Simulizi: Hujuma, Sehemu ya Kwanza (1) Bahari ya Hindi

Simulizi : Hujuma

Sehemu Ya Nne (4)

§§§§§
“Usishtuke Kamanda, ni mimi,” yule mtu akamwambia, kisha akaanza kuvuta hatua za haraka haraka kuelekea moja ya majengo yaliyokuwa hapo mtaani, memgi yalionekana kama magofu tu kutokana na mapigano ya muda mrefu ya wenyewe kwa wenyewe, yaliachwa mahame. Aliingia ndani kufungua mlango mmoja uliochoka akampa ishara Kamanda aingie, naye akafanya hivyo. Kilikuwa ni chumba kidogo chenye kitanda na kiti kimoja, zaidi ya hapo hakukuwa na kitu chochote ndani yake.

“Fasendy!” Kamanda aliita, alikuwa haamini kama mwanamke huuo kayaokoa maisha yake.
“Ndiyo mimi Fasendy, lazima nilipe fadhila uliyonifanyia kule Uganda,” Fasendy alijibu huku akijiketisha kitandani, “Sikiliza Kamanda, fanya mambo yako yote lakini hakikisha unakuja kulala hapa na si vinginevyo, hapa ni sehemu salama sana kuliko kwingine kokote, mahoteli yote yamewekwa watu wanakusaka, kila kona unasakwa, kwa sababu shughuli uliyoionesha ndani ya haya masaa sabini na mbili imewashtua maharamia, wamejipanga upya,” Fasendy alimuasa.

“Umejuaje yote hayo?” Kamanda akauliza.
“Aaaah Kamanda, nafahamu mengi sana kuhusu hili swala unalolifuatilia ambayo wewe na serikali yako hamjui …” kabla hajamaliza sentensi yake, Amata akampiga swali, “Ina maana unajua Jamir alipo?” akauliza.
“Kamanda, ndugu yako Jamir yupo hai lakini katika hali mbaya sana na hivi tunavyoongea kesho wamepanga kumuua ili na kutuma viungo vyake kwenu Tanzania,” Fasendy alijibu.
“Wapi yupo nikamwokoe? Pamoja na wale ishirini na tano,” Kamanda akauliza kwa shauku kubwa, alipata nguvu za mapambano baada ya kujua kuwa Jamir bado yuko hai.
Fasendy aliinama kichwa chini hakujua la kujibu, “Sikia Kamanda Amata, najua Jamir yuko hai, lakini huwezi kuamini kuwa sijui kafichwa wapi.”

“Ok, lazima nijue alipo, kabla ya jogoo kuwika kesho alfajiri niwe naye mikononi mwangu na nijue wengine wako wapi, wacha wayachukue hayoi makombora lakini hawa binadamu ndiyo wa muhimu kwanza,” Kamanda aliongea kwa utulivu, “Asante kwa kuniokoa,” akanyanyuka.
“Unaenda wapi?” Fasendy naye akanyanyuka na kusimama mbele yake.
“Naenda Jazeera Palace, nataka kumjua aliyeweka mwili wa Hassna kwenye gari ile ni nani,” Kamnda alieleza.
“Amata, unahatarisha maisha yako, nimeshakwambi kila hoteli hapa inatazamwa sasa wewe unataka kujitoa tena mzima mzima,” Fasendy alilalamika.

“Hapana, muda hausubiri mtu, nina mengi ya kufanya, kama ni kufa wacha waniue sasa ama zao ama zangu,” Kamanda akamshika Fasendy mabegani, “Niache niende, tuonane hapa usiku wa saa 2 mi na wewe.” Akampita.
“Kamanda!” Fasendy akaita, Kamanda Amata akageuka kumtazama mwanamke huyo, “Uwe mwangalifu sana hawa jamaa ni hatari,” akamsisisitizia.

Kamanda Amata akatoka na kurudisha ule mlango akamwacha Fasendy ndani, akatokomea mitaani kwa hadhari kubwa ili asionekane ovyo. Kando ya barabara alikutana na kijana aliyekuwa akiuza vitu mbalimbla, Amata akanunua kofia aina ya cap na miwani ya jua, akaendelea na safri yake mpaka kituo cha tax.
“Jazeera palace,” akamwambia yule kijana naye akaondoka na kwa kasi. Dakika tano tu alikuwa mbele ya hoteli hiyo, akateremka na kulipa ile tax, kisha kwa kuzunguka nyuma ya hoteli hiyo alifanikiwa kuingia kwenye korido za maofisi mbalimbali, alipishana na watu bila kujulikana mpaka kwenye ofisi ya usalama, akafungua mlango na kuingia ndani bastola mkononi.

“Tulia, sitaki fujo,” kawapa amri vijana wawili waliomo ndani ya chumba, akawatoa vitini na kuwaweka chini kisha akaiendea mashine ya inayorekodi matukio ya kila siku, akarudisha nyuma mpaka saa 5:22 asubuhi ya siku hiyo. Akatazama kwa makini tukio lile.

Vijana watatu walifika karibu kabisa na gari yake, wakafungua buti ya gari yao n a kutoa kitu kilicho katika mfuko mweusi, mwili wa mwanadamu, wakautia kwenye gari ya Amata. Kamanda Amata alijaribu kutazama sura za wale vijana, akaziweka akilini, kama kuna kipajai cha ajabu ambacho Amata alipewa ni kukariri vitu vingi tofauti kwa wakati mmoja, alihifadhi zile sura na baadae akajaribu kuinasa namba ya ile gari akaipata, akaamu kuingia msakoni. Wakati alipokuwa akitaka kutoka, alimkuta kijana mmoja kati ya wale akiwa anabofyabofya kitu kama simu ndogo, Amata akamwangalia yule kijana kwa jicho baya, akachomoa bastola na kumnyooshea.

“Nakuua, niambie ulikuwa unawasiliana na nani?” akauliza Kamanda akiwa kakunja ndita usoni mwake, akakinyakua kile kidubwana na yule jamaa akataka kujifanya anajua, akamshika suruali Amata, konde zito la upande upande likatua shavuni mwake na kumtoa jino, akaendelea kujifanya mbishi, teke kali likapiga usoni mwake yule kijana akajigonga vibaya kisogo chake ukutani, akatua chini akiwa kimya. Kamanda Amata akatoka na kuufunga mlango kwa nje kisha akatokomea pasipojulikana.

Alikuwa katikati ya mji, jua kali likiwaka, Kamanda Amata alitembea kwa haraka haraka, alipofika anapopahitaji, alatupa macho yake huku na kule akahakikisha usalama upo, akaingia kwenye mlango wa chuma wa nyumba hiyo akatulia tuli, ukimya ulitawala nyumba yote, nyumba ya Hassna, hakukuonekana dalili ya mtu, akiwa na bastola yake mkononi, alivuta hatua za taratibu huku akiangaza kwa umakini kuona kama kuna hatari yoyote, sebule ilikuwa nyeupe, hakuna mtu. Aliendelea mpaka chumbani, alisukuma mlango wa chumba cha kwanza, akatazama huku na kule, hakuna mtu, akakiacha chumba hicho na kukifikia kile cha Hassna, akasukuma mlango kwa nguvu kwa mguu wake, akatulia na ukimya ukamfuatia, akaingia kwa mnyato, akatupa macho yake kwa ufundi kabisa huku revolver yake ikiwa mkononi imeshikwa kwa umakini wa hali ya juu.

Chumbaq kilikuwa shaghala baghala, vitu vilikuwa vimetawanyika huku na huko, akajua kwa vyovyote kabla ya kifo cha Hassna lazima kuna purukushani kubwa ilifanyika, Kamanda Amata akasogelea kabati kubwa lililokuwa pembeni, kioo chake kilikuwa kimepasuka vibaya na kumwagika chini, damu zilionekana katika mbao ya kabati hilo, kwenye kijimeza kidogo kilichounganishwa na ile meza ya vipodozo kulikuwa na picha moja kwenye fremu, ilitulia ikiwa haijui nini kiliendelea, Kamanda Amata akaiendea na kuiiunua akaitazama sura ya Hassna iliyojaa katia fremu hiyo ndogo, akaibusu, kisha akatoka taratibu na kukiendea chumba alicholala usiku uliopita, mlango ulikuwa wazi.

Akashusha pumzi, akaiweka bastola yake vizuri na kuingia kwa ghafla akajirusha mpaka kwenye kona ya chumba alipoinua jicho tu alikutana na mtu aliyetoka katika mlango wa bafuni kwa kasi akimwendea pale chini, pole sana , akampa pole ya kimoyomoyo, wakati tayari ile bastola mkononi mwake ilikuwa imebanja na kumfumua bega, yule mjinga akajibwaga chini damu ikitoka kama maji. Kamanda Amata akahakikisha hakuna mwingine mle ndani, akamwende na kumkanyaga kwa nguvu pale kwenye jeraha.

“Kwa nini mmemuua huyu mwanamke?” akamwuliza. Yule bwana hakujibu, badala yake alikuwa katoa macho, “Sema!” Kamanda aling’aka na kuukandamiza mguu wake kwenye jeraha kwa nguvu zaidi, “Nani aliwatuma?” aliuliza tena.
“Sh.. sh…sharon,” akajibu kwa taabu huku damu zikizidi kumwagika. Kamanda A,ata akachutama karibu yake, “Nitampata wapi?” akamwuliza. Kwa taabu sana yule mtu akasema, ““Jidka Dabaqayn, 512,” kinywa chake kilionekana kama kinataka kuongea kitu lakini kilishindwa, kikainamia upande mwingine, andipela.

“Shiit !” Kamanda akajikuta akiropoka, akamwacha yule mtu na kusimama wima akimwangalia pale chini, Jidka Dabaqayn 512 akajisemea moyoni na kujiondoa taratibu kwenye ile nyumba. Akatokea mlango wa nyuma aliopitishwa asubuhi na Hassna, akatokea uwani, moja kwa moja akaelekea mahali palipowekwa turubai kubwa ambapo palikuwa pamefunikwa pikipiki kubwa sana aina ya Honda cc 350, akaliondoa lile turubai na kuitazama ile pikipiki kubwa, Hassna naomba nitumia chombo hiki ili nilipe kisasi kwa wakati kwa wabaya wako, akasema kimoyo moyo huku akiitazama ile mashine.

Hakuwa na muda wa kupoteza aliitikisa na kuchungulia kwenye tenki, mafuta yalikuwepo, akaliwasha na kuliacha hapo kwa muda kadhaa kabla ya kuliondoa. “Mi sielewi kabisa mnavyoniambia eti yule sheitwani amewatoroka,” Shalabah alikuwa akiongea kwa hasira, “Mtu mmeshamuwekea mtego na akakamatwa na polisi, ilikuwa ni kumfumua risasi ya kichwa tu.”

“Shalabah, hapa mi naona kuna hujuma inayofanyika, humuhumu miongoni mwetu kuna msaliti ambaye anajua wazi yule jamaa alipo lakini anampa maelekezo kutokla kwetu,” akajibu mtu mwingine.
“Ndiyo, ndiyo, hata mimi nimeliona hilo,” mwingine akadakia.

“Nani huyo niambieni sasa hivi ni lazima apate adhabu kali, tumeshapoteza watu wengi mpaka sasa, na alipofikia sasa atagundua siri nyingine nzito ambayo hatuko tayari yeye kuijua, nani anatuhujumu? Nani?” Shalabah alikuwa mkali.
“Mwanamke uliyemkodi kwa ajili ya kumuua huyu shetani ndiye anayetuhujumu,” akajibu yule kijana. Shalabah akanyamaza kimya, hana la kusema, akakaumbuka tukio la Fasendy kuipiga risasi bahasha ya kamanda Amata mkononi badala ya kumuua na kusingizia alitingishwa.

“Sasa mkaniletete Fasendy, namchinja mbele ya macho yenu, yuko wapi kwanza?” Shalabaha akahoji.
“Tulikuwa naye Sierra 5 kabla ya kubadilishana lindo lakini hata hivyo kuna wakati aliondoka na hatukujua alienda wapi.
“Fasendy,” Shalabah akasema kwa sauti ndogo huku akionekana wazi hasira kuutawala moyo wake, kifua chake kikipanda na kushuka kwa hasira, akapumua kwa nguvu, akaingiza mkono mfukoni na kutoa simu yake ya mkononi akabofya namba Fulani nakuiweka simu sikioni.

Kwa mwendo wa taratibu, Kamanda Amata alipita nyumba moja baada ya nyingine akisoma vibao vilivyoning’inizwa milangoni kuonesha namba za viwanja, ilikuwa ni barabara kubwa inayopita katikati ya majumba ya kifahari yaliyotengwa huku na huku, bila shaka ulikuwa ni mtaa wa wazito, Jidka Dabaqayn. Moyo wake ulipiga kwa nguvu alipokutana na kibao chenye namba 512 ambazo chini yake kulikuwa na picha ya mapanga mawili yaliyowekwa mtindo wa X akajua amefika kwani alielewa nini maana ya alama hiyo. Akaegesha pikipiki lake nje na kuusukuma mlango, ulikuwa wazi akaingia kwa hatua za taratibu.

SHARON aliinama kwenye sinki lililo pembezoni mwa meza yake ya chakula, alijitazama kwenye kioo kilichowekwa juu kidogo ya koki za bomba la maji lililofungwa katika snki hilo. Mshtuko mkubwa ulimpata, kwenye kioo hakuona taswira yake peke yake, alikuwa na mgeni aliyesimama nyuma yake. Akashusha pumzi kwa nguvu, akafikiri cha kufanya, aliwahiwa. Kamanda Amata aliyeonekana usoni kuwa na hasira alisimama bila kuzungumza akimtazama mtu huyo anayeitwa Sharon.

Sharon aligeuka kwa ghafla ili amashtukize Kamanda, ndipo alipokutana ngumi nzito ya mbavu zake kutoka chini, akatoa mguno wa maumivu. Kabla hajatulia konde linguine lilitu kwenye korodani, Kamanda alikuwa bado kachutama chini wakati alikuwa akimkwepa Sharon. Sharon alilia kama mtoto huku mikono ikiwa imejishika sehemu nyeti. Kamanda Amata aliinuka kutoka pale na kujirusha mwa mtindo wa frying kick, na guu lake la kulia likapiga upande wa shavu la Sharon na kumpeleka chini akiangukia meza ya chakula na kusababisha ivunjike vibaya, Sharon alikurupuka na kunyanyuka haraka, kama mtu aliyezinduka usingizini, akainua kiti cha mbao na kumrushia Kamanda Amata, lakini kikapigwa kwa usatadi na mguu wa Amata kikatupwa pembeni. Kabla Sharon hajafanya lolote, makonde mazito mfululizo yalitua katika pande tofauti za mashavu yake, Sharon akavunjika taya.
“Kwa nini mmemuua Hassna? Ana kosa gani kwenu?” akamuuliza
“Alikuwa jeuri hataki kutuambia ulipo,” akajibu kwa ujeuri huku akivujwa na damu sehemu mbalimbali.
“Mashetani wakubwa nyie, sasa mtanitambua mi nani,” kamanda alipokuwa akimaliza kusema hayo, Sharon alirusha teke lililopiga sehemu ya tumbo ya Kamanda, akapepesuka na kujipiga nyuma ya kochi, kabla hajajiweka sawa, Sharoni alikuwa tayari amejiweka sawa mkononi mwake akiwa na nusu kiti kilichovunjika, Kamtiga nacho Amata lakini kabla hakijamfikia Kamanda akageuka na kumpa mgongo, kile kiti kilitua mgongoni na kuvunjika tena, Kamanda Amata akageuka haraka na kumpa dhoruba ya ghafla, karate mbili za nguvu zilizotua shingoni mwake zilimlegeza, kabla akili haijamkaa sawa, alipigwa mapigo ya judo na kumfanya asijitambue, akajibwaga chini kama gunia.

“Sharon, udhalimu haulipwi,” Kamanda alimwambia huku akiichomoa bastola yake aina ya magnum 22, bila huruma alifyatua risasi na kuvunja goti la Sharon, kilio cha uchungu kilimtoka Sharon.
“Maswali yangu ni matatu tu, yuko wapi Jamir na wale wengine ishirini na tano? Nani mnayemfanyia kazi? Nani anayewapa siri kutoka Tanzania?”
Badala ya kujibu Sharon alibaki kujiangalia jeraha lake pale mguuni lilivyokuwa likitoa damu.
“Nakuuliza wewe!” Kamanda aling’aka na kumkanyaga kwa mguu wake pale gotini.
“Aaaaaaaiiiiggghhhrrrrr!!!!” Sharon alilia kwa uchungu, “Unaniumiza bwana,” akapiga kelele.
“Kumbe wewe unaumia ila unawaumiza hawaumii, jibu maswali yangu haraka,” alimuamrisha huku akinyoshea bastola katika mguu mwingine.
“Yaani we braza huna hata huruma wewe, binadamu gani wew…” kabla hajamaliza sentensi yake, teke moja kali la nguvu la mguu wa kulia lilitua katikati ya uso wa Sharoni na kumpeleka sakafuni.
“Nasema, nasema,” akalalama.
“Sema, haraka!” kamanda alipiga kelele, huku sura yake ikiwa imejikunja ndita, lakini bado Sharon alikuwa mbishi, Kamanda Amata akarudisha bastola yake kiunoni na na kuchomoa kisu kidogo chembamba, akamchoma pajani.
“Aaaaaiiiiiggghhhhhh! Basi basi nasema, aaaaaa weweeeee, nasema kila kitu, na- na- na- ssseeeemmmma” alipiga yowe la uchungu.
Kamanda Amata alaitikisa kidogo kile kisu kikiwa bado ndani ya nyama, “Jamir yuko wapi?” akauliza.
“Yupo yupo, yupo kule,” akajibu kwa taabu sana huku akiugulia maumivu.
“Kule wapi?” Kamnda akauliza.
“Bandani, bandani, yuko bandani, mzima hajafa,” Sharon akajibu.
“Bandani ndo wapi? Nijibu,” kamanda akaendelea kuhoji, akakisukuma kidogo kile kisu.
“Aaaaiighhhh, basi baaassssssssiiiii, niache nitasema,” akakohoa kidogo, “Kiwanda cha cha nguuuuoo,” akajibu kwa taabu huku mwili ukimtetemeka, macho yake yakianza kupoteza nguvu, damu ikimwishia mwilini.
“Nani unayemfanyia kazi, nani bosi wako?”
“Mr. Shalabah, Mr. Shal…” kabla hajamaliza, Kamanda Amata alimwachia ghafla na kujitupa pembeni, risasi iliyopigwa kutoka dirishani kwa minajiri ya kumuua Amata ilikosa shabaha nakupiga katikati ya paji la uso la Sharoni, akajibwaga na kutoa yowe la mwisho la kuagana na roho yake. Kamanda Amata kwa kasi ya ajabu alichomoa kisu na kuruka nacho huku akikirusha kwa ustadi sana kumuelekea huyo aliyefyatua risasi ile, alisikia mfurulizo wa risasi na kisha kimya kikatawala. Amata akasonya akiwa tayari na bastola mkononi, akainuka na kutazama dirishani, hakuna mtu, kakimbia? Alijiuliza, akatazma mezani akaona simu ya Sharoni ikiwakawaka akainyakuwa na kuitia katika mfuko wa shati kisha akaliendea dirisha, na kumkuta mtu akimalizia kukata roho, huku kile kisu kikiwa kimechoma katikati ya moyo wake na kuuzuia usifanye kazi.
Akaitazama saa yake ilikuwa inakimbilia saa kumi alasiri, akatoka kwa mwendo wa haraka haraka na kukwea pikipiki yake, akaondoka eneo lile. Baada ya mwendo wa dakika kama tatu hivi akasimama na kuichomoa ile simu mfukoni, akaifyatua na kutazama simu zilizopigwa, simu ya mwisho kabisa ilikuwa imeandikwa Chief akaitazama namba ile na kuipiga kisha akaweka sikioni.
“Hey Sharon, mbona hupokei simu kaka?” Shalabah alilalamika bila kusubiri hata salamu.
“Jaribu kuwaheshimu marehemu Chief,” akajibu Kamanda Amata.
§§§§§
Wakati Sharon akipata kichapo kutoka kwa Kamanda Amata huku akibwabwaja siri, Shalabah au Chief alikuwa akiendelea na kikao cha dharula na wapiganaji wake, aliipokea simu akijuwa ni Sharon anayepiga, alishtuka kusikia sauti nzito asiyoijua.
Shalabah aliitoa simu sikioni na kuitazama kwenye kioo, alijua labda kuna makosa katika kuitambua simu hiyo, la, ni yenyewe ya Sharon.
“Unasemaje?” akauliza baada ya kuiweka tena sikioni.
“Heshimu marehemu sio unaita ‘Sharon!’ ita marehemu Sharon,” Kamanda alijibu kwa nyodo na gadhabu.
“Ina, inn-a maana Sh- shar- Sharon amekufa?” Shalabah alipata kigugumizi ghafla.
“Bado wewe kabla jogoo hajawika, nitaitwaa roho yako,” Kamanda alizidi kumchanganya Shalabah.
“Kwani we nani?”
“Ninyi mnamtafuta nani? Mimi ni Amata Ric, Kamanda Amata, Tanzania Secret Agency namba moja,” alipojitambulisha akakata simu.
Shalabah akabaki katoa macho kama mjusi aliyebanwa na mlango, simu ikimdondoka bila kujua, akajiachia na kutua kitini mikono akaibwaga mezani, akashusha pumzi ndefu, kisha akawaangalia waliokuwa mbele yake.
“Namtala Fasendy hapa haraka, aletwe,” akatoa amri huku mwili ukimtetemeka, vijana waliokuwa hapo wakatoka na kufanya waliloagizwa.


Walipoondoka, aliufunga mlango kwa ndani na kuinua simu yake ya mezani, akaongea maneno machache na kuiweka chini katika kitako chake. Dakika mbili baadae, yule mwanaume mfupi, menene asiye na shingo aliingia ofisini hapo.
“Vipi Shalabah,” alimuuliza.
“Hussein,” akaita kwa sauti ya chini, Huseein akamsogelea na kusimama mbele yake, “Sharon ameuawa,” akamwambia.
“Sharon, no! haiwezekani Sharon afe kijingajinga hivyo, Sharon ni mpiganaji kaka, afe kikondoo namna hiyo, mtu kaka Torabola miaka nenda miaka rudi, usiwe mjinga Shalabah, huyo nyau anataka kuwachanga kisaikolojia ili mjitokeze ovyo kumsaka awamalize, tuma mtu kwa Sharin sasa,” Hussein, my mnene alimwambia Shalabah.
“Hivi inawezekana ee?” Shalabah akajibu kama mtu aliyekurupushwa usingizini. Tumaini jipya likachanua ndani ya moyo wake. Inawezekana, kamteka sasa anatucheza shere? Akanyanyuka kitini, “Naenda kwa Sharon, nyumbani,” akamwambia Hussein.
Hussein akamuonesha ishara ya kidole ya kumkataza, “Usikurupuke, utauawa, lazima ujue kuwa unayepambana naye ni mtu wa vita, ana mbinu nyingi za kukunasa kama vile kinyonga anavyomnasa mdudu, vipi kama yupo hapo ndani kwa Sharon kakutegea ukifika akumalize? Shalabah, tuliza akili.”
Shalabah akajiona jinsi alivyotaka kufanya ubwege, akarudi na kuketi na muda huo huo mlango uligongwa, akanyanyuka na kuufungua, Fasendy akasukumiwa ndani.
“Mwanamke mshenzi sana wewe, unataka kutuzunguka sisi? Ama kweli, kikulacho ki nguoni mwako,” Shalabah akasema kwa hasira.
“Vipi huyu, Shalabah?” Hussein akauliza.
“Huyu ni hayawani, ametuuza kwa yule shetani mara kadhaa, anatusaliti,” Shalabah alijibu huku akiuma meno. Huseein akamwangalia Fasendy pale chini, akatikisa kichwa.
“Mwanamke, umejihukumu mwenyewe, mpelekeni bandani, akatwe kichwa alfajiri ya kesho pamoja na yule Mtanzania,” Hussein akatoa amri na kisha wale vijana wakaondoka na Fasendy.
“Tuma mtu kwa Sharon akamwangalie, usimwambie kuna nini,” Hussein akamwambia Shalabah, naye mara moja akafanya hivyo.
8
KAMANDA Amata aliegesha pikipiki yake kando ya ghorofa kubwa lililozungukwa na maduka mbalimbali yaliyokuwa yakiuza bidhaa anuai. Akaengesha pikipiki yake panapohusika, kisha akatulia pembeni akiitazama gari iliyosimama mita kama mia moja pembeni yake, aliijua fika kwani ndiyo aliyoiona kwenye picha za kamera za usalama pale hotelini, gari iliyohusika kwenye mauaji ya Hassna, leo mpaka kieleweke, alijisemea moyoni huku akiweka vizuri miwani yake.
Alilolitarajia likatimia, watu wawili wakaja kwenye ile gari, mwanamke na mwanaume, kwa haraka alimtambua yule mwanamke, mhudumu wa mapokezi katika hoteli ya Jazeera Palace, na aliitambua sura ya yule mwanaume kwani naye alimuona katika wale watatu walioleta ule mwili pale hotelini,
“Shiiit!!!” alijisemea kwa sauti ndogo, “mwanamke mseng* huyu,” akamtukana kwa sauti ileile ya kujisikia mwenyewe. Ile gari ikageuzwa pale maegeshoni na kuingia barabarani.
Kamanada Amata akatikisa kichwa akajua mchezo aliochezewa pale hotelini, pindi alipokutana na yule mwanamke pale mapokezi, akachukuliwa kuzungushwa nyuma na kupewa ujumbe kuwa, polisi wanamtafuta kila mahali, ni wakati huo huo ambapo wale jamaa walikuja kuweka ile maiti kwenye gari yake, hakutaka nione kitendo hicho, huyu ni mmoja wao, alipowaza hilo ndipo alipokumbuka kuwa alipewa ujumbe kwenye kibahasha kidogo na alikwishasau kukisoma, akaingiza mkono mfukoni na kukitoa kile kibahasha, akakichana na ndani hakukuwa na ujumbe wowote zaidi ya kidubwasha kidogo kama heleni, alikigeuzaguza na kukielewa kidubwasha hicho, akakipachika sikioni na kukiminya katika kitufe chake kilichotengenezwa kwa jiwe la yaspi safi.
…Kamanda Amata, karibu sana Mogadishu, nilijua kuwa utakuja na nilikuwa nakusubiri kwa hamu sana. Hii ni salamu yangu kwako mimi Fasendy. Nakumbuka sana yote uliyonitendea kule Ugandam hukupenda nife uliniacha hai, name nashukuru Mungu sikudhurika ijapokuwa nililala kitandani kwa miezi mingi hadi uti wa mgongo wangu ulipounga sawa. Nimetumwa kukuua, kukutoa roho yako, lakini siwezi fanya hivyo kwako Abadan. Najua uliko lakini hujui niliko. Hawa jamaa ni hatari sana na wamepania kukuua. Jana nilikuweka kwenye shabaha yangu lakini kwa kukusalimu niliipiga bahasha iliyokuwa mkononi mwako. Na sasa wamegundua kuwa nilifanya makusudi, wamenibaini kwani utendaji wa kazi yangu umekuwa mzito sana siku hizi, nakupenda Kamnda, nakupenda sana, lakini hili litanifanya niwe matatizoni na hawa watu, ninajua mengi. Ila najua wataniua, wataniua tu, lakini nitafanya niwezalo kukusaidia, usinitafute ila nitakutafuta mimi…
Baada ya ule ujumbe kwisha kile kidubwasha kikatoa sauti ya bip, akakipachua pale sikioni na kukiweka mkononi, kiligeuka rangi na kuwa cheusi, kimeungua, akakitupa, alijua wazi hakijaungua kwa hitilafu bali ndivyo kilivyotengenezwa ili mtu akimaliza kusikiliza ujumbe wake basi huungua ili mwingine asije kupata siri hiyo. Akatoka pale aliposimama na kulikwea pikipiki lake tena akatazama kule ilikokwenda ile gari, akainua simu yake na kupiga namba alizokuta kwenye ile kadi aliyopewa na yule mwanamke wa hotelini.
“Hello,” akaita
“Yes Hello Jaffar,” yule mwanadada akaijibu.
“Nahitaji kuonana na wewe sijui itawezekana?” Kamanda akauliza.
“Yeah, bila shaka, labda uniambie ni wapi name nitakuja,” yule mwanamke akajibu.
“Sawa nafikiri wewe ni mwenyeji zaidi, hivyo unajua mazingira mazuri yote yako wapi, nataka uje peke yako, umesikia, peke yako,” Amata alisisitiza lakini alijuwa wazi kuwa lazima wabaya wake watafika mahali hapo na hilo ndilo alilolitaka haswa.
“Medinnah Club, saa 3:30 usiku, nitakuwa peke yangu,” yule mwanamke akajibu.
“Ok, tukutane saa hiyo!”
Uchovu ulikuwa wazi kwa Kamanda Amata, alitamani ajipumzishe lakini kila alipofikiria ni wapi kwa kujipumzisha ilimuia ngumu kupata jibu. aliliwasha pikipiki lake na kuifuata ile gari nyuma nyuma ingawaje tayari ilikuwa imekwishamuacha hatua kadhaa, alivuta mafuta ya pikipiki ile kubwa na haikumchukua muda kuiona ikiwa inakunja kona kushoto na kuiingia Jidka Afgooye, ikapunguza mwendo na kwenda taratibu mpaka katika nyumba nyingi zilizzojipanga kwa mstari ulionyooka katika eneo hilo. Akiwa umbali kama wa mita mia mbili kutoka iliposimama ile gari, Kamanda Amata alipunguza mwendo.
Nataka nijue anapoishi huyu mwanamke, alipomuona akiingia kwenye ile nyumba yeye akaendelea kusubiri mpaka ile gari iondoke, dakika tano baadae yule mwananmke alitoka pale kwenye dirisha la gari nakuingia ndani ya nyumba hiyo, ile gari ikaanza kuondoka taratibu, Kamanda Amata naye akaanza kuifuata taratibu. Ile gari ilizunguka mtaa wa pili na watatu ikachanja mbuga kuelekea nje kidogo ya mji. Kamanda Amata yeye aliifuata bila kuipoteza akihakikisha kuwa lazima ampate mtu huyo anayeendesha gari hiyo.
Ile gari ikaingia Jidka Waxaracadde na kuendelea na safari, akaiona ikiacha njia kuingia kushoto na kusimama getini, ikapiga honi kwa mtindo wake na geti lile likafunguliwa ile gari ikaingia na geti likafungwa nyuma yake.
Mogadishu Textile, ni maneno makubwa juu ya paa la ghala hilo kubwa lililojengwa nje kidogo ya mji wa Mogadishu au Moqdishu kama wenyewe wanavyouita. Kamanda Amata akapita kwa mwendo wa kawaida na kuyasoma yale maandishi, kiwanda cha nguo, akajisemea mwenyewe huku akiendelea na safari yake isiyo na ukweli wowote. Alipojiridhisha kuwa hiyo gari imeingia katika jengo hilo akaamua kurudi kwenda kupumzika ili kulipisha giza lifike kwanza naye amalize kazi yake.
Katika jengo lile lile, gofu alilooneshwa na Fasendy, aliingia taratibu kabisa na kujifungia huku pikipiki yake nayo akiifungia humo. Njaa ilimchonyota kwelikweli, lakini hakuwa na jinsi alihitaji kupumzika kwanza, na hamu yake kubwa ilikuwa ni kumsubiri Fasedny waliyepanga kukutana hapo jioni ya siku hiyo. Akajilaza usingizi juu ya kijitanda kidogo huku bastola yake ikiwa mkononi imeshikwa tayari kwa lolote.

§§§§§
SHALABAH aliangusha machozi alipoukuta mwili wa Sharon ukiwa umelala bila uhai huku macho yakiwa yametoka pima kama mtu aliyekuwa akitafuta sindano gizani. Alimtikisa lakini hakujibu lolote. Akanyanyuka na kuwaangalia vijana aliokuwa nao kwa gadhabu.
“Hifadhini mwili huu tutauzika kama desturi yetu, yatima huyu hakuwa na ndugu kama ninyi mlivyo,” aliwaambia vijana wake aliokuwa nao. Akanyanyuka na kutoka nje, moja kwa moja akaingia garini mwake na kuketi, akainua simu ya upepo na kuanza kuongea.
“Sierra 4, Sierra 4,” akaita.
“Sierra 1 unasikika,” sauti ikajibu.
“Sharon ameuawa mchana wa leo, naomba sasa kuwa maini na ulinzi kila kona ya Mogadishu lakini cha msingi pia ni kila mtu kujilinda mwenyewe, adui yetu amekuwa kama mbogo aliyejeruhiwa, atararua kila amwonaye, kwa kuwa sasa hajui nini anafanya, popote akioneka alipuliwe hapohapo,” akatoa maagizo na kukata simu. Kisha akawasha gari yake na kuondoka eneo hilo.
§§§§§
“ Nashindwa kukuelewa unachoniambia Shalabah,” Mr. Lonely alikuwa akiongea na kijana wake anayemwamini kabisa Shalabah kwa mtindo wake uleule wa kuoneka kwenye luninga, “Hivi inakuwaje kamtu kamoja kanawasumbua ninyi mko zaidi ya mia? Iaingia akilini kweli, yeye ana bastola nyie mna bunduki kubwa za kisasa, mnashindwa kumtengua kiuno, anawaua kama mtu anavyoua inzi.”
“Mzee, tumetega kila aina ya mtego lakini yule jamaa kaikwepa,” Shalabah akajibu.
“Ukiona anakwepa mitego yenu basi ujue kuwa ninyi si wategaji wazuri,” Lonely alidakia.
“Sio hivyo Mr. Lonely,” Shalabah akalalamika.
“Sasa nini? Na yule tuliyemkodi anafanya nini?” akauliza.
“Hilo ndilo liakuja, yule mwanamke tumegundua kuwa ni msaliti anatusaliti kwa kumpa siri zetu adui,” Shalabah akaeleza. Mr. Lonely akashtuka kidogo, “Ati, anatusaliti?” akauliza kwa wahka mkubwa.
“Ndiyo anatusaliti,”
“Sasa umeamua nini kwa hilo?” akauliza kwa ukali.
“Tumemuweka chini ya ulinzi na kesho asubuhi tunakata kichwa,” Shalabah akajibu.
“Safi sana, mwanamke hana akili yule, mumkate kichwa na nyama yake mniletee niwape samaki wale,” kisha akamwangalia Shalabah aliyekuwa ameketi kwenye sofa kubwa akitazamana na luninga hiyo, “Sasa nataka ulinzi maridadi, kesho jioni inaingia meli kubeba makombora yote kumi yaliyobaki, najua hilo unafamu, sasa hakikisha hatutaki fujo kazini,” Mr Lonely aliongezea ombi hilo. Shalabah akaliacha jumba hilo na kuendelea na shughuli zake zingine.
Jumba kubwa la Mr Lonely lilikuwa ni jumba pekee sana katika mji wa Mogadishu, kila aliyepita alipenda japo kupata picha ya jumba hilo lenye bustani ya kupendeza, matunda ya msimu na mambo mengi ya kuvutia. Ndani yake kulikuwa na mtu anayaeishi. Ukiacha jumba hilo, ndani yake kuna ghorofa iliyojengwa chini ya ardhi, ghorofa hiyo ndiyo ilikuwa akiishi mwenye Mr Lonely. Mr Lonely alikuwa akiishi peke yake katika jumba hilo, mfanya kazi wake wa upishi na msaidizi wake ndio watu pekee waliokuwa wakiishi ndani ya kasri hilo, lakini amini usiamini hata wao hawajawahi kumuona, wanapomaliza kupika chakula tu hukiweka mahala Fulani juu ya kitu kama meza hivi, na kile chakula uingia ndani na baadae kutoka. Alikuwa na pesa nyingi kuliko watu wanavyodikiria. Alijipa jina la Mr. Lonely kwa sababu alikuwa akiishi peke yake hakuwa na mke wala hakuwa na mtoto, kwa ujumla alikuwa hana uwezo wa kuzaa, enzi za ujana wake alikuwa ni mwanajeshi katika jeshi la Sardenia, wakati wa vita ya pili ya dunia alikamatwa na askari wa Kijerumani na katika kumpa mateso ili kupata siri za kijasusi walimkata uume akabaki kibubutu. Alifanikiwa kutoroka kwa watesi wake hao lakini hakufanikiwa kupata uume wake. Lonely hakupenda kuonekana na watu, na wengi walijua kuwa mtu huyo amekwishakufa zamani kwani Mr. Lonely halikuwa jina lake halisi.
DAR ES SALAAM TANZANIA
Saa 12 jioni.
MADAM S alikuwa akifungafunga ofisi tayari kuelekea kwenye kikao cha baraza la usalama la Taifa ambacho kilikuwa kimepangwa kufanyika jioni hiyo katika ukumbi mdogo wa Kilimanjaro Square ulipo ndani ya jengo la Ikulu ya Dar es salaam. Kilikuwa kikao nyeti na wadau wote wa usalama walikuwa wakihitajika ili kutathimin hali halisi ya usalama kwa ujumla.
Madam S aliegesha gari yake katika maegesho ya jengo hilo nyeti sana katika Taifa la Tanzania, jengo linalopitisha maamuzi magumu juu ya nchi hii. Kila aliyeshuka kwenye gari siku hiyo alionekana kuwa na mawazo mengi sana kuliko ilivyo kawaida. Mkuu wan chi aliwata haraka na mara moja bila kuchelewa.
Ndani ya ofisi hiyo waliketi katika mtindo wa yai mbele yao kukiwa na meza kubwa kabisa ya mbao safi iliyokuwa na chupa za maji juu yake. Dakika chache baadae aliingia Rais wan chi kupiti mlango tofauti na ule waliopitia wale wajumbe. Wote walisimama kwa heshima na kutoa saluti kali kwa waliopaswa kufanya hivyo. Mkuu wan chi akawapa ishara ya kuketi nao wote wakafanya hivyo.
“Nimekuiteni hapa ghafala lakini kama mnavyojua usalama wan chi yetu upo mikononi mwetu, hata kama nikikuita saa nane za usiku hauna budi kufika,” akakohoa kidogo kusafisha koo, “Sasa ndugu wajumbe nitawapa hii taarifa hapa ambayo ilifika leo asubuhi katika ofisi yangu, na haikuwa busara kama nisingewaambia, hivyo tumeitengeneza kwa vitini namna hiyo na kila mtu naomba apitie kwa harakaharaka aone kilichomo,” akawambia na katibu wake akagawa vitini hivyo kwa kila mjumbe. Kati ya wote ni Madam S tu aliyeonekana kutochanganyikiwa na taarifa hiyo kwa kuwa yeye ndiye aliyeiwasilisha kwa Rais asubuhi hiyo. Hakuna aliyeongea wala kunongona, ila vijasho viliwatiririka kila mmoja kwa jinsi zake.
Kishapo Rais akaendelea, “Natumaini mmesoma na mmeelewa sivyo?” wote wakajibu “Ndivyo!” kisha akaendelea, “Hivi hili Taifa tunalipeka wapi? Kama viongozi tunaopewa dhamana tunakuwa wa kwanza kutafuna mali ya umma na huu umma utaishije wazee wangu? Nadhani wenyewe mmeona hapo kilichofanyika kule Msanga Mkuu miaka zaidi ya kumi iliyopita, ukisoma ndipo sasa utagundua hujuma mbaya iliyofanywa na baadhi ya viongozi wa serikali, leo hii tunapohangaika kuliokoa Taifa vijana wetu akina Gwamaka wanachinjwa, wanamwaga damu kwa ajili ya hawa watu. Wajumbe, taarifa hii imeletwa na Kamanda Amata aliyeko Somalia katika uwanja wa vita, yeye mwenyewe anasema ni uwanja wa vita, lakini ameweza kupa siri hii kubwa na mbaya kabisa, ni aibu!” Rais aliongea kwa wahka kubwa.
Waziri wa mambo ya ndani akauliuza, “Mheshimiwa, yeye Kamanda hii siri ameipataje huko Somalia? maana nimeichunguza na nimeona huku mwisho imesainiwa na mtu ambaye tayari ni marehemu The Chammeleone ijapokuwa saini yenyewe imefutika futika, lakini nimeitambua,” baada ya kusema hilo kila mjumbe akafungua mwisho wa faili lake na kutazama. Kila mmoja alitikisa kichwa.
“Mimi hilo silijui, mi nataka muone hiyo taarifa, na ninatoa amri, waziri wa Mambo ya ndani hawa watu wakamatwe mara moja, aliyekkuwa hai akamatwe aliyekufa mali zake zikamatwe, tutajua la kufanya,” Rais akasisitiza kwa uchungu, “Naomba hilo lifanyike leo maana tumepoteza wapiganaji ishirini na hatujui wako wapi, Gwamaka kijana wetu mahiri wa JW amechinjwa kama kuku, Sebeki komandoo wetu ameuawa kwa bomu, Jamir hatujui aliko Daudi nae alkadharika na meli yetu kubwa ya kisasa vyote hivi vinatughalimu naoma zoezi hili lifanyike usiku huu, na huyu Mr X kama ilivyoanishwa hapa najua nani nitampa kazi ya kumsaka.” Baada ya mazungumzo machache kikao kilivunjwa majira ya saa 2:30 usiku na kila mtu akatawanyika.
Wakiwa nje Madam S alikuwa akibadilishana mawazo na viongozi wenzake wakiongea hili na lile.
“Madam S!” akasikia akiitwa pembeni, akatazama huyo amwitae akamuona ni waziri wa ulinzi ambaye naye alikuwamo katika kikao hicho.
“Madam S, kijana wako anafanya kazi nzuri sana, lakini hii siri kaipata vipi?” akauliza.
“Ah hilo swala gumu mimi kujibu, yeye anajua mbinu zake jinsi ya kupata vitu kama hivi, na siyo hiyo tu amegundua siri nyingi sana juu ya hujuma hii, na wote wanaohusika, pale orodha uliyoiona na ndogo wapo na wengine wengi,” Madam akajibu. Waziri wa ulinzi alioneka uso wake kusawajika kwa mawazo ya dharula yaliyokuja bila kutegemewa.
“Huyu ni kijana mahiri sana katika kazi yake,” waziri wa ulinzi akasifia.
“Nami najivunia kuwa naye,” Madam S akamjibu. Katika moyo wa Waziri wa ulinzi kulikuwa na jambo lililojificha jambo hilo lisiloonekana kwa macho lilisomwa haraka sana na Madam S akaona lazima lifanyiwe kazi haraka iwezekanavyo, akaingia katika gari yake na kujifungia mlango huku vyoo vyote vikiwa juu, akafyatua kidubwasha chake cha kuongelea na kukisogeza karibu na kinywa chake.
“Hey Gina, uko wapi au umesinzia?” Madam S aaiuliza.
“Nipo mama, nipo palepale Magogoni,” akajibu.
“Ok, sogea hapa katika lango la Ikulu ila usiegeshe gari, ifuatilie gari namba STK 110A Toyota Landi Cruiser kisha nipe maelezo kila hatua.
“Copy” Gina akajibu.
Dakika tano baadaye, Gina alikuwa akisogea taratibu na gari yake binafsi aina ya Toyota Mark II akilifuata lile gari aliloelekezwa, akiwa peke yake ndani ya gari hiyo alikuwa akisikiliza muziki mwororo wa Whitney Huston uliokuwa ukipigwa kutoka katika chombo cha gari hiyo. Walipita barabara ya Kivukoni moaja kwa moja mpaka mtaa wa Magogoni na kukunja kushoto kuufuata mtaa huo walipofika barabara ya Luthuli wakakunja kulia. Gari aliyokuwa akiifuatilia Gina iliingia Sokoine Drive na kuambaa mpaka kwenye mzunguko mdogo unaoziunganisha Sokoina drive, barabara ya Chimara, ya Garden na ile ya Samora. Akaingia barabara ya Chimara na kutokea Ocean Roada akakunja kushoto.
CHANZO : Deusdedit Mahunda
Muda wote huo Gina alikuwa makini kuifuatilia gari hiyo mpaka ilipofika katika eneo la Sea View, Upanga, ikaingia katika moja ya majumba mazuri yaliyojipanga hapo.
SOMALI HIGH COMMISION, lilikuwa bango la ukubwa wa wastani likining’inia katika lango kuu la nyumba hiyo ambapo ile gari ilikuwa ndani yake, Gina akainua mkono wake na kubofya kitufe Fulani katika saa yake na kuisogeza karibu na kinywa chake na kuongea.
“Madam S, shabaha ni Somali High Commision,” alimpa ujumbe.
“Chukua vithibitisho kama unaweza Gina,” Madam S akatoa amri.
“Copy,” akajibu.
§§§§
Waziri wa Ulinzi alikaribishwa katika sebule kubwa ndani ya jumba hilo lililotandikwa zuria la gharama sana lenye manyoya ya samba, akakaribishwa kiti na kuketi, mhudumu wa ndani akamlete kinywaji baridi kwani alikuwa anajua kiongozi huyo upendelea kinywaji gani. Baada ya muda kidogo balozi wa Somalia aliungana naye pale sebuleni.
“Ndiyo komredi, nipe habari maana uliponipigia simu nilishtuka kidogo,” yule Balozi akaanzisha mazungumzo.
“Ni hivyo, tulikuwa tumeitwa Ikulu na swala lilikuwa hilihili swala letu la miaka mingi, juu ya ile plant kule Msanga Mkuu, kiukweli sisri hii sio siri tena kwani ipo ofisini kwa mkuu wan chi na amekwisha amuru baadhi ya vigogo wa serikali wakamatwe usiku huu, waliostahafu na hata waliokuwa kazini,” akapiga funda moja. Kabla hajaendelea kuongea balozi akaingiza kauli.
“Lakini, akaunti yako imeshaitika? Mi yangu tayari, na nataka niende likizo nyumbani ili nikamalize na bwana Lonely maana alinambia ikikamilika kuna donge linguine, simtokusahau Komredi,” yule balozi alikuwa akiongea kwa furaha sana wakati mwenzake alikuwa kwenye mawazo mazito.
“Swala sio pesa, je ukigongewa mlango usiku huu kuwa unatakiwa ukajieleze Ikulu itakuwaje?” akauliza yule Waziri.
“Aaa Koredi, hapa ni nchi nyingine, hilo haliwezekani kwa maana unaweza kuharibi uhusiano wa kidiplomasia,” akajibu yule Balozi.
“Ok, hali iko hivyo lakini swala si unajua liemeisha!” Waziri akasema.
“Ndiyo najua na nimepata taarifa kuwa kesho ule mzigo utaondoka pale kuelekea Afghan, tumemaliza kazi wacha tunywe kaka,” aliongea kwa Kiswahili kilichochanganyika na kiarabu, vinywaji vikaletwa na wawili hao wakaburudika.
§§§§§§
“Vipi umepata lolote?” Madam S akamwuliza Gina.
“Yap, mheshimiwa amekaa sana pale kwa balozi nafikiri walikuwa na kikao kizito najua,” Gina akaeleza akaonesha na vielelezo vya picha ya ile gari ikiwa inatoka katika lango la nyumba ya balozi.
“Good Girl, unaanza kukomaa sasa Gina, endelea hivyohivyo ili wakati mwingine nikuweke mstari wa mbele,” Madam S alimtania huku akimpigapiga mgongoni, kisha akendelea “ Sikiliza Gina, siku zote unapotaka kufanya jambo la hatari inabidi uzingatie mambo matatu ya kiusalama, je ninapokwenda nitaajihakikishia vipi usalama wangu? Hilo ni swali muhimu sana najua unafahamu kuwa unatakiwa kuaangalia sana usalama wako, hivyo uwe mwangalifu.”
“Mama usijali, katika swala la usalama niko vizuri tu labda itokee bahati mbaya, Kamnda kanifundisha mengi sana,” Gina akaeleza.
“Najua, na anakupenda pia, anapenda uwe mke wake, lakini nasikitika kwamba haiwezekani,” Madam S alaimwambia.
“Ah! Madam, Kamanda simuezi, kisimpitie mbele kabeba,” Gina alijibu.
“Hapana hafanyi vile makusudi, wakati mwingine inabidi awe vile ni moja ya kazi, huwa anapenda kutumia wanawake kupata siri anazozihitaji ijapokuwa wakati mwingine ni kazi na dawa,” wote wakacheka na kugonganisha viganja vya mikono yao.
Rejea MOGADISHU
ILIKUWA imetimu saa mbili usiku Kamnda Amata alipokurupuka kutoka katika ndoto mbaya, sauti kali ya Fasendy ilimshtua kutoka katika ndoto hiyo. Akaketi juu ya kitanda kile kidogo akihema kwa nguvu, njaa ilikuwa kali sana alihisi hawezi kufanya lolote kwa jinsi alivyo, hakuwa na nguo za kubadilisha lakini hilo kwake halikuwa tatizo. Akainuka na kuiendea chupa yake ya maji, akapiga mafunda kama kumi ya nguvu kisha mengine akanawa, alihitaji kuoga lakini hakukuwa na bafu kati kijichumba hicho, inaonekana kilikuwa ni sehemu ya maficho ya Fasendy kwa jinsi kilivyo.
Akatoka na kuangalia nje, mbala mwezi ilikuwa badoa haijaanza kung’aza mji huo, alijichomoza na kulitoa pikipiki lake akaufunga mlango na kulikwea, akaondoka eneo hilo. Safari hiyo iliishia kwenye mkahawa mmoja wapo uliopo mtaa wa tatu, hakujali lolote aliegesha pikipiki yake na kuingia mkahawani, akaagiza chakula kinachofaa.
MEDDINAH CLUB
WAKATI Kamanda Amata akijipatia chanjo ya tumbo, kule klabu ya Meddina vijana watano walikuwa wameketi katika kona tofauti za ukumbi huo, wote wakiwa wameagizwa kuhakikisha wanammaliza Amata usiku huo. Walipewa taarifa na yule mwanamke mhudumu wa hoteli, yeye alifanywa kama chambo tu cha kumzubaisha Kamnda Amata usiku huo ili maharamia wale wamalize kazi yao.
Walishajua ni wapi wataketi, hivyo kila mmoja alikuwa tayari na bastola iliyoshindiliwa risasi, hawakutakiwa kutoa taarifa yoyote zaidi ya kifo cha Amata, ndiyo iliyokuwa ikisubiriwa na Shalabah usiku huo, na aliamini hilo kwani alijuwa vijana aliowapeleka kule ni mahiri kati shabaha kuliko unavyofikiria.
§§§§§
Saa tatu kamili usiku huo, Kamanda Amata alifika nyumbani kwa yule mhudumu wa hoteli kwani machale yalikwishamcheza kuwa lazima hawezi kuja peke yake, hakuwa na haja ya kwenda Meddinah klabu, aliamua kumaliza mchezo huko uswahilini na kuwaacha wanaomsubiri kama wapo wabaki midomo wazi kupiga miayo. Aliegesha pikipiki yake nje na kuvuta hatua kuielekea nyumba hiyo.
Alipoufikia mlango alitulia kidogo, akautazama vizuri ulikuwa haujafungwa, mlango ulikuwa wazi na uwazi mdogo ulikuwa ukionesha mpaka sebuleni, akachungulia ndani kwa jicho la kijnja hakukuwa na mtu sebuleni. Akasita kuingia,usije kuwa mtego, akajiwazia, baadae akaamua kugonga, hakujibiwa, akausukuma taratibu na kuingiza mwili wake ndani ya nyumba hiyo, utulivu ulikuwa umeijaza sebule yote, kwa mbali alikuwa akisikia miguno ya watu waliokuwa mapenzini, yaani katikati ya sherehe, akasogea karibu na korido inayoelekea huko vyumbani, alichokisikia kilikuwa sahihi. Yule mwanamke alikuwa kitandani na mwanaume wakifanya ngono. Akawatazama kupitia uwazi mdogo wa maungio ya mbao za mlango ambao haukushikamana vizuri, watu na starehe zao, akawaza.
Taratibu akamtazama vizuri yule mwanaume, akamjua sura yake, akaikumbuka ni moja ya wale watatu waliomuua Hassna, hakuwa na papara, Kamanda akarudi sebuleni, bastola mkononi akaketi mahala tulivu na kusubiri wamalaize vyao. Muda si mrefu alianza kusikia vicheko vikali, akajua wameshamaliza dhambia zao, na kweli dakika hizo hizo alisikia hekaheka za kwenda bafuni kuoga mwanamke akisisitiza kuwa anawahi miadi. Viatu vya kiume vikasikika viukigonga sakafu kuja sebuleni, Amata akanyanyua bastola lake, revolver, akalitazamisha kule kwenye korido, yule mwanaume akasogea bila kumwona kwa maana alikuwa kama kivuli, yule bwana akaliendea jokofu na kujichaguli kinywaji alipogeuka kurudi kitini akakutana uso kwa uso na domo la bastola. Akatetemeka na kuangusha chupa na glass vilivyokuwa mkononi mwake.
CHANZO : Deusdedit Mahunda
“Keti chini taratibu sitaki vurugu,” alimwambia kwa sauti ya chini, yule jamaa akaketi bila tabu, mita moja ilikuwa katikati yao ili isitokee shida yoyote. Na mara ileile yule mwanamke naye akatokea, akakutana na dhahama hiyo.
“Na wewe njoo, haya mpekue huyo kila alichonacho weka mezani, haraka,” yule mwanamke hakuamini akionacho akafanya hivyo akamaliza.
“Haya we mwanamke, unanifanya mimi mjinga sivyo? Nina uhakika kabisa kuwa huyu bwana alishirikiana na Sharon na mtu mwingine kupakia ule mwili wa Hassna kwenye gari yangu pale hotelini, wewe hili unalijua, na ni dakika ileile uliponichukua na kunizungusha nyuma ukinambia kuwa polisi wananitafuta,” akatulia kidogo, “ sasa mimi si mjinga, nilikufuatilia yangu pale mjini supa maketi ukiwa na huyuhuyu mwanaume kwenye gari namba (akazitaja) na nikajua kuwa huwezi kuja kwenye miadi peke yako, na hilo nina uhakika, sasa miadi yetu ni hapa.”
Hakuna aliyekuwa na la kuongea, wote walikuwa kimya, baada ya muda kidogo kama sekunde tatu hivi yule bwana akauliza, “Unataka nini kwetu sasa?” aliamua kujitutumua ilia aonekane mwanaume mbele ya huyo mwanamke wake.
Risasi moja ya revolver ilifyatuka na kufumua pega la mwanaume huyo.
“Huwa siulizwi maswali ya kitoto,” Amata alimwambia. Kilio cha maumivu kilitawala mle ndani yule mwanamke akipiga makelele kama kachanganyikiwa, akasimama kumuendea Amata, “Sitaki muuanie nyumbani kwangu, sita…” hakumaliza, kofi moja zito kutoka katika kono la Kamnda likamfikisha chini salama.
“Nitawaacha hai mkiniambia tu bandani ndio wapi basi,” Kamanda akawaambia.
“Bandani, bandani, bandani? We Jeinah mwambei atuache, jamani mwambie,” yule mwanamke akawa akimlazimisha mwanaume kusema.
“Mogadishu Textile,” yule mwanaume akamasema maneno hayo mawili, alipomaliza tu, risasi nyingine ilifumua kichwa chake na kumuacha marehemu, Kamanda Amata akamchukua yule mwanamke akamkamata mkono na kutoka naye nje akimkokota mpaka kwenye pikipiki yake.
“Panda!,” alimwamuru baada ya yeye kuwa tayari juu ya mashine hiyo. Yule mwanamke akapada.
“Sasa unanipeleka wapi jamani?” akauliza yule mwanamke.
“Utajua tukifika,” akajibu Amata na kuondoka kwa kasi eneo lile.
§§§§§§
Fasendy alitupiwa ndani ya chumba chenye giza, chumba ambacho hakikuwana kitu chochote wa mtu yeyote, alijiketisha karibu kabisa na kona ya chumba hicho, giza likiwa limemzunguka kila upande. Kila mara mwili wake ulimsisimka kana kwamba kuna jambo la hatani ndani ya chumba hicho, lakini hakuweza kuona kwa macho yake ya kawaida. Hata alipojaribu kutazama hapa na pale labda atapata sehemu ya kujiokolea, bado hali ilikuwa ni ndoto.
Akatulia palepale alipofikia tangu mwanzo akisubiri hatima yake lakini bado hakukubali kufa kijinga namna hiyo. Haiwezekani alijiwazia mwenyewe na kujipa moyo wa kuendelea kukaa humo, lakini kichw achake kilionesha wazi kuwa ni ni mtu mwenye fikra nzito na ngumu. Fasendy alikuwa akijaribu kutazama njia ya kutorokea.
Utulivu ulichukua nafasi katika masaa hayo ya usiku, aliamini kabisa kuwa Amata anaweza kuibuka kama mzimu na kuwaokoa, ijapokuwa alikuwa na uhakikia kuwa Amata hajui ni wapi alipo lakini alijipa moyo kuwa anawezaa kuongea naye kihisia kama ilivyo kwa majasusi wengi. Ukuta uliotenganisha vyumba vya jengo hilo ulikuwa ni ukuta mwembamba kama sita hivi. Kutoka mbali alisikia watu waliongea kuelekea upande alipofungwa yeye, lakini wale watu walipofika pale hawakufanya lolote juu yake bali walikwenda mpaka mlango wa pili na kuingia.
“We mbwa koko, bado masaa machache tunakata kichwa chako, tuwapelekee zawadi mabosi wako kama tulivyofanya kwa yule mwenzio,” sauti hiyo iliyoongelewa kwa lugha ya kihabesh ilipenya katika ngoma za masikio ya Fasendy, akajua kwa sentensi hiyo kwa vyovyote atakuwa anaambiwa Jamir. Akasubiri viumbe wale waondoke pale na baada ya hapo alianza kufanya mawasiliano na mtu wa chumba cha pili kwa jinsi ya ajabu, na alielewa wazi kuwa kama ni Jamiri basi atajibu tu lugha hiyo. Fasendy alijipekua mifukoni kuona kama ana kitu chochote cha chuma lakini hakuwa nacho, alifikiri mara mbili na mwisho wake akakumbuka kuwa ana pete ya dhahabu kidoleni mwake, akaivua na kuishika kwa vidole barabara kabisa akaitumia ile pete kugonga gonga ukuta uliotenganisha vyumba hivyo. Jinsi alivyokuwa akigonga ilikuwa ni kwa mtindo maalumu, akagonga mara kadhaa na kusikiliza kama kuna jibu lolote kutoka upande wa pili, haikuwa hivyo.
§§§§§
Wakati Fasendy akifanya yite hayo, Jamir alikuwa amejilaza sakafuni, akiwa na uchovu na njaa ya siku kadhaa, mwili wake haukuwa na nguvu za kutosha kufanya lolote. Alihisi kuwa ni mwisho wake umekwishafika. Ingawaje yeye ni komandoo mzoefu aliyeshiriki vita ya ukombozi ya Comoro lakini njaa ilikuwa ni komandoo mkubwa zaidi. Jamir hakuona jua tangu afungiwe kwenye chumba hicho, alidhoofu kwa mengi, mawazo, aliiwaza sana familia yake aliona bora kama angeuawa lakini moyoni mwake bado alikuwa na mambo mengi aliyoyahifadhi ambayo angependa amwambie mtu yeyo te yule ili ayafikishe nyumbani Tanzania, kwani aliamini kuwa kwa mambo hayo basi hujuma hiyo ingepatiwa ufumbuzi.
Alishtuka kutoka kwenye kausingizi ka mpito, akatulia kimya akisikiliza kijisauti hafifu cha kitu kinachogonga katika ukuta wa upande wa pili. Alisikiliza kwa makini, kwa kufunga milango. Kwanza alifikiri ni mdudu ambaye anafanya hivyo lakini aligundua kuwa si mdudu kwa sababu mpangilio wa sauti ile ya kugonga ulikuwa ni ule ule kila ukirudia na nafasi kati sauti moja na nyingine nin ileile kila inaporudia, alielewa nini maana ya ule ugongaji.
…Jamir, Jamir… ilikuwa maana ya kule kugonga kulikofanywa kutoka upande wa pili, Jamir akainua kichwa chake kuutazama ule ukuta, hakuwa na nguvu ya kusimama ilimbidi kutambaa chini kuelekea eneo lile amalosikia ile sauti, akasota na kusota kwa kutumia tumbo mpaka akafuika eneo lile akatega sikio kusikiliza kutoka katika ukuta ule. Ukimya ulitawala, Jamir akakata tama akajua labda kweli ni mdudu, lakini mara kadhaa alijiuliza kama ni mdudu kwa nini agonge kwa jinsi ileile kila wakati? Hakupata jibu. akavua kiatu chake kwa taabu sana ambacho mbele kilikuwa na utepe wa chuma kwa ndani kidogo na ulitokeza nje kwa nusu milimita, haikuwa rahisi kugundua kama kuna chuma mbele ya kiatu hicho. Kwa kutumia nguvu hafifu za mkoni aliingiza ndani ya kiatu chake vidole vyake na kufyatua chuma kile, kikachomoza kwa mbele akakifungua kwa taabua nacho kikatoka, kama ni mdudu basi hatojibu, alijisemea.
Alikumbuka alipokuwa Urusi katika mafunzo ya kikombandoo waliwahi kufundishwa jinsi mbalimbali ya kuwasiliana na mtu mwingine pasi na waliokuzunguka kujua, ikiwemo lugha ya macho, vidole, na hata hiyo ya kugonga kitu na kusikiliza idadi ya mapigo ya kitu hicho, mpangilio wake katika makundi na nfasi kati ya kundi moja na kundi linguine. Ilikuwa kila kundi la mapigo linatengeneza silabi Fulani na unapoziunganisha kitaalamu unapata neno kamili.
Kwa jinsi Fasendy alivyogonga alikuwa akiita Jamir, Jamir. Kwa nguvu kidogo alizonazo nay eye akajibu ka kugonga vilevile kwa mtindo ulele akilirudia lile jina, Jamir. Mara upande wa pili akausiki ukigonga tena ukimpa ujumbe mwingine tofauti, mtu wa upande wa pili alijitambulisha kwa jina lake nay eye ni nani kwa mtindo uleule na akampa ujumbe Jamir kuwa ana uhakika usiku huo wataokolewa na Kamanda Amata kwani tayari yupo Mogadishu kwa siku tano.
Jamir alijikuta anajivuta na kuketi sawasawa, kitendo ambacho alikuwa hawezi kukifanya hapo kabla, mara baada ya kusikia jina la mtu huyo, Kamanda Amata, alipata matumaini ya kuishi, aliamini sasa mkobozi kafika kama si yeye kukombolewa basi wale wengine wote, lakini mpaka muda huo ni yeye tu Jamir alikuwa anajua walipo kwani alisikia mara kadhaa maharamia hao wakiongea juu yao ama kwa redio au kwa ana kwa ana.
Hakuwahi kukutana na Kamnada Amata tangu kuzaliwa kwake, lakini alizisikia sifa za kijana huyo machachari, mkorofi, jasusi la kimataifa ambalo linayanyima usingizi mashirika makubwa ya kijasusi kama CIA kwa jinsi anavyotumia akili katika kazi yake.
§§§§§§
Kamanda Amata alimbwaga yule mwanamke mhudumu wa hoteli katika chumba kile kidogo cha kwenye gofu.
“Siwezi kutumia risasi yangu kuua mrembo kama wewe, utakaa hapa na adhabu yako utaiona nikirudi,” Kamanda Amata akamwambia yule mwanamke aliyekuwa akilia muda wote, akachukua kamba na kumfunga miguu yake yote kwa pamoja kisha akamfunga mikono kwa nyuma na kumtupia kitandani akihakikisha hana jinsi ya kujiokoa. Akamtazama usoni na kutikisa kichwa, akatoka na kufunga ule mlango kwa nje akakwe pikipiki lake na kupotelea mitaani.
Ilitimu saa nne za usiku wakati Kamanda Amata alipokuwa amesimama pembezoni mwa jengo kubwa, godown la nguo, Mogadishu Textile, alikuwa akisubiri muda wake ufike ndipo aanze kazi aliyokuwa ameipanga, aliamini kwa vyovyote kadiri ya maelekezo ya wale wa kwanza kuwa hapo ndiyo bandani. Akalisogeza pikipiki lake kwa kulikokota mpaka karibu na jiwe moja kubwa lililofanya kitu kama pango akalipachika hapo, akajitazama alikuwa na bastola tatu, lakini ni moja tu iliyokuwa imejaa swwasawa nyingine zilitumika hapa na pale, nitapata nyingine hukohuko, alijisemea na kutoka kwenye lile jiwe, akautazama ukuta mkubwa uliozunguka jengo hilo, akajaribu na kutazama pande zingine akagundu ni urefu sawa kutoka kila upande. Juu ya ule ukuta kulikuwa na waya maalumu wa kuzuia wezi, daima waya huu huwa na umeme. Hakuwa na nmna ya kuupanda, alizunguka kuelekea lango kuu, kutoka mbali aliona walinzi wawili wakiwa pale mlangoni. Nitapitaje? Ni swali lililopita akilini mwake, alilisogelea lile lango huku akiwatama vizuri wale walinzi waliokuwa pale langoni, mmoja akiwa ameketi kibandani akimuliwa vizuri kabisa na taa ya umeme na mwingine alikuwa akitembea huku na huko. Akiwa katika kutafakari hilo mara akasikia honi za gari kutoka nyuma yake akalipisha na gari lile kubwa, gari la maji lilikuwa likiingia katika jengo hilo. CHANZO : Deusdedit Mahunda
Ilikuwa nafasi pekee kwake, kwa wepesi sana alidandia ngazi ya nyuma na kupanda haraka kisha akajibwaga katika keria ya juu kabisa ya tanki hilo akalala kimya. Ile gari ikasimama kwa ukaguzi na dakika mbili tatu ikaruhusiwa kuingia ndani, hivyo ikamsaidia Kamnda kufika ndani kabisa ya jengo lile lenye ua mkubwa katikati likiwa limezungukwa na maghala makubwa kama manne hivi. Akatulia kutoka kule juu ya gari akisikiliza kinachoendelea, yule dereva akaondoa lile lori kutoka hapo aliposimama akiongea na mtu mwingine, akapita kwenye magari mabovu ili kupata sehemu nzuri ya kuegesha, ni nukta hiyohiyo ya kuyapita yale magari mabovu Kamnada Amata aliporuka kwa ustadi na kutua chini kisha kwa haraka akaingia katika moja ya magari hayo yaliyochoka, akatulian akiangalia mienendo ya watu waliopo eneo hilo. Hakukuwa na watu wengi, nje katika uwa huo mkubwa palikuwa na vijana watatu, bila shaka walikuwa ni walinzi kutokana na silaha walizozibeba katika migongo yao, Kamanda Amata alijaribu kutazama huku na kule hakuona daliliya mtu mwingine, hivyo alikwishahesabu kuwa upande wan je kulikuwa na watu watano na wote wana silaha. Hakujua kuhusu ndani ya majengo hayo.
Lengo lake lilikuwa ni kufanya uokozi usio na madhara, alimtaka Jamir tu aondoke naye, na alijua akimpata Jamir basi kazi itakuwa imekwisha kama sio kumalizika. Alihitaji kuingia ndani ya maghala yale lakini hakujua ni lipi hasa Jamir atakuwa amefungiwa, hakuyapa muda mawazo hayo, aliutazama mlango mkubwa ambao ulionekana umefungwa, na mwisho wa jengo lile refu kulikuwa na mlango mdogo ambao aliona yule dereva akiingia baada ya kuliacha lile lori lake maegeshoni. Kwa harakaharaka aliona ni kama mwendo wa mita mia mbili hamsini, na akikimbia ni kama robo dakika atakuwa ameufikia, lakini kulikuwa na taa zilizokuwa zikimulika eneo hilo, kazi ipo!
Hakukuwa na jinsi, alitazama wale jama walivyoketi, kisha kama kishada alichomoka na kukimbia bila kufanya ukelele lakini hakufanikiwa kufika katika ule mlango, akiwa katikati mlinzi mmoja upande wa uani ambako yeye Kamnda hakumuona tangu mwanzo alimbaini.
“Hey!!!” akaita.
Mwito huo ulimshtua Amata akatumia akili ya haraka sana badala ya kunyoosha anakokwenda, akakunja kona ya ghafla na kumfuata yule mlinzi alipo kwa maana alijua kuwa akipiga zaidi kelele zake itakuwa ni hatari kwake, aliruka hewani na miguu yake ikatua katika shingo ya yule mlinzi aliyekuwa akiandaa bunduki yake kumlenga Amata. Alimnasa kwa miguu na kushuka nae mpaka chini kwa utulivu, akambana sawasawa mpaka roho ikamtoka. Samahani sikutaka kukuua lakini imebidi, alimwambia kwa mawazo huku akimvuta taratibu mpaka chini ya gari bovu, akaitazama ile bunduki, itanisaidia akawaza, akachukua na koti la yule marehemu akajivika akaiweka bunduki mgongoni, sasa haikuwa na haja ya kukimbia, alitembea akiambaa na ukuta kuufuata ule mlango.
“Swaleh! Wapi unaenda?” mlinzi mwingine akauliza baada ya kumuona Amata akielekea kule mlangoni. Hakuoneasha wasiwasi wowote badala yake alichanganya miguu na kukimbia kwa mwendo wa taratibu huku akionesha ishara kuwa anaingia ndani atatoka muda si mrefu kwa kutumi mkono wake. Wale wenzake hawakuendelea kumfuatilia walimuacha aende. Kamanda Amata alipofika mlangoni na kuingia, kwenye korido nyembamba inayotokea ndani ya ghala hilo alikutana na yule dereva aliyekuwa akitoka wakati huo. Yule dereva akasimama akimwangalia mtu huyo.
“We huku vipi? Si mmeshaambiwa msiingia ndani kwa kuwa huku tayari kuna wengine!” yule dereva alizungumza. Kwa kauli hiyo Kamanda Amata akajua kuwa ndani kuna walinzi wengine, akatumia viganja vya mikono yake kumpiga kwa nguvu mabegani, yule dereva na jinsi alivyokonda alikosa nguvu ya kustahimili pigo hilo, alirudi nyuma kwa nguvu na kujibamiza ukutani, kabla hajatua chini alijikuta akitazamana na domo la bastola iliyoshikwa kikakamavu na mwanaume aliyesimama mbele yake. Mwili ulimtetemeka, midomo ikamchezacheza, hakuamini anachokiona, akifikiria jinsi eneo hilo linavyowekwa ulinzi na wale maharamia ambao kila wanapoteka meli, mali zote huhifadhiwa kwenye maghala haya. Mkono wa kushoto wa kamanda amata ukainuka na kuweka kidole cha shahada katika midomo yake akiwa anamwambia yule dereva kimya! Yule bwana alisimama kama sanamu huku taratibu mkojo ukimtoka na kulowesha suruali yake. Kamanda Amata akatazama kushoto na kulia hakuna mtu. Akamsogelea yule jamaa palepale alipo, akamkaba koo kwa kono lake la kushoto.
“Yuko wapi ndugu yangu mliyemteka?” akamwuliza, lakini yule jamaa hakuna alichojibu zaidi ya kuzidi kutetemeka, macho yake alikuwa akiyageuzia upande wa kushoto mara nyingi, Kamanda akaelewa kama huyo ndugu yake hayupo huko kushoto basi kuna hatari nyingine, kengele za hatari zikamuashiria hilo. Mara ghafla akajikuta akipigwa na kitu kutoka nyuma, kilitua kichwani kikafanikiwa kumchana ngozi ya kisogoni na kuruhusu damu kuvuja. Kwa kuwa aliyepiga hakuwa mzoefu hakuweza kutimiza alilokusudia. Kamanda Amata hakujali maumivu yake, aligeuka na kufyatua risasi na yule mtu akatupwa nyuma akaanguka chini kama mzigo akiwa hana uhai, alipogeuka tu alikutana uso kwa uso na mtu mwingine, alipotaka kufyatu risasi, ile bastola ilishikwa na kitu kama kamba au mnyororo ikamtoka na kuangukia chini. Hakupoteza muda, alimtemea mate yule jamaa, kwa ujinga wake akakwepa, konde moja zito likatua upande wa sikio, akayumba na kujishika sikio, Kamanda Amata akaruka na kujizungusha hewani, mguu wake ukatua sahavuni mwa yule bwana, akaanguka chini kama gunia la mashudu.
Kabla Kamanda hajajiweka sawa, yule bwana alinyanyuka haraka na kusimama akimkabili Amata, yule bwana alipanga mikono yake na kuiweka miguu katika mtindo wa kupendeza, moja kwa moja kichwani mwa Amata ikaonekana anataka pambano la mikono, hewaa nitakuonesha, Amata akajisemea huku naye akijiweka tayari. Yule bwana akaanza makeke, akarukaruka na kurusha mguu wake wa kulia juu akauzungusha kwa kasi na kuuteremsha katika mtindo unaojulikana kama axe kick , labda hakujua anapambana na mtu wa namna gani, Kamanda Amata alijua pigo hilo litatua wapi katika mwili wake, kwa haraka akainua mikono yake na kuiweka katika mtindo wa X, mguu wa yule bwana ukatua katikati ya mikono ile na papo hapo Amata akaubana ule mguu na kupiga teke moja kali lililotua kwenye korodani za yule jamaa, akalegea, Kamanda Amata akauzungusha ule mguu na kuushtua mifupa yake, yule bwana alishindwa kusimama na kujibwaga chini. Teke kali la usoni liliruhusu damu za yule bwana kutiririka na kumrudisha chini, Kamnda Amata alimuwahi na kumkanyaga kifuani, akachomoa bastola nyingine na kumuoneshea.
“Kuwa mpole,” akamwambia yule bwana aliyekuwa anataka kujikukurusha bila sababu, akatulia mbele ya domo hilo la bastola.
“Yuko wapi mtu wangu?” akauliza. Yule bwana akabaki kushangaa tu, hakuwa na la kujibu. Wakati huo huo aliskia michakacho ya miguu ya watu waliokuwa wakija ndani kutoka nje, akajiweka tayari, nukta hiyo hiyo, alimuona mmoja aliyeingia mlangoni na bunduki aina ya SMG, Kamanda Amata akajirusha upande wa pili na risasi zilizotoka kwenye bunduki hiyo zikachimba ukuta. Kamanda Amata alipotu akainua bastola yake iliyokuwa chini, sasa mikononi mwake zilikuwa bastola mbili, alijibiringisha chini na kutua kwa magoti, bila kuchelewa bastola yake ilikohoa na kumtumpa mbali yule askari aliyekuwa mlangoni, risasi ya pili ilipiga bega la yule aliyekuwa akipambana naye, naye akalala chini kimya. Kamanda Amata akamruka na kujibanza nyuma ya kitu kama kabati, akawasikia watu waliokuwa wakija wakikimbia.
“Upande huu,” mmoja alimwambia mwenzie.
“Hapana mimi nimesikia huku,” mwingine alijibu.
Kamanda Amata akatulia palepale akawa anaangalia watu hao ni upande gani watatokea, alipoona wanakuja wote wawili kutoka mbele akarudisha bastola moja kwenye kikoba chake na kubaki na moja. Mtu wa kwanza akapita, wa pili alipofika lile eneo, akamdaka kwa mkono mmoa na kumvuti nyuma ya lile kabati, akampiga kabala ya maana na kumuwekea bastola katika sikio lake, alihakikisha yule kijana hawezi hata kupiga kelele.
§§§§§
FASENDY alishtuka alipusikia mlio wa bastola, akatulia kusikiliza kwa makini, akasikia wa pili kisha watu wakiongea ongea akajua kumekucha, akajua mzee wa kazi ameingia, akainuka na kuanza kupiga push up kujiweka tayari kwa mapambano, alichemsha mwili. Kisha akachukua ile pete yake na kugongagonga ukutani kuongea na Jamir upande wa pili, aligonga gonga kama dakika moja na nusu hivi kisha akatulia.
Upande wa pili nao ukaanza kugongwagongwa, Fasendy akatega sikio na akili yake kusikiliza mlio huo hafifu kutokana na nguvu ndogo aliyokuwa akitumia Jamir kugonga.
…Kamanda Amata bila shaka ameshafika…
Ndivyo Fasendy alivyokuwa akimwambia Jamir kwa ule mtindo.
…Nimesikia milio ya risasi, lakini sina uwezo hata wa kutembea…
Akajibu Jamir, kisha kila mmoja akatulia kwenye selo yake akisubiri kuona kinachoendelea.
Fasendy aliuendea mlango wa kijichumba hicho alichofungiwa, akajaribu kupapasa na kukipata kitasa, akajaribu kukitikisa lakini kilikuwa kimefungwa sawia, hakuweza hata kuutikisa ule mlango. Akahama kwenda upande mwingine, akajikwaa kwenye kitu kama chuma na kuanguka chini, “Shenzy” akatukana na kumalizia na tusi la nguoni, akakivuta kile chuma kumbe kilikuwa ni kipande tu, akainuka nacho na kusogea karibu na ukuta, afanye nini, akili ikamzunguka.
…Jamir sogea mbali na huu ukuta…
Alitumi lile chuma kugongagonga ukuta kumpa ujumbe ule Jamir, ikawa hivyo. Kwa pigo moja la nguvu, Fasendy aliupiga ukuta kwa lile chuma na ule ukuta ukaonesha udhaifu, ulikuwa ni ukuta wa inchi tano tu, pigo la pili liliangusha vitofali kama vine hivi, pigo la tatu likashusha vingine kama vitano, pigo la tatu likatengeneza tundu la yeye kupita, mara ule mlango wa kile chumba ukafunguliwa. Fasendy kwa kutumia hisia tu, akajua hapa nimekwisha, akaruka kwa ustadi wa hali ya juu na kupenya kwenye lile tundu akadondokea chumba cha Jamir, Mungu si Athumani na wala Athumani si Mungu, Fasendy alikuwa ameruka na lile chuma mkononi mwake, alipotu sakafuni akajibiringa vizuri na kulirusha kwa nguvu lile chuma kulenga lile tundu.
Yule mlinzi alipoona Fasendy kapenya kwenye lile tundu aliamua kumfuata, alipomulika na tyochi yake na kujaribu kuchungungulia ndipo alipokutana nachuma hilo lenye tundu katikati, lilipiga usoni na kumsababishia maumivu makali. Yowe la uchungu lilimtoka na nukta hiyohiyo kama akili yao ilifanana, Fasendi alijirusha akatua kushoto mwa lile tundu akilipa mgongo na kuegemea ule ukuta kumbe na jinsi hiyohiyo Jamir alipata nguvu za ghafla na kujirusah akatua upande wa kulia wa tundu hilohilo akaketi vilevile kama Fasendy.

§§§§§§

Mlinzi mmoja alikuwa akihangaika kupiga simu ndani ya chumba kilichotumika kama ofisi, lakijni kila alipoweka sikioni kimya, kila aliporudia na kuweka sikio kimya, akaipiga chini ile simu alipogundua kuwa laini zote za simu zimekatwa, hakuna simu ya kutoka nje ya maghala hayo, alipogeuka tu alikutana na uso kwa uso na Kamanda Amata. Akajaribu kujichekesha, lakini akakuta uso wa Amata umedinda kwa hasira hakuna cheko wala tabasamu.
“Twende ukafungue,” akamuamuru yule mtu. Naye kwa haraka akachukua funguo na kutangulia mbele huku Kamanda Amata akiwa nyuma yake.
“Shamsiiiiii usifungueeee!!!” kelele ilitoka upande wa juu, Kamanda Amata akatazama kwa haraka na kujitupa mbele akampamia yule jamaa mwenye funguo wakaenda wote chini, akammnyang’anya funguo na kuzibana kwa meno, akachomoa kisu na kukirusha, kikampata yue jamaa kooni, akadondoka kutoka pale juu mpaka chini.
“Ingieni ingieni, yupo huku!” kelele ilitoka kwa chini, kamanda Amata alitazama harakaharaka akaona watu kadhaa wenye silaha wakiingia ndani ya ghala hilo, kasheshe. Kamanda Amata alipokuwa akiondoka, yule bwana aliyekuwa na funguo akamdaka mguu, Teke la kisigino likatua kwenye pua yake, akaguna na kumuachia, Amata akageuka na kumzabua tekea kali la uso, lililomdondosha toka juu mpaka chini.
“Yuko juu,” mmoja akasema.
“Aaaaaa anawafunguliaaa,” mwingine akajibu kisha wote wakaanza kupanda ngazi kuelekea kwenye ile njia ya chuma iliyojengwa juu. Kamanda Amata alifika mlango wa kwanza na kujaribu kufungua lakini ulikuwa haufunguki. Alipotazama mbele kulikuwa na milango kama mine hivi. Mara akasikia mlango mmoja ukigongwa kwa ndani, akajua ni huohuo akaukimbilia na kutumbukiza funguo, mlango ukajibu.
“Jamir, Jamir,” akaita.
“Kamanda Amata,” sauti ya Fasendy.
“Fasendy!,” naye akaita tena.
“Asante Kamanda, lakini Jamir hawezi kutembea kwa jinsi alivyonieleza,” Fasendy akasema.
“Yuko wapi Jamir?” akauliza.
“Huyu hapa.” Kamanda Amata akavua bunduki aliyokuwa ameipachika mgongoni mwake na kumpa Fasendy, “Haya mama, un trabajo,” akampigapiga mgongoni, kisha akmuendea Jamir aliyekuwa bado ameketi kuuegemea ukuta. Akamtazama lakini hakuweza kufanya lolote kwa wakati huo, maharamia sasa walikuwa wakikimbia kwenye ile njia ya chuma kuelekea kule waliko Amata na watu wake.
Fasendy akajitokeza mlangoni na kuiinua ile bunduki akaiweka sawa kwa kuiondoa usalama, akafyatua risasi mfululizo kuwaelekea wale jamaa, kelele za mayoe zikasikika wengine walijirusha chini bila kuambiwa wengine walianguka wakiwa hawana uhai, Fasendy alipoangalia chini, aliona bado kuna wengine, kazi ngumu.
“Kamanda, tutoroke hapa hapafai,” alimwambia Kamanda Amata kwa lugha ya Kiswahili ambayo wale maharamia walikuwa hawajui chochote. Alipotaka kutoka pale alipo kuja ndani alikomuwacha kamanda na Jamir, alirudi tena nje na kumfuata askari aliyelala chini bila uhai, akachomo bunduki lake kubwa na kutoroka nalo. Akaingia kwenye kile chumba akihema akamkabidhi Amata lile jibunduki. Kamanda alipolipokea, akatukana tusi la nguoni, akalipachika begani mwake, lilikuwa ni RPG 7, akalitegua na kulifyatua, lile grenade lake likafyatuka na kupiga ukuta ulio mbele yao likaacha tundu kubwa la kupita Suzuki.
“Fasendy twendeee!!!” Kamanda aliita kisha akamnyanyua Jamir na kutoka naye kwenye lile tundu, akajirusha mpaka chini, Fasendy naye akafanya vivyo hivyo. Kamanda Amata akachomoa bastola moja na kumpatia Jamir hata kama hakuwa na nguvu, ili mradi ajitetee kwa lolote.
§§§§§§
SIMU ya kitandani iliita kwa fujo, Shalabah akaamka na kutoa tusi baya, tusi lilikuwa likimlenga huyo anayepiga hiyo simu. Akainyanyua na kuiweka sikioni.
“Hello, Hello, Chieeef, Chiefff,” ilikuwa sauti ya mtu anayehongea kwa kihoro.
“Nini wewe ongea,” Shalabah akajibbu kwa ukali.
“Tumevamiwa Chief, tut u tume vvvamiwa, bandani!” yule mtu akasema.
Shalabah alijikuta anaishiwa nguvu, akasimama haraka akatoka kitandani na kuliendea kabati lake akafungua na kuto bastola mbili na shot gun moja akataka kutoka ndani.
“Wewe!” ilikuwa sauti ya mkewe ikitoka pale kitandani,” Shalabah akageuka na kumwangalia, “Sasa mbona unaondoka bila nguo?” akauliza mkewe.
Shalabah alipojiangalia, akajikuta kweli yuko uchi, kuchanganyikiwa! Akavaa nguo harakaharaka na kuchukua bunduki yake, unajua Somalia kila mtu anakaa na bunduki ndani, akatoka haraka na kuingia garini, akatoka kwa kasi kuelekea bandani. Njiani kote alikuwa akiuma meno kwa hasira, yaani huyu mshenzi kama ni embe nitamtafuna na maganda alijisemea huku akib akibadili gia na kuweka ile ya tano au mkoba kama mnavyoita vijana, akiwa katika barabara kubwa inayojulikana Alipishana na pikipiki kubwa iliyokuwa ikienda kwa kasi ya ajabu, akitazama harakaharaka na kuendelea na safari yake kwenda ghalani, kichwani mwake akiwa kagabhibika sana.
§§§§§§
DAR ES SALAAM ˜TANZANIA
KATIKA chumba kimoja maalum cha mawasiliano, ndani ya jengo la makao makuu ya JW pale Upanga kulikuwa mo jopo la watu takribani sita wa vyeo vya juu kabisa vya Jeshi la Wananchi, kati yao akiwemo Mkuu wa Jeshi la Wananchi Jenerali Kamsumi pamoja na msaidizi wake Brigedia Kyambasa na wengine wane wanaowafuatia kwa vyeo vya kijeshi, walikuwa mo pia wanajeshi wa vyeo vidog lakini sio vya kawaida, pamoja nao, wote walikuwa macho yao katika luninga kubwa iliyofungwa ukutani, pale waliweza kufuatilian operesheni iliyokuwa ikifanywa na Kamanda Amata kule Mogadishu.
TSA 2 alikuwa ndiye mtaalam wa kuunganisha mtambo huo na satellite ambayo iliweza kuwaonesha matukio yote kutokana na muunganiko kati ya ile satellite na ile chip aliyowekewa Amata mwilini mwake, waliweza kuona picha japo zilizofifia lakini bado waliweza kuona kinachoenndelea. Madam S alikuwa kimya kabia akifuatilia huku moyo wake ukiwa na kihoro ndani yake, aliona uzito wa kazi, akajua kweli Kijana wake ana kibarua.
“Eeeeeeeee!!!!!!! Safi sana Kamanda Amata,” ilikuwa ni sauti ya Brigedia Kamsumi aliyesimama ghafla na kushangilia huku akipiga kofi moja kuonesha ishara ya furaha na wengine nao walionekana kumuunga mkono kwa kupiga makofi kwa kazi nzuri alioionesha Kamanda Amata kwa kumuokoa Jamir. Dakika hiyo hiyo, saa ya Madam S ikamfinya kumpa ishara kuwa kuna mesej inaingia, akairuhusu nay o ikaanza kutoa mkanda wenye maandishi.
…Nimemuokoa Jamil lakini hali ni tete ninahitaji msaada…
Madam S alimtazama mkuu wa majeshi na kumpa ishara ya kumsikiliza, akamuonesha uole ujumbe. Yule mkuu hata bila kufuata utaratibu alisimama na kuwageukia wasaidizi wake, wakuu wa vikosi mbalimbali.
“Ndugu tunahitajina kutoa msaada wa haraka, Kamanda Anata ameomba, tunafanyje?” akauliza kwa kutupa swali kwa wasaidizi wake. Hakuchukua hata sekunde kumi, mwanajeshi mmoja mfupi aliyeshupaa alisimama akiwa amechafuka kwa vyeo mbalimbali vya kijeshi, alikuwa amevaa vazi la bluu bahari na kifuani mwake upande wa kushoto chini ya jina lake kulikuwa na picha kubwa ya chuma iliyoonesha alama ya bawa. Alikuwa ni mkuu wa kikosi cha wana anga cha JW.
“Naomba nipeleke tai wawili sasa hivi, ni saa moja tu watakuwa pale, wakatoa msaada wa haraka,” akalieleza jopo huku akivaa kofia yake iliyokuwa mezani muda wote.
“Sasa hiyo vita Kiongozi!” aliongea mwingine bila kujali utaratibu.
“Ndugu wajumbe Jamir ni komandoo wetu na Kamanda Amata sote tunajua kazi yake, Komandoo mmoja ni sawa na batalioni moja , Kamanda Amata akisema jambo lazima lipewe kipaumbele huwezi kujua ni kitu gani anachokabiliana nacho kwa sasa, hatuna budi kutoa uamuzi, Kiongozi fanya uwezalo,” Mkuu wa Majeshi akaruhusu kutumwa ndegevita mbili kwenda Somalia kusaidia operesheni.
§§§§§§
Wakati kikao hicho kikiendelea hali ilikuwa si shwari kwa katika ubalozi wa Somalia, pamoja na kupokea pesa nyingi sana kutokana na biashara ile haramu, Balozi wa Somalia alijipanga kuondoka usiku huo huo, akijua kwamba akisubiri sana itakuwa ni jambo la aibu kuzuiliwa kuondoka nkatika nchi ya ugeni. Alipopewa habari na Waziri wa ulinzi juu ya sakata au opereshani inayoendelea, hakuona haja ya kupoteza muda, maadam alikuwa na uwezo wa kuondoka na usafiri wowote anaotaka, aliamua kuondoka usiku huo huo.
Askari kanzu wa kitengo cha usalama wa Taifa walikuwa wametawanywa kuchunga baadhi ya watu wanaotuhumiwa kwa sakata hilo la hujuma, kila mmoja alitakiwa kuhakikisha mtu aliyepewa kumwangalia asimpotee hata nukta moja na taarifa kila baada ya dakika kumi azitoe katika ofisi ya Usalama wa Taifa. Ulikuwa ni usiku wa aina yake, wenyewe wakiwa wamelala na wake zao wakikenua kwa sababu pesa nyingi zimewafikia siku hiyo na kujaza vitabu vyao vya benki hawakujua kabisa mbilinge lililopo huko nje linalowasubiri pindi tu amri ikitolewa. Hawakuju kama wamepewa ulinzi huo usio rasmi, mwingine aliwaza kununua Vogue, mwingine kujenga hoteli, yule kule kuhamia USA na huyu huku kuongea wake wawili wanafunzi wa sekondari, kila mmoja aliwaza tu atatumiaje pesa hizo.CHANZO : Deusdedit Mahunda
Gina aliinua mkono wake na kusoma saa, ilimuonesha inakimbilia saa saba za usiku, aliendelea kutuli palepale katika barabara ya Sea View akihakikisha anaitazama nyumba ya Balozi wa Somalia, akihakikisha kuwa mtu huyo bado yuko ndani na asiondoke usiku huo, akiwa katika hali hiyo, akaona lango la mbele likifunguliwa na gari moja nyeusi, Marcedes Benz ilitokeza pua yake ikiwa imewasha taa, ikawasha indiketa za kulia na kuingia barabarani kuelekea mjini. Gina akaitazama kwa chati na kuona mtu aliyetuna katika kiti cha nyuma, mara simu yake ikaita, akaichomoa na kuiweka sikioni.
“Ametoka na gari…” ilikuwa sauti iliyotoka kwenye ile simu na kuingia katika sikio la Gina, sauti ya mlinzi wa mlangoni katika nyumba ya balozi, mlinzi wa kampuni binafsi lakini ilhali ni mtu wa idara ya Usalama wa Taifa. Gina aliingia garini na kuondoka kuifuatilia ile gari taratibu, ilipita barabara ya Ocean Road na kuifuata mpaka Magogoni, ilipanda na barabara ya Kivukoni mpaka ikatokea katika kituo cha boti za kwenda Zanzibar, ile gari ikateremka chini kuifuata hiyo barabara na kusimama mbele ya mlango mkubwa. Yule Balozi akateremka, alikuwa peke yake, pale akapokelewa na mtu mwingine mwenye asili ya Kiarabu au Kizanzibari akaingia naye ndani.
Gina alipiegesha gari yake mbele kidogo ya eneo hilo karibu kabisa na nji ya kuingilia ofisi za NASACO, akateremka na kuruka ukuta mfupi ulikuwa eneo hilo akapita kwa uangali bila kufanya kelele mpka eneo ambalo aliweza kuona japo kwa mbali kinachoendelea. Alimuona yule Balozi akteremka ngazi akiongozwa na yule bwana aliyempokea mpka kwenye boti moja ya kifahari iliyokuwa imeegeshwa hapo gatini, wakaagana na yule bwana kisha akaingia katika boti na dakika tatu zilizofuata ile boti ikaondoka kwa kasi. Gina aliitazama mpaka ilipopotelea katika giza la usiku katikati ya bahari, akatoka na kurudi katika gari yake, akaketi nyuma ya usukani, akavua miwani aliyokuwa ameivaa na kufyatua kioo kimoja cha miwani hiyo, akachomo memory card ndogo na kuipachika katika kishikio chake kisha akaingiza mahali Fulani kwenye dashboard, akabofya mahala Fulani na ikafyatuka luninga ndogo ya inchi saba akatazama picha alizokuwa akipiga kwa kutumia miwani hiyo, picha huyo Balozi akiwa pale bandari ndogo, aliitazama picha ya yule bwana aliyekuwa akiagana naye ambaye ndiye aliyempokea, akasoma maandishi ya nyuma ya boti ile yaliyochongwa kwa chuma nyuma yake ‘Sea Cruiser’ ya kiafuataiwa na namba ya usajili. Alipojiridhisha na kila kitu akaondoa gari uake huku akimpa taarifa Madam S kuwa Balozi ametoroka.
MOGADISHU – SOMALIA
FASENDY alimpa chupa ya maji Jamir, akayachukua na kuyanywa kwa fujo, kisha Kamanda Amata akatoa aina Fulani ya vidonge viwili akampa kula, akimwambia asivitafune ameze moja kwa moja. Dakika tano baadaye hali ya Jamir ilianza kurudi, nguvu ziliznza kumrudia, vile vidonnge vilivyokua na mchanganyiko wa vitamin zote na glucose kwa kiwango cha juu. Jamir alisimama japo hakikuwa kwa nguvu ileile lakini alifanikiwa.
“Unajisikiaje?” Kamanda aliuliza.
“Kidogo afadhali, hata naweza kusimama, maana wale jamaa sijui walitaka niweje japo najua walipanga kunikata kichwa asubuhi inayokuja,” Jamir akalekeza. Kamanda Amata akasonya, “Wakakate vichwa vya ndugu zao,” akamaliza kwa maneno hayo. Akamtambulisha kwa Fasendy harakaharaka. Kisha akawaeleza kwa kifupi juu ya yule mwanamke mateka aliyemfunga kamba ambaye alimhifadhi kwenye kile chumba kidogo.
“Tusipoteze muda Kamanda, sasa tunafanya nini?” Jamir akauliza.
“Sasa ni kuvamia ngome yao kuu, nataka tukawaokoe wale wengine ishirini na tano lakinisijui walipo wala huyu (akamuoneshea Fasendy) naye hajui walipo,” Kamanda akaeleza.
“Kamanda, hawa jamaa wamehifadhiwa ndani ya chumba maalum katika bandari ya zamani ya Mogadishu, sasa shida tutaingiaje?” jamir alitoa jibu.
“Mimi nilishawahi kuingia, lakini nilitumia njia ya bahari, nilipiga mbizi na kupitua kwenye bomba kubwa la kutoa na kuingiza maji katika eneo la chini la bandari hiyo,” kamanda alieleza.
“Na hiyo ndo njia pekee salama ya kupita, kuna milango mikubwa mitatu, Kusini kuna mmoja ambao ukiingia unatokea gatini, Kaskazini nako upo mwingine ambao ukiingia unatokea eneo la kuegesha magari ambalo mbele yake kuna majengo yaliyokuwa ofisi na kupitia hapo unaweza kuteremka kwenda chini, njia zote zina ulinzi mkali sana, zinalindwa na watu wasiomjua Mungu ambao kuua kwao ni sherehe,” Fasendy akaeleza. Wote watatu wakatazamana.
“Tungeweza kupita kwa njia hiyo ya kupiga mbizi, lakini vifaa sasa tutapataje,” Jamir akaonesha mashaka kwa hilo. Bado ilikuwa kitendawili, Kamanda Amata alitazama saa yake ilikuwa tayari inakimbilia saa saba za usiku.
“Aaa Kamanda nimekumbuka, kule bandari mpya kuna kitengo cha wapiga mbizi unaonaje tukienda kuazima vifaa?” Fasendy akatoa wazo, Jamir akamwangalia mwanamke yule aliyeshupaa misuli utafikiri mwanaume mnnyanyua vyuma.
“Tukaazime usiku huu?” Jamir akauliza.
“No, yaani tukaazime, tuchukue hivyo vifaa kwa njia yoyote ile, tena naomba tuharakishe kabla ya alfajiri tumalize hii kazi,” Kamanda Amata akasema hayo na kuaharakisha kutoka mle ndani.
“Watakuwa wanatusaka, hivyo tutumie miguu, sio mbali kutoka hapa, nitawaonesha njia ya siri,” Fasendy alieleza kisha akatangulia kutoka na Jamir akafuata na Kamanda Amata akawa nyuma na bastola yake mkononi kulinda usalama. Walizunguka nyuma ya gofu lile na kuteremkia bondeni, wakapita kwenye mikoko na kuambaa na uoto huo mpaka eneo lililokuwa na ukuta ambao uliwezekana kupandika kiurahisi, Fasendy akawaonesha ishara ya kukwea ukuta huo, yeye mwenyewe akawa kwanza kuukwea akifuatiwa na Jamir na baadae Kamanda Amata kisha wote wakatua ndani kwa utulivu, kwa kujificha ficha katika malori ya mafuta yaliyoegeshwa hapo, walipenya na kufanikiwa kufika eneo husika. Kulikuwa na walinzi watatu waliokuwa wakizunguka eneo hilo.
Kamanda Amata akasogea mbele kabisa na kuwatazama wale walinzi jinsi walivyojipanga, akaonesha ishara ya vidole kumuonesha Faendy amtwae mmoja na Jamir amtwae wa pili yeye atamtwaa wa tatu, aliwapa maelekezo kwa mkono wasiue watu wasio na hatia bali wawalaze usingizi wa maana, alipoonesha ishara ya kuruhusu tu, kila mmoja allichomoka alipo na kupiga pigo moja kali kwa watu hao nao wote wakaanguka chini kila mmoja kwa sekunde yake. Kamanda Amata akautazama ule mlango, ulikuwa ni mlango wa chuma, uliofungwa madhubuti kabisa, akamwambia Fasendy na Jamir waangalie usalama huku na huko, pembeni kulikuwa na Fork Lift, mashine ya kuinulia mizigo mizito, akaingia na kuiwasha, nayo haikuwa na hiana hata kama operetta haimjui, akaisogeza taratibu mpaka kwenye ule mlango, akachomeka yale meno uvunguni na kuanza kunyanyua, sekunde thelethini tu ule mlango ulikuwa chini.
Wakatulia kidogo, hakukua na lolote, wakaingia ndani ya chumba hicho, hakika Fasendy hakuwaongopea, walikuta vifaa vya kuogelea vingi vya kutosha, wakachagua na kujibebea kisha wakatoka na kutokomea kizani bila walinzi wan je kujua kinachoendelea ndani.
§§§§§§
Meli kubwa ya mizigo ilikuwa ikisogea taratibu katika bandari ya zamani ya Mogadishu, juu yake kwenye deki ya mbele kulikuwa na watu kama kumi wenye silaha kali wakiwa wamesimama kila mmoja alikuwa akiangalia upande wake. Walikuwa ni Maharamia wa Somalia wakiiongoza meli hiyo kuingia katika gati hilo huku wenzao wa pale bandarini wakifuarahia kwa kupiga risasi hewani kama watu waliorukwa na akili.
Ile meli ilisogea taratibu sana huku ikisindikizwa na boti mbili ndogo, moja kila upande.
“Iweke upande upande karibu na gati kuu,” ilikuwa sauti ya Hussein ikiongea kwenye simu ya upepo. Akatoka na kumwita kijana mmoja.
“Sikia, sasa naomba uweke ulinzi wa kutosha hapa na ulinde kila kona maana sasa ndio tunafanya kazi,” Hussein akamwambia yule kijana, kabla hajamaliza simu yake iliita, akaichomoa na kuiweka sikioni.
“Chief nipe habari, mbona unachelewa huku bandarini?” akaijibu simu na kumtupia swali.
“Hussein, huku ni maafa, yule mshenzi kaondoka na mateka wetu na ametupotezea wapiganaji kama saba hivi,” Shalabah alimpa ujumbe huo Hussein. Simu ikawa nzito haikuweza kukaa sikioni tena, Hussein akahisi kuingiwa na ganzi ya miguu. Mh, safari hii tumepatikana akajiwazia hukua akiwa mpole ghafla.
Ile meli kubwa iliyoandikwa maneno PARPADOS ubavuni mwake, ikasimama gatini kabisa na kufungua mlango wake wa nyuma. Wafanya kazi walikuwa wametingwa kuanza kupanga vitu ndani ya meli hiyo ambayo ilitakiwa ing’oe namnga usiku huohuo isionekane kama ilikuwa eneo hilo. Huseein akaingia kwenye lifti na kushuka mpaka chini ambako shughuli zilikuwa zikiendelea za kuyafungua yale makombora ili kuanza kuyapakia katika ile meli.
§§§§§
Kamanda Amata, Fasendy na Jamir walijitosa ndani ya maji na kupiga mbizi maridadi, kisha wakajivuta kuelekea lile eneo walilokusudia, Kamanda Amata, alikuwa mbele na wengine hao walikuwa wakimfuata, aliufikia ule ukuta uliojengwa ndani ya maji akapapasa na kuufuata kuelekea lile tundu alilopitia siku alipokuja huko chini. Alipofika pale hakuamini anachokiona, lile tundu lilikuwa limefungwa kabisa, akatikisa kichwa kisha akawaonesha ishara wenzake kuwa watafute njia nyingine kuweza kufika ndani ya jengo walitakalo. Kamanda Amata akazunguka mpaka kule kwenye lango kubwa alilojaribu kukata mnyororo na kufuili lake lakini nako alishangaa kuona kumefungwa upya na madhubuti zaidi, akaona kuwa siku hiyo hana ujanja mwingine wa kuingia kwenye ngome hiyo, waliendelea kutalii. Walipozunguka upande wa pili ndiko walikoona kile ambacho hawakukitarajia au hawakukijua, mkuku wa meli kubwa iliyosimama gatini, Fasendy akamuonesha ishara Kamanda Amata kuwa waifuate, kisha yeye akajigeuza ndani ya maji kwa jinzi ya kuoendeza.

Dakika kadhaa waliifikia ile meli kubwa, Kamanda Amata akiwa ndani ya maji aliweza kuona mianga tu ya taa za huko nje na si zaidi, akawatazama wenzake akakuta nao wanamtazama yeye, akawapa ishara ya kuikwea ile meli pale ilipo, akatangulia yeye. Pembeni mwa meli ile kulikuwa na ngazi ya chuma inayopanda kwenda juu, akaikamata na kuikwea taratibu, kichwa chake kikajitokeza nje ya maji akatazama akaona kila mmoja alikuwa bize na shughuli yake, akakwea harakaharaka na kufika juu ambako alijitupia na kudondokea kwenye magunia yaliyopangwa eneo hilo la meli, akatulia kimya. Dakika moja baadae, Jamir alikuwa juu, Kamanda akampa ishara ya kuingia na akmuonesha mahali pa kujibana ili asionekane na watu hao. Fasendy naye akafika, akapewa ishara akaifuata. Wote watatu sasa walikuwa ndani ya deki la meli ile, wakiangalia kila kinachoendelea, wakagawana sehemu za kutega, kila mmoja akavua ile mitungi ya gesi na kubaki na nguo za kawaida. Kamanda Amata alikuwa akifikiri watateremka vipi kule chini ili kuweza kuingia ndani ya himaya ile, himaya ya Maharamia wasiosikia la muhazini wala mnadi sala.
Kamanda Amata hakuona haja ya kupoteza muda, alinyata taratibu na kumuendea Fasendy, “Tunahitaji silaha,” akamnong’oneza, kisha akamwendea Jamir na kumpa ujumbe ule ule, wakajiweka tayari na kupanda juu, akawapa ishara na wote wakapanda kwa kasi ngazi za kwenda juu. Jamir alipoibuka mlangoni tu alikuta uso kwa uso na mtu mmoja aliyekuwa na nia ya kuteremka kule kwenye deki, alimkumba kwa nguvu na kumtupa nyuma, yule kijana aliposimama tu alichezea makonde manne ya maana akarudi ndani, Jamir akajirusha kwa uzuri sarakasi moja matata sana na alipotu mguu wake ukatua tumboni mwa yule mtu, akatoa mguno hafifu wa maumivu, akatulia kimya. Jamir aliivuta bunduki aina ya Sot Gun aliyokuwa nayo mkononi yule mtu, akajivuta mbele kidogo na kutazama huku na kule, hakuna mtu, kisha akatoka mpaka kwenye deki na kumpa ile bunduki Fasendy, yeye akabaki na bastola alipewa na Kamanda Amata.

ITAENDELEA
1.jpeg
 
Mkuu utaimalizia maana ukituonyesha kava la kitabu inamaanisha tununue je ukimalizia raia tutanunua kweli?
 
Simulizi : Hujuma
Sehemu Ya Tano (5)
“Sasa tunavamia, Fasendy utatangulia kwa sababu bunduki yako inaweza kupiga risasi mfululizo, mimi na Jamir tunakuja, tutatumia kamba hiyo hapo juu mpaka paleleee (akaonesha kwa vidole), pale tutajiachi na kufikia kwenye yale magunia kisha kila mtu atachukua nafasi yake, lakini wakati tunashuka Fasendy utakuwa ukipiga risasi kila unayemtaka ili kuwachanganya hawa Maharamia,” Kamanda Amata akatoa maelekezo na wote wakaitikia, Fasend alruka na kuidaka kamba kwa mkono wake mmoja huku ule mwingie ukifyatua risasi kuwalenga wale jamaa, Jamir na Kamanda nao wakafuatia. Watu waliokuwa katika shughulia hiyo waliacha shughuli zao na kukimbia kimbia huku na huko.
“Tumeavamiwaaaaa, tumevamiwaaaa,” kijana mmoja alikuwa akipiga kelele bila mpangilio. Kamanda Alijirusha na kutua kwa miguu yake miwili, mtu wa kwanza kuvaana naye alikuwa na bunduki kubwa mgongoni mwake, akampiga kikumbo na yule mtu akaanguka chini chali, alipotaka kujaribu kuinuka alijikuta akipigwa ngwala moja maridadi na kurudi chini kama mzigo, akachomoa bastola kwa haraka akiwa pale chini, akachelewa kwani risasi ya Jamil ilishafumua kichwa chake, Kamanda Amata akaichuku ile bunduki na kujibana sawia nyuma ya maboksi mengi yaliyozagaa katika lile eneo, alipotazama huku na kule alimuona Jamir aliyeshika bunduki yake kwa umakini kabisa lakini hakumuona Fasendy.
Maharamia wakatoka walikokuwako na kuanza msako wakiwa na silaha nzito nzito.

§§§§§


Gari ya Shalabah iliingia kwa fujo katika eneo la bandari, na nyuma yake alikuwa akifuatwa na Land cruiser iliyobeba wapiganaji wenye silaha. Shalabah akashuka, kwa mwendo wa nusu kukimbia na nusu kutembea alikutana na Hussein mlangoni akiwapanga vijana wake kumsaka Kamanda Amata.
“Hussein,” Shalabah akaita.
“Chief, huyu jamaa katuweza, lakini tutamtia mikononi,” Husseina alimwambia Shalabah.
“Ila ukumbuke wako watatu,” Shalabah akatoa onyo.
“Hatuna muda wa kupoteza ni kumsaka, Mr. Lonely hatotuelewa kama tutashindwa kuwadhibiti watu watatu tu, wakati sisi tuna jeshi kubwa la kutosha,”Hussein alikuwa akimwambia Shalaba.
Mlipuko mkubwa ukasikika upande wa pili, harufu ya baruti ikatapakaa. Shalabah akamwamcha Hussein, akiwa na shotgun mkononi mwake alifungua mlango na kutokea huko kwenye mapambano, alichanganyikiwa alipoona jinsi Kamnada Amata na Jamir wanavyowadhibiti viumbe hao.
§§§§§
“Endelea kudhibiti eneo mi nakwenda kuwatafuta wengine,” Kamanda akamwambia Jamir kisha yeye akahamia upande mwingine akiwaacha wake Maharamia wakiapambana na Jamir, Komandoo mwenye hasira kutoka Tanzania.
Kamanda Amata alteremka ngazi kwenda chini, akiwa kwenye ngazi, alijikuta akipamiwa nyuma yake, alisukumwa kwa mbele na kujibamiza katika ukuta, alipogeuka kumwangangalia ni nani, alipata konde moja kali lililotua shavuni, akayumba kidogo na kumwangalia vizuri mtu huyo aliyemchapa konde hilo. Konde la tatu kutoka kwa yule mtu halikumpata Kamanda, alilipangua kiufundi kwa kuudaka mkono wa huyo mtu kisha akageuka nao na kuuweka begani akauvuta kwa nguvu na kuvunja mifupa. Yule bwana akalia kwa uchungu. Kamanda Amata akageuka na kumchapa makonde ya maana mpaka yule bwana akalala chini kwa utulivu. Kamanda Amata akaendelea kushuka chini.
§§§§§
Ndani ya chumba kikubwa sana kisichokuwa na kitu, kulikuwa na watu kama thelathini hivi wakiwa wamewekwa pamoja, hakukuwa na kiti, wala kitanda, walikuwa wamewekwa tu kama watu waliopo mahabusu. Kati yao kulikuwa na Watanzania ishirini waliotekwa na Maharamia, walikuwa wametulia kimya kabisa, wengine wakicheza karata kupoteza mawazo na wengine wakicheza drafti. Chumba hicho kilichoko chini ya ghala la bandari kilitumika zamani kama stoo ya kuhifadhia vipuli vya meli lakini baada ya kujengwa bandari mpy pale Mogadishu na kuhamisha kila kitu, Maharamia hao walijibinafsishia eneo hilo, hakuna aliyewauliza kwa sababu ndani yao kulikuwa na sauti za wanene. Walihodhi eneo lote hilo, na ukionekana kulifuatilia siku inayofuata ungeamka bila pumzi.
Mmoja wa wale mateka, mwanajeshi wa jeshi la maji wa Tanzania, alishtuka ghafla kutoka usingizini na kuwakuta wenzake ambao walikuwa wakicheza drafti wakiwa wanaendelea na mchezo wao, hawakuwa na usingizi wala hamu ya kulala, kila mmoja aliwaza hatima yao isiyojulikana.
“We vipi, mbona unshtua wenzako?” mmoja akmwuliza.
“Tulieni,” akawaambia huku akiwaoneshea kidole juu kuwapa ishara ya kutega sikio.
“Nini? Kuna nini?” mwingine aliuliza.
“Sikilizeni,” aliendelea kuwasisitizia. Wote walitulia lakini hakuna walichokisikia.
“Ah, achana nae huyo ameshanchanganyikiwa,” mwingine aliyestuka usingizini akajibu kutoka kona ya chumba hicho.
“Oya, sikilizeni AK-47 inavyolalamika huko, kimenuka!” akawaeleza mara hii akiwa amesimama wima.
Mabishano ya milio ya bunduki ilianza kusikika kwa ukaribu, wote walinyanyuka, hakuna aliyelala tena, walijua wazi kwa jinsi sauti zile za milipuko ya risasi zilivyokaribia eneo ambalo wapo wao, kwa vyovyote ni vita ya ukombozi.
§§§§§§
Kamanda Amata aliruka kwenye ngazi na kutua katika mwimo wa ngazi hiyo na kuserereka nayo kuja chini huku mkononi mwake AK-47 ikilalama na kufumua mtu mmoja baada ya mwingine.
“Yuko huku!!!” jamaa mmoja aliita kwa nguvu na wenzake waliokuwa juu wakaanza kuteremka chini kumfuata Amata, lakini walijikuta wanagonga ukuta baada kukutana uso kwa uso na Fasendy aliyekuwa amekamata bunduki kubwa aina ya SCAR H (Special operation Combart Assault Rifle), bunduki ya Kibelgiji, alianza kumwaga njugu na kuwarudisha nyuma wale vijana.
“Rudini msijeee!!!” mwingine aliwazuia wenzake.
“Kamanda, songa mbele,” Fasendy alipiga kelele huku akirudio juu.
Wakati yote hayo yakiendelea, Jamir alikuwa amefunga kazi katika upande wa juu, na alijificha mahala ili aone kama kuna yeyote atakayeleta shida, mkononi mwake alitulia na SMG (SubMachine Gun. Eneo lote lilidhibitiwa na watu watatu waliojipanga vyema.
Fasendy, alikuwa akitembea kwa kunyata kuelekea kwenye ujia mrefu upande wake wa kushoto, huku bunduki yake ikiwa makini mkononi mwake. Mara ghafla alisikia mchakacho wa miguu nyuma yake alipogeuka tu, alikutana na konde zito liliuchana mdomo wake wa chini, akatoa yowe la maumivu. Kabla hajajiweka sawa, konde lingine lilitua shavuni, akajaribu kujitetea mbele ya mtu huyo, lakini ikawa ngumu, alipigwa teke la nyuma ya magoti akajikuta akiiga magoti, na bunduki ikimtoka huku akiachia risasi mfululizo.
“Mshenzi sana we mwanamke, umetugeuka siyo?” ilikuwa ni sauti ya Shalabah, aliyekuwa akiongea huku akimzunguka kusimama mbele yake.
“Nani amewasaliti?” Fasendy akauliza.
“Hujui siyo? Sasa utajua leo, na huyo mwanaume wako huko alikoenda ndiko liliko kaburi lake, hapa hatoki mtu,” Shalabah akajibu.
“Hata wewe hutoki kama ni hivyo,” Fasendy alijibu kijeuri huku damu zikimvuja katika mdomo wake wajuu uliochanika kwa konde la Shalabah.
“Sema mko wangapi?” Shalabah akauliza.
“Hata ukiniua, sintosema Abadan!” Fasendy alijibu kijeuri.
“Unajifanya jeuri sio?” Shalabah alimwambia na kumshushia kipigo cha nguvu, Fasendy hakuonesha makeke yoyote katika hilo alitulia na kujibwaga chini. Kutoka pale chini Lijizungusha kwa kasi na kumchota ngwala Shalabah, lakini Shalabah alikuwa mwepesi na kujigeuza hewani, kisha akatua kwa miguu yake.
“Fasendy, tulipokuwa jeshini mimi nilikuwa mkufunzi wako, tangu lini mwanafunzi akamshinda mwalimu?” Shalabah alijisifu.

§§§§§§


Jamir alisikia mabishano hayo ya Shalabah na Fasendy, taratibu akajitoa katika maficho yake akipiga hatua kusogea kule watu hao wanakoongea, kwa kuwa alikuwa akielewa kwa kiasi Fulani lugha ile, alijua Fasendy yuko matatani, hawakuwa na njia ya mawasiliano katika yao watatu, kila mmoja alipigana na kuwasiliana na mwenzake kwa hisia. Jamir alimuona Shalabah lakini kabla hajafanya lolote Shalabah alihisi uwepo wa mtu mwingine, akachomo bunduki yake na kufyatua risasi upande aliokuwa Jamir.
“Aaaaaaaiiigggghhhh!!!!!” sauti ya mamumivu ya Jamir ilisikika huku akijirusha upande wa pili na kujificha nyuma ya ukuta mwingine.
“Jamiiiiiiirrrrrrrrrrr!!!!!!” Fasendy alipiga ukelele baada ya jamir kuruka upande wa pili huku akitoa yowe la maumivu.
“Umemuumiza Jamir!!!” Fasendy alimpigia kelele Shalabah, lakini alizimwa na kofi kali la shavuni.
“Ndio, nab ado naenda kummalizia kabisa,” Shalabah akamuacha Fasendy pale chini na kukimbilia kwa Jamir, alipofika pale alipoangukia Jamir, hakumuona. Akabaki kapigwa na butwaa, si aliangukia hapa! Akashangaa, hakujua ni vipi au ni wapi jamir katorokea ilhali alikuwa kampiga risasi.
“Shiiitttt!!!” akapiga kelele na kugeuka kurudi kwa Fasendy, nako akapigwa na butwaa la mwaka Fasendy hayupo pale alipomuacha, hawa ni masehetani au binaadamu? Akajiuliza bila jibu, akatazama huku na kule akaelekea kwenye tundu kubwa la dirisha na kumuona Fasendy akiwa chini kabisa, akainua bunduki yake na kufyatua kumlenga, akachelewa, Fasendy alikwishaingia chini ya lile jengo na kushika ngazi za kuteremkia bondeni.
Shalabah akateremka kwa kasi kwenda chini huku bunduki yake ikiwa mkononi mwake, akainua simu yake ya upepo.
“Hussein, wasitoke hao, wanataka kutoroka nimewadhibiti vya kutosha, hawatuwezi,” Shalabah alimwambia Huseein kibonge cha mtu alipokuwa akishuka ngazi kwenda chini, lakini alishangaa sana kuona hajibiwi akaita tena na tena.
§§§§§
Kamanda Amata alijikuta akipigwa na kitako cha bunduki, kilimpiga chini kidogo ya shingo akhisi maumivu kwenye uti wa mgongo, aligeuka na konde zito, lililompeleka chini huyo aliyefanya kiotendo hicho, hakumsubuiri aamke, teke kali la usoni lilimgeuza upande wa pili na kumvunja mwamba wa pua, damu na makamasi vilivuja kwa pamoja.
“Funguo zikowapi?” akamwuliza huku akimfuata, yule jamaa akawa anasota kinyumenyume huku akionesha mkono ndani ya kiofisi Fulani kilichokuwa hapo jirani. Ilioneka ndiye alikuwa mtunza chumba hicho. Kamanda Amata akaingia ndani ya kile kiofisi kwa kurukia miguu miwili na kuutawanya mlango wote, akavuta droo na kuchukua fungu la funguo, akatoka nalo na kujaribu kila inayowezekana kufungua mlango huo, funguo ya tano ilikubali kuufungua, ukafunguka, lakini chumba kilikuwa cheupe hakina mtu, akamgeukia yule jamaa pale nyuma, akakuta hayupo akamuona akimaliziki kwenye kona Fulani ya ujia katika jengo hilo, shabaha madhubuti ndani ya sekunde mbili alimvunja mguu yule bwana akajibwaga chini kama mzigo. Akamuwahi pale pale na kumkamata ukosi wa shati lake.
“Unanifanya mimi bwege sio?” Akamuuliza, huku akimburuza na kurudi naye mpaka pale, “Chumba kikowapi?” akamtupia swali linguine. Yule jamaa alikuwa akiugulia mguu na pua yake.
“Sema haraka, sina muda wa kupoteza,” Kamanda alipiga kelele, akamgeuza chali na kumtumbukiza domo la bastola kinywani mwake, yule bwana akapiga kelele za woga huku macho yakiwa yamemtoka pima.
“Nasema, nnna ssssema!” alibwabwaja, Kamanda akatoa ile bastola, “Malango wa pili kwa ndani kushoto.”
Kamanda akamsonya na kumchapa kofi kisha akaingia ndani ya kile chumba na kukuta mlango mwingine, uliokuwa ukigongwa kutokea ndani lakini sauti hafifu sana ilikuwa ikitoka hapo kwani mlango ulikuwa ni wa chuma kizito. Akatumbukiza funguo na kufanikiwa kuufungua ule mlango.


§§§§§


Hussein alikuwa hajui afanye nini, alikuwa ndani ya chumba cha yale makombora na watu wachache pamoja nao, katika ile manowari kubwa ya JW waliyoiteka, ilikuwa imewekwa mahali maalum ambapo ukija kwa nje huwezi kuiona, kwani walikuwa wameizamisha chini ya bahari na kuifungi kwenye ghala yao iliyopo huko, ghala hiyo ilikuwa na uwezo wa kujazwa maji na kuwa kavu kadiri wanavyoamua wao. Alipokuja Kamanda Amata alikuta imejaa maji yote, lakini wakati wakiwa tayari kuyaondoa yale makombora kulikuwa hakuna hata tone la maji. Tayari makombora mawili yalikwisha ondolewa pale na kuingizwa kwenye ile PARPADOS, meli kubwa iliyoegeshwa nje.
Hussein, mtu mnene asiye na shindo kwa jinsi alivyonenepa, alikuwa kachanganyikiwa kiasi Fulani. Mkono akiwa kakamata shotgun na wale vija aliokuwa nao wote walikuwa wamekamata silaha za aina mbalimbali.
“Lazima atakuja huku mbuzi huyu, ni kuutoboa mwili wake kwa risasi mpaka huwe chandarua,” aliwaambia wale vijana na wote wakaziweka tayari bunduki zao.
Akainua redio yake, ambayo wakati inaongea hakujibu lolote, “Shalabah niko huku chamber, namsubiri huyo mbuzi afike nimmalize,” akamwambia Shalabah.
Kisha akawageukia wale vijana wake, “Mko tayari?”
“Yes Boss,” walijibu lakini walionekana wazi kutetemeka, waliona kama sinema inayotukia hapo, na wao wakiwa ni wamoja wa wachezaji sinema hiyo.

§§§§§§

DAR ES SALAAM – TANZANIA
MADAM S aliirudisha simu yake katika mkoba wake mara baada ya kupata taarifa ya kutoroka kwa Balozi wa Somalia. Akasimama na kuliaga jopo la wanausalama waliopo pale. Chiba alibaki kuangalia mawasiliano kama yanaenda vyema.
Madam S akatoka nje ya jengo la makao makuu ya jeshi, ilikuwa imetimu saa nane za usiku. Akachukua simu yake akabofya namba Fulani na kuiweka sikioni.
“Scoba, nahitaji helkopta haraka sana, inabidi tufike visiwa vya Zanzibar bila kuchelewa,” akaongea na simu hile.
“Umesomeka Madam, Uwanja wa ndege wa jeshi tafadhali kikosi namba KJ 603, haraka,” Scoba akajibu simu ile na kisha kujiandaa kwa safari. Alikwishaambiwa kuwa kwa muda huo wote ahakikishe anakuwa ndani ya eneo hilo la uwanja wa ndege wa Jeshi kwani anaweza kupata taarifa yoyote na ndivyo ilivyokuwa.
Madam S alikuwa katika mwendo wa kasi kuelekea Uwanja wa ndege na wakati huohuo, Gina naye alikuwa katika barabara hiyo kuelekea Uwanja wa ndege.
Wote wakaingia pale kwa tofauti ya dakika moja na sekunde kumi na tano, walikuta Scoba tayari akilipasha moto Chopa akiwa Keisha funga mikanda ya usalama na amekwishavaa vyombo maalum vya mawasiliano.
Madam S akakwea na kuketi katika siti ya mbele alkadhalika Gina akajitupa katika siti ya nyuma, Scoba akawapa ishara ya kufunga mikanda vizuri, akampa ishara Madam S ya kuvaa vyombo vya mawasiliano, milango ikafungwa, Chopa likanyanyuliwa kwa umahiri kabisa.
“Zainzibar, kuna boti iko majini inasafiri kwenda huko nataka tufike kabla yake,” Madam S akamwambia Scoba.
“Umesomeka, nilifikiri unataka tufanye fishing,” akajibu.
“Oh, no! hatuwezi fishing Kamanda hayupo, laity angekuwepo tungemuonesha jinsi tulivyo mahiri katika mambo kama haya,” Madam akajibu. Ile Chopa ikaendelea kupasua mawingu juu ya bahari ya Indi kukitafuta kisiwa hicho maarufu kwa zao la Karafuu.
Ukimya ulichukua nafasi ndani ya Chopa hiyo, wakimtazama kijana huyo mahiri katika kazi hiyo miaka kadhaa akilitawala dude hilo la Kirusi. Wakiwa angani waliona vitu viwili vikiwapita kwa kasi ya ajabu kimoja kushoto na kimoja kulia, ilikuwa ni kasi kuliko kasi unayoijua, wakaona kwa mbele vitu vile vikiwa ka ma kimwondo.
“Nini kile? Isiwe tumetunguliwa Scoba,” Madam S aliuliza.
“Usihofu mama, hakuna wa kutuletea shida kati anga letu wenyewe,” akajibu.
“Sasa kile ni kitu gani?”
“Usiogope ni watanashati wetu hao ni ndege aina ya kivita aina ya MiG-31E nayokwenda kasi kuliko kasi yenyewe, ina uwezo wa kwenda kilomita 3000 kwa saa moja,” Scoba alieleza.
“Waoh!” Madam S akashangaa, “Asante sana Jenerali Kamsumi.”

§§§§§

ILIKUWA ni furaha mateka wale kutoka ndani ya kile chumba, hawakutegemea hata siku moja kama litatokea, mbele yao mwanaume mkakamavu alisimama akihakikisha wote wanatoka ndani salama.
“Asante sana, sasa watatukoma washenzi hawa!” mmoja alisikika wakati akitoka katika chumba kile. Wale mateka walitoka na kutawanyika kila kona. Ilikuwa ni balaa kila anayekutwa alichezea kichapo cha maana na kunyang’anywa silaha yake, msako mkali ulianza ndani ya himaya ile, nje ndani, meli kubwa ya PARPADOS iliwekwa chini ya ulinzi pamoja na watu wake wote waliokuwamo ndani.
Kamanda Amata aliwahesabu wote kwa jumala yao walikuwa kama thelathini na nane hivi, zaidi ya wale ishirini na tano waliotekwa na ile Manowari ya JW kulikuwa na wengine zaidi kutoka Ufaransa, Ubelgiji na nchi za mbali, wote walitekwa meli zao za mizigo na Maharamia hao waliotikisa Dunia.
Eneo zima lilizingirwa na wapiganaji hao waliookolewa punde tu, wakiwa na hasira, waliwakung’uta vibaya Maharamia waliokutana na o hata wengine kupelekea kukimbia eneo.
§§§§§§
Saa ya Kamanda Amata ilimpa ishara ya kuwa kuna ujumbe unaingia, akaiinua na kuiruhusu.
….Dakika 85 hakikisha umewaweka watu wako mahali salama, Tai wako njiani msije mkanyakuliwa kama vifaranga vya kuku…
Ilikuwa ni ujumbe kutoka kwa Chiba, kwa harakaharaka huku akiwa macho huku na kule aliujibu ujumbe ule.

….hakuna sehemu ya kujificha, tutakuwa ndani ya meli kubwa, wasiiweke kwenye shabaha tafadhali…
Siwezi kutoka hapa kabla sijatenganisha roho na mwili ya Shalabah, akawaza Kamanda huku akikimbia tarataibu.
“Kamanda Amata!” ilikuwa sauti ya Fasendy ikiita. Kamanda akageuka nyuma kumtazama mwanamke huyo.
“Vipi?” akamuuliza.
“Shalabah!” akajibu. Amata akakza macho mwa Fasendy aliyekuwa akionekana kuwa na maumivu makali.
“Namtafuta,” akamwambia, Fasendy akampa ishara ya kumfuata, moja kwa moja wakafuata huo ujia mpaka kwenye mlango mmoja uliojitenga peke yake. Fasendy akasimama akamzuia Amata, pumzi yake ilikuwa ikitoka kwa tabu, alionekana kuchoka haraka.
“Fasendy nini?” Kamanda akauliza wakatia akijiandaa kufungua mlango.
“Sikia, ukimuua Shalabah, na Hussein kuna boss wao, Mungu mtu asiyeonekana kwa macho ya binadamu, anaitwa Mr Lonely, ukammalizie,” Fasendy alimwambia Amata.
“Kwa nini unasema hivyo, wewe utakuwa wapi?” akauliza kama mtoto. Fasendy akachomoka mikononi mwa Kamanda na kuteremka ngazi mpaka kwenye mlango mwingine, akampa ishara Kamanda Amata ya kuwa ni hapo, Kamanda hakusubiri, alimpa Fasend ile shotgun kisha akamhesabia moja mpaka tatu na kuubamiza mlango, kisha akaingia mzima mzima na kuruka sarakasi, akiwa hewani wale vijana wa Hussein walimlenga shabaha lakini hawakujua kama hiyo ilikuwa ni janja tu, risasi za Fasendy ziliwamaliza wote watatu na kuwaacha hoi wakiagana na roho zao. Kamanda Amata alipotua chini, konde la kwanza lililtua katika tumbo la Hussein, la pili hapohapo na la tatu.
“Siku yenu imefika,” akamwambia. Husein hakukubali kufa kizembe, alimpiga kichwa Amata, akayumba na kabla hajajiweka sawa, alipigwa ngwara kali iliyomuondoa sakafuni na kumpeleka hewani kabla ya kutua chini kama kifurushi.
“Kumbe ni mwepesi namna hii? Sikutegemea na ninashangaa hata umewezaje kumuua Sharon kwa uteke huu,” Hussein, mtu mnene alijigamba huku akiweka sawa suruali yake aliyoivalia tumbo.
“Aaaaaaiiiiiiiggghhhh!” Sauti ya Fasendy ilisikika. Amata akageuka kutazama kule mlangoni, akamwona Fasendy akiwa kabanwa kabali na mkono wenye nguvu wa Shalabah.
“Afadhali mmekuja wote kunirahishia kazi,” Amata akasema huku akinyanyuka pale chini. Hussein kwa haraka alirudi nyuma na kurukaruka kwa madaha huku akikunja ngumi zake, akarusha konde moja, Kamanda Amata akailikwepa na kumtandika konde la mbavu mpaka Hussein akaguna, kabla hajauachia mkono wa bonge hilo, alimuongeza ngumi nyingine mbili za nguvu ambazo zote zilitua mbavuni na kumlegeza Hussein, almwachia mkono na kumrukia teke moja kali la kuzunguka lililosukuma mpaka kwenye maboksi akajibwaga huko. Kabla hajanyanyuka Kamnda Amata alimuwahi pale pale na kuukamata mkono wake akauzungusha kwa nguvu ukatawanyika mifupa yake kwa ndani, Hussein alilia kama mtoto.
“Mwache huyo mwanamke!!” Amata alimwambia Shalaba wakati akimwacha Husseina na kugeukia upande huo.
“Unasema nini wewe mtoto Changudoa! Unafikiri ulivyowaweza hao na mimi utaniweza? Kwa taarifa yako mimi ndiye niliyemfundisha huyu mwanamke wako michezo yote hii anayoifanya, hapa, sasa kama na wewe unataka kujaribu sogea nikumalize,” Shalabaha akaijigamba mbele ya Amata.
“Sasa kwa nini unajiwekea ngao huyo mwanamke? Kama unaona unauwezo wa kupambana na mimi muache huyo uje kwa mwanaume hapa shoga wewe,” Kamanda Amata akamtia hasira Shalabah. Shalabah akauma meno na kumtupa Fasendy kwa nguvu kiasi kwamaba hakuweza hata kujizuia. Shalabah akiwa na kisu kikali mkononi mwake alimkimbilia Amata huku akiwa kauma meno.
“Iyaaaaaaaaaaaa!!!!!” alipiga makelele akiwa kadhamiria kumdidimiza Amata hicho kisu. Kamnada alishajipanga, aliruka hewani na kuzungusha miguu yake, mguu wa kusoto ukapiga mkono wenye kisu, kikaanguka na wa kulia ukatua kwenye shavu la Shalaba, akayupa na kujibamiza kwenye chuma kubwa lililofungwa hapo kwa ajili ya kuinulia vitu vizito.
9
“Gina hatutakiwi kumkamata Balozi kwa vitisho au nguvu, kwanza nataka ujue ni wapi anakwenda kama ni hapa ndani ya Zanzibar au ana safari nyingine, cha muhimu ni kuwa asiondoke katika nchi ya Tanzania,” Madam S alimwambia Gina ambaye alkuwa akisikiliza kila kitu.
“Sawa Madam,” Gina aliichomoa bastola yake na kuipachika vizuri kiunoni, “Sasa tunashukia wapi?” akauliza.
“Uwanja wa ndege, ningeweza kuwashusha hata Ngome Kongwe lakini usiku huu tutawashtua wananchi,” Scoba alijibu na dakika mojan baadae tayari chopa lile lilikuwa likiweka magurudumu yake juu ya ardhi ya Zanzibar. Madam S akifuatiwa na Gina wakashuka, Scoba akazima injini na kuteremka baadae.
“Karibu Zanziba Madam ijapokuwa umekuja kwa dharula hata Gahawa hatujaandaa, ila sio mbaya karibu sana,” alikaribishwa na kijana mmoja mtu wa makamo anayejulikana kwa jina moja tu Kwame. Kwame alikuwa ametumwa kikazi Zanzibar miaka miwili iliyopita kutoke idara ya Usalama wa Taifa.
“Tumekuja kuchukua mzigo kama inabidi,” Madam S akamwambia.
“Usijali, maagizo yako niliyapata na yanafanyiwa kazi, mzigo lakima muupate,” akajibua Kwame.
“Ok, usafiri?” Madam akauliza.
“Kila kitu kipoa Madam,” akajibiwa kisha wote wakaingia ndani ya Range Rover moja ya buluu, Scoba akaketi nyuma ya usukani kwa kuwa yeye wa idara hiyo.
Walitoka Uwanja wa Ndege na kuchukua barabar ya Nyerere, wakashuka nayo moja kwa moja mpaka hospitali ya Mnazi Mmoj, pale wakaiacha ile barabara ya Kaunda na kuchukua ya kulia. Barabara ya Mtoro mpaka Mkunazini, wakapenye vichochoro.
“Kijana kuna vichochoro havipitwi na magari utagonga!” Kwame alimwambia Scoba.
“Usaijali usiku saa hii hakuna wa kugongwa zaidi ya mchawi,” Scoba wakati anamalizia usemi wake alikuwa ameshatoke barabar ya Jamatini, akashuka nayo mpaka ile ya Mizingani, hapo kwa mwendo wa polepole akasimamisha gari yake. Gina akateremka na kutembea kwa miguu kuelekea katika bandari hiyo ndogo. Hakuingia bandarini kwani usiku huo kulikuwa kumefungwa, chini ya mwembe mkubwa kulikuwa na wazee wameketi walionekana kuwa ni walinzi wa eneo, hilo, waliketi wakinywa kahawa, akawaendea ili kupoteza dakika kadhaa hapo akiisubiri ile boti kuwasili.
Madam S aliitazama saa yake ilikuwa tayari ni saa tisa za usiku, akarudisha mkono chini na kufyatua kitia akajilaza.
“Bibi stahafu sasa! Tuachie vijana,” Kwame alimtania Madam S.
“Ah, Rais wenu hataki nistahafu, anataka nizeekee mpaka siku mnikute nimefia mezani ofisini,” akajibu.

§§§§§

Jamir alijiinua kwa taabu sana kutoka pale alipoangukia baada ya kupatwa na risasi za Shalabah, damu nyingi zilikuwa zikimvuja, katika sehemu ya mbavu hakuwa na nguvu tena zaidi ya kusota na kujibana nyuma ya ndoo kubwa la takataka, alipoona ukimywa umetawala, akainguka na kutembea kwa tabu huku akiifanya bunduki ya AK 47 aliyoiokota kuwa kama mkongojo wa kutembelea. Alifika sehemu yenye dirisha na kuchungulia nje, alisikia milio kadhaa ya bunduki huku watu wakikimbili kwenye ile meli kubwa iliyoegeshwa gatini. Alijikongoja na kuweza kutoka nje, wakati huo wale wanajeshi waliokuwa wametekwa walikuwa tayari melini, alijikokota mpaka lango la kutokea kule gatini, akapiga mbinja kali, wale askari kule juu ya meli walimuona, lakini hakuwajua kama ni mwenzao au la.
“Hima himaaaaaa!!!!!” mmoja akaropoka kwa nguvu na Jamir akaitikia, “Tanzaniaaaaaaaaa!!!!!”. Wawili kati yao wakateremka haraka na kwenda kumsaidia. Kwa mbali waliona gari zilizzokuwa zikija zikiwa zimewasha taa, wakajua sasa mambo yameharibika.
“Kamanda aliyetuokoa hayupo, tutaondokaje bila kumuona?” ubishano ulianza kati yao.
“Mwambie Nahodha asogeze mbali kidogo japo mita mia tano baharini ila tusiondoke,” mwingine alidakia. CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Watu wote waliokuwa wakifanya kwenye ile meli walikamatwa na kufungwa kamba na kuwekwa katika chumba kilicho chini karibu na injini.
Nahodha George, aliyekuwa ndani ya nguo zake nyeupe lakini sasa zilizochafuka na kunuka kwa jasho alikuwa akiuzingisha usukani wa ,eli ile, PARPADOS kuisogeza baharini wakiati wakipanga jinsi ya kumpat Kamanda Amata.
Jamir alilazwa katika kitanda na mwanajeshi mmoja mwenye taaluma ya udaktari akasogea na msaidizi wake nakuanza kumsaidia.
“Vipi?” mkuu wa msafara aliuliza.
“Risasi imeingia pabaya sana sana sijui kama ataweza kupona labda kwa kudura za Mwenyezi Mungu,” yule Daktari alimweleza mwanajeshi huyo mwenye nyota tatu mabegani mwake ambaye tangu mwanzo ndiye aliyekuwa kiongozi wa msafara huo uliokuwa ukielekea huko bahari ya Kaspian.
Jamir alifumbua macho akamtazama yule daktari, “Usiumie Dokta, hata nikifa nimeshafanya kazi niliyotumwa, nimeipigania nchi yangu, Tanzania, nimewapinia watu wangu, Watanzania, fanya unaloweza lakini ukishindwa basi muachie Mungu,” Jamir akafumba macho tena.

§§§§§

Kamanda Amata kwa haraka, alimuwahi Shalabah na kumchapa makonde kadhaa bila upinzani wowote, Shalabah akaiinua kutoka pale alipokuwa ameegemea, “Usifikiri mimi bwege wewe,” akasema. Alimuwahi Amata akamshika kwa vidole vyake kwenye mifupa ya mabega, Kamanda akasikia maumivu na kuhisi ganzi ikimwingia kwa kasi. Shalabaha akamsukuma nyuma na kumchapa konde moja lililomyumbisha na kumwongezea linguine ambalo lilimpeleka chini.
“Bado mtoto mdogo wewe kwenye mapigano,” Shalaba alimwambia Amata huku akikamata ukosi wa shati lake na kumpigisha magoti, kwa kutumia goti lake alimpiga kidefuni, Amata akadondokea nyuma, Fasendy aliyekuwa chini hakuweza kuvumilia, aliinuka na kumuwahi Shalabah akamdandia mgongoni na kumng’ata katika mshipa mkubwa wa shingo.
“Aaaaaaaiiiigggghhhh!!!!” Shalabah akapiga kelele na kumkamata shingo Fasendy kwa nyuma kisha akambinua na kumbwaga upande wa mbele, Fasendy akafikia mgongo, akatoa mguno hafifu wa kukata tama, lakini hakujali, alijinyanyua kiufundi na kuruka sarakasi matata alipita teke moja kali la kuzunguka lakini Shalabah akalikwepa vizuri, teke la pili nalo akalikwepa vilevile, alipotua chini akakuta na pigo kali lililopigwa kwa viganja viwili juu ya matiti yake, Fasendy akasukumwa nyuma kwa nguvu, alipopata nguvu za kusimama, alirudi kwa kasi kumvamia Shalabah.
“Fasendyyyyyyy!!!!!!!!!” Kamanda Amata alipiga kelele baada ya kuona Shalabah akichomoa kisu kutoka katika biatu chake kikubwa alichokuwa amekivaa, lakini alichelewa, Fasendy alikutana na kisu kikali kilichopenya katika tumbo lake pembeni kabisa chini kidogo ya mbavu.
“Aaaaaaaaa, ameniuaaaaa…” yalikuwa ni maneno ya mwisho ya Fasendy, akajibwaga chini, kwa nguvu na kile kisu kikabaki mkononi mwa Shalabah. Kamanda Amata akaainuka kama mbogo, Shalabah akafanya mchezo uleule, alikipima kisu kilipate tumbo la Amata barabara, kumbe mwenzake alishausoma mchezo huo. Alimkwepa kwa sentimita chache na kile kisu kikapita pembeni, Kamanda Amata akajiguza na kuudaka mkono wa Shalabah, aliuvuta kwa nguvu na kuusukuma chini, kisha kwa kisigino chake alipiga korodani za Shalabah, yowe likamtoka, akapiga tena kisha akamvuta mbele kwa nguvu na kumuweka sawa, konde moja la uso, la pili na la tatu yalimtoa fahamu kijana huyo mtukutu. Akageuka na kurudi kichwa kichwa, Kamanda Amata akaruka juu na kumnasa shingo kwa miguu yake akampiga kabala ya miguu na kushuka nae mpaka sakafuni. Shalaba alirusharusha miguu na mikono lakini ile kabala ilikuwa balaa, tungeiita kabali namba tisa, Shalabah alilegea na kutulia kimya, shingo yake ikiwa tayari imevunjwa na miguu ya Kamanda Amata. Akanyanyuka na kumuwahi Fasendy, akamuinua kwa mikono yake na kumfanya kama kaka kwa kuegemea mikono hiyo.
Hussein, akapata uhai ghafla, akazinduka kutoka kwenye mzimio mzito, akamuona Shalabah akiwa kalala chini miguu kaitupa huku na kule ulimi ukimning’inia nje, akaokota bunduki yake iliyokuwa imedondoka si mbali naye, wakatia huo Kamata akiwa na Fasendy akijaribu kumsaidia hili na lile labda atamwamsha, damu zilikuwa zinamvuja kwa wingi. Hussein aliinua ile shotgun na kulenga kisogo cha Kamanda Amata.
“Bastard!” alitamka maneno hayo huku akiondoa akiingiza risasi chemba. Kamanda Amata aliduwaa akapoteza mtandao wa akili yake kwa nukta kadhaa.
§§§§§
Huko nje, lori aina ya Jeifang ziliingia kama kumi hivi na kushusha askari wenye silaha waliovamia eneo lile, wakiwa na bunduki nzitonzito. Walikuja kusaidia wenzao waliozidiwa nguvu na askari wa Kitanzania, walitawanyika huku na huku kwa amri waliyokuwa wakipewa na kiongozi wao aliyekuwa katikati ya lango akiwapa ishara ya mkono kuashiria kushoto ama kulia. Dakika moja baadae wote wakazingira lile eneo na kuazna kusaka kila kona.
KATIKA ANGA LA SOMALIA
“...MiG-31E target 1, MiG-31E,” Rubani katika ndege ya pili iliyopewa jina la target 2 alikuwa akimwita yule wa target 1, wakiwa juu mita 23000 au futi 75,500 kutoka usawa wa bahari. Kadiri ya uzoefu wao tayari walikuwa kwenye anga la Somalia, ili kuweza kupata shabaha waitakayo kutoka na kasi ya ndege hizo, walianza kushuka taratibu kutafuata Mogadishu jambo ambalo ni ndani ya dakika tano tu wangekuwa wameifikia.
Walipohakikisha wameiona ardhi ya Mogadishu walifanya manuva na kila mmoja alikwenda upande wake kwa kuzigeuza ndege hizo ghafla, kisha wakazunguka na mmoja akatokea mashariki huku mingine akitokea Maghalibi.
“…MiG-31E Target 2 ready to engage,” sauti ya rubani wa ndege ya pili ilimwambia yule wa ndege ya kwanza kuwa yuko tayari kufanya mashambulizi. Wakati huo katika kipimo cha shabaha ndani ya ndege zile kila mmoja aliweka eneo analotaka kulipiga. Kwa sekunde iliyo sawa, wote wakabofya vitufe vilivyo katika mkono maalum kwa kazi hiyo ndani ya ndege hizo. Milipuko mikubwa ilitokea, mmoja ulipiga katika lango kulikokuwa nay ale magari yakishuhsa wapiganaji nwengine na mwingine ulipiga eneo lililokuwa na nyumba ya ghorofa iliyotumika kama ofisi au sehemu ya mikutano yao.
“Uuuuuuuuuuhuuuuu!!!!!” rubani wa ndege ya kwanza alishangilia kwa shabaha yake, akainyanyua ndege yake na kuipeleka juuu kwa kwa si kaipoiweka sawa akadondosha makombora manne ya maana yakashuka na kusambaratisha kila kilichosimama, ilikuwa ni hali ya kutisha, moto mkubwa ulifumuka na ndege hizo hazikwenda mbali zikilikuwa zikirandaranda maeneo hayo.
Baada ya kuhakikisha wamesawazisha ndani ya dakika moja waliambiana.
“MiG-31E target 1, Mission succesifull,” wa kwanza akamwambia mwenzake naye akajibu kwa mtindo huohuo wakimaanisha kuwa kazi yao ilikuwa imekamilika kwa ufanisi. Wakazipindua ndege zao na kuongeza kasi kurudi walikotoka na kuacha wapiganaji wa Maharamia wakiwa wameteharuki kwa hali hiyo, wakiokotana huku na huko.
§§§§§
PARPADOS ilipewa amri ya kuondoka haraka karibu na lile eneo la bandari, haikuwa na budi taratibu ilipiga maji kwa makata maji yake na ikazidi kuliacha mbali lile eneo la bandari na kusogea katikati ya bahari.
Poooooooooooo!!!! Honi nzito ilisikika baharini, wale wanajeshi waliokuwa kwenye deki ya ile meli waliitazma nyuma na mbele wanakoelekea na kuona meli nyingine kubwa kwa mbali. Hawakuitambua sawasawa pia kutokana na giza nene la saa tisa usiku.
“Unaombwa kusimamisha meli yako hapo kwa usalama wako,” ilikuwa sauti iliyotoka katika ile meli kubwa waliyoikuta imepiga nanga katikati ya maji, Nahodha wa jeshi la maji la Tanzania hakukaidi, alizima injini na ile meli ikapunguza mwendo taratibu.
BARNATOV LINE, maandishi yaliyosomeka ubavuni mwa meli ile ya kijeshi.

“Colonel, sisi ni wanajeshi wa Tanzania, tuliokuwa mateka chini y maharamia wa Kisomali,” mkuu wa msafara katika meli ya PARPADOS iliyowabeba wale Watanzania na wenzao alijitambulisha kwa niaba ya wote huku akipiga saluti kwa kanali huyo wa jeshi la Urusi.
“Sawa, Captain, je watu wetu mna habari nao?” yule Kanali wa jeshi la Urusi akauliza.
“Ndiyo Kanali wote wako salama kabisa, kama unavyowaona,” akajibu na kisha akawaita wale vijana watano wa jeshi la Urusi, wakapiga saluti kwa mkubwa wao.
Kanali wa Kirusi akatikisa kichwa kuonesha kuwa ameridhika kwa hali hiyo, “Ok, naweza kuondoka na vijana wangu,” akaomba.
“Hapana Colonel, inabidi mje muwachukue kule Tanzania kwani hawa walitoka pamoja nasi Tanzania nasi kwa mission maalum Sir,” yule mkuu wa msafara mwenye cheo cha Captain alimjibu.
“Ok, maadam tumejua wako salama hakuna shida, tutafanya utaratibu wa kuwachukua, asante sana Captain,” yule Kanali wa Kirusi akashukuru na ile meli ikaongeza kasi kuondoka eneo lile. Furaha ya kuokoka kwao ilikuwa dhahiri shahiri nyusoni na mioyoni mwao, waliimba wakacheza wakafungua vinywa vilivyojaa ndani ya meli hiyo na kugida kama hawana akili nzuri.
Jamir alikuwa kalala kimya kitandani huku macho yake ameyafumba, hakujitikisa wala hakufanya kitu chochote. Mara kwa mara daktari aliyekuwa akimwangalia alikuwa akimpima mapigo ya moyo kuona kama yanapiga au yamesimama. MV PARPADOS iliendelea kukata maji haikusimama mpaka katikati ya bahari, ikapiga nanga na wote wakasubiri, Nahodha wa meli hiyo akatafuta mawasiliano na makao makuu ya jeshi (JW) ili kuomba msaada wa haraka kwani wasingeweza kwenda mbali na meli hiyo.
§§§§§§§
Wakati Kamanda Amata akifikiria jinsi ya kujiokoa dhidi ya risasi itakayofyatuliwa na Hussein ambaye alikuwa akikenua meno, “Nimekupata, panya buku wewe!” akitamka maneno hayo, alivuta kifyatulio (trigger) lakini kabla hakijaruhusu risasi kutoka, Kamanda Amata alimshuhudia mtu huyo Kibonge akipaishwa juu na kubwaga kando, damu mithiri ya bomba ilikuwa ikitoka katika kichwa chake. Kamanda Amata akageuka kutazama kule ilikotoka ile risasi. Kidirisha kilichoruhusu mtutu wa bunduki hiyo kupenya kilifunguliwa wazi na mtu mmoja mfupi aliyeshupaa aliteremka na kuruka kwa ndani, akatua kwa miguu yake miwili akasimama. Amata alimtazama lakini hakumjua kwa kuwa alikuwa kavaa sox kuficha uso wake.
“Vipi, amekufa?” yule mtu akauliza kwa Kiswahili safi, Kamanda akamtazama tu bila kujibu wakati mtu huyo alikuwa akivuta hatua huku bunduki yake ikiwa mgongoni, akaenda pale alipolala Fasendy, akapiga goti na kuweka mgongo wa kiganja chake cha kulia katika shingo ya mwanamke huyo, akasikiliza kwa nukta kadhaa baadaye akamgeukia Amata, “Hajafa,” akamwambia.
Yule mtu akasimama na kuvua kofia yake usoni, sasa wakatazamana uso kwa uso na Kamanda Amata hakuna aliyekuwa anamjua mwenzie.
“Naitwa Daud Daud, mwanajeshi wa jeshi la hadhimu la Tanzania, nilikuja Mogadishu kwa operesheni hii lakini mwenzangu aliuawa vibaya na mimi nimiliponywa maisha yangu na huyu mwanamke, hata simjui kwa jina,” akajitambulisha na kutoa maelezo mafupi.
Kamanda Amata akamtazama yule kijana akahakikisha kuwa kweli ni Mtanzania baada ya kuona bendera ya Tanzania iliyobandikwa kwa juu ya mfuko wa kombati alilovaa.
“Naitwa Amata Ric,” lakini kabla hajamalizi Daud akamalizia “…Kamanda Amata.” Wote wakacheka na kupeana mikono.
“Ok Daud tutaongea vizuri, vipi hali ya huko nje kabla hatujatoka?” Amata akauliza.
“Huko nje kumevurugika, ndege vita za JW zilifika na kufanya kazi kubwa sana ya kusambaratisha ngome yote, utajionea mwenyewe,” Daud akajibu.
“Ok, tuna tuna kazi tatu, moja ni kumsaidia huyu dada, pili kufungua hayo makombola na kuchukua vichwa vyake, tatu ninahitajin kuonana na kiongozi wa hawa Maharamia anaewapa jeuri, Mr. Lonely,” Kamanda akamwambia Daud.
Kisha kwa kushirikiana wakaanza kufungua yale Makombora, huko nje moto mkubwa ulikuwa ukiwaka, kwa haraka haraka waliweza kufungua makombora yote nane kwa kuwa mawili tayari yalikuwa yamepakiwa kwenye ile meli PARPADOS.
Kisha wakafunga hivyo vichwa ambavyo kwavyo kuna mlipuko mbaya sana uliohifadhiwa, na hlilo ndilo bomu lenyewe. Vilikuwa ni vizito, wakavikusanya pamoja.
Mara mlango ukafunguliwa, Chammeleone akaingia na vijana wake waliokuwa tayari kwa lolote kutokana na silaha walizozibeba.
Alipiga makofi kumpongeza Amata, “Hongera sana kijana, sasa hapa si pa kukaa, hawa jamaa wako wengi sana, naomba tuondoke haraka,” akawaambia. Kwa kushirikiana na wale wafuasi wake wakabeba vile vichwa na kutoka navyo nje ilhali Kamnda Amata alimbeba mabegani mwake Fasendy, wakatoka ndani ya jengo hilo. Huko nje kulikuwa ni moshi na mioto kila kona, Kamanda Amata aliikubali kazi iliyofanywa na Tai kutoka Tanzania. Wakaelekea kwenye Land Cruiser iliyoegeshwa nje, wakapakia kila kitu na kuondoka eneo hilo.
Kamanda Amata alitulia kwenye landcruiser huku miguuni mwake amemlaza Fasendy aliyekuwa hajitambui, moyoni alikuwa akifikiria mengi sana, jinsi ya kumpata Mr. Lonely, alijua wazi kuwa huyu ndiye mzizi wa genge hili la wahuni ambao kazi zao ni kuteka meli za mizigo huku wakivunja sheria za kimataifa kwa kuzivamia zikiwa katika maji makubwa, maji ya kimataifa.
§§§§§§
DAR ES SALAAM – TANZANIA
Saa 12:00 asubuhi, gari ya Usalama wa Taifa ilisimama kwenye nyumba Fulani huko Masaki. Wanaume wawili wakateremka na kulijongea lango kuu la nyumba hiyo ya kiongozi wa ngazi za juu katika awamu ya kwanza. Mlinzi wa getini akafungua lango na kuwakaribisha vijana hao waliovalia suti nadhifu sana.
“Tuna shida na mzee,” mmoja alimwambia yule mlinzi.
“Shida sasa hivi?” yule mlinzi akauliza.
“Ndiyo sasa hivi,” mwingine akajibu. Yule mlinzi akainua simu ya mezani hapo katika kibanda chake na kupiga ndani ya nyumba hiyo kubwa ya kifalme akampa ujumbe mtumishi wa ndani naye akamwamsha huyo aliyekuwa mheshimiwa.
Alipotoka ndani akiwa katika pyjama alikutana na vijana hao, hakuuliza moja kwa moja aliwatambua kwa jinsi walivyoonekana, askari kanzu.
“Enhe, niwasaidie nini vijana ? mbona asubuhi asubuhi?” akawauliza.
“Mheshimiwa, sisi ni vijana wa Usalama wa Taifa, tumetumwa kutoka Ikulu, Mzee unatakiwa Ikulu kabla ya saa moja asubuhi, hivi tumetumwa kukuchukua,” mmoja akasema.
“Ikulu, kuna nini saa hii, mambo ya Ikulu tulishaachana nayo zamani,” akajitetea.
“Sisi ni wajibu wetu tu kukufikishia ujumbe kama ulivyo, unaitiwa nini utajua hukohuko,” yule kiongozi wa serikali ya awamu ya kwanza akabaki kaduwaa, akarudi ndani na kubadilisha nguo kisha akaondoka na hao vijana kwa kutumia gari waliokuja nayo.
Asubuhi hiyo, watu kama watano walikamatwa na wengine kuwekwa kizuizini, wakati uchunguzi ukiendelea, hawakutakiwa kutoka hata ndani ya nyumba zao, kila kabrasha lililohusiana na mikataba ya kampuni iliyokuwa ikichimba yale madini kule Msanga mkuu liliwekwa mezani upya na Mkaguzi mkuu wa serikali na kamati ya Bunge walianza kuyapitia tena.
ZANZIBAR
Asubuhi hiyo hiyo Gina alikuwa na vijana wengine wawili wa Usalama wa Taifa nje ya hoteli ya Serena pale Zanzibar, tayari kumkamata Balozi wa Somalia ambaye ilionekana alikuwa akishirikiana na Waziri wa Ulinzi kutoa siri za mradi huo na nini kinaendelea.
Waliingia ndani ya chombo cha kuwapandisha juu, Gina akabonya kitufe namba 4 na kile chombo kikawapandisha.
Wakafika mlango namba 456 kama walivyoelekezwa na mtu wa mapokezi. Wakagonga mlango mara tu ukafunguliwa. Wale vijana wakaonesha vitambulisho vyao na moja kwa moja wakaingia ndani ya chumba hicho.
“Mheshimiwa Mr. Balozi, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inakuweka chini ya uangalizi wake kwa muda usiojulikana, hii inatokana na mbinu chafu ulizokuwa ukizifanya kuihujumu nchi hii,” kijana mmoja alimweleza huku akimkazia macho, Mr Balozi aliishiwa nguvu, akajitupa kitandani na kuketi.
“Mnajua mi ni mtu mkubwa sana, halafu hamuwezi kuniambia hayo mnayoniambia bila kibali kutoka serikalini kwangu,” akalalama.
“Hatuwezi kukuweka chini ya ulinzi bila serikali yako kujua, inajua na ndiyo iliyoturuhusu,” yule kijana akamwambia. Mr Balozi hakuwa na ujanja, alijiweka tayari na kuondoka chiini ya uangalizi wa vijana hao mpaka kwenye gari ile aliyokuwapo Madam S, Kwame na Scoba, safari ya kwenda Uwanja wa Ndege wa Zanzibar ikaanza.
Pale waliingia naye kwenye Chopa na kumrudisha Dar es salaam ambako alirudishwa nyumbani kwake na kuwekewa ulinzi wa kutotoka kwenda popote mpaka uchunguzi utakapokamilika.
Halia ilikuwa tete kwa kila aliyejijua kuhusika na sakata hilo, matumbo yalijaa gesi zisizo na sababu, BP za kushika zikaongezeka, lakini katika yote hayo hakuna aliyemuona Bw. Goloko Mikidadi. Kila mmoja alijiuliza yuko wapi mtu huyo aliyewafanya wao kuwa ma-bilionea, hakuna aliyejua kama mwenzi wao, swahiba alikuwa chakula cha samaki wa Mr. Lonely. Hakika zilikuwa siku ndefu mno kwa mabwanyenye hao wenye uchu wa kuliibia Taifa. Hii ilikuiwa ni hujuma, hujuma mbaya kuliko yoyote iliyowahi kutokea.
Viongozi wenye dhamana na Taifa, haohao tena wanaliibia Taifa hilohilo, wanalihujumu na badala watetee Wanachi bado wanawakandamiza, wakilalia minoti ilhali yule wa kijijini anapiga mwayo wa njaa huku mkono wake akiwa kauweka shavuni bila kujua kesho yake inakuwa vipi.
Ni hujuma, watu wanapokuwa tayari kupigania Taifa lao, wanaposonga mstari wa mbele wewe unawakabidhi kwa maadui wanauawa wanadhindwa kulipigania Taifa lao, na wewe unakenua meno yote kwa kuchekelea ilhali familia za watu hao zinalia na kuomboleza zikiwa hazijui kesho na keshokutwa zitakuwa mgeni wa nani.
Waziri wa Ulinzi alikuwa ameketi sebuleni kwake akaiangalia kuninga kubwa kabisa iliyokuwa imening’inizwa ukutani, alivua kofia yake aliyokuwa ameivaa kichwani mwake na kuficha nywele zake zenye asili kama Kiarabu au Kisomali, akaiweka mezani. Ijapokuwa alikuwa na hofu lakini hakupenda kuionesha kwa yeyote, aliendelea kutazama Televisheni, aliendelea kunywa mvinyo wake taratibu. Mara simu yake ikaita kwa fujo, akainyakua na kuitazama kwenye kioo, private number, akasita kuipokea akaiweka tena mezani, akashusha pumzi za nguvu na kuvuta gazeti la Uhuru na kulipekuwa kurasa moja na nyingine kana kawamba hakuwahi kulisoma gazeti hilo.
Mara ile simu ikaita tena, akainyakua na kuona vilevile private namba, akaipokea kwa taabu na kuiweka sikioni. Akasikiliza anachoambiwa, hakika hakikumfurahisha, akajua sasa ni wakati wowote atakuja kuchukuliwa na kufikishwa panapohusika. Hodi ikabishwa mlangoni, akahisi kuchanganyikiwa. Akajua vijana watakuwa wamefika, afanye nini sasa kama mabilioni kayaficha Uswiss wakati wavuja jasho wanashinda na mlo mmoja na mlo wenyewe bado haukidhi mahitaji ya viini lise, ilimradi tu wamekula kujaza tumbo.
Aliikumbuka siku aliyoingizwa kwenye sakata hilo, uroho na uchu wa pesa, sasa aliona wazi vikimtokea puani.
Miaka Sita Iliyopita
Wizara ya Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa
JIONI ya siku hiyo, Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi alichelewa kutoka ofisini kwani alikuwa na kazi nyingi za kumaliza kabla ya safari yake ya kwenda UN kumwakilisha Rais wan chi katika mkutano wa masuala ya usalama hasa katikam nchi za maziwa makuu. Akiwa katika kupangapanga hiki na kile, hodi ilibishwa mlangoni kwake na Katibu wake, Miranda aliingia ndani akiwa na bahasha mkononi, bahasha iliyopendeza kwa rangi na maua, akakbidhiwa, akaipokea na kuichana kuangalia kuna ujumbe gani ndani yake.
Alikuwa akialikwa kwenye hafla maalumu iliyoandaliwa katika makazi ya Balozi wa Somalia nchini Tanzania, wiki moja inayofuata, akatikisa kichwa kuashiria amekubaliana nao.
“Isome kisha ijibu uwatumie taarifa,” akamwambia Miranda.
“Niwaambie nini?” akauliza.
“Positive,” akajibu kwa mkato akimaanisha kuwa amekubaliana na mwaliko huo.
Wiki moja Baadaye
Nyumbani kwa Balozi wa Somalia
Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi alikuwa ni mmoja kati ya wageni mbalimbali kutoka ofisi tofauti za kibalozi na taasisi zisizo za kiserikali walijumuika katika viwanja vya makazi ya Balozi huyo, ilikuwa ni Cocktail party, mara Balozi akamwendea Waziri wa Ulinzi na kumsalimu kwa makeke na bashasha pembeni alikuwa amefuatana na kijana nadhifu, aliyeonekana kashiba pesa, nywele zake hazikumficha kabisa kuwa yeye ni Msomali, lakini huyu alikuwa tofauti kabisa kwani alionekana kutakata kwa pesa.
Wakasalimiana wote watatu wakatambulishana kwa majina na shughuli zao.
“Ndiyo bwana Shalabah, kalibu sana Tanzania,” Waziri wa uUlinzi alimkaribisha kijana huyo kisha mazungumzo yakafuata. Hoja kubwa ilikuwa ni kumjuza Waziri huyo juu ya huo mradi wa Madini ambao unaendelea kati ya wadau mbalimbali waliopo serikalini na waliotoka. Walipenda kumhusisha yeye kwa kuwa ndiye alikuwa mwenye dhamana ya usalama wan chi, alijua kila mpango wa kijeshi katika kurutubisha madini hayo ya Urani yaliyopatikana huko Mtwara, Msanga Mkuu. Aliwasikiliza kwa makini sana, lakini kwa kuwa siku yenyewe ilikuwa fupi akawaomba waonane siku inayofuata mahali Fulani pa utulivu, wakakubaliana kukutana Hoteli Embassy katikati ya jiji usiku wa saa tatu. Walipoagana Mheshimiwa Waziri akapewa bahasha ya khaki, alipoichungulia baadae akiwa nyumbani kwake ilikuwa ni hundi ya milioni tano, bila jasho. Akakenua meno yake kwa furaha ya kujipatia pesa hizo.
Inaonekana huu mradi una pesa, nitawasikiliza kesho, alijiwazia na kuitupia ile bahasha katika briefcase yake ya kazini.
§§§§§§
Ilikuwa ni juu kabisa ya hoteli hiyo, walipoketi watu hawa watatu wakiongea biashara hiyo haramu.
“Tangu mwaka 1990 tumekuwa katika mradi huu na lengo kubwa ni kupata haya madini ama yawe yamerutubishwa au la, kwa kuwa sisi tunafanya biashara na makundi ya Kimataifa ya Kigaidi na yanayofanana na hayo, tuna miradi mikubwa. Sasa shida yetu ni kuwa tunataka haya madini ambayo yako hapa, kwanza kuna plan gani nayo tunajua, sasa kwa hilo tumeona tusubiri yakishatengenezwa makombora hayo ndiyo tunayataka sisi,” Shalabah alimwambia Mh. Waziri, akabaki anatikisa kichwa kuashiri anaelewa.
“Sasa hayo yote mmeyajuaje?” akawauliza.
“Aaah, si nimekwambia tuna watu tangu miaka hiyo waliokuwa wakifanya kazi ya kutuwekea mipango sawa, wakiwemo Mawaziri kadhaa, Katibu wa Wizara ya Madini Bwana Goloko Mikidadi na wengine katika ngazi mbalimbali, sasa tumepata mpango mzima na tumejua kuwa mnayarutubisha na kutengeneza makombora, sisi tunahitaji hayo makombora lakini sasa kama unavyojua hawa wazee wenggine wamestahafishwa, wengine wamefungwa na mambo mengi, tulikuwa na kikwazo kimoja, kulikuwa na mtu ambaye alikuwa ngazi ya juu pale katika bodi ya mradi huo naye aliwekwa na Mwl Nyerere mwenyewe, tukagundua kuwa alikuwa ni Usalama wa Taifa aliyekuwa akitoa siri hizi zote serikalini ndio maana ikapelekea ule mradi kusimamishwa kwa muda kabla ya kuanza tena na ndipo mkataba na kampuni ya Kirusi ukasainiwa, pale tulianza upya tena lakini kwa msaada wa walewale walio nje ambao serikali iliwaondoa kwenye nyadifa zao, tukajipenyeza na kuweza kujua kinachoendelea. Sasa tunataka nawe utusaidie kwa hilo, kujua nini kinaendelea na kwa kuwa information nyingi tunazo sasa ni kuyapata hayo makombola,” akaongea Shalabah.
Mh. Waziri akabakia kumwangali tu akimsikiliza kwa makini sana na kumwelewa kwa kina vile vile, akaijiweka sawa kitini na kuinua glass yake iliyojaa Whisky aina ya John Walker, alipoishusha akajikuna tumbo lake na kujikohoza kwa minajili ya kusafisha koo lake.
“Ok, nimekuelewa bwana Shalabah na bwana Balozi, kila kitu kinawezekana, pesa ipo?” akauliza.
“Pesa kwetu sio ugonjwa Mheshimiwa, tunazo nyingi kama matundu ya chandarua,” Shalabah akajibu na wote wakacheka, kisha Waziri akaendelea, “Ni kweli kama mlivyo na maelezo mengine, mpango nji uleule, na ujue sasa hii sio serikali ya awamu ya kwanza hii ni nyingine, Wanasayansi wetu wa jeshi upande wa milipuko wanashirikiana na wale wa jeshi la Urusi kutengeneza makombora yenye nguvu kubwa nay a masafa marefu ili kuimarisha ulinzi wa mipaka yetu na ile ya Afrika kwa ujumla.”
Shalabah alifurahishwa na manenoi hayo, “Sasa tunaweza kupata hayo Makombora? Tufanya biashara ya pesa nyingi na wapigania uhuru kote duniani, lazima tuhakikishe uhuru wetu unapatikana na nchi zetu kutambulika na kupewa haeshima duniani kote,” akaeleza.
“Na kwa hilo nakuhakikishia nitatoa ushirikiano mkubwa nanyi, kweli lazima tupiganie uhuru wan chi zetu,” Mh. Waziri akaunga mkono.
Kauli ile ikawashtua kidogo Shalabah na yule Balozi.
“Msishtuke, mimi kiasili ni Msomali, wazazi wangu waliingia Tanganyika miaka hiyo, kule Arusha, wakajichanganya na Wamburu hivyo ikawa ngumu kutambulika uhalisia wa uraia wao, nimekulia hapa, nimesoma hapa, na mara kadhaa nakwenda Somalia na kuona harakati kubwa za ukombozi, nilipendezwa nazo na nilitamani niwaunge mkono,” akawaeleza.
“Haujachelewa, wakati ndio sasa!” Balozi akamwambia yule Mheshimiwa.
“Mimi ni mbunge wa Mburu Magharibi, na nimekuwa jeshini kwa miaka mingi kule Monduli mapaka nachaguliwa kuwa Waziri wa Ulinzi ni mbunge wa Mburu Maghalibi, na hili ni kosa kubwa la Serikali ya Tanzania, haina muda wa kuchunguza uraia wa mtu, ilimradi umeishi miaka mingi, wanakupa ubunge wakitaka, uwaziri kama hivi na kadha wa kadha nah ii itawagharimu sana, siwezi kuacha watu wangu wanateseka kupigania uhuru wao eti kwa sababu ni nchi iliyonilea, never,” akaongea kwa hisia.
Kauli ile iliwafurahisha wote walikuwapoa hapo, vinywaji vikaagizwa tena na kuku wazima wawili wakaletwa mezani.
“Sasa sikilizeani, process ya kutengeneza hayo makombora itaanza mwaka ujao na itachukua miaka kama mine hivi mpaka kukamilika kwa sababu ni teknologia mpya inayobuniwa, na awamu ya kwanza tutaangua makombora ishirini na tano mazito, hivyo nitawapa taarifa ya kila kitu,” akawaeleza.
Kikao hicho kisicho rasmi kilihitimishwa majira ya saa tano usiku kwa makubaliano ya kuunganisha nguvu, Waziri wa Ulinzi wa kipindi hicho alikubali kufanya hujuma hiyo kwa Taifa lililomlea na kumpa maisha bila kujali.
MIAKA MINNE BAADAE
MOGADISHU – SOMALIA
“Sasa inabidi uwe bega kwa bega na bwana Goloko Mikidadi kwani yeye ndiye Master Plan wa mradi huu kwa upande wetu, nimefurahi mlivyofanya mbinu za kumuua yule kizabizabina Chamellaon, sasa mambo ni murua,” Shalabah na Hussein walikuwa kwenye kikao kifupi na wadau hao katika kasri la Mr. Lonely.
“Bila shaka! Ila kma nilivyowaambia na imeelezwa katika hilo kabrasha, hisyo ni siri ya serikali, mi nimeitoa kwenu, miaka miwili baadae tutafanya jaribio la kwanza la makombora hayo kule Caspian sasa tunafanyaje, hatuwezi kuyauza kama mishikaki lazima tutumie mbinu makini kuyapata,” yule Waziri alieleza.
“Ndiyo, lazima itumike mbinu ambayo haitaonesha uwepo wa hujuma kati yetu na serikali ya Dodoma,” Goloko alidakia.
“Sawa, hilo mtuachie sisi tu, sisi ndiyo tunajua la kufanya, lakini mnatuhakikishia kuwa kila kitu ni sawa? Hakuna tena kama akina Chamelleone,” Shalabah alionesha wasiwasi.
“Usiwe na shaka kijana, mimi ndiye Waziri wa ulinzi, of cause kuna kidudu mtu kimoja hivi na hiki nitakifanyia kazi mapema tu ili ikiwezekana kama si kukiua basi kukiondoa kazini, na ninajua nitafanya nini,” Waziri aliongea huku kauma meno.
“Nakumaini sana Mheshimiwa,” Shalabah akajibu huku akipigapiga mgongoni.
Siri za serikali juu ya mpango wa kurutubisha na kufanya majaribio ya makombora hayo ulitolewa na Waziri wa Ulinzi kwa kuuza kwa wafanyabiashara hao wakubwa. Pesa ilifanya kila kitu, ilimnunua kila mtu, pesa ilinunua uzalendo na kuweka usaliti na hujuma mahala pake.
Wakapeana mikono na kukumbatiana kwa mafanikio ya kazi yao, na sasa ilisubiriwa tu wakati ufike taratibu nyingine ziendelee.
§§§§§§
Kamanda Amata alipanda ngazi akifuatana na Daudi mpaka katika mlango mmoja uliondikwa MANAGER, hakugonga aliingia tu moja kwa moja na kuufunga nyuma yake, akatoa kofia yake na Daudi akafanya hivyohivyo. Yule Meneja akashtuka kuwaona watu hao, akasimama kama aliyemrishwa.
“Vipi? Kuna tatizo?” akauliza huku akihemaa harakaharaka.
Daudi alitoa bastola yake na kuigongesha mtutu wake juu ya meza ya huyo meneja, huku akimwangalia usoni.
“Pasingekuwa na tatizo tusingekuja lakini kwa kuwa wewe unajua kuwa sisi tulishakufa basi leo mizimu imekutokea, tunamtaka Mr. Lonely, haraka sana, hakuna maelezo, hutaki kutuambia tunakuua hapahapa, hatuna masihara na mtu,” Kamanda akamwambia na wakati huohuo, Daudi alimvuta mkono na kumsogeza pembeni ya meza yake ili asije kubonyeza kitufe cha kuita walinzi.
“Hamna tabu, msiniue nitawaeleza anakoishi lakini huyu mtu sijui kama ni mtu kweli, yupo tu kwa jina, yeye haonekani, utamwona tu katika luninga,” yule meneja akajibu kwa kubabaika.
“Sawa, ni wapi anaishi au hapo ilipo hiyo luninga ni wapi?” Kamanda akauliza.
“Wadada Jaziira, nyumba yake iko pekee yake baada ya kuyapita maghala ya bandari, imezungukwa na ksitu mdogo wa kupandwa,” akajibu huku akiwa amelowa jasho mwili mzima kwa woga.
“Asante sana, nikikuhitaji nitakuja tena,” Kamanda alimwambia huku akiuendea mlango. Daudi alifuata nyuma, baada ya Kamanda kutoka nje ya ofisi ile, Daudi alikuwa ametoka nusu akatazama ndani ya ofisi hiyo kama aliyesahahu kitu, akainua bastola yake yenye kiwambo cha sauti, “Hustahili kushi,” akafyatua risasi na kupiga kwenye paji la uso la meneja huyo, akasota ukutani na kuserereka mpaka akaketin chini damu zikimvuja kisogoni. Daudi akachomoa ufunguo na kuufunga mlango kwa njue, akavaa kofia yake kama mwanzo na kuondoka eneo hilo.
DAR ES SALAAM
Waziri wa Ulinzi aliteremka kwenye gari yake kwa uchovu akiwa na mawazo lukuki, alipokelewa na mhusika na moja kwa moja akaingia ndani ya Ikulu ya Tanzania, akaongozwa mpaka kwenye ofisi maalum ambayo Mheshimiwa Rais na jopo lake la uchunguzi walikuwa humo. Aliingia kwa kitetemeshi, hakuna aliyemsemesha zaidi ya kugongana macho na Madam S. akaoneshwa kiti akaketi.
“Mheshimiwa, nilikuheshimu sana kama mmoja wa wasahauri wangu wa ulinzi wan chi hii lakini nasikitika sana kwa yale uliyoyashiriki na kutufanyia hujuma mbaya kama hii, umekuwa mbunge, tukakupa na uwaziri, ndiyo, umefanya kazi nzuri sana katika wizara yako lakini nasikitika kwamba wewe ndiye unayejulikana kwa jina la Mr X katika watu walioshiriki hujuma hii chafu. Kwa nini umewahujumu Watanzania? Wamekukosea nini?” Mheshimiwa Rais alikuwa akiongea kwa uchungu sana, ukumbi wote ulikuwa kimya kabisa ni kiyoyozi tu kilichokuwa na uhuru wa kutoa mlio humo ndani. Waziri wa ulinzi hakuwa na jibu, kwani aliyokuwa akiambiwa alijua kabisa kuwa ni kweli tupu.
Yakafuata majadiliano marefu katika jopo hilo, na mwisho muafaka ukafikiwa.
“Sasa wewe ni mtu mkubwa serikalini, tunaendelea na uchunguzi na wakati huu wa uchunguzi, hutakiwi kutoka nje ya mji wa Dar es salaam bila kibali change na popote unapoenda nje mji lazima usindikizwe na watu wa usalama, tunazifunga akaunti zako zote, huwezi kutoa wala kuingiza pesa, kwani imeonekana una akaunti Uingereza na jana imepokea mabilioni ya shilingi, hongera sana, nimemaliza, sio peke yako wapo na wengine wengi,” Rais alimaliza kuzungumza. Waziriwa Ulinzi akawekwa kizuizini akiwa anaangaliwa kwa jicho la karibu kwa kila afanyalo. Serikali ilihakikisha ndani ya saa tano imewakamata wote waliohusika na kuahidi kuwafungulia mashitaka. Lakini mtu mmoja hakupatikana na huyu ni Goloko Mikidadi.

§§§§§

Majira ya saa sita mchana, chopa za JW ziliwasili katika Uwanja wa Jeshi la Wananchi, familia, ndugu na jamaa za wapiganaji hao zilikuwa hapo kwa ajili ya kuwapokea ndugu zao. Furaha zilitawala, shangwe na hoihoi. Hakuna aliyetegemea kuona tena sura ya nduguye kwa kuwa walikuwa wakijua wazi jinsi Somalia kulivyo, ama wangeishachinjwa au kuuawa kwa jinsi yoyote ile.
“Karibu nyumbani mpenzi,” ilikuwa ni moja ya sauti kati ya nyingi iliyosikika uwanjani hapo, akimkumbatia mumewe na kumpa busu la mahaba.
“Sikutegemea kama utarudi baba,” mtoto alimwambia baba yake upande mwingine wa eneo hilo. Mkuu wa Majeshi Jenerali Kamsumi pamoja na mwambata wake walikuwa katika eneo hilo kuwapokea wahanga hao. Wanajeshi wale walijipanga mistari miwili na kumsikiliza Mkuu wao alipokuwa akiwaambia maneno mafupi ya faraja, kisha akawapa likizo ya miezi miwili kila mmoja ili wakapumzishe akili zao kabla ya kurejea kazini.
Wale wanajeshi watano wa Urusi wangekabidhiwa kwa Balozi wao baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu katika hospitali ya jeshi ya Lugalo. Watu walitawanyika na kuuacha uwanja huo mkiwa kama walivyoukuta, furaha na shangwe zilihamia majumbani mwao, ikiwamo na kupeana zawadi za ushindi.
§§§§§
MADAM S aliitoa miwani yake usoni na kuiweka mezani huku mbele yake akiwatazama vijana wake makini wa idara ya kijasusi ya serekali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Chiba, Scoba, Gina, Dr. Jasmine.
“Hongereni kwa kazi ngumu ambayo imetuumiza vichwa sana kuikamilisha, kila mtu aliifanya kwa upande wake na kwa pamoja tumeikamilisha, nadhani mmejionea wenyewe, kikulacho ki nguoni mwako, hila za Waziri wa Ulinzi kufanya mpaka Kamanda Amata aondolewe kazini ilikuwa ni kuhakikisha njia nyeupe kwa mpango huu wa kidhalimu, kumbe ndiyo Mr. X. Ili kuhakikisha hujama hii inahitimishwa sawasawa, nawapa kazi, nah ii ni kutoka hapa ofisini na siyo mahali popote, nataka wachunguzwe viongozi wote mmoja baada ya mwingine, na ndani ya mwezi mmoja kila mtu aniletee tafutishi zake nini kimegundulika, lazima kuna makandokando,” Madam S aliwapa maagizo vijana wake watiifu kuhakikisha wananusa kila kona ili kujua lolote linaloambatana na hilo. Wakiwa katika mazungumzo hayo, simu yake ya ofisini ikapata uhai, ikaunguruma kwa fujo kama imepewa adhabu kufanya hivyo, akainyakua na kuiweka sikioni, huku akimpa ishara Chiba ahakikishe amerekodi simu hiyo. Madam S alikuwa na tabia ya kurekodi simu zote zinazoingia katika ofisi yake hata iwe ya kirafiki, nah ii ilimsaidia sana hasa anapokuwa anataka kumbukumbu ya jambo Fulani, lakini si hilo tu, huwa anaandika katika kitabu chake cha kumbukumbu mambo yote yanayotukia kwa kila siku yake,
kikazi na kifamilia.
“Hallo!” aliita katika simu ile.
“Kamanda Amata,”
“Ooh Kamnda, nipe mrejesho, najua kazi umeimaliza na sas bado sikuoni nyumbani nakuhitaji haraka sana,” Madam S alimwambia Kamanda kwenye Simu hiyo.
“Bado sijamaliza kazi ndio maana sijarudi, nipo hapa na Komandoo wa JW, Daudi aliyepotea katika mazingira ya kutatanisha, yuko mzima na salama, tutarudi wote nyumbani, lakini pia tuko, Madam, kuna kazi naimalizia mchana huu kisha nitarudi nyumbani.”
“Usijali Kamanda, nakutakia mema katika kumalizia kazi hiyo, Gina anakumiss sana na anakusubiri kwa hamu,” Madam S akarusha utani ndani ya simu hiyo. Kamanda Amata upande wa pili alicheka sana kisha simu ikakatika.
Madam akawageukia vijana wake, “Mnasalimiwa na Kamanda, atarudi si muda kuna kazi kidogo anamalizia.”
Kila mtu alionekana kuwa na furaha kwa kupata habario hizo kutoka kwa Kamanda. 10
AKIWA NDANI ya suti safi ya rangi nyeusi, kiatu kilichong’azwa kwa Kiwi, nywele zililizowekwa kwa mtindo wa kupendeza, miwani ya jua iliyomkaa vizuri kabisa, Kamanda Amata aliteremka katika gari moja ya gharama sana iliyokuwa ikiendeshwa na mwanamke mrembo kabisa, aliyependeza kwa mavazi yake yenye ving’arong’aro, unaweza kusema ni Muhindi lakini pia utasema ni Mwarabu yote yangewezekana. Gari hiyo aina ya BMW iliegeshwa pembeni tu mwa jumba kubwa la kifahari lenye bustani ya maua ya kupendeza, ukimya ulitawala eneo hilo ni kelelel za ndege tu zilizikika kwa nadra kidogo kutokana na hali ya jangwa ya eneo lile hakukuwa na viumbe kwa wingi, Kamanda Amata hakuona mtu yeyo te katika mazingira ya jumba hilo pweke. Aliiacha gari iliyomleta ikiweka maegesho vizuri, akapanda ngazi kuuelekea mlango mkubwa wa nyumba hiyo, akaitoa simu iliyokuwa mfukoni mwake, simu ya Shalabah, akabofya vitufe fulani Fulani, kisha akashika kitasa cha mlango huo na kuusukuma ndani, ukafunguka, akaingia na kuufunga nyuma yake.
Mbele yake alilakiwa na sebule kubwa, safi isiyo na samani yoyote, akapepesa macho huku na kule labda ataona mlango eneo hilo lakini hakuona kitu zaidi ya mapicha ya ajabuajabu yaliyotulia ukutani na kufanya ndani humo kuwa mwa kuogofya. Akaitazama tena ile simu, na kuitafuta majina yaliyomo katika orodha, yote hakuyajua hata moja, akaamua kuzunguka sebule ile huku akiangalia kwa makini kila kilichowekwa au kuning’inizwa ukutani. Kati ya masanau na mapicha yote yaliyowekwa juu ukutani, ni sanamu moja tu lilikuwa chini kidogo, sehemu ambayo unaweza kuishika kwa mkono wako bila kufanya jitihada yoyote. Akagusa lile sanamu, mara akaona jicho la sanamu hiyo likichezacheza.
“Shiiit!” akatamka kwa sauti hafifu, wakati anatoka eneo lile akaligonga lile sanamu bahati mbaya mara kipande cha ukuta kikasogea pembeni, ukabaki uwazi, ujia mrefu uliingia ndani ya uwazi huo, Kamanda Amata akachomo bastola yake na kuingia ndani ya ule ujia, akapita kwa hadhari kubwa sana akitazama milango iliyojipanga katika ujia huo, lakini kila alipoutikisa mmoja hauukuwa na dalili ya kutikisika seuse kulegea. Mlango wan ne kutoka mwisho, aliposimama tu mbele yake ukafunguka, kulikuwa na kijichumba kidogo kiking’azwa na taa hafifu na muziki laini wa kihindi ulisikika taratibu, akatazama kwa makini mle ndani na juu akaona kuna kamera ya usalama.
Wameniona, akajisemea kwa sauti yake mwenyewe ya kuweza kujisikia yeye tu, akaingia na mara hiyo kijumba kile kikaanza kuteremka chini. Kamanda Amata akateremka kwenye hicho kijumba na kukutana na sebule nyingine kubwa zaidi ya ile, lakini tofauti na ile, hii ilikuwa na kila aina ya samani ya thamani ya juu, viti vyenye nakshi ya dhahabu, viliizunguka meza kubwa sana iliyokuwa hapo, kioo kikubwa cha luninga kilitulia mahala Fulani katika ukuta wa jumba hilo. Mara taa zikawaka zenyewe mle ndani na kufanya mwanga kuwa mkali zidi ya ule wa kwanza. Kamanda Amata akashika bastola yake sawia katika kiganja cha mkono, sauti ya vicheko vya kiume ikaanza kusikika ndani ya sebule ile.
“Aaaaaa ha ha ha ha…. Karibu sana kwenye Kasri ya wasio hai, umekuwa mgeni wangu wa dharula sana siku hii ya leo ukizingati nilikuwa safarini kuondoka, najua kilichokuleta labda umekuja kumfuata huyu ndugu yako…” ile sauti ikasema hayo. Mara ile luninga ikapata uhai ikaonesha picha ya kuogofya sana, mwili wa Goloko Mikidadi uliokuwa umechomwa kwa vyuma vinene upande mmoja na kutokea upande mwingine, akiwa ameachama kinywa chake na macho yamemtoka.
“Shiiit” akang’aka Kamanda Amata, ile sauti ikacheka tena.
“Sasa na wewe utakuwa kama huyu si muda mrefu,” ile sauti iliendelea kuongea.
“Acha ujinga wako, nimekuja kukumaliza wewe unayefanya biashara haramu za kuiharibu dunia,” Kamnada Amata aliongea huku akiwa ameuma meno.
“Aaaaaa ha ha ha ha aaaaaa ha ha ha, wacha kunichekesha, tangu lini mfu akafa tena?” ile sauti ikauliza kwa kebehi huku ikitanguliwa na cheko la dharau, lililomfanya Kamanda Amata kufura kwa hasira.
Aliinua bastola yake na kupiga ile luninga, iksambaratika yote, ikamwagika chini vipande vipande, nyuma ya ile luninga akaona tundu kubwa la kupita hata land cruiser, na kiti kimoja kilicholala chini, mezani palikuwa na kamera ndogo DV Cam, akaruka kile kihunzi na kuingia ndani, akatazama huku na kule akaona mlango mmoja ukiishi kufungwa, akauwahi na kuupiga teke, ukafunguka, akaingia kwa fujo na kuupiga kikumbo mlango mwingine kwa ndani, mara akasikia kelele ya mlio wa injini ya boti iliyokuwa ikiwashwa, akageuka kulia na kuona boti iliyokuwa ikitaka kuondoka, na mtu mmoja alikuwa juu yake, akafyatua risasi ikapiga injini, injini kazima.
Kamanda Amata hakufanya ajizi, risasi moja ya mgongo katikati ya uti, ikagawanya pingili hizo.
“Aaaaaaaaa nooooooo!!!!” ilikuwa sauti ya yule mtu akijibwaga upande wa nyuma, Kamanda Amata akajivuta na kumshika akamvuta mpaka nje ya lile eneo lililokuwa na boti akamlaza sakafuni.
“Leo mfu lazima ufe tena, shetani mkubwa!” Kamanda akamwambia Mr. Lonely.
“Tafadhali, umeshaniumiza, basi niachie uhai wangu, nitakupa pesa nyingi sana,” akaongea kwa tabu.
“Wewe umeacha uhai wa watu wangapi mpaka leo?”
“Nitakupa pesa nyingi,” akalalama.
“Pesa zako zinanuka,” akafyatua risasi moja na kupiga kwenye paji la uso, Mr. Lonely akalala kimya huku ametoa macho ya mshangao.
Alikuwa mwembaba mrefu, mwenye ndevu za kuhesabika, upara ulitawala kichwa chake, mavazi yake ya kawaida yangemfanya aonekane ni mmoja wa masikini huko mtaani.
“Mwisho wa zama zako Mr. Lonely,” Kamanda akasema hayo huku akiipachika ile bastola kwenye mkoba wake ndani ya suti.
Akauacha mwili ule na kutoka ndani ya jumba lile.
Nje kabisa alisimama kulitazama jumba hilo la kifahari, akageuka na kuingia katika gari ileile aliyokuja nayo.
“Twende,” akamwambia yule mwanadada, wakaondoka kuifuata barabara kubwa. Umbali kama wa mita mia moja hamsini, “Simama,” alimwamuru yule dereva mwanadada. Akashuka na kulitazama lile jumba, akinua saa yake na kuizungusha kwenye pete yake ya juu, mlipuko mkubwa ukatokea katika lile jumba, moto na moshi mzito, kishindo kililisambaratisha lile jumba lote lililoitwa la kifahari.

UWANJA WA NDEGE WA ADEN ADDE – MOGADISHU
KAMANDA AMATA akiwa amemkumbatia Fasendy dakika chache kabla ya kuagana, aliyashuhudia machozi ya mwanamke huyo mpiganaji yakikifikia kifua chake, “Sina budi kwenda Fasendy, kwa heri, tutaonana tena.”
“Wapi Kamanda? Hata hii imekuwa ajali tu kukutana, lakini asante kwa kila kitu,” Fasendy akamshukuru Amata.
“Usijali tutaonana popote duniani sio lazima Somalia wala Tanzania,” Kamnda akamwambia kisha akamtoa kifuani pake, akambusu shavuni, akavua saa yake ya kijasusi saa yenye kufanya mambo mengi sana, akampatia Fasendy, “Unikumbuke,” akamwambia.
Fasendy naye akampa kibegi kidogo mkononi mwake, “Unikumbuke,” akamwambia. Kisha Kamanda Amata akaagana na Chamelleon na timu yake, akaondoka kuingia uwanjani tayari kwa safari ya kurudi nyumbani.

˜˜MWISHO˜˜
1.jpeg
 
Story nzuri nadhani kuna kitu cha kujifunza hapa kutokana na maneno haya hapa...

"... na hili ni kosa kubwa la Serikali ya Tanzania, haina muda wa kuchunguza uraia wa mtu, ilimradi umeishi miaka mingi, wanakupa ubunge wakitaka, uwaziri kama hivi na kadha wa kadha nah ii itawagharimu sana, siwezi kuacha watu wangu wanateseka kupigania uhuru wao eti kwa sababu ni nchi iliyonilea, never,” akaongea kwa hisia."
 
Story nzuri nadhani kuna kitu cha kujifunza hapa kutokana na maneno haya hapa...

"... na hili ni kosa kubwa la Serikali ya Tanzania, haina muda wa kuchunguza uraia wa mtu, ilimradi umeishi miaka mingi, wanakupa ubunge wakitaka, uwaziri kama hivi na kadha wa kadha nah ii itawagharimu sana, siwezi kuacha watu wangu wanateseka kupigania uhuru wao eti kwa sababu ni nchi iliyonilea, never,” akaongea kwa hisia."
Nikweli kaka TODAYS
 
Simulizi : Hujuma
Sehemu Ya Tano (5)
“Sasa tunavamia, Fasendy utatangulia kwa sababu bunduki yako inaweza kupiga risasi mfululizo, mimi na Jamir tunakuja, tutatumia kamba hiyo hapo juu mpaka paleleee (akaonesha kwa vidole), pale tutajiachi na kufikia kwenye yale magunia kisha kila mtu atachukua nafasi yake, lakini wakati tunashuka Fasendy utakuwa ukipiga risasi kila unayemtaka ili kuwachanganya hawa Maharamia,” Kamanda Amata akatoa maelekezo na wote wakaitikia, Fasend alruka na kuidaka kamba kwa mkono wake mmoja huku ule mwingie ukifyatua risasi kuwalenga wale jamaa, Jamir na Kamanda nao wakafuatia. Watu waliokuwa katika shughulia hiyo waliacha shughuli zao na kukimbia kimbia huku na huko.
“Tumeavamiwaaaaa, tumevamiwaaaa,” kijana mmoja alikuwa akipiga kelele bila mpangilio. Kamanda Alijirusha na kutua kwa miguu yake miwili, mtu wa kwanza kuvaana naye alikuwa na bunduki kubwa mgongoni mwake, akampiga kikumbo na yule mtu akaanguka chini chali, alipotaka kujaribu kuinuka alijikuta akipigwa ngwala moja maridadi na kurudi chini kama mzigo, akachomoa bastola kwa haraka akiwa pale chini, akachelewa kwani risasi ya Jamil ilishafumua kichwa chake, Kamanda Amata akaichuku ile bunduki na kujibana sawia nyuma ya maboksi mengi yaliyozagaa katika lile eneo, alipotazama huku na kule alimuona Jamir aliyeshika bunduki yake kwa umakini kabisa lakini hakumuona Fasendy.
Maharamia wakatoka walikokuwako na kuanza msako wakiwa na silaha nzito nzito.

§§§§§


Gari ya Shalabah iliingia kwa fujo katika eneo la bandari, na nyuma yake alikuwa akifuatwa na Land cruiser iliyobeba wapiganaji wenye silaha. Shalabah akashuka, kwa mwendo wa nusu kukimbia na nusu kutembea alikutana na Hussein mlangoni akiwapanga vijana wake kumsaka Kamanda Amata.
“Hussein,” Shalabah akaita.
“Chief, huyu jamaa katuweza, lakini tutamtia mikononi,” Husseina alimwambia Shalabah.
“Ila ukumbuke wako watatu,” Shalabah akatoa onyo.
“Hatuna muda wa kupoteza ni kumsaka, Mr. Lonely hatotuelewa kama tutashindwa kuwadhibiti watu watatu tu, wakati sisi tuna jeshi kubwa la kutosha,”Hussein alikuwa akimwambia Shalaba.
Mlipuko mkubwa ukasikika upande wa pili, harufu ya baruti ikatapakaa. Shalabah akamwamcha Hussein, akiwa na shotgun mkononi mwake alifungua mlango na kutokea huko kwenye mapambano, alichanganyikiwa alipoona jinsi Kamnada Amata na Jamir wanavyowadhibiti viumbe hao.
§§§§§
“Endelea kudhibiti eneo mi nakwenda kuwatafuta wengine,” Kamanda akamwambia Jamir kisha yeye akahamia upande mwingine akiwaacha wake Maharamia wakiapambana na Jamir, Komandoo mwenye hasira kutoka Tanzania.
Kamanda Amata alteremka ngazi kwenda chini, akiwa kwenye ngazi, alijikuta akipamiwa nyuma yake, alisukumwa kwa mbele na kujibamiza katika ukuta, alipogeuka kumwangangalia ni nani, alipata konde moja kali lililotua shavuni, akayumba kidogo na kumwangalia vizuri mtu huyo aliyemchapa konde hilo. Konde la tatu kutoka kwa yule mtu halikumpata Kamanda, alilipangua kiufundi kwa kuudaka mkono wa huyo mtu kisha akageuka nao na kuuweka begani akauvuta kwa nguvu na kuvunja mifupa. Yule bwana akalia kwa uchungu. Kamanda Amata akageuka na kumchapa makonde ya maana mpaka yule bwana akalala chini kwa utulivu. Kamanda Amata akaendelea kushuka chini.
§§§§§
Ndani ya chumba kikubwa sana kisichokuwa na kitu, kulikuwa na watu kama thelathini hivi wakiwa wamewekwa pamoja, hakukuwa na kiti, wala kitanda, walikuwa wamewekwa tu kama watu waliopo mahabusu. Kati yao kulikuwa na Watanzania ishirini waliotekwa na Maharamia, walikuwa wametulia kimya kabisa, wengine wakicheza karata kupoteza mawazo na wengine wakicheza drafti. Chumba hicho kilichoko chini ya ghala la bandari kilitumika zamani kama stoo ya kuhifadhia vipuli vya meli lakini baada ya kujengwa bandari mpy pale Mogadishu na kuhamisha kila kitu, Maharamia hao walijibinafsishia eneo hilo, hakuna aliyewauliza kwa sababu ndani yao kulikuwa na sauti za wanene. Walihodhi eneo lote hilo, na ukionekana kulifuatilia siku inayofuata ungeamka bila pumzi.
Mmoja wa wale mateka, mwanajeshi wa jeshi la maji wa Tanzania, alishtuka ghafla kutoka usingizini na kuwakuta wenzake ambao walikuwa wakicheza drafti wakiwa wanaendelea na mchezo wao, hawakuwa na usingizi wala hamu ya kulala, kila mmoja aliwaza hatima yao isiyojulikana.
“We vipi, mbona unshtua wenzako?” mmoja akmwuliza.
“Tulieni,” akawaambia huku akiwaoneshea kidole juu kuwapa ishara ya kutega sikio.
“Nini? Kuna nini?” mwingine aliuliza.
“Sikilizeni,” aliendelea kuwasisitizia. Wote walitulia lakini hakuna walichokisikia.
“Ah, achana nae huyo ameshanchanganyikiwa,” mwingine aliyestuka usingizini akajibu kutoka kona ya chumba hicho.
“Oya, sikilizeni AK-47 inavyolalamika huko, kimenuka!” akawaeleza mara hii akiwa amesimama wima.
Mabishano ya milio ya bunduki ilianza kusikika kwa ukaribu, wote walinyanyuka, hakuna aliyelala tena, walijua wazi kwa jinsi sauti zile za milipuko ya risasi zilivyokaribia eneo ambalo wapo wao, kwa vyovyote ni vita ya ukombozi.
§§§§§§
Kamanda Amata aliruka kwenye ngazi na kutua katika mwimo wa ngazi hiyo na kuserereka nayo kuja chini huku mkononi mwake AK-47 ikilalama na kufumua mtu mmoja baada ya mwingine.
“Yuko huku!!!” jamaa mmoja aliita kwa nguvu na wenzake waliokuwa juu wakaanza kuteremka chini kumfuata Amata, lakini walijikuta wanagonga ukuta baada kukutana uso kwa uso na Fasendy aliyekuwa amekamata bunduki kubwa aina ya SCAR H (Special operation Combart Assault Rifle), bunduki ya Kibelgiji, alianza kumwaga njugu na kuwarudisha nyuma wale vijana.
“Rudini msijeee!!!” mwingine aliwazuia wenzake.
“Kamanda, songa mbele,” Fasendy alipiga kelele huku akirudio juu.
Wakati yote hayo yakiendelea, Jamir alikuwa amefunga kazi katika upande wa juu, na alijificha mahala ili aone kama kuna yeyote atakayeleta shida, mkononi mwake alitulia na SMG (SubMachine Gun. Eneo lote lilidhibitiwa na watu watatu waliojipanga vyema.
Fasendy, alikuwa akitembea kwa kunyata kuelekea kwenye ujia mrefu upande wake wa kushoto, huku bunduki yake ikiwa makini mkononi mwake. Mara ghafla alisikia mchakacho wa miguu nyuma yake alipogeuka tu, alikutana na konde zito liliuchana mdomo wake wa chini, akatoa yowe la maumivu. Kabla hajajiweka sawa, konde lingine lilitua shavuni, akajaribu kujitetea mbele ya mtu huyo, lakini ikawa ngumu, alipigwa teke la nyuma ya magoti akajikuta akiiga magoti, na bunduki ikimtoka huku akiachia risasi mfululizo.
“Mshenzi sana we mwanamke, umetugeuka siyo?” ilikuwa ni sauti ya Shalabah, aliyekuwa akiongea huku akimzunguka kusimama mbele yake.
“Nani amewasaliti?” Fasendy akauliza.
“Hujui siyo? Sasa utajua leo, na huyo mwanaume wako huko alikoenda ndiko liliko kaburi lake, hapa hatoki mtu,” Shalabah akajibu.
“Hata wewe hutoki kama ni hivyo,” Fasendy alijibu kijeuri huku damu zikimvuja katika mdomo wake wajuu uliochanika kwa konde la Shalabah.
“Sema mko wangapi?” Shalabah akauliza.
“Hata ukiniua, sintosema Abadan!” Fasendy alijibu kijeuri.
“Unajifanya jeuri sio?” Shalabah alimwambia na kumshushia kipigo cha nguvu, Fasendy hakuonesha makeke yoyote katika hilo alitulia na kujibwaga chini. Kutoka pale chini Lijizungusha kwa kasi na kumchota ngwala Shalabah, lakini Shalabah alikuwa mwepesi na kujigeuza hewani, kisha akatua kwa miguu yake.
“Fasendy, tulipokuwa jeshini mimi nilikuwa mkufunzi wako, tangu lini mwanafunzi akamshinda mwalimu?” Shalabah alijisifu.

§§§§§§


Jamir alisikia mabishano hayo ya Shalabah na Fasendy, taratibu akajitoa katika maficho yake akipiga hatua kusogea kule watu hao wanakoongea, kwa kuwa alikuwa akielewa kwa kiasi Fulani lugha ile, alijua Fasendy yuko matatani, hawakuwa na njia ya mawasiliano katika yao watatu, kila mmoja alipigana na kuwasiliana na mwenzake kwa hisia. Jamir alimuona Shalabah lakini kabla hajafanya lolote Shalabah alihisi uwepo wa mtu mwingine, akachomo bunduki yake na kufyatua risasi upande aliokuwa Jamir.
“Aaaaaaaiiigggghhhh!!!!!” sauti ya mamumivu ya Jamir ilisikika huku akijirusha upande wa pili na kujificha nyuma ya ukuta mwingine.
“Jamiiiiiiirrrrrrrrrrr!!!!!!” Fasendy alipiga ukelele baada ya jamir kuruka upande wa pili huku akitoa yowe la maumivu.
“Umemuumiza Jamir!!!” Fasendy alimpigia kelele Shalabah, lakini alizimwa na kofi kali la shavuni.
“Ndio, nab ado naenda kummalizia kabisa,” Shalabah akamuacha Fasendy pale chini na kukimbilia kwa Jamir, alipofika pale alipoangukia Jamir, hakumuona. Akabaki kapigwa na butwaa, si aliangukia hapa! Akashangaa, hakujua ni vipi au ni wapi jamir katorokea ilhali alikuwa kampiga risasi.
“Shiiitttt!!!” akapiga kelele na kugeuka kurudi kwa Fasendy, nako akapigwa na butwaa la mwaka Fasendy hayupo pale alipomuacha, hawa ni masehetani au binaadamu? Akajiuliza bila jibu, akatazama huku na kule akaelekea kwenye tundu kubwa la dirisha na kumuona Fasendy akiwa chini kabisa, akainua bunduki yake na kufyatua kumlenga, akachelewa, Fasendy alikwishaingia chini ya lile jengo na kushika ngazi za kuteremkia bondeni.
Shalabah akateremka kwa kasi kwenda chini huku bunduki yake ikiwa mkononi mwake, akainua simu yake ya upepo.
“Hussein, wasitoke hao, wanataka kutoroka nimewadhibiti vya kutosha, hawatuwezi,” Shalabah alimwambia Huseein kibonge cha mtu alipokuwa akishuka ngazi kwenda chini, lakini alishangaa sana kuona hajibiwi akaita tena na tena.
§§§§§
Kamanda Amata alijikuta akipigwa na kitako cha bunduki, kilimpiga chini kidogo ya shingo akhisi maumivu kwenye uti wa mgongo, aligeuka na konde zito, lililompeleka chini huyo aliyefanya kiotendo hicho, hakumsubuiri aamke, teke kali la usoni lilimgeuza upande wa pili na kumvunja mwamba wa pua, damu na makamasi vilivuja kwa pamoja.
“Funguo zikowapi?” akamwuliza huku akimfuata, yule jamaa akawa anasota kinyumenyume huku akionesha mkono ndani ya kiofisi Fulani kilichokuwa hapo jirani. Ilioneka ndiye alikuwa mtunza chumba hicho. Kamanda Amata akaingia ndani ya kile kiofisi kwa kurukia miguu miwili na kuutawanya mlango wote, akavuta droo na kuchukua fungu la funguo, akatoka nalo na kujaribu kila inayowezekana kufungua mlango huo, funguo ya tano ilikubali kuufungua, ukafunguka, lakini chumba kilikuwa cheupe hakina mtu, akamgeukia yule jamaa pale nyuma, akakuta hayupo akamuona akimaliziki kwenye kona Fulani ya ujia katika jengo hilo, shabaha madhubuti ndani ya sekunde mbili alimvunja mguu yule bwana akajibwaga chini kama mzigo. Akamuwahi pale pale na kumkamata ukosi wa shati lake.
“Unanifanya mimi bwege sio?” Akamuuliza, huku akimburuza na kurudi naye mpaka pale, “Chumba kikowapi?” akamtupia swali linguine. Yule jamaa alikuwa akiugulia mguu na pua yake.
“Sema haraka, sina muda wa kupoteza,” Kamanda alipiga kelele, akamgeuza chali na kumtumbukiza domo la bastola kinywani mwake, yule bwana akapiga kelele za woga huku macho yakiwa yamemtoka pima.
“Nasema, nnna ssssema!” alibwabwaja, Kamanda akatoa ile bastola, “Malango wa pili kwa ndani kushoto.”
Kamanda akamsonya na kumchapa kofi kisha akaingia ndani ya kile chumba na kukuta mlango mwingine, uliokuwa ukigongwa kutokea ndani lakini sauti hafifu sana ilikuwa ikitoka hapo kwani mlango ulikuwa ni wa chuma kizito. Akatumbukiza funguo na kufanikiwa kuufungua ule mlango.


§§§§§


Hussein alikuwa hajui afanye nini, alikuwa ndani ya chumba cha yale makombora na watu wachache pamoja nao, katika ile manowari kubwa ya JW waliyoiteka, ilikuwa imewekwa mahali maalum ambapo ukija kwa nje huwezi kuiona, kwani walikuwa wameizamisha chini ya bahari na kuifungi kwenye ghala yao iliyopo huko, ghala hiyo ilikuwa na uwezo wa kujazwa maji na kuwa kavu kadiri wanavyoamua wao. Alipokuja Kamanda Amata alikuta imejaa maji yote, lakini wakati wakiwa tayari kuyaondoa yale makombora kulikuwa hakuna hata tone la maji. Tayari makombora mawili yalikwisha ondolewa pale na kuingizwa kwenye ile PARPADOS, meli kubwa iliyoegeshwa nje.
Hussein, mtu mnene asiye na shindo kwa jinsi alivyonenepa, alikuwa kachanganyikiwa kiasi Fulani. Mkono akiwa kakamata shotgun na wale vija aliokuwa nao wote walikuwa wamekamata silaha za aina mbalimbali.
“Lazima atakuja huku mbuzi huyu, ni kuutoboa mwili wake kwa risasi mpaka huwe chandarua,” aliwaambia wale vijana na wote wakaziweka tayari bunduki zao.
Akainua redio yake, ambayo wakati inaongea hakujibu lolote, “Shalabah niko huku chamber, namsubiri huyo mbuzi afike nimmalize,” akamwambia Shalabah.
Kisha akawageukia wale vijana wake, “Mko tayari?”
“Yes Boss,” walijibu lakini walionekana wazi kutetemeka, waliona kama sinema inayotukia hapo, na wao wakiwa ni wamoja wa wachezaji sinema hiyo.

§§§§§§

DAR ES SALAAM – TANZANIA
MADAM S aliirudisha simu yake katika mkoba wake mara baada ya kupata taarifa ya kutoroka kwa Balozi wa Somalia. Akasimama na kuliaga jopo la wanausalama waliopo pale. Chiba alibaki kuangalia mawasiliano kama yanaenda vyema.
Madam S akatoka nje ya jengo la makao makuu ya jeshi, ilikuwa imetimu saa nane za usiku. Akachukua simu yake akabofya namba Fulani na kuiweka sikioni.
“Scoba, nahitaji helkopta haraka sana, inabidi tufike visiwa vya Zanzibar bila kuchelewa,” akaongea na simu hile.
“Umesomeka Madam, Uwanja wa ndege wa jeshi tafadhali kikosi namba KJ 603, haraka,” Scoba akajibu simu ile na kisha kujiandaa kwa safari. Alikwishaambiwa kuwa kwa muda huo wote ahakikishe anakuwa ndani ya eneo hilo la uwanja wa ndege wa Jeshi kwani anaweza kupata taarifa yoyote na ndivyo ilivyokuwa.
Madam S alikuwa katika mwendo wa kasi kuelekea Uwanja wa ndege na wakati huohuo, Gina naye alikuwa katika barabara hiyo kuelekea Uwanja wa ndege.
Wote wakaingia pale kwa tofauti ya dakika moja na sekunde kumi na tano, walikuta Scoba tayari akilipasha moto Chopa akiwa Keisha funga mikanda ya usalama na amekwishavaa vyombo maalum vya mawasiliano.
Madam S akakwea na kuketi katika siti ya mbele alkadhalika Gina akajitupa katika siti ya nyuma, Scoba akawapa ishara ya kufunga mikanda vizuri, akampa ishara Madam S ya kuvaa vyombo vya mawasiliano, milango ikafungwa, Chopa likanyanyuliwa kwa umahiri kabisa.
“Zainzibar, kuna boti iko majini inasafiri kwenda huko nataka tufike kabla yake,” Madam S akamwambia Scoba.
“Umesomeka, nilifikiri unataka tufanye fishing,” akajibu.
“Oh, no! hatuwezi fishing Kamanda hayupo, laity angekuwepo tungemuonesha jinsi tulivyo mahiri katika mambo kama haya,” Madam akajibu. Ile Chopa ikaendelea kupasua mawingu juu ya bahari ya Indi kukitafuta kisiwa hicho maarufu kwa zao la Karafuu.
Ukimya ulichukua nafasi ndani ya Chopa hiyo, wakimtazama kijana huyo mahiri katika kazi hiyo miaka kadhaa akilitawala dude hilo la Kirusi. Wakiwa angani waliona vitu viwili vikiwapita kwa kasi ya ajabu kimoja kushoto na kimoja kulia, ilikuwa ni kasi kuliko kasi unayoijua, wakaona kwa mbele vitu vile vikiwa ka ma kimwondo.
“Nini kile? Isiwe tumetunguliwa Scoba,” Madam S aliuliza.
“Usihofu mama, hakuna wa kutuletea shida kati anga letu wenyewe,” akajibu.
“Sasa kile ni kitu gani?”
“Usiogope ni watanashati wetu hao ni ndege aina ya kivita aina ya MiG-31E nayokwenda kasi kuliko kasi yenyewe, ina uwezo wa kwenda kilomita 3000 kwa saa moja,” Scoba alieleza.
“Waoh!” Madam S akashangaa, “Asante sana Jenerali Kamsumi.”

§§§§§

ILIKUWA ni furaha mateka wale kutoka ndani ya kile chumba, hawakutegemea hata siku moja kama litatokea, mbele yao mwanaume mkakamavu alisimama akihakikisha wote wanatoka ndani salama.
“Asante sana, sasa watatukoma washenzi hawa!” mmoja alisikika wakati akitoka katika chumba kile. Wale mateka walitoka na kutawanyika kila kona. Ilikuwa ni balaa kila anayekutwa alichezea kichapo cha maana na kunyang’anywa silaha yake, msako mkali ulianza ndani ya himaya ile, nje ndani, meli kubwa ya PARPADOS iliwekwa chini ya ulinzi pamoja na watu wake wote waliokuwamo ndani.
Kamanda Amata aliwahesabu wote kwa jumala yao walikuwa kama thelathini na nane hivi, zaidi ya wale ishirini na tano waliotekwa na ile Manowari ya JW kulikuwa na wengine zaidi kutoka Ufaransa, Ubelgiji na nchi za mbali, wote walitekwa meli zao za mizigo na Maharamia hao waliotikisa Dunia.
Eneo zima lilizingirwa na wapiganaji hao waliookolewa punde tu, wakiwa na hasira, waliwakung’uta vibaya Maharamia waliokutana na o hata wengine kupelekea kukimbia eneo.
§§§§§§
Saa ya Kamanda Amata ilimpa ishara ya kuwa kuna ujumbe unaingia, akaiinua na kuiruhusu.
….Dakika 85 hakikisha umewaweka watu wako mahali salama, Tai wako njiani msije mkanyakuliwa kama vifaranga vya kuku…
Ilikuwa ni ujumbe kutoka kwa Chiba, kwa harakaharaka huku akiwa macho huku na kule aliujibu ujumbe ule.

….hakuna sehemu ya kujificha, tutakuwa ndani ya meli kubwa, wasiiweke kwenye shabaha tafadhali…
Siwezi kutoka hapa kabla sijatenganisha roho na mwili ya Shalabah, akawaza Kamanda huku akikimbia tarataibu.
“Kamanda Amata!” ilikuwa sauti ya Fasendy ikiita. Kamanda akageuka nyuma kumtazama mwanamke huyo.
“Vipi?” akamuuliza.
“Shalabah!” akajibu. Amata akakza macho mwa Fasendy aliyekuwa akionekana kuwa na maumivu makali.
“Namtafuta,” akamwambia, Fasendy akampa ishara ya kumfuata, moja kwa moja wakafuata huo ujia mpaka kwenye mlango mmoja uliojitenga peke yake. Fasendy akasimama akamzuia Amata, pumzi yake ilikuwa ikitoka kwa tabu, alionekana kuchoka haraka.
“Fasendy nini?” Kamanda akauliza wakatia akijiandaa kufungua mlango.
“Sikia, ukimuua Shalabah, na Hussein kuna boss wao, Mungu mtu asiyeonekana kwa macho ya binadamu, anaitwa Mr Lonely, ukammalizie,” Fasendy alimwambia Amata.
“Kwa nini unasema hivyo, wewe utakuwa wapi?” akauliza kama mtoto. Fasendy akachomoka mikononi mwa Kamanda na kuteremka ngazi mpaka kwenye mlango mwingine, akampa ishara Kamanda Amata ya kuwa ni hapo, Kamanda hakusubiri, alimpa Fasend ile shotgun kisha akamhesabia moja mpaka tatu na kuubamiza mlango, kisha akaingia mzima mzima na kuruka sarakasi, akiwa hewani wale vijana wa Hussein walimlenga shabaha lakini hawakujua kama hiyo ilikuwa ni janja tu, risasi za Fasendy ziliwamaliza wote watatu na kuwaacha hoi wakiagana na roho zao. Kamanda Amata alipotua chini, konde la kwanza lililtua katika tumbo la Hussein, la pili hapohapo na la tatu.
“Siku yenu imefika,” akamwambia. Husein hakukubali kufa kizembe, alimpiga kichwa Amata, akayumba na kabla hajajiweka sawa, alipigwa ngwara kali iliyomuondoa sakafuni na kumpeleka hewani kabla ya kutua chini kama kifurushi.
“Kumbe ni mwepesi namna hii? Sikutegemea na ninashangaa hata umewezaje kumuua Sharon kwa uteke huu,” Hussein, mtu mnene alijigamba huku akiweka sawa suruali yake aliyoivalia tumbo.
“Aaaaaaiiiiiiiggghhhh!” Sauti ya Fasendy ilisikika. Amata akageuka kutazama kule mlangoni, akamwona Fasendy akiwa kabanwa kabali na mkono wenye nguvu wa Shalabah.
“Afadhali mmekuja wote kunirahishia kazi,” Amata akasema huku akinyanyuka pale chini. Hussein kwa haraka alirudi nyuma na kurukaruka kwa madaha huku akikunja ngumi zake, akarusha konde moja, Kamanda Amata akailikwepa na kumtandika konde la mbavu mpaka Hussein akaguna, kabla hajauachia mkono wa bonge hilo, alimuongeza ngumi nyingine mbili za nguvu ambazo zote zilitua mbavuni na kumlegeza Hussein, almwachia mkono na kumrukia teke moja kali la kuzunguka lililosukuma mpaka kwenye maboksi akajibwaga huko. Kabla hajanyanyuka Kamnda Amata alimuwahi pale pale na kuukamata mkono wake akauzungusha kwa nguvu ukatawanyika mifupa yake kwa ndani, Hussein alilia kama mtoto.
“Mwache huyo mwanamke!!” Amata alimwambia Shalaba wakati akimwacha Husseina na kugeukia upande huo.
“Unasema nini wewe mtoto Changudoa! Unafikiri ulivyowaweza hao na mimi utaniweza? Kwa taarifa yako mimi ndiye niliyemfundisha huyu mwanamke wako michezo yote hii anayoifanya, hapa, sasa kama na wewe unataka kujaribu sogea nikumalize,” Shalabaha akaijigamba mbele ya Amata.
“Sasa kwa nini unajiwekea ngao huyo mwanamke? Kama unaona unauwezo wa kupambana na mimi muache huyo uje kwa mwanaume hapa shoga wewe,” Kamanda Amata akamtia hasira Shalabah. Shalabah akauma meno na kumtupa Fasendy kwa nguvu kiasi kwamaba hakuweza hata kujizuia. Shalabah akiwa na kisu kikali mkononi mwake alimkimbilia Amata huku akiwa kauma meno.
“Iyaaaaaaaaaaaa!!!!!” alipiga makelele akiwa kadhamiria kumdidimiza Amata hicho kisu. Kamnada alishajipanga, aliruka hewani na kuzungusha miguu yake, mguu wa kusoto ukapiga mkono wenye kisu, kikaanguka na wa kulia ukatua kwenye shavu la Shalaba, akayupa na kujibamiza kwenye chuma kubwa lililofungwa hapo kwa ajili ya kuinulia vitu vizito.
9
“Gina hatutakiwi kumkamata Balozi kwa vitisho au nguvu, kwanza nataka ujue ni wapi anakwenda kama ni hapa ndani ya Zanzibar au ana safari nyingine, cha muhimu ni kuwa asiondoke katika nchi ya Tanzania,” Madam S alimwambia Gina ambaye alkuwa akisikiliza kila kitu.
“Sawa Madam,” Gina aliichomoa bastola yake na kuipachika vizuri kiunoni, “Sasa tunashukia wapi?” akauliza.
“Uwanja wa ndege, ningeweza kuwashusha hata Ngome Kongwe lakini usiku huu tutawashtua wananchi,” Scoba alijibu na dakika mojan baadae tayari chopa lile lilikuwa likiweka magurudumu yake juu ya ardhi ya Zanzibar. Madam S akifuatiwa na Gina wakashuka, Scoba akazima injini na kuteremka baadae.
“Karibu Zanziba Madam ijapokuwa umekuja kwa dharula hata Gahawa hatujaandaa, ila sio mbaya karibu sana,” alikaribishwa na kijana mmoja mtu wa makamo anayejulikana kwa jina moja tu Kwame. Kwame alikuwa ametumwa kikazi Zanzibar miaka miwili iliyopita kutoke idara ya Usalama wa Taifa.
“Tumekuja kuchukua mzigo kama inabidi,” Madam S akamwambia.
“Usijali, maagizo yako niliyapata na yanafanyiwa kazi, mzigo lakima muupate,” akajibua Kwame.
“Ok, usafiri?” Madam akauliza.
“Kila kitu kipoa Madam,” akajibiwa kisha wote wakaingia ndani ya Range Rover moja ya buluu, Scoba akaketi nyuma ya usukani kwa kuwa yeye wa idara hiyo.
Walitoka Uwanja wa Ndege na kuchukua barabar ya Nyerere, wakashuka nayo moja kwa moja mpaka hospitali ya Mnazi Mmoj, pale wakaiacha ile barabara ya Kaunda na kuchukua ya kulia. Barabara ya Mtoro mpaka Mkunazini, wakapenye vichochoro.
“Kijana kuna vichochoro havipitwi na magari utagonga!” Kwame alimwambia Scoba.
“Usaijali usiku saa hii hakuna wa kugongwa zaidi ya mchawi,” Scoba wakati anamalizia usemi wake alikuwa ameshatoke barabar ya Jamatini, akashuka nayo mpaka ile ya Mizingani, hapo kwa mwendo wa polepole akasimamisha gari yake. Gina akateremka na kutembea kwa miguu kuelekea katika bandari hiyo ndogo. Hakuingia bandarini kwani usiku huo kulikuwa kumefungwa, chini ya mwembe mkubwa kulikuwa na wazee wameketi walionekana kuwa ni walinzi wa eneo, hilo, waliketi wakinywa kahawa, akawaendea ili kupoteza dakika kadhaa hapo akiisubiri ile boti kuwasili.
Madam S aliitazama saa yake ilikuwa tayari ni saa tisa za usiku, akarudisha mkono chini na kufyatua kitia akajilaza.
“Bibi stahafu sasa! Tuachie vijana,” Kwame alimtania Madam S.
“Ah, Rais wenu hataki nistahafu, anataka nizeekee mpaka siku mnikute nimefia mezani ofisini,” akajibu.

§§§§§

Jamir alijiinua kwa taabu sana kutoka pale alipoangukia baada ya kupatwa na risasi za Shalabah, damu nyingi zilikuwa zikimvuja, katika sehemu ya mbavu hakuwa na nguvu tena zaidi ya kusota na kujibana nyuma ya ndoo kubwa la takataka, alipoona ukimywa umetawala, akainguka na kutembea kwa tabu huku akiifanya bunduki ya AK 47 aliyoiokota kuwa kama mkongojo wa kutembelea. Alifika sehemu yenye dirisha na kuchungulia nje, alisikia milio kadhaa ya bunduki huku watu wakikimbili kwenye ile meli kubwa iliyoegeshwa gatini. Alijikongoja na kuweza kutoka nje, wakati huo wale wanajeshi waliokuwa wametekwa walikuwa tayari melini, alijikokota mpaka lango la kutokea kule gatini, akapiga mbinja kali, wale askari kule juu ya meli walimuona, lakini hakuwajua kama ni mwenzao au la.
“Hima himaaaaaa!!!!!” mmoja akaropoka kwa nguvu na Jamir akaitikia, “Tanzaniaaaaaaaaa!!!!!”. Wawili kati yao wakateremka haraka na kwenda kumsaidia. Kwa mbali waliona gari zilizzokuwa zikija zikiwa zimewasha taa, wakajua sasa mambo yameharibika.
“Kamanda aliyetuokoa hayupo, tutaondokaje bila kumuona?” ubishano ulianza kati yao.
“Mwambie Nahodha asogeze mbali kidogo japo mita mia tano baharini ila tusiondoke,” mwingine alidakia. CHANZO : Deusdedit Mahunda
Watu wote waliokuwa wakifanya kwenye ile meli walikamatwa na kufungwa kamba na kuwekwa katika chumba kilicho chini karibu na injini.
Nahodha George, aliyekuwa ndani ya nguo zake nyeupe lakini sasa zilizochafuka na kunuka kwa jasho alikuwa akiuzingisha usukani wa ,eli ile, PARPADOS kuisogeza baharini wakiati wakipanga jinsi ya kumpat Kamanda Amata.
Jamir alilazwa katika kitanda na mwanajeshi mmoja mwenye taaluma ya udaktari akasogea na msaidizi wake nakuanza kumsaidia.
“Vipi?” mkuu wa msafara aliuliza.
“Risasi imeingia pabaya sana sana sijui kama ataweza kupona labda kwa kudura za Mwenyezi Mungu,” yule Daktari alimweleza mwanajeshi huyo mwenye nyota tatu mabegani mwake ambaye tangu mwanzo ndiye aliyekuwa kiongozi wa msafara huo uliokuwa ukielekea huko bahari ya Kaspian.
Jamir alifumbua macho akamtazama yule daktari, “Usiumie Dokta, hata nikifa nimeshafanya kazi niliyotumwa, nimeipigania nchi yangu, Tanzania, nimewapinia watu wangu, Watanzania, fanya unaloweza lakini ukishindwa basi muachie Mungu,” Jamir akafumba macho tena.

§§§§§

Kamanda Amata kwa haraka, alimuwahi Shalabah na kumchapa makonde kadhaa bila upinzani wowote, Shalabah akaiinua kutoka pale alipokuwa ameegemea, “Usifikiri mimi bwege wewe,” akasema. Alimuwahi Amata akamshika kwa vidole vyake kwenye mifupa ya mabega, Kamanda akasikia maumivu na kuhisi ganzi ikimwingia kwa kasi. Shalabaha akamsukuma nyuma na kumchapa konde moja lililomyumbisha na kumwongezea linguine ambalo lilimpeleka chini.
“Bado mtoto mdogo wewe kwenye mapigano,” Shalaba alimwambia Amata huku akikamata ukosi wa shati lake na kumpigisha magoti, kwa kutumia goti lake alimpiga kidefuni, Amata akadondokea nyuma, Fasendy aliyekuwa chini hakuweza kuvumilia, aliinuka na kumuwahi Shalabah akamdandia mgongoni na kumng’ata katika mshipa mkubwa wa shingo.
“Aaaaaaaiiiigggghhhh!!!!” Shalabah akapiga kelele na kumkamata shingo Fasendy kwa nyuma kisha akambinua na kumbwaga upande wa mbele, Fasendy akafikia mgongo, akatoa mguno hafifu wa kukata tama, lakini hakujali, alijinyanyua kiufundi na kuruka sarakasi matata alipita teke moja kali la kuzunguka lakini Shalabah akalikwepa vizuri, teke la pili nalo akalikwepa vilevile, alipotua chini akakuta na pigo kali lililopigwa kwa viganja viwili juu ya matiti yake, Fasendy akasukumwa nyuma kwa nguvu, alipopata nguvu za kusimama, alirudi kwa kasi kumvamia Shalabah.
“Fasendyyyyyyy!!!!!!!!!” Kamanda Amata alipiga kelele baada ya kuona Shalabah akichomoa kisu kutoka katika biatu chake kikubwa alichokuwa amekivaa, lakini alichelewa, Fasendy alikutana na kisu kikali kilichopenya katika tumbo lake pembeni kabisa chini kidogo ya mbavu.
“Aaaaaaaaa, ameniuaaaaa…” yalikuwa ni maneno ya mwisho ya Fasendy, akajibwaga chini, kwa nguvu na kile kisu kikabaki mkononi mwa Shalabah. Kamanda Amata akaainuka kama mbogo, Shalabah akafanya mchezo uleule, alikipima kisu kilipate tumbo la Amata barabara, kumbe mwenzake alishausoma mchezo huo. Alimkwepa kwa sentimita chache na kile kisu kikapita pembeni, Kamanda Amata akajiguza na kuudaka mkono wa Shalabah, aliuvuta kwa nguvu na kuusukuma chini, kisha kwa kisigino chake alipiga korodani za Shalabah, yowe likamtoka, akapiga tena kisha akamvuta mbele kwa nguvu na kumuweka sawa, konde moja la uso, la pili na la tatu yalimtoa fahamu kijana huyo mtukutu. Akageuka na kurudi kichwa kichwa, Kamanda Amata akaruka juu na kumnasa shingo kwa miguu yake akampiga kabala ya miguu na kushuka nae mpaka sakafuni. Shalaba alirusharusha miguu na mikono lakini ile kabala ilikuwa balaa, tungeiita kabali namba tisa, Shalabah alilegea na kutulia kimya, shingo yake ikiwa tayari imevunjwa na miguu ya Kamanda Amata. Akanyanyuka na kumuwahi Fasendy, akamuinua kwa mikono yake na kumfanya kama kaka kwa kuegemea mikono hiyo.
Hussein, akapata uhai ghafla, akazinduka kutoka kwenye mzimio mzito, akamuona Shalabah akiwa kalala chini miguu kaitupa huku na kule ulimi ukimning’inia nje, akaokota bunduki yake iliyokuwa imedondoka si mbali naye, wakatia huo Kamata akiwa na Fasendy akijaribu kumsaidia hili na lile labda atamwamsha, damu zilikuwa zinamvuja kwa wingi. Hussein aliinua ile shotgun na kulenga kisogo cha Kamanda Amata.
“Bastard!” alitamka maneno hayo huku akiondoa akiingiza risasi chemba. Kamanda Amata aliduwaa akapoteza mtandao wa akili yake kwa nukta kadhaa.
§§§§§
Huko nje, lori aina ya Jeifang ziliingia kama kumi hivi na kushusha askari wenye silaha waliovamia eneo lile, wakiwa na bunduki nzitonzito. Walikuja kusaidia wenzao waliozidiwa nguvu na askari wa Kitanzania, walitawanyika huku na huku kwa amri waliyokuwa wakipewa na kiongozi wao aliyekuwa katikati ya lango akiwapa ishara ya mkono kuashiria kushoto ama kulia. Dakika moja baadae wote wakazingira lile eneo na kuazna kusaka kila kona.
KATIKA ANGA LA SOMALIA
“...MiG-31E target 1, MiG-31E,” Rubani katika ndege ya pili iliyopewa jina la target 2 alikuwa akimwita yule wa target 1, wakiwa juu mita 23000 au futi 75,500 kutoka usawa wa bahari. Kadiri ya uzoefu wao tayari walikuwa kwenye anga la Somalia, ili kuweza kupata shabaha waitakayo kutoka na kasi ya ndege hizo, walianza kushuka taratibu kutafuata Mogadishu jambo ambalo ni ndani ya dakika tano tu wangekuwa wameifikia.
Walipohakikisha wameiona ardhi ya Mogadishu walifanya manuva na kila mmoja alikwenda upande wake kwa kuzigeuza ndege hizo ghafla, kisha wakazunguka na mmoja akatokea mashariki huku mingine akitokea Maghalibi.
“…MiG-31E Target 2 ready to engage,” sauti ya rubani wa ndege ya pili ilimwambia yule wa ndege ya kwanza kuwa yuko tayari kufanya mashambulizi. Wakati huo katika kipimo cha shabaha ndani ya ndege zile kila mmoja aliweka eneo analotaka kulipiga. Kwa sekunde iliyo sawa, wote wakabofya vitufe vilivyo katika mkono maalum kwa kazi hiyo ndani ya ndege hizo. Milipuko mikubwa ilitokea, mmoja ulipiga katika lango kulikokuwa nay ale magari yakishuhsa wapiganaji nwengine na mwingine ulipiga eneo lililokuwa na nyumba ya ghorofa iliyotumika kama ofisi au sehemu ya mikutano yao.
“Uuuuuuuuuuhuuuuu!!!!!” rubani wa ndege ya kwanza alishangilia kwa shabaha yake, akainyanyua ndege yake na kuipeleka juuu kwa kwa si kaipoiweka sawa akadondosha makombora manne ya maana yakashuka na kusambaratisha kila kilichosimama, ilikuwa ni hali ya kutisha, moto mkubwa ulifumuka na ndege hizo hazikwenda mbali zikilikuwa zikirandaranda maeneo hayo.
Baada ya kuhakikisha wamesawazisha ndani ya dakika moja waliambiana.
“MiG-31E target 1, Mission succesifull,” wa kwanza akamwambia mwenzake naye akajibu kwa mtindo huohuo wakimaanisha kuwa kazi yao ilikuwa imekamilika kwa ufanisi. Wakazipindua ndege zao na kuongeza kasi kurudi walikotoka na kuacha wapiganaji wa Maharamia wakiwa wameteharuki kwa hali hiyo, wakiokotana huku na huko.
§§§§§
PARPADOS ilipewa amri ya kuondoka haraka karibu na lile eneo la bandari, haikuwa na budi taratibu ilipiga maji kwa makata maji yake na ikazidi kuliacha mbali lile eneo la bandari na kusogea katikati ya bahari.
Poooooooooooo!!!! Honi nzito ilisikika baharini, wale wanajeshi waliokuwa kwenye deki ya ile meli waliitazma nyuma na mbele wanakoelekea na kuona meli nyingine kubwa kwa mbali. Hawakuitambua sawasawa pia kutokana na giza nene la saa tisa usiku.
“Unaombwa kusimamisha meli yako hapo kwa usalama wako,” ilikuwa sauti iliyotoka katika ile meli kubwa waliyoikuta imepiga nanga katikati ya maji, Nahodha wa jeshi la maji la Tanzania hakukaidi, alizima injini na ile meli ikapunguza mwendo taratibu.
BARNATOV LINE, maandishi yaliyosomeka ubavuni mwa meli ile ya kijeshi.

“Colonel, sisi ni wanajeshi wa Tanzania, tuliokuwa mateka chini y maharamia wa Kisomali,” mkuu wa msafara katika meli ya PARPADOS iliyowabeba wale Watanzania na wenzao alijitambulisha kwa niaba ya wote huku akipiga saluti kwa kanali huyo wa jeshi la Urusi.
“Sawa, Captain, je watu wetu mna habari nao?” yule Kanali wa jeshi la Urusi akauliza.
“Ndiyo Kanali wote wako salama kabisa, kama unavyowaona,” akajibu na kisha akawaita wale vijana watano wa jeshi la Urusi, wakapiga saluti kwa mkubwa wao.
Kanali wa Kirusi akatikisa kichwa kuonesha kuwa ameridhika kwa hali hiyo, “Ok, naweza kuondoka na vijana wangu,” akaomba.
“Hapana Colonel, inabidi mje muwachukue kule Tanzania kwani hawa walitoka pamoja nasi Tanzania nasi kwa mission maalum Sir,” yule mkuu wa msafara mwenye cheo cha Captain alimjibu.
“Ok, maadam tumejua wako salama hakuna shida, tutafanya utaratibu wa kuwachukua, asante sana Captain,” yule Kanali wa Kirusi akashukuru na ile meli ikaongeza kasi kuondoka eneo lile. Furaha ya kuokoka kwao ilikuwa dhahiri shahiri nyusoni na mioyoni mwao, waliimba wakacheza wakafungua vinywa vilivyojaa ndani ya meli hiyo na kugida kama hawana akili nzuri.
Jamir alikuwa kalala kimya kitandani huku macho yake ameyafumba, hakujitikisa wala hakufanya kitu chochote. Mara kwa mara daktari aliyekuwa akimwangalia alikuwa akimpima mapigo ya moyo kuona kama yanapiga au yamesimama. MV PARPADOS iliendelea kukata maji haikusimama mpaka katikati ya bahari, ikapiga nanga na wote wakasubiri, Nahodha wa meli hiyo akatafuta mawasiliano na makao makuu ya jeshi (JW) ili kuomba msaada wa haraka kwani wasingeweza kwenda mbali na meli hiyo.
§§§§§§§
Wakati Kamanda Amata akifikiria jinsi ya kujiokoa dhidi ya risasi itakayofyatuliwa na Hussein ambaye alikuwa akikenua meno, “Nimekupata, panya buku wewe!” akitamka maneno hayo, alivuta kifyatulio (trigger) lakini kabla hakijaruhusu risasi kutoka, Kamanda Amata alimshuhudia mtu huyo Kibonge akipaishwa juu na kubwaga kando, damu mithiri ya bomba ilikuwa ikitoka katika kichwa chake. Kamanda Amata akageuka kutazama kule ilikotoka ile risasi. Kidirisha kilichoruhusu mtutu wa bunduki hiyo kupenya kilifunguliwa wazi na mtu mmoja mfupi aliyeshupaa aliteremka na kuruka kwa ndani, akatua kwa miguu yake miwili akasimama. Amata alimtazama lakini hakumjua kwa kuwa alikuwa kavaa sox kuficha uso wake.
“Vipi, amekufa?” yule mtu akauliza kwa Kiswahili safi, Kamanda akamtazama tu bila kujibu wakati mtu huyo alikuwa akivuta hatua huku bunduki yake ikiwa mgongoni, akaenda pale alipolala Fasendy, akapiga goti na kuweka mgongo wa kiganja chake cha kulia katika shingo ya mwanamke huyo, akasikiliza kwa nukta kadhaa baadaye akamgeukia Amata, “Hajafa,” akamwambia.
Yule mtu akasimama na kuvua kofia yake usoni, sasa wakatazamana uso kwa uso na Kamanda Amata hakuna aliyekuwa anamjua mwenzie.
“Naitwa Daud Daud, mwanajeshi wa jeshi la hadhimu la Tanzania, nilikuja Mogadishu kwa operesheni hii lakini mwenzangu aliuawa vibaya na mimi nimiliponywa maisha yangu na huyu mwanamke, hata simjui kwa jina,” akajitambulisha na kutoa maelezo mafupi.
Kamanda Amata akamtazama yule kijana akahakikisha kuwa kweli ni Mtanzania baada ya kuona bendera ya Tanzania iliyobandikwa kwa juu ya mfuko wa kombati alilovaa.
“Naitwa Amata Ric,” lakini kabla hajamalizi Daud akamalizia “…Kamanda Amata.” Wote wakacheka na kupeana mikono.
“Ok Daud tutaongea vizuri, vipi hali ya huko nje kabla hatujatoka?” Amata akauliza.
“Huko nje kumevurugika, ndege vita za JW zilifika na kufanya kazi kubwa sana ya kusambaratisha ngome yote, utajionea mwenyewe,” Daud akajibu.
“Ok, tuna tuna kazi tatu, moja ni kumsaidia huyu dada, pili kufungua hayo makombola na kuchukua vichwa vyake, tatu ninahitajin kuonana na kiongozi wa hawa Maharamia anaewapa jeuri, Mr. Lonely,” Kamanda akamwambia Daud.
Kisha kwa kushirikiana wakaanza kufungua yale Makombora, huko nje moto mkubwa ulikuwa ukiwaka, kwa haraka haraka waliweza kufungua makombora yote nane kwa kuwa mawili tayari yalikuwa yamepakiwa kwenye ile meli PARPADOS.
Kisha wakafunga hivyo vichwa ambavyo kwavyo kuna mlipuko mbaya sana uliohifadhiwa, na hlilo ndilo bomu lenyewe. Vilikuwa ni vizito, wakavikusanya pamoja.
Mara mlango ukafunguliwa, Chammeleone akaingia na vijana wake waliokuwa tayari kwa lolote kutokana na silaha walizozibeba.
Alipiga makofi kumpongeza Amata, “Hongera sana kijana, sasa hapa si pa kukaa, hawa jamaa wako wengi sana, naomba tuondoke haraka,” akawaambia. Kwa kushirikiana na wale wafuasi wake wakabeba vile vichwa na kutoka navyo nje ilhali Kamnda Amata alimbeba mabegani mwake Fasendy, wakatoka ndani ya jengo hilo. Huko nje kulikuwa ni moshi na mioto kila kona, Kamanda Amata aliikubali kazi iliyofanywa na Tai kutoka Tanzania. Wakaelekea kwenye Land Cruiser iliyoegeshwa nje, wakapakia kila kitu na kuondoka eneo hilo.
Kamanda Amata alitulia kwenye landcruiser huku miguuni mwake amemlaza Fasendy aliyekuwa hajitambui, moyoni alikuwa akifikiria mengi sana, jinsi ya kumpata Mr. Lonely, alijua wazi kuwa huyu ndiye mzizi wa genge hili la wahuni ambao kazi zao ni kuteka meli za mizigo huku wakivunja sheria za kimataifa kwa kuzivamia zikiwa katika maji makubwa, maji ya kimataifa.
§§§§§§
DAR ES SALAAM – TANZANIA
Saa 12:00 asubuhi, gari ya Usalama wa Taifa ilisimama kwenye nyumba Fulani huko Masaki. Wanaume wawili wakateremka na kulijongea lango kuu la nyumba hiyo ya kiongozi wa ngazi za juu katika awamu ya kwanza. Mlinzi wa getini akafungua lango na kuwakaribisha vijana hao waliovalia suti nadhifu sana.
“Tuna shida na mzee,” mmoja alimwambia yule mlinzi.
“Shida sasa hivi?” yule mlinzi akauliza.
“Ndiyo sasa hivi,” mwingine akajibu. Yule mlinzi akainua simu ya mezani hapo katika kibanda chake na kupiga ndani ya nyumba hiyo kubwa ya kifalme akampa ujumbe mtumishi wa ndani naye akamwamsha huyo aliyekuwa mheshimiwa.
Alipotoka ndani akiwa katika pyjama alikutana na vijana hao, hakuuliza moja kwa moja aliwatambua kwa jinsi walivyoonekana, askari kanzu.
“Enhe, niwasaidie nini vijana ? mbona asubuhi asubuhi?” akawauliza.
“Mheshimiwa, sisi ni vijana wa Usalama wa Taifa, tumetumwa kutoka Ikulu, Mzee unatakiwa Ikulu kabla ya saa moja asubuhi, hivi tumetumwa kukuchukua,” mmoja akasema.
“Ikulu, kuna nini saa hii, mambo ya Ikulu tulishaachana nayo zamani,” akajitetea.
“Sisi ni wajibu wetu tu kukufikishia ujumbe kama ulivyo, unaitiwa nini utajua hukohuko,” yule kiongozi wa serikali ya awamu ya kwanza akabaki kaduwaa, akarudi ndani na kubadilisha nguo kisha akaondoka na hao vijana kwa kutumia gari waliokuja nayo.
Asubuhi hiyo, watu kama watano walikamatwa na wengine kuwekwa kizuizini, wakati uchunguzi ukiendelea, hawakutakiwa kutoka hata ndani ya nyumba zao, kila kabrasha lililohusiana na mikataba ya kampuni iliyokuwa ikichimba yale madini kule Msanga mkuu liliwekwa mezani upya na Mkaguzi mkuu wa serikali na kamati ya Bunge walianza kuyapitia tena.
ZANZIBAR
Asubuhi hiyo hiyo Gina alikuwa na vijana wengine wawili wa Usalama wa Taifa nje ya hoteli ya Serena pale Zanzibar, tayari kumkamata Balozi wa Somalia ambaye ilionekana alikuwa akishirikiana na Waziri wa Ulinzi kutoa siri za mradi huo na nini kinaendelea.
Waliingia ndani ya chombo cha kuwapandisha juu, Gina akabonya kitufe namba 4 na kile chombo kikawapandisha.
Wakafika mlango namba 456 kama walivyoelekezwa na mtu wa mapokezi. Wakagonga mlango mara tu ukafunguliwa. Wale vijana wakaonesha vitambulisho vyao na moja kwa moja wakaingia ndani ya chumba hicho.
“Mheshimiwa Mr. Balozi, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inakuweka chini ya uangalizi wake kwa muda usiojulikana, hii inatokana na mbinu chafu ulizokuwa ukizifanya kuihujumu nchi hii,” kijana mmoja alimweleza huku akimkazia macho, Mr Balozi aliishiwa nguvu, akajitupa kitandani na kuketi.
“Mnajua mi ni mtu mkubwa sana, halafu hamuwezi kuniambia hayo mnayoniambia bila kibali kutoka serikalini kwangu,” akalalama.
“Hatuwezi kukuweka chini ya ulinzi bila serikali yako kujua, inajua na ndiyo iliyoturuhusu,” yule kijana akamwambia. Mr Balozi hakuwa na ujanja, alijiweka tayari na kuondoka chiini ya uangalizi wa vijana hao mpaka kwenye gari ile aliyokuwapo Madam S, Kwame na Scoba, safari ya kwenda Uwanja wa Ndege wa Zanzibar ikaanza.
Pale waliingia naye kwenye Chopa na kumrudisha Dar es salaam ambako alirudishwa nyumbani kwake na kuwekewa ulinzi wa kutotoka kwenda popote mpaka uchunguzi utakapokamilika.
Halia ilikuwa tete kwa kila aliyejijua kuhusika na sakata hilo, matumbo yalijaa gesi zisizo na sababu, BP za kushika zikaongezeka, lakini katika yote hayo hakuna aliyemuona Bw. Goloko Mikidadi. Kila mmoja alijiuliza yuko wapi mtu huyo aliyewafanya wao kuwa ma-bilionea, hakuna aliyejua kama mwenzi wao, swahiba alikuwa chakula cha samaki wa Mr. Lonely. Hakika zilikuwa siku ndefu mno kwa mabwanyenye hao wenye uchu wa kuliibia Taifa. Hii ilikuiwa ni hujuma, hujuma mbaya kuliko yoyote iliyowahi kutokea.
Viongozi wenye dhamana na Taifa, haohao tena wanaliibia Taifa hilohilo, wanalihujumu na badala watetee Wanachi bado wanawakandamiza, wakilalia minoti ilhali yule wa kijijini anapiga mwayo wa njaa huku mkono wake akiwa kauweka shavuni bila kujua kesho yake inakuwa vipi.
Ni hujuma, watu wanapokuwa tayari kupigania Taifa lao, wanaposonga mstari wa mbele wewe unawakabidhi kwa maadui wanauawa wanadhindwa kulipigania Taifa lao, na wewe unakenua meno yote kwa kuchekelea ilhali familia za watu hao zinalia na kuomboleza zikiwa hazijui kesho na keshokutwa zitakuwa mgeni wa nani.
Waziri wa Ulinzi alikuwa ameketi sebuleni kwake akaiangalia kuninga kubwa kabisa iliyokuwa imening’inizwa ukutani, alivua kofia yake aliyokuwa ameivaa kichwani mwake na kuficha nywele zake zenye asili kama Kiarabu au Kisomali, akaiweka mezani. Ijapokuwa alikuwa na hofu lakini hakupenda kuionesha kwa yeyote, aliendelea kutazama Televisheni, aliendelea kunywa mvinyo wake taratibu. Mara simu yake ikaita kwa fujo, akainyakua na kuitazama kwenye kioo, private number, akasita kuipokea akaiweka tena mezani, akashusha pumzi za nguvu na kuvuta gazeti la Uhuru na kulipekuwa kurasa moja na nyingine kana kawamba hakuwahi kulisoma gazeti hilo.
Mara ile simu ikaita tena, akainyakua na kuona vilevile private namba, akaipokea kwa taabu na kuiweka sikioni. Akasikiliza anachoambiwa, hakika hakikumfurahisha, akajua sasa ni wakati wowote atakuja kuchukuliwa na kufikishwa panapohusika. Hodi ikabishwa mlangoni, akahisi kuchanganyikiwa. Akajua vijana watakuwa wamefika, afanye nini sasa kama mabilioni kayaficha Uswiss wakati wavuja jasho wanashinda na mlo mmoja na mlo wenyewe bado haukidhi mahitaji ya viini lise, ilimradi tu wamekula kujaza tumbo.
Aliikumbuka siku aliyoingizwa kwenye sakata hilo, uroho na uchu wa pesa, sasa aliona wazi vikimtokea puani.
Miaka Sita Iliyopita
Wizara ya Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa
JIONI ya siku hiyo, Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi alichelewa kutoka ofisini kwani alikuwa na kazi nyingi za kumaliza kabla ya safari yake ya kwenda UN kumwakilisha Rais wan chi katika mkutano wa masuala ya usalama hasa katikam nchi za maziwa makuu. Akiwa katika kupangapanga hiki na kile, hodi ilibishwa mlangoni kwake na Katibu wake, Miranda aliingia ndani akiwa na bahasha mkononi, bahasha iliyopendeza kwa rangi na maua, akakbidhiwa, akaipokea na kuichana kuangalia kuna ujumbe gani ndani yake.
Alikuwa akialikwa kwenye hafla maalumu iliyoandaliwa katika makazi ya Balozi wa Somalia nchini Tanzania, wiki moja inayofuata, akatikisa kichwa kuashiria amekubaliana nao.
“Isome kisha ijibu uwatumie taarifa,” akamwambia Miranda.
“Niwaambie nini?” akauliza.
“Positive,” akajibu kwa mkato akimaanisha kuwa amekubaliana na mwaliko huo.
Wiki moja Baadaye
Nyumbani kwa Balozi wa Somalia
Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi alikuwa ni mmoja kati ya wageni mbalimbali kutoka ofisi tofauti za kibalozi na taasisi zisizo za kiserikali walijumuika katika viwanja vya makazi ya Balozi huyo, ilikuwa ni Cocktail party, mara Balozi akamwendea Waziri wa Ulinzi na kumsalimu kwa makeke na bashasha pembeni alikuwa amefuatana na kijana nadhifu, aliyeonekana kashiba pesa, nywele zake hazikumficha kabisa kuwa yeye ni Msomali, lakini huyu alikuwa tofauti kabisa kwani alionekana kutakata kwa pesa.
Wakasalimiana wote watatu wakatambulishana kwa majina na shughuli zao.
“Ndiyo bwana Shalabah, kalibu sana Tanzania,” Waziri wa uUlinzi alimkaribisha kijana huyo kisha mazungumzo yakafuata. Hoja kubwa ilikuwa ni kumjuza Waziri huyo juu ya huo mradi wa Madini ambao unaendelea kati ya wadau mbalimbali waliopo serikalini na waliotoka. Walipenda kumhusisha yeye kwa kuwa ndiye alikuwa mwenye dhamana ya usalama wan chi, alijua kila mpango wa kijeshi katika kurutubisha madini hayo ya Urani yaliyopatikana huko Mtwara, Msanga Mkuu. Aliwasikiliza kwa makini sana, lakini kwa kuwa siku yenyewe ilikuwa fupi akawaomba waonane siku inayofuata mahali Fulani pa utulivu, wakakubaliana kukutana Hoteli Embassy katikati ya jiji usiku wa saa tatu. Walipoagana Mheshimiwa Waziri akapewa bahasha ya khaki, alipoichungulia baadae akiwa nyumbani kwake ilikuwa ni hundi ya milioni tano, bila jasho. Akakenua meno yake kwa furaha ya kujipatia pesa hizo.
Inaonekana huu mradi una pesa, nitawasikiliza kesho, alijiwazia na kuitupia ile bahasha katika briefcase yake ya kazini.
§§§§§§
Ilikuwa ni juu kabisa ya hoteli hiyo, walipoketi watu hawa watatu wakiongea biashara hiyo haramu.
“Tangu mwaka 1990 tumekuwa katika mradi huu na lengo kubwa ni kupata haya madini ama yawe yamerutubishwa au la, kwa kuwa sisi tunafanya biashara na makundi ya Kimataifa ya Kigaidi na yanayofanana na hayo, tuna miradi mikubwa. Sasa shida yetu ni kuwa tunataka haya madini ambayo yako hapa, kwanza kuna plan gani nayo tunajua, sasa kwa hilo tumeona tusubiri yakishatengenezwa makombora hayo ndiyo tunayataka sisi,” Shalabah alimwambia Mh. Waziri, akabaki anatikisa kichwa kuashiri anaelewa.
“Sasa hayo yote mmeyajuaje?” akawauliza.
“Aaah, si nimekwambia tuna watu tangu miaka hiyo waliokuwa wakifanya kazi ya kutuwekea mipango sawa, wakiwemo Mawaziri kadhaa, Katibu wa Wizara ya Madini Bwana Goloko Mikidadi na wengine katika ngazi mbalimbali, sasa tumepata mpango mzima na tumejua kuwa mnayarutubisha na kutengeneza makombora, sisi tunahitaji hayo makombora lakini sasa kama unavyojua hawa wazee wenggine wamestahafishwa, wengine wamefungwa na mambo mengi, tulikuwa na kikwazo kimoja, kulikuwa na mtu ambaye alikuwa ngazi ya juu pale katika bodi ya mradi huo naye aliwekwa na Mwl Nyerere mwenyewe, tukagundua kuwa alikuwa ni Usalama wa Taifa aliyekuwa akitoa siri hizi zote serikalini ndio maana ikapelekea ule mradi kusimamishwa kwa muda kabla ya kuanza tena na ndipo mkataba na kampuni ya Kirusi ukasainiwa, pale tulianza upya tena lakini kwa msaada wa walewale walio nje ambao serikali iliwaondoa kwenye nyadifa zao, tukajipenyeza na kuweza kujua kinachoendelea. Sasa tunataka nawe utusaidie kwa hilo, kujua nini kinaendelea na kwa kuwa information nyingi tunazo sasa ni kuyapata hayo makombola,” akaongea Shalabah.
Mh. Waziri akabakia kumwangali tu akimsikiliza kwa makini sana na kumwelewa kwa kina vile vile, akaijiweka sawa kitini na kuinua glass yake iliyojaa Whisky aina ya John Walker, alipoishusha akajikuna tumbo lake na kujikohoza kwa minajili ya kusafisha koo lake.
“Ok, nimekuelewa bwana Shalabah na bwana Balozi, kila kitu kinawezekana, pesa ipo?” akauliza.
“Pesa kwetu sio ugonjwa Mheshimiwa, tunazo nyingi kama matundu ya chandarua,” Shalabah akajibu na wote wakacheka, kisha Waziri akaendelea, “Ni kweli kama mlivyo na maelezo mengine, mpango nji uleule, na ujue sasa hii sio serikali ya awamu ya kwanza hii ni nyingine, Wanasayansi wetu wa jeshi upande wa milipuko wanashirikiana na wale wa jeshi la Urusi kutengeneza makombora yenye nguvu kubwa nay a masafa marefu ili kuimarisha ulinzi wa mipaka yetu na ile ya Afrika kwa ujumla.”
Shalabah alifurahishwa na manenoi hayo, “Sasa tunaweza kupata hayo Makombora? Tufanya biashara ya pesa nyingi na wapigania uhuru kote duniani, lazima tuhakikishe uhuru wetu unapatikana na nchi zetu kutambulika na kupewa haeshima duniani kote,” akaeleza.
“Na kwa hilo nakuhakikishia nitatoa ushirikiano mkubwa nanyi, kweli lazima tupiganie uhuru wan chi zetu,” Mh. Waziri akaunga mkono.
Kauli ile ikawashtua kidogo Shalabah na yule Balozi.
“Msishtuke, mimi kiasili ni Msomali, wazazi wangu waliingia Tanganyika miaka hiyo, kule Arusha, wakajichanganya na Wamburu hivyo ikawa ngumu kutambulika uhalisia wa uraia wao, nimekulia hapa, nimesoma hapa, na mara kadhaa nakwenda Somalia na kuona harakati kubwa za ukombozi, nilipendezwa nazo na nilitamani niwaunge mkono,” akawaeleza.
“Haujachelewa, wakati ndio sasa!” Balozi akamwambia yule Mheshimiwa.
“Mimi ni mbunge wa Mburu Magharibi, na nimekuwa jeshini kwa miaka mingi kule Monduli mapaka nachaguliwa kuwa Waziri wa Ulinzi ni mbunge wa Mburu Maghalibi, na hili ni kosa kubwa la Serikali ya Tanzania, haina muda wa kuchunguza uraia wa mtu, ilimradi umeishi miaka mingi, wanakupa ubunge wakitaka, uwaziri kama hivi na kadha wa kadha nah ii itawagharimu sana, siwezi kuacha watu wangu wanateseka kupigania uhuru wao eti kwa sababu ni nchi iliyonilea, never,” akaongea kwa hisia.
Kauli ile iliwafurahisha wote walikuwapoa hapo, vinywaji vikaagizwa tena na kuku wazima wawili wakaletwa mezani.
“Sasa sikilizeani, process ya kutengeneza hayo makombora itaanza mwaka ujao na itachukua miaka kama mine hivi mpaka kukamilika kwa sababu ni teknologia mpya inayobuniwa, na awamu ya kwanza tutaangua makombora ishirini na tano mazito, hivyo nitawapa taarifa ya kila kitu,” akawaeleza.
Kikao hicho kisicho rasmi kilihitimishwa majira ya saa tano usiku kwa makubaliano ya kuunganisha nguvu, Waziri wa Ulinzi wa kipindi hicho alikubali kufanya hujuma hiyo kwa Taifa lililomlea na kumpa maisha bila kujali.
MIAKA MINNE BAADAE
MOGADISHU – SOMALIA
“Sasa inabidi uwe bega kwa bega na bwana Goloko Mikidadi kwani yeye ndiye Master Plan wa mradi huu kwa upande wetu, nimefurahi mlivyofanya mbinu za kumuua yule kizabizabina Chamellaon, sasa mambo ni murua,” Shalabah na Hussein walikuwa kwenye kikao kifupi na wadau hao katika kasri la Mr. Lonely.
“Bila shaka! Ila kma nilivyowaambia na imeelezwa katika hilo kabrasha, hisyo ni siri ya serikali, mi nimeitoa kwenu, miaka miwili baadae tutafanya jaribio la kwanza la makombora hayo kule Caspian sasa tunafanyaje, hatuwezi kuyauza kama mishikaki lazima tutumie mbinu makini kuyapata,” yule Waziri alieleza.
“Ndiyo, lazima itumike mbinu ambayo haitaonesha uwepo wa hujuma kati yetu na serikali ya Dodoma,” Goloko alidakia.
“Sawa, hilo mtuachie sisi tu, sisi ndiyo tunajua la kufanya, lakini mnatuhakikishia kuwa kila kitu ni sawa? Hakuna tena kama akina Chamelleone,” Shalabah alionesha wasiwasi.
“Usiwe na shaka kijana, mimi ndiye Waziri wa ulinzi, of cause kuna kidudu mtu kimoja hivi na hiki nitakifanyia kazi mapema tu ili ikiwezekana kama si kukiua basi kukiondoa kazini, na ninajua nitafanya nini,” Waziri aliongea huku kauma meno.
“Nakumaini sana Mheshimiwa,” Shalabah akajibu huku akipigapiga mgongoni.
Siri za serikali juu ya mpango wa kurutubisha na kufanya majaribio ya makombora hayo ulitolewa na Waziri wa Ulinzi kwa kuuza kwa wafanyabiashara hao wakubwa. Pesa ilifanya kila kitu, ilimnunua kila mtu, pesa ilinunua uzalendo na kuweka usaliti na hujuma mahala pake.
Wakapeana mikono na kukumbatiana kwa mafanikio ya kazi yao, na sasa ilisubiriwa tu wakati ufike taratibu nyingine ziendelee.
§§§§§§
Kamanda Amata alipanda ngazi akifuatana na Daudi mpaka katika mlango mmoja uliondikwa MANAGER, hakugonga aliingia tu moja kwa moja na kuufunga nyuma yake, akatoa kofia yake na Daudi akafanya hivyohivyo. Yule Meneja akashtuka kuwaona watu hao, akasimama kama aliyemrishwa.
“Vipi? Kuna tatizo?” akauliza huku akihemaa harakaharaka.
Daudi alitoa bastola yake na kuigongesha mtutu wake juu ya meza ya huyo meneja, huku akimwangalia usoni.
“Pasingekuwa na tatizo tusingekuja lakini kwa kuwa wewe unajua kuwa sisi tulishakufa basi leo mizimu imekutokea, tunamtaka Mr. Lonely, haraka sana, hakuna maelezo, hutaki kutuambia tunakuua hapahapa, hatuna masihara na mtu,” Kamanda akamwambia na wakati huohuo, Daudi alimvuta mkono na kumsogeza pembeni ya meza yake ili asije kubonyeza kitufe cha kuita walinzi.
“Hamna tabu, msiniue nitawaeleza anakoishi lakini huyu mtu sijui kama ni mtu kweli, yupo tu kwa jina, yeye haonekani, utamwona tu katika luninga,” yule meneja akajibu kwa kubabaika.
“Sawa, ni wapi anaishi au hapo ilipo hiyo luninga ni wapi?” Kamanda akauliza.
“Wadada Jaziira, nyumba yake iko pekee yake baada ya kuyapita maghala ya bandari, imezungukwa na ksitu mdogo wa kupandwa,” akajibu huku akiwa amelowa jasho mwili mzima kwa woga.
“Asante sana, nikikuhitaji nitakuja tena,” Kamanda alimwambia huku akiuendea mlango. Daudi alifuata nyuma, baada ya Kamanda kutoka nje ya ofisi ile, Daudi alikuwa ametoka nusu akatazama ndani ya ofisi hiyo kama aliyesahahu kitu, akainua bastola yake yenye kiwambo cha sauti, “Hustahili kushi,” akafyatua risasi na kupiga kwenye paji la uso la meneja huyo, akasota ukutani na kuserereka mpaka akaketin chini damu zikimvuja kisogoni. Daudi akachomoa ufunguo na kuufunga mlango kwa njue, akavaa kofia yake kama mwanzo na kuondoka eneo hilo.
DAR ES SALAAM
Waziri wa Ulinzi aliteremka kwenye gari yake kwa uchovu akiwa na mawazo lukuki, alipokelewa na mhusika na moja kwa moja akaingia ndani ya Ikulu ya Tanzania, akaongozwa mpaka kwenye ofisi maalum ambayo Mheshimiwa Rais na jopo lake la uchunguzi walikuwa humo. Aliingia kwa kitetemeshi, hakuna aliyemsemesha zaidi ya kugongana macho na Madam S. akaoneshwa kiti akaketi.
“Mheshimiwa, nilikuheshimu sana kama mmoja wa wasahauri wangu wa ulinzi wan chi hii lakini nasikitika sana kwa yale uliyoyashiriki na kutufanyia hujuma mbaya kama hii, umekuwa mbunge, tukakupa na uwaziri, ndiyo, umefanya kazi nzuri sana katika wizara yako lakini nasikitika kwamba wewe ndiye unayejulikana kwa jina la Mr X katika watu walioshiriki hujuma hii chafu. Kwa nini umewahujumu Watanzania? Wamekukosea nini?” Mheshimiwa Rais alikuwa akiongea kwa uchungu sana, ukumbi wote ulikuwa kimya kabisa ni kiyoyozi tu kilichokuwa na uhuru wa kutoa mlio humo ndani. Waziri wa ulinzi hakuwa na jibu, kwani aliyokuwa akiambiwa alijua kabisa kuwa ni kweli tupu.
Yakafuata majadiliano marefu katika jopo hilo, na mwisho muafaka ukafikiwa.
“Sasa wewe ni mtu mkubwa serikalini, tunaendelea na uchunguzi na wakati huu wa uchunguzi, hutakiwi kutoka nje ya mji wa Dar es salaam bila kibali change na popote unapoenda nje mji lazima usindikizwe na watu wa usalama, tunazifunga akaunti zako zote, huwezi kutoa wala kuingiza pesa, kwani imeonekana una akaunti Uingereza na jana imepokea mabilioni ya shilingi, hongera sana, nimemaliza, sio peke yako wapo na wengine wengi,” Rais alimaliza kuzungumza. Waziriwa Ulinzi akawekwa kizuizini akiwa anaangaliwa kwa jicho la karibu kwa kila afanyalo. Serikali ilihakikisha ndani ya saa tano imewakamata wote waliohusika na kuahidi kuwafungulia mashitaka. Lakini mtu mmoja hakupatikana na huyu ni Goloko Mikidadi.

§§§§§

Majira ya saa sita mchana, chopa za JW ziliwasili katika Uwanja wa Jeshi la Wananchi, familia, ndugu na jamaa za wapiganaji hao zilikuwa hapo kwa ajili ya kuwapokea ndugu zao. Furaha zilitawala, shangwe na hoihoi. Hakuna aliyetegemea kuona tena sura ya nduguye kwa kuwa walikuwa wakijua wazi jinsi Somalia kulivyo, ama wangeishachinjwa au kuuawa kwa jinsi yoyote ile.
“Karibu nyumbani mpenzi,” ilikuwa ni moja ya sauti kati ya nyingi iliyosikika uwanjani hapo, akimkumbatia mumewe na kumpa busu la mahaba.
“Sikutegemea kama utarudi baba,” mtoto alimwambia baba yake upande mwingine wa eneo hilo. Mkuu wa Majeshi Jenerali Kamsumi pamoja na mwambata wake walikuwa katika eneo hilo kuwapokea wahanga hao. Wanajeshi wale walijipanga mistari miwili na kumsikiliza Mkuu wao alipokuwa akiwaambia maneno mafupi ya faraja, kisha akawapa likizo ya miezi miwili kila mmoja ili wakapumzishe akili zao kabla ya kurejea kazini.
Wale wanajeshi watano wa Urusi wangekabidhiwa kwa Balozi wao baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu katika hospitali ya jeshi ya Lugalo. Watu walitawanyika na kuuacha uwanja huo mkiwa kama walivyoukuta, furaha na shangwe zilihamia majumbani mwao, ikiwamo na kupeana zawadi za ushindi.
§§§§§
MADAM S aliitoa miwani yake usoni na kuiweka mezani huku mbele yake akiwatazama vijana wake makini wa idara ya kijasusi ya serekali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Chiba, Scoba, Gina, Dr. Jasmine.
“Hongereni kwa kazi ngumu ambayo imetuumiza vichwa sana kuikamilisha, kila mtu aliifanya kwa upande wake na kwa pamoja tumeikamilisha, nadhani mmejionea wenyewe, kikulacho ki nguoni mwako, hila za Waziri wa Ulinzi kufanya mpaka Kamanda Amata aondolewe kazini ilikuwa ni kuhakikisha njia nyeupe kwa mpango huu wa kidhalimu, kumbe ndiyo Mr. X. Ili kuhakikisha hujama hii inahitimishwa sawasawa, nawapa kazi, nah ii ni kutoka hapa ofisini na siyo mahali popote, nataka wachunguzwe viongozi wote mmoja baada ya mwingine, na ndani ya mwezi mmoja kila mtu aniletee tafutishi zake nini kimegundulika, lazima kuna makandokando,” Madam S aliwapa maagizo vijana wake watiifu kuhakikisha wananusa kila kona ili kujua lolote linaloambatana na hilo. Wakiwa katika mazungumzo hayo, simu yake ya ofisini ikapata uhai, ikaunguruma kwa fujo kama imepewa adhabu kufanya hivyo, akainyakua na kuiweka sikioni, huku akimpa ishara Chiba ahakikishe amerekodi simu hiyo. Madam S alikuwa na tabia ya kurekodi simu zote zinazoingia katika ofisi yake hata iwe ya kirafiki, nah ii ilimsaidia sana hasa anapokuwa anataka kumbukumbu ya jambo Fulani, lakini si hilo tu, huwa anaandika katika kitabu chake cha kumbukumbu mambo yote yanayotukia kwa kila siku yake,
kikazi na kifamilia.
“Hallo!” aliita katika simu ile.
“Kamanda Amata,”
“Ooh Kamnda, nipe mrejesho, najua kazi umeimaliza na sas bado sikuoni nyumbani nakuhitaji haraka sana,” Madam S alimwambia Kamanda kwenye Simu hiyo.
“Bado sijamaliza kazi ndio maana sijarudi, nipo hapa na Komandoo wa JW, Daudi aliyepotea katika mazingira ya kutatanisha, yuko mzima na salama, tutarudi wote nyumbani, lakini pia tuko, Madam, kuna kazi naimalizia mchana huu kisha nitarudi nyumbani.”
“Usijali Kamanda, nakutakia mema katika kumalizia kazi hiyo, Gina anakumiss sana na anakusubiri kwa hamu,” Madam S akarusha utani ndani ya simu hiyo. Kamanda Amata upande wa pili alicheka sana kisha simu ikakatika.
Madam akawageukia vijana wake, “Mnasalimiwa na Kamanda, atarudi si muda kuna kazi kidogo anamalizia.”
Kila mtu alionekana kuwa na furaha kwa kupata habario hizo kutoka kwa Kamanda. 10
AKIWA NDANI ya suti safi ya rangi nyeusi, kiatu kilichong’azwa kwa Kiwi, nywele zililizowekwa kwa mtindo wa kupendeza, miwani ya jua iliyomkaa vizuri kabisa, Kamanda Amata aliteremka katika gari moja ya gharama sana iliyokuwa ikiendeshwa na mwanamke mrembo kabisa, aliyependeza kwa mavazi yake yenye ving’arong’aro, unaweza kusema ni Muhindi lakini pia utasema ni Mwarabu yote yangewezekana. Gari hiyo aina ya BMW iliegeshwa pembeni tu mwa jumba kubwa la kifahari lenye bustani ya maua ya kupendeza, ukimya ulitawala eneo hilo ni kelelel za ndege tu zilizikika kwa nadra kidogo kutokana na hali ya jangwa ya eneo lile hakukuwa na viumbe kwa wingi, Kamanda Amata hakuona mtu yeyo te katika mazingira ya jumba hilo pweke. Aliiacha gari iliyomleta ikiweka maegesho vizuri, akapanda ngazi kuuelekea mlango mkubwa wa nyumba hiyo, akaitoa simu iliyokuwa mfukoni mwake, simu ya Shalabah, akabofya vitufe fulani Fulani, kisha akashika kitasa cha mlango huo na kuusukuma ndani, ukafunguka, akaingia na kuufunga nyuma yake.
Mbele yake alilakiwa na sebule kubwa, safi isiyo na samani yoyote, akapepesa macho huku na kule labda ataona mlango eneo hilo lakini hakuona kitu zaidi ya mapicha ya ajabuajabu yaliyotulia ukutani na kufanya ndani humo kuwa mwa kuogofya. Akaitazama tena ile simu, na kuitafuta majina yaliyomo katika orodha, yote hakuyajua hata moja, akaamua kuzunguka sebule ile huku akiangalia kwa makini kila kilichowekwa au kuning’inizwa ukutani. Kati ya masanau na mapicha yote yaliyowekwa juu ukutani, ni sanamu moja tu lilikuwa chini kidogo, sehemu ambayo unaweza kuishika kwa mkono wako bila kufanya jitihada yoyote. Akagusa lile sanamu, mara akaona jicho la sanamu hiyo likichezacheza.
“Shiiit!” akatamka kwa sauti hafifu, wakati anatoka eneo lile akaligonga lile sanamu bahati mbaya mara kipande cha ukuta kikasogea pembeni, ukabaki uwazi, ujia mrefu uliingia ndani ya uwazi huo, Kamanda Amata akachomo bastola yake na kuingia ndani ya ule ujia, akapita kwa hadhari kubwa sana akitazama milango iliyojipanga katika ujia huo, lakini kila alipoutikisa mmoja hauukuwa na dalili ya kutikisika seuse kulegea. Mlango wan ne kutoka mwisho, aliposimama tu mbele yake ukafunguka, kulikuwa na kijichumba kidogo kiking’azwa na taa hafifu na muziki laini wa kihindi ulisikika taratibu, akatazama kwa makini mle ndani na juu akaona kuna kamera ya usalama.
Wameniona, akajisemea kwa sauti yake mwenyewe ya kuweza kujisikia yeye tu, akaingia na mara hiyo kijumba kile kikaanza kuteremka chini. Kamanda Amata akateremka kwenye hicho kijumba na kukutana na sebule nyingine kubwa zaidi ya ile, lakini tofauti na ile, hii ilikuwa na kila aina ya samani ya thamani ya juu, viti vyenye nakshi ya dhahabu, viliizunguka meza kubwa sana iliyokuwa hapo, kioo kikubwa cha luninga kilitulia mahala Fulani katika ukuta wa jumba hilo. Mara taa zikawaka zenyewe mle ndani na kufanya mwanga kuwa mkali zidi ya ule wa kwanza. Kamanda Amata akashika bastola yake sawia katika kiganja cha mkono, sauti ya vicheko vya kiume ikaanza kusikika ndani ya sebule ile.
“Aaaaaa ha ha ha ha…. Karibu sana kwenye Kasri ya wasio hai, umekuwa mgeni wangu wa dharula sana siku hii ya leo ukizingati nilikuwa safarini kuondoka, najua kilichokuleta labda umekuja kumfuata huyu ndugu yako…” ile sauti ikasema hayo. Mara ile luninga ikapata uhai ikaonesha picha ya kuogofya sana, mwili wa Goloko Mikidadi uliokuwa umechomwa kwa vyuma vinene upande mmoja na kutokea upande mwingine, akiwa ameachama kinywa chake na macho yamemtoka.
“Shiiit” akang’aka Kamanda Amata, ile sauti ikacheka tena.
“Sasa na wewe utakuwa kama huyu si muda mrefu,” ile sauti iliendelea kuongea.
“Acha ujinga wako, nimekuja kukumaliza wewe unayefanya biashara haramu za kuiharibu dunia,” Kamnada Amata aliongea huku akiwa ameuma meno.
“Aaaaaa ha ha ha ha aaaaaa ha ha ha, wacha kunichekesha, tangu lini mfu akafa tena?” ile sauti ikauliza kwa kebehi huku ikitanguliwa na cheko la dharau, lililomfanya Kamanda Amata kufura kwa hasira.
Aliinua bastola yake na kupiga ile luninga, iksambaratika yote, ikamwagika chini vipande vipande, nyuma ya ile luninga akaona tundu kubwa la kupita hata land cruiser, na kiti kimoja kilicholala chini, mezani palikuwa na kamera ndogo DV Cam, akaruka kile kihunzi na kuingia ndani, akatazama huku na kule akaona mlango mmoja ukiishi kufungwa, akauwahi na kuupiga teke, ukafunguka, akaingia kwa fujo na kuupiga kikumbo mlango mwingine kwa ndani, mara akasikia kelele ya mlio wa injini ya boti iliyokuwa ikiwashwa, akageuka kulia na kuona boti iliyokuwa ikitaka kuondoka, na mtu mmoja alikuwa juu yake, akafyatua risasi ikapiga injini, injini kazima.
Kamanda Amata hakufanya ajizi, risasi moja ya mgongo katikati ya uti, ikagawanya pingili hizo.
“Aaaaaaaaa nooooooo!!!!” ilikuwa sauti ya yule mtu akijibwaga upande wa nyuma, Kamanda Amata akajivuta na kumshika akamvuta mpaka nje ya lile eneo lililokuwa na boti akamlaza sakafuni.
“Leo mfu lazima ufe tena, shetani mkubwa!” Kamanda akamwambia Mr. Lonely.
“Tafadhali, umeshaniumiza, basi niachie uhai wangu, nitakupa pesa nyingi sana,” akaongea kwa tabu.
“Wewe umeacha uhai wa watu wangapi mpaka leo?”
“Nitakupa pesa nyingi,” akalalama.
“Pesa zako zinanuka,” akafyatua risasi moja na kupiga kwenye paji la uso, Mr. Lonely akalala kimya huku ametoa macho ya mshangao.
Alikuwa mwembaba mrefu, mwenye ndevu za kuhesabika, upara ulitawala kichwa chake, mavazi yake ya kawaida yangemfanya aonekane ni mmoja wa masikini huko mtaani.
“Mwisho wa zama zako Mr. Lonely,” Kamanda akasema hayo huku akiipachika ile bastola kwenye mkoba wake ndani ya suti.
Akauacha mwili ule na kutoka ndani ya jumba lile.
Nje kabisa alisimama kulitazama jumba hilo la kifahari, akageuka na kuingia katika gari ileile aliyokuja nayo.
“Twende,” akamwambia yule mwanadada, wakaondoka kuifuata barabara kubwa. Umbali kama wa mita mia moja hamsini, “Simama,” alimwamuru yule dereva mwanadada. Akashuka na kulitazama lile jumba, akinua saa yake na kuizungusha kwenye pete yake ya juu, mlipuko mkubwa ukatokea katika lile jumba, moto na moshi mzito, kishindo kililisambaratisha lile jumba lote lililoitwa la kifahari.

UWANJA WA NDEGE WA ADEN ADDE – MOGADISHU
KAMANDA AMATA akiwa amemkumbatia Fasendy dakika chache kabla ya kuagana, aliyashuhudia machozi ya mwanamke huyo mpiganaji yakikifikia kifua chake, “Sina budi kwenda Fasendy, kwa heri, tutaonana tena.”
“Wapi Kamanda? Hata hii imekuwa ajali tu kukutana, lakini asante kwa kila kitu,” Fasendy akamshukuru Amata.
“Usijali tutaonana popote duniani sio lazima Somalia wala Tanzania,” Kamnda akamwambia kisha akamtoa kifuani pake, akambusu shavuni, akavua saa yake ya kijasusi saa yenye kufanya mambo mengi sana, akampatia Fasendy, “Unikumbuke,” akamwambia.
Fasendy naye akampa kibegi kidogo mkononi mwake, “Unikumbuke,” akamwambia. Kisha Kamanda Amata akaagana na Chamelleon na timu yake, akaondoka kuingia uwanjani tayari kwa safari ya kurudi nyumbani.

˜˜MWISHO˜˜View attachment 1217605

Safi sana... Story nzuri sana...

Chapter Closed...



Cc: mahondaw
 
Habari mambo naitwa Mr Equator Nimeandika ujumbe huu kuku omba swala moja tu!
Mimi nimetengeza website ya ku share story ambayo ni EquatorStory
Je umekuwa ukipata tabu kupost story zako hapa?
Hili ndo suluhisho lako.
Mimi nataka nkupe nafasi ya kuwa mmoja wapo wa kwanza kutumia hii website
unda account yako na uweze kupost story yako mpya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom