Wadau nawasalimu wote. Ninayo simu aina ya htc one v ambayo ni simu moja nzuri sana kwa maoni yangu. Nimeitumia muda mrefu sasa. ina almost vitu muhimu ninavyovihitaji. Shida pekee ambayo inanifanya kuiona haifai ni pale inaposhindwa kushika mitandao ya Voda, airtel na hata Tigo ukiwa mbali kidogo na minara hata kama km 7 tu kutoka mnara. Nimesikia simu kubwa kama hii unaweza kuiseti ikashika mtandao mahali karibu popote. Je ni kweli? kama kweli unaseti vipi? Wataalamu nisaidieni.