Simu feki: Mambo yanayowezekana hauyajui

giftcharles

Senior Member
Aug 11, 2015
147
76
Simu feki zinapingwa duniani kote

Kila mtu anafahamu kwamba mwezi wa 6 mwaka huu, wametangaza kuzizima simu zote feki Tanzania, imeleta utata sana ukizingatia kwamba asilimia kubwa ya watanzania walikuwa wakizitegemea simu feki.

Kwa zaidi ya miaka kumi dunia ilizikubali hizi simu ziwe kwenye soko, Baada ya kushtuka kwa kiasi gani simu hizi zinaleta hasara kwenye jamii, sehemu nyingi za dunia zinachukua hatua na walioahi walichukua hatua muda mrefu uliopita, kama Kenya walivyofanya matangazo yao mwaka 2012.

Kwa mtazamo wangu mimi, Tanzania imechelewa sana kuamka, Lakini nadhani ni kwa sababu inaeleweka ni kiasi gani watu wanazitegemea simu hizi.Pamoja na kwamba zinakaribiba kupotea, kuna mambo ambayo watu bado hawayaelewi kuhusu simu hizi.
simu feki
Nakupa hapa list ya mambo ambayo inawezekana hauyajui kuhusu simu hizi, nitaacha na links chini ya post hii kwa mtu anayetaka kusoma zaidi kuhusu mifano nitakayoitumia ndani ya post hii, twende basi…

1.Uchafu alioutupa Marekani ndio vifaa vya simu feki kutoka china

Marekani inatengeneza taka nyingi sana zinazotokana na vifaa vya kompyuta na simu mbovu, kwa miaka mingi sana nchi kubwa huwa zinasafirisha taka zao kwenye nchi ambazo zinaendelea, lakini hiyo ilikuwa kabla ya mwaka 1989 baada ya watu kulalalmika, ziliwekwa sheria dhidi ya mambo hayo.

Lakini Marekani haikuacha kutuma taka zake kwenda China, Unaweza ukadhani kwamba China ingeweza kuzikataa, lakini hawafanyi hivyo kwa sababu taka hizo ndizo zinabadilishwa kuwa simu nyingi feki zinazosafilishwa kwenye nchi zetu.

China inamji unaojihusisha na kazi ya kuzipokea taka hizi na kuzifanya ziwe tayari ili kubadilishwa kuwa bidhaa nyingi tofauti tunazoziita feki(sina jina kwa sababu ni limewekwa siri), Kwa muujibu wa “60 minutes” ya BBC1, mji huu hautembelewi na watu wengi, kwa sababu “hewa ya huo mji ni mchafu na maji yake yanasumu“.
simu feki

2. Kulipuka kwa simu feki ni rahisi kuliko unavyoweza dhania

Watu wengi huwa wanasikia hiki kitu na kupuuzia kwa sababu hawasikii kikitokea lakini “simu feki zinalipuka vibaya kama bomu”, maneno hayo alisema Michael Sathre, baada ya kulipukiwa simu yake mkononi mwake mwenyewe.

Kuna ripoti nyingi sana hapa duniani za simu kulipuka, zote zilihusisha betri feki iliyoshindwa kustahimili kazi, Sio utani kupoteza mkono kisa tu ulishindwa kutumia kuongeza hela ili upate orijino.

Hii nadhani ndyo sababu moja ambayo mimi inanifanya nikubali kuzimwa kwa kwa hizi simu feki zote.Unaweza ukasoma zaidi kuhusu simu iliyolipuka hapa www.cbsnews.com/news/exploding-cell-phones-spur-recalls.

3.Kama ulidhani soko la simu feki linatisha Tanzania, nakwambia China ndio linatisha zaidi

Wachina wakiona upenyo wowote wakuingiza hela, hata kama ni kwa kutumia jina la mtu mwingine watautumia, tena kwa kujazana bila aibu yoyote, Hii ilithibitishwa mwaka 2011, Kuna duka la Apple lilifunguliwa ndani ya Shanghai,China likiwa na mwonekano kama wa maduka ya Apple, wahudumu waliovaa kama wahudumu wa kawaida wa apple na bidhaa zao zote zikiwa za apple.

Lakini kinachochekesha ni kwamba duka lile halikuwa na mahusiano yoyote na kampuni ya apple, hakuna bidhaa yao hata moja iliyokuwa ya apple. Watu wanaotumia duka lile kununua simu zao wakiulizwa, wanasema kwamba wao hawajali kama simu zao ni feki au ni orijino, kama zinafanya kazi basi zinafaa kutumika.

Japokuwa duka hilo limevuta macho ya watu duniani kote kiasi cha kuongelea na BBC kwenye habari zao za kimataifa, Apple hajaongea chochote kuhusu duka hilo.

Ukiangalia hiyo video hapo chini ndio utaelewa vizuri zaidi…

(SAMAHANI! ili nisizidishe links video nimeiweka hapa simu feki: Mambo yanayowezekana hauyajui - TzaLive)

4.Fungulia mbwa ya simu feki ilikuwa baada ya China kujiunga na WTO

Kama hauifahamu WTO, ni makubaliano yaliyofanya na mataifa ili kuweza kufanya biashara pamoja bila ya kuwa na matatizo, Kabla ya mwaka 2001, China ilikuwa hairuhusu kampuni za ndani ya nchi yake kufanya biashara na nchi za nje, kwa hiyo bidhaa kama simu feki zilikuwa hazizoki.

Baada ya Kujiunga na WTO, ndipo simu viwanda vingi vidogo vilipoibuka ndani ya china na soko la simu feki lilipoanza kuteka dunia.

5.Dhana ya kwamba zimetengenezwa kwa ajili ya waafrika ni uwongo.

Kuna watu wanaosema kwamba hizi simu zilitengenezwa kwa ajili ya kuwauzia waafrika, Lakini hiyo sio kweli kwa sababu hata nchi kubwa kama marekani inayotumia mitambo ya kisasa kukagua bidhaa, bado inaidadi kubwa tu ya bidhaa feki zinazoingia ndani.

Kwa mtazamo ni rahisi kusema kwamba zimeletwa kwa ajili ya waafrika kwa sababu soko lake kubwa ni la waafrika, Lakini hiyo ni kwa sababu tu ya bei yake rahisi inayowavutia watu wengi wanaishi kwa kipato kidogo.

6.China ndiye msambazaji mkubwa lakini zipo nchi zingine kama Vietnam, South Korea na Thailand

Kila sehemu mada ya simu feki inapoingia, nchi itakayitajwa huwa ni China tu, hiyo ni kwa sababu china ndiye anayesambaza kwa wingi zaidi ukilinganisha na wengine lakini, wapo wengine wanaofanya biashara kwa ukubwa kama China.

Swali la kujiuiza tu hapo ni kwa nini nchi zote hizi zipo ndani ya bara moja, Asia.

Mambo madogo…

7.Simu feki zinachangia asilimia 2-3 ya mzunguko wa fedha hapa duniani.

Zingatia kwamba nimesema duniani, hela inayoongelewa hapo ni kubwa mno.

8.Simu feki zimechangia watu wengi sana kupoteza kazi zao.

Ni rahisi sana kuelewa watu wanapotezaje kazi kwa sababu ya simu feki, baada ya kuja simu hizi, watu wengi sana waliamia kwenye simu feki, kwa sababu ya urahisi wake wa bei, ndio maana marekani nafasi za kazi zaidi ya 700,000 zilipotea kwa sababu ya simu feki.

Mwisho

Kusema kwamba dunia ilipata hasara tupu baada ya kuja hizi simu ni uwongo kwa sababu zimewasaidia watu wengi sana, Kama mimi simu yangu ya kwanza nakumbuka ilikuwa ni mchina uliofeki kati ya feki, zimejitahidi kudumu muda mrefu kwenye nchi nyingi kwa sababu zinakubalika na watu wengi lakini kila mtu alikuwa anajua tayai kwamba lazima kuna siku zitapingwa.

Kama umeipenda hii post unaweza share na majamaa na marafiki kupitia link zilizopo juu na chini ya hii post.

Kama unamaoni unaweza kuniachia kwenye sehemu ya comments hapo chini.


Links

1.Counterfeit electronic components - Wikipedia, the free encyclopedia

2.Exploding Cell Phones Spur Recalls
 
Japo zinatuokoa lkn zifungwe tu maana ni majanga juu ya matatizo.
Niko radhi simu yangu ianze kufungiwa.

Nna-Swali kwa wataalamu 'ati hakuna kompyuta FEKI....Pc,Laptop, na n.k.
 
2. Kulipuka kwa simu feki ni rahisi kuliko unavyoweza dhania

Watu wengi huwa wanasikia hiki kitu na kupuuzia kwa sababu hawasikii kikitokea lakini “simu feki zinalipuka vibaya kama bomu”, maneno hayo alisema Michael Sathre, baada ya kulipukiwa simu yake mkononi mwake mwenyewe.

Kuna ripoti nyingi sana hapa duniani za simu kulipuka, zote zilihusisha betri feki iliyoshindwa kustahimili kazi, Sio utani kupoteza mkono kisa tu ulishindwa kutumia kuongeza hela ili upate orijino.

Hii nadhani ndyo sababu moja ambayo mimi inanifanya nikubali kuzimwa kwa kwa hizi simu feki zote.Unaweza ukasoma zaidi kuhusu simu iliyolipuka hapa www.cbsnews.com/news/exploding-cell-phones-spur-recalls.

Angalia sana habari unazozichukua google, hiyo habari ni ya mwaka 2004,

2004.PNG


Rate ya simu original zinazoungua inaweza kuwa kubwa kuliko hata hizo fake unazofikiria hapa.
Niletee source ya taarifa kuhusu kuungua kwa simu fake iliyotokea miaka ya karibuni.
Mi nakuletea hii hapa Baada ya Samsung Galaxy S3 naS4 kuwaka moto, Iphone 6 nayo Yalipotiwa Kuripuka ikiwa Mfukoni ! .
 
Japo zinatuokoa lkn zifungwe tu maana ni majanga juu ya matatizo.
Niko radhi simu yangu ianze kufungiwa.

Nna-Swali kwa wataalamu 'ati hakuna kompyuta FEKI....Pc,Laptop, na n.k.

sijawahi sikia kuhusu kompyuta nzima iliyofeki lakini vifaa kama processor na cooling fan nimekutana nazo feki mimi mwenyewe mara nyingi sana
 
Angalia sana habari unazozichukua google, hiyo habari ni ya mwaka 2004,

View attachment 330708

Rate ya simu original zinazoungua inaweza kuwa kubwa kuliko hata hizo fake unazofikiria hapa.
Niletee source ya taarifa kuhusu kuungua kwa simu fake iliyotokea miaka ya karibuni.
Mi nakuletea hii hapa Baada ya Samsung Galaxy S3 naS4 kuwaka moto, Iphone 6 nayo Yalipotiwa Kuripuka ikiwa Mfukoni ! .

Mmh sina uhakika kuhusu rates za simu zinazolipuka kwa sababu rekodi kama hizo sijaweza kuzipata sehemu yoyote, wala sijui na wewe unatumia rekodi zipi kama ushahidi wako.

Sidhani kwamba kwa sababu simu mbili mpya zimelipuka saizi ndyo sababu ya kusema kwamba orijino ndio zinazolipuka zaidi.Jinsi nilivyoandika hata kichwa cha habari hapo juu, haikuwa kwa maana ya kufananisha ipi inalipuka zaidi lakini kuonesha kwamba zina historia ndefu ya kulipuka.

Kusema kwamba Samsung au Iphone wametengeneza simu yenye betri yenye matatizo saizi, haimaanishi kwamba simu zao zote zitakazofwata zitakuwa na matatizo hayo, inawezekana kwamba hata sio toleo zima la simu mpya zinatatizo kama hilo.

Lakini simu feki zinauhakika wa kutoa bidhaa kibao zenye matatizo, ndio maana kuna mfululizo wa kesi za watu kuumia kisa simu feki kama DailyTech - Chinese Man Killed By Exploding Cell Phone na kesi zingine za watu kupata majeraha makubwa tangia miaka ya mwanzoni ya 2000.

Nadhani saizi umeelewa maana ya hii post, hapakuwa na mfananisho wowote kati ya simu fake na orijino, pia hamna data yoyote inayoweza thibitisha kwamba simu orijino ndizo zinazolipuka zaidi ya feki hata kinyume chake pia
 
Angalia sana habari unazozichukua google, hiyo habari ni ya mwaka 2004,

View attachment 330708

Rate ya simu original zinazoungua inaweza kuwa kubwa kuliko hata hizo fake unazofikiria hapa.
Niletee source ya taarifa kuhusu kuungua kwa simu fake iliyotokea miaka ya karibuni.
Mi nakuletea hii hapa Baada ya Samsung Galaxy S3 naS4 kuwaka moto, Iphone 6 nayo Yalipotiwa Kuripuka ikiwa Mfukoni ! .

OK nimeipitia link yako vizuri zaidi na hiyo blog post haijaongelea simu kulipuka, bali tatizo moja kubwa walilonalo Iphone kwa miaka mingi sana, simu zao huwa zinawaka moto baada ya simu yenyewe kupindishwa kwa muda mrefu.

Aina ya mlipuko ninaouongelea mimi unahusisha kupasuka kama bomu na kusababisha madhara zaidi hata ya kuunguza ngozi tu.
 
OK nimeipitia link yako vizuri zaidi na hiyo blog post haijaongelea simu kulipuka, bali tatizo moja kubwa walilonalo Iphone kwa miaka mingi sana, simu zao huwa zinawaka moto baada ya simu yenyewe kupindishwa kwa muda mrefu.
Mantiki yenyewe haikuwa iphone, bali ni simu original kuwaka moto kama hizo S3, S4 na hiyo Iphone 6 maana wewe pale juu ulidai fake huwa zina mtindo huo na umeshindwa kuleta ushahidi hapa.

Aina ya mlipuko ninaouongelea mimi unahusisha kupasuka kama bomu na kusababisha madhara zaidi hata ya kuunguza ngozi tu.[/QUOTE]

We ni simu gani inayoweza kulipuka kama bomu ?
Mbona ni senseless kabisa, soma hapa Kinachoua bomu linapolipuka ni nini?
 
Mantiki yenyewe haikuwa iphone, bali ni simu original kuwaka moto kama hizo S3, S4 na hiyo Iphone 6 maana wewe pale juu ulidai fake huwa zina mtindo huo na umeshindwa kuleta ushahidi hapa.

Aina ya mlipuko ninaouongelea mimi unahusisha kupasuka kama bomu na kusababisha madhara zaidi hata ya kuunguza ngozi tu.

We ni simu gani inayoweza kulipuka kama bomu ?
Mbona ni senseless kabisa, soma hapa Kinachoua bomu linapolipuka ni nini?[/QUOTE]


1.Ikague vizuri link uliyoweka halafu uniambie kama kuna simu nyingine zaidi Iphone iliyoongelewa

2.Sina haja ya kutoa mifano mia ili nieleweke, mmoja unatosha na ndio nimekuwekea juu hapo mkuu

3.Kama unauliza kuhusu simu kulipuka kama bomu naomba uingie hapa na usome sio upitie pitie juu tu Exploding cell phonesprompt warnings

-maneno yake mwenyewe aliyetokewa na tukio ni "Curtis Sathre said it was like a bomb going off. His 13-year-old son Michael stood stunned, his ears ringing, hand gushing blood and body covered in black ash."
 
1.Ikague vizuri link uliyoweka halafu uniambie kama kuna simu nyingine zaidi Iphone iliyoongelewa
Title ya habari nayo hujaisoma vizuri, "Baada ya Samsung Galaxy S3 na S4 kuwaka moto, Iphone 6 nayo Yalipotiwa Kuripuka ikiwa Mfukoni !"

2.Sina haja ya kutoa mifano mia ili nieleweke, mmoja unatosha na ndio nimekuwekea juu hapo mkuu

Mfano wako ni mfano uliokufa maana habari yako ni ya 2004, utatumiaje kuvalidate 2016
Leta mfano ulio hai utaeleweka.
 
Simu feki zinapingwa duniani kote

Kila mtu anafahamu kwamba mwezi wa 6 mwaka huu, wametangaza kuzizima simu zote feki Tanzania, imeleta utata sana ukizingatia kwamba asilimia kubwa ya watanzania walikuwa wakizitegemea simu feki.

Kwa zaidi ya miaka kumi dunia ilizikubali hizi simu ziwe kwenye soko, Baada ya kushtuka kwa kiasi gani simu hizi zinaleta hasara kwenye jamii, sehemu nyingi za dunia zinachukua hatua na walioahi walichukua hatua muda mrefu uliopita, kama Kenya walivyofanya matangazo yao mwaka 2012.

Kwa mtazamo wangu mimi, Tanzania imechelewa sana kuamka, Lakini nadhani ni kwa sababu inaeleweka ni kiasi gani watu wanazitegemea simu hizi.Pamoja na kwamba zinakaribiba kupotea, kuna mambo ambayo watu bado hawayaelewi kuhusu simu hizi.
simu feki
Nakupa hapa list ya mambo ambayo inawezekana hauyajui kuhusu simu hizi, nitaacha na links chini ya post hii kwa mtu anayetaka kusoma zaidi kuhusu mifano nitakayoitumia ndani ya post hii, twende basi…

1.Uchafu alioutupa Marekani ndio vifaa vya simu feki kutoka china

Marekani inatengeneza taka nyingi sana zinazotokana na vifaa vya kompyuta na simu mbovu, kwa miaka mingi sana nchi kubwa huwa zinasafirisha taka zao kwenye nchi ambazo zinaendelea, lakini hiyo ilikuwa kabla ya mwaka 1989 baada ya watu kulalalmika, ziliwekwa sheria dhidi ya mambo hayo.

Lakini Marekani haikuacha kutuma taka zake kwenda China, Unaweza ukadhani kwamba China ingeweza kuzikataa, lakini hawafanyi hivyo kwa sababu taka hizo ndizo zinabadilishwa kuwa simu nyingi feki zinazosafilishwa kwenye nchi zetu.

China inamji unaojihusisha na kazi ya kuzipokea taka hizi na kuzifanya ziwe tayari ili kubadilishwa kuwa bidhaa nyingi tofauti tunazoziita feki(sina jina kwa sababu ni limewekwa siri), Kwa muujibu wa “60 minutes” ya BBC1, mji huu hautembelewi na watu wengi, kwa sababu “hewa ya huo mji ni mchafu na maji yake yanasumu“.
simu feki

2. Kulipuka kwa simu feki ni rahisi kuliko unavyoweza dhania

Watu wengi huwa wanasikia hiki kitu na kupuuzia kwa sababu hawasikii kikitokea lakini “simu feki zinalipuka vibaya kama bomu”, maneno hayo alisema Michael Sathre, baada ya kulipukiwa simu yake mkononi mwake mwenyewe.

Kuna ripoti nyingi sana hapa duniani za simu kulipuka, zote zilihusisha betri feki iliyoshindwa kustahimili kazi, Sio utani kupoteza mkono kisa tu ulishindwa kutumia kuongeza hela ili upate orijino.

Hii nadhani ndyo sababu moja ambayo mimi inanifanya nikubali kuzimwa kwa kwa hizi simu feki zote.Unaweza ukasoma zaidi kuhusu simu iliyolipuka hapa www.cbsnews.com/news/exploding-cell-phones-spur-recalls.

3.Kama ulidhani soko la simu feki linatisha Tanzania, nakwambia China ndio linatisha zaidi

Wachina wakiona upenyo wowote wakuingiza hela, hata kama ni kwa kutumia jina la mtu mwingine watautumia, tena kwa kujazana bila aibu yoyote, Hii ilithibitishwa mwaka 2011, Kuna duka la Apple lilifunguliwa ndani ya Shanghai,China likiwa na mwonekano kama wa maduka ya Apple, wahudumu waliovaa kama wahudumu wa kawaida wa apple na bidhaa zao zote zikiwa za apple.

Lakini kinachochekesha ni kwamba duka lile halikuwa na mahusiano yoyote na kampuni ya apple, hakuna bidhaa yao hata moja iliyokuwa ya apple. Watu wanaotumia duka lile kununua simu zao wakiulizwa, wanasema kwamba wao hawajali kama simu zao ni feki au ni orijino, kama zinafanya kazi basi zinafaa kutumika.

Japokuwa duka hilo limevuta macho ya watu duniani kote kiasi cha kuongelea na BBC kwenye habari zao za kimataifa, Apple hajaongea chochote kuhusu duka hilo.

Ukiangalia hiyo video hapo chini ndio utaelewa vizuri zaidi…

(SAMAHANI! ili nisizidishe links video nimeiweka hapa simu feki: Mambo yanayowezekana hauyajui - TzaLive)

4.Fungulia mbwa ya simu feki ilikuwa baada ya China kujiunga na WTO

Kama hauifahamu WTO, ni makubaliano yaliyofanya na mataifa ili kuweza kufanya biashara pamoja bila ya kuwa na matatizo, Kabla ya mwaka 2001, China ilikuwa hairuhusu kampuni za ndani ya nchi yake kufanya biashara na nchi za nje, kwa hiyo bidhaa kama simu feki zilikuwa hazizoki.

Baada ya Kujiunga na WTO, ndipo simu viwanda vingi vidogo vilipoibuka ndani ya china na soko la simu feki lilipoanza kuteka dunia.

5.Dhana ya kwamba zimetengenezwa kwa ajili ya waafrika ni uwongo.

Kuna watu wanaosema kwamba hizi simu zilitengenezwa kwa ajili ya kuwauzia waafrika, Lakini hiyo sio kweli kwa sababu hata nchi kubwa kama marekani inayotumia mitambo ya kisasa kukagua bidhaa, bado inaidadi kubwa tu ya bidhaa feki zinazoingia ndani.

Kwa mtazamo ni rahisi kusema kwamba zimeletwa kwa ajili ya waafrika kwa sababu soko lake kubwa ni la waafrika, Lakini hiyo ni kwa sababu tu ya bei yake rahisi inayowavutia watu wengi wanaishi kwa kipato kidogo.

6.China ndiye msambazaji mkubwa lakini zipo nchi zingine kama Vietnam, South Korea na Thailand

Kila sehemu mada ya simu feki inapoingia, nchi itakayitajwa huwa ni China tu, hiyo ni kwa sababu china ndiye anayesambaza kwa wingi zaidi ukilinganisha na wengine lakini, wapo wengine wanaofanya biashara kwa ukubwa kama China.

Swali la kujiuiza tu hapo ni kwa nini nchi zote hizi zipo ndani ya bara moja, Asia.

Mambo madogo…

7.Simu feki zinachangia asilimia 2-3 ya mzunguko wa fedha hapa duniani.

Zingatia kwamba nimesema duniani, hela inayoongelewa hapo ni kubwa mno.

8.Simu feki zimechangia watu wengi sana kupoteza kazi zao.

Ni rahisi sana kuelewa watu wanapotezaje kazi kwa sababu ya simu feki, baada ya kuja simu hizi, watu wengi sana waliamia kwenye simu feki, kwa sababu ya urahisi wake wa bei, ndio maana marekani nafasi za kazi zaidi ya 700,000 zilipotea kwa sababu ya simu feki.

Mwisho

Kusema kwamba dunia ilipata hasara tupu baada ya kuja hizi simu ni uwongo kwa sababu zimewasaidia watu wengi sana, Kama mimi simu yangu ya kwanza nakumbuka ilikuwa ni mchina uliofeki kati ya feki, zimejitahidi kudumu muda mrefu kwenye nchi nyingi kwa sababu zinakubalika na watu wengi lakini kila mtu alikuwa anajua tayai kwamba lazima kuna siku zitapingwa.

Kama umeipenda hii post unaweza share na majamaa na marafiki kupitia link zilizopo juu na chini ya hii post.

Kama unamaoni unaweza kuniachia kwenye sehemu ya comments hapo chini.


Links

1.Counterfeit electronic components - Wikipedia, the free encyclopedia

2.Exploding Cell Phones Spur Recalls
We ni simu gani inayoweza kulipuka kama bomu ?
Mbona ni senseless kabisa, soma hapa Kinachoua bomu linapolipuka ni nini?


1.Ikague vizuri link uliyoweka halafu uniambie kama kuna simu nyingine zaidi Iphone iliyoongelewa

2.Sina haja ya kutoa mifano mia ili nieleweke, mmoja unatosha na ndio nimekuwekea juu hapo mkuu

3.Kama unauliza kuhusu simu kulipuka kama bomu naomba uingie hapa na usome sio upitie pitie juu tu Exploding cell phonesprompt warnings

-maneno yake mwenyewe aliyetokewa na tukio ni "Curtis Sathre said it was like a bomb going off. His 13-year-old son Michael stood stunned, his ears ringing, hand gushing blood and body covered in black ash."[/QUOTE]
Mmi pia km fundi wa simu na changia km ifuatavyo 1.simu feki zilizo nyingi zina ic moja hapo ina maanisha mfumo wa mawasiliano,wa ku chagi,sauti,n.k uko kwenye ic moja ikiungua hiyo ic simu unatupa 2.file zake hazipo kwasabubu simu hizo haziko kwenye mfumo rasmi 3.hata ukitafuta ufumbuzi wa utengenezaji wa simu hizo kwenye mtandao hakuna
 
Japo zinatuokoa lkn zifungwe tu maana ni majanga juu ya matatizo.
Niko radhi simu yangu ianze kufungiwa.

Nna-Swali kwa wataalamu 'ati hakuna kompyuta FEKI....Pc,Laptop, na n.k.
computer karibia mara zote zinakuwa ni amd na intel

hawa jamaa wanakuwa na total controll ya vitu kama motherboard, ram, hdd nk huwezi kuweka kifaa ambacho haja ki approve ndio maana soko la pc lipo safe.

hata simu kabla ya kuja mediatek soko lilikuwa salama sababu soc za qualcomm na exynos zinatolewa kwa makampuni maalum tofauti na mediatek.
 
computer karibia mara zote zinakuwa ni amd na intel

hawa jamaa wanakuwa na total controll ya vitu kama motherboard, ram, hdd nk huwezi kuweka kifaa ambacho haja ki approve ndio maana soko la pc lipo safe.

hata simu kabla ya kuja mediatek soko lilikuwa salama sababu soc za qualcomm na exynos zinatolewa kwa makampuni maalum tofauti na mediatek.
mtk ni tatizo uki factory reset ama hardware reset hakuna imei km hakuna imei hakuna network simu ina andika invalid imei
 
computer karibia mara zote zinakuwa ni amd na intel

hawa jamaa wanakuwa na total controll ya vitu kama motherboard, ram, hdd nk huwezi kuweka kifaa ambacho haja ki approve ndio maana soko la pc lipo safe.

hata simu kabla ya kuja mediatek soko lilikuwa salama sababu soc za qualcomm na exynos zinatolewa kwa makampuni maalum tofauti na mediatek.
Asante mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom