Kiranja Mkuu
JF-Expert Member
- Feb 18, 2010
- 4,066
- 4,085
Raisi wangi muongo, mwingi wa ahadi zisizotekelezeka.
Alipoingia madarakani alianza kwa kulihutubia bunge, hotuba, kali iliyojaa msisimko. Tukajua tumepata raisi anayekuja na kulikomboa taifa letu.
Siku chache baadae,akaja na mpya akasema ana orodha ya wala rushwa wote na atawataja hadharani ili wafikishwe mahakamani na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.
hakuwataja.
Siku chache tena baadae, akaja na mpya, ana majina ya wafanyabiashara wa madawa ya kulevya, akatuambia atawataja, na watafikishwa mahakamani.
Hakutajwa hata mtu mmoja. Amina wa chifupa akajidai kulivalia njuga swala hili kule dodoma, akajikuta ndio umekuwa mwanzo wa safari yake kuelekea kwenye pumziko la kudumu milele.
kikwete hakuwataja wafanyabiashara hao, na wala hamna hata mmoja aliyepelekwa mahakamani zaidi ya wale wanaokutwa na kete mbili.
Baadae tena akaja na majina ya wanaofadhili mtandao wa ujambazi nchi, unaovunja mabenki, wizi wa magari na wizi wa kwenye taasisi za fedha. Wimbo wa chiriku wa kikwere ukawa ni ulele.
kimya kikuu.
Uozo unaongezeka kila siku iendayo kwa mungu. Hali ya uchumi imekuwa ngumu kuliko kawaida. Tuliahidiwa maisha bora kwa kila mtanzania, tumepata bora maisha kwa kila mtanzania, na sasa wimbo wao huo wa maisha bora hauimbwi tena, amekaa kimya akitucheka akitucheka tunavyopiga miayo ya njaa.
Haka kajamaa kameshindwa kabisa kutimiza ahadi zake nyingi alizotuahidi. Ametutapeli kura zetu.
Hakika mwaka huu simpi kura yangu hata kwa dawa.
Alipoingia madarakani alianza kwa kulihutubia bunge, hotuba, kali iliyojaa msisimko. Tukajua tumepata raisi anayekuja na kulikomboa taifa letu.
Siku chache baadae,akaja na mpya akasema ana orodha ya wala rushwa wote na atawataja hadharani ili wafikishwe mahakamani na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.
hakuwataja.
Siku chache tena baadae, akaja na mpya, ana majina ya wafanyabiashara wa madawa ya kulevya, akatuambia atawataja, na watafikishwa mahakamani.
Hakutajwa hata mtu mmoja. Amina wa chifupa akajidai kulivalia njuga swala hili kule dodoma, akajikuta ndio umekuwa mwanzo wa safari yake kuelekea kwenye pumziko la kudumu milele.
kikwete hakuwataja wafanyabiashara hao, na wala hamna hata mmoja aliyepelekwa mahakamani zaidi ya wale wanaokutwa na kete mbili.
Baadae tena akaja na majina ya wanaofadhili mtandao wa ujambazi nchi, unaovunja mabenki, wizi wa magari na wizi wa kwenye taasisi za fedha. Wimbo wa chiriku wa kikwere ukawa ni ulele.
kimya kikuu.
Uozo unaongezeka kila siku iendayo kwa mungu. Hali ya uchumi imekuwa ngumu kuliko kawaida. Tuliahidiwa maisha bora kwa kila mtanzania, tumepata bora maisha kwa kila mtanzania, na sasa wimbo wao huo wa maisha bora hauimbwi tena, amekaa kimya akitucheka akitucheka tunavyopiga miayo ya njaa.
Haka kajamaa kameshindwa kabisa kutimiza ahadi zake nyingi alizotuahidi. Ametutapeli kura zetu.
Hakika mwaka huu simpi kura yangu hata kwa dawa.