Simple equation inayoitesa CCM na Taifa

Ukweli ni kwamba wananchi wanataka chama mbadala wa CCM kuongoza inchi. Ndiyo maana kila chama cha upinzani kinapoibuka huwa na nguvu sana kiushidani. Na CCM imekua ikitumia raslimali nyingi pamoja na vyombo dola kubaki madatakani na kujaribu kuua upinzani kila unapopata nguvu. Na hapo ndipo kama taifa mtego ulipo. Hili taifa haitakuja liendee kama mfumo huu wa siasa hautobadilika. Kumbuka ili taifa liendelee tinahitaji siasa safi pia.
Anzia NCCR ya Mrema, CAF ya Maalim na Lipumba na sasa CHADEMA katika nyakati tofauti Serikali zinazo ongozwa na CCM zimetumia resource kubwa kuhakikisha opposition parties zinakufa. Resources zikitumika kudhofisha chama A chama B kinapata nguvu ukihamishia resources kuua chama B chama C kinaibuka kwani ni matakwa ya wenye inchi . As a result miaka nenda rudi sehemu kubwa ya esources za inchi zitakua zinatumika kukandamiza na kuuwa upinzani utakaokuwa unaibuka kwa namna nyingine. Kwa kuwa hivyo Tanzania haitokuja ipige hatua kubwa kimaendeleo. Suruhisho either turudi mfumo wa chama kimoja au turuhusu democrasia ya kweli. Kubaki vuguvugu hivi ni hasara kubwa kwa taifa ingawa yaweza kuwa faida kwa CCM na familia zao.
Umeongea point kubwa sana jumapili ya leo
 
Resources zikitumika kudhofisha chama A chama B kinapata nguvu ukihamishia resources kuua chama B chama C kinaibuka kwani ni matakwa ya wenye inchi .
'Resource' pekee waliyonayo kwa sasa hivi na ndio kinga yao kubwa ni vyombo vya ukandamizaji tu pekee- polisi, tume na wengine.

Wangetegemea pesa pekee, kama wanavyofanya kuwanunua wabunge na madiwani wasingefurukuta kwa aina yoyote mbele ya wananchi waliowakinai.

Pangetokea ushawishi wa kutosha kuvionyesha hivi vyombo vya wananchi kukataa kutumika kisiasa ingekuwa kazi rahisi sana kuwaondoa CCM.
 
Wapinzani watakuwepo na Chama kikuu cha upinzani kitakua ni ACT.
Wabunge wa Upinzani kutoka Zanzibar upande wa Pemba hawaepukiki.
Zanzibar hasa Pemba hakuna unafiki mkubwa wa kutafuta utajiri wadhulma kama Bara na wale wa Unguja.
Kinacholeta ubaguzi wa kisiasa sio vyama Bali ni watu wabinafsi waliopo kwenye vyama vya siasa wanaowaza kupata maslahi makubwa na familia zao na msingi wa yote ni kutumia umaskini wa watu na kujenga mazingira ya kuwa endelevu.

Bara hakuna haja ya kuwa na upinzani mpaka wananchi watakapoamka na kuweka pembeni ubinafsi wao na kupigania haki na utu wa mwanadam.

Kuwategemea matajiri kama Mbowe,Lowasa,Sumaye,Dr.Mashinji n kuleta mabadiliko ni ndoto mana wanalinda maslahi na heshima zao kwanza.

Ni lazima atokee Mtu mwenye kujitoa sana kiroho,kijamii ,kiitikadi na kisiasa.
Kidoooogo Zito anaweza na angekua na chama kama Chadema bila shaka mtiti ungekua mkubwa.

Mwingine ni Lisu.
Ni watu wenye mitizamo ya mbali kisiasa.

Hata hivyo CCM itakuja kuanguka ghafla na kabla ya 2025 patakua na katiba mpya.



Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu 1000 digits hebu nifafanulie hapo uliposema CCM itaanguka ghafla kabla ya 2025!

Vile vile Katiba mpya ya nchi itapatikana kabla ya 2025
 
..kuna MADOGO wengi ambao hawaiogopi / hawaiheshimu CCM tofauti na wazee watu wazima wamefikisha umri wa kupiga kura. Hao ndiyo tatizo na watakuja kuiangusha CCM.
 
Boss Los técnicos Umeongea kwa Hisia kali .. Ila nitoe mimi huko, Natumaini wahusika wamekusikia na watafanyia kazi Ushauri na Maoni yako. Tatizo Watawala wanacheza Mind Set zetu.


Baadhi ya Giants wa dunia kipindi cha nyuma waliamini kama wewe lakini ghafla mambo yaliwageukia na kugharimu maisha yao na wakazikwa.

Ni lazima tujifunze kuendana na wakati.
Vazi likibana shona lingine la sivyo utavaa nguo isiyo na staha pengine ukajikuta uchi.

Ujinga wa ccm ni kudhani wanayo support ya watu wengi wenye afya ya mwili na akili nyuma yao , kumbe wamejaa watu dhaifu, wanyonge na wajinga waliokata tamaa na wasio na matumaini ya kuishi, wakidhani umaskini wao umesababishwa na watu wenye afya ya mwili na akili ambao wengi wako nyuma ya fikra huru.

Siku hadi siku kundi hili la fikra huru linazidi kuongezeka mtaani logarithmically.
Wakati hao wajinga ambao ni mtaji wao wanapungua arithmetically na sasa kuna kila dalili hili kundi la wajinga ambao ni mtaji wao linataka kulingana na hawa wenye afya ya mwili na akili, hii inamaanisha mtaji wao unaisha.

Katika mazingira hayo uchaguzi huru ni kizungumkuti na ikitokea mtu akawahakikishia ulinzi wapiga kura machafuko huwa makubwa kwa mazingira hayo ambayo kimsingi huleta mabadiliko makubwa ambayo hawata yataka siku zote.

Ni vyema ccm ijiongezee mtaji wa wapiga kura kwa kukoma kuwapa watu maisha magumu na manyanyaso kwa kibri na jeuri. Kupanga na kuunda sera rafiki kwa maisha ya watu.

Kama sivyo anguko litawaramba na kuanza kung'ang'ania madaraka na hatimaye mtavuna mnachokipanda

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukweli ni kwamba wananchi wanataka chama mbadala wa CCM kuongoza inchi. Ndiyo maana kila chama cha upinzani kinapoibuka huwa na nguvu sana kiushidani. Na CCM imekua ikitumia raslimali nyingi pamoja na vyombo dola kubaki madatakani na kujaribu kuua upinzani kila unapopata nguvu. Na hapo ndipo kama taifa mtego ulipo. Hili taifa haitakuja liendee kama mfumo huu wa siasa hautobadilika. Kumbuka ili taifa liendelee tinahitaji siasa safi pia.

Anzia NCCR ya Mrema, CAF ya Maalim na Lipumba na sasa CHADEMA katika nyakati tofauti Serikali zinazo ongozwa na CCM zimetumia resource kubwa kuhakikisha opposition parties zinakufa. Resources zikitumika kudhofisha chama A chama B kinapata nguvu ukihamishia resources kuua chama B chama C kinaibuka kwani ni matakwa ya wenye inchi .

As a result miaka nenda rudi sehemu kubwa ya esources za inchi zitakua zinatumika kukandamiza na kuuwa upinzani utakaokuwa unaibuka kwa namna nyingine. Kwa kuwa hivyo Tanzania haitokuja ipige hatua kubwa kimaendeleo. Suruhisho either turudi mfumo wa chama kimoja au turuhusu democrasia ya kweli. Kubaki vuguvugu hivi ni hasara kubwa kwa taifa ingawa yaweza kuwa faida kwa CCM na familia zao.
Nimepapenda hapo faida kwa familia zao
 
Ukweli ni kwamba wananchi wanataka chama mbadala wa CCM kuongoza inchi. Suruhisho either turudi mfumo wa chama kimoja au turuhusu democrasia ya kweli.
Mkuu Kagoshima, wananchi wepi hao unao wazungumzia wanaotaka chama mbadala wa CCM?.
Kipimo cha wananchi kutaka chama mbadala ni kipi?.
Tujifunze kuwa wakweli toka ndani ya nafsi zetu, chama kipate ushindi wa kishindo cha asilimia 99.9% halafu useme watu wanataka chama mbadala. Kipimo pekee cha sauti ya watu ni kupitia kwenye sanduku la kura, natumaini kazi nzuri kwenye serikali za mitaa umeiona, October inakwenda kukamilika kwenye uchaguzi mkuu na wembe uliotumika kunyolea kwenye serikali za mitaa, unakwenda kutumika kwenye uchaguzi mkuu!.
P
 

Matatizo ya uchumi yajayo ndio yatakayoiua ccm hii. Kinachofanyika sasa hivi ni kuzalisha kundi la watu wasiokuwa na cha kupoteza (mtu ataogopa polisi na vyombo vya dola pale tu anapokuwa na kitu cha kupoteza). Itakapofikia optimum number ya wasio na cha kupoteza (na hawana matumaini) polisi watavua magwanda na siku hiyo kila mtu anaejipambanua na ccm hii ataikana kwa nguvu zote.
 
Matatizo ya uchumi yajayo ndio yatakayoiua ccm hii. Kinachofanyika sasa hivi ni kuzalisha kundi la watu wasiokuwa na cha kupoteza (mtu ataogopa polisi na vyombo vya dola pale tu anapokuwa na kitu cha kupoteza). Itakapofikia optimum number ya wasio na cha kupoteza (na hawana matumaini) polisi watavua magwanda na siku hiyo kila mtu anaejipambanua na ccm hii ataikana kwa nguvu zote.
Ama tuombe siku hiyo ifike, ama utasubiri sana kama sio kusubiri milele!.
Ukweli ni CCM itatawala milele!, take it or leave it
P
 
Magufuli ni kiski cha mpingo. Mabeberu wote duniani wanafyata mkia kwa Magu
Wanafyata mkia kwa Magufuli,lakini Magufuli anaufyatua kwa mabeberu kwakuwa anatambua kuwa maisha bila mabeberu haiwezekani,barabara zote zinazojengwa zinajengwa kwa msaada wa mabeberu, reli inayojengwa ni kazi ya mabeberu, kiwanja cha ndege Chato ni kazi ya mabeberu, daraja la kigamboni kazi ya mabeberu, ni juzi tu mabeberu wamepiga chafya ya kuzuia mkopo wao Lumumba yote iliweweseka kiasi cha kutaka kumtoa roho Zitto.
 
Ama tuombe siku hiyo ifike, ama utasubiri sana kama sio kusubiri milele!.
Ukweli ni CCM itatawala milele!, take it or leave it
P

Paskali; unaanza kunifanya niamini kuwa sasa hivi unaishi nje ya nchi.
 
Ama tuombe siku hiyo ifike, ama utasubiri sana kama sio kusubiri milele!.
Ukweli ni CCM itatawala milele!, take it or leave it
P
Aysee, una akili kisoda.

Baada ya kuitwa kwenye kamati kuna kitu walikuharibu.

Pia, una scandal fulani mbaya sana wewe na mwalle.

Sishangai kwanini unaweza kuandika upupu, CCM itatawala milele.

Something is wrong in your brain cells.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
28 Reactions
Reply
Back
Top Bottom