Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 46 YA 50.
WARDA ?? Kesho inatakiwa tuanze safari ya kwenda katika kampuni yenye jina lako ili tukamalize ushetani uliopo ndani ya kampuni ile daah natamani nimuone mwanangu ????
AKWELINA ?? Pole sana usijali utamuona mtoto wako kesho tunaenda kumsaidia mtoto wako mimi nahitaji kumsaidia baba yangu kipenzi kakinga nimemkumbuka sana baba yangu .
Walilala baada ya kuzungumza mambo mengi kuhusu safari yao. Yalipofika majira ya saa tisa usiku warda alikuwa bado hajalala alisimama akachukua sindano ya madawa ya kulevya akamchoma akwelina , Akwelina alistuka ghafla akalala tena warda alisimama akautafuta ufunguo kwa muda mrefu kwa bahati nzuri aliupata ufunguo ule akachukua begi lake akaondoka moyoni mwake alisema :-
“” Nisamehe sana akwelina kwa hiki nilichokutendea inabidi nimpelekee ufunguo Julius ili nimpate mtoto wangu ”’
Warda aliondoka alipofika barabarani alipanda gari moja kwa moja hadi gest ( nyumba ya wageni ). Asubuhi palipopambazuka warda alichukua gari akaanza safari kuelekea katika kampuni, Safari ilikuwa ndefu sana warda akiwa ndani ya gari alisikia gari linasimama ghafla dereva wa gari hilo alishuka na kukimbia warda alishindwa kuelewa akatoka kwenye gari alipotazama mbele ya gari alimuona akwelina akiwa ameshika bunduki Warda ali……
Warda alipatwa na mshangao mkali sana kwa kile alichokiona mbele yake alianza kurudi nyuma huku akiwa anatetemeka , Akwelina alimfuata akiwa na hasira zilizojaa moyoni mwake, Warda alipiga magoti akasema :-
WARDA__ Nisamehe akwelina najua nimekosa sana lakini nilifanya kitendo kile kwa ajili ya maisha yako , sikia akwelina kwa hali yeyote pamoja na uwezo ulionao hauwezi kupambana na askari waliopo ndani ya kampuni ile kifupi kuna askari wengi wenye nguvu na uwezo wa juu sana na ndio maana niliamua kuchukua ufunguo huu ili nikamsaidie mtoto wangu nafahamu Julius anahitaji ufunguo huu pekee na ningekueleza haya usinge kubali akwelina binti yangu Mimi ningefanyaje Mimi akwelina ?
AKWELINA ___ Siku zote baba yangu aliniambia kwamba “” Binti yangu akwelina katika maisha yako usimuamini binadamu yeyote hata Mimi japo nimekulea lakini usije ukaniamini kwa sababu nafsi zetu huwa zinabadirika muda wowote ishi maisha yako yote lakini kumbuka binadamu sio wa kumuamini”” Kupitia maneno ya baba niliishi na wewe kwa akili sana na sindano ile niliibadirisha ili bila wewe kujua na ndio maana leo hii unaniona hapa. Sitaki kuzungumza mengi kwanza naomba ufunguo pili utaendesha gari hili hadi katika kampuni hiyo najua kwa uwezo wa mungu nitashinda tu.
Akwelina alichukua ufunguo toka kwa warda kisha akampandisha kwenye gari kwa nguvu , Warda akaendesha gari kuelekea katika kampuni hiyo. Monna alishindwa kuvumilia utumwa katika mikono ya Patrick kutokana na kukosa uhuru, Monna aliishi maisha ya mateso katika mikono ya patrick, siku zote monna aliishi akiwa anajuta kwa vitendo alivyomfanyia kakinga monna alikumbuka siku moja walipokuwa wanaishi kijiji kabla monna hajampokea akwelina, kakinga alimwambia monna :-
“” Mke wangu naomba nikueleze maneno haya kwa sababu nakupenda sana mbali na kukupenda sisi ni yatima wewe na mimi sote hatuna wazazi katika dunia hii, Wewe ndio mama yangu hali kadhalika na Mimi ndio baba yako kwahiyo nakuomba mke wangu nipende kama nilivyo katika maisha yako yote kwani ninaamini katika dunia hii hakuna mwanaume anaekupenda kama Mimi chunga sana tamaa, Dunia hii kuna wanaume wengi lakini wengi wao ni waongo na wenye mapenzi ya dhati kama Mimi tupo wachache sana mke wangu __????
Monna alilia sana kwa kumbukumbu hizo alijuta sana kwa kuruhusu kumpoteza mwanaume aliyekuwa na mapenzi ya dhati kwake , Wakati huo upande wa kakinga alikuwa na mawazo sana kwa kwa kumwamini sana monna , kakinga akiwa katika mawazo hayo alimtazama mtoto wake bilali akamuona bilali analia sana Kakinga alipojaribu kumgusa bilali alimuona bilali anapiga magoti mbele yake bilali akasema :-
BILALI__ Nisamehe sana baba yangu sikutambua kama Julius alikuwa ananidanganya nimekutesa baba yangu daaah najilaumu sana nisamehe sana baba yangu nisamehe baba .
KAKINGA ___ Usijali kijana wangu yote haya sio makosa yako ni mipango yake mungu pekee sisi wanadamu siku zote ni wakosaji mwanangu usijali nimekusamehe .
Bilali alimkumbatia baba yake akiwa anatokwa na machozi kwa wingi sana Kakinga alimtuliza bilali. Baada ya siku mbili Akwelina na warda walikuwa bado wapo njiani akwelina alimuuliza warda baada ya kukaa ndani ya gari kwa muda mrefu :-
AKWELINA __ Bado muda gani tufike ?
WARDA ___ Bado kama siku tatu tufike binti yangu .
AKWELINA __ Ongeza mwendo .
Usiku wa siku hiyo mama mzazi wa akwelina alikuwa ndani ya chumba chenye kutisha , Chumba ambacho kilikuwa na wadudu wengi na chenye kutoa harufu mbaya sana mama wa akwelina aliteswa mno na wadudu waliokuwa ndani ya chumba hicho. Mama wa akwelina akiwa ndani ya mateso hayo kwa mbali alisikia sauti yenye huzuni ya mwanaume ikiomba maji ya kunywa, Mtu huyu aliomba maji kwa muda mrefu ilibidi mama wa akwelina aifute ile sauti alipofika karibu alimuona mtu amechakaa kama chizi amekaa chini akiendelea kuomba maji mama akwelina alipomtazama vizuri alistuka kumuona mtu yule ni STEVEN mume wake kipenzi ….
WARDA ?? Kesho inatakiwa tuanze safari ya kwenda katika kampuni yenye jina lako ili tukamalize ushetani uliopo ndani ya kampuni ile daah natamani nimuone mwanangu ????
AKWELINA ?? Pole sana usijali utamuona mtoto wako kesho tunaenda kumsaidia mtoto wako mimi nahitaji kumsaidia baba yangu kipenzi kakinga nimemkumbuka sana baba yangu .
Walilala baada ya kuzungumza mambo mengi kuhusu safari yao. Yalipofika majira ya saa tisa usiku warda alikuwa bado hajalala alisimama akachukua sindano ya madawa ya kulevya akamchoma akwelina , Akwelina alistuka ghafla akalala tena warda alisimama akautafuta ufunguo kwa muda mrefu kwa bahati nzuri aliupata ufunguo ule akachukua begi lake akaondoka moyoni mwake alisema :-
“” Nisamehe sana akwelina kwa hiki nilichokutendea inabidi nimpelekee ufunguo Julius ili nimpate mtoto wangu ”’
Warda aliondoka alipofika barabarani alipanda gari moja kwa moja hadi gest ( nyumba ya wageni ). Asubuhi palipopambazuka warda alichukua gari akaanza safari kuelekea katika kampuni, Safari ilikuwa ndefu sana warda akiwa ndani ya gari alisikia gari linasimama ghafla dereva wa gari hilo alishuka na kukimbia warda alishindwa kuelewa akatoka kwenye gari alipotazama mbele ya gari alimuona akwelina akiwa ameshika bunduki Warda ali……
Warda alipatwa na mshangao mkali sana kwa kile alichokiona mbele yake alianza kurudi nyuma huku akiwa anatetemeka , Akwelina alimfuata akiwa na hasira zilizojaa moyoni mwake, Warda alipiga magoti akasema :-
WARDA__ Nisamehe akwelina najua nimekosa sana lakini nilifanya kitendo kile kwa ajili ya maisha yako , sikia akwelina kwa hali yeyote pamoja na uwezo ulionao hauwezi kupambana na askari waliopo ndani ya kampuni ile kifupi kuna askari wengi wenye nguvu na uwezo wa juu sana na ndio maana niliamua kuchukua ufunguo huu ili nikamsaidie mtoto wangu nafahamu Julius anahitaji ufunguo huu pekee na ningekueleza haya usinge kubali akwelina binti yangu Mimi ningefanyaje Mimi akwelina ?
AKWELINA ___ Siku zote baba yangu aliniambia kwamba “” Binti yangu akwelina katika maisha yako usimuamini binadamu yeyote hata Mimi japo nimekulea lakini usije ukaniamini kwa sababu nafsi zetu huwa zinabadirika muda wowote ishi maisha yako yote lakini kumbuka binadamu sio wa kumuamini”” Kupitia maneno ya baba niliishi na wewe kwa akili sana na sindano ile niliibadirisha ili bila wewe kujua na ndio maana leo hii unaniona hapa. Sitaki kuzungumza mengi kwanza naomba ufunguo pili utaendesha gari hili hadi katika kampuni hiyo najua kwa uwezo wa mungu nitashinda tu.
Akwelina alichukua ufunguo toka kwa warda kisha akampandisha kwenye gari kwa nguvu , Warda akaendesha gari kuelekea katika kampuni hiyo. Monna alishindwa kuvumilia utumwa katika mikono ya Patrick kutokana na kukosa uhuru, Monna aliishi maisha ya mateso katika mikono ya patrick, siku zote monna aliishi akiwa anajuta kwa vitendo alivyomfanyia kakinga monna alikumbuka siku moja walipokuwa wanaishi kijiji kabla monna hajampokea akwelina, kakinga alimwambia monna :-
“” Mke wangu naomba nikueleze maneno haya kwa sababu nakupenda sana mbali na kukupenda sisi ni yatima wewe na mimi sote hatuna wazazi katika dunia hii, Wewe ndio mama yangu hali kadhalika na Mimi ndio baba yako kwahiyo nakuomba mke wangu nipende kama nilivyo katika maisha yako yote kwani ninaamini katika dunia hii hakuna mwanaume anaekupenda kama Mimi chunga sana tamaa, Dunia hii kuna wanaume wengi lakini wengi wao ni waongo na wenye mapenzi ya dhati kama Mimi tupo wachache sana mke wangu __????
Monna alilia sana kwa kumbukumbu hizo alijuta sana kwa kuruhusu kumpoteza mwanaume aliyekuwa na mapenzi ya dhati kwake , Wakati huo upande wa kakinga alikuwa na mawazo sana kwa kwa kumwamini sana monna , kakinga akiwa katika mawazo hayo alimtazama mtoto wake bilali akamuona bilali analia sana Kakinga alipojaribu kumgusa bilali alimuona bilali anapiga magoti mbele yake bilali akasema :-
BILALI__ Nisamehe sana baba yangu sikutambua kama Julius alikuwa ananidanganya nimekutesa baba yangu daaah najilaumu sana nisamehe sana baba yangu nisamehe baba .
KAKINGA ___ Usijali kijana wangu yote haya sio makosa yako ni mipango yake mungu pekee sisi wanadamu siku zote ni wakosaji mwanangu usijali nimekusamehe .
Bilali alimkumbatia baba yake akiwa anatokwa na machozi kwa wingi sana Kakinga alimtuliza bilali. Baada ya siku mbili Akwelina na warda walikuwa bado wapo njiani akwelina alimuuliza warda baada ya kukaa ndani ya gari kwa muda mrefu :-
AKWELINA __ Bado muda gani tufike ?
WARDA ___ Bado kama siku tatu tufike binti yangu .
AKWELINA __ Ongeza mwendo .
Usiku wa siku hiyo mama mzazi wa akwelina alikuwa ndani ya chumba chenye kutisha , Chumba ambacho kilikuwa na wadudu wengi na chenye kutoa harufu mbaya sana mama wa akwelina aliteswa mno na wadudu waliokuwa ndani ya chumba hicho. Mama wa akwelina akiwa ndani ya mateso hayo kwa mbali alisikia sauti yenye huzuni ya mwanaume ikiomba maji ya kunywa, Mtu huyu aliomba maji kwa muda mrefu ilibidi mama wa akwelina aifute ile sauti alipofika karibu alimuona mtu amechakaa kama chizi amekaa chini akiendelea kuomba maji mama akwelina alipomtazama vizuri alistuka kumuona mtu yule ni STEVEN mume wake kipenzi ….