Simulizi: Kazi ya Kutengeneza Majeneza

Sehemu ya 97

Nilibaki nimezubaa nikiwaangalia Wale watu bila ya kusema chochote kwani tayari moyo wangu mpaka wakati huo ulishakufa ganzi kutokana na maajabu yaliyokuwa yakiendelea kunitokea.

Ghafla, yule mama wa jirani aliaga na kuondoka zake huku akidai kuwa, alibandika chungu cha mboga muda mrefu anachelewa inaweza kuungua au hata kukauka ndani ya chungu.

Wakati anaongea hivyo alikuwa hatua kadhaa mbele akiondoka zake. Nilimsindikiza kwa macho halafu nilipoacha kumwangalia niliwageukia wale watu ambao bado walikuwa wamesimama wakiniangalia kwa shauku ya kusikia nitakachoongea baada ya kuacha kumwangalia yule mama jirani.

"Hivi si mmefuata jeneza lenu?" niliwauliza nikiwasoma sura.
"Ndiyo jeneza letu! Unajua jana tulishindwa kupata usafiri," alijibu mmoja kati ya wale wenye kanzu.

"Kwani jana hamkuja kulichukua?" niliwauliza kwa kuwatega.
"Atupe nani?" yule yule mmoja alinijibu kwa sauti ya uhakika zaidi kuliko mwanzoni.
Niliguna kidogo kisha nikajibalaguza ili nisije kuonekana kuna kitu juu ya jeneza lao hilo ambalo wamelifuatilia.

Wakati huo huo wazo la faraja lilinijia kwamba huenda yakatokea maajabu kama ilivyokuwa kwa wale wanajeshi, kwamba jeneza lilikuwepo ndani huku mimi nje nikipata homa ya bure tu.
"Nisubirini kidogo," niliwajibu nikiwa naingia bandani kwangu.

Hali niliyoikuta ni ile ile! Jeneza la watu sikulikuta. Nilihisi jasho jembamba sana likinitoka mwilini, maswali kibao yalinijaa kichwani, likiwemo la kwamba nitawajibu nini wale watu wafiwa?

"Bwana fundi tunashukuru sana bwana," sauti ya mmoja wao iliniambia kwa kutokea nje. Sikujua wanashukuru nini?

Wanashukuru kwa kugundua wamelipoteza jeneza lao au wanashukuru wamelipata?
Wakati natoka nje nikawajibu ukweli, ghafla nikahisi mikono inaniuma kama vile nimetoka kubeba kitu kizito sana muda mfupi uliopita.

Kufika nje, niliwakuta wale watu wanabeba lile jeneza kwa kusaidiana kila pembe.
Nilitoa macho kuwaangalia nao wakionekana kuelemewa nalo.
Walilitoa wapi, sijui.

Nilijiangalia mikono na kugundua kuwa, ilikuwa na vumbi vumbi, halafu tena ilionekana imekuwa myekundu sana kutokana na damu kukandamizwa na kitu nilichobeba au kushika.

Palepale nikagundua kuwa kwa vyovyote vile hali niliyojisikia nayo ilitokana na kulibeba lile jeneza.

Niligundua pia kwamba, lile jeneza lilikuwa ndani ila kutokana na hali ya miujiza ndiyo maana sikuliona.

Lakini kitu cha ajabu ambacho kilisigua akili yangu ni kitendo cha yule mama wa jirani kuondoka kwa haraka wakati wale wafiwa wamefika kulifuata jeneza lao.

Kwa nini asisubiri au kwa nini asiwaulize imekuaje wamefuata jeneza lao wakati jana yake usiku walimfuata yeye, akawajibu mimi nilishaondoka na wao wakamwambia wananifuata nyumbani ili niende kuwatolea!
Sasa iweje aondoke?

Hili lilinishangaza sana tena liliniogopesha zaidi ya kunishangaza. Wale watu walivyopotea tu machoni kwangu, yule mama jirani alitoka nje kwake na kusimama kwenye ngazi.

"Wamekwenda?" aliniuliza kwa mbali yule mama.

"Akina nani?" nami nilimjibu kwa mbali hivyo hivyo.
"Si wale wateja wako," alisema.
"Wamekwenda," alirudi ndani haraka sana.

Je, nini kiliendelea?
 
Sehemu ya 98.

Siku hiyo hiyo saa kumi na moja jioni nilikuwa nimekwenda nyumbani kwa mzee mmoja ambaye aliniita kwa ajili ya kwenda kumsaidia kurekebisha kitasa cha mlango wake.

Ili kufika nyumbani kwa yule mzee unapita jirani na nyumba ya yule mama.
Wakati natengeneza kitasa yule mzee aliniuliza kwa nini napatana sana na yule mama wakati watu wengine majirani wanamuogopa kama ukomo. Sikumjibu zaidi ya kutabasamu tu.

Wakati narudi kibandani kwangu sasa huku nikiwa peke yangu, nilipofika usawa wa nyumba ya yule mama, kwenye dirisha la chumba cha mwisho kabisa, dirisha lilikuwa wazi nikachungulia ndani ili kuona.

Ni ajabu lakini ndivyo ilivyokuwa jamani. Niliona mlima wa majeneza ndani ya chumba hicho kilichokuwa na mwanga hafifu sana.

Niliganda kwa muda nikikodolea macho kuangalia ndani zaidi. Kila kona ya chumba hicho hicho majeneza yalikuwa yamesimamishwa kwa kubebanishwa kila moja juu baada ya jingine.

"Mungu wangu," nilisema kwa mshangao baada ya kuona yale majeneza.
"Unashangaa nini! Mwanaharamu wewe," sauti iliniambia bila kumwona aliyekuwa akisema.

Nikaondoka haraka sana.
Nilitembea huku nikijaribu kuikumbuka ile sauti kama inaweza kuwa ya mtu ninayemfahamu. Lakini sivyo. Haikuwa ya yule mama wala ya mwanamke mwingine ninayemfahamu.

Nilifika kibandani kwangu huku nikijishika mdomo kwa kuendelea kushangazwa na tukio lile. Niliweza kuyakumbuka karibu majeneza matano kati ya yote niliyoyaona kwamba, niliyatengeneza mimi.

Mfano hata lile lililochukuliwa siku hiyo hiyo na wale watu lilikuwa juu zaidi ya mengine kwenye ukuta wa mbele kabisa wa chumba kile.

"Huyu mama ana matatizo gani! Ina maana majeneza yoote yale namtengenezea yeye au? Mbona yapo mle kwake?" nilijisemea moyoni huku nikiangalia nyumbani kwa yule mama.

"Ulikuwa una shida gani kijana?" yule mama aliniuliza akitoka nyumbani kwake akija kwangu. Sura yake ilionekana kukasirika kupita kawaida.

"Hapana mama angu nilikwenda kutengeneza kitasa cha mlango hapo nyumba ya jirani," nilimjibu huku nikitetemeka mwili mzima kwa woga.

Tangu nilipoanza kumfahamu huyu mama, sikuwahi kumwona yule mama jirani akiwa amekasirika kama siku hiyo. Na sidhani kama itakuja kutokea tena siku kama ile.
"Unanidanganya hata mimi siyo. Unanijua vizuri wewe?" aliniuliza kwa sauti ya ukali sana.

Macho yake yalianza kubadilika rangi na kuwa mekundu kama yaliyojaa damu. Halafu alionekana kwamba kama angekuwa na silaha yoyote ile angenitwanga nayo. Hata kama ni jembe la kulimia kwani alikuwa akisema huku akiangaza huku na kule kama anayetafuta kitu cha kunipigia.

"Hapana mama. Kweli kabisa hata ukienda nyumbani kwa yule mzee watakuambia kwamba nilikuwa pale nikitengeneza kitasa cha mlango," nilisema kwa sauti ya kuomba huruma.

Nguvu ziliniishia kabisa baada ya kugundua kuwa, yule mama amebadilika sura siku hiyo kuliko siku yoyote ile nyuma ambazo niliwahi kumwona.

Hakuwa rafiki ingawa wa mashaka kama zamani. Alinigeukia kabisa.
"Twende nyumbani kwangu haraka sana," aliniambia akiwa amesimama mbele yangu huku amenishikia kiuno kama vile alikuwa akisutana na mimi.

Mambo ambayo sikuyazoea mimi katika makuzi yangu.

"Sawa mama," nilimkubalia huku nikianza kutembea. Na yeye alianza kutembea kuelekea nyumbani kwake lakini huku kila baada ya hatua mbili anageuka nyuma kuniangalia kama naendelea kumfuata.
Alipopandisha ngazi za nyumbani kwake, mimi pia nilipandisha licha ya kwamba aligeuka kuniangalia kama bado niko nyuma yake.

"Ingia ndani," aliniambia kwa amri.
Nilihisi kutaka kujisaidia haja ndogo pale pale, lakini nikaibana.

Je, nini kiliendelea?
Tukutane kesho...
 
Sehemu ya 98.

Siku hiyo hiyo saa kumi na moja jioni nilikuwa nimekwenda nyumbani kwa mzee mmoja ambaye aliniita kwa ajili ya kwenda kumsaidia kurekebisha kitasa cha mlango wake.

Ili kufika nyumbani kwa yule mzee unapita jirani na nyumba ya yule mama.
Wakati natengeneza kitasa yule mzee aliniuliza kwa nini napatana sana na yule mama wakati watu wengine majirani wanamuogopa kama ukomo. Sikumjibu zaidi ya kutabasamu tu.

Wakati narudi kibandani kwangu sasa huku nikiwa peke yangu, nilipofika usawa wa nyumba ya yule mama, kwenye dirisha la chumba cha mwisho kabisa, dirisha lilikuwa wazi nikachungulia ndani ili kuona.

Ni ajabu lakini ndivyo ilivyokuwa jamani. Niliona mlima wa majeneza ndani ya chumba hicho kilichokuwa na mwanga hafifu sana.

Niliganda kwa muda nikikodolea macho kuangalia ndani zaidi. Kila kona ya chumba hicho hicho majeneza yalikuwa yamesimamishwa kwa kubebanishwa kila moja juu baada ya jingine.

"Mungu wangu," nilisema kwa mshangao baada ya kuona yale majeneza.
"Unashangaa nini! Mwanaharamu wewe," sauti iliniambia bila kumwona aliyekuwa akisema.

Nikaondoka haraka sana.
Nilitembea huku nikijaribu kuikumbuka ile sauti kama inaweza kuwa ya mtu ninayemfahamu. Lakini sivyo. Haikuwa ya yule mama wala ya mwanamke mwingine ninayemfahamu.

Nilifika kibandani kwangu huku nikijishika mdomo kwa kuendelea kushangazwa na tukio lile. Niliweza kuyakumbuka karibu majeneza matano kati ya yote niliyoyaona kwamba, niliyatengeneza mimi.

Mfano hata lile lililochukuliwa siku hiyo hiyo na wale watu lilikuwa juu zaidi ya mengine kwenye ukuta wa mbele kabisa wa chumba kile.

"Huyu mama ana matatizo gani! Ina maana majeneza yoote yale namtengenezea yeye au? Mbona yapo mle kwake?" nilijisemea moyoni huku nikiangalia nyumbani kwa yule mama.

"Ulikuwa una shida gani kijana?" yule mama aliniuliza akitoka nyumbani kwake akija kwangu. Sura yake ilionekana kukasirika kupita kawaida.

"Hapana mama angu nilikwenda kutengeneza kitasa cha mlango hapo nyumba ya jirani," nilimjibu huku nikitetemeka mwili mzima kwa woga.

Tangu nilipoanza kumfahamu huyu mama, sikuwahi kumwona yule mama jirani akiwa amekasirika kama siku hiyo. Na sidhani kama itakuja kutokea tena siku kama ile.
"Unanidanganya hata mimi siyo. Unanijua vizuri wewe?" aliniuliza kwa sauti ya ukali sana.

Macho yake yalianza kubadilika rangi na kuwa mekundu kama yaliyojaa damu. Halafu alionekana kwamba kama angekuwa na silaha yoyote ile angenitwanga nayo. Hata kama ni jembe la kulimia kwani alikuwa akisema huku akiangaza huku na kule kama anayetafuta kitu cha kunipigia.

"Hapana mama. Kweli kabisa hata ukienda nyumbani kwa yule mzee watakuambia kwamba nilikuwa pale nikitengeneza kitasa cha mlango," nilisema kwa sauti ya kuomba huruma.

Nguvu ziliniishia kabisa baada ya kugundua kuwa, yule mama amebadilika sura siku hiyo kuliko siku yoyote ile nyuma ambazo niliwahi kumwona.

Hakuwa rafiki ingawa wa mashaka kama zamani. Alinigeukia kabisa.
"Twende nyumbani kwangu haraka sana," aliniambia akiwa amesimama mbele yangu huku amenishikia kiuno kama vile alikuwa akisutana na mimi.

Mambo ambayo sikuyazoea mimi katika makuzi yangu.

"Sawa mama," nilimkubalia huku nikianza kutembea. Na yeye alianza kutembea kuelekea nyumbani kwake lakini huku kila baada ya hatua mbili anageuka nyuma kuniangalia kama naendelea kumfuata.
Alipopandisha ngazi za nyumbani kwake, mimi pia nilipandisha licha ya kwamba aligeuka kuniangalia kama bado niko nyuma yake.

"Ingia ndani," aliniambia kwa amri.
Nilihisi kutaka kujisaidia haja ndogo pale pale, lakini nikaibana.

Je, nini kiliendelea?
Tukutane kesho...
Kesho tena Shunie
Mbona nitateseka!!!!

Asanteh kwa utamu huu
 
Sehemu ya 98.

Siku hiyo hiyo saa kumi na moja jioni nilikuwa nimekwenda nyumbani kwa mzee mmoja ambaye aliniita kwa ajili ya kwenda kumsaidia kurekebisha kitasa cha mlango wake.

Ili kufika nyumbani kwa yule mzee unapita jirani na nyumba ya yule mama.
Wakati natengeneza kitasa yule mzee aliniuliza kwa nini napatana sana na yule mama wakati watu wengine majirani wanamuogopa kama ukomo. Sikumjibu zaidi ya kutabasamu tu.

Wakati narudi kibandani kwangu sasa huku nikiwa peke yangu, nilipofika usawa wa nyumba ya yule mama, kwenye dirisha la chumba cha mwisho kabisa, dirisha lilikuwa wazi nikachungulia ndani ili kuona.

Ni ajabu lakini ndivyo ilivyokuwa jamani. Niliona mlima wa majeneza ndani ya chumba hicho kilichokuwa na mwanga hafifu sana.

Niliganda kwa muda nikikodolea macho kuangalia ndani zaidi. Kila kona ya chumba hicho hicho majeneza yalikuwa yamesimamishwa kwa kubebanishwa kila moja juu baada ya jingine.

"Mungu wangu," nilisema kwa mshangao baada ya kuona yale majeneza.
"Unashangaa nini! Mwanaharamu wewe," sauti iliniambia bila kumwona aliyekuwa akisema.

Nikaondoka haraka sana.
Nilitembea huku nikijaribu kuikumbuka ile sauti kama inaweza kuwa ya mtu ninayemfahamu. Lakini sivyo. Haikuwa ya yule mama wala ya mwanamke mwingine ninayemfahamu.

Nilifika kibandani kwangu huku nikijishika mdomo kwa kuendelea kushangazwa na tukio lile. Niliweza kuyakumbuka karibu majeneza matano kati ya yote niliyoyaona kwamba, niliyatengeneza mimi.

Mfano hata lile lililochukuliwa siku hiyo hiyo na wale watu lilikuwa juu zaidi ya mengine kwenye ukuta wa mbele kabisa wa chumba kile.

"Huyu mama ana matatizo gani! Ina maana majeneza yoote yale namtengenezea yeye au? Mbona yapo mle kwake?" nilijisemea moyoni huku nikiangalia nyumbani kwa yule mama.

"Ulikuwa una shida gani kijana?" yule mama aliniuliza akitoka nyumbani kwake akija kwangu. Sura yake ilionekana kukasirika kupita kawaida.

"Hapana mama angu nilikwenda kutengeneza kitasa cha mlango hapo nyumba ya jirani," nilimjibu huku nikitetemeka mwili mzima kwa woga.

Tangu nilipoanza kumfahamu huyu mama, sikuwahi kumwona yule mama jirani akiwa amekasirika kama siku hiyo. Na sidhani kama itakuja kutokea tena siku kama ile.
"Unanidanganya hata mimi siyo. Unanijua vizuri wewe?" aliniuliza kwa sauti ya ukali sana.

Macho yake yalianza kubadilika rangi na kuwa mekundu kama yaliyojaa damu. Halafu alionekana kwamba kama angekuwa na silaha yoyote ile angenitwanga nayo. Hata kama ni jembe la kulimia kwani alikuwa akisema huku akiangaza huku na kule kama anayetafuta kitu cha kunipigia.

"Hapana mama. Kweli kabisa hata ukienda nyumbani kwa yule mzee watakuambia kwamba nilikuwa pale nikitengeneza kitasa cha mlango," nilisema kwa sauti ya kuomba huruma.

Nguvu ziliniishia kabisa baada ya kugundua kuwa, yule mama amebadilika sura siku hiyo kuliko siku yoyote ile nyuma ambazo niliwahi kumwona.

Hakuwa rafiki ingawa wa mashaka kama zamani. Alinigeukia kabisa.
"Twende nyumbani kwangu haraka sana," aliniambia akiwa amesimama mbele yangu huku amenishikia kiuno kama vile alikuwa akisutana na mimi.

Mambo ambayo sikuyazoea mimi katika makuzi yangu.

"Sawa mama," nilimkubalia huku nikianza kutembea. Na yeye alianza kutembea kuelekea nyumbani kwake lakini huku kila baada ya hatua mbili anageuka nyuma kuniangalia kama naendelea kumfuata.
Alipopandisha ngazi za nyumbani kwake, mimi pia nilipandisha licha ya kwamba aligeuka kuniangalia kama bado niko nyuma yake.

"Ingia ndani," aliniambia kwa amri.
Nilihisi kutaka kujisaidia haja ndogo pale pale, lakini nikaibana.

Je, nini kiliendelea?
Tukutane kesho...
Hivi kesho??????
 
Inaogopesha mno
Umenikumbusha mchezaji Vincent Price alikuwa anapenda kuigiza kama Dracula, niliwahi kumsikia alikuwa hapendi kuangalia filam zake kwa vile zilikuwa zinatisha na hata alikuwa akiwashauri wanawe eti wasiangalie.
 
Sehemu ya 99.

Niliingia huku nikitetemeka sasa kwani akili zangu zilianza kuniambia kuwa, kuna uwezekano mkubwa nakwenda kutolewa uhai na huyu mama kwa sababu ya kukasirika baada ya kugundua nilichungulia ndani kwake na kuona majeneza yaliyorundikana.

"Pita huku," aliniambia yule mama huku akifungua mlango ambao nilibaini haraka sana kuwa ni wa kuingilia chumbani. Lakini usawa wa chumba hicho si kile chenye chumba nilichoona majeneza. Moyoni nilijiambia tutaona huko huko.

Nilipozama ndani ya chumba hicho huku na yeye akiwa ndani kabisa, alinigeukia na kuniuliza.

"Unataka nikuoneshe nini katika mambo unayoyahitaji?"
Sikuwa na jibu lolote kwani sikujua alikuwa na lengo gani.

"Nakuuliza wewe unataka nikuoneshe nini?" alinifokea huku akinikaba koo kwa hasira.
"Hee! Yamefikia huko mama?" nilimuuliza.
"Nani mama yako? Nani mama yako?" aliniuliza kwa ukali ule ule. Macho yake yalitoka na kuwa makubwa kuliko kawaida.
"Basi samahani sana. Nioneshe chochote utakacho," nilimjibu huku nikijaribu kujitetea kujiondoa kutoka kwenye kule kunishika koo kwa nguvu.
"Ona," aliniambia akiwa bado amenishika.
Sikujua nione wapi, kwa hiyo nikawa namshangaa.

"Nimekwambia ona," alisema kwa sauti zaidi. Safari hii akinyoosha kidole kwenye mguu. Nikaona sehemu iliyopona kidonda (jeraha)
Haraka sana, akili yangu ilikumbuka kuwa mguu huo ndiyo ule niliouona nyumbani kwangu usiku mpaka nikashangaa sana.
"Umeona?" aliniuliza.

"Nimeona mama," nilimjibu.
"Njoo huku," aliniita akienda mbele.
Hapo alikuwa ameniachia kule kunishika.
Nilimfuata nyuma nyuma, yeye akikatisha vyumba. Nilishangaa kuiona ile nyumba kwamba, kumbe ni kubwa kiasi kile. Lakini kwa nje haioneshi kama kubwa.

"Ingia," aliniambia huku yeye akifungua mlango kuingia kwenye chumba kimoja ambacho mlango wake ulikuwa na mchoro wa kichwa cha mtu kisichokuwa na nyama (fuvu)

"Angalia humu ndani hadi uchoke, si wakati ule uliangalia kwa kuiba," aliniambia akinipisha niingie vizuri ndani ya chumba kile

Sikutaka kumbishia chochote kile, niliangalia kama alivyotaka. Sikuona kitu chochote.
Nilipogeuza shingo kumwangalia, akaniuliza.
"Umeona nini?"

"Sijaona kitu chochote kile," nilimjibu.
Kufumba na kufumbua mimi na yeye tulikuwa nje ya kibanda changu. Mimi nikiwa napiga nyundo kwenye msumari, yeye amesimama akiwa ameshika kiuno.
"Ukitaka kujua ubaya wangu endelea na tabia hii ya kukagua kagua mambo yangu. Mimi sitaki kabisa, kweli nakwambia bwana," alisema kwa ukali yule mama jirani akiniambia mimi.

"Unakuja kwangu halafu unachungulia, unachungulia nini?" aliendelea kusema.
"Siku zile hivyo hivyo ukaniuliza eti kama nyumbani kwangu naishi na kijana, ule ni upekepeke nisioutaka," alikazana kusema yule mama wa jirani.

Nilishangaa kuona tupo pale tena kwa ghafla, lakini sikusema kitu zaidi ya kumsikiliza tu na kuendelea kumshangaa sana.

Kwa upande mwingine unaweza kusema mpaka pale nilikuwa nimeshapata majibu, kuwa yule mama ndiye mbaya wangu wa siku zote. Ndiye yeye aliyekuwa akinifanyia maajabu yote yale.

Nilikumbuka na ule mguu alionilazimisha kuuangalia na kukuta una lile kovu. Ndiyo kabisa nikawa nimemjua yeye ndiye mbaya wangu.

Kitu kingine ambacho naamini kabisa mpaka leo kwamba ndicho kilichokuwa kikinifanya niendelee kuteseka kwa muda mrefu ni kuwa, inaonekana licha ya kunifanyia mabaya yake, pia alikuwa amenichezea ili kunifunga kinywa nisiseme kwa mtu wala nisiwe na wazo la kutafuta msaada wowote. Lakini hasa kisa kilikuwa nini hadi anifanyie mambo yote yale, sikujua na wala sijaijua mpaka sasa.

Baada ya kunisema sana aliondoka huku akiendelea kusema kuwa, atahakikisha sidumu mahali pale.

Hilo sikujali kabisa, kwani kama angeniingia moyoni mwangu angegundua kuwa, hata mimi nilishachoka kuwa pale kama mahali pangu pa kazi. Tabu na mateso niliyokuwa nikiyapata pale Mungu mwenyewe ndiye anayejua. Na ndiyo maana hata mdogo wangu alishindwa kuvumilia hata kufikisha mwezi mmoja tu, akaaga kurudi nyumbani Tanga. Najua kisa ni vituko tu.

Alipozama tu, kuna mzee mmoja alikuja na kuniambia kuwa, anataka kutengenezewa jeneza la mtoto wa miaka mitano, lakini wakati akitoa kipimo nikamwambia.

"Siku hizi nimeacha kutengeneza majeneza."
Alishangaa sana lakini nilibaki na msimamo huo huo, kwamba siku hizi nimeacha kutengeneza majeneza.

Je, nini kiliendelea?
 
Sehemu ya 100.

"Kwanini, mbona biashara nzuri sana. Wenzako wanatajirika kwa sababu hiyo," aliniambia yule mzee.
"Acha watajirike," nilimjibu nikimaanisha moyoni.

Alinikazia macho kisha akaamha kuondoka bila kuniaga. Nilimwangalia anavyoondoka mpaka alipozama.

"Ninyi ndiyo wachawi wenyewe," nilimwambia moyoni nikiwa nimekasirika sana.

Jioni ya siku hiyo, nilitoka mapema kidogo kurudi nyumbani, lakini baada ya kuoga nilikwenda kukaa kwenye kijiwe kimoja cha wazee ambapo panauzwa kahawa.

Wazee walikuwa wakiongea mambo mbali mbali, yapo ambayo mimi nilikuwa nachangia, pia yapo ambayo nilikuwa sichangii neno kutokana na kutoyafahamu.
Mzee mmoja alianzisha mada iliyonifurahisha sana. Kwani kwa sehemu kubwa mada hiyo ilikuwa ikinihusu mimi na matatizo yangu.

Sikumbuki mada ilianza vipi, ila mzee alisema kuwa, kuna mtu anatokewa na matatizo makubwa sana, amekwenda kwa waganga wote, lakini bila mafanikio.
"Siku moja alimfuata babu mmoja aliyekuwa akimtuhumu ni mbaya wake, akamwambia kila kitu kuhusu yeye.

Yule babu alikasirika akamwambia nitakua mimi, akamwambia jaribu uone kazi, kumbe ilikuwa ndiyo dawa yake. Alimkomesha," alisema yule mzee.
Mimi nilitega masikio kusikiliza tu njia zote hizo mpaka nilipohakikisha kuwa, aliloliongea alikuwa amemaliza.

Niliwaza, ina maana hata mimi nikimtokea yule mama jirani na kumsema anaweza kubadilika au kuniacha!
Lakini je, badala ya kuniacha akaamua kunitoa roho itakuwaje?
Niliendelea kuwaza.

Niliporudi nyumbani, kabla ya kuingia ndani kwangu nilisikia kelele za Tv kutoka kwenye Tv moja ya mpangaji mwenzangu mmoja, nikajua anaangalia mpira. Nilibisha hodi na kuingia ndani kwake ili na mimi niangalie mpira.

Kufika, nilimkuta huyo mtu na mkewe na watoto wao wawili wakiangalia kipindi cha dini kwenye Tv moja.
"Karibu ukae tunasikiliza neno la Mungu," alisema mwanamke huku akinionesha kiti nikae.

"Haya asante," nilimjibu, lakini ghafla sauti ikawa kama imekatika.
Halafu nikaona giza mbele yangu kiasi cha kunifanya nishindwe kuona mbele wala Tv. Pale pale kichwa kiliniuma sana tena kwa ghafla.

"Kaa," yule mwenyeji aliniambia.
Nilikaa bila kujibu kitu, kwani kwa hali yangu ilivyokuwa isingekuwa rahisi nisimame au nitoke kwenda kwangu.

Nilikaa kwa kujitupa tii, kisha nikajishika uso na kupekecha macho kwani yaliendelea kutoona kabisa.

"Vipi?" mwanamke aliniuliza.
Aligundua kuwa sikuwa katika hali nzuri.
"Nashangaa sioni ghafla," nilimjibu huku nikiendelea kusuguasugua macho ili nione.
Waliacha kuangalia neno la Mungu na kunishika mkono ili wanipeleke nyumbani, lakini nilikataa kwamba nitakaa pale kwao mpaka kile kipindi kwenye Tv kitakapokwisha hata kama sitakiona.
"Ha! Kwa nini sasa?" alihoji mwanaume.
"Basi tu," nilimjibu.

"Hapana, sasa utakaa wakati huoni, twende kwako hali ikiendelea hivyo twende hospitali," alisema mwanaume lakini niliendelea kukataa katakata kwamba nitakaa pale hadi kile kipindi cha dini kwenye Tv kiishe.

Namshukuru Mungu kwani walinielewa wakaniacha nikiwa nimekaa na wao wakiendelea kuangalia. Lakini nilimsikia mke akimwambia mumewe kwamba waniache kama nilivyoamua mwenyewe.

Kusikia nilikuwa nasikia kama kawaida, na kuna wakati nilimsikia mhubiri akisema.
"Sasa nakwenda kuomba kwa wenye matatizo mbalimbali, wakapate kufunguliwa kutoka kwenye matatizo yao."

Je, nini kiliendelea?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom