendua kitufe cha juu cha night dress yake.

Alvin alishindwa kupumua kwa sekunde kadhaa kabla ya kugeuka na kuufunga mlango kwa nguvu, bila kusubiri kuona kile ambacho Lisa alikusudia kumwonyesha.

Lisa alishusha pumzi ya ahueni huku akizitazama kola zake. Aliona ni jambo la kuchekesha kwamba Alvin alikuwa ameondoka kabla hajamuonyesha chochote. Licha ya hasira yake mbaya, bado alikuwa muungwana mwenye heshima. Ilikuwa nadra sana kukutana na mtu kama huyo, licha ya kuishi naye nyumba moja.

SURA YA10

Usiku wa manane. Lisa aliamshwa na kelele za paka aliyekuwa akihema bila kukoma. Alishuka kitandani na kuwasha taa. Charlie alikuwa amelala chini ya meza, akijtupa kwa udhaifu. "Charlie." Lisa alishtuka na kumwita, akanyoosha mkono kumchukua yule paka, lakini sauti kali na nzito ya Alvin ilisikika nyuma yake.

"Pisha njiani." Mikono ya Alvin iliganda hewani. Akasogea mbele kumnyanyua yule paka. “Ni nini kilimtokea?” Alivin akauliza kwa sauti isiyo ya kawaida. Lisa alijihisi amepotea na kukosa cha kusema kuona paka huyo mzuri akiteseka.

"Nini unadhani; unafikiria nini?" Alvin alimtazama kwa hasira machoni pake. “Yeye ni paka tu lakini umekuwa ukimlisha takataka za kila aina. Unafikiri tumbo lake linaweza kumudu?”

Lisa alijisikia kujuta kabisa. Alikuwa ameona paka waliopotea wakila karibu kila kitu walichoweza kupata mitaani. Hakuwahi kufikiri kuwa paka nao wnaweza kuvimbiwa na vyakula. "Samahani." Lisa alimwangukia Alvin kumtaka radhi.

"Sitakuacha salama endapo jambo baya likimtokea Charlie!" Alvin aliwaka, akamtazama kwa macho mabaya kwa muda mrefu kabla ya kuinuka na kushika funguo za gari. Kisha akatoka nje ya nyumba haraka huku akiwa amemkumbatia Charlie wake.

Lisa akamfuata Alvin haraka. “Naifahamu hospitali nzuri ya mifugo inayofanya kazi masaa ishirini na nne. Ngoja nikuonyeshe njia,” Lisa alisema kwa wasiwasi lakini Alvin akaminya midomo yake kwa kejeli bila kumkubalia.

Walipofika kwenye egesho la gari, Lisa haraka akafungua mlango wa kiti cha abiria ili akae wakati mkono wenye nguvu ulipomvuta kwa nguvu kutoka nyuma ukisindikizwa na sauti kali, “nani kakuruhusu uingine humu?” Lisa, ambaye alikuwa amevaa slippers, alijikongoja nyuma. Akiwa amepoteza usawa wake, alianguka chali na kutua chini.

Alvin akasimama mbele ya gari. Alimtazama kwa dharau kali ambayo ilitoka kwa macho yake yenye giza. “Ondoka hapa mara moja. Sitamani kukuona hapa nitakaporudi nyumbani. Sitauliza tena kwa upole.” Kisha akambeba Charlie ndani ya gari. Harrier nyeusi ikaondoka kwa kasi nje ya geti na kupotea kwa muda mfupi.

Akiwa amebaki peke yake kwenye eneo lenye giza la kuegesha magari, macho ya Lisa yalibubujikwa na machozi huku akilitazama gari lile likiondoka. Machozi ambayo alikuwa akiyazuia siku nzima hatimaye yalimwagika usoni mwake kama bwawa lililofurika.

Kila mtu alikuwa anampa wakati mgumu. Hakuhisi kana kwamba alikuwa wa familia ya Masawe tena. Charlie ndiye pekee aliyebaki ambaye alikuwa mzuri kwake. Lakini naye hakuweza hata kubaki naye tena. Midomo yake ikabadilika na kuwa tabasamu la huzuni. Ghafla, taswira ya Charlie akijirusha mapema ikamjia akilini na akasikitika sana.

Lisa alijua kwamba Alvin hakupendezwa naye, lakini aliendelea kumsumbua hata hivyo ili kufikia lengo lake mwenyewe. Alipuuza kabisa utu wake. Je, hii ilistahili kweli? Hata akamuweka Charlie katika maumivu haya. Labda wakati wake wa kuondoka ulikuwa umefika. Alisimama na kurudi nyumbani kuchukua vitu vyake ili kuondoka.

Ilikuwa ni saa nane usiku, Lisa hakutaka kuvuruga usingizi wa rafiki yake Pamela, kwa hiyo aliendesha gari hadi kwenye hoteli ya nyota tano iliyokuwa karibu mara moja. Akaingia Masaki Ocean View Hotel. Katika chumba cha mapokezi, alichukua kadi yake ya benki na kumkabidhi mhudumu wa mapokezi. Ilirudishwa mikononi mwake sekunde chache baadaye. "Samahani kukufahamisha kuwa kadi hii haiwezi kutumika."

Alishtuka, akaipokea na kumpa mhudumu kadi nyingine. Hata hivyo, alishindwa kufanya malipo hayo hata baada ya majaribio kadhaa na kadi zake nyingine zote. Hatimaye ilimjia akilini kwamba kadi zake zote za benki zilikuwa zimefungwa, na nani? Masawe! Ingawa alikuwa amepata shilingi milioni kadhaa katika miaka michache iliyopita kutokana na kufanya kazi katika miradi kadhaa, alikuwa amekabidhi pesa hizo kwa mama yake bila kujibakiza. Kwa kawaida alitumia kadi za benki alizopewa na baba yake, Jones Masawe, kwa matumizi yake ya kila siku, lakini kadi hizo zote zilisimamishwa kwa wakati huo. Alichokuwa amebakisha ni kadi ya malipo ambayo haikuwa na zaidi ya shilingi milioni tano.

Mhudumu wa mapokezi akakosa subira. "Ikiwa huna uwezo wa kukaa katika hoteli yetu, kuna nyumba ya wageni iliyo umbali wa mita 300 baada ya kupinduka kupitia lango kuu."

"Hivi ndivyo unavyowatendea wateja wako?" Lisa alichukizwa.

“Mimi ni mkweli tu. Hupaswi kuja kwenye hoteli ya nyota tano ikiwa huna uwezo wa kumudu.”
Lisa alikuwa amekasirika sana mpaka kufikia muda huo. Hakutarajia mwenyewe, mwanamke kijana kutoka kaya tajiri ya Masawe kuwa siku moja angekabiliwa na unyonge kama ule.

“Naweza kumudu vyema.” Alijigamba. Alichukua kadi yake ya malipo lakini akaanza kusita. Chumba cha bei nafuu zaidi katika hoteli hiyo kilikuwa angalau shilingi laki tano kwa siku. Kwa kuzingatia hali yake ya kifedha kwa muda huo, asingeweza kujua ni lini angerudi kwa familia ya Masawe tena. Sasa alikuwa hana kazi na hana makazi. Angewezaje kuishi katika siku zijazo ikiwa angetumia kila kitu alichokuwa amebakisha?

“Sawa, acha kujifanya. Ondoka. Hapa si mahali unapofaa,” mhudumu wa mapokezi alisema kwa jeuri. Lisa alikimeza kiburi chake na kuondoka pale hotelini huku begi lake likiburuta nyuma yake.

Hoteli nyingi hazikuwa na vyumba vya ziada usiku ule. Alizunguka kwa muda kabla ya kuingia katika hoteli ya bajeti ambayo ilikuwa ikitoza karibu elfu ishirini kwa usiku.
Bila kujua, watembea usiku hawakosekani. Yaani unaweza kufanya jambo usiku ukidhani hakuna aliyekuona, lakini asubuhi ukashangaa kujikuta umeanikwa kwenye magazeti. Ndivyo ilivyokuwa kwa Lisa, hakutegemea kama kullikuwa kuna mtu akimpiga picha wakati akiingia kwenye hoteli hiyo ya bei nafuu na kuituma kwa ‘group la whatsapp’ la wanafunzi wenzake wa shule ya sekondari.....ITAENDELEA......

TUKUTANE KURASA 11-12 KUJUA NINI KITAENDELEA KWA BINTI MREMBO LISA AMBAE ANAPITIA WAKATI MGUMU SANA SI NYUMBANI KWAO HATA KWA MUME WAKE BANDIA ALVIN. LAKINI TUNASEMA HAKUNA LENYE MWANZO LIKAKOSA MWISHO SASA ACHA TUKAONE MWISHO WAKE.

Kusoma simulizi hii kitabu cha kwanza mpaka mwisho gharama ni 2000, lipia sasa kisha unicheki whatsapp utumiwe simulizi yako haraka.

Namba za kulipia

0628924768 (Halotel) JUMA HEMBA
0694288555 (Airtel) JUMA HEMBA
0764736557 (Voda) HADIJA KIRUNGI

Ukilipa njoo whatsapp kwa namba 0628924768

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
JINA LA SIMULIZI...........................LISA
SPONSORED BY.....SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP........................0628924868
SEHEMU YA..................................11&12

SURA YA11

Alvin, ambaye alikuwa amefika katika hospitali ya wanyama wa ndani, Pet Care House mtaa wa Kahama, Masaki Oyster Bay, alikaribishwa vizuri na daktari wa mifugo. Hospitali hiyo ilikuwa inafahudumia masaa ishirini na manne.

Aivin alikuwa na wasiwasi utadhani aliyempeleka pale hospitali ni mwanaye. Alikuwa akingoja mlangoni huku akiwa amebana midomo yake kwa nguvu. Mwanaume huyo alijawa na majuto huku akitafakari juu ya uamuzi wake wa kuoa mwanamke asiyemfahamu kwa chochote.

Dakika 15 baadaye, mlango wa chumba cha uchunguzi ulifunguliwa, akatoka Dr Lewis. Alvin akasogea mbele mara moja, uso wake wote ukiwa umesisimka. "Paka anaendeleaje?"

Dk Lewis alirekebisha miwani yake kabla ya kufunua tabasamu la kuonyesha matumaini. "Paka wako ana ujauzito wa wiki mbili." Alvin akaishia kuguna tu. Alikosa la kusema. “Hongera sana kwa nyongeza mpya katika familia yako." Dk Lewis akatabasamu.

Alvin alivuta pumzi kwa kasi huku akiizuia hamu yake kali ya kufoka. Wiki mbili?
Hiyo ilikuwa kabla ya kuhamia Dar. Baadhi ya paka dume bila shaka lazima walichukua fursa ya Charlie alipokuwa bado anaishi Nairobi. Bila shaka angemwadhibu mhusika ikiwa angefanikiwa kumpata.

“Um… Huonekani kufurahishwa na habari hizo. Je, tuuondoe?” Dk. Lewis, ambaye alikuwa mzoefu wa wanyama wadogo wa nyumbani, alikuwa amesitawisha hisia kali ya wanyama hao. "Ikiwa ni hivyo, tunaweza kufanya operesheni ya kuuondoa ujauzito wa paka, lakini ni ukatili. Nilimfanyia X-Ray mapema na ameonekana amebeba watoto watatu. Ni bahati nzuri…”

Kabla hajamalizia sentensi yake Alvin aliuliza kwa sauti nzito, "Paka hutapika kama binadamu anapokuwa mjamzito?"

“Inategemea hali ya kila paka,” daktari alieleza kwa utulivu huku akitabasamu, “baadhi ya watu ambao hawajui vizuri watafikiri paka ana matatizo ya tumbo au amelishwa chakula kibaya.”

Ndivyo alivyofikiria Alvin, hata akapelekea lawama kwa Lisa. Alionekana kukumbuka kumsukuma chini kabla hajaondoka. Kwa maneno mengine, alikuwa amemshtaki kimakosa. Akiwa amechanganyikiwa, alipigapiga kichwa chake akijilaumu kwa hasira. Alijiuliza yule mwanamke alikuwa anaendeleaje muda huo. Alikuwa ameondoka ama alikuwa bado yupo nyumbani kwake?

“Sawa, ninataka kujua zaidi njia bora ya kumhudumia paka wakati wa ujauzito.” Alvin alituliza akili yake na kumwambia yule daktari.

Kwa dakika kumi zilizofuata, daktari yule wa mifugo alielezea mchakato huo kwa undani na akampa mwongozo wa ujauzito wa paka mwishoni. "Paka mjamzito lazima aangaliwe katika ulaji wake wa lishe. Paka wako ni dhaifu sana, kwa hivyo kuharibika kwa mimba kunaweza kutokea kwa urahisi. Ni bora ukiajiri mtu wa kumtunza.”

Alvin alishindwa cha kusema. Ni nani angemhudumia paka wake nyumbani?
Kwa sababu fulani, ghafla alikumbushwa ujuzi wa kipekee wa Lisa wa kupika. Ikamjia kwamba huenda alikuwa mkorofi sana kwake. Kweli, labda angeacha kwanza kuleta mada ya kuondoka kwake nyumbani wakati atakaporudi baadaye.

Kurudi nyumbani, alifungua mlango na kuwasha taa. Kuna kitu alihisi hakiko vizuri. Mlango wa chumba cha wageni ulikuwa wazi na hakukuwa na mtu yeyote. Hakuweza kupata hata vazi moja la nguo za kike mle ndani. Lisa alikuwa ameondoka.

Ndita zilikunjamana usoni mwa Alvin. Charlie aliinama kwa uvivu mikononi mwake. Alitazama chumbani kabla ya kuinamisha kichwa chake kwa kukata tamaa. Alvin alichanganyikiwa lakini alifikiri kwamba kuondoka kwake kungeweza kuwa bora zaidi. Hata hivyo, hawakupaswa kujihusisha sana katika maisha ya kila mmoja wao. Angeweza kumlipa kwa fidia kubwa zaidi siku ya talaka yao. Kwa upande wa Charlie, vizuri, angeweza kuajiri yaya wakati wowote.

SURA YA12

Saa nne asubuhi Lisa aliamka kutoka kwenye kochi akijisikia mnyonge.
Baada ya kuangalia ndani ya chumba usiku kabla hajalala, aligundua kulikuwa na nywele nyingi kitandani. Shuka za kitanda zilionekana kuwa hazijafuliwa kwa muda mrefu. Chumba hakikuwa kisafi, hivyo aliishia kusinzia kwenye kochi badala yake. Pamela alipiga simu wakati anakaribia kwenda kuoga.

“Babe, si unaishi na mumeo? Uliishiaje kwenye hoteli ya bajeti ndogo?" Pamela aliuliza kwa mshangao.

Lisa akashangaa! “Umejuaje kuhusu hili?”

"Mambo yote yapo hadharani, Janet alikupiga picha na kutuma kwa group, kila mtu anazungumza juu yako kwenye group la whatsapp." Kulikuwa na ladha ya kuchanganyikiwa katika sauti yake. "Huyo msichana mbaya, Janet Kileo, hata alielezea maisha yako ya zamani. Aliwaambia group zima kwamba umefukuzwa kutoka kwa familia ya Masawe kwa sababu dada yako mkubwa amerudi. Wanafiki wale wote waliokuwa wakihusudu hadhi yako kama bosi lady sasa wanakudhihaki waziwazi.”

"Oh," Lisa alinong'ona.

Janet Kileo alikuwa binti kutoka katika kaya nyingine tajiri sana. Yeye na Lisa walisoma darasa moja katika shule ya sekondari. Lakini, Janet alikuwa akimwonea wivu Lisa kwa sura yake nzuri na mafanikio bora ya masomo, kwa hivyo hawakuwahi kuwa marafiki wa karibu zaidi. Kwa hiyo kila alipopata nafasi ya kumdhalilisha Lisa alifurahi sana na kuitumia ipasavyo.

Pamela aliuliza huku akihisi kukasirika. "Nini kinaendelea? Hujawahi kukanyaga hoteli yenye hadhi ya chini kama hiyo tangu uzaliwe.”

“Mambo yamebadilika Pamela. Baba yangu amesimamisha kadi zangu zote za benki na sina la kufanya juu yangu. Jana usiku, Alvin alinifukuza nyumbani kwake.”

“Kwa nini hukuja kwangu?”

"Ilikuwa usiku sana na sikutaka kukusumbua."

“Lisa , wewe ni mpumbavu sana. Niambie ulipo.”

Dakika 40 baadaye, Pamela alijitokeza kwenye nyumba hiyo ya kulala wageni akionekana kama alikuwa na haraka. Alimhurumia rafiki yake baada ya kuchungulia kwenye chumba kidogo na chenye mazingira duni. Kulikuwa na hata rundo la taka za kadi zilizopenyezwa kupitia mlangoni na makahaba waliokuwa wakitafuta biashara.

"Twende, tuondoke mahali hapa mara moja na ukakae kwangu." Pamela aliongea haraka.

“Hapana, wewe una mpenzi. Kwa kuongeza, sio wazo nzuri kwa muda mrefu. Nina mpango wa kukodisha mahali." Lisa akatikisa kichwa kukataa ofa hiyo nzuri.

Baada ya kuzingatia, Pamela alikubali. “Hilo si wazo mbaya. Ethan alikuja kwangu tena jana usiku akikutafuta. Anaudhi sana.”

Lisa alihisi koo lake likikaza kwa sauti ya jina hili. Kulikuwa na wakati ambapo Ethan angemuunga mkono kwa kila kitu. Hata hivyo, alivunjika moyo sana alipokumbuka yale aliyosema jana yake. "Yeye ndiye mtu wa mwisho ninayetamani kumuona sasa hivi."

“Mimi pia.” Pamela alitikisa kichwa, na kuongeza. “Kumbe wewe sasa umeolewa, lakini kwa nini Alvin alikufukuza nyumbani usiku wa manane?”

Lisa alilazimisha tabasamu la uchungu kabla ya kueleza kwa ufupi kilichotokea. Pamela alihisi huruma sana kwa rafiki yake. “Yule mtu ni mgonjwa. Wewe ni nusu yake nyingine kisheria. Sasa paka anakuwaje muhimu kwake kuliko wewe?"

"Hata miye nashangaa shoga yangu, ila ni ya kuacha tu!" Lisa alisema kwa unyonge sana.

Pamela alisita. “Um… Naam, ulikuwa uamuzi wako kuolewa naye hata hivyo.”

“Lakini ulikuwa ni ushauri wako.” Lisa alijutia chaguo lake.

Pamela akaachana na habari za Alvin. “Sawa, twende tukatafute chakula. Ninajua mahali pazuri ambapo chakula humkumbusha mtu nyumbani. Tunaweza kuanza kutafuta nyumba baada ya kujali matumbo yetu kwanza. Lo, kwa nini tusimualike Cindy Tambwe pia?”

Wakiwa njiani kuelekea mgahawani, Lisa alimpigia simu Cindy Tambwe ambaye alikuwa ni rafiki wake wa karibu pia. “Nipo na Pamela tunaenda kula chakula. Ni muda umepita tangu tulipokutana mara ya mwisho. Je! unaweza kuungana nasi?"

"Niko kwenye shooting ya video ya wimbo wangu mpya. Pole.” Cindy aljibu kifupi.
"Ni sawa. Tutafanya wakati mwingine.” Lisa akakata simu. Cindy Tambwe alikuwa ni msanii wa bongo fleva.

"Anazidi kuwa maarufu kila siku. Asingefikia hapo alipo kama usingeandika na kumtungia nyimbo wakati ule,” Pamela alitoa maoni yake baada ya simu kukatika.

"Sisi bado ni marafiki hata hivyo. Ni kawaida kuwa ana shughuli nyingi.”
•••
Grapefruit ulikuwa ni mgahawa unaowika sana pande za masaki ambao ulikuwa umefunguliwa muda si mrefu. Kulikuwa na ua mkubwa uliotengenezwa katikati ya mgahawa huo.
Magari ya kifahari yalipatikana nje ya mgahawa huo muda wote. Hili lilikuwa eneo ambalo ni matajiri tu wangeweza kumudu. Wawili hao wakaegesha gari na kuelekea mgahawani. Waliweza kuwaona watu wachache waliowafahamu mara tu walipoingia mahali hapo, wakiwemo Lina Jones, Janet Kileo, na vile vile Cindy Tambwe.

“Cindy!” Pamela alimwita yule msichana. Cindy, ambaye alikuwa amevaa miwani ya jua, alifunua tabasamu lisilo la kawaida. Akiwa amekasirika, Pamela aliwaendea wanawake hao akiwa na Lisa.

“Ulituambia kwamba upo location unafanya shooting, cha ajabu upo hapa na hawa wanafiki. Je! unajua wao ni akina nani? Janet ni adui mkubwa wa Lisa na Lina ndiye mbweha mwenye nyuso mbili aliyeiba mpenzi wake.” Pamela alimtapikia maneno Cindy maneno makali.

“Unamwita nani mbweha mwenye sura mbili? Chunga maneno yako." Janet akasonga mbele kumsukuma Pamela kwa jeuri. Lisa alinyoosha mkono kumshika rafiki yake huku akilitazama lile kundi la wanawake kwa dharau.

Asingeenda pale kama angejua kuwa hilo lingetokea. Hata hivyo, hakuweza kukataa kwamba Cindy alikuwa amemkatisha tamaa kweli. “Cindy, kwa nini unatembea nao? Ni jambo moja mimi kukosana na Lina, lakini unapaswa kujua vizuri zaidi kuliko mtu yeyote kuhusu historia yangu na Janet.”

“Kwa nini?” Janet aliunganisha mkono wake na Cindy huku sura ya uvivu ikienea usoni mwake. “Inabidi uulize kweli? Sio tu kwamba umepoteza haki ya urithi wa familia ya Masawe, lakini pia umeamua kukaa katika hoteli ya hadhi ya chini. Mtu kama wewe hastahili kuwa rafiki wa Cindy. Yeye ndiye mwimbaji maarufu zaidi kwa sasa wakati wewe ni nyota ambayo imeanguka. Wewe si mtu tena.”

Lisa alimkazia macho Cindy na kumwambia, "nataka kusikia kutoka kinywani mwako."

Cindy alivua miwani yake ya jua na kumtupia jicho la kejeli Lisa. “Sio vibaya umenikutaniza leo kwani nimechoka kukukwepa kila mara kwa visingizio pia. Kusema kweli, hata kama ungekuwa hujui kusoma hata picha huoni kweli?”

Lisa alijiona kuwa hafai alipokuwa akiisoma sura hiyo iliyopambwa kwa uzuri mbele ya macho yake. Ethan na Cindy walichagua tu kuwa wema kwake kabla ya hii kwa sababu alikuwa akifuata mstari kama mrithi wa familia ya Masawe.

"Cindy, unasema kweli?" Pamela akafoka, “Umesahau jinsi ulivyoonewa na Janet kipindi kile? Au jinsi Lisa alivyokusaidia kwa kukuandikia nyimbo…”

“Acha kujaribu kunishawishi kwa kutumia mambo ya zamani. Mimi na yeye hatupo kwenye ulimwengu mmoja tena,” Cindy alimkatisha kwa dharau. “Pamela, pokea ushauri wangu. Lisa hana kitu kwa sasa, atakushusha tu hadhi yako. Ni bora kukaa mbali naye.”

"Nyamaza! Marafiki wanapaswa kusaidiana bila kutarajia kupata kitu kama malipo. Huelewi hilo?” Hasira katika sauti ya Pamela ilikuwa dhahiri.

"Achana nao Pamela, hakuna maana kubishana nao." Lisa alimshika mkono Pamela, uso wake haukuonyesha hisia zozote. “Tumekuja kula chakula. Twende zetu.”

Pamela aliwatazama sana wasichana hao watatu kabla ya kuongozwa na Lisa .
“Lisa , huyo mwanamke amerukwa na akili au vipi? Umekuwa rafiki mkubwa kwake. Cindy asingekuwa hapa alipo leo bila msaada wako. Ina maana amesahau jinsi Janet alivyokuwa akimfanyia jeuri shuleni? Ninajuta kutotambua rangi halisi za Cindy kabla ya hili.”

Lisa alishusha macho yake chini. Uso wake maridadi na mrembo ulibaki bila kustaajabisha.

“Lisa mchane, mpe makavu yake!” Pamela alimsisitiza.

"Ni kweli, lakini ingefaa nini?" Pembe za midomo ya Lisa zilibadilika na kuwa tabasamu la kujidharau. Kulikuwa na hali ya huzuni ikiangaza pande zote katika macho yake. “Lakini huu ndio ukweli wa mambo. Tazama wazazi wangu wote walionizaa wananidharau kabisa huku Ethan ambaye kimsingi nilikua naye amenitelekeza. Sina kazi, sina makazi na sipendwi. Si Cindy pekee anayenitendea hivi.” Pamela alimtazama rafiki yake, akisikitika kwa hasira.

"Baba yangu alisema mwenyewe, nafasi inayonifaa katika Kibo Group ni msaidizi wa Lina pekee. Ninaweza kuondoka kwenye kampuni ikiwa nitakataa kukubalina naye.” Tabasamu la kusikitisha lilienea usoni mwake. "Ni wazi, sikutaka hivyo, kwa hivyo niliondoka."

Pamela alijaribu kumtia moyo. "Achana naye. Hakika utang'ara zaidi mahali pengine kwa uwezo wako."

Wakati huo huo, mhudumu aliwakaribia. "Samahani, bibi, una nafasi?"

"Ndio, nilizungumza na Meneja Luka kupitia simu mapema." Pamela alimpa ishara meneja aliyesimama kando ya mapokezi. Ili kuweza kupata huduma ya chakula katika mgahawa huo, ilitakiwa kuweka oda mapema maana nafasi zilikuwa haba. Meza ziliandaliwa maalum kwa wateja waliokuwa wametoa oda zao.

Meneja Luka alitembea kuelekea kwao. “Bi. Masanja, nimekuandalia meza yako maalumu uliyoagiza. Niruhusu nikuonyeshe njia.”

Wakati huo huo sauti ya Janet ilisikika nyuma yao. “Meneja Luka, nimeleta marafiki kadhaa pamoja nami leo. Kuna meza iliyotayari?" Janet na wenzake walikuwa hawajaweka oda kabla.

Meneja alionekana kushangaa. Macho yake yalimtoka alipomwona Cindy akiwa miongoni mwa wale wasichana. "Huyu anaweza kuwa mwimbaji Cindy Tambwe?"

Janet akatabasamu kwa utamu. "Meneja Luka, hakika macho yako ni mazuri sana. Nilimwambia Cindy kwamba chakula cha hapa ni cha kipekee. Ratiba yake inamruhusu muda huu, kwa hiyo tumekuja naye hapa, tunahitaji meza iliyotayari. Cindy hana muda wa kusubiri.” Janet alisema huku akitabasamu.

Meneja Luka alichanganyikiwa na hali hiyo. "Miss Tambwe ana sauti nzuri na mimi ni shabiki yake. Ni bahati mbaya kuwa nafasi zote zimejaa kwa sasa. Itabidi msubiri tuwaandalie.”

"Si ulisema umewaandalia meza moja?" Janet alimtupia jicho Lisa kwa kona ya macho yake.

Pamela alijawa na hasira mara moja. "Tuliweka oda mapema. Ungekuwa na shida ya kula hapa na wewe ungeweka oda yako mapema."

Meneja Luka alikuwa hajui la kufanya. Wote wawili walikuwa mabinti kutoka familia tajiri za Masaki. Lisingekuwa jambo la hekima kumuudhi hata mmoja wao.

Janet aliachia tabasamu hafifu huku akimnyooshea Lina kidole. “Meneja Luka, sihitaji kukuambia Cindy ni nani, lakini huenda hujui kuhusu huyu binti hapa. Jina lake ni Lina Jones Masawe na baba yake ni mkurugenzi mkuu wa Kibo Group. Hivi karibuni atakuwa mrithi wa familia pia. Kuhusu huyo rafiki wa Bi Masanja, yeye ni msaidizi tu wa Miss Masawe hapa.

Hilo lilimshangaza meneja. Kibo Group ilikuwa miongoni mwa makampuni yaliyofanikiwa zaidi nchini. Lilikuwa jina ambalo kila mtu alikuwa akilifahamu. Isitoshe, Janet pia alitoka katika familia tajiri. Kwa kulinganisha, Pamela na rafiki yake walionekana kuwa kama panzi mbele ya tai.

Pamela alilipiza kisasi kwa hasira. “Mrithi wa familia asiye na uwezo? Huyo ni mwizi tu asiye na haya ambaye anapenda kukwapua vitu vya wengine.”

Kulikuwa na mabadiliko kidogo kwenye uso wa Lina. Janet alimkazia macho meneja huyo huku uso wake ukiwa na tabasamu. "Utatupatia nafasi sasa, Meneja Luka?"

“Ndiyo, kabisa.” Meneja Luka aliamua ndani ya sekunde chache. "Bi Masanja, nilikumbuka tu kwamba nilikubali kutenga meza kwa ajili ya Miss Kileo kabla yako... Um, tafadhali tutakuandalia ya kwako baadaye!"

Lisa alikodoa macho huku akihema kwa hasira. "Meneja Luka, unatuchukulia kama wajinga?"

Pamela akakunja mikono yake. “Unadhani unaweza kutuonea kijingajinga? Simu moja tu kwa kaka yangu mkubwa hivi sasa na mgahawa wako utafunga mlango ndani ya sekunde chache.

“Meneja Luka, usijali. Tutawajibika kikamilifu.” Lina alitabasamu.

Meneja alijiamini kwa msaada huo. “Bi Masanja, mimi ni mfanyakazi tu. Huwezi kunitishia kwa kujivunia cheo. Tafadhali ondoka mara moja na uache kuwasumbua wateja wetu.”

“Nisipofanya hivyo? Sikiliza meneja, huwezi kutupotezea muda wetu bure. Ikiwa siwezi kupata mlo wangu hapa, basi hakuna mtu mwingine anayeweza kula pia.” Pamela alichukua chombo karibu na yeye na kukipiga chini kwa hasira.

Hisia za hasira zilitawala kwenye uso wa meneja kwa mfululizo wa haraka. “Waondoe hapa,” aliwaagiza watumishi waliokuwa karibu.

Kabla Lisa hajajibu, yeye na Pamela walisukumwa kwa nguvu hadi mlangoni na wanaume kadhaa wenye nguvu. wahudumu walikuwa katili hasa kwao. Akiwa amevaa viatu virefu, Lisa alipoteza usawa na kuanguka chini. Licha ya hayo, wahudumu walijifanya kutotambua na kuendelea kumtoa nje ya mgahawa kabla ya kusimama. Lisa alijiona kana kwamba hakuwa kitu zaidi ya gunia. Mikono na magoti yake hakuhisi kama ni yake tena.

"Mwacheni!" Sauti ya mtu fulani ilisikika nyuma yao. Moyo wake uliruka mapigo.
Inawezekana ikawa…ITAENDELEA..

Unafikiri nini kitafuata hapo maana mambo ni moto mambo ni fire, lakini sina cha kusema nikuombe tuungane pamoja katika sehemu inayofuata ya mkasa huu wa kusisimua unaokwenda kwa jina la LISA.

KUSOMA FULL STORY NICHEKI WHATSAPP 0628924768

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
JINA LA SIMULIZI............................LISA
SPONSORED BY.......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP..........................0628924768
SEHEMU YA...................................13&14

SURA YA13

Lisa aliinua kichwa chake, lakini mhudumu alimfukuza nje ya mgahawa kabla ya kuangalia vizuri. Mtu mrefu na mwenye nguvu alikaribia ghafla. Alionekana mzuri kiasili akiwa amevalia mavazi nadhifu. Sifa zake za usoni zilifafanuliwa isivyo kawaida na mwonekano mzuri. Alvin Kimaro! Hili lilimshangaza. Hakutarajia kukutana na mtu huyo mahali pale, achilia mbali wakati ambao alikuwa akionekana kuonewa na kudharirishwa sana. La, tayari hakumpenda kwa kuanzia. Labda angependekeza talaka mara tu baada ya tukio hilo.

Sam alitokea nyuma yake na kumtambua Lisa mara moja. Alikuwa amemwona binti huyo hapo awali kwenye hafla zingine, bila kusahau kwamba alikuwa mmoja wa mabinti wachache warembo aliopata kuwafahamu, laakini, haikuwa kawaida kumuona katika hali kama ile ya kufadhaika.

“Alvin, huyu si…” Sam aliacha sentensi yake ikining'inia hewani baada ya Alvin kumtupia jicho la onyo.

"Lisa , uko sawa?" Pamela alifanikiwa kujinasua kutoka kwa mhudumu aliyemshika na kumpa rafiki yake mkono.

“Nipo sawa…” Lisa alimwitikia huku akimtazama Alvin.

Pamela pia alimtambua mtu huyo. Alijua kuwa alikuwa mzuri, lakini alipopata fursa ya kumwangalia kwa karibu kulimfanya atake kupiga kelele kwa mvuto wake. Mbali na yeye, Janet Kileo, Lina Masawe na Cindy Tambwe nao walikuwa wamemkazia macho mtu huyo. Hawakuwa wamemwona mtu mwenye sura nzuri ajabu na umaridadi wa kipekee namna hiyo. Alikuwa nani?

Alvin alikunja ndita kwenye paji la uso wake kabla ya macho yake meusi kutua kwenye uso wa meneja. "Hiivi ndivyo mgahawa wako unavyowachukulia wateja wake?"

Meneja Luka aliogopa sana. Hakujua mtu huyu alikuwa nani, lakini hali yake na mwonekano wke wa kuvutia ulikuwa wa kutisha. Mbali na hilo, mwanamume huyo aliandamana na Kijana maarufu Sam Harrison, ambaye jina lake lilijulikana karibu kila sehemu ya kitongoji kile. Meneja alijwana na wasiwasi bila kujua ni kitu gani kingemkuta.

Wakati tu anataka kufunua mdomo wake kwa ajili ya kujibu, Janet alisogea mbele huku akitabasamu. “Kaka Harrison, huyu bwana hapa lazima atakuwa rafiki yako. Kweli, niliweka oda na Meneja Luka mapema ili kupata nafasi kwa ajili ya chakula na hawa marafiki zangu kadhaa wa karibu. Tulipojitokeza, hata hivyo, Lisa na Pamela nao wakajitokeza na kuendelea kumsumbua meneja ili awape nafasi yetu badala yake…”

“Janet, unaweza kukosa aibu kiasi gani? Ni sisi tulioweka oda kwanza. Ninyi watatu ndio mmetuingilia bila sababu,” Pamela alibishana, “Meneja Luka alifikiri ilikuwa rahisi kutudhulumu kwa sababu ya umaarufu wenu.”

Meneja aliongea kwa jazba, “Ndugu Harrison, usiwasikilize. Nilifanya kazi yangu kulingana na sheria za mgahawa. Wanawake hawa wawili walianza kufanya fujo, kwa hivyo sikuwa na chaguo ila kufanya hivyo."

Lina aliingilia kwa unyonge, “Lisa, najua hunipendi sana, lakini hakuna sababu ya kufanya mambo kuwa magumu kwa Meneja Luka. Anafanya kazi yake tu.”

Tabasamu lilitanda usoni mwa Lisa . "Hivi, hujawahi kuchukizwa na unafiki wako mwenyewe?"

Sam hakujua la kusema baada ya kusikia mabishano yaliyokuwa yanakinzana kutoka kwa wasiachana hao. Akageuka kumwangalia rafiki yake. "Nini unadhani, tufanye nini?"

Lisa alishtuka na nuru ikamtoka machoni. Alidhani Alvin alikuwa bado akimchukia hadi wakati huo. Hakuwa na mategemeo kwamba angeweza kuangukia upande wake.

“Huu ndio mgahawa ambao umekuwa ukipendekeza tuje kupata chakula?” Sauti ya chini ya Alvin iliambatana na sura ya kejeli. "Meneja wa mgahawa hata hajitambui, hajui kuzingatia sheria za msingi za ukarimu. Mtu kama yeye hastahili nafasi ya usimamizi.”

Mwangaza uliangaza machoni mwa Lisa . Alinyanyua kichwa kumtazama Alvin akiwa haamini.

Meneja alihisi kuchukizwa kidogo aliposikia kauli ya Alvin. Kweli? Je, alimwona kama mwanamume asiye na akili? Meneja Luka alishtuka sasa. ““Ndugu Harrison, mimi sina hatia. Bi Kileo, lazima unisaidie...”

Janet pia hakutarajia kama mgeni huyo angechukua upande wa Lisa. “Kaka Harrison, rafiki yako ni mgeni mjini, kwa hiyo anaweza kuwa hafahamu rangi halisi za Lisa na Pamela—”

Macho ya Sam yaliyochanua yaliganda huku akiachia tabasamu, akifunua meno yake meupe na safi kabla ya kumkatisha Janet. "Sijui mengi kuhusu Pamela Masanja, lakini nimesikia kuhusu Lisa Jones Masawe. Sio tu kwamba yeye ni binti mdogo wa familia ya Masawe, lakini pia anasimama kati ya mabinti bora kabisa kwa uwezo na sura yake nzuri. Aliingia katika chuo kikuu cha New South Wales nchini Marekani akiwa na umri wa miaka 21 na amekuwa akitengeneza rekodi ya kuvutia ya kitaaluma katika kampuni ya Kibo Group tangu arejee kutoka nje ya nchi na shahada yake ya uzamili mwaka jana. Yeye si sawa na nyinyi vipepeo vya kijamii mnaohudhuria karamu baada ya karamu.”

Alisisitiza kwa makusudi maneno 'vipepeo vya kijamii' kuwakejeli mabinti hao watatu.

Muda mfupi baadaye, Cindy alilazimisha tabasamu lisilo la kawaida. "Kaka Harrison, kuhudhuria sherehe na karamu ni njia mojawapo ya kupanua mzunguko wetu wa kijamii kama warithi wa siku zijazo, Lisa ambaye si mrithi wa biashara ya familia, hahitajiki kuhudhuria hafla kama hizo.” Alvin alikodoa macho.

"Wewe ni nani wa kuongea nami kwa sauti kama hiyo?" Sam alidhihaki. Rangirangi zilitoka kwenye uso wa Cindy papo hapo.

Lina naye alitabasamu vibaya kabla hajasema. “Kaka Harrison, unalifanya jambo hili kuwa gumu.”

"Ninyi nyote mlianza kwanza, kwa hivyo mnaweza kujilaumu wenyewe. "Sam aligeuza midomo yake kwa dharau. "Kama ninyi ndiyo warithi basi biashara za familia zenu zinaenda kutoweka. Tukiweka kando ukweli kwamba Miss Janet Kileo alihonga kupata elimu yake kutoka shule ya sekondari hadi chuo kikuu, Binti huyu mwingine wa Masawe pia hana elimu na hana uzoefu. Lakini, anatumai kurithi biashara ya familia yenye mafanikio. Kama si kejeli ni nini? Hakuna mtu mwingine mwenye uwezo katika familia ya Masawe?"

Lina na Janet wote walikuwa hawajiwezi kwa aibu. Lisa na Pamela walikuwa wakijaribu sana kutaka kumpongeza mtu huyo kwa matusi yake sahihi na ya moja kwa moja.

Hatimaye, Janet alijibu kwa masikitiko, “Inaonekana kama Ndugu Harrison amedhamiria kuwapendelea wale wawili siku ya leo. Cindy, Lina, tunapaswa kuondoka tukale chakula chetu mahali pengine.” Lina hakutaka kukaa hapo hata kwa sekunde moja zaidi. Aliitikia kwa kichwa na kujiandaa kuondoka eneo lile akiwa na Cindy.

"Subiri ..." Alvin alipaza sauti ghafla, akakunjua tabasamu na kuinua ndita usoni mwake. "Mnaweza kuondoka, lakini lazima muondoke kwa njia ile ile kama walivyokuwa wakiondolewa wenzenu sasa hivi."

Lisa alipigwa na butwaa huku macho yake yakiwa yametua kwa Alvin. Alishikwa katika wakati wa hisia tofauti. Hakutarajia kama Alvin angemtetea. Kwa namna fulani, hakuweza kujizuia kuhisi anavutiwa naye tena.

Wakati huo, Lina na wasichana wengine hawakuweza tena kujizuia. Janet alifoka, “Unafikiri wewe ni nani? Unajua sisi ni akina nani?"

Alvin alitulia huku akimtupia jicho Sam. Sam alitazama kando kwenye kundi la wahudumu kwa tabasamu. “Mnataka mimi binafsi nimpigie simu bosi wenu? Mtu atakayewaburuta kwa nguvu zaidi atalipwa bonus.”

Kila mtu katika mgahawa huo alifahamu Sam ni nani, mtu maarufu na mwenye pesa. Hata bosi wa watumishi wale angemtendea kwa adabu. Kikundi cha wahudumu kilikimbia mara moja kumburuta Lina na wale mabinti wengine wawili nje na mhudumu mmoja akiwadharirisha kikatili zaidi kuliko vile walivyofanyiwa kina Lisa. Mabinti wote watatu walikuwa wamekuja wakiwa wamevalia vizuri, lakini vurumai lile liliwaacha wakiwa hawataminiki kabisa. Hata gauni refu la Lina lilichanika baada ya kunaswa kwenye kitalu cha maua. Lisa na Pamela walitazama hali hiyo huku vinywa vyao vikiwa vimelegea.

Akiwa amepiga magoti mbele ya wawili hao, Meneja Luka aliomba msamaha, “Lazima nimekuwa kipofu sasa hivi, Bi Jones na Bi Masanja. Ilikuwa ni kosa langu. Natumai nyinyi wawili mtakuwa wakarimu wa kunisamehe.”

Lisa alimtazama kwa siri Alvin. Alipotambua kwamba Alvin hakusema neno lolote, Lisa akamwambia meneja, “Tuna bahati iliyoje kukutana na Harrison hapa, la sivyo, kwa jinsi tulivyokuwa tukiburuzwa sijui ingekuweje. Kwa hali hiyo sitakusemehe na pia nitafikisha malalamiko yangu kwa bosi wako ana kwa ana.”

Sam alisema kwa tabasamu, “Si lazima uonane naye ana kwa ana. Nitampigia bosi wao baada ya dakika moja na hataonekana tena tena kwenye mgahawa huu.”

Meneja Luka alianguka chini kwa maumivu. “Ndugu Harrison nisamehe, nina watoto na mke nyumbani, mama yangu naye ni mgonjwa…Nikipoteza hiki kibarua nitaishije?.

SURA YA14

Kwa kweli Pamela alifurahishwa na hali hiyo. Kwa bahati mbaya, alimuona Lisa akiwa amesimama pembeni ya Alvin akiwa ameganda bila kusema neno lolote. Akiwa na mawazo ya ghafla, alitumia bega lake kumpiga kikumbo kwa jeuri rafiki yake wa karibu. Kwa msukumo wa ghafla, Lisa alienda akaangukia mikononi mwa Alvin. Lisa hakuwahi kuwa karibu sana nna Alvin kiasi kile. Harufu laini na tamu ikajaza pua yake. Lisa alipatwa na mshtuko wa ubongo mara moja. Kamwe hakutarajia kwamba angemdaka na kumweka mikononi mwake, alifikiri angemsukumia mbali. Ilikuwa tofauti kabisa na matarajio yake.

Lisa alihisi kuwa macho ya Alvin yalikuwa yakimtoka. Akiwa na ufahamu, alitoka mikononi mwake kwa haraka. "Samahani, ilikuwa ajali."

“Acha kujifanya. Sio mara yako ya kwanza kufanya hivi.” Alvin alijibu. Lisa alikosa la kusema.

Akiwa na hasira ya kusukumwa kwa kushtukizwa, Lisa alielekeza macho yake kwa mchonganishi wake. Aligundua kuwa Pamela na Sam walikuwa wakimtazama kwa udadisi. Sam alitoa kikohozi chepesi. "Tumekutana hapa kwa bahati tu, basi tupate chakula pamoja, sawa?”

Macho ya Pamela yakang'aa. “Hakika. Nilikuwa nikisubiri tu kufanya toast na wewe kukushukuru kwa kutuokoa.”

“Twende zetu.” Pamela na Sam walikuwa wa kwanza kuingia mgahawani huku wakipiga soga.

Lisa alipigwa na butwaa. Alisitasita na kumtazama Alvin, lakini Alvin hakujishughulisha hata kumtazama. Akaingiza mkono wake kwenye mfuko wa suruali yake na kuingia moja kwa moja kwenye mgahawa huo. Lisa akamfuata Alvin kwa haraka huku akitaka kujua hali ya Charlie pia. Alikuwa na wasiwasi sana juu ya hilo kwa kuzingatia kwamba alikuwa ametoka kwa Alvin siku moja iliyopita.

Mhudumu aliwaongoza wanne wale hadi kwenye chumba cha kifahari. Kilikuwa ni chumba tofauti na kile walichokuwa wameweka oda wao. Mara Lisa alipoingia ndani ya chumba hicho, alishtuka kuona mazingira ya anasa.

Pamela alimsogelea Lisa kwa furaha na kumnong’oneza sikioni, “Hakika ni mumeo aliyeweka oda ya chumba hiki. Hiki ndicho chumba cha kifahari zaidi katika mgahawa mzima. Ni matajiri tu wenye pesa za kuzechezea ndiyo wanaoweza kumudu gharama ya chumba hiki.” Lisa alishindwa cha kusema.

Pamela alikibana kiuno cha Lisa kwa wivu. "Kwa kweli, mume wako ni mzuri sana. Ingawa alikufukuza kwake kwa kumuumiza paka wake kipenzi, alichokifanya ni kukuokoa ulipokuwa unadhalilishwa. Tazama, amesamehe na kusahau ulichofanya na sasa amekutoa lunch kwa gharama kubwa, jinsi alivyo wa ajabu!”

Lisa alisema kwa dharau, "Hakuja hapa kwa ajili yangu, tumekutana kwa bahati tu."

“Hata kama!” Pamela alimwambia kwa shauku, "Siku ile nilimtazama tu kwa mbali. Sikujua kwamba angegeuka kuwa mtu wa kuvutia sana nikimtazama kwa karibu. Jambo ni kwamba, yeye ni mjomba wa Ethan. Fikiria kuhusu mali, hadhi na mwonekano wa mwanamume huyo jambo ambalo linamweka mpenzi wako wa zamani kwenye kivuli. Ethan atapoteza utulivu wake ikiwa atatokea mbele yake, na hii pia itamfanya Lina ahisi wivu sana.”

Lisa ghafla akawa na shauku ya kufikiria namna ya kujidai ya Lina.

"Nyie wawili mnanong'onezana nini masikioni?" Sam aliuliza huku akicheka.

Hapo ndipo Lisa alipogundua kwamba wanaume wawili waliokuwa kwenye chumba hicho cha kifahari walikuwa wamewatolea macho. Alikuwa na aibu papo hapo. “Asanteni sana jamani, leo tumepata bahati ya kuingia katika chumba hiki cha kifahari cha faragha.”

"Sogea uketi karibu na mumeo, atakuwa ameku’miss sana!" Sam alijibu kwa utani.

Maneno yake makali ya utani yalimuacha Lisa akiona aibu. "Acha utani, Harrison."

"Wacha tuanze kuagiza chakula." Alvin alifungua menyu, macho yake yakionyesha ukali. Baada ya kuagiza chakula alichokitaka, aliweka menyu juu ya meza.

Sam alimpenyeza menyu kwa Lisa . "Agiza chakula, shemeji."

Lisa ambaye alikuwa akinywa juisi, karibu apariwe aliposikia akiitwa shemeji. Alikohoa kwa nguvu mara kadhaa. Kutokana na macho ya Sam ya dhihaka, ikamjia kwamba Sam tayari alikuwa ameshajua kuhusu ndoa yake na Alvin. Ilivyoonekana, Alvin na Sam walikuwa na uhusiano wa karibu.

“Usiniite hivyo. Nitaachwa wakati wowote.” Lisa alimjibu Sam wakati anapokea menyu kwa aibu. Lisa aligiza chakula alichokitaka na kukabidhi menyu kwa Pamela.

Baada ya muda kila mtu alikuwa kishaagiza chakula alichokitaka. Wakati wanasubiri vyakula vyao viletwe, Pamela akatoa simu yake na kuanza kujadili jambo na Lisa. “Unapanga kukodisha sehemu gani? Nadhani ghorofa hii ni nzuri sana. Inagharimu dola 800 tu kwa mwezi.”

“Nani anapanga kukodisha nyumba?" Sam aliuliza baada ya kuibia mazungumzo yale.

Pamela alipumua. “Ni Lisa . Hana namna zaidi ya kukodisha mahali kwani amefukuzwa kutoka kwa familia ya Masawe. Hana pa kukaa kwa sasa na amebakiwa na pesa kidogo sana. Alikaa kwenye hoteli ya hadhi ya chini sana jana usiku. Ni hatari sana kwa usalama wake.” Akiinamisha kichwa chake kwa aibu, Lisa alikunywa juisi yake kimya kimya.

Sam aligeuza kichwa kumtazama Alvin, kisha akalalama. “Alvin, ungewezaje kumruhusu mkeo mrembo akae mahali pa hatari kiasi hiki, ina maana huna uwezo wa kumtunza?”

Lisa mara moja akageuka na kumtetea. "Ni kosa langu. Nilimlisha Charlie chakula kisichofaa na kumfanya atapike. Alvin alikuwa sahihi kunifukuza. Vipi lakini, Charlie anaendeleaje sasa? Yupo sawa?”

Sam alijibu huku akitabasamu, “Usijilaumu. Charlie ni—”

Kabla Sam hajaendelea, Alvin alikatisha hotuba yake. “Hali yake si nzuri. Msamaha wako hauna maana."

Kwa msemo wa ajabu Sam alimuonea huruma Lisa ambaye alihisi hastahili kulaumiwa. Huu ulikuwa ukatili sana kwa Alvin.

Lisa aligeuka rangi ghafla. Alikuwa akifikiri kuwa hali ya Charlie ilikuwa nzuri na kwamba Alvin alimsaidia kwa sababu hasira yake ilikuwa imepungua.

"Umepanga kufanyaje?" Alvin alizungumza tena ghafla.

Lisa alikuwa ameduwaa. "Sina pesa kwa hivyo sina lolote.”

Alvin akatumia nafasi hiyo kumwambia, "daktari alisema kuwa Charlie anahitaji kupumzika. Chakula chake na mazingira ya kuishi yanapaswa kuzingatiwa vizuri. Ikiwa unajisikia hatia kweli, unaweza kumtunza na kumpa chakula chake mara tatu kwa siku katika kipindi hiki. Usimruhusu kula chakula cha mafuta, badala yake, tayarisha chakula kibichi na chenye lishe ambacho ni rahisi kwa tumbo lake kusaga.”

"Kohoooh!, kohooh!." Sam alikabwa kikohozi baada ya kusikia Alvin akitamka maneno hayo bila aibu, wakati alijua kabisa kwamba paka wake ni mjamzito. Hatimaye alikuja kugudua kwamba Alvin alitaka tu kupata yaya wa bure. Mjanja kiasi gani.

Lisa alipigwa na butwaa kwa muda. Kisha alimwangalia na kumuuliza, “Unamaanisha ninaweza kurudi nyumbani kwako?”

Alvin alimkumbusha kwa upole, “Weka kando mawazo yako mengine yote. Kuanzia leo na kuendelea, utaishi kwangu kama mhudumu wa Charlie.”

"Kweli, hakuna shida." Lisa alifurahi sana hivi kwamba macho yake yakang'aa. Kwa mwonekano wa mambo, bado alikuwa na nafasi ya kuwa shangazi wa Ethan pamoja na kwamba alitakiwa kutumika kama mhudumu wa paka kwa wakati huo. Hii ilimaanisha kuwa angeweza kuwa mhudumu wa kibinafsi wa Alvin katika siku za mbeleni.

Macho ya Alvin yalimtoka kwa furaha. Sio tu kwamba hakulazimika kuomba msamaha kwa kile kilichotokea usiku uliopita, lakini pia alikuwa amempata mhudumu wa Charlie. Kwa njia hii, aliweza kuua ndege wawili kwa jiwe moja.

Baada ya chakula, Sam alienda kusuluhisha bili huku Lisa akiwa amesimama pembeni ya Alvin. Ghafla, kadi ya benki ilitupwa mikononi mwake.

"Nenda ukachukue chakula kwenye maduka kwa ajili ya chakula cha jioni cha Charlie baadaye."

"Anakula nini?" Lisa aliishika kadi huku akiwa ameduwaa kwani alikuwa hajawahi kufuga paka.

Alvin akamtupia jicho la dharau. “Nimekuambia mapema. Chakula chenye lishe safi na salama.”

Lisa alishangaa kuona maisha ya paka yalikuwa bora kuliko ya mwanadamu, akamuuliza tena. “Kwa hiyo unarudi nyumbani usiku huu? Unahisi kula nini? nitakuandalia.”

“Chochote.” Baada ya kusema hivyo Alvin aliondoka na Sam.

Akiwatazama wawili hao wakiondoka, Pamela alisema kwa kucheka, “Sijui kuna pesa ngapi kwenye kadi hii, Lisa, hutakiwi kuwaza tena!”

"Sina uhakika. Sitatumia pesa hizi kwa matumizi yangu kwa vile ni zake.” Lisa akatikisa kichwa. "Lazima nitafute kazi haraka iwezekanavyo ndani ya siku hizi mbili."

“Sawa basi. Endelea hivyo. Kwa kuwa mpango wa kutafuta nyumba umesitishwa, nitaenda kutazama filamu na Patrick. Alisema atakuja kunichukua.” Alisema Pamela.

Baada ya Pamela kuingia kwenye gari lake, Lisa naye aliliendea gari lake.


Mara tu alipofika kwenye gari lake, Lisa alimwona Ethan akiwa ameegemea mlango wa gari lake na umbo lake refu, Lisa alijawa na ukakasi tena moyoni mwake. Walisema baada ya mapenzi huja chuki na visasi. Hivyo ndivyo hasa Lisa alivyohisi wakati huo.

Lisa alinyanyua kichwa chake na kumtazama Ethan uso wake wa ajabu. “Ni Lina aliyekuambia nipo hapa?”

Mara moja, macho ya Ethan aliyoyazoea yalionyesha hali ya kufadhaika. "Lisa , hata uwe na hasira na wivu kiasi gani, hukupaswa kumfanyia dada yako hivyo."

Lisa alishangaa, lakini upesi alitabasamu na kusema, "Alikuambia juu yake, sivyo?"

“Niligundua hilo hata bila yeye kuniambia. Kuna mtu alituma tukio la leo kwenye whatsapp,” Ethan alijibu. “Ulipata mtu wa kumdhaliliisha dada yako hadharani na kumtoa nje ya mgahawa kwa njia ya aibu. Kando na dada yako, Janet na rafiki yako mkubwa Cindy pia wamedhalilika vya kutosha. Tabia yako mbaya inasikitisha sana.”

Midomo myembamba ya Ethan ilifunguliwa na kufungwa kwa umaridadi. Lisa alikuwa amemsikia akisema maneno matamu mara nyingi. Wakati huo hata hivyo, alivunjika moyo sana. “Ndio, mimi ni mbaya sana. Kwa hiyo upo hapa kulipiza kisasi dhidi yangu kwa niaba ya mchumba wako?”

“Bado hujatambua kosa lako kwa wakati huu,” Ethan akaongeza kwa hasira, Baba yako na Mama yako tayari wamekasirishwa na wewe. Kwa nini huwezi kuwa na tabia nzuri? Watu sasa wanakuona wewe kama mwendawazimu tu.”

“Ndiyo, ni mwendawazimu,” Lisa alikiri waziwazi. "Lakini mwisho wa siku atajulikana mwendawazimu ni nani na timamu ni nani!"

“Lisa !” Ethan alishindwa kujizuia na kugonga gari kwa ngumi. “Umeniangusha sana. Nimekuwa nikijaribu sana kuvumilia kwa ajili ya maisha yetu ya baadaye, nikitumaini kwamba nitaweza kuchukua kampuni ya Lowe hivi karibuni. Na wewe je? Angalia ulichofanya. Sio tu kwamba uliondoka kwenye kampuni na kuishi bila kazi, lakini sifa yako pia imeharibiwa. Huwezi kujirekebisha kidogo?”

Lisa alitamani sana angeropoka maneno haya, 'ninafanya kazi kwa bidii ili kuunganisha utambulisho wangu kama shangazi yako, mpuuzi wewe.' Lakini akaishia kumwambia Ethan kwa hasira. “Ninafanya kazi kwa bidii kwa ajili yangu na si yako."

Ethan alifoka kwa hasira, “Unajitahidi tu kumdhalilisha Lina, sivyo? Ukiendelea kufanya hivi, Lina atakuzidi wewe. Ndiyo, anaweza kuwa na sifa za chini za elimu na amekulia mashambani, lakini yeye ni mwerevu, mwenye bidii, na huwa anakesha akifanya kazi usiku kucha!”

“Lo, umeona pointi nyingi zaidi kwake sasa!” Lisa alimdhihaki.

Aliposikia hivyo, Ethan alifikiri kwamba Lisa alikuwa na wivu. Pamoja na hayo, alionyesha kujieleza pasipo kueleweka. “Sasa si wakati wa kuwa na wivu Lisa. Unapaswa kuelewa dhana ya kobe na sungura—”

“Nani mwenye wivu? Ethan,” Lisa alimkatisha Ethan, “uliniacha mimi na kuchumbiana na Lina. Ni nini kinakupa haki ya kunilazimisha kufanya kazi kwa bidii kwa ajili yako? Je, ina maana kwamba utaniacha nikiacha kufanya kazi kwa bidii? Kweli, unataka mwanamke unayempenda au mwanamke anayelingana na hadhi yako na anayeweza kukusaidia?"

“Kama sina mapenzi na wewe, ningepoteza muda wangu kukutana na wewe hapa?” Ethan alijibu kwa kukosa subira. “Nisikilize. Nenda nyumbani ukaombe msamaha kwa wazazi wako na dada yako ili urudi Kibo Group hivi karibuni,”

“Kuna faida gani ya kurudi Kibo Group? Hata nifanye kazi kwa bidii kiasi gani, Lina anaweza kuharibu mafanikio yangu wakati wowote.” Lisa alicheka ghafla. "Kwa kweli, machoni pako mafanikio hayo sio yangu bali ni yako wewe uliyeyapigania."

Maneno yake ya uchokozi yalimfanya Ethan achemke kwa hasira. “Kama nisingekuwa mimi, ungeweza kushinda mradi wa hoteli ya Lublin? Kwa nini hutafakari udhaifu wako? Si ajabu huwezi kuelewana na kila mtu.”

“Uko sahihi. Afadhali ukae mbali nami, basi.” Lisa alimjibu kijeuri. Lisa alikasirika sana hadi meno yake yaligongana. Alipofungua mlango kwa nguvu, alisema kwa ukali, “Usije tena kukutana nami. Ninachukizwa sana kuuona uso wako sasa hivi.”

"Unasema nini?" Ethan alikunja sura kwa kiburi. "Haujajiangalia kwenye kioo kabla ya kuniambia hivyo?"

“Ndiyo, ninaonekana mbaya. Sistahili kuwa na mtu mtukufu kama wewe, handsome Lowe.” Lisa alitoa tabasamu baridi, kisha akafunga mlango wa gari lake kwa nguvu. Aliwasha gari na kuondoka kwa kasi kubwa. Ethan aliyebaki pale alinyanyua mguu wake na kuupiga teke mti uliokuwa kando yake kwa hasira.

Muda huo Lina alimpigia simu huku akiongea kwa sauti ya wasiwasi. “Ethan, ulienda kukutana na Lisa sivyo? Mshauri tu vizuri. Usiwe na hasira naye."

Alipofikiria usemi huo wa huruma kwa Lisa, Ethan hakuweza kujizuia kusema, “Amekufanyia mambo mabaya sana, na bado unathubutu kumuonea huruma?”

“Lazima nimsaidie tu. Ninamuhurumia, kwa kweli." Akiwa amehuzunika na kusikitika, Lina aliongeza, “Kwa mawazo yake naonekana kama jambazi aliyempokonya kila kitu, hajui kuwa si mimi ninayeweza kufanya maamuzi kuhusu mambo ya kampuni. Ni baba yangu ndiye anayeamua yote. Kwa upande wako, ninakupenda sana. Licha ya kujua kuwa una hisia naye, siwezi kujizuia kushindania penzi lako. Utanilaumu kwa kuwa mbinafsi sana, Ethan?”

“Hapana, sijawahi kukulaumu. Usifikiri sana.” Ethan akamjibu kwa upole.

“Sawa, Ethan. Nitakusaidia ili uweze kuchukua kampuni ya Lowe. Najua unapanga kufanya kazi kwenye mradi wa familia ya Kileo siku za karibuni, ndiyo maana ninawasiliana mara kwa mara na Janet ili nimshawishi wakubali.”

"Asante." Hatimaye Ethan aliona ni kwanini alifanya hivyo. Moyoni mwake alimuonea huruma Lina kwani alijua haikuwa rahisi kwake kuelewana na Janet.

“Usiseme hivyo. Niko tayari kufanya lolote kwa ajili yako.” Lina alisema taratibu...ITAENDELEA....

Unafikiri nini kitafuata hapo maana mambo ni moto mambo ni fire, lakini sina cha kusema nikuombe tuungane pamoja katika sehemu inayofuata ya mkasa huu wa kusisimua unaokwenda kwa jina la LISA.
LIPIA USOME HARAKA.

Vitabu vinazidi kuandikwa na baadhi vimekamilika lakini pia unaweza kusoma kwa kulipia kulingana na episode unazotaka.

Episode - 20 Tsh 1000/=
Episode - 30 Tsh 1500/=
Episode - 40 Tsh 2000/=
Episode - 50 Tsh 2500/=

Namba za kulipia

0628924768 (Halotel) JUMA HEMBA
0694288555 (Airtel) JUMA HEMBA
0764736557 (Voda) HADIJA KIRUNGI

"Lipia utumiwe similizi yako sasa whatsapp 0628924768"

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
JINA LA SIMULIZI............................LISA
SPONSORED BY.......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP..........................0628924768
SEHEMU YA...................................15&16

SURA YA15

Gari aina ya Maserati ilisogea kando ya barabara pana. Muda wote wa safari, Lisa alitetemeka huku akihisi baridi ya kimwili na kiakili. Kamwe hakutarajia kwamba siku moja yeye na Ethan wangeishia kuwa maadui wakubwa. Jambo hilo lilimfanya ajiulize kama yeye ndiye aliyekuwa akimpenda sana. Kwa nini apoteze imani kwake, awe na mawazo mabaya kumhusu, na kutemndea kwa ubinafsi kiasi kile? Inaweza kuwa kwa sababu hakuwahi kupenya akilini mwake.

Muda mfupi baadaye, simu yake iliita. Ilikuwa ni simu kutoka kwa mama yake. Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Lisa kupokea simu kutoka kwa mama yake tangu atoke nyumbani. Lisa alijua fika kwamba simu hiyo haikuwa ya kumruhusu kurudi nyumbani, lakini aliitikia wito huo licha ya nafsi yake. “Mama—”

“Usiniite mama”. Sina binti mkatili hivyo!” Sauti ya hasira ya Mama Masawe ilitoka upande wa pili. “Rudi umuombe msamaha dada yako sasa hivi!”

“Msamaha?” Lisa alishangaa sana. “Kwanini usimuulize Lina alichonifanyia? Yeye—”

“Dada yako ni mkarimu, tofauti na wewe. Ulichofanya ni kuwa na mzozo na Janet. Familia ya Kileo ni moja ya familia tajiri zaidi. Dada yako alianzisha urafiki na Janet kwa makusudi ili kuhakikisha kwamba familia za Masawe na Kileo zitaelewana vizuri na kushirikiana kibiashara. Na wewe je? Unachokifanya ni kuzidi kumkoroga tu Janet na hata kumuumiza dada yako. Ilikuaje nikamlea binti mbaya kama wewe?"

"Sitarudi." Lisa hakuzungusha maneno.

Mama Masawe alinguruma, “Usirudi tena, na sitakuhesabu kama binti yangu tena!”

Lisa akavuta pumzi kwa nguvu. “Umewahi kuwa na wasiwasi kuhusu mimi? Kabla hajarudi huyo kipenzi wako Lina, ulifikiri siku zote kwamba sikuwa mzuri kama wengine hata nilivyofanya kazi kwa bidii. usingeongea nami na kunisema vizuri ila kunifokea tu kunizaba makofi. Kweli mimi ni binti yako?” Baada ya kulia kwa uchungu, machozi yalimtoka. Hakika alilemewa na mafadhaiko. Hakujisikia tena kurudi katika nyumba hiyo.

Lisa alishuka kisha akajivuta na kuelekea kwenye duka la vyakula vya wanyama wa nyumbani ili kuuliza kuhusu mambo yanayohusiana na kumhudumia paka. Lisa alikabidhiwa kitabu kilichoandikwa 'Mapishi ya Chakula kwa Paka Wajawazito'. Muuzaji alimwambia kuwa kumhudumia pakamwenye matatizo ya tumbo ni sawa na kumhudumia pakamwenye mimba.

"Hata hivyo, mapishi yaliyomo humu yanajumuisha virutubisho vyote ambavyo paka anahitaji. Hakupaswi kuwa na shida yoyote ikiwa utatayarisha chakula cha paka wako kulingana na kitabu hiki”

Baada ya kufikiria kidogo, Lisa alikinunua kile kitabu na kuelekea dukani kununua viungo.

Saa kumi jioni, Lisa alirejea nyumbani kwa Alvin. Charlie alipogundua kurudi kwake, aliinama kwa uvivu na kujibanza kwenye kona yake bila kusogea. Jambo hilo lilimfanya Lisa azidi kuvunjika moyo. Kwa hilo, aliamua kwenda kumuandalia Charlie chakula cha haraka haraka. Kwa kuzingatia kwamba paka alihitaji kula chakula chepesi, alitayarisha vipande vichache vya samaki na kutia ndani karoti na mboga zilizokaushwa. Kwa kuongezea, alimtengenezea paka yule sambusa chache kama vitafunio.

Alvin alitoka kazini na kurudi nyumbani jioni. Kupitia mlango wa kioo wa jikoni, alimwona Lisa akiwa na shughuli ya kupika jikoni. Dakika moja alikuwa akikata mboga na dakika iliyofuata akawa anapika kwenye sufuria.

Harufu ya kupendeza ya mboga ilitoka kwenye ufa wa mlango wa kioo na kuchochea tumbo lake. Alihisi kushikwa na njaa kidogo ghafla. Alvin alipotazama kando kwenye meza, aliona sambusa, ambazo zilikuwa na umbo la pembetatu kama kawaida, kwenye sahani nyeupe ya udongo. Kwa rangi zake angavu, sambusa zile zilionekana kupendeza kabisa.

Kama kuonja tu hivi, alichukua uma na kuchoma sambusa moja na kuipeleka mdomoni. Ilikuwa na ladha tofauti kabisa na sambusa alizoziwea. Ladha yake ilikuwa ya ajabu kidogo. Ilionekana kuwa sambusa hizo zlikuwa na nyama ya kuku na viungo vingine visivyojulikana, lakini haikuwa na mafuta sana. Pengine ingekuwa sawa kuongeza kipande zaidi cha sambusa. Kwa muda mrefu alikuwa amejua kwamba Lisa alikuwa mzuri katika kuandaa kifungua kinywa. Lakini, hakujua kuwa angeweza kutengeneza vitafunwa vya ubunifu kama vile pia.

"Umerudi, Alvinny." Lisa alipofungua mlango ili atoke jikoni akiwa na sinia iliyojaa vyakula vilivyopikwa, alishangaa kumuona Alvin ambaye alikuwa karibu kumaliza sambusa aliyokuwa ameshika. Kumtazama kwake kulimfanya Alvin akose raha kidogo. Alidhani kuwa alifurahi sana kumuona akila vitafunwa aliyotengeneza. Kwa mawazo hayo, alikohoa kidogo na kusafisha koo lake. "Kitindamlo ulichotengeneza kina ladha nzuri sana."

Lisa alitetemeka, akijiuliza sana ingekuwaje ikiwa angejiua baada ya kumwambia kwamba vitafunwa hivyo vilikusudiwa kwa paka. Baada ya kubadilisha dhamiri yake kwa muda, hatimaye alilazimisha tabasamu. “Nimekutengenezea makusudi. Ni vizuri kujua kwamba unaona ni kitamu.”

Alvin alimtazama kwa jeuri na kumwambia. "Unahitaji tu kumzingatia zaidi Charlie."

"Najua, najua." Lisa aliitikia kwa kichwa huku akionyesha upendo. "Siwezi kupuuzia."

Alvin alimbeba Charlie na kumweka kwenye mikono yake kabla ya kubadilisha mada. "Alikula nini jioni ya leo?"

"Vipande vya samaki wakavu. Hapendi mboga, kwa hivyo niliongeza karoti kwenye samaki. Amemaliza vipande yote sita ya samaki.”

“Sawa.” Alvin aliitikia.

Lisa alipomaliza tu sentensi yake, alianza kuwa na mashaka kuhusiana na hamu ya kula ya Charlie. Aliambiwa kwamba paka walikula kidogo sana, lakini Charlie alikuwa na hamu kubwa sana,alimaliza kila kitu alichomtengea.

“Nimemaliza kuandaa chakula cha jioni. Unaweza kuanza kula.” Lisa alimwambia Alvin.

Lisa aliweka uma na vijiko kwenye meza. Alikuwa ametayarisha Nyama ya nguruwe, saladi na ndizi mshale za kuchomwa, na juisi ya matunda kwa chakula cha jioni. Kuangalia saladi, Alvin alihisi kuwa inafanana na ubora wa chakula kinachotolewa kwenye migahawa ya kifahari. Ilikuwa bila shaka kwamba upishi wa Lisa ulikuwa wa ajabu. Chakula alichotengeneza kinaweza kuonekana kuwa cha kawaida, lakini kilikuwa na ladha nzuri zaidi ikilinganishwa na chakula kinachotolewa kwenye migahawa huko nje.

Akiwa na hamu kubwa ya kula, Alvin alimaliza chakula kwa miguno kadhaa. Baada ya kumaliza kula, alimsifu, "Upishi mzuri."

“Asante.” Lisa aliona aibu na kuhisi kufarijika kwa neno la kushukuru kutoka kwa Alvin.

“Tangu utotoni, nimeazimia kuwa mke kwa ajili ya mume wangu wa baadaye. Ninachotarajia ni kumpatia chakula kizuri kila siku baada ya kutoka kazini.” Lisa alitazama upande wa Alvin mara baada ya kumaliza kuongea.

Alvin alikuwa akitazama chini, akimpigapiga paka kwenye mapaja yake. Aliposimama na kujiandaa kutoka kuelekea chumbani kwake, ghafla alikiona kile kitabu kiitwacho 'Mapishi ya Chakula kwa Paka Wajawazito' kwenye kochi la sebule hiyo.

Alikunja uso akishangaa kwamba Lisa amegunduaje kuwa Charlie ni mjamzito.
Kwa bahati mbaya, Lisa alitoka jikoni baada ya kuosha vyombo. Alipomwona akiwa ameshika kitabu hicho, alieleza, “Nilienda kwenye duka la wanyama wa nyumbani leo. Muuzaji aliniambia kwamba mapishi ya kutuliza tumbo la paka yanafanana kabisa na yale ya paka wajawazito, kwa hiyo nilinunua kitabu hiki.”

Macho ya Alvin yakalegea. Ilionekana kuwa bado alikuwa hajui hilo. Alipopekua-pekua kitabu bila mpangilio, aliona kichocheo anachokifahamu kwa ghafla. Uso wake mzuri uliganda. Baada ya muda, Alvin alinyanyua kitabu na kumuonyesha Lisa picha hiyo kwenye kijitabu. "Kwa hivyo hii ndiyo sambusa uliyonitengenezea kwa makusudi, sivyo?"

Kitu kama shoti ya umeme klipita kwenye mwili wa Lisa. Alionekana kusahau kwamba alitengeneza sambusa za paka mapema kulingana na maelekezo ya mapishi katika kitabu kile. “Ah… Hiyo ilikuwa kweli…lakini si uliona kitamu?” Lisa alijikanyagakanyaga.

“Kwa hiyo unaweza kunitengenezea chochote mradi tu nitakiona kitamu?” Alvin alimwangalia kwa sura iliyojaa hasira. Wakati huo, alianza kuhisi kichefuchefu baada ya kugundua kuwa alikuwa amekula chakula cha paka.

Lisa alijihisi mnyonge. "Kweli, nilimtengenezea Charlie, lakini sikuwepo wakati unakula na hata ulikisifu kuwa ni kitamu. Wakati huo… niliogopa sana kukuambia ukweli.”

“Lisa !” Alvin akasaga meno. Akiwa ameishi miaka 28 ya maisha yake, hii ilikuwa mara yake ya kwanza kutaka kumuua mwanamke!

Lisa alikosa maneno yakujitetea mbele ya Alvin akabaki akijikanyagakanyaga tu. "Kwa kweli, viungo ... ni lishe nzuri sana."

"Kwa kuwa chakula hicho kina lishe, kwa nini usile mwenyewe?"Alimuuliza kwa hasira Alvin

"Lo, sioni kitamu."

"Umefanya vizuri."

Wakati akimnyooshea kidole, Alvin alikumbuka kusifu ladha ya chakula. Alikasirika sana hadi uso wake ukawa mbaya.

Lisa alitaka kueleza zaidi, lakini Alvin alikuwa tayari ameshaingia chumbani kwake na kuufunga mlango kwa nguvu. Ah hapana, alikuwa amekasirika sana.

SURA YA16

Lisa alikuwa mwisho wa akili yake. Mwanzoni alipanga kumfurahisha baada ya kupewa nafasi nyingine ya kuendelea kukaa naye. Hata hivyo, tayari alikuwa amemchukiza aliporudi nyumbani kwa muda usiozidi saa moja tu. Kwa nini alikuwa na safari ndefu kabla ya kufikia lengo lake la kuwa shangazi wa Ethan? Dakika kumi baadaye, Lisa bila haya alibisha hodi kwenye mlango wa Alvin.

“Potelea mbali.” Sauti ya ukali ilisikika.

Lisa alifumba macho kwa kuchanganyikiwa. Kwa kuwa bado alikuwa amekasirika wakati huo, alipaswa kusubiri hasira zake zituame kabla ya kuzungumza naye tena.
Alienda kuoga kwanza. Alibadilisha nguo na kuvaa seti ya pajama za kupendeza, akaziacha nywele zake ndefu nyeusi zianguke kwenye mabega yake. Alipojitazama kwenye kioo na kujikonyeza, alivutiwa na uzuri wake. Kwa ngozi nzuri na macho makubwa, alijiona kuwa msafi na mwenye kuvutia kweli. Aliamini kuwa mwonekano wake ungemfanya Alvin amtende kwa uangalifu.

"Unafanya nini?" Ghafla sauti ya Alvin ilisikika pembeni yake.

Lisa alitetemeka kwa hofu. Alitikisa kichwa na kugundua kuwa Alvin alikuwa akimwangalia kwa dhihaka na kikombe cha kahawa katika mkono wake wa kulia.
Aliingia saa ngapi? Mbona hakusikia nyayo zozote?

“Mimi…” Lisa alijing’atang’ata. Ni wazi kuwa alikuwa anafanya mazoezi kwa siri jinsi ya kumnasa.

“Nilivutiwa na urembo wangu huku nikijitazama kwenye kioo,” alijibu kwa aibu baada ya kugugumia kwa muda.

Alvin alishindwa cha kusema. Hakika kukosa haya kwa Lisa kulikuwa kumefikia kiwango kingine kipya. Hata hivyo, ilimbidi akubali kwamba uso wa mwanamke huyo ulikuwa mzuri, safi na maridadi. Hata huko Nairobi, jiji lililojaa wanawake warembo, hakukuwa na wanawake wowote ambao walionekana kuwa warembo kiasili kama yeye.

"Ninachoweza kuona ni kujitoongozesha kwako tu." Mara baada ya kumaliza sentensi yake kwa maneno ya dharau, Alvin aligeuka na kwenda kujimwagia maji.

Lisa alimfuata. “Bado umekasirika? Nifanye nini ili kuzima hasira yako? Nitakula sambusa za paka pia, sawa?"

Alvin alikunja midomo yake ghafla na kuchukua pakiti ya chakula cha paka kutoka kwenye kabati. "Sitaweza kutuliza hasira yangu hadi umalize pakiti hii nzima."

Lisa alishtuka kumkuta Alvin akiwa mkatili kiasi kile. “Hii ni… tofauti. Lile nililotengeneza lina virutubishi, na hata uliliona kuwa litamu—”

“Nyamaza.” Uso wa Alvin ulijawa hasira kwa kutajwa kwa tukio hilo. “Usijali, hutakufa kwa kula chakula cha paka. Viungo vyake ni pamoja na samaki na nyama ya ng'ombe ambayo imechaguliwa kwa uangalifu. Lo,hata hivyo, pia kuna prebiotics ambayo inaweza kuboresha mfumo wako wa usagaji chakula pamoja na taurine, kalsiamu, chuma, na zinki ambazo zinaweza kuimarisha mwili wako. Ni lishe iliyoje!”

“Ikiwa ni lishe bora, kwa nini usile pamoja nami?” Lisa alimwambia kwa upole. Baada ya kuchukua chakula cha paka, alijimiminia bakuli lake. Alikula mara moja huku akivumilia radha isiyoelezeka mdomoni mwake.

Alvin hakutarajia kuwa Lisa angekula kweli chakula cha paka. Kwa hilo, hasira yake ikafifia kiasi. "Vipi ina ladha tamu eeh?" Alimzihaki huku akicheka.

"Kitamu kabisa. Unataka kula pamoja nami?" Lisa alisema kwa hasira. Hali ya mazingira iligeuka kuwa ya kukera dakika tu alipomaliza kuzungumza.

Kwa tabasamu la dharau, Alvin aliongeza pakiti nyingine ya chakula cha paka kwenye bakuli lake. “Kweli? Kwa kuwa unaona kuwa ni kitamu, unaweza kula zaidi.”

Kweli mtu huyo alistahili kuishi peke yake milele kwa tabia hiyo. Hatimaye, Lisa alilazimika kula pakiti mbili za chakula cha paka ili tu kumridhisha Alvin.

"Kazi nzuri." Alvin akaingiza mkono mfukoni na kurudi chumbani kwake akiwa ameridhika. Alipoingia chumbani kwake, aligeuza kichwa kumuangalia Lisa ambaye alikuwa amegeuka na kukimbilia chooni. Macho yake meusi yaliangaza kwa hisia ya kejeli aliposikia akipiga mswaki.

Kwa kuchukizwa na chakula cha paka, Lisa hakuweza kulala vizuri usiku mzima. Alipoamka asubuhi na mapema siku iliyofuata, bado alihisi harufu ya samaki mdomoni mwake.Kwa bahati mbaya, ilimbidi kuamka mapema ili kumwandalia Alvin kifungua kinywa. Aliapa kumfanya fisadi yule apendezwe naye. Kisha, angemkanyaga chini na kulipiza kisasi juu yake. Kufikia wakati Alvin anarudi nyumbani kutoka kukimbia kwake asubuhi, alishtuka kugundua karamu kubwa imetanda kwenye meza.

“Wewe…” Alvin alishtuka baada ya kuzidiwa na harufu ya mahanjumati.

“Alvlisa, nilijisikia vibaya kwamba ulikula sambusa za paka jana usiku kwa hiyo nimekuandalia kiamsha kinywa kitamu sana.” Lisa alisema kwa uchangamfu huku akimnywesha bakuli la uji wa lishe.

Kulikuwa na mwonekano wa ajabu usoni mwake. "Ni sawa. Tayari uliadhibiwa jana usiku na inatosha.”

Lisa alisimama huku akiwa na hisia kali kooni. "Kwa kweli nilikuwa nimechoka baada ya kula chakula cha paka jana usiku," alijibu polepole sekunde chache baadaye.
Akashusha macho yake chini bila kutoa maelezo zaidi.

“Unakwenda kazini? Niikushushe tena kwenye kituo cha daladala?” Aliuliza kabla ya kuelekea mlangoni mara baada ya kumaliza kifungua kinywa chake.

Lisa alishtuka lakini punde akatingisha kichwa huku na huko. "Nilifukuzwa kazi." Ukiwa ulisikika kwa sauti yake.

Lisa alikuwa amemwambia kwamba alikuwa akifanya kazi katika kampuni ya familia yao na uhusiano kati yake na familia ya Masawe ulionekana kuwa mbaya sana. "Sawa, hutalala njaa kwa kufukuzwa kazi. Unaweza kuzingatia tu kumtunza Charlie nyumbani." Alvin alimwambia.

“Ninapanga kutafuta kazi nyingine. Lakini usijali, sitairuhusu inizuie kumtunza Charlie.”

"Vyovyote," alinong'ona na kuondoka nyumbani......ITAENDELEA....

- Unafikiri nini kitafuata maana mambo yanazidi kuwa moto na ugumu unazidi kumuelemea Lisa...lakini kwa leo tuishie hapa nikuombe muda wako katika episode inayofuata ili kujua ni kipi kitajiri kwenye mkasa huu wa kusisimua na kuburudisha.
LIPIA USOME HARAKA.

Vitabu vinazidi kuandikwa na baadhi vimekamilika lakini pia unaweza kusoma kwa kulipia kulingana na episode unazotaka.

Episode - 20 Tsh *1000/=
Episode - 30 Tsh *1500/=
Episode - 40 Tsh *2000/=
Episode - 50 Tsh *2500/=

Namba za kulipia

0628924768 (Halotel) JUMA HEMBA
0694288555 (Airtel) JUMA HEMBA
0764736557 (Voda) HADIJA KIRUNGI

"Lipia utumiwe similizi yako sasa whatsapp 0628924768"

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
JINA LA SIMULIZI............................LISA
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP..........................0628924768
SEHEMU YA....................................17&18

SURA YA17

Kwa siku kadhaa zilizofuata, Lisa alijishughulisha sana na kutafuta kazi. Kulikuwa na fursa nyingi kwa kampuni za kubuni mambo ya ndani au majukumu yanayohusiana na usanifu majengo. Lakini ili kuficha asili yake kama binti wa familia ya Jones Masawe, ilibidi afanye uzoefu wake wa kitaalam wa zamani kuwa siri. Mbali na hilo, makampuni mengine makubwa yalikuwa tayari kumwajiri kama msaidizi, kutokana na umri wake mdogo.

Akiwa hana mbadala bora, alichagua kufanya kazi na kampuni ndogo iitwayo Imperial Design. Ofisi nzima ilikuwa zaidi ya futi za mraba mia moja tu. Wabunifu wao wote walishughulikia kila kitu ikiwa ni pamoja na kubuni mipango na kusambaza vipeperushi vya matangazo nje ya ofisi.

Hii ilikuwa mara yake ya kwanza kufanya kazi kama hiyo. Hapo mwanzoni alijihisi kujisumbua lakini muda si muda akawa amezoea kazi hiyo. Baadhi ya wapita njia walipokea vipeperushi vyake lakini mara nyingi zaidi, watu walikuwa wakipita tu kana kwamba hawamuoni.

Siku moja Lisa akiwa kwenye majukumu yake ya kusambaza vipeperushi kwenye foleni ya magari katikati ya jiji, gari nyeusi aina ya Lamborghini ikasimama mbele yake. Hilo lilimshangaza. Lilikuwa ni gari la Ethan.

“Lisa , kwa nini unasambaza vipeperushi mitaani…” Lina alitoka kwenye kiti cha abiria.
Lisa alihisi fundo la moto katikati ya kifua chake. Ethan aliwahi kumwambia kwamba kiti cha abiria cha gari lake kilikuwa ni kwa ajili yake tu. Lakini sasa kilikuwa kimekaliwa na Lina. Kejeli iliyoje?

“Ningekuwa wapi tena, Kibo Group?" Maneno yake yalikuwa ya kutojali.

Lina alikunja midomo yake kana kwamba alikuwa amekasirika. “Sikuwa na maana hiyo…”
“Ni nini maana ya maneno hayo? ” Ethan alishuka ghafla kwenye gari na kuubamiza mlango nyuma yake. “Jiangalie vizuri. Wewe ni binti mdogo wa familia ya Masawe. Huoni aibu? Dada yako anakuuliza kwa mema tu we unamjibu dharau.”

Lisa aliinua macho yake, na kuona karaha kwenye uso wa Ethan. Maumivu makali yaliujaza moyo wake kana kwamba kuna mtu alikuwa anachonga tundu kwa patasi.
“Kwa nini nione aibu? Ninafanya kazi kwa uaminifu kwa kusambaza vipeperushi badala ya kuwaibia wengine.”

“Ethan hakumaanisha hivyo. Anadhani haupaswi kufanya kitu kama hii. Lisa rudi nyumbani uendelee na kazi Kibo Group!” Lina alisema mara moja, “Angalia, tumepata mkataba wa ukarabati na usanifu wa Wasafi Media kuhusu studio zao za kifahari. Tunazungumza juu ya vyumba zaidi ya elfu, kwa hivyo faida inaweza kuwa zaidi ya mabilioni. Njoo unisaidie. Sisi ni ndugu wa tumbo moja na tunapaswa kufanya kazi pamoja ili kufanya Kibo Group kuwa bora zaidi.”

Lisa ambaye tayari alikuwa akijihisi kuchanganyikiwa kutokana na kupigwa na jua kali kwa muda wa saa moja, alikasirika zaidi. “Huchoki kuwa mnafiki kila dakika? Huwezi kukaa mbali nami? Sina nguvu ya kurumbana na wewe kila wakati.”

“Inatosha,” Ethan alimfokea kwa hasira. "Lina anakupa mkono kwa fadhili lakini unamchukulia tu kwa mabaya zaidi. Huwezi kuwa mstaarabu kidogo?”

“Mimi?” Lisa hakuamini masikio yake. “Wewe ni kipofu hata usimwone ni mwanamke wa aina gani? Tungeachana kama si kwa sababu yake?”

“Lina ananipenda kupita kiasi, lakini wewe? Lakini wewe hunipendi kama yeye.” ethan aliongea bila kujiamini.

“Sawa, penzi langu halifananishwi na lake. Ondoka, toka machoni mwangu sasa hivi." Lisa alishindwa kujizuia na kuwarushia wale wawili vipeperushi kwa hasira utadhani vilikuwa vinaweza kuwaumiza.

“Mwanamke mwendawazimu!” Ethan alitangulia mbele ya Lina na kumsukuma kidogo Lisa kutoka kwao. Lisa alipoteza usawa na kuanguka chini. Vipeperushi vilitawanyika kote kwenye kwenye barabara.

Wakati anatazama juu, tayari Ethan alikuwa akimuongoza Lina kuelekea kwenye gari huku vidole vyao vikiwa vimeunganishwa. Lina alitazama nyuma ili kumkosha Lisa kwa tabasamu. Lamborghini kisha likatoweka kwa mbali na kumwacha Lisa akiwa katika maumivu makali. Ni kana kwamba mtu alikuwa amemchuna ngozi akiwa hai. Hakutarajia Ethan angemtetea Lina namna hiyo, hata alikuwa tayari kumuumiza kwa sababu yake.

Ilionekana dhahiri kuwa umbali kati yao ulikuwa ukiongezeka zaidi. Lisa hakuhisi ameshindwa hapo awali, lakini kwa wakati huu, alihisi kama amepoteza kila kitu.

Wakati huo Alvin alikuwa kwenye foleni ya magari akiwa njiani kutoka mahakama kuu alikokuwa akipinga kesi. Akiwa anangojea taa ya trafiki igeuke kijani, aligundua kuwa kando ya barabara kulikuwa na vipeperushi. Mwanamke aliyevalia shati jeupe aliinama chini kutoka kiunoni ili kuokota kipeperushi kimoja baada ya kingine.

Alikunja uso kidogo huku akimkumbuka Lisa akiwa amevaa vazi kama hilohilo kabla ya kuondoka nyumbani asubuhi ya siku hiyo. Taa ilipogeuka kijani. Alvin alipiga U-turn na kuegesha gari lake kando ya barabara. Akamsogelea yule mwanamke, akainama na kuokota kikaratasi na kumkabidhi.

“Niache,” Lisa alisema kwa sauti ya kukaba akidhani ni Ethan ndiye aliyerudi. “Sitaki kuona uso wako…”

Aliinua macho yake. Ingawa maono yake yalififishwa na machozi yaliyokuwa yanatoka machoni mwake, sura ya kweli ya mshangao ilitanda usoni mwake alipotambua sifa za mwanamume huyo maridadi.

“Alvin… Kimaro.”

Alvin akakunjauso kidogo. Alikuwa akimwita 'Alvlisa' kila wakati na alihisi ajabu kumsikia akimwita kwa jina lake kamili.

“Nani amekuudhi?” Alvin alifuta matone ya machozi karibu na macho mekundu ya Lisa yenye uvimbe. Ilikuwa dhahiri kwamba alikuwa akilia. Alvin alizoea kumuona Lisa akiwa mcheshi mbele yake. Hii ilikuwa mara ya kwanza kwake kumuona akilia.

Akiwa amechanganyikiwa, Lisa aliuma mdomo wake huku akimtukana mwanaume huyo kwa siri. 'Yote ni kwa sababu ya mpwa wako mjinga. Hawakumfundisha adabu katika familia? Yeye ni mbinafsi, si mwaminifu, na ana kichwa kilichojaa sh*t.'

Lakini, hakuthubutu kusema hayo. “Mimi…Kuna mtu alimwaga vipeperushi vyangu chini,” alijibu huku akionekana kuhuzunika.

Mshtuko ulitanda usoni mwa Alvin alipotazama kikaratasi mkononi mwake. Hakutarajia kama kazi yake yake mpya ingemfanya asambaze vipeperushi mitaani. Aligundua kutokana na uchunguzi wake kwamba Lisa alikulia katika mazingira ya kupendeza na yaliyoboreshwa.

"Unadai kuwa umehitimu kutoka Chuo Kikuu Marekani lakini hii ndiyo aina ya kazi unayofanya?"

Lisa aliona haya kidogo na kujitetea. "Nilihusika katika usanifu wa uwanja wa michezo wa Azam Chamazi na uwanja wa ndege wa Chato. Kando na hilo, pia nina uzoefu katika usimamizi wa miradi, lakini watu hawaniamini kwa sababu ya umri wangu. Siwezi kufichua utambulisho wangu kama binti mdogo wa familia Masawe kwa sababu uhusiano wangu na familia yangu hauko sawa. Ndio maana naweza kuchagua tu kazi ya kuwa msaidizi katika kampuni kubwa au kuwa mbunifu katika kampuni ndogo.” Lisa alieleza huku akikusanya vipeperushi vyake haraka.

"Sitaki kuwa msaidizi kwa sababu hiyo kimsingi itanitaka kufanya kazi za kiutawala zisizo za kawaida. Mtu aliye juu zaidi bila shaka atajinufaisha zaidi kwa ujuzi wangu kwa kudai ubunifu wangu ni wake. Afadhali nianze kujenga CV yangu katika kampuni ndogo.

Sio tu kwamba ninaweza kushiriki asilimia ya faida wakati wa kufunga mikataba, lakini kusimamia mradi pia kunatoa malipo mazuri. Baada ya mwaka wa kufanya hivi, pengine naweza kutunza pesa za kutosha, kujenga timu yangu na kuanzisha biashara yangu mwenyewe. Ugumu huu ni wa muda tu."

"Hutaki kurudi Kibo Group?" Alvin aliuliza.

Lisa alitikisa kichwa kimya kimya. “Nitategemea misaada kutoka kwa wengine kwa mpaka lini? Ni vyema zaidi nikajifunza kujitegemea.”

Alvin alishangaa kweli. Kutokana na mazingira aliyokulia, aliona watu wengi wakipigania umaarufu na mali za familia zao kila mara. Sio watu wengi walio na mawazo sawa juu ya maisha kama Lisa.Alvin akamtazama Lisa aliyekuwa ameinama kuokota vile vipeperushi. Kwa mara ya kwanza, alikuwa na kiwango kipya cha heshima kwa binti huyo.

“Viache.” Alvin alimwambia.

“Siwezi.” Lisa alitikisa kichwa kutoka kushoto kwenda kulia bila kusita. "Nitakuwa na shida ikiwa bosi atagundua kuwa vipeperushi vimetawanyika hovyo barabarani badala kuvisambaza kwa watu. Ofisi haifanyi vizuri na tunapaswa kujituma. Kando na hilo, kuviacha vipepeprushi vimetawanyika hovyo barabarani ni uchafuzi wa mazingira.

“Sawa, ngoja nikusaidie basi.” Alvin alimsaidia Lisa kukusanya vipeperushi vyote vilivyokuwa vimetawanyika. Wakiwa katika kuokota uso wa Lisa ulionekana kugeuka rangi. "Nini tatizo? Mashavu yako yanawaka moto.” Alvin alinyanyua macho yake ili kumtazama kwa haraka Lisa.

“Mimi…mimi… Kuna joto sana. Nimepigwa sana na jua,” Lisa aliingiwa na kigugumizi. Alikwepa macho ya Alvin mara moja kwa kuinamisha kichwa chake chini.

Alvin akakunja uso. "Nenda kapumzike chini ya kivuli."

“Ni sawa.” Lisa alitikisa kichwa kwa nguvu. Ilikuwa ni kutokana na matarajio yake kwamba shetani angeweza kuwa malaika pia. Kwa kweli, mbali na kuwa na tabia ya kuongea bila kuficha na pengine kuwa mkali, Alvin hakuonekana kuwa mtu mbaya kiasi hicho.

Iliwachukua kama dakika tano kukusanya vipeperushi vyote. Lisa alihisi kichwa kikizunguka pale aliposimama. Hakuweza kuuzuia mwili wake kuyumba na kuangukia mbele ghafla. Alifikiri angetua chini kifudifudi wakati mkono wenye nguvu ulipomvuta kutoka nyuma. Alijikongoja kidogo kabla ya kuweza kusimama sawa tena. Macho yake yalikutana na macho ya Alvin.

"Labda ni shinikizo la chini la damu kutoka kwa kuinama kwa muda mrefu sana." Lisa alijifuta jasho kwenye paji la uso wake. "Pia inaweza kuwa sababu ya joto."

"Ingia kwenye gari." Alvin akageuka na kufungua mlango wa gari. “Nitakupeleka nyumbani.”

“Hapana, hapana. Sijamaliza kugawa vipeperushi. Nitapumzika kwa muda mfupi na niendelee baadae kidogo.” Haraka akatingisha kichwa.

Kuchanganyikiwa kulimjaa huku akimtazama Lisa kwa ung’ang’anizi wake. Alikuwa tayari kupata kiharusi kwa ajili tu ya kukamilisha kazi yake. Alianza kumuona kama mjinga fulani.

"Ni karibu wakati wa chakula cha mchana kwa Charlie. Uliahidi kutoruhusu kazi yako iingie kati ya nyakati zake za chakula.” Alvin alimkumbusha.

"Nilimtengenezea chakula cha mchana kabla ya kuondoka nyumbani." Moyo wa Lisa ukaanza kushuka tena kwa huzuni. Alikaribia kufikiria kuwa hatimaye ameanza kuelewana naye vizuri.

Alvin akanyanyua uso wake kwa hasira. “Yaani unadiriki kumlisha paka wangu kiporo wakati unajua ana matatizo ya tumbo?”

Lisa alikosa la kusema. Ilikuwa ni makosa kwa paka kula chakula kilichopoa? Lisa hakuwa na chaguo lingine, Lisa akaingia kwenye gari.

SURA YA18

Wakati wa safari, Lisa alipokea simu kutoka kwa bosi wake. "Hakukuwa na msongamano mkubwa wa magari huko, kwa hivyo nimebadili na kwenda sehemu nyingine." Lisa alidanganya.

“Sawa Miss Jones, endelea na kazi nzuri. Labda trafiki itaongezeka baada ya saa ya chakula cha mchana. Tumia fursa hiyo kutoa vipeperushi haraka uwezavyo. Nilikubali kukuajiri kwa sababu nadhani mwonekano wako mzuri unaweza kuvutia wateja. Lazima ufanye kazi kwa bidii. Mbunifu mkubwa hana maana kama hatuwezi kufunga mikataba.”

“Nitajitahidi.” Lisa alikata simu kimya kimya.

Alvin aliiba mtazamo wake nje ya pembe za macho yake. Gari halikuwa pana, hivyo alisikia mazungumzo yote na bosi wake. "Unapaswa kutafuta kazi mahali pengine."

Lisa aligeuza midomo yake kwa tabasamu la uchungu. “Haijalishi nitapata kazi kampuni gani. Kila kitu kitakuwa kigumu mwanzoni." Alvin aligonga vidole vyake kwenye usukani bila kutoa maoni zaidi.

Walipokuwa wakipita kwenye barabara moja maarufu jijini, waliona jengo moja la kuvutia na lenye muundo wa kipekee. “Mahali gani hapo?” Alvin aliuliza kawaida.

"Hiki ni Kituo cha Utamaduni na Teknolojia cha Taifa." Lisa alimjibu na hapo hapo kitu fulani kilikuja akilini mwake ghafla. "Ujenzi umekamilika hivi karibuni. Nilipokuwa Kibo Group nilitaka kuomba mradi wa kudizaini mambo ya ndani lakini nilipoondoka sikuwa na maana hata kuufikiria sasa.

“Kwa nini?” Alvin aliuliza.

"Wanafanya mchakato wazi wa zabuni. Kampuni ndogo kama yetu haina hata sifa ya kujiunga na mchakato wa zabuni.” Lisa alijibu.

"Hata hivyo, kampuni yako haitaweza kupata zabuni hata kama ingekuwa na fursa ya kushirikia." Alvin alisema.

“Hiyo si kweli.” Lisa alipinga. Kujiamini kulionekana katika sauti yake. “Nilitawazwa bingwa katika Tuzo ya AM nchini Marekani. Kampuni nyingi zilinipa nafasi ya kufanya nazo kazi. Wakati huo, kwa kuwa nilikuwa na hakika kwamba ningerithi biashara ya familia, nilikataa ofa hizo na kurudi Kibo Group. Sithubutu kusema hakuna mtu mwingine katika tasnia nzima ambaye ni bora katika kubuni kuliko mimi.

Alvin akatikisa kichwa chake akishangaa hali ya kujiamini ya Lisa. "Sawa, ninaweza kukutengenezea nafasi ya kujiunga na mchakato wa zabuni kama unajiamini."

Lisa akajiweka sawa pale kitini huku macho yakiwa yamemtoka kwa mshangao. Midomo yake yenye kupendeza kama waridi iligawanyika kidogo kana kwamba hakuamini masikio yake. "Una uhakika?"

“Ni juu yako iwapo utaibuka mshindi. Nionyeshe kama kweli una uwezo kama vile unavyojiagmba kwangu.” Alvin alimwambia akiwa bado amekazia macho barabarani.

“Kwa hakika sijisifu. Nina imani naweza kushinda hili.” Alihisi ubongo wake ukibubujikwa na msisimko. “Alvlisa, wewe ndiye bora zaidi…” Alimwita kwa jina hilo kila mara alipomfurahisha—wakati mwingine kwa upole, wakati mwingine akijaribu kumshawishi kitu, lakini, hii ilikuwa mara yake ya kwanza kufurahia sana.

Alvin aligeuka kumwangalia Lisa. Macho yake angavu ya mviringo yalipepea juu ya mashavu yake yaliyopigwa na jua. Ilikuwa ngumu kuweka kwa maneno haiba na ushawishi ulioandikwa usoni mwake Alikwepa macho yake mara moja. Vidole vyake viliruka kwa shida kufungua vifungo karibu na shingo yake kwani ghafla alihisi joto likipanda mwilini mwake.

“Ikiwa unafikiri hivyo kweli, basi unifanyie chakula kitamu baadaye.” Alvin alichomekea.

“Hakuna tatizo hata kidogo. Ninaweza kupika chochote utakachoomba.” Lisa alifurahi. Baada ya kuishi pamoja kwa muda mfupi, Alvin tayari alijua kwamba Lisa alikuwa mzuri katika kupika. Alipofikiria chakula alichotayarisha hapo awali alihisi njaa. Hata hivyo, alijali sana kuokoa hadhi yake ili kupenyeza ombi hilo.

“Simama hapa kwa muda. Nitaenda kununua nyama ya nguruwe,” Lisa alisema ghafla walipoendesha gari karibu na bucha ya nguruwe. Alvin hakuwa ameongea chochote lakini Lisa alijua kwa namna fulani nyama ya nguruwe choma ndicho chakula alichopenda zaidi.

Alipomtazama Lisa aliyekuwa anaelekea buchani, Alvin alichukua simu yake kwa tabasamu hafifu na kumpigia Sam. "Tengeneza mpango ili Lisa Jones kutoka ‘Imperial Design’ aweze kushiriki katika mchakato wa zabuni ya mradi wa Kituo cha Utamaduni na Teknolojia cha Taifa."

Hili lilimshangaza Sam. “Sijawahi kusikia ukiongelea kuhusu kampuni hiyo. Je, unajaribu kumsaidia Lisa? Hii ni nje ya tabia yako."

"Tabia gani?" Alvin aliuliza kwa kejeli

Sam alikaa kimya lakini akajiwazia, 'Tabia ya mtu asiye na huruma na asiyejali.' Bila shaka, Sam hakuthubutu hayo ila akasema baada ya kimya kifupi. “Namfahamu vizuri msimamizi wa kituo hicho, Mzee Kamote. Je, nimuweke sawa ili kuipa kampuni ya Lisa mradi huo? Nijuavyo, kampuni zingine nyingi kubwa, pamoja na Kibo Group, zinashiriki katika zabuni pia. Ni ushindani mkali.”

“Hakuna haja ya hilo.” Alvin alimwambia. “ Nataka apate nafasi tu ili apambane yeye mwenyewe. Ikiwa atashindwa kupata mradi huo, inamaanisha kuwa hana uwezo. Hakikisha tu ni mashindano ya haki."

Sam alivutiwa. Mwanaume huyo kwa kweli hakuwa na huruma hata kwa mkewe mwenyewe. "Sawa, nitafanya kama unavyosema."

Dakika tano baadaye, Lisa alirudi akiwa na mfuko wa nyama ya nguruwe. "Nafasi ya kushiriki imepatikana" Alvin alimwambia ka uchangamfu.

Lisa alionekana kushtuka. ‘Mbona haikuchukua hata muda? Huyu mjomba wa Ethan lazima awe mtu mwenye nguvu.’ Lisa alijiwazia. “Asante,” alisema kwa dhati.

Kingo za mdomo wa Alvin zilijikunja kwa kutabasamu. "Sasa, twende nyumbani ukaniandalie chakula kitamu, tena kama umeotea leo nina hamu na nyama ya nguruwe choma."

Lisa alitabasamu na kumwambia, "sitafanya hivyo. Ninafikiria kutengeneza rost la nyama ya nguruwe na viazi.” Alvin akasinyaa ghafla. Hakuwa na la kusema.

"Pfft." Lisa akacheka. “Nakutania mwaya. Ninapanga kukutengeneza nyama ya nguruwe choma safi na ndizi bila kusahau saladi…”

"Lisa Masawe!" Alvin alitamka kila neno kwa uangalifu kwa sauti ya ukali kidogo. “Wewe mwanamke unathubutu vipi kunitania?

Lisa alipotambua kwamba Alvin alikuwa amekasirika, alitoa ulimi wake haraka na kusema kwa njia ya kucheza, “Je, ni vigumu kukubali kwamba unapenda nyama ya nguruwe choma? Hakuna aibu kukiri unachokipenda mbele ya mke wako!” Alvin hakusema kitu akaishia kutoa mkoromo wa dharau.

Lisa aliuliza tena kwa tabasamu, "Mimi najua wewe unapenda nyama ya nguruwe, wewe unajua mimi ninapenda kula nini?"
"Chakula cha paka," Alvin alitania na mara wote wakaangua kicheko. Kwa muda mfupi kulikuonekana kujaa furaha tupu ndani ya gari.

"Mimi ninapenda kukula wewe zaidi." Lisa alliinua midomo yake kwa kupendeza na kukonyeza macho yake kwa utani huku akimwamgalia Alvin.

Alvin akamtupia jicho la pembeni. "Hakuna mtu aliyekuonya kuhusu kuchezea mwanaume kwenye gari?"

Lisa akawa na wasiwasi na mawazo ya Alvin. Inawezekana kwamba alihisi anazungumzia ‘kula’ ya namna gani? Lisa akakohoa kwa aibu. Kufikiria jambo hilo kulimfanya aone haya usoni. Yeye hakuwa na nia hiyo.

"Itasababisha ajali mbaya." Lisa akavunga. Sauti yake ilikuwa baridi kama ndoo ya maji ya barafu. Alvin akaguna tu na kunyamaza. Alitabasamu kidogo baada ya kuona aibu imeandikwa usoni mwake. Walipofika nyumbani, alimtengenezea chakula cha mchana kitamu. Avin hakurudi tena kazini kutokana na kushiba sana

....ITAENDELEA.....

Unafikiri nini kitafuata hapo maana mambo ni moto mambo ni fire, lakini sina cha kusema nikuombe tuungane pamoja katika sehemu inayofuata ya mkasa huu wa kusisimua unaokwenda kwa jina la LISA.
LIPIA USOME HARAKA.

Vitabu vinazidi kuandikwa na baadhi vimekamilika lakini pia unaweza kusoma kwa kulipia kulingana na episode unazotaka.

Episode - 20 Tsh 1000/=
Episode - 30 Tsh 1500/=
Episode - 40 Tsh 2000/=
Episode - 50 Tsh 2500/=

Namba za kulipia

0628924768
(Halotel) JUMA HEMBA
0694288555 (Airtel) JUMA HEMBA
0764736557 (Voda) HADIJA KIRUNGI

"Lipia utumiwe similizi yako sasa whatsapp 0628924768"

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
JINA LA SIMULIZI............................LISA
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP..........................0628924768
SEHEMU YA....................................19&20

SURA YA19

Ndani ya chumba cha mikutano, mkurugenzi wa kampuni ya Imperial Design, Bw. Erick Zayumba alikuwa tayari amepokea habari za kushiriki mchakato wa zabuni kutoka kituo cha Utamaduni na Teknolojia9 cha Taifa. Kama mtoto anayebubujika kwa msisimko juu ya lollipop, aliitisha mkutano wa dharura. Walioshiriki katika mkutano huo ni pamoja na Lisa, meneja wa mradi, na mbunifu mwingine, Juma Masudi.

"Miss Jones, sikufikiria kwamba binti kama wewe ungeweza kuwa na uwezo kama huu. Umetupatia fursa ya kushiriki katika zabuni. Huu ni mradi mkubwa ambao serikali ya Tanzania imekuwa ikijenga kwa miaka mitano iliyopita. Itakuwa moja ya alama za Taifa katika siku zijazo.

Bw. Zayumba hakuweza kuacha kummiminia pongezi. "Hata kama hatuwezi kupata mradi huu, kuweza kushiriki katika zabuni pia ni msukumo mkubwa kwa mustakabali wa kampuni yetu."

“Mkurugenzi, nina uhakika tunaweza kushinda zabuni kwa dhana nzuri. Tunahitaji kuwa na imani ndani yetu wenyewe. Ingawa saizi ya kampuni yetu ni ndogo, tunaweza kuwa bora kuliko wabunifu wengine. Hili si jambo dogo, lakini tunaweza kulifanyia kazi,” Lisa alisema kwa dhati.

Msimamizi wa mradi akasema, “Si rahisi hivyo. Miongoni mwa washindani wetu ni kampuni mbili zilizoorodheshwa kwenye soko la hisa, bila kusahau kampuni zingine kadhaa zilizo na uzoefu wa miongo kadhaa katika uwanja huo. Nadhani Kibo Group labda atakuwa mshindi wa zabuni hii"

Lisa alihisi hisia za kubana kifuani mwake baada ya kutajwa kwa Kibo Group. Hakujua ni mbunifu gani angewawakilisha Kibo Group kwenye zabuni hiyo. Hata hivyo, hakuwa na wasiwasi. Hakuna aliyewajua vizuri wabunifu waliofanya kazi kwenye Kibo Group kuliko yeye. Watu hao walikuwa na uzoefu wa kutosha lakini hawakuwa na ubunifu.

Baada ya kufikiria kwa ufupi, Lisa alisema, “Mkuregenzi Zayumba, tunapaswa kuwa wajasiri na kuchukua changamoto. Kituo cha Utamaduni na Teknolojia kitakuwa wazi kwa umma katika siku zijazo. Nadhani tunaweza kuchanganya vipengele vya kitamaduni na dhana za sayansi katika muundo ili kuwapa watumiaji uzoefu tofauti wa maendeleo ya siku zijazo."

"Hatua nzuri," Zayumba alipongeza. "Sawa, wewe na Juma mnaweza kushirikiana kufanya kazi ya kubuni. Tumebakiza nusu mwezi hadi tarehe ya mwisho. Acha miradi mingine kando na ujikite katika kuboresha wazo hili."

Lisa alikuwa na wasiwasi baada ya kusikia hivyo. Ingawa hawakuwa wametumia muda mwingi pamoja, aliona kwamba Juma angeweza kuwa mtu asiye na hisia. Siku zote alikuwa akitumia ukweli kwamba alikuwa mkubwa kwake kwa miaka miwili kumkosoa au kumpa maagizo wakati yeye mwenyewe hakuwa na uwezo wa kufanya kazi hizo vizuri.

Mara nyingi zaidi kuliko hivyo, Juma aliiga tu miundo kutoka kwa wabunifu wengine. Mtindo huu wa kufanya kazi unaweza kutumika kwa miundo ya kawaida ya mambo ya ndani, lakini hakuwa na sifa za kushughulikia miradi mikubwa kama hiyo.

Lisa alipendekeza kwa upole baada ya kufikiria hili. “Mkurugenzi Zayumba, nadhani ni bora kama mimi na Juma tukafanya kazi kwa kujitegemea. Baada ya yote, kila mbunifu ana mawazo tofauti na kufanya kazi pamoja kunaweza kusababisha migogoro. Mbali na hilo, sisi bado ni vijana, kwa hivyo ushindani unaweza kutupa msukumo mpya.”

Zayumba alikaa kimya kana kwamba anazingatia pendekezo hilo. Kwa upande mwingine, Juma alichukua wazo hilo kama tusi la kibinafsi. "Unamaanisha nini? Unafikiri wewe ni bora kuliko mimi—”

“Hapana, ninapendekeza ushindani wa haki.” Lisa alijibu.

"Wewe ni mdogo kwangu kwa miaka michache na huna uzoefu. Badala ya kujifunza kutoka kwa mkubwa wako, unajifanya uko juu sana na unajiamini kupita kiasi katika uwezo wako.” Sauti ya Juma ilikuwa kali. "Siku 15 hazitoshi kwa mradi mkubwa kama huu. Sio tu kwamba unakataa kunisaidia, lakini pia ungependa kuunda muundo wako mwenyewe. Je, kujionyesha ni muhimu kwako kuliko mafanikio ya kampuni?”

Lisa akavuta pumzi ndefu. "Ni kweli kwamba mimi ni mdogo kwa miaka michache, lakini nimeshiriki katika miradi kadhaa mikubwa kama hii hapo awali. Isitoshe nilisoma ng’ambo—”

Kingo za midomo ya Juma zilibadilika na kuwa tabasamu la kejeli. “Kwa hiyo kama umesoma nje ya nchi itakuwaje? Je, kuzungumza lugha ya ziada kwa namna fulani hukufanya uwe wa pekee zaidi? Usingejiunga na kampuni yetu ndogo kama una uwezo kama unavyodai. Tuonyeshe ushahidi badala ya kupiga tarumbeta yako mwenyewe. Pia naweza kudai kuwa nilishiriki katika kubuni Ikulu ya Chamwino, una ushahidi gani?.”

"Nimesema kwamba hii inapaswa kuwa mashindano ya haki kulingana na uwezo."
Lisa aligeuka kumtazama bosi wao. “Mkurugenzi Zayumba, mimi ndiye niliyekupatia nafasi ya kushiriki katika zabuni. Hata hivyo, siku 15 baadaye, unaweza kuchagua mchoro wa muundo unaopendelea zaidi. Ninaamini hukumu yako na sitakuwa na pingamizi lolote juu yake.” Sentensi ya mwisho iliyosemwa kwa heshima ya kweli ilimfurahisha Erick Zayumba.

“Sawa, hiyo inatosha. Masudi, angalia sauti yako. Miss Jones sio msaidizi wako hata hivyo.” Mkutano ulimalizika kwa maelezo hayo. Mkurugenzi Zayumba kisha akatoka chumbani.

Baada ya tukio hili, Juma aliichukua kama dhamira ya kibinafsi ya kumdhihaki na kumdharau Lisa katika kila nafasi inayowezekana. Lisa hakusumbuliwa na mwanaume huyo hata kidogo. Uwezo wake haukuweza kulinganishwa na wake katika miaka milioni.

Katika siku 15 zilizofuata, Lisa alijikita kabisa katika mchakato wa kubuni wa kituo hicho.Wakati fulani, Alvin alikuwa anaamka katikati ya usiku na kuona chumba chake bado kina mwanga. Duru za giza chini ya macho yake kila asubuhi pia zilizidi kuonekana. Hakutoa maoni yake juu ya hilo. Baada ya yote, ilikuwa vizuri kwamba mwanamke kijana alikuwa na nia ya kupigana. Roho hiyo ya mapigano ndiyo iliyomfanya Alvin afikie mafanikio hayo.

Tarehe ya mwisho ilifika kwa kufumba na kufumbua. Alvin alirudi nyumbani baada ya kukaa siku nzima kupinga kesi. Aliona tabasamu la kung'aa ambalo lilimulika usoni mwa Lisa.

“Imekamilika?” Aliuliza Alvin.

“Ndio, huu ni mchoro wangu. Nijulishe unachofikiria.” Lisa alifungua laptop na kutoa.
Furaha ya kuridhka ilienea kwenye macho ya Alvin. Kwa mtazamo wa kwanza, alihisi kana kwamba alikuwa akisafiri kupitia handaki la angani lililozingirwa na mwanga wa nyota unaong'aa.

Alianza kuelezea dhana nyuma ya muundo wake. "Mchoro huu unaitwa 'Jicho la Ulimwengu'. Angalia, hufikirii kwamba nebula nyingi hapa zinafanana na jozi za macho yanayopepesa? Ninaamini lengo kuu la safari yetu ya baadaye liko katika ulimwengu wa baadaye. Hapa kuna Ulimwengu wa Dimensional wa Nne, iliyoundwa kwa mtindo wa…”

Alvin alisikiliza kwa makini alipokuwa akifafanua maelezo kwa uhakika. Macho yake yalibaki kutulia kama maji japo kwa siri alitawaliwa na mshangao kwa ndani.
Ubunifu huo kwa uhakika ulifaa kabisa kwa muundo wa mambo ya ndani wa kituo cha Taifa cha Teknolojia na Utamaduni.

Hakika, hapo awali Alvin alikuwa amemdharau Lisa. Hakutarajia binti aliyezaliwa katika familia bora kama yeye angejua mengi kuhusu kubuni., lakini, utendaji wake ulizidi matarajio yake. Alikuwa bora zaidi kuliko wabunifu wengi maarufu ambao alikuwa amefanya nao kazi hapo awali. Lisa alikuwa na talanta sana katika uwanja huo. Kulikuwa na haiba isiyoelezeka alipokuwa amejikita katika kazi.

"Nini unadhani, unafikiria nini?" Lisa alipepesa macho kwa shauku baada ya kutambulisha muundo huo. Kung'aa kwa macho yake kulionyesha kuwa hakika alikuwa akivuna pongezi.

“Inaridhisha,” Alvin alisema kwa upole, akijifanya haoni msisimko machoni mwake.

Kwa kusifiwa na Alvin, Lisa alipiga kelele kwa furaha utadhani alikuwa tayari kishashinda. “Unadhani nina nafasi?” Aliuliza Lisa.

“Usijiamini sana. Daima kuna mtu mwenye talanta bora zaidi huko nje." Alvin alipunguza shauku ya Lisa.

Lisa alichanganyikiwa kwa kutopokea sifa alizotarajia. Ilionekana kama mwisho wa mazungumzo. "Hakika nitashinda hii." Alifunga kompyuta yake kabla ya kugeuka na kuondoka, akizungusha nywele zake kama mkia wake wa farasi kwa fahari hewani. Hakujua kwamba Alvin nyuma yake alikuwa akitabasamu kwa furaha kutokana na kufurahishwa na kazi yake.

SURA YA20

Siku iliyofuata, Mkurugenzi Zayumba hakuweza kuacha kutabasamu wakati Lisa alipomuonyesha mchoro wake. Aliamua kuendelea na mchoro wake hapo hapo. Uso wa Juma Masudi ulikuwa mwekundu kwa hasira. Aliinamisha kichwa chake chini ili wengine wasitambue uchungu wake.

Siku ya zabuni. Lisa alienda haraka eneo la tukio. Alipofika, alimwona Lina na timu yake wakishuka kwenye gari la kampuni. Kivimbe kilijitengeneza kooni mwa Lisa. Ilikuwa ni hisia ya ajabu kuona sura zilizozoeleka na kiongozi wao mpya. Wale watu waliokuwa wakifanya kazi pamoja naye sasa walikuwa wakimfuatilia kwa karibu Lina. Walitupa macho yaliyojaa dharau na kejeli kwa Lisa.

"Halo, tazama, ni mbunifu mkubwa, Lisa Jones. Umefukuzwa kwenye nafasi yako lakini bado unajitokeza kwa ajili ya zabuni, ujasiri gani?” James alisema kwa dhihaka.

“Niko hapa kama mwakilishi wa kampuni ninayofanyia kazi kwa sasa,” Lisa alijibu kwa upole. "Cheka yote unayotaka, lakini unapaswa kujua uwezo wangu."

“Uwezo?” James alidhihaki. "Ulipata nafasi kwetu kwa sababu ya bosi Masawe. Wewe si kitu tena baada ya kuondoka Kibo Group.”

“Binamu usiseme hivyo. Yeye ni dada yetu, hata hivyo,” Lina alisema kwa mzaha, “Lisa , unawakilisha kampuni gani leo? Tunaweza kuwa wapinzani, basi.”

"Wewe ndiye mbunifu wa Kibo Group?" Lisa aliishiwa nguvu. Jones masawe alimdekeza sana binti huyu kiasi cha kumpitishia mradi. Lina alianza tu kujifunza kubuni chini ya nusu mwaka uliopita. Angewezaje kuwa na uwezo kweli wa kushiriki mpaka zabuni?

"Hiyo ni sawa. Nilitengeneza mchoro mzima peke yangu." Hisia ya ajabu ilijidhihirisha katika moyo wa Lisa baada ya kuhisi tabasamu la maana lililotapakaa usoni mwa Lina.

"Sina imani na msimamo wako wa maadili." Alidhihaki huku akidhani labda Lina alichukua kazi ya mtu mwingine.

“Lisa, najua una wivu kwamba mimi na Ethan tunachumbiana, lakini hupaswi kunidhalilisha kila tunapokutana, hiyo si haki.” Lina alisema kwa sauti iliyojaa malalamiko.

"Lisa , wewe ni mtu mbaya sana," James naye alimtukana.

"Nyie ni kundi la vichaa." Lisa hakuweza kuhangaika kuendelea kubishana nao. Aligeuka kwa nia ya kuondoka.

“Simama hapo hapo. Huwezi kuondoka bila kumuomba msamaha Lina,” Juma alifoka nyuma yake.

“Acha aende, usihangaike naye. Hawezi kushinda hata hivyo.” Lina alimpotezea.

Lisa akaongeza mwendo. Alikuwa karibu kupoteza akili yake kukabiliana na mwanamke huyo mnafiki. Lina alipaswa kujiunga na tasnia ya burudani kutokana na kipaji chake cha asili katika uigizaji, na siyo tasnia ya ujenzi. Hakika aliingia kwenye tasnia ya ujenzi kwa bahati mbaya.

Lisa alikusanyika pamoja na mkurugenzi Zayumba na wengine kwenye ghorofa ya pili. Zamu ya kuwasilisha ubunifu wao ilikuwa ni baada ya Kibo Group. Lisa hakuwaza sana. Baada ya yote, alijiamini sana na uwezo wake.

Muda wa zabuni kuanza ukawadia. Mtu wa kwanza ambaye alionyesha dhana yao alikuwa mwakilishi kutoka kampuni ya samani za nyumbani. Lisa aliona kwamba Mzee Kamote wa kamati ya maandalizi aliitikia kwa kichwa tu bila kuonyesha kupendezwa sana. Makampuni mengine matano ya kubuni mambo ya ndani yaliwasilisha baada ya hapo.

Michoro yao haikuwa mibaya lakini haikuvutia kwa namna yoyote ile. Halafu ikaja zamu ya Lina akiwa kama mwakilishi wa Kibo Group. Alikuwa amevalia suti nadhifu ya rangi ya hudhurungi. Kwa mbali alikuwa mbunifu mdogo zaidi kati ya wote ambao walikuwa wamekwisha wasilisha mawazo yao kwenye jukwaa. Watazamaji walionyesha dharau kwenye nyuso zao kwa sababu ya umri wake mdogo. Lakini, wakati alipoonyesha muundo wake, kila mtu alishangaa.

Lisa aliruka kutoka kwenye kiti chake, akiwa amejawa na mshangao. Hii ilikuwa kazi ambayo aliitengeneza baada ya nusu mwezi wa kukosa usingizi usiku. Iliangukiaje mikononi mwa Lina? Alikunja ngumi kama mipira, macho yake yakiwa yanawaka moto mkali.

“Haya, yule aliye mbele, tafadhali unaweza kukaa chini? Unatukinga kuona vizuri." Mtu mmoja kutoka kampuni nyingine alipiga kelele nyuma yake, akiwa amekasirika.

Ni kana kwamba hakuweza kusikia lolote kati ya hayo. Macho yake yalibaki yakimtazama Lina kimauaji. Mwishowe Lina alimwangazia Lisa tabasamu la ucheshi kutoka kwenye jukwaa kabla ya kuendelea kuelezea dhana hiyo. "Huu ni Ulimwengu wa Dimensional wa Nne ambao nilibuni. Ni ulimwengu wa ajabu, ambao haujagunduliwa…”

Macho ya Mzee Kamote sasa yalikuwa yakimetameta kwa uzuri, na hata wengine miongoni mwa watazamaji walianza kutoa pongezi zao. "Msanifu huyu kijana kutoka Kibo Group anavutia sana. Sio mbaya."

"Nilisikia kuwa ni binti mkubwa wa Jones Masawe, mkurugenzi wa Kibo Group.”

“Kweli? Ni kweli ana talanta na anajua. Hakika atakuwa mbinifu wa hatari sana akipata uzofu.”

Lisa alimkatisha kwa sauti kubwa kwani hakuweza kuvumilia zaidi. "Utataja Jicho la Ulimwengu na Ligi Ishirini Elfu Chini ya Bahari? Pamoja na maeneo ya utafiti wa kitaaluma na nafasi za kubadilishana kisanii kwa kutumia teknolojia za hali ya juu kama vile kuta za pazia za umeme, maji baridi ya mito na mifumo mipya ya taa ya LED?"

Kimya cha kikuu kilifunika ukumbi. Lina alisitisha hotuba yake na kumtazama Lisa kwa uso wa mshtuko."Unajuaje maelezo ya dhana yangu?"

Lisa alicheka, damu yake sasa ilikuwa inachemka chini ya ngozi yake. "Hii ni miundo na dhana zangu. Umeiba kila undani wa mawazo yangu. Hivi ndivyo kampuni yako kubwa inavyofika kileleni mwa tasnia, kwa kuiba kazi za watu wengine?”

"Unasema aliiba dhana yako?" Mzee Kamote alikunja uso.

"Huu niubunifu wangu. Nina ushahidi kwenye laptop yangu pia. Nimetumia kiasi kikubwa cha muda na juhudi kuweka mawazo haya katika michoro, hata kuanzisha mchoro wa karatasi kutoka mwanzo. Nina mchoro yote kuanzia mwanzo." Lisa alijitetea.

"Nionyeshe." Mzee Kamote alimwambia mara moja.

Lisa alichukua laptop yake mara moja, lakini kwa mshtuko mkubwa, hati zote zilikuwa zimepotea. Alishindwa kupata michoro ya awali aliyoiweka kwenye mkoba wake pia. Kwa kasi ya umeme, aliinua kichwa chake kuelekea kwa Juma ambaye alikuwa amesimama karibu. "Umefuta hati zangu?" Hakuweza kufikiria mtu mwingine yeyote isipokuwa mtu huyu.

“Umerukwa na akili? Mimi ni mwenzako.” Juma akasimama kwa hasira.

Lina ambaye bado alikuwa amesimama kwenye jukwaa alisema kwa sauti ya ukali, “Lisa , inatosha. Tunaweza kutatua mzozo wetu wa kibinafsi wakati mwingine, lakini huu ni wakati muhimu kwa Kibo Group. Tafadhali usiniaibishe mbele za watu kwa ushuhuda wa uongo.”

Mzee Kamote ambaye ndiye msimamizi mkuu wa zabuni ile, alionekana kufadhaika. "Nyinyi wawili mnajuana?"

Lina alijibu kabla Lisa hajapata nafasi, “Ni dada yangu mdogo. Mambo yamekuwa magumu kati yetu kwa sababu ya mambo fulani ya kifamilia…”

James alipiga ngumi mezani huku akinyanyuka kwenye kiti. “Lina, si lazima umyamazie kila wakati. Anajaribu kuharibu sifa yako ili aweze kurithi biashara ya familia ya Masawe. Mwanamke huyu katili lazima awe ameangalia mipango yako ya muundo.”

"Sikweli." Hasira ndani ya Lisa iliwaka kama moto wa petroli.

“Basi tuonyeshe ushahidi wako. Sasa unawashtaki wengine bila ushahidi thabiti. Unajua Lina amemwaga damu na jasho kiasi gani katika mradi huu? Na bado una ujasiri wa kumlaumu?”

Juma Masoud alisimama ghafla. “Lo, si ajabu michoro uliyotuonyesha ilikuwa bora kuliko yangu. Ni kwa sababu umenakili kazi ya mtu mwingine. Inavyoonekana, bado unafanyia kazi Kibo Group. Mkurugenzi Zayumba, mwanamke huyu anatudanganya.”

Zayumba ni dhahiri hakufurahishwa. "Lisa Masawe, wanasema ukweli?" Kwa uaminifu wote, hakuamini Lisa angeweza kuja na kazi ile ya kuvutia peke yake, kutokana na umri wake mdogo.

"Mkurugenzi Zayumba, huoni kwamba Juma amehongwa?" Lisa alijitetea kinyonge.

Juma alijieleza kwa haraka, “Sijuani na mtu hata mmoja anayefanya kazi Kibo Group. Bosi Zayumba, nimekuwa nikifanya kazi nawe kwa miaka mingi sasa. Si unajua mimi ni mtu wa aina gani?”

“Sawa, nimesikia vya kutosha. Siwezi kumudu kupoteza zaidi heshima yangu hapa.” Erick Zayumba alisimama kwa urefu wake wote akionekana kuhuzunika. "Hatujahitimu kushiriki katika zabuni hii. Lisa Masawe, wewe si mfanyakazi tena wa kampuni yetu.” Kisha, akaondoka pamoja na Masudi.

Jeuri ikajaa machoni mwa James. “Hata watu wa kampuni yako hawako upande wako. Sifa yako lazima iwe mbaya."

"James, Lina, kumbukeni kwamba kila kitu mlichonifanyia kitawarudia." Lisa alipoteza utulivu wake. Alichukua chupa ya maji na kuwarushia.

Mzee Kamote alikasirika sana. “Mtoeni hapa. Walimruhusuje mtu wa aina hii kwenye zabuni mwaka huu?”

.....ITAENDELEA.....

Unafikiri nini kitafuata hapo maana mambo ni moto mambo ni fire, lakini sina cha kusema nikuombe tuungane pamoja katika sehemu inayofuata ya mkasa huu wa kusisimua unaokwenda kwa jina la LISA.
LIPIA USOME HARAKA.

Vitabu vinazidi kuandikwa na baadhi vimekamilika lakini pia unaweza kusoma kwa kulipia kulingana na episode unazotaka.

Episode - 20 Tsh 1000/=
Episode - 30 Tsh 1500/=
Episode - 40 Tsh 2000/=
Episode - 50 Tsh 2500/=

Namba za kulipia

0628924768
(Halotel) JUMA HEMBA
0694288555 (Airtel) JUMA HEMBA
0764736557 (Voda) HADIJA KIRUNGI

"Lipia utumiwe similizi yako sasa whatsapp 0628924768"

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
JINA LA SIMULIZI............................LISA
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP..........................0628924768
SEHEMU YA....................................21&22

SURA YA 21

Punde, walinzi wawili waliingia ndani na kumchukua Lisa kwa nguvu. Mvua kubwa ilikuwa ikimiminika nje. Lisa alisukumwa kwenye mvua na walinzi bila huruma. Maji ya mvua yalimwagika bila huruma kutoka juu, yakamlowanisha kabisa kutoka kichwa hadi miguu.

Moto uliokuwa ukiwaka ndani yake ulizimwa na mvua ndani ya sekunde chache. Kilichochukua nafasi yake ilikuwa ni manung'uniko na huzuni. Hakuelewa. Je, kwa namna fulani alimkosea nini Lina katika maisha yao ya zamani?

Lisa alikuwa ametumia bidii sana kuanza upya. Lakini, Lina aliendelea kumlenga mara kwa mara, hata kumharibia sifa katika tasnia ya usanifu wa mambo ya ndani. Ni nani mwingine ambaye bado angethubutu kumwajiri wakati ujao?

Milango ilifunguka baada ya muda fulani. Lina alimsogelea Lisa huku akijikinga na mvua chini ya mwavuli. Sura ya uvivu ilioshwa juu ya uso wake. “Lisa , asante sana. Muundo wako umenipatia nafasi ya kushinda mradi huu. Una talanta kweli."

Lisa aliinua kichwa chake, macho yake yakiwa yamewaka moto. Lina akatabasamu. “Usikasirike sana. Mradi ungekuwa wangu hata kama nisingetumia ubunifu wako. Ethan alikuwa tayari ametengeneza mazingira ya ushindi. Labda hujui kwamba mjomba wake ni rafiki mzuri wa mzee Kamote? Ubunifu wako ulikuwa kielelezo tu cha mpango huo."

‘Mjomba wa Ethan? Alvin si ndiyo mjomba wake Ethan? Alikuwa na maana gani?’ Lisa alijiwazia.

Lisa alihisi kana kwamba mnyama wa porini alikuwa akipasua moyo wake vipande vipande na makucha yake makali. Upumuaji wake ukawa wa kusuasua. Alikuwa amemshukuru kwa dhati Alvin kwa kumpigania kupata nafasi.

Hakujua kwamba tayari alikuwa ameamua mwisho kabla. Kwanini alimdanganya hali alijua ni juhudi gani alikuwa amemimina katika mradi huo? Macho yake yaling'aa, lakini hakuweza kujua ikiwa ni kwa sababu ya mvua au machozi yake mwenyewe.

Kwa kawaida Lina alijivunia kuteseka kwa Lisa. "Ni aibu hakuna mtu katika tasnia atakayekuajiri tena baada ya kugundua tabia yako mbaya. Maskini. Lakini usijali, nitawatunza wazazi wetu vizuri. Niachie mimi nisimamie Kibo Group na kumlinda Ethan.” Lina akacheka tena kwa dharau. "Kusema kweli, Ethan anafikiria vibaya sana juu yako. Ana aibu baada ya kukuona ukitoa vipeperushi mitaani. Aliniambia kuwa wewe hukuwa mchumba sahihi kwake.”

"Lina, nimekukosea kitu gani?" Akiwa amehuzunishwa, Lisa alipoteza hatua ya mwisho ya kujizuia. Alimrukia Lina akamtupa chini na kumkaba kooni. Lina hakuonekana kufadhaika bali alidhihirisha tabasamu la fumbo.

Kabla Lisa hajaelewa maana yake, nguvu kali ilimchuna mgongo wake na kumtupa kwenye dimbwi lenye tope. Aliinua kichwa chake na kumuona Ethan akiharakisha kumsaidia Lina kusimama. Kisha akavua koti lake na kumfunika Lina.

“Sijambo, lakini usijali sana kuhusu Lisa, ana hasira. Amevunjika moyo kutokana na kupoteza zabuni.” Lina alitetemeka katika kumbatio la Ethan.

“Mbona bado unamjali?” Ethan alimkazia macho Lisa aliyekuwa pale chini huku akiwa amebana meno. “Angalia umegeuka kuwa nini. Huna moyo hata unamdhulumu dada yako mwenyewe. Siamini kabisa kuwa nilikuwa nakupenda.”

Uhusiano walioujenga tangu utotoni ulivunjwa kabisa wakati huo. Lisa alimkazia macho usoni. Hakuweza hata kutambua kwanini hakuzijua rangi zake halisi mapema. “Ndio hivyo, najuta kwamba nilikuwa nakupenda pia. Lazima nilikuwa kipofu.”

“Thubutu kusema hivyo tena.” Ethan alikasirishwa na maneno yake. "Si tu kwamba umevunja sheria za zabuni lakini pia huwezi kutofautisha mema na mabaya!"

Lisa alipiga kelele juu nusura mapafu yake yapasuke. “Unafikiri anaweza kuja na ubunifu huo kutokana na uwezo wake mdogo? Labda ulijua tangu mwanzo lakini uliamua kumkinga hata hivyo. Sijali kama unampenda ila kwanini mniangushe ili nisipate mafanikio, enyi wapenzi msio na haya!”

"Chunga mdomo wako." Ethan alimpiga kofi usoni, na kumfanya Lisa kuyumbayumba na kushuka chini tena.

Shavu la Lisa lilikuwa linamuunguza, lakini maumivu ya shavuni hayakuwa kitu ukilinganisha na yale aliyokuwa akiyasikia ndani kabisa ya moyo wake. Yule mwanaume aliyeahidi kumtunza milele alikuwa wapi?

Yule mtu aliyesema hana hisia na mwanamke mwingine alikuwa wapi? Yule mwanaume aliyemsihi amsubiri siku chache zilizopita alikuwa wapi?Kwa bahati nzuri, hakuamini maneno yake. Hakuwa na ujasiri wa kufanya hivyo.

Ethan alikodoa macho. Akimtazama Lisa aliyekuwa anagalagala kwenye tope na kuzidi kumkandamiza kwa maneno ya kumuumiza zaidi. “Usifikiri kwamba kila mtu ni mbaya kama wewe. Ninajua kwa kweli kwamba Lina alikuwa amekesha usiku mwingi ili kubuni muundo huu. Ndio, alianza kujifunza, lakini ana talanta. Kila kitu kilichotokea leo ni bahati mbaya uliyojitakia. Tambua kosa lako na uanze upya kabla haujachelewa.”

Kwa hayo, Ethan alimchukua Lina kwenye mikono yake na kutembea kuelekea kwenye Lamborghini. Wakati gari lake lilipotokomea mbali likimuacha nyuma kwa mara ya pili, Lisa alipoteza matumaini kabisa kwa mtu huyo. Kuanzia wakati huo, upendo wowote aliohisi kwake hapo awali ulibadilishwa na chuki na dharau.

"Oh, maskini wewe." James alimsogelea huku akiwa ameshika mwamvuli, akitabasamu akiwa amekazia macho. "Binti mdogo wa familia ya Masawe ambaye hapo awali alikuwa juu ya kila mtu sasa amepoteza nguvu zake zote."

Akiwa amechoka, Lisa hakuweza kujisumbua kukabiliana na mwanaume huyo. Akaanza kuliendea gari lake kimya kimya.

Sauti ya James ilisikika nyuma yake. “Mjomba Masawe na Aunt Masawe bila shaka wameshafahamu kuhusu tukio la leo. Ni dhahiri kwamba wanampendelea Lina kuliko wewe. Usiwe na ndoto ya kurudi kwa familia ya Masawe tena kwa sababu hakuna mtu huko anayekaribisha uwepo wako.”

Slam! Lisa alifunga mlango na kuondoka bila kumjali kabisa mtu huyo. Maneno yake hayakuwa habari ngeni kwake. Maisha yake yalikuwa duni vya kutosha. Hakuna aliyempenda wala kumjali kwelikweli.

SURA YA 22

Saa kumi na mbili za jioni, Alvin alirudi nyumbani kutoka kazini. Hapo awali, hata kama Lisa alikuwa ametingwa muda huo, nyumba hiyo ilikuwa na mwanga mkali kila wakati na kujazwa na harufu nzuri. Daima angeweza kumuona akizunguka jikoni kwa bidii akitayarisha chakula cha jioni. Lakini siku hiyo, hata hivyo, kulikuwa na giza tu.

Aliwasha taa na kumkuta Lisa akiwa amejikunyata kwenye kochi. Nywele zake zilikuwa zimevurugika na macho yake yalionekana kuwa na huzuni. Aliegemeza kidevu chake juu ya kichwa cha Charlie huku akimshika paka karibu na mikono yake. Alionekana kukosa uhai na raha ya maisha. Kwa kuwa daima alikuwa akionekana mwenye nguvu na mng'ao mbele yake, Alvin alihisi ajabu kidogo kuona upande wake huo ambao hakuwahi kuuona.

"Zabuni haikuenda vizuri?" Alvin alivua koti lake na kulitupia kwenye kochi kama kawaida. "Kushindwa mara moja sio jambo kubwa. Bado wewe ni kijana—”

“Ninastahili kudanganywa kama mpumbavu kwa sababu mimi ni kijana?” Lisa alipandisha hasira. "Watu kama wewe ambao wako juu ya jamii hawajali hata kidogo kuhusu hisia za watu wengine wa chini, sivyo?" Lisa aliamini kuwa Alvin alikuwa amempendelea mpwa wake Ethan kupata nafasi ya zabuni kwa ajili ya Lina.

Dokezo la kero lilimwangazia usoni mwake. Alvin alidhani mwanamke aliyekasirika alikuwa akimalizia hasira yake kwake. "Kwa tabia hii, ulistahili kushindwa."

“Hiyo ni kweli, mimi ni mtu aliyeshindwa. Kushindwa kwangu kikubwa ni kukuamini.”
Lisa alikunja ngumi. Ingawa ilikuwa wazi kuwa hakumpenda, alikuwa mke wake kwa sheria angalau. Hata hivyo, alikuwa amemdanganya kama mjinga.

"Usiuume mkono unaokulisha." Alvin alikasirishwa na maneno yake. “Hata usingepata nafasi ya kushiriki katika zabuni kama nisingekupa shavu. Ikiwa ningejua hivi ndivyo ungefanya, basi bila shaka nisingejisumbua.”

"Asante sana. Nakuomba uachane na mambo yangu siku zijazo.” Alicheka huku akisimama. Charlie akaruka kutoka kwenye kumbatio lake. Paka alihisi hali ya wasiwasi kati ya wamiliki wake wawili na akaamua kwenda kujibanza kwenye kona.

Hakuwa na hasira tu na mtazamo wake bali pia alikatishwa tamaa kikweli. Hapo awali, baada ya kuona miundo yake, alidhani alikuwa na talanta kweli. Lakini, watu wengi katika ulimwengu huu wamezaliwa na talanta, kwa hivyo kungekuwa na mtu bora na hodari huko nje kila wakati. Kushindwa mara moja kulitosha kwake kuona rangi zake halisi. Kusema kweli, aliwadharau watu kama hawa.

“Kumbuka ulichosema. Kuanzia leo, mbali na kumtunza Charlie, sitaki chochote cha kufanya na wewe. Sio lazima kunipikia pia. Itanifanya niwe mgonjwa tu.” Kisha, akamchukua paka kwa mkono mmoja, akashika koti lake na mwingine, na kuondoka nyumbani.

Kimya cha kutisha kilitanda nyumba. Alikuwa amemkumbatia paka kupata joto ili kuufariji moyo wake baridi mapema lakini na yeye alikuwa ametoweka pia. Akili ya Lisa ilimtoka. Jua polepole lilififia gizani. Alitoka nyumbani na kuelekea baa.

Mhudumu alimletea chupa kadhaa za bia. Alitoa kizibo kutoka kwenye chupa mojawopo na kuanza kuchukua mikupuo mikubwa. Hakuwahi kupenda kunywa hapo awali. Ni kwa wakati huo tu ndipo alipogundua faida ya kuzima huzuni ya mtu kwa pombe.

Aliwatupia macho vijana waliokuwa wakicheza kwenye jukwaa lililokuwa karibu naye alipokuwa akinywa, akiwaza jinsi maisha yake yalivyokuwa rahisi zamani. Maisha bila wasiwasi na kila mtu kando yake. Hatua kwa hatua, maono yake yalianza kufifia.

Hakumwona mtu aliyekuwa akimwangalia kwa karibu kutoka kwenye kona. Muda mfupi baadaye, mtu huyo alipiga simu. "Janet, unadhani nimemwona nani?"

"Nani?"
"Lisa Masawe! Anakunywa peke yake kwenye baa. Ah, yeye bado ni mrembo kama zamani.

Janet alishtuka papo hapo. "Utani huo!"

Janet hakusahau fedheha aliyopata kwa kutupwa nje ya mgahawa mara ya mwisho. Tukio hilo lilimfanya awe kicheko kati ya marafiki zake. Alifurahi kusikia kuhusu kilichotokea katika hafla ya zabuni siku hiyo. Hata hivyo, hiyo haikutosha. Alitaka kumwangamiza kabisa Lisa. Kidogo hakutarajia fursa hiyo kumwangukia kwa wakati muafaka.

"Zakayo, bado unavutiwa naye?" Janeth alimuuliza jamaa huyo.

“Si sana, lakini siku zote amekuwa akinidharau tulipokuwa shuleni. Ninatamani sana kuona jinsi alivyo tu.” Zakayo alisema kwa ukali, “ili awe na heshima kwangu.”

"Hakika, nitakupa nafasi." Janet akamwambia mpango wake. Mawimbi ya shauku yalipita ndani yake kama mkondo wa maji. “Una uhakika kuhusu hili—”

“Usijali, nitakuunga mkono. Lisa hana mtu wa kumtetea upande wake sasa. Ikiwa kitu kama hiki kitatokea, familia ya Masawe itakuwa na hamu zaidi ya kukata uhusiano naye.” Janet alimhakikishia.

“Amekwisha, basi nitaimba vizuri usiku wa leo.”Zakayo aliachia tabasamu baya la uchu huku akitazama sura ya mrembo huyo.

Lisa alikuwa amelewa sana wakati huo. Alikumbuka bila kufafanua kuona mhudumu akimkaribia na pombe nyingine. Hakuweza kukumbuka kama alikuwa ameiagiza, lakini glasi yake ilikuwa tupu hivyo alikunywa cocktail bila kusita. Muda si mrefu, alianguka kwenye kochi akiwa amefumba macho

....ITAENDELEA....

Unafikiri nini kitafuata hapo maana mambo ni moto mambo ni fire, lakini sina cha kusema nikuombe tuungane pamoja katika sehemu inayofuata ya mkasa huu wa kusisimua unaokwenda kwa jina la LISA.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
JINA LA SIMULIZI............................LISA
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP..........................0628924768
SEHEMU YA....................................23&24

SURA YA 23

Ndani ya jumba la kifahari la Sam, paka Charlie alikuwa amejikunja karibu na kiti. Alvin akajaza bakuli lake na samaki wadogo. Paka alikula mara kadhaa kabla ya kugeuka kwa dharau. Sam alidhihaki. "Paka wako ana maringo sana. Samaki huyu ni maalum katika nyumba yangu."

"Inamaanisha wapishi wako sio wa kiwango." Alvin naye alikuwa amejisevia kipande cha kuku lakini ghafla akakosa hamu ya kuendelea kula. Alikuwa amezoea kula vyakula vya Lisa vilivyopikwa nyumbani. Vyakula hivyo vilivyowekwa mbele yake vilikuwa na ladha ya takataka ikilinganishwa na chakula alichotengeneza Lisa.

“Unapaswa kurudi nyumbani kwa chakula cha jioni, basi,” Sam alisema kwa hasira, “Milo yako iliyopikwa nyumbani ndiyo bora zaidi. Nenda nyumbani kwako ukamwambie Lisa akuandalie chakula.”

“Usimtaje tena huyo mwanamke.” Uso wa Alvin ulianguka.

"Alikukosea nini tena safari hii?" Sam alikumbushwa kitu ghafla. "Leo ilikuwa siku ya zabuni, sivyo?"

"Nilisema, usimtaje," Alvin alionya.

Sam alishika midomo yake bila kutoa maoni zaidi. Alifikiria kwa muda huku akimkazia macho Alvin. Sahani yake iliyokuwa kwenye meza ilibaki vilevile bila kuguswa.

Sam aliachia tabasamu kisha akamwambia Alvin. “Unajua nilikutana na nani kwenye hoteli ya Sleep Way hapo awali kabla ya mchakato wa zabuni? Mzee Kamote anayesimamia kituo cha Utamaduni na Teknolojia cha Taifa, Kelvin Mushi wa Golden Corporation na pia Ethan Lowe kutoka Lowe Enterprises. Nilisikia alikuwa anatoka na Lisa hapo awali.”

“Utaacha lini kumtaja huyu mwanamke?” Ni dhahiri Alvin alikasirika. Kusikia jina la mwanamke huyo kulipelekea damu yake kuchemka, hasa alipokuwa akihusishwa na mtu mwingine.

“Sikiliza.” Sam aliweka uso wake serious. “Ethan na Lina watachumbiana mwezi ujao, bila kusahau kwamba yeye ni mpwa wa Kelvin Mushi. Kibo Group ilikabidhiwa rasmi mradi wa kituo cha Utamaduni a Teknoloji cha Taifa kutokana na zabuni ya leo. Huoni kuwa kuna jambo fulani mara tu unapowaunganisha watatu hao pamoja?”


Alvin alikuwa hajui mtandao wa familia hizo, lakini kwa namna fulani alielewa picha hiyo sasa. "Kwa maana hiyo kamati ya zabuni ilicheza rafu?" Alvin alipandwa na hasira baada ya kumaliza kuzungumza. "Je, sikukuambia uhakikishe mchakato wa zabuni unafanyika kwa usawa na haki?"

Sam alionekana kukosa raha kidogo. "Hapo awali, nilimwambia mzee Kamote kutoa nafasi ya ushiriki kwa Imperial Design na kutekeleza shindano hilo kwa njia ya haki. Labda Mzee Kamote alidhani kwamba nilimwambia airuhusu kampuni ndogo kushiriki katika zabuni ili kupata umaarufu tu. Hakujua nia yangu ya kumtunza Lisa .”

Alvin akalipapasa paji la uso wake. Haikuwa ajabu Lisa aliondolewa licha ya muundo wake wa ajabu. Isitoshe, alionekana kushangaza mapema jioni ya siku hiyo.
Baada ya kuwaza kidogo, akatoa simu yake na kumpigia Hans, msaidizi wake. "Nisaidie kuangalia kilichotokea wakati wa zabuni leo."

Sam akamwambia, "Ninaweza kujua juu yake kwa urahisi kwa kuuliza sehemu."

Alvin akacheka. "Sina imani na wewe tena." Baada ya kutafakari, Sam aligundua kuwa suala hilo lilitokana na uzembe wake.

Papo hapo, simu iliendelea kutetema kwa sababu ya utitiri wa meseji za kikundi cha whatsapp. Baada ya kuzitazama meseji hizo, Sam akatikisa kichwa na kuhema. "Starehe zinawaponza sana mabinti wa siku hizi. Binti huyu anaonekana mzuri sana. Kwa bahati mbaya, tukio la aina hii likifichuliwa litamharibia kabisa sifa yake!”

Alvin hakuelewa kwanini Sam aliongea maneno yale lakini baadaye aligundua kuwa alikuwa akitazama picha ya mwanamke aliyelala kifudifudi kitandani kwenye simu yake. Kulingana na mgongo wa mwanamke huyo, ilionekana kuwa alikuwa na kiuno chembamba. Jinsi suruali yake ya jeans na shati ilivyoonyesha umbo lake ilimfanya aonekane mwenye kuvutia sana. Binti huyo alikuwa anarushwa kwenye video ya moja kwa moja kupitia youtube.

Alvin alikumbuka kuwa Lisa alikuwa amevaa vazi kama hilo jioni hiyo. Akashika simu. “Hii imetokea wapi?”

“Sina uhakika. Labda hoteli fulani. Kwa nini?”

Alvin aliinua kichwa chake na kumtazama Sam. "Huyu ni Lisa!"

Sam akashangaa. “Jamani. Imeelezwa hapa juu kuwa kutakuwa na video ya moja kwa moja Telegram ikimuonyesha anafanya mapenzi saa moja na nusu usiku, ni ndani ya dakika 15 tu kutoka sasa.

"Piga simu polisi sasa hivi." Alvin aliagiza kisha haraka akawasha kompyuta katika chumba cha maktaba cha Sam Ndani ya dakika moja, aliweza kufuatilia anwani ya IP ambapo Lisa alikuwa amefungiwa kwa ajili ya kurekodiwa.

Kwa bahati nzuri, hoteli aliyokuwaamefungiwa Lisa ilikuwa jirani sana na makazi ya Sam.
•••
Ndani ya hoteli, Lisa alikuwa na kizunguzungu na kichefuchefu sana. Alifumbua macho yake kwa dhiki, na kugundua kuwa alikuwa kwenye kitanda kikubwa cha ajabu. Alikuwa na hisia ya kuzama. Alitaka kuketi, lakini aligundua kuwa hakuwa na chembe ya nguvu.

“Acha kuhangaika.” Mwanaume mnene na mwenye nguvu alikuja akiwa amejifunga taulo tu mwilini.

Lisa alikaribia kutapika. Baada ya kumtazama kwa makini, alimkuta anamfahamu. “Wewe ni… Zakayo Tarimo?”

"Sikutarajia ungenitambua." Zakayo alicheka huku akiutazama mwili wake. “Ulikuwa na dharau kabisa kwangu enzi hizo, sivyo? Kwa muda mrefu nilitaka kukuharibia wewe binafsi.” Pamoja na hayo, akamshika.

“Potelea mbali!” Akiwa amejawa na karaha, Lisa alinyanyua miguu yake kwa shida kumpiga teke. Lakini, kwa sababu ya kukosa nguvu, alishikwa kirahisi na Zakayo.

“Tazama, watu wengi wanatutazama sasa kupitia Telegram." Zakayo alitumia nguvu zake zote kukokota miguu ya lisa na kuivuta mbele. Lisa hakuziona kamera mbili zilizowekwa pembeni ya kitanda hadi Zakayo alipomkumbusha.

Hali ya hofu na kufadhaika ambayo haijawahi kutokea ilimkumba. “Niache sasa, wewe mwanaharamu! Ninaweza kuwa katika hali ya aibu, lakini haimaanishi kuwa unaweza kunifanya chochote. Baba yangu na mama yangu hawatakuruhusu utoke salama.”

"Sahau. Wazazi wako watachukizwa na jinsi unavyoonekana sasa hivi.” Zakayo alimkandamiza mabega yake kwa nguvu zake zote, kisha akararua shati lake kwa nguvu.

“Msaada…” Lisa alipiga makelele bila mafanikio yoyote. Kwa nini ilimbidi Mungu amtendee hivi? Tayari alikuwa mnyonge sana. Alikuwa ametengwa na wapendwa wake na familia, na hata heshima yake ilikuwa ikivuliwa sasa.

Macho yalimtoka Lisa ghafla. "Sitakuacha hata kama nitakufa." Kisha akauma ulimi wake kwa nguvu. Zakayo alimpiga kofi zito sana hadi kichwa kikamzunguka. Ilimchukua muda mrefu kabla ya kupata fahamu zake.
Wakati huo, macho ya Lisa yalikuwa yamefifia. Ilionekana kana kwamba alikuwa amechanganyikiwa kwa kuhisi anapoteza roho yake.

Zakayo aliachia tabasamu la kinyama. “Hakuna mtu atakayekuja na kukuokoa. Afadhali unisikilize kwa utiifu.” Kabla hata hajamaliza, mlango wa chumba ulipigwa teke na kufunguka!

"Wewe ni nani?" Kwa hofu, Zakayo aliinuka haraka.

Alvin alihisi kutapika kwa kuuona mwili wake ulionona. Alipotazama kitandani, aliona uso wa Lisa ukiwa umejikunja na shati lake lililolegea lililochanika katikati. Kwa hasira, Alvin alimpiga Zakayo kwa nguvu usoni. "Mimi ni mtu anayekupeleka jela." Alvin alijibu swali lake la awali.

Ikizingatiwa kuwa Alvin alikuwa na nguvu na mkatili, Zakayo alipigwa chini kwa muda mfupi. Alvin alizitoa zile kamera na kumtupia Zakayo. Baada ya hapo, alivua suti yake na kumfunga kwa haraka Lisa aliyekuwa pale kitandani.

“Lisa, unajisikiaje?” Hakuthubutu kumgusa uso wake uliokuwa umevimba. Akampiga tu mgongoni.

“Usi… Usiniguse.” Lisa alikuwa bado ana kizunguzungu. Alipogundua kuwa mtu fulani alikuwa akijaribu kumgusa, midomo yake ilitetemeka bila kujua kama ishara ya kupinga. Machozi yalianza kumtoka pia.

“Usiogope. Ni mimi. Hakuna atakayekuumiza.” Akamgusa kichwa kwa upole.

Baada ya kunusa harufu laini ya kiume ambayo aliifahamu, mara alijisikia utulivu. Macho yake matupu yalionyesha polepole ishara ya kuelewa. Alianza kufahamu mtu aliyekuwa mbele yake ni nani. "Alvlisa, ninaota?" Alihisi mtu huyo alikuwa amekuja kumwokoa katika ndoto yake.

“Hii si ndoto. Utakuwa sawa.” Alvin alifuta machozi kwa upole kwenye pembe za macho yake.

Mara akasikia msururu wa shughuli nyuma yake. Alipogeuka tu, alimuona Zakayo akihangaika kuinuka kwa lengo la kukimbia kisirisiri. "Subiri hapa." Akamuweka Lisa chini kwa wepesi, kisha akamgeukia Zakayo. “Ulimfanya nini sasa hivi?”

Zakayo aliogopa sana hadi akaanguka magotini. Alipotaka kukimbia tu, kiti kilimgonga kwa nyuma. Hakuweza kunyanyuka hata kidogo. Kumuona yule mtu mrefu akimsogelea, Zakayo alishikwa na woga. Hakujua ni kwa nini nyuma ya Lisa kulikuwa na mtu mwenye nguvu kiasi hicho wakati Janet alimwambia kuwa Lisa hana msaada. “Sikumgusa. Ulikuja nikiwa namvua nguo, kweli. Naapa!"

"Ulimpiga, si ndiyo?" Alvin alimkokota Zakayo juu, kisha akainua mkono wake ili kumpiga kofi. Punde, uso mzuri wa Zakayo ulivimba kama mpira. "Ni asante kwako kwamba nilimpiga mtu kofi kwa mara ya kwanza." Alvin alimwachia Zakayo wakati maafisa wachache wa polisi walikuja kumkamata.

Lisa alikaa kitandani katika hali ya udhaifu huku akitazama hali ilivyokuwa. Alvin alipogeuka, alilazimisha tabasamu. Muda kidogo baadaye, alianguka na kuzirai. Alvin akambeba na kukimbilia nje.

Sam, ambaye alikimbilia pale muda huo, aliona hali hiyo na kupata mshtuko. "Yuko sawa?"

"Fuatilia kilichotokea usiku wa leo. Sitaki kumuona mtu huyo tena.” Alvin alipunguza hasira yake na kumpa Sam amri. Kwa hayo, alielekea hospitali haraka.

SURA YA24

Huko yumbani kwa familia ya Kileo, Janet Kileo alipoona kusitishwa kwa ghafla kwenye video ya moja kwa moja ya Lisa na Zakayo, alihisi kuchanganyikiwa. Mtu ambaye alionekana ghafla kwenye video hiyo ya moja kwa moja muda ule alionekana kuwa wa mtu wa ajabu ambaye alikuwepo katika Mkahawa wa Grapefruit siku kadhaa nyuma na kuwatetea kina Pamela na Lisa. Baadaye, alitafuta mtu wa kumchunguza mwanamume huyo na kugundua kwamba alikuwa ni wakili tu.

Wakati huo, simu yake ikaita. Mtu fulani alimpigia simu na kumwambia, “Bi Kileo, Zakayo amekamatwa na polisi.”

"Tafuteni njia ya kumdhamini." Janet alitoa agizo.

“Miss Kileo… naogopa hilo haliwezekani. Sam Harrison ameshika bango na kutuamuru tumfungulie Zakayo kesi ya ubakaji. Kwa ushahidi uliopo lazima Zakayo aende miaka 30 jela. Sam mwenyewe amesema atasimamia kesi hiyo.”

Moyo wa Janet ulishituka. "Sasa hakikisheni mnamuonya Zakayo afunge mdomo wake kwa ajili ya familia yake. Akinitaja tu mmwambie na baba yake atamfuata jela."

“Sawa.”
•••
Akiwa amelazwa hospitalini Lisa aliamka kwa sababu ya maumivu usoni mwake. Alifumbua macho, akajikuta yuko hospitalini. Alijiuliza ni nani aliyempeleka hapo. Huku akiwa ameduwaa, sura nzuri ya Alvin ilimulika akilini mwake.

“Umeamka,” Alvin alimuuliza.

Lisa alipogeuza kichwa chake, alimuona Alvin akinyanyuka kutoka kwenye kochi kwa sura iliyojiandaa kwa matusi. "Kama mwanamke aliyeolewa, ulienda kwenye baa peke yako kunywa pombe. Lisa huna akili.”

Mwanzoni, aliguswa kidogo. Kabla hata hajaongea, alihisi kama kamwagiwa ndoo ya maji baridi. Aliona aibu sana. “Uko sahihi. Karibu nisahau kuwa nimeolewa.”

Macho ya Alvin yalionyesha hasira. Wakati huo, yeye ndiye aliyekuwa ameungama kwake kwa hiari yake mwenyewe na kuendelea kumsumbua. Sasa, alidai kuwa amesahau kuwa alikuwa ameolewa. Alitaka nini kwenye maisha yake?

“Bado hujajifunza kosa lako. Laiti si mimi niliyefanikiwa kufika kwa wakati, ungekuwa umebakwa na heshima yako kuharibiwa milele. Ninajali heshima yangu hata kama wewe hujijali.”

“Usijali. Hakuna anayejua kama nimeolewa na wewe.” Lisa alikata tamaa sana. Alipojitokeza katika dakika ya mwisho, mwanzoni aliona mwanga wa matumaini, akifikiri kwamba anamjali. Aligundua kuwa kumbe alikuwa anajali utu wake tu.

Alvin alichukizwa na tabia yake. "Kweli, inaonekana kwamba nilikuwa mkarimu kupita kiasi. Sikupaswa kukuokoa, sivyo?”

Kwa jinsi alivyokuwa amechoka, Lisa hakutaka kubishana naye tena. Alifunga macho yake kimya. Akiwa ameshika blanketi, akalisogeza karibu na mwili wake na kujibanza mithili ya kware asiyejiweza.

Kuangalia uso wake uliojeruhiwa, Alvin alimhurumia sana. Hakuwa na uhakika ni nini kilikuwa kikimsumbua. Lisa alipokuwa amepoteza fahamu mapema, Alvin alihisi kutaka kumuua Zakayo. Sasa akiwa macho alitamani kumzaba kibao kwa kwa upumbavu wake uliomsababishia matatizo. Kumuona Lisa hatamki kusema neno lolote kwa wakati huo kulimfanya Alvin anyong'onyee.

Wodi ilikaa kimya kwa muda kabla ya Sam kuingia ndani. "Zakayo amekiri kila kitu polisi…” Usemi wa Sam ulikatika ghafla baada ya kuona hali tofauti mle ndani. Mmoja alikuwa amekaa kwenye sofa kwa utulivu, huku mwingine akiwa amejificha chini ya blanketi. Mazingira yalikuwa ya ajabu. “Nini kimewapata nyinyi wawili?"

“Alisema nini?” Alvin alipuuza swali lake na kumuuliza kwa hasira.

“Anadai kwamba yeye ni rafiki wa Lisa wa shule ya sekondari. Tangu wakati huo alikuwa amempenda Lisa, lakini Lisa hakupendezwa naye kwa sababu ya ubaya wake na malezi duni. Kwa hivyo, alianza kuweka chuki dhidi yake. Kisha, akatokea kumuona Lisa akinywa pombe peke yake kwenye baa. Pia alisikia kwamba amefukuzwa nyumbani kwa akina Masawe na kwamba hana mtu wa kumtegemea, hivyo akamkamchanganyia pombe apoteze fahamu ili ambake…”

Alvin alikunja uso, kisha akamtazama Lisa . "Ni kweli?"

Lisa aliitikia kwa kichwa na uso uliosinyaa kwa huzuni. "Amekuwa na sifa mbaya tangu enzi zetu za shule kwani kila mara alikuwa akichokozana na wasichana katika darasa letu na hata kuwachungulia mara kwa mara kwenye choo cha wanawake. Nilikuwa nikichukizwa sana na mtu wa aina hii. Haina uhusiano wowote na pesa au mwonekano wake. Sikujua kwamba tabia yake imeendelea kuwa mbaya kadiri anavyokuwa mtu mzima.”

Sam akahema. "Hiki ndicho kinachotokea wakati mtu anaandamwa na mikosi. Utakutana na mtu mwendawazimu kwa urahisi. Usijali, atakaa jela milele.”

Lisa akafungua midomo yake mikavu lakini hakusema lolote. Alvin alimtupia jicho na kusema, “Wakati video inarushwa moja kwa moja, watu wengi walikuwa wakiitazama. Uso wa Lisa ulionekana?"

Sam alitikisa kichwa kwa aibu. "Hata hivyo, chochote kinachopaswa kuondolewa kwenye video kimeondolewa. Video haitasambazwa mtandaoni, lakini… idadi kubwa ya watu mtandaoni walikuwa wakiitazama wakati huo. Wengi lazima tayari wanajua kuhusu hilo.”

Lisa alishika blanketi. Kwa kuzingatia kwamba familia ya Masawe tayari haikumpenda, asingeweza tena kurudi nyumbani kwao kwa hakika. Alicheka kwa huzuni huku akihisi kufadhaika moyoni. "Ni sawa. Hainisumbui.” Alijifariji kwa maneno, lakini, hakuna mtu aliyemjali sana.

Baada ya sekunde kadhaa za ukimya, Alvin aligeuka na kumwambia Sam, “Nenda katengeneze mazingira ili polisi wamsifie Lisa kwenye jukwaa lao la umma kuwa ni wakala wa siri. Kama si yeye ambaye alishirikiana na polisi, polisi wasingeweza kuwakamata watu hao ambao walirusha video haramu za moja kwa moja kama vile Zakayo Tarimo.”

Lisa alipigwa na butwaa kwa muda, akimtazama kwa sura ya mshangao. Je, aliogopa kwamba angeharibu sifa yake au alimjali sana? Hakuweza kuonekana kumfahamu.

Sam aliinua kidole gumba. “Ajabu. Kwa njia hiyo, naamini watu hawatamsengenya Lisa na badala yake watamsifu. Nitashughulikia sasa hivi.”

Baada ya Sam kuondoka, ghafla Lisa aliachwa kwenye uso wa Alvin. “Asante kwa leo.”

Alvin akainama kwa utulivu na kukoroma. "Hatimaye unazungumza kama mwanadamu."

Lisa alikosa la kusema. Kutokana na mambo mengi yaliyomtokea kwa siku chache, hakuwa na nguvu ya kuzungumza naye kwa wakati huo tayari.

“Unataka kula kitu?” Alvin aliuliza.

Alipouliza tu hivyp Lisa akakumbuka hakuwa amekula chakula cha mchana na cha jioni. Asingejisikia vizuri ikiwa angepigwa dripu akiwa na tumbo tupu, lakini, hakutaka kumsumbua Alvin. “Nitaagiza tu take away kwa kutumia simu yangu.”

“Sawa. Ikiwa hujui la kusema, bora unyamaze.” Alvin alikasirika sana. Licha ya uwepo wake, angependelea kuagiza chakula kwa kutumia simu yake kuliko kukubali msaada wake. Moyoni mwake alikuwa anamfikiriaje?

“Lala tu upumzike. Nitakuletea kitu.” Alvin alimwambia na kutoka.

Baada ya kuondoka, Lisa alitoa kicheko cha uchungu. Sio kwa sababu hakutaka msaada wake, bali aliogopa kumtegemea kwa kila kitu, kwani, alikuwa mjomba wa Ethan—mtu ambaye angeweza kumwacha wakati wowote.

Dakika 20 baadaye, Alvin aliingia na chombo cha chakula. Lisa alijaribu kuamka kwa nguvu lakini alishindwa kutegemeza mwili wake kutokana na maumivu makali.

“Acha kuhangaika. Daktari alisema unahitaji angalau siku mbili kupona. Wakati anaongea, Alvin alimsaidia kukaa kwa kumkumbatia. Kifua chake kilishikamana na mgongo wake kupitia shati lake jembamba, ambalo lilimpa joto fulani. Lisa kisha alianza kuona haya usoni.

Kwa bahati nzuri, alikuwa mwepesi wa kutosha kuweka mto nyuma ya mgongo wake na kumwachia baadaye. Alipofungua chombo cha chakula, kulikuwa na sahani tatu za wali na supu ya nyama na maharage. Alinyoosha mkono wake na kugundua kwamba hakuweza kuinua kijiko.

“Kaa kwa kutulia, acha kuhangaikahangaika.” Baada ya kumkaripia, Alvin alichota kijiko cha supu ili kumlisha. Lisa alistaajabu kwani hakuwahi kumjali kwa namna ile. Hata hivyo, alikuwa anasumbuliwa na tumbo. Bila kujisumbua, aliinamisha kichwa chini na kuinywa ile supu. Alifikiri kwamba chakula kilichouzwa mbele ya lango la hospitali hiyo kingekuwa vibaya, lakini kikawa kitamu.

Kwa kuogopa kwamba angekosa hamu ya kula, aliharakisha kasi yake ya kula. Baada ya kula nusu bakuli la wali, alisema, “Sawa. Nimetosheka."

"Hapana. Kula kidogo zaidi.” Alvin alikunja uso na kuendelea kumlisha. Lisa hakuwa na jinsi zaidi ya kuendelea kula akiwa ameinamisha kichwa chake. Alinyanyua macho yake kwa siri kumtazama Alvin mara kwa mara.
Uso wa Alvin ulijidhihirisha vizuri. Macho yake meusi yalikuwa yamemkazia sana wakati anakula.

Baada ya kumaliza sahani ya wali, Lisa alilala chini kwa msaada wa Alvin. “Umeiona simu yangu?”

“Hapana, sijaipata. Labda kuna mtu alichukua baada ya kuzirai. Nitakununulia nyingine baadaye.” Mara Alvin alipomaliza kuongea, simu yake iliita. Alitoka nje na simu yake na kumuona Hans akiwa anamsubiri nje.

“Bwana Kimaro, nimechunguza suala kuhusu zabuni. Nilisikia kwamba wakati mbunifu wa Kibo Group, Lina Jones, alipotambulisha kazi yake wakati wa hafla ya zabuni jana, Lisa alidai katika hali ya kufadhaika kwamba Lina alikuwa ameiba kazi yake.”

"Kulikuwa na kitu kama hicho?" Macho ya Alvin yalidhihirisha mshangao.

"Ndiyo. Mzee Kamote alimwomba Lisa kutoa ushahidi. Lisa alikuwa na michoro ilihifadhiwa kwenye kompyuta yake lakini baada ya kuiangalia tena akakuta imetoweka. Alimshuku Juma Masudi kutoka Imperial Design, akisema kuwa alihusika kuhujumu kazi yake licha ya kutokuwa na ushahidi wa hilo. Baada ya hapo, alitofautiana na Imperial Design hadharani na baadaye akatolewa nje ya ukumbi, na kazi pia amefukuzwa.”

“Akatolewaa nje?” Alvin alirudia maneno hayo.

“Ndiyo.” Hans akaitikia kwa kichwa. Akiwa amefanya kazi na Alvin kwa miaka kadhaa, Hans alijua kuwa Alvin alikuwa kakasirika sana.

"Kibo Group iliwasilisha ubunifu gani jana?" Alvin aliuliza

"Nilimwomba mtu apige picha yake." Hans akamkabidhi Alvin simu yake na umwonyesha picha ya michoro ya Kibo Group. Baada ya Alvin kuitazama, uso wake uliangaza kwa mshangao.
Alikuwa ameiona michoro ya Lisa hapo awali. Ilikuwa sawa kabisa na hiyo ya Kibo Group aliyoiona kwenye picha. Haishangazi Lisa hakuonekana kuwa sawa aliporudi jana yake. Hakuridhika na pengine alikuwa na kinyongo dhidi yake. Ilikuwa ni kwa sababu alikuwa amemfanya kushiriki katika tukio la zabuni lisilo la haki.

Muda kidogo, Alvin akamrudishia Hans simu na kusema. "Nadhani Mzee Kamote amefanya mambo mengi kama haya katika miaka iliyopita. Ni wakati wa kumfichua kwa ulimwengu.”

Hans alielewa mara moja ujumbe wake. "Nimeelewa. Ikitokea kuwa Mzee Kamote amedhibitika kufanya udanganyifu na kupoteza nafasi yake, mradi unaohusisha ushirikiano kati ya Kituo cha Utamaduni na Teknolojia cha Taifa na Kibo Group…”

“Bila shaka, utasitishwa,” Alvin alisema bila kujali, “Zuia kampuni zote zinazopanga kufanya kazi na Kibo Group hivi karibuni. Kuhusu Lina… Mchokoze kwa maneno.”

“Sawa. Na ikiwa mchakato wa zabuni utapangwa upya, Lisa atashughulikia mradi huo? Lakini, kampuni ya Imperial Design imemfukuza kazi!”

"Achana na mradi. Ana uwezo wa kubuni, lakini hawezi kusimamia kazi yenye changamoto kubwa kama hii…” Alvin alidhihaki mara mbili. "Mlete Juma Masudi hapa." .....ITAENDELEA.....

Juma Masudi kazi anayo, sasa sijui nini kitakwenda kutokea baada ya kufikishwa mbele ya Alvin, yangu macho tu sasa nikuombe tuungane pamoja kwenye sehemu inayofuata kujua kini kitajiri kwenye mkasa huu wa kusisimua
LIPIA USOME HARAKA.

Vitabu vinazidi kuandikwa na baadhi vimekamilika lakini pia unaweza kusoma kwa kulipia kulingana na episode unazotaka.

Episode - 20 Tsh 1000/=
Episode - 30 Tsh 1500/=
Episode - 40 Tsh 2000/=
Episode - 50 Tsh 2500/=

Namba za kulipia

0628924768 (Halotel) JUMA HEMBA
0694288555 (Airtel) JUMA HEMBA
0764736557 (Voda) HADIJA KIRUNGI

"Lipia utumiwe similizi yako sasa whatsapp 0628924768"

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
JINA LA SIMULIZI............................LISA
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP..........................0628924768
SEHEMU YA....................................25&26

SURA YA 25

Wakati Alvin anarudi wodini, Lisa alikuwa anahangaika kitandani, akionekana kujaribu kuamka. Lakini, aliacha kuhangaika dakika moja alipomwona akiingia.

“Unajaribu kufanya nini?” Kwa mawazo ya kufikiriwa vibaya na Lisa, Alvin alizungumza kwa sauti ya upole.

Macho ya Lisa yakaangaza. “Unaweza kunitafutia mhudumu binafsi? Nitamlipa.”

Alvin alimuuliza kwa upole. “Unataka kwenda chooni?” Alvin hakungoja Lisa ajibu. Alisogea kuelekea kwake. Kisha, akavuta blanketi na kumbeba.

Lisa alipiga kelele kwa mshtuko akilalamika kwa aibu. “Niweke chini haraka.”

“Sawa. Basi nenda huko peke yako.” Kwa vile alikuwa mkaidi, Alvin aliamua kumweka chini moja kwa moja. Lisa alipoteza usawa wake. Alitetemeka bila utulivu na akaanguka mikononi mwa Alvin moja kwa moja kana kwamba hakuweza kupinga kumkumbatia. Akajawa na aibu.

“Alvin.”

"Wewe ndiye uliyeanguka mikononi mwangu." Alvin alivutiwa kuona hali yake ya aibu mara chache. Lisa alikasirika sana hata akakosa la kusema. Baada ya hapo, Alvin akambeba tena upesi na kuelekea chooni.

“Nilikuambia unitafutie tu mlezi.” Lisa alilalamika kwa aibu, aliona haya kwa Alvin kumsaidia katika shida zake za faragha.

“Kwa hiyo utakaa na mkojo wako hadi mlezi atakapokuja? Unafikiri ninaweza kumpata mlezi mara moja?” Alvin aliuliza kwa kejeli huku akimuweka kwenye kiti cha choo.

Kilichomsikitisha zaidi Lisa ni kwamba hakuwa na hata nguvu ya kuvua suruali yake. Hatimaye, alihitaji msaada tu wa Alvin. Kufikia wakati anarudi kitandani, alikuwa na aibu sana hivi kwamba alijibanza ndani ya blanketi. Moyoni, Alvin aliona ni jambo la kufurahisha.

Saa moja baadaye, Alvin alipata mlezi wa kumhudumia Lisa mle wodini. Hata hivyo, Lisa alikuwa amepitiwa na usingizi wakati huo. Alvin alikuwa na kesi ya kutetea mahakamani asubuhi iliyofuata, na alikuwa bado hajatayarisha hati za kesi hiyo. Kwa hiyo, alitoa amri kwa mlezi na baadaye akaondoka.

Lisa alipozinduka usiku wa manane, alimkuta mwanamke mwenye sura ya upole aliyeonekana kuwa na umri wa miaka 40 hivi pembeni ya kochi.

Mwanamke huyo aliamka na kumueleza Lisa, “Mimi ndiye mlezi ambaye Bw. Kimaro ameniajiri kukutunza.”

“Nashukuru.” Lisa alijibu na kuuliza, “na yeye kaenda wapi?”

Mlezi akajibu kwa kicheko, “Bw. Kimaro ana wasiwasi sana juu yako. Alikaa hadi saa tano usiku. Hata aliniamuru nisilale kwani ungeamka usiku. Pia, ameajiri mpishi mkuu kutoka hospitalini ili akuandalie milo mitatu na kuhakikisha kwamba chakula kina lishe ya kutosha na kisafi.”

Lisa alipepesa macho akihisi kana kwamba hajazinduka kutoka kwenye ndoto yake. Jinsi mlezi alivyomuelezea Alvin ilikuwa tofauti kabisa na jinsi alivyokuwa akifikiria.

Mlezi aliongezea, “nimeona kila aina ya wanandoa hospitalini. Bw. Kimaro ni mgumu kwa nje lakini ndani ni laini.”

Lisa alijitenga kidogo. Akikumbuka jinsi Alvin alivyojitokeza na kumuokoa usiku wa jana yake, alihisi kwa uaminifu kwamba alikuwa mpole.

Asubuhi, Lisa aliporudi kutoka kuchunguzwa, kulikuwa na watu wengine wawili wodini ambao ni Alvin na Juma Masudi, aliyekuwa mbunifu mwenzake kule Imperial Design. Haikuweza kufahamika ni kitu gani kilikuwa kimempata Masudi ambacho kilimsababishia michubuko mibaya.

Juma alipiga magoti baada ya kumuona Lisa. "Samahani, Bi Jones. Nilikuwa na njaa tu ya pesa. Lina alinilipa milioni tano ili kuiba michoro yako. Ilikuwa ni kosa langu. Nisamehe tafadhali. Nakuomba."

Juma alikuwa akitetemeka kwa hofu kubwa. Kinyume chake, Lisa naye alikuwa akitetemeka kwa hasira. Angempiga ngumi kwa nguvu ikiwa angekuwa na nguvu za kufanya hivyo. “Kwanini nikusamehe? Unajua umeharibu nini? Uliharibu sifa na hadhi yangu kama mbunifu. Mtu mchafu kama wewe huna sifa ya kuwa mbunifu hata kidogo."

“Ndiyo, sijahitimu chuo chochote,” Bila kuinua kichwa chake, alisema kwa wasiwasi, “Ndiyo maana siwezi kubuni tena.”

Lisa alipigwa na butwaa. Hapo ndipo alipogundua kwamba mikono yake yote miwili ilikuwa ikining’inia chini na vifundo vyake vimefungwa bandeji. “Mikono yako…”

Alvin aliinuka taratibu na kuinua macho yake bila kujali. "Kwa kuwa ameamua kuwa mwizi badala ya kuwa mbunifu, hataweza kubuni tena. Bora akawe ombaomba."

Juma alitetemeka huku akitambaa chini. Lisa hakujua alifanyaje kwenye mikono yake. Juma alikuwa mtu mwenye majivuno, mwenye kiburi. Ni lazima Alvin ndiye aliyemfanya aishie katika mazingira hayo. Hakuwa na huruma na Juma. Baada ya yote, hakuwa amezingatia hali yake wakati akifanya mambo ya aina hiyo. "Vema, umepata kile unachostahili. Natumai, utageuka kuwa mtu bora zaidi."

“Sawa. Hakika sitafanya tena. Nitahama kabisa Dar es Salaam na sitawahi kutokea mbele yenu,” Juma alisema huku akitetemeka.

“Potea!” Alvin alimwamuru kwa sauti na Masudi akapotea kama upepo.

Baada ya Juma Masudi kuondoka, Alvin akatupa simu mpya mkononi mwa Lisa. Lisa aliinua simu na kutazama. Kulikuwa na rekodi ndani yake ambayo ilirekodi kile ambacho Juma alikuwa amesema muda ule. "Ni juu yako kushughulikia rekodi hiyo katika simu ninayokupa." Alvin akampiga jicho. “Punguza hasira yako wakati ujao. Ulipoteza katika zabuni kwa sababu tu hukutunza vizuri kazi yako. Lichukulie hili kama somo. Unahitaji kuwa mwangalifu na kila mtu mahali pa kazi."

Lisa alimtazama kwa sura iliyoduwaa lakini ngumu. Alidhani kwamba Lina alishinda zabuni kwa sababu Alvin na Mzee Kamote walimtengenezea mazingira. Kwa wakati huo, alishangaa kidogo, huku akijilaumu kwanini alimhisi vibaya bila kuwa na uhakika. Pengine Lina alikuwa anajiropokea tu kwamba mjomba wake Ethan amemfanyia mpango wa kushinda zabuni kwa Mzee Kamote.

“Mbona unawaza sana?” Alvin akamzindua Lisa kwa swali.

Wakati huo, Lisa alipaswa kujisikia kushukuru sana kwake. “Mimi tu… Hakuna. Nasema tu, asante sana,” Lisa alisema kwa dhati.

“Kwa kweli unapaswa kunishukuru, lakini haina maana kunishukuru kwa maneno hivi,” Alvin alidhihaki.

“Nitakutengenezea nyama choma ya nguruwe mara nitakapopona. Huwezi kula kila siku, ingawa. Vinginevyo, utakuwa na ugonjwa wa ini…”

“Usinipangie maisha yangu wewe! Nani alisema napenda nyama ya nguruwe choma? Nilikuwa nakula tu kwa sababu hicho ndicho chakula unachoweza kuandaa vizuri zaidi kati ya vyakula vyote ulivyowahi kuniandalia.” Alvin alikatiza kwa kujibaraguza.

Lisa alimjua Alvin. Alvin asingekubali kukiri kwake jambo lolote hata kama ni kweli kwani hakupenda kupoteza hadhi yake mbele ya Lisa.

Lisa alijaribu kuzuia hamu ya kucheka. Licha ya kushangazwa na kukataa kwake kusema ukweli, alitikisa kichwa kukiri. “Ndiyo. Ni kosa langu, na nimejitafakari. Halafu, simu ni kiasi gani? Pia mlezi na hospitali wananidai kiasi gani? Acha niwalipe.”

Lisa alijisikika kuogopa kiasi kuelekea mwisho wa sentensi yake. Akiwa na kiasi kidogo tu cha pesa kwenye kadi yake ya benki, huenda asingeweza kumudu, lakini aliongea hivyo tu ili na yeye kumwonyeshea kiburi Alvin.

"Hakuna haja. Nitachukulia gharama hizo kama malipo yako kwa kuwa mhudumu wa Charlie." Alvin alimwambia Lisa kwa kejeli.

“Lakini…” Lisa alitaka kupinga.

"Nimesema nitalipa pesa yote," Alvin aliingilia kati. “Naenda ofisini sasa hivi. Nitamwambia mlezi akusaidie katika mchakato wa kuachiliwa kesho. Fika nyumbani mapema ili kumtunza Charlie.

"Sawa nitafanya." Lisa hakuwa na namna ila kukubali tu.
SURA YA 26

Saa kumi na moja asubuhi Pamela alifika kwa haraka pale hospitalini. Alipomwona Lisa, hasira zilimpanda. “Bado sisi ni marafiki? Hata hukunifahamisha kuhusu jambo hili zito. Isingekuwa mimi kuuliza namba za Harrison, nisingegundua kuwa upo hospitalini.”

"Nilidondosha simu yangu, na sijabadilisha SIM kadi nyingine." Lisa alimwambia kwa upole.

Uso wa Pamela ulionyesha wasiwasi alipoushika mkono wa Lisa. “Ni nini hasa kiliendelea jana usiku? Kweli ulikua wakala wa siri wa polisi?"

Lisa mara moja akagundua. Inavyoonekana, polisi walikuwa wametoa tangazo rasmi. "Ni nini kinachozunguka kwa sasa?"

Pamela aliyazuia macho yake ambayo yalikuwa yakimetameta. "Watu wengine wanaamini, wakati wengine hawaamini."

“Hiyo ni kawaida. Watu wengi wamekuwa wakingojea nyakati zangu za aibu kwa muda mrefu.” Lisa alimweleza kwa kifupi Pamela kilichotokea wakati wa mchakato wa zabuni jana yake.

Pamela alikasirika sana na kusema kwa uchungu. “Ethan ni mwanaharamu. Huo ni upuuzi gani aliokufanyia? Hivi yeye ni binaamu kweli? Mbona zamani alikuthamini sana na sasa amebadilika kabisa? Lina alimroga vipi hadi akupige?”

“Labda alinipenda zamani kwa kuwa alijua mimi ndiye ningekuwa mrithi. Lakini sasa upepo umebadilika na yeye kabadilika, anampenda tu mwanamke mrithi wa familia tajiri ya Masawe. Kwake, haijalishi yeye ni nani cha muhimu ni urithi tu alionao.” Lisa aliongea kwa uchungu sana..

“Habari nilizozisoma asubuhi ya leo ziliripoti kwamba Mzee Kamote na bodi inayosimamia Kituo cha Utamaduni na Teknolojia cha Taifa walihusika mara kwa mara katika kupokea hongo, kwa hivyo anasimamishwa kazi na kuchunguzwa. Tukio la zabuni la jana pia limebatilishwa. Kulingana na maoni yaliyotolewa mtandaoni, wengi wanadhani kuwa Kibo Group ilimpa Mzee Kamote rushwa ambayo ilichangia Kibo Group kupata matokeo ya zabuni hiyo hapo jana.

Lisa alipigwa na butwaa. “Hii inawezekanaje?”

“Kwa nini nikudanganye? Ngoja nikuonyeshe habari hiyo.” Pamela aliwasha simu yake haraka na kutafuta tovuti ya habari hiyo ili kumuonyesha Lisa. Lisa alishangaa kabisa. Alihisi kuwa kuna jambo geni kuhusu sadfa hiyo.

"Yajayo yanafurahisha!" Pamela alisema kwa furaha kubwa, "Unaona, makampuni mengi makubwa ya tasnia ya ujenzi yalishiriki katika zabuni jana, na walitumia muda mrefu na rasilimali nyingi za wafanyakazi na nyenzo katika maandalizi ya tukio hilo. Juhudi zao zote zimeishia bure sasa. Nadhani kituo kimemchukiza kila mtu.”

Lisa aliamini hivyo baada ya kuwaza. Hata hivyo, ilikuja kama habari njema kwake kwamba juhudi za Lina hazikufaulu.
•••
Ndani ya ofisi za Kibo Building Design Group, Jones Masawe, mkurugenzi mkuu, alikuwa amekasirika sana hivi kwamba kifua chake kilikuwa hatarini kupasuka muda wowote. Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Lina kumuona baba yake akivimba kwa hasira. Akiwa ameinama upande mmoja, hakuthubutu kusogea hata kidogo.

Siku moja tu nyuma, wasimamizi wakuu wa kampuni walikuwa wamesherehekea mafanikio ya zabuni ya Kituo Cha Teknolojia Na Utamaduni Cha Taifa, lakini kesho yake furaha hiyo ilianza kuyeyuka taratibu baada ya kusikia kuwa Mzee Kamote alikuwa amekamatwa na TAKUKURU. Je, angefanya nini ikiwa kuhusika kwa Mzee Kamote katika hongo kungefichuliwa?

“Mama…” Lina alimwangalia mama yake, kwa wasiwasi. Mama Masawe alimpiga bega na kumfariji. “Usijali. Kwa kuzingatia hali ya baba yako kwa miaka mingi, ataweza kusuluhisha hili tatizo.”

"Hata kama naweza kusuluhisha, sifa ya Kibo Group itaathiriwa kwa kiasi kikubwa," Jones Masawe alijibu kwa hasira.

Mama Masawe alimkodolea macho mumewe. "Hii sio kazi ya Lina. Amefanya kwa kadri yake. Yeyote kutoka kwa kampuni ambaye angejihusisha nayo angekumbana na hali kama hii. Kwa kweli, kuna mtu alipanga kumdanganya Mzee Kamote.

“Sina maana ya kumlaumu…” Kabla hata Jones Masawe hajamaliza sentensi yake, meneja mkuu ghafla akaingia ndani na kusema, “Bw. Masawe, kuhusu mpango wa ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa klabu ya Simba, mratibu alitupigia simu hivi punde na kutufahamisha kwamba hawatafanya kazi na sisi tena. Pia, Hoteli ya Kimataifa ya Holmes ilisema kwamba hawatafikiria kufanya kazi nasi.”

Jones Mwasawe alihisi kizunguzungu huku akiwa amefura kwa hasira. Hii ndiyo miradi miwili mikubwa ambayo Kibo Group ilikuwa ikilenga kwa muda wa miaka miwili iliyopita na ilikuwa karibu kuipata.

Meneja mkuu kisha akaongeza, “Mbali na hayo, kampuni yetu ilituma maombi ya kutembelea maonyesho ya dunia katika nchini ya India mapema, lakini sasa wametukataa moja kwa moja. Bw. Masawe, je kampuni yetu imemkosea nani? Ni wazi kuna mtu anayeichafua Kibo Group nyuma ya mgongo wetu.”

Jones alianza kutetemeka. Yeye ndiye alikuwa ameongoza Kibo Group kwa juhudi na kwa miaka mingi na hakuwahi kugombana na mtu. "Siku zote nimekuwa nikifanya kwa uangalifu katika tasnia hii kwa miongo kadhaa. Sijawahi kumuudhi mtu yeyote.”

“Inaweza kuwa… Lisa ?” Lina aliongea kwa kusitasita. “Usinielewe vibaya. Sijaribu kumsema vibaya. Haikuwa suala kubwa wakati Lisa aliponikokota nje ya Mgahawa wa Grapefruit wakati huo. Lakini, Janet na Cindy walikuwa wamekasirika sana wakati huo. Walisema kwamba wangefanya jambo kuhusu hilo. Wote hawa wanatoka kwenye familia za matajiri wenye ushawishi mkubwa. Huoni kwamba tatizo linaweza kuwa lilianzia hapo?”

"Hakika inahusiana na Lisa!” Mama Masawe alinguruma.

“Mwambie arudi.” Usemi wa Jones uligeuka kuwa wa kusikitisha.

"Bw. Masawe, kuna jambo moja ambalo huenda hulijui…” Meneja mkuu alisita kabla ya kusema, “Video ya moja kwa moja kwenye chaneli moja ya yotube ilionyesha matukio machache ya aibu jana usiku, na Lisa akatokea kuwa mhusika wa kike. Hata hivyo, video hiyo ilizimwa wakati polisi walipoingia na kuwakamata watu hao. Baada ya tukio hilo, polisi waliondoa video zote zilizosambazwa mtandaoni na kutangaza kwamba Lisa alikuwa wakala wa siri wa polisi!”

Lina alishangaa kwa kufoka, “Hiyo ilikuwa hatari! Yeye hata hajapitia mafunzo ya upolisi, sasa amekuwaje wakala wa siri?”

Mama Masawe aliuma meno. “Ni wakala gani wa siri? Kuna uwezekano mkubwa alijifanya kuwa wakala wa polisi baada ya kupata matatizo. Ni lazima polisi ndio waliomuokoa. Ni aibu iliyoje.”

Meneja mkuu akasema, “Ndiyo. Hicho ndicho kimekuwa kikienea katika mtandao. Inajadiliwa sana kuwa maisha ya Lisa ni ya fedheha. Sifa yake imeharibiwa sana.”

“Ni kiumbe mbaya sana. Kwa sababu yake, sifa ya familia ya Masawe imeharibiwa.” Akiwa amekasirika kwa hasira, Jones Masawe alichukua chombo kwenye meza na kukitupa. “Tafuteni njia ya kumrudisha. Sitaki abaki nje na kuendelea kuwa fedheha kwa familia.”....ITAENDELEA.....

Kwa leo naomba tuishie hapa tumeona Lisa bado akiendelea kusakamwa na kuchukwa na familia ya Masawe lakini wote tunataka kufahamu mwisho wake utakuwaje, mwisho wa kuandamwa kwa Lisa utakuwaje....basi niseme tuungane tena katika sehemu inayofuata ili kujua hatima ya mambo!.

Kama umahitaji Simulizi hii basi tucheki whatsapp kwa namba 0628924768 ili upate maelekezo ya kulipia.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
JINA LA SIMULIZI............................LISA
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP..........................0628924768
SEHEMU YA....................................27&28

SURA YA 27

Lisa aliruhusiwa kutoka hospitali baada ya siku mbili. Alvin binafsi aliendesha gari hadi hospitali kumchukua. Akikumbuka jinsi alivyotendewa kwa ukarimu isivyo kawaida, Lisa alijisikia faraja sana. Akiwa anaendesha gari kurejea nyumbani, Alvin alipitia kwenye maduka kufanya shopping kwanza.

"Charlie amekuwa mbaguzi sana wa chakula wakati haukuwa karibu naye kumpikia siku chache zilizopita. Nunua viungo zaidi na umtayarishie kitu kizuri.” Alvin alimwambia Lisa.

Akiwa anautazama uso wake wa kifahari, Lisa alijiuliza sana ikiwa ni Charlie au ni Alvin ambaye alikuwa mbaguzi wa chakula.

"Unasubiri nini? Harakisha." Alvin alimkurupua. Alikuwa amechoshwa na vyakula visivyopendeza ambavyo Hans alimletea kwa siku mbili zilizopita.

“Oh.” Lisa alifungua mkanda na kushuka kwenye gari. Kwa kuwa alikuwa amemfanyia wema na hisani kubwa wakati huo, alipanga kumwandalia chakula kizuri ili kuonyesha kuwa anajali fadhila zake.

Alipokuwa akiingia kwenye jengo la maduka, zaidi ya aina kumi ya mapishi ya Charlie yalimwangazia akilini mwake. Kulikuwa na viungo vingi sana alihitaji kununua. Pia alikusudia kupata mtindi, maziwa mabichi, matunda, na vyakula vingine.

Baada ya duru moja ya ununuzi, aligundua kuwa mkokoteni ulikuwa tayari umejaa. Hakika ilikuwa ni shida kwake kubeba vitu vyote peke yake. Baada ya kufikiria kidogo, alimtumia Alvin ujumbe kwenye WhatsApp. [Alvlisa, nimenunua vitu vingi, na sidhani kama naweza kubeba kila kitu. Unaweza kunisaidia kubeba mifuko michache?]

Baada ya kutuma ujumbe huo, hakusikia kutoka kwake kwa muda wa dakika tano. Alipumua na kuacha kuwa na matarajio makubwa kwake na kufikiria kubeba mwenyewe mizigo ile. Akiwa katikati ya mawazo yake, ghafla aliona kivuli kikubwa cha mtu kikiibuka. Alipoinua kichwa chake, umbo refu na wima la Alvin likatokea mbele yake.

"Nilitaka tu ununue viungo vya Charlie, lakini umekuja kununua duka zima." Alvin alimkejeli Lisa baada ya kuona lundo la vitu alivyokuwa amenunua.

Lisa alieleza haraka, “Nilikuwa nikifikiri kwamba wewe na Charlie hamjaweza kula chakula chochote kinachofaa siku chache zilizopita, kwa hivyo nimenunua zaidi…”

Alvin aliinua mkono wake na kumkatisha kwa kukunja uso, “Nilikula vizuri. Alikuwa Charlie ambaye hakula vizuri, usijumuishe na mimi. Mimi si mbaguzi wa chakula.”

“Una uhakika?”

"Ndio, Charlie hakula vizuri." Alvin alihakiki usemi wake.

Ili kumwokoa asipoteze heshima yake, Lisa aliitikia kwa kichwa na kueleza kwa fikira, “Vitu ninavyonunua vyote ni vya lazima. Unahitaji kula mtindi, maziwa freshi, na matunda kila siku ili mwili wako upate lishe ya kutosha. Huenda ukaonekana mzima sasa, lakini unafanya kazi kwa bidii kila siku na hata kunywa pombe kwa nyakati fulani. Kwa hiyo, ni lazima utunze mwili wako na kula mlo kamili unapokuwa nyumbani.”

Alvin aliposikia hivyo alipigwa na butwaa. Macho yake yalifichua hisia zinazokinzana.
Kabla ya hii, hakuna mtu aliyejali kuhusu lishe yake. Watu wengine walichojali zaidi ni uwezo wake wa kuleta manufaa kwa familia ya Kimaro na kama alikuwa ametimiza mahitaji ya familia ya Kimaro.

Lisa kisha akaongeza, “Ninahitaji viungo hivi katika upishi wangu. Pia nilinunua hizi tambi ili nikupikie ukichelewa kutoka kazini. Tunahitaji toilet papers na sabuni za maji kwa ajiliya usafi pia.”

Wakati huo, Alvin alikuwa chini ya hisia kwamba mwanamke huyu alipaswa kuwa mke wake, kutokana na kwamba alikuwa anajali sana kila kitu ndani ya nyumba.

Akionyesha kisanduku cha karatasi, Lisa aliendelea, “…hii tishu itawekwa kwenye gari lako. Kwa hiyo si mara zote utalazimika kutumia karatasi ya tishu iliyotolewa kwenye kituo cha mafuta. Aina hii ya tishu ni nafuu sana…”

"Tangu lini ninatumia karatasi ya tishu iliyotolewa bure kwenye kituo cha mafuta?"

“Ipo kwenye gari lako. Bado ipo.” Kwa kuogopa kwamba alikuwa na wasiwasi juu ya kuokoa heshima yake, Lisa alijifanya kuwa alipenda vitu alivyotumia Alvin. “Haijalishi. Ninapenda kwa kuwa unatumia vitu visivyo na bei sana. Nimefurahi kukutana na mwanamume ambaye anaishi maisha ya kujali matumizi mazuri ya pesa. Wewe ni mfano wa mwanaume kamili ninayependa kuishi naye."

Akiwa amezidiwa na pongezi hizo za ghafla, Alvin aliinamisha kichwa chini. Jinsi alivyotazama juu na kumwangalia kwa macho angavu ilimkumbusha mara ya kwanza walipokutana. Ikilinganishwa na mwonekano wake mbaya siku mbili zilizopita, sura yake isiyo na aibu sasa hivi ilimfanya ajisikie vizuri.

"Haupaswi kufanya kazi kama mbunifu. Unapaswa kuwa mama wa nyumbani." Alvin alimtania.

Lisa alicheka. "Nataka tu kuwa mama wa nyumbani na chumbani pia."

"Nenda ulipe bili sasa." Alvin alimwambia kwa kupotezea.

Muuzaji mwenye shauku ambaye alikuwa akitangaza bidhaa fulani aliharakisha hadi kwenye kaunta ya kulipia na kuwazuia wawili hao. “Halo bwana na bibie. Je! ninyi mnataka kununua Durex? Tuna promosheni ianyoendelea ambapo unanunua moja na kupata moja bila malipo. Ni kweli inaokoa pesa.”

Lisa aliona haya kuona kisanduku kidogo cha kondomu mkononi mwa muuzaji. “Hapana… Hakuna haja. Hatuhitaji.”

“Ohhh. Nyote wawili ni watu waliooana hivi karibuni, kwa hiyo mnapanga kupata mtoto?” Muuzaji aliuliza bila kujua lolote.

“Ndiyo.” Akiogopa kwamba muuzaji angeendelea kuwasumbua Lisa alinong'ona kitu na kisha akamvuta Alvin mbele.

"Nani kasema anataka kupata mtoto?" Alvin alimtazama Lisa kwa jicho kali.

“Nilikuwa namdanganya tu aende zake, au unataka kuzinunua?" Lisa aliuliza kwa kawaida.

“Acha kuota. Hata kama ningenunua, sitaitumia na wewe.” Licha ya maneno yake ya kikatili, sura ya Lisa ilitabasamu kwa furaha.

Baada ya wao kuondoka kwenye maduka, Alvin aliendesha gari kurudi nyumbani Walipofika nyumbani, Lisa aliingia moja kwa moja jikoni kuandaa chakula. Mwanzoni Lisa alifikiri kwamba alikuwa ameandaa chakula kingi sana. Mara tu Alvin alipoanza kula, alifikiri chakula kisingetosha. Alionekana kuwa na njaa ya siku mbili. Chakula kiliisha kwa muda mfupi. Baada ya chakula cha mchana, Alvin na Charlie walilala kwenye kochi kwa uvivu, akijipumzisha kidogo ili chakula kishuke taratibu.

“Unapanga kufanya nini baadaye? Utaendelea kutafuta kazi?” Alvin alimuuliza Lisa

“Tulizungumzie hilo baadaye. Nitaenda kusajili laini ya simu kwanza.” Lisa ajibu.

“Usijali kuhusu hilo. Ikiwa huwezi kupata kazi, kaa tu nyumbani unipikie. Kama una shida ya pesa nitakupatia kiasi chochote muda wowote unaotaka.” Alvin alimwambia huku akitoka.

Lisa alipigwa na butwaa kwa muda. “Unakwenda kazini sasa hivi?”

"Ndio, bado nina kazi nyingi ya kushughulikia." Mara baada ya kuondoka, Lisa alitupia macho muda huo ambao ulionyesha ni saa saba mchana. Kwa kweli alimuonea huruma kwani kuwa bosi haikuwa rahisi. Hakuwa na hata mapumziko baada ya chakula cha mchana. Pengine alikuwa ameiba tu muda nje ya ratiba yake yenye shughuli nyingi ili kumchukua hospitali.

SURA YA28

Baada ya Lisa kusajili laini ya simu mchana huo, simu yake ilionyesha zaidi ya simu kumi ambazo hazikupokelewa. Alikuwa amerudisha namba yake ileile ya zamani. Simu hizo zilipigwa na Pamela Masanja, Jones Masawe, na Mama Masawe, na watu wengine wengi. Je, inawezekana kwamba walikuwa na wasiwasi juu yake baada ya kujua kilichomtokea? Bila kujali sababu, alimpigia simu mama yake.

“Mama…”

“Hatimaye umenipigia simu tena.” Sauti ya hasira ya Mama Masawe ilisikika. “Unakusudia kukaa nje hadi lini? Njoo nyumbani sasa hivi.”

Ule msemo 'njoo nyumbani' ulimfanya Lisa ahisi uchungu ndani kabisa, akauliza kwa hasira. “Hapo bado ni nyumbani kwangu?”

“Lisa, ikiwa hautarudi sasa, usirudi milele. Huhitaji tena kumtambua baba yako na mimi pia.” Mama Masawe alikata simu mara baada ya kumaliza kuongea.

Baada ya kusitasita, hatimaye Lisa aliamua kurudi nyumbani. Kwani, Jones na Mama Masawe ndio waliomzaa na kumlea. Pia alitaka kuwapelekea rekodi iliyo na maneno ya Juma Masudi nyumbani na waisikie ili wajue rangi halisi za Lina.

Saa moja baadaye, aliendesha gari hadi kwenye jumba la kifahari la familia ya Masawe. Ingawa ilikuwa imepita zaidi ya mwezi mmoja tu tangu aondoke nyumbani hapo, alihisi kwamba watu wanaoishi hapo walikuwa wageni kabisa kwake.

Baada ya kuegesha gari lake aliingia ndani. Jones, Mama Masawe, na Lina wote walikuwa sebuleni. Mara tu Lisa alipoona sura ya Lina, chuki iliwaka ndani yake. “Baba, Mama, unajua kwamba Lina aliiba mpango wangu, na yeye—”

“Lisa, sijali kunishtaki nje, lakini unawezaje kuthubutu kunirushia matope hapa?” Tabasamu la uchungu lilienea kwenye uso wa Lina. "Tayari nimesema sijafanya."

Mama Masawe alivuta uso mrefu pia. “Kwa nini unamwakia tu dada yako kwa maneno makali kila unapomwona?”

“Nina ushahidi.” Lisa mara moja akatoa simu yake na kucheza rekodi ya Juma Masudi. Mara tu Lina aliposikia sauti ya Juma, sura yake ilibadilika kidogo. Hata hivyo, upesi alipata utulivu na kusema kwa huzuni, “Ulimpata wapi mtu huyu wa kumlaghai kurekodi haya? Juma ni nani? Hata simfahamu.”

Lisa aligeuka na kumtazama baba yake kwa macho mekundu kidogo. “Baba, Lina alihamisha mamilioni ya pesa kwenye akaunti ya Juma ambayo unaweza kuangalia mwenyewe. Alikulia kijijini na alijifunza kubuni tu baada ya wewe kumkubali. Kwa kuzingatia kwamba alijifunza kwa muda mfupi tu, angewezaje kutokeza na muundo mzuri kama huo?”

"Baba na mama, sikufanya hivyo." Machozi yalitiririka usoni mwa Lina.

Mama Masawe alikunja uso na kunyoosha mkono wake. "Lisa , nionyeshe hiyo rekodi." Akiwa na moyo mpole kidogo, Lisa akamkabidhi simu kwa utiifu. Mama Masawe alifungua faili ya kurekodi na kulifuta mara moja.

"Mama, wewe ... kwanini?" Lisa alishangaa kwa kitendo cha hicho cha mama yake, lakini alivyotaka kumpokonya simu yake, alikuwa ameshachelewa.

Mtazamo wa Mama Masawe ulidhihirisha ukatili wake kwa mara nyingine tena. “Siwezi kukuacha uharibu sifa na mustakabali wa dada yako kwa rekodi hii ambayo inaweza kuwa ya uwongo. Afadhali kuifutilia mbali.”

Lisa alichanganyikiwa sana hivi kwamba alitetemeka. Mara moja, alitoa kicheko kisicho na maana. “Sasa naona. Ninyi nyote hata hamjali ikiwa rekodi ni ya kweli au la. Mnachojali ni kumkingia kifua Lina tu. Unawezaje kuwa mkatili hivyo? Mimi pia ni binti yako.”

Jones alipiga meza na kusimama. “Kama ningejua mapema kwamba ungekuwa mtu hatari sana, ningalikuacha wakati huo. Angalia mambo ya ajabu ambayo umefanya. Umepoteza sifa yako kwa kufanya jambo la aibu tena hadhahari na kurekodwa kwenye video. Je, mtu yeyote mwenye heshima angependa kukuoa katika siku zijazo? Pili, ni nani aliyekukosea hadi ukatufanya kupoteza miradi mikubwa michache?”

"Sijui unazungumza nini." Lisa akatikisa kichwa huku akilia. “Kama wazazi wangu, hamna wasiwasi nami tangu mlipoona nimekutana na matatizo kama hayo?”

“Hicho ndicho unachostahili,” Mama Masawe alizungumza kwa njia ya dharau, “Si ajabu Ethan alikutupa kwa sababu haujitambui kabisa.”

Lisa alishindwa kabisa kusema. Hata wazo dogo la matarajio ndani yake lilikatishwa tamaa. Alijiona mjinga sana. Hakupaswa kurudi. Ukweli haukuwajali baba yake wala mama yake hata kidogo. Muhimu zaidi alikuwa ni Lina.

Akiwa amehuzunika, Lisa alinyoosha mkono wake kwa mama yake. “Nirudishie simu yangu mama, nitaondoka. Mtu mwenye aibu kama mimi hastahili kurudi. Sistahili kuwa na uhusiano na ninyi nyote pia.”

"Unapanga kuendelea kuzurura mitaani na kuleta aibu kwa familia yetu sivyo?" Jones alicheka. “Afadhali ukae nyumbani na kutafakari matendo yako. Ukiamua kusema ukweli, nitafikiria kukurudisha kwenye kampuni.”

Mara Jones alipomaliza kuzungumza, alipiga makofi. Walinzi wachache walitoka kwenye mlango na kumkamata Lisa mara moja.

“Nyie mnajaribu kufanya nini? Mnaniteka nyara, huh?” Lisa alikasirika. Kamwe katika ndoto zake kali hakuwahi kufikiria kuwa familia yake ingewahi kumfanyia kitendo kama hicho.

“Ninamfundisha tu binti yangu somo. Mleteni juu na kumfungia chumbani.” Jones Masawe alisema.

Lina akashauri haraka, “Usifanye hivi baba. Baada ya yote, Lisa bado ni mdogo na hajakomaa. Zaidi ya hayo, daima kuna wageni wanaokuja kututembelea hapa. Haitakuwa nzuri ikiwa atapiga mayowe kutoka juu.

Jones alishtuka. “Uko sahihi. Kwanini… Hebu tumpeleke mbali kabisa tukamfungie katika nyumba ya Old Moshi.”

Lisa alianza kuingiwa na hofu. Katika miaka michache iliyopita, alikuwa amerudi huko kijijini kwao Mbokomu, Moshi vijijini mara moja tu kwa ajili ya shughuli za matambiko. Nyumba hiyo ilikuwa imejengwa na ukoo wa Masawe miaka mingi sana iliyopita. Ingawa sehemu ya nyuma ya nyumba ilikuwa imerekebishwa kidogo, eneo jirani lilikuwa ukiwa na la kutisha. Hatimaye Lisa alielewa ni kwanini Lina alimuombea apelekwe huko. “Lina, wewe ni mtu mbaya sana—”

Mama Masawe alimpiga Lisa kofi usoni. "Nyamaza! Dada yako anajaribu kukuombea, kumbe unamtukana. Hakika wewe ni mbaya sana!”

"Mpelekeni sasa hivi." Jones alipunga mkono wake. Akiwa amechanganyikiwa na mabadiliko ya tabia ya Lisa , alijiuliza ni kitu gani kilimfanya awe mbaya kiasi kile.

Akiwa amepitiwa na usingizi, Lisa hakujua safari ya gari iliendelea kwa muda gani. Aliachwa moja kwa moja kwenye nyumba ya zamani ya kijijini baada ya hapo.

Walinzi wachache wakafunga mlango mkuu mara moja. Hata madirisha yalifungwa kwa misumari. Mbaya zaidi hakukuwa na umeme wala maji. Hata blanketi hakupewa, na ukizingatia baridi la milima ya old Moshi kipindi hicho, Lisa alihisi kuganda. Kwa vile simu yake ilikuwa kwa Mama Masawe, hakujua muda huo ulikuwa ni saa ngapi.

Nyumba hiyo kubwa ya zamani ilikuwa imejengwa kwenye eneo kubwa, ikiwa imezungushiwa na ukuta mkubwa yapata mzunguko wa kiwanja cha mpira. Ndani yake kulijaa pori la migomba na miti ya miparachichi na mifenesi hivyo kuifanya nyumba ile kubwa kuwa ya kutisha sana ndani yake. Upepo ulivuma na hivyo kugonga mlango na madirisha, sauti ya kutisha ya popo waliokimbizana pia ilisikika. Lisa karibu awe mwendawazimu. Akajikunja juu ya kitanda kwa uwoga mkubwa, hakuthubutu kusogea hata kidogo. Aliogopa giza. Aliogopa sana.

Mara tu alipogundua kuwa dirisha limefunguliwa, alikimbilia huko. Bibi mzee aliweka bakuli la wali kupitia dirishani. Mara Lisa alimshika mkono na kumsihi, “Bibi naomba uniache niende. Ikiwa hilo haliwezekani, angalau washa taa na unipe kitanda na blanketi, tafadhali.”

"Hapana. Hili ni agizo kutoka kwa bwana na bibi Masawe" Bibi kizee alijitenga na mikono yake kikatili. Kisha, kulikuwa na kishindo kwenye dirisha likifungwa.

Akiwa amesimama gizani, Lisa alikuwa anaumia sana hivi kwamba alishindwa kupumua. Alikuwa amefanya nini hasa? Kwanini kila mtu alimtenda hivi? Alikuwa amevuliwa utu wake. Hata uhuru na maisha yake ulichukuliwa pia. Alimchukia Lina, Bw. Masawe, Bi. Masawe, na Ethan kabisa. Hata hivyo, hakuweza kukata tamaa.

Alitaka kubaki hai na kulipiza kisasi. Alijaza wali mdomoni. Hakukuwa na kitu kingine zaidi ya wali. Mbaya zaidi mchele ulikuwa umevunda. Machozi yalimwagika usoni mwake. Ikiwa hakuna mtu angekuja kumwokoa, labda asingeweza kutoka nje ya nyumba hiyo akiwa hai.

Bibi kizee alitoa simu kwa mbali kidogo na mlango mkuu. "Lina, nimefanya kila kitu kulingana na maagizo yako."

“Sawa. Anza kupunguza halijoto kesho. Natumai ... atafia nyumbani."

“Usijali. Kwa mwonekano wa mambo, hakika hataweza kuishi kwa zaidi ya siku nne.”....ITAENDELEA.....

Unafikiri nini kitafuata hapo maana Lisa yupo kwenye wakati mgumu sana lakini kwa leo tuishie hapa naomba tukae kwa kutulia kusubiri sehemu inayofuata tuone mpango wa Lina utatimia au utafeli...!!

LIPIA USOME HARAKA.

Vitabu vinazidi kuandikwa na baadhi vimekamilika lakini pia unaweza kusoma kwa kulipia kulingana na episode unazotaka.

Episode - 20 Tsh 1000/=
Episode - 30 Tsh 1500/=
Episode - 40 Tsh 2000/=
Episode - 50 Tsh 2500/=

Namba za kulipia

0628924768 (Halotel) JUMA HEMBA
0694288555 (Airtel) JUMA HEMBA
0764736557 (Voda) HADIJA KIRUNGI

"Lipia utumiwe similizi yako sasa whatsapp 0628924768"

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
JINA LA SIMULIZI............................LISA
AUTHOR...........................JOMBA WAJO
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP.........................0628924768
SEHEMU YA..................................29&30

SURA YA 29

Baada ya Alvin kutoka kazini, alienda moja kwa moja kwenye mkutano kuhusu kesi ya kimataifa ya kifedha usiku. Akiwa amekunywa pombe wakati wa mkutano, alihisi kizunguzungu kidogo. Mara baada mkutano kumalizika, alirejea nyumbani. Hali ya nyumba ilikuwa tulivu na kimya. Baada kuingia ndani ya nyumba hiyo na kuwasha taa, Charlie alimkimbilia. Aliendelea kulia ‘mieww…mieww..’ huku akikumbatia mguu wake.

"Charlie, unataka nini, huh?" Alvin akatikisa kichwa chake taratibu. Baada ya muda kidogo, aliona kitu kibaya kwa Charlie ambacho hakuweza kufahamu hadi alipoisugua pua yake kwenye bakuli tupu. Charlie alikuwa na njaa. Je, Lisa hakumlisha? Mara moja akammiminia chakula cha paka Charlie ambaye alionekana kuwa na njaa kali. Alvin alikwenda chumbani kumtafuta Lisa, na kugundua kuwa alikuwa hajarudi. Uso wake ukajawa simanzi ghafla.

Mwanamke huyu amekuwa akisababisha matatizo yasiyoisha. Hapo awali alilazwa hospitalini, na sasa kwa kuwa hatimaye alikuwa amerudi nyumbani kwake, alimwacha Charlie katika hali kama hiyo. Bado alikuwa hajarudi ingawa tayari ilikuwa ni usiku sana. Akatoa simu yake ili ampigie, lakini simu yake ilikuwa imezimwa. Je, kuna jambo jingine lililomtokea?

Baada ya kuitoa simu yake, Alvin alifuatilia mahali alipo Lisa. Kwa bahati nzuri, alipomkabidhi simu siku hiyo, alikuwa amewasha ufuatiliaji wa eneo (gps) kwa kuhofia matukio mabaya yangeweza kumtokea tena. Baada ya kufuatilia eneo lake, Alvin alimtumia ujumbe Hans. [Niangalizie eneo hili.]

Dakika moja baadaye, Hans alipiga simu, “Hii ni nyumba ya familia ya Masawe ambapo wazazi wa Lisa wanaishi.”

"Nimeelewa." Alvin alikata simu kwa hasira.

Alvin alishindwa kabisa kumtafakari Lisa. Alikuwa tu akionyesha ladha ya fadhila baada ya yeye kumtendea wema. Sasa alikuwa ameenda nyumbani kwao bila kumpigia hata simu kwanza. Mbaya zaidi alikuwa amezima simu yake. Alikuwa na maana gani?

Je, hakuwa na mpango wa kurudi nyumbani kwake baada ya kusamehewa na familia ya Masawe?

“Afadhali asirudi milele” Alvin alijiapiza moyoni. Asingemjali tena hata kama angekuwa na matatizo. Kamwe asingetarajia kwamba Lisa angekuwa hana moyo kiasi hicho.

Hakukuwa na habari juu yake kwa siku tatu zaidi. Hakujibu hata simu zake. Kilichomshusha moyo zaidi Alvin ni kwamba hakula vizuri katika siku hizo tatu. Hata alitembelea mgahawa ambao ulitoa chakula kitamu zaidi kama ilivyopendekezwa na Sam, lakini aliona chakula hicho hakikupendeza.

Wakati fulani, alishuku kwamba jambo fulani linaweza kuwa limetokea kwa Lisa. Hata hivyo, kila alipowasha simu yake kuangalia mahali alipo, mara zote ilimuonyesha yupo kwenye nyumba ya familia ya akina Masawe. Wazazi wake wa kumzaa wasingeweza kumdhuru, aliamini hivyo. Ni wazi kwamba alikuwa ameamua kumsahau na kumpuuza kwa makusudi.

Katika siku tatu mfululizo alikuwa amepooza sana ofisini. Muda wa kutoka kazini ulipofika, mara moja alifungasha vitu vyake na kuondoka. Kisha akagongana na Sam mlangoni. “Unaenda nyumbani kumtunza Charlie? Lisa bado hajarudi?"

"Usimtaje tena mwanamke huyu." Alvin aliendelea mbele akionekana kutokujali.

Sam alishtuka. “Sikuwa na jinsi zaidi ya kukuuliza kwani Pamela aliniomba kujua kuhusu Lisa. Alisema hajaweza kuwasiliana naye, hivyo ana wasiwasi kwamba kuna jambo limempata.”

"Siku zote hizi amekuwa katika nyumba ya familia ya Masawe, sivyo?" Alvin alisimama akiwa ameganda palepale. Ilieleweka kuwa Lisa hakumpigia tena simu kwani wote wawili walikuwa wamekutana tu muda si mrefu, lakini Pamela alikuwa rafiki yake mkubwa.

“Ngoja nimpigie simu tena.” Sam alijaribu kupiga simu.

Alvin alishuka kwa kutumia lifti bila kumsubiri. Akiwa njiani kuelekea nyumbani, alihisi mambo yanazidi kuwa mengi huku akiwaza. Hata hivyo, aliogopa kwamba huenda akawa anawaza kupita kiasi juu ya Lisa wakati Lisa mwenyewe hata hamfikirii kabisa. Bila kutarajia, Alvin alipokea simu kutoka kwa Sam mara baada ya kufika nyumbani kwake.

“Hilo haliwezekani kabisa. Sasa hivi Pamela aliniambia kwamba alitembelea familia ya Masawe. Wakamwambia Lisa ameenda nje ya nchi kupumzika, lakini hawakumpa namba yake ya mawasiliano. Damn, kuna kitu kinaweza kuwa kimemtokea?"

Alvin alikunja uso. “Sifikirii hivyo. Baada ya yote, yeye ni binti wa damu kabisa wa familia ya Masawe.

“Labda sivyo. Pamela alisema kuwa familia ya Masawe ina upendeleo sana kwa Lina na inambagua Lisa.

“Sawa. Nitaifuatilia hiyo.” Alvin alisema.

Akiwa na hasira, Alvin kisha akampigia Hans simu. "Tafuta ni wapi Lisa alionekana mara ya mwisho."

Saa moja baadaye, Hans alimletea habari fulani. “Lisa alienda kwenye nyumba ya familia ya Masawe siku tatu zilizopita. Muda mfupi baada ya kuingia ndani ya nyumba hiyo, familia ya Masawe ilielekea kwenye nyumba ya zamani iliyoko Moshi kwa kutumia gari lao. Pengine atakuwa yupo huko.”

“Unamaanisha kuwa anaweza kuwa kafungiwa?”

"Uwezekano mkubwa sana. Familia ya Masawe haingeenda huko isipokuwa kwa matambiko yao ya familia wakati wa mapumziko ya mwisho wa mwaka. Isitoshe, mahali hapo ni mbali sana.”

Alvin aliishika simu yake kwa nguvu. “Fanya uchunguzi ujue mahali nyumba hiyo ilipo kisha unichukue. Nitatembelea nyumba hiyo mimi mwenyewe."

SURA YA 30

Kwa kuzingatia kwamba Moshi iko mbali sana kutokea Dar es Salaam, Hans aliendesha gari kwa saa sita kabla ya kufika huko. Tayari ilikuwa ni saa sita usiku walipofika. Nyumba ya ukoo wa Masawe ilikuwa katika kijiji cha Mbokomu wilaya ya Mosh vijijini. Alvin aliposhuka tu ndani ya gari ndipo alipogundua kuwa mahali hapo palikuwa na ukiwa wa kutisha. Palizungukwa na ukuta mkubwa wenye eneo sawa na uwanja wa mpira. Migomba mingi na miti mikubwa ya miparachichi pamoja na mifenesi ilizunguka jumba hilo na kuliweka katikati. Hakuna mtu aliyeishi humo kwa wakati wote. Jumba hilo lilitumika sanasana kwa ajili ya wanaukoo wa Masawe kukutana mwisho wa mwaka. Kutoka kwa mlango mkuu, ilionekana kuwa nyumba hiyo ilikuwa ya miaka ya sabini au themanini hivi.

Alvin aligonga mlango, lakini hakukuwa na majibu. Kwa hivyo, mara moja alipanda juu ya ukuta. Dakika alipokanyaga chini, miale ya mwanga ilimulika.

"Wewe ni nani? Mbona unaingia ndani ya nyumba usiku wa manane?”

Alvin aligeuka nyuma na kumuona bibi kizee aliyekuwa ameshika tochi. “Natafuta mtu. Niligonga mlango sasa hivi, lakini hukufunguliwa.”

“Mimi pekee ndiye ninayeishi hapa. Ondoka sasa hivi.” Bibi kizee alimsukuma. Alvin alimsukuma tu yule bibi kizee akarudi nyuma. Alichukua tochi na kuelekea kwenye ile nyumba ya ghorofa moja. Alipotazama huku na kule, akapata mshtuko. Aligundua kuwa madirisha yote yalikuwa yamefungwa kwenye sakafu zote mbili huku mlango nao ukiwa umefungwa.

"Fanya haraka uondoke sasa, au nitaita polisi." Kwa hofu, bibi kizee alimsukuma Alvin kwa nguvu zaidi.

“Afadhali upige simu polisi waje wakukamate kwa kosa la kumfunga mtu kinyume cha sheria.” Usemi wake ulithibitisha zaidi dhana yake. Yule bibi kizee akaogopa mara moja.

Alvin akapiga hatua kubwa mbele, kisha akaupiga teke mlango kwa nguvu. Hata baada ya kuupiga kwa muda mrefu, bado alishindwa kuuvunja ule mlango. Alipoona shoka pembeni ya nyumba, alivunja dirisha moja kwa kutumia shoka hilo na kuruka ndani ya nyumba.

Harufu mbaya ikajaa puani mwake. Kwa kuwa nyumba hiyo haikuwa na umeme, ilimbidi kumtafuta Lisa chumba kwa chumba. Hatimaye, alimkuta amejikunja kwenye kona ya kitanda cha mbao.

Bado alikuwa amevalia nguo ile ile ambayo aliiona kabla ya kuondoka mchana ule. Kulikuwa na baridi kali kwenye milima ile ya Old moshi. Hata hivyo, hakukuwa na blanketi na mito kwenye kitanda alichokuwa amelalia Lisa. Hakukuwa na hata na tandiko la kitanda.

Alipomkaribia, aliweza kuhisi harufu iliyokuwa ikitoka mwilini mwake. Hata hivyo, hakuweza kuwa na kinyaa juu ya harufu hiyo. Alimkimbilia na kumtikisa kwa nguvu, lakini hakuonyesha kushtuka. Mwili wake ulikuwa wa baridi kama barafu, huku uso wake ukiwa mweupe kama kipande cha muhogo. Kwa bahati nzuri, aligundua kutoka kwenye ncha ya pua yake kwamba bado alikuwa akipumua kwa shida, au angefikiria kuwa amekufa. Alvin akambeba na kukimbilia mlango mkuu. Bibi kizee aliyekuwa amejificha nyuma ya mlango aliingiwa na hofu baada ya kutambua hali ya Lisa . Kwa kuogopa kukaa tena, mara moja alikimbia kwa kutumia mlango wa nyuma. Alvin hakuwa na muda wa kumkimbilia kumshika. Ikiwa asingempeleka Lisa hospitalini muda huo, bila shaka angeweza kufa.

Wakiwa njiani kuelekea hospitalini, Lisa alibaki ametulia mikononi mwa Alvin. Alvin aliinamisha kichwa chake huku akimtazama usoni. Mashavu yake yalikuwa yamekonda, huku midomo yake kama jeli ilikuwa mikavu na yenye kupasuka. Alivin hakuamini hakuamini kabisa baada ya kujionea tukio hilo. Lisa alikuwa binti wa damu wa familia ya Masawe lakini walimfanyia unyama kama ule. Walikuwa wabaya sana! Ndani kabisa, Lisa alielemewa na kufadhaika na mateso. Alvin alimuonea huruma mwanamke huyo. Wakati huo huo, alijilaumu tena kwa kutomtafuta mapema.

Alvin alimpeleka Lisa katika hospitali ya Mawenzi. Alvin alikosa utulivu wakati akisubiri nje ya chumba cha dharura. Karibu nusu saa baadaye, daktari alitoka kwenye chumba cha dharura na kusema, "Ikiwa mngechelewa kufika hapa kwa saa moja baadaye, tusingeweza kumwokoa.”

“Amezinduka?” Alvin alipumua kwa huzuni. Hatimaye uzito ulikuwa umeondolewa moyoni mwake.

"Ndio, lakini mwili wake umedhoofika sana. Pia, ana homa ya nimonia.” Akiwa amemkazia uso Alvin, daktari aliongeza, “Hajapata maji ya kunywa kwa angalau siku tatu, na pengine hakula chakula cha kutosha pia ama chakula alichokula kilikuwa hakifai. Inawezekana itamchukua nusu mwezi hivi kupona.”

Sio tu kwamba Alvin alishtuka, bali pia Hans alipigwa na butwaa. "Je, akina Masawe wana chembe ya ubinadamu kweli?"

Uso wa Alvin ukaanguka. "Itume habari yote kwenye mitandao, eleza kila kitu kilichotokea leo ili ulimwengu ujue rangi halisi za familia ya Jones Masawe."

“Sawa.” Hans akakubali.

Baada ya Lisa kupata huduma ya kwanza, kesho yake safari yakurejea Dar ikaanza. Lisa aliota ndoto ambapo alikuwa karibu kufa. Hata hivyo, alipokea kumbatio la uchangamfu kutoka kwa mtu aliyesitasita kumwacha aende zake. Ikaja akilini mwake kwamba alikuwa kweli ... bado yuko hai!

Hili ndilo wazo lililompata Lisa mara ya kwanza alipofumbua macho yake.
Wakati huo, mwili wake ulikuwa umefunikwa na blanketi ya joto. Kulikuwa na taa ndogo inayowasha wodini, na kiyoyozi kilikuwa kimewashwa. Hakuwa katika nyumba ya zamani ya giza. Hii ilikuwa ni baada ya kufika Dar es Salaam ambapo Alvin alimpeleka kwenye hospital binafsi ya Premier Care clinic, Masaki.

"Lisa , hatimaye umeamka, mwanamke aliyelaaniwa!" Pamela alimrukia kwa macho mekundu na kusema kwa sauti ya kilio, "Unaendelea kulazwa hospitali baada ya hospitali, na kila wakati hali ni mbaya zaidi kuliko hapo awali. Umenitisha sana.”

“Ni wewe uliyeniokoa?” Lisa aliuliza kwa mshangao. Alikumbuka tu kwamba alihisi kizunguzungu na alionekana kuwaka. Tumbo pia lilikuwa likimuuma sana. Kwa kweli alifikiri kwamba angekufa kwa vile aliteswa sana na njaa, baridi na kiu.

“Hapana, ni Alvin ndiye aliyekuokoa.” Pamela alimwambia. “Nilikuwa nimeenda nyumbani kwenu kukutafuta, lakini haukuwepo. Nilisikia ulipelekwa Moshi na kufungiwa kwenye jumba lenu la ukoo. Mara moja niliwasiliana na Alvin, na akaenda kukuokoa usiku huo. Hapo awali, ulikuwa katika hospitali ya Mawenzi kwa matibabu. Umekuwa katika hali nzuri tangu jana, kwa hivyo Alvin alikuhamisha hadi Hospitali hii. Hajalala vizuri kaka wa watu kwa siku chache zilizopita kwani alikuwa akikutunza kila wakati. Nimemuomba aende nyumbani akapumzike.”

"Ni yeye …?" Lisa alinong'ona kwa kutokuamini, macho yake yakiwa mekundu.
Kinyume na matarajio yake, alikuwa amemwokoa kutoka kwenye matatizo tena na tena. Kwa kweli, hakuwa amemfanyia kitu kingine chochote kando na kumpikia yeye na Charlie mara chache. Alikuwa na deni kubwa kwake.

"Hapo zamani, ulidai kwamba yeye ni mtu asiyejali. Nadhani yeye ni mzuri sana, pamoja na kasoro zake ndogondogo." Pamela aliongeza, “Hata aliviambia vyombo vya habari habari kuhusu wewe kufungwa na kunyanyaswa na familia ya Masawe. Hisa za Kibo Group zimekuwa zikishuka tangu jana, na wengi wanawakosoa baba na mama yako mtandaoni. Hutapingana na wazo lake, sivyo?

“Sitathubutu!” Kwa kutajwa kwa familia ya Masawe, macho ya Lisa yalionyesha hisia kubwa ya chuki. “Kwa vile walipanga kuniua, sitawaacha salama. Nitalipiza kisasi kwao hivi karibuni au baadaye!

Pamela alipumua. “Usijali, Kibo group imeumizwa sana safari hii. Thamani yake ya soko imeshuka kwa angalau dola milioni kadhaa.

Lisa alisema bila kujali, "Pamela, nitawafanya wale wote walionidhulumu walipe gharama siku moja."

Pamela alipigwa na butwaa alipohisi mabadiliko ya mtazamo wa Lisa . “Kwa kweli, unaweza kumwomba Alvin akusaidie. Hufikirii… ameanguka kwa ajili yako?”....ITAENDELEA....

Sasa Lisa ameamua ila atufahamu kama kweli ataweza kuwashughulikia wabaya wake au maneno tu anaongea ili kujifurahisha, basi kwa leo tuishie hapa lakini sehemu inayofuata itakupa majibu ya maswali yako.

LIPIA USOME HARAKA.

Vitabu vinazidi kuandikwa na baadhi vimekamilika lakini pia unaweza kusoma kwa kulipia kulingana na episode unazotaka.

Episode - 20 Tsh 1000/=
Episode - 30 Tsh 1500/=
Episode - 40 Tsh 2000/=
Episode - 50 Tsh 2500/=

Namba za kulipia

0628924768 (Halotel) JUMA HEMBA
0694288555 (Airtel) JUMA HEMBA
0764736557 (Voda) HADIJA KIRUNGI

"Lipia utumiwe similizi yako sasa whatsapp 0628924768"

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
JINA LA SIMULIZI............................LISA
AUTHOR...........................JOMBA WAJO
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP.........................0628924768
SEHEMU YA..................................31&32

SURA YA31

Alvin na Sam walingia hospitalini pale mida ya jioni. Sam aliweka kikapu cha matunda kwenye meza ya kahawa, kisha akamsalimia Lisa kwa tabasamu. "Shemeji, unajisikia vizuri?"

"Vizuri zaidi." Lisa kwa siri alitazama pembeni kwa Alvin aliyekuwa kasimama kimya. Lisa alipepesa macho yake kwa utii. "Samahani kwa kukuletea shida tena."

“Ni vyema kama umelitambua hilo. Nilidhani wewe ni mjinga tu.” Alvin alikasirika bila sababu kumuona Lisa akiwa amekonda mithili ya mfuko wa mifupa. Maneno makali yakamtoka kinywani mwake. “Sijapata amani hata siku moja tangu nikuoe. Sitaki kuhojiwa na polisi ukiwa umekufa siku moja. Unaelewa?"

"Haitatokea tena wakati ujao." Lisa aliuma mdomo wake uliopauka kuzuia machozi yasiendelee kuchuruzika mashavuni mwake.

Upepo wa kufadhaika ulimpitia. Alvin hakutaka kuendelea kumfundisha, lakini alihitaji aache kufanya makosa ya kipumbavu namna hii. “Simu niliyokununulia iko wapi? Kwa nini iliachwa nyumbani kwa akina Masawe?”

"Mama yangu alinidpokonya na kuikatalia."

"Kweli wewe ni nguruwe." Alvin alifoka.

“Uko sahihi. Tafadhali niite Nguruwe Masawe kuanzia sasa.”

Mapovu ya kicheko kilichoshindwa kuzuilika yalitoka kwenye midomo ya Sam, na kulainisha hali ya wasiwasi katika wodi ya hospitali. “Sawa, Alvin, acha kumponda. Hakuna mtu ambaye angetarajia ukatili kama huo kutoka kwa wazazi wake waliomzaa.”

Lisa alitetemeka. Baada ya kuona hivyo, Alvin aligeuza macho yake kwa Lisa na kumuonya. "Kaa mbali na familia hiyo ikiwa unataka kubaki hai."

"Hiyo ni sawa." Sam aliitikia kwa kichwa. “Zingatia tu kumwandalia rafiki yangu chakula. Tazama jinsi amekuwa na hasira baada ya kutoweza kufurahia milo yako iliyopikwa nyumbani katika siku chache zilizopita.”

“Sam Harrison.” Alvin akatupa jicho la hatari upande wake.

Sam aliacha kusema mara moja. Lisa hakuweza kupinga tabasamu usoni mwake. “Nitapona hivi karibuni na nianze kukupikia tena.”

"Kaa kimya na uzingatie kupona." Sauti ya Alvin ilikuwa ya ukali kama kawaida, lakini maneno yake yalileta uchangamfu moyoni mwake.

“Alvin, asante, kweli.” Lisa alishukuru kwa dhati.
•••
Siku mbili baadaye, Ethan akiwa kwenye ofisi za kampuni yao, ‘Lowe Enterprises’, alikutana na habari ya Lisa mtandaoni iliyosambazwa pamoja na cheti cha matibabu kilichotolewa na Dk Johnson. Ethan alishtushwa sana. Mara moja, aliingia kwenye gari na kukimbilia kwenye makazi ya akina Masawe.

Alipofika, aliwahoji wanandoa hao wazee huku akijaribu sana kuzuia hasira yake. “Mjomba Jones na Shangazi Masawe, ni kweli mlimfungia Lisa kwenye makazi ya zamani ambapo mlikataa kumpa maji na kumlisha chakula kibovu?”

“Upuuzi gani huu Ethan. Ulikua na sisi muda wote. Unafikiri tunaweza kufanya hivyo?" Johes Masawe alikasirika na kufadhaika kwa wakati mmoja. “Kwa kweli, nilimweka kwenye makazi ya zamani lakini alitunzwa vizuri na watumishi kwa chakula kitamu kila siku. Yeye ni binti yangu wa kuzaliwa, hata hivyo. Ningewezaje kuwa mkatili hivyo?”

"Lakini inaenea mtandaoni kwamba ..."

Lina alimkatisha kwa huzuni, "Zote ni habari za uwongo. Sielewi kwa nini Lisa angeidharau familia yake kama hivi baada ya kuondoka kwenye makazi ya zamani na marafiki zake. Mama na Baba wana wasiwasi sana juu yake. Walimweka tu katika makao ya zamani ili asichangamane na watu wabaya na kuharibu sifa yake huko mitaani tena.”

Hilo lilimshangaza Ethan. Maneno magumu yalienea usoni mwake baada ya kukumbuka uvumi aliosikia muda si mrefu uliopita. Sasa, alielewa uamuzi wa familia ya Masawe. “Samahani, sikuwaelewa nyote.”

Mama Masawe aliweka mkono juu ya kifua chake kwa huzuni. "Sijali maoni ya watu juu yetu mtandaoni kwani tumeshindwa kama wazazi. Lakini Kibo Group ambayo tumetumia muda mwingi na juhudi kuijenga iliharibiwa mara moja. Hisa za kampuni ziko chini kabisa kwa siku kadhaa zilizopita na thamani yake ya soko ilipungua kwa zaidi ya dola milioni. Kinachotia wasiwasi zaidi ni kwamba kila mtu mtandaoni anaisusia Kibo Group sasa. Mambo yatakuwa mabaya sana ikiwa hii itaendelea."

Ethan alikatishwa tamaa na alichokisikia. Kufaulu au kutofaulu kwa kampuni ya Kibo Group kulimuathiri sana yeye mwenyewe. "Tunahitaji kudhibitisha kwa umma kuwa familia ya Masawe iko kwenye uhusiano mzuri na Lisa. Kisha, tunaweza kuajiri kundi la watu kutangaza hili mtandaoni ili kufuta uvumi huo.”

“Ni wazo zuri.” Johes alikubali kwa kichwa. "Tarehe ya sherehe yako ya uchumba inakaribia. Vyombo vya habari pia vitakuwepo. Tunahitaji tu Lisa kujitokeza ili kubadilisha taswira ya kampuni.”

“Atajitokeza kweli?” Lina alimtazama Ethan kwa wasiwasi. “Ujue bado anakupenda. Sidhani kama anaweza akaja."

“Nitafikiria jambo fulani la kumshawishi Lisa ahudhurie.” John Masawe alisema.
•••
Lisa alilazwa hospitalini kwa siku tatu kabla ya kuruhusiwa kurudi nyumbani. Aliporudi nyumbani alishangaa kuona kwamba Charlie alikuwa ameongezeka unene. Alifikiri kwamba paka huyo angekuwa dhaifu kwa kukosa mtu wa kumtunza ipasavyo siku chache zilizopita.

Alvin alipofika nyumbani baadaye usiku huo, alimsikia Lisa akinung'unika wakati akimlisha paka. “Charlie, inabidi uache kula sana. Angalia ukubwa wa tumbo lako. Ni kana kwamba una mimba ya kujifungua!”

Tumbo la mimba la Charlie lilikuwa likiongezeka kadiri siku zilivyopita. Alvin asingeweza kuweka siri hiyo kwa muda mrefu zaidi. Hata hivyo, bado ilikuwa bora kuwa na mtu wa kumhudumia nyumbani. Alvin alitokea tena akiwa amevaa nguo za kawaida za mapumziko. Lisa alikuwa tayari ameshaandaa meza ya chakula.

Lisa alimwandalia Alvin meza ya shukrani iliyojumuisha aina zake zote za vyakula anavyopenda. Macho ya Alvin yaliwaka kwa furaha baada ya kuvitazama vyakula vilivyotapakaa mezani. “Nimechoshwa na kula vyakula vilivyochomwa na kukaangwa. Tengeneza hata supu au kitoweo wakati mwingine,” Alvin alijivungisha kama kawaida yake huku akivishambulia.

Baada ya chakula cha jioni, Alvin alirudi kwenye chumba cha maktaba kuendelea na kazi. Alvin aliendelea na kazi hadi karibu saa sita usiku. Lisa alitayarisha kahawa na kumpelekea. Alvin alikuwa ameketi kwenye dawati, akichanganua hati zilizo chini ya mwanga mkali huku akirejelea kompyuta ya mkononi kwa wakati mmoja. Jozi ya miwani yenye fremu za dhahabu ilikaa kimya kwenye daraja la pua yake.

"Utaendelea kutazama hadi lini?" Lisa alimuuliza Alvin wakati akimkaribisha kikombe cha uji wa ulezi.
Alvin akafunga laptop yake na kugeuka kumwangalia kwa utulivu kisha akapokea kikombe cha kahawa.

“Sijawahi kukuona umevaa miwani hapo awali. Nilikaribia kuzimia kwa sababu ya haiba yako ya kuvutia,”Lisa alisema huku akitabasamu.

“Bado hujaacha maneno yako?”

Lisa akaguna. Hatimaye, muda mfupi baadaye, alizungumza tena, “Mwonekano wako mzuri hunivutia kwa njia tofauti kila siku. Kadiri ninavyokutazama, ndivyo ninavyozidi kuvutiwa nawe. Haichoshi…”

Kabla Lisa hajamaliza sentensi yake, ghafla mkono mkubwa ulionekana kumziba mdomo. Mkono wa Alvin ulinuka kama msonobari mkavu. Harufu hafifu ilimtuliza kwa kushangaza. Muhimu zaidi, mkono wake ulikuwa na joto sana!

"Nyamaza." Macho ya Alvin yalipepesa chini ya lenzi za miwani yake.
Alihisi mashavu yake yakiungua pia.

Baada ya kuondoa mkono wake, aliweka kikombe cha kahawa kwenye meza. "Ninahisi lazima uwe umechoka kufanya kazi usiku kucha. Kikombe cha kahawa kitakuchangamsha kidogo."
Alvin aliitazama ile kahawa iliyochanganywa kwenye mazima. Hakika ilionekana kumvutia.
"Lisa , unajaribu kunifanya nishindwe kulala, hujui kahawa kufukuza usingizi?"

"Hapana, kahawa haifukuzi usingizi." Alimshawishi. “Itakuchangamsha tu na kukufanya ujisikie na nguvu mpya kimwili na kiakili."

Alvin aimtazama huku pembe za mdomo wake zikicheza kwa dharau. "Sawa. nitakunywa. Ila nikikosa usingizi ujue tutakesha wote hapa.”

“Usijali. Hata ukisema tulale pamoja hadi asubuhi, nitafanya.” aliahidi.

“Sithubutu kutegemea hilo. Ninaweza kufa kabla hata halijatokea.” Alvin alijibu huku akijinywea kahawa yake.

Lisa ambaye alikuwa ametoka tu kudhihakiwa, alitoka nje ya maktaba akiwa ameudhika. Aliapa kumthibitishia kuwa ipo siku angemtaka tu!.

SURA YA32

Saa saba usiku Lisa alishtushwa na ndoto zake mbaya, ndipo akagundua kuwa alikuwa anatokwa na jasho kwenye paji la uso wake. Mara moja akawasha taa. Utulivu ulikuja juu ya mwili wake taratibu huku mwanga ukitawala giza.
Alikuwa ameota juu ya kufungiwa ndani ya nyumba ile yenye giza tena. Sehemu hiyo ilijaa kila aina ya kelele za kutisha usiku. Kwa hofu, alijikunja ndani ya shuka.

Ilikuwa ni shida kwake kulala peke yake sasa. Baada ya muda wa kufikiria, alijifunika blanketi na kubisha hodi kwenye mlango wa chumba cha kulala cha Alvin.

“Nani huko?” Alvin, ambaye alikuwa amekereka kwa kuamshwa usiku wa manane, aliuliza kwa sauti iliyojaa hasira.

“Ni mimi.” Lisa aliitikia kwa hofu. Nusu dakika ikapita kimya kabisa. Alipotaka kukata tamaa, mlango ulifunguliwa ghafla kutoka ndani. Alvin akatokea upande wa pili wa mlango. Nywele zake zilikuwa zimevurugika na macho yake meusi yalionekana kuogopesha.

"Afadhali uwe na sababu nzuri ya kunisumbua."

“Naogopa kulala peke yangu…” Lisa alitetemeka.

Alivin aliinua macho yake taratibu. Jasho lilikuwa likimvuja Lisa usoni kwa sababu ya hofu. Hata hivyo, alishangazwa na blanketi alilokuwa ameshikilia mikononi mwake.

"Hii ni mbinu yako nyingine ya kunitongoza?" Alvin alikiri moyoni mwake kuwa karibuni uzalendo ungemshinda. Hata hivyo, alikuwa amechoka sana na kazi za kutwa nzima na bado alihitajika kuamka mapema kwa ajili ya kesi mahakamani kesho yake. “Ni usiku sana. Nahitaji kulala hata kama wewe huna haja ya kulala.”

"Sio hivyo." Lisa hakutaka kubaki peke yake chumbani kwake. Aliongeza nguvu na kuvuta kona ya mkono wake. “Tangu nifungiwe kwenye nyumba ya giza kijijini naogopa kulala peke yangu usiku. Ninasumbuliwa na jinamizi la kutisha. Tafadhali niruhusu nilale japo kwenye sakafu ya chumba chako. Niko serious.”

“Si ulikuwa umelala vizuri hospitalini?”

"Nilikuwa na mlezi wakati huo." Lisa alijitetea huku akitetemeka.

Ni Alvin ambaye alikuwa amemuokoa kutoka kwenye nyumba hiyo ya zamani. Mahali hapo palikuwa kimya sana na giza muda wote kama usiku. Hata mwanaume angepatwa na kiwewe baada ya kufungiwa mle ndani kwa siku tatu.

Lisa aliona kusita kwake kama kukubali, na akatoa ahadi haraka. "Naapa sitakusumbua."

“Kumbuka ahadi yako.” Alvin alirudi kitandani kwake bila wasiwasi.

Baada ya kupata kibali chake, Lisa haraka akaweka blanketi kwenye sakafu karibu na kitanda chake. Alvin alikaa makini kwa muda mfupi lakini punde akapitiwa na usingizi. Hata hivyo muda fulani baadaye, kilio cha Lisa kilimwamsha tena.

“Fungua mlango… Tafadhali… ni baridi… giza sana… ninaogopa.”

Alvin akajiinua kutoka kitandani. Mwangaza wa mbalamwezi uliomiminika kupitia dirishani ulimulika kivuli chini. Lisa aliyekuwa amejikunja ndani ya blanketi alikuwa ameziba masikio yake kwa nguvu. Mwili wake wote ulikuwa ukitetemeka kwa hofu.

“Lisa amka. Ni ndoto tu.” Alvin alitoka kitandani ili kumvuta mikono. Lakini, Lisa alikuwa kazama kabisa katika ndoto hiyo mbaya. Uso wake wa hofu ulikuwa umepauka kama kauzu. Akiwa hana njia nyingine, akamvutia kifuani kwake na kumpigapiga mgongoni taratibu.

"Ni sawa. Uko salama sasa…” Sauti ya Alvin ilikuwa na athari ya kutuliza ambayo polepole ililegeza mkazo mwilini mwake.

Uso wake mdogo ulisukumwa kifuani mwake. Nywele zake za giza zinazong'aa zilikuwa zimening'inia mabegani mwake huku nyuzi kadhaa zikiwa zimepigwa plasta kwenye ukingo wa uso wake wa kusikitisha lakini mzuri. Pia alitoa harufu hafifu ya kutuliza. Hii haikuwa harufu ya manukato, badala yake, ilikuwa harufu ya shampoo yake. Hakuwahi kutambua jinsi shampoo yake ilinukia vizuri hadi wakati huu. Harufu hiyo ilimfunika taratibu hadi akafumba macho hatimaye. Aliwaza kumwachia mara baada ya kutulia kabisa. Hata hivyo, ilikuwa tayari asubuhi iliyofuata alipofungua tena macho yake.

Wawili hao walijikuta wakitumia kitanda kimoja, shuka moja na mto mmoja. Mkono wake wa kushoto na mguu wa kushoto ulikuwa umewekwa juu ya mwili mwake. Kulikuwa na tabasamu la kudumu kwenye pembe za midomo yake. Ilionekana alikuwa na usingizi mzuri.

Alvin pia hakujisikia raha. Alihisi hata kwa sekunde ya haraka kwamba walikuwa kama wanandoa wapya. Alvin aliwaza bila kufikiria kwa sekunde chache kabla ya kunyanyua blanketi kwa uangalifu ili asimame. Bila kutarajia, mtazamo chini ya blanketi ulimshangaza. Karibu vifungo vyote vya pajama za Lisa vilitenguliwa. Wakati huo Lisa naye alifungua macho yake polepole. Macho yao yalikutana na mboni zake zlipanuka polepole.

Alipiga kelele kwa mshtuko sekunde tu alipogundua kuwa alikuwa amelala mikononi mwa Alvin. Lisa alinyanyuka kwa haraka na kujiweka mbali na mwanaume huyo. "Kwa nini ... kwa nini umenileta kitandani kwako?"

Alvin alidhihaki kwa kutoamini. “Ulinizunguka huku ukilia wakati ukiota ndoto mbaya jana usiku. Nilikuwa nikikufariji na kukutuliza…”

“Umenifariji?” Aliona jambo hili kuwa gumu kuamini.

Uso wa Alvin ukajaa hasira. “Unajaribu kusema nini? Lisa, sema kweli sasa hivi. Je, jana usiku kilikuwa ni kitendo cha makusudi? Ulikuja chumbani kwangu ili kunitega, huh?"

“Sijui unazungumza nini. Nililala vizuri sana.” Alikumbuka bila kufafanua kuwa alipata ndoto mbaya mwanzoni, lakini alihisi amani wakati sauti ya upole ilinong'ona masikioni mwake. Subiri, sauti hiyo ya upole ilikuwa ya Alvin?

Alvin alimtazama kwa macho makali wakati anainuka na kusimama. "Kabla hujaendelea kuongea, angalia hali ya nguo zako za kulalia."

Akiwa amechanganyikiwa, Lisa alishusha macho yake. Sura ya mshtuko na aibu ilimwangazia usoni mwake alipojiona alivyokuwa kifuani. Mikono yake iliruka kukifunika kifua chake mara moja.

Alvin akafoka. “Uigizaji mzuri. Nina hakika ulifungua vifungo hivyo kwa siri ili kunitega.”

“Sina haja ya kufanya hivyo.” Lisa alijisikia kulia wakati huu. “Vifungo vilifunguka vyenyewe. Si kosa langu kuwa na matiti makubwa.”

"Kwa hivyo kama una matiti makubwa ndiyo uyaache waziwazi? Sema tu ukweli kuwa unajaribu kunitega." Alvin alisema huku akimtazama Lisa kwa dharau.

“Ndiyo! Um… Ninaweza kueleza hili. Ni kwa sababu mimi…nakupenda kupita kiasi,” Lisa alisema kwa sauti iliyotiwa chumvi. Akiwa amechanganyikiwa, alisonga mbele na kuishika shingo ya Alvin.

Kwa kweli, Alvin alishtushwa na kitendo chake cha ghafla na ambacho hakuwa amekitarajia.
‘Je, mwanamke huyu alikuwa akijaribu kumlazimisha busu?’ Alvin alijiuliza huku picha ya midomo yake nyororo ikaingia akilini mwake. Alisita kwa sekunde kadhaa kabla ya kusikia maumivu makali mashavuni mwake. Lisa alikuwa amempiga Lovebite!. Alvin alimsukuma Lisa kwa nguvu huku mkono wake ukiruka kufunika sehemu aliyong’atwa.

“Lisa, unathubutu vipi? Usifikiri sitakuadhibu kwa hili.” Macho ya Alvin yalikuwa kama miali ya moto.

Lisa akacheka tu kwa mzaha huo na kumwambia. “Kwani hujawahi kuiona kwenye sinema za kihindi? Waigizaji wakuu huwa wanamng’ata mtu wanayempenda sana. Nilikuwa najaribu tu kuacha alama kwako.”

Alvin akapiga hatua kadhaa mbele, huku akiwa ameuma meno kwa hasira. "Unanichukulia kama mjinga sivyo?"

"Sawa, unaweza kuning’ata na wewe kulipiza kisasi." Lisa alijikaza na kuinamisha uso wake karibu na Alvin. "Ning’ate kwa nguvu kadri uwezavyo. Ukining’ata kwa nguvu zaidi nitajua unanipenda zaidi.”

Bila hata kujiuliza, Alvin alikiweka kichwa cha Lisa katikati ya viganja vyake na kumng'ata kwa nguvu kwenye shavu. Shavu nene la Lisa lilikuwa nyororo na laini kama jeli. Hakutaka kusogeza midomo yake mbali.

“Loo!” Lisa alipiga kelele kwa uchungu.

Hatimaye, Alvin baada ya kuona meno yakiwa yameganda kwenye mashavu yake yaliyonenepa, alimwachia. "Kumbuka adhabu hii."

Lisa alijifanya mwenye haya licha ya maumivu. "Hapana, hii siyo adhabu, huu ni uthibitisho wa upendo wako."

"Endelea kuota." Alvin alicheka kwa kejeli kabla ya kuingia bafuni na kufunga mlango kwa nguvu. Taswira kwenye kioo ilionyesha alama za meno kwenye shavu lake mwenyewe. Alihisi kukimbilia mlangoni ili kumchana mwanamke huyo vipande vipande.

Ilimbidi awe mahakamani siku hiyo kwa hiyo ilimbidi aende akiwa amevalia barakoa. Akiwa amekasirika, Alvin alipata tu kifungua kinywa kidogo kabla ya kuondoka nyumbani.

Saa tatu asubuhi Alvin aliwasili ofisini kwao. Sam alimpokea kwa swali, “kwa nini umevaa barakoa? Unaumwa?" Alvin alikataa kujibu. "Eh, ni vizuri kuwa unajali na kuvaa barakoa ili kuzuia kueneza korona. ” Sam alimpongeza baada ya kumuona yupo kimya.

Baada ya kukamilisha taratibu kadhaa za kiofisi, walielekea katika mahakama ya Kisutu kwa ajili ya kusimamia kesi. Dakika kumi baada ya kuwasili kwao, kesi ilikuwa karibu kuanza. Sam nusura aangue kicheko hadharani wakati Alvin alipotoa barakoa yake na kufichua alama za meno kwenye shavu lake.

"Ni nini …?"

"Nimeng’atwa na mbwa." Sauti kali ya Alvin ilisikika kwa vitisho. Aliingia ndani ya chumba cha mahakama kwa hatua kubwa.

Sam hakuweza kujizuia tena kuangua kicheko. Alvin alifikiri angeweza kumpumbaza? Mwanamume huyo alikuwa ameng’atwa na mwanamke. Hakuwahi kumuona Alvin akiona aibu vile. Kwa hiyo alimpiga picha kwa siri na kuituma kwenye group lao la whatsapp...ITAENDELEA....

Kwa leo naomba tuishie hapa najua unaendelea kuburudika na simulizi hii kali sana ambayo ndio itakuwa funga mwaka na fungua mwaka Mungu akijaalia, kwahiyo basi nikusihi tuungane katika episode inayofuata ili kujua nini hatima ya Lisa na Alvin endapo Lisa atatambua kuwa Alivin si mjomba wa Ethan....

SOMA SIMULIZI HII HARAKA

Unaweza lipia na kusoma simulizi hii kwa njia ya Whatsapp kwa kununua episode.

Episode - 20 Tsh 1000/=
Episode - 30 Tsh 1500/=
Episode - 40 Tsh 2000/=
Episode - 50 Tsh 2500/=

Namba za kulipia

0628924768 (Halotel) JUMA HEMBA
0694288555 (Airtel) JUMA HEMBA
0764736557 (Voda) HADIJA KIRUNGI

"Lipia utumiwe similizi yako sasa whatsapp 0628924768"

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
JINA LA SIMULIZI............................LISA
AUTHOR...........................JOMBA WAJO
SPONSORED BY......SIMULIZI ZA DULLY
WHATSAPP.........................0628924768
SEHEMU YA..................................33&34

SURA YA 33

Lisa alipumzika nyumbani kwa siku kadhaa, akisubiri alama za meno shavuni kwake kutoweka kabla ya kwenda kutafuta kazi mpya. Lakini, kila alikotuma maombi ya kazi, alipokea maoni hasi tu.

"Bi Jones, samahani lakini hatuajiri waizi wa kazi za wangine."

"Bi Jones, kashfa yako imekuwa habari ya kawaida katika sekta ya ujenzi. Hakuna mtu anayethubutu kukuajiri tena.”

"Bi Jones, familia ya Jones Masawe imetangaza kwenye mtandao wa sekta nzima kwa siri kwamba mtu yeyote ambaye atathubutu kukuajiri atakuwa anawadharau waziwazi."

Lisa alikutana na majibu kama hayo kwenye mahojiano ya kazi na makampuni kadhaa aliyotuma maombi. Alikatishwa tamaa kabisa na kupandwa hasira kwani alikuwa ametumia muda mwingi na bidii katika elimu yake lakini bado hakuweza kupata kazi.

“Pipiii…” Mara akagutushwa na sauti ya honi. Gari lililokuwa karibu naye lilipiga honi mara kadhaa. Hakutambua kama mtu huyo alimkusudia yeye hadi alipomwita jina lake. "Lisa !"

Lisa alitazama kwenye gari hilo na kuona uso mzuri ukichungulia nyuma ya dirisha la Range Rover. “Joseph? Unafanya nini hapa?" Lisa alipatwa na mshangao wa furaha baada kumuona mwandamizi wake kutoka Chuo Kikuu cha New South Wales alikokuwa ameenda kusoma.

“Nina ofisi katika jengo hili. Nilikuona ukitoka nje nikashangaa unafanya nini hapa." Joseph aliegesha gari lake pembeni na kumpa ishara aingie ndani. Lisa alipoingia ndani ya gari alijibu kwa kinyonge, “Nimekuja kwa mahojiano ya kazi, lakini sijafanikiwa.”

“Hata wewe hukuweza kufanikiwa na sifa zako?” Joseph aliona jambo hilo kuwa gumu kuamini.

“Nimekosana na familia yangu na wananichafua kwenye mtandao mzima wa sekta ya ujenzi. Sifa yangu yote inazidi kuporomoka!” Lisa alimwambia Joseph kwa huzuni na kumweleza kila kitu kwa undani wake.

“Siamini kwamba unaweza kuiba kazi za wengine. Inapaswa kuwa kinyume chake." Tabasamu likatanda usoni mwa Joseph. "Sawa, nimeanzisha kampuni mpya hapa Dar es Salaam na bado sina wafanyikazi wa kutosha. Njoo ujiunge na timu yangu."

Lisa alishtuka na kuguswa wakati huo huo. “Huna shaka nami hata kidogo?”

"Najua wewe ni mtu mzuri wa tabia na ninafahamu vyema vipaji vyako. Nilikuwa nimekupendekezea hapo awali kwamba tuanzishe biashara pamoja huko Uganda baada ya kuhitimu, lakini ulisisitiza kusaidia biashara ya familia na kukaa karibu na mpenzi wako. Vipi umeolewa sasa hivi?" Joseph aliuliza.

Lisa akainamisha kichwa kwa aibu na kujibu. "Tuliachana."

Joseph alionekana kushangaa lakini haraka akamfariji kwa upole. "Ni sawa. Bado wewe ni kijana na mrembo. Nina hakika unaweza kupata mtu bora zaidi.”

"Inatosha kuzungumza juu yangu.” Lisa akahamisha mada. “Unafanya vizuri sana kwenye kazi. Nilisikia umekuwa mbunifu watatu bora zaidi huko Uganda na hata kuchapisha vitabu kadhaa.” Lisa alitania huku akitabasamu. "Na sasa unajaribu kushindana hapa Bongo pia?"

"Jiunge na kampuni yangu ikiwa unadhani nina uwezo. Ninahitaji watu wenye talanta kama wewe,” Joseph alimshawishi kwa bidii, “naweza kukupa mshahara mkubwa. Unaweza pia kuwa mwanahisa biashara itakapoingia sokoni.”

"Sawa, nitakuandalia chakula cha jioni leo ili kusherehekea kuwa bosi wangu." Lisa hakika hakutarajia mshangao huu wa kupendeza. Alimpigia simu Alvin na kumwambia. “Sitakuwa nyumbani kuandaa chakula cha jioni. Panga mwenyewe."

Alvin alikasirika sana siku hiyo kwa sababu wengine walikuwa wakimdhihaki kwa siri kutokana na alama za meno kwenye shavu lake. “Nini tena muda huu? Usifanye ujinga wako ukidhani nitakuokoa tena. Sina muda.” Alvin alimjibu kwa hasira.

Lisa alimwambia kwa upole. "Ninaenda tu kula chakula cha jioni na rafiki yangu niliyekutana naye nikiwa nasoma nje ya nchi."

Alvin alicheka kwa kejeli. "Loo, kwa hivyo ni rafiki kutoka chuo kikuu wakati huu. Usisahau jinsi ulivyotekwa hotelini na rafiki yako wa shule ya sekondari mara ya mwisho.”

"Nilikuwa nakupa taarifa tu. Kwaheri.” Lisa alikata simu kwa papara.

Hali ya kukatishwa tamaa iliangaza machoni pa Joseph alipouona uso wake wenye hasira. “Mpenzi mpya? Au mume?”

Alitoa macho kwa mshtuko. "Hapana. Ni mwenzangu tu… Housemate.” Lisa hakuwa amekosea hata hivyo kwa kujibu vile. Ingawa Alvin alikuwa mume wake halali wa ndoa, mwanamume huyo alikataa kukiri hilo. Kwa hivyo, uhusiano wao ulikuwa wa maonyesho tu.

Joseph alitoa tabasamu hafifu. "Ilionekana kama unazungumza na mpenzi wako."

“Um… Kweli?” Lisa alihisi mapigo ya moyo yakirukaruka. Hivi ndivyo alivyokuwa akitangamana na Alvin. Labda ilisikika tu kwa sababu walikuwa wakiishi katika nyumba moja.

Ilikuwa ni muda mrefu sana tangu alipokutana na Joseph huko Marekani. Wawili hao walifurahia jioni pamoja na chakula cha jioni kilidumu hadi saa tatu usiku. Alimpa lifti na kumpeleka hadi nyumbani kwani siku hiyo Lisa hakuwa anatumia gari lake.

“Kumbuka kuripoti kwangu kesho asubuhi. Nimechukua mradi wa jengo la kifahari katika eneo la Mbezi Beach. Utaenda kuchukua vipimo kesho."

“Hakika.” Lisa alimpungia mkono wa kwaheri. Macho yake yaliikodolea gari hiyo aina ya Range Rover kwa mbali kabla hajageuka kuelekea nyumbani.

Kwa bahati mbaya, alimgundua Alvin, akiwa amevaa nguo za kawaida za mapumziko akimtazama chini kwa hasira kutoka kwenye ngazi. Charlie alikuwa ametulia mikononi mwake, akionekana kama alikuwa karibu kulala.

“Rafiki yako ni mwanaume?” Alvin aliuliza kwa hasira, ndita zilizokuwa zimekunjwa katikati ya macho yake zingeweza kumfinya inzi hadi kufa. Alipofikiria jinsi ambavyo alilazimika kuvumilia chakula kilichotengenezwa mgahawani vibaya wakati Lisa alifurahia jioni hiyo kula na kucheka na mwanaume mwingine, hasira ilimpanda kama mawimbi ya bahari.

“Ndiyo, yeye ni mwandamizi wangu kutoka chuo kikuu…”

Alvin alimkatisha. “Lisa, ngoja nikukumbushe kuwa umeamua kuolewa na mimi. Afadhali uangalie matendo yako hata kama tuko kwenye ndoa ya mkataba. Sitaki kusalitiwa.”

Tabasamu usoni mwa Lisa likaganda. “Unasemaje? Nilitoka tu kwenda kula chakula cha jioni na rafiki. Je, unanifikiria miye ni mhuni sana?”

"Nani anajua? Nimekufahamu kwa muda mfupi tu.” Alvin aliongea kwa tabasamu la kejeli. "Mbali na hilo, huwezi kwenda tu kwa chakula cha jioni na kusahau kuhusu jukumu lako kama mhudumu wa Charlie. Unawajibika kwa ajili yake kwani wewe ndiwe uliyemsababishia ugonjwa.”

“Charlie yuko sawa sasa. Nadhani hata aliongezeka kilo chache,” Lisa alijibu kwa upole. Bila shaka angebishana naye ikiwa asingekuwa kaokoa maisha yake mara mbili.

Alvin alicheka. “Sawa, kwa nini ameongezeka uzito? Unapaswa kujitafakari. Nataka umtunze paka, sio kumnenepesha.”

Lisa alishindwa cha kusema. Kuongezeka kwa hamu ya kula kwa Charlie lilikuwa kosa lake pia.
Alikaribia kushindwa kuzuia hasira iliyokuwa ikifuruma kifuani mwake. "Sawa, nitampa paka chakula kidogo kuanzia sasa."

"Hilo halitasaidi pia." Alvin bado alimkalia vibaya. “Je, ikiwa paka ndani yake atakuwa na utapiamlo?”

“Sawa, unataka nini basi? Samahani, lakini mimi si mfugaji wa paka kitaaluma.” hatimaye Lisa alisema kwa hasira.

“Hata mimi sijui.” Alvin naye akajibu kwa ukali. “ Ifanyie utafiti na umfikirie zaidi Charlie. Mpeleke matembezini ukiwa huru. Usimpe chakula tu kisha umruhusu alale siku nzima.” Kisha kusema hayo, Alvin alitembea kuelekea kwenye bustani ya jirani na Charlie mikononi mwake.

Lisa aliishia kumshangaa tu mwanamume yule mwenye gubu. Alitaka kushiriki naye furaha ya kupata kazi mpya, lakini hakuweza kujisumbua kuzungumza naye kwa sekunde nyingine zaidi. Alipokuwa akiingia ndani kuelekea chumbani kubadilisha nguo, sauti kali ilisikika nyuma ya mgongo wake. "Nina njaa."

Alitazama nje na kumwona mtu aliyeketi kwenye bustani, akionekana kama mnyama mwenye njaa kali anayesubiri kulishwa.

Lisa alikataa, kwani bado alikuwa amekasirika kutokana na kejeli zake hapo awali. "Samahani, mimi ni mhudumu wa paka wako, sio mhudumu wako." Alisisitiza maneno matatu ya mwisho.

Alvin alionekana kutopenda. Alichia tabasamu la kejeli na kuongea kwa sauti ya kutetema. "Huu ndio upendo unaotangaza kuwa wewe ni mke wangu?"

'Ninachotaka ni nafasi ya kuwa shangazi wa Ethan! Umeipata hiyo!' Lisa alijiwazia, lakini hakuthubutu kuyasema maneno hayo kwa sauti. Akiwa amekasirika kidogo, aliingia jikoni na kuanza kuandaa chakula.

Alvin alikuwa akisubiri chakula kwa hamu akiwa anazunguka bustanini na paka wake. Hakuna chochote zaidi ya chakula alichotayarisha Lisa kilichomtia hamu tena. Labda alikuwa amemtilia dawa kwenye chakula alichokuwa anakula muda wote huo.

••••••

Baada ya kifungua kinywa asubuhi iliyofuata Alvin alikuwa amevaa kiofisi tayari kuelekea kazini alipogundua Lisa naye alikuwa amebadilika na kuvaa kimtoko-mtoko hivi. Lisa alikuwa amevaa shati la waridi iliyokolea na suruali ya jeans iliyombana kidogo. Alionekana kama mfanyabiashara hodari, lakini mavazi hayo pia yaliangazia umbo lake mwanana. Isitoshe, alikuwa amejipodoa kidogo na hereni za lulu zilining'inia chini ya masikio yake. Aliona ni vigumu kumvua macho mrembo huyo.

Alvin aligundua kuwa Lisa alikuwa akitoka. “Unatoka kwenye miadi yako tena?” Sauti yake ilikuwa ya chini ikionyesha kutofurahishwa kwake.

“Hapana, naenda kazini. Nilipata kazi mpya jana. Nitakuwa nyumbani kuandaa chakula cha jioni na pia kumtembeza Charlie baada ya hapo.”

Alvin hakupata maneno ya kubishana na hilo. Pamoja na hayo, hakuwa na wasiwasi kuhusu kazi yake. Akamuuliza. "Unagawa vipeperushi tena?"

"Hapana. Mimi ndiye mbunifu mkuu wakati huu." Alicheka kabla ya kuchukua mkoba wake na kuondoka mlangoni.

Alvin alimfuata nyuma yake na kutoka naye pamoja. Koo lake lilihisi kukauka huku akiibia jicho lingine la umbo lililopinda la yule mwanadada. “Unataka lifti?”

“Hapana, asante.” alikataa bila kusita. “Nitaendesha gari.” Alvin hakuwa na la kusema.

Saa mbili na nusu asubuhi Lisa aliingia katika eneo lake jipya la kazi kwa wakati ufaao. Ilikuwa ni mshangao kujua kwamba wafanyakazi wengine wote walikuwa vijana na wenye shauku. Mbali na hilo, wote walikuwa wahitimu tofauti ambao walikuwa wamesoma nje ya nchi.

Joseph alimtambulisha Lisa kwa wafanyakazi wenzake kabla ya kuingia naye ofisini. Kisha alitoa ramani. "Hii ni nyumba ya Bw. Kelvin Mushi yenye ukubwa wa mita za mraba 3,000 katika eneo maarufu la Mbezi Beach. Huyu mtu aliwahi kuwekeza ng'ambo biashara zake na ndivyo nilivyokutana naye. Tumefahamiana kwa muda mrefu sasa.” Joseph alitikisa kichwa kwa umakini. "Anapanga kutulia nyumbani hapa Dar es Salaam kwa hiyo anataka kutengeneza jumba hili kwa ajili ya makazi. Fanya bidii kwenye mradi huu. Hakuna kikomo cha gharama kwenye ukarabati, lakini kila kitu lazima kiwe kamili. Ana mradi mwingine unaosubiri kuzinduliwa mwishoni mwa mwaka. Natumai kujenga naye ushirikiano wa muda mrefu.”

Tabasamu likatanda tena usoni mwa Joseph. “Kwa kweli, rafiki wa kike wa mpwa wa Bw. Mushi anatoka katika historia ya ubunifu majengo na mambo ya ndani, lakini Bw. Mushi hakutaka kutumia kampuni hiyo kwa sababu hapendi sana ubunifu wao hivyo anakarabati jumba lake kwa siri bila kumwambia mtu mwingine yeyote wa familia yao, kwa hivyo na wewe huna budi kuficha hili. Usifanye mambo kuwa magumu kwa Bw. Mushi.”

Bila kukawia, Lisa alitoka ofisini na kuendesha gari hadi Mbezi Beach. Hiki ni miongoni mwa viitongoji vya kifahari zaidi hapa Dar es Salaam. Ni matajiri tu ndio wanaweza kumudu kujenga mali hapo.

Gari lake lilisimamishwa na mlinzi kwenye mlango wa geti, hivyo ikabidi atembee hadi ndani. Mwanamume aliyeonekana kuwa na umri wa miaka 30 hivi alikuwa amesimama kando ya kidimbwi cha kuogelea. Mtu huyo mrefu alionekana kuwa na sura ya upole. Suti nyeusi ya biashara iliyotengenezwa kwa ufundi ilimpendeza sana.

Kwa mshangao, Lisa aliuliza kwa utulivu, “Bw. Mushi?”

“Ndiyo. Je, wewe ni mbunifu kutoka kampuni ya Joseph? Wewe ni mdogo kuliko nilivyotarajia." Mshangao wa kweli uliangaza machoni pa Kelvin Mushi.

“Joseph alinitangulia mwaka mmoja katika chuo kikuu. Bw. Mushi, unakaribishwa kunibadilisha ikiwa haujaridhika baada ya kuona kazi yangu.” Maelezo ya Lisa yalikuwa shwari na ya kujiamini. "Mbali na hilo, sidhani umri una uhusiano wowote na uwezo. Wewe mwenyewe ni kijana sana, Bw. Mushi.”

Kelvin alitabasamu. "Siwezi kubishana na hilo."

Lisa alimpatia Kelvin business card yake. Kelvin akaitazama. "Lisa Jones Masawe. Jina maarufu sana hili."

“Ni jina la kawaida kabisa.” Lisa alihisi moyo wake ukirukaruka. Kwa kuhofia kwamba huenda amesikia kuhusu uvumi mbaya unaoenezwa na familia ya Masawe. “Ikiwa haujali, Bw. Mushi, unaweza kuniambia mawazo yako tunapozunguka jumba hili la kifahari.”

Kelvin aliongoza njia na kumuonyesha kila sehemu ya jumba hilo. Mbali na hilo, alitaja matakwa yake ya kuwa na ukumbi wa mazoezi, ukumbi wa michezo, uwanja wa mpira wa kikapu, na bwawa la kuogelea la ndani. Lisa alikuwa na wazo la jumla la liliendana na matamanio yake. Katika chini ya nusu saa, alimpatia mchoro mzuri mikononi mwake.

Kelvin aliutazama mchoro ule, hakuweza kupata kitu cha kubaini makosa. Mpango huo wa kubuni ndio hasa alikuwa ameufikiria. "Bi jones, wewe ni mzuri kama wabunifu wakubwa ambao nimewaona kutoka nje ya nchi. Sio mbaya. Wazo la bwawa hili la kuogelea la ndani ni la kibunifu kweli.”

"Itaonekana bora zaidi baada ya kuisanifu." Lisa aliongezea.

“Hakika, una muda wa wiki moja. Ningependa kuanza ukarabati haraka iwezekanavyo.” Kelvi akampa Lisa business card yake. “Unakaribishwa kunitafuta ofisini kwangu michoro itakapokamilika. Hii ni kadi ya jina langu."
Kadi ile ilionyesha Kelvin Mushi alikuwa ni mkurugenzi wa kampuni ya Usafirishaji, Golden Corporation.

Baada ya kuondoka kwenye jumba lile, Lisa alipanga kuangalia miundo ya majengo mengine ya kifahari katika kitongoji hicho. Alipotoka tu nje ya geti, aliona Harrier nyeusi ikiingia kwenye moja ya majengo makubwa ya kifahari. Hilo lilikuwa gari la Alvin.

‘Ina maana amenunua nyumba huku pia?’ Lisa alijiuliza bila majibu kabla ya kushtuliwa na sauti ya kiume. “Kwa nini uko hapa?” sauti aliyoifahamu vizuri ilisikika nyuma yake ghafla. Ethan alikuwa kasimamisha gari pembeni kidogo mwa barabara akitazamana naye. Lisa alitazama na kumwona Ethan akitoka kwenye Lamborghini yake. Wakati huo alikuwa akigeuka ili kuondoka, lakini alishtuka kidogo kugongana naye hapo.

“Mimi ndiye ninayepaswa kuuliza. Wewe na Lina mnapanga kununua jumba la kifahari hapa, au unatafuta nini huku?" Lisa alirudisha swali.

“Hapana. Niko hapa kuangalia nyumba ya mjomba wangu. Jumba lake linahitaji kukarabatiwa na ninapanga kumshawishi kukabidhi mradi huo kwa Lina.” Ethan alimwambia Lisa huku akimkazia macho usoni. “Unaona Lisa, ningeweza kumshawishi mjomba akupatie huo mradi wa kukarabati jengo lake la kifahari kama mimi na wewe tungekuwa bado tunaelewana vizuri.” Ethan alimwambia kwa kujidai.

Hapo awali Lisa aliliona gari la Alvin na punde akamwona Ethan mitaa hiyohiyo, je hii ilikuwa ni bahati tu? Kwa kuwa wawili hao walikuwa wamefuatana na aliamini walikuwa na uhusiano wa mjomba na mpwa, Lisa alihisi kuwa Alvin alikuwa amenunua jumba la kifahari huko Mbezi Beach na Ethan alitaka amshawishi ili ampatie Lina kwa ajili ya kulikarabati. Hilo lilimuuma sana Lisa.

Ethan alitabasamu kwa dharau alipoona hali ya mawazo imeifunika sura ya Lisa. " Unajutia maamuzi yako sasa? Na bado, utajuta sana!”

Lisa alikasirishwa na maneno ya Ethan nusu ya kutema damu. Lisa alimshangaa Ethan kwa kufikiri alikuwa akimuwazia yeye. Ni mawazo ya Alvin ambayo yalimfanya akose raha muda huo. Alijiuliza kwanini Alvin anunue jumba huko kisirisiri kisha amkabidhi Lina mradi wa kukarabati jumba hilo? Hicho ndicho hasa kilikuwa kikimuuma Lisa. hata kama hakuridhika na ubunifu wa Lisa, ulikuwa ni uamuzi wake kuchagua kampuni nyingine yoyote ya kubuni muundo wa ukarabati wa jumba lake, lakini siyo kukabidhi mradi wa ukarabati kwa Lina!

"Sawa, mjomba wako ndiye mwenye uamuzi wa mwisho juu ya nani atampa kazi ya ukarabati, sio wewe. Labda atashawishiwa kwa urahisi na mke wake. Maneno yako ni kama kinyesi tu kwangu." Lisa alimjibu Ethan kwa hasira.

Ethan alikunja uso baada ya kusikia hivyo. “ Mjomba wangu bado hajaoa. Isitoshe mimi na yeye zinaiva sana, na kwa kawaida huwa anakubali chochote ninachomwambia.”

Lisa alitabasamu kwa dharau. “Hakika muombe akufanye mrithi wa mali zake na uone kama atakubali.”

“Umerukwa na akili.” Uso Ethan ulibadilika kwa hasira. “Si ajabu kwamba Mjomba Jones na Shangazi masawe walikufungia kwenye jumba lao huko Moshi. Hakika unastahili.”

Maneno yake yalichochea chuki iliyozikwa ndani ya moyo wa Lina. "Ethan, unafahamu lakini unachokiongea?"

“Kwani nimekosea? Uliwaambia waandishi wa habari kwamba familia ya Masawe ilikufungia na kukutesa. Lakini unaonekana mwenye nguvu na mwenye afya kwangu, kana kwamba umekuwa ukiishi vizuri. Uwepo wako ni bahati mbaya sana kwa familia ya Masawe. Unajua kwamba kwa sababu ya shutuma zako, sifa ya Kibo Group zimeharibiwa na bei yao ya hisa imeshuka sana? Thamani ya soko ya kampuni ilipoteza dola milioni mbili kwa usiku mmoja.”

Lisa alihisi hamu kubwa ya kummeza Ethan mzima mzima. "Kitu pekee kinachonifanya nisikitike ni kwamba, mwanzoni nilipoteza muda wangu kukupenda sana bila kujua kuwa huna akili hata kidogo. Akili ulizonazo zinakutosha kujua chakula tu na njia ya kwenda chooni, basi!"

Ili kuepuka asije akapandisha hasira mbaya nakufanya mambo yasiyotarajiwa, Lisa aliwasha gari, akakanyaga mwendo na kuanza kuondoka.

SURA YA34

"Subiri." Ethan alimzuia na kumwambia. “Sherehe yetu ya uchumba na Lina imepangwa mwishoni mwa mwezi huu. Lazima uhudhurie sherehe hiyo. Ni wewe uliyeharibu sifa ya Kibo Group hivyo unawajibika kuiokoa.”

“Bullsh*t! Niondokee hapa ,wenda wazimu wewe. Siwezi kusubiri kuona Kibo Group ikifilisika kabisa. Ulisaliti uhusiano wetu na bado una jeuri ya kunidai nijitokeze kwenye sherehe yako ya uchumba. Una wazimu nini! Huna hata aibu?!" Lisa alilaani.

Ethan hakuonesha hata wasiwasi. Alizidi kumzuia Lina na kumwambia tena.“Sherehe yetu itaambatana na kumbukumbu ya kuadhimisha miaka 80 ya kuzaliwa kwa bibi yako. Alikupenda sana tangu ukiwa mdogo, unajua! Na afya yake inazidi kuzorota kila siku, na nani anajua amebakisha muda gani? Bado hutaki kuhudhuria?”

Mwili wote wa Lisa ulimsisimka huku akimtazama Ethan kwa hasira kali. “Yaani sherehe ya kuzaliwa bibi yangu mnaijumuisha na mambo yenu ya kijinga?”

"Na ukiacha kuja bibi yako atasema unamdharau, kumbuka bibi yako ndiye mtu pekee aliyebaki anakupenda!" Maneno ya Ethan yalijaa dharau.

“Usijali. Nitakuja." Lisa alikubali kwa hasira na kuondoka. 'Nitakuwepo na mjomba wako Alvin. Nataka kukuangamiza wewe na mchumba wako asiye na maana kabisa!’ Lisa alijisemea kimoyomoyo wakati anaondoka. 'Nataka kumfanya mjomba wako kuwa mtiifu kwangu 100%. Lina hataweza kujiunga na familia yenu mradi tu sitakubali!' Lisa alijiwazia kwa hasira.

Ethan alitikisa kichwa kwa dharau wakati akimwangalia Lisa akitokomea kwa mbali. Baada ya Lisa kupotea machoni mwake, Ethan alitembea kuelekea kwenye jumba la kifahari la mjomba wake, Kelvin Mushi.

Kelvin alikuwa akikagua mchoro alioachiwa na Lisa kwenye kiti cha mapumziko chini ya mti. Alikunja uso na kuuficha mchoro ule kwa siri baada ya kugundua kuwasili kwa mpwa wake.

"Mjomba, lini utaanza kukarabati jumba lako?" Ethan alikuwa ameona mchoro kabla haujafichwa.

"Ulisikia kutoka kwa bibi yako sivyo?"

“Ndiyo,” Ethan alijibu huku akitabasamu. “Umelidhamiria kweli jambo hili? Acha Kibo Group ishughulikie suala hilo. Lina mwenyewe ni mbunifu mzuri. Mpe nafasi.”

Kelvin alizuia hamaki yake alipoinuka na kusimama. "Ethan, najua mambo kadhaa kuhusu wabunifu katika kampuni ya Kibo Group. Mtindo wao wa ubunifu ni wa kifahari lakini ni wa kizamani sana na unatofautiana sana na malengo yangu. Nimeishi nje ya nchi kwa muda mrefu sana na ninapendelea mitindo fulani ya kigeni.”

"Sawa, unaweza kuwasilisha mawazo yako kwa Kibo Group. Sifa ya kampuni yao imeathiriwa sana hivi karibuni. Mjomba, tafadhali unaweza kuwasaidia?”

"Hapana." Kelvin alipunga mkono wake hewani bila kusita. "Naweza kukubaliana na chochote mbali na hili. Nina viwango vya juu vya makazi yangu. Nimekutana na Lina hapo awali. Kusema kweli, hana uzoefu na hajui chochote kuhusu vifaa vya kisasa vilivyo kwenye fasheni. Ataharibu tu nyumba yangu.”

Ethan aliona aibu kidogo. Ni mchumba wake walikuwa wakijadiliana, hata hivyo, hivyo alizidi kumpigania. "Lakini alifanya vyema katika mradi wa Kituo cha Utamaduni na Teknolojia..."

"Usisahau kuwa alishinda zabuni kwa sababu tu nilimpambania! Ukaribu wangu na Mzee Kamote ndiyo ulimpa nafasi hiyo." Sura ya kutofurahishwa ilijiosha usoni mwa Kelvin alipokuwa akiongea kuhusu hili. "Mbali na hilo, unapaswa kushukuru kwamba Mzee Kamote hakutufichua au tungekuwa katika matatizo makubwa."

Ethan alihisi moyo wake kuzama. "Sawa, sio jambo kubwa ikiwa hukubaliani. Kwa hiyo unaenda kwa mbunifu gani? Nauliza kwa udadisi tu na si kingine.” Ethan aliuliza huku macho yake yakiwa yamelenga kwenye mchoro.

"Joseph Ruta, ni rafiki yangu kutoka Uganda. Alifungua tawi hapa Dar es Salaam.” Kelvin alikabidhi mchoro huo kwa mpwa wake. "Hii imeundwa na mmoja wa wabunifu wake. Alitoa mchoro wa jumba zima la mita za mraba 3,000 kwa chini ya nusu saa, bila kusahau kutoa maelezo ya undani kikamilifu kulingana na mapendekezo yangu. Nimeridhika sana.”

“Lisa?” Ethan aliganda kwa sekunde kadhaa alipoona saini ya Lisa chini kulia mwa mchoro. Alikumbuka kugongana naye getini hapo awali. Ilivyoonekana, alikuwa hapo kubuni muundo wa jumba la mjomba wake.

"Ndio, huyo ndiye." Kelvin alijibu kwa dhati.

"Mjomba, huwezi kumwajiri Lisa," Ethan alisema kwa uchungu, "Yeye ni binti mdogo wa familia ya Jones Masawe niliyekuambia hapo awali. Aliwahi kuwa mpenzi wangu lakini amekuwa na sifa mbaya sana. Sio tu kwamba aliiba kazi ya mtu mwingine, lakini pia aliharibu sifa ya wazazi wake mwenyewe.”

Hili lilimshangaza Kelvin. Haishangazi alidhani jina hilo halikuwa geni akilini mwake. Lakini alipokumbuka tabia ya fadhili na adabu ya Lisa, alikunja uso. "Sidhani kama anahitaji kuiga wengine, kutokana na talanta zake. Nimepata uzoefu mzuri wa kushughulika na watu wa aina zote katika ulimwengu wa biashara. Yeye ni kipaji adimu, na sidhani kama yeye ni mtu asiyeheshimika. Kinyume chake kabisa, Ethan, nadhani una chuki dhidi yake!”

“Kweli humjui vizuri Lisa mjomba!”

“Mbona unanishangaza? Tulipozungumza kwa simu siku za nyuma, hukuweza kuacha kumpongeza lakini sasa umechukizwa naye ghafla. Je, alikukosea kwa namna fulani? Ni wewe uliyemsaliti kwanza nikikumbuka vizuri.”

Ethan hakuwa na neno la kukanusha jibu ambalo hakulitarajia. Kelvin akaendelea kumhutubia. "Vile vile, unaendelea kujivunia vipaji vya Lina, lakini sioni uwezo wake. Kama si kweli kwamba yeye ndiye mrithi wa familia ya Masawe, nisingemtazama kwa mara ya pili mwanamke kama yeye.” Kelvin alichukua mchoro kutoka kwenye mikono ya mpwa wake na moja kwa moja akaelekea mlangoni. Kelvin alikuwa tayari ameondoka muda mrefu wakati Ethan alipotulia tena kiakili.......ITAENDELEA......

Eheee sasa ile siku tuliyokuwa tukiisubiri kwa hamu imetimia, Lisa tayari ametambua kwamba Kelvin ndiye mjomba wa Ethan sasa atafanya nini na tayari amedondokea kwa Alvin...!? hapo ni patamu sana lakini acha tusubiri sehemu inayofuata kujua nini kitajiri.

SOMA SIMULIZI HII HARAKA

Unaweza lipia na kusoma simulizi hii kwa njia ya Whatsapp kwa kununua episode.

Episode - 20 Tsh 1000/=
Episode - 30 Tsh 1500/=
Episode - 40 Tsh 2000/=
Episode - 50 Tsh 2500/=

Namba za kulipia

0628924768 (Halotel) JUMA HEMBA
0694288555 (Airtel) JUMA HEMBA
0764736557 (Voda) HADIJA KIRUNGI

"Lipia utumiwe similizi yako sasa whatsapp 0628924768"

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI.......LISA
KURASA.......31-35

SURA YA31

Alvin na Sam walingia hospitalini pale mida ya jioni. Sam aliweka kikapu cha matunda kwenye meza ya kahawa, kisha akamsalimia Lisa kwa tabasamu. "Shemeji, unajisikia vizuri?"

"Vizuri zaidi." Lisa kwa siri alitazama pembeni kwa Alvin aliyekuwa kasimama kimya. Lisa alipepesa macho yake kwa utii. "Samahani kwa kukuletea shida tena."

“Ni vyema kama umelitambua hilo. Nilidhani wewe ni mjinga tu.” Alvin alikasirika bila sababu kumuona Lisa akiwa amekonda mithili ya mfuko wa mifupa. Maneno makali yakamtoka kinywani mwake. “Sijapata amani hata siku moja tangu nikuoe. Sitaki kuhojiwa na polisi ukiwa umekufa siku moja. Unaelewa?"

"Haitatokea tena wakati ujao." Lisa aliuma mdomo wake uliopauka kuzuia machozi yasiendelee kuchuruzika mashavuni mwake.

Upepo wa kufadhaika ulimpitia. Alvin hakutaka kuendelea kumfundisha, lakini alihitaji aache kufanya makosa ya kipumbavu namna hii. “Simu niliyokununulia iko wapi? Kwa nini iliachwa nyumbani kwa akina Masawe?”

"Mama yangu alinidpokonya na kuikatalia."

"Kweli wewe ni nguruwe." Alvin alifoka.

“Uko sahihi. Tafadhali niite Nguruwe Masawe kuanzia sasa.”

Mapovu ya kicheko kilichoshindwa kuzuilika yalitoka kwenye midomo ya Sam, na kulainisha hali ya wasiwasi katika wodi ya hospitali. “Sawa, Alvin, acha kumponda. Hakuna mtu ambaye angetarajia ukatili kama huo kutoka kwa wazazi wake waliomzaa.”

Lisa alitetemeka. Baada ya kuona hivyo, Alvin aligeuza macho yake kwa Lisa na kumuonya. "Kaa mbali na familia hiyo ikiwa unataka kubaki hai."

"Hiyo ni sawa." Sam aliitikia kwa kichwa. “Zingatia tu kumwandalia rafiki yangu chakula. Tazama jinsi amekuwa na hasira baada ya kutoweza kufurahia milo yako iliyopikwa nyumbani katika siku chache zilizopita.”

“Sam Harrison.” Alvin akatupa jicho la hatari upande wake.

Sam aliacha kusema mara moja. Lisa hakuweza kupinga tabasamu usoni mwake. “Nitapona hivi karibuni na nianze kukupikia tena.”

"Kaa kimya na uzingatie kupona." Sauti ya Alvin ilikuwa ya ukali kama kawaida, lakini maneno yake yalileta uchangamfu moyoni mwake.

“Alvin, asante, kweli.” Lisa alishukuru kwa dhati.
•••
Siku mbili baadaye, Ethan akiwa kwenye ofisi za kampuni yao, ‘Lowe Enterprises’, alikutana na habari ya Lisa mtandaoni iliyosambazwa pamoja na cheti cha matibabu kilichotolewa na Dk Johnson. Ethan alishtushwa sana. Mara moja, aliingia kwenye gari na kukimbilia kwenye makazi ya akina Masawe.

Alipofika, aliwahoji wanandoa hao wazee huku akijaribu sana kuzuia hasira yake. “Mjomba Jones na Shangazi Masawe, ni kweli mlimfungia Lisa kwenye makazi ya zamani ambapo mlikataa kumpa maji na kumlisha chakula kibovu?”

“Upuuzi gani huu Ethan. Ulikua na sisi muda wote. Unafikiri tunaweza kufanya hivyo?" Johes Masawe alikasirika na kufadhaika kwa wakati mmoja. “Kwa kweli, nilimweka kwenye makazi ya zamani lakini alitunzwa vizuri na watumishi kwa chakula kitamu kila siku. Yeye ni binti yangu wa kuzaliwa, hata hivyo. Ningewezaje kuwa mkatili hivyo?”

"Lakini inaenea mtandaoni kwamba ..."

Lina alimkatisha kwa huzuni, "Zote ni habari za uwongo. Sielewi kwa nini Lisa angeidharau familia yake kama hivi baada ya kuondoka kwenye makazi ya zamani na marafiki zake. Mama na Baba wana wasiwasi sana juu yake. Walimweka tu katika makao ya zamani ili asichangamane na watu wabaya na kuharibu sifa yake huko mitaani tena.”

Hilo lilimshangaza Ethan. Maneno magumu yalienea usoni mwake baada ya kukumbuka uvumi aliosikia muda si mrefu uliopita. Sasa, alielewa uamuzi wa familia ya Masawe. “Samahani, sikuwaelewa nyote.”

Mama Masawe aliweka mkono juu ya kifua chake kwa huzuni. "Sijali maoni ya watu juu yetu mtandaoni kwani tumeshindwa kama wazazi. Lakini Kibo Group ambayo tumetumia muda mwingi na juhudi kuijenga iliharibiwa mara moja. Hisa za kampuni ziko chini kabisa kwa siku kadhaa zilizopita na thamani yake ya soko ilipungua kwa zaidi ya dola milioni. Kinachotia wasiwasi zaidi ni kwamba kila mtu mtandaoni anaisusia Kibo Group sasa. Mambo yatakuwa mabaya sana ikiwa hii itaendelea."

Ethan alikatishwa tamaa na alichokisikia. Kufaulu au kutofaulu kwa kampuni ya Kibo Group kulimuathiri sana yeye mwenyewe. "Tunahitaji kudhibitisha kwa umma kuwa familia ya Masawe iko kwenye uhusiano mzuri na Lisa. Kisha, tunaweza kuajiri kundi la watu kutangaza hili mtandaoni ili kufuta uvumi huo.”

“Ni wazo zuri.” Johes alikubali kwa kichwa. "Tarehe ya sherehe yako ya uchumba inakaribia. Vyombo vya habari pia vitakuwepo. Tunahitaji tu Lisa kujitokeza ili kubadilisha taswira ya kampuni.”

“Atajitokeza kweli?” Lina alimtazama Ethan kwa wasiwasi. “Ujue bado anakupenda. Sidhani kama anaweza akaja."

“Nitafikiria jambo fulani la kumshawishi Lisa ahudhurie.” John Masawe alisema.
•••
Lisa alilazwa hospitalini kwa siku tatu kabla ya kuruhusiwa kurudi nyumbani. Aliporudi nyumbani alishangaa kuona kwamba Charlie alikuwa ameongezeka unene. Alifikiri kwamba paka huyo angekuwa dhaifu kwa kukosa mtu wa kumtunza ipasavyo siku chache zilizopita.

Alvin alipofika nyumbani baadaye usiku huo, alimsikia Lisa akinung'unika wakati akimlisha paka. “Charlie, inabidi uache kula sana. Angalia ukubwa wa tumbo lako. Ni kana kwamba una mimba ya kujifungua!”

Tumbo la mimba la Charlie lilikuwa likiongezeka kadiri siku zilivyopita. Alvin asingeweza kuweka siri hiyo kwa muda mrefu zaidi. Hata hivyo, bado ilikuwa bora kuwa na mtu wa kumhudumia nyumbani. Alvin alitokea tena akiwa amevaa nguo za kawaida za mapumziko. Lisa alikuwa tayari ameshaandaa meza ya chakula.

Lisa alimwandalia Alvin meza ya shukrani iliyojumuisha aina zake zote za vyakula anavyopenda. Macho ya Alvin yaliwaka kwa furaha baada ya kuvitazama vyakula vilivyotapakaa mezani. “Nimechoshwa na kula vyakula vilivyochomwa na kukaangwa. Tengeneza hata supu au kitoweo wakati mwingine,” Alvin alijivungisha kama kawaida yake huku akivishambulia.

Baada ya chakula cha jioni, Alvin alirudi kwenye chumba cha maktaba kuendelea na kazi. Alvin aliendelea na kazi hadi karibu saa sita usiku. Lisa alitayarisha kahawa na kumpelekea. Alvin alikuwa ameketi kwenye dawati, akichanganua hati zilizo chini ya mwanga mkali huku akirejelea kompyuta ya mkononi kwa wakati mmoja. Jozi ya miwani yenye fremu za dhahabu ilikaa kimya kwenye daraja la pua yake.

"Utaendelea kutazama hadi lini?" Lisa alimuuliza Alvin wakati akimkaribisha kikombe cha uji wa ulezi.
Alvin akafunga laptop yake na kugeuka kumwangalia kwa utulivu kisha akapokea kikombe cha kahawa.

“Sijawahi kukuona umevaa miwani hapo awali. Nilikaribia kuzimia kwa sababu ya haiba yako ya kuvutia,”Lisa alisema huku akitabasamu.

“Bado hujaacha maneno yako?”

Lisa akaguna. Hatimaye, muda mfupi baadaye, alizungumza tena, “Mwonekano wako mzuri hunivutia kwa njia tofauti kila siku. Kadiri ninavyokutazama, ndivyo ninavyozidi kuvutiwa nawe. Haichoshi…”

Kabla Lisa hajamaliza sentensi yake, ghafla mkono mkubwa ulionekana kumziba mdomo. Mkono wa Alvin ulinuka kama msonobari mkavu. Harufu hafifu ilimtuliza kwa kushangaza. Muhimu zaidi, mkono wake ulikuwa na joto sana!

"Nyamaza." Macho ya Alvin yalipepesa chini ya lenzi za miwani yake.
Alihisi mashavu yake yakiungua pia.

Baada ya kuondoa mkono wake, aliweka kikombe cha kahawa kwenye meza. "Ninahisi lazima uwe umechoka kufanya kazi usiku kucha. Kikombe cha kahawa kitakuchangamsha kidogo."
Alvin aliitazama ile kahawa iliyochanganywa kwenye mazima. Hakika ilionekana kumvutia.
"Lisa , unajaribu kunifanya nishindwe kulala, hujui kahawa kufukuza usingizi?"

"Hapana, kahawa haifukuzi usingizi." Alimshawishi. “Itakuchangamsha tu na kukufanya ujisikie na nguvu mpya kimwili na kiakili."

Alvin aimtazama huku pembe za mdomo wake zikicheza kwa dharau. "Sawa. nitakunywa. Ila nikikosa usingizi ujue tutakesha wote hapa.”

“Usijali. Hata ukisema tulale pamoja hadi asubuhi, nitafanya.” aliahidi.

“Sithubutu kutegemea hilo. Ninaweza kufa kabla hata halijatokea.” Alvin alijibu huku akijinywea kahawa yake.

Lisa ambaye alikuwa ametoka tu kudhihakiwa, alitoka nje ya maktaba akiwa ameudhika. Aliapa kumthibitishia kuwa ipo siku angemtaka tu!.

SURA YA32

Saa saba usiku Lisa alishtushwa na ndoto zake mbaya, ndipo akagundua kuwa alikuwa anatokwa na jasho kwenye paji la uso wake. Mara moja akawasha taa. Utulivu ulikuja juu ya mwili wake taratibu huku mwanga ukitawala giza.
Alikuwa ameota juu ya kufungiwa ndani ya nyumba ile yenye giza tena. Sehemu hiyo ilijaa kila aina ya kelele za kutisha usiku. Kwa hofu, alijikunja ndani ya shuka.

Ilikuwa ni shida kwake kulala peke yake sasa. Baada ya muda wa kufikiria, alijifunika blanketi na kubisha hodi kwenye mlango wa chumba cha kulala cha Alvin.

“Nani huko?” Alvin, ambaye alikuwa amekereka kwa kuamshwa usiku wa manane, aliuliza kwa sauti iliyojaa hasira.

“Ni mimi.” Lisa aliitikia kwa hofu. Nusu dakika ikapita kimya kabisa. Alipotaka kukata tamaa, mlango ulifunguliwa ghafla kutoka ndani. Alvin akatokea upande wa pili wa mlango. Nywele zake zilikuwa zimevurugika na macho yake meusi yalionekana kuogopesha.

"Afadhali uwe na sababu nzuri ya kunisumbua."

“Naogopa kulala peke yangu…” Lisa alitetemeka.

Alivin aliinua macho yake taratibu. Jasho lilikuwa likimvuja Lisa usoni kwa sababu ya hofu. Hata hivyo, alishangazwa na blanketi alilokuwa ameshikilia mikononi mwake.

"Hii ni mbinu yako nyingine ya kunitongoza?" Alvin alikiri moyoni mwake kuwa karibuni uzalendo ungemshinda. Hata hivyo, alikuwa amechoka sana na kazi za kutwa nzima na bado alihitajika kuamka mapema kwa ajili ya kesi mahakamani kesho yake. “Ni usiku sana. Nahitaji kulala hata kama wewe huna haja ya kulala.”

"Sio hivyo." Lisa hakutaka kubaki peke yake chumbani kwake. Aliongeza nguvu na kuvuta kona ya mkono wake. “Tangu nifungiwe kwenye nyumba ya giza kijijini naogopa kulala peke yangu usiku. Ninasumbuliwa na jinamizi la kutisha. Tafadhali niruhusu nilale japo kwenye sakafu ya chumba chako. Niko serious.”

“Si ulikuwa umelala vizuri hospitalini?”

"Nilikuwa na mlezi wakati huo." Lisa alijitetea huku akitetemeka.

Ni Alvin ambaye alikuwa amemuokoa kutoka kwenye nyumba hiyo ya zamani. Mahali hapo palikuwa kimya sana na giza muda wote kama usiku. Hata mwanaume angepatwa na kiwewe baada ya kufungiwa mle ndani kwa siku tatu.

Lisa aliona kusita kwake kama kukubali, na akatoa ahadi haraka. "Naapa sitakusumbua."

“Kumbuka ahadi yako.” Alvin alirudi kitandani kwake bila wasiwasi.

Baada ya kupata kibali chake, Lisa haraka akaweka blanketi kwenye sakafu karibu na kitanda chake. Alvin alikaa makini kwa muda mfupi lakini punde akapitiwa na usingizi. Hata hivyo muda fulani baadaye, kilio cha Lisa kilimwamsha tena.

“Fungua mlango… Tafadhali… ni baridi… giza sana… ninaogopa.”

Alvin akajiinua kutoka kitandani. Mwangaza wa mbalamwezi uliomiminika kupitia dirishani ulimulika kivuli chini. Lisa aliyekuwa amejikunja ndani ya blanketi alikuwa ameziba masikio yake kwa nguvu. Mwili wake wote ulikuwa ukitetemeka kwa hofu.

“Lisa amka. Ni ndoto tu.” Alvin alitoka kitandani ili kumvuta mikono. Lakini, Lisa alikuwa kazama kabisa katika ndoto hiyo mbaya. Uso wake wa hofu ulikuwa umepauka kama kauzu. Akiwa hana njia nyingine, akamvutia kifuani kwake na kumpigapiga mgongoni taratibu.

"Ni sawa. Uko salama sasa…” Sauti ya Alvin ilikuwa na athari ya kutuliza ambayo polepole ililegeza mkazo mwilini mwake.

Uso wake mdogo ulisukumwa kifuani mwake. Nywele zake za giza zinazong'aa zilikuwa zimening'inia mabegani mwake huku nyuzi kadhaa zikiwa zimepigwa plasta kwenye ukingo wa uso wake wa kusikitisha lakini mzuri. Pia alitoa harufu hafifu ya kutuliza. Hii haikuwa harufu ya manukato, badala yake, ilikuwa harufu ya shampoo yake. Hakuwahi kutambua jinsi shampoo yake ilinukia vizuri hadi wakati huu. Harufu hiyo ilimfunika taratibu hadi akafumba macho hatimaye. Aliwaza kumwachia mara baada ya kutulia kabisa. Hata hivyo, ilikuwa tayari asubuhi iliyofuata alipofungua tena macho yake.

Wawili hao walijikuta wakitumia kitanda kimoja, shuka moja na mto mmoja. Mkono wake wa kushoto na mguu wa kushoto ulikuwa umewekwa juu ya mwili mwake. Kulikuwa na tabasamu la kudumu kwenye pembe za midomo yake. Ilionekana alikuwa na usingizi mzuri.

Alvin pia hakujisikia raha. Alihisi hata kwa sekunde ya haraka kwamba walikuwa kama wanandoa wapya. Alvin aliwaza bila kufikiria kwa sekunde chache kabla ya kunyanyua blanketi kwa uangalifu ili asimame. Bila kutarajia, mtazamo chini ya blanketi ulimshangaza. Karibu vifungo vyote vya pajama za Lisa vilitenguliwa. Wakati huo Lisa naye alifungua macho yake polepole. Macho yao yalikutana na mboni zake zlipanuka polepole.

Alipiga kelele kwa mshtuko sekunde tu alipogundua kuwa alikuwa amelala mikononi mwa Alvin. Lisa alinyanyuka kwa haraka na kujiweka mbali na mwanaume huyo. "Kwa nini ... kwa nini umenileta kitandani kwako?"

Alvin alidhihaki kwa kutoamini. “Ulinizunguka huku ukilia wakati ukiota ndoto mbaya jana usiku. Nilikuwa nikikufariji na kukutuliza…”

“Umenifariji?” Aliona jambo hili kuwa gumu kuamini.

Uso wa Alvin ukajaa hasira. “Unajaribu kusema nini? Lisa, sema kweli sasa hivi. Je, jana usiku kilikuwa ni kitendo cha makusudi? Ulikuja chumbani kwangu ili kunitega, huh?"

“Sijui unazungumza nini. Nililala vizuri sana.” Alikumbuka bila kufafanua kuwa alipata ndoto mbaya mwanzoni, lakini alihisi amani wakati sauti ya upole ilinong'ona masikioni mwake. Subiri, sauti hiyo ya upole ilikuwa ya Alvin?

Alvin alimtazama kwa macho makali wakati anainuka na kusimama. "Kabla hujaendelea kuongea, angalia hali ya nguo zako za kulalia."

Akiwa amechanganyikiwa, Lisa alishusha macho yake. Sura ya mshtuko na aibu ilimwangazia usoni mwake alipojiona alivyokuwa kifuani. Mikono yake iliruka kukifunika kifua chake mara moja.

Alvin akafoka. “Uigizaji mzuri. Nina hakika ulifungua vifungo hivyo kwa siri ili kunitega.”

“Sina haja ya kufanya hivyo.” Lisa alijisikia kulia wakati huu. “Vifungo vilifunguka vyenyewe. Si kosa langu kuwa na matiti makubwa.”

"Kwa hivyo kama una matiti makubwa ndiyo uyaache waziwazi? Sema tu ukweli kuwa unajaribu kunitega." Alvin alisema huku akimtazama Lisa kwa dharau.

“Ndiyo! Um… Ninaweza kueleza hili. Ni kwa sababu mimi…nakupenda kupita kiasi,” Lisa alisema kwa sauti iliyotiwa chumvi. Akiwa amechanganyikiwa, alisonga mbele na kuishika shingo ya Alvin.

Kwa kweli, Alvin alishtushwa na kitendo chake cha ghafla na ambacho hakuwa amekitarajia.
‘Je, mwanamke huyu alikuwa akijaribu kumlazimisha busu?’ Alvin alijiuliza huku picha ya midomo yake nyororo ikaingia akilini mwake. Alisita kwa sekunde kadhaa kabla ya kusikia maumivu makali mashavuni mwake. Lisa alikuwa amempiga Lovebite!. Alvin alimsukuma Lisa kwa nguvu huku mkono wake ukiruka kufunika sehemu aliyong’atwa.

“Lisa, unathubutu vipi? Usifikiri sitakuadhibu kwa hili.” Macho ya Alvin yalikuwa kama miali ya moto.

Lisa akacheka tu kwa mzaha huo na kumwambia. “Kwani hujawahi kuiona kwenye sinema za kihindi? Waigizaji wakuu huwa wanamng’ata mtu wanayempenda sana. Nilikuwa najaribu tu kuacha alama kwako.”

Alvin akapiga hatua kadhaa mbele, huku akiwa ameuma meno kwa hasira. "Unanichukulia kama mjinga sivyo?"

"Sawa, unaweza kuning’ata na wewe kulipiza kisasi." Lisa alijikaza na kuinamisha uso wake karibu na Alvin. "Ning’ate kwa nguvu kadri uwezavyo. Ukining’ata kwa nguvu zaidi nitajua unanipenda zaidi.”

Bila hata kujiuliza, Alvin alikiweka kichwa cha Lisa katikati ya viganja vyake na kumng'ata kwa nguvu kwenye shavu. Shavu nene la Lisa lilikuwa nyororo na laini kama jeli. Hakutaka kusogeza midomo yake mbali.

“Loo!” Lisa alipiga kelele kwa uchungu.

Hatimaye, Alvin baada ya kuona meno yakiwa yameganda kwenye mashavu yake yaliyonenepa, alimwachia. "Kumbuka adhabu hii."

Lisa alijifanya mwenye haya licha ya maumivu. "Hapana, hii siyo adhabu, huu ni uthibitisho wa upendo wako."

"Endelea kuota." Alvin alicheka kwa kejeli kabla ya kuingia bafuni na kufunga mlango kwa nguvu. Taswira kwenye kioo ilionyesha alama za meno kwenye shavu lake mwenyewe. Alihisi kukimbilia mlangoni ili kumchana mwanamke huyo vipande vipande.

Ilimbidi awe mahakamani siku hiyo kwa hiyo ilimbidi aende akiwa amevalia barakoa. Akiwa amekasirika, Alvin alipata tu kifungua kinywa kidogo kabla ya kuondoka nyumbani.

Saa tatu asubuhi Alvin aliwasili ofisini kwao. Sam alimpokea kwa swali, “kwa nini umevaa barakoa? Unaumwa?" Alvin alikataa kujibu. "Eh, ni vizuri kuwa unajali na kuvaa barakoa ili kuzuia kueneza korona. ” Sam alimpongeza baada ya kumuona yupo kimya.

Baada ya kukamilisha taratibu kadhaa za kiofisi, walielekea katika mahakama ya Kisutu kwa ajili ya kusimamia kesi. Dakika kumi baada ya kuwasili kwao, kesi ilikuwa karibu kuanza. Sam nusura aangue kicheko hadharani wakati Alvin alipotoa barakoa yake na kufichua alama za meno kwenye shavu lake.

"Ni nini …?"

"Nimeng’atwa na mbwa." Sauti kali ya Alvin ilisikika kwa vitisho. Aliingia ndani ya chumba cha mahakama kwa hatua kubwa.

Sam hakuweza kujizuia tena kuangua kicheko. Alvin alifikiri angeweza kumpumbaza? Mwanamume huyo alikuwa ameng’atwa na mwanamke. Hakuwahi kumuona Alvin akiona aibu vile. Kwa hiyo alimpiga picha kwa siri na kuituma kwenye group lao la whatsapp.

SURA YA 33

Lisa alipumzika nyumbani kwa siku kadhaa, akisubiri alama za meno shavuni kwake kutoweka kabla ya kwenda kutafuta kazi mpya. Lakini, kila alikotuma maombi ya kazi, alipokea maoni hasi tu.

"Bi Jones, samahani lakini hatuajiri waizi wa kazi za wangine."

"Bi Jones, kashfa yako imekuwa habari ya kawaida katika sekta ya ujenzi. Hakuna mtu anayethubutu kukuajiri tena.”

"Bi Jones, familia ya Jones Masawe imetangaza kwenye mtandao wa sekta nzima kwa siri kwamba mtu yeyote ambaye atathubutu kukuajiri atakuwa anawadharau waziwazi."

Lisa alikutana na majibu kama hayo kwenye mahojiano ya kazi na makampuni kadhaa aliyotuma maombi. Alikatishwa tamaa kabisa na kupandwa hasira kwani alikuwa ametumia muda mwingi na bidii katika elimu yake lakini bado hakuweza kupata kazi.

“Pipiii…” Mara akagutushwa na sauti ya honi. Gari lililokuwa karibu naye lilipiga honi mara kadhaa. Hakutambua kama mtu huyo alimkusudia yeye hadi alipomwita jina lake. "Lisa !"

Lisa alitazama kwenye gari hilo na kuona uso mzuri ukichungulia nyuma ya dirisha la Range Rover. “Joseph? Unafanya nini hapa?" Lisa alipatwa na mshangao wa furaha baada kumuona mwandamizi wake kutoka Chuo Kikuu cha New South Wales alikokuwa ameenda kusoma.

“Nina ofisi katika jengo hili. Nilikuona ukitoka nje nikashangaa unafanya nini hapa." Joseph aliegesha gari lake pembeni na kumpa ishara aingie ndani. Lisa alipoingia ndani ya gari alijibu kwa kinyonge, “Nimekuja kwa mahojiano ya kazi, lakini sijafanikiwa.”

“Hata wewe hukuweza kufanikiwa na sifa zako?” Joseph aliona jambo hilo kuwa gumu kuamini.

“Nimekosana na familia yangu na wananichafua kwenye mtandao mzima wa sekta ya ujenzi. Sifa yangu yote inazidi kuporomoka!” Lisa alimwambia Joseph kwa huzuni na kumweleza kila kitu kwa undani wake.

“Siamini kwamba unaweza kuiba kazi za wengine. Inapaswa kuwa kinyume chake." Tabasamu likatanda usoni mwa Joseph. "Sawa, nimeanzisha kampuni mpya hapa Dar es Salaam na bado sina wafanyikazi wa kutosha. Njoo ujiunge na timu yangu."

Lisa alishtuka na kuguswa wakati huo huo. “Huna shaka nami hata kidogo?”

"Najua wewe ni mtu mzuri wa tabia na ninafahamu vyema vipaji vyako. Nilikuwa nimekupendekezea hapo awali kwamba tuanzishe biashara pamoja huko Uganda baada ya kuhitimu, lakini ulisisitiza kusaidia biashara ya familia na kukaa karibu na mpenzi wako. Vipi umeolewa sasa hivi?" Joseph aliuliza.

Lisa akainamisha kichwa kwa aibu na kujibu. "Tuliachana."

Joseph alionekana kushangaa lakini haraka akamfariji kwa upole. "Ni sawa. Bado wewe ni kijana na mrembo. Nina hakika unaweza kupata mtu bora zaidi.”

"Inatosha kuzungumza juu yangu.” Lisa akahamisha mada. “Unafanya vizuri sana kwenye kazi. Nilisikia umekuwa mbunifu watatu bora zaidi huko Uganda na hata kuchapisha vitabu kadhaa.” Lisa alitania huku akitabasamu. "Na sasa unajaribu kushindana hapa Bongo pia?"

"Jiunge na kampuni yangu ikiwa unadhani nina uwezo. Ninahitaji watu wenye talanta kama wewe,” Joseph alimshawishi kwa bidii, “naweza kukupa mshahara mkubwa. Unaweza pia kuwa mwanahisa biashara itakapoingia sokoni.”

"Sawa, nitakuandalia chakula cha jioni leo ili kusherehekea kuwa bosi wangu." Lisa hakika hakutarajia mshangao huu wa kupendeza. Alimpigia simu Alvin na kumwambia. “Sitakuwa nyumbani kuandaa chakula cha jioni. Panga mwenyewe."

Alvin alikasirika sana siku hiyo kwa sababu wengine walikuwa wakimdhihaki kwa siri kutokana na alama za meno kwenye shavu lake. “Nini tena muda huu? Usifanye ujinga wako ukidhani nitakuokoa tena. Sina muda.” Alvin alimjibu kwa hasira.

Lisa alimwambia kwa upole. "Ninaenda tu kula chakula cha jioni na rafiki yangu niliyekutana naye nikiwa nasoma nje ya nchi."

Alvin alicheka kwa kejeli. "Loo, kwa hivyo ni rafiki kutoka chuo kikuu wakati huu. Usisahau jinsi ulivyotekwa hotelini na rafiki yako wa shule ya sekondari mara ya mwisho.”

"Nilikuwa nakupa taarifa tu. Kwaheri.” Lisa alikata simu kwa papara.

Hali ya kukatishwa tamaa iliangaza machoni pa Joseph alipouona uso wake wenye hasira. “Mpenzi mpya? Au mume?”

Alitoa macho kwa mshtuko. "Hapana. Ni mwenzangu tu… Housemate.” Lisa hakuwa amekosea hata hivyo kwa kujibu vile. Ingawa Alvin alikuwa mume wake halali wa ndoa, mwanamume huyo alikataa kukiri hilo. Kwa hivyo, uhusiano wao ulikuwa wa maonyesho tu.

Joseph alitoa tabasamu hafifu. "Ilionekana kama unazungumza na mpenzi wako."

“Um… Kweli?” Lisa alihisi mapigo ya moyo yakirukaruka. Hivi ndivyo alivyokuwa akitangamana na Alvin. Labda ilisikika tu kwa sababu walikuwa wakiishi katika nyumba moja.

Ilikuwa ni muda mrefu sana tangu alipokutana na Joseph huko Marekani. Wawili hao walifurahia jioni pamoja na chakula cha jioni kilidumu hadi saa tatu usiku. Alimpa lifti na kumpeleka hadi nyumbani kwani siku hiyo Lisa hakuwa anatumia gari lake.

“Kumbuka kuripoti kwangu kesho asubuhi. Nimechukua mradi wa jengo la kifahari katika eneo la Mbezi Beach. Utaenda kuchukua vipimo kesho."

“Hakika.” Lisa alimpungia mkono wa kwaheri. Macho yake yaliikodolea gari hiyo aina ya Range Rover kwa mbali kabla hajageuka kuelekea nyumbani.

Kwa bahati mbaya, alimgundua Alvin, akiwa amevaa nguo za kawaida za mapumziko akimtazama chini kwa hasira kutoka kwenye ngazi. Charlie alikuwa ametulia mikononi mwake, akionekana kama alikuwa karibu kulala.

“Rafiki yako ni mwanaume?” Alvin aliuliza kwa hasira, ndita zilizokuwa zimekunjwa katikati ya macho yake zingeweza kumfinya inzi hadi kufa. Alipofikiria jinsi ambavyo alilazimika kuvumilia chakula kilichotengenezwa mgahawani vibaya wakati Lisa alifurahia jioni hiyo kula na kucheka na mwanaume mwingine, hasira ilimpanda kama mawimbi ya bahari.

“Ndiyo, yeye ni mwandamizi wangu kutoka chuo kikuu…”

Alvin alimkatisha. “Lisa, ngoja nikukumbushe kuwa umeamua kuolewa na mimi. Afadhali uangalie matendo yako hata kama tuko kwenye ndoa ya mkataba. Sitaki kusalitiwa.”

Tabasamu usoni mwa Lisa likaganda. “Unasemaje? Nilitoka tu kwenda kula chakula cha jioni na rafiki. Je, unanifikiria miye ni mhuni sana?”

"Nani anajua? Nimekufahamu kwa muda mfupi tu.” Alvin aliongea kwa tabasamu la kejeli. "Mbali na hilo, huwezi kwenda tu kwa chakula cha jioni na kusahau kuhusu jukumu lako kama mhudumu wa Charlie. Unawajibika kwa ajili yake kwani wewe ndiwe uliyemsababishia ugonjwa.”

“Charlie yuko sawa sasa. Nadhani hata aliongezeka kilo chache,” Lisa alijibu kwa upole. Bila shaka angebishana naye ikiwa asingekuwa kaokoa maisha yake mara mbili.

Alvin alicheka. “Sawa, kwa nini ameongezeka uzito? Unapaswa kujitafakari. Nataka umtunze paka, sio kumnenepesha.”

Lisa alishindwa cha kusema. Kuongezeka kwa hamu ya kula kwa Charlie lilikuwa kosa lake pia.
Alikaribia kushindwa kuzuia hasira iliyokuwa ikifuruma kifuani mwake. "Sawa, nitampa paka chakula kidogo kuanzia sasa."

"Hilo halitasaidi pia." Alvin bado alimkalia vibaya. “Je, ikiwa paka ndani yake atakuwa na utapiamlo?”

“Sawa, unataka nini basi? Samahani, lakini mimi si mfugaji wa paka kitaaluma.” hatimaye Lisa alisema kwa hasira.

“Hata mimi sijui.” Alvin naye akajibu kwa ukali. “ Ifanyie utafiti na umfikirie zaidi Charlie. Mpeleke matembezini ukiwa huru. Usimpe chakula tu kisha umruhusu alale siku nzima.” Kisha kusema hayo, Alvin alitembea kuelekea kwenye bustani ya jirani na Charlie mikononi mwake.

Lisa aliishia kumshangaa tu mwanamume yule mwenye gubu. Alitaka kushiriki naye furaha ya kupata kazi mpya, lakini hakuweza kujisumbua kuzungumza naye kwa sekunde nyingine zaidi. Alipokuwa akiingia ndani kuelekea chumbani kubadilisha nguo, sauti kali ilisikika nyuma ya mgongo wake. "Nina njaa."

Alitazama nje na kumwona mtu aliyeketi kwenye bustani, akionekana kama mnyama mwenye njaa kali anayesubiri kulishwa.

Lisa alikataa, kwani bado alikuwa amekasirika kutokana na kejeli zake hapo awali. "Samahani, mimi ni mhudumu wa paka wako, sio mhudumu wako." Alisisitiza maneno matatu ya mwisho.

Alvin alionekana kutopenda. Alichia tabasamu la kejeli na kuongea kwa sauti ya kutetema. "Huu ndio upendo unaotangaza kuwa wewe ni mke wangu?"

'Ninachotaka ni nafasi ya kuwa shangazi wa Ethan! Umeipata hiyo!' Lisa alijiwazia, lakini hakuthubutu kuyasema maneno hayo kwa sauti. Akiwa amekasirika kidogo, aliingia jikoni na kuanza kuandaa chakula.

Alvin alikuwa akisubiri chakula kwa hamu akiwa anazunguka bustanini na paka wake. Hakuna chochote zaidi ya chakula alichotayarisha Lisa kilichomtia hamu tena. Labda alikuwa amemtilia dawa kwenye chakula alichokuwa anakula muda wote huo.

••••••

Baada ya kifungua kinywa asubuhi iliyofuata Alvin alikuwa amevaa kiofisi tayari kuelekea kazini alipogundua Lisa naye alikuwa amebadilika na kuvaa kimtoko-mtoko hivi. Lisa alikuwa amevaa shati la waridi iliyokolea na suruali ya jeans iliyombana kidogo. Alionekana kama mfanyabiashara hodari, lakini mavazi hayo pia yaliangazia umbo lake mwanana. Isitoshe, alikuwa amejipodoa kidogo na hereni za lulu zilining'inia chini ya masikio yake. Aliona ni vigumu kumvua macho mrembo huyo.

Alvin aligundua kuwa Lisa alikuwa akitoka. “Unatoka kwenye miadi yako tena?” Sauti yake ilikuwa ya chini ikionyesha kutofurahishwa kwake.

“Hapana, naenda kazini. Nilipata kazi mpya jana. Nitakuwa nyumbani kuandaa chakula cha jioni na pia kumtembeza Charlie baada ya hapo.”

Alvin hakupata maneno ya kubishana na hilo. Pamoja na hayo, hakuwa na wasiwasi kuhusu kazi yake. Akamuuliza. "Unagawa vipeperushi tena?"

"Hapana. Mimi ndiye mbunifu mkuu wakati huu." Alicheka kabla ya kuchukua mkoba wake na kuondoka mlangoni.

Alvin alimfuata nyuma yake na kutoka naye pamoja. Koo lake lilihisi kukauka huku akiibia jicho lingine la umbo lililopinda la yule mwanadada. “Unataka lifti?”

“Hapana, asante.” alikataa bila kusita. “Nitaendesha gari.” Alvin hakuwa na la kusema.

Saa mbili na nusu asubuhi Lisa aliingia katika eneo lake jipya la kazi kwa wakati ufaao. Ilikuwa ni mshangao kujua kwamba wafanyakazi wengine wote walikuwa vijana na wenye shauku. Mbali na hilo, wote walikuwa wahitimu tofauti ambao walikuwa wamesoma nje ya nchi.

Joseph alimtambulisha Lisa kwa wafanyakazi wenzake kabla ya kuingia naye ofisini. Kisha alitoa ramani. "Hii ni nyumba ya Bw. Kelvin Mushi yenye ukubwa wa mita za mraba 3,000 katika eneo maarufu la Mbezi Beach. Huyu mtu aliwahi kuwekeza ng'ambo biashara zake na ndivyo nilivyokutana naye. Tumefahamiana kwa muda mrefu sasa.” Joseph alitikisa kichwa kwa umakini. "Anapanga kutulia nyumbani hapa Dar es Salaam kwa hiyo anataka kutengeneza jumba hili kwa ajili ya makazi. Fanya bidii kwenye mradi huu. Hakuna kikomo cha gharama kwenye ukarabati, lakini kila kitu lazima kiwe kamili. Ana mradi mwingine unaosubiri kuzinduliwa mwishoni mwa mwaka. Natumai kujenga naye ushirikiano wa muda mrefu.”

Tabasamu likatanda tena usoni mwa Joseph. “Kwa kweli, rafiki wa kike wa mpwa wa Bw. Mushi anatoka katika historia ya ubunifu majengo na mambo ya ndani, lakini Bw. Mushi hakutaka kutumia kampuni hiyo kwa sababu hapendi sana ubunifu wao hivyo anakarabati jumba lake kwa siri bila kumwambia mtu mwingine yeyote wa familia yao, kwa hivyo na wewe huna budi kuficha hili. Usifanye mambo kuwa magumu kwa Bw. Mushi.”

Bila kukawia, Lisa alitoka ofisini na kuendesha gari hadi Mbezi Beach. Hiki ni miongoni mwa viitongoji vya kifahari zaidi hapa Dar es Salaam. Ni matajiri tu ndio wanaweza kumudu kujenga mali hapo.

Gari lake lilisimamishwa na mlinzi kwenye mlango wa geti, hivyo ikabidi atembee hadi ndani. Mwanamume aliyeonekana kuwa na umri wa miaka 30 hivi alikuwa amesimama kando ya kidimbwi cha kuogelea. Mtu huyo mrefu alionekana kuwa na sura ya upole. Suti nyeusi ya biashara iliyotengenezwa kwa ufundi ilimpendeza sana.

Kwa mshangao, Lisa aliuliza kwa utulivu, “Bw. Mushi?”

“Ndiyo. Je, wewe ni mbunifu kutoka kampuni ya Joseph? Wewe ni mdogo kuliko nilivyotarajia." Mshangao wa kweli uliangaza machoni pa Kelvin Mushi.

“Joseph alinitangulia mwaka mmoja katika chuo kikuu. Bw. Mushi, unakaribishwa kunibadilisha ikiwa haujaridhika baada ya kuona kazi yangu.” Maelezo ya Lisa yalikuwa shwari na ya kujiamini. "Mbali na hilo, sidhani umri una uhusiano wowote na uwezo. Wewe mwenyewe ni kijana sana, Bw. Mushi.”

Kelvin alitabasamu. "Siwezi kubishana na hilo."

Lisa alimpatia Kelvin business card yake. Kelvin akaitazama. "Lisa Jones Masawe. Jina maarufu sana hili."

“Ni jina la kawaida kabisa.” Lisa alihisi moyo wake ukirukaruka. Kwa kuhofia kwamba huenda amesikia kuhusu uvumi mbaya unaoenezwa na familia ya Masawe. “Ikiwa haujali, Bw. Mushi, unaweza kuniambia mawazo yako tunapozunguka jumba hili la kifahari.”

Kelvin aliongoza njia na kumuonyesha kila sehemu ya jumba hilo. Mbali na hilo, alitaja matakwa yake ya kuwa na ukumbi wa mazoezi, ukumbi wa michezo, uwanja wa mpira wa kikapu, na bwawa la kuogelea la ndani. Lisa alikuwa na wazo la jumla la liliendana na matamanio yake. Katika chini ya nusu saa, alimpatia mchoro mzuri mikononi mwake.

Kelvin aliutazama mchoro ule, hakuweza kupata kitu cha kubaini makosa. Mpango huo wa kubuni ndio hasa alikuwa ameufikiria. "Bi jones, wewe ni mzuri kama wabunifu wakubwa ambao nimewaona kutoka nje ya nchi. Sio mbaya. Wazo la bwawa hili la kuogelea la ndani ni la kibunifu kweli.”

"Itaonekana bora zaidi baada ya kuisanifu." Lisa aliongezea.

“Hakika, una muda wa wiki moja. Ningependa kuanza ukarabati haraka iwezekanavyo.” Kelvi akampa Lisa business card yake. “Unakaribishwa kunitafuta ofisini kwangu michoro itakapokamilika. Hii ni kadi ya jina langu."
Kadi ile ilionyesha Kelvin Mushi alikuwa ni mkurugenzi wa kampuni ya Usafirishaji, Golden Corporation.

Baada ya kuondoka kwenye jumba lile, Lisa alipanga kuangalia miundo ya majengo mengine ya kifahari katika kitongoji hicho. Alipotoka tu nje ya geti, aliona Harrier nyeusi ikiingia kwenye moja ya majengo makubwa ya kifahari. Hilo lilikuwa gari la Alvin.

‘Ina maana amenunua nyumba huku pia?’ Lisa alijiuliza bila majibu kabla ya kushtuliwa na sauti ya kiume. “Kwa nini uko hapa?” sauti aliyoifahamu vizuri ilisikika nyuma yake ghafla. Ethan alikuwa kasimamisha gari pembeni kidogo mwa barabara akitazamana naye. Lisa alitazama na kumwona Ethan akitoka kwenye Lamborghini yake. Wakati huo alikuwa akigeuka ili kuondoka, lakini alishtuka kidogo kugongana naye hapo.

“Mimi ndiye ninayepaswa kuuliza. Wewe na Lina mnapanga kununua jumba la kifahari hapa, au unatafuta nini huku?" Lisa alirudisha swali.

“Hapana. Niko hapa kuangalia nyumba ya mjomba wangu. Jumba lake linahitaji kukarabatiwa na ninapanga kumshawishi kukabidhi mradi huo kwa Lina.” Ethan alimwambia Lisa huku akimkazia macho usoni. “Unaona Lisa, ningeweza kumshawishi mjomba akupatie huo mradi wa kukarabati jengo lake la kifahari kama mimi na wewe tungekuwa bado tunaelewana vizuri.” Ethan alimwambia kwa kujidai.

Hapo awali Lisa aliliona gari la Alvin na punde akamwona Ethan mitaa hiyohiyo, je hii ilikuwa ni bahati tu? Kwa kuwa wawili hao walikuwa wamefuatana na aliamini walikuwa na uhusiano wa mjomba na mpwa, Lisa alihisi kuwa Alvin alikuwa amenunua jumba la kifahari huko Mbezi Beach na Ethan alitaka amshawishi ili ampatie Lina kwa ajili ya kulikarabati. Hilo lilimuuma sana Lisa.

Ethan alitabasamu kwa dharau alipoona hali ya mawazo imeifunika sura ya Lisa. " Unajutia maamuzi yako sasa? Na bado, utajuta sana!”

Lisa alikasirishwa na maneno ya Ethan nusu ya kutema damu. Lisa alimshangaa Ethan kwa kufikiri alikuwa akimuwazia yeye. Ni mawazo ya Alvin ambayo yalimfanya akose raha muda huo. Alijiuliza kwanini Alvin anunue jumba huko kisirisiri kisha amkabidhi Lina mradi wa kukarabati jumba hilo? Hicho ndicho hasa kilikuwa kikimuuma Lisa. hata kama hakuridhika na ubunifu wa Lisa, ulikuwa ni uamuzi wake kuchagua kampuni nyingine yoyote ya kubuni muundo wa ukarabati wa jumba lake, lakini siyo kukabidhi mradi wa ukarabati kwa Lina!

"Sawa, mjomba wako ndiye mwenye uamuzi wa mwisho juu ya nani atampa kazi ya ukarabati, sio wewe. Labda atashawishiwa kwa urahisi na mke wake. Maneno yako ni kama kinyesi tu kwangu." Lisa alimjibu Ethan kwa hasira.

Ethan alikunja uso baada ya kusikia hivyo. “ Mjomba wangu bado hajaoa. Isitoshe mimi na yeye zinaiva sana, na kwa kawaida huwa anakubali chochote ninachomwambia.”

Lisa alitabasamu kwa dharau. “Hakika muombe akufanye mrithi wa mali zake na uone kama atakubali.”

“Umerukwa na akili.” Uso Ethan ulibadilika kwa hasira. “Si ajabu kwamba Mjomba Jones na Shangazi masawe walikufungia kwenye jumba lao huko Moshi. Hakika unastahili.”

Maneno yake yalichochea chuki iliyozikwa ndani ya moyo wa Lina. "Ethan, unafahamu lakini unachokiongea?"

“Kwani nimekosea? Uliwaambia waandishi wa habari kwamba familia ya Masawe ilikufungia na kukutesa. Lakini unaonekana mwenye nguvu na mwenye afya kwangu, kana kwamba umekuwa ukiishi vizuri. Uwepo wako ni bahati mbaya sana kwa familia ya Masawe. Unajua kwamba kwa sababu ya shutuma zako, sifa ya Kibo Group zimeharibiwa na bei yao ya hisa imeshuka sana? Thamani ya soko ya kampuni ilipoteza dola milioni mbili kwa usiku mmoja.”

Lisa alihisi hamu kubwa ya kummeza Ethan mzima mzima. "Kitu pekee kinachonifanya nisikitike ni kwamba, mwanzoni nilipoteza muda wangu kukupenda sana bila kujua kuwa huna akili hata kidogo. Akili ulizonazo zinakutosha kujua chakula tu na njia ya kwenda chooni, basi!"

Ili kuepuka asije akapandisha hasira mbaya nakufanya mambo yasiyotarajiwa, Lisa aliwasha gari, akakanyaga mwendo na kuanza kuondoka.

SURA YA34

"Subiri." Ethan alimzuia na kumwambia. “Sherehe yetu ya uchumba na Lina imepangwa mwishoni mwa mwezi huu. Lazima uhudhurie sherehe hiyo. Ni wewe uliyeharibu sifa ya Kibo Group hivyo unawajibika kuiokoa.”

“Bullsh*t! Niondokee hapa ,wenda wazimu wewe. Siwezi kusubiri kuona Kibo Group ikifilisika kabisa. Ulisaliti uhusiano wetu na bado una jeuri ya kunidai nijitokeze kwenye sherehe yako ya uchumba. Una wazimu nini! Huna hata aibu?!" Lisa alilaani.

Ethan hakuonesha hata wasiwasi. Alizidi kumzuia Lina na kumwambia tena.“Sherehe yetu itaambatana na kumbukumbu ya kuadhimisha miaka 80 ya kuzaliwa kwa bibi yako. Alikupenda sana tangu ukiwa mdogo, unajua! Na afya yake inazidi kuzorota kila siku, na nani anajua amebakisha muda gani? Bado hutaki kuhudhuria?”

Mwili wote wa Lisa ulimsisimka huku akimtazama Ethan kwa hasira kali. “Yaani sherehe ya kuzaliwa bibi yangu mnaijumuisha na mambo yenu ya kijinga?”

"Na ukiacha kuja bibi yako atasema unamdharau, kumbuka bibi yako ndiye mtu pekee aliyebaki anakupenda!" Maneno ya Ethan yalijaa dharau.

“Usijali. Nitakuja." Lisa alikubali kwa hasira na kuondoka. 'Nitakuwepo na mjomba wako Alvin. Nataka kukuangamiza wewe na mchumba wako asiye na maana kabisa!’ Lisa alijisemea kimoyomoyo wakati anaondoka. 'Nataka kumfanya mjomba wako kuwa mtiifu kwangu 100%. Lina hataweza kujiunga na familia yenu mradi tu sitakubali!' Lisa alijiwazia kwa hasira.

Ethan alitikisa kichwa kwa dharau wakati akimwangalia Lisa akitokomea kwa mbali. Baada ya Lisa kupotea machoni mwake, Ethan alitembea kuelekea kwenye jumba la kifahari la mjomba wake, Kelvin Mushi.

Kelvin alikuwa akikagua mchoro alioachiwa na Lisa kwenye kiti cha mapumziko chini ya mti. Alikunja uso na kuuficha mchoro ule kwa siri baada ya kugundua kuwasili kwa mpwa wake.

"Mjomba, lini utaanza kukarabati jumba lako?" Ethan alikuwa ameona mchoro kabla haujafichwa.

"Ulisikia kutoka kwa bibi yako sivyo?"

“Ndiyo,” Ethan alijibu huku akitabasamu. “Umelidhamiria kweli jambo hili? Acha Kibo Group ishughulikie suala hilo. Lina mwenyewe ni mbunifu mzuri. Mpe nafasi.”

Kelvin alizuia hamaki yake alipoinuka na kusimama. "Ethan, najua mambo kadhaa kuhusu wabunifu katika kampuni ya Kibo Group. Mtindo wao wa ubunifu ni wa kifahari lakini ni wa kizamani sana na unatofautiana sana na malengo yangu. Nimeishi nje ya nchi kwa muda mrefu sana na ninapendelea mitindo fulani ya kigeni.”

"Sawa, unaweza kuwasilisha mawazo yako kwa Kibo Group. Sifa ya kampuni yao imeathiriwa sana hivi karibuni. Mjomba, tafadhali unaweza kuwasaidia?”

"Hapana." Kelvin alipunga mkono wake hewani bila kusita. "Naweza kukubaliana na chochote mbali na hili. Nina viwango vya juu vya makazi yangu. Nimekutana na Lina hapo awali. Kusema kweli, hana uzoefu na hajui chochote kuhusu vifaa vya kisasa vilivyo kwenye fasheni. Ataharibu tu nyumba yangu.”

Ethan aliona aibu kidogo. Ni mchumba wake walikuwa wakijadiliana, hata hivyo, hivyo alizidi kumpigania. "Lakini alifanya vyema katika mradi wa Kituo cha Utamaduni na Teknolojia..."

"Usisahau kuwa alishinda zabuni kwa sababu tu nilimpambania! Ukaribu wangu na Mzee Kamote ndiyo ulimpa nafasi hiyo." Sura ya kutofurahishwa ilijiosha usoni mwa Kelvin alipokuwa akiongea kuhusu hili. "Mbali na hilo, unapaswa kushukuru kwamba Mzee Kamote hakutufichua au tungekuwa katika matatizo makubwa."

Ethan alihisi moyo wake kuzama. "Sawa, sio jambo kubwa ikiwa hukubaliani. Kwa hiyo unaenda kwa mbunifu gani? Nauliza kwa udadisi tu na si kingine.” Ethan aliuliza huku macho yake yakiwa yamelenga kwenye mchoro.

"Joseph Ruta, ni rafiki yangu kutoka Uganda. Alifungua tawi hapa Dar es Salaam.” Kelvin alikabidhi mchoro huo kwa mpwa wake. "Hii imeundwa na mmoja wa wabunifu wake. Alitoa mchoro wa jumba zima la mita za mraba 3,000 kwa chini ya nusu saa, bila kusahau kutoa maelezo ya undani kikamilifu kulingana na mapendekezo yangu. Nimeridhika sana.”

“Lisa?” Ethan aliganda kwa sekunde kadhaa alipoona saini ya Lisa chini kulia mwa mchoro. Alikumbuka kugongana naye getini hapo awali. Ilivyoonekana, alikuwa hapo kubuni muundo wa jumba la mjomba wake.

"Ndio, huyo ndiye." Kelvin alijibu kwa dhati.

"Mjomba, huwezi kumwajiri Lisa," Ethan alisema kwa uchungu, "Yeye ni binti mdogo wa familia ya Jones Masawe niliyekuambia hapo awali. Aliwahi kuwa mpenzi wangu lakini amekuwa na sifa mbaya sana. Sio tu kwamba aliiba kazi ya mtu mwingine, lakini pia aliharibu sifa ya wazazi wake mwenyewe.”

Hili lilimshangaza Kelvin. Haishangazi alidhani jina hilo halikuwa geni akilini mwake. Lakini alipokumbuka tabia ya fadhili na adabu ya Lisa, alikunja uso. "Sidhani kama anahitaji kuiga wengine, kutokana na talanta zake. Nimepata uzoefu mzuri wa kushughulika na watu wa aina zote katika ulimwengu wa biashara. Yeye ni kipaji adimu, na sidhani kama yeye ni mtu asiyeheshimika. Kinyume chake kabisa, Ethan, nadhani una chuki dhidi yake!”

“Kweli humjui vizuri Lisa mjomba!”

“Mbona unanishangaza? Tulipozungumza kwa simu siku za nyuma, hukuweza kuacha kumpongeza lakini sasa umechukizwa naye ghafla. Je, alikukosea kwa namna fulani? Ni wewe uliyemsaliti kwanza nikikumbuka vizuri.”

Ethan hakuwa na neno la kukanusha jibu ambalo hakulitarajia. Kelvin akaendelea kumhutubia. "Vile vile, unaendelea kujivunia vipaji vya Lina, lakini sioni uwezo wake. Kama si kweli kwamba yeye ndiye mrithi wa familia ya Masawe, nisingemtazama kwa mara ya pili mwanamke kama yeye.” Kelvin alichukua mchoro kutoka kwenye mikono ya mpwa wake na moja kwa moja akaelekea mlangoni. Kelvin alikuwa tayari ameondoka muda mrefu wakati Ethan alipotulia tena kiakili.

SURA YA35

Lisa alitumia karibu siku nzima akifikiria kuhusu sherehe ya uchumba wa Ethan na Lina.Hatimaye, ilikuwa wakati wa kurudi nyumbani. Aliharakisha kurudi nyumbani mara moja, lakini Alvin hakurudi mapema hadi ilipokuwa usiku sana.

"Nadhani nilikuona Mbezi Beach leo." Lisa alimwambia Alvin kwa uso mkavu.

“Ulikuwepo huko leo?” Alvin alikodoa macho kwa mshangao.

“Ndiyo, ulikuwa unafanya nini pale?” Tabasamu likatanda usoni mwake. "Labda umenunua nyumba katika eneo hilo?"

"Hapana." Alvin alikanusha huku akichukua ‘chopsticks’ kutoka mezani. “Sam alikuwa amenisumbua kumsindikiza huko kutazama eneo lake. Siyo kwamba siwezi kununua nyumba kubwa ila ninahofia woga wako. Majumba ya kifahari huwa ni makubwa sana, yatakutisha na majinamizi yako.”

Lisa alimsikia maelezo yake lakini angemwamini ikiwa Ethan asingesema wazi kwamba mjomba wake alinunua jumba la kifahari huko Mbezi Beach. Kwa akili ya Lisa, Alvin ndiye alikuwa mjomba wa Ethan, kwa hiyo hakuelewa nia yake ya kuficha jambo hilo kwake. Alikuwa hapendi afahamu kuhusu mali zake, au alikuwa akipanga kumpatia Lina kukarabati jumba hilo ndiyo maana aliamua kumficha? Lisa angeweza kukubali uwezekano wa wazo la kwanza lakini wazo la pili lilimchefua nyongo. Aliichukia sana familia ya Masawe kwa kujaribu kuchukua maisha yake, pamoja na kinyongo chake kisicho na mwisho dhidi ya Lina.

"Ni sawa ikiwa ulifanya hivyo. Sitakulazimisha kuniajiri kama mbunifu wako,” alisema kwa mzaha nusunusu.

"Tayari nimesema sijanunua, unanilizamisha ili iweje?" Jibu lake lilikuwa la moja kwa moja.

Lina aliizungusha vidole vyake kwenye meza na kubadilisha mada ya mazungumzo. “Sawa, basi, labda pengine kuna hafla utakayohudhuria hivi karibuni? Labda utahitaji mwenzi wa kike wa kuambatana naye?”

“Hapana.” Alvin alijibu kifupi.

“Um… Sawa.” Lisa alishangaa. Alitaka kuuliza, ‘vipi kuhusu sherehe ya uchumba ya mpwa wako?’ lakini alisita. Alijishaua tu kwa kusema, “lakini mimi ninahitaji mwenza.”

Alvin akaziweka chopsticks juu ya meza na kumtazama moja kwa moja machoni. "Unajaribu kusema nini?"

“Bibi yangu atafikisha miaka 80 mwisho wa mwezi. Kumbukumbu ya kuzaliwa kwake inaadhimishwa pamoja na sherehe ya uchumba ya Ethan na Lina. Sina chaguo ila kujitokeza. Bibi yangu amekuwa mkarimu sana kwangu tangu nilipokuwa mdogo. Je, ungependa kwenda pamoja nami?” Lisa alijipa ujasiri kusema hivyo. Alimtazama kwa macho ya kutarajia.

Ilimchukua Alvin sekunde kadhaa kutoa jibu lake. “Nakumbuka nilikuambia kabla hatujafunga ndoa kwamba sitakutana na watu wa familia yako.”

"Kwa hiyo hata kwenye sherehe ya uchumba hutaenda?" Lisa aliuliza kwa kufoka.

“Kwa nini niende, Ethan au Lina wanahusiana nini na mimi?” Alvin aliuliza Haikuwa na maana yoyote kwake kwani hakuijua familia hiyo hata kidogo.

'Kwa hiyo wewe si mjomba wa Ethan?' Lisa alitaka kuuliza hivyo, akasita. Hata hivyo, ikiwa angeuliza hivyo, huenda angekisia kwamba alimjia kwa nia isiyofaa. Hivyo akasema, “kwa sababu watu wengine wengi mashuhuri jijini watahudhuria sherehe hiyo pia, kwa hivyo nilifikiri…”

“Samahani, lakini sina mpango wa kuhudhuria hafla za viwango vya chini kama hivyo.” Alvin alizima mada kwa kauli ya kejeli.

Lisa alikosa la kusema. Kiwango cha chini? Alikataa kuhudhuria sherehe ya uchumba wa mpwa wake kwa sababu hiyo? Alikuwa bora kiasi gani wakati huo? Je, huu ulikuwa ni mtazamo wa kiburi wa kila mtu aliyerudi nyumbani baada ya kukaa miaka mingi nje ya nchi? Maswali magumu yalitawala uso wake.

“Mbali na hilo, nitakushauri usiende pia. Siwezi kuhangaika kwenda kukuokoa tena pindi familia ya Masawe itakapokufanyia ushenzi.” Alvin alimuonya kwa ukali huku akimkodolea macho.

Lisa alipoteza hamu ya kula ghafla. Alichukua simu yake na kuanza kuchati na Pamela kupitia WhatsApp.

Lisa: [Na ulisema Alvin anaweza kuwa na hamu kidogo nami? Samahani, lakini sijisikii hata kidogo. Kila sekunde ninayotumia naye hufanya damu yangu ichemke.]

Pamela: [Hey, endelea kujaribu. Je, tunaweza kutoka kula chakula cha jioni? Imekuwa siku nyingi sana.]

Lisa : [Hapana. Alvin atachukia nikiondoka nyumbani.]

Pamela: [Haya, wewe si mlinzi wake wa nyumbani. Unamdekeza sana.]

Akiwa hana chaguo lingine, Lisa alipanga vyombo na kutokea tena baadaye akiwa kabadilisha mavazi. “Nitatoka kwa muda kidogo baadaye.”

"Wapi?" Macho ya Alvin yalijawa na kero. "Unaenda kunywa pombe tena au kwa familia ya Masawe? Au unaenda kwenye miadi na mwandamizi wako? Usisahau bado unapaswa kumpeleka Charlie matembezini baada ya kula."

Lisa alipoteza ujasiri wa kusema ukweli. "Ninaenda kufanya shopping na Pamela. Hali ya hewa inazidi kuwa joto na ninahitaji nguo mpya."

Alvin alimtazama juu na chini kabla ya kutoa maamuzi. "Sawa, nahitaji nguo mpya pia, kwa hivyo ninulie chache pia. Tumia tu kadi ya benki niliyokupa mara ya mwisho,” Alvin alisema kwa uvivu.

Lisa alikosa la kusema. Kwa kweli hakuwa na nia ya kwenda shopping ila alitaka tu kufurahia chakula cha jioni na Pamela. “Sawa, sawa, nitakwenda kukunulia. Unavaa saizi gani?"

"Hata hujui ninavaa saizi gani bado una ndoto ya kunikaribia kitandani kwangu?" Alvin aliongea akiwa seroius, ilibidi kwanza Lisa acheke.

"Sawa, unatafuta nguo za bei gani?" Lisa alimuuliza tena.

“Yoyote, mradi utaipenda.” Alvin pia hakuwa na uhakika. Baada ya yote, siku zote alikuwa na wabunifu binafsi wa kutengeneza nguo zake.

Dakika kumi baadaye, Pamela alifika akiwa kwenye gari lake. Lisa aliingia ndani ya gari huku akionekana kukata tamaa. “Twende dukani. Alvin anataka nikamnunulie nguo.”

“Lakini vipi kuhusu chakula? Bado sijapata chakula tangu mchana nilikuwa busy kweli.” Pamela alisema kwa kuchanganyikiwa. Lisa hakuwa na jinsi zaidi ya kumwambia ukweli. Pamela alimtazama tena kwa dharau. “Heshima yako imeenda wapi? Umekuwa mnyonge sana kwa Alvin tofauti na zamani. Mbona kwa Ethan hukuwa hivi?”

“Huelewi. Alvin hutumia kisingizio cha jinsi nilivyosababisha Charlie awe mgonjwa dhidi yangu,” alijibu Lisa. "Mbali na hilo, aliokoa maisha yangu mara mbili na ninataka kulipa fadhila."

"Hakuna mtu mwingine anayemdhibiti mkewe namna hii," Pamela alidhihaki.

“Sawa, achana naye. Najua mimi ni mlinzi wake wa nyumbani.” Lisa aliyekuwa amekaa kwenye kiti cha abiria alionekana kukata tamaa. “Unadhani nisipojishusha naweza kusimama mbele ya kina Ethan kama shangazi yao? Sherehe ya uchumba wao inakaribia.”

Pamela alitikisa kichwa kufikiria hili. “Labda Alvin anakuchukulia wewe kama mfanyakazi wa nyumbani ambaye unapika vizuri. Lazima ubadili mawazo yake kidogo, na njia bora ya kufanya hivyo ni kumwonjesha mapenzi yako.”
Lisa alibaki kimya. "Jaribu kuwa mke mpaka kitandani kwake, usiishie jikoni tu." Pamela akamtupia jicho la kustaajabisha. “Unajua ninachomaanisha.”

Lisa alipigwa na butwaa. Uso wake ukajawa na aibu. "Anaweza kunitoa kitandani mara moja."

“Unaweza kumlewesha hoi. Wanaume hupoteza kujizuia mara wanapokuwa walevi. Mambo yatakuwa mazuri zaidi ikiwa utapata mimba ya mtoto wake. Nafasi yako kama malkia wa familia itaimarishwa bila wewe kuendelea kupigana. Sawa, ni lazima upange hili vizuri. Tegeshea karibu na siku baada ya hedhi yako kwani utakuwa na uwezo wa kunasa mimba zaidi wakati huo.”

Akili ya Lisa ilikuwa imechanganyikiwa na mawazo mengi tofauti. Hakuwa na mpango wa kubeba mimba ndani ya uhusiano wao usioeleweka? “Lakini hanipendi. Familia kama hiyo sio mazingira bora kwa mtoto…”

“Lazima uwe umejitayarisha kwa hili ulipoamua kuoana naye bila kusita,” Pamela alimkatalia, “Mbali na hilo, si unataka kulipiza kisasi wewe? Hii ndiyo njia bora ya kujumuika katika familia ya Lowe na kuwaletea matatizo kwa kutumia nafasi yako kama mke wa Alvin Kimaro. Fikiria kuhusu hili! Na hawawezi kukutukana kwa sababu utapewa nafasi ya juu kuliko wao katika uongozi wa familia.”

"Wazo zuri." Lisa alionekana kuafiki. "Lakini kwa nini wewe hujafanya hivyo na Patrick?”

Pamela akakosa majibu.

TUKUTANE KURASA 36-40

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom