Simulizi -2 Hours of Memories (Espionage and Science)

singanojr

JF-Expert Member
Sep 24, 2020
1,405
7,864
MASAA MAWILI YA KUMBUKUMBU
2hours of memories.

By
SINGANO JR

Kopi halisi ya kitabu kimeandikwa mwaka 2020 na kupitiwa upya mwaka 2021.

Haki zote zimehifadhiwa

ONYO
Hauruhusiwi kunakili ama kusambaza kitabu hichi bila idhini ya mwandishi
Jatua kali za kisheria zitachukuliwa.

NB:SIMULIZI HII NI YA KUTUNGA HAIHUSIANI NA NA MATUKIO YOYOTE HALISIA

VITABU VINGINE VYA MWANDISHI
MY DREAM MY FAVOURITE
UMOJA NAMBA TISINI NASABA (WARAKA WA RAISI WA MWISHO )
UMOJA NAMBA TISINI NA SABA(BOOK OF ALL NAMES)
BAADA YA ATHARI(MASAA M AWILI YA KUMBUKUMBU)
DREAMSI OF CODES(NDOTO ZA KIKANUNI)

Ni tabia kwa jamii nyingi za Kiafrika kuchukulia baadhi ya matukio katika jamii kama jambo la kawaida pasipo kuzingatia athari zake katika wakati ujao .

Simulizi ya MASAA MAWILI YA KUMBUKUMBU ni simulizi ambayo itakwenda kukuonesha ni kwa jinsi gani kunakuwa na athari pale tunapochukulia kila jambo linalotokea katika jamii kuwa la kawaida. Ungana nami mwandishi SINGANOJR katika simulizi hii ya kusisimua kabisa.

UTANGULIZI
CIA(Central intelligence Agency) ni idara shirikishi ya kiusalama ndani ya taifa la Marekani, inayofanya kazi kwa kukusanya taarifa zote za kiintelijensia ulimwenguni , taarifa zote hizo baada ya kukusanywa na kufanyiwa uchambuzi wa kina zinapelekwa kwa DNI(Director Of National Intelligence)na huyu DNI anapeleka moja kwa moja kwenda kwa raisi.

Ushawahi kujiuliza tofauti kati ya NSA na CIA basi jibu ni kwamba NSA ni kirefu cha NATIONAL SECURITY AGENCY ni moja ya chombo shirikishi cha kiusalama ndani ya serikali ya Marekani kinachohusika na kukusanya taarifa za kiintellijensia kama ilivyo kwa CIA ila utofauti ni kwamba CIA inahusika na ukusanyaji wa taarifa katika mataifa ya nje (International Intelligence) ambazo ni husianishi , au kwa maneno mengine taarifa ambazo zinahusisha Marekani moja kwa moja au kwa njia isio ya moja kwa moja na hawa CIA wanafanya kazi kwa kusambaza mawakala(Agents) kila kona ya dunia , na hawa ndio wanakusanya taarifa hizo na kisha kuzituma makao makuu ya CIA ambayo yapo Lengley, Virginia na hawa mawakala wanaruhusiwa kushirikiana na vyombo vingine vya kiintelijensia katika kukusanya taarifa zao, kwa mfano MOSSAD, M16 na mashirika mengineyo.

Sasa ukija kwenye NSA ni kwamba misheni au kazi ya hii idara ni kuhakikisha kila intelijensia inayotumwa au inayotoka ndani ya CIA au nje ni ya uhakika, na wanahakikisha taarifa kwa kuvunja vunja kwa kutumia matarakishi yenye teknolojia ya hali ya juu kabisa ambayo yana ulinzi mkubwa.

Yaani ndani ya hiki kitengo mambo yote ya udukuzi wa taarifa na mengineyo husianishi na hayo yanafanyika , kwa hio kila taarifa inayofika hapa mara nyingi inahakikiwa na kutafsiriwa na baada ya hapo ndio inafanyiwa maamuzi .

Kwa hio hawa agent wa NSA sio wadhurulaji kama ilivyo kwa CIA agent, hawa kazi zao wanazifanya wakiwa wamejichimbia katika makao makuu yao yaliopo huko Fort Maede ,Meryland.

CIA hii yenyewe ilianzishwa mwezi wa Tisa mwaka 1947 huku NSA ikiundwa mwezi wa kumi na moja mwaka 1962.

NSA imegawanyika katika makundi mawili kutokana na misheni zao , kundi la kwanza linafahamika kwa jina la SID kirefu chake ni Signal Intelligence Directorate halafu kundi la pili ni IAD yaani Information Assurance Directorate , Kundi la kwanza yaani SID kazi yao kubwa ni kutengeneza taarifa zilizokuwa katika mfumo wa mawimbi ya kieletroniki au mfumo ambayo imetumika kama target, yaani kwa mfano mawasiliano, Rada na mifumo yote ya siraha sasa hawa SID ni kuangalia nia na matendo ya taarifa hizo zinahusianaje au zina athari gani kwa Taifa, yaani kwa mfano wanaweza wakapata taarifa yoyote ile kwa kutumia njia ya kimitandao yaani tuchukulie labda unapanga tukio la kigaidi halafu mawasiliano ya mipango unafanya kupitia mitandao , sasa hawa wajuba kazi yao ni kutafuta hizi taarifa.

Sasa baada ya SID kukamilisha kazi yao hawa IAD kazi yao ni kulinda mifuno ya nchi ya kitaarifa .yaani hawa wanazuia wadukuzi kwa kuboresha mifumo yao ya kitaarifa , na unaambiwa mifumo ya ulinzi wa taarifa ya kimarekani ndani ya NSA inakuwa updated kila baada ya sekunde ili kutoruhusu mwanya wowote wa leakage au udukuzi.

CIA yenyewe imegawanyika katika makundi makuu manne kutokana na misheni zao au kazi ndani ya kitengo kuna kundi la kwanza hili linadili na taarifa za site (sehemu husika)duniani kote kundi hili linafahamika kama Directorate of Intelligence, kundi lingine ni National clandestine kazi yake ni kuandaa lakini pia kuongoza misheni zote za siri, Directorate of support hili nalo kazi yake kubwa ni kutoa sapoti kwa makundi yote matatu na mwisho kuna Directorate of Science and Technology humu sasa ndio kuna maswala ya kiteknolojia katika janja zote .

Sasa hizi idara zinafanyake kazi , jibu ni kwamba kuna wakati hawa NSA wanapata intel(Taarifa) kupitia mitandao sasa baada ya kuipata tuchukulie labda intel hio wameipata katika mawasiliano ya Iraq na Pakistan , Sasa unakuta kuna muda wanataka kuihakiki hii taarifa au ifanyiwe kazi ndio hapo sasa watawahitaji CIA , kwa hio kuna muda hii NSA inashirikiana kwa ukaribu zaidi na FBI pamoja na CIA .
Sasa kama nilivyokuonesha muundo huu wa kiintelijensia wa taifa la Marekani turudi sasa kwenye simulizi yetu .

****
Lengley, Virginia CIA HQ, 2021 FEBRUARY 0800Am
Ilianza kama siku tulivu ndani ya makao makuu haya , ambayo yalikuwa na pilika pilika za kiusalama, kwani kila mfanyakazi alionekana kuwa bize kuhakikisha kila mtu anatimiza majukumu yake , kama ilivyokuwa moja ya falsafa kwa wazungu “muda ni mali” basi kwa pilika pilika hizo waliendana na falsafa yao hio .

Basi asubuhi hio ndani ya ofisi ya DCI`s(Director of the Intelligence Agency) alionekana bwana George crispian mkuu wa kitengo cha Directorate of science and Technology akiwa ameambatana na Jane Smith mkuu wa kiitengo cha Directorate of Intelligence , wote asubuhi hio walionekana kuwa na jambo la muhimu la kuripoti kwa mkuu huyo wa CIA bwana Luis Tenet .

Jambo walilokuwa wanazungumzia asubuhi hio ilikuwa ni juu ya misheni iliopewa jina la Dragon X Trail , misheni ambayo ilikuwa ikienda kufanyika nchini Tanzania.

Mbele ya meza hio kubwa iliokuwa imezungukwa na watu wa tatu juu yake kulikuwa na fomu ama bahasha tatu ambapo kila bahasha ilikuwa na taarifa iliokuwa jumuishi juu ya misheni Dragon X, bahasha namba moja ilikuwa na taarifa kutoka NSA , fomu hii au bahasha ilikuwa imebeba taarifa ya picha, hapa nazungumzia picha kama picha, na picha hizo zilikuwa zikizionyesha ubongo wa binadamu , lakini pia zilikuwa zikionyesha pia Screenshot ya jumbe za meseji kupitia mtandao wa Watsapp, jumbe hizo zilikuwa zikitoka kwa Profesa au daktari ndani ya hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwenda kwa mkuu (CEO) wa kampuni ya kitehama ifahamikayo kwa jina la EARTH TECH INC, kampuni iliokuwa na makazi yake ndani ya Taifa la Tanzania mkoani Arusha.

Fomju ya pili ambayo hii sasa haikutoka NSA bali ilikuwa imetoka ndani ya CIA na ilikuwa imewasilishwa kwa DCI na mkuu wa kitengo cha Directorate of intelligence yaani Bi Jane Smith, Fomu hii ilikuwa imejaa nyaraka zenye taarifa kutoka kwa Undercover Agent(wakala) kutoka Tanzania(jina halikutajwa).

Fomu ya tatu hii ilikuwa ipo kwenye meza ya mkuu wa CIA ndani ya fomu hii juu kabisa ya ukurasa wa kwanza kulikuwa na maandishi ya DRAGON X TRAIL MISSION APPROVAL ikiambatana na neno Confidential , fomu hii ilikuwa imetoka kwa Raisi wa USA kupitia ofisi ya DNI kwenda kwa CIA.

Sasa basi ndani ya ofisi watu hao walionekana kujadili jambo , lakini baada ya kama nusu saa hivi , waliongezeka watu wawili watu hawa walikuwa ni wakuu wa vitengo viwili yaanni Directorate of support pamoja na ile ndogo kabisa ya Directorate of clandestine .
Walikuwa wote ni wanaume na baada ya kuungana , walionekana kuwa katika kikao na mwisho wa kikao walionekana walikuwa wakijadili mtu ambae anakwenda kuiongoza misheni hio ya DRAGON X TRAIL.

Lakini kati ya wale watu wawili walioingia ndani ya ofisi hio kwa kuchelewa mmoja alionekana kutoa faili na juu ya hilo faili likuwa na nembo kubwa ya alama ya UMOJA NAMBA TISINI NA SABA yaani U-97 na faili hilo lenyewe likiambatana na neno CONFIDENTIAL
Hii misheni ni nini haswa , kwanini ifanyiwe ndani ya Taifa laTanzania , jibu la jambo hilo linakuja kupitia tukio ambalo ndani ya Taifa lilionekana ni tukio la kawaida kabisa kutokea katika jamiii , lakini kumbe ni jambo ambalo lilikuwa limebeba athari kubwa kwa jamii ..
Tukio hilo linakwenda kwa jina la MASAA MAWILI YA KUMBUKUMBU ni tukio la kusisimua lililotengeneza sababu ya kuundwa kwa misheni iliofahamika kwa jina la DRAGON X TRAIL.

Lakini ni tukio ambalo lilipelekea kufichuka kwa siri kuu ya UMOJA NAMBA TISINI NA SABA siri ya kitabu cha BOOK OF ALL NAMES
Huo ni utangulizi wa kitabu changu kinacho enda kwa jina la MASAA MAWILI YA KUMBUKUMBU.

Sasa kwa wewe ambae ushakwisha kusoma UMOJA NAMBA TISINI NA SABA (waraka wa raisi kabla ya kifo ) basi nakuomba usome na tukio lililotokea katika kitabu cha MASAA MAWILI YA KUMBUKUMBU ili upate maana halisi ya ya code name U-97 je ni nini maana halisi ya hilo neno , je kuna umoja huo kwenye jamii au duniani kwa ujumla wake basi usisite kusoma.

Mambo makuu mawili utakayo yapata kuyajua katika kitabu hiki ni pamoja na jinsi gani mashirika makubwa ya kimitandao yanavyokagua mawasiliano ya wateja wao wote dunia nzima .

Utapata kujua nini nini kiligunduliwa katika BLUE BOOK project, pia utakuja kugudnua namna projekti hio ilivyo changia uundwaji wa project ya TOP ON FILE project iliokuwa ipo chini ya STAR LABS pamoja na IBM .

Je, unataka kujua ni nini kilichonyuma ya DRAGON X TRAIL MISSION hakikisha haukosi kusoma

NB kitabu hiki kwa sasa kinapatikana kwa njia ya softcopy (PDF,DOC and EPUB) kina season 1&2 kila season ina vipande 50 kila episode inapatikana kwa bei ya ofa 4000 tu mpaka kesho kutwa ambappo itapatikana kwa kila season 6000
Lipia kupitia namba 0687151346 jina ISSAI SINGANO ukishalipia nitumie

SEHEMU YA 01
Ni siku ya ijumaa , siku ambayo Ilikuwa imetawalia na jua kali sana ndani ya wilaya ya Korogwe mkoa wa Tanga ,wilaya hii ilikuwa imetawalia na eneo la tambarare kwa ukubwa wake , licha ya baadhi ya maeneo kuwa na misitu na baadhi ya miti ,lakini kwa maeneo ya mjini hayakuwa na miti mingi sana masalani katika pembe ya barabara kuu iliokuwa ikiunganisha mkoa wa moshi –Arusha na Pwani – Dar es salaam .

Wilaya ya korogwe ni wilaya ya pili kwa kuwa na maendeleo ya wastani , ukiachana na wilaya ya Tanga mjini ambako ndio makao makuu ya mkoa .

Pembezoni mwa barabara hiyo iliyokuwa ikiunganisha mkoa wa Tanga ,Arusha na Dar es salaam alionekana kijana mmoja akiwa anatembea kwa unyonge sana huku akionekana akiwa amechoka sana ukizingatia na jua lilivyokuwa kali ilikuwa ni zaidi ya taabu mbele ya barabara hio huku mgongoni akiwa amebeba mfuko mmoja mdogo ambao ulionekana kuwa mifuko ya zamani sana , mifuko hii ilikuwa ukiubeba mgongoni huku ukiwa na kamba ambazo zilitumika kama mikanda ya begi na ndani ya mfuko huo alionekana akiwa amebeba nguo .

Licha ya kijana huyu kuonekana akitembea barabarani lakini hata mavazi yake yaliwakilisha kile kilichokuwa kikiendelea katika maisha yake , alitembea kwa umbali mrefu kidogo mpaka akafika sehemu moja iitwayo Mwembeni sehemu ambayo ndio anaingia mjini Korogwe.

"Hapa sina hata hela ila lazima nifike jijini Dar kwa njia yoyote ile , pia nitakula nitashiba ngoja uone, kwanza nikale kwenye kibanda kile mgahawani pale”.

Aliwaza yule kijana huku akikisogelea kibanda kwa kujiamini kabisa na wakati huo hakuwa hata na shilingi mia mfukoni zaidi ya mfuko wake wa kubeba mgongoni.

Baada ya kufika ndani ya mgahawa ule alitafuta meza ambayo kuna mzee mmoja nae alikuwa akipata chakula .
"Mzee shikamoo!"
"Marhaba kijana" Aliitika huku akiendelea kula na hakutaka maongezi zaidi kwani kwa muonekano wa yule kijana aliona kabisa kaja eneo lile kwa ajili ya kumuomba hela ili na yeye apate chakula ,kwani mara nyingi alizoea kuona vijana wengi wenye tabia hiyo kuja sehemu ile na kuomba hela.

“Karibu kaka nikuletee chakula gani?"Aliongea muhudumu.
“Weka msosi kama anao kula huyu mzee " Aliongea vile makusudi maana aliona huyu mzee kama alikuwa akidhania kuwa atamuomba hela kwa hio aliagiza vile ili kumkomoa.

“Kaka chakula chake hicho ni elfu kumi utaweza kulipa?"
“We muhudumu mteja si kakuagiza ,we lete kama alicho omba unahoji maswali ya nini" Aliongea yule mzee huku akitaka kuona kweli kama atamudu bei ya chakula.

Ndani ya muda mfupi muhudumu aliweka chakula kwenye meza na jamaa huyu bila ya kupoteza muda aliamka na kunawa mikono na kuanza kula msosi huu kwa mbwembwe zote mpaka akamaliza , huku yule mzee aliekuwa akila chakula bado alikuwepo pale pale kwenye ile meza akichati na simu yake kubwa na yote alifanya vile kutaka kuona kama huyu kijana ataweza kulipia kile chakula , maana ukizingatia jinsi mavazi yake yalivyo chanika chanika halafu ale chakula cha zaidi ya elfu kumi ilikuwa nikichekesho na alitaka kuona mwisho wake.

Kijana baada ya kumaliza kula chakula kile aliagiza maji ya buku ya uhai na kisha akanywa kidogo na pale pale yule muhudumu alikuja kwa lengo la kuchukua hela .

Lakini kabla hajakaribia meza waliokuwepo aliitwa na mteja mwingine kwa ajili ya kuchukua hela . "Mzee " Aliita yule kijana na yule mzee akaangalia na kuitika lakini cha kushangaza yule kijana alifumba jicho moja kwa sekunde mbili na kisha kuliachia .na bila ya kuongea chochote alinyanyuka na kuchukua maji yake na kutoka ndani ya ule mgahawa lakini wakati anakaribia kutoka mara yule muhudumu alimwita.

"Wee kaka mbona hujalipia na unataka kuondoka?"
" Nishamwachia yule mzee hela na inayobaki tumia mrembo ee"Basi yule dada alimfuata yule mzee na kumuomba ampe hela alioachiwa na kumbuka kijana hakutoa hela yoyote pale zaidi ya kula na kuondoka.

"Anhaa kweli kaniachia elfu ishirini na inayobaki kasema.. inayobaki tumia mremboo" Aliongea yule mzee huku akitoa walleti kitu kilichomshangaza yule muhudumu maana hela katoa kwenye walleti lakini hakutaka kujihangaisha sana zaidi ya kupokea na kufurahia kwani yule kijana alikuwa ametumia elfu kumi na moja kwa hio ilio baki ilikuwa elfu tisa .

Yule mzee baada ya masaa mawili kupita alijikuta akiwa amekaa pale pale hotelini lakini ni kama mtu alierudiwa na kumbukumbu.
"Duuh! hivi yule kijana alilipa ?" alijiuliza huku akinyanyuka na kumfata yule muhudumu na kumuuliza. " Ndio alilipa mbona tena hela alikuachia wewe au ushasahau na kanipa mpaka chenchi".

"Unasema hela nimetoa mimi?" Aliuliza yule mzee kwa mshangao "Mhmh ndio mzee tena hela si umetoa kwenye walleti yako wewe?"
Yule mzee bila kujiuliza alitoa waleti yake na kuanza kuhesabu hela zake lakini alijikuta akipagawa maana ni kweli kuna upungufu wa shiringi elfu ishirini.

"Umesema ameondoka saa ngapi?"
"Muda mrefu kama masaa mawili yaliopita "
"Duuh! ..basi asante kwa chakula " Alisema yule mzee huku akijikuta akipata mfadhaiko kwani hela yake kamlipia yule kijana huku akiwa hana kumbukumbu ya aina yoyote ile .

"Daah! leo nimeumbuka yule dogo lazima atakuwa mchawi yule sio bure , ila siku nitamkamata tuu hela yangu haiendi buree , ila atakuwa yupo vizuri maana kama ni chuma ulete asingeniweza nimezindikwa vya kutosha na pia hirizi yangu ipo kiunoni iweje ameniweza?"

Yule mzee alikubaliana na yalio mtokeo na kuondoka zake ...... yule kijana ni nani ? swali hilo likabaki kwenye kichwa chake.

**********
1995 -DAR ES SALAAM 1800hours PM
Katika moja ya maeneo ambayo yanasifika kama sehemu(Neighbourhood) ambazo matajiri wengi huishi ndani ya jiji la Dar es salaam ni Masaki na Osterbay , na hili sio kwa hapa Tanzania tu lakini pia kwenye nchi nyingi na majiji makubwa huwa na maeneo ambayo yamejitenga kama maeneo ambayo wanaishi walio nazo kwa mfano tu China kuna Central park hii ni moja ya sehemu ambayo inaaminika matajiri wengi wanaishi , kwa hio sio jambo la kushangaza sana ,nijambo la kawaida kwa watu kuonesha uwezo wao wa kipesa pale wanapokuwa nazo , yapo maeneo mengi ndani ya majiji tofauti makubwa duniani ambayo matajiri wengi wamejitenga na watu wa vipato vya chini.

Ndani ya eneo hili la Masaki wakati familia nyingi zikiwa ndani ya mageti yao katika maeneo haya tulivu ,kuna familia moja ambayo haina muda mrefu tangu ihamie maeneo hayo alionekana dada mmoja ambae alikuwa akisukumiwa nje na mlinzi wa nyumba hio baada ya kupata maelezo kutoka kwa bosi wake huyo ambaye alifunga ndoa hivi karibuni na kuhamia maeneo hayo ya ushuani, kwani baba yake alikuwa tajiri mkubwa aliekuwa akihusika na biashara za usafirishaji wa mizigo (Cargo Transit And Swift Logistic Company) kampuni ambayo ilikuwa ikisifika sana kwa usafirishaji wa mizigo ambayo makao yake makuu yalikuwa maeneo ya mikocheni nyuma kidogo kabla hujakaribia jengo la Airtel ambalo kwa miaka hio ya tisini jengo hilo halikuwepo.

Na moja ya wafanyakazi wa kampuni hio ni kijana Samiri ambae alikuwa ndio CEO(Mkurugenzi mtendaji ) wa kampuni hio huku baba yake akiwa mwenyekiti wa bodi ya kampuni hio kubwa Africa Mashariki.

Tukirudi huku Masaki baada ya mwanadada yule kufukuzwa alijikuta akilia sana huku akianza kukumbuka siku alio kutana na Samir katika biashara zake za uchangudoa lakini kutokana na matakwa ya mteja wake kutotumia kondomu basi alijikuta akibeba ujauzito bila mategemeo .lakini kama ilivyokuwa kwa wadada wengi wapatapo ujauzito wa kutotarajia basi huwa wanachukua maamuzi ya kutoa mimba hizo na wazo hilo lilimjia Irene mwanadada ambae alipata ujauzito kutoka kwa Samir lakini kilicho muhuzunisha na kuchukua maamuzi ya kuicha mimba ikue ni baada ya kuambiwa na daktari wakati akitaka kutoa mimba hio kwamba kama atatoa mimba hio kuna aslimia tisini za kutoweza kupata ujauzito tena na asilimia kumi za kupata ujauzito tena ndipo daktari alipo mshauri kwenda kujifikiria kwanza kama atoe ujauzito huo asipate mtoto maisha yake yote ama auche ..ulikuwa ni uchaguzi mgumu sana kwake ukizingatia na hali ya maisha alio kuwa nayo, alijikuta akilia sana usiku mpaka alipo kuja kuamka na kupata wazo la kumtafuta mtu alie mpa ujauito huo kuona kwamba ni kipi atamwambia , kama angeweza kukubali uja uzito huo.japo alikuwa na uhakika mdogo sana wa kukubaliwa na huyo mwanaume alie mjua kwa jina la Samir kwani alijulikana sana kwa utajiri alio kuwa nao pamoja nakupenda maisha fulani ya kuonekana pamoja na kununua dada poa kila anapojisikia .

Irene hakupata shida kupajua sehemu anayoishi Samir alifanikiwa kufika nyumbni hapo na aliruhusiwa na kuingia ndani na kumkuta Samir na mke wake shani ambae licha ya kuwa wachumba wa muda mrefu ndio walioana siku chache tuu zilizo pita ,baada ya Irene kumkuta Samir, Samir kwanza alishtuka kwani anamkumbika vizuri Irene japo hakumfahamu jina ila alimkumbuka kwa kumnunua na kulala nae hotelini.

"Samahanini jamani kwa kuwaingilia na jioni hii " Aliongea Irene
"Hakuna shaka karibu" Walimkaribisha Irene aliekuwa akiendelea kushangaa mandhari ya kuvutia ya nyumba hio na kujisemea kuwa kuna watu wanaishi sehemu nzuri sana.
" Ninamazungumzo na wewe kaka "
" Okey hapa au nje ya hapa " Aliongea Samir
"Hata hapo nje tafadhari" Basi Samir alitoka na irene mpaka nje kwa ajili ya mazungumzo huku mke wake japo alitamani kusikia kilichokuwa kinakwenda kuongelewa ila alijikuta akikubaliana na mume wakekuongea na Huyo mwanamke.
" Nadhani unanikumbuka vizuri ?" Alianzisha maongezi Irene
" Ndio sura yako inakuja kuja hivi "
"Sitaki kwenda mkato mkato nimekuja sio kwa ajili ya kukubebesha hili swala ila nimekuja unipe ushauri na kama utapata moyo wa kunisaidia maana hapa nilipo nimwchanganyikiwa sijui cha kufanya ."
"Mbona unanitisha dada jambo gani hilo?"
"Siku ile ulivyokuja kupata huduma kwangu kama unakumbuka ulikataa kutumia kondomu na mimi sikutarajia lakini nimepata ujauzito wako"

"Whaat!!!.., wewe dada una kichaa?" Aliongea Samir kwa mpayuko ulio sababisha hata mke wake alie kuwepo sebuleni kuja kuangalia kinacho endelea .
"Mume wangu nini tena?"
"Shania hakuna kitu mke wangu kuna jambo limenishangaza hapa”
" Mhmh haya " Shania alirudi ndani na kuwaachaa
Lakini samir pale pale alienda mpaka getini na kumuita mlinzi aitwae Juma
"Wewe juma unaruhusu je watu wa ajabu ajabu wanaingia nyumbni kwangu " alisahau kama yeye mwenyewe ndo alimruhusu”.
" Bosi samahani sitorudia tena " Juma alijibu na kuomba msamaha japo hakufanya kosa
" Sasa sikia nenda kamtoe pale kimya kimya mke wangu asijue haraka sana , usilete watu vicha vichaa ndani kwangu"
Juma bila kupinga oda ya bosi wake alikwenda kumburuza Irene kimya kimya na kumsukumia nje ya getii"
Samir alijikuta akipata hasira na wasi wasi juu ya jambo lile haraka haraka aliingia chumbani kwake na kuvuta droo na kutoa kiasi cha pesa huku mke wake akimuangalia tu
" Mume wangu unapeleka wapi hizo pesa ?"

"Subiri nakuja kukuhadithia mke wangu “ huku akitokà nje
" Juma yuko wapi?"
“Nishamtoa nje "
"Sikia hebu nifungulie haraka haraka " Juma alifungua na na Samir akatoka nje na bahati ni kwamba Irene hakwenda mbali.
"Sikia we kahaba naomba usije ukakanyaga nyumbani kwangu kuanzia leo sitaki kujua unacho ongea ni cha kweli ama uongo , shika hii pesa utajua mwenyewe cha kufanya " Aliongea Samir na kumtupia zile hela chini.

"Irene alijikuta akilia sana ila upande mwingine alipata nafuu baada ya kupata zile hela kwani pia haikuwa nia ya yeye kwenda kukubaliwa kwa mimba ile ila alitaka tu kubahatisha kama anacheza mchezowa bahati nasibu,maana ni naninagekubali mimba ya mwanamke anajiuza.

“Samahani sana kaka kwa kusababishia mawazo na kukukosesha amani lakini jisikie huru kabisa sikuja kukuambia tulee hii mimba ila nimekuja unipe msaada wa kimawazo , lakini nakuhakikishia hii mimba nitaelea lakini hakika mwanangu hatokuja kujua kama wewe ndio baba yake japo huo ndo ukweli kama hii mimba ni yako naomba usahau kuhusu hili nitaitumia hii pesa kama moja ya matumizi kwa mwanao atakapo zaliwa kwaheri" Aliongea Irene maneno hayo na akaondoka zake huku Samir nae baada ya kumwangalia mwanadada huyo mpaka alipo yokomea ndipo akaondoka zake.

SEHEMU YA 02
Irene baada ya kurudi kwenye chumba chake alicho panga maeneo ya Sinza alifungua zile hela na kuanza kuzihesabu na kuzikuta ni milioni mbili na hamsini kwanza alishukuru sana kwa hela ile na kuona ni msaada mkubwa sana ambao amepata , ndipo alipoamua kuacha biashara yake ya kujiuza na kuanzisha biashara ya kuuza mkaa katika eneo la Tegeta mbuyumi biashara ambayo ili muwezesha kujipatia kipato huku kiasi kidogo alicho kuwa akipata akitunza benki kwa ajili ya mwanae atakae jifungua ,basi hatimae baada ya miezi tisa alifanikiwa kujifungua mtoto wa kiume aliempa jina la Peter.

Mtoto Peter maendeleo yake ya ukuaji hayakuwa mabaya na hatimae alifikisha umri wa miaka sita alianzishwa shule darasa la kwanza, siku zilizidi kusonga hatimae Peter alifikisha darasa la saba ndipo mama yake Irene alipopata ajali ya kugongwa na gari ilikuwa ni ajali moja yakusikitisha sana kwani alifia hapo hapo lakini kilicho washangaza wengi ni mazingira halisi ya ajali hio kwani ni kama mgongaji alidhamiria kumgonga mama Peter kwani baada ya ajali hio kutokea gari halikusimama na wala namba za gari hakuna alieweza kuziona .
Ilikuwa ni ajali mbaya sana ajali ambayo ilimfanya Peter kuwa yatima kwani mama yake alishawahi kumwambia kuwa baba yake alikwisha kufariki , mtoto Peter alilia sana na kuhuzunika kumpoteza mama yake hasa kwa wakati huo ambao bado alikuwa bado akimuhitaji sana kwani ndo kwanza alikuwa darasa la saba , majirani walimuonea sana huruma Peter , walijitahidi sana kumfariji lakini kumfariji huko hakukuzaa matunda ,lakini haikuwa na jinsi kwani tayar mama amekwisha kufariki.

Basi baada ya siku chache Irene au Mama Peter alipumzishwa katika makabuli ya Sinza.
Basi maisha kwa mtoto Peter yaliendelea na uzuri ni kwamba mama yake alikuwa alimuwekea pesa benki basi Peter hakupata shida sana ya matumizi na baada ya miezi kadhaa kupita Peter alifanikiwa kumaliza darasa la saba ndipo alipo anza kuendeleza biashara ya mama yake ya uuzaji mkaa huku mara nyingi pesa alio kuwa akiipata aliitunza kwani bado alikuwa na safari ndefu ya kusoma na kutokana na msaada wa majirani zake basi walimfanya Peter asijisikie kuwa mpweke sana.

Basi baada ya miezi kadhaa matokeo ya kidato cha kwanza yalitoka huku Peter akiongoza katika somo la hisabati na sayansi kwa mkoa wa Dar es salaam kwa kupata A kwa kila somo ilikuwa ni habari njema sana kwa kijana Peter na kwa wale ambao walikuwa wakimpenda, lakini bahati pia ikamwangukia Peter kwani wanafunzi wote ambao walifanya vizuri katika masomo ya sayansi walipata ufadhili chini ya kampuni ya R&J foundation kwa kuwalipia ada wanafunzi hao pamona na matumizi kwa kipindi chote cha masomo, na moja ya wanafunzi walio pata ufadhili wa masomo hayo alikuwa ni Peter huku sheria ya mkataba huo ni kusomea katika shule za serikari ama za jeshi kwa shule yoyote ile yenye bweni.

Kwa upande wa Peter baada ya kwenda ofisini kwa ajili ya kukamilisha usajili wa ufadhili huo alikutana na mwanamama mrembo ambae japo umri umeenda lakini alionekana kama kijana kwa uzuri wake pamoja na mavazi aliovaa yalikuwa ya bei ghari.
Basi Peter alikaribishwa vizuri na kujieleza pamoja na historia yake , na baada ya hapo alichagua shule ya Makongo sekondary lakini akikataa kukaa hostel kama sheria za ufadhili huo.

“Kukaa hostel za shule ama kutokaa bado hakutakuwa na mantiki kama tui mwanafunzi mnae mfadhili hatafanya vizuri katika masomo yake , mimi naona nitafanya vizuri zaidi kama nitakaa nyumbni na kwenda shuleni asubuhi"

“Okey ni sawa lakini lazima uelewe kwamba kama itatokea umefanya vibaya katika masomo yako basi tutaacha kukufadhili "
" Hakuna shida " Peter alifurahi sana na hatimae mwezi wa kwanza alianza kusoma katika shule hio ya Makongo shule ya jeshi iliopo kati ya Mbezi beach na Mwenge ndani ya eneo la Lugalo. .
********
Tukirudi kwa kijana tuliemuona Korogwe baada ya kutoka mgahawani pale alichukua barabara kuu huku akidhamiria kutafuta stendi ya mabasi ,kwani alipo uliza aliambiwa stendi utaipata mbele huko, ndipo alipoamua kunyoosha pasipo kujali jua ambalo lilikuwa likimuwakia alitembea huku akipoozea na maji alio chukua pale mgahawani

"Japo Mungu hakunijaalia uwezo wa akili lakini alichonipa namshukuru Asante Mungu nimeshiba"Aliongea huku akizidi kusonga mbele mpaka akafikia eneo moja liitwalo Majengo ndipo alipo msimamisha mtu na kuuliza stendi ya mabasi .. baada ya kuelekezwa alifuata barabara hio hatimae aliingia stendi, lakini wakati anatembea aalikuwa akiyafikiria mausia alio kuwa akipewa na mama yake kabla hajafariki.

"Mwanangu najua una uwezo wa kumpumbaza mtu kwa muda mfupi na kumfanya afanye kile ukitakacho lakini isiwe chanzo cha wewe kuanza kuwadhulumu watu mali zao na kufanya uhalifu , hakikisha unajipatia kipato kilicho halali , shida zako zisikufanye ukiuke sheria za ulimwengu kumbuka hiko ulicho jaaljwa na Mungu ni kama zawadi ila sio siraha ya kuwachapia watu "

Hayo ni maneno ambayo kijana huyu ambaye bado hatujapata kumjua jina akiyakumbuka maneno ambayo aliusiwa na mama yake kipenzi kabla ya kupatwa na umauti.

"Mama nisamehe sana ila sina jinsi lazima ni utumie uwezo wangu nilio nao ili nifikishe Dar kutafuta maisha."
Aliongea kijana huyu na wakati huo akiingia stendi hapo,moja kwa moja aliinyoosha kwa wakata tiketi na kudhamiria kukata tiketi lakini wakati huo hakua hata na shilingi mia mfukoni zaidi ya mavazi yake yaliochakaa huku baadhi ya sehemu zilionekana zimechanika.
"Dogo unaelekea Dar?, njoo nikukatie tiketi chapu gari linafika sasa hivi" Aliongea moja ya watu wanao kata tiketi kama unavyojua mbwembwe zao , lakini kilicho mfurahisha kijana huyu ni mkataji tiketi yule kutombagua kutokana na mavazi yake.
"Dogo unaitwa nani?
"Unasema?"
"Jina lako nani?"
"Naitwa bahati masumbuko"
" Dogo kweli wewe kwa muonekano wako masumbuko kakuzaa kwa bahati "
"Hata mimi naona broo”
"Poa toa hela chapu tiketi yako hii hapa na gari lile ndo linaingia"
"Broo.." Aliita kijana huyu ambae jina lake ni Bahati masumbuko na pale pale akachezesha jicho lake kwa staili ya ajabu kama vile anakukonyeza

"Dogo shika tiketi yako nilisahau kumbe ulianza kutoa pesa"Aliongea yule jamaa huku Bahati akipokea tiketi yake na kwenda kupanda gari.

"Nisamehe sana broo mimi sio mchawi ila inanibidi kufika Dar kutafuta maisha nitakuja kukulipa" Alijiongelesha mwenyewe Bahati huku akiingia ndani ya basi.

Baada ya Masaa mawili yule mkata tiketi alijikuta kama anatoka usingizini kwani ndo anakumbuka kuwa yule dogo hakutoa pesa na gari ishaondoka

"Yule dogo nilimuachia achia je au mchawi , ngoja nimpigie Ayubu achukue hela aache uhuni( Ayubu ni konda) au alilinipa sikumbuki” Huku akitoa simu na kuanza kupiga .
Simu ilimshtua Ayubu ambae alikuwa bize akiangalia movie ya Majuto kwenye Tv ya gari aliichomoa na kuweka sikioni baada ya kuona ni rafiki yake
"Oya mzee kuna dogo sijui nimemuachia achia vpe nimemkatia tiketi lakini hela hajatoa anaitwa Bahati Masumbuko hebu fanya mpango uichukue"
"Una uhakika hajatoa au umesahau. Kama ametoa?"
"Nina uhakika ila sikumbuki vizuri"
"Sasa una uhakika halafu hukumbuki vizur jibu sahihi ni lipi ,ndo maana nakwambia uache kuvuta bangi mchana wewe"
"Oya Ayubu hebu muulize tuu kama amenipa au hajanipa? "
"Poa ngoja nimcheki"

Konda wala alikuwa anamkumbuka vizuri bahati kutokana na muonekano wake wa mavazi halafu isitoshe kapanda gari ya Luxury
"Dogo vpe eti ulipo kata tiketi ulitoa hela?"

"Wewe konda na wewe sasa kaingia je humu kama hajatoa pesa au kisa anamavazi yalio chakaa ndio kinachokutia wasi wasi?" Alijibu mama mmoja aliekuwa akionekana na rafudhi ya kitanga Tanga .
"Mama mimi nimeuliza tu maana aliempa tiketi kanambia ana uhakika ila hakumbuki vizuri kama alitoa hela"
"Sasa ushasema ana uhakika na hakumbuki vizuri jibu ni kwamba kijana ametoa pesa mfyuu..".
"Wewe dogo ulitoa hela "

" Nilitoa ndio" Alijibu Bahati Masumbuko na kumfanya konda atulie nakurudi zake mbele huku safari ikiendelea
"Hapa nikifika kwanza niitafute milimani city niingie, kisha niitafute Kariakoo ndio mambo mengine yaendelee"Aliwaza Bahati Masumbuko huku akijikuta anafurahi kwani ndoto zake ya kulioana jiji la Dar muda si mrefu zinaenda kutimia hayo yalikuwa ndio mawazo ya n bwana Masumbuko hakuwaza nani atampokea atakaa kwa nani au atalala wapi na kuishi vipi.

Ndani ya muda wa saa moja kuelekea na nusu ndio muda ambao basi alilo panda Bahati Masumbuko ndio lilikuwa likiingia stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani yaani Ubungo basi ilijiegesha kwenye eneo lake na kuruhusu abiria watoke kwani walikuwa wamefika .
Bahati nae aliamshwa kutoka usingizini kwani alikuwa amesinzia tokea muda mrefu na hata gari lilivyo fika hakujua limefika mda gani
"Wewe amka gari lishafika Ubungo" Aliongea mama aliekuwa amekaa pembeni yake huku akichukua begi lake na kutoka nje .
Bahati alijikuta akianza kushangaa baada ya kuona upande wa pili taa zinawaka kwenye jengo lililopo hapo ubungo , alichukua kijimfuko chake na kutoka haraka mpaka nje ya basi na kuanza kuendelea kushangaa.

******
Peter alianza shule kidato cha kwanza na siku kadri zilivyokuwa zikisogea alijikuta akifahamika haraka sana kutokana na uwezo wake wa akili darasani huku akionyesha ubingwa wake zaidi katika somo la .Mathematics(hesabu) na komputa(Tarakishi), ndani ya miaka miwili tu Peter alikuwa moto sana kwenye somo la komputa na hisabati kwani alikuwa ameshajua kila kitu kuhusu komputa
"Vipi Peter "
"Safi niambie kaka"

"Vipi baadae nataka nije getoni kwako unisaidie kunielekeza maswala ya Excel na Publisher yananizingua kinoma " Aliongea jamaa mmoja afahamikae kwa jina la John ambae yeye alikuwa kidato cha nne na Peter cha pili.
"Poa hakuna shida wewe njoo " Alimjibu huku wakitembea mpaka walipo fikia eneo la Smart area .eneo ambalo hapo shuleni hauruhusiwi kutembea zaidi ya kukimbia.

Peter wakati buo yeye alikuwa akiishi Mbezi Beach ambako alipangishiwa Apartment(nyumba) na wafadhili wake baada ya Peter kuonyesha uwezo mkubwa darasani, japo Peter alikuwa akilipiwa kila kitu lakini hakuacha kufanya biashara yake ya mkaa ambauo ilikuwa ni kama urithi kutoka kwa mama yake Irene. Na kila pesa aliokuwa akiptata kwenye biashara hio nusu alikuwa akiweka benki na nusu alikuwa akitumia kwenye matumizi yake madogo madogo

"Baada ya muda wa jioni kukaribia John alikuja nyumbni anapoishi Peter
"Mzee ndio maana uko vizuri kwenye komputa kumbe una madesktop himu ndani"
"Ndio mzee naanza maandalizi ya kozi nitakayo soma nikimaliza shule tuu maana sina mpango wa kusoma kidato cha tano na cha sita nataka nipitie diploma kwanza"
"Unataka usome kozi gani sasa mzee"
"Nataka nipige Computer science "
"Duuh kweli mzee we fuata kipaji chako kitakutoa kimaisha "
Basi John alielekezwa na Peter mpaka pale alipoelewa ndio aliondoka.

Baada ya miaka saba kupita Peter alikuwa ni kichwa cha kuotea mbali sana katika maswala ya komputa na wakati huo alikuwa chuo kikuu akimalizia kuchukua degree yake ya Computa sayansi katika chuo cha Dar es salaam .

Siku moja ikiwa ni wikiend Peter alikuwa maeneo ya mlimani city ambapo yeye alikuwa upande wa nje kwani tayari alikiwa ashanunua kilichomleta pale ,kwani siku bio alikuja kununua simu ya ndoto yake simu aina ya Sumsung galaxy note 10 ila wakati yupo anajiandaa kuondoka mara aliona gari moja zuri sana likiingia mahali hapo na kwenda mpaka kupaki mita kadhaa kutoka miguuni mwake alijikuta akiliangalia gari hilo lakini alijikuta akipata kushangaa zaidi baada ya kumuona moja ya msichana mrembo sana alievalia gauni jekundu akishuka kwenye gari hio ,wakati anaendelea kushangaa alishuka mwanaume ambae Peter alimjua kwani alikuwa maarufu sana ncbini ambae watu walipenda kumuita bosi Samir.

"Huyu mtoto atakuwa wa huyu bosi , huyu demu nitafanya jui chini nilale nae"
"Aiyaaa...mamaaaa simu yanguu jamani mwiziii..." Peter alijikuta akiropoka kwani simu alio kuwa amenunua muda sio mrefu uliopita imepakuliwa kwa kushangaa kwake.....

SEHEMU YA 03
Bahati Masumbuko baada ya kufika stendi ya mabasi muda ule wa saa moja alijikuta akikosa uelekeo wa kwenda kwani hakujua achukue njia ipi atokee wapi.

"Nitalala hapa hapa hadi kesho" Alijiongelesha huku akiangalia namna ya kulala hapo stend.
"Wewe dogo bado uko hapa tuu ?" Aliongea konda aliekuja nae
"Ndio broo nataka nilale hapa ila nina njaa kweli nisaidie elfu moja"
" Yaani uweze kupanda gari la Luxury ,ushindwe kupata hela ya kula , na ndugu wako wako wapi?
"Broo sijaja huku kwa ajili ya ndugu nimekuja kutafuta maisha ,kama unanisaidia hio buku nisaidie"
"Siwezi kukupa kwanza nina uhakika hela ya nauli hukutoa ..tambaa ..endelea kutafuta maisha" Aliongea yule mchaga huku akiondoka zake akimuacha Bahati Masumbuko palepale pale .

"Haja kubwa imenibana sijui napata wapi choo ..ingekuwa kuna hata sehemu ilio jificha kama kichaka ningeenda kuutua" Bahati aliongea huku akitembea huku hajui hata anaelekea upande gani.
"Wewe dogo unapitaje hapa bila kutoa tiketi wala hela" Aliongea mzee mmoja ambae alikuwa amekaa kwenye kiti na vijana wawili waliokuwa wakikusanya hela kwa anaeingia na kutoka pale Ubungo kwenye geti la kutokea "
"Tiketi ya nini na kwa nini nitoe hela?"
" Wewe dogo ndio unaanza kuja Dar au unajifanya huelewi"
" Ndo nimekuja leo natafuta sehemu ya kujisadia "
"Sasa toa hela upite "
"Sina hela yoyote hapa "
"Pita lakini siku nyingine huwezi kupita hapa bila hela au kuonyesha tiketi "
"Sasa najisaidia wapi?"
" Una muuliza nani nenda kule utaona choo dogo pisha wenzako wapitee"
Bahati alitembea huku akizungusha shingo kila mahali alitembea na kukiona choo na kwakuwa hajui kusoma hata kusoma kitu kinacho endelea aliingia ndani ya choo kile nakujisaidia alivyomaliza alifunga mshipi wake na kutoka.
"Wewe!"

"Unaongea na mimi?"
" Ndio hujatoa hela"
" Hela ya nini”
" Soma hapo ukutani”
“Nilipasoma si pameandikwa choo"
"Malizia kusoma maneno yote" Hapo ndio bahati kiwewe kilimshika maana kusoma alikuwa hajui na hata maneno alio tamka kuwa ni choo alibahatisha tu kwa sababu hapo ni choo.
"Nishamaliza kusoma"
“Toa sasa "
"Nitoe nini??"
"Hivi wewe hujui kusoma si umeona hapo kumeandikwa choo cha kulipia”
"Mimi sina hela”
"Bwana eeh hebu ondoka tuu na unabahati leo niko vizuri ningekudekisha humu ndani"
" Yaani huku kila kitu unaambiwa toa hela , hata kujisaidia"
Bahati baada ya kutoka eneo lile nakuona , alitembea tembea pembezoni mwa vibanda ambavyo vingine ndio vilikuwa vinafungwa kwa kuwa muda umeenda sana lakini kuna wengine bado hawajafunga aliendelea kushangaa huku na kule na kujikuta tayari ashafika barabarani ,huku njaa ikimsumbua maana chakula alicho kula Korogwe kilikuwa kishaisha.
" Broo vipi?"
"Poa" Alijibu jamaa mmoja ambae alikuwa akichoma mahindi pembeni kidogo na barabara inayo elekea Mawasiliano
"Mlimani city iko wapi"Yule jamaa alimwangalia Bahati kwanzia mavazi
"Vipi dogo ndio unaanza kuja Dar leo nini?"
" Kwa nini broo?”
"Dogo hii Dar kwa hayo mavazi yako ungekua chokoraa au mtu anaeishi Dar asiekuwa na maisha mazuri angekuwa analijua jiji lote kwa kurandaranda"
"Anhaa..ndio broo mimi ndo nimekuja ndo nimeingia usiku huu "
"Sasa Mlimani city unataka mwenda kufanya nini?"
"Nataka nikaangalie Mlima city ulivyo nyumbani watu wanahadithia sana”
"Wewe sasa utaenda kesho pale huwezi kuruhusiwa saizi unaweza kuitwa kibaka pale ila na hayo mavazi sijui kama watakukubalia kwani ndugu zako wako wapi?".
"Sina ndugu yoyote mimi nilikuwa na mama tu kafariki kaniacha mwenyewe ndio nimekuja kutafuta maisha na historia yangu ya mama kuwa na ndugu sijui"
Bahati alikaa pale na yule kijana wakiendelea kupiga stori mpaka yule jamaa alipomaliza kazi yake ya uuzaji mahindi huku vikibaki vipande vichache na kwakuwa bahati hakula alimuomba vile vilivyo baki kwani alikuwa na njaa na yule kijana akampa huku akiondoka zake.

"Wewe dogo mbona unanifuata?"
"Broo si tunaenda wote nyumbani au umesahau kuwa mi mdogo wako " Aliongea Masumbuko huku akimkimkonyeza kwa staili flani hivi ili ampumbaze akili yake.
" |Poa twende mdogo wangu "
Bahati alitabasamu na kufuata nyuma mpaka wakapanda daladala kuelekea maeneo ya Mwenge ndani ndani huko sehemu moja ambayo ilikuwa ikisifika sana kutokana na Mamantilie mmoja ambae anafanya biashara zake hapo alifahamika kwa jina la Mama mchafu , ni katibu na kota za jeshi, basi baada ya kijana yule kushuka huku nyuma akifuatiwa na Bahati Masumbuko.
"Dogo ingia ndani acha kusimama nje mbu wanaingia”
"Aliongea yule muuza mahindi"
Baada ya Masumbuko kuingia yule kijana au muuza mahindi aliwasha jiko lake la gesi ndani ya chumba chake hicho ambacho alipanga kwenye nyumba hio yenye wapangaji wengi.
"Unapika ugali?”

“Ndio chambua hizo dagaa tupike chapu"
Baada ya kupika ugali na kumaliza walikula na kushiba na kisha wakalala kifupi walitumia muda mchache sana kumaliza mambo yote hayo kwanzia kusafiri kwenye daladala mpaka kufika na kupika haikuzinidi masaa mawili.
"Huyu akija kushtuka kumbukumbu nilizo muwekea zitakuwa zimeisha atanitoa nduki huyu” Aliwaza Masumbuko huku akitafuta usingizi mpaka pale alipopitiwa na kulala.
Wakati wamelala yule muuza mahindi alishtuka kutoka usingizini kutokana na haja ndogo iliombana ,lakini alijikuta akishtuka baada ya kugusa mwili wa mtu , alijikuta akikimbilia taa na kuiwasha, jamaa alijikuta akipatwa na mshangao na kuanza kuangalia mlango kama alisahau kifunga lakini alijikuta akiwa amefunga kabisa.

"Huyu dogo si nilikutana nae kule ubungo kapafahamu vipi hapa nyumbani kwangu na kaingiaje humu ndani sikumbuki kama nilimfungulia mimi wala kuja nae" Jamaa alianza kujiuliza maswali kibao huku hata mkojo ulio mbana ulikata ghafla alianza kumuasha Bahati ambae alionekana kanogewa na usingizi kweli kama yupo nyumbani kwake.
"Wewe toka ndani kwangu , nani karuhusu kuingia hapa ndani si nilikuacha Ubungo wewe na umepajuaje hapa au uliniangalia kwenye darubini zako za kichawi".
"Broo wewe si ndio ulio niruhusu kuja hapa au ushasahau hata ugali tulikula wote" Aliuliza Bahati huku akijisahau kuwa alimpumbaisha akili yake.

"Unasema hata ugali ...huku akiangalia sufuria alio pikia ugali alijikuta akizidi kuchanganyikiwa maana sio sufuria ya kawaida aliokuwa akiitumia kupika labda kuongezeke mtu mwingine ndio hubadilisha.
"Bwana ee.. we toka bhna utakuwa mchawi wewe sio bure kama sio jini "
" Broo sasa usiku huu nitaenda wapi"

"Utajua mwenyewe we umekujaje hapa shika mfuko wako ondoka bwana tafuta ungo wako urudi kwenu bwana " Huki akimsukumia nje na kufunga mlango na kupanda kitandani lakini alikaa kidogo tu mkojo ukaanza kuuma tena maana ni kawaida kwa binadamu yoyote pale apatwapo na mshtuko mara nyingi hata ulikuwa unanjaa inapotea kwa kuwa damu nyingi hukimbilia ubongoni na kupunguza kazi upande wa tumbo na kwenye mfumo wa utoaji wa taka mwili hii kwa kingereza inaitwa (Sympathetic na Parasympathetic ) hii ndo inaweza kukufanya kuruka hata ukuta ukiwa kwenye hatari lakini baada ya kutulia ile sehemu ulioruka huwezi tena kuruka.

Aliamua kutoka aende chooni lakini ile anafungua mlango alimkuta Bahati kaegamia ukuta huku akiwa amekaa na usingizi uliisha kutokana na mbu walivyo kuwa wakimsumbua.
"Wee mchawi sijui jini bado upo hapa tuu??."
"Broo.."Aliita Bahati na kisha yule muuza mahindi alimuangalia usoni na hapo hapo Bahati alifumba macho na kufumbua kwa staili ya kukonyeza.

"Dogo ingia ndani ulale mbona upo hapa nje kuna mbu unashindwaje kugonga mlango” Aliongea yule kijana huku akielekea chooni kisha akakojoa na kurudi Masumbuko alirudi zake ndani na kuendelea kulala.
"Wewe chriss wee chrisssii….!" Ilisikika sauti kutoka nje ikiita kwa sauti na kumfanya Chriss ambaye alikuwa usingizini kushtuka , lakini kilichomshangaza na kumpandisha hasira ni baada ya kumuona Masumbuko tena ndani hapo kalala tena kajiachia.
“Wee chrisss zamu yako ya kusafisha choo leo wewe jishaue tu umelalala hapo nakuita hauitiki"

Chriss alimsikia Pamela ambae ni mpangaji mwenzake ambae mara nyingi ndio alikuwa kama kiongozi ndani ya nyumba hio aliwakumbusha wapangaji wenzake ambao walikuwa hawatimizi wajibu wao kama vile kudeki choo na kulipa kodi ya umeme.
Sasa huyu kijana ambae ndio tumejua jina lake anaitwa Chriss aliamuamsha Masumbuko kwa kumsukuma na mguu.
"Wewe dogo jana si nilikufukuza wewe ikawaje tena upo umelala hapa ndani , na nilihakikisha kabisa baada ya kukufukuza nilifunga mlango , sasa sitaki kujua wewe ni mchawi ama ni nani nataka uchukue vitu vyako uondoke na usirudi hapa nikikuona tena nakuitia mwizi"

Aliongea huku akimpa mfuko wake Bahati Masumbuko aliekuwa akifikicha macho na kumsukumia nje na kisha kufunga mlango.
"Huyu dogo si bure huyu lazima atakuwa mchawi , ni aibu hii watu wakijua nimelala na jini , wanaweza wakasema nimelala na popo bawa, hajanipasuia mayi kweli huyu ." ?Huku akijigusa gusa gusa akjihakiki kama yuko salama sehemu zake za nyuma.
Masumbuko baada ya kutolewa nje kwa kusukumwa hakuona haja tena ya kukaa pale pale zaidi ya kutembea huku akipania kweli kwenda mlimani city , alitembea kwa kushangaa shangaa akipita vichochoro ,wakati akitembea ndani ya vichochoro hivyo alishuhudia baadhi ya vijana wakipokonyana kitu kama kijibegi na vijana hao walionekana kama mateja au vibaka na ni kweli walikuwa ni vibaka na hapo palikuwa ndio chimbo lao na maeneo yao ya kazi yalikuwa Ubungo yote mpaka Mawasiliano na Mlimani city na kila walichokwapua walikuwa wakirudi hapo kwa ajili ya kupeana mawazo jinsi kuviuza vile walivyo iba ,lakini kwa Bahati hakulijua hilo kwani ndio kwanza kaingia jijini aliwakariri sura huku akipita zake mpaka akaja kutokezea Mwenge alitembea katikati ya mabanda ya nguo na kuja kuibukia kwenye barabara ya Samunujoma na wakati wote huo alikuwa akishangaa mataa ya Pale mwenge.
"Broo vipii?"
"Poa"

"Naulizia huko Mlimani city ni wapi maana sioni mlima nikaufuatisha "
Jamaa alimwangalia na kisha kumjibu kuwa aendelee kwenda na hio barabara ataona mlima mkubwa huko mbele , wakati anatembea mara wale vijana ambao walionekana kuwa ni wavutaji bangi na vibaka walimpita huku wakiongea kwa kubishana , Bahati alianza kuwafuatisha . , aliwafuatisha huku pasipo sababu ya msingi ya kuwafuata ,alitembea umbali mrefu lakini kutokana na kushangaa kwake alijikuta akiwapoteza wale vibaka ..alitembea ndipo alipo kuja kupita eneo ambalo ni zuri na watu mbali mbali pamoja na magari yalikuwa yakiingia alisimama pembeni ya geti ..lakini wakati akishangaa mara alijikuta akishikilia kichwa na kudondoka karibu na geti ambapo magari huingia na kutoka huku akitingisha miguu kama mtu nwenye kifafa , wale walinzi ilibidi wamuwahi na kumsogeza pembeni na baada ya muda kidogo alitulia na kushtuka jambo ambalo liliwashangaza hata wale walinzi.
"Baba shikamoo .. nina njaa naomba unipe chochote nile au hela"

"Kwa hio we kijana ukiwa na njaa ndio unadondoka na kuamka halafu unaomba hela”
"Hapana huu ni hali nimezaliwa nayo mzee wangu "
Yule mzee alienda na kutoa kisha akampa ule mkate.
"Sikia kijana hii ni Dar tumia akili upate pesa usipende kuomba omba na wakati una afya njema , kwanza una miaka mingapi? "
"Kumi na saba sasa"
"Sasa kumi na saba ni mingi sana , ngoja nikufundishe jinsi ya kupata hela , ni hivi sikiliza ..angalia ni kitu gani mwenzako hawezi kufanya na wewe unaweza kukifanya ukishakipata mwambie huyo mtu umsaidie kukifanya ila mwambie akulipe”
"Anhaa... kwa hio nifanye halafu niombe hela, hlafu mzee hapa mbona watu wanaingia na kutoka hapa ni wapi"
"Wewe kijana kwanza unaitwa nani?”
“Naitwa Bahati masumbuko”
“Sasa Masumbuko si umeona pale pameandikwa Mlimani city na hapa ni mlimani city”
"Mzee mbona sasa hakuna mlima na sioni hayo magemu ya kuvaa miwani kama watu walivyokuwa wanasema"
"We dogo hata sikuelewi ngoja kwanza nifungulie watu wenye pesa zao , aliongea huku akivuta kamba kuruhusu gari lipite pale na kulionyesa sehemu ya kupaki , huku akiona moja ya mdada ambae kapendeza kweli kweli akiwa amevalia gauni jekundu na baada ya kushuka, alishuka tajiri mmoja maarufu Samir.

Lakini mzee yule akifunga uzio yule huku nje ndio kijana Peter alikuwa anatoka kununua smartphone yake huku akiishikilia kwakuwa alikuwa haamini kama angekuja kumiliki simu kama hio , lakini alijikuta akishangaa gari ambayo iliingia kwani ilikuwa ni nzuri sana lakini kilichomfanya ajisahau kabisa ni baada ya kumuona msichana mrembo hatari na kujikuta akisahau kama yupo barabarani kwani wakati anashangaa wale vibaka waliikwapua simu na kisha kutimka kuelekekea mafichoni kwao, huku tukio hilo likishuhudiwa na Bahati na yule mzee ambae alisharudi alipo Masumbuko. Peter hata sauti haikutoka alijikuta akikaa chini huku haamini kilicho mtokea simu ya milioni moja na nusu imekwapuliwa alijikuta akichanganyikiwa.

"Kaka vipi .. naenda kuileta ila unipe hela" Peter alisikia sauti ilio mfanya ainue uso wake na kumwangalia huyo anaemuongelesha "
" Oya chalii hebu toka tuu hapa usinivuruge mimi , wewe ni wale wale ondoka bhn" Aliongea Peter kwa hasira huku akitaka kuondoka kwani aliona ameshapoteza kila kitu alianza kutembea na kujikuta akigeuza na kumfata yule kijana ambae amesimama pale pale maana alichukia kuambiwa yeye ni wale wale wa kuiba.
" Wewe unawajua wale ?"
" Wewe nipe hela nikakiletee simu yako "
"Poa nenda nitakupa laki moja ukiirudisha"
" Hio hela mpe huyu mzee hapa anishikie mpaka nitakapo rudii"
" Mzee nafanyia kazi mbinu yako ya kutafuta pesa"
" Wewe kijana sijamaanisha hivyooo" Lakini mzee alichelewa kwani Masumbuko alikuwa amekwisha kimbia
 
Ndg yangu nkuulize hivi unawezaje kuandika story tofauti tofauti mda mchache hivyo nipe siri ya mafanikio
 
Ndg yangu nkuulize hivi unawezaje kuandika story tofauti tofauti mda mchache hivyo nipe siri ya mafanikio
Uandishi kwangu ni hobby mkuu.. Nadhani hio ndio siri kubwa.. Naandika kila siku chchote kinachonijia kichwani Napenda kusoma vitabu pia so always nakua na idea ... Lakini kwangu pia ninachojifunza na kukijua natamani na jamii ikijue so nimeona njia ya kuhamisha kile ninachokijua kutoka kwangu kwenda kwa jamii kwa mafunzo zaidi ni kupitia uandisbi.
 
Uandishi kwangu ni hobby mkuu.. Nadhani hio ndio siri kubwa.. Naandika kila siku chchote kinachonijia kichwani Napenda kusoma vitabu pia so always nakua na idea ... Lakini kwangu pia ninachojifunza na kukijua natamani na jamii ikijue so nimeona njia ya kuhamisha kile ninachokijua kutoka kwangu kwenda kwa jamii kwa mafunzo zaidi ni kupitia uandisbi.

Good
 
SEHEMU YA 04
Yalipita zaidi ya masaa kama mawili bila Bahati kurudi na Peter alikuwa bado yupo pale anasubiri.
"Kijana mimi sidhani kama ataweza hio kazi na kurudi na hata kama anajua maficho yao ukute saizi ashachezea kichapo cha maana , mimi naona uchukue hela zako tu hizi uondoke kuliko kupoteza muda"
"Mimi mzee nishaamua hapa, nasubiri mpaka nimuone akija najua na yeye ni kibaka lazima awajue vibaka wenzie na ataileta simu hapa" Aliongea Peter huku akijishangaa kwanini kumwamini Bahati.
" Hakuna shida kama unaa amini atarudi subiri ila yule sio kibaka kaja Dar jana tu"
"Mimi naingia ndani kwanza kupunguza mawazo nikitoka atakuwa asharudi aliongea Peter na kuingia ndani na moja kwa moja aliamua aende duka la nguo kuona kama kuna toleo jipya la mavazi kwani Peter alipendelea sana kuvaa , japo Mungu amembaliki sura nzuri ya kumvutia mwanamke lakini pia hakutaka kuonekana mchafu alipenda sana kuwa smart, aliendelea kuangalia baadhi ya mavazi lakini hakutaka kuuliza hata bei kwani hapo ilikuwa sio chimbo lake la kununulia mavazi ila yeye alitaka tu kuangalia ni vazi gani jipya limeingia ili akalitafute Kariakoo maana bei ya hapo asingewezana nayo, aliangalia huku akikosa kabisa hata hamu ya kuendelea kuangalia maana mawazo ya kupoteza simu yake yalikuwa yakimwendesha.
Kila akikumbuka jinsi ambavyo hela alizipata kwa tabu sana na sasa hana hata uhakika wa kuipata tena kumwamini Bahati Masumbuko ni kama alibeti tu , alijikuta hasira za kupoteza siimu zikimpanda huku akitoka nje bila hata ya kuwa makini kwani ile anapita alijikuta akigongana na yule msichana alie mchanganya muda mfupi mpaka kupelekea kuibiwa simu, na binti yule kudondoka chini huku akiteguka mguu jambo ambalo Samir tajiri alilishuhudia na kumfanya apandishe jazba na kumfata Peter na alivyo mkaribia alimchapa vibao kama viwili vikali jambo lililowakusanya watu walio kuwepo ndani humo kuangalia huku wengine wakirekodi.
"Wewe unamfanyia makusudi mwanangu kwa kumgonga makusudi halafu ili uje kusema bahati mbaya ee" Samir alikuwa kapandisha hasira kweli kweli na alivyo jumlisha na stressi zake kutoka nyumbani kwake.
"Mzee wangu naomba unisamehe ni bahati mbaya tuu" Aliongea Peter kwa sauti ya kipole .
" Kijana nitokee mbele yangu kabla sijakuvuruga vuruga mimi nyie vijana najua tabia zenu , hizi zote ni janja za kumtaka mtoto wangu sasa nakwambia kaa mbali na mwanangu kwa hili umefeli kabuni mbinu nyingine fala wewe , kwanza huna hadhi” Alifoka kweli na matusi juu tajiri pasipo kujua anae mfokea ni mtoto wake.
Peter hakutaka kusikiliza zile dharau za yule ta tajir aliamua kuondoka zake huku akiwa ameghafirika kweli na kuona jambo lile ni kama dharau alitoka mpaka nje ya uzio , lakini alijikuta akikodoa jicho baada ya kumkuta Bahati amekaa na yule mzee huku akiwa ameshikilia ile simu , jambo ambalo lilimfanya Peter hata asahau kwa muda kilicho tokea huko ndani.
"Wewe jamaa ni noma , aisee umeipataje pataje?"
"Wewe hutakiwi kujua nimeipataje simu yako hio hapo na pesa yangu hii hapa nishachukua ila kama una kitu hujui kufanya nitafute nikufanyie unipe pesa" Aliongea masumbuko.
"Daah... poa aisee asante sana" Aliongea Peter huku akiweka simu yake kwenye kijibegi lakini alisimama baada ya kuona gari ya boss Samir inatoka alijikuta misuli ya uso ikimpanda aliliangalia mpaka lilipo tokomea huku akikumbuka maneno ya dharau na matusi aliotolewa na tajir huyu.
"Mzee ushauri wako mzuri sana nishapata hela" Aliongea Bahati Masumbuko baada ya Peter kuondoka.
"Sasa ushauri wangu wa pili katafute nguo nzuri uvae na viatu na chakula uje uingie mlimani city"
"Mzee sasa hizo nguo napatia wapi mimi sijui pa kuzinunulia maana mimi mgeni huku nimekuja jana tuu"
"Sasa kumbe wewe ni mgeni , kaa hapo namwachia mwenzangu hii elfu therathini ulio nipa asubuhi hii itakuwa malipo kwa kukusindikiza ukanunue hizo nguo”
"Hapo mzee umesema la maana "
********
MIAKA ISHIRINI NA TANO NYUMA.
Tukirudi nyuma miaka iliopita baada ya Irene ambae ndio mama yake Peter kufukuzwa nyumbani baada ya Irene kuondoka tu Shania alipata wasiwasi juu ya kile Irene alichokuwa akiongea na mme wake na kilichompa mashaka zaidi ni baada ya mume wake kuingia na kuchukua hela na kisha kutoka nje , alivyoona tu mume wake katoka ndipo alipo mfuata mlinzi.
"Wewe Juma , Samir kaenda wapi?"
"Itakuwa kamkimbilia yule dada alietoka hapa muda si mrefu"
Shania alirudi zake ndani huku akijikuta wivu na wasiwasi vikimuendesha ,aliogopa sana kuchukuliwa mume wake.
"Ila ngoja arudi anipe maelezo " huku akikaa kitandani na ndani ya muda mfupi tuu samir aliingia
"Umesema utaniambia kuhusu yule mwanamke ni nani"
"Ndio mke wangu yule msichana kuna siku moja nilipata accident na kujikuta nikigonga bidhaa zake sasa kwa sababu nilikuwa na haraka nilisimamisha kidogo na kuchungulia na kuondoka sasa siku zilivyo pita nilisahau kabisa , sasa ndo kaja kasesma nimemuharibia biashara yake anataka fidia "
"Mhmh haya mume wangu siku nyingine uwe unaomba hata msamaha huoni sasa imeleta picha mbaya"
"Ni kweli mke wangu ila nishamlipa Mara tatu ya anacho nidai"
" Kama ni hivyo sawa" Aliongea Shania huku akisoma kitu kwa mume wake na kikampa ishara Fulani isio ya kawaida.
"Mke wangu natoka kidogo"
Wakati Samir anatoka Shania hakuchelewa alipiga simu sehemu na ndani ya muda mfupi aliingia jamaa mmoja hivi mwenye marasta.
"Niambie bosi "
"Salama tu , nimekuita kuna kazi nikupe "
"Kazi gani hio?
"Kuna mwanamke nataka unipe taarifa zake nahisi kuna mahusiano yanaendelea na mume wangu ambayo siyajui ,maana kaingia hapa ndani ila kumuona tu nikapata wasiwasi
" Sasa hakuna shida we niambie sehemu anayo patikana nimtafute”
" Hata sijui anapokaa na hata picha yake sina "
"Lakini si umesema ameingia hapa nyumbani si ndio"
"Ndio "
" Basi twende tukaangalie CCCTV camera za leo tunaweza pata
picha yake”
" Daah! halafu kweli hata sikulifikiria hiloo"
Waliingia chumba cha kamera na kuangalia na kweli waliweza kupata vidio ambayo inaonesha sura ya irene .
“Sasa hapa kazi imeisha we nitoe mpunga wa kuanzia kazi si unajua mwenyewe lazima nizunguke na gari”
" Ndio nakutumia kwa njia ile ile ya siku zote”
"Poa"
Baada ya yule marasta ambae jina lake ni Bosco kupewa hela ya kianzio kwa kazi alitoka pale huku akimuhakikishia shania kuwa kazi itaenda vizuri, lakini siku zilienda na kupita hawakuweza kumuona Irene na hata Shania alijifungua mtoto wa kike mzuri kweli na jina lake alimwita Rania.
Baada ya miaka kupita wakati huo Rania anaingia darasa la saba Tanganyika International school ndipo Sosco alipompigia simu na kumwambia Shania kuwa amempata Irene . wakati huo Shania alikwisha ijifungua tena watoto mapacha wa kike ambao walipewa majina ya Nasma na Najm.
"Boss nahitaji maelekezo yako tuu nishampata anapofanyia kazi ni huku barabara ya kuelekea Tegeta wanapaita Mbuyuni " Aliongea Bosco
"Sasa we endelea kumpeleleza unipe taarufa zote zinazo muhusu" aliongea Shani au Mama rania na zilipita siku tano ndipo Bosco alikutana na Shania
"Nipe taarifa ulio ipata "
"Jina anaitwa Irene , anafanya kazi ya kuuza mkaa ana mtoto mkubwa kama Rania anasoma la saba kuhusu baba wa mtoto inasemekana keshafariki kabla ya kujifungua na kingine ni kwamba pia alishawahi kufanya biashara ya udadapoa "
"Nataka unitaftie picha ya huyo peter unileteee na hakikisha unapata mswaki anaotumia "
"Wa nini sasa huo Madam "
"Wewe fanya kama nilivyo kuagiza"
Bosco baada ya kuachana na bosi wake alianza kutafta njia ya kupata mswaki wa kijana Peter na picha yake aliumiza kichwa sana juu ya kuvipata hivyo vitu lakini alijikuta akipata suruhu
Siku ilivyo ingia asubuhi asubuhi alitoka kwake na kuendesha gari yake aina ya Spacio mpaka Sinza nyumbani kwa Irene na kuegesha gari karibu kabisa na nyumba yake huku akiangalia nyumba hio kupitia kwenye gari na haikuchukua muda mrefu alimuona Peter akitoka nje huku akipiga mswaki huku akishikilia ndoo ya maji na kuingia bafuni , Bosco baada ya kuona Peter kaingia bafuni alikimbia mpaka nyuma ya bafu ambalo kuna kama kidirisha na mawazo yake yalikuwa sahihi kwani alikuta mswaki upo juu ya kile kidirisha hakuchelewa aliuchukua na kuuweka kwenye kijimfuko na kuondoka , Peter baada ya kumaliza kuoga alinyoosha mkono achukue mswaki wake ila hakuuona aliachana nao baada ya kujua kuwa lazima utakuwa umedondokea kwa nje .
“Bosco baada ya kupata mswaki ule alirudi kwenye gari na kusubiri haikuchukua muda mrefu alimuona Peter akitoka akielekea shule . alitoa kamera yake na kumpiga picha kama nne na kisha akaondoka
"Madam kila kitu nimepata"
“Safi sasa njoo nyumbani " Aliongea Mama rania
"Bosco alienda mpaka nyumbani kwa Samir na kuingia ndani na kisha akatoa flash na kijimfuko kikiwa na mswaki ,Shania aliingia chumbani kwake na kutoka na laptop kisha akaanza kuzingalia hizo picha.
"Mh bosco asante sana pesa yako hii hapa ila nitakupa kazi nyingine muda si mrefu”
" Sawa bosi" huku akiondoka zake .
Shania au Mama rania hakutaka kulembesha alichukua mswaki wa mumewe na ule wa Peter na kwenda kwa Dokta Azizi Aghakan na kumuomba afanyie vipimo vya DNA .
" Dokta azizi hakutaka kuuliza sana maana anamjua shania na ni rafiki wa samir basi alifanya vipimo vile na baada ya siku mbili Dokta Azizi aliprint majibu yale na kisha kusaini ile karatasi na kuandika jina lake kama invyofanyika katika mahospitali mengi na kisha kumpatia shania
"Vipi Mama Rania hivi ni vipimo vya nani haswa”
"Kuna rafiki yangu mmoja hivi anasumbuliwa na nme wake na ana mtoto sema hajui ni wa baba yupi kwani alilala na wanaume wawili ndani ya siku moja sasa anataka ajue na kaniomba msaada "
"Anhaaa... hakuna shida , majibu yake haya hapa "
Shania au Mama rania alijikuta akitoa macho kwani vipimo vile vilikuwa ni asilimia 99 vinafanana , ilimaanisha Peter na Samir ni kitu na baba yake , jambo lilimghafirisha sana shania maana alijihisi kichwa kikimuuma na tumbo kukoroga alirudi zake nyumbani huku akimkuta mme wake anacheza na Nasma na Najma .
"Vipi mke wangu mbona unaonekana umechoka sana "
"Ndio nimezunguka sana leo ndo maana vipi washapewa chakula hao watoto "
" Ndio washapewa "
"Halafu nataka nitoke tena kwenda saluni mara moja "
"Si ungepumzika sasa mke wangu "
"Hapana mume wangu umesahau kesho tuna kwenda kwenye send off ya Mama Asma "
" Anhaa sawa mke wangu ni kweli nilisahau kidogo "
" Baada ya Shania kutoka haraka haraka alimpigia simu Bosco na wakutane Mikocheni " na ndani ya masaa machache bosco alifika na kuingia ndani ya gari .
" Sasa sikia Bosco nataka Irene na mtoto wake uwapoteze kwenye huu uso wa dunia "
"Mhmh Madam kwa nini???"
" Wewe hupaswi kuuliza fanya kama ninavyo kuambia ukikamilisha hili nataka uondoke hapa Dar nitakupa milioni mia ".
"Asiee kama ni hizo naomba hio kazi maramoja nitawasababishia ajari wote wawili tusishtukiwe "
"Safi sana nitakupa hamsini ukimaliza nakuongezea ila nataka utoweke baada ya kazi
"Hakuna shida boss kazi imeisha "
,"Bosco tamaa ya pesa ilimuendesha kila alipo fikiria kiasi cha pesa alicho ahidiwa alijikuta akizid kupata munkari wa kuwauawa , japo hakuwahi kuuwa hapo kabla ila hela ilikuwa kama shetani kwake kwani ndani ya siku tano kupita tayari alikuwa ameshasababisha ajari ya Irene aliefariki hapo hapo .
"Bossi kazi tayari niingizie pesa nisepe "
"Sawa we chukua gari na uondoke nitakuingizia" Aliongea Shania huku akionekana kufurahi
"Yule mtoto nitamwacha ili hata nitakapo kuja kuomba msamaha kwa mungu anisamehe " Alijisemea Bosco wakati huo akipanda basi kuelekea rukoa wa Sumbawanga.
Baada ya ajali Shania alipata amani na kuendelea kuwalea watoto wake kwa malezi bora huku Rania akizidi kuwa mrembo kwa jinsi alivyozidi kukuwa na kuwafanya wanaume wengi wamtamani .
Kiufupi familia nzima ya Samir ilikuwa imebarikiwa sana kwani alizaa warembo haswa watoto waliobarikiwa sura shepu na kila kitu yaani kila mwanaume aliekuwa akiwaangalia watoto wa tajiri huyo alikuwa lazima apate shoti za upande wa chini wa mwili na kila msichana alikuwa na muonekano wake na wote hawakufanana ingawa Nasma na Najma kuzaliwa mapacha lakini hawakufanana kabisa ila wote walikuwa warembo haswaa..
Kwa upande wa Rania yeye alikuwa akimaliza shahada yake ya uchumi ndani ya chuo kikuu cha Dar es salaam , huku Najma yeye yeye hakuchukua mtaala wa kitanzania kama dada yake kwani kati ya watoto wake Samir Najma alikuwa ana mashauzi sio ya kitoto . Nasma yeye alichukua mtaala wa kitanzania ndio maana Najma yeye alikuwa tayari ashafika chuo na alikuwa akisomea huko Marekani maswala ya Fashion and Designing , upande wa Nasma yeye hakwenda kujikweza alipenda sana kuishi maisha ya kawaida ndio maana hata baba yake alivyomuambia kusomea chuo nje ya nchi alikataa na kipindi hicho alikuwa ndo anamaliza kidato cha sita ndani ya shule ya Alfa na Omega iliopo mikocheni. Lakini japo ya wasichana hawa kuwa warembo lakini wote watatu hawakuwahi kuwa na mahusiano na mwanaume yoyote yule mpaka umri huo na hii ni kutokana na malezi walio lelewa , kwani samir aliwawekea ulinzi mkali sana na mwanaume ambae alionekana kumsogelea msichana wake alipigwa mkwara hata kutishiwa maisha.
*********
“Boss Samir naona leo umekuja kupata moja moto moja baridi sio kawaida yako "
Aliongea Hemedi ambae ni rafiki mkubwa sana wa Samir , Hemedi alikuwa na yeye ni mfanya biashara mkubwa hapa nchini akimiliki mabasi ya abiria huku Samir yeye akiwa mfanya biashara wa mizigo na kuuza magari.
"Rafiki yangu yaani leo kidogo tuu nimtoe mtu jicho pale Mlimani city"
"Ahahahaha.. kwanini sasa au ni yale yale yakumlinda Rania?”
"Ndio si kuna bwege kaja kujigonganisha na mwanangu ili kumpata yaani aliniboa kweli yaani maana nilijua yote ile ni janja tu ya kumgonga Rania”
"Hahahaha...uwe unapunguza hasira unajua rafiki yangu kumlinda mwanamke haiwezekani ,wewe inabidi umpe elimu ya jinsia mwanao tu umfanye ajielewe maamuzi yawe juu yake”
"Ni kweli lakini nisipo kuwa mkali lazima watamchezea tu mimi nawajua watoto wa kike sio kama sisi"
"Sasa vipii kuhusu mali zako maana mkeo ashafunga uzazi yule au utamrithisha huyo Rania”
"Yaani hilo swala linaniumiza kichwa yaani , ningekuwa na mtoto wa kiume nisingekuwa na hizi stress"
"Lakini si ulisema kuna mwanamke alishakuja akakwambia ni mjamzito , kwanini usilifuatilie hilo swala"
"Ni kweli ,unajua najilaumu sana mpaka sasa hivi yaani , maana sikumuuliza jina wala sehemu anayoishi na kwakuwa kazi yake ya ukahaba haikuwa rasmi huwezi kupata taarifa zake pale Sinza alipokuwa akijiuza maana wale hawajiandikishi kama waajiriwa kama tunavyofanya sisi tunavyo ajili watu "
"Daah.. ni kweli rafiki yangu ila mimi naona ni vyema kuendelea kumtafuta , nitakuunganisha na jamaa yangu mmoja hivi ni mzuri sana katika kutafuta watu"
"Ni kweli inabidi sasa niweke tumaini kwa huyo mwanamke kama kweli hakutoa mimba kama alivyosema siku ile na kama alijifungua mwanaume nitamrithisha mali zangu zote .
" Kweli kabisa na vipi mwanao Nasma yule mwenye msimamo mkali "
"Tena hata usimwongelee huyo mjinga , kwanza hataki kukaa nyumbani anakaa huko Mbezi Beach kapewa hela na mama yake kanunua nyumba"
"Hahahaha... sema napenda sana msimamo wake yule atakuja kukuletea beshima ndani ya familia halafu hapendi unavyomfatilia na hakuogopi pia ".
 
SEHEMU YA 05
Yule mzee ambae kwa jina lake anaitwa mzee Msabaha lakini jina lililozoeleka mtaani kwake alikuwa akiitwa Jicho la jamii hii ni kutokana na kuwasaida vijana wengi kimawazo pia kuwafanya vijana wengi kubadili mitizamo yao juu ya maisha ndio maana wengi walipenda kumuita Jicho la jamii , Huyu Msabaha historia ya maisha yake mzee alifanya vitu vya ajabu ajabu huko mkoani Rukwa mpaka alipo kuja kufiwa na mke wake na watoto wake wawili kwa kukosa hela za matibabu jambo ambalo lilimsononesha sana na kumpa mawazo mengi ndipo alipoamua kuhamia jijini Dar es salaam pamoja na mtoto wake Issa .
Mzee msabaha kutokana na changamoto nyingi alizopitia katika maisha yake alijikuta akijifunza mambo mengi na kujiona wakati wa ujana wake alipoteza sana wakati ndipo alipoanza kuwasaidia vijana wengi kubadilisha maisha yao .
"Mzee haya magorofa wanajengwaje jengwaje mbona marefu hivii"
“Hahha ...wanajenga na vifaaa ndio maana ,ngoja utaona mbeleni huko kuna majengo yanajengwa”.
"Bahati na yule mzee hatimae walifika Ubungo ambapo baada ya kufika mzee alimpeleka Bahati mpaka sehemu inayouzwa mitumba, walichaguwa mitumba mbali mbali ilio gharimu shilingi elfu ishirini pamoja na viatu ..
"Sasa kwasababu umeniambia hunapakuishi twende ukakae siku mbili tatu kwangu ila ni hizo siku tatu tuu unatakiwa utafute chumba maana mwanangu akirudi hamtoelewana".Aliongea Mzee Msabaha huku wakiondoka eneo.hilo kutafuta kituo cha dalala, baada ya kufika nyumbani kwa yule mzee maeneo ya ukonga waliingia kwenye nyumba moja nzuri hivi ilio zungushiwa ukuta na kupakwa rangi ya bluu
"Mzee unaishi sehemu ni nzuri sana ".
"Ndio hapa ni kwa mwanangu ni mkorofi kweli kasafiri ndio maana nakwambia siku tatu uwe umetafuta chumba”
"Niambie mbinu nyingine ya kupata hela mzee wangu "
"Subiri nitakuambia usiwaze kijana , nitakwambia kabla sijarudi kazini ila tutaondoka wote maana bado sijakuamini vizuri "
"Sawa mzee kwanza nataka nikaone Mlimani city".
“ sasa mbinu nyingine nikwambie , kwanza umeishia darasa la ngapi"
"Mimi nimeishia la saba ila nilionewa huruma tu ,maana nilikuwa kila siku wa mwisho nilikuwa napata sifuri nikifaulu nilikuwa ninapata tatu , mama yangu aliniambia kuwa sina akili maana alikuwa akinifundisha sana ndio maana hata kusoma sijui "
"Kwa hio hujui kusoma?"
"Ndio sijui kusoma kabisa "
"Sio shida sana , ila kwakuwa leo umeweza kutengeneza laki moja kwa siku basi jiweke kwenye kundi la wenye akili."
"Sawa mzee wangu"
"Halafu hebu niambie uliwezaje kuchukua ile simu, kwa wale vibaka "
"Niliwaibia"
"Ahahaha..safii"
"Sasa njia nyingine ni shida za watu wa ile sehemu unayoishi, nikuangalia je unaweza kuwasaidia shida zao ili wewe wakusaidie pesa ,kwa hio kesho katafute shida za watu hata kwa kuuliza kwenye majumba halafu fikiria jinsi ya kuwasaidia"
"Mzee , lakini mimi kufikiria siwezi ndo maana nilikuwa nikipata sifuri "
"Basi wewe katafute shida za watu popote pale halafu njoo nitakusaidia kufikiria”
"Hapo sawa mzee wangu , shida yangu unisaidie kufikiria tuu mengine nitayatatua mwenyewe”
****
"Niaje Peter!"
"Poa Steve mishe vipi hatujaonana siku mbili hizi "
"Ndio kuna mzee mmoja aliharibikiwa na komputa , jana nilishinda hukooo na juzi nilikuwa kwa demu flani hivi aliniita nimkune hahaha"
"Nakuelewa wewe kwa totozi"
"Halafu naona ushanunua tayari ile simu ulioniambia?"
"Wewe acha tuu mzee kidogo tuu niipoteze, si mzee wakati natoka nikaona pini la demu linaingia pale Mlimani sasa si akanizubaisha maana nilidata ghafla , sasa kule kujisahau si vibaka si wakaikwapua"
"Kweli huyo demu atakuwa kiboko maana hujawah kudatishwa na mwanamke wewe, Demu gani huyo?"
"Demu wa tajiri mmoja hivi"
"Daaa aisee!!..,Sasa ikawaje?"
"Kuna jamaa mmoja mchafumchafu hivi akaja akasema nimpe hela akailete mwanzoni sikumuamini lakini nilijikuta nikibeti kwa kumpa laki moja akailete mzee ...” Peter alihadithia vyote
"Hivi huyo jamaaa ana akili kweli yaani ameweza kuipata simu baadala ya kwenda kuiuza yeye kaileta kwako na umesema maisha yamempiga, Huyo jamaa mwaminifu sana "
"Ndo hivyoo mzee ila kesho nitamcheki kama vipi nimuongeze hata laki moja nyingine"
"Daah! ..fanya hivyo aisee kaokoa milioni moja na laki nane sio mchezo ujue"
"Sasa kuna lingine mzee ambalo liliniudhi na kunitibua nyongo na lazima nilipize kisasi"
"Mhmh lipi hilo?"
"Mzee si wakati nipo ndani ya Maduka ndani mle Mlimani, Yule ghashi alienizubaisha si nikagongana nae bahati mbaya sasa kumbe mzee wake alikuwepo pale mzee si kaja kanilamba vibao na kunitukana juu nilighafirika kishenzi, yaani ila muache yule mzee yeye anajifanya tajiri ila tutaonyeshana mimi nitatumia akili yeye atumie pesa tuone kama atanishinda "
"Ni tajiri yupi huyoo tumfanyizie anakuonaje Kimsela wakati wewe ndio genius Tz nzima"
"Samir mzee yule mwenye pesa chafu hapa town"
“Kama ni yule mzee ni sawa kupokea vibao , unajua nasikia kabahatika kuzaa madem tu ila nasikia ni visu balaa .. kuna huyo mmoja anaitwa Nasma ni noma kamaliza Alfa ni kisu balaa ila hakuna anaemsogelea mana jamaa nasikia kaweka watu kuwafuatilia wanae na ukionekana kuwafatilia wanakukamata unakula kichapo kama onyo ukirudia wanakupoteza kabisa”
"Sasa ndio anipige bila kosa nitahakikisha wanae wote nawatoa bikra ngoja uone labda wasiwe mabikra"
"Bikra tena mzee hahhahaha... pale huwezi huyo Nasma huchomoi nasikia ni mgumu balaa"
"Wewe hata awe mgumu vipi nitawapata tu nawatoa bikra wote , ikiwezekana namgonga hata mke wake hawezi kuniabisha kingese vile"
"Mimi mzee! , langu jicho ila nakushauri uwe makini mzee " Aliongea Steve maana alijua Peter akiamua jambo tena ambalo ni la kisasi anahakikisha mpaka linafanikiwa.
"Kwa hio upo siriasi mzee unaenda kuanzisha battle na yule mzee?"
"Ulifikiri na kutania ,Wewe subiri uone kesho kwanza nitafanya uchunguzi ni wajue watoto wake wote wa kike nitamfanya amlalamikie Mungu kwa kumpa watoto wa kike tu, yaani nagonga nyumba nzima ndio kisasi changu kitaishia hapo tuone kama kweli atawalinda".
"Hahahahahaha...wewe utamuua yule mzee wewe ...yaaani uwapige rungu wote aisee hakuachi hai hahahaha... daah! ila mzee una visa vya kijinga ujuE"
"Wewe si unaona vya kijinga , wewe subiri misheni inaanza kesho hawezi kuniabisha vile, aisee mimi uonevu sipendi kwenye maisha yangu ,na sitoweza kamwe kuruhusu jambo la kuonewa kwenye maisha yangu"
Ilikuwa ni siku nyingine siku ambayo jua lilichomoza kwa miale mikali ,Jua lilikuwa kama Alarm kwa baadhi ya watu kuwaamsha na kujiandaa kwenda makazini, huku wengine wakitumia kuchomoza kwa jua kama ishara ya kwamba Mungu amewapa siku nayingine katika maisha yao na hupiga goti na kumshukuru Mungu, lakini hali ilikuwa tofauti kwa kijana Peter yeye aliona jua hilo kama ishara njema ya kwenda kufanikisha lile lililopo ndani ya akili yake ambalo lilikuwa likimuumiza roho sana hata kujikuta kuliota ndotoni.
Peter baada ya kuamka aliingia bafuni katika Apartment hio alio pangisha yenye vyumba viwili vya kulalia na sebule , alijimwagia maji na kujiweka sawa baada ya kumaliza alichagua nguo nzuri ambayo itamtoa siku hio kama hulka yake ya uvaaaji wa mavazi,basi jamaa alitokaelezea sana ukijumlisha na Mungu alivyomjalia Uhendisamu vijana kwa Kiswahili kisicho sanifu tunasema ‘Aliua’.
Kwa uchache ni kwamba Peter alikuwa hazoeleki kwenye macho ya wadada wengi wa pale chuoni(CoET) kutokana na umaridadi wake katika swala la uvaaji pia ukichangizwa na sura ambayo alirithi kutoka kwa mama yake na baba yake ambae hamjui , lakini japo ya Peter kuwa na umaridadi ila hakuwa na demu(Mchumba , Rafiki wa kike ) hata mmoja sio kwamba walikuwa hawampendi ila Peter hakupenda kujishughulisha na hizo habari na wengi walimshobokea huku wengine wakijirahisha kwake lakini walishindwa,mpaka wakati mwingine wasichana wa UDSM kuona jamaa labda ana matatizo , tetesi hizo zilivuma chuoni hapo huku washikaji wa Peter wakimuambia agonge hata demu mmoja lakini Peter alikataa.
Ni siku hio Peter aliamka na mawazo ya kulipa kisasi kutokana na kudharilishwa na aliamua japo hakutaka kumchezea mwanamke yoyote yule ila kutokana na kuchukia unyanyaswaji na uonevu, Peter alifunga nyumba yake huku akichukua kiasi cha pesa laki mbili na kukiweka kwenye Walleti yake huku dhumuni ni kwenda kumtafuta kijana aliemsaidia kupata simu yake, baada ya kutoka nje aliingia kwenye pikipiki yake aina ya Honda ambayo aliipata kama zawadi kwenye maonesho ya Tehama ,miaka hamsini ya chuo kikuu cha Dar es salaam.
Alipitia pale Mlimani city nakumtafuta yule mlinzi na muda huo hakukumkuta ila aliacha maagizo kuwa anahitaji kuonana na kijana aliemsaidia kupata simu yake na kisha kuwahi chuoni kwa ajili ya kipindi ,Na baada masaa mawili ya kipindi Peter alitoka maana hakuwa na kipindi kingine mpaka saa nane .
"Oya Peter niaje mzee"Alisalimia Steve ambae yeye pia alikuwa mwanafunzi wa UDSM-CoeET alikuwa anachukuwa Eectronic Enginearing ( Yaani digrii ya uhandisi wa kutengeneza vifaa vya Elektroniki)
"Safi vipi mzee"
"Safiii mzee sasa nimepata habari nzuri kuhusu yule ghashi wa Boss Samir"
"Enhe niambie!"
"Yule ghashi(Msichana) anasoma hapa UDSM , anasomea uchumi mzee na anafanya pia kazi kama manager kwenye benki inayosemekana ni ya mama yake”
"Huyo ghashi atakuwa na mtonyo nitahakikisha hata pesa nazinyonya"
"Ndio mzee nasikia hii benki ni ya yule mke wa boss Samir na yeye ndio mtendaji mkuu wa hio benki(CEO)na pia ni mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa hio benki”.
"Sasa hebu nipe data mzee za huyo mtoto"
"Mzee yule demu kwa taarifa zake sijui kama pale unaweza kula mzigo maana nasikia demu anajielewa ile mbaya japo kuwa baba yaje anamlinda ila nasikia washikaji chuoni wamekwama , wamepigwa chagga wengi , hata mtoto wa waziri wa fedha yule mshikaji HB na mpole sana pia kapigwa chaga ."
"She fall under my preference category"
"Kivipi sasa mzee?"
"Ushasahau kuwa nataka kuwatoa familia nzima bikra, nikiwakuta hawana kisasi changu hakitakuwa na nguvu nataka niwatoe bikra wote"
"Duuh! mzee ...sasa si ndio itakuwa ngumu kuwapata , hivi unafikiri demu aliejitunza miaka yake yote ampe tu mtu bila michujo mingi akate utepe , hio haiwezekani mpaka akupende "
"Mimi nina akili bhna nitafikiria jinsi ya kumpata tu ,ila pia kisasi changu lazima kitimie nitahakikisha watoto wake wanamfanya baba yao atoe machozi”
"Daah! ... poa mzee kuwa tu makini ,halafu demu mwenyewe anaitwa Rania , mimi naelekea class nina kipindi kingine"
"Poa uje home baadae basi unipe Source code(Taarifa) zake fresh , mimi natoka kidogo kuna mshikaji nimcheki "
"Poa wa No syntax Error"
“Hahaha.. No Syntax Error Bro” Msemo wa No syntax Error ulikuwa ukipendwa sana na kijana Peter , ilikuwa ni falsafa yake aliojijengea katika swala zima la kuandika mistari ya Codes kwa kutumia Programing Language nyingi , Mara nyingi hupenda kuwaambia wenzie kuwa kazi yake haina Syntax Error kwani lugha ya Komputa ipo kichwani kama anavyozungumza Kiswahili.
Alipanda Honda yake na kuelekea getini na kutoka kabisa akielekea upande wa kushoto , aliendesha mpaka geti ama kizuizi Ndani ya Mlimani city na bahati nzuri alimkuta kijana alie mfuata .
"Mzee shikamoo"
"Marhaba kijana za toka jana?"
"Salama kabisa nimekuja kuongea na kijana wako mara moja"
"Oya niaje?"
"Safii , jana nilisahau hata kujitambulisha naitwa Peter wewe je ?”
"Naitwa Bahati masumbuko"
"Sasa Masumbuko nimekuja nikuongeze chochote nimefikiria jana nikaona ulinisaida sana na pamoja na uaminifu wako nimeona ni kuongeze laki moja ziwe laki mbili kamili"
"Laki mbili ni shilingi ngapi?"
"Hahahaha..inamaana hujui laki mbili?"
"Mimi sijui nimeenda shule lakini nina matatizo ya kufikiria na hesabu sijui kabisa yaani mimi ni kilaza"
"Anhaa... namaanisha hela kama za jana ukiziongeza tena"
"Anhaa. sasa mimi shida yangu ni chumba cha kulala maana sina pakulala basi"
"Anhaa kwakuwa shida yako ni chumba nitakukodisha mimi nina chumba sikitumii nitakupa ulale humo hii laki moja inabidi ununue godoro kitanda kipo "
"Sawa inabidi tuongee na yule mzee maana ndio ananisaidia kufikiria ,hata jana kuleta ile simu kafikiria yeye mimi nikaenda kuichukua”.
“He is weird…!!” Alijisemea Peter
Alijikuta akimshangaa maana hajawahi kukutana na mtu wa sampo hio japo anajua kuna watu wenye matatizo ya kufikkria ambao kisayansi ni Dyscalculia yaani watu ambao hawana uwezo wa kusoma hesabu , watu wa aina hii mara nyingi huwa na matatizo ya kufikiria pia ndio maana Peter alishangaa baada ya kukutana na mtu huyo.
Usishangae sana kama kwenye jamii yenu kuna mtu ambae anajitahidi kusoma hesabu lakini kila anavyojaribu hawezi na huu ugonjwa au hali inaitwa Dyscalculia/Dyslexia na umegawnyika mara mbili kuna wale ambao wanakuwa nusu yaani Partial dyscalculia na Critical/complete yaani hawa hata moja jumlisha moja hawajui na hawa ndio mara nyingi wanakuwa hata kusoma hawajui na hata wajitahidi vipi hawawezi lakini pia wanaonyesha ishara(Signs and symptoms) za kutoweza kufikiria vyema(Intellectual disability), kwa mfano kuwa na tabia za kitoto au hata maongezi yao yanakuwa hayajanyooka .
Basi Peter aliongea na yule mzee na mzee yule alifurahi kwani kwanza hakutaka kukaa na Bahati kutokana na ukorofi wa mwanae pindi umletapo mtu asie mjua na hii ni kama kulipiza kisasi baada ya yeye na baba yake kunyanyasika kwa kipindi kirefu kabla hawajafanikiwa .
"Kwahio Peter utakuwa unanisaida kufikiria ili nijue jinsi ya kutengeneza hela"
"Poa usiwaze , yaani lazima utakuwa na pesa tu, panda twende nyumbani ukapaone ili tukatafute godoro maana kitanda tayari kipoo"
Walifika mpaka Mbezi Beach ambako ndio kijana Peter alipangishiwa Apartment nzima na wafadhili wake.
"Kwa hio unasema nitakaa hapa?"
"Ndio mimi nalala kule juu kabisa flour ya nne"
"Ndo nini hio flou?"
"Hahahahaha!..sema we jamaa unafurahisha eti flou ..haha."
"Umeona ukifika hapa una bonyeza kama hivi halafu unasubiria mlango ufunguke kama hivyo , halafu una bonyeza hii namba nne si unaiona hii , unaangalia kile kijitaa chekundu kikiweka namba kama ulio bonyeza mlango utafunguka na utakuwa umefika.....” Peter alimwelekeza jinsi ya kufungua lift mpaka akaelewa ndio wakaingia kwenye chumba cha Peter.
Kwaufupi Peter wafadhili wake walikuwa wakimpenda sana maana hata sehemu anayo ishi ilikuwa ni ya hadhi ya juu sana na wamefanya hivyo kutokana na kutarajia mambo makubwa sana kutoka kwa Peter kutokana na uwezo wake mkubwa wa akili.
Peter baada ya kumuelekeza Bahati kila kitu pamoja na kununua godoro alimwacha Bahati akiangalia Tv na yeye kwenda mpaka makao makuu ya benki ya X ambako aliambiwa kuwa ndio sehemu ambayo anafanya kazi Rania kama Assistant Manager( Meneja Msaidizi) .
Baada ya kufika nje ya jengo moja refu maeneo ya posta mtaa wa Samora alisimamisha pikipiki yaje na moja kwa moja aliingia ndani ya lift kwenye jengo hilo mpaka flour namba kumi na alienda mpaka sehemu ya mapokezi .
"Za saa hizi sister?? "
" Poa karibu tukuhudumie"
"Nimekuja kuonana na Meneja "
"Manager Msaidizi katoka kazini tayari"
"Kwani anatoka saa ngapi??"
"Anatoka saa tano "
"Okey sawa "Aliongea Peter huku akitoka bila hata ya kujua huyo meneja alitaka kuongea nae nini.
"Oya nimekuja muda mrefu kinoma nimemkuta mshikaji wako hapa simuelewi elewi kasema umempa chumba" Aliongea Steve baada ya Peter kurudi.
"Yeah ni kweli mzee ndio jamaa nilie kuwa nakwambia alisaidia kupata simu yangu , kasema anashida ya chumba cha kupanga ndio nikaamua nimpe hiki ambacho sikitumiii"
"Anhaaa... jamaa anaonekana mgeni sana kwenye mambo mengi"
"Atajua taratibu taratibu"
"Halafu jamaa bonge la Hb ila kakosa matunzo tuh"
"Ushaanza mambo yako , kwanza hebu nipe habari za yule mtoto Rania maana nimeenda mpaka anapo fanyia kazi ila sijamkuta "
"Sasa wewe umeenda kufanya nini?"
"Ujue hata sijui kilichonipeleka nimejikuta tu nimeenda na sikua hata na cha maana "
"Hahahha... ushaanza kuchanganyikiwa, ndio maana nilikuambia wale hutowaweza wewe tulizana tu na makomputa yako ndio unayoyaweza kuyatongoza yakufanyie unachotaka lakini sio binadamu"
"Wewe nipe taarifa zake , maswala ya kuweza au kutoweza niachie mimi"
"Sina taarifa, Ni kama nilivyo kuambia kuwa mtoto ni kisu hatari yaani ni mzuri balaa na uzuri wake umezidi kwa kuwakatalia watu wengi pale UD.., kajijengea heshima kubwa mtu wangu , kiufupi hajawahi toka na mtu wa aina yoyote yule mpaka sasa hivi japo hatujui sana ila ndo hivyoo.."
"Nataka nikafanye kazi ndani ya benki yao "
"Benk X unazungumzia"
"Ndio"
"Utaingiaje ingiaje pale wewe sio kila mtu anaweza kufanya kazi Benki "
"Naenda kufanya kazi kama IT"
"Sio shida , shida ni kivipi watakukubali kama IT wao, Unajua hapa tunazungumzia benki kubwa benki inayoingiza mabilioni ya faida kwa mwaka , wafanyakazi wa pale sio wamchezo mchezo ni wale wenye high qualified credentials"
"Nitawatengenezea tatizo halafu nitaenda kuomba kazi na hilo tatizo ndo litanipa kazi kwani nitatumia kama njia ya kufanya Interview "
"Tatizo gani"
"Nitajaribu kuhack system(kuchakachua mifumo) yao ya benk ,Najua nitaweza tu"
"Mzee hio ni htfari unaweza kupelekwa jera achana na huo mpango wako utajiharibia maisha kuna kitu kinitwa Cyber crime Act
"Wewe subiri utaona nina Plan zangu kama Scofield , wewe utaona"
Highlight:Cybercrime(Uhalifu wa kimitandao)ni uhalifu unaotokana na matumizi mabaya ya teknolojia au Tehama katika kufanya vitendo visivyokubalika kama vile kusambaza picha za ngono(Pornography Trafficking) ,wizi wa pesa mitandaoni au mali ,Kuiba uhusika(Identity stealing ),uchakachuzi(Hacking) na vitendo vyote ambavyo ni husianishi na matumizi ya Tehama.
Zipo sheria ( Tanzania Cyber crime Act 2015) zinazozuia au kupambana na uhalifu huu wa kimitandao , Hivyo kitendo chochote cha CyberAttack kitakupelekea kwenda jera na ni uhalifu kama uhalifu mwingine na sheria inasema hivi , “Kwa mtu yoyote atakaebainika au kukutwa na hatia ya kufanya kosa la wizi wa taarifa , uchakachuzi,au kuharibu taarifa , kusambaza virusi kwenye mifumo na makosa mengine husianishi adhabu yake ni kwenda jera kwa muda usiopungua miaka mitatu mpaka mitano au kulipa faini kiwango kisichopungua milioni kumi au vyote kwa pamoja.
 
SEHEMU YA 06

Steve hakutaka kupingana na rafiki yake huyo kwa sababu alikuwa anajua ni mbishi sana kwenye swala ambalo ashalifanyia maamuzi , alimuacha na kuangalia kile kitakacho tokea , lakini sio kuangalia tu pia alikuwa na hamu ya kuona kama kweli Peter atafanikisha kutembea na watoto wote watatu wa Tajiri Samiri Watoto wanao sifika kwa kuwa wazuri mtaa mzima wa ushuani .
“Halafu Steve hebu niambie umesema kuwa watoto wa tajir Samir ni watatu na ukasema kati yao kuna mzuri Zaidi, Je unamjua au kuwa na picha yake kama ulivyokuwa unampigia debe?”
“Hahaha… Aisee huyo demu anaeitwa Nasma wala hata simfahamun sema nilizisikia tu Habari zake kwa rafiki yangu mmoja hivi ambae ashahamishiwa Canada huko kimasomo”
“Kwa hio ha hajawahi kumuona?”
“Sio kuwahi kumuoana kiufupi hajulikani na ninacho sikia hata kwao hakai na hata watu wa huo mtaa hawamjui maana nasikia alivyokuwa mdogo alikuwa akivaa Nicab”
“Sasa hapo kazi itakuwa ngumu ila lazima nimfahamu tu , halafu si umesema kamaliza Six au?”
“Ndio kamaliza Form Six na anatarajia kuingia chuo , ila mimi nakushauri anza kwanza na Rania”
“Wewe nataka data zote nikianza kazi yangu nataka iende kwa mipango maalumu , vipi huyo mwingine?”
“Nani.. Najma?”
“Najma anafahamika bro sana kwa sababu ni mwanamitindo , ngoja nikuoneshe akaunti yake Insta ..”
“Hebu tuone” Steve alimuonesha Peter Account ya Instagram ya mwanadada huyo , jambo lilomfanya Peter apagawe kwa urembo wa Najma alikuwa mzuri balaa japo hakuwa na kalio kubwa ila alikuwa na shepu Fulani hivi ya kuvutia na kwa mavazi alioonekana akipigwa nayo picha yalimuonesha kuwa alikuwa na kipaji cha Umodel .
“Mzee sio poa huyu mtoto ni mkali balaa mzee sijapata onaa..”
“Wewe huyu mbona wa kawaida nasikia huyo Nasma ni kisu, ni mzuri hadi anaboa unaambiwa kila kitu kajaliwa mtoto”
**********
JNIA AIRPORT DAR ES SALAAM -1500HOURS
Ndani ya sehemu ya kutokea wageni ndani ya uwanja wa ndege wa dar es salaam alionekana mwanadada mmoja mrembo sana aliEvalia mavazi ya kileo ,alikuwa amependeza haswa hata baadhi ya wasafiri walio kuwa wakitoka eneo hilo walikuwa wakimkodolea macho kwani mrembo huyo alikuwa amebalikiwa haswa , viatu vyake flani vya mchuchumio(high Heels) Jimmy Choo Brand, huku akiwa amevalia kigauni kifupi cha Pink kilimfanya mwanadada huyo kuzidi kuonekana mrembo , huku pembeni akionekana mwanadada mmoja alie kauzu akiburuza begi na kwa muonekano wake tu alionekana kuwa huyo alikuwa ni msaidizi wa mrembo huyo . baada ya kutoka nje kabisa ya terminal 3 hatimae ilisikika sauti .
“Najmaaa… my Young sister” Alikimbiliwa na mwanadada mwingine ambae nae alizua gumzo kwa waendesha Taksi na hata pia wapita njia , kwani alikuwa ni mzuri haswa na kiufupi alikuwa kapendeza , alikuwa amevalia jeans brandi ya Levi`s na kijibrazia flani cha rangi ya Samawati huku akipendezeshwa Zaidi na viatu vyake vya High heels pamoja na saa ilioonekana kuwa ya thamani kubwa, alikuwa na nywele ndefu zilizomfunika shingo nyeusi za kung`aa na weupe wake kumuonesha kama mrembo flani hivi kutoka ufilipino.
“Jamani mdogo wangu nimekumisije .. halafu umekuwa mkubwa na kuzidi kuwa mzuri” aliongea” Na huyo si mwingine ila ni Rania na alionekana yuko mahali hapo kwa ajili ya kumpokea Najma.
“Dada uko peke yako?”
“Ndiyo baba na mama wamebanwa na majukumu ya kikazi na pacha wako usie mpenda nilimpigia simu ila kasema haji”
“Huyo nae achana nae bora umekuja dada yangu jamani nakupendaa .. nimekumisi sanaa..” Aliongea Najma huku akijidekeza kwa Rania.
“Hata mimi mdogo wangu twende nyumbani tutaongea vizuri tukifika nyumbani”
Basi baada ya hapo walingia kwenye gari na huku safari ilianza kuelekea nyumbani kwao Masaki na hawakuchukuwa muda mrefu hatimae waliingia ndani na kwa bahati nzuri wazazi wao walikuwa washarudi na walikuwa wakimsubiria .
“Waoh!.. mwanangu Najma” Alikumbatiana na mama yake na baadae akahamia kwa baba yake ambae muda wote alikuwa akimwangalia Najma kwa mshangao .
“Daadiii nimekumisi sana ..” Aliongea Najma na kumfanya baba yake atoe tabasamu na huku akionekana kama amekosa furaha .
“Karibu nyumbani mwanangu” Aliongea Samir au Baba Rania na kisha kuwacha waendele kupiga soga yeye akipandisha kwenda juu chumbani kwake .
“Daah! tatizo lingine limerudi na alivyozidi kuwa mzuri n fikiri nitakuwa na kazi ya ziada ya kufanya , ila huyu boya atakae bahatika kupata moja ya mtoto wangu na kumgonga jamaa atainjoi sana daaH!.. sijua kwanini Mungu kanipa wanawake tu ni kipimo kingine hiki” Aliongea Samir kwa hisia hukuaakisugua meno yake na kuonyesha wivu wa wazi kabisa juu ya Watoto wake .
“Mama mwanao umpendaye sijamuona hapa nyumbani” Aliongea Najma na kumfanya mama yake amwangalie kwa huzuni maana anajua Najma asivyo mpenda Nasma .
“Najma mwanangu nawapendeni nyie wote watatu kwa mapenzi sawa “
“Mama hata usiongee ulifikiri nakuonea wewe mwenyewe matendo yako ndio yanaongea”
“Najma twende ndani ukanionyeshe zawadi ulizo niletea mpenzi b ,utaniua kwa shauku mdogo wangu” Aliongea Rania ili kuvuruga ile mada maana hata yeye anajua kuwa mama yake anampenda sana Nasma kuliko wao wote , kiufupi Mama Rania alikuwa na mahaba mazito kwa mwanae huyo Nasma na hakutaka kabisa mwanae ateseke na jambo lolote lile na kila alichokuwa akikitaka alimpatia na mara nyingi aligombana sana na mumwe wake kwa kumpa uhuru Nasma lakini Samir alishindwa kwani Shani mke wake alisimama kidete katika kumtetea Nasma
Upande mwingine wa Maisha ya Rania aliishi akiwa mpweke sana na mpaka kufikia umri alio kuwa nao hakuwahi hata siku moja kuwa na Rafiki wa kiume zaidi ya rafiki zake wa kike tu , na hio sio kutokana kuwa alikuwa hapendwi , alikuwa akipendwa sana na wanaume wengi sana kwenye Maisha na kama ni wanaume kumuota Rania basi wengi wao nadhani walikuwa washazaa na Rania katika ndoto maana Rania katika shule zote alizo pitia mpaka alipo fikia hapo alipo aliacha historia kwa kuwa msichana mzuri sana na hata kwa sasa chuoni alikuwa gumzo , lakini jambo moja tu katika maisha yake ambalo lilikuwa likimkoseha raha ni kuachwa na kila mwanaume ambae anaonesha kuwa na nia ya kuwa nae na mwanaume wake wa mwisho kumuacha na kujiona kuanzia siku hio ana mkosi wa kutopendwa japo kajaaliwaa uzuri ni kijana Thomasi .
Kifupi Rania alitokea kumpenda Thomasi kijana alie kuwa akisoma nae hapo hapo chuoni UDSM ,lakini alijikuta siku moja akilia sana baada ya kijana huyo kumwandikia ujumbe wa maneno ambayo siku zote alikuwa akiyasikia kwa kila mwanaume ambae alitaka kuanzisha nae mahusiano au alionyesha nia ya kumpenda , pasipo kujua yote hayo mkandarasi alikuwa ni baba yake kwani kutokana na mapenzi alio kuwa nayo kwa Rania basi alikuwa akimlinda sana kiasi cha kila mwanaume atakae kuwa akimsogelea mwanae basi alimteka na kwenda kumpa vitisho , na hio ni siku kadhaa zilikuwa zimepita tokea Rania aanze mazoea na kijana Thomasi jambo ambalo kutokana na ucheshi wa Thomasi kumfaanya Rania afurahi sana lakini siku moja alipo achana na Thomasi wakati wakirejea nyumbani wakiwa kwenye gari moja yaani gari ya Rania na kumshusha katika kituo cha Moroco kwani kijana huyo alikuwa akiishi maeneo hayo basi ndio siku lilitokea tukio la kijana huyo kutekwa .
Wakati akishuka ndipo gari nyeusi yenye vioo tinted aina ya Verossa ilifunga breki kwenye miguu yake na akavutwa ndani ya gari kimya kimya na kisha kufunikwa kitambaa na kutishiwa kutotoa sauti ya aina yoyote ile la sivyo atamwagwa ubongo wake , baada ya gari ile kuondoshwa alikuja kufunuliwa kitambaa ndani ya jengo moja chakavu lililokuwa na vyuma vyuma vilivyozagaa hakujua mahali eneo alilokuwepo , ila mbele yake kulikuwa na wanaume ambao sura zao zilionyesha uadui..
“Kijana unamjua huyu?” Aliuliza jamaa mmoja mwenye midevu alievalia suti na miwani,
Thomasi alitingisha kichwa baada ya kuona picha ni ya Rania
“Sasa hatutaki kupoteza muda kiufupi sisi hatutaki kujua mahusiano yako na huyu mwanamke ila kuanzia leo hakikisha humsogelei tena kwenye Maisha yako ,kama unapenda kuvuta oksijeni na hili ni onyo endapo utaonekana nae tena basi jua utaitwa marehemu , na ukitoka hapa usjie kumwambia kuna watu wamekuteka na hilo ni kosa lingine , na sharia inayotuongoza kwa watu wambea ni kifo kwa njia ya kunyongwa .. umesikia?”
“Ndio sitorudia tena”
Basi baada ya kupigwa mikwara ya kutosha alirudishwa kwa mtindo ule ule na kisha kwenda kushushwa eneo lile lile alipo chukuliwa , Thomas hakuamini kama amenusurika maana alijua ilikuwa ni mwisho wake na asingeweza kumuona mama yake alieko huko kijijini anaemtegemea kwa vingi.
“Aisee simsogelei tena yule mwanamke na kwanzia leo nafuta kila kitu kinacho muhusu” Aliongea Thomasi huku kwa mawazo alijikuta yupo nje ya geto lake
Siku ambayo Rania alikuwa na furaha kwa kumpata Thomasi na kuona Maisha yake yanaenda kuwa na furaha ni siku ambayo hakuisahau katika Maisha yake ni baada ya kusoma ujumbe mfupi wa maandishi kutoka kwa Thomasi.
“Rania naomba unisamehe ila kwanzia sasa naomba ukae mbali na mimi na fanya kama hunijui naomba tafadhari sikupendi kabisa ,Nimegundua wewe ni mkosi katika maisha ya watu“
Maneno hayo yalimfanya Rania atoe kilio cha kwikwi na mama yake alienda na kuchukua simu na kusoma ujumbe ule hakika hata yeye mwenyewe aliumia baada ya kuusoma , alijitahidi kumbembeleza Rania ili atullie lakini hakufanikiwa ndipo kwa hasira alitoka na gari mpaka ofisini kwa mumewe .
“Hivi mume wangu mbona unapenda kumfanya Rania asiwe na furaha eh , mbona unapenda alie , nakuuliza wewe , mpaka lini utaacha kumfatilia mwanao” Aliongea Mama Rania kwa hisia baada ya kuingia ofisini humo bila hata ya kugonga mlango.
“Mama Rania nadhani swala hili tushaliongea wewe mahaba yako yapo kwa Nasma na ya kwangu yapo kwa Rania sasa naomba tusiingiliane katika hili na kama unataka niache basi kubali Nasma afanye kile nikitakacho” Aliongea Samir na kisha kuendelea kuangalia tarakishi yake ya kampuni ya Apple na Shani au Mama Rania hakuwa na jinsi zaidi ya kutoka kwani udhaifu wake ulikuwa kwa Nasma na mume wake alijua kuutumia udhaifu wake vizuri , hakuwa na jinsi zaidi ya kukaa kimya na kumhurumia mwanae.
Upande wa Rania kwanzia siku hiyo hakutaka kabisa shobo na mwanaume wa aina yoyote ile na aliapia hatokuja kumruhusu mwanume kumshobokea kwani aliona ni kukaribisha maumivu ndani ya moyo wake tu , jambo ambalo lilimfurahisha sana Samiri na kuona sasa tofauti na ile nguvu ya kutumia kumlinda mwanae sasa imepungua na Habari za kufrahisha zilikuwa zikiletwa na kijana wake Pierre mwanafunzi ambae analipwa kwa kazi ya kumfatilia Rania awapo chuoni. .
“Bossi aisee leo kuna boya kapigwa chagga(kukataliwa) na mwanao hatari huwezi amini kilicho tokea” Aliongea Pierre baada ya kuingia ofisini hapo na kuanza kuhadithia ..
****
Masaa matatu nyuma kabla ya Rania kwenda kumpokea mdogo wake.
Alikuwa chuoni ndani ya kikao cha Wanafunzi na serikari yao(DARUSO) kwa ajili ya kuzungumzia sherehe ya mahafali ya wanao hitimu , baada ya kikao hicho kuisha ndani ya ukumbi wa Nkurumah hall .watu wote walitawanyika lakini ile Rania alipo toka nje ya ukumbi huo ndipo kioja cha mwaka kilipo tokea na hii ni baada ya mwanaume mmoja mtanashati kuingia kati kati ya watu na kisha kupiga goti huku akiwa ameshikilia maua mbele ya Rania na kufanya jambo lile liwe kivutio kwa wanafunzi wote walio kuwepo eneo lile .
“Rania naomba uwe mpenzi wangu tafadhari nakupenda sana naomba unikubalie mwenzio nateseka sana juu yako naomba unipokee ..” Ni baadhi ya maneno yalio mtoka kijana huyo huku akiwa amenyoosha ua kumkabidhi Rania kama anapokea Sakramenti ya Ubatizo ubarikio kwa jinsi alivyopiga magoti , lakini jambo la kushangazwa na lilo acha gumzo ni pale Rania alipochukuwa yale maua na kumpiga nayo yule kijana usoni na kisha kumwambia
“ UNIKOMEEE” na kisha kuondoka , jambo lile lilikuwa ni jambo la kushangaza sana alilo lifanya Rania na ukizingatia yule kijana alionekana mpole na alijulikana kuwa ni mtoto wa Gavana ya benki kuu ya Tanzania(BOT) kijana aitwae Damsoni.
“Hahahaha. Daah! , aisee mimi ni ninja p , Rania kanifurahisha sana yaani kesho kutwa naenda kumnunulia gari jipyaa la milioni mia nane Rolls Royce , yaani mwaka huu watachezea chambavu sanaa yaani daah!.. yajayo yanafurahisha” Alijiongelesha Samir baada ya kushuhudia video nzima ya kilicho tokea.
***********
“Oya wewe bwege umelala mpaka saa hizi hata chuo hujaenda unakosa uhondo na muvi za kifilipino” Aliongea Steve na kumfanya Peter alieamka kivivu ,maana siku hio hakwenda chuo kabisa .
“Ushaanza mambo yako mzee , ngoja kwanza ni kanywe maji” Aliongea Peter huku akitembea akielekea sebuleni ambako alimkuta Bahati masumbuko akiangalia katuni huku akipiga miayo .
“Mzee hutoaamini hii muvi ina muhusu Rania mzee” Aliongea Steve na kumfanya Peter aache kumimina maji kwenye glass na kukimbilia simu alio ishika Steve na kuikwapua na kasha kuplay video.
“Hahahahahahaha.. daah! .. huyu jamaa ni falaa” Peter alicheka sana na kumfanya Steve nae aanze kumuunga mkono kwenye kucheka na Masumbuko alivyo ona wezake wanacheka na yeye bila kujiuliza mara mbili mbili nae akaunganiasha na kuanza kucheka.
“Safii sana” Aliongea Peter na kumfanya Steve aache kucheka na ashangae
“Mzee nini sasa kama na wewe unataka kuwa maarufu sasa mfuate huyu demu”
“Steve hizi ndo type zangu sasa na kuanzia sasa ninaanza misheni rasmi, kwanza kanifurahisha sana , safiii” Aliongea Peter na kumfanya Steve amuone Peter ashaanz kuwehuka
“Mama endelea kunitunzia bikra yangu hio ,mwezi huu naitoa” Aliongea Peter na kumfanya Steve aendelee kumshangaa mwenzake na kuona sasa kichaa cha Malaria kishaanza kumpanda Peter.
Highlight:parental favouritism(Upendeleo wa wazazi au mzazi kwa mtoto zaidi ya wengine),Mzazi au wazazi kumpenda mtoto mmoja tofatuti na mwingine ni jambo ambalo linatokea bila kuelewa (Unconscious),wanasaikolojia wanasema kwamba kumpendelea mtoto mmoja zidi ya mwingine halihusianishi na mapenzi (Doesn’t involve in loving one more than onother),Lakini pia tafiti zinaonyesha kwamba upendeo kwa mttoto mmoja una athari kubwa sana kwa mtoto ambae hapati mapenzi sawa na mwingine.
Ushauri :Wazazi kuweni makini sana na tabia zenu katika kuwalea watoto kwani swala hili sio swala la kuchukulia mzaha , lina athari kubwa sana kwa watoto moja wapo ni kupelekea watoto kutopendana kwa kuoneana wivu.
SEHEMU YA 07
" Najua Rafiki yangu wewe hausadiki maneno yangu ninayo kuambia , hivi unafikiri kwanini kampuni kubwa kama ile imeniamini na kunisomesha mpaka kufikia hapa” Aliongea Peter
"Najua Rafiki yangu wewe kwa upande wa kichwa uko izuri, lakini jaribu kutofautisha hivi vitu viwili mapenzi na akili za darasani , mapenzi hayajawahi kumuacha mtu salama hata wewe najua unafuatilia historia za watu walio kuwa na akili sana duniani , lakini wote hao walikuwa wakiteswa na mapenzi”
" Umeongea fact , lakini mimi kwenye Maisha yangu sitaki kujilinganisha na watu wengine , ili kumpata mwanamke siku zote unatakiwa ujaribu kuendana na mazingira anayopenda na ukifanikiwa hilo lazima ujitahidi kuishi Maisha kidogo sio yako kama unataka kumpata kila mwanamke ,lakini pia ukishagundua tatizo kuu la mwanamke ni nini huo ndio utakuwa udhaifu wake”
"Wewe jamaa kwa hio unaamini unaweza kupata kila mwanamke kama tu utaendana na mazingira yake”
"Ndio kabisa ndo maana wanaume ambao mara nyingi wanapenda kuonyesha uhalisia wao halisi out of true love ndio wanaongoza sana kwenye kuachwa na wanawake na kuishia kuumia , sasa wewe ngoja nitakuonyesha jinsi nitakavyo wachengua akili hawa wanawake wa huyu mwehu alie nidhalilisha , nitahakikisha anajuta kwa kitendo kile , lakini pia nataka nimfundishe yeye kazi yake ni kuzaa tu na kuwalea watoto kwenye mazingira bora sio kuwalinda wasiwe na wapenzi”
"Sawa wewe kwa ubishi nakuelewa Sana , Sana yaani ndio maana nakuacha ufanye unavyotaka japo sitaki uingie kwenye matatizo , ila kuwa makini tu yule mzee ana watu wanawafuatilia wale Watoto mimi nakutahadharisha tu”
"Sikia Steve , unajua wewe ni Zaidi ya Rafiki yangu na tumetoka mbali sana na ndio ulikuwa kama mtu wangu wa karibu nipatwapo na matatizo , lakini nataka nikwambie tu yaani hata sielewi kitendo cha yule boya kunidhalilisha kisa demu kinaniuma sana yaani , kinanifanya nakosa hata usingizi na sijawahi kuhisi hivi kabla , lazima ajutie kunifanyia vile”
"Daah! sawa mimi nakupa ushauri kuwa tu makini , lakini pia kumbuka visasi sio vizuri kabisa vinaweza kukupelekea kwenye matatizo makubwa”
"Hilo naelewa mshikaji wangu ila usiwaze mimi kuna upande wangu wa pili bado haujaujua , ila utanielewa soon”
"Halafu Bahati umekula tokea asubuhi” Aliuliza Peter huku akimwangalia Bahati alie kuwa akiangalia katuni.
"Sijala chochote, sina hela na uliniambia utanisaidia kufikiria ili niweze kupata hela”
"Hahahaha.. Peter huyu mshikaji anavituko eti utanisaidia kufikiria…” Aliongea Steve akimwangalia Masumbuko.
"Halafu hata uso hajanawa , umesikia sasa chukua hizo pakiti moja ya tambi kwenye kabati la jikoni pika na chukua juice ule mimi kuna kazi nafanya” Aliongea Peter na kumuacha Steve na Bahati pale sebuleni na \steve
"Oya broo nisaidie kupika basi” Aliongea Bahati
"Halafu wewe mshikaji unanionaje?, mimi najua kupika na kazi zote za nyumbani ila mama aalivyo mleta House girl sijawahi kupika na kufanya kazi za nyumbani”
"Kwani housi geli ni nani?”
"Wewe jamaa mshamba sana , ni mtu yoyote anaejua kupika na kufanya kazi za nyumbani”
" Anhaaa.. hapo nimekuelewa "
Bahati ajijikuta akianza kuwaza maana hata hizo tambi mwenyewe hata hazijui zikoje na kupika si ndio mtihani kabisa na kiufupi alikuwa mvivu sana kwenye kupika na maswala ya kazi ndogo ndogo za nyumbani , ila alitabasamu.
"Huyu si amesema hausi geli ndio anajua kufanya kazi na kupika basi hata yeye ni hausi geli” Alifikiria Masumbuko kwa lugha yake mbovu na kisha alimgeukia Steve ambae alikuwa akiweka simu yake mfukoni kwa ajili ya kuondoka.
"Broo" Aliita Bahati na pale pale akamkonyeza .
Steve aliweka begi chini na kila kitu na kuanza kufanya usafi pale sebleni na kupanga kila kitu vizuri, huku Bahati alikuwa akitabasamu tuu na kuendelea kuangalia katuni akiwa amejichanua kwenye sofa.
Peter alikuwa yupo chumbani kwake alikuwa kuna baadhi ya vitu kwenye laptop yake anavifanyia kazi, lakini alianza kuvutiwa na harufu nzuri ya vitu kukaangwa maana alikuwa ameacha mlango wazi.
"Huyu dogo kumbe anajua kupika namna hii , ana maajabu mengi sana ya kufurahisha” Na ile harufu ilizidi kusambaa maana madirisha yalikuwa yamefungwa , jambo lilo mfanya Peter njaa kuanza kumtekenya , kitendo kilicho mpelekea kukosa uvumilivu na kujikuta akitoka kuangalia kunapikwa nini , lakini alishangaa maana B?ahati alimkuta sebleni akiangalia katuni.
"Wewe Masumbuko demu wako kaja nini mbona kuna chakula kizuri kina kaangwa huko, halafu kumbe upo vizuri hapa sebleni pamependeza”
"Ni hausi geli” Aliongea Bahati na kumfanya Peter ashangae , lakini wakati anafikiria huyo hausi geli kabla hajauliza swali lingine ndipo alipomwona Rafiki yake akiwa kavaa Aproni na kijikofia cha kipishi huku akiwa amebeba sahani ya tambi na nyama za kukaanga na kuleta mpaka kwenye kijimeza.
"Mabosi zangu leo nimechelewa mnisamehe nimechelewa kuwapikia chakula” Aliongea Steve kwa adabu , jambo lililo mfanya Peter kwanza amwangalie Rafiki yake anavyo ongea , alijikuta akishangaa na wakati akiendelea kumwangalia alimwona Steve akienda kutoa juice.
"Ahhahahahahaa.. haha uwiiiii.. eeee..steve .. hahaha dahh we jama wewe ahahaha.. mama ..aaaa” Peter alikuwa akicheka hadi mbavu zinauma.
"Bossi chakula tayari aliongea Steve jambo lililomfanya peter afungulie kicheko cha nguvu mpaka kushika tumbo huku machozi yanamtoka , sio yeye tu hata Bahati japo alikuwa anajua alicho mfanyia mwenzake lakini na yeye aliungana kucheka , na kumfanya Steve nae aunge kucheka.
"Daah! .. mwanangu Steve wewe ni bonge la muigizaji aisee daah!.. . kaka unajua” Aliongea Peter pasipo kujua kuwa mwenzake akili ishapumbazwa muda na bahati . Baada ya Peter kucheka mpaka kuchoka ,.
"Sema mzee unajua pia kupika hadi nimeumwa njaa” Aliongea Peter huku akiisogelea sahani , kwani Bahati tayari alikuwa akila tambi kwa fujo.
"Mabossi zangu mimi naenda sokoni kununua nyanya na vitu vingine maana vimeisha nataka nikanunulie soko la tegeta”
Peter alijikuta akipaliwa na kuanza kucheka upya
"Kwa hio .. hahah.. daah.. hahaha .. Steve bhan hela hii hapa hahaha.." Huku akitoa elfu ishirini , na peter alijua wote huo ni utani tuu Steve aliamua leo kumuigizia maana alikuwa anamjua sana Steve kwenye maswala ya utani , lakini alijikuta akitoa jicho baada ya kumuona kweli anaondoka .
"Wewe steve acha ujinga bwana .. cut… cut” Aliongea Peter akimwambia akacut . yaani kuacha kuendelea kuigiza . lakini Steve alitokomea kwenye lift.
Sasa Peter alijikuta akimuacha tu kwakuwa alijua atarudi muda si mrefu lakini kadri muda unavyo songa hawakuweza kumuona Steve, Peter alijikuta akipatwa na wasiwasi kwani kuna jambo aliona haliko sawa ila alipuuzia maana aliona ni matani ya Steve.
Bahati yeye baada ya kushiba alijikuta akipitiwa na usingizi pale pale juu ya sofa ..
Huku upande wa Steve alifika sokoni na kununua kila kitu na kisha kwenda sehemu ya kupandia magari bahati nzuri alipata gari la Bagamoyo kwenda kawe , alipanda baada ya kupanda kulisikika ving`ora kuashilia kuwa kuna kiongozi anapita lakini baada ya nusu saa magari yaliruhusiwa lakini msongamano wa magari ulikwa mkubwa na wakajikuta wakipoteza lisaa na kama dakika tano hivi , ndipo steve alipo jikuta akili ikimrudia na kujishangaa amebeba kapu la nyanya na vitunguu na vitu vingine , alianza kuvuta kumbu kumbu lakini hazikuja kabisa na kumbukumbu ya mwisho alikumbuka alikuwa kwa Rafiki yake na alikuwa anaongea na Bahati.
Alijikuta kama amechanganikiwa na kuanza kujiongelesha mwenyewe hadi watu wakamshangaa
"Hapana kuna mchezo nimechezewa yule dogo lazima atakuwa mchawi , aisee nitakacho mfanya ngoja"
Bahati nzuri magari yaliruhusiwa na walikuwa wapo mbuyuni na zipita dakika chache alikuwa akiingia ndani ya geti ya nyumba anayoishi Rafiki yake huku akiwa na mfuko wake wa nyanya akitembea utadhani hatofika .
*******
GLOABAL RESEARCH &TECHNOLOGY CORPOTATION {GRTC}
GRTC ni kampuni ambayo ilikuwa ikijihusisha na maswala ya tafiti mbali mbali katika maswala yote ya mazingira na maswala ya kiteknolojia na kazi yao kubwa ilikuwa ni katika swala la kuendeleza(maintainance ) , kujaribu(Testing) na kupambanua (Test and evaluation ) na pia katika kutoa huduma na vifaa vyenye uwezo mkubwa katika maswala ya kufanya tafiti mbali mbali duniani .
Kampuni hii yenye makao yake nchini marekeni katika jimbo la Virginia iliamua kuunganisha nguvu zake katika maswala yake ya utafiti na kampuni kubwa za utafiti katika bara la Africa na Asia mabara ambayo katika swala zima la utafiti yalikuwa yakikuwa kwa kasi kubwa sana na hii yote ni kutokana na kuimarika na kukua kwa kasi kwa teknolojia katika mabara haya na pia katika michango yao mbalimbai mbali ya kuzuia majanga na kutabili mambo ya hali ya hewa na pia katika kuibua vipaji vingi katka maswala ya ugunduzi(innovation).
Miaka ishirini nyuma ndio mwaka ambao kampuni hii ilipoingia nchini Tanzania kwa kusaini mkataba na kampuni kubwa ya maswala ya kiteknolojia Africa ijulikanayo kwa jina la EARTH TECH INC. kampuni ambayo makao yake makuu yalikuwa katika jiji la Arusha nchini Tanzania , kampuni hii ambayo ilikuwa ikimilikiwa na mwanamama Proffesa Gladness Rafaeli Mswaki, mwanamama alie kuwa gumzo miaka iliopita na kupelekea kuwa na vugu vugu la uvunjaji wa haki za binaadamu katika nchi ya marekani na Africa , vuguvugu lillidumu na kuja kufikia tamati baada ya nchi kubwa dunniani kutoruhusiwa kuingilia maswala ya kisiasa na ya kiungozi katika mataifa ya Africa.
Lakini pia mwanamaa huyu alieleta mapinduzi makubwa sana ya kiteknolojia katika bara la Afrika na kuchangia katika uvumbuzi wa vipaji vingi sana vya wanafunzi walio kuwa na uwezo mkubwa wa kufikiria na katika maswala ya ki uvumbuzi katika medani mbali mbali .
Mkataba huu ulikuwa na dhumuni kubwa la kushirikishana tafiti mbali mbali mbali zinazohusu afya , maswala ya kiteknolojia , na mambo ya utabiri wa hali ya hewa na pia katika kuhakikisja dunia inakuwa sehemu salama . hayo ndio madhumuni makubwa ya mkataba huu ambao ulikuwa ukiangaziwa na mashirika makubwa duniani yakiwemo NASA,UN,CIA,RAW,R&J,SPACE X na mengine mengi na ufadhili huu ulikuwa mkubwa kutokana na kwamba mataifa mengi waliamini mashirika haya yanaenda kuleta mageuzi katika maswala ya kiteknolojia kupitia tafiti mbali mbali katika ngazi zote ambazo zitafanywa tafiti.
Kampuni hii iliingia kwenye mpango wa utafiti mkubwa ambao uikuwa ukiaminika kuwa endapo utakwenda kukamilika utakuja kuleta mapinduzi makubwa ya kiteknolojia kwa ujumla wake na utafiti huo ulikuwa ukihusu kutua(landing) kwa kiumbe kutoka galaxy(nje ya mfumo wa jua ) nyingine kiumbe ambacho kitaalamu kinajulikana kwa jina la Allien yaani kiumbe kutoka nje ya dunia na kupitia tafiti za awali zilizo kuwa zimefanywa na kampuni hii miaka minne nyuma waligundua kuwa kiumbe hiki kilitua katika upande wa bara la Africa katika nchi ya Tanzania mpakani na Kenya , na hizi ni taarifa kutoka kwa tafiti ambazo bado hazikuwa na Ushahidi wa kutosha wa kulithibitisha swala hilo na tafiti hii ilifanywa miaka mitano nyuma na kupitia ripoti iliotumwa na timu ya wana anga(Astronauts) waliopo katika kituo angani (International Space Station) taarifa zilisema kuwa kifaa kilichokuwa kimebeba kiumbe hiki kilionekana katika Rada zao kwa dakika moja na sekunde saba tu na kilionekana kikiingia katika anga ya chini(Atmosphere) kabisa ya dunia na kuhusu taarifa kamili ya uelekeo ilionyesha Afrika katika nchi ya Kenya na Tanzania lakini bado jambo hilo halikuwa na uhakika kutokana na spidi ya kifaa hicho.
Lakini kutokana na nadharia nyingi sana ambazo wanasayansi wengi walikuwa nazo kichwani moja ya nadharia hizo ni moja ya mwanasansi Stephan Hawking kwamba viumbe hawa wanakuja duniani kwa ajili ya kujidharisha (reproduce ) kutokana na kwamba wao hawana uwezo mzuri wa kukiendeleza kizazi chao katika sayari walizopo hivyo basi walikuwa wakija duniani kwa ajili ya kupata msaada huo(incubation help) , lakini pia ipo nadharia nyingine inayo sema kuwa viumbe hawa wapo kwenye mpango wa kutaka kuitawala dunia hivyo njia ambazo wanaona ni sahihi basi ni njia ya kutaka kuufanya ulimwengu kuwa na viumbe wenye uwezo mkubwa kiakili ili uweze kuwasaidia katika kazi yao hiyo , hio ni moja ya nadharia ya kusadikika pia hii ilithibitishwa na mwanasayasni mmoja mtafiti akihusisha uwezo wa kufikiria wa binadamu wa karne ya sasa na ukuaji wa teknolojia kuwa ni vitu viwili tofauti , lakini ipo moja ambayo ndio ilio Amsha shauku ya wanasayansi duniani hii inasema kwamba kama tu viumbe hao watatua kwenye dunia au kupita na sehemu hio kukawa na mama mjamzito wa miezi ilio chini ya mitatu(First Trimister) basi kuna uwezekano wa kiumbe hicho kitakacho zaliwa kuwa na akili nusu ya viumbe hao katika kufikiria , jambo hili ndio jambo lilo iinua marekani kwa kutumia kivuli cha kampuni ya GRTC kuingia mkataba na kampuni ya EARTH TECH INC ya Tanzania huku wao katika uhalisia wakiwa kama wafadhili wa mpango huo.
Kampuni ilio chini ya profesa Gladness na yenyewe ilivutiwa na taarifa hii na hii ni kutokana na uthibitisho wa picha kutoka NASA zilizo kuwa zikionesha kiumbe hiko kikiingia katika anga ya dunia nI picha zilizo rekodiwa na kituo cha wana anga ISS (International Space Station) ndipo profesa huyu alipo shawishika katika kuingia mkataba na kampuni hii kwa kuamini kuwa endapo jambo hilo litafanikiwa basi kmpuni yake na Africa kwa ujumla itaingia katika ushindani mkubwa wa kiteknolojia na kutoa ile kasumba juu ya waafrika kutowategemea wazungu kwa kila kitu, ndipo mwanadada huyu kupitia kampuni ya baba yake na mama yake alipowashauri kufadhili wanafunzi wote nchini ambao wataonyesha uwezo mkubwa darasani kwa shule zote huku akiamini kama kweli nadharia hio itakuwa ya ukweli basi lazima angefanikiwa kumpata huyo mtoto mwenye uwezo mkubwa wa akili ,lakini hili wanasayansi wengi hawakuzingatia athari za viumbe hao kama kweli tu watakuwa wamebainika au kuthibitishwa kama ni kweli wapo, wengi waliangalia faida zitakazopatikana na upatikanaji wa mtu mwenye akili nyingi ambae atasaidia katika ukuaji wa Teknolojia.
Lakini baada ya miaka ishirini kupita siku ya leo ndo walikuwa kwenye kikao cha juu ya utafiti huo ulio hudhuliwa na wadau mbali mbali duniani katika maswala ya teknlojia akiwemo Jeff Bezos ,Elon musk , Billgeti wa Microsoft na wengineo wengi na kikao hiki kilikuwa kikifanyika katika ukumbi mkubwa wa kampuni ya R&J company ulioko Dar es salaam.
Na hii ni kutokana na wau wengi kuvutiwa na Roboti lililokuwa chini ya kampuni ya EARTH TECH INC , roboti lilokuwa likifanana kwa asilimia sabini na tisa na binadamu na siku hio lilitazamiwa kuwa ndio litakuwa linasherehesha mkutano huo wa wana jumuia ya sayansi Duniani..
" Ladies and gentlemen now we are moving on, to the main point of our Agenda ,I would like to welcome Professor Gladness to read Research Report”
Ailongea roboti A2 ambalo ndo lilikuwa host(Muongeaji) na hapo hapo Gladness alitoka akiwa kapendeza kweli kweli pamoja na uzuri wake usioisha hamu ya kuutazama .
Gladness alisoma ripoti ile na mwisho alisema kuwa kutokana na uchunguzi ulio fanyika kupitia ufadhili wa wanafunzi katika vitendo na nadharia ni wanafunzi kumi na wote wanatofautuna na uwezo wao kidogo sana na wanafunzi hao ni Peter..,Hashim,na Steve….
Uhusiano wa ripoti huu ulitokana na pendekezo la kwanza kuangalia mwenendo wa kuibuka kwa wanafunzi wenye akili kama swali la utafiti ripoti.
“…… hivyo basi hitimisho tulilo fikia ni kwamba kuna uwezekano wa kutokuwa na mwanamke aliekuwa mjamzito wakati kiumbe hicho kina pita au p kiumbe hicho hakikupita kabisa katika maeneo yalio fanyiwa uchunguzi , au makisio ya ndharia yalikuwa sio sahihi (failing of hypothesis).
Mapendekezo yake yakawa ni kufanya utafiti zaidi ili kuja na suluhu ya kufumbua fumbo hilo gumu. Hayo ndio maneno yaliomtoka Gladness na kuwanyong`onyesha wafadhiri.
"Madam una mpango gani juu ya hili” Aliuliza Merry ambae alikuwa ni msadizi wake
"Nimeandaa mpango na nina uhakika asilimia mia moja utakwenda kukamilika aliongea Gladness huku akipotelea nje kabisa .
**********
Baada ya Rania kuchukuana na mdogo wake Najma na kupewa zawadi alizo ahidiwa na mdogo wake huyo alijikuta wakifurahi sana .
" Hivi dada bado tuu hujapata mchumba?” Aliuliza Najma na kumfanya Rania apoe ghafla
"Mdogo wangu wewe acha tuu naona kama nina mkosi katika kupata wanaume kwani kila mwanaume alie kuwa akinitongoza leo, kesho ananiambia hanitaki , sasa hivi nimeridhika na hali yangu ya kutokuwa na mwanume kabisa sitaki kuumia tena”
"Dada pole ila nina uhakika utapata mwanaume hivi karibuni”
"Mimi sitaki tena wanaume nimeshakata tamaa na ninacho mshukuru Mungu ni kwamba wanaicha kabla ya kunitumia”
"Khaa dada ina maana bado wewe ni bikra”
"Ndio wewe ishatoka”
"Mimi bado kusema ukweli sijapata kuona typu(aina) yangu mpaka sasa , na wanao nitongoza wote nawapiga vibuti”
"Kwa hio mdogo wangu we unataka type(aina) gani labda”
"Mimi nataka mwanaume anaendana na mimi na asie na tamaa kabisa kwani sitaki wanichezee”
“Kwa hio wote uliokutana nao hakuna type yako ?”
"Kwakweli sijaona , lakini pia sitamani mwanaume wa kiafrika nataka wanaume wa kihindi hindi tuu”
"Hahaha .. mdogo wangu sasa hao wahindi hindi utawapata wapi si bora uende huko uhindini”
"Ndio nitakuwa naenda maana nawapenda sana wanaume wa kihindi naamini lazima nitampata”
"Wewe na Nasma mmejiwekea vipingamizi vikubwa kwenye Maisha yenu mtakosa ndoa”
" Kwani dada unataka uniambie Nasma bado hana bwana”
"Amtoe wapi na wakati hata kukutana na wanaume hataki na wote walio mtongoza kawakatalia , yaani ni mgumu hataki kabisa mazoea na mwanamme wa aina yoyote ile” .
"Hahahah daah! hii nyumba jamani kwahio sisi wote mabikra na halafu wazuri , jamani ni maajabu na hakuna atakae amini hata umwambie”
" Ni kweli hawawezi kuamini”
**********
"Wewe , mwehu umenifanyia nini muda ule ukanipumbaza akili yangu eh?, nakuuliza” Alikuwa ni Steve aliekuwa akipiga makelele huku akiwa amemshika tai Bahati jambo lilo mkurupusha Peter na kuja sebuleni,kwanza alitaka kucheka ila alijikaza .
"Vipi Steve maigizo yako yameisha?”
"Huyu boya lazima atakuwa mchawi kuna kitu kanifanyia na kunipumbaza akili” Aliongea kwa jazba huku akizidi kumkaba Bahati pale chini ya sofa .
"Mpaka aseme alicho nifanyia , sema wee boya wewe mchawi umenifanyia nini na kuiharibu akili yangu?”
"Inamaana Steve sio kama yote uliokuwa ukiyafanya hayakuwa maigizo ilikuwa uhalisia”
"Sio maigizo mimi ninacho kumbuka nilikuwa najiandaa kutoka hapa nyumbani kwako niende home sasa huyu boya kaniomba nimpikie nikakataa na akaniangalia usoni akanikonyeza ndio nimekuja kushtuka nipo kwenye gari na kapu la nyanya , leo lazima aniambie yeye ni nani na kama ni mchawi namua hapa chini”
"Ngoja nasema” Aliongea Bahati kwa sauti ndogo maana alikuwa akikabwa sana na kukosa pumzi ndipo Steve alipomuachia.
“Haya sema”
"Mimi sio mchawi lakini nimezaliwa na uwezo wa ajabu wa kuufanya ubongo wako kutofanya kazi kama kawaida na kuupa mawazo nitakayo mimi kwa muda flani ndio akili zako zinapo kurudia na nina fanya kwa kuchezesha macho tu” Aliongea Bahati na kumfanya Steve na Peter washangae kwa kutoamini.
"Wewe jamaa sio uwezo wa ajabu huo ni uchawi umerithishwa ila hujui tu” Aliongea steve
"Ni kweli mimi sio mchawi”
"Tutaamininije kama wewe sio mchawi aliongea peter?”
“Wewe si umesema utanisaidia kufikiria , basi fikiria jinsi utakavyo amini”Aliongea Bahati
"Huo ni uchawi lazima , ila nimepata wazo Peter” Aliongea Steve na kumfanya Peter amwangalie .
" Unaonaje tukampeleka kanisani akaombewe?”
"Hapo ni kweli ila mimi la kwangu ni tofauti kidogo , kama kweli yeye sio mchawi tunataka akalifanye jambo hilo kwa mchungaji ambadilishe mawazo yake”
"Hapo kweli Peter . yeye si amesema kila anacko kitaka mtu afikiria anaweza kumfanya mwingine afikirie, basi tumpeleke kwa Mwamposa akamfanye afikirie kutupa sadaka zote za jumapili”
" Hahaha.. sema wewe mjinga mawazo yako daa” .
" Sio mawazo yangu mimi nina uhakika huyu ni mchawi kwa alicho nifanyia hapana aisee na kwa Mwamposa alivyokuwa na nguvu za Mungu yule lazima akakamatike”
“ Oya Bahati wewe ni Rafiki yangu na kuamini , unauhakika kuwa wewe sio mchawi ?”
" Ndio mimi sio mchawi na twende kwa huyo mchungaji uone asiponipa sadaka zote”
"Hahaha daah! yaani leo nyie mnanifurahisha kweli , kwahio Steve tumpeleke kwakuwa kataka mwenyewe ila mimi siliafiki mia kwa mia”
"Wewe bwana kama hutoenda nitampelekea mimi na kuhusu mipango ya kuonana na mchungaji nitamtumia mama yangu maana anajuana na Mama mchungaji”
" Kwa hio lini tuna mpeleka?”
"Kesho kutwa tena nasikia makonda atakuwepo”
"Basi hakuna shida .. ila hii itakuwa hatari ila lazima tuwe na mpango wa kulifanya hilo” .
"Nyie fikirieni tu ikifika mtaniambia nikachukue hilo kapu la sadaka muone



Wasilialia nami kwa kugusa hapa

ITAENDELEA
 
Simulizi ndefu hii hio ni table of contect
Screenshot%20(7).jpg
 
SEHEMU YA 08

“Profesa unaweza kunidokeza kwa ufupi kile ambacho unaenda kufannya juu ya kumpata huyo mtu kwani naona wawekezaji hawajaridhika na majibu ulio wapa?” Aliuliza secretary wa Profesa Gladness .
“Mery kwa sasa siwezi kulizungumzia swala hili , ila kuna Signal Pattern ambazo ninahitaji kuziingiza kwenye system ya Nimrod na nadhani nitapata majibu”
“Sawa profesa mimi nakuaminia sana katika utatuzi wako wa mambo , katika swala la kufikiria ukijumlisha na maroboti yako”
“Nashukuru lakini kuna kitu pia nataka unisaidie kukifanya nataka umfuatile Peter kwa kile anbacho anafanya sasa hivi wasiliana na Gift akusaidie”
“Sawa madam”
“Gladness profesa kama moja ya majina mengi ambayo watu wengi nchini Tanzania na nje ya nchi walikuwa wakimuita, kutokana na heshima yake kubwa ambayo nchi ya Tanzania ilimtunuku pamoja na vyuo vikuu Duniani ,alienda mpaka sehemu maalumu ya uwanja mdogo wa ndege ,na kupanda chopa yake ya kifahari kabisa kuelekea nyumbani kwake pembeni ya Kijiji cha Singisi kwani huko ndio yalikuwa makazi yake maalumu ,akimiliki eneo kubwa ndani ya Kijiji ,sehemu iliokuwa ikiitwa village G lakini jina maarufu sana lilikuwa ni Kijiji Cha Maroboti , kwa kifupi ndani eneo hilo kulikuwa mandhari nzuri sana kiasi kwamba hakuna eneo ambalo ni ghali Zaidi kwa utengenezzaji wake ndani ya Taifa la Tanzania kwa makazi binafsi, hio ni kutokaqna na miundombinu yake ya kiteknolojia.
Lakini jambo la kushangaza ndani ya Kijiji hicho ambacho kilikuwa kimezungushiwa ukuta mkubwa sana kiasi kwamba huwezi kuona eneo la ndani kwa kile kinacho endelea ni kwamba ndani ya eneo hili hakukuwa na binadamu hata mmoja Zaidi ya Gladness anaeishi ndani hapo, pamoja na maroboti peke yake na hio ndio mbinu ambayoGladness aliamua kuishi nayo kwani kwa mambo yote yalio mtokea katika maisha yake hakutaka kuamini kabisa binadamu.
Yeye aliamini roboti haliwezi kukusaliti kama utaliwekea ulinzi mzuri wa kutodukuliwa . na ndio maana ndani ya mji wake huo hakukuwa na binadamu na jambo ambalo ndio linazidi kumpa umaarufu sana na kufanya eneo hilo watu wengi kutamani kufika kwa ajili ya utalii.
Ndani ya nyumba yake hio kulikuwana maroboti ya aina tano kuna roboti linaitwa Laurel hili lilikuwa linahusika na ufanyaji wa kazi za ndani yaani House keeper lakini hili lilikuwa na sura ya kike kabisa na kwa mfano unaweza ukapishana nalo sokoni pasipo kugundua kuwa ni roboti na lilikuwa limesetiwa kufanya kazi moja tu ambayo ni kuhakikisha Gladness anapata chakula chenye uwiano wa virutubisho.
Roboti lingine lilikuwa likiitwa Sophia lilihusika na usafi wa nyumba nzima pasipo mazingira kwani hio ni kazi ya roboti lingine ambalo hili halikuwa na muundo wa kibinadamu ila lilikuwa na muundo wa mnyama pundamilia na Gladness alipenda sana mnyama aina ya pundamilia na ndio maana likaitwa Zebra , ukiliona utashangaa kwani lina uwezo wa kusimama wakati wa kufanya kazi ila kutembea lazima litembee kwa miguu yote mine.
Maroboti mawili yalio baki yalikuwa yakiitwa Nimrod na Rochis haya yote hayakuwa na sura za kibinadamu ila yalionekana kama maroboti kabisa bila ngozi na Gladness aliyatengeneza haya kwa ajili ya kuwa kama kivutio na kazi ya haya maroboti yalikuwa yakimsaidia Gladness katika maswala yake ya kufikiria , yaani yana uwezo wa kumskani binadamu na kujua anacho fikiria na kuchukua mawazo yako na kuanza kutengeneza njia mbadala ya suluhisho kwa kile unacho fikiria , hii ndio teknolojia ya mwisho kabisa na ya kushangaza ambayo Gladness alifikia na teknolojia hii ilipigwa vita na binadamu kutoruhusiwa kuingia kwenye jamii kwa minajili kwamba ingeifanya dunia kutokuwa salama ,Teknolojia hii ilitengenezwa kwa mfumo wa Brain Nerve Transmission , japo ni teknolojia kubwa lakini ilikuwa haina uwezo wa kujua kile mtu amabcho unafikiria kabisa kwa asilimia mia moja lakini ilikuwa na uwezo wa kupata mawazo ya mtu yaliofikia kiwango flani (Threshold level) katika ubongo , ilikuwa ikifanya kazi kwa njia mbili ya kwanza ni kufananisha kazi unayofanya kwa kuupdate(kuchukua matukio mapya) matukio yote yanayo tokea katika mazingira unayofanyia kazi na kurekodi jinsi ubongo unavyotafsiri mawimbi katika seli zake, huu ni mwendelezo wa teknolojia ya MRI(MAGNETIC RESONANCE IMAGING) sasa yote hayo yaliwezekana pale Gladness alivyoweza kuvumbua kifaa kifahamikacho kwa jina la NEUORON TRANSIMISSION PATTERN DETECTOR(NTPD), kifaa hichi kinafanya kazi kwa msingi wa kwamba kila jambo linalo mtokea binadamu lina transimission signal pattern and sequence unique(usambazaji wa taarifa wa kimpangilio wa kipekee)ambao ni za kipekee sana kiasi cha kupelekea NTPD kunasa hizi pattern , na jambo hili kwa Gladness lilifanikiwa kwa kupata ushirikiano mkubwa na professor wa utafiti wa maswala ya Ubongo kutoka Australia profesa anaefahamika kwa jina la Robert Callister , kwani yeye ndie aliekuja na ugunduzi wa kwamba ubongo wa binadamu unazalisha Unique pattern signal(muundo pekee wa kitaarifa) katika ubongo ,hivyo profesa gladness kwa kutumia ripoti ya utafiti wa Robert Callister aliweza kuvumbua kifaa kifahamikacho kwa jina la NTPD kama nilivyokielezea.
Yaani kwamba kila jambo linalotokea kwenye Maisha ya binadamu likifikia Threshold(kiwango ) level flani basi linatengeneza mfumo tofautishi wa jinsi unavyo kwenye ubongo, sasa maroboti haya yamefungwa hiko kifaa ambacho kazi yake ni kurekodi hizo pattern na kama zitajirudia basi zitafananisha na tukio lililokutokea na kuzifananisha na data za tukio lililotokea nyuma na kuja na output (tokeo ) llilo tokea kwahio udhaifu wa maroboti haya ni kwamba yanafanya kazi kwa mtu mmoja tu sio watu wote kutokana na kwamba kama litafanya kazi kwa mtu mwingine litachanganya matukio na kutoa False Output (tokeo la uongo), kwa hio hayana uwezo wa kutafsiri kabisa kile mtu anacho waza lakini pia usahihi wa roboti hili ili lisitoe output ya uongo limewekewa Threshold Level (kiwango) qualification device, hiki ni kifaa ambacho kilikuwa kikichuja taarifa ambazo hazikuwa na umuhimu na kuchukua zile zenye umuhimu Zaidi . .
Tukiachana na maajabu hayo turudi kwenye simulizi.
****
Peter hakuwa akipata usingizi mzuri hata yeye mwenyewe alikuwa akijishangaa kwani kila alivyo kuwa akilala alikuwa akimkumbuka Tajiri Samir akimfokea hata yeye mwenyewe alikuwa akijishangaa kwanini kila akilala anamuota Tajiri Samir .
“Mimi kitakacho niweka sawa hapa nadhani ni kisasi tu nadhani roho yangu itatulia”. Alijifkiria siku hio akiwa anatoka usingizini kwa kukurupuka baada ya kuota ndoto ya aina moja usiku mmoja mfululizo .
Kulivyo kucha ilikuwa ni Jumamosi na siku hio hakuwa akienda chuo na ratiba yake ilikuwa ikimuambia siku hio ni ya kufua na kisha kwenda kuzurula , basi aliamka kivivu na kutoka mpaka sebuleni na kumkuta Masumbuko kama kawaida yake akiwa anangalia katuni..
“Huyu jamaa kwanza nimpige biti huyu la uhakika asije akanigeuza demu wake huyu maana simuelewi , unaweza jikuta ana kupa kumbukumbu unampa Tigo , mwishowe unakuja kushtuka kakupasulia mayai”
“Vipi Bahati”
“Safi za kuamka?”
“Safi , sasa bahati si unajua mimi ndio namekulea hapa na chochote utakacho kuwa unaomba nitakuwa nakupa sasa usije ukathubutu kunigeuza akili yangu kama ulicho mfanyia Steve jana , na ukifanya hivyo hapa inabidi uhame”
“Sawa wewe ni bosi , lakini pia unanisaidia kufikiria siwezi kufanya hivyo ,ila jambo moja nataka niwe nafanya”
“Jambo gani hilo?”
“Mimi sipendi kazi za kufanya kwa hio nataka niwe naangalia Tv tu na kula na kulala na kutafuta hela ila sio kwa kufanya kazi “
“Sasa we jamaa utapataje hela bila kufanya kazi na nani atakupikia na kukufulia”
“Nisaidie niweze”
“Daah huu mtihani huu , ila ngoja nitamwambia Steve tutafanyaje ila hebu sema unavyomfanya mtu asahau nikupe njia”
“Anhaa yaani kama natengeneza wazo ninalo taka kufanya nalihamisha kwa mtu mwingine na yeye analifanya”
“Kwa Bluetooth au nini?”
“Ndo nini?”
“Mh huyu jamaa mchawi huyu ila ngoja tuone hio kesho” Alijiongelesha Peter maana kila sayansi anayo tumia ili kulifanya jambo la Masumbuko liweze kufanikiwa ilikuwa ikigoma kabisa na kuona uwezo wake wa akili umefikia mwisho .
“Sasa sikia fanya hivi kila unapoanza kutengeneza hilo wazo lako kabla hujalituma , sijui kwa Bluetooth au nini hakikisha unatengeneza njia ya kuingilia na kutokea”
“Sasa hapo sijakuelewa”
“Ni hivi kabla ya kuanza kubadilisha mtu akili yake ili baadae asijue ulicho mfanyia mpe mawazo ambayo sio wewe unayo yafikiria ila mtengenezee wazo yeye mwenyewe.
“Sasa hapo ndio inakuwa ngumu kwangu mimi sielewi kabisa”
“Sasa sikia fanya hivi si kwa mfano unataka mtu akufulie, akupikie na kukufanyia usafi basi mfanye huyo mtu awaze kukufulia , najua hutonielewa ngoja kwanza twende hapo nje kwanza kuna mdada mmoja mwembaba ana maringo sana na anajifanya kwao matajiri sasa tutamchukulia mazoezi huyo”
Basi waliingia kwenye lift na kushuka mpaka chini kabisa na kuingia huko na kumkuta dada mmoja hivi na Peter akamuonyesha Masumbuko .
“Sasa sikia nenda kwa yule dada na kisha muombe aje akusaidie kufanya usafi kwani wewe umechoka na kabla hajajibu mpe mawazo ya kukubali na kuja kufanya kile ulicho omba , nenda sasa mimi nasubiria”
Masumbuko kama kawaida yake alimsogelea yule dada mmoja mwembamba ambae wakati huo alikuwa akianika nguo zake za ndani kwa kuzifunika na khanga nyepesi , Masumbuko wala hakutaka kumuita kwani alimsogelea na kumgusa na yule dada alishtuka kwa nguvu na kumuangalia masumbuko kwanzia chini hadi juu.
“Dada za saa hizi”
“Salama nikusadie nini?”
“Kuna kazi nataka unisadie”
“Kazi gani hio”Aliongea huku akimwangalia Masumbuko kwa dharau.
“Kupika , kuosha vyombo na kufua” Aliongea na kasha akamkonyeza kama kawaida
“Haya twende maana hizo ni kazi ndogo sana”
Basi kama kawaida Masumbuko alimuongoza mdada yule na kuingia ndani , na wakati kitendo hicho kinaendelea Peter alikimbilia ndani na kisha kuanza kutoa nguo zake zote na kuziweka mkao wa kufuliwa, ila kuna kitu kilimjia Peter ,akukumbuka kuwa kama atampa nguo zote hatomaliza ndani ya masaa mawili , kwani ndani ya muda huo atakuwa akili yake isharudi, lakini wakati akiendelea kuwaza waliingia na huyo msichana na jina lake alifahamika kama Angeli.
“Sasa Angeli wewe utanifulia hizi nguo zangu , mimi nitakusaidia kupika” Aliongea Peter.
Basi kama utani vile Angeli alianza kufua nguo za Peter na kuchukua na nguo za Masumbuko na kuanza kuzifua na kutokana uwezo wa angaeli katika kufuaa ulikuwa wa haraka aliwezakufua nguo nyingi kwa wakati mmoja , Huku Peter yeye akifurahia msaada huo maana kwenye vitu ambavyo hakuwa akivipenda basi ilikuwa ni kufua . wakati Angel akiendelea kufua ndio wakati ambao na Steve aliingia ndani hapo nyumbani kwa Peter huku akionekana kama kuna kitu cha maana ambacho kimemleta, lakini alijikuta akishtuka baada ya kumuona Angeli akifua , alimjua vyema mwanadada huyu kwa maringo yake na kuna siku yeye naPeter washawahi kupanga mbinu ya kumkomoa mwanadada huyo.
“Oya braza nimekuja na ujumbe mzuri kabisa” Aliongea Steve mara baada tu ya kumuona Peter akiingia hapo sebuleni akiwa ameshikilia juice .
“Niambie ujumbe gani huo mzee wa mipango”
“Kuhusu kesho mzee nimeongea na maza nimempiga swaga wewe nimemuambia nina rafiki yangu ana mapepo hivyo naomba kesho amkutanishe na nabii amekubali”
“Hahaha.. kwa hio kesho ndio siku.”
“Ndio , oya wewe mchawi kesho siku yako subiri uone kitakacho kutokea kesho twaenda toa mapepo yako yote , oya halafu peter Anjeli mmefanyia ninii..?huyu mchawi wako”
“Haha .. ndio .. tumemtia Virusi sipati picha varangati linalo kwenda kutokea baada ya masaa mawili”
“Hahaha .. mtachambwa leo kitaa kitawajua hiki na ninavyo mjua asivyokuwa na dogo huyo..”
“Haha sasa ulifikiiri litakuwa dogo . nimefanya hili kumkomesha tu si unajua dharau zake ..”
“Nyie mtajuana wenyewe , sasa hakikisha unampanga mshikaji aelewe ila mpango umebadilika , inabidi aombewe tu tusichukue sadaka”
“Hahaha .. unajua Steve ni kwamba moyo wako unamwamini Masumbuko ila akili yako ndio inakupa changamoto ,ndio maana huna msimamo na unahofia isije ikawa kweli jamaa akasepa na sadaka ikawa mengine , wewe unatakiwa kuamua kitu kimoja , mimi mwenyewe nimeunganisha formula zote kupata sababu ya jamaa kuwa hivi, lakini majibu sijapata kabisa ila bado naamini jamaa ana uwezo wa ajabu na sina shaka na hilo”
“Hapana mzee , ila kweli upande mwingine sina uhakika unajua inaweza ikawa kweli jamaa ana uwezo wa ajabu ila inabidi aombewe tu halafu tutatafuta sehemu ya kuujaribu uwezo wake tena”
“Mimi ni nawazo juu ya ule mpango wangu”Alibadilisha mada
“Wazo gani hilo”
“Jumatatu naingia Rasmi kwenye benki ya yule mrembo kuendeleza misheni yangu , ila pale nataka kwanza kuhack system ya benki kwa upande wa ATM yaani nataka mtu akitoa hela mfumo umwambie hakuna mtandao na kama ataingia mtandao watu wa benki wataambulia neno system error na najua mfumo wao wa kibenki unalindwa na teknolojia ya EARTH INC sasa mimi nitaufunga na hao EARTH INC hawatajua namna ya kuufungua na ndipo nitaenda kuomba kazi na interview angu ni kutatua tatizo hilo.
“Acha kujidanganya wewe , huwezi , hivi haka kakichwa kako utakafananisha na kayule professa alietengeneza ile teknolojia” Aliongea huku wakiwa wanakunywa juice na nyama wa kukaanga na viazi yaani chipsi nyama huku Steve akizidi kukomalia kwamba hawezi , basi baada ya muda wa masaa mawili ndio muda ambao Angeli anamalizia kuanika nguo za Peter na sasa alikuwa akikusanya mabeseni maana nguo alikuwa kazianika nje kabisa ya jengo hilo kwani lilikuwa na uwazi , lakini alijikuta akijishangaa ameshika mabeseni , sasa kuna jambo ambalo alikuwa akijiuliza ila hakuwa akipata majibu ni kuhusu hayo mabeseni yalifikaje kwenye mikono yake na kilicho mshangaza ni kwamba hakumbuki kumuona mtu mwingine aliekuwa akifua nje hapo Zaidi yake kwani alishangazwa na nguo nyingi za kiume ambazo zilikuwa zimeanikwa , lakini alijikuta akipuuzia baada ya kukumbuka mara ya mwisho alikuwa akiombwa na mkaka mmoja ambae hakumjua akitaka kumsaidia kufua , sasa yeye aliunganisha matukio na kuona huenda alifua mwenyewe baada ya yeye kumkatalia kwani alikuwa hakumbuki , alijikuta akikimbilia ndani na kuangalia ndani , lakini alijikuta akipigwa na mshangao baada ya kuona muda umeenda sana na muda huo ulikuwa ni saa sita mchana .
“ Hivi muda wote huo nilikuwa nafanya nini mbona muda umeenda sana huu “ alijiuliza hukua akionekana kuwa na haraka kwani alivaa nguo na kujiweka sawa kisha akachukua mkoba wake na kuondoka, lakini licha ya kukimbilia nje ya geti hilo alikuwa bado akijiuliza maswali yaliokosa majibu, ni kweli alikumbuka kijana mgeni kwenye macho yake kumuomba kumfuulia na kumpikia , lakini katika akili yake alijua kwamba asingeweza kumkubalia mwanaume huyo kwani alikuwa akiijua tabia yake.
Sasa wakati anaondoka Steve yeye alikuwa dirishani na alimuona Angeli akiondoka na kuonekana kwa na haraka”Alijikuta akishangaa na kumuita Peter.
“Virusi vishaisha nguvu hahaha.. halafu ukute pale hakumbuki chochote kilicho endelea masikinii “
“ Halafu unajua Peter unapenda kuchukulia mambo simple sana huyu jamaa sio mtu mzuri sana nashangaa hata huogopi unakaa nae , wewe ngoja siku akupasulie mayai ndo utaelewa , ila ngoja tuone hio kesho”Aliongea maneno mengi mfululizo yasiokuwa yamenyooka , ni kama alikuwa akiongea na kujijibu yeye mwenyewe , huyo alikuwa ni kijana Steve.
“Unajua kuna muda hata mimi nakuaga namuogopa ila kama kesho akiombewa na vikaisha basi itakuwa fresh ila visipo basi nitampiga mkwala na uzuri hajui kufikiria”
Basi ilifika muda wa saa kumi jioni muda ambao Peter ratiba yake ilikuwa ni kwenda Beach na siku hio Peter hakutaka kumuacha Rafiki yake Masumbuko maana muda huo alikuwa akimchukulia kama Rafiki yake , basi kutokana na ndani ya apartment yao kulikuwa na mashine ya kunyolea basi Peter alianza kumnyoa nywele Masumbuko na kumuweka katika hali ya usafi na kisha akampa nguo za kuvaa maana walikuwa wakilingana kama mapacha .
Siku hio masumbuko alipendeza kiasi kwamba usingejua ni masumbuko aliekuwa ametokea kijijini siku tatu nyuma alikuwa amependeza kweli kweli na kilicho mfanya Masumbuko kupendeza ni kwamba alikuwa Hb mmoja matata sana, ni kwamba tu alikuwa amekosa matunzo , hata Peter mwenyewe alikiri jamaa ni Hb . , basi wote walitoka mpaka chini ambako Peter alikuwa amepaki pikipiki yake.
“Kesho kutwa tu mzee nanunua gari kali na ya maana” Aliongea peter baada ya kufikia pikipiki yake.
“Haha boss una hela sana” Aliongea Masumbuko maana alipendelea kumuita Peter boss”
“Kesho kutwa kuna sehemu utanipeleka tukatengeneze pesa mimi nitakusadia kufikiria “ Aliongea Peter nakumfanya Masumbuko atabasamu na hapo hapo waliondoka kuelekea upande wa Kawe kwani ndio Peter alikuwa amepanga kwenda siku hio.
Ilikuwa ni siku ya kwanza kwa bwana Masumbuko kuona bahari na kiufupi alikuwa akishangaa sana jinsi maji yalivyo kuwa yakienda na kurudi, Masumbuko aliona furaha kweli siku hio hasa kwa kuona watu wakiogelea , alitamani na yeye kwenda,wakati huo Peter alikuwa kakaa upande mmoja hivi ambao ulikuwa umejengewa sehemu ya kupumzika ila kwa nje kulikuwa na kama mawe makubwa hivi , Peter alikuwa amekaa huku akimwangalia Masumbuko aliekuwa upande mwingine wa kulia kwake akishangaa maji na watu wanavyo ogelea . lakini kuna jambo alijikuta likimvutia macho na hilo ni baada ya kumuoana mdada mmoja hivi anapita kwa chini yake akiwa amevalia gauni flani hivi refu kidogo lilo ishia kwenye magoti huku likiwa limempendeza ukijumlisha na Hijab aliovaa , Peter alitamani kuona sura ya mwanadaa yule kwani alikuwa kampa mgongo alikukuwa akiangalia maji ambayo yalikuwa yakimgusa miguuni mwanadada huyo, lakini kile ambacho Peter alikuwa akikifikiria na kutamani hatimae kilitokea kwani mrembo huyo aligeuza uso wake kidogo na kumfanya peter amuone na kusababisha mshtuko kwa Peter kwani mwanadada huyo alionekana kuwa na kasura ka kipole kazuri mno ambako Peter kwenye kumbukumbu zake za ubongo zilimwambia kabisa hakuwahi kuona mwanamke mzuri wa mfano huo, maana ukiachana na shepu ambayo mwanamke huyo alikuwa nayo aalikuwa na umbo namba nane jambo ambalo lilimfanya Peter achanganyikiwe na uzuri wa mwanadada huyo na kumsahau kabisa Masumbuko.
Sasa kilicho mfanya Peter aamke ni pale alipomuona mwanadada huyo akitembea kuelekea upande wa kushoto kwake ambako kulikuwa na mawe mawe sehemu ambayo siku hio haikuwa ikifikiwa na maji kutokana na kuwa na maji kidogo(Kupwa na kujaa kwa maji), waswahili wanasema maji yameenda kulii . na siku nyingine sehemu hio huwa inakuwaga na maji yanayofikia kingo za kuta ambazo zimejengwa kwani kwa juu kulikuwa kumejengwa sehemu ya kujipumzishia kama ushawahi kutembelea Kawe Beach utakuwa ushafahamu ninachojaribu kukuelezea, sasa mwanadada huyo alikuwa akielekea upande huo sasa kwasababu upande huo ulimfanya Peter kutokumuona basi alisimama na kuanza kumfuatilia kwa nyuma huku akijifanya hamfatilii yupo kwenye mishe zake .
Lakini ghafla walikuja vijana wawili ambao walioneka kama vibaka kabisa japo miili yao ilikuwa imejazia na walikuwa vifua wazi sasa eneo ambalo walikuwepo kwa juu watu hawawezi kuona kinacho endelea kwa chini ya mawe hayo na kwa wakati huo aliekuwa akiona kitendo hicho ni Peter peke yake sasa wale majamaa baada ya kumfikia yule mdada si wakaanza kumzingira na kwakuwa yule dada alikuwa kashika pochi basi mmoja akawa anavuta ile pochi ili kumnyang`anya , jambo ambalo Peter alitaka kujipa ushujaa mbele ya mwanadada huyo kwani alifika sehemu ile na kuleta ubabe , lakini kilicho mtokea Mungu ndio aliekuwa anajua maana jamaa mmoja alimlamba peter mtama na kudondokea kwenye maji sasa dondoka ya Peter ilikuwa ya kizembe sana alidondoka chini kwa mgongo lakini akabiringita na kujikuta uso ukizama kwenye tope.







SEHEMU YA 09

Masumbuko kitendo cha Peter kupigwa mtama alikiona kwani wakati Peter anamfauta nyuma yule mwanadada alimuona , hakuweza kuvumilia kitendo kile na ndio maana alivyomuona p yupo kwenye matatizo alikimbilia upande ule ule na kuwafikia .
“Vipi na wewe chalii unataka ufanyiwe kama mwenzako hapo chini?”
“Wazee kiroho safi acheni ugomvi na tambaeni kabla hamjanijua upande wangu wa pili ulivyo” Aliongea Masumbuko kwa sauti ambayo hata kama ni mtoto kibaka asingetishika nayo maana kwanza haikutoka na pili mtu mwenyewe ambae alikuwa akiongea alikuwa akionekana mzembe.
“Hivi wewe unaweza kutufanya nini sisi wewe?” Aliongea jamaa yule yule aliempiga mtama Peter na aliyomfikia Masumbuko akamshika kwenye shingo na kuanza kuminya na kumfanya Masumbuko akohoe. .
“Wewe si unapenda kuingilia ambayo hayakuhusu na huyu mbea mwenzaio, sasa leo hii tutakuonyesha njaa zetu tulizokuwa nazo , tunazitolea kwako na huyu mpuuzi maana siku nyingi tulikuwa tukiwatafuta machawa kama nyie”
Sasa kilicho mpoza yule jamaa ni wakati alipo kuwa akiminya shingo alikuwa akimkodolea macho Masumbuko , na hio ndio ikawa kama kosa lake kwani Masumbuko hakutaka kuiachia nafasi hio na hapo hapo yule jamaa alimuachia na kisha alimuweka vizuri Masumbuko Shati yake na kisha alimsogelea yule mwenzake , sasa yule mwenzake muda wote alikuwa akimshangaa Rafiki yake kwa kitendo kile cha kumuachia Masumbuko na hata wakati Rafiki yake anamsogelea hakuwa na wasiwasi lakini katika hali ya kushangaza alimtwanga mwenzake ngumi nzito ya mdomoni na kumfanya jamaa achie ukulele wa maana jambo ambalo lilimfanya hata Peter acheke kutokana na sauti jamaa alio itoa . sasa jamaa ni kama vile kaingiwa na kichaa maana alianza kumtembezea kichapo mwenzake cha maana huku yule mwanadada akipatwa na mshangao wa ajabu kwa kile kilicho kuwa kinatokea sehemu ile , maana ilikuwa si hali ya kawaida mtu kumgeuka mwenzake na kuanza kumpiga .
Sasa yule jamaa aliekuwa anapigwa baada ya kuona kazidiwa na kuona hapa hapakaliki aliamua kuchomoka nduki na kuwaacha wakina Peter na Masumbuko na yule msichana mrembo, sasa hapo Peter aliekuwa anajifuta futa kwa matope aliduwaa baada ya msichana yule kutoa kitambaa na kumpa Peter .
“Asante” Aliongea Peter
“Wala lazima nikushukuru wewe maana leo nyie ndo mli niokoa” Aliongea kwa mapozi na kumfanya Peter aanze kulewa na mapozi yale huku yule dada macho hayakutoka kwa Masumbuko .
“Boss tuondoke bwana turudi zetu nyumbani nikaangalie katuni”
“Poa ngoja twende” Aliongea Peter maana hakutaka kuondoka na kumuacha yule msichana, alitamani walau kusema neno lolote lakinii alishindwa na yule msichana alikuwa ndio wakwanza kuaga na kuondoka huku tembea yake ilimfanya peter kujiona kama yuko ulimwengu mwingine kabisa na kwenye ulimwengu huo hakuna binadamu mwingine Zaidi yake huyo mrembo , Peter alisimama mpaka pale Masumbuko alipomshtua ndio akili yake ilirudi kwenye hali ya kawaida na kisha waliamua kuondoka sehemu hio na kurudi walipo kuwa wameacha pikiiki yao na kisha kupanda na kuelekea maeneo ya nyumbani kwao .
Huku upande mwingine alionekana yule mrembo akifuatwa na mwnadada alievalia suti safi na miwani na baada ya kumfikia alimpa heshima .
“Boss nilikuwa na wasiwasi ulikuwa wapi?” Aliongea yule msichana huku akifungua mlango kwa ajili ya mwanadada huyo kuingia .
“Lucy hivi kwenye Maisha yakoo ushawahi kuona tukio ambalo mpaka leo hii huamini, yaani kama maajabu maajabu hivi?” Aliongea yule msichana .
“Kwa kweli bosi hapana sijawahi kuona ila nishawahi kusikia mambo ambayo mpaka leo hii sijawahi kuyaamini”
“Mambo gani hayo hebu niambie” Aliongea yule msichana huku akionekana kweli akihitaji kujua maana alionyesha uso wa shauku .
“Boss leo una nini mbona hata sikuelewi tumetoka nyumbani kwako ukiwa na mawazo ila sasa hivi unaniuliza mambo ambayo siyaelewi nini kimekupata”
“Wewe nii jibu bhana Lucy nina maana yangu”
“Ndio nishawahi kusikia kuwa kuna watu wanachuna Ngozi za binadamu katika kijiji chetu kwenye msitu mmoja wakati ukipita usiku ila sijawahi kuamini mpaka leo”
“Na wewe Lucy bhana mimi sitaki maajabu kama hayo bhana” Aliongea hukua akitoa kisauti flani cha kuvutia nna kumfanya Lucy amwangalie boss wake huyo kupitia kioo cha gari upande wa juu na kutabasamu tu huku akijisemea mwenyewe moyoni kuwa boss wake alikuwa mzuri nyakati zote , yaani awe amenuna au anacheka alikua akionesha uzuri wa kipekee sana na hata wakati mwingine alikuwa akimtamani hata asagane nae na ndio hivyo tu alikuwa ni boss wake hakuwa na pakumwanzia mwanadada huyu alikuwa ni wale wanawake wanaopenda wanawake wenzao kwa kingereza wanaitwa Lesbian. .
“Ila boss unaonekana leo kuna kitu kimekupata, si ndio boss maana ulivyo kuja ni tofauti na tunavyo ondoka”
“Ndio mwenzako kidogo tu ni ibiwe lakini huwezi amnini kuna kijana kanifanya nisiamini kile ambacho kimetokea” Aliongea msichana huyu ambae jina lake hatujamtambua bado . na alianza kumuhadithia Lucy huku gari ikikaribia geti moja kubwa sana upande wa kushoto mbele kidogo na shule ya Mbezi beach , lilikuwa ni jumba kubwa lilionekanakuwa na ghorofa mbili . basi geti lilifunguliwa na gari kwenda kuegeshwa kwenye moja ya magari mawili yalio onekana kuwa ya kifahari sana maana gari moja lilikuwa ni BMW ya rangi ya pink na kwa muonekano wake ilionekana gari hio ni mpya , lakini pia kulikuwa na gari nyingine aina ya Aud ya rangi flani ya majivu yenye texture flani hivi ya rangi ya blue na ilikuwa iking`aa na kuifanya kuvutia sana kimuonekano . basi baada ya gari hioo kusimama yule msichana mrembo alishuka na kuingia ndani ya nyumba hio .
“Mamii..”Sauti ya yule msichana ikiita mama ilisikika na hapo msichana yule alikwenda kumkumbatia mwanamke mmoja aliekuwa akionekana mzuri pia na kwa muonekano wake usingezania ama ungeshituka kwa msichana yule kumuita yule mwanamama mama.
“Yaani mwanangu nilivyo kumisi , yaani kweli Nasma hata kuja kunisalimia mama yako, kama tu ndugu zako hutaki kuonana nao mwanangu, mpaka niamue kutoka nyumbani na kukufuata huku”
“Mom nakumisi sana ila sitaki kukutana na baba na Najma”
“Hata kama ungekuja ofisini kwangu kunisalimia mwanangu hivi unajua ni kiasi gani na kupenda”
“Lakini mama pale ni benki na haparuhusiwi watu kuingi mara kwa mara hasa kwa shida zao binafsi”
“Mhmh , sio vizuri lakini ili mradi nimmekuona haina shida sana , nimekuja kujua chuo una anza lini maana nasikia muhula ushaanza”
“Nitaanza kwenda wiki ijayo mama”
“Sawa mwanangu mimi nakuamini sana na chochote utakacho taka nitakupatia sawa mama ee”
“Sawa mama .
Huyu alikuwa ni mke wake Tajiri Samir ajulikanae kama mama rania na siku hio alikuwa amekuja kumuona mtoto wake wa kike ajulikanae kwa jina la nasma pacha wake najma.
*****
Basi upande mwingine tunamuona Peter wakiwa na Masumbuko wakiwa sebleni wamekaa wanangalia movie .
“ Hivi Bahati pale ulimfanyia nini yule jamaa , na maanisha ulimpa kumbukumbu gani ?”
“Pale nilimpa mawazo ya kumpiga mwizi anaetaka kuiba”
“Hahaha .. aisee nikaju hujui kufikirfia ila kuna kipindi kingine unakuwa unajua kufikiria” Aliongea Peter huku picha ya yule msichana ikiwa haimtoki kichwani maana kuna muda mwingine alimfananisha Masumbuko na yule msichana na kujikuta akifurahia pasipo kujua kuwa anaota.
Basi ilikuwa ni siku ya jumapili siku ambayo ilikuwa ikisubiliwa kwa hamu na Steve huku akiamni kabisa siku hio mapepo ambayo yalikuwa yakimsumbua bwana Masumbuko yanakwenda kutoka ama kutolewa hio ni kutokana na kumuamini sana Mwamposa na siku hio aliamini asilimia mia kuwa mapepo hayo yataenda kutolewa na kwa upande mwingine aliamiini pia atakwenda kumuokoa Rafiki yake peter kwani alimuona kabisa kwa namna moja ama nyingine kajiingiza kwenye mdomo wa simba kwa kukaa nyumba moja na mchawi.
Basi alijianda haraka haraka ikiwa muda huo ni saa kumi na moja kwani mama yae aliamini kuwa siku hio inakuwa na msongamano watu wengi kwa hio kama kweli anataka kumuona mchungaji laivu basi anatakiwa kuwahi. Alitumia masaa machache kujiandaa na alimaliza na kutoka kuelekea kwa Rafiki yake peter kwa ajili ya kukutana .
Huku nyumbani kwa Peter muda huo hakuna hata mmoja aliekuwa ameamka sio Peter wala si Bahati Masummbuko wote walikuwa wakiuchapa usingizi na hio ni kutokana na Peter kutokuwana mazoea ya kwenda kanisani tokea akiwa mdogo . na kifupi hata mlango wa kanisani alikuwa haujui .
“ Oya nyie washikji bado tu mmelala au mmeshasahau kuwa tunaenda kwa mtumishi leo”Aliongea Steve baada ya kufika na kukuta wenzake wamelala na kuona Peter hakuwa na wasiwasi na uwezo wa ajabu wa Masumbuko ila mwenye wasiwasi alikuwa ni yeye mwenyewe .
“Mzee kuna kuchoka si unajua hii wikiend na akili yangu ishajiseti kila wikiend na amka saa tatu” Aliongea Peter huku akijivuta .
“Kwa hio tunaenda ama hatuendi?”
“Ngoja tunaenda ngoja ni muamshe Bahati tujiandaae tuondoke tupe nusu saa tu tutakuwa tushamaliza”
*****
Siku hio ndani ya eneo la mtumishi wa Mungu Boniface mwamposa kanisa la Inuka Uangaze kulikuwa na watu wengi sana, eneo ambalo likuwa likipatikana katika viwanja vya Tanganyika park Kawe , watu walikuwa wamefurika kweli kweli jambo ambalo kwa peter alijikuta akishangaa kwani hakuwahi kufika eneo hilo siku ya jumapili .
“Duu! Aisee ni noma kweli watu wote hawa wamekuja kuombewa” .
“Hapa si wote wengine wanakuja kwenye ibada kama kawaida, ila wengine wanakuja kwa ajili ya shida zao na ndio maana unaona wamejazana sana siku hii ya leo, pia sio siku zote siku nyingine za kati kati wanakuwa ni wachache” Aliongea Steve huku wakitafuta sehemu ya kukaa huku Steve akitafuta namba ya mama yake ili kumtumia ujumbe .
Basi ibada iliendelea huku wanao tao shuhuda wakitoa na wanao ombewa wakiombewa na wengine wakishangilia kwa ajili ya watu waliopona hapo hapo .
Kwa upande wa peter hakuwa akiaminni kama watu wale walikuwa wakipona , maanaa kwake ni vitu ambavyo hakuwa akiviamini sana na hata kwa wakati huo hakujua kabisa yeye ni Mkristo ama Muislamu kwani tokea amezaliwa hakuwahi kwenda kanisani hata siku moja na pia hakuwahi kwenda msikitini hata siku moja na hata mama yake hakuwahi kumpeleka na hicho ndo kilicho mfanya iwe ngumu kwake kufanya maamuzi ya dini yake .
Sasa ibada baada ya kuendelea hatimae mama yake Steve ambae alikuwa ni moja ya wasimamizi wa hapo(Shemasi) alikuja na kumchukuwa Masumbuko na kisha kumpeleka mbele kabisa kwenye jukwaa na kisha mama Steve akamwambia mchungaji kuwa huyo kijana ana mapepo makali sana yanamsumbua kwa hio yanatakiwa yatoke .
“Ameeni ,, bwana yesu asifiwee , leo kijana huyo chochote kilicho ndani yake kinakwenda kutoka hapa mbele yenu wote tuseme Ameni…..” Mambo ndio yalianza kama hivyo kabla ya Masumbuko kufanyiwa maombi na watu walikuwa na hamu kweli ya kuona kile kinacho enda kutokea hususani wamama waliojazana hapo kwani ndio waliokuwa wakionekana kuwa wengi.
“Kijana una Amini” Aliuliza mchungaji
“Ndio nina amini nimeambiwa nina mapepo , sasa hapa nipo kwa ajili ya kusibiitisha walio nileta kuwa sina mapepo” Aliongea Masumbuko na kufanya watu waamini sasa kuwa kweli huyu kijana yamemjaa na ni yale makali kabisa.
Sasa mchungaji Mwamposa alianza kazi yake ya kupiga maombi ya nguvu na kumfanya Masumbuko kwanza adondoke chini na kuanza kutingisha miguu kwa kasi ya ajabu huku akisema maneno ya ajabu ajabu kiasi cha kufanya watu wasielewe anazungumza lugha gani , maombi yalizidi kuendelea mpaka ikafikia wakati sasa ilibidi afungwe miguu na mikono maana alikuwa akileta shida kweli kweli na mchungaji alikua akitoka jasho balaa kwani , kuna watu ashawahi kuombea ila siku hio alikuwa amekutana na mtu mwenye kitu cha ajabu ndani yake , na kilicho mchanganya ni lugha ambazo masumbuko alizo kuwa akizitoa.
“Huku upande wa Steve alijikuta akitabasamu kwa kumuona sasa Bahati kakamatika na pale hachomoki na kwa upande wa Peter alijikuta akiamini kabisa maneno ya Rafiki yake na kuona kuwa kweli Bahati alikuwa na mapepo ya hali ya juu.
“Nilikwambia Peter sasa si unaona sasa yule kuwa alikuwa na mapepo mengi sana ambayo yalikuwa yakimsumbua na pale kakutana na mtumishi”.
“Aisee naanza kuamini kwa mbali . daaH hadi namuonea huruma”
Basi baada ya maombi kumaliza hatimae Masumbuko alitulia kabisa na kisha akaamka na mtumishi akampa maiki na kumuuliza unajisikiaje .
“Mtumishi nashukuru sana kwa sasa najisikia mwepesi kweli na nadhani kweli kilichokuwa kinanisumbua ni mapepo maana kichwa kilikuwa kizito”
Aliongea ,masumbuko na kuwafanya watu washangilie utukufu wa bwana
“Sasa kijana kwanza jina lako ni nani ?“
“Naitwa Bahati Masumbuko .”
“Sasa Bahati masumbuko nataka nikutangazie kwanzia leo Masumbuko yako yote ambayo yalikuwa yakikuandama yanakwenda kuisha na kwanzia sasa jina lako linakwenda kuleta mambo mapya katika Maisha yako ..Wote tuseme Ameeni” Wakina mama wote kwa kushangilia walisema “AMEEN”
Basi baada ya ibada kuisha watu walitawanyika na kila mmoja kuelekea njia yake huku Masumbuko ,Steve na Peter waliamua kurudi nyumbani ,Steve alijihis amani ndani ya myo wake na kuona kuwa sasa atakuwa na amani na Rafiki yake peter atakuwa na usalama.
“Bahati sasa kuanzia sasa ni Rafiki yangu kama Peter na kuanzia sasa tutakuwa kama ndugu yaani mimi wewe na Peter na tutasaidiana kwenye lolote lile” Aliongea Steve huku akionekana kuwa na amani sana siku hio na hata sura yake ilionyesha furaha.
“Sawa asante kama nina kwenda kuwa Rafiki yako kuanzia sasa na boss wangu hapa”
“Bahati sasa huna haja ya kuniita boss niite Peter sasa hivi kama mchungaji alivyo sema kuwa utakwenda kuwa na Maisha mapya yasio na masumbuko ndani yake”
****
Huku upande wa nyumbani kwa Nasma yaani yule mrembo aliesaidiwa na Bahati na Peter alijikuta lile tukio likijirudia rudia ndani ya akili yake na kumfanya muda wote amuwazie Kijana Bahati Masumbuko , alitamani amuone tena amuulize ni kwa jinsi gani ameweza kufanya tukio la namna ile kwani kwake aliona ni maajabu sana , kuna muda mwingine alijikuta akijilaumu kwa kuto wauliza hata majina watu wale ambao kwake alikuwa akiwachukuliwa kama watu walio muokoa .
Lakini mtu ambae alikuwa akimkumbuka sana na kutaka kumuona alikuwa ni Masumbuko na jambo moja ambalo alikuwa akitaka kuliju kwa Masumbuko ni kwanini yule mwizi alimwachia yeye na kwenda kumpiga mwenzake alitaka kujua ni nini kile kimetokea na katumia uwezo gani , kuna muda mwingine alikuwa akijiuliza labda yule kijana alikuwa mchawi , lakini kutokana na kuto amini katika uchawi alijikuta akitaka sana kujua na aliona labda kuna kitu anaweza kukipata kupitia Masumbuko ambacho kinaweza kumsaidia,alikuwa ni mwenye kujawa na shauku kubwa mno.
“Jamani halafu yule kaka ni mzuri nimempenda alivyo kuwa anaongea bila woga eti kisa aniokoe” Aliongea kwa sauti na kumfanya Lucy aliekuwa pembeni yake amwangalie
“Nasma utakuwa ushapenda mwanaume tayari wewe sijawahi kukuona kwenye hali kama hii”
“Lucy bhana sio hivyo kuna kitu kinanifanya nikose majibu ya moja kwa moja ndio maana”Aliongea kwa kujitetea jambo ambalo lilimfanya Lucy amwangalie na kuona hapa huyu ashaanza kupenda ila tu bado hajitambui .
“Haha… sema wewe hujui hivyo vitu vinavyoanzaga kwakuwa ni mgeni ila nakuambia muda tu ndo utaongea jinsi utakavyo kuwa unamfikiria ndio chembe chembe za mapenzi zinavyo anza kujijenga”
****
Sasa huku upande mwingine tuna muona jamaa mmoja kabisa tofauti akiingia ndani ya ofisi ya bosi Samir na kisha kutoa heshima na kisha kuanza kuongea .
“Boss juzi kuna vijana walimsaidia Nasma na picha zao ni hizi hapa na kwa maelezo ya Lucy ni kwamba Nasma siku hizi anamfikiria sana mmoja wapo kati ya hawa na inaonesh kabisa tayari ashaanza kutengeneza chembe chembe za mapenzi”
“Unasema huyu mpuuzi huyu ndio alimsaidia mwanangu ?” Aliongea tajir Samir baada ya kuona picha ya Peter na kumfanya amkumbuke hapo hapo kuwa ashawahi kukutana nae na ni yule aliemchapa vibao Kule Mlimani.
“Ndio mmoja wao ni huyo hapo boss”
“Pumbavu hapa Ramso hakuna cha msaada huyu ni janja yake tu yakutaka kumla mwanangu huyu , alishindwa kwa Rania sasa anahamia kwa Nasma sasa sikiliza hakikisha unamfatilia Nasma kwa ukaribu na kama ukimuona tuu ana mahusiano ya karibu na Nasma mfanyizieni kama kawaida, umenielewa ?”.
“Ndio boss “
“Sawa unaweza kwenda”
“Pumbavu saana huyu dogo najua sana anacho kitafuta kwangu na hizi ni dalili mbaya sana kama hafuati mali zangu huyu ni bahati , haiwezekani kila mahali matukio yanapo tokea anakuwepo , ila muache huyu lazima nimpoteze muache aingie kwenye anga zangu” Aliwaza Tajiri Samir huku hasira zikimpanda kweli kweli na wivu ukimsumbua moyo wake, na muda mwingine alikuwa akiona labda Mungu alimkomoa kumpa Watoto wa kike halafu warembo.
*****
Huku ndani ya benki kubwa ya kibiashara hapa nchini benki ambayo wafanya biashara wakubwa walikuwa wakiweka pesa zao ndani ya benki hio , benki ambayo kwa ujumla wake ilikuwa na wateja wengi sana na si ndani tu ya nchi hii ila mpaka nchi nyingine zote za mashariki na kati.
Benki hii ilikuwa na uwekezaji mkubwa na watu wengi walikuwa wakiipenda benki hii kutokana na kwamba ulinzi wake pamoja na teknolojia yake, teknolojia ambayo ilivumbuliwa miaka ya nyuma na mwanadada Gladness au waweza kumuitwa Profesa na kufanya benki hii ipendwe na watu wengi kwa kuamini kuwa hakuna mtu duniani ambae anaweza kumshinda Gladness katika maswala ya teknolojia na kutokana na jina lake kuwa kubwa ndio ilio pelekea watu wengi kuiamini na kuweka pesa zao ndani ya hio benki ,na moja ya matajiri wakubwa ambao waliweka hela ndani ya benki hio ni bilionea mpya Laizer kutoka Arusha na wengineo wengi kama wakina Mwamedi(Mo) na baadhi ya makampuni makubwa kama Puma na mengineyo mengi , kiufupi benki hii ilikuwa na uzito wa pesa nyingi na si hilo tu hata baadhi ya wizara ilikuwa ikitumia kupitisha miamala yao katika benki hii.
Benki hii ilikuwa ikiongozwa na mwanama Shania Kiango yaani mke wa Tajiri Samir na mwanzoni benki hii haikuwa maarufu lakini kutokana na ndoa ya Shani mtoto wa marehemu tajiri Kiango na Samir Rafaeli Mswaki basi ilijizoelea umaarufu mkubwa na umaarufu huo ulifanya benki hio ikuwe na kuwa moja ya benki kubwa sana zinazo ongoza hapa nchini ,kigezo cha Shania kiango kuongoza benki hio kubwa sio ndoa bali elimu aliokuwa nayo ya kibenki na uwezo mkubwa katika maswala ya uongozi.
Mwanamama huyu anajikuta akiwa kwenye wakati mgumu sana hii ni kutokana na malalamishi ya wateja wengi wakilalamikia mfumo wa benki hio kubadilika ghafla , kwani walio kuwa wakitoa pesa kwenye ATM walikuwa wakikosa pesa zao , lakini pia waliokuwa wakitoa pesa nyingi ambao walitumia kuingia ndani kabisa ya benki kwenye matawi waliishia kuambiwa kuwa siku hio mtandao unasumbua , lakini ukweli sio kuwa mtandao ulikuwa unasumbua ila ni kutokana na kwamba mfumo ulikuwa ukiwaambia kuwa kuna error zimetokea.
Jambo ambalo lilianza kumfikia meneja msaidizi makao makuu ambae alikuwa ni Rania mtoto wa CEO na yeye akalibeba na kulipeleka kutoka kwake na kwenda kwa mama yake kutokana na siku hio meneja kutokuwepo kazini kutokana na matatizo ya kifamilia kwa hio Rania kukaimu nafasi hio..
Mwanamama Shania alijikuta akichanganyikiwa kwani tangu kuanzishwa kwa benki hio hakukuwa na historia ya tukio kama hilo kutokea na kama ni matatizo yanayo husu mtandao basi hayakuwa ya aina hio na maranyingi yalikuwa yakitatuliwa kwa muda mchache sana
"Rania hebu wasilina na wataalamu wa IT waangalie kuna tatizo gani kwani hii ni hatari kwa image ya benki kama jambo hili litawafikia wateja wetu”
Aliongea CEO kwa kuchanganyikiwa huku akizunguka huku na huko na kwa upande wa meneja mkuu na yeye alijikuta akiwa kwenye kuchanganyikiwa kwani iwapo jambo hilo lingewafikia wateja na kuharibu taswira ya benki basi wangepata hasara kubwa sana ambayo isingevumilika ,na kwa hesabu za haraka wangepoteza mabilioni ya pesa .
Rania alienda kwa IT na kuwakuta wako bize kuchezesha vidole kwenye komputa zao na kwakuwa hawa wote waliletwa hapo na professa Gladness na ndio walikuwa wakiujua mfumo huo wa ulinzi wa benki, lakini siku hio walijikuta kwenye wakati mgumu kwani kila walivyokuwa wakifanya na kujaribu kuingiza Special Code hakuna tokeo lolote la maana ambalo lilitokea na meneja alipeleka majibu moja kwa moja kwa CEO na kuzidi kumchanganya na hapo CEO aliamua kumpigia simu wifi yake ambae ni profesa Gladness.
Simu ilimkuta professa Gladness akiwa zake maabara akifanya baadhi ya kazi zake za hapa na pale kama ratiba yake ilivyo kuwa ikimuambia , sasa wakati wakumaliza kuongea na simu aliliita roboti lake lifahamiklo kwa jina ya Rochis na kulipa maelekezo . Na kwa spidi ya ajabu lilianza kucalculate baadhi ya data na ilionekana nembo ya picha ya benki X.
“ONE TWO TWO ZERO CONFIRMED CODE IS IN COMMAND INTERFERNCE WITH ONE ZERO ZERO CODE , IP ADRESS ONE NINE SIX POINT FOUR ONE ZERO CONFIRMED” Maneno hayo yalitoka kwa roboti na kumfanya Gladness anyanyuke na kujikuta akishangaa na kutabasamu kwa wakati mmoja na hapo hapo alichukua simu yake na kupiga namba flani .
****
Peter wakati huo hakuwa hata na habari kwani muda huo alikuwa wakishindana kucheza game na Steve rafiki yake huku ,Masumbuko akiangalia katuni kwenye laptop ya Peter .
“Hivi peter mpango wako wa kulipiza kisasi ndio umeghairi au?” Aliuliza Steve huku akiendelea kucheza game .
“Unajua Steve wewe unanichukulia simple simple sana, mimi mambo yangu natumia akili nyingi sana katika kuyafanya na kitu ambacho kina nifanya situmii muda mrefu… No syntaxError” .
“Hahaha… no sytanx Error, Una maanisha nini?”
“Namaanisha kuwa ndani ya dakika mbili kabla ya hili game kuisha nitapigiwa simu ya kwenda kuanza kazi rasmi benki X” Aliongea Peter na kumfanya Steve acheke lakini kweli ile game linaisha simu iliita na namba ilikuwa mpya na Peter kwa majigambo aliweka loudspeaker ili Steve asikie .
“Hellow nadhani naongea na Peter mimi ni Mkurugenz mtendaji wa benki X kutoka makao makuu posta nataka kukutaarifu kwanzia sasa kuwa umeajiliwa kwenye benki yetu kama mkuu wa kitengo cha ulinzi wa benki kama ulivyo omba na kuanzia sasa unahitajika kutokana na dharura inayohitaji uwepo wako , mengine utayajua na kupata melekezo kamili hapa hapa na gari itakuja kukuchukua muda si mrefu jiandae tafadhari ni muhimu sana” .
SEHEMU YA 10

Professa gladness alijikuta akiwa kwenye mshangao wa hali ya juu kwani zile kodi zilizo tumwa zilikuwa ni nyepesi sana kwa mtu yoyote katika kuziandika kama angekuwa na taaluma ya coding na zikaingiliana na mfumo wa benki ambao aliugundua na watu wengi wakauamini kwa ubora wake , lakini siku hio alipo pigiwa simu na kuona kuwa kuna mtu amefanikiwa kuandika code ambazo zinatoa maelekezo tofauti na mfumo wenyewe lilikuwa kwake ni jambo la kushangaza na alitabasamu kwani lilikuwa ni jambo ambalo hata yeye hakulitegemea na kwakuwa hakuwahi kupata changamoto kama hio na siku zote alikuwa akitafuta mtu wa kumpa changamoto basi alitabasamu.
Lakini kilichomfurahisha Zaidi ni kwamba mtu ambae kafanya hayo ni mtu ambae alikuwa akimfuatilia kwa muda mrefu kutokana na uwezo wake darasani na alikuwa akiamini kuwa kijana peter atakuja kuwa mtu mkubwa sana hapo baadae katika maswala ya sayansi kutokana na ujuzi wake na siku hio ndio aliamini kuwa yule mtu ambae alikuwa akimtafuta kwa siku nyingi sana keshampata .
****
Huku benki CEO alitulia baada ya kupiga simu kwa Peter na kuona kuwa sasa swala linakuja kutatuliwa muda mfupi ujao , japo hakuamini moja kwa moja kuwa kuna mtu ambae anaweza kulitatua swala hilo Zaidi ya IT ambao alikuwa amewajiri na professa mwenyewe , lakini alijikutta akipata ahueni kidogo na kumwamini profesa, kwani alikuwa akimuamini sana ukiachana kuwa ni wifi yake ila upande mwingine wa kikazi alikuwa akimuamini sana na hata benki yake kufika hapo ilipo ni kutokana na mchango wa proffessa.
****
Tukirudi siku mbili nyuma kijana Peter hakutaka kushindwa katika mpango wake wa kulipiza kisasi kwa Tajiri Samir na ndo maana aliona kabisa njia rahisi ya kulifanikisha hilo ni kwenda kufanya kazi na familia yake, kwani aliamini kupitia kufanya kazi na familia hio utakuwa ni ushindi wa kwanza ambao lazima ungemchanganya sana Tajiri Samiri .
Kutokana na uwezo mkubwa aliokuwa nao Peter aliweza kutengeneza program ambao ilikuwa na special code ambazo zilikuwa zikifanana sana na code ambazo zilikuwa zikitumiwa na mfumo wa benki x ulio kuwepo , japo za kwake zilikuwa na utofauti katika kutoa maelekezo na aliamini kama code hizo angeweza kuzipandikiza katika mfumo wa benki hio lazima zingevuruga mfumo mzima wa kibenki katika maswala ya kufanya miamala na kutoa maelekezo ambayo alikuwa akiyataka yeye . lakini kabla ya hayo kwakuwa nia yake ilikuwa ni kufanya kazi katika benki ile basi aliona jambo la kwanza la kufanya ni kutuma maombi ya kazi tena katika cheo kikubwa sana ndanii ya benki kwa mtu wa pembeni ngemuona kama chizi au wazo lake ni la kiuendawazimu.
Kwakuwa alikuwa akijua kila kitu kuhusu jinsi ya kuomba kazi katika benki hio basi alijaza fomu online na kisha akaituma huku akiamini kuwa lazima kazi hio aipate kwa vyovyote vile akishamaliza kutuma hizo code na aliamiani hakuna IT hata mmoja ambae atakuwa na uwezo wa kuzifuta code zake hizo katoka mfumo huo wa benki ,aliamiini mtu mmmoja tu ndio alikuwa na uwezo wa kuweza kujua code hizo zilikuwa zikimaanisha au kitu gani na huyo alikuwa ni alie utengeneza mfumo huo yaani Profesa Gladness , na alicho kifanya ni kuambatanisha kijifile kidogo kilicho kuwa kinatoa maelekezo ambayo moja kwa moja aliamini lazima professa gladness lazima atayaona kama tu akijaribu kutafuta ni kipi kimeingilia mfumo huo wa kibenki.
Na ni kweli kwani baada ya profesa kupigiwa simu na Shania kuhusu benki X kuwa na tatizo , na alipo liamrisha roboti lake lifanyie kazi yake aliona hako kajiujumbe , na ndiko kaliko mfanya atabasamu na kumrudishia jibu Mama rania na kumpa maelekezo ya kumuajiri huyo anaekuja kutatua tatizo hilo.
*****
Tukiriudi ndani ya benki tunamuaona CEO pamoja na meneja wakizunguka zunguka katika ofisi zao kwani kila mmoja alijawa na wasiwasi wa juu ya kile kilichokuwa kikiendelea kwani aliona kama jambo hilo litadumu muda mrefu basi lingeathiri taswirsa ya kiulinzi ya kutokuaminika na ndio maana alikuwa akitamani kijana Peter kufika mapema , lakini pia aliona kama alikuwa akichukua muda mrefu kufika na ndio maana macho yake yote yalikuwa nje ya geti la kuingilia benki hapo.
Huku upande wa mrembo Rania katika ofisi yake alikuwa na wasiwasi huo huo na alitamani sana kumuona huyo mtu akiingia hapo na kurekebisha kile kilichotokea
Mpaka muda huo hakuna aliekuwa akijua kuwa ulikuwa ni mpango wa Peter kuomba kazi ndani ya benki ,alinyanyuka na kwenda moja kwa moja mpaka kwenye ofisi ya mama yake.
“ Mama bado tu hajafika , wateja wanazidi kusumbua”Aliongea Rania mara baada tu ya kuingia katika ofisi ya mama yake .
“Bado jamani , ukute sijui kuna foleni njiani maana kakataa usafiri kasema anakuja na gari yake sasa hapo ndipo nachanganyikiwa”
Rania alilisogela dirisha pamoja na mama yake kuangalia katika geti kuu la kuingilia ili wamuone huyo alie kuwa akitarajiwa kufika .
Wakati wakiendelea kuangalia huku kila mmoja akiwa akiwaza jambo lake kichwani mara kuna pikipiki aina ya Honda iliingia na kupaki , na CEO pamoja na mwanae walikuwa na mawazo sawa kwani wote walidhania kuwa huyo ni mteja kama wateja wengine, baada ya dakika kama mbili hivi baada ya mtu yule waliedhania kuwa ni mteja kupita na kuingia ndani ya jengo hilo walisikia mlango wa ofisi yake ukifunguliwa na wote pamoja na mwanae walijikuta wakigeuka .
“Boss ashafika “
“ Nani kashafika , mwambie aingie” Aliongea CEO kwa kuchanganya swali na jibu kwa wakati mmoja
Hapo ndio kila mtu alishangaa kwani alionekana kijana mmoja sharobaro mwenye muonekano wa kuvutia akiingia ndani hapo huku akiachia tabasamu na wote walishangaa kwanza mtu huyo walimuona akiwa akiingia ndani ya benki hio na wote kudhania kuwa ni mteja .
“Kijana tunaomba radhi kama umekuja kwa ajili ya huduma leo mtandao unasumbua kidogo” Aliongea mama rania na kumfanya peter atabasamu na akalisogelea sofa na kisha kukaa .
“Nadhani wewe ndio mkurugenzi wa benki hii , mimi ninaitwa Peter nipo hapa kwa maelekezo yako” Aliongea Peter nakumfanya CEO ashangae na kumeza mate , huku kwa Rania yeye kilicho mshangaza ni kwamba alikuwa akijaribu kuvuta kumbukumbu ni wapi ameshawahi kuonana na huyo mwanaume .
“Kumbe ni wewe , samahani sana muonekanao wako umenichnganya kidogo”.
“Asante sana , nipo hapa kuti wito na kusikia hilo tatizo ambalo lilikuwa linahitaji uwepo wangu”
“Nadhani unafahamina na Profesa Glladness”
“Ndio ni mwalimu wangu”
“Anhaa hapo sawa ndio maana kakupendekeza katika swala hili nadhani anakuamini sana na kwa msaada wake ndio maana tumekupatia ajira , lakini kabla sijayazungumza hayo naomba kwanza ukashughulikie swala ambalo limetokea siku hii ya leo ambalo limewapa watu tabu sana katika kulitatua”
“Sawa nitaangalia kama nitakuwa na uwezo wa kuling`amua , lakini kabla ya hapo naomba jambo hili liwe na malipo tofauti na ya aijira kwni inatakiwa kazi nianze baada ya kusaini mkataba wa kazi .
“Ni kweli usemalo , ila kwasababau jambo hilo tunataka liishe mapema naomba ukalikamilishe mapema halafu tutaongea malipo”
“Mkurugenzi mimi naomba nikalione hilo tatizo kwanza halafu nitasema malipo yangu baada ya kuona ugumu wa kazi yenyewe”
Wakati huo mazungumzo hayo yanaendelea Rania alikuwa akimwangalia sana kijana huyo anavyo ongea kwa kujiamini na maringo Fulani hivi ambayo yalianza kumkera kwa namna moja .
Basi waliongozana wote Rania na mkurugenzi mpaka chumba cha mitambo ya kibenki na waliwakuta wafanyakazi wakiongozwa na mkuu wa kitengo hicho wakijaribu kuchezesha vidole vyao katika komputa zao .
“Jamani nadhani sasa niwatambulishe mtu mwingine kwenu na huyu ndio atakuwa mkuu wenu na aliekuwa mkuu wa hapa atahamishiwa mwanza kwenye tawi letu kule” Aliongea mkurugezi na kuwafanya watu wote walio kuwemo mule ndani wamwangalie Peter kwa macho flani ya chuki na kisha walinyanyuka kwenye viti kwani waliambiwa na mkurugrnzoi wampishe mtaalamu afanye yake .
Peter kwa mbwembe alishika keybord na kuanza kuandika wa spidi sana kiasi kilicho mshangaza hata CEO na mEMeneja msaidizi na alitumia dakika moja tu aligonga ‘ENTER’
“ Mkurugenzi nadhani ukinipa bilioni moja tu inatosha”
“Unauhakika utaweza kurudisha katika hali yake ya kawaida”
“ Ndio kama umekubaliana na hayo malipo”
“ Sawa fanya kazi hela hio ipo” Alikuwa very desparate wazungu wanaongeaga hivyo.
“Mamaaa.. hela yote hio”Aliongea Rania baada ya kuona mama yake kakubali kirahisi.
“Mwanangu tukianza kujadiliana kuhusu bei tunapoteza muda kwa sasa na hela hio ni ndogo sana ukichana na kitu ambacho tunaweza kupoteza ni Zaidi ya mabilioni, Reputation ndio biashara mwanangu na ndicho ninachojaribu kukilinda hapa”
Rania alitoka pale kihasira na kuondoka na kumuacha CEO na Peter kwenye kile chumba.
Basi Peter alianza kuchezesha vidole vyake kwa spidi ya hali ya juu kwa muda wa nusu saa mfumo ulikuwa tayari umerudi katika hali yake .
Lakini wakati Petr anaendelea kufanya kazi yake CEO alikuwa akimwamgalia sana Peter kwa macho ya kurembua huku kijisketi chake cha suti alichovalia kikiwa kimempanda na kuonyesha mapaja yake yalio nona kwani muda wote huo alikuwa ameketi , kiufupi alikuwa tayari ashamtamani Peter kimapenzi na nhata yeye alikuwa akijishangaa hilo pepeo linatokea wapi .
“Mkurugenzi tayari mtandao umerudi” Aliongea baada ya kumgeukia , lakini ni kama CEO hakusikia chochote kwani bado alikuwa amemkodolea macho Peter na alijikuta akimwangalia CEO kwanzia chini mpaka kichwani . kiufupi CEO alikuwa akionekana sana mrembo.
Japo mwanamama huyu kuwa na Watoto watatu ambao walikuwa kwakubwa ile usingeweza dhania mama huyo ana watoto kama hao , maana bado umbo lake lilikuwa likiita na kuvutia sana na sura yake iliokuwa imejaliwa lips za kuvutia vilimfanya azidi kupendeza.
Peter alijikuta akipandwa na pepo kwani na yeye alikuwa akiangalia mapaja ya mwana mama huyo na kujikuta dunguso yake ikisimama wima , lakini wote walijikuta wakishtuka baada ya Rania kuingia .
“Mama mtandao umerudi kama kawaida” Aliongea kwa furaha baaada ya kuingia ndani hapo.
Mama Rania alijikuta akipumua kwa kasi na kufurahi kwa tatizo hilo kuisha na hapo hapo walirudi ofisini na Peter alisainishwa mkataba wa kazi huku akiwa mwanafunzi mwenye ajira yenye mshahara mkubwa , mshaharawa milioni tano kwa mwezi , huku na malipo yake bilioni moja yakifanyika na alitoka hapo akiwa bilionea , na siku hio hakutaka kufanya uzembe kwani kitu cha kwanza alikuwa akifikiriani kununua gari , na alipo toka hapo moja kwa moja alienda showroom ya magari na kuchukua gari.
***
Profesa Gladness baada ya kupokea simu kutoka kwa CEO wa benki X kuwa mtandao umerudi kama kawaida , aliishia kutabasamu na kisha alijiandaa na kutoka kuelekea ofisini kukutana na Mery ambae alitaka kumpa baadhi ya maelekezo , na kwakuwa kutoka kwake kwenda ofisini alikuwa akitumia chopa basi alitumia muda mfupi sana kufika ofisini kwake .
“ Merry nadhani nishampata yule mtu niliekuwa nikimtafuta kwa muda mrefu sana ”
“ Kweli professa hongera sana niliamini kuwa lazima umpate”
“Yeah hata mimi nilikuwa naamini hilo ila nashukuru kwa sasa nadhani naenda kukamilisha lengo langu nililo kuwa nikiota kwa muda mrefu sana”
“Hongera sana profesa , sasa haujaniambia ni nani huyo?”
“Ngoja nitakuambia muda ukifika , nikishamleta hapa kwenye kampuni”
“Sawa madam natamani kweli kumuona huyo mtu anafananaje ambae anakwenda kuibadilisha dunia na kurithi mikoba yako”
*****
Steve hakutaka kuamini kile rafiki yake alichokuwa akimwambia kwania aliona kuwa yote yalikuwa ni maigizo na ndo maana baada ya Peter kuondoka hakutaka kuondoka mahali hapo mpaka amuone Peter akirudi kutoka huko aliko kuwa ametoka kwani aliamini peter alikuwa akimdanganya na hakukuwa na ukweli wowote ule , wakati wakiendelea kusubiri kama masaa mawili hivi baada ya kupita ndipo walipo sikia mlio wa pikipiki ukiingia ndani ya geti la nyumba hio na kumfanya Steve anyanyuke haraka na kuelekea dirishani kuangalia ni nani anae ingia , lakini kitu kilichomshangaza ni kwamba aliona pikipiki ya Peter kwani alikuwa akiijua kabisa lakini mwendeshaji hakuwa Peter mwenyewe kwani alikuwa ni mtu mwingine kabisa .
Wakati akiendelea kushangaa ndipo aliposhuhudia gari moja kali sana ilio kuwa ikionekana kabisa kuwa gari hio ilikuwa ni mpya ikiingia ndani ya geti lao na kitu kilichonfanya azidi kulikodolea macho gari lile ni kutaka kujua ni nani anakwenda kutoka ndani ya gari lile.
Lakini alijjikuta akipanua mdomo kama kabanwa na mlango kwania alimuona Rafiki yake akitoka kwa mbwembwe zote ndani ya gari ile aina ya aud .
Aliishia kusema tu peter
ITAENDELEA


WASILIANA NAMI KWA KUGUSA HAPAA
 
SEHEMU YA 11
“Peter usiniambie hii gari ni ya kwako?.”Aliongea steve
“ Hahaha.. steve tatizo lako una ugua ugonjwa wa kutokuniamini ila huo ndo ukweli kila unacho kiona ni uhalisia kwanzia sasa .
“ Wewe jamaa utakuwa jini , mimi hata siamini , unajua thamani ya hii gari wewe huwezi kununua kabisa , asiee siwezi kuku amini .
“Na mimi sitaki ni kuamiinishe vitu kama hivi nataka wewe mwenyewe kwa macho yako ndio uamini . huku akitoka mahali hapo na kuingia ndani akimuacha nyuma Steve aliekuwa akiendelea kukodolea macho gari lile .
****
Mwanadada Najma toka aingie ndani ya jijji la Dar alianza kuvuma kwa haraka sana na hii ni kutokana na kuanza kujihusisha katika maswala ya mavazi na mitindo , jambo ambalo lilimfanya kufatiliwa na watu wengi kwani mavazi yake yalionekana kuwa vutia watu wengi sana ikiwemo mastaa mbali mbali wa muziki na waigizaji swala ambalo kupitia kwao lilimfanya na yeye kujulikana kwa kipindi cha muda mchache sana .

Na moja ya mpango wake ulikuwa huo kwanza ni kufanya jina lake livume kwanza kabla hajatambulisha kampuni yake ambayo ilikuwa mbioni kukamilika .

Lakini kitu kingine kilicho mvumisha sana mitandaoni ni kwa urembo alio kuwa nao mwanadada najma , kwani hata mastaa mbali mbali walionekna kujigonga kwake jambo ambalo liliwafanya waandishi wa habari mbali mbali kutaka kujua kama mwanadada huyo kuna mwanaume ambaye anatoka nae kimapenzi , lakini japo kwa kufatilia sana na kumuuliza mwanadada huyo kuhusu mwanaume ambaye anatoka nae kimapenzi lakini alisema kuwa hana mwanaume ambae anatoka nae kimapenzi kwa wakati huu na aliongezea kabisa kuwa hakuna mwanaume yoyote ambae ashakuwa nae kabisa katika mapenzi , majibu yalio inua swali lingine kama yeye bado ni bikra . lakini jibu alilo litoa lilifanya swala hilo lizidi kumvumisha kwani alijibu kuwa yeye bado ni bikra na bado hajawahi kukutana na mwanaume yoyote mpaka wakati huo jibu ambalo kwa watu wengi hawakuweza kuliamini kabisa

Na ni kweli kwa mtu wa kawaida asingeweza kuliamini jambo kama hilo kwani ni kama kitu ambacho kimezoeleka katika jamii yetu kuwa wanawake wengi hujihusisha na mapenzi wakiwa wadogo kabisa na hususani kwa wale wasichana ambao wanaonekana kuwa warembo, ni vigumu sana kwa wao kuwa bikra kwa umri alio kuna nao Najma .

“Rehema hivi unajua nawashangaa watu wengi , hivi kwani mtu akisema kuwa ni bikra kwanini jambao hilo wanaliona kama ni uongo mkubwa .

“Najma unajua wewe ni msichana mrembo sana, na hata kusoma kwenyewe hujasomea hapa nchini kwa hiyo ukizungumza swala kama hilo ni vigumu sana kwa watu kuamini na hata mimi wenyewe siwezi kukuamini”.

“ Hahaha.. kwa hio hata wewe haumani kama mimi ni bikra au ?”.

“ Sio kama sikuamini ila mazingira yananishawishi na kunifanya nisikuanini”.
“ Basi hata mimi mwenyewe siwezi kuwaamininsha kuhusu jambo hili naamini mwanaume wangu wa kwanza kuja kukutana nae ndio atakuja kuamnini na akiamini yeye inatosha”
“ Ni kweli “
Huyo alikuwa ni Rafiki yake Najma ajulikane kwa jina la Rehema , ni marafiki waliokutana katika maswala hayo hayo ya mitindo na kuunda urafiki wao.
" Najma mwanangu sasa hivi ushakwisha kuwa maaarufu sana ni lini una kwenda kuanzisha kampuni yako kama ulivyo sema”
“Mama kuhusu kampuni ndio nakamilisha kila kitu na nadhani ndani ya mwezi ujao nitaitangaza rasmi na kuifungua”
“Wow! mwanangu uko vizuri sana , kuna muda niliona maamuzi ya Nasma kusomea hapa nyumbani yalikuwa sio sahihi , wewe sasa hivi ndio unaanza maisha yeye ndio anaanza Maisha ya chuo”
“ Ni kweli mama sema Nasma umemdekeza sana kiasi kwamba hataki kukaa mbali na wewe huoni sasa ulivyo muharibu”
“ Hapana nasma sijamdekeza ila alio chukua ni maamuzi yake wala hayanihusu mimi, kwani wote nimewalea kwenye malezi yalio sawa .
Wakati wanaendelea mara aliingia Tajiri Samir
“ Dadii, pole na kazi”
“Asante sana my daughter” .Huku akimwanaglia mke wake na kumpita bila hata ya kumsalimia na kuelekea juu ghorofani na kumfanya hata najma kuona kuwa wazazi wake hao kuna ugomvi .
Mama rania aliinuka na kisha kufata nyuma kuelekea chumbani kwake .
“Baba rania vipi kuna tatizo mume wangu , mbona unaonekana hauko sawa”
“Sikia mke wangu wala hakuna tatio ila nakuomba kwanzia kesho yule kijana mlie muajiri nisimuone pale , mfukuzeni”
“Mume wangu mbona s sikuelewi nitamfukuzaje mtu ambae ameanza kazi, pasipo kosa lolote si nitaonekana kichaa mimi , labda unipe hio ssababu kama nitaona ni ya maana nitamfukuza”
“Mama rania ukitaka tuelewane na kama mimi ni mume wako basi nakuomba ufanye kama ninavyo kuambia kabla sijachukuwa hatua nyingine”
“Mimi kama hautonipa sababu maalumu siwezi kufanya jambo kama hilo na isitoshe mimi sio niliomleta pale alie niambia nimlete kwenye benki ni dada yako na kama una tatizo basi anza kuongea nae na mimi nitafuata maagizo yake”
“Umeona sasa kumbe kaenda mpaka kwa dada, hii yote ni janja siwezi kukubali “ Aliongea Tajiri Samiri.
“Mbona sikuelewi mume wangu .. janja gani hio unayo izungumzia …”
“Mama rania naomba uniache , na kesho nisimuone pale benki la sivyo nitamfanyia kitu kibaya ambacho hautakkuja kusahau . aliongea huku akiingia bafuni .
Mama rania ilibidi atokea mpaka sebleni ambako alijikuta akiwa na mawazo , alikaa hapo sebleni .
“ Mamii.. mbna uko mwenyewe na unaonekana hauko sawa”
“Mwanangu rania hebu kaa kwanza maana najihisi kuchanganyikia kwa wakati mmoja”
“Kwani kuna nini mama”
“Unajua baba yako kwanza ana nichanganya maana sijui hata kajuajee kama kuna mtu mpya leo tumemuajiri maana karudi ananiambia nimfukuze”
“Unamzungumzia yule peter?”
“ Ndio
Rania alijikuta kuanza kukumbuka tukio la kule mlimani city akiwa na baba yake .
“Haa .. nimemkumbuka sasa , nilikuwa nikijiiuliza na mimii nimemuona wapi aa…”
“Umemkumbuka kivipi.”.
*****
MAREKAN-CALFORNIA 1900HRSPm
Ni katiaka jiji la calfornia ndani ya hoteli moja ya kifahali ijulikanayo kwa jina la Paradise ndani ya upande wa VVIP walionekana watu wawili wakiwa kwenye meza huku wakionekana wakiwa katika mavaz ya suti za gharama ya hali ya juu kabisa na walionekana sio watu wa Maisha ya hali ya chini kwani ukiachana na mazingira ya eneo hilo la hotelini lakini pia muonekano wao ulishashiria kuwa hao ni watu waliokuwa na ukwasi wa pesa..
Na hawa watu walikuwa wakifamika kwa jina la James Howard ambae alikuwa ni CEO na mkuregenzi wa makampuni ya IBM pamoja na bwana Mardon snart ambae na yeye alikuwa ni mkurengenzi na profesa wa maabara kubwa ijulikanayo kwa jina la THE STAR LABS .
“ Bwana Howard nimeomba hii appointment ya leo tukutane kwani nina jambo muhimu sana la kukwambia kuhusu mpango wetu wa kuishinda kampuni ya Space x katika harakati za kwenda anga za juu.
“Niambie comredi ni jambo gani hilo”
“Ni kuhusu professa Gladness , kwa taarifa kutoka kwa shushushu wetu ni kwamba professa tayari ashampata binadamu ambae nina uhakika atakuwa na mahusiano kabisa na alien”
“Una maainsha ashampata huyo mtu anaedhaniwa kuwa na akili nyingi ambazo ndio zitatuwezesha kuisukuma dunia mbele katika maswala ya kiteknolojia”
“Ndio kabisa japo bado hatujamfahamu kwa sura kwani mtu wetu bado haja tauambia kama huyo mtu ni nani haswa”
“Kama ni hivyo nadhani ni swala mabalo tulikuwa tunalisubiria kwa muda mrefu sana kupata hata taarifa yoyote inayo husiana na swala hilo .
“Ni kweli kabisa na ndio maana nimeona ni wakati maalumu wa kumuingiza Queen ndani ya Tanzania kwa ajili ya kumleta huyo mtu kabla hata hawajaanza kumtumia .
“Hilo halina shaka kabisa naungana na wewe katika hili , kwani kama tutweza kumpata mapema basi mambo yatakwenda kukamilika kama tuilivyo panga na tutakwenda kuitawala dunia katika Nyanja zote za teknolojia.”
“ Ni kweli kabisa”Huku wakigongesheana chears kufurahia mazungumzo yao kwani yalionekana kuwa na tija kwa pande zote mbili yaani kampuni ya IBM na STAR LABS
***
Los Angels -1930Pm
Huku upande mwingine ndani ya jiji la Los Angels alionekana mwanadada mrembo akiwa ndani ya chumba akiwa na mwanaume , mwanaume huyo akimwangalia mwanadada huyo akiwa akicheza kwa mapozi na kumfanya mwanaume huyo kupagawa kabisa kwani alikuwa amezubaa akiangalia kiuno hicho cha mwanadada huyo aliejaliwa kama malaika , mwanaume yule aliinuka kwenye kitanda ambacho amekalia na kumsogelea mwanadada huyo na kumsika kiuno na kusababisha mwanadada huyo kushituka kwa mtekenyo aliouhisi , na alimgeukia yule mwanaume na kutabasamu na kisha katika hali ya kushitukiza mwanaume yule alikanyagwa kwa kiatu cha aina ya heels na kutoa mlio wa maumivu lakini kabla hajakaa sawa alipigwa kwa staili maridadi kabisa kigoti cha tumbo kwa mzunguko na kumfanya kuinama na hapo ndipo mlangoni kuliingia njemba mbili ambazo zilionekana zimejazia miili yao kwa misuli , lakini ni kama mwanadada yule hakujali kwani pale pale alishika shingo ya yule mwanaume na kisha akizungusha na kuivunja pale pale kitendo kilicho amsha hamasa kwa wale njemba kwani walimfuata kwa kasi ya ajabu sana kumvamia lakini mwanadada yule aliruka moja ya sarakasi matata sana ya mzunguko na kwenda kutua kwenye gauni lake na kisha akalivaa huku njemba moja ikifata huku ikiwa imedhamiria kurusha ngumi nzito na kama ingempata mwnadada yule basi angekuwa hana hata jino moja lakini katika dakika moja yale manjemba yalionekana kuwa chini yote yakiwa tokwa na mapovu midomoni huku wakionekana wakipigania Maisha yao .
“Queen ….. ilisikika sauti kutoka mlangoni na kumfanya mrembo yule kuachia tabasamu ambalo ungezania ni la mtu mmoja mpole sana . kumbe alikuwa ni muuaji .
*****
Steve kila kitu ambacho alikuwa akikisikiliza kwa Rafiki yake, kilimfanya apatwe na mshangao wa kuto kuamini kabisa huku kwa wakati mwingine akiamini kuwa Peter alikuwa mtu hatari sana na sio kama alivyo kuwa amemzoea , kwani kitendo cha kuwaonyesha salio la benki kwenye akaunti yake kilimfanya kila kitu kuwa katika uhalisia wake na kuona kila anacho kifanya Rafiki yake kipo katika ukweli na wala hakukuwa na maigizo hata moja.
“Kaka kaka nimekuamini wewe ni mtu hatari sana aisee , unajua nilikuwa nakuchukulia poa sana ila sasa nimeona kweli uko seriasi aisee..mzee wa no syntax Error”
“Steve huu ni mwanzo tuu nitahakikisha yule mzee anatoa machozi kwa kucheeza na mtu mwenye akili zangu kama mimi , yaani nitamfanya aishi Maisha ya wasi wasi .
“Daaah kwa hizi dalili kweli inaonesha kweli kabisa unaenda kumfanya aishi Maisha ya kimawazo sana”
“ Unajua Steve kuna kitu nilicho kigundua ni kwamba yule mzee inaonekana hana mtoto wa kiume na hili ndilo jambo ambalo linamsumbua sana kichwa kwani anaona zile mali zake zitaenda kwa mwanaume ambae ataona na mtoto wake na ndio maana kila mtu anaeona yupo karibu na mwanae anaona anamtongoza”
“Hahaha.. ni kweli hata mimi nimeanza kuona hilo”
“ Sasa hapo ndipo nitamfanya alie na kuishi kwa wasi wasi kwani nitacheza na watoto wake wote na kuwafanya wanipende kiasi cha kufa na nitawatumia kuchukua mali zote, ili nimfundishe adabu”
“Peter huko unakoenda sasa ni mbali kuhusu mali achana nazo kwanini usifanye tu kuwatoa bikra uachane nao halafu uendelee na Maisha yako kwani hiko kisasi kinaweza kukufanya usiishi kwa furaha”
“Mimi nishaamua Steve na kwa sasa tuachane na hayo , kwanza hebu takale bata kidogo kwanza na ndinga mpya”
“Haha kweli hapo umeongea ni wakati wa kula bata huu , ila nataka tukamchukue mshikaji wangu anaishi Morocco anajua viwanja balaa .
“Anhaa unamzungumzia Sebastiani”
“Ndio yule jamaa .basi hakuna noma twende zetu , halafu Masumbuko hachoki kuangalia makatuni yake .
“Daah halafu umenikumbusha unaonaje tukienda nae kula bata”
“Wewe ulifikiri namuacha , huyu ni kama ndugu yangu kwa sasa na simwachi popote naenda nae .”
Basi walivaa nguo za kuvutia kabisa huku Masumbuko akiwa ndio ametoka chicha kwania alionekana moja ya bonge la Hb huku akifuatiwa na Peter na kama ungewaona Peter na Masumbuko ungedhania kuwa ni mapacha kwani walikuwa wakifana kila kitu japo sura kidogo zimetofautiana ila miili yao ilikuawa ikilingana kwa kila kitu na nguo ambayo angevaa peter basi na masu,mbuko nae alikuwa akivaa .
Walichukuwa nusu saa tu kufika Morocco ambako anaishi Rafiki yake Steve aitwae Sebastiani , na bahati nzuri walimkuta Sebastiani huo ndio wakati ambao alikuwa akijiandaa kwa ajili ya kwenda misele lakini alipomuna Rafiki yake akiwa na Peter wakiwa kwenye gari moja la bei ghali alijikuta akishangaa.
Steve alimwita Sebastiani na kisha wote kwa pamoja waliingia ndani ya gari.
“Steve huyu mshikaji ndio ulio niambia kuwa ana uwezo wa kubadilisha mawazo ya mtu .
“ Yeah ndio huyu anaitwa bwana Bahati Masumbuko”
“Haha .. basi leo nitaona uwezo wake kuna demu namkubali balaa ila kila siku ananichomolea na washikaji wameniambia kiwanja chake cha bata sasa nataka leo bwana Bahati akanisaidie kulifanya hilo”
“Jamaa saivi hana uwezo kama huo mzee acha kujisumbua kama hunaswaga wewe tuachie wababe”.Aliongea steve kwa majiagambo .
“Wewe mimi kama ashawahi kukugeuza house girl basi naamini kazi lazima ataiweza leo , na naamini hilo”
“Haya tutaona mzee , aliongea Steve na kumfanya Peter alikuwa akiendesha gari kutabasamu mazunguzmo yalivyokuwa yakiendelea na wakati hu ndio waliokuwa wakiingia club ya mji kati sinza kwenye hoteli moja ilio kuwa ikiaminika sana kwa kuwa na bata sana kwani kulikuwa warembo kibao pamoja na wasanii wengi walio kuwa wakipenda sana kuhudhuria ndani ya hoteli hio .
Peter aliegesha gari yake pembeni kidogo na moja ya gari moja kali sana ya rangi ya pink BMW X7 New model 2020, Peter alijukuta akiangalia na kisha kutoka na wenzake wote .
Ndani ya hoteli hio katika upande wa Bar mambo yalikuwa si mambo kwani walionekana warembo wengi na Mabrazameni wakiwa katika mikao ya kula bata , huku wakina Peter wakiwa wamekaa upande mmoja wa kona ndani ya club hio huku kila mmoja akionekana kufurahishwa na kinacho endelea humo ndani.
Wakati wakiendelea mara walimuona msichana mmoja mkali sana mrembo,moja ya wasichana ambao walikuwa ni maaarufu sana na alikuwa kawika hivi karibuni na si mwingine ni Najma akiwa na msichana Rehema .
“Unajua Steve ni kwambie nini wale watoto wa yule Tajiri ni shida yaani ni wazuri ila ubaya ni kwamba inaonekana mzee wake ana walinda sana”Aliongea Sebastini huku sauti yake ikiliwa na kelele za mziki mnene humo ndani , kwani hata ongea yake ilikuwa ni ya sauti kubwa
“Tajiri gani huyo Sebstiani” Aliuliza peter.
“ Si boss Samir na mtoto wake yule pale kile kisu kikali kabisa kilicho vaa mavazi ya kihasara hasara halafu kinasema kipo bikra”
Peter aliinua macho na kumuangalia ule msichana lakini kwakuwa mle ndani mlikuwa na mwanga hafifu basi hakuweza kumuona vizuri japo alikuwa akionakana mzuri hata kwa taa zile za club za giza giza.
“Hahaha … kama ni hivyo basi nishapata udhaifu wa kuwapata hawa wanawake wa huyu Tajiri”Aliongea Peter na kumfanya Steve amuangalie .
Na hapo peter akinyanyuka na kuondoka hilo eneo . na alionekana kabisa alikuwa akielekea chooni kwani mkojo ullikuwa umembana sana , aliingia sehemu ya wanaume ya kujisaidiana kisha kunawa mikono na kisha akatoka hapo ndipo alipo jikuta akikosa umakini kwani ile anakaribia upande wa vyoo vya wanawake ndipo alipojikuta akigongana na msichana na kwakuwa yeye alikuwa na nguvu na yule msichana alikuwa amevalia viatu vya mchuchumio basi alijukuta akikosa balansi na kuelekea chini lakini kabla hata hajatua tayari Peter alikuwa ashamuwahi .
Huku upande wa marafiki zake Peter , Sebastiani aliijikuta macho yake yakiganda kwa mwanadada mrembo alie valia kigauni Fulani kifupi kilichovuka magoti kwenda chini akiingia ndani ya club hio alikuwa ni mrembo haswa mpenzi msomaji , ni wale wadada wanaitwa ma Blackbeuty wenye maumbo matata sana .
“Sasa bwana Masumbuko mtu mwenyewe ninamtaka naona ashawadia sasa nataka unifanyie kazi kwa kutumia uchawi wako , ukifanikiwa na kupa hela ya maana .
Maneno hayo ya hela yalimfanya bwana Masumbuko kutabasamu na kuitika kwa kichwa kuonesha kuwa amekubaliana na maneno hayo.
SEHEMU YA 12

“Sasa kaka unataka nikifika pale ni fanye nini na kama uwezo wangu sina maana niliombewa itakuwaje?”
“Wewe mimi naamini uwezo wako unao bhana hebu nenda kafanye ninavyo kuambia uje uchukue pesa yako achana na hawa wagalatia wanaomwamini tapeli Mwaposa” Aliongea sebastiani huku akishindwa kufikiria kuwa kuna hatari gani kwa jambo ambalo alikuwa akitaka kulifanya .
“Oya Sebastiani muache Masumbuko bhana uwezo wake aliokuwa nao ni kwamba hana kwani zile zilikuwa ni nguvu za giza na zishatolewa”
“Nyie majamaa mbona si waelewi kuna kipi kinaendelea hapa?” Aliuliza Peter baada ya kuwafikia wenzake .
“Halafu wewe ulienda kuserebuka nini?” Aliuliza steve
“Acha tu yalio nikuta huko ni majanga Zaidi ya majanga ila nitawaambia kilicho tokea tukirudi home”
“Masumbuko sasa hebu nenda bhna achana na huyu Snura majanga sijui majanga gani watu tuko kwenye starehe zetu bwana” Aliongea Sebastiani kwa kilevii kwani wakati huo pombe zilikuwa zishaanza kumkolea.
“Masumbuko japo alikuwa na uoga aliamka kivivu na kuelekea upande wa kushoto ambako ndiko msichana mrembo kutoka UDSM ajulikanae kwa jina la Stella ndio alikuwa upande huo akiwa na marafiki zake.
Peter na mwenzake Steve walijikuta wakipatwa na hofu kwa kudhania kuwa Masumbuko hana uwezo wowote wa kumbadilisha mtu kimawazo na kumpa kumbukumbu nyingine za masaa mawili , waliogopa lakini kila mmoja kwa wakati huo walikuwa wakitaka kujua kama kweli Masumbuko alikuwa na uwezo wake kwani tokea aombewe hakujaribu uwezo wake hata maramoja kwahio hio ni kama jaribio analoenda kulifanya na ndio maana wakina Steve walikuwa wakingoja kwa hamu kuona kama kweli ulikuwa ni uchawi au ulikua ni uwezo ambaoo alikuwa amezaliwa nao.
“Hey! habari zenu” Alisalimia kimapozi Masumbuko na hata mimi mwenyewe msimuliaji sikujua kuwa hayo mapozi kajifunzia wapii kwani alisalimia kiswaga Zaidi na kuwafanya wale waremboo wainue macho yao na kumwangalia Masumbuko .
“Hi” walijibu wale wadada kimapozi Zaidi maana na wao walikuwa washaanza kumkubali Masumbuko kwani muonekano wake ulikuwa bomba Zaidi .
“Samahani Stella naomba kuongea na wewe mara moja”
“Ongea tu.” Alianza kuleta nyodo .
“Naomba tukae meza ya pembeni kidogo ni jambo binafsi kama hutojali mrembo” Aliongea Masumbuko huku akijifanya kama mtu mwenye hela zake huku akitabasamu.
Stella kivivu sana aliamka japo alikuwa anajua kabisa ambacho anakwenda kuambiwa ila muonekano wa Masumbuko kidogo ulimfanya ajiinue bila kutaka na kusogea pembeni .
“Enhe ulikuwa wasemaje kaka yangu?” .
“Naitwa Virus” Aliongea Masumbuko alipo jitambulisha na kumfanya dada yule amwangalie kwa mshangao wa jina lake .
“Mhmh! , haya virus ulikuwa unasemaje”
“Stella unajua kuwa katika wasichana ambao nimewaona ni warembo wewe unaongoza , na kwa macho yangu ninavyokutizama ni kwamba urembo wako ni wa kipekee sana na unakufanya unaonekana kuwa mremb Zaidi ya wengine”(Shughuli ya Masumbuko hio )
“Yule boya anaongea nini na yule demu mbona kama ana mtongoza vile” . Aliongea Sebastiani baada ya kumuona Masumbuko ilo pozi alilowekewa na Stella na kumfanya wivu umkabe .
“Haha… tulia wewe yule ndio masumbuko haha.. angalia demu mpaka kakunja nne , chalii ashaanza kuchangamka yule channeli ya Sinema Zetu imemchangamsha” Aliongea Steve na kmfanya Sebastiani aanze kujutia kwa kitendo ambacho amekifanya kumuagiza Masumbuko
“Hivi wewe Sebastiani yaani unamwamini mwanaume mwenzio kwenda kukutngozea demu kama yule , Masumbuko anaweza asiwe vizuri kwenye vitu vingine lakini anahisia yule na hata yeye anapenda warembo kama wale , ila ngoja tuone”
“Mhmh sasa virus kaka yangu kwanza umenijuaje juaje, na hii ni mara yangu ya kwanza kukuona na kama ukisema hapa club ni kwamba nimekuja leo tu na sijawahi kufika hapa hata mara moja na marafiki zangu ndio walio nilazimisha kuja hapa ,hivyo umenijuaje?” Aliongea stella huku alikiuwa akianza kabisa kuonesha kujitetea mbele ya masumbuko .
“Hivi unadhani Stella ni nani asie kujua pale chuoni kwenu kwa uzuri ulio kuwa nao , lakini tuachane na hayo huu ndio mwanzo wa mimi na wewe kufahamiana , kiukweli Stella nimetokea kukupenda sana na nataka usiku huu tuwe pamoja” Aliongea Masumbuko na kumfanya Stella kushtuka maana hakutarajia neno hilo maana yeye alidhania anatongozwa kumbe anaombwa gemu .
“Unasema usiku huu…” Aliongea Stella kwa kuhamaki lakini hapo hapo ndipo Masumbuko alipoanza kufanya yake kwani wakati Stella akiwa amemkodolea macho ndio wakati huo huo Masumbukoo alipompa mawazo ya kumkubalia hapo hapo( Masaa mawili ya kumbukumbu )
“Okey virus nimekukubalia lakini naomba usinichezee nakupenda Virus .” Aliongea Stella na kumfanya Masumbuko atabasamu na kuona kwamba nguvu zake hazijapotea .
Sasa huku upande kwa wakina Sebastiani hali ilikuwa ni mbaya kwani kuna muda Sebastiani alitaka anyanyuke akawakatishe wakina Masumbuko na Stella kwani aliona kabisa dalili mbaya za demu anayempenda kwenda kwa Masumbuko .
“Sebastiani tulia bhana wewe wakati ulipo kuwa unamwagiza si ulitaka akajitoe muhanga sasa wewe tulia tuone mpaka mwisho hili muvi la kufurahisa na kusisimua” Aliongea Peter huku akimzuia Sebastiani .
Sasa kilicho wafanya wapagawe ni pale walipo waona Masumbuko na Stella wakiamka na kuwasogelea maarafiki zake huku wakiangalia na kwa kutabasamu .
“Jamani huyu ni mpenzi wangu kuanzia leo anaitwa virus ‘ alingea stella na kuwafanaya wenzake waanze kumshangaa , maana walikuwa wakimjua Stella kwani alikuwa mgumu sana kwa wanaume .
“Shosti mbona leo unatupa surprise za usiku usiku jamani” Aliongea moja wa marafiki zake aitwae Nusura .
“ Jamani tutaongea kesho maana naenda kupumzika na shemeji yenu kwa sasa”
Hapo ndipo marafiki walipo achwa mdomo wazi kwani wakati wanaendelea kushangaa tayari walikuwa washaanza kutoweka
“Mhmh .. makubwaa.., Stella huyu huyu.. au kuna uchawi”
“Bwana wee Nusura acha mwenzio akale bata , kwanza humuoni yule mkaka alivyo kuwa handsome lazima achanganyikiwe”
Sasa wakati Masumbuko wanaendelea kupiga hatua kwa jili ya kuingia kweye lift kwenda flour za juu ambako kulikuwa na vyumba vya kulala ndipo walipo kutana na Sebastiani mbele yao .
Masumbuko kwanza aliogopa ila alijikuta akitulia na kisha kumsogelea Sebastiani, sasa Sebastiani alikuwa amemkodolea jicho Masumbuko na Masumbuko hakutaka kufanya makosa hapo hapo kwani tayari alikuwa ashachezesha mboni za macho na kumpa mawazo Sebastiani ya uhudumu wa bar kwa masaa mawili huku yeye akienda kula kitumbua cha mrembo Stella .
Wakina Peter na Steve wlikuwa kwenye mshangao hasa pale walipo muona Sebastiani akiwapisha kabisa Masumbuko kwa hiari yake na kisha yeye akaanza kukusanya chupa za bia na kuzipeleka kwenye kaunta .
Jambo hilo lilimfanya Peter aangue kicheko huku akimwangalia Steve ambae alikuwa kwenye mshangao wa kile kilicho kuwa kinatokea kwani alishuhudia Rafiki yake Sebastiani akiokota chupa za bia na kuona kuwa tayri hapo Masumbuko alikuwa ashatumia uwezo wake.
“Steve unaona mwanzoni haukumwamiini Masumbuko lakini ona sasa kinacho tokea , Masumbuko mwenyewe alikuwambia ule uwezo kazaliwa nao ila wewe ukampeleka kwa mchungaji , mwangalie sasa Steve , hahahaha… halafu mna amuona kama masumbuko hasimamishi wewe na rafiki yako mna mpa mrembo kama yule .. ngoja akapewe dozi haha..”
******
STAR LAB ni kampuni kubwa ambayo ilikuwa ikihusika na maswala mbalimbali ya kiteknolojia hususani katika maswala ya utafiti wa maswala ya kisayansi katika upande wa kibailojia zaidi na pia ilikkuwa ikihusika na na mawasiliano na uundaji wa maroboti , kampuni hii inamilikiwa na tajiri mkubwa ajulikanae kwa jina la Snart jina maarufu sana au Profesa Snart , au Mardon Snart
Licha ya kumpuni hii kujihusisha na maswala mbali mbali kama maswala ya kiugunduzi lakini ilikuwa na project ya siri ambayo walikuwa wakihitaji kuja kuikamilisha kati ya kampnuni hio na kmpuni ya IBM ilio kuwa ikimilikiwa na Tajiri Howard , Project hio ilipewa jina la kodi TOP ON FILE PROJECT jina hili alikuja nalo Profesa Snart , kodi ya project hii ilikuja kutokana na falsafa ya profesa huyu iliokuwa ikisema
“If you want to succeed make sure your name is top on file”
Unaambiwa profesa huyu ndio profesa pekee mzungu ambae alikuwa na lugha ile ya kitaa , au ya kinegro , alikuwa na matusi balaa , lakini alikuwa ni jembe alikuwa na kichwa hatari sana na hata kuna kipindi unaambiwa anaitwa kwenda kufundisha katika baadhi ya vyuo vikubwa kama vile Havard , Chicago , Michigani na vinginevyo vikubwa , unaambiwa kipindi chake alikuwa akitumia lugha ya kinegro kuliko formal language , lakini wanafunzi wanaelewa mpaka wanalewa.
Sasa ndipo alipokuja na ‘Poject Top On file’
****
MIAKA KUMI NA NANE NYUMA
TOP ON FILE PROJECT
Miaka kumi na nane nyuma ndio ilikukwa miaka ya mafanikio ya kampuni hii ya STARLABS kwa kile walicho kitengeneza katika maswala ya tafiti zao za maswala ya anga yaani mawasiliano ambayo yalikuwa yanahusisha viumbe kutoka sayari nyingine kwa kile ambacho walikuwa wakiamini kuwa katika sayari nyingiine kuna uwezekano mkubwa wa watu kuishi kama hapa duniani , lakini kutokana na swala hilo. Professa Snart alikuja na nadharia ambayo aliifikiria baada tu ya taarifa ya kushuka kwa kiiumbe kutoka sayari nyingine kilicho pita katika maeneo ya Africa rejea Blue Book Project.
Lakini kutokana na watu kuja na nadharia nyingi, nadharia moja tu ya profesa Alan walker kutoka chuo kikuu cha Monash Australia ndio ilimvutia Profesa Snart nadharia hio ilikuwa hivi kama kiumbe kutoka sayari(Alien) nyingine kwa jinsi inavyodhaniwa kuwa na uwezo mkubwa sana wa kusoma mawazo ya bianadamu basi kama kingepita wakati mwanamke yeyote atakuwa kwenye ujauzito wa miezi mitatu(First Trimister) basi kuna uwezekano mkubwa wa kiiumbe kitakacho zaliwa kuwa na akili nusu kama za Alien kwani aliamini kuwa Alien walikuwa wana uwezo wa ku manipulate genes(kuchakachua mfumo wa kawaida wa viini virithishi vya binadamu na kuweka vya kwao ) .
Ndipo proffessa snart alipo kuja na nadharia yake moja ambayo ilipata support kutoka kwa kampuni kubwa ya teknolojia ya IBM nakuja kuzaa Top On File Project, nadharia hio ilikuwa ni kutumia muundo wa DNA ambazo zilikuwa zimehifadhiwa katika kitengo cha sayansi ya taifa la maarekani, DNA hizo ambazo zilikuwa zikiaminika kwamba zilikuwa na muundo kama wa kiumbe kutoka sayari nyingine kwa kile kinaacho semekana kuwa muundo huo ulikuwa tofauti kabisa na muundo wa DNA za binadamu wa kawaida , haikuwahi kujulikana ni kwavipi kitengo cha sayanzi cha marekani kilikuwa na muundo wa DNA hizo, na unaambiwa ni tafiti nyingi zimefanyika kujaribu kuweza kugundua DNA hizo kuhusiana na kiumbe chochote duniani lakini mpaka wakati huo hakuna mwanasayansi ambae aliweza kupata muundo wa DNA hizo kwa viumbe hai wote wanaopatikana katika uso wa dunia na ndipo walipokuja kuhitimisha kwamba muundo wa DNA hizo ni za viumbe kutoka sayari nyingine (Alien).
Ndipo Proffesa Snart alipoamua kutumia muundo huo kutengeneza kiumbe kilicho kuwa na vinasaba vya aina hio na unaambiwa ni jambo lililomchukua miaka mingi kukamilisha muundo huo , lakini kutokan na nadharia yake kutokuwa katika swala la uhalisia aliamua kutumia yai la mwanamke na kulirutubisha kwa mbegu za mwanaume kwa kutumia tube (vitro fertilization ) , na kisha aliamua kutumia mionzi ambayo aliimuilika kwenye lile yai ambalo lilikuwa tayari limekwisha kurutubishwa na kisha kuweka muundo ule wa DNA hii ni kutokana na kwamba mionzi hio ilikuwa tayari ina mulika kwa muundo maalumu unaofanana na DNA zile zilizohifadhiwa katika kituo cha sayanzi cha taifa la Marekani .
Mwanzoni jambo hilo aliona kama halina uwezo wa kufanikiwa lakini baada ya miezi kadhaa alijikuta akiwa mwenye furaha sana na kuona swala lake hilo limefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana kwani aliona dalili nzuri za utafiti wake .
Lakini baada ya miezi tisa hatimae mtoto alitoka katika tube ambayo alikuwa akimfanya akuwe(grow) , lakini jambo ambalo lilimfanya akate tamaa ni kwamba mtoto aliekuwa ametengenezwa alikuwa ni binadamu wa kawaida sio kama vile alivyo kuwa ametegemea kwani alijua kabisa kutakuwa na utofauti lakini hakukuwa na utofauti wa aina yoyte kwa mtoto alie mtengeneza na hata DNA zake hazikubadilika na hapo hapo ndipo alifikia maamuzi ya kutangaza kuwa projekti yake hio imefeli ,kwani ilipita miaka kadhaa ya mtoto huyo kukua, na jinsia yake alikuwa wa kike , lakini kutokana na kwamba alitumia pesa zake nyingi sana katika kumtengeneza mtoto huyo aliamua kumtumia mtoto huyo katika kurudisha kile alicho poteza , ndipo alipoamua kumpa jina la Queen rasmi .
Queen baada ya kufikisha miaka kadhaa ya kukua kwake alipelekwa katika kambi ya jeshi nchini Cuba ambako alidumu mpaka akawa msichana wa miaka kumi ndipo alipo tolewa na kupelekwa nchini Thailland , ambako alidumu kwa miaka mitatu na kisha kupelekwa katika msitu wa Amazoni.
Na mafunzo aliokuwa akifundishwa kwenye msitu wa Amazon yaliikuwa ni mafunzo ya ukatili sana kama uuaji na kadhalika .
Baada ya miaka kumi na saba ndipo Queen alipo rudi nchini Marekani ambako alianza kufundishwa sasa jinsi ya kuishi kama mwanamke, kwani waliamini kwa uzuri ambao alikuwa nao Queen basi ingekuwa ni siraha tosha kwa shughuli za kiujambazi na mauaji na yote hayo ilikuwa ni mipango ya bwana |Snart kumtumia Queen katika harakati zake za biashara za magendo lakini pia katika maswala yake ya kupora mali za watu na kuua washirika wake. .
Queen baada ya kurudi mafunzonii ambako alikuwa ni moto wa kuotea mbali sana kwani hakuna kitu ambacho alikuwa hakijui sio mapigano sio ufundi sio maswala ya kuendesha ndege , vitu vyote hivyo alikuwa na uwezo navyo .
Siku Queen alipotolewa katika mafunzo ya kuishi kama nwanamke alionekana kuwa mrembo wa kuvutia sana , kwani kila mwanaume aliekuwa akimuona alipagawa kwa urembo wa Queen , ilikuwa sio tembea yake kila kitu ambacho alikuwa akifanya Queen kilionekana kuwa ni kivutio kwa watu wengi , huku watu wengi wakimuona mwanamke huyo kuwa mwanamke ambae hajawahi kutokea katika eneo hilo la Calfornia kwa uzuri.
Uzuri na umaarufu wa Queen ulimpa sababu Profesa Snart kumfungulia Queen kampuni kubwa ya mitindo , kwani ndani ya miezi kadhaa Queen alikuwa ni maarufu sana na kuwa na wafuasi wengi katika mitandao ya kijamii, huku mastaa mbali mbali wakiwa wanamfatilia kwa kina , lakini kwa kipindi chote hiko alikuwa akijua baba yake mzazi ni bwana Snart, tajiri na msomi mwenye roho mbaya sana , Na alichokuwa hakijui Queen ni kuhusu mama yake mzazi kwni bwana Snart aliishia kumdanganya Queen kuwa mama yake alikkufaga kwa saratani ya kizazi .
Lakini juu ya yote Queen aliokuwa akiyafanya hakuna mtu hata mmoja aliekuwa akijua msichana huyo alikuwa ni muuaji mkubwa sana kuwahi kuwepo katika uso wa dunia tena mwanamke , kwani tokea alipokuwa mdogo yeye alikuwa akifundishwa kuua tu , na alichukulia swala la kuua kama anavyo chinja kuku au mnyama buchani kwani hakuwa na huruma hata kidogo na ni kwamba mchana alikuwa akionelkana kama msichana mmoja mstaarabu na mrembo lakini mambo ambayo alikuwa akiyafanya yalikuwa usikuy ni ya kutisha na hakuwahi kufeli katika kazi au misheni zote alizo pewa katika kukamilisha mauaji.
Lakini jambo jingine ambalo Queen alikuwa nalo ni kulawitiwa na baba yake bwana Snart kwani alianza kulawitiwa tokea akiwa mdogo akiwa na miaka saba tu kabla ya kwenda mafunzoni na kwakuwa kipindi hicho alikuwa mdogo basi alikuwa kila siku alikuwa akilawitiwa na bwana Snart na hata alipo kuja kurudi akiwa mkubwani kama vile alikuwa ameolewa na bwana huyo kwani alikuwa akifanya mapenzi na bwana snart huku akijua kabisa ni baba yake , lakini kutokana na yale mafunzo aliokuwa akipewa wakati akiwa mafunzoni yalimfanya kuona ni jambo la kawaida kwake kwani aliona ni moja ya kutii kile ambacho bosi wake alikuwa akitaka kwani kwa upande mwingine alimchukulia baba yake kama bosi wake na kila jambo analo fanya ana tii kile ambacho bosi wake anataka atii.
“Hio ndio historia fupi ya mremboo Queen na Failed project Top on file .
****
Siku mbilii baadae baada ya Queen kumaliza mauji ya Tajiri mmoja na siku ambayo Profesa Snart anakutana na Howard ndio siku ambayo bosi wake ambae alikuwa akijua ni baba yake bwana Snart alimuita na kumpa misheni ya kwenda nchini Tanzania kwa ajili ya kumfatilia mtu ambae alikuwa akijua kuwa huyo ndie mtu ambae atakuja kuleta mageuzi makubwa katika maswala ya kiteknolojia , kama tu watafanikiwa kumpata katika mikono ya proffesa Gladness
Alipewa kila kitu kitakacho msaidia katika kazi yake na alitakiwa kuingia nchini kama mtalii na kwakuwa likuwa maarufu sana swala hilo lili rahisisha kila kitu na kilicho kuwa kikisubiriwa ni mwanadada huyo mrembo kuingia ndani ya nchi ya Tanzania huku akija kwenye maswala ya utalii na katika maswala ya ziara kama mrembo, kwanii aliahidi kuwa atatembelea baadhi ya vituo vya watoto yatima na kutoa msaada na serikali kama unavyojua kujali misaada basi walimkubalia mara moja ..
***
DAR ES SALAAM –Present
Tukirudi masaa mawili kadhaa nyuma ndani ya hoteli aliokuwemo Peter na marafiki zake , akiwa chooni baada ya kugongana na mwanadada yule ambae Peter kwa wenge lake wala hakuwa amemuangalia sura na kumfahamu Zaidi ya kumuachia na kisha akaondoka zake , lakini kwa mdada yule alikuwa katika hali ya mshituko kwani hilo lilikuwa ni jambo la kwanza katika Maisha yake kumtokea kudakwa na mwanaume , msichana huyo hakuw mwingine bali alikuwa ni Najma mtoto wa tajiri Samir .
Najma alijikuta hata alipo kuwa na wenzake alikuwa akiwaza tukio liilo tokea nyuma kidogo kwani kwake aliliona tukio hilo kama la kipekee sana kuwahi kumtokea , na hata alipo kuwa na wenzake kuna muda alikuwa akizungusha zungusha kichwa kumtafuata mwanaume huyo japo sura yake ameikariri lakini alihitaji kumuona hata kumwambia asante kwani wakati anadakwa na Peter alikuwa kwenye mshangao na mshtuko mkubwa sana na hakuweza kuzungumza chochote kwani alipokuja kuwa sawa mwanaume yule alikuwa ameshaondoka mbele yake .
“ Najma vipi mwenzetu kulikoni huko bafuni , maana tokea umerudi unaonekana kama hauko sawa hivi”.
“ Rehema wewe acha tu kilicho nitokea leo sipati hata picha yaani ni jambo ambalo halijawahi kunitokea kabisa kwenye Maisha yangu”
“Mhmh jambo gani hilo shosti mbona tunatishana sasa na wakati hapa duniani hakuna jambo jipya kila kitu ni marudio ya kile kilichowatokewa watu nyuma”
“Nitakuambia kesho tukiwa kazini lakini daah ..!!”
****
“Umekumbuka nini Rania , mbona kama upo kwenye mshangao tu halafu hauniambii “
“Mama yule mkaka tulishawahi kukutana nae Mlimani city” Huku akianza kumuhadithia mama yake kila kitu .
“Unajua mama pale alipo kuja nilikuwa nikivuta picha nimemuona wapi kwani sura yake nilikuwa nikiikumbuka”
“Mhmh sasa kwani si alikugonga bahati mbaya sasa baba yako kwanini akapaniki”
“Mimii hata sijui labda baba atakuwa anafahamiana nae?”
Mama rania alitingisha kichwa kuashiria kuwa amemuelewa mwanae lakini kama kuna kitu alikifikiria , na kitu hicho alikiona kuwa ni wivu tu wa mume wake ndio ulio kuwa ukimsumbua .
“Lakini kale kakijana nimekapenda , kanaonekana ni kastaarabuu halafu kana akili , huoni kalivyo kuwa kanaongea kuhusu ile pesa ya malipo kwa jili ya kazi napaenda watu wanai jiamini kama vile na wanaojichukulia ni wathamani” Alifikiria mama Rania huku kuna wajidudu kama walikuwa wakimtekenya na alitamani kesho kukuche ili akamuone tena kwani aliamini siku inayo fuata ndio siku yake rasmi ya pita kuanza kazi rasmi .
*****
Hakuna alie kuwa ameamini kama Masumbuko alikuwa ametoka na mrembo Stella na kwenda kulala nae , na Steve hakutaka jambo lilie liishie hivi hivi kwani aliamua kwenda mpaka upande ambako kulikuwa na lift na kweli alipo fika aliona lift ikijifunga na kuona kabisa lift inaelekea upade wa juu wala sio chini.
Masumbuko haikujaulikana sikua hio alikuwa amedhamiria ama laa kwani alitoka na mrembo huyo na moja kwa amoja walifika mapokezi huku akiwa ameshikwa kino na mrembo Stella , na Masumbuko kwa jinsi alivyo kuwa akionekana utadhani ni mzoefu wa muda mrefu katika mambo hayo .
Baada ya kufika pale mapokezi Masumbuko kama kawaida yake alimkonyeza yule dada na yule dada aliandika majina yao na kila akawapa funguo na hakutoa hata shilingi.
Baada ya kufika tu mrembo Stella ni kama vile alikuwa na siku nyingi hakuwahi kufanya mapenzzi kwani alianza kumpeleka lipsi zake na kuzigusisha na za Masumbuko na Masumbuko muda huo ni kama alikuwa kwenye mshtuko kwani hata hakutoa ushirikiano ,lakini kadiri muda ulivyo kuwa una kwenda alijikuta akianza kupata ufundi na yeye kuanza akuonyesha ushirikaiano katika kitendo kile, walichukua muda mfupi tu na Stella kama vile alikuwa akicheleweshwa kwani alivua nguo mwenyewe na kubakiwa na ya ndani tu huku akimvua Masumbuko tisheti alio kuwa amevaa .
Stella aligundua kitu katika Masumbuko kuwa alikuwa mgeni katika mambo hayo na hapo ndipo alipo ona kuwa kuna haja ya kumfundisha . kila kitu ili kuendana na yeye na kupata ile raha alio kuwa akiitaka . sasa si ndo akafungua mkanda wa Masumbuko na kushusha suruali ya masumbuko na kisha akamvua boksa.
Hapo ndipo macho yalimtoka Stella kwani hakuamini kile alicho kuwa akikiona .
SEHEMU YA 13
Dunguso ya masumbuko haikuwa imewika hata kidogo kwani kalikuwa kadogo kabisa kiasi kwamba kalikuwa kamemezwa kabisa , yaani hakakuonekana kabisa na kalikuwa bado hajatahiliwa , ilikuwa ni jambo la kuchekesha na kuhuzunisha kwa wakati mmoja na haikueleweka kuwa Masumbuko alikuwa hana uwezo wa kusimamisha au laa maana kwa hali hio aliokuwa nayo ilikuwa ni ya kusikitisha sana na kusisimua , mzuka alio kuwa nao Stella wote ulikuwa umeisha , alijaribu kila njia lakini hakuona mafanikio yoyote mpaka pale alipo enda bafuni na kujituliza mwenyewe haja zake na baada ya kutoka huko alikuwa amejichokea na kupitiwa na usingizi fofofo akiwa hana hata nguo huku Masumbuko yeye akikodolea jicho tu mwili wa Stella ulivyokuwa umeumbika.
Masumbuko yeye hakulala kwani ilipopita lisaa tu alivaa nguo zake haraka haraka na kisha akatoka eneo hilo na kuwatafuta wenzake , bahatii nzurii ni kwamba wakati huo ilikuwa bado wakina Peter walikuwa wapo , wakimwangalia Sebastiani anavyo zunguka huko na huko kutafuta chupa zilizo zagaa huku akiwafanya wahudumu waliokuwepo mahali hapo kumshangaa kwani hakuwa mfanyakazi wa eneo hilo .
“Vipi wewe muhuni mbona umerudi mapema ushamaliza kazi ?“ Aliulliza steve kwa shauku kabisa .
“Yeah nimempiga moja tu mtoto kazimia , halafu sijalipia bili ndio maana nimeondoka kabla kumbukumbu hazijarudi”.
“Wewe jamaa ni noma aisee , kwahio kazi umepiga fresh kabisaa” Aliuliza Steve ni kama vile alikuwa haaminii na pia hakuridhishwa na majibu ya Masumbuko .
“Tayari kazi na ndio maana niko hapa”
“Hebu kwanza Masumbuko ina maana bado uwezo wako wa kumpa mtu kumbukumbu bado unao”
“Ndio bado ninao si unaona kabisa mwenzenu kule kawa muhudumu”
“Hahaha.. sema una dhambi wewe , kwahio yule demu ulimpa mawazo gani maana Sebastiani alikutuma ukamsaidie ila wewe ulibuka na yule mtoto?”.
“Mwenyewe hata sijui hata kwanini nimefanya vile , nadhani kwakuwa ni mzuri sana na ndo maana nilighairi kumfanyia Sebastiani nikajifanyia mwenyewe”
“ Hahaha.., ila umemkomesha siku nyingine hato kuamini na kukupa kazi ambazo hazina maana na faida kwako maana kama pale lingetokea la kutokea kesi ingekuwa kwako na si kwake”
“Ni kweli umemkomesha ila adhabu ulio mpa sio ya kitoto sipati picha pale kumbukumbu zake zitakapo rudi”
“ Oya wadau nadhani huu ni muda wetu wa kuondoka si mnajua tena kesho nina ratiba ya chuoni na ya kwenda kazini” Aliongea Peter
“ Sasa unamaanisha tumuache Sebastiani hapa hapa au? “.
“ Hapana simaanishi hivyo namaanisha tuondoke nae”.
“Sasa tunaondoka nae vipi , au masumbuko unampa kumbu kumbu zingine za kuondoka na sisi”
“|Huo uwezo sina nikishampa mtu kumbukumbu mpaka arudiwe na fahamu ndio naweza kumpa zingine”
“ Mimi nina wazo ngoja muone , aliongea Peter huku akinyanyuka na kumfata Sebastiani pale alipo .
“Sebastaini wewe ni muhudumu mzuri sana na mshahara wako utaongezeka mara mbili kwani nina mpango wa kukuongeza mshahara , sasa kwa leo naomba twende nikupitise nyumbani kwako kijana wangu” Aliongea hayo maneno Peter akijifanya yeye ndio bosi wa Sebastiani .
Sebastiani kwanza hakutaka kumwamini Peter kwa moja na badala yake aliangalia wale wahudumu na kwa Peter alivyo ona jambo hilo mara ile ile aliwakonyeza wahudumu na wakamuelewa kwani hata wao walikuwa wakimshangaa Sebastiani kwa kile alicho kuwa akifanya , kwani hakuwa mfanyakazi wapale .
“ Kaka unaweza kwenda kupumzika tu sasa kazi zimeisha” Aliongea yule muhudumu wa kike na kumfanya Sebastiani aondoke na Peter na kwenda kuungana na wenzake huku Steve baada ya kumuona Rafiki yake ilibidi aangue kicheko cha chini chini .
Masumbuko aliinama na kumnong'oneza Peter akimwambia wampeleke nyumbani mapema kabla masaa mawili ya kumbu kumbu kuisha , jambo ambalo hata Peter mwenyewe alilikubali na kumuona kwa Masumbuko tokea aombewe kidogo akili yake ilikuwa ikifanya kazi maana alikuwa anatoa michango mizuri ya kimawazo na hata lile jambo la kwenda kumchukuwa yule Stella aliona kama jambo hilo kama yalikuwa ni mawazo mazuri.
“Ila unaweza ukawa huna uwezo wa kufikiria ila lkija swala la wanawake ukawa na uwezo wa kufikiria tena ule mzuri tu”
“ Unamaanisha nini Steve” Aliuliza Peter.
“Wewe hujaona alicho kifanya Masumbuko “
“ Hahahaha… dah kweli yani hata mimi nimeshangaa , Masumbuko kanifanya nifurahi sana leo”
Na wakati huo walikuwa tayari wakiingia eneo ambalo sebastianii aiikuwa akiishi .
Walimshusha na kisha baada ya kuona kabisa Sebastiani kaingia na kufunga mlango wote waliondoka mahali hapo na kuelekea nyumbani .
*****
Baada ya masaa mawili ndio wakati ambao mwanadada Stella ndio alikuwa akishtuka kutoka usingizini , na akiwa na akili zake timamu kabisa , kwani baada tu ya kuamka kwanza alijishangaa akiwa uchi na akiwa ndani ya hoteli hio kwani alicho kuwa anakumbuka mara mwisho alikuwa na mwanaume alie jitambulisha kwake anae itwa Virus na kumbu kumbu zake zilikuwa zikimkumbusha kuwa Virus alikuwa akimtongoza na hakujua kama alimpa jibu , lakini kingine kilicho mchanganya ni kuwa ndani ya chumba hicho, kwani alikuwa hakumbuki kabisa kuja ndani ya chumba hicho .
“Nimefikaje hapa??”
Alijiuliza huku akijaribu kujipapasa sehemu zake za siri kuona kuwa kafanya ngono , lakini kweli wakati anajipapasa aligundua kabisa sehemu zake zina ute ute ulioganda juu ya mashavu ya kitumbua na hapo hapo alijua kabisa aliingia (sasa haikuelweka alipo ingia bafuni hakujiosha au laa ) na mwanaume , lakini swali liliokuwa likija ndani ya kichwa chake ni kwa jinsi gani aliingia ndani hapo na mwanaume alie ingia hapo ndani ni nani maana alikuwa hakumbuki kabisa .
Lakini wakati akijiuliza mara mlango wa hapo chumbani kwake uligongwa na hapo alijua labda ndio mtu alieingia nae , alitoa khanga kwenye kijimkoba chake haraka haraka na kujifunga na kisha alienda kufungua mlango .
“Wewe dada mmechukua chumba lakini nakumbuka kabisa hamkutoa pesa , kwani kumbu kumbu zangu zinaniambia hivyo kwani mahesabu kila nikijumlisha hayakai sawa”.
“ Mimi na nani hatukutoa pesa! ..” Aliuliza Stella kwa mshangao na kumfanya na mhudumu nae kushangaa kwa swali hilo na kuona labda ni dharau .
“Wewe dada si ulingia na bwana wako humu kwanza hebu muite atoe hela zamu yangu ishaisha nataka kuondoka”
“Dada humu ndani niko mwenyewe kwanza naomba uingie kwanza uniambie ni mwanume gani niliingia nae maana mimi mwenyewe sielewei niliingia saa ngapi humu ndani”
Yule muhudumu alijikuta kuna vitu vikimshangaza na hata yeye alijishangaa kwani katika kumbu kumbu zake hakuwa na uhakika kuwa alililipwa pesa au laa maana hata hapo kwenda kuwagongea ni kwamba mahesabu hayakuwa sawa kabisa .
Basi yule dada alianza kumwelezea Stella kilicho tokea na hapo ndipo Stella kumbu kumbu zake zikamwambia kabisa mwanaume aliefanya nae mapenzi alikuwa ni Virus na alipo jaribu kuunganisha matukio aligundua lazima kuna kitu yule mkaka alimfanyia na kuona hivyo aliamua kutoa pesa na kumlipa muuhudumu na kisha akaingia bafuni kwa jili ya kuoga .
“Daah.. ! yaani kitumbua kimeliwa na hela ya chumba nimelipia mimi. Yule mwanume nitamtafuta mahali popote pale na nitahakikisha namfunga” Alijiapia Stella huku hasira zikimkaba kwani alikuwa akijiheshimu sana na hata siku moja hakudhania ataliwa na mwanaume kitumbua chake pasipo ya ridhaa yake.
Alitoka zake bafuni na hapo ndipo alipoikumbuka simu yake , aliifungua na kujikuta akitoa macho kwani alikuta missed call ishirini zilizo kuwa zikitoka kwa mpenzi wake James .
“Mama yangu namweleza nini mimi James?”
Stella alijikuta machozi yakimtoka mfululizo kwani alikuwa akimpenda sana James , na kilicho mfanya alie ni siku hio kuona kabisa kafanya usaliti kwa mwanaume anae mpenda .
Alifungua upande wa messeji na kukuta messeji moja tu ilio mwambia awashe data na messeji hio ilikuwa ikitoka kwa James , aliingia haraka haraka online na kufungua na hapo ndipo mapigo yake ya moyo yalipo simama baada ya kuona picha zake akiwa na mwanaume aliejitambulisha kwake kama virus akiwa ameshiliwa kiuno japo mwanaume alie mshikilia kiuno hakuonekana vizuri kutokana na taa za club ila alionekana yeye kabisa huku akiwa amezungushiwa mkono kwenye kiuno.
“Mimi na wewe hu undo mwisho wake , nimekuaga nasafiri kumbe wewe ulikuwa unafurahia kutokuwepo kwangu ili ufanye mambo yako , naomba kwanzia sasa tusijuane na ndoa nimesema hakuna na kwakuwa na kuheshimu na nilikupenda sana picha hizi sito waambia wazazi wako nitabeba lawama zote mimi na hii ndio zawadi ninayo kupa kukufichia maovu yako , Maisha mema ”
Hiyo ilikuwa ni meseji kutoka kwa mchumba wake stella aitwae james .
“lea alijikuta akianza kulia kilio cha kwikwi kwa kutokuamini mambo yalio kuwa yakimtokea alilia sana usiku huo huku akiona huo wote ulikuwa ni mpango wa kuvuruga mahusiano yake .
******
Mzee Elvice alikuwa ni moja ya matajiri wakubwa sana ndani ya Tanzania kwani alikuwa akimiliki mabasi mengi ya kusafiria , kiufupi kama utamfananisha mzee Elvice basi utamfananisha na Abood kwa utajiri wake , Mzee Elvice alikuwa akiishi kaatika jiji la mwanza ambako ndilo yalikuwa makao makuu ya kampuni yake ya mabasi .
licha ya kuwa Mzee Elvice alikuwa Tajiri lakini pia alikuwa ni mbunge kupitia chama cha CCM katika jimbo la Mwanza mjini na watu wa Mwanza walikuwa wakimuamini sana Mzee Elvice na kumpenda .
Familia ya mzee Elvice ilikuwa imejaariwa Watoto watatu , yaani wakiume wawili na wakike mmoja , ambao majinayao yalikua ni Moses , Lewisi na Stella .
Stella ndio alikuwa mtoto wa mwisho katika familia ya Mzee Elvice jambo ambalo lilimfanya Stella kupendwa sana na baba yake , kwanza alikuwa msichana pekee katika familia lakini pia Stella ndio moja ya Watoto wa mzee Elvice waliokuwa na akili sana .
Miaka minne nyuma ndio mrembo Stella alipojiunga katika chuo cha UDSM kwa ajili ya kusomea masomo yake ya sheria kama kitu alicho kuwa akitaka kusomea tokea akiwa mdogo
Mwaka huo alioingia ndio mwaka ambao ulimpa umaarufu sana kutokana na uzuri wake lakini kutokana pia na kazi ya baba yake kuwa mwanasiasa na Tajiri kwa wakati mmoja . lakini licha ya kwamba Stella alikuwa mzuri na kufatiliwa na wanafunzi wengi wa chuo hicho kwa ajili ya kutoka nae kimapenzi hakuwa na historua mbaya ya umalaya kwani mwanaume wa kwanza kutoka nae kimapenzi alikutana nae akiwa First year aliejulikana kwa jina la Abasi lakini walikuja kutengana baadala ya kumfumania Abasi na mwanamke mwingine jambo lilio mfanya aumie sana kwani alikuwa amempenda Abasi alijaribu kumsamehe Abasi kwa mara kadhaa kwa jambo hilo lakini hakubadilika na hapo ndipo alipoamua kuachana nae na kuja kukutana na kijana James kijana mpole alie kuwa amejaliwa uzuri wa sura na mwili , James yeye pia alikuwa akitokea katika familia iliokuwa ikijiweza kiuchumi lakini pia kilicho fanya uchumba wa James na Stella kuzidi kuimarika ni kutokana walikuwa wanapendana sana lakini pia familia zao zilikkuwa zikifahamiana , kwani baada tu ya mapenzi yao kuanza familia ililigundua hilo na liliwafanya wanafamilia kufurahia uhusiano huo na kuamua kuwabriki watoto wao katika safari ya mapenzi , na kipindi ambacho uhusiano wao unaanza ni wakati wapo mwaka wa pili mwishoni na uchumba wao ulidumu sana na kutokana na hilo walikuwa wakipanga kuoana pale ambapo Stella atamaliza chuo kwani James wakati huo alikuwa ashamaliza tayari chuo kwani kozi yake ilikuwa ni ya miaka mitatu na ya Stella ilikuwa ni miaka mitano .
Na familia zao walikuwa tayari kwenye mipango ya mwisho kabisa ya kuhakikisha Watoto wao wanaona kwani kilicho baki ilikuwa ni kusubiriwa kwa mwanadada Stella kumaliza chuo tu na ndipo ndoa ifungwe .
Lakini katika kipindi chao cha mapenzi kama ilivyo kuwa kwa binadamu wengi hawatapenda kukuona unafuraha na mambo yako yanakunyoonkea na hilo ndilo lililotokea kwa Stella kwani Rafiki yake wa karibu sana aliekuwa akimwamini sana hakupendezwa na mahusiano ya James na Stella na aliapia kwa namna moja ama nyingine lzima ayavunje mahusiano hayo na Rafiki yake huyo alikuwa akiitwa Lea .
Lea nae alikuwa akimpenda sana James japo kwa kujaribu kila mbinu ya kumuweka kaatika himaya yake lakini alishindwa kutokana na msimamo wa James kwani James nae alikuwa akimpenda sana Stella , jambo hilo lilizidi kuinua chuki baina ya Lea na Stella pasipo hata kwa Stella kujua kuwa Rafiki yake alikuwa akimchukia ,kwani kila kitu walikuwa wakishirikiana na Lea alikuwa akimsaidia Stella pindi anapoumwa na hivyo hivyo kwa Stella alikuwa akimsaidia Lea pale apatwapo na shida mbali mbali na uzuri ni kwamba Lea na Stela wote walikuwa wakisoma kozi moja ya uwanasheria . jambo ambalo lilikuwa ni gumu sana kwa Stella kumgundua kuwa Rafiki yake huyo alikuwa akimzunguka na alikuwa akivaa mask awapo mbele yake lakini anapokuwa mbali na yeye alikuwa akimfitinia.
Lea alijaribu kutafuta mbinu mbali mbali za kuwafanya James na Stell watengane lakini hakuweza kufanikiwa kutokana na kuwa maisha ya Stella hapo chuoni yalikuwa ya kipekee sana na hakuwa mtu wa starehe kama ilivyo kwa Rafiki yake ambae kila wikiendi alikuwa akienda kwenye starehe hususani club na Lea alikuwa akidanga sana.
Siku ambayo James alikuwa akimuaga Stella kuwa anaeleka Kenya kwa ajili ya kufatilia bishara za baba yake , siku hiyo Lea alisikia kila kitu na kuona hiyo ni nafasi ya mwisho kwake kukamilisha mpango wake wa kuawaachanisha Stella naJjames ili yeye achukue nafasi hio. Kwani katika mbinu alizowahi kufanya ni moja ya kila siku kumwambia James kuwa Stella anachepuka lakini kutokana na James kumwamini sana Stella hakuweza kushawishika na maneno ya Lea, ndio kitu kilicho mfanya Lea kuona lazima atafute Ushahidi ili kumwaminisha James na Lea alimuhakikishia James kuwa lazima amletee Ushahidi lakini James hakumpa ushirikiano .
Lakini alichokosea James ni kuto kukaa chini na Stella na kuzungumzia swala hilo, kwani James toka aanze kuwa na mahusiano na Stella walifanya mapenzi mara mbili tu na zote hizo ilikuwa ni kila mwaka katika siku ya kuzaliwa kwa Stella na kiufupi James alikuwa bize sana na mambo yake ya biashara kwani alikuwa si mkaaji sana na Stella .
Lakini kama ilivyokuwa kwa binadamu wengi na wanasaikoloojia wamelithibitisha hilo kupitia tafiti mbali mbali kuwa jinsi unavyo sikia neno la aina moja kila siku basi neno hilo linaweza kukufanya ubadili msimamao wako . na hivyo ndivyo ilivyo kuwa kwa James kadri Lea alivyo kuwa akimweleza kila siku kuhusu kuchepuka kwa Stella basi kila siku manano hayo japo mwanzoni alikuwa hayapi kipaumbele ila kadri siku zinavyo sogea na kwa jinsi alivyo kuwa akishuhudia wenzake wanavyo salitiwa na wapenzi wao ndivyo msimamao wake kuhusu stella ulivyo kuwa ukilegea ,na kuanza kutokumuamini Stella ,ndipo siku moja alipo muambia Lea kuwa amletee Ushahidi sio maneno tu , jambo hilo kwa Lea alilichukulia kama ushindi kwake na ndio maana siku zote alikuwa akitafuta siku ambayo atautengeneza Ushahidi kwa namna yoyote ile .
Na siku hiyo aliichukulia kama ushindi kwake siku hio alikuwa amepanga kutoka kwenda club na Stella na hiyo ni baada ya kumshawishi sana , lakini kilicho mpa nguvu ya kufanya hivyo ni maneno ya Rafiki yake Sebastiani.
Sebastiani na Lea walikuwa wakifahamina tokea kipindi kirefu sana na Lea alikuwa akimsaidia sana Sebastinai katika mambo mbali mbali kwani Lea pia kwao zilikuwa zipo na ndio maana alikuwa akimsaidia Sebastiani , lakini jambo moja ni kwamba siku moja Lea alimkopesha Sebastiani kiasi cha milioni tano kwa ajili ya biashara ambayo Lea mwenyewe hakujua inahusiana na nini , na Lea kwakuwa alikuwa nazo kwenye akaunti yake na Sebastia ni alikuwa rafiki yake basi hakuona jinai kumkopesha Rafiki yake huyo , lakini baada ya mwaka kupita Sebastiani alipo kumbushwa na Lea kuhusu pesa yake ,Sebastiani hakuwa na jipya zaidi ya kumwambia Lea kuwa biashara ilipata hasara , na kutoa ahadi atamlipa kwa wakati wowote kwanzia siku hizo za karibuni ,jibu ambalo kwa Lea alikubaliana nalo kinyonge . lakini siku alipo kumbuka kuwa anaweza kumtumia katika mpango wake wa kuvunja mahusiano ya Stella na James ndipo alipo ona jambo hilo litafanikiwa kwa kumtumia Sebastiani na siku moja alikutana na Sebastini kwa ajili ya kuzungumzia swala hilo na kwakuwa Sebastiani alikuwa anadaiwa basi alimwahidi lea kuwa atamsaidia Lea katika hilo.
Ndipo Sebastiani siku moja alipohadithiwa na Rafiki yake Steve kuhusu Masumbuko ,jambo la kwanza kukumbuka ni mpango wa Lea , na alimfata Lea na kumpanga kuhusu swala hilo na Lea alifurahi sana , lakini jambo hilo lilileta ugumu kutokana na Maisha ya Stell kutopenda kwenda club huku Sebastiani akimwambia Lea kuwa akitaka mpango wake ukamilike basi ampeleke Stella club , na katika kipindi chote hicho Lea anapanga mipango yake na Sebastiani , Sebastiani hakuwahi kumuona Stella hata mara moja , lakini siku ambayo alikutana na Stella mapigo yake ya moyo yalisimama hapo hapo kwani uzuri wa Stella ulimpagawisha sana na kuona kuwa James atakapo achana na Stella basi yeye atahakikisha anakuwa na Stella kimahusiano na kutokana na tamaa zake hizo zilimpa nguvu ya kukamilisha mpango wa Lea
Basi siku ambayo Stella alikubali kwenda club na Lea, ndio siku moja nyuma aliagana na mpenzi wake james akisafiri kueleka Kenya kibiashara .
Na ndio siku ambayo mpango wa kumwachanisha Stella na James ulisukwa na watu wawili yaani Lea na Sebastiani, huku Rafiki yao mwingine aitwae nusura hakuwa na hili wala lile .
Na siku hio club baada ya Lea kumuona Masumbuko aliona mpango wao unaenda kama alivyo panga na yote yalio kuwa yakiendela hapo alikuwa akiwapiga picha na hata wakati Stella anakuja kumtambulisha Masumbuko kama mpenzi wake na kumfanya Lea ashtuke kwani mpango wake ulikuwa ni Stella kwenda kulala na Sebastiani lakini kilicho mshangaza ni Stella kumtambulisha Virus kama alivyojitambulisha , lakini kwake hakuona jambo hilo lina muhusu kwani aliona hana cha kupoteza na ndio maana hata wakati Stella anamtambulisha Masumbukoo kama Virus alikuwa akirekodi kila kitu.
Na hata wakati Stella kashikiliwa kiuno na Masumbuko alipiga picha tena kwa usanifu mzuri kabisa na hapo hapo alizituma kwa james kwa njia ya watsapp ndipo James baadala ya kuziona aliamua kumpigia simu lea na kumuuliza , lakini lea alimwambia kuwa ‘si yeye alikuwa akimuona mmbea’ basi hayo yote alikuwa kifanya kwa ajili yake kwani yeye alikuwa akimpenda sana na hakutaka amuoe Stella mwanamke kahaba .
Maneno hayo yalimuumiza sana James kwani aliamini kila kitu kwani hata sauti ya Stella kumtambulisha mwanaume Virus kama mpenzi wake aliyasikia kabisa na jambo hilo lilimfanya kujiona mjinga kabisa ndipo alipo anza kumpigia simu sana Stella , akitaka asikie chochote kutoka kwake lakini alijikuta akipiga simu mara nyingi bila kupokelewa ,
Hata jambo hilo la simu , Lea alikuwa ashalijua mapema kwani alikuwa ameweka simu ya Rafiki yake kwenye ‘silent mode’
James alikasirika moja kwa moja na hapo ndipo alipo amua kuandika ujumbe mrefu kwa njia ya watsapp na kuuvunja uhusiano wake na Stella ulio dumu muda mrefu sana kisa ni MASAA MAWILI YA KUMBUKUMBU


UNAWEZA PATA SOFTCOPY YA SIMULIZI HII YOTE.

SIMULZI ZANGU NYINGINE NI
-UMOJA NAMBA TISINI NA SABA
-NDOTO ZA KIKANUNI
-BOOK OF ALL NAMES (UMOJA NAMBA TISINI NA SABA )
-MY DREAM MY FAVOURITES)

KUHUSU UTARATIBU WA MALIPO
WASILIANA NAMI KWA KUGUSA HAPAA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom