Simu za kichina.

Jaguar

JF-Expert Member
Mar 6, 2011
3,438
1,026
Nipo ndani ya Coaster naelekea home Tunduma.Kuna abiria washamba wawili wanashindana kupiga music iliyomo kwenye simu zao,yaani gari zima ni kelele tupu mpaka kero.Sasa najiuliza,hivi hizi simu za kichina ni SIMU YENYE REDIO au ni REDIO YENYE SIMU?
 
Duh! cm za mchina sa hv ni kero..alafu awe nayo mtu asiyekuwa mwelewa kaweka mziki kafungulia sauti hadi mwisho yani tabu tupu mi mwnyw hayo yananikuta mara kibao..
 
duh kama jana ndani ya bus kuna jamaa katupigia nyimbo ya dini toka dar mpaka dom na kisim chake mchina.mwenyewe alikua anajiona mjaaanja anausikilizia wimbo mpaka anasinzia.nilitamani nimkate makofi basi tu
 
Ni ulimbukeni tu, na simu za mchna zilivojaa mwanjelwa sipati picha wasafwa wanavowasumbua wageni kwa michina yao.
 
Hizo simu tunaambiwa ni sub-standard. Hazipitii TBS. Hatujui madhara yake. Sauti si tatizo kwani inaweza kurekebishwa.
 
Ni ulimbukeni tu, na simu za mchna zilivojaa mwanjelwa sipati picha wasafwa wanavowasumbua wageni kwa michina yao.
Mkuu kama ulijua vile,hao akina mama walipandia pale pale mbeya mjini,yaani nilikereka sema basi tu sikutaka shari na mtu.
 
duh kama jana ndani ya bus kuna jamaa katupigia nyimbo ya dini toka dar mpaka dom na kisim chake mchina.mwenyewe alikua anajiona mjaaanja anausikilizia wimbo mpaka anasinzia.nilitamani nimkate makofi basi tu
Buhahahaah!
 
mi naona ni ufa yenye Cm maana ni kelele utafikiri mtu amefungulia sub woofer.
 
sasa hapo nani wa kulaumiwa? Ni umaskini tulionao watz wengi. Mi mwenyewe sizipendi simu za kichina! Ila ni rahisi kuzipata. Ila sijui kuhusu ubora wake na madhara yake labda. TATIZO NI UMASKINI!
 
sasa hapo nani wa kulaumiwa? Ni umaskini tulionao watz wengi. Mi mwenyewe sizipendi simu za kichina! Ila ni rahisi kuzipata. Ila sijui kuhusu ubora wake na madhara yake labda. TATIZO NI UMASKINI!

Kwanini anunue simu ya gharama kubwa wakati simu ya bei nafuu (Mchina) ipo? Hilo suala la kelele ni settings tu, yaweza kuwa ushamba but the volume can be minimized. Swali ninalojiuliza ni hili hivi kuwa na simu ya Kichina ni umaskini?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom