Simulizi: Kazi ya Kutengeneza Majeneza

Sehemu ya 101

Niliinua kichwa kama vile naona nikijikuta kama nategemea kupata kitu fulani kutoka kwenye maombi hayo.
Kichwa kiliniuma zaidi ya nilivyowahi kuumwa siku za nyuma, lakini sikutaka kutoka mpaka nione nini matokeo yake.

Ghafla macho nayo yakauma kama vile yaliingia mchanga. Ilibaki kidogo tu nipige kelele za kuomba msaada kutoka kwa wale wenye nyumba yao, lakini sijui nilipata wapi ujasiri nikatulia kimya nikisubiria nisikie hayo maombi yatakavyokuwa yakiombwa na yule mtu aliyekuwa akisema.

"Kwani akiomba hivyo hata mimi wa nyumbani ninayeona naweza kupona?" niliwauliza.

"Ndiyo maana wamekitangaza kwenye tivii ili kila mtu aone," alijibu mwanamke.
"Kwa hiyo mimi nitajuaje kama nimepona?"
"Utajua tu, kinachokuuma kitapona," aliposema hivyo nikabaki navumilia tu litakalotokea na litokee sasa kwani nilikuwa tayari kwa lolote

Nikiwa katika hali ya kutoona, nilijiwa na picha ya ajabu sana. Yule mama jirani alinisimamia mbele yangu na kuniuliza.
"Unadhani utakuwa umemaliza tatizo siyo?"
Nilimjibu ndiyo nitakuwa nimemaliza tatizo, akaniuliza tena.

"Na nyumba hii unayokaa utahama au?"
Nilijibu sihami kokote, liwalo na liwe kwa sababu mwenye nyumba hatuna ugomvi naye.

Akanisogelea huku akiinua mikono juu na kukunjua vidole kama vile alitaka kunikaba sehemu. Nikamkwepa akacheka sana huku akizidi kunisogelea.

"Naombenu mtu anishike mkono," niliwaambia wale wenyeji wangu. Lakini mwanaume akasema itakuwa vyema wanipeleke kwangu kama ni imani tayari nimeshaonesha sana mbele ya Mungu, lakini nikakataa kwamba sitaki mpaka nione mwisho wa maombezi yale siku ile.

Nikamsikia muombaji akisema kuwa, kama magonjwa ni mengi au kuna matatizo ulalie juu ya kifua chako upande wa moyo kwani ndiyo binadamu alipo.

Nilifanya hivyo kisha nikaanza kumsikia akiomba kwa sauti. Alisema nguvu zote za giza zikashindwe. Mipango yote ya shetani pia ikashindwe mara moja kwa kila mtu aliyekuwa ukumbini au kanisani kule na au waliokuwa wakiangalia tivii.

Mara ghafla, macho yangu yakaona tena na pia kichwa kikapona pale pale haraka sana. Sikuamini, niliangalia huku na kule na kutaka kupiga kelele, lakini mwenye chumba kile akanizuia akisema kuwa, si busara kama ni kusema nisubiri kwanza.

Nilikuwa mwepesi sana tofauti na siku nyingine yoyote. Nilijihisi kuwa, nilikuwa nimebeba mzigo mzito kwa siku nyingi sana sasa nilikuwa nimeutua kwa hiyo nilikuwa sina mzigo tena. Lo! Nilisema mwenyewe.
Nilijaribu kufumba macho na kuyafumbua, nikaona kama kawaida tu.

Kila mtu mle chumbani kwa mwenyeji wangu aliniangalia mimi na mahubiri yalikuwa yamemalizika wakati huo.
Pale pale mjukuu wa mwenye nyumba alibisha hodi akaulizia kama niko kule naitwa na bibi yake.

"Amesema uende haraka sana," yule mjukuu aliniambia.
"Kuna nini kwani, anaumwa?" nilimuuliza.
"Sijui, amesema uende haraka," alisema akiondoka zake.

Niliwaaga wale watu huku wakiniambia kama nilijisikia kupona nihakikishe habari hizo siziweki hadharani haraka vile, nikawakubalia.
Niliingua kwa yule bibi na kumkuta amekaa na wajukuu wake wengine na binti yake wa mwisho wakiongea.

Bibi aliponiona tu mimi alikunja sura ingawa ilikuwa usiku lakini nilitambua hilo.
"Kaa hala, nyinyi ondokeni," aliseam akimaanisha mimi nikae watoto waondoke pale sebuleni kwake.

"Nimekuita kukwambia jambo moja tu muhimu. Kuanzia kesho nakitaka chumba changu unachoishi, tena ninaposema nakitaka kesho maana yake nakitaka haraka sana. Kama ni pesa bado unayoitumikia kukaa hapa mimi nitakurudishia, nimegundua wewe si mtu mwema kwangu, unataka kuniua wewe."

Je, nini kiliendelea?
 
Sehemu ya 102

Sikujua kwanini yule mzee aliniambia maneno yale kwamba nihame, tena katika kipindi cha siku moja tu na pesa zangu atanirudishia.
Kabla sijamuuliza kwanini maneno yake yalikuwa yakijirudia kichwani mwangu bila kupata jibu.

"Bibi nimekuelewa lakini kwa nini umesema nataka kukuua?" nilimuuliza kwa sauti yenye adabu nikiamini kuwa, kama amesikia kitu kibaya kutoka kwangu angeniambia.
"We unajua, halafu nakushangaa unaniuliza," alinijibu hivyo.

"Mh!" nilijikuta nikiguna. Kumbe kitendo hicho kilimpandisha hasira zaidi.
"Unaguna siyo? Sasa utakiachia hukiachii?" aliniuliza.

"Nitakuachia bibi yangu," nilimjibu kwa busara.

"Eee nakitaka chumba changu ukinizungusha utajua mimi nani?" aliniambia.

Niliaga na kuondoka mpaka chumbani kwangu. Lakini nilipomuaga si kwamba aliitika, alibaki kimya akionekana kama anatetemeka kwa hasira.

Nikiwa chumbani, nilijiinamia nikifikiri kisa hasa ambacho huenda ndicho kilichomfanya yule bibi anifukuze kwake, sikukipata haraka.
Lakini kwa kuhisi, huenda kule kukaa kwangu kwenye maombi kwenye Tv ya jirani yangu ndiko kulikomkera.

"Lakini alijuaje kama niliingia mle?" nilijiuliza.
Mara mlango uligongwa, nikaitikia kwa kusema, karibu. Aliingia yule jirani ambaye nilikuwa kwake nikiangalia Tv.

"Vipi muda huu, bado uko sawa?" aliniuliza.
"Bado naamini niko sawa moja kwa moja," nilimjibu.

"Enhe, vipi bibi kakuitia nini?" aliniuliza akikaa kitandani.

Kwa jinsi alivyonikuta nimejiinamia kwa vyovyote vile alijua niko katika hali gani.
"Aa unajua kanieleza habari ya ajabu sana."
"Kwamba?"

"Eti anataka chumba chake kesho."
"He!" yule jirani alihamaki sana.
"Ndiyo hivyo?" nilimjibu.
"Kwani kodi imekwisha?"
"Hapana, bado sana tu."
"Sasa?"

"Sijajua lakini kuna kisa tu, lazima."
Alitulia kwa muda kisha akaniangalia na kusema.
"Unajua huyu bibi anadaiwa kuwa si mtu mzuri."

"Ni mchawi?" niliuliza kwa kudakia na kukatisha mazungumzo yake.
"Ni kama hivyo, lakini sasa yeye uchawi wake si kwamba anaroga...!"
".....ila?" nilidakia kwa shauku.

"Ana mambo ya kuchezea watu nasikia. Mimi hajawahi, lakini huenda kuna damu na damu, maana kama ni kinga mimi sina kinga yoyote ile," alisema jirani yangu.

Pale pale mawazo yangu yakahamia mbali sana. Niliwaza maajabu yote yaliyokuwa yakinitokea.

"Au labda amekuona ukiingia kwangu?" yule jirani aliniuliza na kunikatisha kutoka kwenye mawazo yangu.

"Sidhani ila labda kama ulivyosema ni mtu mwenye kufanyia wenzake mambo ya ajabu ajabu, labda kama alikuwa akinifanyia mimi, sasa nilipoingia kwako na kukaa ili kusikiliza neno la Mungu ndiyo darubini yake ikamwambia," nilidhani.

"Ewaa! Itakuwa hivyo tu. Lazima hapo umepatia haswa. Yule madudu yake yamemwambia kuwa umeingia kwangu na ulikuwa ukiangalia Tv ya mahubiri, sasa hatakii," jirani yangu alisema.

"Lakini kama ni hivyo, mbona hata wewe ulikiwa unaangalia?" nilimuuliza jirani.
"Sasa mimi hajawahi kunichezea, labda wewe ujikague hajawahi kukuchezea?" aliniuliza jirani.

Pale pale nikaanza kuwaza toka siku ya kwanza nahamia pale.
"Inawezekana!" nilimjibu.
"Amewahi?"
"Nadhani, tena si mara moja wala mbili wala tatu, wala nne."
"Wala tano? Basi ni kila siku, wewe ni wake," alisema jirani yangu.

Mara mlango uligongwa, nikatoka kuangalia aliyeugonga badala ya kumwitikia karibu kama nilivyofanya kwa huyu jirani.

"Bwana mdogo lengo langu ni kukusisitizia kuhusu chumba changu, sawa?" ni yule bibi aliniambia akiwa amesimama mbele yangu.
"Sawa bibi," nilimjibu bila kusubiri majibu, nikafunga mlango kurudi ndani.
"Amesemaje?" yule jirani aliniuliza kwa shauku.

"Chumba chake tu."
"Khaa! Sasa mbona anakidai kwa mtindo wa ugomvi?" aliniuliza.

"Ndo na mimi namshangaa," nilimjibu.
Jirani yangu alisimama huku akiniuliza sasa nitafanyaje kuhusu kuhama. Je, nina sehemu ya kwenda?

Nilimjibu kuwa, nitakachokifanya ni kuhamisha vitu vyangu na kuvipeleka kwa kaka angu wa Manzese.
Yule ambaye nilifikia kwake wakati natoka Tanga.

Niliamua kutoka usiku huo huo kwenda kumjulisha mambo yote ingawa naye sikuwahi kumwambia matatizo yaliyokuwa yakinitokea siku za nyuma.

Nikiwa njiani akili yangu ikawa inasumbuka juu ya tabia ya yule bibi na yule mama jirani kule kazini.

Kwamba kati ya wao wawili nani hasa mbaya wangu. Kila kitu kilionesha ni yule mama, lakini sasa mbona yule bibi naye anakuwa kama ndiye mhusika?

Nilijiuliza mwenyewe nikielekea Manzese kwa yule kaka wa rafiki yangu ambaye na mimi nilimchukulia kama kaka yangu.
"Au labda yule bibi kwa uwezo wake mkubwa wa mambo haya alikuwa akitumia watu kunifanya nisimtambue!" nilisema kwa sauti nikiwa peke yangu.

Je, nini kiliendelea?
 
Sehemu ya 103.

Nilipofika nyumbani Manzese na kumuelezea yule kaka yangu kuhusu matatizo yaliyonipata kwa jinsi alivyoyapokea, nilianza kuhisi kuwa, huenda aliniona muongo. Huenda nilifukuzwa tu kwenye nyumba kwa matatizo ya kutolipa kodi, sasa nilikuwa nahitaji msaada wa makazi ndiyo maana nimeamua kusingizia matatizo ya kutisha.

"Kwa hiyo sasa kuhusu kutengeneza hayo majeneza umeamuaje, utaachana nayo au kwa sababu umehama kule kwa mtu uliyekuwa unamdhani ndiye mbaya wako, utaendelea?" aliniuliza tena.

"Akili zangu zinaniambia niachane kabisa na kazi ya kuchonga majeneza," nilimjibu.
"Unaweza kunipa sababu tatu za kuacha kutengeneza majeneza?" aliniuliza akinikazia macho.

Nilikaa kimya kwa muda kisha nikamwangalia na kumjibu.
"Kwanza kabisa, imenifanya niishi bila amani kwa muda mrefu sasa," nilimwambia akatingisha kichwa kuonesha kuwa anakubaliana na mimi.

"Pili, kwa sababu mambo yenyewe yana nguvu ya ushirikina, naweza kusema niendelee nikajikuta napoteza maisha hivi hivi hata kama nitakuwa nimehama kule!"
Alitingisha kichwa tena kuonesha kunielewa.
"Tatu inabidi nitulize akili kwanza kuhusu mambo ya majeneza kwani naamini ndiyo yaliyoniletea matatizo yote haya."

Yule kaka aliniangalia na kuniambia kuwa, hata yeye aliponiuliza alitaka kusikia mtazamo wangu lakini ukweli ni kwamba hakubaliani na mimi kuendelea kutengeneza majeneza.

Basi usiku huo huo tulikodisha gari na kwenda kuchukua vyombo vyangu nyumbani kwa yule bibi. Lakini mwenyewe hatukumkuta. Tuliambiwa ametoka, lakini hakuna aliyejua alikwenda wapi!
Nilimwaga yule jirani yangu niliyekuwa nikiangalia Tv kwake, naye akanitakia kila la kheri akisema kuwa, kila lililotokea ni mpango wa Mungu wa Israel.

Kwa hiyo nikawa nimehama rasmi nyumbani kwa yule bibi na kukaa kwa yule kaka yangu.
Pesa za kutafutia chumba kingine cha kuishi nilikuwa nazo, lakini niliamua kuwa, nitakuwa hapo kwa kaka yangu kwa siku kadhaa nikipumzisha akili na mwili pia.

Kesho yake asubuhi nilikwenda kazini kama kawaida. Nilifanya kazi zangu kama kawaida ingawa nilikuwa naogopa kama angetokea mtu na kusema anataka kuchongewa jeneza ingekuwaje?

Kwenye saa tisa hivi, nilimuona yule mama jirani akitokea kwa mbali huku ameshika begi kubwa mkono wa kulia na kimkoba kidogo mkono wa kushoto.
Alionekana kutabasamu huku akiniangalia kwa hamu kubwa.

Alipifika, nilimpokea begi kubwa mpaka nyumbani kwake. Aliniuliza za siku nyingi nikamjibu salama.

Lakini kwamba alisafiri mimi sijui.
Nilipomuuliza akasema aliondoka wiki mbili zilizopita kwenda Moshi.

Alipata safari ya ghafla na alishindwa kuniaga kwa sababu aliondoka asubuhi sana na mabasi ya Moshi yanayoondoka saa kumi na mbili asubuhi.

Alinichangamkia sana na kunionyesha upendo wote. Moyoni niliamini jirani huyu ndiye mwenyewe, lakini yule aliyekuwa akinifanyia visa siye, ni wa kugeza tu ili niamini ni huyu.

"Kumbe jirani yangu ulisafiri bwana," nilimwambia nikiwa siamini.
"Ee mwanangu, kakini kazi vipi, zinaendelea vizuri?" aliniuliza.

"Vizuri tu."
"Sawa," alinijibu.
Nikarudi kazini kwangu na kuendelea na kazi zangu kama kawaida.
Mpaka jioni inaingia sikuona mtu kutaka kutengenezewa jeneza wala kusema amefiwa. Wala yule mama sikumuona akija na vituko vyake. Na watu walikuwa wakiingia na kutoka kwake kama zamani.

Wengine niliokuwa nawafahamu waliingia huku wakimuuliza huju nasikia, "Kumbe umerudi?"
Jioni nilipofunga kazi, nilikwenda kumwaga mama nikamkuta yupo na wanawake watano wakisali. Walisema wanasali jumuiya, nikaaga na kuondoka zangu.
Mpaka nafika kwa kaka sikuona kituko wala maajabu.

Usiku nililala kwa amani na sharehe mpaka asubuhi iliyofuata nikaamka na kwenda kazini. Nikajua mambo yaliisha siku ile ile nilipoangalia yale mahubiri kwenye Tv.
Ndipo nilipobaini kuwa, yule bibi mwenye nyumba ndiye aliyekuwa mbaya wangu, ila alivaa sura ya watu mbali mbali akiwemo yule mama jirani ili kujificha nisimjue kama ni yeye.

Mpaka ninapoongea kwa kaka nilihama, sasa hivi naishi Mwembechai, kazi yangu ni hii hii ya useremala, lakini sichongi majeneza wala kuyahifadhi kazini kwangu.

Naogopa sana! Tena sana! Baadhi ya watu kwenye nyumba tunazoishi ni wabaya sana. Mtu unapanga kwake halafu anakufanya mbuzi wake!

Anakufunga akilini huku akikuchezea anavyotaka. Ni dhambi kubwa kwa Mungu.

MWISHO.
 
Sehemu ya 98.

Siku hiyo hiyo saa kumi na moja jioni nilikuwa nimekwenda nyumbani kwa mzee mmoja ambaye aliniita kwa ajili ya kwenda kumsaidia kurekebisha kitasa cha mlango wake.

Ili kufika nyumbani kwa yule mzee unapita jirani na nyumba ya yule mama.
Wakati natengeneza kitasa yule mzee aliniuliza kwa nini napatana sana na yule mama wakati watu wengine majirani wanamuogopa kama ukomo. Sikumjibu zaidi ya kutabasamu tu.

Wakati narudi kibandani kwangu sasa huku nikiwa peke yangu, nilipofika usawa wa nyumba ya yule mama, kwenye dirisha la chumba cha mwisho kabisa, dirisha lilikuwa wazi nikachungulia ndani ili kuona.

Ni ajabu lakini ndivyo ilivyokuwa jamani. Niliona mlima wa majeneza ndani ya chumba hicho kilichokuwa na mwanga hafifu sana.

Niliganda kwa muda nikikodolea macho kuangalia ndani zaidi. Kila kona ya chumba hicho hicho majeneza yalikuwa yamesimamishwa kwa kubebanishwa kila moja juu baada ya jingine.

"Mungu wangu," nilisema kwa mshangao baada ya kuona yale majeneza.
"Unashangaa nini! Mwanaharamu wewe," sauti iliniambia bila kumwona aliyekuwa akisema.

Nikaondoka haraka sana.
Nilitembea huku nikijaribu kuikumbuka ile sauti kama inaweza kuwa ya mtu ninayemfahamu. Lakini sivyo. Haikuwa ya yule mama wala ya mwanamke mwingine ninayemfahamu.

Nilifika kibandani kwangu huku nikijishika mdomo kwa kuendelea kushangazwa na tukio lile. Niliweza kuyakumbuka karibu majeneza matano kati ya yote niliyoyaona kwamba, niliyatengeneza mimi.

Mfano hata lile lililochukuliwa siku hiyo hiyo na wale watu lilikuwa juu zaidi ya mengine kwenye ukuta wa mbele kabisa wa chumba kile.

"Huyu mama ana matatizo gani! Ina maana majeneza yoote yale namtengenezea yeye au? Mbona yapo mle kwake?" nilijisemea moyoni huku nikiangalia nyumbani kwa yule mama.

"Ulikuwa una shida gani kijana?" yule mama aliniuliza akitoka nyumbani kwake akija kwangu. Sura yake ilionekana kukasirika kupita kawaida.

"Hapana mama angu nilikwenda kutengeneza kitasa cha mlango hapo nyumba ya jirani," nilimjibu huku nikitetemeka mwili mzima kwa woga.

Tangu nilipoanza kumfahamu huyu mama, sikuwahi kumwona yule mama jirani akiwa amekasirika kama siku hiyo. Na sidhani kama itakuja kutokea tena siku kama ile.
"Unanidanganya hata mimi siyo. Unanijua vizuri wewe?" aliniuliza kwa sauti ya ukali sana.

Macho yake yalianza kubadilika rangi na kuwa mekundu kama yaliyojaa damu. Halafu alionekana kwamba kama angekuwa na silaha yoyote ile angenitwanga nayo. Hata kama ni jembe la kulimia kwani alikuwa akisema huku akiangaza huku na kule kama anayetafuta kitu cha kunipigia.

"Hapana mama. Kweli kabisa hata ukienda nyumbani kwa yule mzee watakuambia kwamba nilikuwa pale nikitengeneza kitasa cha mlango," nilisema kwa sauti ya kuomba huruma.

Nguvu ziliniishia kabisa baada ya kugundua kuwa, yule mama amebadilika sura siku hiyo kuliko siku yoyote ile nyuma ambazo niliwahi kumwona.

Hakuwa rafiki ingawa wa mashaka kama zamani. Alinigeukia kabisa.
"Twende nyumbani kwangu haraka sana," aliniambia akiwa amesimama mbele yangu huku amenishikia kiuno kama vile alikuwa akisutana na mimi.

Mambo ambayo sikuyazoea mimi katika makuzi yangu.

"Sawa mama," nilimkubalia huku nikianza kutembea. Na yeye alianza kutembea kuelekea nyumbani kwake lakini huku kila baada ya hatua mbili anageuka nyuma kuniangalia kama naendelea kumfuata.
Alipopandisha ngazi za nyumbani kwake, mimi pia nilipandisha licha ya kwamba aligeuka kuniangalia kama bado niko nyuma yake.

"Ingia ndani," aliniambia kwa amri.
Nilihisi kutaka kujisaidia haja ndogo pale pale, lakini nikaibana.

Je, nini kiliendelea?
Tukutane kesho...
Huyu mama hela za kununulia majeneza anazipata wapi,isijekuwa anauhujumu uchumi
 
Sehemu ya 103.

Nilipofika nyumbani Manzese na kumuelezea yule kaka yangu kuhusu matatizo yaliyonipata kwa jinsi alivyoyapokea, nilianza kuhisi kuwa, huenda aliniona muongo. Huenda nilifukuzwa tu kwenye nyumba kwa matatizo ya kutolipa kodi, sasa nilikuwa nahitaji msaada wa makazi ndiyo maana nimeamua kusingizia matatizo ya kutisha.

"Kwa hiyo sasa kuhusu kutengeneza hayo majeneza umeamuaje, utaachana nayo au kwa sababu umehama kule kwa mtu uliyekuwa unamdhani ndiye mbaya wako, utaendelea?" aliniuliza tena.

"Akili zangu zinaniambia niachane kabisa na kazi ya kuchonga majeneza," nilimjibu.
"Unaweza kunipa sababu tatu za kuacha kutengeneza majeneza?" aliniuliza akinikazia macho.

Nilikaa kimya kwa muda kisha nikamwangalia na kumjibu.
"Kwanza kabisa, imenifanya niishi bila amani kwa muda mrefu sasa," nilimwambia akatingisha kichwa kuonesha kuwa anakubaliana na mimi.

"Pili, kwa sababu mambo yenyewe yana nguvu ya ushirikina, naweza kusema niendelee nikajikuta napoteza maisha hivi hivi hata kama nitakuwa nimehama kule!"
Alitingisha kichwa tena kuonesha kunielewa.
"Tatu inabidi nitulize akili kwanza kuhusu mambo ya majeneza kwani naamini ndiyo yaliyoniletea matatizo yote haya."

Yule kaka aliniangalia na kuniambia kuwa, hata yeye aliponiuliza alitaka kusikia mtazamo wangu lakini ukweli ni kwamba hakubaliani na mimi kuendelea kutengeneza majeneza.

Basi usiku huo huo tulikodisha gari na kwenda kuchukua vyombo vyangu nyumbani kwa yule bibi. Lakini mwenyewe hatukumkuta. Tuliambiwa ametoka, lakini hakuna aliyejua alikwenda wapi!
Nilimwaga yule jirani yangu niliyekuwa nikiangalia Tv kwake, naye akanitakia kila la kheri akisema kuwa, kila lililotokea ni mpango wa Mungu wa Israel.

Kwa hiyo nikawa nimehama rasmi nyumbani kwa yule bibi na kukaa kwa yule kaka yangu.
Pesa za kutafutia chumba kingine cha kuishi nilikuwa nazo, lakini niliamua kuwa, nitakuwa hapo kwa kaka yangu kwa siku kadhaa nikipumzisha akili na mwili pia.

Kesho yake asubuhi nilikwenda kazini kama kawaida. Nilifanya kazi zangu kama kawaida ingawa nilikuwa naogopa kama angetokea mtu na kusema anataka kuchongewa jeneza ingekuwaje?

Kwenye saa tisa hivi, nilimuona yule mama jirani akitokea kwa mbali huku ameshika begi kubwa mkono wa kulia na kimkoba kidogo mkono wa kushoto.
Alionekana kutabasamu huku akiniangalia kwa hamu kubwa.

Alipifika, nilimpokea begi kubwa mpaka nyumbani kwake. Aliniuliza za siku nyingi nikamjibu salama.

Lakini kwamba alisafiri mimi sijui.
Nilipomuuliza akasema aliondoka wiki mbili zilizopita kwenda Moshi.

Alipata safari ya ghafla na alishindwa kuniaga kwa sababu aliondoka asubuhi sana na mabasi ya Moshi yanayoondoka saa kumi na mbili asubuhi.

Alinichangamkia sana na kunionyesha upendo wote. Moyoni niliamini jirani huyu ndiye mwenyewe, lakini yule aliyekuwa akinifanyia visa siye, ni wa kugeza tu ili niamini ni huyu.

"Kumbe jirani yangu ulisafiri bwana," nilimwambia nikiwa siamini.
"Ee mwanangu, kakini kazi vipi, zinaendelea vizuri?" aliniuliza.

"Vizuri tu."
"Sawa," alinijibu.
Nikarudi kazini kwangu na kuendelea na kazi zangu kama kawaida.
Mpaka jioni inaingia sikuona mtu kutaka kutengenezewa jeneza wala kusema amefiwa. Wala yule mama sikumuona akija na vituko vyake. Na watu walikuwa wakiingia na kutoka kwake kama zamani.

Wengine niliokuwa nawafahamu waliingia huku wakimuuliza huju nasikia, "Kumbe umerudi?"
Jioni nilipofunga kazi, nilikwenda kumwaga mama nikamkuta yupo na wanawake watano wakisali. Walisema wanasali jumuiya, nikaaga na kuondoka zangu.
Mpaka nafika kwa kaka sikuona kituko wala maajabu.

Usiku nililala kwa amani na sharehe mpaka asubuhi iliyofuata nikaamka na kwenda kazini. Nikajua mambo yaliisha siku ile ile nilipoangalia yale mahubiri kwenye Tv.
Ndipo nilipobaini kuwa, yule bibi mwenye nyumba ndiye aliyekuwa mbaya wangu, ila alivaa sura ya watu mbali mbali akiwemo yule mama jirani ili kujificha nisimjue kama ni yeye.

Mpaka ninapoongea kwa kaka nilihama, sasa hivi naishi Mwembechai, kazi yangu ni hii hii ya useremala, lakini sichongi majeneza wala kuyahifadhi kazini kwangu.

Naogopa sana! Tena sana! Baadhi ya watu kwenye nyumba tunazoishi ni wabaya sana. Mtu unapanga kwake halafu anakufanya mbuzi wake!

Anakufunga akilini huku akikuchezea anavyotaka. Ni dhambi kubwa kwa Mungu.

MWISHO.
Woyooo babe me love u
 
Kwa mara ya kwanza nimesoma story bampa to bampa hongera mleta story,
Sio wengine wanaringa mpaka wanafikia hatua wanaomba pesa bila ya aibu.
 
Sehemu ya 103.

Nilipofika nyumbani Manzese na kumuelezea yule kaka yangu kuhusu matatizo yaliyonipata kwa jinsi alivyoyapokea, nilianza kuhisi kuwa, huenda aliniona muongo. Huenda nilifukuzwa tu kwenye nyumba kwa matatizo ya kutolipa kodi, sasa nilikuwa nahitaji msaada wa makazi ndiyo maana nimeamua kusingizia matatizo ya kutisha.

"Kwa hiyo sasa kuhusu kutengeneza hayo majeneza umeamuaje, utaachana nayo au kwa sababu umehama kule kwa mtu uliyekuwa unamdhani ndiye mbaya wako, utaendelea?" aliniuliza tena.

"Akili zangu zinaniambia niachane kabisa na kazi ya kuchonga majeneza," nilimjibu.
"Unaweza kunipa sababu tatu za kuacha kutengeneza majeneza?" aliniuliza akinikazia macho.

Nilikaa kimya kwa muda kisha nikamwangalia na kumjibu.
"Kwanza kabisa, imenifanya niishi bila amani kwa muda mrefu sasa," nilimwambia akatingisha kichwa kuonesha kuwa anakubaliana na mimi.

"Pili, kwa sababu mambo yenyewe yana nguvu ya ushirikina, naweza kusema niendelee nikajikuta napoteza maisha hivi hivi hata kama nitakuwa nimehama kule!"
Alitingisha kichwa tena kuonesha kunielewa.
"Tatu inabidi nitulize akili kwanza kuhusu mambo ya majeneza kwani naamini ndiyo yaliyoniletea matatizo yote haya."

Yule kaka aliniangalia na kuniambia kuwa, hata yeye aliponiuliza alitaka kusikia mtazamo wangu lakini ukweli ni kwamba hakubaliani na mimi kuendelea kutengeneza majeneza.

Basi usiku huo huo tulikodisha gari na kwenda kuchukua vyombo vyangu nyumbani kwa yule bibi. Lakini mwenyewe hatukumkuta. Tuliambiwa ametoka, lakini hakuna aliyejua alikwenda wapi!
Nilimwaga yule jirani yangu niliyekuwa nikiangalia Tv kwake, naye akanitakia kila la kheri akisema kuwa, kila lililotokea ni mpango wa Mungu wa Israel.

Kwa hiyo nikawa nimehama rasmi nyumbani kwa yule bibi na kukaa kwa yule kaka yangu.
Pesa za kutafutia chumba kingine cha kuishi nilikuwa nazo, lakini niliamua kuwa, nitakuwa hapo kwa kaka yangu kwa siku kadhaa nikipumzisha akili na mwili pia.

Kesho yake asubuhi nilikwenda kazini kama kawaida. Nilifanya kazi zangu kama kawaida ingawa nilikuwa naogopa kama angetokea mtu na kusema anataka kuchongewa jeneza ingekuwaje?

Kwenye saa tisa hivi, nilimuona yule mama jirani akitokea kwa mbali huku ameshika begi kubwa mkono wa kulia na kimkoba kidogo mkono wa kushoto.
Alionekana kutabasamu huku akiniangalia kwa hamu kubwa.

Alipifika, nilimpokea begi kubwa mpaka nyumbani kwake. Aliniuliza za siku nyingi nikamjibu salama.

Lakini kwamba alisafiri mimi sijui.
Nilipomuuliza akasema aliondoka wiki mbili zilizopita kwenda Moshi.

Alipata safari ya ghafla na alishindwa kuniaga kwa sababu aliondoka asubuhi sana na mabasi ya Moshi yanayoondoka saa kumi na mbili asubuhi.

Alinichangamkia sana na kunionyesha upendo wote. Moyoni niliamini jirani huyu ndiye mwenyewe, lakini yule aliyekuwa akinifanyia visa siye, ni wa kugeza tu ili niamini ni huyu.

"Kumbe jirani yangu ulisafiri bwana," nilimwambia nikiwa siamini.
"Ee mwanangu, kakini kazi vipi, zinaendelea vizuri?" aliniuliza.

"Vizuri tu."
"Sawa," alinijibu.
Nikarudi kazini kwangu na kuendelea na kazi zangu kama kawaida.
Mpaka jioni inaingia sikuona mtu kutaka kutengenezewa jeneza wala kusema amefiwa. Wala yule mama sikumuona akija na vituko vyake. Na watu walikuwa wakiingia na kutoka kwake kama zamani.

Wengine niliokuwa nawafahamu waliingia huku wakimuuliza huju nasikia, "Kumbe umerudi?"
Jioni nilipofunga kazi, nilikwenda kumwaga mama nikamkuta yupo na wanawake watano wakisali. Walisema wanasali jumuiya, nikaaga na kuondoka zangu.
Mpaka nafika kwa kaka sikuona kituko wala maajabu.

Usiku nililala kwa amani na sharehe mpaka asubuhi iliyofuata nikaamka na kwenda kazini. Nikajua mambo yaliisha siku ile ile nilipoangalia yale mahubiri kwenye Tv.
Ndipo nilipobaini kuwa, yule bibi mwenye nyumba ndiye aliyekuwa mbaya wangu, ila alivaa sura ya watu mbali mbali akiwemo yule mama jirani ili kujificha nisimjue kama ni yeye.

Mpaka ninapoongea kwa kaka nilihama, sasa hivi naishi Mwembechai, kazi yangu ni hii hii ya useremala, lakini sichongi majeneza wala kuyahifadhi kazini kwangu.

Naogopa sana! Tena sana! Baadhi ya watu kwenye nyumba tunazoishi ni wabaya sana. Mtu unapanga kwake halafu anakufanya mbuzi wake!

Anakufunga akilini huku akikuchezea anavyotaka. Ni dhambi kubwa kwa Mungu.

MWISHO.

Mwisho mzuri
Asante kwa simulizi nzuri ingawa inaogopesha sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom