Simulizi: Harakati za Jason Sizya

Bishop Hiluka

JF-Expert Member
Aug 12, 2011
7,141
14,677
safari buzwagi.JPG


(Kutoka kwa mwandishi wa stori za kusisimua zilizowahi kuchapishwa hapa JF za Taxi; Kizungumkuti!; Laiti Ningejua!; Hekaheka!; Hadi Lini! na nyinginezo)

Na Bishop Hiluka

0685 666964 | bjhiluka@yahoo.com



Kijasho Jepesi


Saa 12:15 asubuhi…

Wala sikujua kitu gani kilikuwa kimeukatisha ghafla usingizi wangu! Niliyafumbua macho yangu taratibu nikayatembeza mle chumbani kuangalia huku na kule, nikakutana na ukungu wa kiza chepesi machoni. Hali ile ikanifanya niyatulize vizuri mawazo yangu huku nikijaribu kufikiria pale nilikuwa wapi.

Hata hivyo, sikulipata jibu la haraka na hivyo niliamua kupeleka mikono yangu huku na kule nikijaribu kupapasa pale nilipokuwa nimelala. Sikuchukua muda kugundua kuwa nilikuwa nimelala juu ya kitanda chenye foronya laini na mto wa kuegemeza kichwa.

Kitanda kilikuwa kikubwa cha samadari cha futi sita kwa sita kilichokuwa katikati ya chumba kikubwa. Kwa kufanya vile taratibu fahamu zangu zikaanza kurejewa na uhai.

Niliweza kugundua kuwa nilikuwa nimelala kitandani chumbani kwangu ila sikuweza kukumbuka haraka muda huo ulikuwa ni wa saa ngapi, ingawa hisia zangu ziliniambia kuwa tayari kulikuwa kumeanza kupambazuka kutokana na kusikia sauti za majogoo waliokuwa wakishindana kuwika kwenye mabanda.

Pia niliweza kusikia, kwa mbali, sauti za ndege angani walioshindana kuimba nyimbo nzuri na kuruka huku na kule kwenye vilele vya miti mikubwa iliyokuwa nje ya ile nyumba na kandokando ya barabara ya mtaa ule wa Ng’ambo mjini Tabora, eneo la jirani kabisa na uwanja wa mpira wa Ali Hassan Mwinyi.

Nilikuwa nimelala peke yangu pale kitandani na nilipojichunguza nikagundua kuwa nilikuwa nimejifunika shuka lakini sikuwa nimevaa nguo yoyote mwilini mwangu hali iliyonistaajabisha sana! Sikuwa na kawaida ya kulala bila nguo hata kama ingekuwa ni wakati wa joto kali kiasi gani, bado nisingeweza kulala bila nguo.

Haraka nikataka niamke na kuketi pale kitandani lakini hilo halikufanikiwa kwani kichwa changu kilikuwa kizito mithili ya mtu aliyekuwa ametwishwa kiroba cha mchanga, hali hiyo ilinifanya niyafunge macho yangu taratibu na kuendelea kujilaza.

Nikiwa bado nimelala pale kitandani mawazo yalianza kupita kichwani kwangu mfano wa filamu, nilijaribu kukumbuka nilirudi vipi usiku pale nyumbani na nilikuwa na nani. Mara ikanijia picha ya usiku wa kuamkia siku hiyo. Nikakumbuka kuwa nilikuwa katika eneo la Chemchem mtaa wa Baruti mpaka majira ya saa saba za usiku.

Usiku huo nilikunywa pombe nyingi na kula nyama choma, na kama isingekuwa ushawishi wa rafiki yangu Majaliwa Nzilwa, haki ya nani nisingetia mdomoni pombe siku hiyo.

Majaliwa Nzilwa, jamaa fulani mfupi na mcheshi sana ambaye tulipenda kutaniana muda wote, alikuwa rafiki yangu wa muda mrefu tangu tukisoma katika Shule ya Msingi Gongoni iliyopo katika Manispaa ya Tabora.

Ukaribu wetu uliwafanya wengi kudhani tulikuwa ndugu kwa kuwa muda mwingi tulipenda kuwa pamoja hasa kila nilipotoka kazini, na licha ya urafiki wetu, Majaliwa pia alikuwa mshauri wangu mkubwa katika mambo yangu mbalimbali.

Hayo niliyakumbuka vema, na si akili ya pombe, picha ilikuwa inapita kichwani kwangu kama niliyekuwa naangalia filamu. Nilikumbuka kuwa Majaliwa alininunulia chupa kubwa ya pombe kali aina ya Grant’s Whisky nikaanza kugida kama maji, kisha alimwagiza Masawe mchoma nyama atuchomee ubavu mzima wa mbuzi. Baadaye tena alinunua chupa kubwa ya K Vant na chupa kadhaa za Savannah.

Usiku huo nilikunywa sana kwa kuwa sikuwa sawa kisaikolojia, nilikuwa nimevurugwa kwelikweli! Nilikumbuka pia kwamba baadaye Majaliwa alinitambulisha kwa msichana fulani hivi mwenye asili ya Kiarabu, aliitwa Rahma. Alikuwa msichana mzuri kwa sura na umbo, akiwa na macho mazuri yaliyojawa na haya alikuwa amevaa gauni fupi lililoishia juu kidogo ya magoti yake la rangi ya bluu lenye vidotidoti vyeupe vinavyong’aa.

Alikuwa mrefu na kifua chake kilibeba maziwa ya ukubwa wa wastani huku kiuno chake chembamba kikiwa kimebeba nyonga pana kiasi. Nywele zake zilikuwa nyingi ndefu nyeusi na zilikuwa zimeipendezesha sura yake ya kitoto. Nilikumbuka vyema kuwa Rahma alijitambulisha kwangu kwamba alikuwa mgeni pale Tabora na alitokea Singida. Hivyo tu!

Ni hivyo tu ndivyo nilivyovikumbuka kuwa vilitokea usiku huo, hakuna kingine isipokuwa kuwa na rafiki yangu Majaliwa eneo la Chemchem, kuja kwa huyo mwanamke wa Kiarabu aliyeitwa Rahma, tukala na kunywa, basi! Nilipojaribu kukumbuka mambo mengine kichwa changu kiligoma kabisa kuyakumbuka!

Nikiwa bado nipo kitandani, macho yangu bado nimeyafunga, nilihisi kuchoka mno na mawenge ya usingizi. Si hayo tu, bali pia uvivu ulinijaa na tumboni mwangu njaa ilikuwa inakereza mfano wa seremala aliyekuwa akiranda mbao. Vyote kwa pamoja vilikuwa vinanipa hali ya kutaka kuendelea kubadili uchago.

Akilini, niliutaka utulivu kwa gharama yoyote ile, japo nipate kukimalizia kipande cha usingizi kilichobakia, wala sikujua kingekwisha saa ngapi. Nilichotaka ni kulala tu mpaka pale ambapo mwili wangu ungeniruhusu kuamka. Niliuhisi uzito wa kichwa changu na nilikuwa nina mawenge ya usingizi, ukichanganya na uvivu uliokuwa umesababishwa na mning’inio mkali wa pombe nilizokunywa, vilinipa hali ya kutaka kuendelea kuuchapa usingizi.

Nilipanga nilale na nikiamka niende nikapate supu ya kongoro na chapatti kwa Mama Kashindye, aliyeishi upande wa pili wa barabara ya mtaa huo na baada ya hapo ndiyo nimtafute Majaliwa, huenda yeye angekuwa ana kumbukumbu nzuri ya kilichotokea usiku kuliko mimi.

Nilijiambia kuwa kwa muda huo sikupaswa kuumiza sana kichwa changu kwa hayo mambo ya usiku, sikufikiria kama yalikuwa na umuhimu wowote kwa muda huo, pindi nikiamka ningejua cha kufanya. Hivyo nilijigeuza kuelekea upande mwingine wa kitanda na kuendelea kulala. Sikujali sauti za kukera za majogoo waliokuwa wanashindana kuwika kwenye mabanda na juu ya mapaa. Nilijisemea kuwa kwa sababu nilikuwa nimeanza likizo basi wacha nilale mpaka usingizi ukate kabisa.

Jitihada zangu za kuutafuta usingizi zilikatishwa kikatili na sauti kali ya kitu mfano wa kengele iliyoanza kulia chumbani kwangu, sauti ile iligeuka kuwa kero kubwa masikioni mwangu. Niliposikiliza vizuri nikagundua kuwa ilikuwa ni simu yangu ya mkononi iliyokuwa sehemu fulani mle ndani. Nikawaza kuwa hakuna mtu mwingine ambaye angeweza kunipigia simu muda ule wa alfajiri zaidi ya mpuuzi mmoja tu, Majaliwa! Kwani Majaliwa na mimi tulipenda sana kutaniana na Majaliwa aliongoza kunikera. Kila nilipokasirika yeye aliona raha sana, na ili kukabiliana na hali hiyo ilibidi nimzowee.

Sikuwa na namna yoyote ya kufanya kwani sauti ya simu ilizidi kuniletea kero kubwa masikioni mwangu, na pia nilitambua kuwa kama mpigaji wa simu hiyo, kwa muda huo, angekuwa Majaliwa au mtu mwingine yeyote basi kungekuwa na tatizo na angeendelea kupiga hadi nipokee, hivyo nililitupa pembeni shuka nililojifunika, kisha kwa msaada wa swichi iliyokuwa kando ya kitanda changu nikawasha taa ya mle chumbani huku akili yangu ikiwa imeanza kupoteza utulivu.

Na hapo nikaziona nguo zangu zikiwa zimetupwa tupwa ovyo sakafuni mle chumbani, si hivyo tu niliona pia kifaa fulani kimoja kidogo cha kujipima virusi vya ukimwi ambacho kinauzwa kwenye maduka ya dawa na ki-sindano kidogo cha kutobolea ili kutoa damu. Vifaa hivyo vilikuwa vimetumika.

Kingine nilichokiona pale sakafuni ilikuwa ni mtapakao wa shanga za rangi mbalimbali zivaliwazo na wanawake kiunoni. Jambo hilo likanitia hofu kubwa huku mapigo ya moyo wangu yakianza kunienda mbio isivyo kawaida.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

2

Nilipoutazama mlango wa kuingilia chumbani kwangu nikauona ukiwa umerudishiwa tu. Jasho jepesi likaanza kunitoka sehemu mbalimbali za mwili wangu. Nilishusha pumzi za ndani kwa ndani huku nikimeza mate ya uchungu yaliyonifanya nikunje sura yangu utadhani nilikuwa nimelambishwa kitu cha uchachu.

Nilijitizama mwilini kuona iwapo nilikuwa na dosari yoyote lakini sikuiona, kisha nilizitazama nguo zangu zilizotupwa pale sakafuni na zile shanga zilizotawanyika kwa umakini huku nikijaribu kukumbuka ni nini kilikuwa kimetokea usiku huo, lakini bado kichwa changu kiligoma kabisa kukumbuka!

Niliinuka huku usingizi ukiwa umenitoka kabisa, nikayafikicha macho yangu na kupiga mwayo hafifu wa uchovu huku nikivinyoosha viungo vyangu mwilini. Na hapo nikagundua jambo jingine lililozidi kuniacha hoi, kitanda changu kilikuwa kipo shaghalabaghala na mashuka yalikuwa yamechafuka, moja kwa moja nikahisi kuwa kulikuwa na shughuli pevu iliyokuwa imefanyika usiku huo! Swali kuu lilibaki: nini kilikuwa kimetokea usiku huo, mbona sikuwa nakumbuka chochote?

Sikuujali mlio wa simu iliyokuwa inaendelea kuita bali nilizifuata nguo zangu, nikainyanyua suruali yangu na kuanza kukagua kwenye mifuko, nikaikuta pochi yangu kama nilivyokuwa nikiiweka siku zote na hata nilipoifungua nilizikuta fedha zangu zikiwa zimepangwa kwa namna ileile nilivyopenda kuzipanga. Hadi hapo sikuweza kugundua tofauti yoyote.

Niliachana na ile suruali na kuirushia kitandani, kisha nikafungua droo za kitanda changu ambamo nilikuwa nimeweka vitu vyangu muhimu kama fedha na baadhi ya nyaraka muhimu, pia sikuona kama kulikuwa na dosari yoyote! Nikashusha pumzi ndefu.

Niliyazungusha macho yangu kukitazama chumba changu, kilikuwa kikubwa chenye maliwato ya ndani kwa ndani (master bedroom) na hakikuwa na vitu vingi sana isipokuwa kitanda kikubwa cha samadari cha futi sita kwa sita, cha mbao ngumu za mninga, chenye droo mbili kila upande ambazo juu yake kulikuwa na taa za rangi ya buluu. Pia kulikuwa na kabati kubwa la nguo la ukutani na meza nzuri ya vipodozi maarufu kama ‘dressing table’ iliyokuwa na kioo kirefu cha kujitazama mwili mzima.

Chumba hicho kilikuwa na madirisha mawili mapana ya vioo yaliyokuwa yamefunikwa kwa mapazia marefu yenye nakshi za michoro ya maua.

Hofu ikiwa imeanza kuniingia moyoni niligeuza shingo yangu kutazama kule kwenye simu yangu ambayo muda huo ilikuwa imekatika na kisha ikaanza kuita tena, nilijishauri kisha nikaona nisiiache iendelee kuita zaidi kwani ilikuwa mbioni kukata kwa mara nyingine tena baada ya kuita kwa muda mrefu.

Nikaifuata katika hali ya uvivuvivu na kuupeleka mkono wangu kuichukua lakini kabla sijaishika ikawahi kukata. Niliichukua na kuitazama vizuri nikakuta kulikuwa na miito mitatu ya simu ambayo ilikuwa haijapokelewa (missed calls) na mpigaji alikuwa Eddy. Moyo wangu ukapiga mshindo mkubwa!

Eddy kama tulivyokuwa tumezoea kufupisha jina lake la Edson, alikuwa kaka yangu wa tumbo moja niliyemfuatia kwa kuzaliwa, ndiye alikuwa ananipigia simu alfajiri hiyo! Haikuwa kawaida ya Eddy kunipigia simu labda kama kungekuwepo jambo muhimu sana. Niliikodolea macho ile simu huku mawazo mchanganyiko yakianza kupita kichwani kwangu, akili yangu ikazama kwenye tafakzri nzito na kuwaza kuwa huenda kulikuwa na tatizo ndiyo maana Eddy alikuwa ananipigia simu alfajiri hiyo! Nilijikuta naingiwa na hofu kubwa.

Nikiwa bado najiuliza mara ile simu ikaanza kuita tena, sikutaka kusubiri tena, nikaipokea kwa pupa na kuiweka kwenye sikio langu la kushoto huku nikiipa akili yangu utulivu wa hali ya juu.

“Jason, inamaana bado umelala?” nilimsikia Eddy akiuliza kwa sauti iliyojaa mshangao mara tu nilipoiweka ile simu kwenye sikio langu.

Yeah, bado nimelala, kwani vipi! Au ulitarajia niwe wapi saa hizi?” nilimjibu kwa jazba huku nikihisi karaha ya kukatishwa usingizi wangu kwa swali lisilokuwa na maana.

“Hivi uko serious kweli wewe! Yaani hadi saa hizi umelala wakati unajua kuwa leo tuna safari?” nilimsikia tena Eddy akiongea, safari hii aliongea kwa msisitizo zaidi pasipo chembe yoyote ya mzaha.

“Safari ya kwenda wapi tena, Eddy?” nilimuuliza huku hasira ikiwa imenikaba kooni kwani sikukumbuka kama tulikuwa na safari yoyote siku hiyo.

“Unauliza safari ya kwenda wapi! Hivi uko sawa kweli wewe au umeanza kuchizika! Yaani umesahau leo tunatakiwa kwenda wapi? Mimi nipo hapa stendi na basi litaondoka saa 12:30 asubuhi hii lakini wewe bado umelala nyumbani kwako na huna hata habari! You are not serious, my brother…” Eddy aliongea kwa uchungu mkubwa uliochanganyika na hasira na sauti yake ilionesha wazi kuwa alikuwa amekerwa mno.

Oh my God!” niling’aka kwa mshtuko mkubwa baada ya kukumbuka kuwa siku hiyo mimi na Eddy tulikuwa na safari muhimu sana, safari ya kwenda Kahama kwenye usaili wa kazi katika mgodi wa dhahabu wa Buzwagi. Nilipotaka kuongea nilikuwa nimechelewa kwani Eddy alikwisha kata simu kwa hasira.

Sikuwa na namna nyingine ya kufanya, sitaka kuendelea kumuudhi Eddy na wala sikujiuliza mara mbili kwa kuwa sikutaka tukose kazi kwa sababu ya uzembe wangu, nilimpigia simu Eddy na alipopokea tu nikamwambia anipe dakika kumi ningekuwa nimefika hapo stendi, kisha nikakata simu.

Muda huo akili yangu ilikuwa imeanza kupoteza utulivu wake na sikutaka kupoteza muda, haraka nikakimbilia maliwatoni kujimwagia maji maana nilifahamu nini maana ya kuzingatia muda. Ilinichukua dakika chache tu kujimwagia maji na nilipotoka humo ilikuwa tayari imetimia saa 12:22 alfajiri, hivyo dakika nane tu zilikuwa zimesalia kabla ya basi la NJAMBA EXPRESS tulilokata tiketi halijaondoka.

Baada ya muda mfupi nikawa nimemaliza kujiandaa huku nikiwa katika mwonekano nadhifu kabisa. Nilikuwa nimevaa suruali nyeusi ya kitambaa cha suti cha bei ghali aina ya Dunhill, shati maridadi la mikono mirefu aina ya Levi’s la rangi ya samawati na kiatu ghali cheusi cha ngozi.

Pia nilivaa saa ya mkononi aina ya Quatz na kofia nyeusi kichwani aina ya pama, nikajipulizia manukato ya gharama kubwa aina ya Clive ambayo bei yake ilitosha kabisa kuwa hesabu ya siku tatu ya daladala za Mbagala au Gongo la Mboto. Nikachukua miwani yangu mikubwa myeusi ya jua na hivyo nikawa nimekamilisha utanashati wangu ulionipa mwonekano wa kijanja kwa kila ambaye angeniona.

Kama hiyo haitoshi, kwenye mfuko wa shati niliweka kitambaa cha rangi ya bluu kilichokunjwa kwa unadhifu mkubwa na kuonekana na kila mtu ambaye angenitupia jicho. Nilipomaliza nikachukua vitu muhimu kama vyeti vyangu vya shule na vya taaluma, nguo zangu chache muhimu za kubadilisha na vitu vingine nilivyohisi kuwa vilikuwa muhimu kusafiri navyo, nikavitia ndani ya lile begi dogo la mgongoni lenye mifuko mingi.

Nilipomaliza nikakusanya zile nguo chafu haraka haraka na kuziweka kwenye tenga la nguo chafu, nikakiweka kitanda changu vizuri na kuweka sawa vitu vyangu mle chumbani. Kisha nikatoka kuelekea sebuleni. Sebule yangu ilikuwa nzuri iliyopambwa na seti moja ya makochi ya sofa ya kifahari yaliyopangwa katika mtindo wa kuizunguka ile sebule. Sakafuni kulikuwa na zulia zuri la rangi nyekundu na katikati ya sebule ile kukiwa na meza fupi nyeusi ya kioo yenye umbo la yai.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

3

Upande wa kushoto wa ile sebule kulikuwa na runinga pana iliyofungwa ukutani na chini yake kulikuwa na meza fupi nyeusi yenye sistimu ya muziki, deki ya Dvd, kisimbuzi cha DStv na vinyago viwili vya Kimakonde vilivyokuwa vimepangwa kwa ustadi wa hali ya juu. Pia kulikuwa na jokofu aina ya Boss kwenye kona moja jirani na mlango wa kuingilia chumbani.

Niliitupia jicho haraka haraka ile sebule nikagundua kuwa pia mlango wa kutoka nje ulikuwa umerudishiwa tu pasipo kufungwa na funguo, jambo hilo lilizidi kunichanganya. Hata hivyo, kwa haraka haraka sikuwa nimegundua tofauti yoyote ya kitu kupungua pale sebuleni.

Nilitoka haraka na kutokea katika kishoroba (korido) kipana cha nyumba, nikaufunga mlango wangu haraka haraka kwa ufunguo na wakati nataka kuondoka nikakutana uso kwa uso na mwanadada Zakia aliyekuwa ametoka haraka chumbani kwake, kwenye mlango uliokuwa kwenye kona mwanzo kabisa wa kile kishoroba, baada ya kunisikia.

Zakia alikuwa mke wa mpangaji mwenzangu, Msabaha Jumanne. Nilipomwona tu Zakia moyo wangu ukapiga mshindo kwa nguvu! Zakia alikuwa msichana mrefu wa wastani, mweupe kwa rangi na mwenye umbo kubwa na zuri la namba nane, umbo lililomfanya mtu yeyote aliyemwangalia adhani kuwa alikuwa amefika miaka therathini, ingawa kiuhalisia ndiyo kwanza alikuwa na miaka ishirini na moja tu.

Alfajiri hiyo Zakia alikuwa amevaa nguo nyepesi nyeupe ya kulalia iliyokuwa imeifichua nguo yake nyekundu ya ndani na kulichora vyema umbo lake maridhawa alilokuwa ametunukiwa na Mungu. Pia ile nguo haikuweza kulificha tumbo lake lililokuwa na ujauzito wa miezi minne na kiuno chake chembamba lakini kilichokuwa na misuli imara kilichoshikilia minofu ya mapaja yake manono.

Nyumba ile tuliyoishi, ilikuwa ni kubwa yenye vyumba vine vya kulala, viwili kati ya hivyo vilikuwa vinajitegemea vikiwa na choo cha ndani na sebule. Pia kulikuwa na jiko la pamoja na chumba kingine cha maliwato ya pamoja. Ndani ya nyumba hiyo tuliishi wapangaji watatu, mimi na wengine wawili; Msabaha Jumanne na Adolf Sitta. Wenzangu wawili walikuwa wameoa isipokuwa mimi pekee ambaye sikuwa na mke, na wala sikuwa na mpango wa kuoa.

Zakia alinisogelea huku akinitazama kwa namna ambayo sikuweza kupata tafsiri ya haraka na alionesha kuwa alikuwa na jambo zito alilotaka kuniambia, lakini sikuwa na muda huo. Hadi muda huo nilikuwa nimeshachelewa.

Nilimsalimia haraka haraka huku nikimpita na kuelekea nje, na hata pale alipoanza kunisemesha alishtuka kuona tayari nikiwa nimeshatoka nje ya nyumba, maana nilishajua Zakia alitaka kunieleza kuhusu mgogoro uliozuka usiku kati yake na mumewe Msabaha kuhusiana na ule ujauzito, na angeanza kuongea asingenyamaza maana ni kama aliyetiwa ufunguo.

Tangu apate ujauzito Zakia alikuwa mtu wa kulalamika tu, alikuwa analalamika kila aliponiona kiasi kwamba ilifikia wakati nilianza kujilaumu kwa nini nilifahamiana naye na hata kuanzisha uhusiano wa kimapenzi.

Kwa mara ya kwanza nilikutana na Zakia na baadaye kuanzisha uhusiano wa kimapenzi miezi minne iliyokuwa imepita, siku niliyokwenda kumsalimia mjomba wangu, Japhet Ngelela aliyekuwa anaishi katika nyumba yake aliyojenga eneo la Kiloleni, si mbali sana kutoka kwa wazazi wa Zakia.

Wakati huo ilikuwa ni kabla Zakia hajaolewa na Msabaha ingawa alikuwa tayari mchumba wa mtu. Wakati huo Zakia alikuwa anaishi na wazazi wake katika eneo lile la Kiloleni.

Siku niliyomtokea ilikuwa ni katika ngomba ya Kinyamwezi maarufu kama ‘hiyari ya moyo’ iliyokuwa inapigwa kwenye mkesha wa harusi ya Nyanzala Maige, binti wa mjomba wa Zakia. Ngoma hiyo ilikuwa inapigwa nyumbani kwa mjomba wa Zakia, Mzee Maige, karibu na nyumba ya mjomba Ngelela.

Kama kawaida yangu siku hiyo nilikuwa katika mwonekano wa kileo zaidi, na nilikuwa mmoja kati ya vijana wachache sana waliojaliwa kuwa na maneno matamu yenye kushawishi na kunasa kama ulimbo, maneno ambayo niliyatumia kama silaha ya kuzikamata nyoyo za warembo wengi.

Nilimwona Zakia akiwa na wasichana wenziwe na alikuwa amependeza sana kiasi cha kunitoa udenda. Sikutaka kuondoka bila kumchombeza na hivyo ilibidi nisubiri hadi kiza kilipoanza kuingia nikajaribu bahati yangu kwa kurusha ndoano iliyojaa chambo, ingawa niliamini kuwa siku hiyo nisingekuwa na uhuru mkubwa wa kuongea naye.

Hata hivyo, niliitumia nafasi ya kutokuwepo mjomba pale nyumbani kwa kumwomba Mama Happy, mke wa mjomba wangu aniite Zakia ili niongee naye. Kwa kuwa nilielewana sana na mke wa mjomba hivyo hakuwa na noma kabisa, aliachia tabasamu, akaniitia.

Zakia hakukataa mwito japokuwa aliniwekea masharti ambayo sikuwa na budi kuyakubali ili nizungumze naye, sharti kubwa lilikuwa la kunipa dakika tano tu za kuongea naye kwa kuwa hakutaka watu wamshtukie hasa ikizingatiwa kuwa alikuwa mchumba wa mtu na wiki chache baadaye angeolewa.

Tukaketi pale sebuleni, sehemu iliyokuwa na tulivu mkubwa kwa kuwa muda huo watu wote, isipokuwa mke wa mjomba, hawakuwepo nyumbani. Hata hivyo, kutokana na maneno yangu matamu yenye kuvuta kama ulimbo tulijikuta tukiongea kwa zaidi ya dakika ishirini na kulielezea dukuduku langu juu yake ambalo lilikuwa moyoni mwangu tangu nilipomtia machoni, kwani Zakia alikuwa mrembo sana.

“Zakia, naomba niwe mkweli tu… wewe ni msichana mrembo mwenye sifa zote… hisia nilizonazo juu yako hazielezeki, ninahisi moyoni mwangu kuna shimo kubwa sana liitwalo mapenzi… shimo la mapenzi juu yako…” Nilijitoa kimasomaso kumkabili Zakia mara tu tulipoketi sebuleni kwa mazungumzo, muda huo moyo wangu ulikuwa unagwaya na kunienda mbio.

“Tangu nilipokutia machoni nimejikuta nikiwa na mwili wa mgonjwa nikisubiri kifo ili nirudi mavumbini, ubongo upo hospitalini na nafsi kwa Mungu. Ni wewe pekee wa kuniponya… wala sikuongopei kwani kwako sina ila wala hila, nimetokea kukupenda sana,” niliongeza.

Zakia alimwemwesa macho yake na kutabasamu kwa aibu kisha aliinamisha uso wake chini na kufikiria kwa sekunde kadhaa huku akivunjavunja vidole vyake vya mikono kisha aliinua uso wake na kuyatuliza macho yake kwenye uso wangu pasipo kupepesa macho.

“Unasema unanipenda?” Zakia aliniuliza huku akiendelea kunitazama kwa umakini usoni kabla ya kuanza kucheka kwa chini chini.

“Ndiyo. Nakupenda sana na siwezi kuendelea kuzificha hisia zangu kwako. Ninanyoosha mikono yangu kuomba zawadi unayodhani itanifaa na sistahili kuona utakachonipa, ni hiari yako kuniwekea mikononi kile unachodhani kinanifaa zaidi…” nilimjibu kwa sauti tulivu.

“Umeanza lini kunipenda au ni baada ya kujua kuwa nimeshachumbiwa?” Zakia aliniuliza huku akinikazia macho.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

4

“Wala si hivyo, ni kwamba moyo wangu umetokea kukupenda sana, nafahamu kuwa kwa uzuri wako wapo wengi waliokutokea na wengine kwa hadhi pengine siwezi kujilinganisha nao, lakini ni juu yako kuyapima maneno yangu katika mizani ya wema na huruma, na uamuzi wote uko mikononi mwako, Zakia…” nilimwambia huku nikiachia tabasamu.

“Haiwezekani bwana. Wewe sema tu kuwa umenitamani, haiwezi kuwa katika kipindi hiki ambacho nimechumbiwa!” Zakia aliniambia huku akinikazia macho yake ya kike.

“Haiwezekani? Kwani ni muda gani mwafaka wa mtu kumpenda mwingine, au huyo mchumba wako anazuia nini kwa mimi kuwa pamoja na wewe?” nilimuuliza huku nikiachia tabasamu la kumlainisha.

“Sijui ila ninachojua ni kwamba wewe umenitamani tu. Yaani unataka kulala na mimi tu ili kuongeza idadi ya wasichana uliolala nao,” Zakia aliniambia.

“Kitu gani kimekufanya ufikiri hivyo? Nakiri kwa moyo wangu wote kwamba nakupenda kuliko ambavyo ninaweza kueleza,” nilisema kwa sauti tulivu.

“Mimi nakufahamu sana, Jason, na sifa zako nazijua…” Zakia aliongea na kunifanya nishtuke kidogo. Nilijiuliza haraka haraka ni nani aliyekuwa amefikisha umbea hadi Kiloleni, miraa ambayo nilidhani kuwa sijulikani.

“Najua ni kwa sababu ya hii ngoma ndiyo maana umenitamani. Yaani ulivyoona tunakata mauno na kuacha mapaja hadharani basi ukapagawa na ndiyo maana umeamua kuniambia jambo hilo,” Zakia alisisitiza.

“Wala sijakutamani. Haki ya Mungu sijakutamani, kwani kupenda ni kazi ya moyo na macho huwa ni shahidi tu, lakini moyo wangu hauhitaji ushahidi wowote kukupenda…” nilisema lakini Zakia alinikata kauli.

“Hakuna lolote, umenitamani tu!” Zakia alisema kisha akaangua kicheko hafifu.

“Sidhani kama unaweza kuusemea moyo wangu, mimi ndiye ninayejua kinachoendelea ndani yangu. Kwanza ni nani aliyekwambia habari zangu mpaka useme unazijua sifa zangu?” nilimuuliza Zakia huku nikiilamba midomo yangu kwa tamaa ya penzi lake.

“Hii dunia ni ndogo sana na hakuna siri. Hata hivyo hayo si muhimu sana kwa sasa… wewe kubali tu kuwa umeyaona mapaja yangu yakakuvutia, na pengine umeziona shanga zangu kiunoni zikakusisimua!” Zakia aliniambia huku akiachia kicheko kikubwa, nami pia nilijikuta nikicheka.

Nilicheka kwa kuwa huo ndiyo ulikuwa ukweli wenyewe. Nilikuwa nimemtamani Zakia kutokana na umbo lake la kuvutia, nilimtamani zaidi baada ya kuyaona mapaja yake yaliyonona, na nilimtamani mno baada ya kuziona shanga alizokuwa amevaa kiunoni na kwa namna alivyokuwa anakata mauno wakati akicheza ngoma, hayo yote yalinifanya nijikute napandwa na mzuka wa ngono. Basi!

Na hata muda ule tulipokuwa tunaongea nilikuwa nakimezea mate kifua chake chenye maziwa madogo yenye chuchu nyeusi zilizosimama wima kama mkuki wa Kimasai kikipanda na kushuka kila alipokuwa anahema. Taswira ya chuchu hizo ilizidi kunivuruga na kuzisulubu hisia zangu. Nilijilamba midomo yangu kwa matamanio na mwili wangu ulisisimkwa sana na kunifanya nitamani kumkumbatia kwa nguvu palepale tulipokuwa tumeketi.

Ni kama vile Zakia alikuwa anayasoma mawazo yangu, aliniambia kuwa isingewezekana mimi na yeye kuwa wapenzi na kwamba alikuwa ananichukulia kama kaka yake kwa kuwa baba yake na mjomba wangu walikuwa marafiki wakubwa.

Na pia alidai kwamba alikwisha chumbiwa na kuvishwa pete na miezi miwili baadaye angeolewa, hivyo asingeweza kuruhusu jambo lolote la aina hiyo litokee kwa kuwa alikuwa hajawahi kumjua mwanamume. Yaani alikuwa bado amefungwa kwenye makaratasi.

“Mtu pekee ambaye anapaswa kuchukua zawadi hii ni mume wangu Msabaha,” Zakia aliniambia kwa namna ya kunitambia huku akijitahidi kunionesha ni kwa namna gani alikuwa amejitunza. Kisha aliachia tabasamu pana la aibu huku akiviminyaminya vidole vya mikono yake kama mtoto anayedeka.

Nilijaribu kumshawishi kwa kila njia ili niweze kumpata hasa baada ya kujua kuwa alikuwa bikra lakini Zakia alisisitiza kuwa yeye si chochote kitu bila huyo mchumba wake maana ndiye mwanaume aliyemfanya kuwa na furaha na kuonekana mzuri machoni pa wanaume wengine.

Siku hiyo nilishindwa kumshawishi Zakia lakini sikukata tamaa. Niliomba namba yake ya simu, akanipa. Na kuanzia hapo sikusita kumpigia simu na kumfanyia hili na lile kila iitwayo leo katika kuonesha kuwa nilikuwa nampenda sana.

Matendo hayo mema kama ya zawadi za hapa na pale, ambayo mwanamke yeyote akifanyiwa huwa yanamfanya kuhisi kuwa anapendwa yalikolezwa kila mara. Lengo langu lilikuwa moja tu, nilikuwa nawekeza katika muda nikiamini kuwa muda si mrefu angeingia kwenye kumi na nane zangu.

Japokuwa nilikuwa nafanya kiutani lakini ndivyo nilivyoweza kupiga hatua zaidi na zaidi na hatimaye siku moja Zakia alifanya kosa kubwa sana ambalo alikuja kulijutia baadaye. Ilikuwa wiki ya pili tu tangu tulipokutana kule kwa mjomba, Zakia alipita mtaani kwetu eneo la Ng’ambo akitoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Kitete kumwona mama yake mdogo aliyekuwa anafanya kazi hapo.

Kwa kuwa nilikuwa nimemwelekeza nyumbani kwangu hivyo aliamua kupita anisalimie na hakuwa amenitaarifu kama angepita kunisalimia kwani alitaka kunifanyia surprise, bahati nzuri akanikuta. Siku hiyo alikuwa amevaa gauni jepesi la rangi ya maruni la kata mikono lililolichora vyema umbo lake na kuishia kwenye magoti yake. Miguuni alikuwa amevaa viatu vya rangi ya maruni vya mchuchumio vyenye visigino virefu.

Alipotokea tu macho yangu yalifanya ziara makini nikimtazama kuanzia juu na hapo nikakutana na tabasamu laini usoni mwake. Kope zake zilikuwa zimekolezwa kwa wanja kisawasawa, macho yake makubwa, meupe na malegevu yaliyonitazama kwa umakini yaliichangamsha akili yangu.

Nywele zake nyeusi na laini alikuwa amezibana kwa nyuma, mkufu mwembamba wa dhahabu uliizunguka shingo yake nyembamba na kisha kidani chake kikapotelea katikati ya mfereji wa matiti yake maangavu yenye chuchu nyeusi kifuani. Alikuwa amebeba mkoba mdogo wa rangi ya maruni wa ngozi ya mamba alioutundika begani na mkononi alivaa bangili nyingi za rangi tofauti zilizovutia kuvutia. Kwa kifupi alikuwa amependeza sana na sikuwahi kumwona akiwa katika mvuto ule.

Nilimkaribisha, hakusita akaingia ndani, nikapata fursa nzuri ya kumchunguza vizuri huku nikikubali kimoyomoyo kwamba Zakia alikuwa mzuri sana kwani kila kitu kilichokaa katika mwili wake kilikaa kwa mpangilio.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

5

“Jason mbona unanitazama sana?” zakia aliniuliza huku akiona aibu baada ya kuniona nikimtazama sana.

“Si siri Zakia, wewe ni mzuri sana, yaani mpaka unaufanya moyo wangu unauma!” nilimwambia Zakia huku nikikunja sura yangu kuonesha maumivu niliyokuwa nayo moyoni.

“Jason, wewe muongo,” Zakia alisema huku akiyatuliza macho yake kuniangalia machoni kama aliyekuwa anayasoma mawazo yangu.

“Kweli, yaani kila nikikuangalia mwili wangu unasisimka,” nilisema huku nikionesha kusisimkwa na kumfanya Zakia acheke.

“Ahsante ila ndiyo hivyo, tayari wajanja wameshaniwahi. Vumilia tu na wewe utampata wako maana hata wewe ni kijana mzuri sana,” zakia alisema huku akinitazama machoni kwa umakini.

“Mzuri wapi! Wewe sema umeamua kunizuga tu,” nilisema huku nikimtazama kwa umakini, muda huo mawazo yangu yalikuwa ni jinsi ya kulianzisha kwani sikutaka kulaza damu.

“Wewe hujioni ila sisi tunaokuona ndiyo tunajua wewe ni handsome wa nguvu!” Zakia alisema na kuachia kicheko.

Sikutaka maneno mengi, nikaanza kubembeleza, nililia sana hadi nikapiga magoti mbele yake nikimtaka anihurumie mwenzake na aniepushe na kilio. Pamoja na yote hayo bado Zakia alionesha msimamo usioyumba.

“Najua ni ngumu sana kunielewa lakini tambua kuwa kwako sina ila wala hila, nina haya na wala sina hidaya, na hili ni ombi linalohitaji huruma yako. Siwezi kukulazimisha lakini nitakuwa mwenye furaha kubwa kama utanikubalia japo kwa siku hii moja tu, na hii itabaki siri yetu maishani,” niliyaumba maneno yangu niliyoyasema huku nikiwa nimeishika miguu yake kama mtu aliyekosa na sasa alikuwa anaomba msamaha.

“Lakini Jason, unajua kabisa kuwa nina mchumba na jinsi gani Msabaha ananipenda na kuniamini, sasa iweje utake nifanye hivi! Vumilia tu ipo siku na wewe utampata mwanamke anayekupenda kwa dhati.”

“Unaweza kuzungumza mambo mengi sana lakini ukweli utabaki palepale kuwa nakupenda kuliko maelezo. Na leo ukiniacha hivi hivi inaweza kuniathiri sana kisaikolojia,” nilimwambia Zakia huku nikiangusha chozi la uongo na kweli.

“Kwa hiyo unahitaji nini hasa?” aliniuliza huku akinitazama kwa umakini.

“Nahitaji penzi lako… ukinipa leo litajenga kumbukumbu chanya maishani mwangu. Litanipa sababu za kutabasamu kila wakati… najua ni usaliti kwa mchumba wako lakini jaribu kunihurumia mwenzio japo kwa siku hii moja tu kisha uniambie koma…” nilimshawishi Zakia huku nikiendelea kudondosha machozi.

“Hapana, hilo halitawezekana kabisa,” Zakia alijibu ingawa niligundua kuwa maneno yake hayakuendana na sura yake kwani alizungumza kwa sauti ya kulegea huku akijitingisha tingisha kwa ishara ya kukataa mgodi wake usichimbwe madini. Kisha alionekana kuanza kuzama kwenye tafakuri iliyozaa ukimya. Ni hapo ndipo alipokuwa amefanya kosa kubwa.

Nilimwaga machozi kwenye miguu yake. Nikashuhudia huruma ikimjia na roho ya kutaka kufanya usaliti ikamtawala. Nilihisi yale maswali kama ‘kwani Msabaha atajua’ yalianza kumjia akilini na akayaruhusu yaendelee kushamiri kichwani kwake. Na hapo nilianza kutumia nafasi hiyo ya ukimya vizuri. Nilianza kumpapasa miguu yake na kumfanya binti wa watu asisimkwe kwa hisia za huba.

“Jason, nakuomba uitoe mikono yako kwani unanipandisha maruhani yangu na mtu wa kuyashusha hayupo hapa, usije ukanipa shida bure,” Zakia aliniambia kwa sauti ya chini iliyobeba mitetemo huku akihema kwa nguvu. Macho yake yalianza kulegea kwa ashki.

Sikuiondoa mikono yangu bali nilizidisha mpapaso miguuni kwake, nikamwona Zakia akiyafumba macho yake kuisikilizia mipapaso yangu na wala hakuendelea kupinga. Kisha nilimnyanyua taratibu na kumshika kiuno chake na kuanza kukiminya minya kiasi na hapo nikahisi hisia zake zikianza kupanda taratibu.

Nikamuegemeza ukutani na kumshika kichwa chake nikakivutia kwangu na kuanza kumnyonya denda la fujo huku nikijitahidi kubadilishana naye mate. Tukaanza kunyonyana denda huku kila mmoja akionekana kuwa na hamu na mwenzake japo Zakia alionekana si mtaalamu sana kwenye mambo hayo. Taratibu nikaanza kumvua nguo zake mpaka akabaki kama zlivyozaliwa kisha nikazivua nguo zangu kwa pupa na kuzirusha kando.

Zakia alipoiona koki yangu jinsi ilivyofura kama nyoka kifutu akatoa yowe dogo huku akifumba macho kwa woga, muda huo mwili wake ulikuwa unatetemeka kwa msisimko. Mkono wangu mmoja ukaanza kuminyaminya chuchu za Zakia na kumfanya aanze kutoa miguno ya raha huku naye akipeleka mkono wake laini kuanza kuichua koki yangu taratibu na kunifanya nihisi raha ikipenya hadi kwenye mifupa yangu. Kisha alichukua mkono wangu na kuanza kunyonya kidole kimoja baada ya kingine huku akitoa mihemo iliyozidi kunisisimua.

Muda mfupi baadaye nikambeba Zakia hadi chumbani kwangu na kumlaza taratibu juu ya kitanda kikubwa cha futi sita kwa sita, muda huo alikuwa anahema kwa pumzi za taratibu na kuyafumba macho yake, nikaupeleka mdomo wangu kwenye shingo yake na kuanza kuinyonya, sikuishia hapo nikautumbukiza ulimi wangu kwenye masikio yeka na kumzidisha ashki, akaanza kulalamika kuwa namtesa.

Sikujali, mdomo wangu ukahamia kwenye chuchu zake ngumu zilizosimama kama mkuki wa Kimasai, nikaanza kuzinyonya taratibu huku nikizungusha ulimi wangu kwenye zile chuchu, wakati huo mikono yangu ilizidi kutambaa sehemu mbalimbali za mwili wake kabla hazijaweka kituo kwenye mgodi wake wa dhahabu, na hapo kidole kimoja cha kati kikaanza kuvinjari kikipekecha taratibu kwenye kinembe chake pasipo kumtia maumivu.

Na hapo Zakia akaanza kulia huku akinikamata kwa nguvu na kunigandamiza kwenye mwili wake, kilio chake hakikuwa cha maumivu bali cha raha isiyo na kifani ambayo hakuwahi kuipata tangu azaliwe! Nikahamishia mdomo wangu kwenye ikulu yake na kuanza kupitisha ulimi wangu taratibu lakini kwa ufundi mkubwa. Zakia akashindwa kuvumilia na kunivutia kifuani kwake huku akiendelea kulia.

Sikutaka kuendelea kumtesa binti wa watu, nikaipaka koki yangu mate kidogo kisha taratibu nikaanza kuizamisha ndani ya mgodi wake wa dhahabu uliokuwa na njia ndogo iliyobana, Zakia aliuma meno yake huku akiyasikilizia maumivu makali yaliyochanganyika na utamu usio na kifani.

Nilipoona sifaidi nikaunyanyua mguu wake mmoja juu kama antena ya kisimbuzi cha StarTimes kisha nikaizamisha vizuri koki yangu ndani ya mgodi huku nikiipanua miguu yake na kufanya koki yangu izame taratibu kwenye mgodi wake wa dhahabu kisha nikaendelea na uchimbaji wangu wa madini, Zakia alionekana kupagawa mno kwa jinsi nilivyokuwa nachimba huku nikipekecha kuelekea pande zote kuu nne za dunia. Muda wote Zakia alikuwa anapiga kelele za kupagawa.

Sikuridhika, nilimsogeza hadi kwenye kona ya ukuta, nikamkunja na kuendelea kuchimba madini kwenye mgodi wake kwa kasi zaidi, Zakia aliizungusha miguu yake kiunoni kwangu na akaibana kwa nyuma huku akiwa amenikumbatia kwa nguvu akinihemea kwenye masikio yangu, kiuno changu chepesi katika uchimbaji wa madini kilifanya kazi kwa kasi ya ajabu na kumfanya Zakia kulalamika kwamba pumzi zilikuwa zinamuishia. Mtanange wa uchimbaji wa madini ulipozidi nilimwona Zakia akihema kwa pupa kama bata mzinga.

Nikamgeza kisha nikamwinamisha japo aliinama kiuvivuvivu huku akionekana kuchoka sana, nikamwekea mto mmoja katika kifua chake, akaulalia huku akiwa amebong’oa, nikazishika nywele zake ndefu na kuzivutia nyuma huku nikiendelea na uchimbaji wa madini na kumfanya Zakia kulia zaidi ya kile kilio cha mara ya kwanza.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

6

“Jason, unaniua mwenziooo… nakufa Jasoooon…” Zakia alilalamika huku akiendelea kulia.

“Hufi Zakia…” nilimwambia huku nikizidisha uchimbaji wa madini. Kilio chake kilizidisha kunipa mzuka wa kuchimba madini.

“Jason niache mwenzio najisikia vibaya,” Zakia alikuwa analalamika lakini sikumsikiliza kwani kwangu raha ndiyo ilizidi kuongezeka.

Hata hivyo niliziachia nywele zake kisha nikaikita miguu yangu kwenye godoro nikawa kama nimekalia stuli huku mikono yangu ikikishika vyema kiuno chake na kuongeza mwendo kasi wa kiuno changu katika kuiendesha koki yangu, safari hii nikawa ninachimba katika kuta zote za mgodi na kumfanya Zakia aanze kutoa miguno kama mtu aliyekuwa anataka kutapika.

Kwa mbali nikaanza kuhisi wazungu wakisogea kwa kasi ya ajabu huku nikipata raha ambazo wanaume tukifikia katika hatua hiyo hata ukiambiwa ufanye kitu chochote unakubali kwani mwili na akili vyote vinahamia katika sayari ya mbali ambayo si rahisi kuifikia katika mazingira ya kawaida. Muda huo nikaona mwili wa Zakia ukikakamaa huku mgodi wake ukiibana vizuri koki yangu.

Mpaka namaliza kuchimba madini Zakia alikuwa hoi, kisha ukimya mkali ukatawala kati yetu kisha nikamwona Zakia akinyanyuka kiuvivuvivu toka kitandani na kuelekea chooni huku akipepesuka mithili ya mlevi. Huko chooni nilimsikia analia huku akijigoa kama aliyekuwa anatapika. Nikainuka na kumfuata kule chooni kwenda kujua alikuwa na tatizo gani!

Nilimkuta akiwa ameinama kwenye sinki la kupigia mswaki huku akiendelea kutapika na kisha alisukutua mdomo wake kwa maji. Dah, nilimtazama huku nikijipongeza moyoni kwani siku hiyo cha mtu kilikuwa kimeliwa na baharia, kama ambavyo chuma huliwa na kutu!

“Vipi una tatizo gani?” nilimuuliza Zakia huku nikimtazama kwa wasiwasi.

Hakunijibu chochote zaidi ya kuniangalia tu kupitia kioo kilichokuwa ukutani juu ya lile sinki la kupigia mswaki. Alikuwa amenuna, alipomaliza kusukutua mdomo wake alifungua bomba la mvua, akajimwagia maji ili kuupa nguvu mwili wake ulionyong’onyea na kurudi chumbani huku nikiwa nyuma yake nikiyaangalia makalio yake makubwa yasiyo na nguo yalivyokuwa yanatetemeka na kupishana.

Hakuwa anazungumza chochote hadi tukafika kitandani, akapanda kitandani na kulala akielekea ukutani kisha akachukua shuka na kujifunika. Nilibaki na alama ya kujiuliza nisijue kitu gani kilichomfanya Zakia kununa kana kwamba kitu nilichomfanyia hakikuwa kizuri. Nami nilipanda kitandani kisha nikalivuta lile shuka nikajifunika huku moyoni mwangu nikiwa na furaha kwa kuukata utepe wa Zakia na kuuzindua rasmi mgodi wake.

“Zakia unaonaje tukiunganisha mzunguko wa pili?” nilimchokoza Zakia huku nikimpapasa makalio yake yaliyonona.

“Nyoo! Hebu niache utaniua mwana wa mwenzio,” Zakia aling’aka huku akiusukuma mkono wangu kwa hasira.

“Kwani nini kimetokea mbona unaonekana kama umenikasirikia, tatizo ni nini?” nilimuuliza Zakia huku nikiilamba midomo yangu.

“Jason, nilikwambia mwenzio sijawahi kufanywa lakini ukaamua kunifanya utadhani ulikuwa na kisasi na mimi! Kama wanaume wote ndio mko hivi hata hiyo ndoa yenyewe itanishinda!” Zakia alilalama.

“Mbona ilikuwa kawaida tu imekuwaje ukatapika?” nilimuuliza kwa sauti tulivu.

“Si kwa jisi ulivyonibinua na kunivuta vuta nywele, kichwa chote kinaniuma utadhani mgonjwa wa malaria.”

“Pole mwaya, sikukusudia ila mzuka ulinipanda maana kuna utamu wake,” nilimwambia Zakia huku moyoni nikijipongeza kwa ushindi mnono wa pointi tatu na magoli matatu nilioupata.

“Utamu gani wakati mwenzio nilikuwa naumia?” Zakia alisema huku akigeuza shingo yake kuniangalia.

“Pole basi mpenzi, vipi tupige basi cha mwisho cha kuisindikizia siku,” nilibembeleza huku nikimshikashika na kila nilipougusa mwili wake nilihisi mwili wangu ukisisimkwa kwa ashki.

“Hapana Jason, ninaumwa mwenzio naomba uniache,” Zakia alisema huku akiutoa mkono wangu kwenye mwili wake.

“Kimoja tu,” nilibembeleza. Zakia alinitazama huku akionekana kutaka ila nafsi yake ilikuwa inasita.

Niliinuka kisha nikachuchumaa na kuyapanua mapaja yake, akayabana akionekana kutotaka niyapanue. Nikapeleka kidole changu kwenye mgodi wake taratibu huku nikimtazama machoni kwa jinsi alivyokuwa anayafumba macho yake kwa hisia kali. Zakia akanyanyua miguu yake juu huku akiwa anatetemeka kama mtu aliyemwagiwa maji ya baridi.

Hali ya kutetemeka ikaniogopesha sana, nikamwachia na kumtazama kwa wasiwasi huku naye akinitazama kwa macho yaliyolegea yakionekana kukosa nguvu ya kuona vizuri.

“Vipi mbona hivyo?” nilimuuliza kwa wasiwasi.

“Nimekuambia ninaumwa mwenzio, naomba uniache nipumzike kidogo ili nipate nguvu za kunifikisha nyumbani maana hapa nilipo sijielewielewi!” zakia aliniambia kwa sauti ya chini ya unyonge.

Nilinyanyuka na kuwacha pale kitandani, sikutaka kumgusa tena! Japo nilimsababishia ugonjwa lakini kwangu lilikuwa ni tendo la furaha sana kuuzindua mgodi wake kwa kukata utepe. Katika maisha yangu nilikuwa na bahati kubwa kukutana na wasichana waliojitunza ila wote walikuwa na bahati mbaya kwani sikuwa na mapenzi ya dhati, nilichotamani ni kulala nao mara moja tu na kisha nikahamishia majeshi kwa wengine.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

7

Baada ya siku hiyo Zakia aliniambia kuwa hakika nilikuwa nimemfanya ajihisi kama yupo katika pepo fulani ya maraha ambayo hakuwahi kuota kuifikia hata siku moja, na laiti angejua kama nilikuwa fundi katika mapenzi kiasi kile basi asingesita kunikubalia tangu siku ya kwanza, na pengine asingekubali kuchumbiwa na mwanamume mwingine zaidi yangu. Alikuwa amefurahishwa sana na kiwango cha hali ya juu cha uchezaji wangu.

Ni kama mioyo yetu ilisemezana na fikra zetu zikalandana maana alinitafuta siku nyingine, tukabanjuka tena, siku hiyo tulibanjuka hadi nafsi zetu zikakinai. Kisha Zakia alikuja tena nyumbani kwangu kwa mara ya tatu na baada ya hapo aliniambia kuwa alitakiwa kukaa ndani kwa kuwa harusi yake ilikuwa imekaribia. Lakini wiki mbili kabla ya harusi Zakia alinifuata nyumbani kwangu akiwa amechanganyikiwa sana. Alikuwa amejawa na huzuni na jasho jembamba lilikuwa likimtoka mithili ya mtu aliyekoswa na risasi. Alipoingia tu ndani kwangu alijibwaga kitandani kama mzoga.

“Vipi mbona hivyo, kwema huko?” nilimuuliza kwa mashaka baada ya kumwona katika hali ile.

“Hivi unavyoniona nimetokea hospitali baada ya kuhisi homa na mara kwa mara natapika, mwanzo nilidhani malaria lakini daktari aliponifanyia vipimo amegundua kuwa nina ujauzito wa mwezi mmoja na wiki mbili,” Zakia alisema huku akilengwalenga na machozi.

“Dah! Sasa…” nilitaka kuongea lakini nikashindwa maana hata sikujua nilitaka kusema nini. Baada ya kutafakari sana hatimaye nikapata wazo.

“Kuna njia mbili za kufanya, moja ni kusubiri hadi Msabaha akishakuoa na wiki chache zikipita jifanye kwenda kupima kisha mwambie kuwa umeshika ujauzito, na njia ya pili ni kuutoa ujauzito kimya kimya.”

“Katika maisha yangu kamwe sikuwahi kufikiria kutoa mimba. Hata ingekuwaje kamwe siwezi kutoa mimba. Najua madhara makubwa ambayo naweza kuyapata kutokana na kutoa mimba. Nishauri vyote ila kwenye kutoa mimba sitoweza,” Zakia alisema kwa msisitizo.

“Ndiyo maana nimekupa njia mbili basi jaribu kusubiri kwanza kisha utamwambia mumeo kuwa umeshika ujauzito uone atalipokeaje suala hilo.”

“Lakini pia najihisi hatia kubwa sana kumbambikizia mimba mtu asiyehusika. Kwanza nimefanya dhambi ya usaliti halafu tena nimbambike na ujauzito! Na kama akigundua kuwa mimba si yake huoni lazima italeta utata?” Zakia alisema kwa huzuni.

Aliiangalia pete yake ya uchumba aliyokuwa amevikwa, akasikitika. Chozi likamtoka. Aliniambia kuwa alitamani hata kuivua ile pete na kuitupa kwa maana roho yake ilionekana kumsuta sana na kumfanya ajione ni mwenye upofu mkumbwa na mwenye dhambi kubwa ya usaliti. Hakika dhambi ya usaliti ilimtafuna! Nami nilijihisi kuchanganyikiwa.

Siku hiyo ilipita bila muafaka, likaja suala jingine lililozidi kunichanganya, baada ya harusi yao Msabaha alihamia kwenye ile nyumba niliyokuwa nikiishi, pale Ng’ambo, na hivyo ilituwia vigumu sana mimi na Zakia kuangaliana machoni kwani dhambi ya usaliti ilikuwa ikitusuta, hata hivyo tuliamua kuwa ibaki siri.

Sasa ndiyo ikaja siku hiyo iliyokuwa imetangulia, ilikuwa alasiri ya siku hiyo Zakia alinifuata akiwa amechanganyikiwa mno.

“Jason, mwenzio sijui hata nifanyaje!” Zakia alisema kwa sauti ya kukata tamaa.

“Kuhusu nini tena!” nilimuuliza huku nikihisi mapigo ya moyo wangu yakienda kasi isivyo kawaida.

“Yaani Msabaha ameshtuka sana baada ya kuambiwa na daktari kuwa nina ujauzito wa miezi minne wakati mimi na yeye tuna miezi miwili tu tangu tuoane.”

“Mungu wangu! Sasa kasemaje?” niliuliza kwa wasiwasi huku nikihisi kijasho jepesi kikinitambaa mwilini.

“Wacha tu, hajaongea kitu chochote zaidi, tulipofika tu nyumbani akaondoka zake bila hata kuaga na wala sijui ameelekea wapi? Yaani hata sijui itakuwaje?”

“Nilikwambia tuitoe ukakataa sasa mimi sipo tayari kwa lolote na ninaomba usije ukanihusisha…”

“Lakini ukweli wewe ndiye baba wa mtoto huyu!” Zakia aliniambia na kunifanya niogope sana. “Hata hivyo, nitajua cha kufanya, ikibidi nitamwambia tu ukweli ili kama ni kuniacha basi aniache tu,” Zakia alisema na kuondoka pasipo hata kusubiri aone ningesema nini.

Siku hiyo nilichanganyikiwa sana na muda wote nilikuwa nasikilizia ili kujua kilichokuwa kikiendelea. Ndipo ilipofika saa tatu usiku nikaona Msabaha akirudi nyumbani ameongozana na jamaa zake wawili, na wakati wakiwa ndani kwao niliweza kusikia ukiibuka mzozo mkubwa baina ya Msabaha na Zakia.

“Haiwezekani. Haiwezekani kabisa. Lazima aseme ukweli, mimi na yeye tumeoana lini na kabla ya hapo hatujawahi kufanya tendo?” niliisikia sauti ya Msabaha akihoji kwa sauti ya juu.

Kisha nilimsikia Zakia akiongea kwa sauti ya chini kidogo na bahati mbaya sikuweza kujua alikuwa akiongea nini.

“Nitaamini vipi? Kwa hiki ulichonifanyia kamwe siwezi kukusamehe mpaka hapo utakaponiambia ukweli aliyekupa hii mimba ni nani?” niliisikia sauti ya Msabaha akiongea kwa hasira, nilihisi labda muda huo alikuwa akizunguka zunguka kwenye chumba hicho.

“Kwa hiyo unaniona mimi malaya? Umewahi kunifumania hata siku moja au uliniona wapi nimetembea na mwanaume?” sauti ya Zakia iliuliza kwa hasira. Kikatokea kitambo kifupi cha ukimya.

“Sasa hiyo mimba umeipataje?”

“Mme wangu kwanza lazima ukubali kuwa nina dhamira nzuri ya kutotaka kukudanganya, dhamira ya kukueleza ukweli, dhamira ya kuomba msamaha. Kama ningekuwa na nia mbaya ningeweza tu kuitoa na usijue,” kisha nilimsikia Zakia akiongeza, safari hii aliongea kwa upole.

“Hivi unafikiri mimi ni mjinga kiasi hicho? Nitawezaje sasa kukuamini endapo tu mimi na wewe tumeoana miezi miwili iliyopita na daktari aliyekupima anasema ina miezi minne? Hivi wewe ni mwanamke usiye na akili kiasi gani hata ukawa unafanya upuuzi kama huu wakati unajua kabisa unaolewa.” Nikamsikia Msabaha akisema kwa hasira.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

8

Kisha nikasikia kwikwi na vilio, Zakia alikuwa analia kwa uchungu. Maneno yake ya kuomba msamaha mbele ya mume wake Msabaha yalionekana kuwa hayakuwa na thamani yoyote kabisa. Muda huo nilitamani hata ardhi ifunguke na mimi nijifiche ndani. Lakini hilo halikuwa jambo rahisi kwa wakati huo. Zakia Aliendelea kulia kila aina ya mlio lakini ilionesha kuwa mume wake alikasirika sana.

Kisha nikamsikia mtu mmoja kati ya wale watu wawili waliokuja na Msabaha akimsihi sana Msabaha asifanye jambo lolote linaloweza kumfanya akaja kujuta baadaye. Ilikuwa ni sauti nzito.

“Hivi ndugu yangu, unaweza kuishi na mwanamke ambaye tayari ana mimba ya mtu mwingine, au mwenye mtoto?” nilimsikia Msabaha akimuuliza yule mtu.

“Kwa mimi binafsi sijui kama naweza, hapo lazima niwe mkweli tu, ingawa wapo wanaume wanaoweza. Ujue upendo hauangalii, kama umempenda mtu kutoka moyoni kwa nini usiishi naye?” nilimsikia yule mtu mwenye sauti nzito akisema.

“Mimi naweza kuishi na mwanamke wa aina hiyo na ndiyo maana sikushauri kufanya uamuzi wowote wa kukurupuka, kwanza jaribu kusikiliza kwanza moyo wako kwenye mapenzi na si mawazo yako au ya watu wengine, kwa maana watu tunatofautiana sana kimalengo huku duniani,” nikaisikia sauti nyingine ikidakia.

“Nimewaelewa kaka zangu lakini nitawezaje kuishi na mwanamke ambaye hataki kuwa mkweli? Amekataa hata kuniambia huu ujauzito ni wa nani?”

“Halafu akikwambia ufanyeje?” mmoja wa wale watu aliuliza.

“Nimjue tu halafu nitaamua cha kufanya,” nikaisikia sauti ya Msabaha akisisitiza kutaka kujua. Nikahisi mwili wangu ukiingiwa na ubaridi mkali sana, moyo wangu ukapiga kite kwa nguvu na kijasho chembamba kikaanza kunitoka.

“Ujue kaka, wakati mwingine ni vema mambo mengine usiyajue utaishi kwa amani maana ukiyajua unaweza kuumia zaidi. Ujue usaliti upo wa aina nyingi ila kitu cha muhimu na cha kujua ni nini chanzo cha usaliti huo? Hawa wanawake si vichaa kiasi hicho mpaka afikie hatua ya kukusaliti bila sababu yoyote, na kama mimba hiyo inaelekea miezi minne na bado amekaa nayo pia kuna la sirini hapo maana angeweza kuitoa kimya kimya bila wewe kujua… usitake kuniambia kuwa eti alikuwa hajui kama ni mjamzito hadi mimba inafikisha miezi minne wakati alishakuwa na dalili za kutapika na kadhalika!”

“Mimi sikatai, najua wapo watoto wengi wanaozaliwa kwenye ndoa si wote ni wa mume halali wa ndoa ila…” nilimsikia Msabaha akiongeza.

“Sawa kabisa, tena familia zetu hizi za Kiswahili ndiyo kabisa, wewe unafanya biashara ya kusafiri miezi kibao au wakati mwingine utakuta mume yupo Shinyanga na mke yupo Tabora, ni ngumu sana kwa kweli, hivyo unaweza ukajikuta kwenye watoto wanne uliozaa na mke wako wawili tu ndio wako,” ile sauti nzito ikadakia.

“Mimi nadhani usifanye jambo kwa kukurupuka, kama mwanamke amekubali kosa, ameomba msamaha na yupo tayari kubadilika kwa nini usimsamehe? Isitoshe dini inatufundisha kusamehe…”

“Unaweza kumsamehe lakini kama anaridhishwa zaidi kimapenzi na huyo mchepuko wake si ataendelea kukusaliti?” nilimsikia Msabaha akiuliza.

“Kakwambia alikutana na huyo mwanamume siku moja tu na hajui yupo wapi, hapo cha msingi ni kuupima upendo. Usaliti hata wanaume tunafanya lakini mara nyingi ni kwa ajili ya tamaa… swali la kujiuliza hapa, je, hao ambao tunachepuka nao hawana wenzi wao? Hivi na hao wenzi wao wakijua huwa wanaachana?” ile sauti ilimuuliza tena Msabaha. Sikusikia kama Msabaha alijibu lolote ila nilimsikia yule mtu akiongea tena.

“Usione hivi, hizi ndoa zina mambo mengi sana cha muhimu ni kuvumiliana, kusameheana na kuyasahau ili tusiwape watu faida, kwani hii ni sehemu tu ya mapito yetu,” sauti nyingine ilisikika na baada ya hapo sikuweza kusikia tena kwani walipunguza sauti, nilichoishia kusikia ilikuwa ni sauti za chini mfano wa minong’ono tu.

Kumbukumbu hizo zilinifanya niweze kukumbuka jambo… nilikumbuka kuwa ni mzozo huo kati ya Msabaha na mkewe Zakia ndiyo ulionifanya kwenda kwa rafiki yangu mzee wa mipango mingi mjini, mzee wa ushauri… Majaliwa Nzilwa.

Ilikuwa saa tatu na nusu usiku nilipomkuta kwenye maskani yake. Na aliponiona tu hakushindwa kugundua kuwa sikuwa sawa, kulikuwa na jambo lililoisumbua sana akili yangu. Nilimweleza na nilitarajia kupata suluhisho na badala yake nikaishia kunywa pombe nyingi hadi nikapoteza kumbukumbu…

_____

“Vipi kaka, safari ya wapi saa hizi? Naona kama una mawazo mengi sana maana muda mrefu tu nakuona umesimama hapo unaongea peke yako!” sauti ya mpangaji mwenzangu Adolf Sitta ilinishtua sana toka kwenye lile lindi la mawazo. Adolf alikuwa amesimama mbele ya nyumba yetu akiiweka sawa pikipiki yake ambayo aliitumia kwa ajili ya shughuli zake.

Sikujua nilikuwa nimesimama hapo nje kwa muda gani kwani alfajiri ile hali ya hewa katika mji wa Tabora ilikuwa ya ubaridi sana na kulikuwa na kiza kizito kilichotawala kana kwamba ilikuwa bado ni usiku sana kutokana na wingu zito jeusi la mvua lililokuwa limetanda angani.

Ndani ya manispaa ya Tabora, moja ya miji mikongwe zaidi nchini Tanzania, eti hakukuwa na taa za barabarani! Hapana, taa zilikuwepo isipokuwa zilikuwa haziwaki! Kwa nini haziwaki? Swali hilo maofisa wa Manispaa ya Tabora au wale wa shirikia la ugavi wa umeme (Tanesco) ndio wangekuwa na jibu.

Muda ule upepo ulikuwa ukivuma na kufanya baadhi ya takataka zilizopo katika mtaa ule kupeperuka huku na kule. Upepo huo ulizidisha hali ya ubaridi na kusababisha baridi kali kupenya kwenye ngozi yangu kavu na kunifanya nitamani kujikunyata.

Nilimsalimia Adolf, na wakati huo nikagundua kuwa alikuwa akijiandaa kuiwasha pikipiki yake ili aondoke kuelekea kwenye shughuli zake, nikamwomba anisogeze hadi stendi kuu ya mabasi, eneo ambalo halikuwa mbali sana kutoka pale tulipokuwa tukiishi.

Wakati tukielekea stendi ya mabasi Adolf aliniuliza kama nilisikia kuhusu mzozo kati ya Zakia na mumewe Msabaha, sikupenda kuliongelea suala lile kwa kuwa lilikuwa linanigusa moja kwa moja hivyo nikamjibu kuwa sikujua chochote na kisha nikabadilisha mada. Nilishukuru kwa kuwa hakuendelea na maongezi kuhusu Zakia na Msabaha.

* * *

Mambo yanaanza kushika kasi, usikose kuufuatilia mkasa huu wa kusisimua
 
safari buzwagi.JPG

9

Mpango Mbadala


Saa 12:40 asubuhi.

HADI nafika katika stendi kuu ya mabasi ya Tabora wingu zito jeusi la mvua lilikuwa bado limetanda angani na hali ya giza iliendelea kutanda. Hata hivyo, taratibu upepo ulianza kuvuma na kuanza kulisukuma lile wingu zito ukilipeleka upande wa magharibi na hivyo kusababisha vumbi litimke huku na kule katika eneo lote la stendi kuu ya mabasi mjini Tabora.

Kwa hali hiyo kila mtu aliyekuwepo eneo hilo alificha uso wake ili vumbi hilo lisije kumletea madhara yoyote, lakini watoto wa mtaani waliokuwa eneo lile walionekana kutoijali hali hiyo na walianza kukimbiakimbia huku na kule kutaka kuyadaka makaratasi na mifuko ya nailoni yaliyokuwa yakipeperushwa na vumbi hilo.

Wao hawakufikiria hata mara moja kwamba vumbi hilo lingeweza kuwaletea madhara kiafya, wao hawakujali hata kesho yao ikoje.

Nilimtafuta Eddy nikamkuta akiwa amejificha kwenye kibanda kimoja cha kupumzikia akijaribu kuliepuka vumbi, alikuwa amekasirishwa sana na kitendo changu cha kuchelewa kwani basi la Njamba Express tulilopaswa kuondoka nalo kwenda Kahama lilikuwa limekwisha ondoka kuelekea Kahama, na mabasi yaliyokuwepo muda huo yalikuwa yanaelekea maeneo mengine ya nchi.

Eddy alikuwa ananitazama kwa jicho kali, jicho lililofikisha ujumbe kwamba hakuwa amependezwa kabisa na kile kilichotokea, hata hivyo nilijikausha nikijifanya sielewi kinachoendelea. Nilimtupia jicho mara moja kisha nikazuga kutazama huku na kule kana kwamba nilikuwa natafuta kitu lakini ukweli nilikuwa nayakwepa macho yake huku nikijaribu kufikiria njia mbadala ya kufanya.

Hata kwa mtazamo wa haraka tu mtu asingeshindwa kubaini kuwa Eddy alikuwa kijana mstaarabu sana na msomi, akiwa na umri wa miaka 30 muda mwingi alikuwa nadhifu mno. Alikuwa mrefu wa futi sita na inchi moja na maji ya kunde, mwenye uso wa umbo duara na sura ya tabasamu muda wote, tabasamu ambalo lilikuwa likizihadaa nyoyo za wasichana wengi ingawa kiuhalisia yeye mwenyewe hakuwa na tabia ya kupenda vidosho.

Alfajiri hiyo alikuwa amevaa suti maridadi ya kijivu ya pande tatu, shati la mikono mirefu la rangi ya samawati, tai shingoni iliyokuwa na rangi za bendera ya taifa, kofia ya kijivu aina ya pama na miguuni alivaa viatu vyeusi vya ngozi halisi ya mamba. Alikuwa amebeba begi dogo la safari begani.

Eddy hakuwa ameoa lakini alikuwa na mchumba aliyeitwa Emmy Mgeleka na walitarajia kuoana miezi michache tu baada ya msichana huyo kuhitimu masomo yake ya Shahada ya Biashara (Business Administration) katika Chuo Kikuu cha St. Augustine cha Tanzania (SAUT) cha jijini Mwanza. Kwa maana hiyo, Eddy hakuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na msichana mwingine yeyote ambaye alijua kuwa hangeweza kumuoa.

Eddy alikuwa mpole, mwenye sauti tulivu ya upole iliyoonekana kuwaburudisha wasichana wengi pindi ipenyapo masikioni mwao kila alipokuwa anaongea nao, na alikuwa mcheshi sana ingawa kwa mtazamo wa haraka haraka mtu yeyote angeweza kudhani hakuwa mzungumzaji. Tabia yake ya upole na ucheshi ilitokana na malezi ya kisemanari aliyoyapata katika Shule ya Seminari ya Itaga, na baadaye alikwenda chuo kikuu kusomea taaluma ya sheria.

Hivyo, masomo ya falsafa na ya sheria yalimfanya Eddy kuamini kuwa si vizuri kuchezea hisia za mwanamke kwani mwanamke ni kiumbe anayeendeshwa kwa hisia na mihemko (emotions), na hivyo husikiliza zaidi sauti ya moyo wake, tofauti na mwanaume ambaye huongozwa na mantiki (logic) kwa maana ya kutumia zaidi akili yake katika kufikiri kabla ya kutenda.

Kwa ujumla, Eddy alikuwa na upekee kama ungejaribu kumlinganisha na vijana wengi wa kileo kwa sababu ya falsafa na misimamo yake binafsi, hakuruhusu mtu yeyote afanye uamuzi kwa niaba yake.

Huo ulikuwa upande wa Eddy, lakini kwa upande wangu ilikuwa tofauti sana kama ungetaka kunilinganisha naye. Japokuwa tulikuwa tumezaliwa toka kwa mama na baba mmoja na kulelewa katika nyumba moja lakini mimi sikuwa kama Eddy. Niliona fahari kubwa kuutumia ujana wangu, na silaha yangu kubwa kwa wasichana ilikuwa ni mwonekano wangu.

Nilikuwa mtanashati niliyejipenda mno kuanzia ndani ya chumba changu hadi kwenye mwili wangu, na kwa mtazamo wa nje mtu yeyote asingesita kunifananisha na mtu yeyote mashuhuri, awe ni mfanyabiashara mkubwa, msanii maarufu au mwanamitindo. Itoshe tu kusema kuwa nilikuwa miongoni mwa vijana wachache sana wenye mvuto wa kipekee kwenye macho ya wasichana warembo.

Nikiwa nimetimiza umri wa miaka 27, nilikuwa na urefu wa futi sita, maji ya kunde na mwenye umbo kakamavu la kimichezo. Kama ilivyokuwa kwa Eddy, hata mimi nilikuwa bado sijaoa, ila tofauti yetu ni kwamba Eddy alikuwa na mchumba lakini kwa upande wangu sikuwa na mwanamke maalumu na pia sikuwa na mpango hata wa kuoa!

Tofauti nyingine kubwa kati yangu na Eddy ilikuwa ni katika mitazamo na misimamo. Eddy aliwaheshimu sana wanawake akiwa hataki kuingia kwenye uhusiano wa kimapenzi na msichana ambaye alijua kuwa asingeweza kumuoa, lakini mimi sikutaka kupitwa na warembo, nilikitamani kila kilichofichwa ndani ya andawea.

Kutokana na utanashati wangu na maneno matamu yenye kushawishi, kila niliposhikwa na haja za kimapenzi ilikuwa rahisi kumpata mwanamke yeyote nimtakaye na nilipomaliza haja zangu niliachana naye, na sikutaka kuwa na mwanamke maalumu kwa kuogopa mambo ya kuoneana wivu. Kitu hicho kilinifanya kuwa na uhuru wa kufanya mambo yangu bila ya kuingiliwa na mtu.

Eneo lote la Gongoni kwa wazazi wangu nilikokulia, mitaa niliyopenda kutembelea na hata pale Ng’ambo nilipohamia miezi kadhaa iliyokuwa imepita, nilikuwa najulikana sana kwa kubadilisha wanawake kama nguo, na sikutaka kabisa kuamini kuwa duniani kulikuwa na mapenzi ya kweli bali mapenzi ya kweli yalipatikana zaidi kwenye riwaya za mapenzi au kwenye michezo ya kuigiza tu.

Kwangu, kiumbe aliyeitwa mwanamke alikuwepo duniani kwa ajili ya kumfurahisha na kumburudisha mwanamume tu, na hivyo katika maisha yangu kuwa na uhusiano na wasichana zaidi ya mmoja halikuwa jambo la kushangaza kabisa!

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

10

Hata hivyo, kuna nyakati ambazo nilikuwa najiuliza kama hawa wanawake ni viumbe dhaifu kupita vyote duniani ama walikuwa viumbe majasiri kulikoni vyote? Kila nilivyofikiria uchungu wanaoupitia katika kutubeba kwenye matumbo yao na kisha kutuzaa katika hali ya uchungu mkubwa, basi nilipiga goti na kuwavulia kofia ya heshima ingawa kulikuwa na mengine lukuki ambayo kila nilipoyafikiria nilijikuta kichwa kikiniuma sana.

Pamoja na kufikiria hivyo bado tabia ya kuwabadili wasichana kama nguo sikuiacha na ilinifanya nigombane na kaka yangu Eddy mara kwa mara, kwani yeye aliamini kuwa mwanamke alistahili kupewa heshima yake kama ilivyokuwa kwa mwanamume.

Mara nyingi Eddy aliniasa kwa kuniambia kuwa “mwanamke unayemchezea leo, ndiye atakayeolewa na mwanamume mwenzako kesho! Je, unajua mke utakayemuoa anafanywa nini leo na mwanamume mwenzako?”

Neno ambalo halikukauka mdomoni mwa Eddy kila mara aliposikia nina uhusiano na mwanamke mwingine lilikuwa ni “Jason, tafadhali usipende kuchezea hisia za mwanamke.” Alipenda kunikumbusha kuhusu tukio la kuhuzunisha la kifo cha mwanadada Belinda Mwikongi, aliyekuwa binti wa Diwani wa Kata ya Gongoni katika Manispaa ya Tabora, mzee Albert Mwikongi.

Belinda alikuwa msichana aliyetokea kunipenda sana na siku zote aliamini kuwa ningemuoa baada ya kumaliza masomo yake ya chuo kama ambavyo nilikuwa nimemuahidi, kumbe moyoni kwangu sikuwa na mpango wowote wa kumuoa bali nilipanga kumchezea tu.

Kilichomfanya Belinda anipende sana na kuniamini zaidi ni kwa sababu mimi ndiye ‘nilimwondolea utoto’ wake baada ya kumlaghai sana na kisha kumwingiza katika dunia ya wakubwa. Hiyo ilikuwa ni baada ya kufanya mtihani wake wa mwisho wa kumaliza kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Uyui hapo Tabora.

Wakati nakutana na Belinda alikuwa na umri wa miaka 18 na alikuwa bado hajamjua mwanamume. Nilipomuuliza kwa nini alikuwa amejitunza hadi wakati huo aliniambia kuwa mtu pekee ambaye alipaswa kuchukua zawadi hiyo ni mume wake pekee na asingeweza kumwamini mtu mwingine yeyote hata mimi japo alikuwa ametokea kunipenda.

Kiukweli nilitumia kila njia hadi kumnasa Belinda na kumwingiza kwenye himaya yangu. Belinda hakuwa mtu wa wanaume kabisa na hakujua chochote kuhusu ulimwengu wa mapenzi. Kilichonisaidia kumnasa ni kwamba nilikuwa mchezaji mzuri sana wa mpira wa kikapu, mchezo ambao Belinda alikuwa anapenda sana kuuangalia.

Hapo ndipo ukawa mwanzo wa uhusiano kati yetu, uhusiano ambao mwanzoni ulianza kwa sharti kwamba tusingekuwa tunakutana faragha mpaka pale ambapo tungeingia kwenye ndoa, hasa kwa kuwa nilikuwa nimeahidi kumuoa pindi tu akishamaliza masomo yake.

Hata hivyo, kutokutana faragha lilikuwa sharti gumu sana kwangu lakini nililipokea kwa shingo upande kwa sababu nilijua tu kuwa ingetokea siku angefanya kosa kwa kuingia kwenye kumi na nane zangu. Siku moja tu alipojisahau nami nikautumia mwanya huo huo kumfunga goli la kiufundi, na hapo ndipo pazia la mapenzi yetu lilipofunguka rasmi.

Wakati matokeo ya mtihani wake yakiwa ndiyo kwanza yametoka ndipo alipogundua uwepo wa mabadiliko mengi katika mwili wake ikiwemo kutapika na kutoona siku zake za kila mwezi. Aligundua hilo baada ya kuona imepita miezi miwili na hali yake ya kimwili ikianza kubadilika.

Baada ya kugundua jambo hilo alinitumia ujumbe mfupi kwenye simu yangu ya mkononi kunieleza kuhusu mabadiliko katika mwili wake na kwamba mama yake alikuwa ameanza kumshtukia na hivyo alikuwa ana mpango wa kumpeleka hospitali kupimwa ujauzito. Kiukweli jambo lile lilinishtua sana, na hivyo nikawa natafuta namna ya kujinasua kwa kuwa sikuwa tayari kuingia kwenye majukumu ya kutunza familia.

Kesho yake alinipigia simu lakini sikupokea akaamua kunifuata nyumbani na kunikuta nikiwa na msichana mwingine aliyeitwa Rahma, na hapo nikaamua kumkana jambo lililomuumiza sana. alilia sana lakini bado nilishikilia msimamo wangu ule ule ya kwamba simjui, na wala sikujali. Hata hivyo, japokuwa sikuamini kuwa duniani kulikuwa na mapenzi ya kweli lakini ukweli ulibaki kuwa Belinda alikuwa ananipenda kikweli kweli!

Pamoja na kumkana kwamba sikumjua lakini chozi lake liliniumiza sana na kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nilihisi hatia ikinikaba moyoni mwangu. Hata hivyo, sikutaka kuonesha kama nilikuwa nimeumizwa wakati nilipokuwa mbele ya Rahma, msichana ambaye siku hiyo ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kukutana naye.

Siku iliyofuata kaka yangu Eddy alinipigia simu na nilipopokea tu nikashtushwa na sauti yake ya huzuni, akanipa taarifa za kuhuzunisha kwamba Belinda alikuwa amekufa baada ya kunywa sumu. Na kwamba alikuwa ameacha barua fupi iliyokutwa kando ya maiti yake, chumbani kwake ikielezea kuwa “aliamua kujiua kwa sababu asingeweza kuishi huku akimshuhudia mwanamume ampendaye akimsaliti na wanawake wengine…” hata hivyo, katika barua hiyo hakuwa ametaja jina la mwanamume huyo.

Taarifa ile ilinichanganya sana na kifo cha Belinda kiliniumiza sana nikiamini kuwa mimi ndiye niliyesababisha mauti yake. Hata hivyo, sikuwa na namna nyingine yoyote ya kufanya kwani maji yalikwisha mwagika na yasingeweza tena kuzoleka. Ilibidi nimsahau na maisha mengine yaendelee.

Eddy alitarajia kuwa kifo cha Belinda kingekuwa funzo kwangu lakini haikuwa hivyo, ni kama niliyekuwa na pepo la ngono, niliendelea na maisha ya ‘kula ujana’ na walimbwende wa kila rika, kila umbo, kila rangi na kadhalika kila nilipopata nafasi ya kufanya hivyo. Niliamini kuwa maisha yangu yasingeweza kuwa ya furaha kama nisingeiridhisha nafsi yangu ilivyotaka.

Nilikula ujana kwa kubanjuka na warembo mbalimbali nikiamini kuwa huo ndiyo ulikuwa muda wangu sahihi wa kuyafurahia maisha yangu maana kuna wakati ungefika nisingeweza tena kubanjuka nao, hata mwanamuziki Samba Mapangala aliwahi kuimba kuwa “Vunja mifupa kama bado una meno…

______

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

11

“Unajua sikuelewi kabisa! Umesababisha tumechelewa basi halafu unafika hapa unaamua kusimama tu na husemi kitu! Sijui tunafanyaje sasa?” sauti yenye hasira ya Eddy ilinizindua kutoka kwenye mawazo yangu.

Na hapo nikakumbuka kuwa tangu nilipofika hapo stendi kuu ya mabasi sikuwa nimefanya jitihada yoyote na muda wote nilikuwa nimesimama mbele ya eddy nikimkodolea macho, ingawa kiuhalisia sikuwa nikimwona kutokana na kutopea kwenye lindi la mawazo ya kumfikiria Belinda. Muda huo vumbi lilikuwa limetulia na hali ya hewa ilirudi katika hali tulivu katika eneo hilo lote.

Baada ya kugutuka toka kwenye lindi la mawazo sikuona kama nilikuwa na namna nyingine ya kufanya ili kusahihisha uzembe wangu uliosababisha tuachwe na basi zaidi ya kutafuta njia mbadala ya kutufikisha tuendako. Lakini kwanza nilimwomba Eddy msamaha kwa yote yaliyotokea na kumuahidi kwamba ningelipia gharama zote ambazo zingejitokeza kwa kuwa ni mimi niliyesababisha tuachwe na basi.

Kwa kuwa Eddy alikuwa mtu mpole na mwenye kusamehe haraka hakusita kunisamehe na kutaka kujua nini nilikuwa nafikiria baada ya basi tulilopaswa kuondoka nalo kutuacha.

Kisha nilimwacha nikashika uelekeo wa kwenye jengo la ghorofa tatu lililokuwa na maandishi makubwa juu ya ‘Guru Malls’, kwa kuwa katika jengo lile kulikuwa na vibanda viwili pembeni yake vimeandikwa ATM, vyenye mashine za kutolea fedha. Kibanda kimoja kilikuwa kwa ajili ya wateja wa benki ya NMB na kingine cha CRDB.

Mara tu nilipofika pale niliwakuta watu wawili na mmojawao alikuwa ndani ya kibanda cha ATM cha NMB akitoa fedha huku mwingine, msichana mmoja alikuwa amesimama peke yake kando ya kibanda cha ATM cha CRDB akionekana kama mtu aliyekata tamaa.

Mwanzoni sikuwa nimemchanganyia vizuri macho wala kumjali kutokana na haraka zangu za kutaka kutoa fedha ili niwahi stendi kukata tiketi, niliingia katika kibanda cha ATM ya benki ya CRBD kisha nikapenyeza kadi yangu ya Visa nikipanga kuchukua fedha ya kutosha kwa ajili ya safari na matumizi mengine ya njiani.

Wakati natoka nilijikuta navutiwa sana na yule msichana aliyekuwa bado amesimama peke yake pale nje ya kibanda cha ATM ya benki ya CRBD huku nikijiuliza ni wapi nilipata kumwona kwani sura yake haikuwa ngeni kabisa machoni mwangu.

Alikuwa msichana mrefu na mweusi mwenye haiba nzuri ya kuvutia. Nywele zake zilikuwa ndefu na alikuwa amezifunika kwa kofia ya kapelo. Alikuwa na sura ndefu kiasi yenye macho makubwa yaliyolegea, pua yake ilikuwa ndefu na mdomo laini wenye kingo pana kiasi zilizopakwa lipstick ya rangi nzuri ya chocolate pamoja na vishimo vidogo mashavuni mwake vilinifanya nibabaike kidogo kwa uzuri wake wakati nilipomtazama.

Muda huo alikuwa amevaa blauzi nyepesi nyekundu iliyoyaficha vyema matiti yake yenye ukubwa wa wastani na juu yake alivaa jaketi zito la bluu la kitambaa cha dengrizi na suruali ya bluu ya kitambaa cha dengrizi iliyombana na kunasa vizuri kwenye kiuno chake chembamba kilichofinywangwa katika namna ya kulifanya umbo lake liweze kuitaabisha kila nafsi ya mwanamume yeyote asiyekuwa na msimamo.

Miguuni alivaa buti ngumu za kike za ngozi na mgongoni alikuwa amebeba begi dogo la mgongoni lenye mifuko mingi yenye vipenyo tofauti.

Nilijiuliza mara mbili kama niliwahi kumwona sehemu yoyote kabla ya hapo na sikutaka kuendelea kuumiza akili yangu, nikamsogelea huku nikimtazama kwa umakini zaidi. Nikamtambua.

“Sharifa!” nilimwita kwa mshangao mkubwa huku nikimtazama kwa udadisi. “Ni wewe au naota?” niliuliza kwa sauti iliyomshtua yule msichana.

Yule msichana alinitazama kwa umakini zaidi na kujikuta akipatwa na mshangao mkubwa. Hakuyaamini macho yake na kujikuta akiachia kinywa wazi baada ya kunitambua. Kila mmoja wetu alishangaa sana kwani hakuna aliyekuwa amemtambua mwingine kabla ya hapo.

“Jason!” Sharifa alimaka kwa mshangao.

“Siamini macho yangu!” nilisema nikiwa bado nashangaa. “Long time no see!” nilimwambia huku nikinyoosha mkono wangu kumsalimia.

Sharifa alinyoosha mkono wake kunisalimia kwa bashasha zote huku akionekana kubabaika kidogo na utanashati wangu, kwa kweli niseme kioo cha kabati langu siku zote hakikuacha kuniridhisha kuwa nilikuwa miongoni mwa wanaume wachache wenye mvuto wa hali ya juu kwa wasichana warembo wa sampuli ya Sharifa.

Nilikutana kwa mara ya kwanza na Sharifa siku nilipokuwa natoka nchini Afrika Kusini nilikokwenda kwa masomo ya chuo kikuu. Sharifa alikuwa anafanya kazi Kiwanja cha Ndege Cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam katika dirisha la ofisi ya uhamiaji pale kiwanjani.

Wakati nawasili nilipanga mstari wa foleni kwenye dirisha la ofisi ya uhamiaji pale uwanjani na zamu yangu ilipofika nilipenyeza pasi yangu ya kusafiria kwenye dirisha dogo la kioo la chumba kilichokuwa kimemuhifadhi msichana mmoja mrembo.

Yule msichana alikuwa amevaa sketi fupi nyeusi yenye miraba myeupe iliyoishia sentimita chache juu ya magoti yake na yenye mpasuo mfupi ulioliacha nusu wazi paja lake, blauzi ya bluu ya mikono mirefu na viatu vyenye vikanyagio virefu vya mchuchumio. Aliipokea pasi yangu ya kusafiria huku akiliachia tabasamu lake maridhawa na kulifanya lizisumbue fikra zangu. Alikuwa anayazingatia vizuri maadili ya kazi yake kwa kutabasamu mbele ya abiria waliowasili jioni hiyo.

Na alipoipokea ile pasi niliiegemeza mikono yangu juu ya sakafu ya kipande kidogo cha ubao mfupi kilichokuwa mbele ya lile dirisha huku nikiinama kidogo ili niweze kuliona vizuri tabasamu lake. Macho yetu yalipogongana kila mmoja alijikuta akitabasamu na hapo nikajikuta nikivutiwa vizuri na uzuri wake.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

12

“Hujambo Miss Tanzania!” nilimtania yule msichana, hata hivyo hakuitikia salamu yangu na badala yake alizidi kutabasamu tu huku akiikagua pasi yangu ya kusafiria.

“Jason Sizya!” nilimsikia yule msichana akilitamka jina langu taratibu pasipo kunitazama.

“Ndiyo mimi, au umewahi kumsikia mtu mwingine akiitwa jina hilo?” nilimuuliza yule msichana huku nikitabasamu.

Yule ofisa wa uhamiaji hakujibu bali alibaki ameduwaa huku macho yake yakifanya kituo kwenye uso wangu.

Sikutaka kumlaumu msichana baada ya kumwona akiduwaa kidogo, sikushtuka kwa kuwa nilifahamu fika kuwa nilikuwa nimependeza sana na pia nilikuwa na mvuto kwenye macho ya wasichana warembo kama yeye.

Suti yangu nyeusi ya bei ya ghali ya single button aina ya Piacenza kutoka Italia, shati langu jeupe la mikono mirefu aina ya Maria Santangelo kutoka Italia, tai nyekundu shingoni aina ya Massimo dutti kutoka Hispania, saa ya mkononi ya madini ya dhahabu aina ya Alpha GMT-Dead Ringer, begi zuri jeusi la safari lenye magurudumu madogo na manukato ya gharama niliyojipulizia vilichangia kuunogesha utanashati wangu.

Alimalizia kugonga mhuri kwenye pasi yangu ya kusafiri kisha akazungusha kiti chake hadi ilipokuwa tarakilishi (computer) yake ya mezani halafu akaanza kubonyeza vitufe fulani kwenye kicharazio (keyboard) na hapo nikajua alikuwa anaingiza taarifa zangu. Mambo yote yalikuwa chapchap kwani alimaliza haraka kuingiza taarifa zangu kwenye tarakilishi yake na hivyo taarifa zangu zikawa zimeidhinishwa rasmi.

Bila kupoteza muda niliipokea pasi yangu ya kusafiria na kuitia mfukoni huku tabasamu langu la kichokozi likiendelea kuweka kituo usoni kwangu na kuzisumbua hisia za yule ofisa uhamiaji.

“Unaitwa nani?” nilimuuliza kwa sauti ya chini kabla sijaondoka ili majirani wasisikie na kunishuku kuwa nilikuwa kwenye harakati za kumtongoza.

Swali langu likaonekana kumfurahisha zaidi, akatabasamu kidogo kiasi cha kuyafanya meno yake meupe yaliyopangika vizuri mdomoni yaonekane na vishimo vidogo vya mashavu yake vikajitokeza.

“Unasema?” aliniuliza kana kwamba hakuwa amelisikia swali langu, na hapo nikagundua kuwa alipenda kusikia nikirudia swali langu.

“Mimi nimekutajia jina langu lakini mbona wewe hujaniambia jina lako?” nilimuuliza huku nikikikagua kifua chake kilichobeba matiti ya wastani na hapo nikahisi mwili wangu ukisisimkwa zaidi.

“Mmh! Hebu wacha uongo wako Jason… wala hukunitajia jina lako bali nimeliona mwenyewe kwenye pasi yako ya kusafiria,” yule msichana alisema kwa sauti laini ya kubembeleza huku akiangua kicheko hafifu.

“Oh! Poa poa… nisamehe kwa hilo hata hivyo ningependa tu kulifahamu jina lako,” nilisema huku nikicheka kidogo.

“Sharifa Mdashi,” yule msichana alisema huku akiendelea kunitazama kwa tabasamu.

“Sharifa! Jina lako tamu kama ulivyo mwenyewe,” nilinong’ona na hapo akashindwa kujizuia na kuachia kicheko.

“Usinichekeshe Jason na mwishowe nikasahau kuwa nipo kazini, umejuaje kama mimi mtamu?” Sharifa aliongea kwa sauti ya chini huku akiendelea kucheka.

“Basi nakuahidi kuwa sitorudia tena kukuchekesha, mrembo wangu,” nilimwambia lakini yeye aliendelea kucheka kisha akaniuliza.

“Kwa hapa Dar unafikia wapi?” swali lake lilinifanya nipumbazike kidogo, nilimtazama kwa kitambo kabla ya kumjibu.

“Sijajua ni wapi nitafikia ila itakuwa ni maeneo ya mjini,” nilimjibu huku nikiilamba midomo yangu.

“Utafikia hotelini?” aliniuliza kwa shauku.

“Bila shaka,” nilimjibu kwa sauti tulivu. “Vipi, ungependa tuonane baadaye?” nilimuuliza huku nikiyatuliza macho yangu kwenye uso wake. Akaonesha kusita sana.

“Basi nipe namba yako ya simu ili baadaye tuwasiliane nitakapokuwa nimepata hoteli pengine tukaonana,” nilimwambia huku nikiendelea kuyatuliza macho yangu kwenye uso wake.

Sharifa alishusha pumzi kisha aliipenyeza kwenye lile tundu la kioo kadi ndogo yenye jina na mawasiliano yake (business card) aliyoitoa toka kwenye mkoba wake mdogo wa begani uliokuwa juu ya meza yake huku akijitahidi kutokuonesha namna yoyote ya kuyavuta macho ya watu waliokuwa wakimtazama. Nikiwa nimeifahamu vizuri hali hiyo nami nikapitisha haraka mkono wangu kuipokea ile kadi na kuitia ndani ya mfuko wa koti langu la suti. Kisha nilishusha pumzi na kumeza funda kubwa la mate.

“Ahsante mrembo,” nilimshukuru kisha nilinyoosha mkono wangu kumpa, na wakati tukipeana mkono wa kuagana nikapitisha kidole changu cha shahada katikati ya kiganja chake kumtekenya.

Kitendo kile kilimfanya ashtuke kidogo na kuruka huku akiutoa haraka mkono wake kutoka kwenye kiganja changu. Sikuishia hapo, nikamkonyeza kidogo kumchombeza lakini nikihakikisha watu wengine hawaoni kitendo kile. Kisha nilikamata begi langu la safari na kuanza kuliburuta.

“Ahsante na wewe Jason, uende salama,” Sharifa aliniambia huku akianza kumhudumia mtu mwingine aliyekuwa nyuma yangu.

Wakati natembea kuelekea nje ya kiwanja cha ndege nilikuwa na kila hakika kuwa macho ya Sharifa yalikuwa yananisindikiza kwa nyuma, hata hivyo sikugeuka kulithibitisha hilo.

Nilipofika nje ya jengo nilipokelewa na dereva mmoja wa teksi, mtu mzima mwenye umri wa miaka hamsini na kitu, mrefu mwembamba na mtu asiye na maneno mengi aliyeonekana kuniona haraka kabla ya wenzake. Yule mzee alinisaidia begi langu huku kisha tukaongozana hadi kwenye teksi yake iliyokuwa imeegeshwa karibu na tulipoifikia alifungua buti la gari na kuliweka lile begi na mimi nikafungua mlango wa nyuma na kuingia.

Alipomaliza kuhifadhi begi langu kule nyuma kwenye buti la gari akaja na kufungua mlango wa dereva, kisha safari ya kuelekea mjini ikaanza wakati ile teksi ilipoanza kuyaacha maegesho ya kiwanjani pale na kuingia Barabara ya Nyerere.

“Unaelekea wapi bosi wangu?” yule dereva wa teksi aliniuliza pasipo kunitazama wakati gari likiingia Barabara ya Nyerere, nikakumbuka kuwa sikuwa nimemwambia wapi naelekea.

“Unaifahamu hoteli yoyote nzuri iliyopo jirani na kituo cha mabasi ya mikoani cha Ubungo?” nilimuuliza.

“Zipo nyingi kama Landmark Hotel, Blue Pearl Hotel, MIC Hotel, Whitemark Hotel, Kagame Hotel, Kibadamo Royal Hotel, Royal Njombe Hotel na kadhalika,” yule dereva aliniambia

“Nipeleke ilipo Landmark Hotel,” nilimwambia yule dereva baada ya kufikiria kidogo.

Ilikuwa ni hoteli ya hadhi yenye nafasi ya kutosha na baada ya kukamilisha taratibu za pale hotelini nilipewa chumba namba 43 kilichokuwa upande wa dirishani orofa ya tatu. Chumba kilikuwa cha kisasa chenye vitu vyote muhimu kama seti moja ya runinga bapa, kitanda kikubwa, jokofu dogo, kabati la nguo la ukutani, simu ya mezani, kiyoyozi, seti mbili za makochi ya sofa na meza ndogo.

Kisha nilimpigia simu Sharifa kumtaarifu kuhusu hoteli na chumba nilichofikia na tukakubaliana kuwa angekuja kunitembelea baada ya kutoka kazini. Na kweli, ilipofika saa 2:15 usiku nikiwa chumbani kwangu nimejipumzisha, nikitazama runinga huku bia baridi ikishuka taratibu kwenye koo langu nilisikia mlango wa chumba changu ukigongwa taratibu.

Niliinuka haraka na kuufungua kidogo huku nikichungulia nje, macho yangu yakagongana na macho ya Sharifa. Nikampisha aingie, Sharifa aliingia akiwa na wasiwasi kidogo. Kwa sekunde kadhaa nilibaki nimeduwaa nikimtazama Sharifa ambaye alikuwa anatazama chini kwa aibu.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

13

Usiku huo Sharifa alikuwa amevaa amevaa gauni fupi jekundu lililoishia juu kidogo ya magoti yake na lilikuwa limeushika vyema mwili wake. Miguuni alivaa viatu virefu vyekundu vya mchuchumio na begani alikuwa ametundika mkoba mzuri mwekundu wa ngozi ambao ulionekana kumgharimu fedha nyingi.

Oh my Gosh! What a beautifull angel…” (Mungu wangu! Kama malaika…) niliwaza huku nikimkazia macho Sharifa. Alikuwa amependeza sana na kuzidi kuichanganya akili yangu.

“Karibu sana Sharifa, nimefurahi kukuona tena,” nilimwambia huku nikilamba midomo yangu kwa matamanio.

“Hata mimi nimefurahi kukutana tena na wewe,” Sharifa alisema huku akiangalia chini kwa aibu, alionekana kuwa hawezi kumtazama mwanamume usoni kwa sekunde tatu mfululizo bila kukwepesha macho yake na kutazama kando kwa jinsi alivyojaa haiba na aibu.

Nilimkaribisha kwenye sofa lililokuwa mle chumbani na mimi nikaenda moja kwa moja kwenye jokofu dogo lililokuwemo mle ndani ambalo lilisheheni vinywaji mbalimbali.

“Mrembo, sijui unatumia kinywaji gani?” niligeuza shingo yangu kumuuliza Sharifa.

“Chochote utakachonichagulia,” Sharifa alisema kwa sauti laini iliyozidi kunipagawisha huku akiachia tabasamu pana.

Niliilamba midomo yangu na kuchukua chupa kubwa ya Konyagi kisha nikammiminia kwenye bilauri na kumpa.

Tulikunywa huku tukiongea na kufahamiana zaidi na mwishowe tukajikuta tukiwa kitandani. Sharifa alikuwa mtundu sana na kwa kutumia mikono yake alipiga magoti na kunipa manjonjo kwa kutumia mdomo wake, jambo lililonifanya nitamani kupiga kelele kwa raha niliyoipata.

Haukupita muda nilijikuta nikiwa katika hali mbaya na sikuweza tena kuvumilia, hivyo tukaingia ulingoni. Ulikuwa ni mpambano mkali na kila mmoja alionesha ufundi na kutaka kuutawala mchezo. Tulibadili kila aina ya mfumo wa uchezaji ili mradi kujihakikishia ushindi mnono mwisho wa mchezo, Sharifa alijitahidi kunionesha mautundu aliyokuwa nayo.

Mimi pia sikuwa nyuma, nilimfanya ahisi kuchanganyikiwa na kutoa miguno kwa raha aliyoisikia huku akihororoja maneno mengi na viapo kuwa hajawahi kupata utamu kama niliokuwa nampa. Hadi dakika tisini za mchezo wote tulikuwa hoi tukitweta kama wakimbiaji wa mbio ndefu…

_____

Mawazo juu ya Sharifa na kukutana kwetu mara ya kwanza yalipita haraka haraka akilini mwangu na kunisisimua mno, nilimtazama Sharifa ambaye sasa alikuwa amesimama mbele yangu kwa matamanio.

“Vipi mbona upo hapa?” nilimuuliza kwa shauku.

“Nilihitaji kuchukua fedha lakini nimesahau kadi ya ATM nyumbani, hapa namsubiri mtu aniletee ila naona anachelewa maana kuna sehemu muhimu sana natakiwa kufika kabla ya saa 1:30 asubuhi hii,” Sharifa alisema huku akionekana kukata tamaa.

“Kwani siku hizi unaishi hapa Tabora?” nilimuuliza tena kwa shauku.

“Yeah, nimehamishiwa Tabora Airport, nina mwaka na nusu sasa,” Sharifa aliniambia na kunifanya nipatwe na mshangao.

“Upo hapa hapa Tabora lakini hatuonani! Au unafungiwa ndani?” nilimuuliza huku nikimtazama kwa umakini.

“Hapana, majukumu tu… halafu mwenzio sasa hivi nimeolewa na mume wangu ndiye meneja wa Kiwanja cha Ndege hapa Tabora,” Sharifa alisema kwa sauti ya chini huku akiangalia pembeni. Na muda huo tukaiona gari ndogo aina ya Toyota Rav 4 nyeusi likija eneo hilo.

“Huyo ndo mume wangu ameniletea kadi ya ATM,” Sharifa aliniambia kwa sauti ya chini kunitahadharisha.

Niliitupia jicho saa yangu ya mkononi na kumuaga kisha nikaondoka haraka kurudi stendi ya mabasi, muda huo ilikuwa inaelekea kutimia saa 12:45 asubuhi.

Jua lilikuwa limeanza kuchomoza ingawaje hali ya hewa katika mji wa Tabora kipindi hicho ilikuwa ya baridi. Pilika za watu zilikuwa zimeanza kushamiri na hivyo kuufanya mji wa Tabora kuanza kuchangamka. Tofauti na hivyo hapakuwa na ziada nyingine kwani miji mingi ya Tanzania kwa namna moja au nyingine ilikuwa inafanana kwa mandhari na maendeleo.

Nilifika pale stendi nikakuta pakiwa pametawaliwa na pilikapilika nyingi za kibinadamu muda huo. Nikamfuata mpiga debe mmoja kijana wa rika langu wa pale stendi ya mabasi niliyekuwa nafahamiana naye, na wakati huo wapiga debe wengine walianza kunizogoma kutaka kujua ni wapi nilikuwa naelekea ili wanikatie tiketi.

Yule mpiga debe nilimweleza hali halisi iliyojitokeza kwamba mimi na kaka yangu Eddy tulikuwa na safari ya kuelekea Kahama na basi la Njamba Express lakini lilikwisha tuacha.

Yule mpiga debe aliniambia kuwa ni vyema tungekata tiketi kwenye basi la MAMBOSASA aina ya Yutong la kisasa lililokuwa linaelekea Singida na kwamba, tukifika Nzega tushuke na hapo ingekuwa rahisi sana kupata mabasi ya kueleka Kahama.

Halikuwa wazo baya, na hivyo akatukatia tiketi mbili za kuelekea Nzega kwa basi la Mambosasa ambalo tuliambiwa kuwa lingeondoka pale Tabora saa 1:30 asubuhi. Hata hivyo hatukuweza kupata tiketi za namba za siti zilizokuwa zinafuatana, badala yake Eddy alipata tiketi yenye kiti nambari 23 na mimi nilikuwa na tiketi ya kiti nambari 29.

Nilipoitupia macho saa yangu ya mkononi nikagundua kuwa ilishatimia saa 12:50 asubuhi, kwa maana hiyo tulikuwa na dakika 40 za kufanya mambo mengine kabla ya safari yetu kuanza. Nilimshauri Eddy kuwa tulipaswa kutafuta mgahawa mzuri eneo lile ambapo tungeweza kupata kifungua kinywa haraka haraka kabla ya kuianza safari yetu.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

14

Muda huo njaa ilikuwa inaniuma sana utadhani nilikuwa na vidonda tumboni. Ili kukabiliana na mning’inio uliosababishwa na pombe kali nilizokunywa nilipanga kutafuta supu nzito kwa kuwa pombe nilizokuwa nimekunywa usiku zilikuwa zinanivuruga tumbo langu na kichwa changu kilinivangavanga sana.

Muda mfupi baadaye tulikuwa ndani ya mgahawa wa Sonerick uliokuwa katika mtaa wa Market jirani na ile stendi ya mabasi ya Tabora. Huo ulikuwa mgahawa mzuri wenye huduma zote muhimu hususan aina mbalimbali ya vyakula na utulivu wa kutosha. Tulipoingia ndani ya mgahawa huo niligundua kuwa kulikuwa na watu wengi asubuhi hiyo waliokuwa hapo kupata huduma ya kifungua kinywa.

Tulitafuta meza moja iliyojitenga kwenye kona moja ya mgahawa ule na kuketi. Sehemu ile tuliyoketi ilituwezesha sote kuona nje ya mgahawa ule kupitia kuta safi za vioo zilizokuwa zikitazamana na barabara iliyotenganisha ule mgahawa na stendi ya mabasi.

Mhudumu mmoja wa mgahawa ule alipokuja kutusikiliza nikamuagiza supu nzito ya ng’ombe yenye saladi na chapati mbili. Eddy yeye aliagiza mchemsho wa kuku wa kienyeji na saladi ya mboga za majani.

Vyakula vile vilipoletwa na mhudumu tukaanza kuvishambulia, na wakati tukipata mlo nikawa na wasaa mzuri wa kulichunguza eneo lile kwa makini. Niliyatembeza macho yangu eneo lile katika namna ya kuzichunguza sura za watu waliokuwemo mle ndani ya mgahawa. Kwa kufanya vile nikagundua kuwa wengi walionekana kuwa wasafiri, kati yao akina mama na watoto walikuwa wachache ukilinganisha na wanaume.

Nikiwa bado ninaendelea na uchunguzi wangu dhidi ya watu waliokuwa eneo lile mara nikajikuta nikivutiwa na msichana mmoja aliyekuwa ameketi peke yake kwenye meza iliyokuwa mbali kidogo na pale kwenye meza yetu. Msichana yule alikuwa akinywa maziwa ya moto na samosa.

Alikuwa msichana mrefu na mweusi mwenye haiba nzuri ya kuvutia. Alikuwa amevaa blauzi nyepesi nyeupe ya mikono mirefu iliyoyaficha vema matiti yake imara madogo na juu yake alikuwa amevaa shati zito jeusi la kitambaa cha dengrizi na chini alivaa sketi fupi nyeusi ya dengrizi na raba nzuri za kike.

Alikuwa na nywele fupi na alikuwa amezifunika kwa kitambaa. Sura yake ilikuwa ndefu kiasi yenye macho makubwa na legevu ya kike, na pua yake ilikuwa ndefu na midomo yake ilikuwa laini yenye kingo pana kiasi. Nilijikuta nikibabaika kidogo kwa uzuri wake wakati nilipomtazama.

Sikutaka kulaza damu, nilinyanyua sahani yangu kubwa iliyokuwa na bakuli la supu ya ng’ombe yenye saladi juu yake na chapati mbili, nikaanza kupiga hatua za haraka kumfuata yule msichana huku nikimwacha Eddy akinishangaa. Wakati nilipomkaribia uso wangu ulianza kutengeneza tabasamu la kirafiki. Msichana yule akageuza shingo yake kuniangalia wakati nilipokuwa nikifika kwenye meza yake, na hapo nikamsalimia huku nikiketi pale mezani.

“Habari za asubuhi, mrembo?” nilimsalimia huku nikiachia tabasamu pana usoni kwangu, yule msichana alinitazama kwa mshangao kidogo kabla ya kulegeza uso wake na kutabasamu

“Nzuri, karibu!” aliitikia salamu yangu na kunikaribisha huku akiniangalia kwa utulivu, na kwa ukaribu ule nikaweza kuutathmini vizuri uzuri wake.

“Ahsante. Na wewe pia unasafiri?” nilimtupia swali yule mrembo huku nikiendelea kutabasamu.

“Hapana! Mimi nilimsindika mtu, ameshaondoka na Njamba Express,” yule msichana alijibu huku akitikisa kichwa chake taratibu.

“Kwani unaishi hapa hapa Mboka? Sehemu gani?” nilimtupia maswali mfululizo yaliyomfanya asite kwanza na kuniangalia usoni katika namna ya kunishangaa kidogo.

“Ndiyo naishi hapa hapa Tabora, naishi Ng’ambo,” alijibu na hapo hapo nikamdaka na swali jingine.

“Ng’ambo sehemu gani?”

“Jirani na nyumba ya Mama Kashindye, karibu na Zimbabwe Lodge.”

“Aisee! Mbona sijawahi kukuona?” nilimuuliza kwa mshangao huku nikijaribu kuvuta picha kama nilishawahi kumwona sehemu.

“Lakini mimi nakufahamu, si unaitwa Jason!” alijibu bila kusita na kunifanya nizidi kushangaa, kabla mshangao wangu haujanitoka akaniwahi kwa swali. “Vipi unasafiri?”

“Ndiyo, naenda Kahama, ingawa ni mara yangu ya kwanza kwenda huko” nilimjibu yule msichana huku nikijitahidi kumwangalia kwa makini lakini sura yake ilikuwa ngeni machoni kwangu.

“Unaenda Kahama kufanya nini?” aliniuliza huku akiendelea kuniangalia usoni.

“Kuna mambo fulani ya kikazi naenda kuyashughulikia,” nilimjibu kwa kujiamini huku uso wangu ukiendelea kutengeneza tabasamu la kirafiki na kwa kufanya hivyo tabasamu langu lilifanikiwa kuziteka hisia zake kwani nilimuona akipumbazika kidogo na utanashati wangu.

Kitendo cha kusema kuwa alikuwa akinifahamu na aliishi eneo la Ng’ambo kilinifanya niwe makini sana katika maneno yangu kwa kujua kuwa alikuwa akiyajua mengi yanayonihusu, ingawa moyoni niliapa kuwa lazima aingie kwenye orodha ya wasichana waliopaswa kushughulikiwa. Pia nilijihisi fahari nilipogundua kuwa watu wengi waliokuwa mle ndani ya mgahawa walikuwa wakigeuza shingo zao kututazama kwa jicho la wivu. Hakika tulipendeza sana na kuonekana kama wapenzi tulioshibana na kuendana vizuri sana.

“Unaondoka na basi gani maana basi la kuelekea Kahama ni Njamba Express na tayari limeshaondoka kitambo!” yule msichana aliniuliza kwa mshangao huku akinikazia macho.

“Naondoka na Mambosasa Trans hadi Nzega kisha nitatafuta gari nyingine ya kutufikisha Kahama.”

Okay! Kahama ni mji mzuri sana unaokua kwa kasi, naufahamu vizuri kwani nimewahi kufika huko mara kadhaa,” yule msichana alisema huku akinyanyua kikombe chake cha maziwa na kunywa.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

15

Nami nikapata nafasi ya kunywa supu huku nikimwangalia kwa jicho la wizi na hapo nikagundua kuwa hata yeye pia alikuwa akiniangalia kwa jicho la wizi na macho yake hayakuhama kwangu badala yake yalikuwa makini kufuatilia kwa karibu kila tukio nililokuwa nikilifanya.

“Wewe unalifahamu jina langu, lakini mimi sijajua mwenzangu unaitwa nani?” nilimuuliza yule mrembo huku nikiendelea kutabasamu.

“Mimi?” yule mrembo aliniuliza kwa kuzuga huku akifahamu fika kuwa nilikuwa naongea na yeye.

“Ndiyo! Si vibaya kama majirani tukifahamiana, endapo hutojali,” niliongea kwa sauti tulivu huku macho yangu yakiwa yameweka kituo usoni kwake.

“Naitwa Ziada…” alinijibu huku akiachia kicheko hafifu kisha akashusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Ziada wa nani?” nilimuuliza ili nijue kama alikuwa ameolewa au la!

“Mmh!” alinionekana kusita huku macho yake yakionesha kutoelewa nilichokuwa nikimaanisha.

“Namaanisha Ziada wa bwana nani, au ni binti wa nani?” nilisema kwa utulivu huku nikimwangalia usoni kujaribu kuyasoma mawazo yake.

“Hafidhi,” alijibu kwa mkato. Nikashindwa kuelewa huyo Hafidhi ni baba yake au mumewe na hivyo ikabidi nitumie njia nyingine kuuliza.

“Vipi umeolewa?” nilimtupia swali jingine baada ya kuona bado sijafanikiwa kupata jibu muafaka nililohitaji. Swali hilo likamfanya asite kidogo na kuinamisha kichwa chake chini, kisha aliinua uso wake kuniangalia na kuachia tabasamu huku akiviminyaminya vidole vya mikono yake.

“Sijaolewa ila nina mchumba,” alinijibu kwa utulivu huku akitabasamu.

“Mchumba wako yuko wapi?” nilimuuliza swali jingine lililomfanya kuniangalia kwa mshangao.

“Yupo, unataka kumwona?” yule msichana aliniuliza huku akiachia tabasamu ambalo liligeuka kuwa kicheko hafifu na kabla sijajibu akanitupia swali, “Wewe je, mbona hutaki kuoa?” swali lake likanifanya nitabasamu kidogo.

“Bado sijabahatika kumpata mwanamke anayenipenda kwa dhati aliye tayari kuolewa,” niliongea kwa utulivu huku nikiyatuliza macho yangu kwenye uso wake.

“Mmh, we muongo! Inawezekanaje kwa mwanaume mzuri kama wewe kusema kuwa bado hujabahatika kumpata anayekupenda! Kwanza umesoma, una maisha mazuri na ninaamini hakuna mwanamke atakayekataa ukimwambia unataka kumuoa labda kama amelogwa!” Ziada alisema kwa mshangao.

“Kweli?” nilimuuliza huku nikiachia kicheko hafifu.

“Wallahi tena!” Ziada alisema huku akipitisha kidole cha shahada shingoni kwake.

Muda huo huo nilimsikia Eddy akiniita na kuniambia kuwa gari letu lilikuwa linaondoka, wakati huo yeye alikuwa anaondoka haraka kuelekea kwenye gari.

Niliitupia jicho saa yangu na kugundua kuwa ilikuwa imetimia saa 1:30 asubuhi. Haraka nikatoa simu yangu ya mkononi na kumpa Ziada nikimtaka aandike namba yake ya simu. Bila ajizi aliandika namba yake kwenye simu yangu na hapo hapo nikaipiga, ikaita kisha nikamwahidi kuwa ningemtafuta baada ya kurudi Tabora.

* * *

Endelea kuufuatilia mkasa huu wa kusisimua, hakika hutoujutia muda wako....
 

Similar Discussions

14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom